BIBLIA INAFUNDISHA NINI Hasa? - Akamaihd.net

227
BIBLIA INAFUNDISHA NINI Hasa?

Transcript of BIBLIA INAFUNDISHA NINI Hasa? - Akamaihd.net

bh

-SW

15

01

22

BIBLIAINAFUNDISHA

NINI Hasa?BIBLIA

INAFUNDISHA

bh-SW

Omba ufundishwe Biblia bila malipo.

s

bh

-SW

15

01

22

BIBLIAINAFUNDISHA

NINI Hasa?

BIBLIAINAFUNDISH

Abh-SW

Omba ufundishwe Biblia bila malipo.

s

BIBLIAINAFUNDISHA

NINI Hasa?

Photo Credits: ˛ Page 7: Courtesy American Bible Society ˛ Page 19:Earth: NASA photo ˛ Pages 24-5: WHO photo by Edouard Boubat ˛ Pages 88-9:Explosion: Based on USAF photo; child: Based on WHO photo by W. Cutting

˘ 2005Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania

WACHAPISHAJIPrinted by Watch Tower Bible and Tract Society of South Africa NPC

1 Robert Broom Drive East, Rangeview, Krugersdorp, 1739, R.S.A.

Chapa ya Machi 2016

Kitabu hiki hakiuzwi. Ni sehemu ya kazi ya elimu ya Bibliaya ulimwenguni pote inayotegemezwa kwa michango ya hiari.

Isipokuwa iwe imeonyeshwa vingine,Maandiko yamenukuliwa kutoka katika

Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

What Does the Bible Really Teach?Swahili (bh-SW)

Made in the Republic of South AfricaKimefanyizwa Katika Jamhuri ya Afrika Kusini

KITABU HIKI NI CHA

SURA UKURASA

Je, Hivi Ndivyo Mungu Alivyokusudia? � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 3

1. Ukweli Kumhusu Mungu � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 8

2. Biblia—Kitabu Kutoka kwa Mungu � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 18

3. Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia? � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 27

4. Yesu Kristo Ni Nani? � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 37

5. Fidia—Zawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu � � � � � � � � � � � � � � 47

6. Wafu Wako Wapi? � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 57

7. Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa � � � � � 66

8. Ufalme wa Mungu Ni Nini? � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 76

9. Je, Tunaishi Katika “Siku za Mwisho”? � � � � � � � � � � � � � � � � � � 86

10. Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu � � � � � � 96

11. Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke? � � � � � � � � � � � � 106

12. Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu � � � � � � � � � � � � � � � � 115

13. Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 125

14. Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha � � � 134

15. Ibada Ambayo Mungu Anakubali � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 144

16. Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli � � � � � � � � � � � � 154

17. Mkaribie Mungu Katika Sala � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 164

18. Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu � � � � � � � � � � � � 174

19. Kaa Katika Upendo wa Mungu � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 184

Nyongeza � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 194

YALIYOMO

KATIKA magazeti, televisheni, na re-dio, kuna habari nyingi kuhusu visavya ugaidi, vita, na uhalifu. Hebufikiria pia mahangaiko yako mwenye-we. Labda unasumbuliwa na ugonjwafulani au umefiwa na mtu unayempe-nda. Huenda ukahisi kama alivyohisiAyubu, aliyesema kwamba maishayake yalikuwa ‘yamejaa masumbuko.’—Ayubu 10:15, Verbum Bible.

Hebu jiulize:

ˇ Je, hivi ndivyo Mungu alivyoku-sudia maisha yangu na yawanadamu wengine yawe?

ˇ Ninaweza kupata wapi msaada wakukabiliana na matatizo yangu?

ˇ Je, dunia itapata kuwa na amani?

Biblia inajibu maswali hayo kwanjia ya kuridhisha.

Je, Hivi Ndivyo MunguAlivyokusudia?

BIBLIA INAFUNDISHA KWAMBAMUNGU ATATIMIZA MAMBO

HAYA DUNIANI.

“Atafuta kila chozi kutoka katika machoyao, na kifo hakitakuwapo tena, walamaombolezo wala kilio wala maumivu

hayatakuwapo tena.”—Ufunuo 21:4

“Kilema atapandajuu kama vile paa

anavyofanya.”—Isaya 35:6

“Macho ya vipofuyatafunguliwa.”

—Isaya 35:5

4

‘Wale wote waliomondani ya makaburi yaukumbusho watatoka.’

—Yohana 5:28, 29

“Hakuna mkaajiatakayesema:

‘Mimi ni mgonjwa.’”—Isaya 33:24

“Kutakuwa na wingi wa nafakaduniani.”—Zaburi 72:16

FAIDIKA NA MAFUNDISHO YA BIBLIA

Usidhani kwamba mambo yali-yo kwenye kurasa zinazotangulia nindoto tu. Mungu ameahidi kwambaatatimiza mambo hayo, na Bibliainaeleza jinsi atakavyofanya hivyo.

Hata hivyo, Biblia ina faidanyingine nyingi. Inaweza ku-kusaidia kuwa na maishayenye kuridhisha hata sasa.Hebu tua kidogo, ufikiriemahangaiko na matatizoyako mwenyewe. Huendayanatia ndani ukosefu wapesa, matatizo ya familia,matatizo ya afya, au kifocha mpendwa. Biblia inawe-za kukusaidia kushughulikana matatizo leo na inaweza ku-kufariji kwa kujibu maswali kamahaya:

ˇ Kwa nini tunateseka?

ˇ Tunawezaje kushughulika na mahangaiko ya maisha?

ˇ Tunawezaje kufanya maisha ya familia yetu yawe yenyefuraha zaidi?

ˇ Inakuwaje tunapokufa?

ˇ Je, tutapata kuwaona wapendwa wetu waliokufa?

ˇ Tunawezaje kuwa na hakika kwamba Mungu atatimi-za ahadi zake kuhusu wakati ujao?

6 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Kusoma kitabu hiki kunaonyesha kwamba ungependa ku-jua yale ambayo Biblia inafundisha. Kitabu hiki kitakusaidia.Sehemu ya chini ya kurasa kuna maswali yanayoambata-na na mafungu. Mamilioni ya watu wamefurahia kuwana mazungumzo ya Biblia pamoja na Mashahidi wa Ye-hova kwa njia ya maswali na majibu. Tunatumaini kwambawewe pia utafurahia kufanya hivyo. Mungu na akubarikiunapochukua hatua hiyo yenye kusisimua na kuridhisha yakujifunza mambo ambayo Biblia inafundisha hasa!

IJUE BIBLIA YAKO

KUNA vitabu 66 katika Biblia. Kila kitabu kina sura na mi-stari, ili kurahisisha usomaji. Maandiko yanapotajwa kati-ka kitabu hiki, nambari inayofuata jina ndiyo sura ya kitabuau barua katika Biblia, nayo nambari inayofuata ni mstari.Kwa mfano, “2 Timotheo 3:16” ni barua ya pili kwa Timo-theo, sura ya 3, mstari wa 16.

Ukifungua na kusoma maandiko yaliyo katika kitabu hiki,utazoea kuitumia Biblia. Pia, mbona usianze kuisoma Bib-lia kila siku? Ukisoma sura tatu hadi tano hivi kila siku, una-weza kuisoma Biblia nzima kwa mwaka mmoja.

Je, Hivi Ndivyo Mungu Alivyokusudia? 7

JE, UMEWAHI kuona jinsi ambavyo watoto huuliza maswa-li? Wengi wao huanza kuuliza maswali mara tu wanapojuakuongea. Wanakutazama wakiwa wamekodoa macho kwahamu na kuuliza maswali kama vile: Kwa nini anga ni bluu?Kwa nini nyota zinametameta? Ni nani aliyewafundishandege kuimba? Huenda ukajaribu sana kujibu,lakini mara nyingi si rahisi. Hata baada yakuwapa jibu bora, huenda bado wakauliza:Kwa nini?

2 Si watoto peke yao wanaouliza ma-swali. Tunapoendelea kukua, sisi huulizamaswali. Tunauliza maswali ili tupatemwongozo, tujue hatari tunazohitaji kue-puka, au kwa sababu tu tunataka kujua.Hata hivyo, inaonekana kwambawatu wengi huacha kuuliza ma-swali, hasa yaliyo muhimu zaidi.Wao huacha kutafuta majibu.

3 Fikiria swali lililo katika jalada

1, 2. Kwa nini ni vizuri kuuliza maswali?3. Kwa nini watu wengi hawajitahidi kupata ma-jibu ya maswali muhimu zaidi?

SURA YA KWANZA

UkweliKumhusu Mungu

Je, kweli Mungu anakujali?

Mungu ana utu wa aina gani? Je, ana jina?

Je, tunaweza kuwa na uhusiano wakaribu pamoja na Mungu?

la kitabu hiki, maswali yaliyo katika utangulizi wa kitabuhiki, au yale yaliyo mwanzoni mwa sura hii. Hayo ni baadhiya maswali muhimu zaidi unayoweza kuuliza. Hata hivyo,watu wengi hawajitahidi kupata majibu ya maswali hayo.Kwa nini? Je, Biblia ina majibu? Watu fulani hufikiri kwa-mba Biblia haieleweki. Wengine huogopa kuuliza maswaliili wasiaibishwe au kudharauliwa. Hali wengine huamuakwamba maswali hayo yanaweza kujibiwa tu na viongozina walimu wa dini. Wewe unaonaje?

4 Bila shaka ungependa kupata majibu ya maswali mu-himu zaidi maishani. Haikosi, nyakati nyingine wewehujiuliza: ‘Maisha yana kusudi gani? Je, kusudi pekee la ma-isha ni kuzaliwa, kuzeeka, na kufa? Kwa kweli Mungu anautu gani?’ Ni vizuri kuuliza maswali kama hayo, na nimuhimu kutafuta majibu yenye kuridhisha na yenye kute-gemeka bila kukata tamaa. Yule mwalimu mashuhuri, YesuKristo, alisema hivi: “Endeleeni kuomba, nanyi mtapewa;endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi,nanyi mtafunguliwa.”—Mathayo 7:7.

5 ‘Ukiendelea kutafuta’ majibu ya maswali hayo muhi-mu, utafaidika sana. (Methali 2:1-5) Hata uwe umeambiwanini na watu wengine, kuna majibu, na unaweza kuya-pata katika Biblia. Majibu hayo si magumu, yasiyoeleweka.Isitoshe, yatakupa tumaini na shangwe. Na yanaweza ku-kusaidia kuishi maisha yenye kuridhisha sasa. Kwanza, natufikirie swali moja ambalo limewahangaisha watu wengi.

JE, MUNGU ANA HURUMA NA JE, ANAJALI?6 Watu wengi hujibu hapana. Wanasema, ‘Ikiwa Mungu

anajali, ulimwengu ungekuwa tofauti sana.’ Leo, ulimwe-ngu umejaa vita, chuki, na mateso. Isitoshe, kila mmoja

4, 5. Ni maswali gani muhimu zaidi tunayoweza kuuliza maishani,na kwa nini tutafute majibu?6. Kwa nini watu wengi wanafikiri kwamba Mungu hajali wanadamuwanapoteseka?

Ukweli Kumhusu Mungu 9

wetu huwa mgonjwa, huteseka, na kufiwa na wapendwawake. Ndiyo sababu watu wengi husema, ‘Ikiwa Munguanatujali na kuhangaikia matatizo yetu, kwa nini hazuiimambo hayo yasitupate?’

7 Isitoshe, nyakati nyingine walimu wa dini huwafanyawatu wafikiri kwamba Mungu hana huruma. Jinsi gani?Msiba unapotokea, wanasema ni mapenzi ya Mungu. Kwakweli, walimu hao wanamlaumu Mungu kwa sababu yamambo mabaya yanayotukia. Je, huo ndio ukweli kumhu-su Mungu? Biblia inafundisha nini hasa? Andiko la Yakobo1:13 linajibu: “Mtu akiwa chini ya jaribu, yeye asiseme:‘Mungu ananijaribu.’ Kwa maana Mungu hawezi kujaribi-wa na mambo maovu wala yeye mwenyewe hamjaribuyeyote.” Kwa hiyo, Mungu hasababishi kamwe uovu ambaounaona ulimwenguni. (Ayubu 34:10-12) Ni kweli kwambaanaacha mambo mabaya yatukie. Hata hivyo, kuna tofautikubwa kati ya kuacha jambo litukie na kulisababisha.

8 Kwa mfano, wazia baba mwenye hekima na busara ali-ye na mwana ambaye tayari ni mtu mzima na badoanaishi nyumbani kwa wazazi wake. Mwana huyo akiasi nakuamua kuondoka nyumbani, baba yake hamzuii. Mwa-na huyo anaishi maisha mapotovu na kupata matatizo. Je,baba ndiye aliyesababisha matatizo ya mwanaye? Hapana.(Luka 15:11-13) Vivyo hivyo, Mungu hawazuii wanadamuwakishaamua kufuata njia isiyofaa, hata hivyo hasababishimatatizo yanayowapata. Kwa hiyo, basi, si haki kumlaumuMungu kwa sababu ya matatizo yote yanayowapata wana-damu.

9 Mungu ana sababu nzuri za kuwaacha wanadamu wa-

7. (a) Walimu wa dini wamewafanyaje watu wengi wafikiri kwambaMungu hana huruma? (b) Biblia inafundisha nini hasa kuhusu maja-ribu ambayo huenda yakatupata?8, 9. (a) Unaweza kutumia mfano gani kuonyesha tofauti iliyopokati ya kuacha uovu uwepo na kuusababisha? (b) Kwa nini si haki ku-mlaumu Mungu kwa kuwaacha wanadamu wafuate njia isiyofaa?

10 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

fuate njia isiyofaa. Akiwa Muumba wetu mwenye hekimana nguvu, hahitaji kutueleza sababu hizo. Hata hivyo, Mu-ngu hutueleza kwa sababu ya upendo. Utajifunza kuhususababu hizo katika Sura ya 11. Lakini uwe na hakika kwa-mba Mungu hasababishi matatizo yanayotupata. Badalayake, anatupa tumaini pekee la utatuzi!—Isaya 33:2.

10 Isitoshe, Mungu ni mtakatifu. (Isaya 6:3) Hilo linama-anisha kwamba yeye ni safi wala hana uovu hata kidogo.Kwa hiyo, tunaweza kumtumaini kabisa. Hatuwezi ku-watumaini wanadamu ambao nyakati nyingine wanakuwawafisadi. Hata wanadamu wenye mamlaka ambao ni wa-nyoofu zaidi mara nyingi hawana uwezo wa kuondoamadhara yanayosababishwa na watu wabaya. Lakini Mu-ngu ana nguvu zote. Anaweza na ataondoa madhara yoteyanayowapata wanadamu kwa sababu ya uovu. Mungu ata-kapochukua hatua, atakomesha uovu milele!—Zaburi37:9-11.

MUNGU ANAHISIJE KUHUSU UKOSEFU WA HAKI?11 Mungu anahisije kuhusu mambo yanayoendelea uli-

mwenguni na maishani mwako? Kwanza kabisa, Bibliainafundisha kwamba Mungu ni “mpenda-haki.” (Zaburi37:28) Kwa hiyo anapendezwa sana na mambo yanayofaana kuchukizwa na mambo yasiyofaa. Anachukia ukosefuwa haki wa kila namna. Biblia inasema kwamba Mungu‘aliumia moyoni mwake’ uovu ulipokuwa mwingi duni-ani wakati uliopita. (Mwanzo 6:5, 6) Mungu hajabadilika.(Malaki 3:6) Bado anachukia kuona mateso yanayoende-lea ulimwenguni pote. Pia, Mungu anachukia kuona watuwakiteseka. Biblia inasema, “yeye anawajali ninyi.”—1 Pe-tro 5:7.

10. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba Mungu ataondoa ma-dhara yote yanayotokana na uovu?11. (a) Mungu anahisije kuhusu ukosefu wa haki? (b) Mungu anahi-sije kuhusu kuteseka kwako?

Ukweli Kumhusu Mungu 11

12 Tunawezaje kuwa na hakika kwamba Mungu anachukiakuona watu wakiteseka? Uthibitisho mwingine ndio huu.Biblia inafundisha kwamba Mungu alimuumba mtu kwamfano wake. (Mwanzo 1:26) Kwa hiyo, tuna sifa nzuri kwasababu Mungu ana sifa nzuri. Kwa mfano, je, wewe husu-mbuka unapowaona watu wasio na hatia wakiteseka? Ikiwaunasumbuka kwa sababu ya ukosefu huo wa haki, uwe nahakika kwamba Mungu husumbuka hata zaidi.

13 Jambo moja la pekee kuhusu wanadamu ni kwambatuna uwezo wa kuonyesha upendo. Mungu pia ana sifa hiyo.Biblia inafundisha kwamba “Mungu ni upendo.” (1 Yoha-na 4:8) Tuna upendo kwa sababu Mungu ana upendo.

Je, upendo ungekuchochea kukomeshamateso na ukosefu wa haki unaoonaulimwenguni? Kama ungekuwa nauwezo wa kufanya hivyo, je, ungeyako-mesha? Bila shaka ungeyakomesha!Uwe na hakika kwamba Mungu ata-komesha mateso na ukosefu wa haki.Ahadi zinazotajwa katika utangulizi wakitabu hiki si ndoto tu au matumainiyasiyo na msingi. Bila shaka ahadi zaMungu zitatimia! Hata hivyo, ili kua-mini ahadi hizo, unahitaji kujua mengizaidi kumhusu Mungu anayezitoa.

MUNGU ANATAKA UMJUE14 Ukitaka mtu akujue, unaweza ku-

12, 13. (a) Kwa nini tuna sifa nzuri kamavile upendo, nao upendo unatufanya tuwena maoni gani kuhusu ulimwengu? (b) Kwanini unaweza kuwa na hakika kwamba Mu-ngu atachukua hatua kuhusiana na matatizoya ulimwengu?14. Mungu anaitwa nani, na kwa nini tuna-paswa kulitumia jina lake?

Unapotakamtu akujue,unamwambiajina lako,sivyo? Munguanatujulisha jinalake katikaBiblia

12 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

fanya nini? Utamwambia jina lako, sivyo? Je, Mungu anajina? Dini nyingi hujibu kwamba jina lake ni “Mungu” au“Bwana,” lakini hayo si majina yake binafsi. Hayo ni majinaya heshima kama vile “mfalme” na “rais.” Biblia inafundi-sha kwamba Mungu ana majina mengi ya heshima. Baadhiya majina hayo ni “Mungu” na “Bwana.” Hata hivyo, Bibliainafundisha pia kwamba Mungu ana jina lake binafsi, yaa-ni, Yehova. Andiko la Zaburi 83:18 linasema hivi: “Wewe,ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye UliyeJuu Zaidi, juu ya dunia yote.” Ikiwa Biblia yako haina jinahilo, unaweza kutazama Nyongeza iliyo kwenye ukurasa wa195-197 wa kitabu hiki ili ujue ni kwa nini. Ukweli ni

Biblia inafundisha kwambaYehova ni Muumba wa ulimwengu

mwenye upendo

kwamba jina la Mungu linapatikana mara elfu kadhaa kati-ka hati za zamani za Biblia. Kwa hiyo, Yehova anataka ulijuejina lake na kulitumia. Tunaweza kusema kwamba anatu-mia Biblia kujitambulisha kwako.

15 Mungu alijipa jina lenye maana. Jina lake, Yeho-va, linamaanisha kwamba anaweza kutimiza ahadi yoyoteanayotoa na kufanya jambo lolote analokusudia.� Jina laMungu ni la pekee, halina kifani. Ni lake peke yake. Yehovani wa pekee katika njia mbalimbali. Jinsi gani?

16 Tuliona kwamba andiko la Zaburi 83:18 linasema hivi

� Unaweza kupata habari zaidi kuhusu maana ya jina la Mungu na ji-nsi linavyotamkwa katika Nyongeza iliyo kwenye ukurasa wa 195-197.

15. Jina Yehova linamaanisha nini?16, 17. Tunaweza kujifunza nini kumhusu Yehova kutokana na maji-na haya ya heshima: (a) “Mweza-Yote”? (b) “Mfalme wa umilele”?(c) “Muumba”?

Upendo wababa kwa watotowake unaonyeshaupendo mkubwa

zaidi ambao Babayetu wa mbinguni

anatuonyesha

14 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

kumhusu Yehova: “Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi.”Vivyo hivyo, Yehova peke yake ndiye anayeitwa “Mweza-Yote.” Andiko la Ufunuo 15:3 linasema: “Matendo yako nimakuu na ya ajabu, Yehova Mungu, Mweza-Yote. Njia zakoni za uadilifu na za kweli, Mfalme wa umilele.” Jina“Mweza-Yote” linatufundisha kwamba Yehova ndiye mwe-nye nguvu zaidi kuliko wote. Nguvu zake hazina kifani; ninyingi sana. Nalo jina “Mfalme wa umilele” linatukumbu-sha kwamba Yehova ni wa pekee katika njia nyingine. Yeyepeke yake ndiye amekuwapo nyakati zote. Andiko la Zaburi90:2 linasema: “Tangu wakati usio na kipimo mpaka wakatiusio na kipimo [au, milele] wewe ni Mungu.” Maneno hayoyanatuchochea tumheshimu, sivyo?

17 Pia, Yehova ni wa pekee kwa sababu yeye peke yakendiye Muumba. Andiko la Ufunuo 4:11 linasema: “Unasta-hili, Ee Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu naheshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote, na kwasababu ya mapenzi yako vilikuwako navyo vikaumbwa.”Kila kitu unachoweza kuwazia, iwe viumbe wa roho mbi-nguni ambao hawaonekani, nyota zinazotapakaa katikaanga la usiku, matunda yanayokua mitini, au samaki waliobaharini na kwenye mito, vyote vipo kwa sababu Yehovandiye Muumba!

JE, UNAWEZA KUMKARIBIA YEHOVA?18 Kusoma kuhusu sifa za Yehova za ajabu, huwafanya

watu fulani wamwogope. Wanahisi kwamba Mungu yukojuu sana wasiweze kumkaribia, nao ni duni machoni pake.Lakini je, hayo ni maoni yanayofaa? Biblia haifundishi hi-vyo. Inasema hivi kumhusu Yehova: “Hayuko mbali sanana kila mmoja wetu.” (Matendo 17:27) Hata Biblia inatu-himiza hivi: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.”—Yakobo 4:8.

18. Kwa nini watu fulani wanahisi kwamba hawawezi kamwe kumka-ribia Mungu, lakini Biblia inafundisha nini?

Ukweli Kumhusu Mungu 15

19 Unawezaje kumkaribia Mungu? Kwanza kabisa, ende-lea kujifunza kumhusu kama unavyofanya sasa. Yesualisema: “Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupa-ta ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, najuu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.” (Yohana 17:3) Naam,Biblia inafundisha kwamba kujifunza kumhusu Yehova naYesu huongoza kwenye “uzima wa milele”! Kama tulivyoo-na, “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:16) Pia, Yehova anasifa nyingine nyingi nzuri zenye kuvutia. Kwa mfano, Bib-lia inasema kwamba Yehova ni “Mungu mwenye rehemana neema, si mwepesi wa hasira naye ni mwingi wa fadhi-li zenye upendo na kweli.” (Kutoka 34:6) Yeye ni ‘mwemana yuko tayari kusamehe.’ (Zaburi 86:5) Mungu ana subira.(2 Petro 3:9) Yeye ni mshikamanifu. (Ufunuo 15:4) Kadiriunavyozidi kujifunza mengi katika Biblia, ndivyo utakavyo-zidi kujua jinsi Yehova ameonyesha sifa hizo na nyinginenyingi zenye kuvutia.

20 Ni kweli kwamba huwezi kumwona Mungu kwa sa-babu yeye ni roho asiyeonekana. (Yohana 1:18; 4:24;1 Timotheo 1:17) Hata hivyo, ukijifunza kumhusu katikaBiblia, utaujua utu wake. Kama mtunga-zaburi alivyose-ma, unaweza “kuuona uzuri wa Yehova.” (Zaburi 27:4;Waroma 1:20) Unapozidi kujifunza kumhusu Yehova, ata-kuwa halisi zaidi kwako nawe utampenda na kumkaribiazaidi.

21 Utaelewa hatua kwa hatua ni kwa nini Biblia inatufu-ndisha kumwona Yehova kuwa Baba yetu. (Mathayo 6:9)Mbali na kwamba ametupa uhai, anataka tuwe na mai-sha bora iwezekanavyo, kama vile baba yeyote mwenyeupendo angewatakia watoto wake. (Zaburi 36:9) Pia, Biblia

19. (a) Tunawezaje kuanza kumkaribia Mungu, nasi tutapata faidagani? (b) Ni sifa gani za Mungu zinazokuvutia zaidi?20-22. (a) Kwa kuwa hatuwezi kumwona Mungu, je, inamaanishakwamba hatuwezi kumkaribia? Eleza. (b) Huenda watu fulani wasiona nia mbaya wakakusihi ufanye nini, lakini unapaswa kufanya nini?

16 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

inafundisha kwamba wanadamu wanaweza kuwa rafiki zaYehova. (Yakobo 2:23) Hebu wazia—wewe unaweza kuwarafiki ya Muumba wa ulimwengu!

22 Unapoendelea kujifunza mengi zaidi katika Biblia,huenda watu fulani wasio na nia mbaya wakakusihi ua-che kujifunza. Huenda wakaogopa kwamba utabadili diniyako. Lakini usimruhusu mtu yeyote akuzuie kufanya ura-fiki pamoja na Mungu.

23 Ni kweli kwamba kuna mambo ambayo hutaelewamwanzoni. Unyenyekevu unahitajiwa ili kuomba msaada,lakini usisite kuuliza kwa sababu ya aibu. Yesu alisema kwa-mba ni vizuri kuwa mnyenyekevu kama mtoto mchanga.(Mathayo 18:2-4) Kama tujuavyo, watoto huuliza maswalimengi. Mungu anataka upate majibu. Biblia inawasifuwatu waliokuwa na hamu ya kujifunza kumhusu Mungu.Waliyachunguza Maandiko kwa uangalifu ili kuhakikishakwamba mambo waliyokuwa wakijifunza ni ya kweli.—Ma-tendo 17:11.

24 Njia bora zaidi ya kujifunza kumhusu Yehova ni kui-chunguza Biblia. Biblia ni tofauti na vitabu vingine vyote.Jinsi gani? Sura inayofuata itazungumzia habari hiyo.

23, 24. (a) Kwa nini unapaswa kuendelea kuuliza maswali kuhusumambo unayojifunza? (b) Ni habari gani itakayozungumziwa katikasura inayofuata?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Mungu anakujali.—1 Petro 5:7.

ˇ Jina la Mungu ni Yehova.—Zaburi 83:18.

ˇ Yehova anataka umkaribie.—Yakobo 4:8.

ˇ Yehova ana upendo, fadhili, na rehema.—Kutoka 34:6; 1 Yohana 4:8, 16.

Ukweli Kumhusu Mungu 17

HEBU wazia jinsi ulivyohisi ulipopata zawadi ya pekee ku-toka kwa rafiki yako. Haikosi ulisisimuka na kufurahikwelikweli. Mtu anapokupa zawadi anaonyesha kwambaanakuthamini. Bila shaka, ulimshukuru rafiki yako kwa sa-babu ya zawadi hiyo.

2 Biblia ni zawadi kutoka kwa Mungu, nasi tunapaswakuithamini kwelikweli. Kitabu hicho cha pekee hufunuamambo ambayo hatungejua kwa njia nyingine yoyote.Kwa mfano, Biblia hutuambia kuhusu kuumbwa kwa mbi-ngu zenye nyota, dunia, hali kadhalika mwanamume namwanamke wa kwanza. Biblia ina kanuni zenye kutegeme-ka zinazotusaidia kukabiliana na matatizo na mahangaikoya maisha. Inaeleza jinsi Mungu atakavyotimiza kusudilake na kuleta hali bora duniani. Biblia ni zawadi nzurikama nini!

3 Pia, Biblia ni zawadi inayochangamsha moyo kwa sa-babu inatueleza jambo fulani kumhusu Mpaji mwenyewe,

1, 2. Kwa nini tunaweza kusema kwamba Biblia ni zawadi nzuri kuto-ka kwa Mungu?3. Yehova anaonyesha nini kwa kutupa Biblia, na kwa nini hilo lina-tuchangamsha?

SURA YA PILI

Biblia—Kitabu Kutoka kwa Mungu

Biblia inatofautianaje na vitabu vingine?

Biblia inawezaje kukusaidia kukabilianana matatizo yako?

Kwa nini unaweza kuamini unabiimbalimbali ulio katika Biblia?

Yehova Mungu. Kwa kuwa ametupa Biblia, ni wazi kwambaanataka tumjue vizuri. Kwa kweli, Biblia inaweza kukusaidiakumkaribia Yehova.

4 Leo, watu wengi wana Biblia. Biblia imechapishwa kati-ka lugha zaidi ya 2,300 ikiwa nzima au kwa sehemu na kwahiyo zaidi ya asilimia 90 ya watu ulimwenguni wanaweza ku-ipata. Kwa wastani, Biblia zaidi ya milioni moja hugawanywakila juma! Mabilioni ya nakala za Biblia zimechapishwa ziki-wa nzima au kwa sehemu. Kwa kweli, hakuna kitabu kinginekilicho kama Biblia.

5 Isitoshe, Biblia ‘imeongozwa na roho ya Mungu.’ (2 Timo-theo 3:16) Jinsi gani? Bibliayenyewe inajibu hivi: “Wanadamuwalisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa naroho takatifu.” (2 Petro 1:21) Kwa mfano: Huenda babu aka-mwomba mjukuu wake amwandikie barua. Mjukuu huyoataandika mawazo na maagizo ya babu huyo. Kwa hiyo, kwakweli barua hiyo ni ya babu huyo wala si ya mjukuu wake.Vivyo hivyo, Biblia ina ujumbe wa Mungu wala si wa watu

4. Ni nini kinachokupendeza kuhusu kugawanywa kwa Biblia?5. Biblia ‘imeongozwa na roho ya Mungu’ jinsi gani?

“Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya”inapatikana katika lugha nyingi

19

waliotumiwa kuiandika. Kwa hiyo, Biblia kwa kweli ni “nenola Mungu.”—1 Wathesalonike 2:13.

NI SAHIHI NA YENYE UPATANO6 Biblia iliandikwa kwa kipindi cha zaidi ya miaka 1,600.

Walioiandika walikuwa watu wa hali mbalimbali walioishinyakati tofauti. Baadhi yao walikuwa wakulima, wavuvi, nawachungaji. Wengine walikuwa manabii, waamuzi, na wa-falme. Luka aliyeandika Injili alikuwa daktari. Licha yamalezi mbalimbali ya watu walioiandika, Biblia ina upatanotangu mwanzo mpaka mwisho.�

7 Kitabu cha kwanza cha Biblia kinatuambia jinsi matatizoya wanadamu yalivyoanza. Kitabu cha mwisho kinaonyeshakwamba dunia yote itakuwa paradiso, au bustani. Biblia nzi-ma inazungumzia mambo ambayo yametukia kwa maelfuya miaka, na kila sehemu inatusaidia kuelewa jinsi kusudi laMungu linavyotimizwa. Upatano wa Biblia hauna kifani, nahilo halishangazi kwa kuwa Biblia ni kitabu kutoka kwa Mu-ngu.

8 Biblia ni sahihi kisayansi. Hata ilizungumzia mambo ya-liyokuja kugunduliwa baadaye. Kwa mfano, kitabu chaMambo ya Walawi kina sheria walizopewa Waisraeli wazamani kuhusu usafi na kuwatenga wagonjwa ili kuepu-ka maambukizo ingawa mataifa jirani hayakujua mambohayo. Wakati ambapo watu walikuwa na maoni yasiyo sahi-hi kuhusu umbo la dunia, Biblia ilisema kwamba dunia nimviringo au duara. (Isaya 40:22) Biblia ilisema kwa usahihikwamba dunia ‘imetundikwa pasipo na kitu.’ (Ayubu 26:7)Biblia si kitabu cha sayansi. Hata hivyo, inapozungumzia

� Ijapokuwa watu fulani husema kwamba sehemu fulani za Bibliazinapingana, madai hayo hayana msingi. Ona sura ya 7 ya kitabu Bib-lia—Neno la Mungu au la Binadamu? kilichochapishwa na Mashahi-di wa Yehova.

6, 7. Kwa nini upatano wa Biblia ni wa pekee sana?8. Toa mifano inayoonyesha kwamba Biblia ni sahihi kisayansi.

20 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

mambo ya sayansi, hufanya hivyo kwa usahihi. Tunatarajiakitabu kutoka kwa Mungu kiwe hivyo, sivyo?

9 Pia, Biblia ni sahihi na inategemeka kuhusu mambo yakihistoria. Inasimulia mambo hususa yaliyotokea. Mbali nakutaja majina ya watu, inaonyesha pia ukoo wao.� Tofautina wanahistoria wa ulimwengu ambao mara nyingi hawatajikushindwa kwa mataifa yao, waandikaji wa Biblia walikuwawanyoofu, hata waliandika kuhusu makosa yao wenye-we na ya taifa lao. Kwa mfano, katika kitabu cha Bibliacha Hesabu, mwandikaji Musa anakiri kosa lake kubwa li-lilofanya aadhibiwe vikali. (Hesabu 20:2-12) Si rahisi kuonaunyoofu wa aina hiyo katika masimulizi mengine ya kihisto-ria lakini unapatikana katika Biblia kwa sababu ni kitabu chaMungu.

KITABU CHENYE HEKIMA10 Biblia ‘ni yenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia,

kwa kunyoosha mambo,’ kwa sababu imeongozwa na rohoya Mungu. (2 Timotheo 3:16) Naam, Biblia ni kitabu chenyefaida. Inaeleza kinaganaga hali ya wanadamu. Hilo halisha-ngazi kwa kuwa Mtungaji wake ni Yehova Mungu, Muumba!Anaelewa fikira na hisia zetu kuliko tunavyozielewa. Isitoshe,Yehova anajua tunachohitaji ili tuwe na furaha. Anajua piamambo tunayopaswa kuepuka.

11 Fikiria yale yanayoitwa Mahubiri ya Mlimani ya Yesu ka-tika Mathayo sura ya 5 mpaka ya 7. Katika mahubiri hayobora, Yesu alizungumzia mambo mbalimbali kama vile jinsi

� Kwa mfano, angalia ukoo wa Yesu unaofafanuliwa katika Luka 3:23-38.

9. (a) Biblia ni sahihi na inategemeka kihistoria jinsi gani? (b) Unaji-funza nini kuhusu Biblia kutokana na unyoofu wa watu walioiandika?10. Kwa nini haishangazi kwamba Biblia ni kitabu chenye faida?11, 12. (a) Yesu alizungumzia mambo gani katika Mahubiri yake yaMlimani? (b) Ni mambo gani mengine muhimu yanayozungumziwakatika Biblia, na kwa nini shauri lake lina faida sikuzote?

Biblia—Kitabu Kutoka kwa Mungu 21

ya kupata furaha ya kweli, jinsi ya kutatua mizozano, jinsi yakusali, na jinsi ya kuwa na maoni yanayofaa kuelekea vituvya kimwili. Maneno ya Yesu yanachochea na yana faida leokama yalivyokuwa alipoyasema.

12 Kanuni fulani za Biblia zinahusu maisha ya familia, ma-zoea ya kazi, na mahusiano pamoja na wengine. Kanuni zaBiblia zinawahusu watu wote, na shauri lake ni lenye fai-da sikuzote. Kupitia nabii Isaya, Mungu anataja hekima iliyo

Isaya, mwandikajiwa Biblia alitabirikuanguka kwaBabiloni

katika Biblia: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayeku-fundisha ili ujifaidi mwenyewe.”—Isaya 48:17.

KITABU CHA UNABII13 Biblia ina unabii mwingi, baadhi yake umetimizwa. Kwa

mfano, kupitia nabii Isaya aliyeishi katika karne ya naneK.W.K., Yehova alitabiri kwamba jiji la Babiloni lingeha-ribiwa.� (Isaya 13:19; 14:22, 23) Habari hususa zilitolewakuonyesha jinsi ambavyo uharibifu huo ungetokea. Majeshiyanayovamia yangekausha mto wa Babiloni na kuingia jijinibila hata kupigana. Si hayo tu. Unabii wa Isaya hata ulitajajina la mfalme ambaye angeshinda Babiloni, yaani, Koreshi.—Isaya 44:27–45:2.

14 Miaka 200 hivi baadaye, usiku wa Oktoba 5/6,539 K.W.K., jeshi lilipiga kambi karibu na Babiloni. Ni nanialiyekuwa amiri wa jeshi hilo? Mfalme wa Uajemi anayeitwaKoreshi. Kwa hiyo, wakati ulikuwa umefika wa kutimizwakwa unabii huo wa ajabu. Lakini je, jeshi la Koreshi lingeva-mia Babiloni bila kupigana kama ilivyotabiriwa?

15 Wababiloni walikuwa na sherehe usiku huo na walihisiwakiwa salama katika jiji hilo lenye kuta kubwa. Wakati hu-ohuo, Koreshi alikuwa akigeuza kwa ustadi mkondo wa majiya mto uliokuwa ukipita katika jiji hilo. Muda si muda majiyalikuwa yamepungua kiasi cha kwamba majeshi yake ya-ngeweza kuvuka mto na kukaribia kuta za jiji. Hata hivyo,jeshi la Koreshi lingeingiaje Babiloni lenye kuta kubwa? Kwasababu moja au nyingine, usiku huo malango ya jiji hilo ha-yakuwa yamefungwa!

� Ufupisho K.W.K. humaanisha “Kabla ya Wakati wa Kawaida,”ambao ni sahihi zaidi kuliko K.K. (“Kabla ya Kristo”). Ufupisho W.K.humaanisha “Wakati wa Kawaida,” ambao mara nyingi huitwa A.D.,au Anno Domini, ikimaanisha “Katika Mwaka wa Bwana Wetu.”

13. Yehova alimwongoza nabii Isaya aandike habari gani hususa ku-husu Babiloni?14, 15. Unabii wa Isaya kuhusu Babiloni ulitimizwaje?

Biblia—Kitabu Kutoka kwa Mungu 23

16 Ilitabiriwa hivi kuhusu Babiloni: “Hatakaliwa kamwe,wala hatakuwa na makao kwa kizazi baada ya kizazi. Na hapoMwarabu hatapiga hema lake, na hakuna wachungaji wata-kaoruhusu makundi yao kulala hapo.” (Isaya 13:20) Unabiihuo ulitabiri hata mambo ambayo yangetokea baada ya jijihilo kuanguka. Ulionyesha kwamba jiji la Babiloni lingeachwaukiwa daima. Unaweza kuona utimizo wa maneno hayo.Eneo lenye ukiwa la Babiloni la kale, kilometa 80 hivi kusinimwa Baghdad, nchini Iraq, linathibitisha kwamba unabii huuwa Yehova kupitia nabii Isaya umetimizwa: “Nami nitamfagiakwa ufagio wa maangamizi.”—Isaya 14:22, 23.�

17 Kuchunguza jinsi Biblia ilivyo kitabu chenye unabii wakutegemeka ni jambo lenye kuimarisha imani, sivyo? Ikiwa

� Unaweza kupata habari zaidi kuhusu unabii wa Biblia, katika bro-shua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, ukurasa wa 27-29, iliyochapishwana Mashahidi wa Yehova.

16. (a) Isaya alitabiri nini kuhusu mambo ambayo yangepata jijila Babiloni? (b) Unabii wa Isaya kuhusu ukiwa wa Babiloni ulitimi-zwaje?17. Kutimizwa kwa unabii wa Biblia kunaimarishaje imani?

24 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Yehova tayari ametimiza ahadi zake za wakati uliopita, tunakila sababu ya kuamini kwamba atatimiza pia ahadi yakeya kuifanya dunia iwe paradiso. (Hesabu 23:19) Kwa kwelituna “tumaini la uzima wa milele ambao Mungu, asiyewe-za kusema uwongo, aliahidi nyakati za zamani za kale.”—Tito1:2.�

“NENO LA MUNGU LIKO HAI”18 Kutokana na mambo ambayo tumechunguza katika

sura hii, ni wazi kwamba kwa kweli Biblia ni kitabu chapekee. Hata hivyo, thamani yake haitokani tu na upatano

� Kuharibiwa kwa Babiloni ni mfano mmoja tu wa unabii wa Bib-lia ambao umetimizwa. Mifano mingine inatia ndani kuharibiwa kwaTiro na Ninawi. (Ezekieli 26:1-5; Sefania 2:13-15) Pia, unabii wa Da-nieli ulitabiri milki za ulimwengu ambazo zingetawala baada ya Babi-loni. Zilitia ndani Ugiriki na muungano wa Umedi na Uajemi. (Danieli8:5-7, 20-22) Unaweza kupata habari zaidi kuhusu unabii mbalimba-li unaomhusu Masihi uliotimizwa na Yesu Kristo, katika Nyongezailiyo kwenye ukurasa wa 199-201.

18. Mtume Mkristo Paulo anasema maneno gani yenye kuchocheakuhusu “neno la Mungu”?

Magofu ya Babiloni

Biblia—Kitabu Kutoka kwa Mungu 25

wake, usahihi wake wa kisayansi na wa kihistoria, hekimailiyomo, na unabii uliomo unaotegemeka. Mtume MkristoPaulo aliandika: “Neno la Mungu liko hai nalo lina nguvuna ni lenye makali zaidi kuliko upanga wowote wenye ma-kali kuwili nalo huchoma hata kufikia kugawanya nafsi naroho, na viungo na urojorojo wake, nalo linaweza kutambuafikira na makusudio ya moyo.”—Waebrania 4:12.

19 Kusoma “neno” la Mungu au ujumbe ulio katika Bib-lia kunaweza kubadili maisha yetu. Kunaweza kutusaidiatujichunguze vizuri zaidi. Huenda tukadai kwamba tuna-mpenda Mungu, lakini jinsi tunavyoitikia mafundisho yaNeno lake, Biblia, lililoongozwa na roho kutaonyesha wazimawazo yetu na hata mwelekeo wa moyo wetu.

20 Kwa kweli, Biblia ni kitabu kutoka kwa Mungu. Ni ki-tabu ambacho tunapaswa kusoma, kujifunza, na kukipenda.Onyesha kwamba unaithamini zawadi hiyo kutoka kwa Mu-ngu kwa kuendelea kujifunza yaliyomo. Kwa kufanya hivyo,utaelewa hata zaidi kusudi la Mungu kwa wanadamu. Surainayofuata itazungumzia kusudi hilo na jinsi litakavyotimi-zwa.

19, 20. (a) Biblia inawezaje kukusaidia ujichunguze? (b) Unawezajekuonyesha kwamba unaithamini Biblia ikiwa zawadi ya pekee kutokakwa Mungu?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Biblia imeongozwa na roho ya Mungu nakwa hiyo ni sahihi na inategemeka.—2 Timo-theo 3:16.

ˇ Habari iliyo katika Neno la Mungu inahusumaisha ya kila siku.—Isaya 48:17.

ˇ Ahadi za Mungu zilizo katika Biblia zitatimi-zwa hakika.—Hesabu 23:19.

26 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

KUSUDI la Mungu kwa dunia ni zuri ajabu. Yehova ana-taka dunia ijae watu wenye furaha na afya. Biblia inasemakwamba ‘Mungu alipanda bustani katika Edeni na kuchi-pusha kila mti wenye kutamanika kwa macho ya mtu naulio mwema kwa chakula.’ Baada ya Mungu kumuumbamwanamume na mwanamke wa kwanza, Adamu na Hawa,aliwaweka katika makao hayo mazuri na kuwaambia: “Zae-ni, muwe wengi, mjaze dunia na kuitiisha.” (Mwanzo 1:28;2:8, 9, 15) Kwa hiyo Mungu alikusudia wanadamu wawe nawatoto, waieneze bustani hiyo duniani pote, na kuwatunzawanyama.

2 Je, unafikiri kusudi la Yehova Mungu kwamba wana-damu waishi katika dunia iliyo paradiso litatimia? Munguanasema hivi: “Mimi nimesema hilo; pia nitalitimiza.” (Isa-ya 46:9-11; 55:11) Naam, Mungu atatimiza kusudi lake!Kuhusu dunia, anasema kwamba “hakuiumba tu bila saba-bu,” bali “aliiumba ili ikaliwe na watu.” (Isaya 45:18)Mungu alitaka dunia ikaliwe na watu wa aina gani? Nayealitaka wakae humo kwa muda gani? Biblia inajibu: “Wa-adilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juuyake.”—Zaburi 37:29; Ufunuo 21:3, 4.

1. Ni nini kusudi la Mungu kwa dunia?2. (a) Tunajuaje kwamba kusudi la Mungu kwa dunia litatimia?(b) Biblia inasema nini kuhusu wanadamu kuishi milele?

SURA YA TATU

Mungu Ana KusudiGani kwa Dunia?

Mungu ana kusudi gani kwa wanadamu?

Mungu amepingwaje?

Maisha yatakuwaje duniani wakati ujao?

3 Ni wazi kwamba kusudi la Mungu halijatimia bado.Leo watu wanakuwa wagonjwa na kufa; hata wanapiga-na na kuuana. Mambo yaliharibika. Hata hivyo, hapanashaka kwamba Mungu hakukusudia dunia iwe kama ili-vyo leo! Ni nini kilichotukia? Kwa nini kusudi la Munguhalijatimia? Hakuna kitabu chochote cha kihistoria kili-choandikwa na mwanadamu kinaweza kutuambia kwasababu matatizo yalianzia mbinguni.

ADUI ATOKEA4 Kitabu cha kwanza cha Biblia kinataja kuhusu mpinza-

ni wa Mungu aliyetokea katika bustani ya Edeni. Anaitwa“nyoka,” ingawa hakuwa mnyama halisi. Katika kitabu chamwisho cha Biblia anaitwa “Ibilisi na Shetani, anayeipoto-sha dunia nzima inayokaliwa.” Pia anaitwa “yule nyoka wazamani.” (Mwanzo 3:1; Ufunuo 12:9) Malaika huyo mwe-nye nguvu, au kiumbe asiyeonekana mwenye mwili wakiroho, alitumia nyoka kuzungumza na Hawa, kama vilemtu mwenye ustadi anavyoweza kufanya ionekane kanakwamba sauti inatoka katika mwanasesere au sanamu. Bilashaka kiumbe huyo alikuwapo Mungu alipokuwa akiitaya-risha dunia kwa ajili ya wanadamu.—Ayubu 38:4, 7.

5 Kwa kuwa uumbaji wote wa Yehova ni mkamilifu, basi,ni nani aliyemfanya “Shetani Ibilisi”? Kwa ufupi, mmojakati ya wana wenye nguvu wa Mungu aligeuka akawa Ibili-si. Jinsi gani? Leo mtu ambaye wakati fulani alikuwa mzurina mnyoofu anaweza kugeuka na kuwa mwizi. Hilo lina-wezekanaje? Huenda mtu akaruhusu tamaa mbaya iingiemoyoni mwake. Akiendelea kuisitawisha, tamaa hiyo ina-weza kuwa na nguvu sana. Kisha akipata nafasi, anaweza

3. Ni hali gani zenye kuhuzunisha zilizopo duniani leo, na ni maswa-li gani yanayozuka?4, 5. (a) Ni nani hasa aliyetumia nyoka kuzungumza na Hawa?(b) Mtu aliyekuwa mzuri na mnyoofu anawezaje kugeuka na kuwamwizi?

28 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

kutenda kulingana na tamaa hiyo mbaya ambayo imeku-wa ikisitawi moyoni mwake.—Yakobo 1:13-15.

6 Ndivyo ilivyokuwa kuhusu Shetani Ibilisi. Huendaalimsikia Mungu akiwaambia Adamu na Hawa wazae wa-toto na kuijaza dunia. (Mwanzo 1:27, 28) Haikosi Shetanialiwaza hivi: ‘Kwani, si wanadamu hao wote wanaweza ku-niabudu mimi badala ya kumwabudu Mungu!’ Kwa hiyo,tamaa mbaya ikaanza kusitawi moyoni mwake. Mwisho-we, akaamua kumdanganya Hawa kwa kumwambiauwongo kumhusu Mungu. (Mwanzo 3:1-5) Basi, akawa“Ibilisi,” jina linalomaanisha “Mchongezi.” Wakati huo-huo akawa “Shetani,” jina linalomaanisha “Mpinzani.”

7 Kwa kutumia uwongo na ujanja, Shetani Ibilisi aliwafa-nya Adamu na Hawa wamwasi Mungu. (Mwanzo 2:17; 3:6)Mwishowe, wakafa kwa sababu ya uasi kama Mungu ali-vyokuwa amesema. (Mwanzo 3:17-19) Kwa kuwa Adamualipoteza ukamilifu alipoasi, wazao wake wote walirithidhambi kutoka kwake. (Waroma 5:12) Hali hiyo inawezakulinganishwa na sufuria inayotumiwa kuoka mikate. Iki-wa sufuria hiyo imejikunja, kila mkate utakaookwa katikasufuria hiyo utakuwaje? Kila mkate utakuwa na alama, aukasoro. Vivyo hivyo, kila mwanadamu amerithi “kasoro”ya kutokamilika kutoka kwa Adamu. Ndiyo sababu wana-damu wote huzeeka na kufa.—Waroma 3:23.

8 Shetani alipowashawishi Adamu na Hawa wafanyedhambi dhidi ya Mungu, alianzisha uasi. Alikuwa akipingautawala wa Yehova. Ni kana kwamba Shetani aliku-wa akisema: ‘Mungu ni mtawala mbaya. Yeye husemauwongo na kuwanyima raia wake vitu vizuri. Wanadamu

6. Mmoja kati ya wana wenye nguvu wa Mungu aligeukaje na kuwaShetani Ibilisi?7. (a) Kwa nini Adamu na Hawa walikufa? (b) Kwa nini wazao wotewa Adamu huzeeka na kufa?8, 9. (a) Yaelekea Shetani alidai nini? (b) Kwa nini Mungu hakuwa-haribu waasi hao mara moja?

Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia? 29

hawahitaji kutawaliwa na Mungu. Wanaweza kujiamuliayaliyo mema na mabaya. Na watakuwa na maisha mazu-ri zaidi nikiwatawala.’ Mungu angeshughulikiaje upinzanihuo? Watu fulani husema kwamba afadhali Mungu ange-waua tu waasi hao. Lakini je, kufanya hivyo kungetatua

Shetani angewezaje kumwahidiYesu falme zote za ulimwengu

ikiwa hazikuwa zake?

30 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

upinzani wa Shetani? Je, kungethibitisha kwamba utawalawa Mungu ndio unaofaa?

9 Yehova hangewaua waasi hao mara moja kwa sababuyeye ni Mungu mwenye haki kabisa. Aliamua kwamba wa-kati ulihitajiwa ili kutatua upinzani wa Shetani kwa njiayenye kuridhisha na kuthibitisha kwamba Ibilisi ni mwo-ngo. Kwa hiyo Mungu akaamua kwamba atawaachawanadamu wajitawale kwa muda fulani chini ya uvutanowa Shetani. Sura ya 11 ya kitabu hiki itaeleza sababu iliyo-mfanya Yehova aamue hivyo na kuruhusu muda wakutosha upite kabla ya kutatua masuala hayo. Hata hivyo,kwa sasa ni vizuri kujiuliza hivi: Je, Adamu na Hawa wa-likuwa na sababu ya kumwamini Shetani ambaye hakuwaamewafanyia jambo lolote zuri? Je, walikuwa na msingiwowote wa kuamini kwamba Yehova ambaye alikuwaamewapa vyote walivyokuwa navyo, ni mwongo na mkati-li? Wewe ungefanyaje?

10 Ni vizuri kufikiria maswali hayo kwa sababu kilammoja wetu anakabili masuala hayo leo. Naam, wewe unanafasi ya kuunga mkono upande wa Yehova na kumpi-nga Shetani. Unaweza kumkubali Yehova kuwa Mtawalana kuonyesha kwamba Shetani ni mwongo. (Zaburi 73:28;Methali 27:11) Inasikitisha kwamba, kati ya mabilioni yawatu ulimwenguni pote, ni wachache tu wanaoamua kufa-nya hivyo. Hilo linatokeza swali muhimu, Je, kweliBiblia inafundisha kwamba Shetani anatawala ulimwenguhuu?

NI NANI ANAYEUTAWALA ULIMWENGU HUU?11 Yesu hakuwa na shaka yoyote kwamba Shetani ndiye

10. Unawezaje kuunga mkono upande wa Yehova na kumpinga She-tani?11, 12. (a) Kushawishiwa kwa Yesu kunaonyeshaje kwamba Shetanindiye mtawala wa ulimwengu huu? (b) Ni nini kingine kinachothibi-tisha kwamba Shetani ndiye mtawala wa ulimwengu huu?

Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia? 31

mtawala wa ulimwengu huu. Pindi moja Shetani ali-mwonyesha Yesu kimuujiza “falme zote za ulimwengu nautukufu wazo.” Kisha Shetani akamwahidi Yesu: “Nitakupamambo yote haya ukianguka chini na kunifanyia tendo laibada.” (Mathayo 4:8, 9; Luka 4:5, 6) Hebu fikiria: Je,Shetani angeweza kumshawishi Yesu kwa kutoa ahadihiyo ikiwa hakuwa mtawala wa falme hizo? Yesu haku-pinga kwamba serikali zote hizo za ulimwengu hazikuwaza Shetani. Bila shaka, Yesu angepinga ikiwa hazikuwa zaShetani.

12 Bila shaka, Yehova ndiye Mungu Mweza-Yote, Muu-mba wa ulimwengu wetu wa ajabu. (Ufunuo 4:11) Hatahivyo, Biblia haisemi kamwe kwamba Yehova Mungu auYesu Kristo ni watawala wa ulimwengu huu. Yesu alimwi-ta Shetani “mtawala wa ulimwengu huu.” (Yohana 12:31;14:30; 16:11) Hata Biblia inamwita Shetani Ibilisi “munguwa mfumo huu wa mambo.” (2 Wakorintho 4:3, 4) Ku-husu mpinzani huyo au Shetani, mtume Mkristo Yohanaaliandika: “Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu zayule mwovu.”—1 Yohana 5:19.

JINSI ULIMWENGU WA SHETANIUTAKAVYOONDOLEWA

13 Ulimwengu unazidi kuwa hatari mwaka baada yamwaka. Kuna majeshi mengi yanayopigana, wanasiasa wa-fisadi, viongozi wa kidini wanafiki, na wahalifu sugu.Haiwezekani kuubadili ulimwengu kwa ujumla. Biblia ina-sema kwamba hivi karibuni Mungu atauondolea mbaliulimwengu huu mbovu katika vita vya Har–Magedoni. Ki-sha ataleta ulimwengu mpya wenye uadilifu.—Ufunuo 16:14-16.

14 Yehova Mungu alimchagua Yesu Kristo awe Mta-

13. Kwa nini tunahitaji ulimwengu mpya?14. Mungu amemchagua nani awe Mtawala katika Ufalme Wake, nahilo lilitabiriwaje?

32 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

wala wa Ufalme au serikali Yake ya mbinguni. Biblia ili-tabiri hivi zamani: “Kwa maana kuna mtoto ambayeamezaliwa kwetu, kuna mwana ambaye tumepewa; na uta-wala wa ukuu utakuwa juu ya bega lake. Naye ataitwa. . . Mkuu wa Amani. Hakutakuwa na mwisho kwa ha-bari ya wingi wa huo utawala wa kifalme na kwa amani.”(Isaya 9:6, 7) Kuhusu serikali hiyo, Yesu aliwafundisha wa-fuasi wake wasali hivi: “Ufalme wako na uje. Mapenzi yakona yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mathayo6:10) Kama tutakavyoona baadaye katika kitabu hiki, kari-buni Ufalme wa Mungu utaondolea mbali serikali zote zaulimwengu huu nao utatawala badala ya serikali hizo. (Da-nieli 2:44) Kisha Ufalme wa Mungu utaleta paradisoduniani.

ULIMWENGU MPYA U KARIBU!15 Biblia inatuhakikishia hivi: “Kulingana na ahadi yake

[Mungu] tunangojea mbingu mpya na dunia mpya, nahumo uadilifu utakaa.” (2 Petro 3:13; Isaya 65:17) Nyakatinyingine Biblia inapotaja “dunia,” inamaanisha watu wa-naoishi duniani. (Mwanzo 11:1) Kwa hiyo “dunia mpya”yenye uadilifu ni jamii ya watu watakaopata kibali cha Mu-ngu.

16 Yesu aliahidi kwamba katika ulimwengu mpya unao-kuja, wale wanaopata kibali cha Mungu watapokea zawadiya “uzima wa milele.” (Marko 10:30) Tafadhali funguaYohana 3:16 na Yohana 17:3 katika Biblia yako, na uso-me yale ambayo Yesu alisema tunapaswa kufanya ili tupateuzima wa milele. Sasa ona baraka zinazotajwa katika Bib-lia zitakazofurahiwa na wale wanaostahili kupokea zawadihiyo ya pekee kutoka kwa Mungu katika dunia itakayoku-wa Paradiso.

15. “Dunia mpya” ni nini?16. Ni zawadi gani yenye thamani sana ambayo Mungu atawapa walewalio na kibali chake, na tunapaswa kufanya nini ili tuipokee?

Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia? 33

17 Hakutakuwa na uovu, vita, uhalifu, na ujeuri. “Mtumwovu hatakuwako tena . . . Bali wapole wataimilikidunia.” (Zaburi 37:10, 11) Kutakuwa na amani kwa sa-babu ‘Mungu atakomesha vita mpaka kwenye mwisho wadunia.’ (Zaburi 46:9; Isaya 2:4) Kisha “mwadilifu atachipu-ka, na wingi wa amani mpaka mwezi utakapokuwa haupotena”—yaani, milele!—Zaburi 72:7.

18 Waabudu wa Yehova wataishi kwa usalama. Nyakatizote Waisraeli katika nyakati za Biblia walipomtii Mungu,waliishi kwa usalama. (Mambo ya Walawi 25:18, 19) Lita-kuwa jambo zuri ajabu kufurahia usalama kama huo katikaParadiso!—Isaya 32:18; Mika 4:4.

19 Hakutakuwa na upungufu wa chakula. Mtunga-zaburialiimba hivi: “Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani; juuya milima kutakuwa na mafuriko.” (Zaburi 72:16) YehovaMungu atawabariki waadilifu wake, na “hakika dunia ita-toa mazao yake.”—Zaburi 67:6.

20 Dunia nzima itakuwa paradiso. Kutakuwa na makaona bustani zenye kupendeza katika sehemu zilizokuwa zi-meharibiwa na wanadamu wenye dhambi. (Isaya 65:21-24;Ufunuo 11:18) Kadiri wakati unavyopita, sehemu za duniazinazokaliwa zitapanuka mpaka dunia yote iwe yenye ku-pendeza na kuzaa sana kama bustani ya Edeni. Na Munguhatakosa kamwe ‘kufumbua mkono wake na kutoshelezatamaa ya kila kitu kilicho hai.’—Zaburi 145:16.

21 Kutakuwa na amani kati ya wanadamu na wanyama.Wanyama mwitu na wa kufugwa watalisha pamoja. Hata

17, 18. Tunawezaje kuwa na hakika kwamba kutakuwa na amani nausalama duniani pote?19. Tunajuaje kwamba kutakuwa na chakula kingi katika ulimwengumpya wa Mungu?20. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba dunia nzima itaku-wa paradiso?21. Ni nini kinachoonyesha kwamba kutakuwa na amani kati ya wa-nadamu na wanyama?

34 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

mtoto mdogo hataogopa wanyama ambao ni hatari leo.—Isaya 11:6-9; 65:25.

22 Magonjwa hayatakuwapo. Akiwa Mtawala wa Ufalmewa mbinguni wa Mungu, Yesu ataponya watu kwa kiwangokikubwa zaidi kuliko alivyofanya alipokuwa duniani. (Ma-thayo 9:35; Marko 1:40-42; Yohana 5:5-9) Hatimaye,“hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’”—Isaya33:24; 35:5, 6.

23 Wapendwa waliokufa watafufuliwa wakiwa na tumainila kuishi milele. Wote wanaolala katika kifo walio katika ku-mbukumbu ya Mungu watafufuliwa. “Kutakuwa na ufufuowa waadilifu na wasio waadilifu pia.”—Matendo 24:15; Yo-hana 5:28, 29.

24 Wale wanaoamua kujifunza kuhusu Muumba wetuMtukufu, Yehova Mungu na kumtumikia wana tumai-ni zuri kama nini! Yesu alikuwa akizungumzia Paradisoya wakati ujao hapa duniani alipomwahidi hivi yule mte-nda maovu aliyetundikwa pamoja naye: “Utakuwa pamojanami katika Paradiso.” (Luka 23:43) Tunapaswa kujifunzamengi zaidi kumhusu Yesu Kristo, atakayetumiwa kuletabaraka hizo zote.

22. Ni hatua gani itakayochukuliwa kuhusiana na magonjwa?23. Kwa nini ufufuo utaleta shangwe mioyoni mwetu?24. Unaonaje kuhusu kuishi katika Paradiso duniani?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Kusudi la Mungu la kuifanya dunia iwe pa-radiso litatimia.—Isaya 45:18; 55:11.

ˇ Shetani ndiye anayeutawala ulimwengu huu.—Yohana 12:31; 1 Yohana 5:19.

ˇ Katika ulimwengu mpya unaokuja, Munguatawabariki sana wanadamu.—Zaburi 37:10,11, 29.

36 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

KUNA watu wengi mashuhuri ulimwenguni. Baadhi yaowanajulikana sana katika jamii zao, majiji yao, au nchizao. Wengine wanajulikana ulimwenguni pote. Hata hi-vyo, kujua tu jina la mtu fulani mashuhuri, hakumaanishikwamba unamjua vizuri. Haimaanishi kwamba unajuamalezi yake na utu wake kabisa.

2 Watu ulimwenguni pote wamesikia kumhusu YesuKristo, ingawa aliishi duniani miaka 2,000 hivi iliyopita.Hata hivyo, wengi hawajui kwa kweli Yesu alikuwa nani.Baadhi yao husema kwamba alikuwa mtu mzuri tu. We-ngine wanadai kwamba alikuwa nabii tu. Na wenginewanaamini kwamba Yesu ni Mungu na anapaswa kuabu-diwa. Je, anapaswa kuabudiwa?

3 Ni muhimu ujue ukweli kumhusu Yesu. Kwa nini?Kwa sababu Biblia inasema: “Uzima wa milele ndio huu,waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekeewa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.” (Yo-hana 17:3) Ndiyo, kujua ukweli kumhusu Yehova Munguna Yesu Kristo kutakuwezesha kupata uzima wa milelekatika paradiso duniani. (Yohana 14:6) Isitoshe, Yesu alio-nyesha kwa njia bora zaidi jinsi ya kuishi na kuwatendea

1, 2. (a) Kwa nini kujua jina la mtu mashuhuri hakumaanishi kwa-mba unamjua vizuri? (b) Watu wana maoni gani yanayotofautianakumhusu Yesu?3. Kwa nini ni muhimu ujue ukweli kumhusu Yesu?

SURA YA NNE

Yesu Kristo Ni Nani?

Yesu ana jukumu gani muhimu?

Alitoka wapi?

Alikuwa mtu wa aina gani?

wengine. (Yohana 13:34, 35) Katikasura ya kwanza ya kitabu hiki tuli-

zungumzia ukweli kumhusu Mungu. Sasa, natuchunguze mambo ambayo Biblia inafundisha ku-

mhusu Yesu Kristo.

MASIHI ALIYEAHIDIWA4 Zamani kabla ya Yesu kuzaliwa, Biblia ilikuwa imetabi-

ri kuja kwa yule ambaye Mungu angemtuma akiwa Masihi,au Kristo. Majina “Masihi” (kutokana na neno la Kie-brania) na “Kristo” (kutokana na neno la Kigiriki)yanamaanisha “Mtiwa-Mafuta.” Huyo aliyeahidiwaangetiwa mafuta, yaani, angewekwa rasmi na Mu-ngu katika cheo cha pekee. Katika sura za baadaye

4. Majina “Masihi” na “Kristo” yanamaanisha nini?

Baada ya kubatizwa, Yesuakawa Masihi, au Kristo

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

za kitabu hiki, tutajifunza mengi kuhusu jukumu muhimula Masihi kuhusiana na kutimia kwa ahadi za Mungu. Piatutajifunza kuhusu baraka ambazo Yesu anaweza kutuleteahata sasa. Hata hivyo, kabla Yesu hajazaliwa, watu wengi wa-lijiuliza, ‘Ni nani atakayekuwa Masihi?’

5 Katika karne ya kwanza W.K., wanafunzi wa Yesu waNazareti walisadiki kabisa kwamba ndiye alikuwa Masi-hi aliyeahidiwa. (Yohana 1:41) Simoni Petro, mmoja wawanafunzi hao, alimwambia Yesu waziwazi: “Wewe ndiyeKristo.” (Mathayo 16:16) Hata hivyo, wanafunzi hao wa-ngewezaje kuwa na hakika kwamba Yesu kwa kweli ndiyeMasihi aliyeahidiwa? Namna gani sisi?

6 Manabii wa Mungu walioishi kabla ya Yesu walitabirimambo mengi kumhusu Masihi. Mambo hayo yangewa-saidia watu wengine kumtambua. Kwa mfano: Tusemeumeombwa uende kwenye kituo cha mabasi chenye shu-ghuli nyingi au kwenye kituo cha magari-moshi aukwenye uwanja wa ndege kumpokea mtu ambaye huja-pata kukutana naye. Ingefaa ikiwa mtu fulani angekupahabari zaidi kumhusu, sivyo? Vivyo hivyo, kupitia mana-bii wa Biblia, Yehova ametueleza mambo mengi kuhusuutendaji wa Masihi na mambo ambayo yangempata. Kuti-mia kwa unabii huo mbalimbali kungewasaidia watuwaaminifu wamtambue waziwazi.

7 Fikiria mifano miwili tu. Kwanza, zaidi ya miaka700 mapema, nabii Mika alitabiri kwamba Yule aliyea-hidiwa angezaliwa Bethlehemu, mji mdogo katika Yuda.(Mika 5:2) Yesu alizaliwa wapi hasa? Katika mji huo-huo! (Mathayo 2:1, 3-9) Pili, karne nyingi mapema, unabiiulio katika Danieli 9:25 ulionyesha mwaka hususa ambao

5. Wanafunzi wa Yesu walisadiki nini kumhusu?6. Toa mfano unaoonyesha jinsi Yehova amewasaidia watu waamini-fu kumtambua Masihi.7. Ni mambo gani mawili yaliyotabiriwa kuhusiana na Yesu ambayoyalitimia?

Yesu Kristo Ni Nani 39

Masihi angetokea, yaani, 29 W.K.� Kutimia kwa unabiihuo na unabii mwingine mbalimbali kunathibitisha kwa-mba Yesu alikuwa Masihi aliyeahidiwa.

8 Uthibitisho zaidi wa kwamba Yesu ndiye Masihi ulio-nekana wazi mwishoni mwa mwaka wa 29 W.K. Huondio mwaka ambao Yesu alimwendea Yohana Mbatizaji iliabatizwe katika Mto Yordani. Yehova alikuwa amemwahi-di Yohana kwamba angempa ishara ili amtambue Masihi.Yohana aliona ishara hiyo Yesu alipobatizwa. Biblia inasi-mulia lililotukia: “Baada ya kubatizwa Yesu akapanda maramoja kutoka katika maji; na, tazama! mbingu zikafunguli-wa, naye akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa, ikijajuu yake. Tazama! Kulikuwa pia na sauti kutoka mbinguniiliyosema: ‘Huyu ni Mwanangu, mpendwa, ambaye nime-mkubali.’” (Mathayo 3:16, 17) Baada ya kusikia na kuonakilichotukia, Yohana hakuwa na shaka kwamba Yesu alitu-mwa na Mungu. (Yohana 1:32-34) Wakati roho ya Munguau nguvu ya utendaji ilipomiminwa juu yake siku hiyo, Yesuakawa Masihi au Kristo, ambaye aliwekwa rasmi kuwa Kio-ngozi na Mfalme.—Isaya 55:4.

9 Utimizo wa unabii wa Biblia na ushuhuda wa Mungumwenyewe unaonyesha wazi kwamba Yesu ndiye Masihialiyeahidiwa. Lakini Biblia inajibu maswali mengine mawilimuhimu kumhusu Yesu Kristo: Alitoka wapi? Na alipokuwamwanadamu, alikuwa mtu wa aina gani?

YESU ALITOKA WAPI?10 Biblia inafundisha kwamba Yesu aliishi mbinguni

� Unaweza kupata maelezo kuhusu unabii wa Danieli uliotimia ku-husiana na Yesu katika Nyongeza, ukurasa wa 197-199.

8, 9. Uthibitisho wa kwamba Yesu alikuwa Masihi ulionekanaje wazialipobatizwa?10. Biblia inafundisha nini kuhusu maisha ya Yesu kabla ya kuja du-niani?

40 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

kabla ya kuja duniani. Mika alitabiri kwamba Masihi ange-zaliwa Bethlehemu na alisema pia kwamba asili Yake “nikutoka nyakati za kale.” (Mika 5:2) Mara nyingi, Yesumwenyewe alisema kwamba aliishi mbinguni kabla yakuwa mwanadamu. (Yohana 3:13; 6:38, 62; 17:4, 5) Akiwakiumbe wa roho mbinguni, Yesu alikuwa na uhusiano wapekee pamoja na Yehova.

11 Yesu ni Mwana mpendwa zaidi wa Yehova—na kunasababu nzuri. Anaitwa “mzaliwa wa kwanza wa viumbevyote,” kwa sababu aliumbwa kwanza na Mungu.� (Wako-losai 1:15) Kuna jambo lingine linalomfanya Mwana huyuawe wa pekee. Yeye ni ‘Mwana mzaliwa-pekee.’ (Yohana3:16) Hilo linamaanisha kwamba ni Yesu peke yake aliye-umbwa moja kwa moja na Mungu. Pia Mungu alimtumiaYesu peke yake kuumba vitu vingine vyote. (Wakolosai1:16) Pia, Yesu anaitwa “Neno.” (Yohana 1:14) Hilo li-namaanisha kwamba alizungumza kwa niaba ya Mungu,akiwasilisha ujumbe na maagizo kwa wana wengine waBaba yake, yaani, malaika na wanadamu.

12 Je, Mwana huyo mzaliwa wa kwanza yuko sawa naMungu kama wengine wanavyoamini? Biblia haifundishihivyo. Kama tulivyoona katika fungu lililotangulia, Mwa-na huyo aliumbwa. Basi ni wazi kwamba alikuwa namwanzo, lakini Yehova Mungu hana mwanzo wala mwi-sho. (Zaburi 90:2) Mwana huyo mzaliwa-pekee hakujaribukamwe kuwa sawa na Baba yake. Biblia inafundisha wazikwamba Baba ni mkuu kuliko Mwana. (Yohana 14:28;

� Yehova anaitwa Baba kwa sababu yeye ndiye Muumba. (Isaya64:8) Yesu anaitwa Mwana wa Mungu kwa sababu aliumbwa na Mu-ngu. Vivyo hivyo, malaika wengine na Adamu wanaitwa wana wa Mu-ngu.—Ayubu 1:6; Luka 3:38.

11. Biblia inaonyeshaje kwamba Yesu ndiye Mwana mpendwa zaidiwa Yehova?12. Tunajuaje kwamba Mwana mzaliwa wa kwanza halingani na Mu-ngu?

Yesu Kristo Ni Nani 41

1 Wakorintho 11:3) Yehova peke yake ndiye “MunguMweza-Yote.” (Mwanzo 17:1) Kwa hiyo, hakuna yeyoteanayelingana naye.�

13 Yehova na Mwana mzaliwa wake wa kwanza walikuwana uhusiano wa karibu mabilioni ya miaka kabla ya mbinguzenye nyota na dunia kuumbwa. Walipendana kwelikwe-li! (Yohana 3:35; 14:31) Mwana huyo mpendwa alikuwatu kama Baba yake. Ndiyo sababu Biblia inamwita Mwanahuyo “mfano wa Mungu asiyeonekana.” (Wakolosai 1:15)Ndiyo, kama vile mwana wa mwanadamu anavyoweza kufa-nana na baba yake katika njia mbalimbali, Mwana huyo wakimbingu alionyesha sifa na utu wa Baba yake.

14 Mwana mzaliwa-pekee wa Yehova alikubali kuachamakao yake mbinguni na kuja kuishi duniani kama mwa-nadamu. Lakini huenda ukajiuliza, ‘Iliwezekanaje kiumbewa roho kuzaliwa kama mwanadamu?’ Ili kutimiza hilo,Yehova alifanya muujiza. Alihamisha uhai wa Mwanawake wa kwanza kutoka mbinguni na kuutia katika tumbola bikira Myahudi aliyeitwa Maria. Yesu hakuwa na babawa kibinadamu. Basi, Maria alimzaa mwana mkamilifu nakumwita Yesu.—Luka 1:30-35.

YESU ALIKUWA MTU WA AINA GANI?15 Mambo ambayo Yesu alisema na kutenda alipokuwa

duniani yanatusaidia kumjua vizuri. Pia, kupitia Yesu tu-napata kumjua Yehova vizuri zaidi. Kwa nini? Kumbukakwamba Mwana huyo anamwakilisha Baba yake kika-

� Unaweza kupata uthibitisho zaidi unaoonyesha kwamba Mwanamzaliwa wa kwanza halingani na Mungu, katika Nyongeza, ukurasawa 201-204.

13. Biblia humaanisha nini inapomwita Mwana “mfano wa Munguasiyeonekana”?14. Mwana mzaliwa-pekee wa Yehova alizaliwaje akiwa mwanadamu?15. Tunawezaje kumjua Yehova vizuri zaidi kupitia Yesu?

42 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

milifu. Ndiyo sababu Yesu alimwambia mwanafunzi wakehivi: “Yule ambaye ameniona mimi amemwona Babapia.” (Yohana 14:9) Vitabu vinne vya Biblia vinavyoitwaInjili, yaani, Mathayo, Marko, Luka, na Yohana, vinatua-mbia mengi kuhusu maisha, utendaji, na sifa za YesuKristo.

16 Watu wengi walimjua Yesu kuwa “Mwalimu.” (Yoha-na 1:38; 13:13) Alifundisha nini? Ujumbe wake wa msingiulikuwa “habari njema ya ufalme,” yaani, Ufalme wa Mu-ngu, serikali ya mbinguni itakayotawala dunia nzima nakuwaletea wanadamu watiifu baraka za milele. (Matha-yo 4:23) Ujumbe huo ulikuwa wa nani? Yesu mwenyewealisema hivi: “Yale ninayofundisha si yangu, bali ni yakeyeye aliyenituma,” Yehova. (Yohana 7:16) Yesu alijua kwa-mba Baba yake anataka wanadamu wasikie habari njemaya Ufalme. Katika Sura ya 8, tutajifunza mengi zaidi kuhu-su Ufalme wa Mungu na mambo ambayo utatimiza.

17 Yesu alifundisha wapi? Kila mahali penye watu—ma-shambani, majijini, vijijini, sokoni, na nyumbani kwao.Yesu hakungoja watu wamjie. Alienda walipokuwa. (Marko6:56; Luka 19:5, 6) Kwa nini Yesu alijitahidi sana na kutu-mia wakati mwingi kuhubiri na kufundisha? Kwa sababuMungu alitaka afanye hivyo. Sikuzote Yesu alifanya mape-nzi ya Baba yake. (Yohana 8:28, 29) Hata hivyo, kulikuwana sababu nyingine iliyomfanya ahubiri. Aliusikitikia umatiwa watu waliokuja kumwona. (Mathayo 9:35, 36) Walikuwawamepuuzwa na viongozi wao wa kidini ambao walipa-swa kuwafundisha kweli kumhusu Mungu na makusudiyake. Yesu alijua kwamba watu hao walitamani sana kusikiaujumbe wa Ufalme.

16. Yesu alifundisha ujumbe gani wa msingi, nayo mafundisho yakeyalitoka wapi?17. Yesu alifundisha wapi, na kwa nini alijitahidi sana kuwafundishawengine?

Yesu Kristo Ni Nani 43

18 Yesu alikuwa mchangamfu na mwenye hisia nyingi.Kwa hiyo watu walimwona kuwa mtu mwenye fadhilina urafiki. Hata watoto walifurahia ushirika wake. (Mar-ko 10:13-16) Yesu hakuwa na ubaguzi. Alichukia ufisadi naukosefu wa haki. (Mathayo 21:12, 13) Aliwaheshimu wa-nawake ingawa wakati huo walikuwa wakidharauliwa nakunyimwa haki zao. (Yohana 4:9, 27) Yesu alikuwa mnye-nyekevu kikweli. Pindi moja, aliosha miguu ya mitumewake, kazi ambayo kwa kawaida ilifanywa na mtumishi wahali ya chini.

19 Yesu alihangaikia mahitaji ya wengine. Hilo lilione-kana wazi alipoongozwa na nguvu za roho ya Mungukufanya miujiza ya uponyaji. (Mathayo 14:14) Kwa mfano,mtu fulani aliyekuwa na ukoma alimjia Yesu na kuse-ma: “Ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.” Yesu alihisi

18. Ni sifa zipi za Yesu zinazokuvutia sana?19. Ni mfano gani unaoonyesha kwamba Yesu alihangaikia mahitajiya wengine?

Yesu alihubiri kila mahali penye watu

kana kwamba yeye mwenyewe ndiye aliyekuwa akiumiana kuteseka. Alimsikitikia, akaunyoosha mkono wake, aka-mgusa, na kusema: “Ninataka. Takasika.” Na mtu huyoaliyekuwa mgonjwa akapona. (Marko 1:40-42) Je, unawe-za kuwazia jinsi mtu huyo alivyohisi?

MWAMINIFU MPAKA MWISHO20 Yesu aliweka mfano bora wa utii mshikamanifu kwa

Mungu. Aliendelea kuwa mwaminifu kwa Baba yake wambinguni chini ya hali zote na licha ya upinzani na ma-gumu mbalimbali. Yesu alifaulu kupinga kwa uthabitivishawishi vya Shetani. (Mathayo 4:1-11) Wakati mmoja,baadhi ya watu wa ukoo wa Yesu mwenyewe hawaku-mwamini, hata walisema kwamba alikuwa “amerukwa naakili.” (Marko 3:21) Hata hivyo, Yesu hakuwaruhusu wa-mkengeushe; bali aliendelea kufanya kazi ya Mungu.

20, 21. Yesu aliwekaje mfano bora wa utii mshikamanifu kwa Mungumpaka kifo?

45

Ijapokuwa alitukanwa na kutendewa vibaya, Yesu alijizuia,hakujaribu kuwadhuru wapinzani wake.—1 Petro 2:21-23.

21 Yesu aliendelea kuwa mwaminifu mpaka alipokufakifo cha kikatili na uchungu mikononi mwa adui zake.(Wafilipi 2:8) Fikiria mambo aliyovumilia usiku wa mwi-sho wa maisha yake akiwa mwanadamu. Alikamatwa,akashtakiwa na mashahidi wa uwongo, akahukumiwa namahakimu wafisadi, akachekwa na umati, na kuteswana askari. Akiwa ametundikwa kwenye mti wa mateso,alivuta pumzi ya mwisho akipaaza sauti: “Imetimizwa!”(Yohana 19:30) Hata hivyo, siku tatu baada ya Yesu kufa,Baba yake wa mbinguni alimfufua na kumfanya hai kati-ka roho. (1 Petro 3:18) Majuma machache baadaye, alirudimbinguni. Akiwa huko, ‘aliketi kwenye mkono wa kuumewa Mungu’ na kungoja apokee mamlaka ya kifalme.—Wa-ebrania 10:12, 13.

22 Yesu alitimiza nini kwa kuendelea kuwa mwaminifumpaka kifo? Kifo cha Yesu kinatuwezesha kupata uzima wamilele katika dunia itakayokuwa paradiso kama vile Yeho-va alivyokusudia mwanzoni. Sura inayofuata itazungumziajinsi kifo cha Yesu kinavyotuwezesha kupata uzima.

22. Yesu alitimiza nini kwa kuendelea kuwa mwaminifu mpaka kifo?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Utimizo wa unabii na ushuhuda wa Mungumwenyewe unathibitisha kwamba Yesundiye Masihi au Kristo.—Mathayo 16:16.

ˇ Yesu aliishi mbinguni akiwa kiumbe waroho kabla ya kuja duniani.—Yohana 3:13.

ˇ Yesu alikuwa mwalimu, mtu mchangamfu,na aliweka mfano bora wa kumtii Mungukikamili.—Mathayo 9:35, 36.

46 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

NI ZAWADI gani bora zaidi ambayo umewahi kupokea? Za-wadi muhimu si lazima iwe ya bei ghali. Kwa kweli, thamaniya zawadi haitegemei kiasi cha pesa kilichotumiwa kui-nunua. Badala yake, zawadi inapokufurahisha au kutimizamahitaji muhimu, basi ina thamani kubwa kwako.

2 Katiya zawadinyingi ambazoungependakupokea, kunamoja iliyo bora zaidi kuliko zote. Ni zawadi kutoka kwa Mu-ngu. Yehova ametupatia vitu vingi, lakini zawadi bora zaidiambayo ametupatia ni dhabihu ya fidia ya Mwana wake,Yesu Kristo. (Mathayo 20:28) Kama tutakavyoona katika surahii, fidia ndiyo zawadi bora zaidi ambayo unaweza kupokeakwa sababu inaweza kukuletea furaha isiyo na kifani na ku-ridhisha sana. Kwa hakika, fidia ndiyo wonyesho mkubwazaidi wa upendo wa Yehova kwako.

FIDIA NI NINI?3 Kwa ufupi, fidia ni njia ya Yehova ya kuwakomboa

1, 2. (a) Ni zawadi ya aina gani yenye thamani zaidi kwako? (b) Kwanini tunaweza kusema kwamba fidia ndiyo zawadi yenye thamani ku-bwa zaidi ambayo unaweza kupokea?3. Fidia ni nini, na tunahitaji kuelewa nini ili tuione fidia kuwa za-wadi yenye thamani kubwa?

SURA YA TANO

Fidia—Zawadi Bora ZaidiKutoka kwa Mungu

Fidia ni nini?

Ilitolewaje?

Ina faida gani kwako?

Unaweza kuonyeshaje kwamba unaithamini?

au kuwaokoa wanadamu kutokana na dhambi na kifo.(Waefeso 1:7) Ili kuelewa maana ya fundisho hili la Bib-lia, tunahitaji kufikiria mambo yaliyotokea katika bustaniya Edeni. Tukielewa kile ambacho Adamu alipoteza alipofa-nya dhambi, ndipo tu tunapoweza kujua kwa nini fidia nizawadi yenye thamani kubwa kwetu.

4 Yehova alipomuumba Adamu, alimpa kitu chenye tha-mani sana, yaani, uhai mkamilifu. Wazia faida ambazoAdamu angepata. Kwa sababu alikuwa na mwili mkami-lifu, hangekuwa mgonjwa, hangezeeka, wala kufa. Akiwamwanadamu mkamilifu, alikuwa na uhusiano wa pekeepamoja na Yehova. Biblia inasema kwamba Adamu ali-kuwa “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Kwa hiyo Adamualifurahia uhusiano wa karibu pamoja na Yehova Mungu,kama ule wa mwana na baba mwenye upendo. Yehova ali-zungumza na mwanawe, Adamu, hapa duniani, akampakazi yenye kuridhisha na kumjulisha mapenzi yake.—Mwa-nzo 1:28-30; 2:16, 17.

5 Adamu aliumbwa “kwa mfano wa Mungu.” (Mwa-nzo 1:27) Hilo halimaanishi kwamba Adamu alikuwa naumbo kama la Mungu. Kama tulivyojifunza katika Sura ya1 ya kitabu hiki, Yehova ni roho asiyeonekana. (Yo-hana 4:24) Kwa hiyo, Yehova hana mwili wa nyama nadamu. Kuumbwa kwa mfano wa Mungu kunamaanishakwamba Adamu aliumbwa akiwa na sifa kama za Mu-ngu, kutia ndani upendo, hekima, haki, na nguvu. Adamualikuwa kama Baba yake katika njia nyingine muhimu,alikuwa na uhuru wa kuchagua. Hivyo, Adamu hakuwakama mashine ambayo inaweza tu kufanya kazi ambayoimepangiwa ifanye. Badala yake, angeweza kujifanyia maa-

4. Adamu angepata faida gani kwa kuwa na uhai mkamilifu?5. Biblia inamaanisha nini inaposema kwamba Adamu aliumbwa kwa“mfano wa Mungu”?

48 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

muzi, na kuchagua kati ya yaliyo sawa na kosa. Kamaangechagua kumtii Mungu, angeishi milele katika Paradisoduniani.

6 Basi, ni wazi kwamba Adamu alipokosa kumtii Mu-ngu na akahukumiwa kifo, alileta hasara kubwa sana.Kwa sababu ya dhambi aliyofanya, alipoteza uhai mka-milifu na faida zake zote. (Mwanzo 3:17-19) Inasikitishakwamba Adamu alipoteza uhai wake mkamilifu pamo-ja na wa wazao wake. Neno la Mungu linasema: “Kupitiamtu mmoja [Adamu] dhambi iliingia katika ulimwengu nakifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wotekwa sababu wote walikuwawamefanya dhambi.” (Waroma5:12) Ndiyo, sote tumerithi dhambi kutoka kwa Adamu.Kwa hiyo Biblia inasema kwamba ‘alijiuza’ pamoja na wa-zao wake katika utumwa wa dhambi na kifo. (Waroma7:14) Adamu na Hawa hawakuwa na tumaini kwa kuwawalikataa kumtii Mungu kimakusudi. Lakini namna ganiwazao wao kutia ndani sisi?

7 Yehova alifanya mpango wa kuwakomboa wanadamukupitia fidia. Fidia ni nini? Fidia inahusisha mambo mawi-li ya msingi. Kwanza, fidia ni bei inayolipwa ili kukomboaau kurudisha kitu. Inaweza kulinganishwa na bei inayoli-pwa ili kumkomboa mtu aliyetekwa nyara vitani. Pili, fidiani bei inayofunika, au kulipia gharama ya kitu fulani. Nisawa na bei ambayo mtu hulipa anaposababisha madha-ra. Kwa mfano, mtu akisababisha msiba, anapaswa kulipakiasi kinacholingana au kinachotoshana na thamani ya ki-lichoharibiwa.

8 Hasara kubwa aliyotuletea Adamu ingewezaje kulipwaili tukombolewe kutoka katika utumwa wa dhambi na

6. Adamu alipoteza nini alipokosa kumtii Mungu, na hilo liliathirijewazao wake?7, 8. Fidia inahusisha mambo gani mawili ya msingi?

Fidia—Zawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu 49

kifo? Hebu tuzungumzie fidia ambayo Yehova aliandaa najinsi inavyoweza kukufaidi.

JINSI YEHOVA ALIVYOANDAA FIDIA9 Kwa kuwa uhai mkamilifu wa kibinadamu ulipotea,

hakuna mwanadamu yeyote asiye mkamilifu angeweza ku-urudisha. (Zaburi 49:7, 8) Kilichohitajiwa ni fidia yenyethamani inayolingana na kilichopotezwa. Hilo linapa-tana na kanuni hii ya haki kamilifu inayopatikana katikaNeno la Mungu: “Nafsi itakuwa kwa nafsi.” (Kumbuku-mbu la Torati 19:21) Kwa hiyo, ni nini kingeweza kulipiathamani ya nafsi au uhai mkamilifu wa kibinadamuuliopotezwa na Adamu? Kilichohitajiwa ni “fidia inayo-lingana” ya uhai mwingine mkamilifu wa kibinadamu.—1 Timotheo 2:6.

10 Yehova aliandaaje fidia? Alimtuma mmoja kati yawana wake wakamilifu wa kiroho aje duniani. Lakini Ye-hova hakutuma kiumbe yeyote tu wa roho. Alimtuma yulealiyempenda sana, Mwana wake mzaliwa-pekee. (1 Yoha-na 4:9, 10) Mwana huyo alikubali kwa hiari kuacha makaoyake mbinguni. (Wafilipi 2:7) Kama tulivyojifunza katikaSura ya 4 ya kitabu hiki, Yehova alifanya muujiza alipo-hamisha uhai wa Mwana huyo na kuutia katika tumbo laMaria. Kupitia roho takatifu ya Mungu, Yesu alizaliwa aki-wa mwanadamu mkamilifu wala hakuwa chini ya laana yadhambi.—Luka 1:35.

11 Mtu mmoja angewezaje kuwa fidia kwa ajili ya watuwengi, mamilioni ya wanadamu? Kwanza, mamilioni hayoya wanadamu walipataje kuwa wenye dhambi? Kumbukakwamba kwa kufanya dhambi Adamu alipoteza uhai mka-

9. Ni fidia ya aina gani iliyohitajiwa?10. Yehova aliandaaje fidia?11. Mtu mmoja angewezaje kuwa fidia kwa ajili ya mamilioni yawatu?

50 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

milifu wa kibinadamu wenye thamani sana. Kwa hiyo, ha-ngeweza kuwapitishia wazao wake uhai huo mkamilifu.Badala yake aliwapitishia dhambi na kifo tu. Yesu, amba-ye Biblia inamwita “Adamu wa mwisho,” alikuwa na uhaimkamilifu wa kibinadamu wala hakufanya dhambi ka-mwe. (1 Wakorintho 15:45) Hivyo, Yesu alichukua mahalipa Adamu ili atuokoe. Yesu alilipia dhambi ya Adamukwa kudhabihu uhai wake mkamilifu na kumtii Mungukikamili. Hivyo, Yesu akawapa wazao wa Adamu tumaini.—Waroma 5:19; 1 Wakorintho 15:21, 22.

12 Biblia inaeleza kinaganaga kuhusu mateso ambayoYesu alivumilia kabla ya kufa. Alipigwa mijeledi, akatundi-kwa kikatili, na kufa kwa maumivu makali juu ya mti wamateso. (Yohana 19:1, 16-18, 30; Nyongeza, ukurasa wa204-206) Kwa nini ilikuwa lazima Yesu ateseke sana hi-vyo? Baadaye tutaona kwamba Shetani alitilia shaka ikiwaYehova ana watumishi wa kibinadamu wanaoweza kumtu-mikia kwa uaminifu chini ya majaribu. Kwa kuvumiliakwa uaminifu licha ya mateso makali, Yesu alijibu madaiya Shetani kwa njia bora zaidi. Yesu alithibitisha kwa-mba mwanadamu mkamilifu aliye na uhuru wa kuchaguaanaweza kumtii Mungu kikamili hata Ibilisi afanye nini.Haikosi kwamba Yehova alifurahishwa sana na uaminifuwa Mwana wake mpendwa!—Methali 27:11.

13 Fidia ililipwaje? Mungu aliruhusu Mwana wake mka-milifu asiye na dhambi auawe katika siku ya 14 ya mweziwa Kiyahudi unaoitwa Nisani, mwaka wa 33 W.K. Hi-vyo, Yesu alidhabihu uhai wake mkamilifu wa kibinadamu“mara moja kwa wakati wote.” (Waebrania 10:10) Siku yatatu baada ya Yesu kufa, Yehova alimfufua na kumrudi-sha kwenye uhai wa roho. Akiwa mbinguni, Yesu alimpa

12. Kuteseka kwa Yesu kulithibitisha nini?13. Fidia ililipwaje?

Fidia—Zawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu 51

Yehova alimtoaMwana wake

mzaliwa-pekee awefidia kwa ajili yetu

Mungu thamani ya uhai wake mkamilifu wa kibinada-mu uliotolewa dhabihu kama fidia kwa ajili ya wazaowa Adamu. (Waebrania 9:24) Yehova alikubali thamani yadhabihu ya Yesu kama fidia ya kuwakomboa wanada-mu kutoka katika utumwa wa dhambi na kifo.—Waroma3:23, 24.

JINSI FIDIA INAVYOWEZA KUKUFAIDI14 Licha ya hali yetu yenye dhambi, tunaweza kupata

baraka nyingi sana kwa sababu ya fidia. Na tuzungumziebaadhi ya faida tunazopata sasa na tutakazopata wakatiujao kwa sababu ya zawadi hiyo kubwa zaidi kutoka kwaMungu.

15 Msamaha wa dhambi. Kwa sababu tumerithi kuto-kamilika, si rahisi kufanya yaliyo sawa. Sisi sote hufanyadhambi kwa maneno au kwa matendo. Lakini kupitia dha-bihu ya fidia ya Yesu, tunaweza “kusamehewa dhambizetu.” (Wakolosai 1:13, 14) Hata hivyo, ili kupata msama-ha ni lazima tutubu kikweli. Ni lazima pia tumsihi Yehovakwa unyenyekevu na kumwomba msamaha kwa msingiwa imani yetu katika dhabihu ya fidia ya Mwana wake.—1 Yohana 1:8, 9.

16 Kuwa na dhamiri safi mbele za Mungu. Dhamiri yenyehatia inaweza kutufanya tukate tamaa na kuhisi hatufai.Lakini kwa sababu ya msamaha tunaopata kupitia fidia,kwa fadhili Yehova anatuwezesha tumwabudu tukiwa nadhamiri safi licha ya kutokamilika kwetu. (Waebrania 9:13,14) Hilo linatuwezesha kusema na Yehova tukiwa na uhu-ru. Kwa hiyo, tunaweza kumkaribia kwa uhuru katika sala.(Waebrania 4:14-16) Kudumisha dhamiri safi kunatuweze-sha kuwa na amani ya akili, kujistahi, na kuwa na furaha.

14, 15. Tunapaswa kufanya nini ili “kusamehewa dhambi zetu”?16. Ni nini hutuwezesha kumwabudu Mungu tukiwa na dhamiri safi,na dhamiri hiyo ina faida gani?

Fidia—Zawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu 53

17 Tumaini la uzima wa milele katika paradiso duniani.Andiko la Waroma 6:23 linasema: “Mshahara ambao dha-mbi hulipa ni kifo, lakini zawadi ambayo Mungu hutoa niuzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.” KatikaSura ya 3 ya kitabu hiki, tulizungumzia baraka zitaka-zokuwapo katika dunia itakayokuwa Paradiso wakati ujao.(Ufunuo 21:3, 4) Watu wataweza kupata baraka hizo zoteza wakati ujao, kutia ndani uzima wa milele na afya kamili-fu kwa sababu Yesu alikufa kwa ajili yetu. Ili tupokee barakahizo, tunahitaji kuonyesha kwamba tunathamini zawadiya fidia.

UNAWEZA KUONYESHAJE KWAMBAUNATHAMINI FIDIA?

18 Kwa nini tunapaswa kumshukuru Yehova kwa fidia?Zawadi huwa yenye thamani hasa ikiwa mtoaji ametu-mia wakati, jitihada, au gharama. Mioyo yetu huchochewatunapopata zawadi kutoka kwa mtu anayetupenda kikwe-li. Fidia ndiyo zawadi bora zaidi, kwa sababu Mungu

17. Kwa kuwa Yesu alikufa kwa ajili yetu, tunaweza kupata barakagani?18. Kwa nini tunapaswa kumshukuru Yehova kwa zawadi ya fidia?

Njia moja ya kuonyeshakwamba unathamini

zawadi ya fidia nikujifunza mengi zaidi

kumhusu Yehova

alijidhabihu kwa njia kubwa sana ili kuiandaa. Andiko laYohana 3:16 lasema: “Mungu aliupenda ulimwengu sanahivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee.” Fidiani uthibitisho wa pekee sana wa upendo wa Yehova kwetu.Pia, inaonyesha upendo wa Yesu kwa kuwa alikubali kutoauhai wake kwa ajili yetu. (Yohana 15:13) Kwa hiyo, zawadiya fidia inapaswa kutusadikisha kwamba Yehova na Mwa-na wake wanampenda kila mmoja wetu.—Wagalatia 2:20.

19 Unaweza kuonyeshaje kwamba unathamini zawadi yaMungu ya fidia? Kwanza, jifunze mengi kumhusu Mpa-ji huyo Mkuu, Yehova. (Yohana 17:3) Kujifunza Bibliakwa kutumia kitabu hiki kutakusaidia kumjua zaidi. Kadiriunavyozidi kumjua Yehova, ndivyo upendo wako una-vyozidi kuongezeka. Kisha, upendo huo utakufanya utakekumpendeza.—1 Yohana 5:3.

20 Onyesha kwamba una imani katika dhabihu ya fidiaya Yesu. Yesu alisema: “Yule anayemwamini Mwana anauzimawamilele.” (Yohana3:36) Tunawezakuonyeshajekwa-mba tunamwamini Yesu? Imani ya aina hiyo haionyeshwikwa maneno tu. Andiko la Yakobo 2:26 linasema: “Imanibilamatendo imekufa.”Ndiyo, imaniyakweli inathibitishwakwa “matendo,” yaani, jinsi tunavyojiendesha. Tunaweza ku-onyesha kwamba tunamwamini Yesu kwa kujitahidi sanakumwiga kwa maneno na matendo.—Yohana 13:15.

21 Hudhuria mwadhimisho wa kila mwaka wa Mlo wa Jio-ni wa Bwana. Jioni ya Nisani 14, 33 W.K., Yesu alianzishamwadhimisho ambao katika Biblia unaitwa “mlo wa jioniwa Bwana.” (1 Wakorintho 11:20; Mathayo 26:26-28) Mwa-dhimisho huo pia huitwa Ukumbusho wa kifo cha Yesu.

19, 20. Unaweza kuonyeshaje kwamba unathamini zawadi ya Munguya fidia?21, 22. (a) Kwa nini tunapaswa kuhudhuria Mlo wa Jioni wa Bwanawa kila mwaka? (b) Ni nini kitakachozungumziwa katika Sura ya 6na 7?

Fidia—Zawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu 55

Yesu aliuanzisha ili kuwasaidia mitume wake na Wakristowote wa kweli kuzingatia akilini kwamba kupitia kifo cha-ke akiwa mwanadamu mkamilifu, alitoa nafsi yake au uhaiwake uwe fidia. Yesu aliagiza hivi kuhusu mwadhimishohuo: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”(Luka 22:19) Kuadhimisha Ukumbusho hutukumbushaupendo ulioonyeshwa na Yehova na Yesu kuhusiana na fi-dia. Tunaweza kuonyesha kwamba tunathamini fidia kwakuhudhuria mwadhimisho wa kila mwaka wa Ukumbushowa kifo cha Yesu.�

22 Kwa kweli, fidia iliyotolewa na Yehova ni zawadi yenyethamani sana. (2 Wakorintho 9:14, 15) Zawadi hiyo yenyethamani inaweza kuwafaidi hata wale ambao wamekufa.Habari hiyo itazungumziwa katika Sura ya 6 na ya 7.

� Unaweza kupata habari zaidi kuhusu maana ya Mlo wa Jioni waBwana katika Nyongeza, ukurasa wa 206-208.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Fidia ni njia ya Yehova ya kuwakomboa wa-nadamu kutoka katika dhambi na kifo.—Waefeso 1:7.

ˇ Yehova aliandaa fidia kwa kumtuma Mwanawake mzaliwa-pekee aje duniani ili afe kwaajili yetu.—1 Yohana 4:9, 10.

ˇ Fidia inatuwezesha kupata msamaha wadhambi, dhamiri safi, na tumaini la uzimawa milele.—1 Yohana 1:8, 9.

ˇ Tunaonyesha kwamba tunathamini fidiakwa kujifunza mengi zaidi kumhusu Yehova,kuwa na imani katika dhabihu ya fidia yaYesu, na kuhudhuria Mlo wa Jioni wa Bwa-na.—Yohana 3:16.

56 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

WATU wameuliza maswali haya kwa maelfu ya miaka. Nimaswali muhimu. Hata tuwe nani au tunaishi wapi, tu-ngependa kupata majibu ya maswali hayo.

2 Katika Sura ya 5, tulizungumzia jinsi dhabihu ya fi-dia ya Yesu Kristo ilivyofungua njia ya kupata uzimawa milele. Pia tulijifunza kwamba Biblia inatabiri kuhusuwakati ambapo “kifo hakitakuwapo tena.” (Ufunuo 21:4)Kwa sasa, sisi sote tunakufa. Mfalme Sulemani mwenyehekima alisema: “Walio hai wanajua kwamba watakufa.”(Mhubiri 9:5) Sisi hujitahidi kuishi muda mrefu iweze-kanavyo. Hata hivyo, tungependa kujua ni nini hutupatatunapokufa.

3 Sisi huomboleza wapendwa wetu wanapokufa. Hu-enda tukauliza: ‘Wameenda wapi? Je, wanateseka? Je,wanaweza kutusaidia? Je, tunaweza kuwasaidia? Je, tuta-waona tena?’ Dini za ulimwengu hujibu maswali hayakwa njia tofauti-tofauti. Baadhi ya dini hizo hufundishakwamba ukiishi maisha ya uadilifu, utaenda mbingunilakini ikiwa unaishi maisha mabaya, utateketezwa moto-ni. Dini nyingine hufundisha kwamba watu wanapokufahuenda kuishi katika makao ya roho pamoja na maba-bu zao. Na nyingine hufundisha kwamba wafu huenda

1-3. Watu huuliza maswali gani kuhusu kifo, na dini mbalimbali hu-yajibuje?

SURA YA SITA

Wafu Wako Wapi?

Inakuwaje tunapokufa?

Kwa nini tunakufa?

Je, ingefariji kujua ukweli kuhusu kifo?

ahera wakahukumiwe kisha huzaliwa upya katika mwilimwingine.

4 Dini zote hizo zinafundisha jambo moja la msingi,kwamba sehemu fulani ya mwanadamu huendelea ku-ishi baada ya mwili kufa. Karibu kila dini, za zamanina za sasa, husema kwamba sisi huendelea kuishi mile-le tukiwa na uwezo wa kuona, kusikia, na kufikiri. Hatahivyo, hilo linawezekanaje? Hisia zetu, pamoja na mawa-zo yetu, zinahusiana na jinsi ubongo wetu unavyofanyakazi. Ubongo huacha kufanya kazi mtu anapokufa. Ku-mbukumbu letu na hisia zetu haziendelei kufanya kazibaada ya ubongo kufa.

INAKUWAJE MTU ANAPOKUFA?5 Yehova, Muumba wa ubongo anajua kinachotukia

tunapokufa. Anajua ukweli na katika Neno lake, Biblia,anaeleza hali ya wafu. Biblia inafundisha hivi waziwazi:Mtu anapokufa, hayupo tena. Kifo ni kinyume cha uhai.Wafu hawaoni, hawasikii wala kufikiri. Hakuna sehemuyoyote ya mwili wetu inayoendelea kuishi baada ya mwi-li kufa. Hatuna nafsi au roho isiyoweza kufa.�

6 Baada ya Sulemani kutaja kwamba walio hai wana-jua kwamba watakufa, aliandika hivi: “Lakini wafu,hawajui lolote kamwe.” Kisha akafafanua kweli hiyo yamsingi kwa kusema kwamba wafu hawawezi kupendawala kuchukia na kwamba “hakuna kazi, wala utunga-ji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi.” (Mhubiri 9:5, 6, 10) Vivyo hivyo, andiko la Zaburi 146:4 linase-ma kwamba mtu anapokufa, “mawazo yake hupotea.”

� Unaweza kupata habari zaidi kuhusu “nafsi” na “roho” katikaNyongeza, ukurasa wa 208-211.

4. Dini nyingi hufundisha jambo gani la msingi kuhusu kifo?5, 6. Biblia hufundisha nini kuhusu hali ya wafu?

58 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Sisi hufa wala hatuendelei kuishi baa-da ya mwili kufa. Maisha yetu ni kamamoto. Unapozimika, hauendi popote.Haupo tena.

MAMBO AMBAYO YESUALIFUNDISHA KUHUSU KIFO

7 Yesu Kristo alizungumzia hali yawafu rafiki yake Lazaro alipokufa. Yesualiwaambia wanafunzi wake: “Lazarorafiki yetu anapumzika.” Wanafunzi wa-lifikiri Yesu anamaanisha kwamba Lazaroanapumzika katika usingizi kwa sababuni mgonjwa. Walikosea. Yesu akawaa-mbia: “Lazaro amekufa.” (Yohana 11:11-14) Ona kwamba Yesu alifananishakifo na pumziko au usingizi. Lazaro ha-kuwa mbinguni wala motoni. Hakuwaakikutana na malaika wala mababu. Wala hakuwa aki-badilika ili azaliwe tena akiwa mwanadamu mwingine.Alikuwa akipumzika katika kifo kana kwamba analalausingizi mzito usio na ndoto. Maandiko mengine piahulinganisha kifo na usingizi. Kwa mfano, mwanafunziStefano alipouawa kwa kupigwa mawe, Biblia inasemakwamba ‘alilala usingizi.’ (Matendo 7:60) Hali kadha-lika, mtume Paulo aliwataja watu fulani katika siku zakeambao walikuwa “wamelala usingizi” katika kifo.—1 Wa-korintho 15:6.

8 Je, Mungu alikusudia watu wafe? Hapana! Yeho-va alimuumba mwanadamu aishi milele duniani. Kamatulivyojifunza mwanzoni mwa kitabu hiki, Mungu aliwa-weka wanadamu wawili wa kwanza katika paradiso yenye

7. Yesu alifafanuaje kifo?8. Tunajuaje kwamba Mungu hakukusudia watu wafe?

Moto huenda wapiunapozimika?

Wafu Wako Wapi?

kupendeza. Aliwapa afya kamilifu. Yehova aliwatakiamema. Je, kuna mzazi yeyote mwenye upendo anaye-taka watoto wake wateseke kwa sababu ya uzee na kifo?Bila shaka hakuna! Yehova aliwapenda watoto wake naalitaka waishi milele kwa furaha duniani. Biblia inasemahivi kuwahusu wanadamu: “Wakati usio na kipimo [Ye-hova] ameuweka ndani ya moyo wao.” (Mhubiri 3:11)Mungu alituumba tukiwa na tamaa ya kuishi milele.Naye amepanga jinsi tamaa hiyo itakavyotimizwa.

Yehova aliwaumba wanadamuwaishi milele duniani

60 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

KWA NINI WANADAMU HUFA?9 Kwa nini basi wanadamu hufa? Ili kupata jibu, lazima

tuzingatie kilichotukia kulipokuwa na mwanamume namwanamke mmoja tu duniani. Biblia inaeleza: “YehovaMungu akachipusha katika nchi kila mti wenye ku-tamanika kwa macho ya mtu na ulio mwema kwa ajili yachakula.” (Mwanzo 2:9) Hata hivyo, alikatazwa kufanyajambo moja. Yehova alimwambia Adamu hivi: “Matundaya kila mti wa bustani unaweza kula mpaka ushibe. Laki-ni kuhusu matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabayausile, kwa maana siku utakapokula, utakufa hakika.”(Mwanzo 2:16, 17) Haikuwa vigumu kutii amri hiyo. Ku-likuwa na miti mingine mingi ambayo Adamu na Hawawangekula matunda yake. Lakini amri hiyo iliwapa na-fasi ya pekee ya kuonyesha shukrani kwa Yule aliyewapakila kitu, kutia ndani uhai mkamilifu. Utii wao ungeo-nyesha pia kwamba waliheshimu mamlaka ya Baba yaowa mbinguni na kwamba walitaka mwongozo wake we-nye upendo.

10 Inasikitisha kwamba wenzi hao wa kwanza wa ki-binadamu waliamua kutomtii Yehova. Akiongea kupitianyoka, Shetani alimuuliza Hawa hivi: “Je, ni kweli kwa-mba Mungu alisema msile matunda ya kila mtiwa bustani?” Hawa akamjibu: “Tunaweza kula matundaya miti ya bustani. Lakini kuhusu kula matunda ya mtiulio katikati ya bustani, Mungu amesema, ‘Msiyale, walamsiyaguse ili msife.’”—Mwanzo 3:1-3.

11 Shetani akamwambia: “Hakika hamtakufa. Munguanajua kwamba siku ileile mtakapokula matunda yakemacho yenu yatafunguliwa, nanyi mtakuwa kama

9. Yehova alimkataza Adamu kufanya nini, na kwa nini haikuwa vi-gumu kutii amri hiyo?10, 11. (a) Wenzi wa kwanza wa kibinadamu walikosaje kumtii Mu-ngu? (b) Kwa nini kutotii kwa Adamu na Hawa kulikuwa jambo zito?

Wafu Wako Wapi? 61

Mungu, mkijua mema na mabaya.” (Mwanzo 3:4, 5) She-tani alitaka Hawa aamini kwamba angefaidika kwa kulatunda lililokatazwa. Kulingana na Shetani, Hawa angewe-za kujiamulia lililo sawa na lililo kosa; angefanya atakalo.Shetani pia alidai kwamba Yehova alikuwa amesema uwo-ngo kuhusu matokeo ya kula tunda. Hawa alimwaminiShetani. Kwa hiyo alichukua tunda hilo akala. Kisha aka-mpa mumewe, naye pia akala. Hawakufanya hivyo kwakutojua. Walijua kwamba walikuwa wakifanya kile amba-cho Mungu aliwaambia wasifanye. Kwa kula tunda hilo,walikosa kutii kimakusudi amri rahisi na isiyodai mengi.Walimdharau Baba yao wa mbinguni na mamlaka yake.Hawakuwa na sababu ya kutomheshimu Muumba waomwenye upendo!

Adamu alitoka mavumbini,naye alirudi mavumbini

62 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

12 Kwa mfano: Ungehisije kama ungemlea na kumtunzamwana au binti ambaye angekataa kukutii na hivyo kuo-nyesha kwamba hakuheshimu wala hakupendi? Ungehisiuchungu moyoni. Wazia uchungu ambao Yehova alihisiwakati Adamu na Hawa walipomwasi.

13 Yehova hakuwa na sababu ya kuwaacha Adamu naHawa wasiomtii waendelee kuishi milele. Walikufa kamaYehova alivyokuwa amesema. Adamu na Hawa wakakomakuwapo. Hawakuendelea kuishi mahali pengine wakiwavi-umbe wa roho. Tunajua hivyo kwa sababu ya yale ambayoYehova alimwambia Adamu baada ya kuzungumza nayekuhusu uasi wake.Mungu alisema: ‘Utarudi katika udongo,kwa kuwa ulitolewa katika huo. Kwa maana wewe ni ma-vumbi nawe utarudi mavumbini.’ (Mwanzo 3:19) Mungualimuumba Adamu kutokana na mavumbi ya nchi. (Mwa-nzo 2:7) Kabla ya kuumbwa, Adamu hakuwapo. Kwa hiyo,Yehova aliposema kwamba Adamu angerudi mavumbini,alimaanisha kwamba Adamu hangekuwapo tena. Adamuhangekuwa na uhai kama vile mavumbi yaliyotumiwa ku-muumba yasivyo na uhai.

14 Adamu na Hawa wangekuwa hai leo, lakini walikufakwa sababu waliamua kutomtii Mungu na hivyo wakafa-nya dhambi. Tunakufa kwa sababu wazao wote wa Adamuwamerithi dhambi na kifo kutoka kwake. (Waroma 5:12)Dhambi hiyo ni kama ugonjwa mbaya sana uliorithiwa,ambao hakuna anayeweza kuuepuka. Kifo kinachosaba-bishwa na dhambi ni laana. Kifo ni adui wala si rafiki.(1 Wakorintho 15:26) Tunapaswa kumshukuru Yehovasana kwa sababu ameandaa fidia ili kutuokoa kutokanana adui huyu mwenye kutisha!

12. Ni nini kinachoweza kutusaidia kuelewa jinsi Yehova alivyohisiwakati Adamu na Hawa walipomwasi?13. Yehova alisema ingekuwaje kwa Adamu wakati wa kifo, na hilo li-namaanisha nini?14. Kwa nini tunakufa?

Wafu Wako Wapi? 63

KUNA FAIDA KUJUA UKWELI KUHUSU KIFO15 MamboambayoBiblia inafundishakuhusuhaliyawafu

yanafariji. Kama ambavyo tumeona, wafu hawahisi ma-umivu wala uchungu. Hatuna sababu ya kuwaogopa wafukwani hawawezi kutuumiza. Hawahitaji msaada wetu walahawawezi kutusaidia. Hatuwezi kuzungumza nao. Viongoziwengi wa kidini hudai kwamba wanaweza kuwasaidia wafu,na watu wanaowaamini huwapa pesa. Lakini kujua ukwelikuhusu hali ya wafu hutulinda tusidanganywe na wale wa-naofundisha uwongo.

16 Je, dini nyingi hukubali mafundisho ya Biblia kuhusuhali ya wafu? Nyingi hazikubali. Kwa nini? Kwa sababu ma-fundisho yao yanaongozwa na Shetani. Anatumia dini yauwongo ili kuwafanya watu waamini kwamba baada ya mii-li yao kufa, wataendelea kuishi katika makao ya roho. Huoni uwongo ambao Shetani anatumia pamoja na mambomengine ya uwongo ili kuwafanya watu wamwache YehovaMungu. Anafanyaje hivyo?

17 Kama tulivyoona, dini fulani hufundisha kwamba mtuakiishi maisha mabaya, baada ya kifo ataenda motoni iliateseke milele. Fundisho hilo halimletei Mungu heshima.Yehova ni Mungu mwenye upendo na hawezi kamwe ku-watesa watu hivyo. (1 Yohana 4:8) Wewe ungeonaje ikiwamtu angemtia nidhamu mtoto asiyetii kwa kuishikilia miko-no yake motoni ili aungue? Je, unaweza kumheshimu mtuhuyo? Je, kweli hataungetakakumjua? Hapanahata kidogo!Inaelekea utamwona kuwa mkatili sana. Shetani anataka tu-amini kwamba Yehova huwatesa watu motoni milele—kwamabilioni ya miaka!

15. Kwa nini inafariji kujua ukweli kuhusu hali ya wafu?16. Ni nani anayeongoza mafundisho ya dini nyingi, na kwa njiagani?17. Kwa nini fundisho la mateso ya milele halimletei Yehova he-shima?

64 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

18 Pia Shetani hutumia dini fulani kufundisha kwambabaada ya watu kufa wao wanakuwa viumbe wa roho ambaowanapaswa kuheshimiwa na walio hai. Kulingana na fundi-sho hilo, roho za wafu zinaweza kuwa rafiki wazuri au aduiwenye kuogopesha. Watu wengi wanaamini uwongo huo.Wanawaogopa wafu, wanawaheshimu, na kuwaabudu. Ki-nyume cha hilo, Biblia inafundisha kwamba wafu wanalalanakwamba tunapaswa kumwabudu tu Mungu wa kweli, Ye-hova, Mpaji na Muumba wetu.—Ufunuo 4:11.

19 Kujua ukweli kuhusu wafu hukulinda usidanganywena uwongo wa dini. Pia hukusaidia kuelewa mafundishomengine ya Biblia. Kwa mfano, unapojua kwambawatu wa-napokufa hawaendi katika makao ya roho, ahadi ya uzimawa milele katika paradiso duniani inakuwa na maana zaidikwako.

20 Zamani, mwanamume mwadilifu Ayubu, aliuliza swalihili: “Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena?” (Ayubu 14:14) Je,mtu asiye na uhai anayelala usingizi katika kifo anaweza ku-fufuliwa? Biblia inafundisha jambo lenye kufariji sana kamatutakavyoona katika sura inayofuata.

18. Kuwaabudu wafu kunategemea uwongo gani wa dini?19. Kujua ukweli kuhusu kifo hukusaidia kuelewa fundisho gani li-ngine la Biblia?20. Tutazungumzia swali gani katika sura inayofuata?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Wafu hawaoni, hawasikii wala kufikiri.—Mhubiri 9:5.

ˇ Wafu wanapumzika; hawateseki.—Yohana11:11.

ˇ Tunakufa kwa sababu tulirithi dhambi kuto-ka kwa Adamu.—Waroma 5:12.

Wafu Wako Wapi? 65

WAZIA kwamba unamkimbia adui mkatili. Anakushinda kwanguvu na mbio. Unajua kwamba hana huruma kwa sababuumemwona akiwaua baadhi ya rafiki zako. Kadiri unavyo-kimbia ndivyo anavyozidi kukukaribia. Yaonekana hakunatumaini. Hata hivyo, kwa ghafula, mtu fulani anatokea ilikukuokoa.Ana nguvunyingi zaidi kulikoaduiyako, naye ana-ahidi kukusaidia. Ni jambo lenye kufariji kama nini!

2 Kwa njia fulani, wewe unakimbizwa na adui wa ainahiyo. Sisi sote tunakimbizwa naye. Kama tulivyojifunza ka-tika sura iliyotangulia, Biblia inasema kifo ni adui. Hakunayeyote anayeweza kukishinda. Wengi wetu tumemwo-na adui huyo akiwaua watu tunaowapenda. Lakini Yehovaana nguvu nyingi zaidi kuliko kifo. Yeye ndiye Mwokoa-ji mwenye upendo na tayari ameonyesha kwamba anawezakumshinda adui huyo. Naye anaahidi kwamba atamharibukabisa adui huyo, yaani, kifo. Biblia inafundisha hivi: “Aduiwa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.” (1 Wakorintho15:26) Hiyo ni habari njema!

3 Kwanza, tutazungumzia matokeo ya kifo. Kufanya hivyokutatusaidia kuthamini tumaini fulani lenye kupende-za. Yehova anaahidi kwamba wafu wataishi tena. (Isaya

1-3. Ni adui gani anayetukimbiza sisi sote, na kwa nini kujifunza ma-mbo ambayo Biblia inafundisha kutatufariji?

SURA YA SABA

Tumaini Hakika kwa WapendwaWako Ambao Wamekufa

Tunajuaje kwamba kutakuwa na ufufuo?

Yehova anahisije kuhusu kuwafufua wafu?

Ni nani watakaofufuliwa?

26:19) Watarudishwa kwenye uhai tena. Hilo ndilo tumainila ufufuo.

MPENDWA WETU ANAPOKUFA4 Je, umewahi kufiwa? Huenda ukalemewa na uchungu,

huzuni, na kuhisi kwamba huna la kufanya. Nyakati kamahizo tunahitaji kutafuta faraja katika Neno la Mungu.(2 Wakorintho 1:3, 4) Biblia hutusaidia kuelewa jinsi Ye-hova na Yesu wanavyohisi kuhusu kifo. Yesu aliyekuwa nahisia kama za Babayake, alielewa uchungu wa kufiwa. (Yoha-na 14:9) Yesu alipokuwa Yerusalemu, alikuwa akimtembeleaLazaro na dada zake, Maria na Martha, ambao waliishikatika mji wa Bethania uliokuwa karibu. Wakawa marafikiwakubwa. Biblia inasema: “Yesu alimpenda Martha na dadayake na Lazaro.” (Yohana 11:5) Hata hivyo, kama tulivyojifu-nza katika sura iliyotangulia, Lazaro alikufa.

5 Yesu alihisije rafiki yake alipokufa? Masimulizi hayo ya-naonyesha kwamba Yesu aliungana na familia na rafiki zaLazaro walipokuwa wakimwombolezea. Yesu alipowaona,alilemewa na hisia. “Akaugua rohoni na kutaabika.” Kishamasimulizi hayo yanaendelea kusema kwamba ‘Yesu alito-kwa na machozi.’ (Yohana 11:33, 35) Je, huzuni ya Yesuilimaanisha kwamba hakuwa na tumaini? Hapana. Yesu ali-jua kwamba jambo la kupendeza lilikuwa karibu kutukia.(Yohana 11:3, 4) Hata hivyo, alihisi uchungu na huzuniambayo hutokana na kifo.

6 Kwa njia fulani, huzuni ya Yesu inatutia moyo. Inatufu-ndisha kwamba Yesu na Baba yake Yehova, wanachukia kifo.Lakini Yehova Mungu anaweza kumpiga na kumshinda aduihuyo! Na tuone kile ambacho Mungu alimwezesha Yesu ku-fanya.

4. (a) Hisia za Yesu mtu anapokufa zinatusaidiaje kuelewa hisia za Ye-hova kuhusu kifo? (b) Yesu alikuwa na marafiki gani wa pekee?5, 6. (a) Yesu alitendaje alipokuwa na familia na rafiki za Lazaro wa-liokuwa wakiomboleza? (b) Kwa nini huzuni ya Yesu inatutia moyo?

Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa 67

“LAZARO, NJOO HUKU NJE!”7 Lazaro alikuwa amezikwa pangoni, naye Yesu aliamuru

jiwe lililokuwa kwenye mwingilio wa pango liondolewe. Ma-rtha alipinga kwa kuwa siku nne zilikuwa zimepita, na haikosimwiliwa Lazaroulikuwa umeanza kuoza. (Yohana 11:39) Kwamaoni ya mwanadamu, hakukuwa na tumaini lolote.

8 Jiwe likaondolewa na Yesu akapaaza sauti: “Lazaro, njoohuku nje!” Ikawaje? “Huyo mtu aliyekuwa mfu akatoka.”(Yohana 11:43, 44) Je, unaweza kuwazia shangwe ya watu wa-liokuwapo? Iwe Lazaro alikuwa ndugu yao, mtu wa ukoo,au jirani yao, walijua kwamba alikuwa amekufa. Hata hi-vyo, mtu yuleyule waliyempenda, sasa alikuwa amesimamakati yao. Huenda hilo lilionekana kuwa jambo lisilowezekana.Bila shaka wengi wao walimkumbatia Lazaro kwa shangwe.Huo ulikuwa ushindi ulioje juu ya kifo!

9 Yesu hakudai kwamba alifanya muujiza huo wenye ku-staajabisha kwa nguvu zake. Katika sala aliyotoa kabla yakumwita Lazaro, Yesu alionyesha waziwazi kwamba Yeho-va ndiye Chanzo cha nguvu alizotumia. (Yohana 11:41, 42)Hiyo haikuwa mara ya kwanza kwa Yehova kutumia nguvuzake kwa njia hiyo. Ufufuo wa Lazaro ni mmoja tu katiya miujiza tisa ya ufufuo iliyorekodiwa katika Neno la Mu-ngu.� Inafurahisha kusoma na kujifunza masimulizi hayo.YanatufundishakwambaMungu hanaubaguzi, kwakuwawa-liofufuliwa walitia ndani watoto kwa watu wazima, wanaumekwa wanawake, Waisraeli na watu wasio Waisraeli. Na ni sha-ngwe iliyoje inayotajwa katika masimulizi hayo! Kwa mfano,

� Masimulizi mengine yako katika 1 Wafalme 17:17-24; 2 Wafalme4:32-37; 13:20, 21; Mathayo 28:5-7; Luka 7:11-17; 8:40-56; Matendo 9:36-42; na 20:7-12.

7, 8. Kwa nini huenda watu hawakufikiri kwamba Lazaro angewezakuishi tena, hata hivyo Yesu alifanya nini?9, 10. (a) Yesu alionyeshaje Chanzo cha nguvu alizotumia kumfufuaLazaro? (b) Kusoma masimulizi ya Biblia kuhusu ufufuo kuna faidagani?

68 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Eliya alimfufua mwana wamjane.—1 Wafalme 17:17-24

Mtume Petro alimfufuamwanamke Mkristoaliyeitwa Dorkasi.

—Matendo 9:36-42

Ufufuo wa Lazaroulitokeza shangwe kubwa.

—Yohana 11:38-44

Yesu alipomfufua msichana mdogo, wazazi wake ‘walikuwana shangwe kubwa.’ (Marko 5:42) Kwa kweli, Yehova alikuwaamewapa sababu ya kushangilia ambayo hawangesahau ka-mwe.

10 Bila shaka, watu waliofufuliwa na Yesu walikufa tena. Je,hilo linamaanisha kwamba hakukuwa na maana yoyote yakuwafufua? Hapana. Masimulizi hayo ya Biblia yanathibiti-sha kweli muhimu na yanatupa tumaini.

MAMBO TUNAYOJIFUNZA KUTOKANANA MASIMULIZI YA UFUFUO

11 Biblia inafundisha kwamba wafu “hawajui lolote ka-mwe.” Hawako hai wala hawaendelei kuishi mahali pengine.Masimulizi kuhusu Lazaro yanathibitisha jambo hilo. Ali-pofufuliwa, je, Lazaro aliwasisimua watu kwa kuwaelezamambo aliyoona mbinguni? Au je, aliwaogopesha kwa ku-wasimulia mambo yenye kutisha kuhusu moto wa mateso?Hapana. Biblia haisemi kwamba Lazaro alisema mambohayo. Kwa siku nne alizokuwa amekufa ‘hakujua lolote ka-mwe.’ (Mhubiri 9:5) Lazaro alikuwa amelala usingizi katikakifo.—Yohana 11:11.

12 Masimulizi kuhusu Lazaro yanatufundisha pia kwambaufufuo ni jambo halisi, wala si hadithi tu. Yesu alimfufuaLazaro mbele ya watazamaji wengi. Hata viongozi wa kidi-ni ambao walimchukia Yesu hawakupinga kwamba muujizahuo haukutukia. Badala yake, walisema: “Tufanye nini, kwasababu mtu huyu [Yesu] anafanya ishara nyingi?” (Yohana11:47) Watu wengi walienda kumwona mtu huyo aliyeku-wa amefufuliwa. Kwa hiyo, wengi zaidi wakamwamini Yesu.Kufufuliwa kwa Lazaro kuliwathibitishia kwamba Yesu ali-kuwa ametumwa na Mungu. Huo ulikuwa uthibitisho

11. Masimulizi kuhusu ufufuo wa Lazaro yanathibitishaje ukweli waMhubiri 9:5?12. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba kwa kweli Lazaro ali-fufuliwa?

70 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

wenye nguvu sana hata viongozi fulani wa dini ya Kiyahudiwenye mioyo migumu wakapanga njama ya kumuua Yesuna Lazaro.—Yohana 11:53; 12:9-11.

13 Je, kuamini kwambawatu wanaweza kufufuliwa ni ndo-to tu? Hapana, kwa kuwa Yesu alifundisha kwamba sikumoja “wale wote waliomo ndani ya makaburi” watafufuli-wa. (Yohana 5:28) Yehova ndiye Chanzo cha uhai wote.Basi, si vigumu kuamini kwamba anaweza kuurudisha uhaitena. Ni kweli kwamba Yehova atawafufua wafu walio katikakumbukumbu lake. Je, anaweza kuwakumbuka wapendwawetu waliokufa? Kuna nyota zisizo na hesabu angani, laki-ni Mungu huziita zote kwa majina! (Isaya 40:26) Kwa hiyo,Yehova Mungu anaweza kukumbuka habari zote kuhusu wa-pendwa wetu waliokufa, naye ana uwezo wa kuwafufua.

14 Hata hivyo, Yehova anahisije kuhusu kufufua wafu?Biblia inafundisha kwamba anatamani kuwafufua. Mwa-namume mwaminifu Ayubu aliuliza hivi: “Mtu akifa, je,anaweza kuishi tena?”Ayubu alikuwa akizungumzia kuhusukungoja kaburini mpaka wakati ambapo Mungu angemku-mbuka. Alimwambia Yehova: “Utaita, na mimi mwenyewenitakujibu. Kwa kuwa utaitamani sana kazi ya mikonoyako.”—Ayubu 14:13-15.

15 Hebu fikiria! Yehova anatamani sana kuwafufua wafu.Je, haichangamshi kujua kwamba Yehova anahisi hivyo?Lakini ufufuo wa wakati huo utakuwaje? Ni nani watakaofu-fuliwa, nao watakuwa wapi?

“WOTE WALIOMO NDANIYA MAKABURI YA UKUMBUSHO”

16 Masimulizi ya Biblia kuhusu ufufuo hutufundisha

13. Kwa nini tunaweza kuamini kwamba kwa kweli Yehova atawafu-fua wafu?14, 15. Kama Ayubu alivyosema, Yehova anahisije kuhusu kuwafufuawafu?16. Wafu watakaofufuliwa wataishi katika hali gani?

Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa 71

mengi kuhusu ufufuo ujao. Watu waliofufuliwa hapa du-niani waliungana tena na wapendwa wao. Katika ufufuoujao hali itakuwa bora hata zaidi. Kama tulivyojifunza katikaSura ya 3, Mungu alikusudia dunia yote iwe paradiso. Kwahiyo, wafu hawatafufuliwa waishi katika ulimwengu wenyevita, uhalifu, na magonjwa. Wataishi milele katika dunia hiikwa amani na furaha.

17 Ni nani watakaofufuliwa? Yesu alisema kwamba “wotewaliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sau-ti yake [Yesu] na kutoka.” (Yohana 5:28, 29) Vivyo hivyo,andiko la Ufunuo 20:13 linasema: “Bahari ikawatoa walewafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi [“Hadesi,”kielezi-chini] vikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake.”“Hadesi” ni kaburi. (Ona Nyongeza, ukurasa wa 212-213.)Kaburi hilo litabaki tupu. Mabilioni ya watu wanaopumzi-ka humo wataishi tena. Mtume Paulo alisema: “Kutakuwana ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.” (Matendo24:15) Hilo linamaanisha nini?

18 “Waadilifu” wanatia ndani watu wengi walioishi kablaya Yesu kuja duniani ambao tunasoma juu yao katika Biblia.Huenda ukamfikiria Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Ruthu,Esta, na wengine wengi. Baadhi ya wanaume na wanawakehao wenye imani wanazungumziwa katika Waebrania suraya 11. Lakini “waadilifu” pia wanatia ndani watumishi waYehovawanaokufa siku zetu. Kwa kuwa tuna tumaini la ufu-fuo, hatuogopi kufa.—Waebrania 2:15.

19 Vipi wale wote ambao hawakumtumikia wala kumtiiYehova kwa sababu hawakupata kumjua? Mabilioni hayoya watu “wasio waadilifu” hawatasahauliwa. Wao pia wata-fufuliwa na kupewa nafasi ili wajifunze kumhusu Mungu

17. Ni nani watakaofufuliwa?18. “Waadilifu” watakaofufuliwa wanatia ndani nani, na tumaini hilolinaweza kuwa na matokeo gani maishani mwako?19. Ni nani “wasio waadilifu,” na Yehova amewaonyesha fadhili kwakuwapa nafasi ya kufanya nini?

72 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

wa kweli na kumtumikia. Kwa kipindi cha miaka elfu moja,wafu watafufuliwa na kupewa nafasi ya kumtumikia Yeho-va pamoja na wanadamu waaminifu duniani. Kitakuwakipindi kizuri ajabu! Biblia inakiita kipindi hicho Siku yaHukumu.�

20 Je, hiyo inamaanisha kwamba kila mwanadamu amba-ye amewahi kuishi atafufuliwa? Hapana. Biblia inasemakwamba baadhi ya wafu wako “Gehena.” (Luka 12:5) Ge-hena lilitokana na bonde la takataka lililokuwa nje ya jiji lakale la Yerusalemu. Mizoga na takataka ziliteketezwa humo.Wafu ambao miili yao ilitupwa humo walionwa na Waya-hudi kuwa hawastahili kuzikwa wala kufufuliwa. Kwa hiyo,kwa kufaa Gehena inawakilisha uharibifu wa milele. Inga-wa Yesu atashiriki kuwahukumu walio hai na wafu, Yehovandiye Hakimu mkuu. (Matendo 10:42) Hatawafufua kamwewatu atakaowahukumu kuwa waovu na wasiotaka ku-badilika.

UFUFUO WA KIMBINGU21 Biblia inataja pia ufufuo wa aina nyingine. Watakaopa-

ta ufufuo huo wataishi mbinguni wakiwa viumbe wa roho.Ni ufufuo mmoja tu wa aina hiyo unaotajwa katika Biblia,yaani, ule wa Yesu Kristo.

22 Baada ya Yesu kufa akiwa mwanadamu, Yehova haku-ruhusu Mwana Wake mwaminifu aendelee kukaa kaburini.(Zaburi 16:10; Matendo 13:34, 35) Mungu alimfufua Yesu,lakini si katika mwili wa kibinadamu. Mtume Petro anaele-za kwamba Kristo “aliuawa katika mwili, lakini akafanywakuwa hai katika roho.” (1 Petro 3:18) Kwa kweli, huo

� Unaweza kupata habari zaidi kuhusu Siku ya Hukumu na msingiwa hukumu, katika Nyongeza, ukurasa wa 213-215.

20. Gehena ni nini, na ni nani wanaoenda huko?21, 22. (a) Kuna ufufuo gani mwingine? (b) Ni nani aliyekuwa wakwanza kabisa kufufuliwa akiwa na mwili wa roho?

Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa 73

ulikuwa muujiza mkubwa. Yesu alikuwa hai tena akiwamtu wa roho mwenye nguvu! (1 Wakorintho 15:3-6) Yesundiye wa kwanza kabisa kupokea ufufuo huo mtukufu. (Yo-hana 3:13) Lakini siye wa mwisho.

23 Akijua kwamba angerudi mbinguni baada ya mudamfupi, Yesu aliwaambia wafuasi wake waaminifu kwamba‘angewatayarishia mahali’ huko. (Yohana 14:2) Yesu alise-ma wale wanaoenda mbinguni ni ‘kundi lake dogo.’ (Luka12:32) Kikundi hicho kidogo kitakuwa na Wakristo waami-nifu wangapi? Mtume Yohana anasema hivi katika Ufunuo14:1: “Nikaona, na, tazama! Mwana-Kondoo [Yesu Kristo]amesimama juu ya Mlima Sayuni, na pamoja naye 144,000wakiwa na jina lake na jina la Baba yake limeandikwa juu yamapaji ya nyuso zao.”

24 Wakristo hao 144,000, kutia ndani mitume waamini-fu wa Yesu, watafufuliwa wakaishi mbinguni. Watafufuliwawakati gani? Mtume Paulo aliandika kwamba wangefufu-liwa wakati wa kuwapo kwa Kristo. (1 Wakorintho 15:23)Kama utakavyojifunza katika Sura ya 9, tunaishi katikakipindi hicho cha wakati. Kwa hiyo wachache wanaoba-ki kati ya wale 144,000 ambao wanakufa leo wanafufuliwamara moja na kwenda kuishi mbinguni. (1 Wakorintho 15:51-55) Hata hivyo, idadi kubwa ya wanadamu wana tumai-ni la kufufuliwa na kuishi katika Paradiso duniani wakatiujao.

25 Naam, kwa kweli Yehova atamshinda adui yetu kifo,atamwondolea mbali milele! (Isaya 25:8) Hata hivyo, hue-nda ukauliza, ‘Wale wanaofufuliwa na kwenda mbinguniwatafanya nini huko?’ Watakuwa sehemu ya serikali nzuriya Ufalme huko mbinguni. Tutajifunza mengi zaidi kuhu-su serikali hiyo katika sura inayofuata.

23, 24. “Kundi dogo” lililotajwa na Yesu ni akina nani, na ni wa-ngapi?25. Tutajifunza nini katika sura inayofuata?

74 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Masimulizi ya Biblia kuhusu ufufuo yanatu-pa tumaini hakika.—Yohana 11:39-44.

ˇ Yehova anatamani kuwafufua wafu.—Ayubu14:13-15.

ˇ Wale wote walio kaburini watafufuliwa.—Yohana 5:28, 29.

Katika Paradiso, wafu watafufuka nakuungana tena na wapendwa wao

Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa 75

MAMILIONI ya watu ulimwenguni wanajua sala ambayowengi huiita Sala ya Baba Yetu, au Sala ya Bwana. Majinahayo mawili yanarejelea ile sala inayojulikana sana ambayoYesu Kristo mwenyewe aliitoa kama kielelezo. Ni sala yenyemaana sana, na kuchunguza mambo matatu ya kwanza ka-tika sala hiyo kutakusaidia kujua mambo mengi ambayoBiblia inafundisha.

2 Mwanzoni mwa sala hiyo ya kielelezo, Yesu aliwafundi-sha wasikilizaji wake hivi: “Basi, ninyi msali hivi: ‘Baba yetuuliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje.Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbingu-ni.’” (Mathayo 6:9-13) Mambo hayo matatu yanayoombwayanamaanisha nini?

3 Tayari tumejifunza mengi kuhusu jina la Mungu, Ye-hova. Na kwa kadiri fulani tumezungumzia mapenzi yaMungu, yaani, mambo ambayo amefanya na yale ataka-yowafanyia wanadamu. Hata hivyo, Yesu alimaanisha ninialipotuambia tusali: “Ufalme wako uje”? Ufalme wa Mungu

1. Tutazungumzia sala gani inayojulikana sana?2. Ni mambo gani matatu ambayo Yesu aliwafundisha wanafunziwake waombe?3. Tunahitaji kujua nini kuhusu Ufalme wa Mungu?

SURA YA NANE

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Biblia inatufundisha nini kuhusuUfalme wa Mungu?

Ufalme wa Mungu utafanya nini?

Ufalme huo utatimiza mapenzi yaMungu duniani wakati gani?

ni nini? Ufalme huo utakapokuja, utalitakasaje jina la Mu-ngu au kulifanya liwe takatifu? Na kuja kwa Ufalme huokunahusianaje na kutendeka kwa mapenzi ya Mungu?

UFALME WA MUNGU NI NINI?4 Ufalme wa Mungu ni serikali iliyosimamishwa na Ye-

hova Mungu ikiwa na Mfalme ambaye amechaguliwa naMungu. Mfalme wa Ufalme wa Mungu ni nani? Ni YesuKristo.Yesuakiwa Mfalme, nimkuukulikowatawalawa kibi-nadamu na anaitwa “Mfalme wa wale wanaotawala wakiwawafalme na Bwana wa wale wanaotawala wakiwa mabwa-na.” (1 Timotheo 6:15) Ana nguvu za kufanya mambomengi mazuri kuliko mtawala yeyote wa kibinadamu, hatayule aliye bora zaidi.

5 Ufalme wa Mungu utatawala kutoka wapi? Kwani, Yesuyuko wapi? Unakumbuka, tulijifunza kwamba aliuawa kwe-nye mti wa mateso, na baadaye akafufuliwa. Muda mfupibaadaye, alirudi mbinguni. (Matendo 2:33) Kwa hiyo, hukondiko Ufalme wa Mungu uliko, yaani, mbinguni. Ndiyo sa-babu Biblia huuita ‘ufalme wa mbinguni.’ (2 Timotheo 4:18)Ingawa Ufalme wa Mungu uko mbinguni, utatawala dunia.—Ufunuo 11:15.

6 Kwa nini Yesu ni Mfalme wa pekee? Sababu moja nikwamba, hatakufa kamwe. Ikimlinganisha na wafalmewa kibinadamu, Biblia inamwita Yesu “yeye peke yakeasiyeweza kufa, anayekaa katika nuru isiyoweza kufikiwa.”(1 Timotheo 6:16) Hilo linamaanisha kwamba mambo yotemazuri ambayo Yesu atafanya yatadumu. Naye kwa kweliatafanya mambo mengi mazuri.

7 Hebu fikiria unabii huu wa Biblia kumhusu Yesu: “Rohoya Yehova itatua juu yake, roho ya hekima na ya uelewaji,

4. Ufalme wa Mungu ni nini, na Mfalme wake ni nani?5. Ufalme wa Mungu unatawala kutoka wapi, nao utatawala nini?6, 7. Kwa nini Yesu ni Mfalme wa pekee?

Ufalme wa Mungu Ni Nini? 77

roho ya shauri na ya nguvu, roho ya ujuzi na ya kumwo-gopa Yehova; naye atakuwa na shangwe katika kumwogopaYehova. Na hatahukumu kulingana na sura inayoonekanakwa macho yake tu, wala kukaripia kulingana tu na jambolililosikiwa na masikio yake. Naye atawahukumu kwa uadi-lifu watu wa hali ya chini, atakaripia kwa unyoofu kwaajili ya watu wapole wa dunia.” (Isaya 11:2-4) Maneno hayoyanaonyesha kwamba Yesu atakuwa Mfalme mwadilifu namwenye huruma atakayetawala watu wa dunia. Je, ungepe-nda kuwa na mtawala kama huyo?

8 Jambo lingine kuhusu Ufalme wa Mungu ni kwambaYesu hatatawala akiwa peke yake. Atatawala pamoja na we-ngine. Kwa mfano, mtume Paulo alimwambia Timotheohivi: “Tukiendelea kuvumilia, tutatawala pamoja pia tuki-wa wafalme.” (2 Timotheo 2:12) Naam, Paulo, Timotheo,na waaminifu wengine ambao wamechaguliwa na Munguwatatawala pamoja na Yesu katika Ufalme wa mbinguni. Niwangapi watakaokuwa na pendeleo hilo?

9 Kama tulivyoona katika Sura ya 7 ya kitabu hiki, mtumeYohana aliona katika maono “Mwana-Kondoo [Yesu Kristo]amesimama juu ya Mlima Sayuni [akiwa mfalme mbingu-ni], na pamoja naye 144,000 wakiwa na jina lake na jina laBaba yake limeandikwa juu ya mapaji ya nyuso zao.” Hao144,000 ni nani? Yohana mwenyewe anatuambia hivi: “Haondio wale wanaoendelea kumfuata Mwana-Kondoo popoteanapoenda. Hao walinunuliwa kutoka kati ya wanadamuwakiwa matunda ya kwanza kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 14:1, 4) Ndiyo, ni wafuasi waaminifu waYesu Kristo waliochaguliwa hasa kutawala mbinguni pamojanaye. Baada ya kufufuliwa na kuenda mbinguni, “wata-tawala wakiwa wafalme juu ya dunia,” pamoja na Yesu.

8. Ni nani watakaotawala pamoja na Yesu?9. Ni watu wangapi watakaotawala pamoja na Yesu, na Mungu alia-nza kuwachagua lini?

78 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

(Ufunuo 5:10) Tangu siku za mitume, Mungu amekuwaakiwachagua Wakristo waaminifu ili kukamilisha idadi hiyoya 144,000.

10 Mungu alionyesha upendo kwa kufanya mpango ili Yesuna wale 144,000 wawatawale wanadamu. Kwanza, Yesu ame-wahi kuwa mwanadamu na kuteseka. Paulo alisema kwambaYesu “si mtu ambaye hawezi kuusikitikia udhaifu wetu, baliyeye ambaye amejaribiwa katika mambo yote kama sisi we-nyewe, lakini bila kuwa na dhambi.” (Waebrania 4:15;5:8) Watawala wenzake pia wameteseka na kuvumilia waki-wa wanadamu. Isitoshe, wamepambana na kutokamilika nakukabiliana na magonjwaya aina mbalimbali. Bila shaka, wa-taelewa matatizo yanayowakabili wanadamu!

UFALME WA MUNGU UTAFANYA NINI?11 Yesu alipowaambia wanafunzi wake waombe Ufalme wa

Mungu uje, aliwaambia pia waombe mapenzi ya Mungu ya-tendeke “duniani kama ilivyo mbinguni.” Mungu yukombinguni, na sikuzote malaika waaminifu wamekuwa waki-tenda mapenzi yake huko. Hata hivyo, katika Sura ya 3 yakitabu hiki, tulijifunza kwamba malaika mwovu aliacha kute-nda mapenzi ya Mungu na kuwafanya Adamu na Hawawatende dhambi. Katika Sura ya 10, tutajifunza mengi zai-di kuhusu yale ambayo Biblia inafundisha kumhusu malaikahuyo mwovu, anayeitwa Shetani Ibilisi. Shetani na malaikawalioamua kumfuata, wanaoitwa roho waovu, waliruhusi-wa kuishi mbinguni kwa muda. Kwa hiyo, si wote waliokuwambinguni walikuwa wakitenda mapenzi ya Mungu. Mamboyangebadilika wakati Ufalme wa Mungu ungeanza kutawala.Mfalme mpya aliyetawazwa, Yesu Kristo, angepigana vita naShetani.—Ufunuo 12:7-9.

10. Kwa nini ni mpango wa upendo kwa Yesu na wale 144,000 wali-ofufuliwa kuwatawala wanadamu?11. Kwa nini Yesu aliwaambia wanafunzi wake waombe mapenzi yaMungu yatendeke mbinguni?

Ufalme wa Mungu Ni Nini? 79

12 Maneno yafuatayo ya kinabii yanaeleza jambo ambalolingetukia: “Nikaisikia sauti kubwa mbinguni ikisema: ‘Sasakumekuwa na wokovu na nguvu na ufalme wa Mungu wetuna mamlakaya Kristowake, kwa sababu [Shetani] mshtaki wanduguzetu ametupwachini, anayewashtakimchana na usikumbele za Mungu wetu!’” (Ufunuo 12:10) Je, unaona mambomawili muhimu yanayotajwa katika mstari huo wa Biblia?Kwanza, Ufalmewa Mungu unaanza kutawala Yesu Kristo aki-waMfalme.Pili, Shetanianatupwadunianikutokambinguni.

13 Mambo hayo mawili yamekuwa na matokeo gani? Ku-husu mambo yaliyotokea mbinguni tunasoma hivi: “Kwasababu hiyo furahini, enyi mbingu nanyi mnaokaa nda-ni yake!” (Ufunuo 12:12) Ndiyo, malaika waaminifu waliombinguni wanafurahi kwa sababu baada ya Shetani na ma-laika zake kuondolewa, wote walio mbinguni ni waaminifukwa Yehova Mungu. Kuna amani na upatano kamili wenyekudumu. Mapenzi ya Mungu yanatendeka mbinguni.

14 Hata hivyo, namna gani duniani? Biblia inasema: “Olewa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwe-nu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupicha wakati.” (Ufunuo 12:12) Shetani ana hasira kwa saba-bu ametupwa kutoka mbinguni na ana kipindi kifupi tu chawakati. Kwa hasira anasababisha dhiki, au “ole” duniani.Tutajifunza mengi zaidi kuhusu “ole” hiyo katika sura ina-yofuata. Hata hivyo, kwa kuwa Shetani ametupwa dunianina anasababisha dhiki, tunaweza kuuliza, Ufalme huo utafa-nyaje mapenzi ya Mungu yatendeke duniani?

15 Kumbuka mapenzi ya Mungu kwa dunia. Ulijifunza ku-yahusu katika Sura ya 3. Katika Edeni, Mungu alionyeshakwamba mapenzi yake ni kwamba dunia iwe paradiso ili-

12. Ni mambo gani mawili muhimu yanayotajwa katika Ufunuo12:10?13. Hali imekuwaje baada ya Shetani kutupwa kutoka mbinguni?14. Hali imekuwaje tangu Shetani alipotupwa duniani?15. Mapenzi ya Mungu kwa dunia ni nini?

80 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

yojaa jamii ya wanadamu waadilifu na wasiokufa. Shetanialiwafanya Adamu na Hawa watende dhambi, na hilo likaa-thiri kutimia kwa mapenzi ya Mungu duniani, lakini kusudilake halikubadilika. Bado Yehova anakusudia kwamba “wa-adilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juuyake.” (Zaburi 37:29) Na Ufalme wa Mungu utatimiza hayo.Jinsi gani?

16 Hebu fikiria unabii ulio kwenye Danieli 2:44. Tuna-soma: “Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguniatausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Naufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunjana kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mpaka wa-kati usio na kipimo.” Hilo linatuambia nini kuhusu Ufalmewa Mungu?

17 Kwanza, Ufalme wa Mungu ungesimamishwa “katikasiku za wafalme hao,” au wakati falme nyingine zingekuwazikitawala bado. Pili, Ufalme huo utadumu milele. Hau-tashindwa wala serikali nyingine haitachukua mahali pake.Tatu, tunaona kwamba kutakuwa na vita kati ya Ufalmewa Mungu na falme za ulimwengu huu. Ufalme wa Munguutashinda. Hatimaye, Ufalme wa Mungu ndio utakaokuwaserikali pekee inayowatawala wanadamu. Kisha wanadamuwatafurahia utawala bora zaidi.

18 Biblia inasema mengi kuhusu vita vya mwisho kati yaUfalmewa Mungu naserikali za ulimwenguhuu.Kwa mfano,inafundisha kwamba mwisho unapokaribia, roho waovu wa-taeneza uwongo ili kuwadanganya “wafalme wa dunia nzimainayokaliwa.” Kwa kusudi gani? “Ili kuwakusanya [wafalmehao] pamoja kwa vita vya ile siku kuu ya Mungu Mwe-za-Yote.” Wafalme wa dunia watakusanywa pamoja “mahali

16, 17. Andiko la Danieli 2:44 linasema nini kuhusu Ufalme wa Mu-ngu?18. Vita vya mwisho kati ya Ufalme wa Mungu na serikali za wana-damu vinaitwaje?

Ufalme wa Mungu Ni Nini? 81

panapoitwa katika Kiebrania Har–Magedoni.” (Ufunuo 16:14,16) Kwa sababu ya mambo yanayotajwa katika mistari hiyomiwili, vita vya mwisho kati ya serikali za wanadamu na Ufal-me wa Mungu vinaitwa vita vya Har–Magedoni.

19 Ufalme wa Mungu utatimiza nini kupitia Har–Mage-doni? Fikiria tena mapenzi ya Mungu kwa dunia. YehovaMungu alikusudia dunia ijae jamii ya wanadamu waadilifuna wakamilifu wakimtumikia katika Paradiso. Kwa nini hilohalitendeki sasa? Kwanza, sisi ni watenda dhambi na tuna-kuwa wagonjwa na kufa. Hata hivyo, tulijifunza katika Suraya 5 kwamba Yesu alikufa kwa ajili yetu ili tuweze kuishi mi-lele. Huenda unakumbuka maneno haya yaliyo katika Injiliya Yohana: “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwa-mba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee, ili kila mtuanayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa mile-le.”—Yohana 3:16.

20 Tatizo lingine ni kwamba watu wengi hutenda ma-ovu. Wanasema uwongo, wanaiba, na kujihusisha katikaukosefu wa maadili. Hawataki kutenda mapenzi ya Mungu.Watu wanaotenda maovu wataharibiwa katika vita vya Mu-ngu vya Har–Magedoni. (Zaburi 37:10) Sababu nyingine piainayofanya mapenzi ya Mungu yasitendeke duniani ni kwa-mba serikali haziwatii moyo watu wafanye hivyo. Serikalinyingi hazina uwezo, ni katili, au ni zenye ufisadi. Bibliahusema hivi waziwazi: “Mwanadamu amemtawala mwana-damu kwa kumuumiza.”—Mhubiri 8:9.

21 Baada ya Har–Magedoni, wanadamu watakuwa chiniya serikali moja tu, Ufalme wa Mungu. Ufalme huo utate-nda mapenzi ya Mungu na kuleta baraka nzuri ajabu. Kwamfano, utamwondoa Shetani na roho wake waovu. (Ufunuo20:1-3) Nguvu za dhabihu ya Yesu zitatumiwa ili kuwaondo-lea wanadamu waaminifu magonjwa na kifo. Nao wataishi

19, 20. Kwa nini mapenzi ya Mungu hayatendeki duniani sasa?21. Ufalme utatendaje mapenzi ya Mungu duniani?

82 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Kutupwa kwa Shetani na rohowake waovu kutoka mbingunikulileta ole duniani. Matatizo

hayo yatakwisha karibuni

milele chini ya utawala wa Ufalme. (Ufunuo 22:1-3) Du-nia itafanywa kuwa paradiso. Hivyo, Ufalme huo utafanyamapenzi ya Mungu yatendeke duniani na utalitakasa jinala Mungu. Hilo linamaanisha nini? Hilo linamaanisha kwa-mba hatimaye chini ya Ufalme wa Mungu kila mtu aliye haiatalitukuza jina la Yehova.

UFALME WA MUNGU UTACHUKUAHATUA WAKATI GANI?

22 Yesu alipowaambia wanafunzi wake wasali, “Acha Ufal-me wako uje,” ilikuwa wazi kwamba Ufalme huo haukuwaumekuja. Je, ulikuja Yesu alipopaa kuenda mbinguni? Ha-pana, kwa kuwa Petro na Paulo walisema kwamba baada yaYesu kufufuliwa, unabii huu katika Zaburi 110:1 ulitimizwa:“Neno la Yehova kwa Bwana wangu ni: ‘Keti kwenye mkonowangu wa kuume mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti chamiguu yako.’” (Matendo 2:32-34; Waebrania 10:12, 13) Ku-likuwa na kipindi cha kungoja.

23 Kipindi hicho cha kungoja kingeendelea kwa mudagani? Katika karne ya 19, wanafunzi wanyoofu wa Bib-lia walikadiria kwamba kipindi hicho kingefikia mwishomwaka wa 1914. (Kuhusu tarehe hiyo, ona Nyongeza, ukura-sa wa 215-218.) Matukio ya ulimwengu yaliyoanza mwaka

22. Tunajuaje kwamba Ufalme wa Mungu haukuja Yesu alipokuwaduniani au baada tu ya yeye kufufuliwa?23. (a) Ufalme wa Mungu ulianza kutawala lini? (b) Sura ifuatayo ita-zungumzia nini?

Chini ya utawala wa Ufalme, mapenzi ya Munguyatatendeka duniani kama ilivyo mbinguni

84 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

wa 1914 yanathibitisha kwamba kadirio hilo la wanafunziwanyoofu wa Biblia lilikuwa sahihi. Utimizo wa unabii waBiblia unaonyesha kwamba katika mwaka wa 1914, Kristoalitawazwa kuwa Mfalme, kisha Ufalme wa mbinguni waMungu ukaanza kutawala. Hivyo, tunaishi katika kile “ki-pindi kifupi cha wakati” kinachobaki cha Shetani. (Ufunuo12:12; Zaburi 110:2) Tunaweza pia kusema kwa hakika kwa-mba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utachukua hatua ilimapenzi ya Mungu yatendeke duniani. Je, hiyo ni haba-ri njema kwako? Je, unaamini kwamba inawezekana? Suraifuatayo itakusaidia kuona kwamba Biblia inafundisha ma-mbo haya.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguniinayotawaliwa na Yesu Kristo pamoja na wale144,000 ambao wametoka duniani.—Ufunuo14:1, 4.

ˇ Ufalme huo ulianza kutawala mwaka wa1914, na tangu wakati huo Shetani ametu-pwa duniani kutoka mbinguni.—Ufunuo12:9.

ˇ Karibuni Ufalme wa Mungu utaharibu se-rikali za wanadamu, na dunia itakuwaparadiso.—Ufunuo 16:14, 16.

Ufalme wa Mungu Ni Nini? 85

JE, UMEWAHI kusikiliza habari kwenye redio au televishe-ni na kujiuliza ‘Ulimwengu huu unaelekea wapi?’ Misibahutokea ghafula na bila kutarajiwa hivi kwamba hakunamwanadamu anayeweza kutabiri mambo ya kesho. (Yako-bo 4:14) Hata hivyo, Yehova anajua mambo ya wakati ujao.(Isaya 46:10) Zamani, Neno lake, Biblia, lilitabiri mambomabaya ambayo yangetukia siku zetu na pia likatabiri ma-mbo mazuri ya wakati ujao.

2 Yesu Kristo alizungumza kuhusu Ufalme wa Munguambao utakomesha uovu na kuifanya dunia iwe paradiso.(Luka 4:43) Watu walitaka kujua wakati ambapo Ufalmehuo ungekuja. Hata wanafunzi wa Yesu walimuuliza: “Ninini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umaliziowa mfumo wa mambo?” (Mathayo 24:3) Kwa kujibu Yesualiwaambia kwamba ni Yehova Mungu peke yake anaye-jua kabisa wakati ambapo mwisho wa mfumo huu wamambo utakuja. (Mathayo 24:36) Lakini Yesu alitabiri ma-mbo ambayo yangetokea duniani kabla tu ya Ufalme huo

1. Ni wapi tunapoweza kupata habari kuhusu wakati ujao?2, 3. Wanafunzi walimuuliza Yesu swali gani, naye alijibuje?

SURA YA TISA

Je, Tunaishi Katika“Siku za Mwisho”?

Ni mambo gani yanayotokea leoyaliyotabiriwa katika Biblia?

Neno la Mungu linasema watuwangekuwaje katika “siku za mwisho”?

Biblia inatabiri mambo gani mazurikuhusu “siku za mwisho”?

kuwaletea wanadamu amani na usalama wa kweli. Mamboaliyotabiri yanatukia leo!

3 Kabla ya kuzungumzia mambo yanayothibitisha kwa-mba tunaishi katika “umalizio wa mfumo wa mambo,”na tuzungumzie kwa ufupi vita ambavyo hakuna mwa-nadamu yeyote angeweza kuviona. Vilitukia katika makaoyasiyoonekana ya roho, na matokeo yake yanatuathiri.

VITA MBINGUNI4 Sura iliyotangulia ya kitabu hiki ilieleza kwamba Yesu

Kristo alitawazwa kuwa Mfalme mbinguni mwaka wa1914. (Danieli 7:13, 14) Muda mfupi baada ya kupokeamamlaka ya Ufalme, Yesu alichukua hatua. Biblia inase-ma kwamba “Vita vikatokea ghafula mbinguni: Mikaeli[jina lingine la Yesu] na malaika zake wakapigana na yulejoka mkubwa [Shetani Ibilisi], naye joka mkubwa na mala-ika zake wakapigana.”� Shetani na malaika zake waovu,yaani, roho waovu, walishindwa katika vita hivyo na ku-tupwa duniani kutoka mbinguni. Malaika waaminifu waMungu walifurahi kwamba Shetani na roho wake waovuwalikuwa wametupwa nje. Hata hivyo, wanadamu hawa-ngepata furaha hiyo. Biblia ilitabiri hivi: “Ole wa dunia . . .kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali,akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.”—Ufunuo 12:7, 9, 12.

5 Tafadhali ona matokeo ya vita hivyo vya mbinguni.Kwa hasira, Shetani angeleta ole au taabu duniani. Kamautakavyoona, sasa tunaishi katika kipindi hicho cha taabu.Lakini hakitakuwa kirefu, ni “kipindi kifupi cha wakati.”

� Unaweza kupata habari zinazoonyesha kwamba Mikaeli ni jina li-ngine la Yesu Kristo katika Nyongeza, ukurasa 218-219.

4, 5. (a) Ni nini kilichotokea mbinguni mara tu baada ya Yesu ku-tawazwa kuwa Mfalme? (b) Kulingana na Ufunuo 12:12, matokeo yavita mbinguni yangekuwa nini?

Je, Tunaishi Katika “Siku za Mwisho”? 87

Hata Shetani anajua hivyo. Biblia inaki-ita kipindi hicho “siku za mwisho.”(2 Timotheo 3:1) Tunafurahi sana ku-jua kwamba karibuni Mungu ataondoamatatizo ambayo Ibilisi husababishaduniani. Hebu tuchunguze mambofulani yaliyotabiriwa katika Bibliaambayo yanatendeka leo. Mambo hayoyanaonyesha kwamba tunaishi kati-ka siku za mwisho na karibuni Ufalmewa Mungu utawaletea baraka za mile-le wale wanaompenda Yehova. Kwanza,tuchunguze mambo manne katikaishara ambayo Yesu alisema ingeonye-sha kwamba tunaishi katika siku zamwisho.

MATUKIO MAKUBWA YASIKU ZA MWISHO

6 “Taifa litasimama kupigana na ta-ifa na ufalme kupigana na ufalme.”(Mathayo 24:7) Mamilioni ya watuwameuawa vitani katika miaka 100iliyopita. Mwanahistoria mmoja Mwi-ngereza aliandika hivi: “Watu wengizaidi waliuawa katika karne ya 20 ku-liko wakati mwingine wowote. . . .Katika karne hiyo kulikuwa na mfulu-lizo wa vita, kukiwa na vipindi vifupivichache vya wakati ambapo hakuku-wa na vita mahali fulani ulimwenguni.”Ripoti ya Taasisi ya Worldwatch ili-sema hivi: “Idadi ya watu walioathiriwa

6, 7. Maneno ya Yesu kuhusu vita na upu-ngufu wa chakula yanatimizwaje leo?

88

na vita vya karne [ya 20] ilizidi maratatu ile ya watu walioathiriwa na vitavyote vilivyopiganwa tangu karne yakwanza W.K., hadi mwaka wa 1899.”Zaidi ya watu milioni 100 wameku-fa kwa sababu ya vita tangu mwakawa 1914. Hata ikiwa tunahisi maumivukwa sababu mtu mmoja tunayempendaameuawa vitani, hatuwezi kuelewa ki-kamili taabu na maumivu ya mamilioniya watu wanaofiwa.

7 “Kutakuwa na upungufu wa chaku-la.” (Mathayo 24:7) Watafiti wanasemakwamba kiasi cha chakula kimeonge-zeka sana katika miaka 30 iliyopita.Hata hivyo, bado kuna upungufu wachakula kwa sababu watu wengi hawa-na pesa za kutosha kununua chakulaau mashamba ya kukuza vyakula. Ka-tika nchi zinazoendelea, watu zaidiya bilioni moja ni maskini hohehahe.Wengi wao hawapati chakula. Shiri-ka la Afya Ulimwenguni linakadiriakwamba watoto zaidi ya milioni tanohufa kila mwaka kutokana na uta-piamlo.

8 “Kutakuwa na matetemeko maku-bwa ya nchi.” (Luka 21:11) Kulinganana Uchunguzi wa Kijiolojia wa Ma-rekani, kwa wastani, matetemeko 19makubwa ya nchi yanatazamiwa kila

8, 9. Ni nini kinachoonyesha kwamba una-bii wa Yesu kuhusu matetemeko ya nchi natauni unatimia?

89

mwaka. Matetemeko hayo yana ngu-vu za kutosha kuharibu majengo nakupasua ardhi. Na kwa wastani, kilamwaka kumekuwa na matetemekoyenye nguvu za kutosha kuharibu ma-jengo kabisa. Rekodi zinazopatikanazinaonyesha kwamba matetemeko yanchi yamesababisha vifo vya watu zai-di ya milioni mbili tangu mwaka wa1900. Shirika fulani linasema: “Mae-ndeleo ya kitekinolojia yamepunguzavifo kwa kiwango kidogo tu.”

9 “Kutakuwa na tauni.” (Luka 21:11)Lichayamaendeleoyakitiba, magonjwaya zamani na mapyayamewakumbawa-nadamu. Ripoti moja inasema kwambamagonjwa 20 yanayojulikana sana—kutia ndani kifua kikuu, malaria, nakipindupindu—yameanza tena kueneakatika miaka ya karibuni, na inazi-di kuwa vigumu kuponya aina fulaniza magonjwa hayo kwa dawa. Angalaumagonjwa 30 mapya yamezuka. Baadhiyake ni hatari na hayawezi kutibiwa kwadawa yoyote.

WATU WA SIKU ZA MWISHO10 Biblia haielezi tu mambo ambayo

yangetukia ulimwenguni bali pia ili-tabiri kwamba jamii ya wanadamuingebadilika katika siku za mwisho.Mtume Paulo alieleza jinsi hali ya watu

10. Ni mambo gani yaliyotabiriwa katika2 Timotheo 3:1-5 unayoona watu wakifanyaleo?

90

kwa ujumla ingekuwa. Tunasoma hivikatika 2 Timotheo 3:1-5: “Katika sikuza mwisho kutakuwa na nyakati za ha-tari zilizo ngumu kushughulika nazo.”Kwa sehemu, Paulo alisema kwambawatu wangekuwa

ˇ wenye kujipenda wenyeweˇ wenye kupenda pesaˇ wasiotii wazaziˇ wasio washikamanifuˇ wasio na upendo wa asiliˇ wasiojizuiaˇ wakaliˇ wanaopenda raha badala

ya kumpenda Munguˇ wenye namna ya ujitoaji-ki-

mungu lakini wakizikananguvu zake

11 Je, hivyo ndivyo watu walivyokatika eneo lenu? Bila shaka. Watuwalio na tabia hizo mbovu wako kilamahali. Hilo linaonyesha kwamba hivikaribuni Mungu atachukua hatua kwakuwa Biblia inasema: “Wakati waovuwanapochipuka kama majani na wotewanaotenda mambo yenye kuumizawanapochanuka, ni ili waowapate kua-ngamizwa milele.”—Zaburi 92:7.

11. Kulingana na Zaburi 92:7 ni nini kitaka-chowapata waovu?

91

MABADILIKO MAZURI!12 Kwa kweli siku za mwisho zimejaa ole, kama vile Biblia

ilivyotabiri. Hata hivyo, katika ulimwengu huu wenye mata-tizo mengi, kuna mabadiliko mazuri kati ya waabudu waYehova.

13 KitabuchaDanieli kilitabirihivi:“Ujuziwakweliutakuwamwingi.” Hilo lingetimia wakati gani? “Wakati wa mwisho.”(Danieli 12:4) Hasa tangu 1914, Yehova amewasaidia waleambao kwa kweli wanatamani kumtumikia wapate ujuzi zai-di wa Biblia. Wamepata kuelewa zaidi kweli kuhusu jina laMungu na kusudi lake, dhabihu ya fidiaya Yesu Kristo, hali yawafu, na ufufuo. Isitoshe, waabudu wa Yehova wamejifunzakuwa na maisha yanayowafaidi na kumletea Mungu sifa. Pia,wameelewa vizuri zaidi jukumu la Ufalme wa Mungu na jinsiutakavyorekebisha hali duniani. Wanautumiaje ujuzi huo?Swali hilo linatukumbusha unabii mwingine ambao unatimi-zwa katika siku hizi za mwisho.

14 Kuhusu “umalizio wa mfumo wa mambo,” Yesu Kristoalitabiri hivi: “Habari njema ya ufalme itahubiriwa katika du-nia yote inayokaliwa.” (Mathayo 24:3, 14) Habari njema yaUfalme inahubiriwa duniani pote katika nchi zaidi ya 230, nakwa zaidi ya lugha 400. Habari hizo zinatia ndani: Ufalmeni nini, utafanya nini, na jinsi tunavyoweza kupata barakazake. Mamilioni ya Mashahidi wa Yehova huhubiri kwa bidiihabari njema ya Ufalme. Wanatoka katika “mataifa yote namakabila navikundi vyawatu na lugha.” (Ufunuo 7:9) Mami-lioniyawatu wanaotakakujuayale ambayoBiblia hufundishahasa, hujifunza Biblia pamoja na Mashahidi bila malipo. Kwakweli, huo ni utimizo wenye kuvutia wa unabii hasa kwakuwa Yesu alitabiri kwamba Wakristo wa kweli ‘wangechuki-wa na watu wote’!—Luka 21:17.

12, 13. “Ujuzi wa kweli” umekuwaje mwingi katika hizi “siku zamwisho”?14. Habari njema ya Ufalme imehubiriwa kwa kiwango gani leo, nani nani wanaoihubiri?

92 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

“Habari njema ya ufalmeitahubiriwa katika duniayote inayokaliwa.”—Mathayo 24:14

UTAFANYA NINI?15 Kwa kuwa mambo mengi yaliyotabiriwa katika Biblia

yanatimia leo, je hukubali kwamba tunaishi katika siku zamwisho? Baada ya Yehova kuridhika na kuhubiriwa kwa ha-bari njema, hapana shaka kwamba “mwisho” utakuja.(Mathayo 24:14) “Mwisho” ni wakati ambapo Mungu ata-ondoa uovu duniani. Yehova atamtumia Yesu na malaikawenye nguvu kuwaharibu wote wanaompinga kimakusudi.(2 Wathesalonike 1:6-9) Shetani na roho wake waovu hawata-yapotosha mataifa tena. Kisha Ufalme wa Mungu utawaleteabaraka nyingi wote wanaojitiisha kwa utawala wake mwadili-fu.—Ufunuo 20:1-3; 21:3-5.

16 Kwa kuwa mwisho wa mfumo wa Shetani u karibu,tunahitaji kujiuliza, ‘Ninapaswa kuwa nikifanya nini?’ Una-paswa kuendelea kujifunza mengi kumhusu Yehova namambo anayotaka tufanye. (Yohana 17:3) Jifunze Biblia kwabidii. Uwe na mazoea ya kushirikiana kwa ukawaida pamojana wale wanaojitahidi kufanya mapenzi ya Yehova. (Wae-brania 10:24, 25) Pata ujuzi mwingi ambao Yehova Munguamewaandalia watu ulimwenguni pote, na ufanye mareke-bisho yanayohitajiwa maishani mwako ili upate kibali chaMungu.—Yakobo 4:8.

17 Yesu alitabiri kwamba watu wengi wangepuuza uthi-bitisho kwamba tunaishi katika siku za mwisho. Waovuwataharibiwa ghafula na bila kutarajia. Siku hiyo itaku-ja kama mwizi wakati wa usiku na kuwashtua watu wengi.(1 Wathesalonike 5:2) Yesu alionya hivi: “Kama vile sikuza Noa zilivyokuwa, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa bina-damu kutakavyokuwa. Kwa maana kama vile walivyokuwakatika siku hizo kabla ya gharika, wakila na kunywa, wana-

15. (a) Je, unaamini kwamba tunaishi katika siku za mwisho, kwanini? (b) “Mwisho” utamaanisha nini kwa wale wanaompinga Yeho-va na kwa wale wanaojitiisha kwa Ufalme wa Mungu?16. Unapaswa kufanya nini?17. Kwa nini kuharibiwa kwa waovu kutawashtua watu wengi?

94 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

ume wakioa na wanawake wakiolewa, mpaka siku ambayoNoa aliingia ndani ya safina; nao hawakujali mpaka gharikaikaja na kuwafagilia mbali wote, ndivyo kuwapo kwa Mwanawa binadamu kutakavyokuwa.”—Mathayo 24:37-39.

18 Kwa hiyo, Yesu aliwaambia hivi watu waliokuwa waki-msikiliza: “Jiangalieni ninyi wenyewe kwamba mioyo yenuisilemewe kamwe na kula kupita kiasi na kunywa sana namahangaiko ya maisha, na kwa ghafula siku hiyo iwe juuyenu mara moja kama mtego. Kwa maana itakuja juu yawale wote wanaokaa juu ya uso wa dunia yote. Basi, endelee-ni kukesha wakati wote mkiomba dua ili mpate kufanikiwakuponyoka mambo yote hayo yaliyokusudiwa kutukia, nakusimama [kupata kibali] mbele ya Mwana wa binadamu.”(Luka 21:34-36) Tunapaswa kuyachukua maneno ya Yesukwa uzito. Kwa nini? Kwa sababu wale walio na kibali cha Ye-hova Mungu na cha “Mwana wa binadamu,” Yesu Kristo,wana tumaini la kuokoka mwisho wa mfumo wa mambo waShetani na kuishi milele katika ulimwengu mpya ulio karibusana!—Yohana 3:16; 2 Petro 3:13.

18. Ni onyo gani la Yesu tunalopaswa kuchukua kwa uzito?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Vita, upungufu wa chakula, matetemeko yanchi, na tauni ni mambo yanayoonyeshakwamba tunaishi katika siku za mwisho.—Mathayo 24:7; Luka 21:11.

ˇ Katika siku hizi za mwisho, watu wengiwanajipenda wenyewe, wanapenda pesa naraha badala ya kumpenda Mungu.—2 Timo-theo 3:1-5.

ˇ Katika siku hizi za mwisho, habari njemaya Ufalme inahubiriwa ulimwenguni pote.—Mathayo 24:14.

Je, Tunaishi Katika “Siku za Mwisho”? 95

KWA kawaida kumjua mtu kunatia ndani kuijua familia yakepia. Vivyo hivyo, kumjua Yehova Mungu hutia ndani kuwa-jua vizuri zaidi malaika ambao ni sehemu ya familia yake.Biblia huwaita malaika hao ‘wana wa Mungu.’ (Ayubu 38:7)Kwa hiyo, wana jukumu gani katika kusudi la Mungu? Je,wametimiza lolote katika historia ya wanadamu? Je, malaikawanahusika maishani mwako? Ikiwa ndivyo, jinsi gani?

2 Malaika hutajwa katika Biblia mara nyingi sana. Hebu tu-chunguze baadhi ya maandiko hayo ili tujifunze mengi zaidikuwahusu. Malaika walitoka wapi? Andiko la Wakolosai 1:16linasema hivi: “Kwa njia yake [Yesu Kristo] vitu vingine vyoteviliumbwambinguni na duniani.” Kwa hiyo, viumbewotewaroho wanaoitwa malaika waliumbwa moja kwa moja na Ye-hova Mungu kupitia Mwana wake mzaliwa wa kwanza. Kunamalaika wangapi? Biblia inaonyesha kwamba mamia ya ma-milioni ya malaika waliumbwa, na wote wana nguvu nyingi.—Zaburi 103:20.�

� Andiko la Ufunuo 5:11 linasema hivi kuhusu malaika waadilifu: “He-sabu yao ilikuwa makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu.” Kwa hiyo,Biblia inaonyesha kwamba mamia ya mamilioni ya malaika waliumbwa.

1. Kuna faida gani kujifunza kuhusu malaika?2. Malaika walitoka wapi, na ni wangapi?

SURA YA KUMI

Jinsi Viumbe wa RohoWanavyohusika Maishani Mwetu

Je, malaika huwasaidia watu?

Roho waovu wamekuwa na uvutanogani kwa wanadamu?

Je, tuna sababu ya kuwaogopa roho waovu?

3 Neno la Mungu, Biblia, linatuambia kwamba msingi wadunia ulipowekwa, ‘wana wote wa Mungu walianza kupaa-za sauti kwa kushangilia.’ (Ayubu 38:4-7) Kwa hiyo malaikawalikuwako muda mrefu kabla ya wanadamu kuumbwa,hata kabla ya kuumbwa kwa dunia. Andiko hilo la Biblialinaonyesha pia kwamba malaika wana hisia kwa sababu li-nasema “walipiga vigelegele pamoja kwa shangwe.” Onakwamba “wana wote wa Mungu” walishangilia pamoja. Wa-kati huo, malaika wote walikuwa sehemu ya familia yenyeumoja iliyokuwa ikimtumikia Yehova Mungu.

UTEGEMEZO NA ULINZI WA MALAIKA4 Tangu waliposhuhudia kuumbwa kwa wanadamu wa

kwanza, viumbe wa roho walio waaminifu wamependezwasana na familia ya wanadamu inayoongezeka na wamepe-ndezwa pia na kutimizwa kwa kusudi la Mungu. (Methali 8:30, 31; 1 Petro 1:11, 12) Hata hivyo, kadiri wakati ulivyopita,malaika waliona kwamba wanadamu wengi walikuwa wakia-cha kumtumikia Muumba wao mwenye upendo. Bila shakajambo hilo liliwahuzunisha malaika waliokuwa waaminifu.Kwa upande mwingine, hata mwanadamu mmoja tu anapo-mrudia Yehova, “shangwe hutokea kati ya malaika.” (Luka15:10) Kwa kuwa malaika hupendezwa sana na hali nzuri yawale wanaomtumikia Mungu, haishangazi kwamba Yehovaamekuwa akiwatumia malaika kuwaimarisha na kuwali-nda watumishi wake waaminifu walio duniani. (Waebrania1:7, 14) Fikiria mifano kadhaa.

5 Malaika wawili walimsaidia yule mwanamume mwadili-fu Loti pamoja na binti zake waokoke kuharibiwa kwa majijiyaliyojaa uovu ya Sodoma na Gomora, kwa kuwaongoza

3. Andiko la Ayubu 38:4-7 linatuambia nini kuhusu malaika?4. Biblia inaonyeshaje kwamba malaika waaminifu wanapendezwana utendaji wa wanadamu?5. Biblia inataja mifano gani ambayo inaonyesha jinsi malaika wa-navyowategemeza watumishi wa Mungu?

Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu 97

kutoka katika eneo hilo. (Mwanzo 19:15,16) Karne nyingi baa-daye, nabii Danieli alitupwa katika shimo la simba, hata hivyohakupatwa na madharayoyote naye alisema hivi: “Mungu wa-ngu mwenyewe alimtuma malaika wake na kufunga vinywavyasimba.” (Danieli 6:22) Katikakarne yakwanzaW.K., malai-kaalimweka huru mtume Petrokutoka gerezani. (Matendo 12:6-11) Isitoshe, malaika walimtia nguvu Yesu mwanzoni mwahuduma yake hapa duniani. (Marko 1:13) Pia, muda mfupikabla ya kifo cha Yesu, malaika alimtokea, “akamtia nguvu.”(Luka 22:43) Lazima hilo lilimfariji Yesu kama nini katika nya-kati hizo muhimu sana maishani mwake!

6 Leo, malaika hawawatokei kihalisi watumishi wa Mu-ngu walio duniani. Ingawa hawaonekani, malaikawa Munguwenye nguvu bado huwalinda watumishi wake, hasa dhidiya madhara yoyote ya kiroho. Biblia inasema hivi: “Malaikawa Yehova anapiga kambi pande zote kuwazunguka wa-naomwogopa, na yeye huwaokoa.” (Zaburi 34:7) Kwa ninimaneno hayo yanapaswa kutufariji sana? Kwa sababu kunaroho waovu hatari, wanaotaka kutuangamiza! Ni nani hao?Wanatoka wapi? Wanajaribu kutuumiza jinsi gani? Ili kupa-ta majibu, na tuchunguze kifupi jambo lililotokea mwanzonimwa historia ya wanadamu.

VIUMBE WA ROHO AMBAO NI ADUI ZETU7 Kama tulivyojifunza katika Sura ya 3 ya kitabu hiki, mmo-

ja wa malaika alikuza tamaa ya kuwatawala wengine na hivyoakamwasi Mungu. Baadaye, malaika huyo akaja kuitwa Sheta-ni Ibilisi. (Ufunuo 12:9) Kwa karne 16 tangu alipomdanganyaHawa, Shetani alifanikiwa kuwageuza karibu watu wote wa-ache kumtumikia Mungu isipokuwa waaminifu wachache,kama vile Abeli, Enoko, na Noa.—Waebrania 11:4, 5, 7.

6. (a) Malaika huwalindaje watumishi wa Mungu leo? (b) Tutachu-nguza maswali gani sasa?7. Shetani alifanikiwa kadiri gani kuwageuza watu waache kumtumi-kia Mungu?

98 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

8 Katika siku za Noa, malaika wengine walimwasi Yehova.Waliacha mahali pao katika familia ya Mungu ya kimbingu,wakaja duniani, na kujivika miili yenye nyama. Kwa nini? Tu-nasoma hivi katika Mwanzo 6:2: “Wana wa Mungu wa kweliwakaanza kuwaona mabinti wa wanadamu, kwamba ni we-nye sura ya kupendeza; nao wakajichukulia wake, yaani,wote waliowachagua.” Hata hivyo, Yehova Mungu hakuachi-lia matendo ya malaika hao na ufisadi wao uendelee katiya wanadamu. Alileta mafuriko duniani, akawafagilia mba-li wanadamu wote waovu na kuwahifadhi watumishi wake

8. (a) Malaika fulani walikujaje kuwa roho waovu? (b) Roho waovuwalilazimika kufanya nini ili kuokoka Mafuriko ya siku za Noa?

“Mungu wangu mwenyewe alimtuma malaikawake na kufunga vinywa vya simba.”

—Danieli 6:22

Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu 99

waaminifu. (Mwanzo 7:17, 23) Hivyo, malaika hao waasi,au roho waovu, walilazimika kuiacha miili yao yenye nya-ma na kurudi mbinguni wakiwa viumbe wa roho. Walikuwawamejiunga na Ibilisi, aliyekuwa “mtawala wa roho waovu.”—Mathayo 9:34.

9 Waliporudi mbinguni, malaika hao waasi walitengwa nafamiliaya Mungu, kama alivyotengwa Shetani, mtawalawao.(2 Petro 2:4) Ingawa kwa sasa hawawezi kujivika miili ya kibi-nadamu, bado wana uvutano mbaya sana kwa wanadamu.Shetani, akisaidiwa na roho hao waovu, ‘anaipotosha dunianzima inayokaliwa.’ (Ufunuo 12:9; 1 Yohana 5:19) Jinsi gani?Malaika hao hutumia hasa njia ambazo zinakusudiwa kuwa-potosha wanadamu. (2 Wakorintho 2:11) Hebu tuchunguzebaadhi ya njia hizo.

JINSI ROHO WAOVU WANAVYOPOTOSHA10 Roho waovu hutumia mazoea ya kuwasiliana na pepo

ili kuwapotosha watu. Mazoea hayo huhusisha roho waovu,kwa njia ya moja kwa moja au kupitia mwanadamu mwingi-ne. Biblia hushutumu mazoea ya kuwasiliana na pepo nayohutuonya tujiepushe na kila kitu kinachohusiana na mazoeahayo. (Wagalatia 5:19-21) Roho waovu hutumia mazoea yakuwasiliana na pepo kama vile mvuvi anavyotumia chambokwenye ndoana. Mvuvi hutumia vyambo vya aina mbali-mbali ili kunasa samaki wa namna mbalimbali. Vivyo hivyo,rohowaovu hutumianjia mbalimbali za kuwasilianana pepoili kuwanasa watu wa namna zote.

11 Chambo kimoja kinachotumiwa na roho waovu ni ua-guzi. Uaguzi ni nini? Ni kujaribu kujua habari za wakati ujaoau jambo lisilojulikana. Uaguzi unatia ndani kuangalia nyo-ta, kusoma kadi za karata, kutazama mpira wa kioo, kusoma

9. (a) Ni nini kilichowapata roho waovu waliporudi mbinguni?(b) Tutachunguza nini kuhusiana na roho waovu?10. Kuwasiliana na pepo huhusisha nini?11. Uaguzi ni nini, na kwa nini tunapaswa kuuepuka?

100 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

viganjavya mkono, kutafuta ndege au ishara mbaya, na kufa-siri ndoto. Ingawawatu wengi hufikiri kwamba uaguzi haunamadhara yoyote, Biblia huonyesha kwamba wabashiri hushi-rikiana na roho waovu. Kwa mfano, andiko la Matendo 16:16-18 linamtaja “roho mwovu wa uaguzi” ambaye alimwe-zesha kijakazi kufanya “ufundi wa kubashiri.” Lakini, rohohuyo mwovu alipomtoka, alipoteza uwezo wa kubashiri.

12 Njia nyingine ambayo roho waovu hutumia kuwapo-tosha watu ni kuwachochea watafute habari za wafu. Maranyingi, watu wanaoomboleza kifo cha mpendwa wao hua-mini mambo ya uwongo kuhusu waliokufa. Mtu mwenyeuwezowa kuwasiliana na pepo anaweza kutoa ujumbewa pe-kee au anaweza kuongea kwa sauti kama ya mtu aliyekufa.Ndiyo sababu watu wengi husadiki kwamba wafu wako haina kwamba kuwasiliana nao kutawasaidia walio hai kuvumi-lia huzuni yao. Lakini “faraja” ya aina hiyo ni ya uwongo nani hatari. Kwa nini? Kwa sababu roho waovu wanaweza kuigasauti ya mtu aliyekufana kumpa mtu anayewasiliana na pepo

12. Kwa nini ni hatari kujaribu kuwasiliana na wafu?

Roho waovu hutumia njia mbalimbali kuwadanganya watu

JINSI YAKUWAPINGA

ROHO WAOVU

ˇ Haribu vitu vyakuwasiliana na pepo

ˇ Jifunze Biblia

ˇ Sali kwa Mungu

habari kumhusu mfu huyo. (1 Samweli 28:3-19) Isitoshe,kama tulivyojifunza katika Sura ya 6, wafu hawaendelei ku-ishi. (Zaburi 115:17) Kwa hiyo, “yeyote anayeuliza habarikutoka kwa wafu” amepotoshwa na roho waovu na anatendakinyume cha mapenzi ya Mungu. (Kumbukumbu la Torati18:10,11; Isaya 8:19) Basi, uwe mwangalifu usije ukanaswa nachambo hicho hatari kinachotumiwa na roho waovu.

13 Mbali na kuwapotoshawatu, roho waovu huwatisha pia.Leo, Shetani na roho wake waovu wanajua kwamba wana“kipindi kifupi cha wakati” kabla hawajakomeshwa, na sasani wakatili kuliko wakati mwingine wowote. (Ufunuo 12:12,17) Hata hivyo, maelfu ya watu ambao hapo zamani wali-kuwa wakiwaogopa roho waovu, sasa hawawaogopi kamwe.Ni nini kimewasaidia? Mtu anaweza kufanya nini hata ikiwaanashiriki katika mazoea ya kuwasiliana na pepo?

JINSI YA KUWAPINGA ROHO WAOVU14 Biblia inatueleza jinsi ya kuwapinga roho waovu na ji-

nsi ya kuvunja uhusiano nao. Fikiria mfano wa Wakristo wakarne ya kwanza katika jiji la Efeso. Baadhi yao walikuwana mazoea ya kuwasiliana na pepo kabla ya kuwa Wakri-sto. Walipoamua kuacha mazoea hayo, walifanya nini? Bibliainasema: “Hesabu kubwa ya wale waliozoea kufanya ufu-ndi wa uchawi wakaleta pamoja vitabu vyao wakaviteketezambele ya kila mtu.” (Matendo 19:19) Kwa kuharibu vitabuvyao vya uchawi, Wakristo hao wapya waliwawekea mfanowale wanaotaka kuwapinga roho waovu leo. Watu wanao-taka kumtumikia Yehova wanapaswa kuharibu kila kitukinachohusiana na mazoea ya kuwasiliana na pepo. Vitu hi-vyo vinatia ndani vitabu, magazeti, sinema, vibandiko, namiziki inayowachochea watu kuwasiliana na pepo na kuona

13. Watu wengi ambao zamani waliwaogopa roho waovu wamefau-lu kufanya nini?14. Tunawezaje kuacha kuwasiliana na roho waovu kama walivyofa-nya Wakristo wa Efeso katika karne ya kwanza?

Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu 103

mazoea hayo kuwa yenye kuvutia na kusisimua. Vitu vingi-ne ambavyo pia vinapaswa kuharibiwa ni hirizi au chochotekinachovaliwa ili kumlinda mtu asipatwe na mabaya.—1 Wa-korintho 10:21.

15 Miaka kadhaa baada ya Wakristo wa Efeso kuharibu vita-bu vyao vya uchawi, mtume Paulo aliwaandikia hivi: “Tunakushindana mweleka . . . juu ya majeshi ya roho waovu.”(Waefeso 6:12) Roho waovu hawakuwa wamekata tamaa.Badowalikuwawakijaribu kuwanasa. Kwahiyo, Wakristo haowalihitaji kufanya nini? Paulo alisema, “Zaidi ya mamboyote, ichukueni ngao kubwa ya imani, ambayo kwa kuitumiamtawezakuizimamishaleyote inayowakamotoyayule mwo-vu [Shetani].” (Waefeso 6:16) Kadiri ngao yetu ya imani ilivyona nguvu, ndivyotutakavyowapinga rohowaovu kwa nguvu.—Mathayo 17:20.

16 Basi, tunawezaje kuimarisha imani yetu? Kwa kujifunzaBiblia. Ili ukuta uwe imara, ni lazima msingi wake uwe nanguvu. Vivyo hivyo, ili imani yetu iwe na nguvu ni lazi-ma tuwe na msingi imara, ambao ni ujuzi sahihi wa Neno laMungu, Biblia. Tukisoma na kujifunza Biblia kila siku, imaniyetu itakuwa na nguvu. Sawa na ukuta imara, imani hiyo ita-tukinga dhidi ya uvutano wa roho waovu.—1 Yohana 5:5.

17 Wakristo wa Efeso walihitaji kuchukua hatua gani nyi-ngine? Walihitaji ulinzi zaidi kwa sababu walikuwa wakiishikatika jiji lililojaa mazoea ya roho waovu. Kwa hiyo Pauloaliwaambia hivi: ‘Kwa kila namna ya sala na dua, endeleze-ni sala kila wakati katika roho.’ (Waefeso 6:18) Kwa kuwa sisipia tunaishi katika ulimwengu uliojaa mazoea ya roho wao-vu, tunahitaji kumwomba Yehova kwa bidii ili atulinde dhidiya roho hao waovu. Bila shaka, tunahitaji kulitumia jina laYehova katika sala zetu. (Methali 18:10) Kwa hiyo, tunapa-

15. Tunahitaji kufanya nini ili kuwapinga roho waovu?16. Tunawezaje kuwa na imani yenye nguvu?17. Ni hatua gani nyingine tunayohitaji kuchukua ili kuwapingaroho waovu?

104 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

swa kuendelea kumwomba Mungu ‘atukomboe kutokana nayule mwovu,’ Shetani Ibilisi. (Mathayo 6:13) Yehova atajibusala hizo tunazotoa kwa bidii.—Zaburi 145:19.

18 Roho waovu ni hatari, hata hivyo, ikiwa tunampingaIbilisi na kumkaribia Mungu kwa kufanya mapenzi Yake, ha-tutaishi kwa woga. (Yakobo 4:7, 8) Nguvu za roho waovuzina mipaka. Waliadhibiwa katika siku za Noa, nao watapa-ta hukumu yao ya mwisho. (Yuda 6) Pia, kumbuka kwambamalaika wenye nguvu wa Yehova hutulinda. (2 Wafalme 6:15-17) Malaika hao wangependa sana kuona tukifaulu kuwa-shinda roho waovu. Malaika hao waadilifu wanatushangilia.Basi, na tukae karibu na Yehova na familia yake ya viu-mbe waaminifu wa roho. Na tuepuke pia kila namna yakuwasiliana na pepo na sikuzote tutumie shauri la Neno laMungu maishani mwetu. (1 Petro 5:6, 7; 2 Petro 2:9) Tukifa-nya hivyo, tutashinda vita tunavyopigana na viumbe waovuwa roho.

19 Lakini kwa nini Mungu ameachilia roho waovu na uovuambao umefanya watu wateseke sana? Swali hilo litajibiwakatika sura inayofuata.

18, 19. (a) Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba tutashindavita dhidi ya viumbe waovu wa roho? (b) Sura inayofuata itajibuswali gani?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Malaika waaminifu huwasaidia wale wanao-mtumikia Yehova.—Waebrania 1:7, 14.

ˇ Shetani na roho wake waovu wanawapoto-sha watu na kuwafanya wamwache Mungu.—Ufunuo 12:9.

ˇ Ukifanya mapenzi ya Mungu na kumpingaIbilisi, Shetani atakukimbia.—Yakobo 4:7, 8.

Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu 105

BAADA ya vita vya kikatili katika nchi moja, maelfu ya wa-nawake na watoto waliouawa walizikwa kwenye kaburi laujumla lililozingirwa na misalaba. Kila msalaba ulikuwa naswali hili: “Kwa nini?” Nyakati nyingine swali hilo huumi-za sana. Watu huuliza swali hilo lenye kuhuzunisha wakativita, msiba, ugonjwa, au uhalifu unaposababisha vifo vya wa-pendwa wao wasio na hatia, nyumba zao zinapoharibiwa auwanapoteseka sana katika njia nyingine kwa sababu ya vita.Wanataka kujua kwa nini wanapatwa na misiba hiyo.

2 Kwa nini Mungu anawaacha watu wateseke? Ikiwa Yeho-va Mungu ana nguvu zote, ana upendo, hekima, na haki, kwanini ulimwengu umejaa chuki na ukosefu wa haki? Je, ume-wahi kujiuliza maswali hayo?

3 Je, ni vibaya kuuliza kwa nini Mungu anawaacha wana-damu wateseke? Watu fulani huogopa kwamba kuuliza swalikama hilo kutaonyesha kwamba hawana imani au hawa-mheshimu Mungu. Hata hivyo, unaposoma Biblia utaona

1, 2. Watu wanateseka jinsi gani leo, na hilo huwafanya waulize ma-swali gani?3, 4. (a) Sababu gani si vibaya kuuliza kwa nini Mungu anawaachawanadamu wateseke? (b) Yehova anahisije kuhusu uovu na kuteseka?

SURA YA KUMI NA MOJA

Kwa Nini Mungu AnawaachaWatu Wateseke?

Je, Mungu ndiye anayesababishakuteseka ulimwenguni?

Ni masuala gani yaliyozushwa katikabustani ya Edeni?

Mungu atakomeshaje kuteseka kwa wanadamu?

kwamba watumishi waaminifu wa Mungu waliuliza maswalikama hayo. Kwa mfano, nabii Habakuki alimuuliza Yehovahivi: “Kwa nini unanionyesha jambo lenye kudhuru, naweunaendelea kutazama taabu tupu? Na kwa nini kuna upora-ji na jeuri mbele yangu, kwa nini kugombana hutokea, kwanini mzozo huendelezwa?”—Habakuki 1:3.

4 Je, Yehova alimkemea nabii mwaminifu Habakuki kwakuuliza maswali hayo? Hapana. Badala yake Mungu aliyatiamaneno manyoofu ya Habakuki katika Biblia iliyoandi-kwa kwa mwongozo wa roho. Pia, Mungu alimsaidia kuelewamambo zaidi na kuwa na imani zaidi. Yehova anataka ku-kusaidia vivyo hivyo. Kumbuka, Biblia inafundisha kwamba‘anakujali.’ (1 Petro 5:7) Hakuna mwanadamu anayechukiauovu na kuteseka kwa wanadamu kama Mungu anavyoya-chukia mambo hayo. (Isaya 55:8, 9) Kwa nini basi watuwanateseka sana ulimwenguni?

KWA NINI WATU WANATESEKA SANA?5 Watu wa dini mbalimbali wamewauliza viongozi na wa-

limu wao wa dini kuhusu kinachosababisha watu

5. Watu fulani husema ni kwa nini watu wanateseka, lakini Bibliainafundisha nini?

Yehova atakomesha kabisa kuteseka

107

wateseke sana. Mara nyingi, wanaambiwa kwamba ni mape-nzi ya Mungu na kwamba ndiye aliyepanga zamani mamboyatakayowapata wanadamu kutia ndani misiba yenye kuhu-zunisha. Wengi huambiwa kwamba njia za Mungu haziwezikueleweka au Mungu husababisha vifo vya watu, hata wato-to, ili wakae pamoja naye huko mbinguni. Hata hivyo,kama ulivyojifunza, Yehova Mungu hasababishi mabaya. Bib-lia inasema: “Hasha, Mungu wa kweli asitende kwa uovu, naMweza-Yote kutenda isivyo haki!”—Ayubu 34:10.

6 Je, unajua ni kwa nini watu humlaumu Mungu isivyo-faa kwa sababu ya mambo yote yanayosababisha kutesekaulimwenguni? Mara nyingi, wao humlaumu Mungu Mweza-Yote kwa sababu wanafikiri kwambayeye ndiye anayeutawalaulimwengu huu. Hawajui kweli ya msingi ambayo Biblia hu-fundisha. Ulijifunza kweli hiyo katika Suraya 3 ya kitabu hiki.Shetani Ibilisi ndiye anayeutawala ulimwengu huu.

7 Biblia hueleza hivi waziwazi: “Ulimwengu mzima unakaakatika nguvu za yule mwovu.” (1 Yohana 5:19) Unapofikiriahilo, je, huoni ni kwa nini ulimwengu uko jinsi ulivyo leo?Ulimwenguunaonyeshautuwa kiumbehuyowaroho asiyeo-nekana, “anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa.” (Ufunuo12:9) Shetani ana chuki, ni mwongo, na mkatili. Kwa hiyo,ulimwengu ulio chini yake umejaa chuki, uwongo, na uka-tili. Hiyo ni sababu moja inayowafanya wanadamu watesekesana leo.

8 Kama ilivyozungumziwa katika Sura ya 3, sababu ya pilini kwamba wanadamu si wakamilifu nao wamekuwa wate-nda-dhambi tangu uasi ulipoanza katika bustani ya Edeni.Wanadamu wenye dhambi hung’ang’ania utawala, na hilohutokeza vita, ukandamizaji, na kuteseka. (Mhubiri 4:1; 8:9)

6. Kwa nini watu wengi humlaumu Mungu isivyofaa kwa sababu yamambo yanayosababisha kuteseka ulimwenguni?7, 8. (a) Ulimwengu unaonyeshaje utu wa mtawala wake? (b) “Wa-kati na tukio lisilotazamiwa” pamoja na kutokamilika kwawanadamu kumesababishaje kuteseka?

108 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Sababu ya tatu ni “wakati na tukio lisilotazamiwa.” (Mhubiri9:11) Katika ulimwengu usiotawaliwa na Yehova, watu wana-weza kuteseka kwa sababu ya kuwa mahali pasipofaa wakatiusiofaa.

9 Inatia moyo kujua kwamba Mungu hasababishi kutese-ka. Hasababishi vita, uhalifu, ukandamizaji, au hata misibaya kiasili inayowafanya watu wateseke. Hata hivyo, tunahita-ji kujua, Kwa nini Yehova anawaacha wanadamu waendeleekuteseka? Ikiwa yeye ndiye Mweza-Yote, ana nguvu za kuko-mesha kuteseka. Lakini, kwa nini hachukui hatua? LazimaMungu mwenye upendo ambaye tumejifunza juu yake awena sababu nzuri.—1 Yohana 4:8.

SUALA MUHIMU LAZUKA10 Ili kufahamu ni kwa nini Mungu amewaachawanadamu

waendelee kuteseka, tunahitaji kujikumbusha jinsi kute-seka kulivyoanza. Shetani alipowachochea Adamu na Hawawamwasi Yehova, suala muhimu lilizuka. Shetani haku-pinga nguvu za Yehova. Hata Shetani mwenyewe anajuakwamba nguvu za Yehova hazina kifani. Badala yake, Sheta-ni alipinga haki ya Yehova ya kutawala. Kwa kudai kwambaMungu ni mwongo anayewanyima raia zake mambo mazuri,Shetani alikuwa akidai kwamba Yehova ni mtawala mbaya.(Mwanzo3:2-5) Shetanialidokezakwambahali yawanadamuingekuwa bora pasipo utawala wa Mungu. Alishambulia enzikuu ya Yehova, haki yake ya kutawala.

11 Adamu na Hawa walimwasi Yehova. Ni kana kwambawalisema: “Hatuhitaji kutawaliwa na Yehova. Tunaweza ku-jiamulia mema na mabaya.” Yehova angetatuaje suala hilo?Angewafundishaje viumbe wake wote wenye akili kwambawaasi hao walikosea na kwamba kwa kweli njia yake ndiyo

9. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova ana sababunzuri ya kuwaacha wanadamu waendelee kuteseka?10. Shetani alipinga nini, na jinsi gani?11. Kwa nini Yehova hakuwaangamiza waasi hao katika Edeni?

Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke? 109

bora? Huenda mtu akasema kwamba afadhali Mungu ange-waangamiza mara moja waasi hao na kuanza upya. LakiniYehova alikuwa ametaja kusudi lake kwamba uzao wa Ada-mu na Hawa ujaze dunia, naye alitaka waishi katika paradisoduniani. (Mwanzo 1:28) Yehova hutimiza makusudi yake si-kuzote. (Isaya 55:10, 11) Isitoshe, kuwaangamiza waasi haokatika Edeni hakungejibu suala lililokuwa limezuka kuhusuhaki ya Yehova ya kutawala.

12 Hebu tufikirie mfano mmoja. Wazia kwamba mwali-mu anawafundisha wanafunzi wake jinsi ya kufanya hesabufulani ngumu. Mwanafunzi mmoja mwerevu lakini mwasianadai kwamba mwalimu amekosea. Anadai kwamba mwa-limu ameshindwa, na mwasi huyo anasisitiza kwambaanajua njia bora zaidi ya kufanya hesabu hiyo. Wanafunzifulani wanafikiri kwamba anasema kweli, nao pia wanaa-si. Mwalimu afanye nini? Akiwafukuza waasi hao kutokadarasani, wanafunzi wengine wataonaje? Je, hawataaminikwamba mwanafunzi mwenzao na wale waliojiunga naye

12, 13. Toa mfano unaoonyesha ni kwa nini Yehova amemruhusuShetani autawale ulimwengu huu na kwa nini Mungu amewaruhu-su wanadamu wajitawale.

Je, mwanafunzi ana ujuzi kuliko mwalimu?

wanasema kweli? Huenda wale wanafunzi wengine waliodarasani wakaacha kumwamini mwalimu wao wakifikirikwamba anaogopa kuonyeshwa makosa yake. Basi mwali-mu angemruhusu mwasi huyo awaonyeshe wanafunziwenzake jinsi yeye mwenyewe anavyoweza kufanya hesabuhiyo.

13 Yehova amefanya kama mwalimu huyo anavyofanya.Kumbuka kwamba kuna wengi waliohusika mbali na waa-si hao katika Edeni. Mamilioni ya malaika walikuwawakitazama. (Ayubu38:7; Danieli 7:10) Njiaya Yehovaya ku-shughulikia uasi huo ingekuwa na matokeo makubwa sanakwa malaika wote na hatimaye viumbe wote wenye akili.Kwa hiyo, Yehova amefanya nini? Amemruhusu Shetaniaonyeshe jinsi anavyoweza kuwatawala wanadamu. Munguamewaruhusu pia wanadamu wajitawale wenyewe wakiwachini ya uongozi wa Shetani.

14 Katika mfano uliotolewa, mwalimu anajua kwambayule mwanafunzi mwasi na wale wanaomuunga mkonowamekosea. Lakini pia anajua kwamba kuwapa nafasi ya ku-jaribu kuthibitisha madai yao kutawafaidi wanafunzi wotedarasani. Waasi hao wakishindwa, wale wanafunzi wengi-ne wote wataona kwamba ni mwalimu wao tu anayestahilikulifundisha darasa. Baadaye, mwalimu akiwafukuza waasikutoka darasani, wanafunzi wataelewa sababu iliyomfanyaawafukuze. Vivyo hivyo, Yehova anajua kwamba wanadamuna malaika wote wanyoofu watafaidika wakiona kwambaShetani na waasi wenzake wameshindwa na kwamba wa-nadamu hawawezi kujitawala wenyewe. Kama Yeremia wazamani, watajifunza ukweli huu muhimu: “Ninajua vema,Ee Yehova, kwamba njia ya mtu wa udongo haimo katikauwezo wake. Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa ku-ongoza hatua yake.”—Yeremia 10:23.

14. Kuna faida gani kwa Yehova kuwaruhusu wanadamu wajitawalewenyewe?

Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke? 111

KWA NINI YEHOVA AMEWAACHA WANADAMUWATESEKE KWA MUDA MREFU?

15 Hata hivyo, kwa nini Yehova amewaacha wanadamu wa-teseke kwa muda mrefu? Na kwa nini hazuii mambo mabayayasitendeke? Katika ule mfano tuliotoa, fikiria mambo mawi-li ambayo yule mwalimu hangefanya. Kwanza, hangemzuiayule mwanafunzi mwasi kutoa madai yake. Pili, mwalimuhangemsaidia mwasi huyo kuthibitisha madai yake. Vivyohivyo, kuna mambo mawili ambayo Yehova ameazimia ku-tofanya. Kwanza, hajamzuia Shetani na wale wanaomuungamkono kujaribu kuthibitisha kwamba wanasema kweli. Ndi-yo sababu ameruhusu wakati upite. Kwa maelfu ya miakakatika historia, wanadamu wamejaribu kila aina ya utawala,au serikali za wanadamu. Wanadamu wamefanya maende-leo katika sayansi na katika nyanja nyinginezo, lakini ukosefuwa haki, umaskini, uhalifu, na vita vimeongezeka sana. Sasaimeonekana wazi kwamba utawala wa wanadamu umeshi-ndwa.

16 Pili, Yehova hamsaidii Shetani kuutawala ulimwenguhuu. Kama Mungu angezuia uhalifu usitokee, je, hangekuwaanaunga mkono madai ya waasi hao? Je, watu hawangefikirikwamba labda wanadamu wanaweza kujitawala bila ma-tatizo? Kama Yehova angefanya hivyo, angekuwa anaungamkono uwongo, na “Mungu hawezi kamwe kusema uwo-ngo.”—Waebrania 6:18.

17 Lakini vipi kuhusu madhara ya uasi huo wa muda mrefukumwelekea Mungu? Tunapaswa kukumbuka kwamba Yeho-va ni Mweza-Yote. Kwa hiyo, anaweza na ataondoa mamboyanayowafanya wanadamu wateseke. Kama tulivyojifunza,badala ya dunia kuendelea kuharibiwa itageuzwa iwe Pa-radiso. Matokeo ya dhambi yataondolewa kupitia imani

15, 16. (a) Kwa nini Yehova amewaacha wanadamu wateseke kwamuda mrefu? (b) Kwa nini Yehova hazuii mambo kama vile uhalifu?17, 18. Yehova atachukua hatua gani ili kuondoa madhara ya uta-wala wa wanadamu na uvutano wa Shetani?

112 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

katika dhabihu ya fidia ya Yesu na ufufuo utatangua mato-keo ya kifo. Hivyo, Mungu atamtumia Yesu ‘kuzivunja kaziza Ibilisi.’ (1 Yohana 3:8) Yehova atatimiza yote hayo wakatiunaofaa kabisa. Tunafurahi kwamba hakuchukua hatua kab-layawakati unaofaa kwa sababu subirayake imetupatia nafasiya kujifunza kweli na kumtumikia. (2 Petro 3:9, 10) Kwa sasa,Mungu amekuwa akiwatafuta kwa bidii waabudu wanyoofuna kuwasaidiawavumilie mamboyoyote yanayowakumba nayanayowafanyawatesekekatikaulimwenguhuuwenyetaabu.—Yohana 4:23; 1 Wakorintho 10:13.

18 Huenda wengine wakauliza, Je, mateso haya yote yange-zuiwa iwapo Mungu angewaumba Adamu na Hawa kwa njiaya kwamba hawangeweza kuasi? Ili kujibu swali hilo unahita-ji kukumbuka kwamba Yehova amekupa zawadi fulani yenyethamani.

UTAITUMIAJE ZAWADI AMBAYOMUNGU AMEKUPA?

19 Kama tulivyoona katika Sura ya 5, wanadamu waliu-mbwa wakiwa na uhuru wa kuchagua. Je, unaiona zawadihiyo kuwa yenye thamani? Mungu ameumba wanyamawengi sana, nao wanaongozwa hasa na silika.(Methali 30:24) Mwanadamu ametengene-za mashine zinazoweza kufuata maagizo.Je, tungefurahi ikiwa Mungu angetuumbahivyo? Hapana, tunafurahi kwa kuwa tunauhuru wa kuamua tutakuwa watu wa ainagani, tutaishi maisha ya aina gani, tutaku-wa na marafiki wa aina gani, na kadhalika.

19. Yehova ametupa zawadigani yenye thamani, na kwanini tunapaswa kuithamini?

Mungu atakusaidiakuvumilia unapoteseka

Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke? 113

Tunapenda kuwa na uhuru, na Mungu anataka tuwe nauhuru.

20 Yehova hapendi watu wamtumikie kwa kulazimishwa.(2 Wakorintho 9:7) Kwa mfano: Ni nini kinachoweza kumfu-rahisha mzazi zaidi—mtoto anaposema “nakupenda” kwasababu ameambiwa aseme hivyo au anaposema hivyo mwe-nyewe kutoka moyoni? Kwa hiyo, ni muhimu kufikiria swalihili, Wewe utatumiaje uhuru wa kuchagua ambao Yeho-va amekupa? Shetani, Adamu, na Hawa waliutumia vibayauhuru wao wa kuchagua. Walimkataa Yehova Mungu. Weweutafanya nini?

21 Unaweza kuitumia vizuri zaidi zawadi hiyo yenye thama-ni ya uhuru wa kuchagua. Unaweza kujiunga na mamilioniya watu ambao wamechukua msimamo upande wa Yeho-va. Wanamfanya Mungu ashangilie kwa sababu wanashirikikwa bidii kumthibitisha Shetani kuwa mwongo na mtawalaasiyefaa. (Methali 27:11) Wewe pia unaweza kuchagua kuishimaisha yanayofaa. Hilo litafafanuliwa katika sura inayofuata.

20, 21. Tunawezaje kuitumia vizuri zaidi zawadi ya uhuru wa kucha-gua, na kwa nini tunapaswa kufanya hivyo?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Mungu hasababishi hali mbaya zilizo uli-mwenguni.—Ayubu 34:10.

ˇ Kwa kudai kwamba Mungu ni mwongona kusema kwamba Anawanyima raia zakemambo mazuri, Shetani alipinga haki ya Ye-hova ya kutawala.—Mwanzo 3:2-5.

ˇ Yehova atamtumia Mwana wake, akiwa Mta-wala wa Ufalme wa Kimasihi, kukomeshakuteseka kwa wanadamu pamoja na mato-keo yake.—1 Yohana 3:8.

114 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

UNGEPENDA kuwa na rafiki wa aina gani? Yaelekea unge-penda kushirikiana na mtu aliye na maoni, mapendezi, naviwango kama vyako. Nawe ungevutiwa na mtu mwenye sifanzuri, kama vile unyoofu na fadhili.

2 Katika historia yote, Mungu aliwachagua wanadamu fula-ni wawe rafiki zake wa karibu. Kwa mfano, Yehova alimwitaAbrahamu rafiki yake. (Isaya 41:8; Yakobo 2:23) Mungu ali-mtaja Daudi kuwa “mtu anayekubalika kwa moyo wangu”kwa sababu alikuwa na utuunaompendeza Yehova. (Matendo13:22) Pia, Yehova alimwona nabii Danieli kuwa “mtu mwe-nye kutamanika sana.”—Danieli 9:23.

3 Kwa nini Yehova aliwaona Abrahamu, Daudi, na Danielikuwa rafiki zake? Alimwambia Abrahamu: “Umeisikiliza sautiyangu.” (Mwanzo 22:18) Kwa hiyo Yehova huwakaribia walewanaofanya mapenzi yake kwa unyenyekevu. AliwaambiaWaisraeli: “Tiini sauti yangu, nami nitakuwa Mungu wenu,nanyi mtakuwa watu wangu.” (Yeremia 7:23) Ukimtii Yehova,wewe pia unaweza kuwa rafiki yake!

1, 2. Taja baadhi ya wanadamu ambao Yehova aliwaona kuwa rafikizake wa karibu.3. Kwa nini Yehova huwachagua wanadamu fulani wawe rafiki zake?

SURA YA KUMI NA MBILI

Kuishi MaishaYanayompendeza Mungu

Unawezaje kuwa rafiki ya Mungu?

Dai la Shetani linakuhusuje?

Ni mwenendo gani unaomchukiza Yehova?

Unawezaje kuishimaisha yanayompendeza Mungu?

YEHOVA HUWAIMARISHA RAFIKI ZAKE4 Hebu fikiria faida za kuwa rafiki ya Mungu. Biblia inasema

kwamba Yehova anatafuta nafasi ili “aonyeshe nguvu zake kwaajili yawale ambaomoyowaonimkamilifukumwelekeayeye.”(2 Mambo ya Nyakati 16:9) Yehova anawezaje kuonyesha ngu-vu zake kwa ajili yako? Njia moja inatajwa katika Zaburi 32:8,ambapo tunasoma hivi: “[Mimi Yehova] nitakufanya uwe naufahamu na kukufundisha katika njia unayopaswa kuiendea.Nitakupa shauri jicho langu likiwa linakutazama.”

5 Maneno hayo yanaonyesha kwamba Yehova anakujalisana. Atakupa mwongozo unaohitaji na kukulinda unapo-ufuata. Mungu anataka kukusaidia ushinde majaribu. (Zaburi55:22) Kwa hiyo, ikiwa unamtumikia Yehova kwa moyo kami-li, unaweza kuwa na hakika kama mtunga-zaburi aliyesema:“Nimemweka Yehova mbele yangu daima. Kwa sababu yukoupandewamkonowanguwakuume, sitatikiswa.” (Zaburi16:8;63:8) Ndiyo, Yehova anaweza kukusaidia uishi maisha yana-yompendeza. Lakini, kama unavyojua, kuna adui ya Munguambaye anataka kukuzuia usifanye hivyo.

DAI LA SHETANI6 Sura ya 11 ya kitabu hiki ilieleza jinsi Shetani Ibilisi ali-

vyopinga haki ya Mungu ya kutawala. Shetani alidai kwambaMungu ni mwongo na kudokeza kwamba Yehova alikuwaakiwakandamiza Adamu na Hawa kwa kuwanyima haki ya ku-jiamulia yaliyo mema na mabaya. Baada ya Adamu na Hawakufanya dhambi na wazao wao walipoanza kujaa duniani,Shetani alitilia shaka niayawanadamu wote. Shetani alidai kwa-mba “Watu hawamtumikii Mungu kwa sababu wanampenda.”Ni kana kwamba alisema, “Nikiruhusiwa, ninaweza kumgeu-za mtu yeyote aache kumtumikia Mungu.” Masimulizi kuhusuAyubu yanaonyesha kwamba hivyo ndivyo Shetani alivyoami-ni. Ayubu alikuwa nani, naye alihusikaje katika dai la Shetani?

4, 5. Yehova anaonyeshaje nguvu zake kwa ajili ya watu wake?6. Shetani alidai nini kuhusu wanadamu?

116 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

7 Ayubu aliishi miaka 3,600 hivi iliyopita. Alikuwa mtu mzu-ri, kwa kuwa Yehova alisema: “Hakuna yeyote aliye kama yeyeduniani, mtu asiye na lawama na mnyoofu, mwenye kumwo-gopa Mungu na kujiepusha na ubaya.” (Ayubu 1:8) Ayubualimpendeza Mungu.

8 Shetani alitilia shaka nia ya Ayubu kumtumikia Mu-ngu. Ibilisi alimwambia Yehova: “Je, wewe hukuweka ukutakumzunguka yeye [Ayubu] na kuzunguka nyumba yake na ku-zunguka kila kitu alicho nacho pande zote? Umeibariki kazi yamikono yake, na mifugo yake imeenea kotekote duniani. Laki-ni, ili kuwe na badiliko, tafadhali nyoosha mkono wako, ugusekila kitu alicho nacho, uone kama hatakulaani wewe mbele zauso wako.”—Ayubu 1:10, 11.

9 Hivyo, Shetani alidai kwamba Ayubu alikuwa akimtumikiaMungukwa sababu yavitu alivyokuwa akipata. Pia, Shetani alidaikwamba Ayubu angemwasi Mungu ikiwa angejaribiwa. Yehovaalijibuje dai la Shetani? Kwa kuwa suala hilo lilihusisha nia yaAyubu, Yehova alimruhusu Shetani amjaribu Ayubu. Hivyo, inge-onekana wazi ikiwa Ayubu anampenda Mungu au hampendi.

AYUBU AJARIBIWA10 Punde si punde Shetani alianza kumjaribu Ayubu kati-

ka njia mbalimbali. Baadhi ya mifugo ya Ayubu iliibiwa namingine kuuawa. Watumishi wake wengi waliuawa. Hilo li-lilimletea matatizo ya kiuchumi. Halafu alipata msiba watotowake kumi walipokufa katika dhoruba. Licha ya matukio hayoyenye kuhuzunisha, “Ayubu hakutenda dhambi, wala kumhe-sabia Mungu jambo lolote lisilofaa.”—Ayubu 1:22.

11 Shetani hakukata tamaa. Haikosi alifikiri kwamba ingawa

7, 8. (a) Ni nini kilichomfanya Ayubu awe mtu wa pekee kati ya wa-nadamu wa wakati huo? (b) Shetani alitiliaje shaka nia ya Ayubu?9. Yehova alijibuje dai la Shetani, na kwa nini?10. Ni majaribu gani yaliyompata Ayubu, naye alitendaje?11. (a) Ni dai gani la pili ambalo Shetani alizusha kumhusu Ayubu,na Yehova aliitikiaje? (b) Ayubu alitendaje baada ya kupata ugonjwawenye maumivu makali?

Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu 117

Ayubu alipata thawabu kwasababu ya uaminifu wake

Ayubu angeweza kustahimili kupoteza mali zake, watumishiwake, na watoto wake, angeacha kumtumikia Mungu ikiwaangekuwa mgonjwa. Yehova alimruhusu Shetani amshambu-lie Ayubu kwa ugonjwa wenye kuchukiza sana na wenyemaumivu makali. Lakini hata hilo halikumfanya Ayubu aachekumwamini Mungu. Badala yake, alisema hivi kwa uthabiti:“Mpaka nitakapokata pumzi, sitajiondolea utimilifu wangu!”—Ayubu 27:5.

12 Ayubu hakujua kwamba Shetani ndiye aliyekuwa akisaba-bisha matatizo yake. Kwa kuwa hakujua masuala yaliyozushwana Ibilisi kuhusu haki ya Yehova ya kutawala, Ayubu alidhanikwamba Mungu ndiye aliyesababisha matatizo yake. (Ayubu6:4; 16:11-14) Hata hivyo, alidumisha utimilifu wake kwa Yeho-va. Uaminifu wa Ayubu ulithibitisha kwamba dai la Shetani etiAyubu alikuwa akimtumikia Mungu kwa sababu za kibinafsi, sila kweli!

13 Uaminifu wa Ayubu ulimwezesha Yehova kujibu dai laShetani lenye kuleta suto. Kwa kweli Ayubu alikuwa rafiki yaYehova, na Mungu alimthawabisha kwa sababu ya uaminifuwake.—Ayubu 42:12-17.

JINSI UNAVYOHUSIKA14 Suala la utimilifu kwa Mungu lililozushwa na She-

tani halikumhusu Ayubu peke yake. Wewe pia unahusika.Hilo linaonyeshwa waziwazi katika Methali 27:11, ambapoNeno la Yehova linasema hivi: “Uwe na hekima, mwana-ngu, na kuufanya moyo wangu ushangilie, ili nipatekumjibu anayenidhihaki.” Maneno hayo, yaliyoandikwamamia ya miaka baada ya Ayubu kufa, yanaonyesha kwambabado Shetani anamdhihaki Mungu na kuwashtaki watu-mishi Wake. Tunapoishi maisha yanayompendeza Yehova,tunamsaidia kujibu mashtaka ya uwongo ya Shetani, na

12. Ayubu alijibuje dai la Ibilisi?13. Uaminifu wa Ayubu kwa Mungu ulikuwa na matokeo gani?14, 15. Kwa nini tunaweza kusema kwamba dai la Shetani kumhusuAyubu linawahusu wanadamu wote?

Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu 119

hivyo kuufanya moyo wa Mungu ushangilie. Unahisije kuhu-su hilo? Je, si pendeleo kushiriki kujibu madai ya uwongo yaIbilisi, hata ikiwa utahitaji kufanya mabadiliko fulani maisha-ni mwako?

15 Ona kwamba Shetani alisema: “Kila kitu alicho nachomtu atakitoa kwa ajili ya nafsi yake.” (Ayubu 2:4) Alipo-sema “mtu,” Shetani alionyesha waziwazi kwamba dai lakeliliwahusu wanadamu wote wala si Ayubu tu. Hilo ni jambomuhimu sana. Shetani anatilia shaka utimilifu wako kwa Mu-ngu. Ibilisi angependa kuona ukimwasi Mungu na kuachakuishi maishaya uadilifu matatizoyanapotokea. Huenda She-tani akajaribuje kutimiza hilo?

16 Kama tulivyozungumzia katika Sura ya 10, Shetani hu-tumia njia mbalimbali kujaribu kuwageuza watu waachekumtumikia Mungu. Kwanza, yeye hushambulia “kama si-mba anayenguruma, akitafuta kummeza mtu.” (1 Petro5:8) Hivyo, huenda uvutano wa Shetani ukaonekana wakatiambapo marafiki, watu wa ukoo, au wengine wanapopi-nga jitihada zako za kujifunza Biblia na kuishi kulingana namambo unayojifunza.� (Yohana 15:19, 20) Pia, Shetani “hu-endelea kujigeuza mwenyewe kuwa malaika wa nuru.”(2 Wakorintho 11:14) Ibilisi anaweza kutumia hila kukupo-tosha na kukunasa uache kuishi maisha yanayompendezaMungu. Anaweza pia kutumia mambo yanayovunja moyo,labda kwa kukufanya uhisi kwamba huwezi kumpendezaMungu. (Methali 24:10) Iwe Shetani anatenda kama “simbaanayenguruma” au anajifanya “malaika wa nuru,” dai lake ni

� Hilo halimaanishi kwamba wale wanaokupinga wanaongozwa mojakwa moja na Shetani. Lakini Shetani ndiye mungu wa mfumo huu wamambo, na ulimwengu wote uko katika nguvu zake. (2 Wakorintho 4:4;1 Yohana 5:19) Kwa hiyo, tunaweza kutarajia kwamba wengi hawatafura-hi kuona ukiishi maisha yanayompendeza Mungu, na baadhi yao wata-kupinga.

16. (a) Shetani hutumia njia gani kujaribu kuwageuza watu waachekumtumikia Mungu? (b) Ibilisi anawezaje kutumia njia hizo kukunasa?

120 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

lilelile: Anasema kwamba unapokabili majaribu au vishawi-shi, utaacha kumtumikia Mungu. Unaweza kujibuje dai lakena kuthibitisha utimilifu wako kwa Mungu, kama Ayubualivyofanya?

KUTII AMRI ZA YEHOVA17 Unaweza kujibu dai la Shetani kwa kuishi maisha ya-

nayompendeza Mungu. Hilo linahusisha nini? Biblia inajibuhivi: “Lazima umpende Yehova Munguwako kwa moyowakowote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Ku-mbukumbu la Torati 6:5) Kadiri upendo wako kwa Munguunavyoongezeka, ndivyo utakavyotamani hata zaidi kufanyamapenzi yake. Mtume Yohana aliandika: “Kumpenda Munguhumaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake.” UkimpendaYehova kwa moyo wako wote, utaona kwamba “amri zake simzigo mzito.”—1 Yohana 5:3.

18 Amri za Yehova ni gani? Baadhi yake zinahusu mwene-ndo tunaopaswa kuepuka. Kwa mfano, ona sanduku lenyekichwa “Epuka Mambo Yanayomchukiza Yehova,” kwenyeukurasawa 122. Sanduku hilo lina orodhaya mambo ambayoBiblia inashutumu waziwazi. Huenda baadhi ya mazoea ya-nayotajwa yasionekane kuwa mabaya sana mwanzoni. Lakinibaada ya kutafakari maandiko yaliyotajwa, yaelekea utaonahekima ya sheria za Yehova. Huenda kubadili mwenendowako kukawa jambo gumu zaidi maishani mwako. Hata hi-vyo, kuishi maisha yanayompendeza Mungu huridhisha sanana kuleta furaha. (Isaya 48:17, 18) Huo ni mradi ambao weweunaweza kuufikia. Tunajuaje hivyo?

19 Yehova hatarajii kamwe tufanye mambo yanayopitauwezo wetu. (Kumbukumbu la Torati 30:11-14) Anajuauwezo wetu na udhaifu wetu kuliko hata tunavyojijua.

17. Tuna sababu gani kuu ya kutii amri za Yehova?18, 19. (a) Taja baadhi ya amri za Yehova. (Ona sanduku kwenye uku-rasa wa 122.) (b) Tunajuaje kwamba Mungu hatarajii tufanye mamboyanayopita uwezo wetu?

Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu 121

(Zaburi 103:14) Isitoshe, Yehova anaweza kututia nguvu ili tu-mtii. Mtume Paulo aliandika: “Mungu ni mwaminifu, nayehatawaacha ninyi mjaribiwe kupita mnavyoweza kuhimili,bali pamoja na hilo jaribu ataifanya pia njia ya kutokea kusu-di mweze kulivumilia.” (1 Wakorintho 10:13) Ili kukusaidiakuvumilia, Yehova hata anaweza kukupa “nguvu zinazopitazile za kawaida.” (2 Wakorintho 4:7) Baada ya kuvumi-lia majaribu mengi, Paulo angeweza kusema: “Kwa mamboyote nina nguvu kupitia yeye anayenipa nguvu.”—Wafilipi4:13.

EPUKA MAMBO YANAYOMCHUKIZA YEHOVA

Uuaji.—Kutoka 20:13; 21:22, 23.

Ukosefu wa maadili.—Mambo ya Walawi 20:10,

13, 15, 16; Waroma 1:24, 26,

27, 32; 1 Wakorintho 6:9, 10.

Kuwasiliana na pepo.—Kumbukumbu la Torati 18:

9-13; 1 Wakorintho 10:21, 22;

Wagalatia 5:20, 21.

Kuabudu sanamu.—1 Wakorintho 10:14.

Ulevi.—1 Wakorintho 5:11.

Kuiba.—Mambo ya Walawi

6:2, 4; Waefeso 4:28.

Kusema uwongo.—Methali 6:16, 19; Wakolosai 3:9;

Ufunuo 22:15.

Pupa.—1 Wakorintho 5:11.

Jeuri.—Zaburi 11:5;

Methali 22:24, 25; Malaki 2:16;

Wagalatia 5:20.

Maneno yasiyofaa.—Mambo ya Walawi 19:16;

Waefeso 5:4; Wakolosai 3:8.

Kuitumia damu isivyofaa.—Mwanzo 9:4; Matendo 15:20,

28, 29.

Kukataa kuiandalia familia.—1 Timotheo 5:8.

Kushiriki katika vita aukatika mizozo ya kisiasa yaulimwengu huu.—Isaya 2:4;

Yohana 6:15; 17:16.

Kuvuta sigara au kutumiadawa za kulevya.—Marko 15:23; 2 Wakorintho 7:1.

122 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

KUSITAWISHA SIFAZINAZOMPENDEZA MUNGU

20 Bila shaka, kumpendeza Yehova kunahusisha mengi zai-di kuliko tu kuepuka mambo yanayomchukiza. Unahitaji piakupenda mambo anayopenda. (Waroma 12:9) Je, huvutiwi nawatu walio na maoni, mapendezi, na viwango kama vyako?Yehova huvutiwa na watu kama hao pia. Kwa hiyo, jifunze ku-penda mambo ambayo Yehova anapenda. Baadhi ya mambo

20. Ni sifa gani zinazompendeza Mungu unazopaswa kusitawisha, nakwa nini sifa hizo ni muhimu?

Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu 123

hayo yanatajwa katika Zaburi 15:1-5, ambapo tunasoma kuhusuwatu ambao Yehova anawaona kuwa rafiki zake. Rafiki za Yehovahuonyesha yale yanayoitwa na Biblia, “matunda ya roho.” Yana-tia ndani sifa kama vile “upendo, shangwe, amani, ustahimilivu,fadhili, wema, imani, upole, kujizuia.”—Wagalatia 5:22, 23.

21 Kusoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida kutakusaidiakusitawisha sifa zinazompendeza Mungu. Na kujifunza ma-penzi ya Mungu kutakusaidia kupatanisha mawazo yako namawazoya Mungu. (Isaya 30:20, 21) Kadiri unavyozidisha upe-ndo wako kwa Yehova, ndivyo utakavyotamani hata zaidikuishi maisha yanayompendeza Mungu.

22 Jitihada inahitajiwa ili kuishi maisha yanayompendeza Ye-hova. Biblia husema, kubadili maisha yako ni sawa na kuvuautu wako wa kale na kujivika utu mpya. (Wakolosai 3:9, 10)Lakini kuhusu maagizo ya Yehova, mtunga-zaburi aliandikahivi: “Katika kuyashika kuna thawabu kubwa.” (Zaburi 19:11)Wewe pia utaona kwamba kuishi maisha yanayompendezaMungu kunaleta thawabu kwelikweli. Kwa kufanya hivyo, uta-jibu dai la Shetani na kuufanya moyo wa Yehova ushangilie!

21. Ni nini kitakachokusaidia kusitawisha sifa zinazompendeza Mu-ngu?22. Utatimiza nini kwa kuishi maisha yanayompendeza Mungu?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Unaweza kuwa rafiki ya Mungu kwa kumtii.—Yakobo 2:23.

ˇ Shetani anatilia shaka utimilifu wa wanadamuwote.—Ayubu 1:8, 10, 11; 2:4; Methali 27:11.

ˇ Lazima tuepuke mazoea yanayomchukizaMungu.—1 Wakorintho 6:9, 10.

ˇ Tunaweza kumpendeza Yehova kwa kuchukiamambo anayochukia na kupenda yaleanayopenda.—Waroma 12:9.

124 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

NABII Yeremia alisema hivi: “Kwa kweli Yehova ni Mungu.Yeye ndiye Mungu aliye hai.” (Yeremia 10:10) Isitoshe, Yeho-va Mungu ndiye Muumba wa vitu vyote vilivyo hai. Viumbewalio mbinguni walimwambia hivi: “Uliumba vitu vyote, nakwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako navyo vikaumbwa.”(Ufunuo 4:11) Alipokuwa akimwimbia Mungu wimbo wa sifa,Mfalme Daudi alisema hivi: “Kwako wewe iko chemchemi yauzima.” (Zaburi 36:9) Kwa hiyo, uhai ni zawadi kutoka kwaMungu.

2 Pia, Yehova huutegemeza uhai wetu. (Matendo 17:28) Yeyehutuandalia chakula, maji, hewa, na mahali pa kuishi. (Ma-tendo 14:15-17) Yehova amefanya hilo kwa njia inayofanyamaisha yawe yenye kufurahisha sana. Lakini, ili tufurahie ma-isha kikamili, tunahitaji kujifunza sheria za Mungu na kuzitii.—Isaya 48:17, 18.

KUUHESHIMU UHAI3 Mungu anataka tuuheshimu uhai wetu wenyewe na wa

wengine. Kwa mfano, katika siku za Adamu na Hawa, mwanawao Kaini alimkasirikia sana Abeli, ndugu yake mdogo.Yehova alimwonya Kaini kwamba hasira yake ingeweza

1. Ni nani aliyeumba vitu vyote vilivyo hai?2. Mungu hufanya nini ili kuutegemeza uhai wetu?3. Yehova alionaje kuuawa kwa Abeli?

SURA YA KUMI NA TATU

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai

Mungu anauonaje uhai?

Mungu huonaje kutoa mimba?

Tunawezaje kuonyesha kwambatunauheshimu uhai?

TUNAUHESHIMU UHAI

ˇ kwa kutotoa mimba

ˇ kwa kuacha

kabisa

kuwachukia

wanadamu

wenzetu

ˇ kwa kuacha

kabisa mazoea

machafu

kumfanya atende dhambi nzito. Kaini alipuuza onyo hilo. ‘Ali-mshambulia Abeli ndugu yake, akamuua.’ (Mwanzo 4:3-8)Yehova alimwadhibu Kaini kwa kumuua ndugu yake.—Mwa-nzo 4:9-11.

4 Maelfu ya miaka baadaye, Yehova aliwapa watu wa Israe-li sheria zilizowasaidia kumtumikia kwa njia inayompendeza.Kwa sababu sheria hizo zilitolewa kupitia nabii Musa, nya-kati nyingine zinaitwa Sheria ya Musa. Mojawapo ya sheriahizo inasema: “Usiue.” (Kumbukumbu la Torati 5:17) Hilo li-liwaonyesha Waisraeli kwamba Mungu anathamini uhai wawanadamu na kwamba wanadamu wanapaswa kuuthaminiuhai wa wengine.

5 Namna gani uhai wa mtoto ambaye hajazaliwa? Kulinganana Sheria ya Musa, ilikuwa kosa kumuua mtoto aliye katika tu-mbo la mama yake. Ndiyo, hata uhai wa mtoto huyo ni wenyethamani kwa Yehova. (Kutoka 21:22, 23; Zaburi 127:3) Hilo li-namaanisha kwamba ni kosa kutoa mimba.

6 Kuuheshimu uhai kunatia ndani kuwa na maoni yanayo-faa kuelekea wanadamu wenzetu. Biblia inasema: “Kila mtuanayemchukia ndugu yake ni muuaji, nanyi mnajua kwambahakuna muuaji aliye na uzima wa milele ukikaa ndani yake.”(1 Yohana 3:15) Ikiwa tunataka kupata uzima wa milele, tu-napaswa kuacha kabisa kuwachukia wanadamu wenzetu, kwasababu mara nyingi chuki husababisha jeuri. (1 Yohana 3:11,12) Tunapaswa kujifunza kupendana.

7 Namna gani kuuheshimu uhai wetu wenyewe? Kwa kawa-ida watu hawapendi kufa, lakini watu fulani huhatarisha uhaiwao ili kujifurahisha. Kwa mfano, watu wengi huvuta sigara,hutafuna miraa, au kutumia dawa za kulevya ili kujisisimua.

4. Katika Sheria ya Musa, Mungu alikaziaje maoni yanayofaa kuhu-su uhai?5. Tuoneje kutoa mimba?6. Kwa nini hatupaswi kuwachukia wanadamu wenzetu?7. Taja baadhi ya mazoea yanayoonyesha kwamba mtu haheshimuuhai.

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai 127

Vitu hivyo huudhuru mwili na mara nyingi husababisha kifo.Mtumwenye mazoeaya kutumiavitu hivyohauoni uhai kuwamtakatifu.Mazoea hayo ni machafu machoni pa Mungu. (Wa-roma 6:19; 12:1; 2 Wakorintho 7:1) Ili kumtumikia Mungukwa njia inayompendeza, lazima tuache mazoea hayo. Inga-wa huenda ikawa vigumu sana kuacha mazoea hayo, Yehovaanaweza kutupa msaada tunaohitaji. Naye huthamini tunapo-jitahidi kuuona uhai wetu kuwa zawadi yenye thamani kutokakwake.

8 Ikiwa tunauheshimu uhai, tutazingatia usalama. Hatuta-kuwa wazembe wala kuhatarisha uhai ili kupata raha aumsisimuko tu. Tutaepuka kuendesha magari ovyovyo na ku-shiriki katika michezo yenye jeuri au hatari. (Zaburi 11:5)Sheria ya Mungu aliyowapa Waisraeli wa kale ilisema: “Ikiwautajenga nyumba mpya [yenye paa tambarare], pia utafanyaukuta wa ukingoni kwa ajili ya dari lako, ili usiletee nyumbayako hatia ya damu kwa sababu mtu anaweza kuanguka kuto-ka hapo.” (Kumbukumbu la Torati 22:8) Kupatana na kanuniya sheria hiyo, ngazi za nyumba zinapaswa kuwa katika halinzuri ili mtu asijikwae, aanguke, na kuumia vibaya. Ikiwa unagari, hakikisha kwamba ni salama kuliendesha.Makaoyako augari lako lisihatarishe kamwe uhai wako au wa wengine.

9 Namna gani uhai wa wanyama? Huo pia ni mtakatifu kwaMuumba. Mungu anaruhusu kuua wanyama kwa ajili ya cha-kula na mavazi au ili kuwalinda watu wasipatwe na madhara.(Mwanzo 3:21; 9:3; Kutoka 21:28) Hata hivyo, kuwa mkatili kwawanyama au kuwaua kwa ajili ya kujifurahisha tu ni kosa na nikutoheshimu hata kidogo utakatifu wa uhai.—Methali 12:10.

KUHESHIMU DAMU10 Baada ya Kaini kumuua Abeli ndugu yake, Yehova ali-

8. Kwa nini tunapaswa kuzingatia usalama?9. Ikiwa tunauheshimu uhai, tutawatendeaje wanyama?10. Mungu ameonyeshaje kwamba kuna uhusiano kati ya uhai nadamu?

128 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

mwambia Kaini: “Damu ya ndugu yako inanililia kutoka kati-ka udongo.” (Mwanzo 4:10) Mungu alipotaja damu ya Abeli,alikuwa akizungumzia uhai wa Abeli. Kaini alikuwa ameko-mesha uhai wa Abeli, na sasa ilikuwa lazima Kaini aadhibiwe.Ilikuwa kana kwamba damu ya Abeli, au uhai wake, uli-kuwa ukimlilia Yehova ili haki itekelezwe. Uhusiano kati yauhai na damu ulionyeshwa tena baada ya Mafuriko ya sikuya Noa. Kabla ya Mafuriko hayo, wanadamu walikuwa waki-la matunda, mboga, nafaka, na kokwa tu. Baada ya Mafuriko,Yehova alimwambia Noa na wanawe: “Kila mnyama anayete-mbea ambaye yuko hai anaweza kuwa chakula chenu. Kamanilivyowapa mimea ya majani, nawapeni hao wote.” Hata hi-vyo, Mungu alitoa amri hii: “Isipokuwa tu nyama pamoja nanafsi yake [au,uhai wake]—damuyake—msile.” (Mwanzo 1:29;9:3, 4) Ni wazi kwamba Yehova anahusianisha uhai na damuya kiumbe.

11 Tunaonyesha kwamba tunaheshimu damu kwa kutoi-la. Katika Sheria ambayo Yehova aliwapa Waisraeli, aliamuruhivi: “Na mtu yeyote . . . ambaye katika kuwinda anamkamatamnyama-mwitu au ndege anayeweza kuliwa, basi ataimwagadamu yake na kuifunika kwa mavumbi. . . . Niliwaambia wanawa Israeli: ‘Hamtakula damu ya mwili wa namna yoyote.’”(Mambo ya Walawi 17:13, 14) Amri ambayo Mungu alimpaNoa karibu miaka 800 mapema kuhusu kutokula damu yamnyama bado ilikuwa ikitumika. Maoni ya Yehova yaliku-wa wazi: Watumishi wake wangeweza kula nyama ya mnyamalakini si damu yake. Walipaswa kuimwaga chini na hivyo ku-urudisha uhai wa kiumbe huyo kwa Mungu.

12 Wakristo pia wanapaswa kufuata amri hiyo. Mitumena wanaume wengine waliokuwa wakiongoza kati ya wa-fuasi wa Yesu wa karne ya kwanza walikutana ili kuamua niamri gani zilizopaswa kufuatwa katika kutaniko la Kikristo.

11. Mungu alitoa amri gani kuhusu damu tangu siku za Noa?12. Ni amri gani kuhusu damu iliyotolewa na roho takatifu katikakarne ya kwanza ambayo ingali inatumika leo?

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai 129

Waliamua hivi: “Roho takatifu na sisi wenyewe tumependeleatusiwaongezee ninyi mzigo zaidi, ila mambo haya ya lazima,kuendelea kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sa-namu na damu na vitu vilivyonyongwa [bila kutoa damu] nauasherati.” (Matendo 15:28, 29; 21:25) Kwa hiyo, lazima ‘tue-ndelee kujiepusha na damu.’ Machoni pa Mungu, kujiepushana damu ni muhimu kama kujiepusha na ibada ya sanamu nauasherati.

13 Je, amri kuhusu kujiepusha na damu inahusu kutiwadamu mishipani? Ndiyo. Kwa mfano: Tuseme daktari angeku-ambia ujiepushe na pombe. Je, hilo lingemaanisha kwambahupaswi kunywa pombe lakini unaweza kutiwa pombe mishi-pani mwako? Bila shaka hapana! Vivyo hivyo, kujiepusha nadamu kunamaanisha kutoitia mwilini kwa njia yoyote ile. Kwahiyo, amri ya kujiepusha na damu inamaanisha kwamba ha-tutamruhusu mtu yeyote atutie damu mishipani.

14 Namna gani ikiwa Mkristo amejeruhiwa vibaya auanahitaji kufanyiwa upasuaji mkubwa? Huenda madakta-ri wakasema kwamba anapaswa kutiwa damu mishipani,la sivyo atakufa. Bila shaka, Mkristo hangependa kufa. Ata-jitahidi kuulinda uhai ambao ni zawadi yenye thamanikutoka kwa Mungu kwa kukubali matibabu ya aina nyingi-ne ambayo hayahusishi matumizi yasiyofaa ya damu. Hivyo,atatafuta matibabu ya aina hiyo ikiwezekana na kukubali njianyingine za tiba zisizotia ndani damu.

15 Je, Mkristo avunje sheria ya Mungu ili aishi muda mre-fu kidogo katika mfumo huu wa mambo? Yesu alisema: “Kwamaana yeyote yule anayetaka kuiokoa nafsi yake [au uhai] ata-ipoteza; lakini yeyote yule anayeipoteza nafsi yake kwa ajiliyangu ataipata.” (Mathayo 16:25) Hatutaki kufa. Lakini tukija-ribu kuokoa uhai wetu wa sasa kwa kuvunja sheria ya Mungu,

13. Toa mfano unaoonyesha kwamba amri ya kujiepusha na damuinahusu kutiwa damu mishipani.14, 15. Ikiwa madaktari wanasema kwamba Mkristo anapaswa kuti-wa damu mishipani, afanyeje, na kwa nini?

130 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

tutakuwa katika hatari ya kupoteza uzi-ma wa milele. Basi ni jambo la hekimakutumaini sheria ya Mungu ya uadili-fu, tukiwa na hakika kwamba ikiwatutakufa kwa sababu yoyote ile, Mpaji-Uhai wetu atatukumbuka katika ufufuona kuturudishia uhai ambao ni zawadiyenye thamani.—Yohana 5:28, 29; Wae-brania 11:6.

16 Watumishi waaminifu wa Munguleo, huazimia kwa uthabiti kufuata amriya Mungu kuhusu damu. Hawawezikula damu kwa njia yoyote ile. Walahawawezi kukubali damu kwa sababuza matibabu.� Wana hakika kwambaMungu, aliyeumba damu anajua kina-chowafaa. Je, unaamini kwamba anajua?

MATUMIZI PEKEEYANAYOFAA YA DAMU

17 Sheria ya Musa ilikazia njia moja tuinayofaa ya kutumia damu. Kuhusu iba-dayaWaisraeli wakale,Yehova aliamuruhivi: “Nafsi ya [au, uhai wa] mwili ikokatika damu, nami mwenyewe nimeiwe-ka juu ya madhabahu ili ninyi mfanye upatanisho kwa ajiliya nafsi zenu, kwa sababu damu ndiyo hufanya upatanisho.”(Mambo ya Walawi 17:11) Waisraeli walipofanya dhambi,

� Unaweza kupata habari kuhusu matibabu yasiyohusisha kuti-wa damu mishipani kwenye ukurasa wa 13-17 wa broshua DamuYaweza Kuokoaje Uhai Wako? iliyochapishwa na Mashahidi wa Ye-hova.

16. Watumishi wa Mungu huazimia nini kwa uthabiti kuhusudamu?17. Yehova Mungu alikubali damu itumiwe kwa njia gani ya pekeekatika Israeli la kale?

Ikiwa daktariangekwambia

ujiepushe na pombe,je, ungekubali itiwemishipani mwako?

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai

walipata msamaha kwa kutoa dhabihu ya mnyama na ki-asi fulani cha damu yake kilitiwa kwenye madhabahu katikamaskani au baadaye kwenye hekalu la Mungu. Njia pekeeiliyofaa ya kutumia damu ilikuwa kwa ajili ya dhabihu kamahizo.

18 Wakristo wa kweli hawako chini ya Sheria ya Musa nahivyo hawatoi dhabihu za wanyama na kuweka damu kwe-nye madhabahu. (Waebrania 10:1) Hata hivyo, kutumiwa kwadamu kwenye madhabahu katika Israeli la kale kuliwakilishadhabihu ya mwisho na yenye thamani sana ya Mwana waMungu, Yesu Kristo. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 5ya kitabu hiki, Yesu alitoa uhai wake wa kibinadamu kwa ajiliyetu kwa kuruhusu damu yake imwagwe ikiwa dhabihu. Ki-sha alienda mbinguni na kumtolea Mungu mara moja kwa

18. Tunaweza kupata baraka gani kupitia kwa damu ya Yesu iliyo-mwagwa?

Unaweza kuonyeshaje kwamba unathamini uhai na damu?

132 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

wakati wote thamani ya damu yake iliyomwagwa. (Waebrania9:11, 12) Kwa kufanya hivyo, aliweka msingi wa msama-ha wa dhambi zetu na kutufungulia njia ya kupata uzimawa milele. (Mathayo 20:28; Yohana 3:16) Njia hiyo ya ku-tumia damu imethibitika kuwa muhimu sana! (1 Petro 1:18,19) Tunaweza tu kupata wokovu kwa kuthamini damu ya Yesuiliyomwagwa.

19 Tunapaswa kumshukuru Yehova Mungu sana kwa saba-bu ya kutupa zawadi ya uhai kwa upendo! Je, hilo halipaswikutuchochea kuwaambia wengine kuhusu pendeleo la kupatauzimawa milele kwa msingi wa imani katika dhabihu ya Yesu?Ikiwa tunathamini uhai wa wanadamu wenzetu kama Munguanavyouthamini, tutachochewa kuwahubiria kwa hamu nabidii. (Ezekieli 3:17-21) Tukitimiza jukumu hilo kwa bidii, tuta-weza kusema kama mtume Paulo alivyosema: “Mimi ni safikutokana na damu ya watu wote, kwa maana sikuepuka kuwa-ambia ninyi mashauri yote ya Mungu.” (Matendo 20:26, 27)Kuwahubiriawatu kumhusu Mungu na makusudi yake ni njiabora ya kuonyesha kwamba tunathamini sana uhai na damu.

19. Ni lazima tufanye nini ili tuwe “safi kutokana na damu ya watuwote”?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu.—Zaburi 36:9; Ufunuo 4:11.

ˇ Ni kosa kutoa mimba kwa sababu uhai wamtoto ambaye hajazaliwa ni wenye thamanimachoni pa Mungu.—Kutoka 21:22, 23;Zaburi 127:3.

ˇ Tunaonyesha kwamba tunaheshimu uhaikwa kutouhatarisha na kutokula damu.—Kumbukumbu la Torati 5:17;Matendo 15:28, 29.

Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai 133

YEHOVA MUNGU anataka familia yako iwe na maisha yenyefuraha. Neno lake, Biblia, hutoa maagizo kwa kila mmoja kati-ka familia na kuonyesha jukumu ambalo Mungu anataka kilammoja atekeleze. Kila mmoja katika familia akitimiza jukumulake kulingana na shauri la Mungu, familia itakuwa na furahasana. Yesu alisema: “Wenye furaha ni wale wanaolisikia nenola Mungu na kulishika!”—Luka 11:28.

2 Furaha ya familia inategemea hasa kutambua kwamba fa-milia ilianzishwa na Yehova, ambaye Yesu alimwita “Babayetu.” (Mathayo 6:9) Baba yetu wa mbinguni ndiye aliyeanzi-shakila familiadunianinabila shakaanajuakinacholeta furahakatika familia. (Waefeso 3:14, 15) Kwa hiyo, Biblia inafundishanini kuhusu jukumu la kila mmoja katika familia?

FAMILIA ILIANZISHWA NA MUNGU3 Yehova aliwaumba wanadamu wa kwanza, Adamu na

1. Ni nini siri ya kuwa na familia yenye furaha?2. Furaha ya familia inategemea kutambua nini?3. Biblia inaelezaje mwanzo wa familia ya wanadamu, na tunajuajekwamba yale inayosema ni ya kweli?

SURA YA KUMI NA NNE

Jinsi ya Kufanya Maisha yaFamilia Yako Yawe Yenye Furaha

Ni nini kinachohitajiwa ili kuwa mume mzuri?

Mwanamke anawezaje kufaulu kutimizajukumu lake akiwa mke?

Ni nini kinachohitajiwa ili kuwa mzazi mzuri?

Watoto wanaweza kufanya nini ili maisha yafamilia yawe yenye furaha?

Hawa, na kuwaunganisha kuwa mume na mke. Aliwawe-ka katika paradiso maridadi hapa duniani, bustani ya Edeni,na kuwaambia wazae watoto. Yehova alisema: “Zaeni, muwewengi, mjaze dunia.” (Mwanzo 1:26-28; 2:18, 21-24) Hii si ha-dithi au jambo la kukisiwa tu, kwa sababu Yesu alionyeshakwamba yale ambayo kitabu cha Mwanzo kinasema kuhu-su mwanzo wa familia ni ya kweli. (Mathayo 19:4, 5) Ingawatunapata matatizo mengi na maisha leo hayako kama Mungualivyokusudia,hebutuonenikwanini familia inawezakuwanafuraha.

4 Kila mmoja katika familia anaweza kuchangia furaha yafamilia kwa kumwiga Mungu katika kuonyesha upendo. (Wa-efeso 5:1, 2) Hata hivyo, tunawezaje kumwiga Mungu nahatuwezi kumwona? Tunaweza kujifunza jinsi Yehova anavyo-tenda kwa sababu alimtuma Mwana wake mzaliwa wa kwanzakutoka mbinguni kuja duniani. (Yohana 1:14, 18) Alipokuwaduniani, Mwana huyo, YesuKristo, alimwiga sana Babayake wambinguni hivi kwamba kumwona na kumsikiliza Yesu kuliku-wa sawa na kuwa pamoja na Yehova na kumsikiliza. (Yohana14:9) Kwa hiyo, kila mmoja wetu anaweza kuchangia zaidi fu-raha ya familia kwa kujifunza kuhusu upendo ambao Yesualionyesha na kufuata mfano wake.

KIELELEZO KWA WAUME5 Biblia inasema kwamba waume wanapaswa kuwatendea

wake zao jinsi Yesu alivyowatendea wanafunzi wake. Fiki-ria mwongozo huu wa Biblia: “Waume, endeleeni kuwapendawake zenu, kama vile Kristo pia alivyolipenda kutaniko nakujitoa mwenyewe kwa ajili yake . . . Vivyo hivyo, wau-me wanapaswa kuwa wakiwapenda wake zao kama miili

4. (a) Kila mmoja katika familia anawezaje kuchangia furaha ya fa-milia? (b) Kwa nini familia itapata furaha ikijifunza kuhusu maishaya Yesu?5, 6. (a) Waume wanajifunza nini kutokana na jinsi Yesu anavyo-litendea kutaniko? (b) Mtu anapaswa kufanya nini ili asamehewedhambi zake?

Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha 135

yao wenyewe. Yeye anayempenda mke wake anajipendamwenyewe,kwa maanahakuna mtuanayeuchukia mwiliwakekwa vyovyote; bali huulisha na kuutunza kwa upendo, kamavile Kristo pia anavyolitendea kutaniko.”—Waefeso 5:23, 25-29.

6 Upendo wa Yesu kwa wanafunzi wake ni kielelezo borakwa waume. Yesu ‘aliwapenda mpaka mwisho,’ akadhabihuuhai wake kwa ajili yao, hata ingawa hawakuwa wakamilifu.(Yohana 13:1; 15:13) Vivyo hivyo, waume wanahimizwa hivi:“Endeleeni kuwapenda wake zenu nanyi msiwakasirikie kwauchungu.” (Wakolosai 3:19) Ni nini kitakachomsaidia mumekufuata shauri hilo, hasa ikiwa nyakati nyingine mke wake ha-tendi kwa busara? Anapaswa kukumbuka makosa yake naanachopaswa kufanya ili kupata msamaha wa Mungu. Anapa-swa kufanya nini? Anapaswa kumsamehe kila mtuanayemkosea, kutia ndani mke wake. Bila shaka, mke anapa-swa kufanya vivyo hivyo. (Mathayo 6:12, 14, 15) Je, unaona nikwa nini watu fulani husema kwamba ili ndoa zifanikiwe lazi-ma wenzi wote wawili wawe tayari kusameheana?

7 Waumewanapaswa kukumbuka pia kwamba sikuzote Yesualiwajali wanafunzi wake. Alizingatia udhaifu wao na ma-hitaji yao ya kimwili. Kwa mfano, alisema hivi walipokuwawamechoka: “Njooni, ninyi wenyewe, faraghani katika maha-li pasipo na watu mpumzike kidogo.” (Marko 6:30-32) Wakepiawanastahili kuhangaikiwa kwa upendo.Biblia husema kwa-mba wao ni “chombo dhaifu zaidi” na waume wanaamriwawawape “heshima.” Kwa nini? Kwa kuwa waume na wake piawanashiriki “pendeleo lisilostahiliwa la uzima.” (1 Petro 3:7)Waume wanapaswa kukumbuka kwamba Mungu hupende-zwa na uaminifu wa mtu wala si jinsia yake.—Zaburi 101:6.

8 Biblia inasema kwamba mume “anayempenda mke wakeanajipenda mwenyewe.” Hiyo ni kwa sababu mume na mke“si wawili tena, bali mwili mmoja,” kama Yesu alivyosema.

7. Yesu alizingatia nini, naye aliwawekea waume kielelezo gani?8. (a) Mume ‘anayempenda mke wake, anajipendaje mwenyewe’?(b) Inamaanisha nini kwamba mume na mke ni “mwili mmoja”?

136 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

(Mathayo 19:6) Hivyo basi, hawapaswi kufanya ngono namtu mwingine yeyote. (Methali 5:15-21; Waebrania 13:4) Wa-taepuka kufanya hivyo ikiwa kila mmoja anajali mahitaji yayule mwingine bila ubinafsi. (1 Wakorintho 7:3-5) Kikumbu-sho hiki pia kinafaa: “Hakuna mtu anayeuchukia mwiliwake kwa vyovyote; bali huulisha na kuutunza kwa upendo.”Waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama wanavyo-jipenda wenyewe, wakikumbuka kwamba watatoa hesabukwa Yesu Kristo, aliye kichwa chao.—Waefeso 5:29; 1 Wakori-ntho 11:3.

9 Mtume Paulo alizungumzia ‘upendo mwororo alio naoKristo Yesu.’ (Wafilipi 1:8) Wororo wa Yesu ulikuwa sifa yenyekuburudisha, iliyowavutia wanawake ambao walikuwa wana-funzi wake. (Yohana 20:1,11-13,16) Nao wake hutamani sanawaume zao wawapende kwa wororo.

KIELELEZO KWA WAKE10 Familia ni kama shirika, na ili lifanye kazi vizuri, lina-

hitaji kuwa na kichwa. Hata Yesu anajitiisha kwa Yule aliyeKichwa chake. “Kichwa cha Kristo ni Mungu” kama vile “ki-chwa cha mwanamke ni mwanamume.” (1 Wakorintho 11:3)Kujitiisha kwa Yesu chini ya ukichwa wa Mungu ni mfanomzuri kwa kuwa sote tuna kichwa ambaye tunapaswa kujitii-sha kwake.

11 Wanaume wasio wakamilifu hufanya makosa na maranyingi wao hupungukiwa katika jukumu lao la kuwa vi-chwa vya familia. Kwa hiyo, mke anapaswa kufanya nini?Hapaswi kudharau mambo ambayo mume wake anafanyaau kujaribu kumnyang’anya ukichwa. Mke anapaswa kuku-mbuka kwamba roho ya utulivu na upole ina thamani kubwa

9. Ni sifa gani ya Yesu inayotajwa katika Wafilipi 1:8, na kwa niniwaume wanapaswa kuwaonyesha wake zao sifa hiyo?10. Yesu anawawekeaje wake mfano?11. Mke anapaswa kumwonaje mume wake, na mwenendo wakeunaweza kuwa na matokeo gani?

Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha 137

machoni pa Mungu. (1 Petro 3:4) Akiwa na roho hiyo, itaku-wa rahisi kwake kuonyesha utii wa kimungu hata katika halingumu. Isitoshe, Biblia inasema: “Mke anapaswa kumheshi-mu sana mume wake.” (Waefeso 5:33) Lakini vipi akikataakujitiisha chini ya Kristo akiwa Kichwa chake? Biblia inawasi-hi wake hivi: “Jitiisheni kwa waume zenu wenyewe, ili, ikiwawowote si watiifu kwa lile neno, wavutwe bila neno kupitiamwenendo wa wake zao, kwa sababu wamekwisha kushuhu-dia kwa macho mwenendo wenu ulio safi kiadili pamoja naheshima kubwa.”—1 Petro 3:1, 2.

12 Mume awe ni mwamini au la, mke hatakuwa akimvunjiaheshima ikiwa ataeleza maoni yake kwa njia ya busara hatakama yanatofautiana na ya mume. Huenda maoni yake ya-kawa sawa, na yanaweza kufaidi familia nzima ikiwa mumeatamsikiliza. Ingawa Abrahamu hakukubaliana na mke wakeSara alipopendekeza jinsi ya kutatua tatizo fulani la familia,Mungu alimwambia: “Sikiliza sauti yake.” (Mwanzo 21:9-12)Bila shaka, mume anapofanya uamuzi ambao haupingani nasheria ya Mungu, mke wake anapaswa kuonyesha anajitiishakwake kwa kuunga mkono uamuzi huo.—Matendo 5:29; Wa-efeso 5:24.

13 Mke anaweza kutimiza jukumu lake kwa kutunza fami-lia. Kwa mfano, Biblia inaonyesha kwamba wanawake ambaowameolewa wanapaswa ‘kuwapenda waume zao, kuwapendawatoto wao, kuwa na utimamu wa akili, safi kiadili, wafanya-kazi nyumbani, wema, wakijitiisha kwa waume zao wenyewe.’(Tito2:4, 5) Mke ambaye pia nimama anayefanya hivyo, atape-ndwa na kuheshimiwa daima na familia yake. (Methali 31:10,28) Lakini kwa kuwa ndoa ni muungano wa watu wasio waka-milifu, huenda hali fulani wasizoweza kuvumilia zikawafanyawatengane au kutalikiana. Biblia inaruhusu kutengana hali

12. Kwa nini si kosa mke kueleza maoni yake kwa heshima?13. (a) Andiko la Tito 2:4, 5 linawasihi wanawake ambao wameo-lewa wafanye nini? (b) Biblia inasema nini kuhusu kutengana nakutalikiana?

138 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

fulani zinapotokea. Hata hivyo, kutengana hakupaswi kuchu-kuliwa kivivi hivi tu, kwa kuwa Biblia inashauri: “Mke hapaswikuondoka kwa mume wake; . . . na mume hapaswi kumwachamke wake.” (1 Wakorintho 7:10, 11) Msingi pekee wa Kimaa-ndiko wa talaka ni uasherati.—Mathayo 19:9.

MFANO BORA KWA WAZAZI14 Yesu aliwawekea wazazi mfano bora wa jinsi ya kuwate-

ndea watoto. Wengine walipojaribu kuwazuia watoto wadogowasimkaribie, Yesu alisema hivi: “Waacheni watoto wacha-nga waje kwangu; msijaribu kuwazuia.” Kisha Biblia inasemakwamba ‘aliwachukua watoto akawakumbatia na kuanza ku-wabariki, akiweka mikono yake juu yao.’ (Marko 10:13-16)Kwa kuwa Yesu alitumia wakati pamoja na watoto, je, hupa-swi kufanya hivyo na watoto wako? Wanahitaji wakati wakomwingi. Unahitaji kutumia wakati kuwafundisha kwani Yeho-va anawaagiza wazazi wafanye hivyo.—Kumbukumbu la Torati6:4-9.

15 Kadiri ulimwengu huu unavyozidi kuwa mbovu, ndivyo

14. Yesu aliwatendeaje watoto, nao watoto wanahitaji nini kutokakwa wazazi wao?15. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kuwalinda watoto wao?

Sara aliwawekea wake mfano gani mzuri?

watoto wanavyohitaji wazazi watakaowalinda dhidi ya watuwanaotaka kuwaumiza, kama wale wanaowatendea viba-ya watoto kingono. Fikiria jinsi Yesu alivyowalinda wanafunziwake ambao aliwapenda sana na kuwaita “watoto wadogo.”Alipokamatwa ili auawe baadaye, Yesu alifanya mipango ili wa-nafunzi wake watoroke. (Yohana 13:33; 18:7-9) Ukiwa mzazi,unapaswa kuwa macho kuona njia ambazo Ibilisi anatumiakujaribu kuwaumiza watoto wako. Unahitaji kuwaonya mape-ma.� (1Petro5:8) Huundiowakati ambapohaliyaoya kimwili,ya kiroho, na ya kiadili imo hatarini zaidi kuliko wakati mwi-ngine wowote.

� Habari kuhusu jinsi ya kuwalinda watoto zinapatikana katika suraya 32 ya kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, kilichochapi-shwa na Mashahidi wa Yehova.

Wazazi wanaweza kujifunza nini kutokana na jinsiYesu alivyowatendea watoto?

140 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

16 Usiku uliotangulia kifo cha Yesu, wanafunzi wake walibi-shana kuhusu ni nani aliye mkubwa kati yao. Kwa kuwaYesu aliwapenda, badala ya kuwakasirikia, aliendelea kuwasi-hi kwa maneno na kuwawekea mfano. (Luka 22:24-27; Yohana13:3-8) Ikiwa wewe ni mzazi, je, unaona jinsi unavyowezakufuata mfano wa Yesu unapowarekebisha watoto wako? Nikweli kwamba wanahitaji nidhamu, lakini inapaswa kutolewakwa “kiwango kinachofaa” wala si kwa hasira. Hupaswi ku-zungumza nao bila kufikiri “kama kwa upanga unaochoma.”(Yeremia 30:11; Methali 12:18) Nidhamu inapaswa kutolewakwa njia ambayo mtoto ataithamini baadaye.—Waefeso 6:4;Waebrania 12:9-11.

MFANO KWA WATOTO17 Je, watoto wanaweza kujifunza kutoka kwa Yesu? Ndiyo,

wanaweza! Kupitia mfano wake, Yesu alionyesha jinsi watotowanavyopaswa kuwatii wazazi wao. Alisema: “Kama vile Babaalivyonifundisha, ndivyo ninavyosema.”Akaongezea: “Sikuzo-te mimihufanya mamboyanayompendeza.” (Yohana 8:28, 29)Yesu alimtii Baba yake wa mbinguni, na Biblia inawaambiawatoto wawatii wazazi wao. (Waefeso 6:1-3) Ingawa Yesu ali-kuwa mtoto mkamilifu, aliwatii wazazi wake, Yusufu na Maria,ambao hawakuwa wakamilifu. Hapana shaka kwamba hilo lili-changia furaha ya kila mmoja katika familia ya Yesu!—Luka 2:4, 5, 51, 52.

18 Je, watoto wanaweza kutambua njia wanazoweza kumwi-ga Yesu zaidi na kuwafurahisha wazazi wao? Ni kweli kwambanyakati nyingine watoto huona ni vigumu kuwatii wazazi wao,hata hivyo, Mungu anataka watoto watii. (Methali 1:8; 6:20)Yesu alimtii Baba yake wa mbinguni sikuzote, hata hali zili-pokuwa ngumu. Pindi moja, Mungu alipomtaka Yesu afanye

16. Wazazi wanaweza kujifunza nini kutokana na njia ambayo Yesualishughulikia kutokamilika kwa wanafunzi wake?17. Yesu aliwawekea watoto mfano bora katika njia zipi?18. Kwa nini Yesu alimtii Baba yake wa mbinguni sikuzote, na wato-to humfurahisha nani wanapowatii wazazi wao leo?

Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha 141

jambo gumu sana, Yesu alisema: “Niondolee kikombe hiki[au takwa fulani].” Hata hivyo, Yesu alifanya mapenzi ya Mu-ngu kwa sababu alitambua kwamba Babayake anajua mwendoborawa kufuata. (Luka 22:42) Kwa kujifunza kutii, watotowata-wafurahisha wazazi wao na Baba yao wa mbinguni.�—Methali23:22-25.

19 Ibilisi alimshawishi Yesu, na tunaweza kuwa na hakikakwamba atawashawishi watoto pia wafanye mambo mabaya.(Mathayo 4:1-10) Shetani Ibilisi hutumia mikazo ya marafikiambayo inaweza kuwa mikali sana. Basi ni muhimu sana wato-to wasishirikiane na wale wanaotenda mabaya. (1 Wakorintho15:33) Dina, binti ya Yakobo alishirikiana na watu ambao ha-wakuwa wakimwabudu Yehova, na kufanya hivyo kulimleteamatatizo makubwa. (Mwanzo 34:1, 2) Hebu wazia jinsi familiainavyoweza kuumia mmoja wao akihusika katika mwenendompotovu kingono!—Methali 17:21, 25.

SIRI YA KUWA NA FAMILIA YENYE FURAHA20 Shauri la Biblia linapotumiwa, inakuwa rahisi kukabiliana

� Mtoto ana haki ya kutotiiikiwa mzazi anamwomba avu-nje sheria ya Mungu.—Matendo5:29.

19. (a) Shetani huwashawishiwatoto jinsi gani? (b) Mwene-ndo mbaya wa watoto unawezakuwaathirije wazazi?20. Ili kuwa na maisha ya fa-milia yenye furaha, kila mmojakatika familia anapaswa kufa-nya nini?

Vijana wanapaswakuzingatia nini

wanaposhawishiwa?

142 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

na matatizo katika familia. Kutumia shauri hilo ndiyo siri yakuwa na familia yenye furaha. Kwa hiyo waume, wapendeniwake zenu na kuwatendea kama Yesu anavyolitendea ku-taniko lake. Wake, tiini ukichwa wa waume zenu na mfuatemfano wa mke mwenye uwezo anayetajwa katika Methali 31:10-31. Wazazi, wazoezeni watoto wenu. (Methali 22:6) Akinababa, ‘simamieni nyumba zenu kwa njia nzuri.’ (1 Timotheo3:4,5; 5:8)Nanyiwatoto,watiiniwazaziwenu. (Wakolosai3:20)Hakuna yeyote katika familia aliye mkamilifu kwa kuwa wotehufanya makosa. Kwa hiyo, nyenyekeeni na kuombana msa-maha.

21 Kwa kweli, Biblia ina mashauri na maagizo mengi yenyefaida kuhusu maisha ya familia. Isitoshe, Biblia hutufundi-sha kuhusu ulimwengu mpya wa Mungu na paradiso yakidunia itakayojaa watu wenye furaha wanaomwabudu Ye-hova. (Ufunuo 21:3, 4) Hilo ni tarajio zuri kama nini!Hata sasa, tunaweza kuwa na maisha ya familia yenye fura-ha kwa kufuata maagizo ya Mungu yaliyo katika Neno lake,Biblia.

21. Tuna tarajio gani zuri, na tunawezaje kuwa na maisha ya familiayenye furaha sasa?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Waume wanapaswa kuwapenda wakezao kama miili yao wenyewe.—Waefeso 5:25-29.

ˇ Wake wanapaswa kuipenda familia yao nakuwaheshimu waume zao.—Tito 2:4, 5.

ˇ Wazazi wanapaswa kuwapenda, kuwafu-ndisha, na kuwalinda watoto wao.—Kumbukumbu la Torati 6:4-9.

ˇ Watoto wanapaswa kuwatii wazazi wao.—Waefeso 6:1-3.

Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha 143

YEHOVA MUNGU anatujali sana na anataka tufaidike namwongozo wake wenye upendo. Tukimwabudu kwa njiainayofaa, tutakuwa wenye furaha na tutaepuka matatizomengi maishani. Pia tutapata baraka na msaada wake. (Isa-ya 48:17) Hata hivyo, kuna mamia ya dini ambazo hudaikwamba zinafundisha kweli kumhusu Mungu. Lakini zi-natofautiana katika mafundisho yao kumhusu Mungu namapenzi yake.

2 Unawezaje kujua njia inayofaa ya kumwabudu Yehova?Si lazima ujifunze na kulinganisha mafundishoya dini zote.Unahitaji tu kujifunza yale ambayo Biblia inafundisha hasakuhusu dini ya kweli. Kwa mfano: Katika nchi nyingi kunatatizo la pesa bandia. Unawezaje kutofautisha pesa halali napesa bandia? Je, unahitaji kuchunguza pesa zote bandia?Hapana. Ingekuwa afadhali kama ungechunguza na kujuapesa halali. Baada ya kujua jinsi pesa halali zinavyooneka-na, unaweza kutambua pesa bandia. Vivyo hivyo, tunawezakutambua dini za uwongo kwa kujifunza kutambua diniya kweli.

3 Ni muhimu tumwabudu Yehova katika njia anayokuba-

1. Tutapata faida gani tukimwabudu Mungu kwa njia inayofaa?2. Tunawezaje kujua njia inayofaa ya kumwabudu Yehova, na ni mfa-no gani unaotusaidia kuelewa jambo hilo?3. Yesu alisema tunapaswa kufanya nini ili tupate kibali cha Mungu?

SURA YA KUMI NA TANO

Ibada Ambayo Mungu Anakubali

Je, dini zote zinampendeza Mungu?

Tunaweza kuitambuaje dini ya kweli?

Ni nani walio waabudu wa kweliwa Mungu duniani leo?

li. Watu wengi huamini kwamba dini zote zinampendezaMungu, lakini Biblia haifundishi hivyo. Hata haitoshi tu ku-dai kuwa Mkristo. Yesu alisema: “Si kila mtu anayeniambia,‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika ufalme wa mbinguni,bali yule anayefanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbi-nguni ndiye atakayeingia.” Kwa hiyo, ili tuwe na kibali chaMungu, lazima tujifunze mapenzi ya Mungu na kuyafanya.Yesu aliwaita wale wasiofanya mapenzi ya Mungu “wenyematendoyauasi-sheria.” (Mathayo7:21-23) Diniyauwongohaina thamani yoyote kama vile pesa bandia zisivyo na tha-mani. Isitoshe, dini hizo ni hatari.

4 Yehova anampa kila mtu duniani nafasi ya kupata uzi-ma wa milele. Hata hivyo, ili tuishi milele katika Paradiso,ni lazima tumwabudu Mungu kwa njia inayofaa na tuishimaisha yanayompendeza. Inasikitisha kwamba wengi hu-kataa kufanya hivyo. Ndiyo sababu Yesu alisema: “Ingienikupitia lango jembamba; kwa sababu barabara inayoongozakwenye uharibifu ni pana na kubwa, na wengi ndio wanao-ipitia; lakini lango ni jembamba na barabara inayoongozakwenye uzima ina nafasi ndogo, na wachache ndio wanao-ipata.” (Mathayo 7:13, 14) Dini ya kweli inaongoza kwenyeuzima wa milele. Dini ya uwongo inaongoza kwenye uhari-bifu. Yehova hataki mwanadamu yeyote aharibiwe na ndiyosababu anawapa watu wote nafasi ya kujifunza kumhusu.(2 Petro 3:9) Hivyo basi, uhai wetu unategemea jinsi tuna-vyomwabudu Mungu.

JINSI YA KUITAMBUA DINI YA KWELI5 “Barabara inayoongoza kwenye uzima” inaweza kupati-

kanaje? Yesu alisema kwamba dini ya kweli ingetambuliwakwa matendo ya wafuasi wake. Alisema: ‘Kwa matundayao mtawatambua. Kila mti mzuri huzaa matunda mazuri.’

4. Yesu alimaanisha nini alipozungumzia zile barabara mbili, na kilamoja inaelekea wapi?5. Tunawezaje kuwatambua wafuasi wa dini ya kweli?

Ibada Ambayo Mungu Anakubali 145

(Mathayo 7:16,17) Yaani, wale wanaofuata dini ya kweli wa-ngetambuliwa kwa mafundisho na matendo yao. Waabuduwa kweli hujitahidi kufanya mapenzi ya Mungu wakiwakikundi ingawa hawajakamilika na wanakosea. Hebu tuzu-ngumzie mambo sita yanayowatambulisha wafuasi wa diniya kweli.

6 Watumishi wa Mungu hutumia Biblia kama msingi wamafundisho yao. Biblia yenyewe inasema hivi: “Andiko lotelimeongozwa na rohoya Mungu nalo ni lenye faida kwa ku-fundisha, kwa kukaripia, kwa kunyooshamambo, kwa kutianidhamu katika uadilifu, ili mtu wa Mungu awe na uwe-zo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazinjema.” (2 Timotheo 3:16, 17) Mtume Paulo aliwaandi-kia hivi Wakristo wenzake: “Mlipolipokea neno la Mungu,ambalo mlilisikia kutoka kwetu, mlilikubali, si kama nenola wanadamu, bali, kama vile lilivyo kwa kweli, kama nenola Mungu.” (1 Wathesalonike 2:13) Hivyo, mafundisho namatendoya wafuasi wa dini ya kweli hayategemei maoni audesturi za wanadamu. Yanategemea Neno la Mungu, Biblia,lililoongozwa na roho.

7 Yesu Kristo aliweka mfano mzuri kwa kutumia Neno laMungu kama msingi wa mafundisho yake. Katika sala kwaBaba yake wa mbinguni alisema: “Neno lako ni kweli.” (Yo-hana 17:17) Yesu aliamini Neno la Mungu, na mambo yotealiyofundisha yalipatana na Maandiko. Mara nyingi Yesualisema: “Imeandikwa.” (Mathayo 4:4, 7, 10) Kisha Yesualinukuu andiko. Vivyo hivyo, watu wa Mungu leo hawafu-ndishi maoni yao wenyewe. Wanaamini kwamba Biblia niNeno la Mungu, nao hutegemeza kwa uthabiti mafundishoyao katika yale inayosema.

8 Wafuasi wa dini ya kweli humwabudu Yehova peke yake

6, 7. Watumishi wa Mungu huionaje Biblia, na Yesu aliwekaje mfa-no mzuri kuhusiana na jambo hilo?8. Kumwabudu Yehova kunatia ndani nini?

146 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

WALE WANAOMWABUDU MUNGU WA KWELI

ˇ hutumia Biblia kama msingi wa mafundisho yao

ˇ humwabudu Yehova peke yake na kuwajulisha watu jina lake

ˇ wanapendana kikweli

ˇ wanakubali kwamba Mungu anamtumia Yesu kuwaokoa

ˇ si sehemu ya ulimwengu

ˇ wanahubiri kwamba Ufalme wa Mungu ndio tumaini pekeela wanadamu

na kulijulisha jina lake. Yesu alisema: “Yehova Mungu wakondiye unayepaswa kumwabudu, na yeye peke yake ndiyeunayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.” (Mathayo 4:10)Kwa hiyo, watumishi wa Mungu humwabudu Yehova pekeyake. Ibada hiyo inatia ndani kuwajulisha watu jina la Mu-ngu wa kweli na sifa zake. Zaburi 83:18 inasema: “Wewe,ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uli-ye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.” Yesu aliweka mfanokwa kuwasaidia wengine wamjue Mungu, kama alivyosali:“Nimelifunua jina lako kwa watu ulionipa kutoka ulimwe-nguni.” (Yohana 17:6) Vivyo hivyo, waabudu wa kweli leohuwafundisha wengine kuhusu jina la Mungu, makusudiyake, na sifa zake.

9 Watu wa Mungu wanapendana kikweli bila ubinafsi.Yesu alisema: “Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyini wanafunzi wangu, mkiwa na upendo kati yenu we-nyewe.” (Yohana 13:35) Wakristo wa zamani walipendanakama Yesu alivyosema. Upendo huo unaotegemea kanuniza Biblia, hauzuiwi na tofauti za kikabila, kijamii, na kitai-fa nao huwavuta watu pamoja katika kifungo cha kudumucha undugu wa kweli. (Wakolosai 3:14) Wafuasi wa dini zauwongo hawana undugu kama huowenye upendo. Tunaju-aje? Wanauana kwa sababu ya tofauti za kitaifa au kikabila.Wakristo wa kweli hawatumii silaha wala kuwaua nduguzaoWakristoaumtu mwingineyeyote.Biblia inasema: “Wa-toto wa Mungu na watoto wa Ibilisi ni wazi kwa jambohili: Kila mtu ambaye haendelei kufanya uadilifu hatokanina Mungu, wala yeye ambaye hampendi ndugu yake. . . .Tunapaswa kupendana; si kama Kaini, aliyetokana na yulemwovu akamuua ndugu yake.”—1 Yohana 3:10-12; 4:20, 21.

10 Bila shaka, kuwa na upendo wa kweli hakumaanishi tukutowauawengine.Wakristowakweli hutumiawakati, ngu-

9, 10. Wakristo wa kweli huonyeshana upendo katika njia zipi?

148 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

vu, na mali zao kusaidiana na kutiana moyo bila ubinafsi.(Waebrania 10:24, 25) Wanasaidianawakati wa taabu na ha-wadhulumiani. Wao huishi kulingana na kanuni ya Bibliainayosema “tuwatendee wote mema.”—Wagalatia 6:10.

11 Wakristo wa kweli hukubali kwamba Mungu anamtu-mia Yesu Kristo kutuokoa. Biblia inasema: “Hakuna wokovukatika mwingine yeyote, kwa maana hakuna jina lingi-ne chini ya mbingu walilopewa wanadamu ambalo kupitiahilo lazima sisi tupate kuokolewa.” (Matendo 4:12) Kamatulivyoona katika Sura ya 5, Yesu alitoa uhai wake kuwa fi-dia kwa wanadamu watiifu. (Mathayo 20:28) Isitoshe, Yesuni Mfalme aliyewekwa rasmi na Mungu katika Ufalme wambinguni ambao utatawala dunia yote. Na Mungu anata-ka tumtii Yesu na kufuata mafundisho yake ikiwa tunatakakuishi milele. Ndiyo sababu Biblia inasema: “Yule anaye-mwamini Mwana ana uzima wa milele; yule asiyemtiiMwana hataona uzima.”—Yohana 3:36.

12 Waabudu wa kweli si sehemu ya ulimwengu. Alipo-kuwa ameshtakiwa mbele ya Pilato, mtawala Mroma, Yesualisema: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.”(Yohana 18:36) Katika nchi yoyote ile wanamoishi, wafuasiwa kweli wa Yesu ni raia wa Ufalme wake wa mbinguni nahivyo hawajihusishi kamwe na siasa za ulimwengu huu. Ha-waungi mkono upande wowote. Hata hivyo, waabudu waYehova hawawazuii wengine kujiunga na chama cha kisi-asa, kugombea kiti cha kisiasa au kupiga kura. Waabudu wakweli wa Mungu wanatii sheria hata ingawa hawajihusishina siasa. Kwa nini? Kwa sababu Neno la Mungu linawaa-muru ‘wajitiishe’ kwa “mamlaka zilizo kubwa” za kiserikali.(Waroma 13:1) Matakwaya kisiasayanapopingana na mata-kwaya Mungu, waabudu wa kweli huiga mfano wa mitume

11. Kwa nini ni muhimu kukubali kwamba Mungu anamtumia YesuKristo kutuokoa?12. Kutokuwa sehemu ya ulimwengu kunahusisha nini?

Ibada Ambayo Mungu Anakubali 149

ambaowalisema: “Lazima tumtii Mungu kuwa mtawala ku-liko wanadamu.”—Matendo 5:29; Marko 12:17.

13 Wafuasi wa kweli wa Yesu wanahubiri kwamba Ufalmewa Mungu ndio tumaini pekee la wanadamu. Yesu alita-biri: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia

13. Wafuasi wa kweli wa Yesu wana maoni gani kuhusu Ufalme waMungu, na hivyo wanachukua hatua gani?

Utafaidika sana ukimtumikia Yehovapamoja na watu wake

150 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; nandipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Wafua-si wa kweli wa Yesu Kristo hutangaza Ufalme wa mbinguniwa Mungu kuwa tumaini pekee la wanadamu badala yakuwatia watu moyo wategemee utawala wa kibinadamu ku-suluhisha matatizo yao. (Zaburi 146:3) Yesu alitufundishakusali kwa ajili ya serikali hiyo kamilifu aliposema: “Ufal-me wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kamailivyo mbinguni.” (Mathayo 6:10) Neno la Mungu lilitabirikwamba Ufalme huo wa mbinguni “utazivunja na kuziko-mesha falme hizi zote [zilizopo leo], nao utasimama mpakawakati usio na kipimo.”—Danieli 2:44.

14 Kulingana na mambo ambayo tayari tumezungumzia,jiulize: ‘Ni dini gani inayotumia Biblia kama msingi wa ma-fundisho yake yote na kuwajulisha watu jina la Yehova?Ni dini gani huonyesha upendo jinsi Yehova anavyotu-agiza, ina imani katika Yesu, si sehemu ya ulimwengu, nahutangaza Ufalme wa Mungu kuwa tumaini pekee la wana-damu? Kati ya dini zote duniani, ni dini gani inayotimizamatakwa hayo?’ Uthibitisho unaonyesha wazi kwamba niMashahidi wa Yehova.—Isaya 43:10-12.

UTAFANYA NINI?15 Huwezi kumpendeza Mungu kwa kudai tu kwamba

unamwamini. Kwani, Biblia inasema kwamba hata rohowaovu wanaamini kwamba Mungu yuko. (Yakobo 2:19)Hata hivyo, ni wazi kwamba hawafanyi mapenzi ya Mu-ngu na hawana kibali chake. Ili tukubaliwe na Mungu,haitoshi tu kuamini kwamba yeye yuko, ni lazima tufa-nye mapenzi yake. Ni lazima pia tujitenge kabisa na dini zauwongo na kukubali ibada ya kweli.

14. Ni dini gani inayotimiza matakwa ya ibada ya kweli?15. Mungu anataka tufanye nini mbali na kuamini tu kwamba yeyeyuko?

Ibada Ambayo Mungu Anakubali 151

16 Mtume Paulo alisema kwamba hatupaswi kushiriki ka-tika ibada ya uwongo. Aliandika: “‘Tokeni katikati yao, namjitenge,’ asema Yehova, ‘na mwache kugusa kitu kilichonajisi’; ‘nami nitawakaribisha ndani.’” (2 Wakorintho 6:17;Isaya 52:11) Kwa hiyo, Wakristo wa kweli wanaepuka kituchochote kinachohusiana na dini za uwongo.

17 Biblia inaonyesha kwamba dini zote za uwongo ni se-hemu ya “Babiloni Mkubwa.”� (Ufunuo 17:5) Jina hilolinatukumbusha jiji la zamani la Babiloni, ambako dini zauwongo zilianzia baada ya Mafuriko ya siku ya Noa. Mafu-ndisho na mazoea mengi ambayo ni ya kawaida katika diniza uwongoyalianza zamani huko Babiloni. Kwa mfano, Wa-babiloni waliabudu miungu mitatu-mitatu. Leo, Utatu nifundisho kuu katika dini nyingi. Lakini Biblia inafundishawazi kwamba kuna Mungu mmoja tu wa kweli, Yeho-va, na kwamba Yesu Kristo ni Mwana wake. (Yohana 17:3)Wababiloni waliamini pia kwamba wanadamu wana nafsiisiyoweza kufa ambayo huendelea kuishi baada ya mwilikufa na ambayo inaweza kuteseka motoni. Leo, dini nyingihufundisha kwamba nafsi au roho haiwezi kufa na inawezakuteseka motoni.

18 Kwa kuwa ibada ya Babiloni ya zamani ilienea du-niani pote, Babiloni Mkubwa ya leo inaweza kuitwa kwakufaa milki ya ulimwengu ya dini za uwongo. Na Munguametabiri kwamba milki hiyo ya dini za uwongo itaharibi-wa ghafula. (Ufunuo 18:8) Je, unaona kwa nini unapaswakujitenga na kila sehemu ya Babiloni Mkubwa? Yehova Mu-

� Unaweza kupata habari inayoeleza kwa nini Babiloni Mkubwainawakilisha milki ya ulimwengu ya dini za uwongo katika Nyonge-za, ukurasa 219-220.

16. Tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu kushirikiana na dini zauwongo?17, 18. “Babiloni Mkubwa” ni nini, na kwa nini ni muhimu ‘kuto-ka kwake’ haraka?

152 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

ngu anataka ‘utoke kwake,’ yaani, Babiloni Mkubwa, harakakabla ya kuchelewa.—Ufunuo 18:4.

19 Huenda baadhi ya watu wakaacha kushirikiana nawekwa sababu ya uamuzi wako wa kuacha kushirikiana nadini ya uwongo. Hata hivyo, utafaidika sana ukimtumikiaYehova pamoja na watu wake. Kama wanafunzi wa zamaniwa Yesu ambao waliacha vitu vingine ili wamfuate, utaku-wa na ndugu na dada wengi wa kiroho. Utakuwa sehemuya familia kubwa ya ulimwenguni pote yenye mamilioni yaWakristo ambao wanakupenda kikweli. Nawe utakuwa natumaini zuri la kuishi milele “katika mfumo wa mambounaokuja.” (Marko 10:28-30) Huenda wale ambao waliku-kataakwa sababuya imaniyakowataonayale ambayo Bibliainafundisha na kuwa waabudu wa Yehova.

20 Biblia inafundisha kwamba hivi karibuni Munguataharibu mfumo huu mbovu wa mambo na kuleta uli-mwengu mpya wenye uadilifu chini ya utawala wa Ufalmewake. (2 Petro 3:9, 13) Huo utakuwa ulimwengu mzuri aja-bu! Na katika mfumo huo mpya wenye uadilifu, kutakuwana dini moja tu, aina moja ya ibada ya kweli. Je, si jambo lahekima kuchukua hatua zinazofaa ili kujiunga na waabuduwa kweli sasa hivi?

19. Utafaidikaje ukimtumikia Yehova?20. Washiriki wa dini ya kweli wanatazamia nini wakati ujao?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Kuna dini moja tu ya kweli.—Mathayo 7:13, 14.

ˇ Dini ya kweli inatambuliwa kwa mafundi-sho na matendo yake.—Mathayo 7:16, 17.

ˇ Mashahidi wa Yehova wanamwabudu Mu-ngu kwa njia anayokubali.—Isaya 43:10.

Ibada Ambayo Mungu Anakubali 153

NAMNA gani ukipata habari kwamba eneo lenu lote limeti-wa sumu? Mtu fulani amekuwa akitupa kisiri takataka zenyesumu katika eneo lenu na maisha ya watu yamo hatarinisasa. Utafanya nini? Bila shaka utahama ikiwezekana. Hatahivyo, baada ya kuhama, bado utafikiria swali hili kwa uzi-to, ‘Je, nimeathiriwa na sumu hiyo?’

2 Ndivyo ilivyo kuhusiana na dini za uwongo. Bibliainafundisha kwamba ibada kama hiyo imechafuliwa na ma-fundisho na mazoea machafu. (2 Wakorintho 6:17) Ndiyosababu unapaswa kutoka katika “Babiloni Mkubwa,” amba-yo ni milki ya ulimwenguni pote ya dini za uwongo.(Ufunuo 18:2, 4) Je, tayari umefanya hivyo? Ikiwa ndivyo,unastahili kupongezwa. Hata hivyo, kuna mambo mengiambayo unahitaji kufanya mbali na kujitenga au kujiuzulukutoka katika dini ya uwongo. Baada ya kutoka, una-paswa kujiuliza, ‘Je, bado mimi ninashikilia mambo fulaniniliyozoea kufanya nilipokuwa katika dini ya uwongo?’ Fi-kiria mifano kadhaa.

1, 2. Baada ya kutoka katika dini ya uwongo, unapaswa kujiulizaswali gani, na kwa nini ni muhimu?

SURA YA KUMI NA SITA

Chukua Msimamo Upandewa Ibada ya Kweli

Biblia inafundisha nini kuhusu kutumiamifano katika ibada?

Wakristo huzionaje sikukuuza kidini?

Unaweza kuwaelezaje wengineimani yako bila kuwaudhi?

KUABUDU SANAMU NA MABABU3 Watu fulani wamekuwa na sanamu au vihekalu kati-

ka nyumba zao kwa miaka mingi. Je, wewe ni mmoja wao?Ikiwa ndivyo, huenda ukaona kwamba ni vigumu au ni vi-baya kusali kwa Mungu bila kutumia vitu vinavyoonekana.Huenda hata unavipenda sana baadhi ya vitu hivyo. Laki-ni Mungu ndiye anayesema jinsi anavyotaka aabudiwe, naBiblia inafundisha kwamba hataki tutumie sanamu. (Kutoka20:4, 5; Zaburi 115:4-8; Isaya 42:8; 1 Yohana 5:21) Kwa hiyo,unaweza kuchukua msimamo upande wa ibada ya kweli kwakuharibu vitu vyovyote ulivyo navyo ambavyo vinahusianana ibada ya uwongo. Kwa vyovyote vile, vione vitu hivyo jinsiYehova anavyoviona, yaani, ni ‘vitu vinavyochukiza.’—Ku-mbukumbu la Torati 27:15.

4 Katika dini nyingi za uwongo, mababu pia huabudiwa.

3. (a) Biblia inasema nini kuhusu kutumia sanamu, na kwa nini huendaikawa vigumu kwa wengine kukubali maoni ya Mungu? (b) Unapaswakufanya nini ikiwa una vitu vinavyohusiana na ibada ya uwongo?4. (a) Tunajuaje kwamba kuabudu mababu ni kazi bure? (b) Kwanini Yehova aliwaonya watu wake wasiwasiliane na pepo kwa njia yo-yote?

155

Kabla ya kujifunza kweli ya Biblia, watu fulani waliami-ni kwamba wafu wanaishi katika makao yasiyoonekana yaroho na kwamba wanaweza kuwasaidia au kuwaumiza waliohai. Labda ulikuwa ukijitahidi sana kuwatuliza mababu zakowaliokufa. Lakini kama ulivyojifunza katika Sura ya 6 ya ki-tabu hiki, wafu hawana fahamu wala hawaishi popote. Kwahiyo, ni kazi bure kujaribu kuwasiliana nao. Ujumbe wowoteambao inasemekana unatoka kwa mpendwa aliyekufa, kwakweli unatoka kwa roho waovu. Kwa hiyo, Yehova aliwao-nya Waisraeli wasijaribu kuongea na wafu au kuwasiliana napepo kwa njia yoyote ile.—Kumbukumbu la Torati 18:10-12.

5 Ikiwa zamani ulikuwa ukitumia sanamu au kuabudu ma-babu, unaweza kufanya nini? Soma na utafakari maandikoya Biblia yanayoonyesha maoni ya Mungu. Sali kwa Yehovakila siku kuhusu tamaa yakoya kuchukua msimamo upandewa kweli, na umwombe akusaidie uwe na maoni kama yake.—Isaya 55:9.

KRISMASI HAIKUSHEREHEKEWANA WAKRISTO WA ZAMANI

6 Ibada ya mtu inaweza kuchafuliwa na dini za uwongokupitia sherehe zinazopendwa. Kwa mfano, fikiria Krismasi.Inasemekana kwamba Krismasi ni ukumbusho wa kuzali-wa kwa Yesu Kristo, na karibu dini zote zinazodai kuwa zaKikristohusherehekea Krismasi.Hata hivyo, hakuna lolote li-nalothibitisha kwamba wanafunzi wa Yesu walisherehekeasikukuu hiyo. Kitabu Sacred Origins of Profound Things kina-sema: “Kwa miaka 200 tangu Kristo alipozaliwa, hakuna mtualiyejua siku hususa ambayo alizaliwa, na ni watu wachachetu waliotaka kujua.”

5. Unaweza kufanya nini ikiwa zamani ulikuwa ukitumia sanamu aukuabudu mababu?6, 7. (a) Krismasi inasemekana kuwa ukumbusho wa nini, na je, wa-fuasi wa Kristo wa karne ya kwanza waliisherehekea? (b) Wakati wawanafunzi wa kwanza wa Yesu, sherehe za kuzaliwa zilihusianishwana nini?

156 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

7 Hata kama wanafunzi wa Yesu wangejua tarehe husu-sa ya kuzaliwa kwake, hawangeisherehekea. Kwa nini? Kwasababu, kama vile kitabu The World Book Encyclopediakinavyosema, Wakristo wa zamani “waliona kusherehekeasikukuu ya kuzaliwa kwa mtu yeyote kuwa desturi ya ki-pagani.” Sikukuu pekee za kuzaliwa zinazotajwa katika Bibliani zile za watawala wawili ambao hawakumwabudu Yehova.(Mwanzo 40:20; Marko 6:21) Pia, sikukuu za kuzaliwa zilishe-rehekewa ili kuheshimu miungu ya kipagani. Kwa mfano,mnamo Mei 24, Waroma walisherehekea kuzaliwa kwa mu-ngu wa kike aliyeitwa Diana. Siku iliyofuata, walisherehekeakuzaliwa kwa mungu-jua aliyeitwa Apollo. Hivyo, sherehe zakuzaliwa zilihusianishwa na upagani wala si Ukristo.

8 Kuna sababu nyingine ambayo ingewafanya Wakristo wa-sisherehekee kuzaliwa kwa Yesu. Inaelekea wanafunzi wakewalijua kwamba sherehe za kuzaliwa zilihusiana na ushiriki-na.Kwa mfano, Wagirikina Waromawengiwa kale waliaminikwamba roho fulani ilikuwapo wakati wa kuzaliwa kwa kilamwanadamu na ilimlinda maisha yake yote. Kitabu The Loreof Birthdays kinasema kwamba, “roho hiyo ilikuwa na uhusi-ano wa kichawi pamoja na mungu ambaye siku ya kuzaliwakwake ililingana na siku ya kuzaliwa kwa mtu huyo.” Bilashaka, Yehova hawezi kufurahishwa na sherehe yoyote amba-yo inamhusianisha Yesu na ushirikina. (Isaya 65:11, 12) Basi,watu wengi walianzaje kusherehekea Krismasi?

KRISMASI ILIANZIA WAPI?9 Watu walitenga Desemba 25 kuwa siku ya kusherehe-

kea kuzaliwa kwa Yesu mamia ya miaka baada ya yeyekuishi duniani. Lakini Yesu hakuzaliwa siku hiyo, inaoneka-na alizaliwa mwezi wa Oktoba.� Basi, kwa nini Desemba 25

� Ona Nyongeza, ukurasa 221-222.

8. Kuna uhusiano gani kati ya sherehe za kuzaliwa na ushirikina?9. Desemba 25 ilichaguliwaje kuwa siku ya kusherehekea kuzaliwakwa Yesu?

Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli 157

ilichaguliwa? Inaelekea kwamba baadaye watu fulani walio-dai kuwa Wakristo “walitaka tarehe hiyo ipatane na shereheya kipagani ya Waroma ya ‘kuzaliwa kwa jua lisiloshindwa.’”(The New Encyclopædia Britannica) Wakati wa majira ya ba-ridi kali, jua lilipoonekana kuwa hafifu zaidi, wapaganiwalifanya sherehe ili kulifanya jua lirudi na kuwaletea jotona nuru. Walidhani kwamba jua lilianza kurudi Desemba 25.Katika jitihada za kuwafanya wapagani wawe Wakristo,viongozi wa kidini waliikubali sherehe hiyo na kujaribu kui-fanya ionekane kuwa ya “Kikristo.”�

10 Tangu zamani imejulikana kwamba Krismasi ilitokanana wapagani. Kwa kuwa ilitokana na chanzo kisichopata-na na Maandiko, Krismasi ilipigwa marufuku katikakarne ya 17 nchini Uingereza na piakatika koloni kadhaa za Amerika. Ye-yote ambaye hakwenda kazini sikuya Krismasi alitozwa faini. Hatahivyo, punde si punde, desturi hizoza kale zikarudi, na nyingine mpyazikaongezwa. Kwa mara nyinginetena Krismasi ikawa sikukuu kubwa,na hivyo ndivyo ilivyo leo hii katikanchi nyingi. Hata hivyo, kwa saba-bu Krismasi inahusianishwa na diniza uwongo, wale wanaotaka kumpe-ndeza Mungu hawaisherehekei wala

� Sherehe ya Saturnalia pia ilichangia ku-chaguliwa kwa Desemba 25. Sherehe hiyoinayomheshimu mungu wa kilimo wa Wa-roma ilifanywa Desemba 17 hadi 24. Kati-ka sherehe hiyo ya Saturnalia, watu waliku-la na kunywa, walijitumbuiza na kupeanazawadi.

10. Kwa nini watu fulani hawakusherehe-kea Krismasi nyakati zilizopita?

Je, unawezakula peremende

ambayoimeokotwa

katika mtaro?

158 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

hawasherehekei sikukuu nyingine yoyote iliyotokana na iba-da ya kipagani.�

JE, VYANZO VYA SIKUKUU NI MUHIMU?11 Watufulanihukubalikwamba sikukuukamavile Krisma-

si zilianzishwa na wapagani, hata hivyo, wanahisi kwamba sivibaya kuzisherehekea. Kwani, watu wengi wanaposherehe-kea sikukuu hizo hawafikirii ibada ya uwongo. Pia, pindi hizohuwezesha familia kuwa pamoja. Je, hivyo ndivyo unavyohi-si? Ikiwa ndivyo, huenda sababu inayokufanya uone ugumukuchukua msimamo upande wa ibada ya kweli ni upendowako kwa familia wala si kwa dini ya uwongo. Uwe na hakikakwamba Yehova aliyeanzisha familia anataka uwe na uhusi-ano mzuri na watu wako wa ukoo. (Waefeso 3:14, 15) Hatahivyo, unaweza kuimarisha vifungo hivyo kwa njia ambayoMungu anakubali. Mtume Paulo alisema hivi kuhusu jambolililomuhimu zaidi maishani mwetu: “Endeleeni kuhakikishalile linalokubalika kwa Bwana.”—Waefeso 5:10.

12 Huenda unahisi kwamba leo watu hawaadhimishi siku-kuu kwa sababu ya vyanzo vyake. Je, vyanzo vya sikukuu nimuhimu? Ndiyo! Kwa mfano: Tuseme umeona peremendekwenye mtaro. Je, utaiokota na kuila? Haiwezekani! Pereme-nde hiyoni chafu.Sawa na peremende hiyo, huenda sikukuuhizo zinaonekana kuwa zenye kuvutia, hata hivyo, zimeo-kotwa mahali pachafu. Ili kuchukua msimamo upande waibada ya kweli, tunapaswa kuwa na maoni kama ya nabiiIsaya, aliyewaambia hivi waabudu wa kweli: “Msiguse kituchochote kilicho najisi.”—Isaya 52:11.

� Unaweza kupata habari zaidi kuhusu maoni ya Wakristo wa kwe-li juu ya sikukuu nyingine zinazopendwa na watu wengi, katika Nyo-ngeza, ukurasa 222-223.

11. Kwa nini watu fulani husherehekea sikukuu, hata hivyo, ni ja-mbo gani lililo muhimu zaidi kwetu?12. Eleza ni kwa nini tunapaswa kuepuka desturi na sherehe zenyevyanzo visivyofaa.

Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli 159

TUMIA UTAMBUZIUNAPOSHUGHULIKA NA WENGINE

13 Magumu yanaweza kutokea unapoamua kutosherehe-kea sikukuu. Kwa mfano, huenda wafanyakazi wenzakowakataka kujua ni kwa nini husherehekei sikukuu fulanizinazofanywa kazini. Vipi ukipewa zawadi ya Krismasi? Je,ni vibaya kuikubali? Vipi ikiwa mwenzi wako wa ndoa anaimani tofauti? Unaweza kuhakikishaje kwamba watoto wakohawahisi kwambawamekosa kitu fulanikwa kutosherehekeasikukuu hizo?

14 Unahitaji utambuzi ili kushughulikia kila hali ina-yotokea. Mtu akikupa salamu za sikukuu, unaweza tukumshukuru kwa kukutakia heri. Lakini vipi ikiwa wewe hu-mwona au kufanya kazi na mtu huyo kila siku. Basi, huendaukaamua kumweleza mengi zaidi. Vyovyote vile, tumia bu-sara. Biblia inashauri: “Maneno yenu na yawe yenye neemasikuzote, yenye kukolezwa chumvi, ili mjue jinsi mnavyo-paswa kumjibu kila mtu.” (Wakolosai 4:6) Uwe mwangalifuusije ukawavunjia wengine heshima. Badala yake, waelezemsimamo wako kwa busara. Waeleze waziwazi kwamba ha-kuna ubaya wa kutoa au kupokea zawadi na kuwa nasherehe, hata hivyo ungependa kufanya mambo hayo waka-ti mwingine.

15 Vipi ikiwa mtu anataka kukupa zawadi? Inategemea halimbalimbali. Huenda mwenye kukupa zawadi akasema: “Na-jua kwamba husherehekei sikukuu. Hata hivyo, ningependakukupa zawadi hii.” Basi, huenda ukaamua kwamba kupo-kea zawadi hiyo si sawa na kushiriki katika sikukuu. Bilashaka, ikiwa mwenye kukupa zawadi hajui imani yako, una-weza kumtajia kwamba wewe husherehekei sikukuu hiyo.Hilo litamsaidia kuelewa ni kwa nini ingawa unakubali ku-pokea zawadi yake, hutampa zawadi yoyote. Kwa upande

13. Ni magumu gani yanayoweza kutokea usiposherehekea sikukuu?14, 15. Unaweza kufanya nini ukipewa salamu ya sikukuu au ikiwamtu anataka kukupa zawadi?

160 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

mwingine, huenda isifae kupokea zawadi ikiwa yule anaye-kupa zawadi hiyo anataka kuonyesha kwamba hushikamanina imani yako au kwamba unaweza kuvunja imani yako ilikupata vitu vya kimwili.

NAMNA GANI WASHIRIKI WA FAMILIA?16 Namnagani ikiwawashirikiwa familiawana imani tofau-

ti? Unapaswa kuwa na busara. Hakuna haja ya kubishania kiladesturiau sherehe ambayowatuwakowaukoowanaamua ku-sherehekea. Badala yake, heshimu maoni yao, kama vileungependa waheshimu maoni yako. (Mathayo 7:12) Epukamambo yoyote ambayo yangefanya uonekane kwamba una-sherehekea sikukuu. Lakini utumie busara katika mamboambayo hayahusiani moja kwa moja na sherehe za sikukuu.Bila shaka, sikuzote unapaswa kutenda kwa njia itakayokua-cha ukiwa na dhamiri njema.—1 Timotheo 1:18, 19.

17 Unaweza kufanya nini ili watoto wako wasihisi kwambawamekosa kitu fulani kwa sababu ya kutosherehekea si-kukuu isiyopatana na Maandiko? Inategemea sana mambounayofanya nyakati nyingine. Wazazi fulani hutenga nyaka-ti za kuwapa watoto wao zawadi. Mojawapo ya zawadi borazaidi ambazo unaweza kuwapa watoto wako ni kuwa pamo-ja nao na kuwaonyesha upendo.

UNGA MKONO IBADA YA KWELI18 Ili kumpendeza Mungu, lazima ukatae kushiriki iba-

da ya uwongo na kuchukua msimamo upande wa ibadaya kweli. Hilo linatia ndani nini? Biblia inasema hivi:“Acheni tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na mate-ndo mazuri, bila kuacha kukusanyika pamoja sisi wenyewe,

16. Unawezaje kutumia busara unaposhughulikia mambo yanayo-husiana na sikukuu?17. Unawezaje kuwasaidia watoto wako wasihisi kwamba wanakosakitu fulani wanapowaona wengine wakisherehekea sikukuu fulani?18. Kuhudhuria mikutano ya Kikristo kunawezaje kukusaidia kuchu-kua msimamo upande wa ibada ya kweli?

Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli 161

kama vile wengine walivyo na desturi, bali tutiane moyo,na kufanya hivyo zaidi kwa kadiri mnavyoona siku ile kuwainakaribia.” (Waebrania 10:24, 25) Mikutano ya Kikristo nipindi za furaha ambazo unaweza kumwabudu Mungu kwanjia anayokubali. (Zaburi 22:22; 122:1) Kwenye mikutanohiyo, kuna “ubadilishanaji wa kitia-moyo” kati ya Wakristowaaminifu.—Waroma 1:12.

19 Njia nyingine ya kuchukua msimamo upande wa iba-da ya kweli ni kuwaambia wengine mambo ambayo umejuabaada ya kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova.Kwa kweli, watu wengi ‘wanaugua na kulia’ kwa sababu yauovu unaotendeka ulimwenguni leo. (Ezekieli 9:4) Huendaunajua watu fulani wanaohisi hivyo. Unaweza kuzungumzanaokuhusu tumaini lako lawakatiujao linalotegemea Biblia.Unaposhirikiana na Wakristo wa kweli na kuzungumza nawengine kuhusu kweli nzuri za Biblia ambazo umejifunza,utaona kwamba tamaa yoyote ya kushiriki desturi za dini yauwongo ambayo huenda bado ikawa moyoni mwako itato-weka hatua kwa hatua. Uwe na hakika kwamba utakuwa nafuraha sana na utapata baraka nyingi ukichukua msimamoupande wa ibada ya kweli.—Malaki 3:10.

19. Kwa nini ni muhimu kuzungumza na wengine kuhusu mambouliyojifunza katika Biblia?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Ibada ya sanamu na ibada ya mababu hai-patani na ibada ya kweli.—Kutoka 20:4, 5;Kumbukumbu la Torati 18:10-12.

ˇ Haifai kushiriki katika sherehe zilizoanzi-shwa na wapagani.—Waefeso 5:10.

ˇ Wakristo wa kweli wanapaswa kutumia bu-sara wanapowaeleza wengine kuhusu imaniyao.—Wakolosai 4:6.

162 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Kuunga mkono ibada yakweli huleta furaha ya kweli

DUNIA ni ndogo sana inapolinganishwa na ulimwenguwote mzima. Kwa kweli, Yehova, “Mtengenezaji wa mbi-ngu na dunia,” anayaona mataifa ya wanadamu kuwakama tone dogo la maji katika ndoo. (Zaburi 115:15;Isaya 40:15) Hata hivyo, Biblia inasema: “Yehova yuko ka-ribu na wote wanaomwitia, wote wanaomwitia yeye katikaukweli. Atawatimizia wale wanaomwogopa tamaa yao,naye atakisikia kilio chao cha kuomba msaada.” (Zaburi145:18, 19) Hebu wazia! Muumba mweza-yote yuko kari-bu nasi naye atatusikiliza ‘tukimwitia yeye katika ukweli.’Tuna pendeleo lililoje la kumkaribia Mungu katika sala!

2 Hata hivyo, ikiwa tungependa Yehova asikilize salazetu, ni lazima tusali kulingana na mapenzi yake. Ha-tuwezi kufanya hivyo tusipojua mambo ambayo Bibliainafundisha kuhusu sala. Ni muhimu tujue yale ambayoMaandiko yanasema kuhusu hilo kwa sababu sala inatusa-idia kumkaribia Yehova.

KWA NINI TUSALI KWA YEHOVA?3 Sababu moja muhimu inayotufanya tusali kwa Ye-

1, 2. Kwa nini tunapaswa kuiona sala kuwa pendeleo kubwa, na kwanini ni muhimu tujue mambo ambayo Biblia inafundisha kuhususala?3. Taja sababu moja muhimu inayotufanya tusali kwa Yehova.

SURA YA KUMI NA SABA

Mkaribie Mungu Katika Sala

Kwa nini tunapaswa kusali kwa Mungu?

Ni lazima tufanye nini ili Mungu asikilize sala zetu?

Mungu hujibuje sala zetu?

hova ni kwamba anatuhimiza tufanye hivyo. Neno lakelinatutia moyo: “Msihangaike juu ya kitu chochote, balikatika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shu-krani maombi yenu na yajulishwe Mungu; na amani yaMungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mio-yo yenu na nguvu zenu za akili kwa njia ya Kristo Yesu.”(Wafilipi 4:6, 7) Kwa kweli, hatupaswi kupuuza uandali-zi huo wenye fadhili kutoka kwa Mtawala Mkuu waulimwengu!

4 Sababu nyingine ni kwamba tunaposali kwa ukawa-ida, uhusiano wetu na Yehova unaimarika. Marafiki wakweli hawawasiliani tu wanapohitaji kitu fulani. Bada-la yake, marafiki wazuri huhangaikiana, na urafiki waohuimarika wanapozungumza kwa uhuru kuhusu mao-ni yao, kueleza hisia zao, na mahangaiko yao. Kwa njiafulani, ndivyo uhusiano wetu pamoja na Yehova Mu-ngu ulivyo. Kitabu hiki kimekusaidia kujua mambomengi ambayo Biblia inafundisha kumhusu Yehova, utuwake, na makusudi yake. Umejua kwamba yeye ni

4. Kusali kwa ukawaida kunawezaje kuimarisha uhusiano wetu naYehova?

“Mtengenezaji wa mbinguna dunia” yuko tayarikusikiliza sala zetu

165

Mungu halisi. Sala hukuwezesha kumueleza Babayako wa mbinguni mawazo na hisia zako za moyoni.Unapofanya hivyo, unamkaribia zaidi Yehova.—Yakobo4:8.

TUNAPASWA KUTIMIZA MATAKWA GANI?5 Je, Yehova husikiliza sala zote? Fikiria yale aliyowaa-

mbia Waisraeli waasi katika siku za nabii Isaya: “Hatamjapotoa sala nyingi, mimi sisikilizi; mikono yenu imejaaumwagaji wa damu.” (Isaya 1:15) Kwa hiyo, matendo fu-lani yanaweza kumfanya Mungu asisikilize sala zetu. Basi,ili sala zetu zisikilizwe na Mungu, ni lazima tutimize ma-takwa fulani muhimu.

6 Takwa moja muhimu ni kuwa na imani. (Marko11:24) Mtume Paulo aliandika: “Bila imani haiwezeka-ni kamwe kumpendeza [Mungu] vema, kwa maana yuleanayemkaribia Mungu lazima aamini kwamba yeye yukona kwamba yeye huwa mthawabishaji wa wale wanao-mtafuta kwa bidii.” (Waebrania 11:6) Mbali na kuaminikwamba kuna Mungu anayesikiliza na kujibu sala, me-ngi yanahitajiwa ili kuwa na imani ya kweli. Imanihuthibitika kwa matendo yetu. Maisha yetu ya kila sikuyanapaswa kuthibitisha kwamba tuna imani.—Yakobo2:26.

7 Pia Yehova anataka wale wanaosali, wafanye hivyokwa unyenyekevu na unyoofu. Tuna kila sababu ya kuwawanyenyekevu tunapozungumza na Yehova, sivyo? Kwakawaida, watu huzungumza na mfalme au rais, kwa he-

5. Ni nini kinachoonyesha kwamba Yehova hasikilizi sala zote?6. Ili Mungu asikilize sala zetu, tunapaswa kutimiza takwa gani mu-himu, na tunawezaje kufanya hivyo?7. (a) Kwa nini tunapaswa kuonyesha heshima tunapozungumza naYehova katika sala? (b) Tunawezaje kuonyesha unyenyekevu na unyo-ofu tunaposali kwa Mungu?

166 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

shima, wakitambua cheo chake cha juu. Basi, tunapaswakumheshimu Yehova hata zaidi tunapozungumza naye.(Zaburi 138:6) Kwa kweli, yeye ni “Mungu Mweza-Yote.”(Mwanzo 17:1) Tunaposali kwa Mungu, tunapaswa ku-mfikia kwa njia inayoonyesha kwamba tunatambua kwaunyenyekevu hali yetu mbele zake. Unyenyekevu huo uta-tuchochea kusali kwa unyoofu kutoka moyoni mwetu,na kuepuka sala za kidesturi au za kurudia-rudia.—Matha-yo 6:7, 8.

8 Ikiwa tunataka Mungu atusikilize, tunapaswa kutendakulingana na sala zetu. Yehova anatarajia tujitahidi kadiriya uwezo wetu kutenda kulingana na sala zetu. Kwa mfa-no, tukisali “Utupe leo mkate wetu kwa ajili ya sikuhii,” ni lazima tufanye kwa bidii kazi yoyote tunayowe-za kufanya. (Mathayo 6:11; 2 Wathesalonike 3:10) Tukisaliatusaidie kushinda udhaifu fulani wa kimwili, ni lazimatuwe waangalifu na kuepuka mambo au hali zinazowe-za kututia majaribuni. (Wakolosai 3:5) Mbali na matakwahayo muhimu, kuna maswali kuhusu sala ambayotungependa kujibiwa.

KUJIBU MASWALI FULANI KUHUSU SALA9 Tunapaswa kusali kwa nani? Yesu aliwafundisha wafu-

asi wake wasali kwa ‘Baba yetu aliye mbinguni.’ (Mathayo6:9) Hivyo, sala zetu zinapaswa kuelekezwa kwa YehovaMungu peke yake. Hata hivyo, Yehova anataka tuta-mbue cheo cha Mwana wake mzaliwa wa pekee, YesuKristo. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 5, Yesu alitu-mwa duniani ili awe fidia na kutukomboa kutokakatika dhambi na kifo. (Yohana 3:16; Waroma 5:12) Yeyendiye Kuhani Mkuu na Hakimu aliyewekwa rasmi.

8. Tunawezaje kutenda kulingana na sala zetu?9. Tunapaswa kusali kwa nani, na kupitia nani?

Mkaribie Mungu Katika Sala 167

(Yohana 5:22; Waebrania 6:20) Hivyo, Maandiko yanatua-giza tutoe sala zetu kupitia Yesu. Yeye mwenyewe alisema:“Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna anayekujakwa Baba ila kupitia kwangu.” (Yohana 14:6) Ili salazetu zisikiwe, ni lazima tusali kwa Yehova tu kupitia Mwa-naye.

10 Je, ni lazima tuwe katika hali fulani hususa tuna-posali? Hapana. Yehova hahitaji tufanye jambo fulanihususa tunaposali. Biblia inafundisha kwamba tuna-weza kusali tukiwa katika hali mbalimbali. Tunawezakusali tukiwa tumeketi, tumeinama, tumepiga magoti,na tukiwa tumesimama. (1 Mambo ya Nyakati 17:16;Nehemia 8:6; Danieli 6:10; Marko 11:25) Jambo muhi-mu si kukaa katika hali fulani hususa ili tuonwe nawengine, bali ni kuwa na mwelekeo unaofaa. Isitoshe,tunapokuwa katika shughuli zetu za kila siku au tunapo-kabili hali ya dharura, tunaweza kusali kimyakimyapopote tulipo. Yehova husikiliza sala kama hizo hataingawa hazisikiwi na watu walio karibu nasi.—Nehemia2:1-6.

11 Tunaweza kusali kuhusu nini? Biblia inaeleza: “Hatatukiomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye [Yeho-va] hutusikia.” (1 Yohana 5:14) Basi tunaweza kuombachochote kulingana na mapenzi ya Mungu. Je, ni ma-penzi yake tusali kuhusu mahangaiko yetu? Ndiyo,bila shaka! Kusali kwa Yehova ni kama kuongea narafiki wa karibu. Tunaweza kuongea waziwazi, ‘tukimi-mina moyo wetu’ mbele za Mungu. (Zaburi 62:8)Tunapaswa kuomba roho takatifu, kwa sababu itatusai-dia kufanya mambo yanayofaa. (Luka 11:13) Tunawezapia kuomba mwongozo wa kufanya maamuzi ya heki-

10. Kwa nini hatuhitaji kuwa katika hali fulani hususa tunaposali?11. Ni mahangaiko gani ya kibinafsi tunayoweza kusali juu yake?

168 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

ma na nguvu za kukabiliana na magumu. (Yakobo1:5) Tunapofanya dhambi, tunapaswa kuomba msama-ha kwa msingi wa dhabihu ya Kristo. (Waefeso 1:3, 7)Lakini hatupaswi kusali tu kuhusu mambo ya kibinafsi.Tunapaswa kusali kwa niaba ya watu wengine kama vilefamilia yetu na pia waabudu wenzetu.—Matendo 12:5;Wakolosai 4:12.

12 Katika sala zetu, tunapaswa kutanguliza mambo ya-nayomhusu Yehova Mungu. Bila shaka tuna kila sababuya kumsifu na kumshukuru kutoka moyoni kwa sababuya wema wake wote. (1 Mambo ya Nyakati 29:10-13) Ka-tika sala ya kielelezo iliyo kwenye Mathayo 6:9-13,Yesu alitufundisha tusali jina la Mungu litakaswe, yaani,lionwe kuwa takatifu. Kisha tusali Ufalme wa Mungu ujena mapenzi yake yatendeke duniani kama ilivyo mbi-nguni. Baada ya kuzungumzia mambo hayo muhimukumhusu Yehova ndipo Yesu alipotaja mambo ya kibi-nafsi. Sisi pia tunapomtanguliza Mungu katika sala zetu,tunaonyesha kwamba hatuhangaikii tu mambo yetu we-nyewe.

13 Sala zetu zinapaswa kuwa na urefu gani? Bibliahaisemi sala zinazotolewa faraghani au hadharani zina-paswa kuwa na urefu gani. Tunaweza kutoa sala fupikabla ya kula au sala ndefu faraghani tunapomwele-za Yehova mambo yaliyo moyoni mwetu. (1 Samweli 1:12, 15) Hata hivyo, Yesu aliwashutumu watu waliojionakuwa waadilifu ambao walitoa sala ndefu ili waonekanena watu. (Luka 20:46, 47) Sala za aina hiyo hazimpe-ndezi Yehova. Jambo muhimu ni kusali kutoka moyoni.Hivyo, sala zinazokubalika zinaweza kuwa na urefu mba-limbali ikitegemea hali na mahitaji.

12. Tunawezaje kumtanguliza Baba yetu wa mbinguni katika salazetu?13. Maandiko yanasema nini kuhusu urefu wa sala zinazokubalika?

Mkaribie Mungu Katika Sala 169

14 Tunapaswa kusali mara ngapi? Biblia inatutia moyo‘tusali sikuzote,’ ‘tudumu katika sala,’ na ‘tusali bila ku-acha.’ (Mathayo 26:41; Waroma 12:12; 1 Wathesalonike5:17) Bila shaka, maandiko hayo hayamaanishi kwambatunapaswa kusali kwa Yehova kila dakika. Badala yake, Bib-lia inatuhimiza tusali kwa ukawaida na kumshukuruYehova daima kwa sababu ya wema wake kwetu na ku-mwomba atuongoze, atufariji, na kutuimarisha. Je, haitiimoyo kujua kwamba Yehova haweki mipaka kuhusu ure-fu au mara ambazo tunaweza kuzungumza naye katikasala? Ikiwa tunathamini kikweli pendeleo la sala, tutapatanafasi nyingi za kusali kwa Baba yetu wa mbinguni.

15 Kwa nini tunapaswa kusema “Amina” mwishoni mwasala? Neno “amina” humaanisha “bila shaka,” au “iwehivyo.” Mifano ya kimaandiko inaonyesha kwamba tuna-paswa kusema “Amina” mwishoni mwa sala za kibinafsina za hadharani. (1 Mambo ya Nyakati 16:36; Zaburi41:13) Tunaposema “Amina” mwishoni mwa sala zetu,tunaonyesha kwamba maneno yetu yanatoka moyoni. Tu-naposema “Amina” kimyakimya au kwa sauti baada yamtu fulani kutoa sala hadharani, tunaonyesha kwambatunakubaliana na sala hiyo.—1 Wakorintho 14:16.

JINSI MUNGU ANAVYOJIBU SALA ZETU16 Je, kweli Yehova hujibu sala? Bila shaka! Tuna saba-

bu thabiti ya kuamini kwamba “Msikiaji wa sala” hujibusala zinazotolewa na mamilioni ya wanadamu wanyo-ofu. (Zaburi 65:2) Yehova anaweza kujibu sala zetu kwanjia mbalimbali.

14. Biblia inamaanisha nini inapotuhimiza ‘tusali sikuzote,’ na kwanini hilo linatufariji?15. Kwa nini tunapaswa kusema “Amina” mwishoni mwa sala za ki-binafsi na za hadharani?16. Tunaweza kuwa na uhakika gani kuhusu sala zetu?

170 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

17 Yehova hutumia malaika wake na watumishi wakeduniani kujibu sala. (Waebrania 1:13, 14) Kuna watu we-ngi ambao walisali kwa Mungu ili wapate msaada wakuielewa Biblia na muda si muda wakatembelewa nammoja wa watumishi wa Yehova. Mambo kama hayo ya-naonyesha kwamba malaika wanaongoza kazi ya kuhubirijuu ya Ufalme. (Ufunuo 14:6) Yehova anaweza ku-mchochea Mkristo mwenzetu atusaidie tunaposali wakati

17. Kwa nini tunaweza kusema kwamba Mungu hutumia malaika nawatumishi wake duniani kujibu sala zetu?

Mungu anaweza kusikiasala zako wakati wowote

Mkaribie Mungu Katika Sala 171

wa uhitaji mkubwa.—Me-thali 12:25; Yakobo 2:16.

18 Yehova Mungu piahutumia roho yake taka-tifu na Neno lake, Biblia,kujibu sala za watumishiwake. Tunapoomba msa-ada wa kukabiliana namajaribu, anaweza kutu-jibu kwa kutuongoza nakutuimarisha kwa rohoyake takatifu. (2 Wakori-ntho 4:7) Mara nyingi Biblia hujibu sala zetu za kuombamwongozo. Yehova hutusaidia kufanya maamuzi ya he-kima kupitia Biblia. Tunapojifunza Biblia kibinafsi natunaposoma vichapo vya Kikristo kama kitabu hiki,tunaweza kupata maandiko yanayoweza kutusaidia. Tu-naweza kukumbushwa habari za kimaandiko kwenyemikutano ya Kikristo au na mzee wa kutaniko anayetu-hangaikia.—Wagalatia 6:1.

19 Tukihisi kwamba Yehova anachelewa kujibu salazetu, haimaanishi kwamba hawezi kujibu. Badala yake,tunapaswa kukumbuka kwamba Yehova hujibu sala kupa-tana na mapenzi yake na kwa wakati wake. Anajuamahitaji yetu na jinsi ya kuyatimiza kuliko tuwezavyo.Mara nyingi yeye huturuhusu ‘tuendelee kuomba, ku-tafuta, na kupiga hodi.’ (Luka 11:5-10) Tunapoendelea

18. Yehova hutumiaje roho yake takatifu na Neno lake kujibu sala zawatumishi wake?19. Tunapaswa kukumbuka nini tunapohisi kwamba sala zetu hazi-jibiwi nyakati nyingine?

Yehova anaweza kujibu salazetu kwa kumchochea Mkristomwenzetu atusaidie

kufanya hivyo, tunamwonyesha Mu-ngu kwamba tunatamani sana jambotunaloomba na tuna imani ya kweli. Isi-toshe, Yehova anaweza kujibu sala zetukwa njia isiyo ya moja kwa moja. Kwamfano, anaweza kujibu sala yetu kuhu-siana na jaribu fulani kwa kutupa nguvuza kuvumilia badala ya kuliondoa jaribuhilo.—Wafilipi 4:13.

20 Tunapaswa kushukuru kwambaMuumba wa ulimwengu huu mkubwayuko karibu na wote wanaomwitia kwanjia inayofaa katika sala. (Zaburi 145:18)Na tutumie kikamili pendeleo lenyethamani la sala. Tukifanya hivyo, tuta-

pata shangwe ya kumkaribia zaidi Yehova, ambaye niMsikiaji wa sala.

20. Kwa nini tunapaswa kutumia kikamili pendeleo lenye thamanila sala?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Kusali kwa ukawaida kwa Yehova hutusaidiakumkaribia.—Yakobo 4:8.

ˇ Ili sala zetu zisikiwe na Mungu, ni lazimatusali kwa imani, unyenyekevu na unyoofu.—Marko 11:24.

ˇ Tunapaswa kusali kwa Yehova tu kupitiaMwana wake.—Mathayo 6:9; Yohana 14:6.

ˇ Yehova, “Msikiaji wa sala,” hutumia malaikawake, watumishi wake duniani, roho yake ta-katifu, na Neno lake kujibu sala zetu.—Zaburi 65:2.

173

“TAZAMA! Maji; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?” Swalihilo liliulizwa katika karne ya kwanza na ofisa Mwethio-pia wa makao ya kifalme. Mkristo aliyeitwa Filipo,alikuwa amemthibitishia kwamba Yesu alikuwa Masihialiyeahidiwa. Akiwa amechochewa

1. Kwa nini ofisa Mwethiopia wamakao ya kifalme alitaka kubati-zwa?

SURA YA KUMI NA NANE

Ubatizo na Uhusiano WakoPamoja na Mungu

Ubatizo wa Kikristo hufanywaje?

Unapaswa kuchukua hatua zipi iliustahili kubatizwa?

Mtu hujiwekaje wakfu kwa Mungu?

Ni sababu gani ya pekeeinayomfanya mtu abatizwe?

na yale aliyokuwa amejifunza katika Maandiko, Mwethi-opia huyo alichukua hatua. Alionyesha kwamba anatakakubatizwa!—Matendo 8:26-36.

2 Ikiwa umejifunza kwa makini sura za kwanza za kitabuhiki na mmojawa Mashahidi wa Yehova, huenda ukauliza,‘Ni nini kinachonizuia nisibatizwe?’ Kufikia sasa umeji-funza kuhusu ahadi ya Biblia ya uzima wa milele katikaParadiso. (Luka 23:43; Ufunuo 21:3, 4) Pia umejifunzaukweli kuhusu hali ya wafu na tumaini la ufufuo. (Mhu-biri 9:5; Yohana 5:28, 29) Huenda umekuwa ukihudhuriamikutano ya Mashahidi wa Yehova na umejionea upendowalio nao ambao hutambulisha ibada ya kweli. (Yohana13:35) Zaidi ya yote, huenda umeanza kusitawisha uhusia-no wa karibu pamoja na Yehova Mungu.

3 Unawezaje kuonyesha kwamba unataka kumtumikiaMungu? Yesu aliwaambia hivi wafuasi wake: “Nendenimkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,mkiwabatiza.” (Mathayo 28:19) Yesu mwenyewe alituwe-kea kielelezo alipobatizwa katika maji. Hakunyunyiziwawala kumwagiliwa maji kidogo kichwani. (Mathayo3:16) Neno “batiza” linatokana na neno la Kigiriki li-nalomaanisha “zamisha.” Kwa hiyo, ubatizo wa Kikristounamaanisha kuzamisha, au kutumbukiza kabisa ndani yamaji.

4 Kila mtu anayetaka kuwa na uhusiano pamoja naYehova Mungu anapaswa kubatizwa katika maji. Ubati-zo huonyesha waziwazi kwamba unataka kumtumikiaMungu. Pia unaonyesha kwamba unatamani kufanya ma-penzi ya Yehova. (Zaburi 40:7, 8) Hata hivyo, ili ustahilikubatizwa, ni lazima uchukue hatua fulani.

2. Kwa nini unapaswa kufikiria kwa uzito kuhusu ubatizo?3. (a) Yesu aliwapa wafuasi wake amri gani? (b) Ubatizo wa maji hu-fanywaje?4. Ubatizo wa maji huonyesha nini?

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu 175

UNAHITAJI IMANI NA UJUZI5 Tayari umeanza kuchukua hatua ya kwanza. Jinsi

gani? Labda kwa kujifunza Biblia hatua kwa hatua na kue-ndelea kupata ujuzi kumhusu Yehova Mungu na YesuKristo. (Yohana 17:3) Hata hivyo, kuna mengi ya kujifu-nza. Wakristo wanataka ‘wajazwe ujuzi sahihi wa mapenziyake [Mungu].’ (Wakolosai 1:9) Kuhudhuria mikutano yaMashahidi wa Yehova kutakusaidia kufanya hivyo. Ni mu-himu kuhudhuria mikutano hiyo. (Waebrania 10:24, 25)Kuhudhuria mikutano kwa ukawaida kutakusaidia kuo-ngeza ujuzi juu ya Mungu.

6 Ni kweli kwamba si lazima ujue kila jambo katika Bib-lia ndipo ustahili kubatizwa. Yule ofisa Mwethiopia wamakao ya kifalme alikuwa na kiasi fulani cha ujuzi,hata hivyo, alihitaji kusaidiwa ili kuelewa sehemu fulaniza Maandiko. (Matendo 8:30, 31) Vivyo hivyo, wewe piaunahitaji kujifunza mengi zaidi. Kwa kweli, hutafikia mwi-sho wa kujifunza kumhusu Mungu. (Mhubiri 3:11) Hatahivyo, kabla ya kubatizwa, unahitaji kujua na kukubalimafundisho ya msingi ya Biblia. (Waebrania 5:12) Mafu-ndisho hayo yanatia ndani kweli kuhusu hali ya wafu naumuhimu wa jina la Mungu na Ufalme wake.

7 Ujuzi peke yake hautoshi kwa maana “bila imanihaiwezekani kamwe kumpendeza [Mungu] vema.” (Wae-brania 11:6) Biblia inatuambia kwamba watu fulani wa jijila kale la Korintho waliposikia ujumbe wa Kikristo ‘walia-nza kuamini na kubatizwa.’ (Matendo 18:8) Vivyo hivyo,kadiri unavyozidi kujifunza Biblia, ndivyo unavyopaswakuwa na imani zaidi kwamba hiyo ni Neno la Mungu lililo-

5. (a) Kabla ya kubatizwa, mtu anapaswa kuchukua hatua gani kwa-nza? (b) Kwa nini mikutano ya Kikristo ni muhimu?6. Mtu anapaswa kuwa na ujuzi wa Biblia kiasi gani ili astahili kuba-tizwa?7. Kujifunza Biblia kunapaswa kuwa na matokeo gani kwako?

176 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

ongozwa na roho. Kujifunza Biblia kunapaswa kukusaidiakuwa na imani katika ahadi za Mungu, na kuamini kwa-mba dhabihu ya Yesu inaweza kukuokoa.—Yoshua 23:14;Matendo 4:12; 2 Timotheo 3:16, 17.

KUZUNGUMZA NA WENGINEKUHUSU KWELI ZA BIBLIA

8 Kadiri unavyozidi kuwa na imani, ndivyo utakavyoo-na ikiwa rahisi kuzungumza na wengine mambo ambayoumejifunza. (Yeremia 20:9) Utachochewa sana kuzungu-mza na wengine kuhusu Mungu na makusudi yake.—2 Wakorintho 4:13.

9 Unaweza kuanza kuzungumza na wengine kuhusukweli za Biblia kwa kuanzisha mazungumzo kwa busarapamoja na watu wa ukoo, marafiki, majirani, na wafanya-kazi wenzako. Baada ya muda, huenda ukataka kuhubirirasmi pamoja na Mashahidi wa Yehova. Ukifikia hatuahiyo, mjulishe Shahidi anayekufundisha Biblia. Ikiwa una-stahili kuwa mhubiri, mipango itafanywa ili wewe namwalimu wako mwe na mazungumzo pamoja na wazeewawili wa kutaniko.

10 Kufanya hivyo kutakuwezesha kuwafahamu wa-zee Wakristo wanaolichunga kundi la Mungu. (Matendo20:28; 1 Petro 5:2, 3) Wazee hao wakiona kwamba unaele-wa na kuamini mafundisho ya msingi ya Biblia, unaishikupatana na kanuni za Mungu na kwa kweli unataka kuwammoja wa Mashahidi wa Yehova, watakujulisha kwambaunastahili kushiriki katika huduma ukiwa mhubiri amba-ye hajabatizwa wa habari njema.

8. Ni nini kitakachokuchochea kuzungumza na wengine mamboambayo umejifunza?9, 10. (a) Unaweza kuanza kuwahubiria nani kweli ya Biblia?(b) Unapaswa kufanya nini ikiwa unataka kushiriki katika kazi ya ku-hubiri pamoja na Mashahidi wa Yehova?

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu 177

11 Kwa upande mwingine, huenda ukahitaji kurekebi-sha maisha na mazoea yako ili ustahili kuwa mhubiri.Hilo linaweza kutia ndani kuacha mazoea fulani mabaya.Kwa hiyo, kabla ya kuomba kuwa mhubiri ambaye haja-batizwa, unahitaji kuacha kabisa dhambi nzito kama vileukosefu wa adili katika ngono, ulevi, na kutumia dawa zakulevya.—1 Wakorintho 6:9, 10; Wagalatia 5:19-21.

KUTUBU NA KUGEUKA12 Kuna hatua nyingine zinazotangulia ubatizo. Mtume

Petro alisema: “Tubuni na mgeuke ili dhambi zenu zipa-te kufutwa.” (Matendo 3:19) Kutubu ni kusikitika kikwelikwa sababu ya jambo ulilofanya. Mtu anapaswa kutubuikiwa aliishi maisha yasiyo ya adili na hata yule amba-ye amekuwa akiishi maisha safi kiadili anapaswakufanya hivyo pia. Kwa nini? Kwa sababu wanadamuwote ni watenda dhambi na wanahitaji msamaha waMungu. (Waroma 3:23; 5:12) Kabla ya kujifunza Bib-lia, hukujua mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo hungewezakuishi kulingana na mapenzi yake. Basi, unapaswa ku-tubu.

13 Baada ya kutubu, lazima ‘ugeuke.’ Haitoshi tu ku-sikitika. Unahitaji kukataa maisha yako ya zamani nakuazimia kabisa kufanyayaliyo mema kuanzia sasa na ku-endelea. Ni lazima utubu na kugeuka kabla ya kubatizwa.

KUJIWEKA WAKFU14 Kuna hatua nyingine muhimu inayopaswa kuchu-

kuliwa kabla ya ubatizo. Ni lazima ujiweke wakfu kwaYehova Mungu.

11. Huenda watu fulani wakahitaji kufanya marekebisho gani ili wa-stahili kuwa wahubiri?12. Kwa nini mtu anapaswa kutubu?13. Kugeuka kunamaanisha nini?14. Kabla ya kubatizwa, unahitaji kuchukua hatua gani muhimu?

178 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

15 Unapojiweka wakfu kwa Yehova Mungu katika salainayotoka moyoni, unamwahidi kwamba umejitoa kwa-ke peke yake kwa umilele wote. (Kumbukumbu la Torati6:15) Hata hivyo, kwa nini ujitoe kwake? Tuseme kwambamwanamume ameanza kumchumbia mwanamke. Kadirianavyozidi kuona sifa zake nzuri ndivyo anavyozidi kuvu-tiwa naye. Kwa kawaida, baada ya muda atamwombawafunge ndoa. Ni kweli kwamba kufunga ndoa kutamwo-ngezea majukumu. Hata hivyo, upendo utamchocheakuchukua hatua hiyo muhimu.

16 Baada ya kumjua na kumpenda Yehova, utachochewakumtumikia bila kusita wala masharti yoyote kuhusianana ibada. Yeyote anayetaka kumfuata Mwana wa Mungu,Yesu Kristo, lazima “ajikane mwenyewe.” (Marko 8:34) Tu-najikana wenyewe kwa kuhakikisha kwamba mapendezina miradi yetu binafsi haituzuii kumtii Mungu kikamili.Basi, kabla ya kubatizwa, ni lazima jambo kuu maishanimwako liwe kufanya mapenzi ya Yehova Mungu.—1 Petro4:2.

KUTOOGOPA KUSHINDWA17 Watu fulani husita kujiweka wakfu kwa Yehova kwa

sababu wanaogopa kuchukua hatua hiyo muhimu. Hu-enda wakaogopa kuwajibika mbele za Mungu wakiwaWakristo waliojiweka wakfu. Kwa kuwa wanaogopa ku-mkosea na kumkasirisha Yehova, wanaona ni afadhaliwasijiweke wakfu kwake.

18 Unapoendelea kujifunza kumpenda Yehova, uta-chochewa kujiweka wakfu kwake na kujitahidi kuishi

15, 16. Kujiweka wakfu kwa Mungu kunamaanisha nini, na ni ninihumchochea mtu kufanya hivyo?17. Kwa nini huenda watu fulani wakasita kujiweka wakfu kwa Mu-ngu?18. Ni nini kinachoweza kukuchochea ujiweke wakfu kwa Yehova?

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu 179

kulingana na wakfu huo.(Mhubiri 5:4) Baada ya ku-jiweka wakfu, bila shaka utajitahidi ‘kutembea kwakumstahili Yehova kwa kusudi la kumpendeza yeye.’(Wakolosai 1:10) Kwa sababu unampenda Mungu, haita-kuwa vigumu kwako kufanya mapenzi yake. Bila shakautakubaliana na mtume Yohana, aliyeandika: “KumpendaMungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake;na bado amri zake si mzigo mzito.”—1 Yohana 5:3.

19 Haimaanishi kwamba unahitaji kuwa mkamilifu iliujiweke wakfu kwa Mungu. Yehova anajua uwezo wakonaye hatarajii kamwe ufanye mambo usiyoweza. (Zaburi

19. Kwa nini hupaswi kuogopa kujiweka wakfu kwa Yehova?

Kupata ujuzi sahihi kuhusu Neno laMungu ni hatua muhimu ambayo

mtu anapaswa kuchukua iliastahili kubatizwa

Imani inapaswa kukuchocheauzungumze na wengine kuhusu

mambo ambayo umejifunza

103:14) Anataka ufanikiwe naye atakutegemeza na kukusa-idia. (Isaya 41:10) Bila shaka, ukimtumaini Yehova kabisa,“atanyoosha mapito yako.”—Methali 3:5, 6.

KUONYESHA WAKFU KWA KUBATIZWA20 Kufikiria kwa uzito mambo ambayo tumezungumzia

kwaweza kukusaidia kuamua kujiweka wakfu kwa Yehovakatika sala. Kila mtu anayempenda Mungu kikweli lazima

20. Kwa nini mtu anapaswa kuonyesha hadharani kwamba amejiwe-ka wakfu kwa Yehova?

Je, umejiweka wakfukwa Mungu katika sala? Ubatizo humaanisha

kufa, au kuacha maishaya zamani, na kuanza

maisha mapya ya kufanyamapenzi ya Mungu

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu 181

pia ‘afanye tangazo la hadharani kwa ajili yawokovu.’ (Wa-roma 10:10) Mtu hufanyaje tangazo hilo?

21 Mjulishe mratibu wa baraza la wazee la kutaniko lenukwamba ungependa kubatizwa. Atapanga wazee fulani wa-pitie nawe maswali kadhaa yanayohusu mafundisho yamsingi ya Biblia. Wazee hao wakiona kwamba unastahili,watakujulisha kwamba utabatizwa katika kusanyiko lina-lofuata.�Kwakawaidahotuba inayoelezamaanaya ubatizohutolewa katika makusanyiko hayo. Kisha msemaji hu-waomba wote watakaobatizwa wajibu maswali mawilirahisi ikiwa njia moja ya kutoa “tangazo la hadharani” laimani yao.

22 Ubatizo ndio unaoonyesha hadharani kwamba ume-jiweka wakfu kwa Mungu na sasa wewe ni mmoja waMashahidi wa Yehova. Wanaobatizwa huzamishwa kabisamajini ili kuonyesha hadharani kwambawamejiweka wak-fu kwa Yehova.

MAANA YA UBATIZO WAKO23 Yesu alisema kwamba wanafunzi wake wangeba-

tizwa “katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu.”(Mathayo 28:19) Hilo linamaanisha kwamba anayetakakubatizwa anatambua mamlakaya Yehova Mungu na YesuKristo. (Zaburi 83:18; Mathayo 28:18) Pia anatambua kazina utendaji wa roho takatifu au nguvu ya utendaji ya Mu-ngu.—Wagalatia 5:22, 23; 2 Petro 1:21.

24 Hata hivyo, ubatizo si kutumbukizwa majini tu. Una-

� Ubatizo hufanywa kwa ukawaida katika makusanyiko ya Masha-hidi wa Yehova ya kila mwaka.

21, 22. Unawezaje kutoa “tangazo la hadharani” la imani yako?23. Inamaanisha nini kubatizwa “katika jina la Baba na la Mwanana la roho takatifu”?24, 25. (a) Ubatizo huonyesha nini? (b) Ni swali gani linalohitajikujibiwa?

182 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

wakilisha jambo fulani muhimu sana. Kuzamishwa maji-ni huonyesha kwamba umekufa, au umeacha maishayakoya zamani. Na kuibuka kutoka majini huonyesha kwambasasa umeanza maisha mapya ya kufanya mapenzi ya Mu-ngu. Kumbuka pia kwamba umejiweka wakfu kwa YehovaMungu mwenyewe wala si kwa kazi fulani, mradi fulani,mtu fulani, au tengenezo fulani. Kujiweka wakfu na kuba-tizwa ni mwanzo wa kuwa na uhusiano wa karibu sana naMungu.—Zaburi 25:14.

25 Ubatizo haukuhakikishii wokovu. Mtume Paulo alia-ndika: “Endeleeni kuufanyia kazi wokovu wenu wenyewekwa kuogopa na kutetemeka.” (Wafilipi 2:12) Ubatizo nimwanzotu.Kwahiyobasi,Unawezajekukaakatikaupendowa Mungu? Sura ya mwisho ya kitabu hiki itajibu swalihilo.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Mkristo hubatizwa kwa kuzamishwa kabisamajini wala si kunyunyiziwa maji.—Mathayo3:16.

ˇ Hatua zinazoongoza kwenye ubatizo huanzakwa kupata ujuzi, kisha kuwa na imani, ha-lafu kutubu, mwishowe kugeuka nakujiweka wakfu kwa Mungu.—Yohana 17:3;Matendo 3:19; 18:8.

ˇ Ili kujiweka wakfu kwa Yehova, lazima uji-kane mwenyewe kama watu walivyojikanawenyewe ili kumfuata Yesu.—Marko 8:34.

ˇ Ubatizo huonyesha kwamba umekufa, auumeacha maisha yako ya zamani, na umea-nza maisha mapya ya kufanya mapenzi yaMungu.—1 Petro 4:2.

Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu 183

WAZIA kwamba unatembea barabarani sikuyenye dhoruba kali. Mawingu yanazidi ku-tanda. Radi inapiga na ngurumo zinasikika,kisha mvua kubwa inanyesha. Unakimbiahuku na huku ukitafuta mahali pa kujikinga.Halafu, ng’ambo ya barabara unaona maha-li pa kujikinga. Ni mahali imara, pakavu, napenye kuvutia. Unafurahi kama nini kupao-na mahali hapo!

2 Tunaishi katika nyakati zenye msukosu-ko.Hali za ulimwengu zinaendelea kuzorota.Hata hivyo, kuna mahali salama, kimbiliolinaloweza kutukinga. Ni wapi tunapowe-za kupata kimbilio hilo? Biblia inafundishahivi: “Nitamwambia Yehova: ‘Wewe ni ki-mbilio langu na ngome yangu, Munguwangu, ambaye nitamtegemea.’”—Zaburi91:2.

3 Hebu wazia! Yehova, Muumba anayeu-tawala ulimwengu mzima, anaweza kuwakimbilio letu. Anaweza kutulinda kwa kuwa

1, 2. Tunaweza kupata wapi kimbilio salama leo?3. Tunawezaje kumfanya Yehova kuwa kimbilioletu?

SURA YA KUMI NA TISA

Kaa Katika Upendo wa Mungu

Kumpenda Mungu kunamaanisha nini?

Tunawezaje kukaa katika upendo wa Mungu?

Yehova atawathawabishaje wale wanaokaakatika upendo wake?

Je, utamfanyaYehova awe

kimbilio lakokatika nyakati

hizi zenyemsukosuko?

yeye ana nguvu nyingi kuliko yeyote au chochote ki-nachoweza kutuumiza. Hata tukiumizwa, Yehova anawezakuondoa madhara yote mabaya. Tunawezaje kumfanya Ye-hova kuwa kimbilio letu? Tunahitaji kumtumaini. Isitoshe,Neno la Mungu linatusihi: “Jitunzeni katika upendo waMungu.” (Yuda 21) Ndiyo, tunahitaji kukaa katika upendowa Mungu kwa kudumisha kifungo cha upendo pamoja naBaba yetu wa mbinguni. Ndipo tunapoweza kuwa na hakikakwamba yeye ni kimbilio letu. Tunawezaje kudumisha kifu-ngo hicho?

ZINGATIA UPENDO WA MUNGUNA KUTENDA KUPATANA NAO

4 Ili tuendelee kukaa katika upendo wa Mungu, tunapa-swa kutambua jinsi Yehova ametuonyesha upendo wake.Fikiria baadhi ya mafundisho ya Biblia ambayo umejifu-nza katika kitabu hiki. Akiwa Muumba, Yehova ametupatiadunia iwe makao yetu yenye kupendeza. Ameijaza chakulana maji mengi, mali za asili, wanyama wenye kuvutia, namandhari maridadi. Akiwa Mtungaji wa Biblia, Mungu ame-tujulisha jina lake na sifa zake. Isitoshe, Neno lake husemakwamba alimtuma Mwana wake mpendwa duniani na ku-ruhusu ateseke na kufa kwa ajili yetu. (Yohana 3:16) Zawadihiyo ina maana gani kwetu? Inatupa tumaini la kuwa na ma-isha mazuri wakati ujao.

5 Pia tumaini letu la wakati ujao linategemea jambo fulaniambalo Mungu amefanya. Yehova amesimamisha serika-li ya kimbingu, Ufalme wa Kimasihi. Karibuni itakomeshamateso yote na kuifanya dunia iwe paradiso. Hebu wazia!Tunaweza kuishi humo tukiwa na amani na furaha mile-le. (Zaburi 37:29) Kwa sasa, Mungu ametupa mwongozo wakuishi maisha bora zaidi sasa. Pia ametupa zawadi ya sala,inayotusaidia kuwasiliana naye wakati wowote. Hizo ni ba-adhi ya njia chache tu ambazo Yehova ameonyesha

4, 5. Taja baadhi ya njia ambazo Yehova ameonyesha upendo kwetu.

Kaa Katika Upendo wa Mungu 185

upendo kwa wanadamu wotekwa ujumla na kwako wewe bi-nafsi.

6 Hebu fikiria swali hili: Nita-onyeshajekwamba ninathaminiupendowaYehova? Huendawe-

ngi wakajibu, “Kwa kumpendapia.” Je, hivyo ndivyo unavyohisi? Yesu alisema

kwamba hii ndiyo amri kuu zaidi: “Lazima umpende Yeho-va Mungu wako kwa moyowako wote na kwa nafsi yako yotena kwa akili yako yote.” (Mathayo 22:37) Bila shaka una sa-babu nyingi za kumpenda Yehova Mungu. Lakini je, kuhisitu kwamba una upendo huo kunatosha kuonyesha kwambaunampenda Yehova kwa moyo, nafsi, na akili yako yote?

7 Kama Biblia inavyoonyesha, kumpenda Mungu si hisiatu. Ingawa ni muhimu kuhisi kwamba unampenda Yehova,huo ni mwanzo tu wa kumpenda kikweli. Mti wa matundahutokana na mbegu. Ikiwa unataka kula tunda, je, utato-sheka tu mtu akikupa mbegu ya tunda hilo? Hapana! Vivyohivyo, kuhisi kwamba unampenda Yehova Mungu ni mwa-nzo tu. Biblia inafundisha: “Kumpenda Mungu humaanishahivi, kwamba tuzishike amri zake; na bado amri zake simzigo mzito.” (1 Yohana 5:3) Ili tumpende Mungu kikweli,lazima tuzae matunda mazuri. Ni lazima tuonyeshe kwa ma-tendo kwamba tunampenda.—Mathayo 7:16-20.

8 Tunaonyesha kwamba tunampenda Mungu tunapo-shika amri zake na kufuata kanuni zake. Si vigumukufanya hivyo. Sheria za Yehova si nzito bali zimekusudi-wa kutusaidia kuishi maisha mazuri, yenye furaha, na yenyekuridhisha. (Isaya 48:17, 18) Tunapoishi kupatana na mwo-ngozo wa Yehova, tunamwonyesha Baba yetu wa mbinguni

6. Unawezaje kuonyesha kwamba unathamini upendo ambao Yeho-va amekuonyesha?7. Je, kumpenda Mungu ni kuwa na hisia tu? Eleza.8, 9. Tunawezaje kuonyesha upendo na shukrani kwa Mungu?

Biblia Inafundisha Nini Hasa?

kwamba tunathamini kikweli yale yote ambayo ametufa-nyia. Inasikitisha kwamba ni watu wachache ulimwengunileo wenye uthamini kama huo. Hatutaki kukosa uthaminikama watu fulani walioishi wakati Yesu alipokuwa duniani.Yesu aliwaponya watu kumi wenye ukoma, lakini ni mmojatu aliyerudi kumshukuru. (Luka 17:12-17) Bila shaka tunge-penda kuwa wenye shukrani kama yule mtu mmoja wala sikama wale wengine tisa wasio na shukrani!

9 Ni amri gani za Yehova tunazopaswa kutii? Tumezungu-mzia amri kadhaa katika kitabu hiki, hebu tujikumbushechache. Kutii amri za Mungu kutatusaidia kukaa katika upe-ndo wa Mungu.

MKARIBIE YEHOVA ZAIDI10 Kujifunza juu ya Yehova ni hatua muhimu ya kumkari-

bia. Ni hatua inayopaswa kuendelea daima. Tuseme unaotamoto wakati wa usiku wenye baridi, je, ungeuacha motohuo ufifie na kuzimika? Hapana. Utaendelea

10. Eleza kwa nini ni muhimu kuendelea kupataujuzi juu ya Yehova Mungu.

Kama moto, upendo wako kwa Yehovaunahitaji kuchochewa ili uendelee kuwaka

Kaa Katika Upendo wa Mungu 187

kuongeza kuni ili moto uendelee kuwaka. Huenda uhaiwako unautegemea! Sawa na vile kuni huchochea moto,ndivyo “kumjua Mungu” kunavyoimarisha upendo wetukwa Yehova.—Methali 2:1-5.

11 Yesu alitaka wanafunzi wake waendelee kuimarishaupendo wao kwa Yehova na Neno lake la kweli lenye thama-ni. Baada ya kufufuliwa, Yesu aliwafundisha wanafunzi wakewawili baadhi ya unabii ulio katika Maandiko ya Kiebra-nia ambao ulitimizwa maishani mwake. Matokeo yakawaje?Baadaye walisema hivi: “Je, mioyo yetu haikuwa ikiwaka ali-pokuwa akisema nasi barabarani, alipokuwa akitufunguliaMaandiko?”—Luka 24:32.

12 Ulipojifunza kwa mara ya kwanza mambo ambayo Bib-lia inafundisha hasa, je, hukufurahi sana, ukawa na bidii naupendo mwingi sana kumwelekea Mungu? Bila shaka. We-ngi wamehisi hivyo. Kazi kubwa sasa ni kuendelea kukuzana kuimarisha upendo huo. Hatutaki kuuiga ulimwengu.Yesu alitabiri hivi: “Upendo wa walio wengi zaidi utapoa.”(Mathayo 24:12) Unawezaje kuendelea kumpenda Yehovana kweli zake zilizo katika Biblia?

13 Endelea kupata ujuzi juu ya Yehova Mungu na YesuKristo. (Yohana 17:3) Tafakari au fikiria kwa uzito mambounayojifunza katika Neno la Mungu, na ujiulize: ‘Mambohayo yananifundisha nini juu ya Yehova Mungu? Yanani-saidiaje kumpenda Yehova zaidi kwa moyo, akili, na nafsiyangu yote?’ (1 Timotheo 4:15) Kutafakari juu ya mambohayo kutakufanya umpende Yehova zaidi.

14 Njia nyingine ya kuimarisha upendo wako kwa Yeho-va ni kusali kwa ukawaida. (1 Wathesalonike 5:17) Katika

11. Mafundisho ya Yesu yalikuwa na matokeo gani kwa wanafunziwake?12, 13. (a) Upendo wa watu wengi ulimwenguni kumwelekea Mu-ngu na Biblia ukoje? (b) Tunawezaje kuendeleza upendo wetu?14. Sala inawezaje kutusaidia kuendelea kukaa katika upendo wa Ye-hova?

188 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Sura ya 17 ya kitabu hiki tulijifunza kwamba sala ni zawa-di yenye thamani kutoka kwa Mungu. Kama vile uhusianokati ya wanadamu husitawi kwa sababu ya kuwasiliana kwauhuru na kwa ukawaida, uhusiano wetu na Yehova hukuana kuimarika tunaposali kwa ukawaida. Hatupaswi kusali ki-desturi tu, tukirudia-rudia maneno yaleyale bila hisia walamaana yoyote. Tunapaswa kuzungumza na Yehova kamavile mtoto anavyozungumza na baba anayempenda. Bilashaka, tunataka kuzungumza kwa heshima, lakini wazi-wazi, kwa unyoofu, na kutoka moyoni. (Zaburi 62:8) Ndiyo,funzo la Biblia la kibinafsi na sala inayotoka moyoni ni ma-mbo muhimu katika ibada yetu, nayo hutusaidia kuendeleakukaa katika upendo wa Mungu.

UWE NA SHANGWE KATIKA IBADA15 Funzo la Biblia la kibinafsi na sala ni matendo ya

ibada ambayo tunaweza kufanya faraghani. Hata hivyo, natuchunguze sehemu moja ya ibada yetu tunayofanya hadha-rani, yaani, kuzungumza na wengine kuhusu imani yetu. Je,tayari umezungumza na watu fulani kuhusu kweli za Bib-lia? Ikiwa ndivyo, haikosi umefurahia kufanya hivyo. (Luka1:74) Tunapozungumza na wengine kweli ambazo tume-jifunza juu ya Yehova Mungu, tunatimiza mgawo muhimusana ambao Wakristo wote wa kweli wamekabidhiwa, yaa-ni, mgawo wa kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu.—Mathayo 24:14; 28:19, 20.

16 Mtume Paulo aliiona huduma yake kuwa yenye tha-mani sana, aliiita hazina. (2 Wakorintho 4:7) Kazi boraunayoweza kufanya ni kuzungumza na watu juu ya Yeho-va Mungu na makusudi yake. Yeye ndiye Bwana bora zaidi,na kumtumikia huleta faida zisizo na kifani. Kwa kufanyakazi hiyo, unawasaidia watu wenye mioyo minyoofu wa-mkaribie Baba yetu wa mbinguni na kutembea katika

15, 16. Kwa nini tuione kazi ya kuhubiri Ufalme kuwa pendeleo nahazina?

Kaa Katika Upendo wa Mungu 189

barabara ya uzima wa milele! Hakuna kazi yenye kuridhishakama hiyo. Isitoshe, kuhubiri juu ya Yehova na Neno lakehuongeza imani yako na kuimarisha upendo wako kwa-ke. Na Yehova anathamini jitihada zako. (Waebrania 6:10)

Yehova angependa upate “uzima uliowa kweli.” Je, utaupata?

190 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Kufanya kazi hiyo kwa bidii kutakusaidia kuendelea kukaakatika upendo wa Mungu.—1 Wakorintho 15:58.

17 Tunapaswa kukumbuka kwamba kazi ya kuhubiri Ufal-me ni muhimu sana. Biblia inasema: “Lihubiri neno, fanyahivyo kwa bidii.” (2 Timotheo 4:2) Kwa nini ni muhimu ku-fanya hivyo leo? Neno la Mungu linatuambia: “Ile siku kuuya Yehova iko karibu. Iko karibu, nayo inaharakisha sana.”(Sefania 1:14) Ndiyo, wakati wa Yehova kuharibu mfumohuu wote wa mambo unakaribia sana. Watu wanapaswakuonywa! Wanapaswa kujua kwamba huu ndio wakati wakumchagua Yehova kuwa Mwenye Enzi Kuu wao. Mwisho‘hautachelewa.’—Habakuki 2:3.

18 Yehova anataka tumwabudu pamoja na Wakristo wakweli. Ndiyo sababu Neno lake linasema hivi: “Acheni tufi-kiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri,bila kuacha kukusanyika pamoja sisi wenyewe, kama vilewengine walivyo na desturi, bali tutiane moyo, na kufanyahivyo zaidi kwa kadiri mnavyoona siku ile kuwa inakaribia.”(Waebrania 10:24, 25) Tunapokusanyika pamoja na waami-ni wenzetu katika mikutano ya Kikristo, tuna nafasi nzuri yakumsifu na kumwabudu Mungu wetu tunayempenda. Piatunajengana na kutiana moyo.

19 Tunaposhirikiana na waabudu wa Yehova, tunaimari-sha vifungo vya upendo na urafiki kutanikoni. Tunapaswakuzingatia wema wa wengine, kama Yehova anavyozingatiawema wetu. Usitazamie waamini wenzako wawe wakamili-fu. Kumbuka kwamba wote wamefikia viwango tofauti vyaukomavu wa kiroho, na kwamba kila mmoja wetu hufanyamakosa. (Wakolosai 3:13) Jitahidi kufanya urafiki na walewanaompenda Yehova sana, nawe utafanya maendeleo yakiroho. Ndiyo, kumwabudu Yehova pamoja na ndugu na

17. Kwa nini huduma ya Kikristo ni muhimu leo?18. Kwa nini tumwabudu Yehova pamoja na Wakristo wa kweli?19. Tunawezaje kuimarisha vifungo vya upendo katika kutaniko laKikristo?

Kaa Katika Upendo wa Mungu 191

dada zako wa kiroho kutakusaidia kukaa katika upendo waMungu. Yehova huwathawabishaje wale wanaomwabudukwa uaminifu na kukaa katika upendo wake?

JITAHIDI KUPATA “UZIMA ULIO WA KWELI”20 Yehova huwathawabisha watumishi wake waaminifu

kwa kuwapa uzima, au uhai. Hata hivyo, ni uhai wa ainagani? Je, kweli uko hai sasa? Wengi wetu wangejibu, “Ndiyo.”Kwani, si tunapumua, tunakula, na kunywa? Bila shaka, tukohai. Na tunapokuwa na furaha, huenda tukasema, “Haya ndi-yo maisha!” Hata hivyo, Biblia inaonyesha kwamba, katikamaana halisi, hakuna mwanadamu yeyote ambaye ana uzi-ma wa kweli.

21 Neno la Mungu linatuhimiza ‘tuushike imara uzimaulio wa kweli.’ (1 Timotheo 6:19) Maneno hayo yanaonye-sha kwamba tuna tumaini la kupata “uzima ulio wa kweli”wakati ujao. Ndiyo, tutakapokuwa wakamilifu, tutakuwa nauzima wa kweli, kwa maana tutaishi kama Mungu alivyoku-sudia tuishi. Tutakapoishi katika paradiso duniani tukiwa naafya kamili, amani, na furaha, ndipo tutakapofurahia “uzimauliowa kweli”—uzimawa milele. (1 Timotheo 6:12) Je, hilo situmaini zuri?

22 Tunawezaje ‘kushika imara uzima ulio wa kweli’? Aki-zungumzia jambo hilohilo, Paulo aliwahimiza Wakristo“wafanye mema” na “wawe matajiri katika matendo ma-zuri.” (1 Timotheo 6:18) Basi, ni wazi kwamba tunahitajikutumia kweli ambazo tumejifunza katika Biblia. Lakini je,Paulo alimaanisha kwamba “uzima ulio wa kweli” ni ma-lipo ya kutenda mema? Hapana, kwa maana tumaini hilozuri hutegemea “fadhili zisizostahiliwa” kutoka kwa Mungu.(Waroma 5:15) Hata hivyo, Yehova anapenda kuwathawabi-sha wale wanaomtumikia kwa uaminifu. Angependa upate

20, 21. “Uzima ulio wa kweli” ni nini, na kwa nini tumaini hilo nizuri?22. Unawezaje ‘kushika imara uzima ulio wa kweli’?

192 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

“uzima ulio wa kweli.” Wale wanaokaa katika upendo waMungu ndio watakaopata uzima huo wa milele, wenye fura-ha na amani.

23 Kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza, ‘Je, ninamwabu-du Mungu kupatana na maagizo yake yaliyo katika Biblia?’Ikiwa tunafanya hivyo kila siku, basi tunatembea katika njiainayofaa. Tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova ni ki-mbilio letu. Atawaokoa watu wake waaminifu katika sikuhizi za mwisho zenye taabu za mfumo huu wa kale wa ma-mbo. Pia, Yehova atatukomboa na kutuingiza katika mfumompya mtukufu ulio karibu. Tutakuwa na shangwe iliyoje ku-ishi wakati huo! Na tutakuwa na furaha iliyoje kwa kuwatulifanya maamuzi yanayofaa katika siku hizi za mwisho!Ukifanya maamuzi yanayofaa sasa, utapata “uzima ulio wakweli,” uzima ambao Yehova Mungu alikusudia, kwa umile-le wote!

23. Kwa nini ni muhimu kukaa katika upendo wa Mungu?

MAMBO AMBAYO BIBLIA INAFUNDISHA

ˇ Tunaonyesha kwamba tunampenda Mungukikweli tunaposhika amri zake na kufuatakanuni zake.—1 Yohana 5:3.

ˇ Kujifunza Neno la Mungu, kusali kwa Yeho-va kutoka moyoni, kuwafundisha wenginekumhusu, na kumwabudu katika mikutanoya Kikristo kutatusaidia kukaa katika upendowa Mungu.—Mathayo 24:14; 28:19, 20; Yo-hana 17:3; 1 Wathesalonike 5:17; Waebrania10:24, 25.

ˇ Wale wanaokaa katika upendo wa Munguwana tumaini la kupata “uzima ulio wakweli.”—1 Timotheo 6:12, 19; Yuda 21.

Kaa Katika Upendo wa Mungu 193

HABARI UKURASA

Jina la Mungu—Maana na Matumizi � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 195

Jinsi Unabii wa Danieli Ulivyotabiri Kutokea kwa Masihi � � � 197

Yesu Kristo—Masihi Aliyeahidiwa � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 199

Ukweli Kuhusu Baba, Mwana, na Roho Takatifu � � � � � � � � � � 201

Kwa Nini Wakristo wa Kweli Hawatumii MsalabaKatika Ibada? � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 204

Mlo wa Jioni wa Bwana—Maadhimisho Yanayomletea Mungu Heshima � � � � � � � � � � 206

Maneno “Nafsi” na “Roho” Yanamaanisha Nini Hasa? � � � � � 208

Sheoli na Hadesi Zinamaanisha Nini? � � � � � � � � � � � � � � � � � � 212

Siku ya Hukumu Ni Nini? � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 213

1914—Mwaka Muhimu Katika Unabii wa Biblia � � � � � � � � � � 215

Yule Malaika Mkuu Mikaeli Ni Nani? � � � � � � � � � � � � � � � � � � 218

Kumtambulisha “Babiloni Mkubwa” � � � � � � � � � � � � � � � � � � 219

Je, Yesu Alizaliwa Desemba? � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 221

Je, Tusherehekee Sikukuu? � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � � 222

NYONGEZA

ANDIKO la Zaburi 83:18 limetafsiriwaje katika Biblia yako? BibliaTakatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya husema hivi: “Ili watu wa-jue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yakondiyeUliye Juu Zaidi, juu yaduniayote.”Biblianyingine hutumiamaneno yanayofanana na hayo. Hata hivyo, tafsiri nyingi hazitu-mii jina Yehova, badala yake zinatumia majina ya heshima kamavile “Bwana” au “Mwenyezi.” Ni jina gani linalopaswa kutumiwakatika mstari huo? Jina la heshima au jina halisi Yehova?

Mstarihuo unazungumzia jina halisi. Katika Kiebrania cha awaliambacho kilitumiwa kuandika sehemu ku-bwa ya Biblia, jina halisi la pekee linatumiwakatika mstari huo. Linaandikwa hivi kati-ka herufi za Kiebrania ˘˙˘˝ LYHWHMD KatikaKiswahiliE mara nyingi jina hilo hutafsiri-wa “Yehova.” Je, jina hilo hupatikana katikamstari mmoja tu wa Biblia? Hapana. Li-napatikana katika maandishi ya awali yaMaandiko ya Kiebrania karibu mara 7,000!

Jina la Mungu ni muhimu kadiri gani? Fikiria ile sala ya mfanoambayo Yesu Kristo aliwafundisha wanafunzi wake. Inaanza kwakusema: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe.” (Ma-thayo 6:9) Baadaye, Yesu alisali hivi kwa Mungu: “Baba, litukuzejina lako.” Mungu akajibu kutoka mbinguni, akisema “Nimelitu-kuza na pia nitalitukuza tena.” (Yohana 12:28) Ni wazi kwambajina la Mungu ni muhimu sana. Kwa nini basi watafsiri fula-ni wameliondoa jina hilo katika Biblia wanapotafsiri na kutumiamajina ya heshima badala yake?

Inaonekana kuna sababu mbili kuu. Kwanza, wengi wao hudaikwamba jina hilo halipaswi kutumiwa kwa sababu hakuna ye-yote leo anayejua jinsi lilivyokuwa likitamkwa zamani. Kiebraniacha awali hakikuandikwa kwa kutumia irabu—kama vile a, e, i,o, u. Kwa hiyo, hakuna yeyote leo anayeweza kusema kwa uhaki-ka jinsi watu wa nyakati za Biblia walivyotamka jina YHWH. Hata

Jina la Mungu—Maana na Matumizi

˘˙˘˝Jina la Mungukatika herufiza Kiebrania

195

hivyo, je, hilo lituzuie tusitumie jina la Mungu? Katika nyakati zaBiblia, huendajinaYesu lilikuwa likitamkwaYeshuaau hata Yeho-shua—hakuna yeyote anayejua kwa hakika. Hata hivyo, leo watuulimwenguni pote wanatumia namna mbalimbali za jina Yesu,wakilitamka jinsi linavyotamkwa kwa ukawaida katika lugha yao.Hawasiti kulitumia jina hilo eti kwa sababu hawajui jinsi lilivyo-kuwa likitamkwa katika karne ya kwanza. Pia, ikiwa ungesafirikwenda nchi nyingine, huenda ukaona kwamba jina lako mwe-nyewe linatamkwa kwa njia tofauti kabisa katika lugha nyingine.Kwa hiyo, kutojua jinsi jina la Mungu lilivyokuwa likitamkwa za-mani si sababu ya kutolitumia.

Sababu ya pili ambayo hutolewa mara nyingi inayowafanyawatafsiri fulani waliondoe jina la Mungu katika Biblia inahusi-sha mapokeo ya kale ya Wayahudi. Wengi wao huamini kwambajina la Mungu halipaswi kutajwa. Inaonekana imani hiyo inato-kana na kutoelewa vizuri sheria ya Biblia inayosema: “Usilitumiejina la Yehova Mungu wako kwa njia isiyofaa, kwa maana Yehovahatamwacha bila kuadhibiwayule anayelitumia jina lake kwa njiaisiyofaa.”—Kutoka 20:7.

Sheria hiyo inakataza kulitumia jina la Mungu kwa njia isi-yofaa. Lakini je, inakataza kulitumia jina lake kwa heshima?Hapana. Waandikaji wote wa Maandiko ya Kiebrania (“Aganola Kale”) walikuwa wanaume waaminifu waliotii Sheria ambayoMungu aliwapa Waisraeli wa kale. Hata hivyo, walilitumia jinala Mungu kwa ukawaida. Kwa mfano, walilitia katika zaburi nyi-ngi zilizoimbwa na umati wa waabudu kwa sauti. Yehova Munguhata aliwaagiza waabudu wake waliitie jina lake, na wale walioku-wa waaminifu walifanya hivyo. (Yoeli 2:32; Matendo 2:21) Kwahiyo, Wakristo leo hawasiti kulitumia jina la Mungu kwa heshi-ma, kama Yesu alivyofanya.—Yohana 17:26.

Wanapoliondoajina la Mungu na kutumia majinaya heshimabadala yake, watafsiri wa Biblia hufanya kosa kubwa. Wanamfa-nya Mungu asijulikane, na hali Biblia inawahimiza wanadamuwasitawishe “urafiki wa karibu pamoja na Yehova.” (Zaburi25:14) Ikiwa ungekuwa na rafiki ambaye hujui jina lake, uhusi-ano wenu ungekuwa wa karibu kadiri gani? Vivyo hivyo, watuwasipojulishwa jina la Mungu, Yehova, wanawezaje kumkaribia?

196 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Isitoshe, watu wasipolitumia jina la Mungu, hawawezi kuelewamaana muhimu ya jina hilo. Jina la Mungu linamaanisha nini?

Mungu mwenyewe alimweleza mtumishi wake mwaminifuMusa maana ya jina lake. Musa alipomwuliza Mungu jina lake,Yehova alimjibu: “Nitakuwa kile nitakachokuwa.” (Kutoka 3:14)Tafsiri ya Rotherham inatafsiri hivi maneno hayo: “Nitakuwachochote Nipendacho kuwa.” Kwa hiyo, Yehova anaweza kuwachochote kinachohitajika ili kutimiza makusudi yake.

Hebu wazia kwamba ungeweza kuwa chochote ambacho unge-penda kuwa. Ungewafanyia nini rafiki zako? Ikiwa mmoja waoangekuwa mgonjwa sana, ungeweza kuwa daktari stadi na ku-mtibu. Ikiwa mwingine angefilisika, ungeweza kuwa tajiri nakumsaidia. Hata hivyo, ukweli ni kwamba wewe huna uwezo wakuwa chochote ambacho ungependa kuwa. Hakuna yeyote katiyetu aliye na uwezo huo. Unapoendelea kujifunza Biblia, utafura-hi kuona jinsi Yehova huwa chochote kinachohitajika ili kutimizamakusudi yake. Naye anapenda kutumia nguvu zake kwa niabaya wale wanaompenda. (2 Mambo ya Nyakati 16:9) Walewasiojua jina la Yehova hawawezi kuuona uwezo wake wa kuwachochote anachopenda kuwa.

Ni wazi kwamba, jina Yehova linapaswa kuwa katika Bib-lia. Kujua maana yake na kulitumia kwa uhuru katika ibada yetukunaweza kutusaidia sana kumkaribia Baba yetu wa mbinguniYehova.�

� Unaweza kupata habari zaidi kuhusu jina la Mungu, maana yake, nasababu za kulitumia katika ibada kwenye broshua Jina la Mungu Litaka-loendelea Milele, iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Nyongeza 197

NABII Danieli aliishi zaidi ya miaka 500 kabla ya kuzaliwa kwaYesu. Hata hivyo, Yehova alimpa Danieli ujumbe ambao ungefa-nya iwezekane kujuawakati hususa ambapo Yesu angetiwa mafuta

Jinsi Unabii wa DanieliUlivyotabiri Kutokea kwa Masihi

au kuwekwa rasmi kuwa Masihi au Kristo. Danieli aliambiwa hivi:“Ujue na ufahamu kwamba tangu kutolewa kwa lile neno la kuru-disha na kujenga upya Yerusalemu mpaka Masihi aliye Kiongozi,kutakuwa na majuma 7, pia majuma 62.”—Danieli 9:25.

Ili kujua wakati ambapo Masihi angetokea, kwanza tunahitajikujua mwanzo wa kile kipindi ambacho Masihi angetokea mwi-shonimwake. Kulingana na unabii huo, kingeanzawakati ambapo‘lile neno la kurudisha na kujenga upya Yerusalemu lingetolewa.’Neno hilo lilitolewawakati gani? Kulingana na Nehemia, mwandi-shi wa Biblia, neno la kujenga upya kuta za Yerusalemu lilitolewa“katika mwaka wa 20 wa Mfalme Artashasta.” (Nehemia 2:1, 5-8)

198 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

“MAJUMA 70”

Miaka 490

Majuma 7(Miaka 49)

Majuma 62(Miaka 434)

Juma 1(Miaka 7)

455 406 & K.W.K. W.K. ) 29 33 36

“Lile neno lakurudisha

. . . Yerusalemu”

Yerusalemulajengwa upya

Masihiatokea

Masihi“akatiliwa

mbali”

Mwishowa yale

“majuma70”

Wanahistoriawanathibitisha kwamba mwaka wa 474 K.W.K., ndiouliokuwa mwaka wa kwanza wa utawala wa Artashasta. Kwa hiyo,mwaka wa 20 wa utawala wake ni mwaka wa 455 K.W.K. Kwa hiyo,kile kipindi cha unabii wa Danieli kuhusu Masihi kingeanza mwa-ka wa 455 K.W.K.

Pili, Danieli anaonyesha urefu wa kipindi hicho ambacho “Ma-sihi aliye Kiongozi” angetokea. Unabii huo unataja “majuma 7,pia majuma 62”—jumla ya majuma 69. Kipindi hicho kina urefugani? Tafsiri kadhaa za Biblia zinaonyesha kwamba hayo si maju-maya sikusaba, baliyamiaka.Yaani, kila juma linawakilishamiakasaba. Wayahudi wa kale walizoea kuhesabu majuma ya miaka, auvipindi vya miaka saba. Kwa mfano, kila mwaka wa saba ulikuwamwakawa Sabato. (Kutoka 23:10,11) Kwa hiyo, yale majuma 69 yaunabii yalikuwa vipindi 69 vya miaka 7 kila kimoja, au jumla yamiaka 483.

Sasa tunachohitaji ni kupiga hesabu tu. Tukihesabu miaka 483kuanzia mwaka wa 455 K.W.K., tutafika mwaka wa 29 W.K. Huondio mwaka hususa ambao Yesu alibatizwa na kuwa Masihi!�(Luka 3:1, 2, 21, 22) Je, huo si utimizowenye kustaajabishawa una-bii wa Biblia?

� Kuanzia mwaka wa 455 K.W.K. hadi mwaka wa 1 K.W.K. ni miaka 454.Kuanzia mwaka wa 1 K.W.K. hadi 1 W.K. ni mwaka mmoja (hakukuwa namwaka sufuri). Na kuanzia mwaka wa 1 W.K. hadi mwaka wa 29 W.K. nimiaka 28. Tukijumlisha miaka hiyo tunapata jumla ya miaka 483. Yesu “ali-katiliwa mbali” alipouawa mwaka wa 33 W.K., katika juma la 70 la miaka.(Danieli 9:24, 26) Unaweza kupata habari zaidi kuhusu unabii huo katikakitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! sura ya 11, na Insight on the Scriptures,Buku la 2, ukurasa wa 899-901 au

´Etude Perspicase, Buku la 2, ukurasa wa

995-997. Vitabu hivyo vimechapishwa na Mashahidi wa Yehova.

ILI kutusaidia kumtambua Masihi, Yehova Mungu aliwaongo-za manabii wengi wa Biblia waandike habari kuhusu kuzaliwa,huduma, na kifo cha Mkombozi aliyeahidiwa. Unabii wote huo

Yesu Kristo—Masihi Aliyeahidiwa

Nyongeza 199

wa Biblia ulitimizwa maishani mwa Yesu Kristo. Unabii huo nisahihi sana na una habari kamili. Kwa mfano, hebu tuchungu-ze unabii mbalimbali uliotabiri kuzaliwa kwa Masihi na maishayake ya utotoni.

Nabii Isaya alitabiri kwamba Masihi angetokea katika ukoo waMfalme Daudi. (Isaya 9:7) Kwa kweli, Yesu alizaliwa katika ukoowa Daudi.—Mathayo 1:1, 6-17.

UNABII KUMHUSU MASIHI

TUKIO UNABII UTIMIZO

Azaliwa katika kabila la Yuda Mwanzo 49:10 Luka 3:23-33

Azaliwa na bikira Isaya 7:14 Mathayo 1:18-25

Mzao wa Mfalme Daudi Isaya 9:7 Mathayo 1:1, 6-17

Yehova amtangaza kuwa Mwanawe Zaburi 2:7 Mathayo 3:17

Akosa kuaminiwa Isaya 53:1 Yohana 12:37, 38

Aingia Yerusalemu akiwa amepanda punda Zekaria 9:9 Mathayo 21:1-9

Asalitiwa na mtu wa karibu Zaburi 41:9 Yohana 13:18, 21-30

Asalitiwa kwa vipande 30 vya fedha Zekaria 11:12 Mathayo 26:14-16

Akaa kimya mbele ya waliomshtaki Isaya 53:7 Mathayo 27:11-14

Mavazi yake yapigiwa kura Zaburi 22:18 Mathayo 27:35

Atukanwa akiwa kwenye mti wa mateso Zaburi 22:7, 8 Mathayo 27:39-43

Hakuna mfupa wake uliovunjwa Zaburi 34:20 Yohana 19:33, 36

Azikwa pamoja na matajiri Isaya 53:9 Mathayo 27:57-60

Afufuliwa kabla ya mwili wake kuharibika Zaburi 16:10 Matendo 2:24, 27

Akwezwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu Zaburi 110:1 Matendo 7:56

200 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Mika, nabii mwingine wa Mungu alitabiri kwamba hatimayemtoto huyo angekuwa mtawala na kwamba angezaliwa “Be-thlehemu Efratha.” (Mika 5:2) Wakati ambapo Yesu alizaliwa,kulikuwa na miji miwili huko Israeli iliyokuwa ikiitwa Bethlehe-mu. Mji mmoja ulikuwa karibu na Nazareti, kaskazini mwa nchihiyo, nao ule mwingine ulikuwa karibu na Yerusalemu hukoYuda. Mji wa Bethlehemu, uliokuwa karibu na Yerusalemu, uli-kuwa ukiitwa Efratha zamani. Yesu alizaliwa katika mji huo,kama vile tu unabii ulivyokuwa umetabiri!—Mathayo 2:1.

Unabii mwingine wa Biblia ulitabiri kwamba Mwana wa Mu-ngu angeitwa “kutoka Misri.” Mtoto huyo, Yesu, alipelekwaMisri. Alirudishwa kutoka huko baada ya kifo cha Herode, na hi-vyo, unabii huo ukatimia.—Hosea 11:1; Mathayo 2:15.

Katika ukurasa wa 200, maandiko yaliyoorodheshwa chini yakichwa “Unabii” yanaeleza mambo mengi zaidi kumhusu Ma-sihi. Tafadhali linganisha maandiko hayo na yale yaliyo chiniya kichwa “Utimizo.” Kufanya hivyo kutaimarisha zaidi imaniyako katika ukweli wa Neno la Mungu.

Unapochunguza maandiko hayo kumbuka kwamba maandi-ko yenye unabii yaliandikwa mamia ya miaka kabla ya kuzaliwakwa Yesu. Yesu alisema: “Mambo yote yaliyoandikwa katikasheriaya Musa na katika Manabii na Zaburi juu yangu lazima ya-timizwe.” (Luka 24:44) Biblia inaonyesha wazi kwamba unabiihuo ulitimia kabisa!

WATU wanaoamini Utatu husema kwamba kuna Mungu Baba,Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu. Wote wanaseme-kana kuwa sawa, wenye nguvu zote, na hawana mwanzo. Kwahiyo, kulingana na fundisho la Utatu, Baba ni Mungu, Mwanani Mungu, na Roho Mtakatifu ni Mungu, hata hivyo, Mungu nimmoja tu.

Ukweli Kuhusu Baba,Mwana, na Roho Takatifu

Nyongeza 201

202 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Wengi wanaoamini fundisho la Utatu hukubali kwamba ha-wawezi kulieleza. Lakini, huenda wakafikiri kwamba hilo nifundisho la Biblia. Ni muhimu kutambua kwamba neno “Uta-tu” halipatikani kamwe katika Biblia. Lakini je, wazo lenyewelinapatikana katika Biblia? Ili kujibu swali hilo, hebu tuchungu-ze andiko ambalo wanaounga mkono fundisho hilo hutumiakutetea Utatu.

“NENO ALIKUWA MUNGU”

Andiko la Yohana 1:1 linasema: “Hapo mwanzo kulikuwakoNeno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwaMungu.” (Union Version) Baadaye, katika sura hiyohiyo, mtu-me Yohana anaonyesha waziwazi kwamba “Neno” ni Yesu.(Yohana 1:14) Hata hivyo, kwa kuwa Neno anaitwa Mungu,watu fulani hukata kauli kwamba Mwana na Baba ni Munguyuleyule.

Kumbuka kwamba mwanzoni sehemu hiyo ya Biblia iliandi-kwa katika Kigiriki. Baadaye, mstari huo wa Kigiriki ulitafsiriwakatika lugha nyingine. Hata hivyo, watafsiri fulani wa Bibliahawakusema “Neno alikuwa Mungu.” Kwa nini? Kulingana naufahamu wao wa lugha ya Kigiriki iliyotumiwa kuandika Biblia,watafsiri hao walikata kauli kwamba maneno “Neno alikuwaMungu” yalipaswa kutafsiriwa tofauti. Jinsi gani? Kuna mifanomichache hapa: “Logos [Neno] alikuwa na sifa za kimungu.”(A New Translation of the Bible) “Neno alikuwa mungu.” (TheNew Testament in an Improved Version) “Neno alikuwa pamo-ja na Mungu na alikuwa na utu kama wake.” (The Translator’sNew Testament) Kulingana na tafsiri hizo, Neno si Mungu mwe-nyewe.� Badala yake, kwa sababu ya ukuu wake miongoni mwaviumbe wa Yehova, Neno anaitwa “mungu.” Hapa, jina “mu-ngu” linamaanisha “mwenye nguvu.”

PATA HABARI ZAIDI

Watu wengi hawajui Kigiriki kilichotumiwa kuiandika Bib-

� Kwa habari zaidi kuhusu Yohana 1:1, ona gazeti la Mnara wa Mlinzila Novemba 1, 2008, ukurasa wa 24-25, lililochapishwa na Mashahidi waYehova.

Nyongeza 203

lia. Basi unawezaje kujua alichomaanisha mtume Yohana?Fikiria mfano huu: Mwalimu anawafundisha wanafunzi ja-mbo fulani. Baadaye, wanafunzi wanakuwa na maoni tofautikuhusu jambo walilofundishwa. Wanafunzi hao wanaweza ku-tatuaje tofauti zao? Wanaweza kumwomba mwalimu awapehabari zaidi. Bila shaka, kupata habari zaidi kutawasaidia ku-elewa jambo hilo vizuri zaidi. Vivyo hivyo, ili kuelewa maanaya Yohana 1:1, unaweza kutafuta habari zaidi kuhusu cheo chaYesu katika Injili ya Yohana. Kupata habari zaidi kutakusaidiakujua ukweli.

Kwa mfano, fikiria yale ambayo Yohana aliandika katika suraya 1, mstari wa 18: “Hakuna mwanadamu amemwona Mungu[Mweza-Yote] wakati wowote.” Hata hivyo, wanadamu wame-mwona Mwana, yaani, Yesu kwa kuwa Yohana alisema: “Neno[Yesu] alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufuwake.” (Yohana 1:14, UV) Basi, Mwana angewezaje kuwa ndi-ye Mungu Mweza-Yote? Yohana anasema pia kwamba Nenoalikuwa “pamoja na Mungu.” Basi, mtu anawezaje kuwa pamo-ja na mtu mwingine na wakati huohuo awe ndiye mtu huyo?Isitoshe, katika Yohana 17:3, Yesu anaonyesha waziwazi tofautiiliyopo kati yake na Baba yake wa mbinguni. Anamwita Babayake “Mungu wa pekee wa kweli.” Kisha Yohana anasema hivimwishoni-mwishoni mwa Injili yake: “Haya yameandikwa ilimpate kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo Mwana wa Mungu.”(Yohana 20:31) Ona kwamba Yesu anaitwa, Mwana wa Mungu,wala haitwi Mungu. Habari hiyo ya ziada iliyo katika Injili yaYohana inatusaidia kuelewa andiko la Yohana 1:1. Yesu, yuleNeno, ni “mungu” katika maana ya kwamba ana cheo cha juulakini siye Mungu Mweza-Yote.

CHANGANUA UTHIBITISHO

Ufikirie tena ule mfano wa mwalimu na wanafunzi. Waziakwamba baadhi ya wanafunzi wangali na shaka, hata baada yakusikiliza maelezo ya ziada ya mwalimu wao. Wafanye nini?Wanaweza kumwomba mwalimu mwingine awape habari zaidikuhusu suala hilo. Mwalimu huyo wa pili akiunga mkono ma-elezo ya yule wa kwanza, wanafunzi wengi wataridhika. Vivyo

204 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

hivyo, ikiwa huna uhakika kuhusu alichomaanisha mwandi-shi wa Biblia Yohana alipoandika kuhusu uhusiano kati ya Yesuna Mungu Mweza-Yote, unaweza kupata habari zaidi kutokakwa mwandishi mwingine wa Biblia. Kwa mfano, hebu fiki-ria aliyoandika Mathayo. Kuhusu mwisho wa ulimwengu huu,anamnukuu Yesu akisema: “Kuhusu siku ile na saa ile hakunamtu anayejua, wala malaika wa mbinguni wala Mwana, ila Babatu.” (Mathayo 24:36) Maneno hayo yanathibitishaje kwambaYesu si Mungu Mweza-Yote?

Yesu anasema kwamba Baba anajua mambo mengi kulikoMwana. Hata hivyo, ikiwa Yesu angekuwa ndiye Mungu Mwe-za-Yote, angejua mambo yote anayojua Baba yake. Kwahiyo, basi, Mwana na Baba hawalingani. Hata hivyo, wengi-ne wanadai: ‘Yesu ana nyutu mbili. Hapa anazungumza akiwamwanadamu.’ Na hata kama hilo lingekuwa kweli, namna ganiroho takatifu? Ikiwa hiyo pia ni Mungu yuleyule ambaye ndiyeBaba, mbona Yesu hasemi kwamba roho hiyo inajua mamboanayojua Baba?

Unapoendelea kujifunza Biblia, utaona maandiko menginemengi ya Biblia yanayohusiana na habari hii. Yanathibitishaukweli kumhusu Baba, Mwana, na roho takatifu.—Zaburi 90:2;Matendo 7:55; Wakolosai 1:15.

MSALABA unapendwa na kuheshimiwa na mamilioni ya watu.Kitabu The Encyclopædia Britannica kinasema kwamba msala-ba ni “ishara kuu ya dini ya Kikristo.” Hata hivyo, Wakristo wakweli hawatumii msalaba katika ibada. Kwa nini?

Sababu kuu ni kwamba Yesu Kristo hakufa kwenye msalaba.Kwa kawaida neno la Kigiriki linalotafsiriwa “msalaba” ni stau-ros�. Neno hilo linamaanisha “mti au nguzo iliyo wima.” TheCompanion Bible inasema hivi: “[Neno stau·ros�] halimaanishikamwe vipande viwili vya mbao vilivyokingamana kwa njia yo-

Kwa Nini Wakristo wa KweliHawatumii Msalaba Katika Ibada?

Nyongeza 205

yote ile . . . Hakuna jambo lolote katika [Agano Jipya] lugha yaKigiriki linalodokeza vipande viwili vya mbao.”

Katika maandiko kadhaa, waandishi wa Biblia wanatumianeno lingine kurejelea kifaa ambacho Yesu alifia juu yake. Nineno xy�lon la Kigiriki. (Matendo 5:30; 10:39; 13:29; Wagalatia3:13; 1 Petro 2:24) Neno hilo linamaanisha “mbao” au “kijiti,rungu, au mti.”

Kikieleza kwa nini ni mti tu wa kawaida uliotumiwa maranyingi kuwatundikia waliohukumiwa kifo, kitabu kimoja kina-sema: “Miti haikupatikana kila mahali ambapo palichaguliwakuwatundikia watu waliohukumiwa kifo. Kwa hiyo, nguzozilisimamishwa ardhini. Mara nyingi wahalifu walitundikwakwenye nguzo hizo, mikono yao ikiwa imeinuliwa juu na maranyingi miguu yao ikiwa imefungwa au kupigiliwa misumari.”—Kitabu Das Kreuz und die Kreuzigung, kilichoandikwa na Her-mann Fulda.

Hata hivyo, Neno la Mungu linatoa uthibitisho wenye ku-sadikisha zaidi. Mtume Paulo alisema: “Kristo kwa kutununuaalituachilia huru kutoka katika laana ya Sheria kwa yeye kuwa la-ana badala yetu, kwa sababu imeandikwa: ‘Amelaaniwa kila mtualiyetundikwa juu ya mti.’” (Wagalatia 3:13) Hapa Paulo ananu-kuu andiko la Kumbukumbu la Torati 21:22, 23, ambalo kwawazi linarejelea mti wala si msalaba. Kwa kuwa watu waliouawakwa njia hiyo walionwa kuwa “laana,” haifai Wakristo kupambanyumba zao kwa sanamu za Kristo akiwa ametundikwa.

Hakuna uthibitisho wowote unaoonyesha kwamba wale wa-liodai kuwa Wakristo walitumia msalaba katika ibada kwamuda wa miaka 300 baada ya Kristo kufa. Hata hivyo, katikakarne ya nne, Maliki mpagani Konstantino alijiunga na Wakri-sto waasi-imani na kuutetea msalaba kuwa ishara yao. HataKonstantino awe alikuwa na nia gani, msalaba haukuwa nauhusiano wowote na Yesu Kristo. Kwa kweli, msalaba ulibu-niwa na wapagani. Kitabu New Catholic Encyclopedia kinakirihivi: “Msalaba ulitumiwa na watu walioishi kabla ya enzi zaUkristo na wale ambao hawakuwa Wakristo.” Watu fulani ma-arufu wamesema kwamba msalaba unahusiana na ibada yaviumbe na desturi za kipagani za ngono.

Kwa nini basi ishara hiyo ya kipagani ilienezwa? Yaelekeailienezwa ili kufanya iwe rahisi kwa wapagani kukubali “Ukri-sto.” Hata hivyo, Biblia inashutumu waziwazi matumizi yaishara yoyote ya kipagani. (2 Wakorintho 6:14-18) Biblia ina-kataza pia kila namna ya ibada ya sanamu. (Kutoka 20:4, 5;1 Wakorintho 10:14) Hivyo basi, Wakristo wa kweli wana saba-bu nzuri za kutotumia msalaba katika ibada yao.�

� Ili kupata habari zaidi kuhusu msalaba, ona ukurasa wa 211-215 wakitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko, Chapa ya 2004, kilicho-chapishwa na Mashahidi wa Yehova.

206 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

WAKRISTO wanaamriwa waadhimishe Ukumbusho wa Kifocha Kristo. Maadhimisho hayo yanaitwa pia “mlo wa jioni waBwana.” (1 Wakorintho 11:20) Maadhimisho hayo yana umu-himu gani? Yanapaswa kufanywa wakati gani na jinsigani?

Yesu Kristo alianzisha maadhimisho hayo usikuwa Pasaka ya Kiyahudi mwaka wa 33 W.K. Pasakailikuwa maadhimisho yaliyofanywa mara moja tukila mwaka, siku ya 14 ya mwezi wa Nisani katikakalenda ya Kiyahudi. Ili kukadiria tarehe hiyo, inao-nekana kwamba Wayahudi walisubiri hadi sikusare(Machi 21) ya wakati wa majira ya kuchipua. Hiyondiyo siku ambayo mchana na usiku zinalingana. Mwe-zi wa Nisani ulianza wakati mwezi mpya ulipoonekanakwa mara ya kwanza karibu na Machi 21. Maadhimishoya Pasaka yalifanywa siku 13baadaye.

Yesu aliadhimisha Pasakapamoja na mitume wake, kishabaada ya kumfukuza Yuda Iskariote,

Mlo wa Jioni wa Bwana—MaadhimishoYanayomletea Mungu Heshima

Nyongeza 207

akaanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana. Mlo huo ulichukua mahalipa Pasaka ya Kiyahudi na hivyo unapaswa kuadhimishwa maramoja tu kwa mwaka.

Injili ya Mathayo inasema: “Yesu alichukua mkate na, baa-da ya kutoa baraka, akaumega, akawapa wanafunzi, akasema:‘Chukueni, mle. Huu unamaanisha mwili wangu.’ Pia, aka-chukua kikombe na, akiisha kushukuru, akawapa, akisema:‘Kinyweeni, ninyi nyote; kwa maana hii inamaanisha “damuyangu ya agano,” ambayo itamwagwa kwa ajili ya wengi kwamsamaha wa dhambi.’”—Mathayo 26:26-28.

Watu fulani huamini kwamba Yesu aligeuza mkate kuwamwili wake na divai kuwa damu yake. Hata hivyo, mwili waYesu ulikuwa kamili alipowapa mkate huo. Je, kweli mitumewa Yesu walikuwa wakila mwili halisi na kunywa damu yake?Hapana, kwa kuwa kufanya hivyo kungekuwa kuvunja sheriaya Mungu iliyokataza kunywa damu. (Mwanzo 9:3, 4; Mamboya Walawi 17:10) Kulingana na Luka 22:20, Yesu alisema: “Ki-kombe hiki kinamaanisha agano jipya kwa msingi wa damuyangu, ambayo itamwagwa kwa ajili yenu.” Je, kikombe hi-cho kilikuwa “agano jipya” kihalisi? Hilo halingewezekana kwakuwa agano ni makubaliano wala si kitu halisi.

Hivyo, mkate na divai ni mifano tu. Mkate huwakilisha mwilimkamilifu wa Kristo. Yesu alitumia mkate uliobaki baada ya mlowa Pasaka. Mkate huo uliokwa bila chachu, au hamira. (Kutoka12:8) Mara nyingi Biblia hutumia chachu kuwakilisha dhambiau kuharibika. Kwa hiyo, mkate unawakilisha mwili mkamilifuambao Yesu alidhabihu. Haukuwa na dhambi yoyote.—Mathayo16:11,12; 1 Wakorintho 5:6, 7; 1 Petro 2:22; 1 Yohana 2:1, 2.

Divai nyekundu inawakilisha damu ya Yesu. Damu hiyo ina-fanya agano jipya liwe halali. Yesu alisema kwamba damu yakeilimwagwa “kwa msamaha wa dhambi.” Hivyo, wanadamu wa-naweza kuwa safi machoni pa Mungu na kuwa katika aganojipya pamoja na Yehova. (Waebrania 9:14; 10:16, 17) Agano aumkataba huo huwawezesha wale Wakristo waaminifu 144,000kwenda mbinguni. Watakuwa wafalme na makuhani mbingunina kuwaletea wanadamu wote baraka.—Mwanzo 22:18; Yeremia31:31-33; 1 Petro 2:9; Ufunuo 5:9,10; 14:1-3.

208 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Ni nani wanaopaswa kula mkate na kunywa divai wakati waUkumbusho? Ni wale tu walio katika agano jipya, yaani, walewalio na tumaini la kwenda mbinguni. Roho takatifu ya Mu-ngu huwasadikisha kwamba wamechaguliwa kuwa wafalmembinguni. (Waroma 8:16) Wako pia katika agano la Ufalme pa-moja na Yesu.—Luka 22:29.

Namna gani wale walio na tumaini la kuishi milele katika Pa-radiso duniani? Wanatii amri ya Yesu kwa kuhudhuria Mlo waJioni wa Bwana, lakini wao huwa watazamaji wenye heshimawala hawashiriki mifano. Mara moja kila mwaka, Mashahidiwa Yehova huadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana mnamoNisani 14 baada ya jua kutua. Ingawa ni watu wachache tu uli-mwenguni wanaodai kuwa na tumaini la kwenda mbinguni,maadhimisho hayo yanathaminiwa na Wakristo wote. Ni pindiambayo wote wanaweza kufikiria juu ya upendo usio na kifaniwa Yehova Mungu na Yesu Kristo.—Yohana 3:16.

MANENO “nafsi” na “roho” yanamaanisha nini kwako? We-ngi huamini kwamba maneno hayo yanamaanisha kitu fulanikisichoonekana na kisichoweza kufa kilicho ndani yetu. Waohufikiri kwamba mtu anapokufa kitu hicho kisichoonekanahutoka ndani ya mwili wa binadamu na kuendelea kuishi. Kwakuwa fundisho hilo limeenea sana, watu wengi husha-ngaa wanapogundua kwamba si fundisho la Biblia. Basi, Nenola Mungu linasema nafsi na roho ni nini?

FUNDISHO LA BIBLIA KUHUSU “NAFSI”

Kwanza, tuzungumzie nafsi. Huenda unakumbuka kwambamwanzoni Biblia iliandikwa katika Kiebrania na Kigiriki. Wa-andishi wa Biblia walitumia neno ne�phesh la Kiebrania aupsy·khe� la Kigiriki walipoandika kuhusu nafsi. Maneno hayomawili yanapatikana zaidi ya mara 800 katika Maandiko, na

Maneno “Nafsi” na “Roho”Yanamaanisha Nini Hasa?

Nyongeza 209

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya huyatafsiri yote kuwa “nafsi.” Una-pochunguza jinsi neno “nafsi” linavyotumiwa katika Biblia,utaona kwa wazi kwamba neno hilo humaanisha (1) watu,(2) wanyama, au (3) uhai wa mtu au mnyama. Na tuzungu-mzie baadhi ya Maandiko yanayoonyesha mambo hayomatatu.

Watu. “Katika siku za Noa . . . watu wachache, yaani, nafsinane, walichukuliwa salama kupitia maji.” (1 Petro 3:20) Kwawazi neno “nafsi” katika andiko hilo linamaanisha watu,yaani, Noa, mkewe, wanawe watatu, na wake zao. Andiko la Ku-toka 16:16 lina maagizo kwa Waisraeli kuhusu kuokota mana.Waliambiwa: “Okoteni kiasi chake . . . kulingana na hesabu yanafsi ambazo kila mmoja wenu anazo katika hema lake.” Kwahiyo, kiasi cha mana kilichookotwa kilitegemea kiasi cha watukatika kila familia. Maandiko yafuatayo ya Biblia yanaonyeshamatumizi ya neno “nafsi” kumaanisha watu, Mwanzo 46:18;Yoshua 11:11; Matendo 27:37; na Waroma 13:1.

Wanyama. Tunasoma hivi katika masimulizi ya Biblia kuhu-su uumbaji: “Mungu akaendelea kusema: ‘Maji na yajawe nanafsi hai na viumbe vinavyoruka viruke juu ya dunia kwenyeuso wa anga la mbingu.’ Mungu akaendelea kusema: ‘Duniana itokeze nafsi zilizo hai kulingana na aina zake, mnyama wakufugwa na mnyama anayetambaa na mnyama-mwitu wa du-nia kulingana na aina yake.’ Ikawa hivyo.” (Mwanzo 1:20, 24)Katika andiko hilo, samaki, wanyama wa kufugwa, na wanya-ma-mwitu wote wanaitwa kwa neno lilelile—“nafsi.” Ndege nawanyama wengine wanaitwa nafsi kwenye Mwanzo 9:10; Ma-mbo ya Walawi 11:46; na Hesabu 31:28.

Uhai wa mtu. Wakati mwingine neno “nafsi” humaanishauhai wa mtu. Yehova alimwambia Musa: “Watu wote walioku-wa wakiiwinda nafsi yako wamekufa.” (Kutoka 4:19) Adui zaMusa walikuwa wakiwinda nini? Walitaka kumuua Musa. Ra-heli alipokuwa akimzaa mwanawe Benyamini, ‘nafsi yakeilitoka (kwa sababu alikufa).’ (Mwanzo 35:16-19) Wakati huoRaheli alipoteza uhai wake. Fikiria pia maneno ya Yesu: “Mimindiye mchungaji mwema; mchungaji mwema huitoa nafsiyake kwa ajili ya kondoo.” (Yohana 10:11) Yesu alitoa nafsi au

210 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

uhai wake kwa ajili ya wanadamu. Katika maandiko hayo yaBiblia, ni wazi kwamba neno “nafsi” linamaanisha uhai wamtu. Utapata mifano mingine yenye maana hiyo ya neno“nafsi” kwenye 1 Wafalme 17:17-23; Mathayo 10:39; Yohana15:13; na Matendo 20:10.

Unapoendelea kujifunza Neno la Mungu utaona kwambahakuna popote katika Biblia ambapo neno “nafsi” linahusi-anishwa na “kutoweza kufa” au “kuishi milele.” Badala yake,Maandiko yanasema kwamba nafsi inaweza kufa. (Ezekieli 18:4, 20) Kwa hiyo, katika Biblia mtu ambaye amekufa huitwa‘nafsi iliyokufa.’—Mambo ya Walawi 21:11.

MAANA YA “ROHO”

Hebu tuzungumzie jinsi Biblia inavyotumia neno “roho.”Watu fulani hufikiri kwamba “roho” ni neno lingine lina-lomaanisha “nafsi.” Lakini, si kweli. Biblia inaonyesha wazikwamba “roho” na “nafsi” ni vitu viwili tofauti. Vinatofautia-naje?

Waandishi wa Biblia walitumia neno la Kiebrania ru�ach auneno la Kigiriki, pneu�ma waliporejelea “roho.” Maandiko ye-nyewe yanaonyesha maana ya maneno hayo. Kwa mfano,andiko la Zaburi 104:29 linasema: “[Yehova] ukiiondoa roho[ru�ach] yao, wanakata pumzi, na kurudi katika mavumbi yao.”Andiko la Yakobo 2:26 linasema kwamba “mwili bila roho[pneu�ma] umekufa.” Katika andiko hilo “roho” inamaanishakile ambacho huupa mwili uhai. Bila roho, mwili umekufa.Kwa hiyo, katika Biblia neno ru�ach halitafsiriwi tu “roho” balipia “nguvu” au kani ya uhai. Kwa mfano, Mungu alisema hivikuhusu Mafuriko ya siku ya Noa: “Ninaleta gharika ya maji du-niani ili kuharibu kutoka chini ya mbingu wote wenye mwiliwalio na nguvu [ru�ach] za uhai ndani yao.” (Mwanzo 6:17; 7:15, 22) Hivyo, “roho” inarejelea nguvu isiyoonekana, inayote-ndesha viumbe vyote vilivyo hai.

Nafsi na roho hutofautiana. Mwili unahitaji roho kama vileredio inavyohitaji umeme ili kufanya kazi. Kwa mfano, una-potia betri katika redio na kuiwasha, nguvu zilizo katika betrihuiwezesha redio kufanya kazi. Hata hivyo, redio haiwezi kufa-

Nyongeza 211

nya kazi bila betri. Hali kadhalika, redio ambayo imeondolewakwenye umeme haiwezi kufanya kazi. Vivyo hivyo, roho ninguvu ambayo hutendesha mwili wetu. Kama umeme, rohohaiwezi kuhisi wala kufikiri. Ni nguvu isiyo na utu. Lakini bilaroho au kani ya uhai, “tunakata pumzi na kurudi kwenye udo-ngo,” kama mtunga-zaburi alivyosema.

Andiko la Mhubiri 12:7 linasema hivi linapozungumziakifo cha mwanadamu: “Mavumbi [mwili wake] huirudia nchikama yalivyokuwa, nayo roho yenyewe humrudia Mungu wakweli aliyeitoa.” Roho au kani ya uhai inapoondoka mwi-lini, mwili hufa na kurudi ulipotoka, yaani, kwenye udongo.Vivyo hivyo, nguvu ya uhai hurudi ilipotoka, yaani, kwa Mu-ngu. (Ayubu 34:14, 15; Zaburi 36:9) Hiyo haimaanishi kwambanguvu ya uhai huenda mbinguni kihalisi. Badala yake, ina-maanisha kwamba mtu akifa, tumaini lolote la kuishi tenalinamtegemea Yehova Mungu. Ni kana kwamba uhai wake ukomikononi mwa Mungu. Ni kupitia nguvu za Mungu tu ndiporoho au nguvu ya uhai inaweza kurudishwa ili mtu aweze kui-shi tena.

Inafariji kama nini kujua kwamba hivyo ndivyo Mungu ata-kavyofanya kwa wote wanaopumzika ndani ya “makaburi yaukumbusho!” (Yohana 5:28, 29) Wakati wa ufufuo, Yehovaatamfanyizia mwili mpya yule anayelala katika kifo na kuuhui-sha kwa kutia roho, au nguvu ya uhai ndani yake. Itakuwa sikuya shangwe sana.

Ikiwa ungependa kupata habari zaidi kuhusu maneno“nafsi” na “roho” kama yanavyotumiwa katika Biblia, ona

broshua Ni Nini HutupataTunapokufa? na ukurasa wa221-226 katika kitabu Ku-toa Sababu kwa KutumiaMaandiko, Chapa ya 2004,vilivyochapishwa na Masha-hidi wa Yehova.

KATIKA lugha za awali, Biblia inatumia neno la Kiebrania she�ohl�na neno la Kigiriki hai�des zaidi ya mara 70. Maneno yote mawi-li yanahusiana na kifo. Tafsiri fulani za Biblia hutumia maneno“kaburi,” “kuzimu,” au “shimo.” Hata hivyo, katika lugha nyingihakuna manenoyanayoweza kutoa maana halisi ya maneno hayoya Kiebrania na Kigiriki. Biblia Takatifu—Tafsiri ya UlimwenguMpya hutumia maneno “Sheoli” na “Hadesi” katika vielezi-chini.Maneno hayo yanamaanisha nini hasa? Hebu tuchunguze jinsiyanavyotumiwa katika maandiko mbalimbali ya Biblia.

Andiko la Mhubiri 9:10 linasema: “Hakuna kazi, wala utunga-ji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi [“Sheoli,” kielezi-chini],mahali unapokwenda.” Je, hilo linamaanisha kwamba Sheoli nikaburi hususa, au la mtu mmoja ambamo huenda tumemzikampendwa wetu? Hapana. Biblia inapozungumzia kaburi husu-sa, inatumia maneno mengine ya Kiebrania na Kigiriki, walasi she�ohl� na hai�des. (Mwanzo 23:7-9; Mathayo 28:1) Pia, Bib-lia haitumii neno “Sheoli” kurejelea kaburi ambamo watu wengiwamezikwa pamoja, kama vile kaburi la familia.—Mwanzo 49:30, 31.

Kwa hiyo, basi, “Sheoli” ni mahali pa aina gani? Neno laMungu huonyesha kwamba maneno “Sheoli,” au “Hadesi,” ha-yamaanishi kaburi kubwa la watu wengi. Kwa mfano, andiko laIsaya 5:14 linasema kwamba Sheoli ‘imepanua sana nafsi yakenayo imepanua kinywa chake kupita mipaka.’ Ingawa Sheolitayari imemeza wafu wengi, nyakati zote huonekana kwamba ha-itosheki. (Methali 30:15, 16) Tofauti na mahali hususa pa kuzikia,ambapo ni watu kadhaa tu wanaoweza kuzikwa humo, ‘Sheoli ha-patosheki.’ (Methali 27:20) Yaani, Sheoli hapajai kamwe. Hapanamipaka. Hivyo, Sheoli, au Hadesi, si mahali halisi. Badala yake nikaburi au mahali pa mfano ambapo watu walio wengi hulala usi-ngizi katika kifo.

Fundisho la Biblia kuhusu ufufuo hutusaidia kuelewa vizurizaidi maana ya “Sheoli” na “Hadesi.” Katika Neno la Mungu, She-

Sheoli na HadesiZinamaanisha Nini?

212

Nyongeza 213

oli na Hadesi huhusianishwa na kifo cha watu watakaofufuliwa.�(Ayubu 14:13; Matendo 2:31; Ufunuo 20:13) Neno la Mungu lina-onyesha pia kwamba wale waliomo Sheoli, au Hadesi, si wale tuambao walimtumikia Yehova bali pia wengi ambao hawakumtu-mikia. (Mwanzo 37:35; Zaburi 55:15) Kwa hiyo, Biblia hufundishakwamba kutakuwa na “ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu.”—Matendo 24:15.

� Tofauti na hilo, inasemekana kuwa wafu ambao hawatafufuliwawako “Gehena” wala si Sheoli, au Hadesi. (Mathayo 5:30; 10:28; 23:33)Kama ilivyo kuhusu Sheoli na Hadesi, Gehena si mahali halisi.

UNA maoni gani kuhusu Siku ya Hukumu? Watu wengihufikiri kwamba mabilioni ya watu watasimamishwa mmoja-mmoja mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Kisha kila mmojawao atahukumiwa. Baadhi yao wataishi kwa raha mbinguni,na wengine watateswa milele. Hata hivyo, masimulizi ya Bibliakuhusu hukumu ni tofauti kabisa. Kulingana na Neno la Mu-ngu, si wakati wenye kutisha bali ni wakati wa tumaini nakurudisha hali nzuri.

Mtume Yohana anafafanua hivi Siku ya Hukumu katika Ufu-nuo 20:11, 12: “Nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe nayeye aliyeketi juu yake. Dunia na mbingu zikakimbia kuto-ka mbele zake, na mahali popote hapakupatikana kwa ajili yahizo. Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesi-mama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwavikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafu-nguliwa; hicho ni kitabu cha uzima. Na wafu wakahukumiwakutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabukulingana na matendo yao.” Hukumu hiyo itatekelezwa nanani?

Yehova Mungu ndiye Hakimu au Mwamuzi mkuu wa wa-nadamu. Hata hivyo, ana mwakilishi wa kufanya hukumu.

Siku ya Hukumu Ni Nini?

214 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Kulingana na Matendo 17:31, mtume Paulo alisema kwa-mba Mungu “ameweka siku ambayo katika hiyo anakusudiakuihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa kupitia kwamwanamume ambaye amemweka rasmi.” Hakimu huyo ali-yewekwa rasmi ni Yesu Kristo aliyefufuliwa. (Yohana 5:22)Hata hivyo, Siku ya Hukumu itaanza lini? Itakuwa na urefugani?

Kitabu cha Ufunuo kinaonyesha kwamba Siku ya Hukumuitaanza baada ya vita vya Har–Magedoni, wakati ambapo mfu-mo wa Shetani utaharibiwa.� (Ufunuo 16:14, 16; 19:19–20:3)Baada ya Har–Magedoni, Shetani na roho wake waovu watafu-ngiwa katika abiso kwa miaka 1,000. Wakati huo, wale 144,000watahukumu na kutawala “wakiwa wafalme pamoja na Kristokwa miaka elfu.” (Ufunuo 14:1-3; 20:1-4; Waroma 8:17) Sikuya Hukumu haitakuwa tukio la haraka la saa 24. Itachukua mi-aka 1,000.

Katika kipindi hicho cha miaka 1,000, Yesu Kristo ‘ata-hukumu walio hai na wafu.’ (2 Timotheo 4:1) “Waliohai” watakuwa “umati mkubwa” utakaookoka Har–Magedo-ni. (Ufunuo 7:9-17) Mtume Yohana aliwaona pia “wafu . . .wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi” cha hukumu. Kamaalivyoahidi Yesu, “waliomo ndani ya makaburi ya ukumbushowataisikia sauti yake [Kristo] na kutoka.” (Yohana 5:28, 29; Ma-tendo 24:15) Watahukumiwa kwa msingi gani?

Katika njozi, mtume Yohana aliona ‘vitabu vya kukunjwavikifunguliwa na wafu wakahukumiwa kutokana na mamboyale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendoyao.’ Je, vitabu hivyo vya kukunjwa ni rekodi ya mamboambayo watu walifanya zamani? Hapana, watu hawatahuku-miwa kulingana na mambo ambayo walifanya kabla ya kufa.Tunajuaje? Biblia inasema: “Yeye ambaye amekufa ameondo-lewa hatia ya dhambi yake.” (Waroma 6:7) Hivyo, ni kana

� Kuhusu Har–Magedoni, tafadhali angalia Insight on the Scriptures,Buku la 1, ukurasa wa 594-595, 1037-1038 au

´Etude Perspicase, Buku la

1, ukurasa wa 1073-1075, Buku la 2, ukurasa wa 63-64; na sura ya 20 yakitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, vilivyochapishwa na Masha-hidi wa Yehova.

Nyongeza 215

kwamba wale watakaofufuliwa wataanza upya. Kwa hiyo, vita-bu vya kukunjwa vinawakilisha matakwa mengine ya Mungu.Ili waishi milele, wale watakaookoka Har–Magedoni na walewatakaofufuliwa watahitaji kutii amri za Mungu kutia ndanimatakwa yoyote mapya ambayo huenda Yehova akafunua ka-tika ile miaka 1,000. Hivyo, watu watahukumiwa kulingana nayale watakayotenda katika Siku ya Hukumu.

Wakati wa Siku ya Hukumu, mabilioni ya watu watapatafursa ya kujifunza kwa mara ya kwanza mapenzi ya Mu-ngu na kuishi kupatana nayo. Hivyo, kutakuwa na kazi kubwaya kuwaelimisha watu. “Wakaaji wa nchi yenye kuzaa hakikawatajifunza uadilifu.” (Isaya 26:9) Hata hivyo, si wote wata-kaofanya mapenzi ya Mungu. Andiko la Isaya 26:10 linasema:“Hata mwovu akionyeshwa kibali, yeye hatajifunza uadilifu.Atatenda isivyo haki katika nchi ya unyoofu, naye hatauonaukuu wa Yehova.” Waovu hao wataangamizwa milele wakatiwa Siku ya Hukumu.—Isaya 65:20.

Mwishoni mwa Siku ya Hukumu, wale wanadamu wengi-ne ‘watakuwa hai’ kikamili kwa sababu watakuwa wakamilifu.(Ufunuo 20:5) Hivyo, katika Siku ya Hukumu, wanadamuwatarudishwa katika hali ya ukamilifu waliyokuwa nayo mwa-nzoni. (1 Wakorintho 15:24-28) Kisha kutakuwa na jaribu lamwisho. Shetani atafunguliwa kutoka katika abiso na kuruhu-siwa ajaribu kuwapotosha wanadamu kwa mara ya mwisho.(Ufunuo 20:3, 7-10) Wale watakaompinga wataona utimizokamili wa ahadi hii ya Biblia: “Waadilifu wenyewe wataimili-ki dunia, nao watakaa milele juu yake.” (Zaburi 37:29) Ndiyo,Siku ya Hukumu itakuwa baraka kwa wanadamu wote waami-nifu!

MIAKA mingi mapema, wanafunzi wa Biblia walita-ngaza kwamba mambo muhimu yangetukia mwaka wa 1914.

1914—Mwaka Muhimu KatikaUnabii wa Biblia

216 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Ni mambo gani hayo, na ni uthibitisho gani unaoonyeshakwamba mwaka wa 1914 ungekuwa mwaka muhimu?

Kulingana na Luka 21:24, Yesu alisema: “Yerusalemu lita-kanyagwa-kanyagwa na mataifa, mpaka nyakati zilizowekwaza mataifa zitimie.” Yerusalemu lilikuwa jiji kuu la taifa la Ki-yahudi—kiti cha utawala cha nasaba ya wafalme wa nyumbaya Mfalme Daudi. (Zaburi 48:1, 2) Hata hivyo, wafalme haowalikuwa tofauti na viongozi wa mataifa mengine. Waliketijuu ya “kiti cha ufalme cha Yehova” wakimwakilisha Mungumwenyewe. (1 Mambo ya Nyakati 29:23) Kwa hiyo, Yerusale-mu liliwakilisha utawala wa Yehova.

Hata hivyo, utawala wa Mungu ulianza ‘kukanyagwa-ka-nyagwa na mataifa’ jinsi gani na wakati gani? Mwaka wa607 K.W.K., Yerusalemu liliposhindwa na Wababiloni. “Kiticha ufalme cha Yehova” hakikuwa na mtu, nayo nasaba yawafalme wa uzao wa Daudi ilikatishwa. (2 Wafalme 25:1-26)

“NYAKATI SABA”

Miaka 2,520

Miaka 606 1/4Oktoba 607 K.W.K. hadiDesemba 31, 1 K.W.K.

Miaka 1,913 3/4Januari 1, 1 W.K. hadi

Oktoba 1914

607 & K.W.K. W.K. ) 1914

“Yerusalemu litakanyagwa-kanyagwa na mataifa”

“Atakapokuja yule aliyena haki ya kisheria”

Nyongeza 217

Je, ‘lingekanyagwa-kanyagwa’ milele? Hapana, kwa kuwaunabii wa Ezekieli ulisema hivi kuhusu Sedekia, mfalme wamwisho wa Yerusalemu: “Kiondoe kilemba, na kulivua taji.. . . Hakika hili halitakuwa la mtu yeyote mpaka atakapokujayule aliye na haki ya kisheria, nami nitampa yeye.” (Ezekieli21:26, 27) Kristo Yesu ndiye aliye na “haki ya kisheria” ya tajila Daudi. (Luka 1:32, 33) Kwa hiyo, ‘kukanyaga-kanyaga’ ku-ngeisha wakati ambapo Yesu angekuwa Mfalme.

Tukio hilo kuu lingetokea wakati gani? Yesu alionyeshakwamba Mataifa yangetawala kwa muda fulani uliowekwa.Masimulizi ya Danieli sura ya 4 yanatusaidia kujua urefu wamuda huo. Yanataja ndoto ya kinabii ambayo Mfalme Nebu-kadneza wa Babiloni aliota. Aliona mti mkubwa uliokatwa.Kisiki chake hakingeweza kukua kwa sababu kilikuwa kime-fungwa kwa pingu ya chuma na ya shaba. Malaika alitangazahivi: “Nyakati saba zipite juu yake.”—Danieli 4:10-16.

Katika Biblia, nyakati nyingine miti huwakilisha utawala.(Ezekieli 17:22-24; 31:2-5) Kwa hiyo, kukatwa kwa mti huowa mfano kunaonyesha jinsi utawala wa Mungu, uliowakili-shwa na wafalme wa Yerusalemu, ungekatishwa. Hata hivyo,maono hayo yaliashiria kwamba ‘kukanyagwa-kanyagwa kwaYerusalemu’ kungekuwa kwa muda fulani—kipindi cha “nya-kati saba.” Kipindi hicho kina urefu gani?

Andiko la Ufunuo 12:6, 14 linaonyesha kwamba nyakatitatu na nusu zinatoshana na “siku 1,260.” Kwa hiyo, “nyakatisaba” zingekuwa mara mbili ya kipindi hicho, au siku 2,520.Lakini Mataifa hayakuacha ‘kukanyaga-kanyaga’ utawala waMungu siku 2,520 tu baada ya kuanguka kwa Yerusalemu.Basi, inaonekana kwamba unabii huo ulizungumzia mudamrefu zaidi. Kwa kutegemea andiko la Hesabu 14:34 na Ezeki-eli 4:6, yanayotaja “siku moja kwa mwaka mmoja,” zile“nyakati saba” zingekuwa miaka 2,520.

Miaka hiyo 2,520 ilianza Oktoba 607 K.W.K., Yerusa-lemu lilipoangushwa na Wababiloni na mfalme wa uzao waDaudi akaondolewa katika kiti cha ufalme. Kipindi hicho ki-liisha Oktoba 1914. Wakati huo, “nyakati zilizowekwa zamataifa” ziliisha, na Yesu Kristo akawekwa kuwa Mfalme wa

218 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

mbinguni aliyechaguliwa na Mungu.�—Zaburi 2:1-6; Danieli7:13, 14.

Kama Yesu alivyotabiri, matukio ya pekee ulimwenguni,kama vile, vita, njaa, matetemeko ya nchi, na tauni, yanao-nyesha “kuwapo” kwake akiwa Mfalme mbinguni. (Mathayo24:3-8; Luka 21:11) Matukio hayo yalitoa uthibitisho wa kwa-mba kwa kweli Ufalme wa mbinguni wa Mungu ulizaliwamwaka wa 1914 na “siku za mwisho” za mfumo huu mbovuwa mambo zikaanza.—2 Timotheo 3:1-5.

� Tangu Oktoba 607 K.W.K. hadi Oktoba 1 K.W.K. ni miaka 606. Kwakuwa hakuna mwaka wa sufuri, kuanzia Oktoba 1 K.W.K. hadi Okto-ba 1914 W.K. ni miaka 1,914. Tukijumlisha miaka 606 na miaka 1,914,tunapata miaka 2,520. Unaweza kupata habari kuhusu kuanguka kwa Ye-rusalemu mwaka wa 607 K.W.K., katika makala “Chronology” katika In-sight on the Scriptures au “Chronologie” katika

´Etude Perspicase, kilicho-

chapishwa na Mashahidi wa Yehova.

KIUMBE wa roho anayeitwa Mikaeli hatajwi mara nyingi kati-ka Biblia. Hata hivyo, kila mara anatajwa akitenda jambo fulani.Katika kitabu cha Danieli, Mikaeli anapigana na malaika waovu;katika barua ya Yuda, anabishana na Shetani; na katika Ufunuo,anapigana na Ibilisi na malaika wake waovu. Anapoutetea utawa-la wa Yehova na kupigana na adui za Mungu, Mikaeli anatendakupatana na maana ya jina lake—“Ni Nani Aliye Kama Mungu?”Lakini Mikaeli ni nani?

Nyakati nyingine, watu huitwa majina mbalimbali. Kwa mfa-no, mzee wa ukoo Yakobo aliitwa pia Israeli, na mtume Petroaliitwa Simoni. (Mwanzo 49:1, 2; Mathayo 10:2) Vivyo hivyo,Biblia inaonyesha kwamba Mikaeli ni jina lingine la Yesu Kristo,kabla na baada ya maisha yake duniani. Hebu tuone sababu zaKimaandiko zinazotufanya tukate kauli hiyo.

Malaika Mkuu. Neno la Mungu linamwita Mikaeli “yule mala-ika mkuu.” (Yuda 9) Ona kwamba Mikaeli anaitwa yule malaika

Yule Malaika Mkuu Mikaeli Ni Nani?

mkuu. Hilo linaonyesha kwamba kuna malaika mmoja tu ali-ye mkuu. Isitoshe katika Biblia, jina “malaika mkuu” linatumiwakatika hali ya umoja tu, wala si kwa wingi. Zaidi ya hayo, Yesuanahusianishwa na wadhifa wa malaika mkuu. Kuhusu BwanaYesu Kristo aliyefufuliwa, andiko la 1 Wathesalonike 4:16 lina-sema: “Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni akiwa namwito wenye amri, kwa sauti ya malaika mkuu.” Kwa hiyo sautiya Yesu inafafanuliwa kuwa sauti ya malaika mkuu. Basi, andikohilo linadokeza kwamba Yesu mwenyewe ndiye Mikaeli yule ma-laika mkuu.

Kiongozi wa Jeshi. Biblia inasema kwamba ‘Mikaeli na malaikazake walipigana na yule joka mkubwa na malaika zake.’ (Ufunuo12:7) Kwa hiyo, Mikaeli ni Kiongozi wa jeshi la malaika waami-nifu. Pia kitabu cha Ufunuo kinamtaja Yesu akiwa Kiongozi wajeshi la malaika waaminifu. (Ufunuo 19:14-16) Naye mtume Pa-ulo anamtaja kihususa “Bwana Yesu” na “malaika zake wenyenguvu.” (2 Wathesalonike 1:7; Mathayo 16:27; 24:31; 1 Petro3:22) Kwa hiyo, Biblia inataja Mikaeli na “malaika zake” na Yesuna “malaika zake.” (Mathayo 13:41) Kwa kuwa Neno la Munguhalionyeshi popote kwamba kuna majeshi mawili ya malaikawaaminifu mbinguni—moja likiongozwa na Mikaeli na linginelikiongozwa na Yesu—ni wazi kwamba Mikaeli si mwingine ila niYesu Kristo akiwa katika wadhifa wake mbinguni.�

� Unaweza kupata habari zaidi zinazoonyesha kwamba jina Mikaeli li-namhusu Mwana wa Mungu katika Insight on the Scriptures, Buku la 2,ukurasa wa 393-394 au

´Etude Perspicase, Buku la 2, ukurasa wa 280-281,

kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

KITABU cha Ufunuo kina majina ambayo yana maana ya mfa-no. (Ufunuo 1:1) Kwa mfano, kinataja mwanamke ambaye jina“Babiloni Mkubwa” limeandikwa katika paji la uso wake. Ki-nasema kwamba mwanamke huyo ameketi juu ya “umati namataifa.” (Ufunuo 17:1, 5, 15) Kwa kuwa hakuna mwanamke

Kumtambulisha “Babiloni Mkubwa”

Nyongeza 219

220 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

halisi anayeweza kufanya hivyo, lazima Babiloni Mkubwa awemwanamke wa mfano. Kwa hiyo, kahaba huyo wa mfano ana-wakilisha nini?

Kwenye Ufunuo 17:18, mwanamke huyohuyo wa mfano ana-tajwa kuwa “lile jiji kubwa lililo na ufalme juu ya wafalme wadunia.” Jina “jiji” linarejelea kikundi cha watu. Kwa kuwa ‘jijihilo kubwa’ linaongoza “wafalme wa dunia,” lazima yule mwa-namke anayeitwa Babiloni Mkubwa awe shirika lenye uvutanoulimwenguni pote. Linaweza kuitwa milki ya ulimwengu. Milkiya aina gani? Ya kidini. Ona jinsi maandiko mengine katika ki-tabu cha Ufunuo yanavyotusaidia kufikia uamuzi huo.

Milki inaweza kuwa ya kisiasa, ya kibiashara, au ya kidini.Mwanamke anayeitwa Babiloni Mkubwa si milki ya kisiasa kwasababu Neno la Mungu linasema kwamba “wafalme wa dunia,”au wanasiasa wa ulimwengu huu, “walifanya uasherati” naye.Uasherati wake ni mapatano ambayo amefanya na watawala wadunia na ndiyo sababu anaitwa “kahaba mkubwa.”—Ufunuo17:1, 2; Yakobo 4:4.

Babiloni Mkubwa hawezi kuwa milki ya kibiashara kwa sa-babu “wanabiashara wa dunia,” watamlilia atakapoharibiwa.Isitoshe, wafalme na wanabiashara watamwangalia BabiloniMkubwa wakiwa “mbali.” (Ufunuo 18:3, 9, 10, 15-17) Kwa hiyo,ni wazi kwamba Babiloni Mkubwa, si milki ya kisiasa wala ya ki-biashara, bali ni milki ya kidini.

Hilo linathibitishwa na ile taarifa ya kwamba Babiloni Mku-bwa anapotosha mataifa yote kwa ‘mazoea yake ya kuwasilianana pepo.’ (Ufunuo 18:23) Kwa kuwa mazoea yote ya kuwasi-liana na pepo hutokana na roho waovu, haishangazi kwambaBiblia inamwita Babiloni Mkubwa “makao ya roho waovu.”(Ufunuo 18:2; Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Pia, milki hiyoinapinga vikali dini ya kweli, ikiwatesa “manabii” na “wataka-tifu.” (Ufunuo 18:24) Kwa kweli, Babiloni Mkubwa anachukiasana dini ya kweli hivi kwamba anawatesa kikatili na hata ku-waua “mashahidi wa Yesu.” (Ufunuo 17:6) Hivyo, ni wazikwamba mwanamke huyo anayeitwa Babiloni Mkubwa anawa-kilisha milki ya ulimwenguni pote ya dini ya uwongo, inayotiandani dini zote zinazompinga Yehova Mungu.

BIBLIA haisemi Yesu alizaliwa wakati gani. Hata hivyo, inatupasababu za kutosha kukata kauli kwamba hakuzaliwa Desemba.

Fikiria hali ya hewa wakati huo wa mwaka huko Bethlehe-mu, ambako Yesu alizaliwa. Mwezi wa Kislevu katika kalendaya Kiyahudi (unaolingana na miezi ya Novemba/Desemba)ulikuwa mwezi wa baridi na mvua. Mwezi unaofuata ulikuwamwezi wa Tebethi (Desemba/Januari). Huo ndio mwezi ulio-kuwa na baridi kali zaidi, mara kwa mara kukiwa na thelujikatika nyanda za juu. Hebu tuone Biblia inasema nini kuhusuhali ya hewa ya eneo hilo.

Mwandishi wa Biblia Ezra anaonyesha kwamba Kislevu uli-kuwa mwezi wenye baridi na mvua nyingi. Baada ya kuelezakwamba umati ulikuwa umekusanyika Yerusalemu “katikamwezi wa 9 [Kislevu] siku ya 20 ya mwezi huo,” Ezra anase-ma kwamba watu walikuwa “wakitetemeka . . . kwa sababuya manyunyu ya mvua.” Kuhusu hali za hewa wakati huo wamwaka, watu waliokuwa wamekusanyika walisema: “Haya ni

Je, Yesu Alizaliwa Desemba?

Yesu alipozaliwa, wachungaji namakundi yao walikuwa malishoni

wakati wa usiku

221

majira ya manyunyu ya mvua, wala haiwezekani kusimamanje.” (Ezra 10:9, 13; Yeremia 36:22) Basi, haishangazi kwambawachungaji walioishi karibu na Bethlehemu walihakikishakwamba wao wenyewe na mifugo yao hawakuwa nje malisho-ni mwezi wa Desemba ulipofika!

Hata hivyo, Biblia inasema kwamba wachungaji walikuwamalishoni wakilisha makundi yao usiku ambao Yesu alizaliwa.Isitoshe, mwandishi wa Biblia, Luka anaonyesha kwamba wa-kati huo wachungaji walikuwa “wakiishi nje, wakichungamakundi yao usiku” karibu na Bethlehemu. (Luka 2:8-12)Ona kwamba wachungaji hao walikuwa wakiishi nje, si kwa-mba walikuwa wakitembea-tembea nje wakati wa mchana.Walikuwa na makundi yao malishoni usiku. Je, wangeweza ku-ishi nje wakati wa baridi na mvua huko Bethlehemu mwezi waDesemba? Hapana. Kwa hiyo, matukio hayo ya wakati wa ku-zaliwa kwa Yesu yanaonyesha kwamba hakuzaliwa Desemba.�

Neno la Mungu linatuambia waziwazi wakati ambapo Yesualikufa, lakini halielezi mengi kuhusu wakati ambapo alizali-wa. Hilo linatukumbusha maneno ya Mfalme Sulemani: “Jinani bora kuliko mafuta mazuri, na siku ya kufa kuliko siku yakuzaliwa kwa mtu.” (Mhubiri 7:1) Basi, haishangazi kwambaBiblia ina habari nyingi kuhusu huduma na kifo cha Yesulakini inataja mambo machache tu kuhusu wakati wa kuzaliwakwake.

� Unaweza kupata habari zaidi kwenye ukurasa wa 275-279 wa kitabuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko, Chapa ya 2004, kilichochapishwana Mashahidi wa Yehova.

SIKUKUU za kidini na sikukuu nyingine zinazopendwa na watuwengi ambazo husherehekewa sehemu nyingi za ulimwenguleo, hazikutokana na Biblia. Basi, sikukuu hizo zilianzia wapi?Ikiwa unaweza kufanya utafiti katika maktaba, unaweza kujifu-

Je, Tusherehekee Sikukuu?

222 Biblia Inafundisha Nini Hasa?

nza mengi kuhusu sikukuu zinazopendwa na wengi katika eneolenu. Fikiria mifano michache.

Ista. “Katika Agano Jipya, hakuna lolote linaloonyeshakwamba Ista ilisherehekewa,” yasema The Encyclopædia Bri-tannica. Ista ilianzaje? Ilitokana na ibada ya kipagani. Ingawainasemekana kwamba sikukuu hiyo ni ukumbusho wa kufu-fuka kwa Yesu, desturi zinazohusiana na sikukuu ya Ista si zaKikristo. Kwa mfano, The Catholic Encyclopedia inasema hivikuhusu yule “sungura wa Ista”: “Sungura huyo ni mfano wa ki-pagani na sikuzote huwakilisha nguvu za uzazi.”

Sherehe za Mwaka Mpya. Tarehe na desturi zinazohusianana sherehe za Mwaka Mpya hutofautiana katika nchi mba-limbali. Kuhusu chanzo cha sikukuu hiyo, The World BookEncyclopedia inasema: “Mtawala Mroma Kaisari Yulio aliteua Ja-nuari 1 kuwa Siku ya Mwaka Mpya katika mwaka wa 46 K.W.K.Waroma walitenga siku hiyo kwa ajili ya Yanu, mungu wa ma-lango, milango, na mianzo. Mwezi wa Januari ulipata jina lakekutoka kwa Yanu, aliyekuwa na nyuso mbili—mmoja ukianga-lia mbele na mwingine ukiangalia nyuma.” Kwa hiyo, shereheza Mwaka Mpya zinatokana na mapokeo ya kipagani.

Mkesha wa Siku ya Watakatifu Wote (“Halloween”). TheEncyclopedia Americana inasema: “Desturi fulani-fulani zina-zohusiana na Mkesha wa Siku ya Watakatifu Wote zilitokanana sherehe za kidini za Kiselti za kabla ya enzi za Ukristo. Wa-selti walikuwa na sikukuu kwa ajili ya miungu wawili wakuu—mungu-jua na mungu wa wafu . . . , ambaye sikukuu yakeilikuwa Novemba 1, mwanzo wa Mwaka Mpya wa Kiselti. Polekwa pole, sikukuu hiyo ya wafu ikaingizwa katika desturi za Ki-kristo.”

Sikukuu Nyingine. Haiwezekani kuzungumzia sikukuu zoteulimwenguni. Hata hivyo, sikukuu zinazowatukuza wanada-mu au mashirika ya kibinadamu hazimpendezi Yehova.(Yeremia 17:5-7; Matendo 10:25, 26) Pia, kumbuka kwambaMungu hupendezwa au kuchukizwa na sikukuu za kidini ikite-gemea vyanzo vyake. (Isaya 52:11; Ufunuo 18:4) Kanuni zaBiblia zilizotajwa katika Sura ya 16 ya kitabu hiki zitakusaidiakujua maoni ya Mungu kuhusu sikukuu zisizo za kidini.

Nyongeza 223

Je, ungependa kupata habari zaidi?Unaweza kuwasiliana na Mashahidi wa Yehova kupitia www.jw.org.

bh

-SW

14

08

28

BIBLIAINAFUNDISHA

NINI Hasa?

BIBLIAINAFUNDISH

Abh-SW

Omba ufundishwe Biblia bila malipo.

s