Ukweli Kuhusu - Akamaihd.net

32
!"#2 FEBRUARI 2011 Ukweli Kuhusu Ukweli Kuhusu Uchawi Uchawi PIA: JE, SAYANSI INAPATANA NA BIBLIA? UKU. 22

Transcript of Ukweli Kuhusu - Akamaihd.net

!"#2F E B R U A R I 2 0 1 1

Ukweli KuhusuUkweli Kuhusu

UchawiUchawi

PIA: JE, SAYANSI INAPATANANA BIBLIA? UKU. 22

Ukweli Kuhusu Uchawi3 Ni Nini Huwafanya Watu Wavutiwe na

Uchawi?

4 Ni Nani Chanzo Halisi cha Uchawi?

7 Chanzo cha Kweli cha Mwongozo na Tumaini

8 Kweli ya Biblia Iliwaweka Huru

10 Vijana HuulizaMbona Wazazi Wangu Hawaniachi Nijifurahishe?

13 Mapendekezo ya Kuwalinda Wazee

16 Kitabu KinachotegemekaSehemu ya 4—Muungano wa Umedi na Uajemina Historia ya Biblia

19 Walienda Kutafuta Dhahabu, Wakapata Makao

22 Maoni ya BibliaJe, Sayansi Inapatana na Biblia?

24 Je, Ni Kazi ya Ubuni?Mkia wa Bakteria

25 Maisha Yangu YamekuwaYenye Kuridhisha

28 Je, Una Miradi Inayopatanana Akili?

29 Kuutazama Ulimwengu

30 Mazungumzo ya Familia

32 Wao Si Wachanga Sana

Amkeni!NAKALA ZINAZOCHAPWA 39,913,000HUCHAPISHWA KATIKA LUGHA 83

Amkeni! Februari 2011 3

HUENDA jibu la swali hilo likategemea kwa kia-si kikubwa mahali mtu anapoishi, na pia imani

yake ya kidini pamoja na malezi. Ni nini huwafanyawatu katika eneo lenu wavutiwe na uchawi? Huendawakavutiwa na moja ya sababu zifuatazo.

˘ Udadisi Wanadamu wamezaliwa wakiwa wa-dadisi, na uchawi ni moja kati ya mambo yana-yochochea udadisi wao. Kwa hiyo, watu fulaniwangependa kujua ikiwa kuna nguvu iliyofichikainayoongoza uchawi. Wengine huwaendea wachawiili wajue ni nani wanaowaloga na wengine husima-ma barabarani kuwatazama watu wanaofanya miuji-za. Huenda hata wengine wakahudhuria mkutanowa kuwasiliana na pepo.

˘ Burudani Katika miaka ya hivi karibuni, kume-kuwa na ongezeko la ghafula katika burudani—vita-bu, sinema, na michezo ya kompyuta—kuhusu ucha-wi na ushirikina wa dini za kipagani za kale. Pia,baadhi ya burudani hizo huonyesha jeuri na ngonowaziwazi.

˘ Mahangaiko kuhusu wakati ujao Biblia ilita-biri hivi: “Katika siku za mwisho kutakuwa na nya-kati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.”(2 Timotheo 3:1) Kwa kweli tunaishi katika siku zamwisho, na watu wengi wanawatembelea watu wa-naofanya mambo ya uchawi—kamavile, viongozi wakidini wanaodai kuzungumza na Mungu na wacha-wi wanaodai kuwawanaweza kufanya uaguzi—ili ku-pata mwongozo. Mtu fulani ambaye husoma akili zawatu alisema: “Hii ni moja kati ya biashara chacheambazo haziathiriwi na kuporomoka kwa uchumi.Kwa kawaida watu hawaji kukuona wanapokuwana furaha.” Mbashiri mmoja huko Kanada alisema:“Siku hizi mimi hupigiwa simu na wafanyabiasharamashuhuri ambao hupendelea kuzungumza kupitiasimu zao za kibinafsi kazini au kupitia simu zao zamkononi nao hunong’oneza wanapozungumza wa-kiwa nje ya ofisi zao.” Pia aliongeza hivi: “Hawa niwatu ambao, awali walikuwa na shaka kuhusu ku-mwendea mtu anayesoma akili za watu.”

˘ Magonjwa Mara nyingi katika nchi fulani wa-gonjwa wengi wanaougua sana huacha matibabu yahospitali na kutafuta msaada kutoka kwa wagangawa kienyeji wanaotumia uchawi. Huenda wakaa-mbiwa kuwa wao ni wagonjwa kwa sababu wamelo-gwa. Ili kumsaidia mtu aliyelogwa, huenda marafikiau watu wa familia wakatafuta msaada kutoka kwamchawi ambaye huenda akawaambia walipe kiasikikubwa cha pesa.

˘ Kutafuta ulinzi na bahati njema Katika mae-neo fulani ya Afrika, wanakijiji hutafuta “nabii” wakanisa lenye uvutano mkubwa au mchawi ili afu-kuze roho waovu kutoka katika jamii. Desturi hizohutia ndani kunywa michanganyiko fulani na “majimatakatifu.” Kwingineko piawatu hutumiawachawiili kuleta bahati katika nyumba mpya au kaburi kwakuwa inaaminiwa kwamba roho za wafu zinawezakuwaletea bahati.

˘ Kuwalinda watoto Huko Papua New Guinea,huenda mama akakataa kutoka nje usiku akiwana mtoto wake mchanga. Kwa nini? Anahofu kwa-mba huenda roho waovu wakamdhuru mtoto wake.Huko Uganda, ni kawaida kwa akina mama kuwafu-nga watoto wao hirizi mikononi na miguuni, amba-zowakati mwingine huwa zimetengenezwa kwa ma-koa na shanga, ili kuwalinda kutokana na madhara.

˘ Kifo cha mpendwa Mwandikaji MwingerezaSir Arthur Conan Doyle aliwapoteza mwana, kaka,ndugu-mkwe, na mpwa wake wakati wa Vita vyaKwanza vya Ulimwengu. Akiwa amehuzunika sana,Doyle pamoja na mke wake walienda kwenye miku-tano ya kuwasiliana na pepo wakiwa na matumai-ni ya kuzungumza na mwana wao aliyekufa. Leopia, watu wengi huwaendea watu wanaowasilianana pepo wakiwa na matumaini ya kuzungumza nawapendwa wao waliokufa. Katika nchi fulani, diniza kienyeji pamoja na zile zinazodai kuwa za Kikri-sto hufundisha kwamba kifo husababishwa na rohowaovu waliokasirika. Makanisa hayo hudai kwambalazima watu wafanye matambiko fulani ambayo

Ni Nini Huwafanya Watu Wavutiwe na

Uchawi?

4 Amkeni! Februari 2011

GAZETI HILI HUCHAPISHWA ili kuelimisha familia nzima.Huonyesha jinsi ya kukabiliana na matatizo ya wakati wetu. Huripotihabari, husimulia juu ya watu katika nchi nyingi, huchunguza dinina sayansi. Lakini si hayo tu. Huchunguza sana matukio ya sasa nahutoa maana ya kweli ya matukio hayo, hata hivyo linabaki sikuzotebila kuingilia siasa wala kutukuza jamii moja ya watu kuliko nyingine. Lamaana kuliko yote, gazeti hili hujenga uhakika katika ahadi ya Muumbaya kuleta ulimwengu mpya wenye amani na usalama ambao uko karibukuchukua mahali pa mfumo wa mambo uliopo mwovu na usiotii sheria.

Amkeni! Gazeti hili haliuzwi. Ni sehemu ya kazi ya elimu ya Biblia yaulimwenguni pote inayotegemezwa kwa michango ya hiari.Isipokuwa iwe imeonyeshwa vingine, Maandiko yamenukuliwakutoka katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

Awake! (ISSN 0005-237X) is published monthly by Watchtow-er Bible and Tract Society of New York, Inc.; M. H. Larson, Presi-dent; G. F. Simonis, Secretary-Treasurer; 25 Columbia Heights,Brooklyn, NY 11201-2483, U.S.A., and in England by Watch Tow-er Bible and Tract Society of Britain, The Ridgeway, London NW71RN (Registered in England as a Charity). Periodicals Posta-ge Paid at Brooklyn, N.Y., and at additional mailing offices.� 2011 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania.Haki zote zimehifadhiwa. Printed in Britain.

February 2011 Vol. 92, No. 2 Monthly SWAHILI

hugharimu pesa nyingi sana ili watu zaidi katika ja-mii wasife.

˘ Kuwahofu wafu Imani kuhusu kifo na wafuimewaathiri sana wanadamu. Kwa hiyo, katika nchinyingi watu hufanya matambiko ya kila aina yanayo-tia ndani kuwa na karamu mwaka mmoja baada yamtu kufa, kufagia boma lote la aliyekufa, kunyoanywele zote, na pia kujiumiza, ili wawafurahishewafu au “kuthibitisha” kwamba wanawapenda. Ja-mii fulani katika visiwa vya Pasifiki huwalazimishawajane kuvaa mavazi meusi na kuomboleza kwa

miezi mingi, wakiwa wamejifungia ndani ya nyu-mba na bila kula vyakula ambavyo mpendwa waoaliyekufa alipenda sana. Watu wanaojihusisha nadesturi hiyo wanaweza kushuka moyo au kupatamagonjwa yanayoletwa na njaa au hata kufa.

Ni wazi kwamba kuna mambo mengi yanayowa-vutiawatu kufanya uchawi. Hivyo, ni jambo la maa-na tuelewe chanzo halisi cha mafundisho kuhusuuchawi! Acheni sasa tuchunguze Biblia, kwa saba-bu ndicho kitabu pekee kinachoeleza wazi kuhusuuchawi.

BIBLIA inasema hivi kumhusu Muumbawetu: “Mungu ni nuru na hakuna giza ka-

mwe katika muungano na yeye.” (1 Yohana 1:5)Hilo ni kweli hasa kuhusu mambo ya kiroho.Kwa hiyo, je, Mungu wa kweli anaweza kuwa ndi-ye chanzo cha uchawi? Au je, kuna nguvu fulaniya uovu inayoongoza uchawi?

Baadhi ya mazoea ya kiuchawi ambayo watuhujihusisha sana nayo ni uaguzi na kuwasilianana pepo kutia ndani unajimu, ubashiri wa kutu-mia namba, usomaji wa viganja, kuwasiliana na“wafu” na vilevile ulozi. Mazoea hayo yana histo-

ria ndefu, kwani mengi kati yake yalianzia Babi-loni la kale, ambalo magofu yake yanapatikanahuko Iraki. (Isaya 47:1, 12, 13) Kutoka Babiloni,mazoea ya uchawi yalienea kote katika ulimwe-ngu wa kale na kutia mizizi katika tamaduni najamii nyingi.

Fikiria tukio lililotokea katika jiji la Filipi li-lilokuwa katika Makedonia ya kale. Kikundi ki-dogo cha wahudumu Wakristo, kilichotia ndanimtume Paulo na daktari Luka, kilikutana na msi-chana aliyekuwa na nguvu za kufanya uchawi.Ona jinsi Luka, mwandikaji wa Biblia, alivyofu-

Ni Nani Chanzo Halisi cha

Uchawi?

Lugha: Afrikaans, Albanian, Amharic, Arabic, Armenian, Bislama,Bulgarian, Cebuano, Chichewa, Chinese (cha Kitamaduni)� (limerekodi-wa katika Kimandarini pekee), Chinese (Sahili), Chitonga, Cibemba, Cro-atian, Czech,� Danish,� Dutch,�� English,�� Estonian, Ewe, Fijian,Finnish,� French,��� Georgian, German,�� Greek, Gujarati, Hebrew,Hiligaynon, Hindi, Hungarian, Icelandic, Igbo, Iloko, Indonesian, Ital-ian,�� Japanese,�� Kannada, Kinyarwanda, Kirghiz, Kirundi, Korean,��Latvian, Lingala, Lithuanian, Macedonian, Malagasy, Malayalam, Mal-tese, Myanmar, Norwegian,�� Polish,�� Portuguese,��� Punjabi, Raro-tongan, Romanian, Russian,�� Samoan, Sepedi, Serbian, Sesotho, Sho-na, Silozi, Sinhala, Slovak, Slovenian, Spanish,�� Swahili, Swedish,�Tagalog, Tamil, Thai, Tok Pisin, Tongan, Tsonga, Tswana, Turkish, Ukrai-nian, Urdu, Vietnamese, Xhosa, Yoruba, Zulu� CD zapatikana pia.� MP3 CD-ROM zapatikana pia.� Magazeti yaliyorekodiwa yanapatikana katika www.jw.org.

Je, ungependa kupokea habari zaidi au funzo la Bibliabila malipo? Tafadhali watumie Mashahidi wa Yehova maombi yakoukitumia moja ya anwani zilizo hapa chini. Unaweza kupata orodha kamiliya anwani kwenye www.watchtower.org/address. America, United Statesof: 25 Columbia Heights, Brooklyn, NY 11201-2483. Australia: PO Box 280, Ingleburn,NSW 1890. Britain: The Ridgeway, London NW7 1RN. Burundi: BP 2150, Bujumbura.Congo, Democratic Republic of: BP 634, Limete, Kinshasa. Ethiopia: POBox 5522, Addis Ababa. Kenya: PO Box 21290, Nairobi 00505. Malawi: PO Box 30749,Lilongwe 3. Nigeria: PMB 1090, Benin City 300001, Edo State. Rwanda: BP 529, Kigali.South Africa: Private Bag X2067, Krugersdorp, 1740. Tanzania: PO Box 7992, Dar esSalaam. Uganda: PO Box 4019, Kampala. Zambia: PO Box 33459, 10101 Lusaka.Zimbabwe: Private Bag WG-5001, Westgate.

Amkeni! Februari 2011 5

nua chanzo cha nguvu hizo. Aliandika hivi: “Ki-jakazi fulani mwenye roho, roho mwovu wa uaguzi,akakutana nasi. Yeye alikuwa akiwapatia mabwa-na zake faida nyingi kwa kufanya ufundi wa ku-bashiri.”—Matendo 16:16-18.

Naam, msichana huyo hakupata nguvu hizokutoka kwa Mungu wa kweli, Yehova, bali kutokakwa roho mwovu. Hiyo ndiyo sababu Paulo pa-moja na waandamani wake walikataa kumsikili-za. Huenda unajiuliza hivi: ‘Roho waovu ni nani?Nao walitoka wapi?’ Hebu ona majibu ya Biblia.

Roho Waovu Ni Nani?

Mapema kabla ya kuwaumba wanadamu, Ye-hova aliumba ‘wana wa Mungu’ wa roho hukombinguni, wenye akili na walio wengi sana. (Ayu-bu 38:4, 7) Kama wanadamu, wao pia wana uhu-ru wa kuchagua, na kwa muda mrefu walikuwawashikamanifu kwa Mungu. Lakini kwa ghafulahali hiyo ya furaha ilikatizwa. Jinsi gani?

Baada ya Mungu kuwaumba wanadamu, kiu-mbe mmoja wa roho alianza kutamani kituambacho hakikuwa chake—ibada. Kama vilemtu mwenye ustadi anavyoweza kufanya ione-kane kana kwamba sauti inatoka katika mwana-sesere, malaika huyo mwovu alitumia nyoka ku-mshawishi mwanamke wa kwanza, Hawa, asimtiiMuumba wake. (Mwanzo 3:1-6) Biblia inamta-ja malaika huyo mwasi kuwa “yule nyoka wa za-mani, yeye anayeitwa Ibilisi na Shetani.” (Ufunuo12:9) Yesu alimtaja kuwa “muuaji” ambaye “ha-kusimama imara katika kweli,” halafu akaonge-za hivi: “Anaposema uwongo, yeye husema kuli-ngana na mwelekeowake mwenyewe, kwa sababuyeye ni mwongo na ndiye baba ya uwongo.”—Yo-hana 8:44.

Baadaye, ‘wana wengine wa roho wa Munguwa kweli’ walijiunga katika uasi huo wa Sheta-ni. (Mwanzo 6:1, 2) Wanajulikana kama “walemalaika waliofanya dhambi” na wale “malaikaambao hawakubaki mahali pao pa kwanza baliwakayaacha makao yao wenyewe yanayofaa,” aumahali pao walipogawiwa huko mbinguni. (2 Pe-tro 2:4; Yuda 6) Wakaja kujulikana kama rohowaovu. (Yakobo 2:19) Zaidi ya hilo, wameazimiakuwaondoa watu wengi iwezekanavyo kutokakwenye ibada ya kweli, kama vile tu walivyowafa-nya Waisraeli katika nyakati za Biblia. (Kumbu-kumbu la Torati 32:16, 17) Vivyo hivyo leo pia,kama vile ilivyokuwa nyakati zilizopita, Shetanipamoja na roho waovu hutumia ujanja kufundi-sha uwongo wa kidini.—2 Wakorintho 11:14, 15.

Jilinde!

Hata ingawa roho waovu wana nguvu zinazo-pita zile za wanadamu, kupitia msaada wa Mu-ngu, tunaweza ‘kuchukua msimamo kuwapinga’na kuwa washindi. (1 Petro 5:9) Hata hivyo,ili kupata msaada huo, tunahitaji kujifunza yaleambayo Mungu anataka tufanye na kutenda ku-patana nayo. Akizungumza kuhusu Wakristo wa-lioishi wakati wake, mtume Paulo aliandika hivi:“Sisi . . . hatujaacha kusali kwa ajili yenu na kuo-mba kwamba mjazwe ujuzi sahihi wa mapenziyake katika hekima yote na utambuzi wa kiroho,ili mtembee kwa kumstahili Yehova kwa kusu-di la kumpendeza yeye kikamili.”—Wakolosai 1:9, 10.

Wale ambao walipata ‘ujuzi huo sahihi’ walitiandani watu kadhaa kutoka jiji la Efeso ambaowa-lifanya uchawi. Ona jinsi ujuzi kuhusu kweli uli-vyowasaidia. Biblia inasema hivi: “Hesabu kubwa

6 Amkeni! Februari 2011

ya wale waliozoea kufanya ufundi wa uchawi wa-kaleta pamoja vitabu vyao wakaviteketeza mbeleya kila mtu.” Vitabu hivyo vilikuwa na thamaniya “vipande 50,000 vya fedha,” na hizo zilikuwapesa nyingi sana! (Matendo 19:17-19) Mfano huowa ujasiri ulirekodiwa kwa faida yetu.—2 Timo-theo 3:16.

Kanuni Zitakazokulinda

Kuna mambo mengine tunayoweza kufanyaambayo yatatulinda kutokana na roho waovu.Hebu chunguza kanuni za Biblia zifuatazo.

“Msiamini kila neno lililoongozwa na roho, la-kini yajaribuni maneno yaliyoongozwa na roho ilikuona kama yanatokana na Mungu.” (1 Yoha-na 4:1) Huenda mambo fulani yanayosemwa nawanajimu, watu wanaosoma akili za watu, watuwanaowasiliana na pepo, na wachawi yakawa yakweli. Kwa mfano, yule msichana kutoka Filipialiyekuwa na roho mwovu, alisema ukweli alipo-sema hivi kumhusu Paulo na waandamani wake:“Watu hawa ni watumwa wa Mungu Aliye JuuZaidi, wanaowatangazia ninyi njia ya wokovu.”(Matendo 16:17) Hata hivyo, Paulo na waanda-mani wake hawakukubali awafuate. Badala yake,Paulo aliamuru roho huyo mwovu atoke ndaniyake. Chunguza mambo ambayo dini zinasemana uyalinganishe na yale ambayo Biblia inasema.—Matendo 17:11.

“Basi, jitiisheni kwa Mungu; lakini mpingeni Ibi-lisi, naye atawakimbia ninyi.” (Yakobo 4:7) Rohowaovu ni adui wa Mungu na wako pia. Usijari-bu hata kidogo kuwa mdadisi kuhusu mamboyao yaliyofichika. Badala yake, jitiishe kwa Mu-ngu kwa kutii amri zake zenye upendo, ambazosi zenye kulemea. (1 Yohana 5:3) Kwa mfano,Mungu aliliambia hivi taifa la kale la Israeli: “Asi-patikane ndani yako yeyote . . . anayefanya uagu-zi, mwenye kufanya uchawi au yeyote anayetafutaishara za bahati au mlozi, au anayefunga wengi-ne kwa kuwatakia maovu au yeyote anayetafutashauri kwa mwenye kuwasiliana na pepo au mju-zi wa kubashiri matukio au yeyote anayeuliza ha-bari kutoka kwa wafu. Kwa maana kila mtu ana-yefanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova.”(Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Maoni ya Mu-ngu hayajabadilika.—Wagalatia 5:19, 20.

“Hakuna apizo lolote la bahati mbaya juu ya[watumishi wa Yehova].” (Hesabu 23:23) Walewote ambao wanataka kumpendeza Mungu ha-wapaswi kuwaogopa roho waovu. Kwa kweli,roho haowaovu hata “hutetemeka” mbele za Mu-ngu, kwa sababu wanajua kwamba yeye ana ngu-vu nyingi, ambazo atatumia kuwaharibu. (Yako-bo 2:19) Mungu ataonyesha “nguvu zake kwa ajiliya wale ambao moyowao ni mkamilifu kumwele-kea yeye,” na ‘hatamwacha mwadilifu atikisike ka-mwe.’—2 Mambo ya Nyakati 16:9; Zaburi 55:22.

“Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakiniwafu, hawajui lolote kamwe.” (Mhubiri 9:5) Nenola Mungu linafundisha kwamba mtu akifa, ame-kufa! Hatupaswi kuwaogopa, kwa sababu hawa-wezi kumdhuru mtu yeyote. (Isaya 26:14) Ili wa-wadanganye watu, wakati mwingine roho waovuhujifanya kuwa roho za wafu, na hilo linawezakueleza kwa nini “roho” anayewatokea ni tofautikabisa na mtu halisi walimjua.

“Hamwezi kuwa mkishiriki ‘meza ya Yehova’na meza ya roho waovu.” (1 Wakorintho 10:21,22) Wale wote wanaompenda Yehova kikwe-li wataepuka kabisa vitabu, sinema, na miche-zo ya kompyuta iliyo na mamboya uchawi au ina-yochochea mazoea na imani zinazohusiana nauchawi.� Zaburi 101:3 inasema: “Sitaweka mbeleya macho yangu kitu chochote kisichofaa.” Zai-di ya hilo, mara nyingi burudani zinazohusishauchawi hutukuza jeuri na mwenendo mpotovu,ambao ‘wale wanaompenda Yehova’ wanapaswakukataa kabisa.—Zaburi 97:10.

Roho waovu wamejitahidi sana kuficha utuwao kutoka kwa wanadamu. Lakini hawajafau-lu kabisa kufanya hivyo. Kupitia Biblia, Yehovaamefunua kabisa jinsi walivyo—waongo wabayasana na adui hatari wa wanadamu. Wao ni tofau-ti sana na Muumba wetu, Yehova Mungu! Kamavile habari ifuatayo inavyoonyesha, yeye anatupe-nda, sikuzote yeye hutueleza ukweli, na anatakatuishi milele kwa furaha.—Yohana 3:16; 17:17.� Dhamiri za watu hutofautiana, ikitegemea malezi ya kidini na

pia ukomavu wa kiroho. Jambo kuu ni kwamba kila mtu anapa-swa kudumisha dhamiri safi mbele za Mungu na asisumbue dha-miri za watu wengine kutia ndani watu wa familia. Waroma 14:10, 12 linasema kwamba “sisi sote tutasimama mbele ya kiti chahukumu cha Mungu.”

Amkeni! Februari 2011 7

TOFAUTI na roho waovu, Yehova Mungu nimwenye hekima yote na nguvu zote. Pia,

yeye ndiye mfano bora zaidi wa upendo. (1 Yoha-na 4:8) Shauri lake ni zuri wakati wote, naye hu-tushauri bila malipo, kwa sababu anatujali sana.Mashauri yake ni tofauti kama nini na yale ya wa-bashiri nawatu wanaosoma akili zawatu! Munguanasema: “Haya, ninyi nyote mlio na kiu [ya kiro-ho]! Njooni kwenye maji. Na wale wasio na pesa!Njooni, mnunue mle. Ndiyo, njooni, mnunue di-vai na maziwa bila pesa na bila bei. Kwa ninimnaendelea kulipa pesa kwa ajili ya kitu amba-cho si mkate, na kwa nini kazi yenu ni kwa ajiliya kitu ambacho hakishibishi? Nisikilizeni kwamakini, na mle yaliyo mema, na nafsi yenu ipatefuraha tele katika unono.”—Isaya 55:1, 2.

Kwa sababu Biblia iliandikwa chini ya mwo-ngozo wa Muumba wetu mwenye upendo, inatu-patia tumaini, ulinzi wa kiroho, kusudi maishani,na kanuni bora zaidi za kutuongoza. Hebu chu-nguza maswali yafuatayo pamoja na maandikoya Biblia yaliyoonyeshwa.

Chanzocha Kweli cha

Mwongozona Tumaini

˘ Ninaweza kupata amani ya kweli ya mo-yoni kwa njia gani? Biblia inasema hivi:“Yehova, Mkombozi wako, Mtakatifu waIsraeli, amesema hivi: ‘Mimi, Yehova, niMungu wako, Yeye anayekufundisha ili uji-faidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uendekatika njia unayopaswa kutembea ndaniyake. Laiti ungesikiliza amri zangu! Ndipoamani yako ingekuwa kama mto, na uadi-lifu wako kama mawimbi ya bahari.’”—Isa-ya 48:17, 18.

˘ Je, uovu utaendelea milele? “Wanyoofundio watakaokaa duniani, na wasio na la-wama ndio watakaobaki ndani yake. Naowaovu, watakatiliwa mbali kutoka dunia-ni; nao wenye hila, watang’olewa kutokandani yake.” (Methali 2:21, 22) Ndiyo, wa-nadamu waovu, pamoja na malaika wao-vu, wataharibiwa milele, kana kwambakwa moto.—Ufunuo 20:10, 14.

˘ Je, magonjwa na kuteseka kutaisha?“Tazama! Hema la Mungu liko pamoja nawanadamu, naye atakaa pamoja nao, naowatakuwa watu wake. Na Mungu mwenye-we atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kilachozi kutoka katika macho yao, na kifo ha-kitakuwapo tena, wala maombolezo walakilio wala maumivu hayatakuwapo tena.Mambo ya zamani [matatizo mengi yasasa] yamepitilia mbali.”—Ufunuo 21:3, 4.

Tofauti na roho waovu, Mungu hasemiuwongo kamwe. Kwa kweli ‘hawezi kuse-ma uwongo.’ (Tito 1:2) Zaidi ya hilo, kamavile habari ya mwisho katika mfululizo huuitakavyoonyesha, kweli yake huwawekawatu huru na kuwapa uhai.—Yohana 8:32;17:3.

˘ Susanna alikuwa kuhani wa kike katika dini moja huko Brazili. Alitakakutumia nguvu zake zisizo za kawaida kuwasaidia watu wenye uhitaji. Pia,alifurahia sana “kuzungumza na mama yake aliyekuwa amekufa.” Hata hi-vyo, baada ya muda, “mama” yake alimsihi sana ajiue ili waishi pamoja ka-tika ulimwengu wa roho. Jambo hilo lilimsumbua sana Susanna na hataaliota ndoto mbaya. Kisha Susanna na mume wake wakaanza kujifunza Bib-lia na Mashahidi wa Yehova. Walijitahidi sana ‘kumpinga Ibilisi,’ na mwisho-we ‘aliwakimbia.’ (Yakobo 4:7) Sasa wanaishi kwa amani, na Susanna haotindoto mbaya. Alisema, “Nina sababu nyingi sana za kumshukuru Yehova, la-kini ninashukuru hata zaidi kwamba alitutoa kwenye giza la kiroho.”

˘ Timothy, anayeishi Afrika Magharibi,ni kiziwi na bubu.� Kwa sababu mada-ktari wa kawaida hawakuweza kumsai-dia, aliwaendea waponyaji wa kimuuji-za, lakini wao pia walishindwa.Aliandika, “Nilivunjika moyo sana kuto-kana na uwongo nilioambiwa.” Baada-ye Timothy alianza kujifunza Biblia pa-moja na Mashahidi wa Yehova, ambaowalimweleza kusudi la Mungu la kuo-ndoa magonjwa na ulemavu wote. Ti-mothy anasema, “Ninasubiri kwa hamusiku ambayo katika ulimwengu mpyawa Mungu ‘masikio ya viziwi yatazibuli-wa . . . na ulimi wa bubu utapaaza sautikwa furaha.’ ” (Isaya 35:1-6) Kwa sasa,yeye hufurahia kutumia mashini ndogoya DVD kuwahubiria kweli za Bibliawatu wengine walio na matatizo ya ku-sikia, na kuwasaidia kupata uhuru wakweli.

� Baadhi ya majina yamebadilishwa.

Picha hizi zimeigizwa

YESU KRISTO aliwaambia hivi watu waliokuwawakimsikiliza: “Mtaijua kweli, nayo kweli itawa-

weka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Kama vile mifa-no ifuatayo inavyoonyesha, uhuru huo unatia ndanikuwa huru kutokana na roho waovu, ambao ndio wa-nasema uwongo na kuwadanganya watu wakitumiauchawi.—Yohana 8:44.

Kila moja ya masimulizi haya inaonyesha jinsi kwe-li ya Biblia ina nguvu za kuweka watu huru. Naam,hiyo pekee ndiyo inayowawekawatu huru. Mbona usi-jichunguzie Biblia uone. Hutakatishwa tamaa.

Kweli ya BibliaIliwaweka Huru

˘ Evelyn anayeishi nchini Estonia,alikuwa amejiingiza sana katika uchawi.Kwa sababu Yesu aliwaponya watu, yeye piaalitaka kufanya hivyo. Alitaka hasa kumsai-dia mama yake aliyekuwa na ugonjwa wakudumu. Hivyo, ili atambue na kutibu mago-njwa mabaya alijifunza kutumia pinduli.Baada ya muda, alianza kuchunguza Biblia.Matokeo? Alisema, “Nilitambua kwamba ni-likuwa nimedanganywa sana. Kwa hiyo, nili-teketeza vitabu na pinduli zangu za uchawi.”Sasa anafundisha kweli za Biblia zinazowa-weka watu huru.

˘ Mary alilelewa katika mojawapo ya visi-wa vya Papua New Guinea ambako watuwanawahofu sana wafu. Iwapo mtu angeku-fa katika kijiji chake, Mary angelala chini yakitanda cha mtu mwingine, kwani alihofukuwa roho ya huyo mfu ingemsumbua aki-wa peke yake. Kisha akajifunza kutoka kati-ka Biblia kwamba wafu wamelala—kwambawako kaburini wakisubiri kufufuliwa waishikatika Paradiso duniani. (Luka 23:43; Yoha-na 11:11-14) Tangu wakati huo, Mary haho-fu wafu tena.

˘ Alicia, aliyelelewa na wazazi ambao niMashahidi wa Yehova huko Marekani,alianza kusoma vitabu na kutazama sine-ma za kichawi. Kisha akaanza kufikirikwa uzito kuhusu kweli za Biblia alizoku-wa amejifunza. Alipotambua kwamba ali-kuwa akijaribu ‘kushiriki meza ya Yehovana meza ya roho waovu,’ alibadili njiazake na sasa anafurahia kuwa na dha-miri safi mbele za Mungu.—1 Wakorintho10:21.

9

10 Amkeni! Februari 2011

JE, WEWE hupatwa na hali kama hiyo kilaJumatatu asubuhi shuleni? Huenda ukahi-

si kwamba vijana wengine wanajifurahisha njeya nyumba lakini wazazi wako wanakuzuiausitoke nje—au ni kana kwamba uko katikabustani yenye vifaa vingi vya kuchezea lakinihuruhusiwi kuvitumia. Si eti unataka kufanyakila kitu ambacho vijana wenzako wanafanya.Ungependa tu kujifurahisha mara kwa mara!Kwa mfano, ni burudani gani ambayo weweungependa kujihusisha nayo mwisho-jumahuu?

M kucheza dansi

M kwenda tamasha ya muziki

M kutazama sinema

M kwenda karamu

M jambo lingine ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝

Unahitaji tafrija. (Mhubiri 3:1, 4) Kwa kwe-li, Muumba wako anataka ufurahie ujanawako. (Mhubiri 11:9) Na wazazi wako pia wa-nataka ujifurahishe, ingawa huenda usiaminihilo nyakati nyingine. Hata hivyo, huenda wa-zazi wako wakataka kujua mambo haya mawi-li: (1) utajihusisha na tafrija gani na (2) utaa-ndamana na nani.

Lakini namna gani ikiwa rafiki zako wana-kukaribisha kwenye tafrija lakini hujui wa-zazi wako watasema nini? Unapokabiliwana uamuzi, Biblia inakutia moyo ufikirie fai-da na hasara ya uamuzi wako, na uchanganue

VIJANAHUULIZA

Mbona wazazi wanguhawaniachi nijifurahishe?

Allison,� kijana nchini Australia, huona kila Jumatatu (Sikuya 1) asubuhi shuleni kuwa wakati wenye kuchosha sana.

“Kila mtu huzungumzia mambo aliyofanya mwisho-juma,”anasema. “Wao hueleza mambo yenye kusisimua kama vilekaramu walizohudhuria na waliwabusu wavulana wangapi—hata jinsi walivyokimbia polisi wasiwashike . . . Mambohayo husikika kuwa yenye kuogopesha, lakini yenye kufura-hisha sana! Wao hurudi nyumbani saa 11 asubuhi, na wazaziwao hawajali. Lakini mimi lazima niwe nimelala hata kablawao hawajaanza kujifurahisha!

“Hata hivyo, baada ya kuniambia mambo waliyofanyamwisho-juma, wanafunzi wenzangu huanza kuniuliza nilifa-nya nini. Kwa kweli nilifanya nini? Nilienda kwenye mikutanoya Kikristo. Kisha nikashiriki katika utumishi. Ninahisi ni kanakwamba nilikosa mambo mengi yenye kufurahisha. Kwahiyo, mimi huwaambia kwamba sikufanya lolote. Kisha wana-niuliza kwa nini sikuambatana nao.

“Jumatatu inapokwisha unafikiri kwamba mambo yata-tulia. Lakini wapi! Kufikia Jumanne (Siku ya 2) kila mtu ana-zungumza kuhusu mwisho-juma unaokuja! Mimi huketi tu nakuwasikiliza wakizungumza. Ninahisi ni kana kwamba nime-tengwa!”

� Jina limebadilishwa.

Amkeni! Februari 2011 11

matokeo. (Kumbukumbu la Torati 32:29; Me-thali 7:6-23) Ni uamuzi gani utakaofanya una-poalikwa kuandamana pamoja na rafiki zako?UAMUZI A: USIOMBE RUHUSA—NENDA TU.

Sababu ya kufanya uamuzi huu: Unata-ka kuwaonyesha rafiki zako kwamba unajite-gemea. Unahisi kwamba unajua mengi kulikowazazi wako, au huoni kwamba wanajua kina-chofaa.—Methali 15:5.

Matokeo: Rafiki zako watajua jambo fulanikukuhusu—kwamba unaweza kudanganya. Iki-wa unaweza kuwadanganya wazazi wako, basipia unaweza kuwadanganya rafiki zako. Waza-zi wako wakigundua, watahuzunika na kuhisikwamba umewasaliti, na huenda ukanyimwauhuru zaidi! Kukosa kuwatii wazazi wako nakuondoka tu ni uamuzi wa kipumbavu.—Me-thali 12:15.UAMUZI B: USIOMBE RUHUSA—USIENDE.

Sababu ya kufanya uamuzi huu: Unafikiriakuhusu tafrija yenyewe na kuona kwamba hai-patani na viwango vyako au kwamba baadhiya wale waliokaribishwa si mashirika mazuri.(1 Wakorintho 15:33; Wafilipi 4:8) Kwa upa-nde mwingine, ungependa kwenda lakini hunaujasiri wa kuwaomba wazazi wako ruhusa.

Matokeo: Usipoenda kwa sababu unaonahaifai kwenda, utakuwa na uhakika zaidi una-powajibu rafiki zako. Lakini usipoenda kwasababu tu huna ujasiri wa kuwaomba wazaziwako ruhusa, utashinda nyumbani ukiwa ume-nuna na ukihisi kwamba ni wewe tu ambayehujifurahishi.

UAMUZI C: OMBA RUHUSA—KISHA SUBIRI JIBU.

Sababu ya kufanya uamuzi huu: Unata-mbua kwamba wazazi wako wana mamlakajuu yako na unaheshimu uamuzi wao. (Wako-losai 3:20) Unawapenda wazazi wako na hu-ngependa kuwaumiza kwa kuwadanganya nakwenda tafrija bila kuwajulisha. (Methali 10:1)Pia una nafasi ya kueleza maoni yako.

Matokeo: Wazazi wako wanahisi kwambaunawapenda na kuwaheshimu. Na wanapoo-

na kwamba ombi lako linafaa wanaweza kuku-bali.

Sababu Inayoweza KuwafanyaWazazi Wakatae

Namna gani wazazi wako wakikataa? Hilolinaweza kuvunja moyo sana. Hata hivyo, kue-lewa maoni yao kunaweza kukusaidia kukabi-liana na vizuizi vyao. Kwa mfano, wanawezakukataa kwa sababu ya mambo yafuatayo.

Wana ujuzi na uzoefu mwingi zaidi. Kunauwezekano mkubwa kwamba ungependa kuo-gelea mahali palipo na waokoaji-uhai. Kwanini? Kwa sababu unapokuwa ndani ya majiukiogelea, huwezi kutambua hatari vizuri. La-kini waokoaji-uhai wako katika hali nzuri zaidiya kutambua hatari.

Vivyo hivyo, kwa kuwa wazazi wako wanaujuzi na uzoefu zaidi, wanaweza kutambuahatari ambazo wewe huoni. Kama tu waokoa-ji-uhai, kusudi la wazazi wako si kukuzuia uji-furahishe bali wanataka kukusaidia uepuke ha-tari zinazoweza kukuzuia ufurahie maisha.

Wanakupenda. Wazazi wako wanatakasana kukulinda. Kwa kuwa wanakupenda waohukubaliana na wewe wanapoweza kufanya hi-vyo lakini wanakuzuia mambo fulani wanapo-lazimika kufanya hivyo. Unapowaomba ruhu-sa kufanya jambo fulani, wao hujiuliza ikiwawanaweza kukupa ruhusa na bado wakabi-liane na matokeo ya uamuzi wao. Watasema

“Wazazi wangu wana-niamini hasa kwa sababunina rekodi nzuri ya kutendakwa hekima. Mimi huzungu-mza nao waziwazi kuhusurafiki zangu. Pia siogopikuondoka kwenye karamuiwapo sipendezwi na ma-mbo yanayotendeka.

” Kimberly

12 Amkeni! Februari 2011

ndiyo iwapo tu watakuwa na uhakika kwambahakuna jambo baya litakalokupata.

Wasipokuwa na habari ya kutosha. Wa-zazi wenye upendo hutenda kwa tahadhari.Ikiwa hawaelewi jambo unalowaomba, au wa-kihisi kwamba kuna mambo fulani ambayo hu-waelezi, kuna uwezekano mkubwa kwambawatasema la.

Jinsi ya Kuwafanya Wazazi WakoWaseme Ndiyo

Mambo manne yanahusika.Unyoofu: Kwanza kabisa, unahitaji kujiuli-

za hivi kwa unyoofu: ‘Ni sababu gani hasa ina-yonifanya nitake kwenda? Je, ni tafrija yenye-we, au ni kwamba tu ninataka kuhisi kwambaninapendwa na rafiki zangu? Je, ni kwa saba-bu mtu fulani ninayevutiwa naye atakuwepo?’Kisha waambie wazazi wako ukweli. Wakatifulani hata wao walikuwa vijana, na wana-kufahamu vizuri. Kwa hiyo, kuna uwezekanomkubwa kwamba watatambua nia yako. Wa-tathamini sana kwamba umewaambia ukweli,nawe utafaidika kutokana na hekima yao. (Me-thali 7:1, 2) Kwa upande mwingine, ikiwa hu-tawaambia ukweli, kuna uwezekano mkubwakwamba utaacha kuaminika na huenda wasi-kuruhusu uende.

Wakati unaofaa: Usiwaulize wazazi wakomaswali mengi baada tu ya wao kufika nyu-mbani kutoka kazini au wanapokazia fiki-ra mambo mengine. Zungumza nao wanapo-

kuwa wametulia. Lakini usisubiri hadi dakikaya mwisho kisha uanze kuwalazimisha waku-pe jibu. Wazazi wako hawatafurahi wakilazimi-shwa kutoa jibu haraka. Omba ruhusa mape-ma, na wazazi wako watathamini jambo hilo.

Kuwaridhisha: Usizungumzie mambo ki-juujuu tu. Eleza kihususa jambo unalotaka ku-fanya. Wazazi huwa na wasiwasi wanapoambi-wa “Sijui,” hasa ikiwa wameuliza: “Ni naniatakayekuwepo?” “Je, kutakuwa na mtu mzi-ma wa kusimamia mambo?” au “Tafrija hiyoitakwisha saa ngapi?”

Mtazamo: Usiwaone wazazi wako kuwamaadui. Waone kuwa wako upande wako—nakwa kweli wao wako upande wako. Ukiwana mtazamo huo, hutazungumza kana kwa-mba unazozana, nao watakuwa tayari kushi-rikiana nawe. Wakikataa, waulize sababu yaokwa heshima. Kwa mfano, wakisema hue-ndi kwenye tamasha fulani, jaribu kutambuakinachowafanya wawe na wasiwasi. Je, wanawasiwasi kumhusu mwimbaji? kuhusu maha-li tamasha yenyewe itafanyiwa? watu watakao-kuwepo? au pesa za kiingilio? Epuka kuse-ma mambo kama “Mbona hamniamini,” “Kilamtu anaenda,” au “Wazazi wa rafiki zanguwamewaruhusu waende!” Waonyeshe wazaziwako kwamba umekomaa kiasi cha kutoshakukubali uamuzi wao na kuuheshimu. Uki-fanya hivyo watakuheshimu. Na wakati ujao,huenda wakafikiria kukupa ruhusa.

MBONA USIWAULIZE WAZAZI WAKO?

Je, ungependa kujua maoni ya wazaziwako kuhusu mambo yaliyozungumziwakatika habari hii? Njia pekee unayowezakujua maoni yao ni kwa kuwauliza! Waka-ti unaofaa, zungumza nao kuhusu wasi-wasi wanaopata unapotaka kujifurahisha.Fikiria swali ambalo ungependa kuwauli-za, kisha uliandike hapa chini.

˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝

˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝

˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝

Kama tu waokoaji-uhai,wazazi wako wanawezakutambua vizuri hatarina kukuonya

Amkeni! Februari 2011 13

MSICHANA mdogo anacheza kwa kurukakamba. Kisha anajikwaa na kuanguka.

Muda mfupi baadaye anasimama, akiwa ameaibi-ka kidogo tu. Lakini mwanamke mzee anajikwaana kuanguka ndani ya nyumba na kuvunjika mfu-pa wa nyonga. Anafanyiwa upasuaji na kufanyamazoezi ya viungo kwa miezi mingi baada yahapo. Sasa kwa kuwa anaogopa sana kuanguka,anaepuka kufanya jambo lolote linalohusisha ku-tumia nguvu na hivyo anakuwa dhaifu.

Katika nchi moja, kila mwaka zaidi ya asili-mia 33 ya watu walio na umri wa miaka 65 auzaidi huanguka. Isitoshe, vifo vingi zaidi vya watuwalio na umri huo vinavyotokea kwa sababu yakujeruhiwa vinasababishwa na kuanguka. Hiyondiyo sababu Biblia husema hivi kuwahusu wa-zee: “Wameogopa chochote kilicho juu, na kunavitisho njiani.”—Mhubiri 12:5.

Hata ingawa mara nyingi uzee huja na matati-zo ya kimwili, unaweza kuchukua hatua zinazofaakuboresha usalama na maisha yako. Jambo mojaunaloweza kufanya ni kujitahidi kudumisha afyanzuri na nguvu kwa kadiri fulani. Jambo lingine nikufanya nyumba yako iwe salama.

Dumisha Afya na Nguvu Zako

Kadiri tunavyozeeka huenda viungo vikakosakufanya kazi kwa upatano na tukawa na matatizoya kuona na usawaziko. Huenda pia tukawa dhai-fu kwani misuli na mifupa yetu huanza kudhoo-

fika. Hata hivyo, kufanya mazoezi kwa ukawai-da na kula vizuri kunaweza kupunguza madharahayo. “Ni muhimu kufanya mazoezi yanayomsai-dia mtu asianguke-anguke, asimame wima, kuo-ngeza nguvu, na viungo viweze kunyumbulika,”anasema Nita, daktari wa kunyoosha viungo.

Jarida fulani la Wizara ya Afya na Hudumaza Jamii ya Marekani linasema hivi: “Hata wazeewawe na afya au uwezo gani wa kimwili, wanawe-za kufaidika sana kwa kuendelea kuwa watendajikimwili. Hata ikiwa unapata ugumu wa kusimamaau kutembea, bado unaweza kufanya mazoezi naufaidike. Kwa kweli, katika visa vingi, utaumia zai-di usipofanya chochote.”� Zaidi ya yote, mazoeziyanaweza kukusaidia kukabiliana na ugonjwa wamoyo, maumivu ya viungo, ugonjwa wa mifupa,na kushuka moyo. Yanaweza kuboresha mfumowakowa damu, umeng’enyaji, na usingizi, na yata-kusaidia uwe na ujasiri na uwe na akili iliyo cho-njo.

Ikiwa hujazoea kufanya mazoezi, huenda ika-faa kumwona daktari kwanza. Pia zungumza nayeunapohisi kwamba umekuwa dhaifu au unapo-shikwa na uchungu kifuani wakati wa mazoe-zi. Kwa kweli, chini ya hali hizo, huenda ika-faa kupiga simu ya dharura. Usipuuze dalili kamahizo zinazoweza kuwa hatari! Na inapendekezwa� Gazeti la Amkeni! la Mei 22, 2005 (22/5/2005) lilizungumzia

kwa undani manufaa ya kufanya mazoezi kwa ukawaida.

MAPENDEKEZOYA KUWALINDAWazee

14 Amkeni! Februari 2011

kwamba upimwe macho yako na daktari wa ma-cho mara moja kwa mwaka.

Epuka vyakula ambavyo havina vitamini namadini mengine, hata ikiwa ni rahisi kuvitayari-sha. Wazee wanahitaji hasa vyakula vyenye vita-mini D nyingi na kalisi, kwa kuwa madini hayoyanaweza kusaidia kuongeza uzito wa mifupa nakuifanya isidhoofike upesi. Kwa hiyo, jaribu kulamilo yenye nafaka, matunda, mboga, na bidhaazilizotoka kwa ng’ombe lakini zisizokuwa na ma-futa mengi. Lakini, mwulize daktari kabla ya kufa-nya mabadiliko makubwa ya tabia zako za kula.Anaweza kupendekeza vyakula vinavyofaa na vi-le unavyopaswa kuepuka kwa sababu fulani zaafya.

Zaidi ya hilo jaribu kunywa maji ya kutosha. Nikawaida sana kwa watu wazee kupungukiwa namaji mwilini, hasa wale wanaoishi peke yao katikamakao ya kuwatunzia wazee, na hilo linaweza ku-mfanya mtu aanguke kwa urahisi, achanganyiki-we, afunge choo, ngozi inyauke, apatwe na maa-mbukizo kwa urahisi, na hata kufa.

Boresha Usalama wa Nyumba Yako

Watu wengi huanguka nyumbani. Hata hivyo,kwa kuchukua tahadhari fulani zinazofaa, unawe-za kupunguza sana uwezekano huo. Fikiria kuhu-su nyumba yako unaposoma mambo yafuatayo.Bafu:�������������������������������������������������������������������

˘ Sakafu haipaswi kumfanya mtu ateleze ina-pokuwa na maji.

˘ Kunapaswa kuwa na mkekawa kuzuia utele-zi, na ikiwa una kiti cha kutumiawakati wa kuoga,hakipaswi kukuzuia ufikie mabomba ya maji. Piaikiwa unatumia kifaa cha kunyunyizia maji hue-nda ikafaa uwe umekishika mkononi ili uwe ume-keti muda wote unapooga.

˘ Ni vizuri kuwa na chuma au ubao wa ukuta-ni wa kujishikilia unapoingia au kutoka bafuni auunapotumia choo. Vifaa hivyovinapaswa kuwa vi-meunganishwa kwa njia imara ukutani. Pia, haki-kisha kwamba kiti cha chooni kiko juu kiasi chakutosha ili uweze kuketi na kuinuka bila jitihadakubwa sana.

˘ Acha taa fulani za usiku zikiwa zimewaka auutumie tochi.

Ngazi za Nyumba:�������������������������������������������������������������������˘ Ngazi hazipaswi kuwa na vitu vilivyotapa-

kaa, zinapaswa kuwa katika hali nzuri, na ziwe namwangaza wa kutosha.

˘ Ngazi zinapaswa kuwa na mahali imara pakujishikilia pande zote mbili, vikanyagio visivyona utelezi, na vibonyezo vya kuwasha taa chini najuu ya ngazi.

˘ Kupanda na kushuka ngazi kunaweza kuwa-saidia wazee kuimarisha miguu yao. Hata hivyo,iwapo una matatizo na usawaziko, unapaswa kue-puka kutumia ngazi ukiwa peke yako.Chumba cha Kulala:�������������������������������������������������������������������

˘ Hakikisha kuna nafasi ya kutosha ya kuwezakutembea kuzunguka kitanda na vitu vingine bilatatizo.

˘ Uwe na kiti unachoweza kukalia unapovaa.˘ Hakikisha una taa au tochi karibu unapolala.

Jikoni:�������������������������������������������������������������������˘ Kaunta hazipaswi kuwa na vitu vingi ili uwe-

ze kuweka mboga na vitu vingine kwa urahisi.˘ Sakafu ya jikoni haipaswi kuwa na utelezi

wala kurudisha mwangaza.˘ Vitu vilivyo ndani ya makabati havipaswi

kuwa juu sana au chini sana, bali vinapaswa kuwamahali rahisi kufikiwa bila msaada. Jaribu kuepu-ka kupanda ngazi ili kufikia vitu vilivyo juu na usi-wahi kupanda juu ya kiti!Mambo Mengine:�������������������������������������������������������������������

˘ Hakikisha kuna taa usiku unapoelekea kwe-nye bafu na maeneo mengine unayoweza kutumiausiku.

˘ Huenda ikafaa kutumia mkongojo usiku wa-kati ambapo bado una usingizi au akili haijawachonjo kabisa.

˘ Viti vinapaswa kuwa imara (bila magurudu-mu), viwe na mahali pa kuwekelea mikono, na vi-napaswa kuwa juu kiasi cha kutosha ili uketi nakusimama bila matatizo.

˘ Ili kuzuia usiteguke, unapaswa kurekebisha,kubadilisha, au kuondoa zulia zilizochakaa, zulia zaplastiki zilizoinuka, au vigae vilivyovunjika. Pitishanyaya zote za umeme kwenye ukuta na si njiani.

˘ Mikeka inaweza kumtega mtu na hivyo ina-paswa kuondolewa mahali palipo na zulia. Iki-wa imewekwa kwenye sakafu inayoweza kutelezakama ile ya vigae au mbao, inapaswa kuungani-shwa kwenye kitu kisichoiruhusu iteleze.

˘ Epuka kuvalia sapatu dhaifu au zilizochakaaau zisizo na sehemu ya kushikilia mguu kwa nyu-ma au zinazoweza kuteleza. Usivalie sapatu auviatu vilivyo na visigino vilivyoinuka.

˘ Dawa fulani zinaweza kuwafanya watu waji-hisi kana kwamba wanataka kuzimia au dhaifu.Ukihisi hivyo baada ya kutumia dawa, hakikishakwamba unamweleza daktari. Anaweza kubadi-li kiasi cha dawa unachotumia au hata dawa ye-nyewe.

Ukitambua chochote kinachohitaji kushughuli-kiwa ambacho wewe mwenyewe huwezi kufanyakwa njia iliyo salama, mbona usiombe msaada wawatu wa familia, marafiki, au wale wanaoshughu-likia udumishaji wa jengo lako? Usiahirishe kuli-shughulikia.

Mambo Ambayo WengineWanaweza Kufanya

Ikiwa una wazazi, babu, nyanya, au marafikiwenye umri mkubwa, unaweza kufanya nini ili ku-wasaidia waepuke kuanguka na kuumia? Zungu-mza pamoja nao kwa busara mambo yaliyooro-dheshwa hapo juu na uwasaidie kufanya mipangoya kurekebisha sehemu zinazoweza kuwaletea ma-tatizo. Ikitegemea uhitaji, huenda ukawatayarishiachakula mara moja au mbili kila juma. Pia, wa-zee wanahitaji kufanya mazoezi kwa ukawaida.Je, unaweza kwenda matembezi na kufanya ma-mbo mengine pamoja nao? Wazee wengi watafu-rahi kutoka nje ya nyumba ikiwa wanaandamanana mtu wanayemwamini. Katika nchi fulani, seri-kali hutoa huduma fulani kwa ajili ya wazee kamavile kuwatunzia nyumbani, kuwafanyisha mazoe-zi, na kuhakikisha nyumba zao ni salama. Dakta-ri anaweza kukueleza ikiwa unaweza kufaidika ku-tokana na huduma hizo.

Muumba wetu, ambaye pia anaitwa “Mzee waSiku,” anataka tuwaheshimu wazee, hasa wazaziwalio na umri mkubwa. (Danieli 7:9) Anaamuruhivi: “Mheshimu baba yako na mama yako.” (Ku-toka 20:12) Pia anasema hivi: ‘Unapaswa kusima-

ma mbele ya mtu mwenye mvi, nawe umwonye-she ufikirio mtu mzee, nawe umwogope Munguwako.” (Mambo ya Walawi 19:32) Naam, kuwahe-shimu wazee kunaonyesha kwamba unamwogopaMungu! Wakati uleule, wazee wanaposhukuru ki-kweli kwa msaada wanaopewa, wanawachocheawatu kuwapenda na kuwaonyesha ufikirio kwaheshima. Kuwasaidia wazee kama hao si wajibutu. Ni jambo lenye kufurahisha!

Katika nchi fulani, wazee wanawezakubonyeza kifaa fulani kidogo cha elektro-niki wakati wa dharura ili kuomba msaada,kwa mfano wanapoanguka vibaya. Vifaa hi-vyo vinaweza kuvaliwa shingoni kama mku-fu au vinaweza kufungwa mkononi. Ikiwahuduma hiyo inapatikana katika eneo lenu,huenda ukafikiria kuitumia—hasa ikiwaunaishi peke yako.

KIFAA CHA KUOMBA MSAADAWAKATI WA DHARURA

16 Amkeni! Februari 2011

MAGOFU ya majumba na makaburi ya wafal-me yanatuonyesha kijuujuu tu utukufu, ngu-

vu, na utajiri wa milki ya kale ya Muungano waUmedi na Uajemi. Kabla ya falme hizo mbili kuu-ngana, Umedi ndiyo iliyokuwa ufalme wenye ngu-vu zaidi. Lakini katika mwaka wa 550 K.W.K.,Wamedi walianza kutawaliwa na Mfalme Kore-shi wa Pili, ambaye baadaye alitawala Muunganowa Umedi na Uajemi. Milki hiyo ambayo kitovuchake kilikuwa katika eneo la kaskazini ya Ghubaya Uajemi baadaye ilienea kutoka Bahari ya Aegeahadi Misri na kufikia kaskazini-magharibi mwa In-dia kutia ndani Yudea.

Muunganowa Umedi na Uajemi ulitawala taifala Kiyahudi kwa zaidi ya miaka 200—kuanzia kua-nguka kwa Babiloni katika mwaka wa 539 K.W.K.hadi muungano huo wa Umedi na Uajemi ulipo-shindwa na Wagiriki katika mwakawa 331 K.W.K.Vitabu kadhaa vya Biblia vinataja matukio muhi-mu yaliyotukia wakati huo.

Historia Inayotegemeka

Biblia inatuambia kwamba Mfalme Koreshi waPili aliwaachilia huru Wayahudi waliokuwa mate-ka huko Babiloni, akawaruhusu kurudi Yerusale-mu na kujenga upya hekalu la Mungu ambalo Wa-babiloni waliharibu katika mwaka wa 607 K.W.K.

(Ezra 1:1-7; 6:3-5) Simulizi hilo linaungwa mko-no na maandishi yaliyoandikwa kwenye silinda yaudongo inayoitwa Cyrus Cylinder iliyopatikanakwenye magofu yaBabiloni la kale mwakawa 1879.Maandishi hayo yanamtaja Koreshi kwa jina nakueleza sera yake ya kuwaruhusu mateka warudinchini kwao pamoja na vyombo vyao vya kidini.Mwandikaji wa Biblia, Isaya, aliandika maneno yaYehova ya kinabii kuhusu Koreshi: “ ‘Atatenda ki-kamilifu mapendezi yangu yote’; neno langu kuhu-su Yerusalemu, ‘Atajengwa upya,’ na kuhusu heka-lu, ‘Msingi wako utawekwa.’”—Isaya 44:28.

KITABU KINACHOTEGEMEKA

Sehemu ya 4

Muungano wa Umedi na Uajemina Historia ya Biblia

Hii ni habari ya nne katika mfululizo wenye habari saba katika matoleo ya “Amkeni!” yenye kufuatanayanayozungumzia serikali saba kuu za ulimwengu zinazotajwa katika historia ya Biblia. Kusudi lakeni kuonyesha kwamba Biblia inategemeka na imeongozwa na roho ya Mungu na ujumbe wake unatoatumaini kwamba mateso yanayosababishwa na utawala mkatili wa wanadamu yatakwisha.

Hata Koreshi aliamuru kwamba pesa za kuje-nga upya hekalu ‘zitolewe kutoka katika nyumbaya mfalme,’ linasema andiko la Ezra 6:3, 4. Mane-no hayo yenye kushangaza yanapatana na vita-bu vya historia. “Lilikuwa jambo la kawaida kwawafalme Waajemi kusaidia kujenga upya maeneomatakatifu katika milki yao,” kinasema kitabu Per-sia and the Bible.

Biblia inatuambia kwamba wapinzani wa Wa-yahudi baadaye walimwandikia barua DarioMkuu (ambaye pia aliitwa Dario wa Kwanza)wakipinga madai ya Wayahudi kwamba Koreshialiwaruhusu wajenge upya hekalu. Dario aliamu-ru hati hiyo ya awali itafutwe. Ni nini kilicho-patikana? Kitabu cha kukunjwa kilichokuwa naamri ya Koreshi kilipatikana huko Ekibatana, ulio-kuwa mji mkuu. Dario aliwajibu wapinzani haohivi: “Mimi, Dario, natoa agizo. [Hekalu lijengweupya] mara moja.” Hivyo, upinzani dhidi ya uje-nzi ukakoma.�—Ezra 6:2, 7, 12, 13.

Vitabu vya historia vinaunga mkono maelezohayo. Kwanza, kwa sababu Koreshi aliishi hukoEkibatana wakati wa majira ya kiangazi, na hue-nda alitoa amri hiyo akiwa huko. Pili, vitu vili-vyochimbuliwa vinaonyesha kwamba wafalme waMuungano wa Umedi na Uajemi walipendezwasana na mambo ya kidini ya milki yao na waliandi-ka barua za kutatua mizozo.

Unabii Unaotegemeka

Katika ndoto iliyoongozwa kwa roho ya Mu-ngu, nabii Danieli aliona wanyama wanne

� Wafalme watatu hivi wanaitwa kwa jina Dario.

waliofuatana kutoka kwenye bahari, kila mnya-ma akiwalisha serikali kuu ya ulimwengu amba-yo ingefuata. Mnyama wa kwanza, simba mwenyemabawa, aliwakilisha Babiloni. Wa pili ‘alikuwakama dubu.’ Simulizi hilo linaendelea kusema:“Walikuwa wakimwambia hivi, ‘Simama, ule nya-ma nyingi.’” (Danieli 7:5) Dubu huyo mwenye ku-ogopesha alifananisha Muungano wa Umedi naUajemi.

Kama Danieli alivyotabiri, milki ya Muunganowa Umedi na Uajemi ilikuwa na pupa ya ushindi.Muda mfupi baada ya maono ya Danieli, Kore-shi alishinda Umedi, kisha akapigana na Lidia naBabiloni waliokuwa majirani wake. Mwana wake,Cambyses wa Pili alishinda Misri. Baadaye wata-wala wa Muungano wa Umedi na Uajemi walipa-nua milki hiyo zaidi.

Tuna uhakika gani kwamba ufafanuzi huo nisahihi? Katika maono tofauti lakini yanayohusia-na na hayo, Danieli aliona “kondoo-dume akisu-kuma kuelekea upande wa magharibi na wa kas-kazini na wa kusini.” Unabii huo ulitimia wakatiMuungano wa Umedi na Uajemi ‘uliposukuma’mataifa mengine, kutia ndani taifa lenye nguvula Babiloni. Malaika wa Mungu alifafanua maonohayo alipomwambia Danieli: “Yule kondoo-dumeuliyemwona mwenye pembe mbili anawakilishawafalme wa Umedi na Uajemi.”—Danieli 8:3, 4, 20.

Isitoshe, karne mbili hivi kabla ya kushindwakwa Babiloni, nabii Isaya alitabiri jina la mfal-me Mwajemi atakayelishinda—ambaye wakati

Page

16

,to

p,ti

me

lin

e:E

gyp

tian

wall

relief

an

db

ust

of

Nero

:P

hoto

gra

ph

taken

by

cou

rtesy

of

the

Bri

tish

Mu

seu

m;P

ers

ian

wall

relief:

Mu

s´ ee

du

Lou

vre

,P

ari

s;b

ott

om

,C

yru

sC

ylin

der:

Ph

oto

gra

ph

taken

by

cou

rtesy

of

the

Bri

tish

Mu

seu

m;p

age

17,C

yru

s’to

mb

:�

Ric

hard

Ash

wort

h/age

foto

sto

ck

Silinda inayoitwa Cyrus Cylinder inaelezasera ya kuwarudisha mateka nchini kwao

Bado kaburi la Koreshilinaweza kuonekanakatika magofu ya mji wakale wa Pasargadae,katika Iran ya leo

huo alikuwa bado hajazaliwa—na mbinu amba-yo angetumia kushinda Babiloni. Isaya aliandi-ka hivi: “Yehova amemwambia hivi mtiwa-mafutawake, Koreshi, ambaye mkonowake wa kuume ni-meushika, ili kuyatiisha mataifa mbele yake, . . .nifungue mbele yake milango yenye pande mbili,hivi kwamba hata malango hayatafungwa.” (Isa-ya 45:1) Isaya na pia Yeremia walitabiri kwamba“mito,” au mifereji inayoingiza maji kutoka kwe-nye Mto Efrati, ambao ulikuwa handaki la maji li-lilotoa ulinzi, ingekaushwa. (Isaya 44:27; Yeremia50:38) Wanahistoria Wagiriki, Herodotus na Xe-nophon, wanathibitisha kwamba unabii huo waBiblia ni sahihi, kutia ndani unabii wa kwambaWababiloni walikuwa na karamu usiku ule ambaoKoreshi aliteka jiji hilo. (Isaya 21:5, 9; Danieli 5:1-4, 30) Baada ya kugeuza mkondo wa Mto Efra-ti, majeshi ya Koreshi yaliingia bila upinzani wo-wote kwenye jiji kupitia malango yaliyo kando yamto huo yaliyokuwa yameachwa wazi. Babiloni le-nye nguvu lilianguka katika usiku mmoja!

Tukio hilo lilifanya unabii mwingine utimie. Na-bii Yeremia alikuwa ametabiri mapema kwambawatu wa Mungu wangekaa uhamishoni Babilo-ni kwa miaka 70. (Yeremia 25:11, 12; 29:10) Una-bii huo ulitimia kwa wakati barabara, na wale wa-liokuwa uhamishoni waliruhusiwa kurudi katikanchi yao.

Tumaini Linalotegemeka

Muda mfupi baada ya Muungano wa Umedina Uajemi kushinda Babiloni, Danieli aliandikaunabii ambao unatusaidia kuelewa tukio muhi-mu sana katika kutimizwa kwa mapenzi ya Mu-ngu kwa wanadamu. Malaika Gabrieli alimwa-mbia Danieli wakati hususa ambao Masihi—ule“uzao” ulioahidiwa kwenye Mwanzo 3:15—ange-kuja! Malaika wa Mungu alisema: “Tangu kutole-wa kwa lile neno la kurudisha na kujenga upya

Yerusalemu mpaka Masihi aliye Kiongozi, kuta-kuwa na majuma 7, pia majuma 62,” jumla ya ma-juma 69. (Danieli 9:25) Kipindi hicho kilichotabi-riwa kilianza wakati gani?

Ingawa Koreshi aliwaruhusu Wayahudi warudikwenye nchi yao baada tu ya Babiloni kuanguka,miaka mingi baadaye bado Yerusalemu na kutazake hazikuwa zimerekebishwa. Katika mwakawa 455 K.W.K., Mfalme Artashasta alimruhusuNehemia, mnyweshaji wake Myahudi, arudi Yeru-salemu na kuongoza kazi ya kulijenga upya. (Ne-hemia 2:1-6) Yale majuma 69 yalianza wakatihuo.

Hata hivyo, majuma hayo 69 hayakuwa maju-ma halisi ya siku saba lakini yalikuwa majuma yamiaka. Kwa kweli, tafsiri fulani za Biblia zinase-ma “majuma ya miaka” badala ya kusema “ma-juma.”� (Danieli 9:24, 25) Masihi angekuja baa-da ya kipindi cha “majuma” 69, kila juma likiwana urefu wa miaka 7—jumla ya miaka 483. Una-bii huo ulitimizwa mwaka wa 29 W.K. Yesu alipo-batizwa, miaka 483 ukihesabu kutoka mwaka wa455 K.W.K.�

Kutimizwa kikamili kwa unabii wa Danieli ku-nathibitisha hata zaidi utambulishowa Yesu. Uthi-bitisho huo pia unatupa uhakika kuhusu tumainila wakati ujao. Yesu, akiwa Mfalme wa Ufalmewa mbinguni wa Mungu, ataondoa utawala mka-tili wa wanadamu. Kisha atatimiza unabii mwingi-ne mwingi wa Biblia, kutia ndani unabii unaotabirikufufuliwa kwa wafu ili waishi milele katika Para-diso duniani.—Danieli 12:2; Yohana 5:28, 29; Ufu-nuo 21:3-5.

� Biblia zifuatazo zinatumia usemi “majuma ya miaka”: Ta-nakh—A New Translation of the Holy Scriptures, The Complete Bible—An American Translation, na The Bible—Containing the Old andNew Testaments, ya James Moffatt.� Kwa habari zaidi kuhusu unabii huo, kutia ndani mchoro

unaoonyesha kipindi cha majuma 69 ya miaka, ona ukurasa wa197-199 katika kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

455 K.W.K. 29 W.K.

Kuanzia wakati amri ilitolewa ya kujengaupya Yerusalemu hadi kuja kwa Masihi,miaka 483 ilipita

Amkeni! Februari 2011 19

KATIKA majiji mengi ulimwenguni, mtu ana-posikia kuhusu mji wa Wachina, anafikiria

kuhusu maduka, mikahawa, sherehe, na dansi zadragoni za Wachina. Hata hivyo, kila mji wa Wa-china una historia yake. Miji iliyo huko Aus-tralia leo ilianzishwa na wahamiaji Wachina wa-lioenda huko, wakitarajia kupata utajiri katikamachimbo ya dhahabu yaliyokuwa yamegundu-liwa.

Mlima Mpya wa Dhahabu

Dhahabu ilipogunduliwa huko Australia kati-ka mwaka wa 1851 Wachina walimiminika kwawingi sana katika eneo hilo. Maelfu ya wanaumewalifunga safari yenye magumu baharini kutokadelta ya Mto Pearl, iliyo katika Mkoa wa Guang-dong, China kuelekea upande wa kusini wa du-nia. Hapo awali dhahabu ilikuwa imegunduliwahuko California, Marekani, na Wachina waliozu-ngumza Kikantoni waliyaita machimbo hayo yadhahabu Mlima wa Dhahabu. Kwa hiyo, machi-mbo yaliyogunduliwa huko Australia yakaitwaMlima Mpya wa Dhahabu.

Lakini wanaume hao hawakuhama ili tu waka-tafutedhahabu.China ilikuwa imepatwanavitavyawenyewe kwa wenyewe, misiba ya asili, na umaski-ni, na mambo hayo yalifanya hali iwe ngumu.

Kwa kuhuzunisha, baadhi ya Wachina wakwanza kufunga safari kuelekea Australia hawa-kufanikiwa kuona fuo zake. Walikufa kwa saba-bu ya magonjwa yaliyoenea haraka katika meli zi-lizokuwa zimesongamana watu. Wale waliofaulukufika nchi hiyo mpya waligundua kwamba mai-sha yalikuwa magumu sana kulikowalivyotarajia.Kazi Ngumu Katika Machimbo ya Dhahabu

Wanaume hao walikuwa wapweke sana kwakuwa kulingana na desturi, wanawake na watotowalibaki China ili kulinda mahali pao katika na-saba ya familia. Katika mwakawa 1861, wanaume

WALIENDAKUTAFUTADHAHABU,WAKAPATA MAKAO

Syd

ney

Ch

inato

wn

:�

AR

CO

/G

M¨ uller/

age

foto

sto

ck;gold

min

er:

Joh

nO

xley

Lib

rary

,Im

age

60

52

6,S

tate

Lib

rary

of

Qu

een

sla

nd

Mchimbaji wadhahabu Mchina,miaka ya 1860

20 Amkeni! Februari 2011

Wachina zaidi ya 38,000 waliishi Australia, lakinikulikuwa na wanawake 11 tu Wachina. Hata hi-vyo, ni wachache tu waliokuwa wamepangia kui-shi huko. Wengi wao walikuwa wameazimia ku-rudi nyumbani kwa familia zao wakiwa na utajirina umashuhuri.

Tamaa hiyo iliwafanya watafute dhahabu kwabidii. Wachimbaji hao waliishi katika mahema nawalifanya kazi ngumu kwa saa nyingi chini yajua kali. Mwanzoni, baadhi yao waliogopa kuchi-mba migodi iliyokuwa chini ya ardhi kwa sababuya ushirikina. Hivyo walianza kuchimba juu yaardhi na kusafisha mchanga uliokuwa na dhaha-bu wakitumia milizamu ya mbao. Jitihada zao zi-

lifanikiwa. Rekodi zinaonyesha kwamba kati yamwaka wa 1854 na 1862, kilogramu 18,662 hivi zadhahabu zilizopatikana katika jimbo la Victoriazilipelekwa China.

Kwa kusikitisha, baadhi ya utajiri huo ulifujwakwa kucheza kamari na uraibu wa kasumba—ma-zoea ambayo watu wapweke walijihusisha nayo.Mara nyingi matokeo yalikuwa kuharibika kwaafya na kupoteza mapato na tarajio la kurudi nyu-mbani. Baadhi ya watu hao walisaidiwa na mashi-rika ya Kichina na watu mmojammoja, lakini we-ngine walikufa wakiwa maskini na wapweke.

Wachina hao pia walikabili uhasama kutokakwa wachimbaji wengine waliowaonea wivu na

Ili kuepuka kulipa ada aukodi ya kutua, abiria Wachinawalishuka kutoka kwenye melikabla haijafika kwenye banda-ri kubwa zilizo kwenye pwaniya Australia na mamia ya kilo-mita kutoka machimbo yadhahabu. Mji wa Robe, Kusinimwa Australia, ulikuwa mojakati ya miji waliyotua. Robe uli-kuwa na wakazi kati ya 100na 200, na katika muda wamiezi mitano katika mwaka

wa 1857, Wachina 12,000 hiviwalipitia mji huo.

Katika tendo lenye ku-shangaza lilionyesha uvumilivuna ushirikiano, vikundi vya ma-mia ya wanaume vilipitia se-hemu za ndani za nchi ambayohaikuwa na watu wengi vikiele-kea kwenye machimbo ya dha-habu. Hata hivyo, ilikuwa mba-li kuliko walivyofikiri, na safarihiyo ilichukua majuma mata-no hivi. Walipokuwa njiani, wa-

hamiaji hao walichuma majaniya baharini na kula kangaruuna wombati. Pia walichimba vi-sima na kutengeneza njiaambayo wengine wangefuata.

Wakiwa wamefunga nywelezao nyuma na kuvalia kofia,wanaume hao walikimbia po-lepole kwenye mstari mmojahuku wakiimba. Sarafu za Ki-china zimepatikana kwenyenjia hiyo. Wahamiaji hao wali-tupa pesa zao walipogunduakwamba hazikuwa na thamaniyoyote nchini Australia.

MBALI KULIKO WALIVYOFIKIRI

Image

H17

071

,S

tate

Lib

rary

of

Vic

tori

a

kuwashuku kwa sababu Wachina walishirikia-na kwa ukaribu na kufanikiwa katika uchimba-ji wa dhahabu. Uhasama huo ulitokeza vuruguna mashambulizi dhidi ya Wachina. Dhahabuyao iliporwa, na mahema na mali yao kute-ketezwa. Mwishowe uhasama huo ulipungua.Hata hivyo, miaka 50 hivi baada ya dhahabukugunduliwa, Sheria ya Kuwazuia Wahamiajiya 1901 iliwazuia wahamiaji kutoka Asia ku-hamia Australia. Sheria hiyo ilifutiliwa mbalimwaka wa 1973.

Dhahabu Ilipoisha

Migodi ilipoacha kutokeza dhahabu, Wa-china fulani waliamua kubaki Australia. Kwahiyo, Wachina walianzisha biashara za dobi,mikahawa, na mashamba madogo ya kukuzabidhaa za kuuzwa kwenye miji iliyokuwa namachimbo ya dhahabu. Wachina pia walijuli-kana kuwa watengenezaji bora wa fanicha nawauzaji matunda na mboga. Kwa sababu hiyo,kufikia mwisho wa karne ya 19, kulikuwa najamii au miji ya Wachina katika majiji mengiya Australia, kutia ndani Atherton, Brisbane,Broome, Cairns, Darwin, Melbourne, Sydney,na Townsville.

Kwa sababu kulikuwa na wanawake wacha-che sana Wachina huko Australia, wanaumewengi walibaki wakiwa waseja. Hata hivyo, we-ngine wao walioa wanawake Waaustralia inga-wa wenyeji wengi hawakupenda ndoa za ainahiyo. Baada ya muda, wazao wa ndoa hizo zawatu wa mataifa mawili wakawa sehemu ya ja-mii ya watu wa Australia.

Leo kuna wahamiaji wengi Wachina nchiniAustralia kuliko hapo awali. Wengi wao hujakwa sababu ya masomo ya juu na biashara. Isi-toshe, wahamiaji hao wanatia ndani wanawa-ke wengi. Kinyume na ilivyokuwa hapo awali,kwa sababu ya kubadilika kwa uchumi ulimwe-nguni, wanaume wengi Wachina huhamishiafamilia zao Australia, kisha wao hurudi baraAsia na kufanya kazi huko China, Hong Kong,Singapore, au Taiwan.

Kweli mambo yamebadilika. Lakini kwawa-hamiaji ulimwenguni pote, malengo ni yaleya-le, yaani, kupata usalama na mafanikio katikanchi ya kigeni.

Wayne Qu alikuwa mwanasayansi wa ma-zingira katika Shirika la Kisayansi huko China. Iliapandishwe cheo, Wayne na mke wake Suewalienda Ulaya katika miaka ya 1990 kwa ajiliya masomo ya juu. Wakiwa huko, walikutanana Mashahidi wa Yehova na wakaanza kujifu-nza Biblia pamoja nao. Katika mwaka wa 2000,Wayne na Sue walihamia Australia, na wote wa-wili waliendelea na masomo yao ya juu—Sueakisomea biolojia ya molekuli. Pia waliendeleakujifunza Biblia.

Wayne anaeleza: “Tulikuwa tumetumia miakamingi ili kupata digrii za juu zaidi katika chuo ki-kuu. Hata hivyo, nilijiuliza: ‘Mwishowe, sisi sotetutazeeka, tuwe wagonjwa, na tufe. Je, hilo ndilokusudi la uhai?’ Mambo hayo yote yalionekanakuwa ubatili. Hata hivyo, Biblia ilinipa mimi naSue majibu yenye kuridhisha, yanayopatana naakili kuhusu maswali muhimu maishani.

“Pia, kujifunza Biblia kulituwezesha kuchungu-za wazo ambalo hatukuwa tumewahi kulifikiria,yaani, kuwapo kwa Muumba. Nilisoma kitabuLife—How Did It Get Here? By Evolution or by Cre-ation? kilichochapishwa na Mashahidi na wakatiuleule, nilisoma kitabu kuhusu mageuzi kilichoa-ndikwa na Charles Darwin. Vitabu hivyo, pamojana utafiti wa kisayansi niliofanya, ulinisadikishakwamba kuna Muumba. Sue pia alisadikishwa.

“Jambo lingine lililotusadikisha kwamba kunaMungu ni kwamba Biblia ina nguvu ya kubore-sha maisha. Kwa kweli, kitabu hicho kizurisana kimetupatia tumaini la wakati ujao, mara-fiki wa kweli, na pia kimeimarisha ndoa yetu.Mimi na Sue tulibatizwa mwaka wa 2005, na tu-nafurahi kwamba tumepata kitu chenye thama-ni zaidi kuliko elimu ya juu na ‘dhahabu ambayohuharibika.’”—1 Petro 1:7.

KITU CHENYE THAMANIZAIDI KULIKO DHAHABU

SAYANSI hutusaidia sana kuelewa ulimwe-ngu wa asili kwa kufunua utaratibu, usahi-

hi, na utata ambao watu wengi huona umetoka-na na Mungu mwenye akili na nguvu zisizo nakifani. Kwa maoni yao, sayansi haifunui tu ma-mbo kuhusu ulimwengu wa asili bali pia inatufu-nulia akili ya Mungu.

Maoni hayo yanaungwa mkono na Biblia.Waroma 1:20 inasema hivi: “Sifa [za Mungu]ambazo hazionekani, zinaonekana waziwazi ta-ngu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea,kwa sababu zinaeleweka kwa vitu vilivyofanywa,yaani, nguvu zake za milele na Uungu.” Vilevi-le Zaburi 19:1, 2 inasema: “Mbingu zinatangazautukufu wa Mungu; nalo anga linatangaza kaziya mikono yake. Siku moja baada ya siku nyingi-ne hufanya maneno yabubujike, na usiku mmo-ja baada ya usiku mwingine huonyesha ujuzi.”Hata hivyo, licha ya mambo yake mengi yenyekustaajabisha, ulimwengu wa asili unafunua tubaadhi ya sifa za Muumba wetu.

Sayansi Ina Mipaka

Sayansi haiwezi kutufundisha kweli nyingikumhusu Mungu. Kwa mfano, mwanasayansianaweza kufafanua kila molekuli iliyo ndani yakeki ya chokoleti, lakini je, ufafanuzi wake una-weza kuonyesha kwa nini keki hiyo iliokwa auni ya nani? Ili kupata majibu ya maswali kamahayo ambayo watu wengi wataona ndiyo muhi-mu zaidi, mtu anapaswa kumwuliza yule aliyeo-ka keki hiyo.

Vivyo hivyo, sayansi “inatoa habari nyingi ha-kika,” akaandika Erwin Schrodinger, mwanafizi-

kia kutoka Austria ambaye pia ni mshindi waTuzo la Nobeli, “lakini haifunui chochote . . .kabisa kuhusu mambo yaliyo muhimu kwetu.”Anasema mambo hayo yanatia ndani “Munguna umilele.” Kwa mfano, ni Mungu peke yakeanayeweza kujibu maswali yafuatayo: Kusudi laulimwengu ni nini? Kwa nini sayari yetu ina viu-mbe wengi, kutia ndani viumbe wenye akili? Iki-wa kwa kweli Mungu ndiye mweza-yote, kwanini anaruhusu uovu na kuteseka uendelee? Naje, kuna tumaini lolote kwa wafu?

Je, Mungu amejibu maswali hayo? Ndiyo,Biblia hujibu maswali hayo. (2 Timotheo 3:16)Huenda ukauliza, ‘Kuna uthibitisho gani kwa-mba kwa kweli Biblia ilitoka kwa Mungu?’ Kwamaoni ya wanasayansi, yale ambayo Biblia ina-sema kuhusu ulimwengu unaotuzunguka lazi-ma yapatane na mambo hakika ya kisayansi,kwa hiyo, yale ambayo Biblia inasema hayapa-swi kupingana na kile ambacho ameumba. Je,Biblia inapatana na sayansi? Chunguza mifanomichache.

Biblia Ilitangulia Sayansi

Biblia ilipokuwa ikiandikwa, watu wengi wa-liamini kwamba miungu mbalimbali iliishi uli-mwenguni na kwamba miungu hiyo ndiyo ili-yodhibiti jua, mwezi, hali ya hewa, uzazi, nakadhalika, na vitu hivyo havikudhibitiwa na she-ria za asili. Lakini manabii Waebrania wa kalewa Mungu hawakuamini hivyo. Bila shaka wali-jua kwamba Yehova Mungu angeweza kudhibi-ti moja kwa moja ulimwengu wa asili na alifa-nya hivyo pindi fulani hususa. (Yoshua 10:12-14;

MAONIYA BIBLIA

Je, Sayansi Inapatanana Biblia?

“Mimi hupata shangwe katika kazi yangu ya sayansi ninapovumbua kitu kipya na ku-

jiambia, ‘Kumbe hivi ndivyo Mungu alivyofanya!’ ”

—HENRY SCHAEFER, PROFESA WA KEMIA.

22 Amkeni! Februari 2011

Amkeni! Februari 2011 23

2 Wafalme 20:9-11) Hata hivyo, John Lennox,profesa wa hesabu katika Chuo Kikuu cha Ox-ford, Uingereza, alisema kwamba manabii hao“hawakuhitaji kuacha kuamini kwamba [miu-ngu ya kuwaziwa] ndiyo iliyodhibiti ulimwengu. . . , kwa kuwa hawakuwa wakiamini miunguhiyo. Hawakujihusisha katika imani hiyo ya ki-shirikina kwa sababu waliamini kwamba kunaMungu Mmoja wa Kweli, Muumba wa mbinguna dunia.”

Imani hiyo iliwalinda namna gani na ushiriki-na? Kwanza, Mungu wa kweli aliwafunulia kwa-mba anaongoza ulimwengu kupitia sheria husu-sa. Kwa mfano, zaidi ya miaka 3,500 iliyopita,Yehova Mungu alimwuliza hivi mtumishi wakeAyubu: “Je, umepata kujua sheria za mbingu?”(Ayubu 38:33) Katika karne ya saba K.W.K., na-bii Yeremia aliandika kuhusu “sheria za mbinguna dunia.”—Yeremia 33:25.

Hivyo, wote walioishi nyakati za kale naambao waliamini yale ambayo manabii wa Bib-lia waliandika wangejua kwamba ulimwenguhauongozwi na miungu ya kuwaziwa yenye hisiazinazobadilika-badilika, bali na sheria ambazowanadamu wanaweza kuchunguza na kuelewa.Kwa sababu hiyo, watu waliomwogopa Munguhawakuabudu vitu ambavyo Mungu ameumbakama vile jua, mwezi, nyota, wala hawakuwa naushirikina wowote kuvielekea. (Kumbukumbula Torati 4:15-19) Badala yake, waliona walipa-swa kuchunguza uumbaji wa Mungu ili kuonahekima, nguvu, na sifa nyingine za Mungu.—Za-buri 8:3-9; Methali 3:19, 20.

Kwa kupatana na maoni ya wanasayansi we-ngi leo, Waebrania wa kale pia waliamini kwa-mba dunia ilikuwa na mwanzo. Mwanzo 1:1 ina-sema: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbinguna dunia.” Pia, miaka 3,500 hivi iliyopita, Mu-ngu alimfunulia mtumishi wake Ayubu kwambadunia ‘imeitundikwa pasipo na kitu,’ au inani-ng’inia angani. (Ayubu 26:7) Na pia, zaidi yamiaka 2,500 iliyopita, nabii Isaya aliandika kwa-mba dunia ni mviringo au duara.—Isaya 40:22.�

Naam, Biblia inapatana na yale ambayo sa-yansi inasema kuhusu ulimwengu wa asili. Kwakweli Biblia na sayansi hutusaidia kujifunza ku-mhusu Mungu kwani zinapatana. Kupuuzamoja ni kama kufunga mlango ili tusipate ujuzikumhusu Mungu.—Zaburi 119:105; Isaya 40:26.� Kwa maelezo zaidi kuhusu kuwepo kwa Mungu na usahi-

hi wa Biblia, tafadhali soma broshua Uhai—Ulitokana na Muu-mba? na kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? vilivyochapi-shwa na Mashahidi wa Yehova.

JE, UMEJIULIZA HIVI?

˘ Uumbaji unaweza kutufundisha ninikumhusu Mungu?—Waroma 1:20.

˘ Ni mambo gani kumhusu Munguambayo hatuwezi kujifunza kupitiasayansi?—2 Timotheo 3:16.

˘ Kwa nini manabii wa kale wa Mungu wakweli hawakuwa na ushirikina kuhusuuumbaji?—Yeremia 33:25.

Ulimwengu unaongozwa na sheriahususa—“sheria za mbingu nadunia.”—YEREMIA 33:25

˘ Unapoutazama mkia wa bakteria (bac-terial flagellum) chini ya darubini yenyenguvu sana, unaonekana kuwa mdogosana na usio na maana. Umelinganishwana injini yenye nguvu iliyounganishwa nyu-ma ya boti. Umefanyizwa jinsi gani?

Kuna aina mbalimbali za mikia, lakinihuenda mkia wa bakteria (Kilatini, “mjele-di”) ndio umechunguzwa zaidi. Ukiwaumeunganishwa kwenye ukuta wa che-mbe ya bakteria, mkia huo huzungukana kuwezesha bakteria kusonga mbele,kutua, kurudi nyuma, na kugeuka. Inakadi-riwa kwamba nusu ya bakteria zote zinazo-julikana zina mikia.

Chembe za urithi (DNA) za bakteria auvijidudu zina maagizo kuhusu utendaji wamkia huo na sehemu ya chembe inayouzu-ngusha. Mkia huo umefanyizwa kwa proti-ni 40, ambazo zinaweza kufananishwa nasehemu za injini. Kwa kustaajabisha, mkiahuo hujiunganisha kwa dakika 20 tu!

Kichapo The Evolution Controversy kina-sema hivi: “Mkia wa bakteria unatia ndanimtambo wenye kuzunguka ambao huzu-nguka mara 6,000 hadi 17,000 kwa daki-ka. Jambo la kushangaza hata zaidi nikwamba mashini hiyo inaweza kutua nakugeuka haraka, kisha kuzunguka upandeule mwingine mara 17,000 kwa dakika.”Gazeti New Scientist linautaja mkia wabakteria kuwa “mfano mzuri wa mfumowenye molekuli tata—mashini ndogo sanaambayo hakuna mhandisi yoyote mwana-damu anayeweza kuiunda.”

Wanasayansi hawajaelewa jinsi amba-vyo mkia huo mdogo wa bakteria hujiu-nganisha pamoja ukifuata mpangilio husu-sa unaohitajiwa ili sehemu zote 40zilingane na zifanye kazi vizuri.

Una maoni gani? Je, mkia wa bakteriaulijitokeza wenyewe, au ulibuniwa?

JE, NI KAZI YA UBUNI?

MkiawaBakteria

Bakteriailiyoongezwaukubwa

Mikia

Propela

Kiunganishi kikuu

Bushi

RotaBacterium inset: � Scientifica/Visuals Unlimited, Inc.; flagellumdiagram: Art source courtesy of www.arn.org

Amkeni! Februari 2011 25

KATIKA mwaka wa 1962, nilipokuwa na umriwa miaka kumi, mama yangu alianza kuji-

funza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Baadaya muda, yeye na baba yangu, ambao ni Wachi-na waliozaliwa Indonesia, pamoja na sisi watotowatano tukawa Mashahidi.

Wamishonari na waangalizi wanaosafiri wa-liishi nyumbani kwetu walipotembelea kutani-ko letu ili kututia moyo. Mfano wao mzuri namazungumzo yao yenye kujenga yalinichocheasana. Nilipokuwa na umri wa miaka 19, nilia-mua kuwa mhudumu Mkristo wa wakati wote.Mwaka mmoja hivi baadaye, niliolewa na Jo-sef Neuhardt, mmishonari Mjerumani amba-ye aliyekuja Indonesia mwaka wa 1968. Baadaya fungate, tulihamia Sumatra, kisiwa cha pilikwa ukubwa kati ya visiwa zaidi ya 17,000 vyaIndonesia. Tukiwa huko, niliandamana na Josefkatika kazi yake ya kutembelea makutaniko yaMashahidi wa Yehova akiwa mwangalizi anaye-safiri.

Kuhubiri Sumatra

Mzunguko wetu, au eneo tulilogawiwa lilia-nzia jiji lenye joto na shughuli nyingi la Padang,Sumatra Magharibi, hadi kwenye Ziwa Toba,ziwa maridadi lililotokezwa na mlipuko wa vol-kano ambalo lilikuwa kwenye nyanda za juuhuko Sumatra Kaskazini. Baadaye tuligawi-wa eneo la kusini kwenye kisiwa hicho. Kilamara tulikuwa safarini katika gari letu dogo laVolkswagen, tukipitia barabara za msituni zili-zokuwa na mashimo, tukivuka madaraja yenyekutikisika yaliyojengwa kwa minazi, na kupitakando ya milima mikubwa ya volkano, amba-yo mingine ilikuwa haitendi na mingine iliku-wa hai. Usiku tulilala sakafuni katika nyumbaambazo hazikuwa na umeme, vyoo, au bafu. Tu-lioga na kuosha nguo zetu kwenye maziwa namito. Tuliishi maisha rahisi na tuliwapendawatu. Watu walitukaribisha kwa uchangamfu nakutulisha, na wengi wao walipendezwa na Bib-lia.

Maisha YanguYamekuwa YenyeKuridhishaLIMESIMULIWA NA HERAWATI NEUHARDT

Nilizaliwa huko Cirebon, Indonesia, jiji linalojulika-

na sana kwa vitambaa vya batiki vilivyopambwa kwa

kutiwa rangi ya michoro mbalimbali. Kwa njia fulani,

maisha yangu nikiwa mmishonari yamekuwa kama

kitambaa cha batiki kwa kuwa nimekutana na watu

wa tamaduni mbalimbali wanaoishi Kusini-Mashari-

ki mwa Asia na Pasifiki ya Kusini. Acha nisimulie.

Ziwa Toba

Padang

Sumatra

Borneo

I N D O N E S I A

JAKARTACirebon

JavaPAPUA NEW GUINEA

Daru

PORT MORESBY VISIWAVYA

SOLOMON

Katika eneo la Padang, watu wa Minangka-bau, ambao wengi wao ni Waislamu, walisha-ngaa na kufurahi tulipowaonyesha katika Bib-lia kwamba Mungu ni mmoja—si Utatu, kamadini zinazodai kuwa za Kikristo zinavyofundi-sha. (Kumbukumbu la Torati 6:4) Watu we-ngi walifurahia magazeti ya Mnara wa Mlinzina Amkeni!, na baadaye wengine waliopendezwawalifanya maendeleo mazuri ya kiroho. Katikaeneo la Ziwa Toba, Wabatak, ambao wengi waowalidai kuwa Wakristo, walijua jina la Mungu,Yehova, kwa kuwa waliliona katika Biblia yaoya Kibatak. (Zaburi 83:18) Hata hivyo, walihi-taji uelewaji zaidi kumhusu Mungu na kusudilake kwa wanadamu. Wengi wao walikubali ku-jifunza Biblia na wakawa Wakristo waeneza-inji-li wenye bidii.

Kugusa Mioyo ya Watu Huko Java

Mnamo 1973, mimi na Josef tulipewa mgawohuko Java, kisiwa kilicho nusu ya ukubwa wa Ui-ngereza, kilichokuwa na wakazi zaidi ya milio-ni 80.� Tuliwahubiria Wajava, Wasunda, na watuwa makabila mbalimbali ya Kichina.

Kwa kuwa nililelewa na wazazi Wachina wa-liozaliwa Indonesia, nilizungumza lugha mbali-mbali kama vile Kijava, Kisunda, na Kiindonesia,na pia Kiingereza. Kwa sababu hiyo, nilifurahia

� Leo Java ina watu zaidi ya milioni 120.

kuzungumza kuhusu Biblia na watu katika lughayao ya kienyeji.

Huko Jakarta, mji mkuu wa Indonesia ambaouko kwenye kisiwa cha Java, nilimweleza msicha-na mmoja mwenye umri wa miaka 19 aliyeone-kana kuwa ameshuka moyo kuhusu tumaini lakuishi milele katika Paradiso duniani. Nilipoku-wa nikisoma Biblia, alianza kulia. “Asante sanashangazi kwa kuniambia mambo hayo,” akania-mbia huku akitumia neno linaloashiria upendona heshima. Kisha akaongezea hivi: “Ninahitajirupia nyingine milioni 1.5 [dola 160 za Mareka-ni] kufikia kesho ili kulipa karo ya chuo kikuu, nanilikuwa nimefikiria kuuza ubikira wangu ili ni-pate pesa hizo. Nilikuwa tu nimetoka kusali ni-pate mwongozo. Sasa nimepata jibu. Nimeamuakuahirisha masomo yangu na kubaki safi kiadili.”Msichana huyo alifurahia kujifunza mengi kuto-ka kwa Biblia.

Tangu wakati huo, Wajava wengi, kutia nda-ni Wasunda na Wachina, wamepatanisha maishayao na viwango vya Neno la Mungu. Hilo lime-waletea amani ya akili na furaha kama vile Mu-ngu anaahidi.—Isaya 48:17, 18.

Kalimantan—Makao ya Wadayak

Kutoka Java, mimi na Josef tulihamia Kaliman-tan, mkoa wa Borneo huko Indonesia, ambachondicho kisiwa cha tatu kwa ukubwa ulimwenguni

Herawati akiwa na wanafunzi wa Bibliakatika Visiwa vya Solomon

Nikiwa na Josef hukoUholanzi, kabla tu ya kifochake mwaka wa 2005

Amkeni! Februari 2011 27

(baada ya Greenland na New Guinea). Kisiwahicho cha Borneo chenye misitu mikubwa, mi-lima yenye miamba, na mito mikubwa, ni ma-kao ya Wachina, Wamalay Waislamu, na Wada-yak ambao ni wenyeji wa huko wanaoishi kandoya mito na wakati mmoja walikuwa wakiwakataadui zao vichwa.

Ili kufika maeneo ya mbali ya Wadayak, tulisa-firi kwa mashua au mtumbwi kwenye mito safiiliyopitia msituni. Mamba wakubwa waliota juakwenye kingo za mto, tumbili walitutazama kuto-ka kwenye miti, na ndege walipeperusha manyo-ya yao yenye rangi za kupendeza. Naam, utumi-shi wa umishonari huko ulisisimua sana!

Wadayak wengi waliishi kwenye nyumba zi-lizojengwa juu ya nguzo kwa vifaa vinavyopa-tikana msituni. Nyumba fulani zilikuwa ndogo;nyingine zilikuwa ndefu na familia kadhaa zilii-shi humo. Watu wengi hawakuwa wamewahi ku-mwona mzungu, kwa hiyo watu walitaka sanakumwona Josef. Watoto walikimbia kijijini waki-sema, “Pasta! Pasta!” Kisha watu walikusanyikakumsikiliza mhudumu huyo mzungu. Josef ali-wahubiria kupitia Mashahidi wenyeji ambao wa-limtafsiria na baadaye wakapanga kujifunza Bib-lia na wengi waliopendezwa.

Mgawo Mpya Papua New Guinea

Kwa sababu ya kushinikizwa na wapinzani wakidini, serikali ya Indonesia iliwapiga marufukuMashahidi wa Yehova mnamo Desemba (Mweziwa 12) 1976. Kwa hiyo, mimi na Josef tulipewamgawo huko Papua New Guinea.

Tulipowasili mji mkuu wa Port Moresby, tuliji-funza lugha ya Hiri Motu kwa miezi miwili amba-yo inatumiwa katika biashara. Kisha tukahamiaDaru, kisiwa kidogo kilicho mbali kwenye mkoawa magharibi. Nikiwa huko, nilikutana na Eu-nice, mwanamke mnene, mwenye nguvu, mwe-nye utu wa kupendeza, ambaye meno yake ya-likuwa meusi kwa sababu ya kutafuna tambuukwa miaka mingi. Eunice alipojifunza kwambaMungu anataka watumishi wake wawe safi ki-mwili na pia kiadili na kiroho, aliacha uraibu huona kuwa Mkristo mwaminifu. (2 Wakorintho 7:1)Kila mara tulipoona watu wanyenyekevu waki-fuata mashauri ya Biblia maishani, tuliona ukwe-

li wa maneno haya ya Zaburi 34:8: “Onjeni mwo-ne ya kuwa Yehova ni mwema.”

Baada ya muda, Josef aliwekwa rasmi tenakuwa mwangalizi anayesafiri, na tulitembelea ka-ribu kila sehemu ya Papua New Guinea, nchi ili-yo na lugha 820 hivi. Ili tuwafikie watu wengizaidi, tulijifunza lugha nyingine, yaani, lugha yaTok Pisin, ambayo hutumiwa katika mawasilianonchini humo. Ili kufikia miji na vijiji mbalimba-li, tulitembea kwa miguu, tukasafiri kwa mashua,mtumbwi, na kwa ndege ndogo, na kuvumiliajoto kali, mbu, na malaria.

Kisha katika mwaka wa 1985, tulikubali mga-wo mwingine wa umishonari katika Visiwa vyaSolomon, vilivyoko mashariki ya Papua NewGuinea. Tukiwa huko tulifanya kazi katika ofisiya tawi ya Mashahidi wa Yehova na pia tulisafi-ri kotekote kwenye visiwa hivyo ili kuyatia moyomakutaniko na kuhudhuria makusanyiko ya Ki-kristo. Kwa mara nyingine tena, ilibidi tujifunzelugha mpya—wakati huu tulijifunza Kipijini chaVisiwa vya Solomon. Tulifurahia sana kuzungu-mza na wakazi wa Visiwa vya Solomon wanaope-nda Biblia!

Safari Ngumu Zaidi

Mnamo 2001, serikali ya Indonesia iliondoamarufuku dhidi ya Mashahidi wa Yehova, nasi tu-karudi Jakarta. Hata hivyo, muda mfupi baada yakurudi, iligunduliwa kwamba mume wangu mpe-ndwa alikuwa na kansa ya ngozi ambayo hueneaharaka. Tulienda Ujerumani nyumbani kwa Jo-sef ili apate matibabu. Lakini, kwa kuhuzunisha,mnamo 2005, miaka 33 tangu tulipofunga ndoa,alilala katika usingizi wa kifo na sasa anasubiriwakati atakapofufuliwa katika ulimwengu mpyautakaokuwa Paradiso. (Yohana 11:11-14) Aliku-wa na umri wa miaka 62 na alikuwa ametumikakatika utumishi wa wakati wote kwa miaka 40.

Nilibaki Jakarta, ambako ninaendelea kutumi-ka nikiwa mmishonari. Ninamkosa sana mumewangu mpendwa. Lakini kuwafundisha wenginekweli zenye thamani zinazopatikana katika Nenola Mungu kumenisaidia kukabiliana na hali hiyo,kwa kuwa kuhubiri hunipa uradhi na kusudi mai-shani. Kwa kweli, Yehova amenipa maisha yenyekupendeza na yenye kuridhisha.

28 Amkeni! Februari 2011

1.Kitanda.2.Meza.3.Kiti.4.2,000.5.A.

MAJIBUYAUKURASAWA30NA31

˘ Unataka kufanya nini maishani? Je, unataza-mia mambo yanayopatana na akili, au unaotakuhusu mambo ambayo huwezi kutimiza? Mtufulani aliyechunguza utu wa wanadamu alitoaushauri huu wenye hekima: “Hayo nayo ni burekabisa; ni sawa na kufukuza upepo. Afadhalikuridhika na ulicho nacho kuliko kuhangaikakwa kutamani kitu kingine.”—Mhubiri 6:9, BibliaHabari Njema.

Maneno “ulicho nacho” yanarejelea hali zetuna mambo halisi ya sasa. Kwa kweli, hakunaubaya kujaribu kuboresha maisha yetu. Hata hi-vyo, jambo kuu ambalo Biblia inataja ni kwa-mba si jambo la hekima kufuatia miradi isiyo-patana na akili. Huenda miradi hiyo ikawaumashuhuri, utajiri, mwenzi bora kabisa wandoa, au afya kamilifu.

Isitoshe, huenda wale ambao hufikia miradimingine, kama vile utajiri, wakatamani kupatazaidi. Biblia inasema hivi waziwazi: “Anayependafedha hatatosheka na fedha, wala anayependa

mali hatatosheka na mapato. Hilo pia ni ubatili.”(Mhubiri 5:10) Kwa sababu hiyo, watu wenye he-kima kiroho hujaribu kuridhika na kile ‘walichonacho.’ Naam, wanatambua ukweli wa manenohaya: “Hatukuleta chochote katika ulimwengu,wala hatuwezi kuchukua chochote nje.”—1 Ti-motheo 6:7.

Wanadamu wameumbwa kwa njia ya kwa-mba wale wanaotosheleza mahitaji yao ya kiro-ho ndio wanaopata furaha nyingi zaidi. (Matha-yo 5:3) Tunaweza kufanya hivyo kwa njia gani?Yesu Kristo alisema hivi: “Mwanadamu ataishi,si kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotokakatika kinywa cha Yehova.” (Mathayo 4:4) Ma-neno hayo yenye thamani yanapatikana katikaBiblia, na mtu yeyote anaweza kufaidika nayo.

Maneno kama hayo yanapatikana katikaZaburi 37:4. Inasema hivi: “Upate furaha telekatika Yehova, naye atakupa maombi ya moyowako.” Akiwa Mungu Mweza-Yote, Yehova ata-wapa waabudu wake waaminifu vitu ambavyohakuna mwanadamu anaweza kuwapa: afyakamilifu, vitu vya kimwili, na uzima wa milelekatika Paradiso duniani. (Luka 23:43; Ufunuo21:3, 4) Inapatana na akili kuamini manenohayo.

Je, Una Miradi Inayopatana na Akili?

Marafiki Wachache wa Kweli“Mwingereza wa kawaida ana marafiki watatu

tu wa kweli ambao anaweza kuwategemea,” linase-ma gazeti Daily Telegraph la London. Kulingana nauchunguzi mmoja, baadhi ya sababu zinazowafa-nya watu waache kuwasiliana na “marafiki 36 hivikadiri miaka inavyopita” ni “maisha yenye shughu-li nyingi,” ‘kuacha kuwa na uhusianowa karibu’ na,asilimia 43 kati ya wale waliochunguzwa walisemakwamba sababu nyingine ilikuwa, “kukosana . . . nakuamua kwamba hawatawahi kuwasiliana tena.”Karibu asilimia 20 huwaeleza wafanyakazi wenzaomamboyao ya siri kwa kuwa “hakuna mtu mwingi-ne wanayeweza kuomba mashauri.” Msemaji wawale waliofanya uchunguzi huo alisema: “Unahita-ji sifa ya pekee ili uaminiwe na kutegemewa.”

Meli za Kusafirishia Dawa za KulevyaWalanguzi wa dawa za kulevya nchini Kolombia

wanaboresha mbinu zao za kuingiza kokeini katikanchi za Amerika ya Kati, Marekani, na Mexico.Tangu mwaka wa 1993, meli 42 hivi za kusafirishiadawa za kulevya zinazokaribia kufanana na nya-mbizi zimenaswa na wenye mamlaka nchini Ko-lombia. Karakana kadhaa ambako meli hizo hu-tengenezewa zimepatikana pia. Ingawa meli hizozinazotumia dizeli haziwezi kuingia chini kabisa ya

maji, ni vigumu sana kuziona kwenye rada. Nyingi-ne zinaweza kwenda umbali wa kilomita 3,200, nazinaweza kubeba zaidi ya tani sita hadi kumi za ko-keini, na huenda zikagharimu dola milioni mojahivi (za Marekani) kujenga.

Faida za Familia Kula PamojaIdadi isiyozidi nusu ya vijana Wafini wenye umri wa miaka 14

hadi 16 waliohojiwa katika uchunguzi wa hivi karibuni walisemakwamba wao hula pamoja na familia zao. Uchunguzi huo ulio-nyesha kwamba katika nyumba nyingi hakuna milo inayoandali-wa. Hata hivyo, vijana hutazamia sana pindi hizo za kawaida nazenye kustarehesha za kuwa pamoja na familia zao. Walipouli-zwa kile walichotaka kutoka kwa wazazi wao, walisema hiviwaziwazi: “Vyakula moto, kula pamoja tukiwa familia, namtu anayesikiliza na aliye na wakati wa kuwa pa-moja nasi,” linaripoti gazeti Helsingin Sanomat.Kula pamoja kama familia kunaathiri afya yaakili ya kijana kwa njia kubwa. Kulingana nagazeti hilo, “vijana ambao hula pamoja na fa-milia zao hufanya vizuri shuleni, hawavuti si-gara, hawatumii kileo, au kutumia dawa zakulevya, na hawashuki moyo mara nyingi.”

KUUTAZAMA ULIMWENGU

Karibu robo ya Wajerumani walio chini ya umriwa miaka 40 wanaona ni muhimu kusali kilasiku pamoja na watoto, na kati ya wale wanaoe-nda kanisani, ni watu 4 tu kati ya 10 wa-naoona jambo hilo kuwa muhimu.—APO-THEKEN UMSCHAU, UJERUMANI.

Mtu fulani aliyetoa shahawa iliyokuwana mabadiliko fulani katika chembe zaurithi yanayohusianishwa na ugonjwa wa moyoaliwapitishia ugonjwa huo watoto 9 kati ya 24wanaosemekana kuwa wake. Kati ya hao mmo-ja wao alikufa kutokana na ugonjwa wa moyoakiwa na umri wa miaka miwili.—JAMA, MAREKANI.

“Zaidi ya asilimia 50 ya Warusi wanaamini kwa-mba ufisadi hauwezi kuepukwa na nisehemu ya kudumu ya maisha.”—RIA NOVOSTI, URUSI.

30 Amkeni! Februari 2011

MAZUNGUMZO YA FAMILIA

Ni Nini KimekosekanaKatika Picha Hii?Soma 2 Wafalme 4:8-10. Kisha utazame picha. Ni vitugani vimekosekana? Andika majibu yako kwenye mistariiliyo hapa chini. Unganisha nukta zilizopo ili ukamilishe pi-cha hii, kisha uipake rangi.

1 ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝

2 ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝

3 ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝ ˝

˘ Majibu ya ukurasa wa 30 na 31 kwenye ukurasa wa 28

ZUNGUMZENI PAMOJA: Mwa-namke huyu alionyesha fadhilijinsi gani? Ni kwa njia gani Yeho-va alibariki matendo yake yafadhili kwa sababu ya kumtege-meza nabii wake? DOKEZO:Soma 2 Wafalme 4:32-37. Ni kwanjia gani unaweza kuwaonyeshawatumishi wa Yehova fadhili leo?DOKEZO: Soma Waroma 12:13;Wagalatia 6:10.

UTENDAJI WA FAMILIA: Bilakusema jambo lolote, mshirikimmoja wa familia anaweza kuigi-za sehemu ya mtu mmoja katikasimulizi la Biblia lililotajwa hapojuu. Wengine katika familia waja-ribu kukisia mtu huyo ni nani.

MWANZO1

2

3

4

5

67

89

10

11

12 13

14

1516

17

18

1920

21

22

23

24

25

26

27

28

2930

31

32

3334

35

36

37

38

39

40

41

4243

MWISHO

Kusanya na Ujifunze Kata, kunja katikati, na uhifadhiD

AN

IEL

IK

AD

IY

AB

IBL

IA

2

D A N I E L I

MAMBO MACHACHE KUMHUSU Huendaalikuwa mwana wa mfalme, alizaliwakatika kabila la Yuda. Alikuwa nabiimwaminifu aliyeongozwa na roho yaMungu kuandika kitabu kilichoitwa kwajina lake. Huenda Danieli alikuwa kijanawakati yeye na watu wengine wa familia yakifalme na wakuu walipochukuliwa matekana Nebukadneza hadi Babiloni.

MASWALI

A. Kwa nini Danieli alitupwa katika shimola simba?

B. Rafiki watatu wa Danieli walikuwa namajina gani ya Kiebrania?

C. Danieli alitumikia chini ya falme ganimbili za kigeni?

MAJIBU

A. Alisali kwa Yehova ingawa aliamriwaasifanye hivyo.—Danieli 6:6-17.

B. Hanania, Mishaeli, Azaria.—Danieli 1:6, 7.

C. Babiloni na Muungano wa Umedi naUajemi.—Danieli 5:30; 6:8.

Watu na Nchi4. Majina yetu ni Jorge, Nicolas, na Priscilian. Tunaishinchini Belize, katika Amerika ya Kati. Kuna Mashahidiwangapi wa Yehova nchini Belize? Ni 600, 2,000, au3,500?

5. Ni alama gani inayoonyesha eneo ninaloishi?Chora duara kuzunguka alama hiyo, na uchorealama nyingine kuonyesha eneo unaloishi ki-sha uone kwenu ni umbali gani kutoka Belize.

WatotoWatafute PichaJe, unaweza kupata picha hizikatika toleo hili? Kwa manenoyako mwenyewe, eleza jambolinalotendeka katika kila picha.

40

26

K.W

.K.

Adam

uaum

bw

aAlii

shim

iaka

ya6

00

K.W

.K.

1W

.K.

98

W.K

.

Kita

bu

cha

mw

isho

cha

Bib

liaki

naandik

wa

Alichukuliwa kutokaYerusalemu hadiBabiloni

Yerusalemu

Babiloni

A

B

CD

g11 02-SW

˘ Hivyo ndivyo mama mmoja huko California, Marekani, ali-vyoandika kuhusu jambo linalozungumziwa katika kitabu Ji-funze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Alieleza hivi: “Juma lililopi-ta mwana wetu Javan, mwenye umri wa miaka 3, aliendakwa daktari, na daktari huyo akauliza ikiwa mimi na mumewangu tumemfundisha Javan kuhusu jinsi ya kulinda sehe-mu zake za siri. Nilifurahi kumweleza kuhusu kitabu Mwali-mu, kinachoeleza kwamba ni vibaya kwa mtu yeyote kuche-zea sehemu za siri za mtu mwingine. Daktari huyo alifurahisana kwamba tulikuwa tumezungumzia jambo hilo.”

Mama huyo alisema hivi pia: “Kitabu hicho kinazungumziamambo hayo kwa njia nzuri kabisa.” Sura ambayo mamahuyo alikuwa akizungumzia ina kichwa “Jinsi Yesu Alivyoli-ndwa.” Inafafanua jinsi Baba wa mbinguni wa Yesu alivyomli-nda Mwana wake asiumizwe na Mfalme Herode wakati Yesualipokuwa mchanga asiweze kujilinda. (Mathayo 2:7-23) Ki-tabu hicho kinaonyesha pia jinsi watoto wachanga wanavyo-weza kufundishwa kujilinda mtu anapojaribu kuwatendea vi-baya kingono.

Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho kilicho na ku-rasa 256 na picha zenye kuvutia kilicho na ukubwa kama wagazeti hili. Tafadhali jaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chinina kuituma ukitumia anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodhe-shwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

Wao Si Wachanga Sana

Q Bila masharti, ningepe-nda kupokea kitabu kili-choonyeshwa hapa.

Andika lugha unayotaka.

��������������������������������������

Q Ningependa kujifunzaBiblia nyumbani kwangubila malipo.

Jina �������������������������������������������������������������������������������������������

Anwani ��������������������������������������������������������������������������������������

�������������������������������������������������������������������������������������������������

Jiji/mji ���������������������������������������������������������������������������������������

Nchi ������������������������������������������������������������������������������������������

www.watchtower.org

JIFUNZE KUTOKA KWA

MWALIMU MKUU