USAWIRI WA MCHAKATO WA KUJIUA KATIKA RIWAYA ...

248
USAWIRI WA MCHAKATO WA KUJIUA KATIKA RIWAYA TEULE ZA EUPHRASE KEZILAHABI: NI MWANGWI WA MTANZIKO WA KIJAMII? ADRIA FULUGE SHAHADA YA UZAMIVU KATIKA KISWAHILI CHUO KIKUU CHA DODOMA JULAI, 2021

Transcript of USAWIRI WA MCHAKATO WA KUJIUA KATIKA RIWAYA ...

USAWIRI WA MCHAKATO WA KUJIUA KATIKA

RIWAYA TEULE ZA EUPHRASE KEZILAHABI: NI

MWANGWI WA MTANZIKO WA KIJAMII?

ADRIA FULUGE

SHAHADA YA UZAMIVU KATIKA KISWAHILI

CHUO KIKUU CHA DODOMA

JULAI, 2021

USAWIRI WA MCHAKATO WA KUJIUA KATIKA RIWAYA

TEULE ZA EUPHRASE KEZILAHABI: NI MWANGWI WA

MTANZIKO WA KIJAMII?

NA

ADRIA FULUGE

TASINIFU HII IMEWASILISHWA KWA AJILI YA KUTUNUKIWA

SHAHADA YA UZAMIVU KATIKA KISWAHILI CHUO KIKUU

CHA DODOMA

CHUO KIKUU CHA DODOMA

JULAI, 2021

i

IKIRARI NA HAKIMILIKI

Mimi, Adria Fuluge, ninathibitisha kwamba tasinifu hii ni kazi yangu halisi, na

kwamba haijawahi kuwasilishwa na wala haitawasilishwa katika Chuo Kikuu

kingine chochote kwa ajili ya mahitaji ya kutunukiwa Shahada kama hii au Shahada

nyingine yoyote ile.

Saini:

Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kuzalisha, kutoa kopi, kunakili, ama

kusambaza sehemu yoyote ya tasinifu hii kwa namna yoyote bila kibali cha

maandishi kutoka kwa mwandishi au Chuo Kikuu cha Dodoma.

ii

ITHIBATI YA WASIMAMIZI

Waliotia saini hapa chini wanathibitisha kuwa wameisoma tasinifu hii inayoitwa

“Usawiri wa Mchakato wa Kujiua katika Riwaya Teule za Euphrase

Kezilahabi: Ni Mwangwi wa Mtanziko wa Kijamii?” na wanapendekeza kwamba

itahiniwe na kukubaliwa na Chuo Kikuu cha Dodoma kwa ajili ya kukamilisha

masharti ya kutunukiwa Shahada ya Uzamivu katika Kiswahili ya Chuo Kikuu cha

Dodoma.

Prof. Joshua Samuel Madumulla

Saini Tarehe:

(Msimamizi)

Dkt. Zuhura Abdallah Badru

Saini Tarehe:

(Msimamizi)

iii

SHUKRANI

Ninatambua kuwa hakuna mwingine zaidi anayestahili kupewa sifa, heshima na

utukufu wote, bali ni Mungu baba wa Mbinguni. Hii ni kwa sababu ndiye aliyenijalia

uhai na nguvu hadi kufikia hatua hii. Si kwa uweza wangu, na wala sikustahili

heshima kubwa kiasi hiki, bali ni kwa neema tu, kwani kwa uweza wake, nilijaliwa

nguvu na welewa wa kufanya utafiti huu. Basi, atukuzwe Yeye awezaye kufanya

mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu

itendayo kazi ndani yetu (Efe 3:20).

Aidha, kukamilika kwa kazi hii kulitokana na michango ya watu mbalimbali.

Ninatambua na kuuthamini sana mchango wao wa hali na mali. Hivyo basi, sina budi

kutoa shukrani zangu za dhati kwao. Hata hivyo, kwa kuwa si rahisi kuwataja wote

hapa, itanilazimu kuwataja wachache wafuatao:

Kwanza kabisa, ninapenda kutoa shukrani kwa wasimamizi wangu, Prof. Joshua

Samuel Madumulla na Dkt. Zuhura Abdallah Badru, ambao wamekuwa nami bega

kwa bega na kuhakikisha kuwa kazi hii inakuwa katika kiwango hiki. Licha ya

majukumu mengi waliyo nayo, hawakusita kunishauri na kunipa miongozo bora na

imara iliyowezesha kazi hii kufikia katika kiwango hiki. Asanteni sana.

Pili, ninakishukuru Chuo Kikuu Mzumbe kwa kunipa ufadhili wa masomo yangu na

kuniwezesha kukamilisha Shahada yangu ya Uzamivu bila usumbufu wowote.

Vilevile, nawashukuru wana-Idara wenzangu, hususani Mudiri wa Idara ya Lugha na

Stadi za Mawasiliano, Dkt. Maria Mkunde Kanigi, kwa kunihamasisha. Mungu

awajalie thawabu maridhawa.

Tatu, shukrani zangu za dhati na za upendo zimwendee Dkt. Athumani Salum Ponera

wa Chuo Kikuu cha Dodoma, na baadaye Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu

Nyerere kwa ushauri na miongozo ya mara kwa mara aliyonipa kila nilipohitaji. Pia,

ninawashukuru sana Bw. Selestino Helman Msigala wa Chuo Kikuu cha Dar es

Salaam, Bi. Martina Duwe wa Chuo Kikuu Mzumbe, na Bw. Hassan Hassan wa

Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro, kwa kukubali kupitia na kutoa maoni na

ushauri ulioiboresha zaidi rasimu ya tasinifu hii. Vilevile, ninawashukuru wanafunzi

wenzangu wa Shahada ya Uzamivu Bw. Gervas Kasiga, Bi. Getrude Shima, Bi.

Johari Hakimu, Bi. Martina Duwe, na Bi. Tatu Khamis, kwa ushirikiano mzuri na

iv

kutiana moyo, hasa pale mambo yalipokatisha tamaa kutokana na ugumu wa safari

hii ya uzamivu. Mungu awalinde daima. Wengine wanaopaswa kushukuriwa ni

Regina Tanu wa Mwanza na Rozina Mugabe Bununja wa Ukerewe, kwa

makaribisho mazuri, kuniongoza na kunisaidia kuwapata kwa urahisi watafitiwa

wengine huko Namagondo na Murutunguru, Wilayani Ukerewe.

Tano, ninatoa shukrani zangu za upendo kwa mke wangu mpenzi, Mary Michael

Makongwa, pamoja na familia yangu kwa jumla. Kipekee hawa walionesha

uvumilivu na walinitia moyo, hasa pale nilipotaka kukata tamaa. Pia, walinisaidia

sana katika kipindi chote cha kufanyika kwa utafiti huu. Bila ya nguzo imara ya

familia yangu, huenda kazi hii isingeweza kuwa katika mwonekano huu, ikiwa ni

pamoja na kukamilika kwa wakati.

v

TABARUKU

Tasinifu hii naitabaruku kwa marehemu baba yangu mpenzi, Mzee Nanisa Benedikto

Fuluge. Baba, ninatamani sana leo hii ungekuwepo na kujionea kwa macho yako,

mbegu ya mafanikio uliyoipanda, ambayo sasa matunda yake ni bayana, kwani

yamekomaa na kuiva vilivyo. Mwenyezi Mungu, kwa mapenzi yake, aliutwaa uhai

wako kabla hata ya kushuhudia mafanikio haya. Baba, uangaziwe mwanga wa milele

na upumzike kwa amani. Amina.

Kwa mama yangu mpenzi, Betina Solomon se-Kalenga wa Iringa (Mapanda),

ulinizaa, ulinilea na kunifunza maadili mema ya utu, heshima, utii na uvumilivu.

Sina cha kukulipa zaidi ya kukupa hidaya hii na kukuombea fanaka katika maisha

yako. Unastahili heshima tele. Mungu akupe maisha marefu ya amani na furaha na

akujalie kila thawabu.

Kwa mke wangu mpenzi, Mary Michael Makongwa, pamoja na watoto wetu

wapenzi, Grace, Erick, Agnes na Brightness. Pokeeni zawadi ya upendo na ya

uvumilivu wenu kwangu.

vi

IKISIRI

Tasinifu hii ni matokeo ya utafiti wenye mada inayoitwa ―Usawiri wa Matukio ya

Mchakato wa Kujiua katika Riwaya Teule za Euphrase Kezilahabi: Ni Mwangwi wa

Mtanziko wa Kijamii?‖ Lengo kuu lilikuwa kuchunguza usawiri wa matukio ya

kujiua katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi kama ni mwangwi wa mtanziko

wa kijamii, au la. Malengo mahususi yaliyoshughulikiwa ni matatu: Mosi,

kubainisha usawiri wa matukio yanayounda mchakato wa kujiua katika riwaya teule

za Euphrase Kezilahabi; pili, kubainisha sababu za mitanziko ya wahusika

zinazosawiriwa katika riwaya teule; na tatu, kutathmini uhusiano baina ya usawiri wa

matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya

kujiua katika jamii. Ili kuyafikia malengo hayo, mbinu za aina mbili zilitumika

katika mchakato wa ukusanyaji wa data. Mbinu ya kwanza ilikuwa ni ukusanyaji wa

data za maktabani kwa kusoma na kuchambua kwa makini matini teule na magazeti

mbalimbali yenye taarifa zinazohusiana na mada ya utafiti. Pili, ilikuwa ni mbinu ya

mahojiano na watafitiwa iliyotumika kukusanya data za uwandani. Kimsingi,

shughuli nzima ya ukusanyaji wa data, uchanganuzi wake, na suala la kutafsiri

matokeo ya utafiti ilikitwa katika mkabala wa kitaamuli. Data hizo zilihakikiwa,

kuchanganuliwa na kupangwa katika mada ndogondogo kulingana na namna

zinavyooana kimaudhui. Nadharia za Udhanaishi na Sosholojia ya Kifasihi ndizo

zilizomwongoza mtafiti katika mchakato wa uchambuzi wa data zake.

Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba, matukio yanayosawiriwa katika riwaya

teule ndiyo yaliyounda mchakato wa kujiua kwa wahusika. Katika riwaya ya Rosa

Mistika matukio hayo yanamhusu Rosa Mistika; nayo ni: kupigwa na baba yake,

kuwachongea wasichana wenzake, kuota ndoto, kusimamishwa shule, kufumaniwa

na kufukuzwa chuo. Mengine ni kutoa mimba, kujitenga na kutengwa na jamii yake,

na kuachwa na mchumba wake. Kwa upande wa riwaya ya Kichwamaji matukio

hayo yanayohusu kujiua kwa Kazimoto ni: kunyimwa kazi, Rukia kutiwa mimba,

vifo vya Rukia na mama yake, na kifo cha Kalia. Matukio mengine ni kifo cha mtoto

wake, kuugua ugonjwa wa ajabu, na kujitenga kijamii. Matukio mengine ya kujiua

yanasawiriwa katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo na yanamhusu Tumaini,

yaani matukio ya aibu na fedheha, na tukio la Tumaini kumuua Mkuu wa Wilaya.

Pia, sababu mbalimbali za kijamii, kiutamaduni, kiuchumi, na kifalsafa, zimebainika

kuwa chanzo cha mtu kupata mitanziko ya kimaisha. Mitanziko hiyo husababisha

mtu huyo kuwa katika mkinzano wa mawazo, ambayo humpa wakati mgumu wa

kuamua la kufanya, kwa kuwa uamuzi wowote kwake huwa na madhara. Aidha,

utafiti umebaini kuwa kuna uhusiano mkubwa baina ya matukio ya mchakato wa

kujiua yaliyomo katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii

vii

kwa jumla. Uhusiano huo umebainishwa na kuwekwa katika makundi mawili. Mosi,

uhusiano wa sababu za matukio ya kujiua, ambazo ni kujiua kunakosababishwa na

athari za mahusiano ya kimapenzi, kujiua kunakosababishwa na athari katika malezi

na migogoro ya kifamilia, na kujiua kunakosababishwa na athari za magonjwa. Pili,

uhusiano wa njia zinazotumika katika kujiua. Njia hizo ni kujiua kwa kujinyonga,

kujipiga risasi, kujichoma kisu, na kwa kutumia sumu.

Mchango mpya wa utafiti huu ni pamoja na: Mosi, kubainishwa kwamba kujiua ni

mchakato na siyo tukio la ghafla kama ilivyofahamika awali kupitia tafiti

zilizotangulia miongoni mwa wanajamii. Pili, kuleta mtagusano wa kitaaluma kwa

kuzishikamanisha nyuga mbalimbali, zikiwamo Afya, Saikolojia, Sosholojia, na

Fasihi. Tatu, kinadharia na kiuchambuzi ambapo licha ya kuendeleza nadharia ya

Udhanaishi iliyozoeleka katika uchambuzi wa riwaya teule, nadharia ya Sosholojia

ya Kifasihi pia imetumika. Nne, kwa watunga sera na wakuza mitalaa kuweza

kuchukua hatua madhubuti na za pamoja katika kulishughulikia tatizo la watu kujiua

ili lisiendelee kuzikumba na kuziathiri jamii zetu.

viii

YALIYOMO

IKIRARI NA HAKIMILIKI ......................................................................................... i

ITHIBATI YA WASIMAMIZI ................................................................................... ii

SHUKRANI ................................................................................................................ iii

TABARUKU................................................................................................................ v

IKISIRI ........................................................................................................................ vi

YALIYOMO ............................................................................................................. viii

UFAFANUZI WA VIFUPISHO VILIVYOTUMIKA .............................................. xii

SURA YA KWANZA ................................................................................................. 1

UTANGULIZI WA JUMLA ..................................................................................... 1

1.1 Utangulizi ............................................................................................................... 1

1.2 Ufafanuzi wa Dhana Muhimu ................................................................................ 1

1.2.1 Mchakato ............................................................................................................. 1

1.2.2 Kujiua .................................................................................................................. 1

1.2.3 Riwaya................................................................................................................. 1

1.2.4 Mwangwi............................................................................................................. 3

1.2.5 Mtanziko ............................................................................................................. 3

1.3 Usuli wa Tatizo la Utafiti ....................................................................................... 4

1.4 Tamko la Tatizo la Utafiti ...................................................................................... 8

1.5 Malengo ya Utafiti ................................................................................................. 9

1.5.1 Lengo Kuu ........................................................................................................... 9

1.5.2 Malengo Mahususi ............................................................................................ 10

1.6 Maswali ya Utafiti ................................................................................................ 10

1.7 Manufaa ya Matokeo ya Utafiti ........................................................................... 10

1.8 Mawanda ya Utafiti .............................................................................................. 11

1.9 Muhtasari wa Sura ya Kwanza ............................................................................. 12

SURA YA PILI ......................................................................................................... 13

MAPITIO YA MAANDIKO NA KIUNZI CHA NADHARIA ........................... 13

2.1 Utangulizi ............................................................................................................. 13

2.2 Mapitio ya Maandiko ........................................................................................... 13

2.2.1 Mapitio Kuhusu Kazi za Kezilahabi kwa Jumla ............................................... 13

ix

2.2.2 Mapitio Kuhusu Mchakato wa Kujiua katika Riwaya za Kezilahabi ............... 18

2.2.3 Mapitio Kuhusu Dhana ya Kujiua kwa Mitazamo ya Nje ya Fasihi................. 22

2.2.4 Mwanya Uliotakiwa Kuzibwa na Utafiti .......................................................... 24

2.3 Viunzi vya Nadharia ............................................................................................ 24

2.3.1 Nadharia ya Udhanaishi .................................................................................... 25

2.3.1.1 Misingi ya Nadharia ya Udhanaishi ............................................................... 25

2.3.1.2 Nadharia ya Udhanaishi Ilivyotumika ........................................................... 26

2.3.2 Nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi ................................................................... 26

2.3.2.1 Misingi ya Nadharia ya Kisosholojia ............................................................. 28

2.3.2.2 Nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi Ilivyotumika .......................................... 28

2.4 Muhtasari wa Sura ya Pili .................................................................................... 29

SURA YA TATU ...................................................................................................... 30

METHODOLOJIA YA UTAFITI .......................................................................... 30

3.1 Utangulizi ............................................................................................................. 30

3.2 Usanifu wa Utafiti ................................................................................................ 30

3.3 Mkabala wa Utafiti ............................................................................................... 31

3.4 Eneo la Utafiti ...................................................................................................... 32

3.5 Walengwa wa Utafiti............................................................................................ 34

3.5.1 Wango la Utafiti ................................................................................................ 34

3.5.1.1 Usampulishaji ................................................................................................. 35

3.5.1.2 Sampuli ya Utafiti .......................................................................................... 36

3.6 Ukusanyaji wa Data ............................................................................................. 38

3.6.1 Njia za Ukusanyaji wa Data .............................................................................. 39

3.6.1.1 Usomaji na Uchambuzi Makini wa Matini .................................................... 39

3.6.1.2 Mahojiano ...................................................................................................... 39

3.6.2 Mchakato wa Ukusanyaji Data ......................................................................... 40

3.7 Mbinu za Uchambuzi wa Data ............................................................................. 41

3.8 Itikeli za Utafiti .................................................................................................... 42

3.9 Uhalali na Uthabiti wa Matokeo ya Utafiti .......................................................... 43

3.10 Muhtasari wa Sura ya Tatu ................................................................................ 43

x

SURA YA NNE ......................................................................................................... 44

UWASILISHAJI WA DATA NA MJADALA WA MATOKEO YA UTAFITI 44

4.1 Utangulizi ............................................................................................................. 44

4.2 Matukio ya Mchakato wa Kujiua katika Riwaya Teule za Euphrase

Kezilahabi ....................................................................................................... 44

4.2.1 Muhtasari wa Riwaya ya Rosa Mistika ............................................................. 45

4.2.1.1 Kupigwa na Baba yake................................................................................... 47

4.2.1.2 Kuwachongea Wasichana Wenzake .............................................................. 50

4.2.1.3 Kuota Ndoto ................................................................................................... 52

4.2.1.4 Kusimamishwa Shule, Kufumaniwa na Kufukuzwa Chuo ............................ 55

4.2.1.5 Kutoa Mimba ................................................................................................. 58

4.2.1.6 Kujitenga na Kutengwa na Jamii yake ........................................................... 59

4.2.1.7 Kuachwa na Mchumba Wake ........................................................................ 61

4.2.2 Muhtasari wa Riwaya ya Kichwamaji............................................................... 68

4.2.2.1 Tukio la Kunyimwa Kazi ............................................................................... 69

4.2.2.2 Rukia Kutiwa Mimba ..................................................................................... 72

4.2.2.3 Vifo vya Rukia na Mama Yake ...................................................................... 75

4.2.2.4 Kifo cha Kalia ................................................................................................ 78

4.2.2.5 Kifo cha Mtoto Wake ..................................................................................... 81

4.2.2.6 Kazimoto Kuugua Ugonjwa wa Ajabu .......................................................... 83

4.2.2.7 Kujitenga Kijamii ........................................................................................... 85

4.2.3 Muhtasari wa Riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo ............................................ 88

4.2.3.1 Matukio ya Aibu na Fedheha ......................................................................... 89

4.2.3.2 Tukio la Tumaini Kumuua Mkuu wa Wilaya ................................................ 92

4.3 Sababu za Mitanziko ya Wahusika katika Riwaya Teule za Euphrase

Kezilahabi ....................................................................................................... 96

4.3.1 Sababu za Kijamii ............................................................................................. 96

4.3.1.1 Mahusiano ya Kimapenzi ............................................................................... 96

4.3.1.2 Mfumo wa Malezi ........................................................................................ 111

4.3.2 Sababu za Kiutamaduni................................................................................... 123

4.3.2.1 Suala la Mila na Desturi ............................................................................... 124

4.3.2.2 Suala la Dini ................................................................................................. 135

4.3.2.3 Tatizo la Ndoa na Uzazi ............................................................................... 138

xi

4.3.3 Sababu za Kiuchumi ....................................................................................... 147

4.3.4 Sababu za Kifalsafa ......................................................................................... 155

4.3.4.1 Dhana ya Maisha .......................................................................................... 155

4.3.4.2 Dhana ya Kifo .............................................................................................. 160

4.3.4.3 Dhana Kuhusu Mungu ................................................................................. 166

4.4 Uhusiano wa Mchakato wa Kujiua katika Fasihi na Uhalisi katika Jamii ......... 175

4.4.1 Uhusiano wa Sababu za Matukio ya Kujiua ................................................... 176

4.4.1.1 Kujiua Kunakosababishwa na Athari za Mahusiano ya Kimapenzi ............ 178

4.4.1.2 Kujiua Kunakosababishwa na Athari katika Malezi na Migogoro ya

Kifamilia ....................................................................................................... 181

4.4.1.3 Kujiua Kunakosababishwa na Athari za Magonjwa .................................... 185

4.4.2 Uhusiano wa Njia Zinazotumika katika Kujiua .............................................. 187

4.4.2.1 Kujiua kwa Kujinyonga ............................................................................... 188

4.4.2.2 Kujiua kwa Kujipiga Risasi ......................................................................... 194

4.4.2.3 Kujiua kwa Kujichoma Kisu ........................................................................ 198

4.4.2.4 Kujiua kwa Kutumia Sumu .......................................................................... 199

4.5 Muhtasari wa Sura ya Nne ................................................................................. 202

SURA YA TANO.................................................................................................... 204

MUHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO ......................................... 204

5.1 Utangulizi ........................................................................................................... 204

5.2 Muhtasari wa Tasinifu Hii ................................................................................. 204

5.3 Hitimisho la Tasinifu Hii ................................................................................... 207

5.3.1 Utoshelevu wa Nadharia Zilizotumika............................................................ 207

5.3.2 Mchango Mpya wa Matokeo ya Utafiti Huu .................................................. 208

5.3.3 Mapendekezo Kuhusu Tafiti Zijazo ................................................................ 209

MAREJELEO ........................................................................................................ 211

VIAMBATISHO .................................................................................................... 223

xii

UFAFANUZI WA VIFUPISHO VILIVYOTUMIKA

BAKITA Baraza la Kiswahili la Tanzania

BAKIZA Baraza la Kiswahili la Zanzibar

Bi. Bibi

Bw. Bwana

Co. Company

Dkt. Daktari

DSM Dar es Salaam

DUP Dar es Salaam University Press

EALB East African Literature Bureau

EAPH East African Publishing House

Http Hyper Text Transfer Protocal

IFAMU Idara ya Fasihi, Mawasiliano na Uchapishaji

Juz. Juzuu

Kur. Kurasa

Ltd Limited

M.A Master of Arts

MUM Muslim University of Morogoro

Na. Namba

No. Number

Ph.D Doctor of Philosophy

Prof. Profesa

TATAKI Taasisi ya Taaluma za Kiswahili

Tol. Toleo

TPH Tanzania Printing House

TUKI Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili

UDOM University of Dodoma

UDSM University of Dar es Salaam

Uk Ukurasa

Vol. Volume

1

SURA YA KWANZA

UTANGULIZI WA JUMLA

1.1 Utangulizi

Sura hii inayojenga msingi wa tasinifu ina sehemu saba. Imeanza kwa kufafanua

dhana za msingi zilizotumika katika utafiti huu kwa lengo la kuweka msingi wa

uelewekaji wake kwa wasomaji. Sehemu nyingine ni usuli wa tatizo la utafiti, tamko

la tatizo utafiti, malengo ya utafiti, maswali ya utafiti, manufaa tarajiwa, pamoja na

mawanda ya utafiti.

1.2 Ufafanuzi wa Dhana Muhimu

Sehemu hii inafafanua dhana muhimu zilizotumika katika tasinifu hii. Ufafanuzi huo

umetolewa kwa kuzingatia mitazamo na maoni ya wataalamu mbalimbali, na

baadaye, mtafiti kutoa maana ya jumla kulingana na namna alivyokusudia kuzitumia

katika kazi yake. Dhana zilizotolewa ufafanuzi ni hizi zifuatazo:

1.2.1 Mchakato

TUKI (2014) inafafanua kuwa mchakato ni nomino inayomaanisha mfululizo wa

shughuli unaosababisha kitu fulani kufanyika au lengo fulani kufikiwa. Hii ina

maana kuwa mchakato ni kitendo cha kufanya jambo au kitu fulani hatua kwa hatua,

kwa lengo la kusababisha kitu kingine kitokee, kikiwa na hali au umbo jipya tofauti

na lile lililokuwapo awali. Katika tasinifu hii, dhana hii imetumika kumaanisha jumla

ya matukio, mitanziko na miktadha inayohusiana na maisha ya mtu hadi kuchukua

maamuzi ya kujiua.

1.2.2 Kujiua

BAKIZA (2010) linaeleza kuwa dhana ya ‗kujiua‘ inatokana na kitenzi ‗ua‘ chenye

maana ya kutoa roho ya mja au kufisha. Kulingana na utafiti huu, kujiua ni kitendo

cha mtu kuiangamiza roho kwa kupoteza uhai wake (kufa). Hivyo, dhana ya kujiua

imechunguzwa kwa kuzingatia matukio mbalimbali aliyopitia mhusika hadi kufikia

maamuzi ya kujiua.

1.2.3 Riwaya

Dhana ya riwaya ni tata, kwani hakuna namna moja ya kuielezea. Hii inatokana na

ukweli kwamba pamekuwa na mgogoro wa fikra miongoni mwa wataalamu wa uga

huu kuhusiana na maana halisi ya riwaya. Aidha, wataalamu hao bado

2

hawajakubaliana kuhusu namna ya kuzigawa au kuziainisha riwaya kitanzu. Baadhi

ya wataalamu waliofasili dhana hii ni Mphahlele (1976), Muhando na Balisidya

(1976), Njogu na Chimerah (2008) na Madumulla (2009). Kwa mfano, Mphahlele

(1976) anaeleza kuwa, riwaya ni utanzu wenye maneno kati ya 35,000 na 75,000 au

zaidi. Anaona kuwa, kazi yoyote yenye maneno pungufu ya idadi hiyo haifai kuitwa

riwaya. Maelezo haya hayatofautiani sana na yale ya Muhando na Balisidya (1976)

wanaofafanua kuwa:

… Riwaya yaweza kuanzia maneno 35,000 hivi na kuendelea,

lakini tukisema juu ya urefu na tukaishia hapo tu, jambo hili

halitakuwa na maana. Maana mtu yeyote aweza kuweka habari

yoyote ile katika wingi wa maneno kama hayo. Jambo

muhimu hapa ni kuwa riwaya huwa na mchangamano wa

matukio, ujenzi wa wahusika na dhamira, muundo wake na

hata mtindo (mitindo inayotumiwa) maalumu… Si ajabu kuwa

utunzi wa riwaya wategemea sana jamii yenye ujuzi wa

kuandika kama zana bora ya kuhifadhi (uk. 63).

Ufafanuzi wa Muhando na Balisidya una uzito zaidi ya ule wa Mphahlele, kwa

sababu wao wanaenda hatua kadhaa mbele. Wanaeleza kwamba kinachotakiwa

kuzingatiwa si urefu au wingi wa maneno pekee, bali mchangamano wa matukio,

ujenzi wa wahusika na dhamira, muundo wake, pamoja na mtindo maalumu.

Kwa upande wake, Madumulla (2009) anaeleza kuwa dhana ya riwaya ni telezi

kuifafanua, kwa sababu hubadilika kulingana na mabadiliko ya jamii. Anabainisha

kuwa kuna namna mbili ya kufafanua maana ya riwaya. Namna ya kwanza, ni

ufafanuzi wa riwaya kwa kujikita katika kamusi. Kimsingi, ufafanuzi huu huhitaji

maelezo mafupi ya kiufafanuzi. Namna ya pili ni ufafanuzi unaojikita katika sifa

bainifu zinazoupambanua utanzu huo. Anataja baadhi ya sifa zinazoitambulisha

riwaya kuwa ni matumizi ya lugha ya kinathari, kutofungwa na sheria, urefu na

upana, pamoja na kuwa karibu na uhalisi wa maisha ya jamii.

Kwa jumla, ufafanuzi wa riwaya kulingana na wataalamu hao unadhihirisha kuwa,

riwaya ni andiko ambalo huwa na sifa zifuatazo: masimulizi ya kubuni (ubunifu),

hadithi au simulio la kinathari (usimulizi) na mpangilio au msuko fulani wa matukio

(ploti). Sifa nyingine ni ufungamano na wakati (visa hutendeka katika wakati fulani),

urefu, mawanda mapana (mada zinazozungumziwa, ya wakati, na mahali pa matukio

hayo), na uchangamano (wa visa, dhamira, na wahusika). Katika tasinifu hii, riwaya

3

imerejelewa kuwa ni kazi ya kisanaa inayoandikwa kwa kutumia lugha ya kibunifu.

Kazi hiyo huwa na mawanda mapana katika kuelezea mambo kwa kina. Aidha, ina

uchangamani wa visa na matukio, wahusika, na mandhari, ambayo husawiri maisha

ya watu kulingana na mazingira yao.

1.2.4 Mwangwi

Ni sauti inayorudi baada ya mawimbi ya sauti kugonga mahali na kumrudia

mzungumzaji ambayo, aghalabu, hutokea pangoni, msituni, au kwenye jengo kubwa

na tupu (BAKITA, 2017). Pia, sauti hiyo huweza kusambaa au kutawanyika kwenda

umbali fulani kulingana na ukubwa wa chanzo chake. Katika tasinifu hii, dhana hii

imetumika katika kuchunguza iwapo matukio mbalimbali yanayotokea katika jamii

ni sababu ya watu kuchukua uamuzi wa kujiua au la.

1.2.5 Mtanziko

BAKITA (2017) linaeleza kuwa mtanziko ni dhana inayotokana na kitenzi ‗tanza‘,

ikiwa na maana ya kutatanisha au kushindwa kueleweka vizuri kwa ujumbe uliomo

katika jambo au tukio. Kwa maneno mengine, mtanziko ni hali ya kutatiza,

kukanganya, au kuhangaisha. Dhana hii ambayo katika lugha ya Kiingereza huitwa

―dilemma‖ katika Fasihi iliasisiwa na Sletteboe (1997). Mtaalamu huyu anaielezea

dhana hii kuwa ni hali ya mhusika kuwa katika mkinzano wa mawazo, ambayo

humpa wakati mgumu wa kuchagua la kufanya, kwa sababu uamuzi wowote

anaoamua kuuchukua huwa na madhara kwake. Anaongeza kuwa kuna namna tatu

za mtu mwenye mtanziko, ambazo ni: Mosi, kuwa katika hali kuu mbili au zaidi za

kufanyia uamuzi au uchaguzi. Hoja hii inaungwa mkono na Madumulla (2009)

anayeeleza kuwa, mtu akiwa katika mtanziko mara nyingi, husukumwa katika

ukingo wa kuamua kati ya kufa na kuyaepuka matatizo, au kuishi ili kuendelea na

maisha kwa uvumilivu, yaani hulazimika kufanya uchaguzi kati ya mambo mawili

magumu (dilemma). Kwa mfano, kutosikiliza wosia wa wazazi na kufanya jambo

ambalo jamii inakataza. Pili, uamuzi ambao mhusika hajui matokeo yake

yatakuwaje. Tatu, uamuzi ambao mhusika hajui jambo au uamuzi sahihi ni upi.

Sletteboe anafafanua zaidi kuwa, ili kuufikia uamuzi huo, mhusika hujiuliza maswali

kama vile: kwanza, nataka kufanya au kuchukua uamuzi gani? Na pili, kitu gani ni

sahihi kinachotakiwa kufanyika? Kwa hiyo, kutanzika ni kuwa katika hali ya

4

kushindwa kuamua juu ya jambo fulani, yaani kuwa katika mkinzano wa mawazo

katika kufanya uamuzi wa jambo.

Kwa muktadha wa utafiti huu, dhana hii imetumika kumaanisha athari za matukio

mabaya au ya hatari, ambayo huleta masikitiko, majonzi, huzuni au msiba katika

jamii. Athari hizo huweza kusababisha mtu kuwa katika hali ya kushindwa kuamua

(mtanziko) juu ya jambo fulani.

1.3 Usuli wa Tatizo la Utafiti

Fasihi husawiri ulimwengu kulingana na jadi pamoja na hali ya maendeleo ya jamii,

na hivyo kuzifanya kazi za fasihi kufungamana na muktadha uliozizaa. Mtunzi

huumba kazi yake ya kifasihi kwa kuzingatia mambo yanayoihusu jamii kwa kuwa

fasihi haiwezi kukwepa kaida za jamii husika. Hii inayakinisha hoja kuwa, fasihi ni

zao la jamii. Kwa mantiki hiyo, maisha halisi ndio msingi na mzazi wa fasihi. Dhima

ya jumla ya fasihi ni kusawiri kisanaa hali ya mwanadamu, mazingira yake, uhusiano

wake na mazingira hayo, mahusiano yake ya kijamii, hisia na mawazo yake, kwa

lengo la kuonesha hali ilivyo, kuelewesha, na hata kuleta mabadiliko (Mulokozi,

2017). Ufafanuzi huu unalenga kutoa dira kuwa dhima ya fasihi inatakiwa

kusawiriwa kwa kigezo cha jamii mahususi. Hoja hii haitofautiani na mawazo ya

Selden na wenzake (2005) wanaoeleza kuwa usawiri huo haupaswi kuwa wa tukio

mojamoja, bali kama mchakato mzima wa maisha ya jamii. Wanaongeza kuwa,

msomaji hutakiwa kuchukua tahadhari kutokana na ukweli kuwa kazi ya sanaa siyo

huo ukweli, bali ni njia ya kuakisi ukweli.

Watafiti mbalimbali kama vile Wellek na Warren (1949) na Escarpit (1974)

wanabainisha kuwapo kwa uhusiano baina ya fasihi na jamii. Wanaeleza kuwa

uhusiano huo unatokana na ukweli kwamba, pindi maisha ya jamii yabadilikapo,

mielekeo, tamaduni, pamoja na maadili ya jamii nayo hubadilika. Kwa kuwa fasihi ni

kielelezo cha maisha ya jamii, ni muhimu kuichukulia sanaa hiyo kama zao la jamii,

ambalo pia huweza kuathiri na kuathiriwa na jamii husika. Hoja hii inaungwa mkono

na Vasquez (1973) anaposema kuwa:

… kazi ya fasihi huathiri watu na inachangia katika kuhimiza

au kupuuza dhana zao, maazimio yao, hata maadili yao – ina

msukumo wa kijamii ambao huathiri watu kwa nguvu zake za

5

kihisia na kiitikadi. Ama kwa hakika, hakuna anayebaki kama

alivyokuwa baada ya ‗kuguswa‘ na kazi halisi ya fasihi.

Ni wazi kwamba uwezo wa Fasihi katika kusawiri mambo mbalimbali kama vile

mazingira, uchumi, siasa, mila na desturi, maadili, na saikolojia huweza kuiteka

hadhira na hata kuisababisha ibadili mienendo yake ya maisha. Kwa hali hiyo,

mtunzi anapotunga kazi yake huunganisha vipengele mbalimbali vya uhalisi

kulingana na uwezo alio nao katika kuwasilisha uhalisi huo, hata kama asili hiyo

haikusawiriwa kwa ukamilifu. Hivi ndivyo anavyofanya Euphrase Kezilahabi katika

utunzi wa kazi zake za mwanzo ambazo ni: Rosa Mistika (1971), Kichwamaji

(1974), na Dunia Uwanja wa Fujo (1975). Katika riwaya hizo anasawiri hali ya

mazingira ya jamii yake, kwa kutuibulia matukio ya kujiua.

Kulingana na Shirika la Afya Duniani (2018) na gazeti la Habari Leo la Novemba 5

(2018), kujiua ni janga linalotokea kila siku duniani kote na linawaathiri watu wa

mataifa, tamaduni, jinsi, dini, na matabaka yote. Janga hili linapotokea husababisha

huzuni, majonzi, na matatizo makubwa kwa jamii, hususani katika familia ya

mhusika. Kutokana na hilo, mara nyingi watu hujiuliza maswali mengi wanaposikia

kuwa mtu fulani amejiua. Hujiuliza maswali hayo kwa sababu suala la kujiua ni

gumu, linatisha, na linaogofya. Hii inatokana na namna kila binadamu

anavyoyatazama na kuyapa thamani maisha na mchakato mzima wa kuishi kwake.

Katika hali ya kawaida, kujiua huchukuliwa kama kitendo cha ghafla kinaposikika

masikioni mwa watu. Hata hivyo, kwa maoni yetu, tunaona kuwa kitendo hiki huwa

ni mchakato kwa anayejiua, kwa sababu kabla ya kuchukua uamuzi huo, mhusika

hupitia matukio, mitanziko na miktadha mbalimbali ya kimaisha. Maoni haya

yanaendana na yale ya Muller (1964) na Freeman (1971) wanaoeleza kuwa

mwanadamu huendelea kufa polepole tangu anapozaliwa. Hii inatokana na ukweli

kwamba maisha ya binadamu ni sawa na kitendawili kigumu ambacho jibu lake si

rahisi kulipata. Kutokana na hilo, siku zote binadamu huyo huwa katika mchakato

wa kutaka kutatua kitendawili hicho. Hii ni kwa sababu maisha kwake ni fumbo.

Hali hiyo ya maisha ya binadamu kuwa fumbo ndiyo inayosababisha pia asawiriwe

kwa namna mbalimbali. Kwa mfano, Wamitila (2002) anamsawiri binadamu kama

kiumbe anayeteseka na anayeishi katika ulimwengu usiomjali, aliyezungukwa na

mateso na ubwege, na anayeshindwa kukabiliana au kupatana vyema na uhalisi huo.

6

Hali hiyo ya kuzungukwa na mateso na ubwege huenda ndicho kichocheo cha

kuamua hata kujiua.

Tafiti mbalimbali zinabainisha kuwa kujiua ni tatizo la kisaikolojia linalohusishwa

na michakato kadhaa ya kiafya ambayo hushambulia mfumo wa akili (Freud, 1900;

Ndosi na wenzake, 2004; Glucksman & Kramer, 2017). Zinafafanua zaidi kuwa

msongo wa mawazo, ambao ni tatizo la kisaikolojia, ni chanzo kimojawapo

kinachosababisha mtu kujiua. Hii ni kwa sababu humweka mtu huyo katika hali ya

hofu au wasiwasi kutokana na kuzidiwa na mawazo kwa kukosa jibu la kitu

kilichoko mbele yake au kichwani mwake. Freud (1900) anaeleza kuwa binadamu

huwa na sehemu inayofahamika kama ‗ung‘amuzibwete‘ wa kibinafsi, ambapo fikra

nyingi na mawazo mengi hasi hubuniwa na kuhifadhiwa. Mtaalaamu huyo

anafafanua zaidi kuwa sehemu ya akili ya binadamu huhodhi fikra, mawazo, hofu na

mitazamo hasi, ambayo haiwezi kukubalika katika jamii. Anahusisha masuala ya

saikolojia na ndoto. Anaona kuwa, ndoto huhusisha matukio yaliyotendeka zamani

yanayosheheni maana na ukweli kuhusu maisha. Anaongeza kuwa, kupitia ndoto,

mtu anaweza kukiuka miiko aliyowekewa na kujikamilishia utashi pasipo kukatizwa

wala kukatazwa na wanajamii wengine. Hii ni kwa sababu mwota ndoto, wakati

mwingine, huamini kwamba anayoyaota ni kweli. Hali hiyo huweza kumsababishia

mhusika kuchukua uamuzi autakao, ikiwamo kujiua.

Aidha, wataalamu mbalimbali wamelishughulikia zaidi suala la kujiua kwa jicho la

kisosholojia, kisaikolojia na kiafya (Durkheim, 1979; Practorius, 2006; Tiwari &

Ruhela, 2012; Glucksman & Kramer, 2017; na Shirika la Afya Duniani, 2018).

Baadhi yao kama vile Williams (1970), Friedman (1973), Durkheim (1979),

Neubeck (1986), na Stack (1987) wanabainisha kuwa watu wengi hujiua kutokana na

hali ya kukata tamaa, pamoja na matatizo ya kiakili. Wengine kama vile Glucksman

& Kramer (2017) wanabainisha kuwa kujiua huchochewa na sababu mbalimbali,

zikiwamo za kitabia, kijamii, kibaiolojia, na kiutamaduni; na kwamba, ni vigumu

kumbainisha na kumtambua mtu anayepanga kujiua. Wanataja baadhi ya sababu za

mtu kujiua kuwa ni sonona, maradhi ya hisia mseto, sikizofrenia, matumizi ya dawa

za kulevya, na matumizi mabaya ya pombe na vilevi vingine. Hata hivyo,

wanatahadharisha kuwa, siyo mara zote kujiua ni ishara ya maradhi ya akili.

7

Pia, siyo mara zote maradhi ya akili huweza kusababisha mtu kujiua. Wanabainisha

kuwa kila mtu anayeamua kujiua huwa na sababu zake binafsi zinazomsukuma

kuchukua uamuzi huo. Wanaongeza kuwa, mtu huyo anapobaini kuwa ametengwa

kutokana na mabadiliko ya ghafla ama ya kijamii, kihisia, au kiuchumi,

huchanganyikiwa na huweza kuamua kujiua (Durkheim, 1979). Licha ya tafiti hizo

kufanyika kulingana na malengo yaliyomsukuma kila mhusika, hakuna utafiti

unaoelezea kwa uwazi, matukio yanayounda mchakato wa kujiua na namna

yanavyosawiriwa katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi. Pia, hapajawa na

utafiti wa wazi unaobainisha kama kujiua ni mwangwi wa mtanziko wa kijamii, au

la.

Kimsingi, mchakato wa kujiua unatakiwa pia kushughulikiwa kwa kina katika fasihi,

ikiwamo riwaya, kutokana na ukubwa wa tatizo lenyewe. Tafiti mbalimbali

zinabainisha kuwa kujiua ni tatizo kubwa na linaendelea kukua duniani kote.

Zinafafanua zaidi kwamba lisipofanyiwa kazi kwa kina, litaendelea kuziathiri jamii

nyingi duniani kote, ikiwa ni pamoja na kupoteza nguvu-kazi katika jamii zetu. Kwa

mujibu wa Shirika la Afya Duniani (2018), watu laki nane (800,000) hadi milioni

moja (1,000,000) kila mwaka hujiua duniani kote, huku wengine wengi wakifanya

majaribio ya kujiua. Utafiti huo unaitaja nchi ya Sri Lanka kuwa kinara kwa watu

wake kujiua ikiwa na asilimia 35.3, ikifuatiwa na Lithuania yenye asilimia 32.7, na

Guyana asilimia 29. Kwa upande wa Afrika nchi inayoongoza ni Angola yenye

asilimia 20.5, ikifuatiwa na Afrika ya Kati asilimia 17.5, na Eswatin (zamani ilikuwa

inaitwa Swaziland) yenye asilimia 14.7. Katika Afrika Mashariki, Rwanda inaongoza

kwa kuwa na asilimia 8.5, ikifuatiwa na Burundi asilimia 8, Uganda asilimia 7.2, na

Tanzania asilimia 7. Aidha, ripoti hiyo inabainisha kuwa kitendo hiki cha watu

kujiua kinajitokeza katika marika yote, ingawa kundi linaloongoza ni la vijana wenye

umri kati ya miaka kumi na mitano na ishirini na tisa (15 - 29). Mtafiti anatambua

kuwa ripoti hiyo ni ya kisosholojia, lakini kwa kuwa inazihusu jamii zetu,

alilazimika kulichunguza jambo hilo kwa mwegamo wa kifasihi pia. Hii inatokana na

ukweli kuwa Fasihi ni sanaa ya lugha yenye ubunifu inayojaribu kusawiri vipengele

vya maisha, mahusiano, mazingira na hisia za watu katika muktadha fulani

(Mulokozi, 2017).

8

Kama ilivyobainishwa katika ripoti ya Shirika la Afya Duniani hapo juu, nchi ya

Tanzania pia inakumbwa na tatizo la watu kujiua na linazidi kukua na kuongezeka

mwaka hadi mwaka. Katika kuthibitisha ukubwa wa tatizo hilo, gazeti la Habari Leo

(2018) linaeleza kwamba watu wanaojiua hapa nchini idadi yao ni kubwa na

linatisha. Taarifa hiyo inazidi kubainisha kuwa idadi ya watu waliojiua kwa

kujinyonga kuanzia mwaka 2016 hadi Juni mwaka 2018 ni mia tatu thelathini na tatu

(333). Inazidi kubainisha kuwa idadi ya watu waliojiua mwaka 2016 ni 131. Uwiano

wa kijinsi ni kama ifuatavyo: Mwaka 2016 wanaume walikuwa 106 na wanawake

25. Mwaka 2017 wanaume 81 na wanawake 7, na mwaka 2018 kuanzia mwezi

Januari hadi Juni, matukio ya kujiua yaliongezeka hadi kufikia 113. Taarifa hiyo

inaitaja Mikoa iliyoongoza kwa watu kujiua kwa kujinyonga kuwa ni Mwanza

matukio 29, Mbeya matukio 18, Dodoma matukio 11, Tabora matukio 11, na

Shinyanga matukio 8. Ikumbukwe kuwa matukio haya ni yale tu yaliyoweza

kuripotiwa na kumbukumbu zake kuhifadhiwa, kwani inawezekana kabisa kuwa

yako mengine ambayo hayakuripotiwa.

Kushamiri kwa tatizo hilo duniani kote, ikiwamo Tanzania, kulileta hamasa na

msukumo wa kufanyika kwa utafiti huu. Msukumo huu ulitokana na ukweli kwamba,

licha ya tatizo hili kushughulikiwa zaidi katika nyuga za Afya, Saikolojia na

Sosholojia, bado linaendelea kushamiri siku hadi siku. Aidha, tafiti za Fasihi ya

Kiswahili zilikuwa hazijabainisha kwa uwazi matukio ya mchakato wa kujiua

pamoja na sababu za mitanziko ya wahusika katika riwaya teule. Pia, uhusiano wa

matukio ya mchakato wa kujiua yanayosawiriwa katika riwaya teule na vichocheo

vya matukio ya kujiua katika jamii haukutathminiwa. Kutokana na hilo, mtafiti

alipata hamasa ya kulishughulikia suala hili kwa mwegamo wa kifasihi kama njia

mojawapo ya kutoa mchango wa uga huu wa Fasihi katika jitihada za kulipatia

suluhisho tatizo hili. Kwa hiyo, utafiti huu ulikusudia kuchunguza usawiri wa

mchakato wa kujiua katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi, ili kubaini kama

kujiua huko ni mwangwi wa mtanziko wa kijamii, au la.

1.4 Tamko la Tatizo la Utafiti

Tafiti mbalimbali za kisosholojia, kisaikolojia na kiafya zimefanyika kuhusu tatizo

la kujiua (Durkheim, 1979; Practorius, 2006; Tiwari & Ruhela, 2012; Glucksman &

Kramer, 2017; na WHO, 2018). Miongoni mwa hizo zililenga kuchunguza ukubwa

9

wa tatizo la watu kujiua, sababu za jumla za kujiua, pamoja na athari zitokanazo na

mtu kujiua. Katika Fasihi ya Kiswahili, tatizo hili la kujiua halijashughulikiwa kwa

kina. Mathalani, tafiti chache zimefanyika kuhusiana na dhana ya maisha kwa jumla

ikihusishwa na nadharia ya udhanaishi. Baadhi ya wataalamu waliolishughulikia

suala hili katika Fasihi ya Kiswahili ni Mulokozi (1983 & 2010), Musau (1985),

Mlacha (1985), Madumulla (1993), Mbatiah (1998), Wamitila (2003), Senkoro

(2007), na Fuluge (2013).

Licha ya tafiti hizo kufanyika na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike, bado lipo

tatizo la watu kujiua kama ilivyofafanuliwa kwenye ripoti ya utafiti uliofanywa na

Shirika la Afya Duniani (2018) na Habari Leo (2018), kama ilivyokwishaelezwa

katika usuli wa tasinifu hii. Kutokana na hali hiyo, zinahitajika jitihada za pamoja

katika kukabiliana nalo, kwani kama halitashughulikiwa kwa kina, litaendelea

kuziathiri jamii zetu, hususani vijana ambao ni nguvu-kazi ya taifa. Pamoja na kuwa

dhima mojawapo ya Fasihi ni kusawiri kisanaa hali ya mwanadamu, mazingira yake,

uhusiano wake na mazingira hayo na hata kuleta mabadiliko bado katika Fasihi ya

Kiswahili hapajawa na utafiti wa kina uliofanyika kwa lengo la kulisawiri tatizo la

kujiua kwa umahsusi wake na kutoa elimu ya namna ya kukabiliana nalo kwa jamii.

Aidha, matukio ya mchakato wa kujiua na sababu za mitanziko ya wahusika

zinazosawiriwa katika kazi za Fasihi hazijabainishwa wazi. Pia, hakuna utafiti

uliofanyika kwa lengo la kutathmini uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya

mchakato wa kujiua katika kazi za fasihi na vichocheo vya matukio ya kujiua katika

jamii. Hivyo, utafiti huu ulilenga kuchunguza usawiri wa matukio ya mchakato wa

kujiua katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi ili kubaini kama kujiua huko ni

mwangwi wa mtanziko wa kijamii au la.

1.5 Malengo ya Utafiti

Tasinifu hii iliongozwa na lengo kuu na malengo mahususi.

1.5.1 Lengo Kuu

Lengo kuu la tasinifu hii lilikuwa kuchunguza usawiri wa mchakato wa kujiua katika

riwaya teule za Euphrase Kezilahabi kama ni mwangwi wa mtanziko wa kijamii, au

la.

10

1.5.2 Malengo Mahususi

a) Kubainisha namna matukio yanayounda mchakato wa kujiua katika riwaya

teule za Euphrase Kezilahabi yanavyosawiriwa;

b) Kubainisha sababu za mitanziko ya wahusika zinazosawiriwa katika riwaya

teule za Euphrase Kezilahabi;

c) Kutathmini uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua

katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii.

1.6 Maswali ya Utafiti

Maswali yaliyoongoza utafiti huu na kuwezesha kufikiwa kwa malengo mahususi

yaliyokusudiwa ni haya yafuatayo:

a) Matukio yanayounda mchakato wa kujiua katika riwaya teule za Euphrase

Kezilahabi yanasawiriwa namna gani?

b) Sababu za mitanziko ya wahusika zinazosawiriwa katika riwaya teule za

Euphrase Kezilahabi ni zipi?

c) Kuna uhusiano gani baina ya usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua

katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii?

1.7 Manufaa ya Matokeo ya Utafiti

Matokeo ya utafiti uliofanyika yatakuwa na manufaa makubwa katika uga wa Fasihi

na jamii kwa jumla. Manufaa hayo ni pamoja na:

Mosi, kusaidia jamii kufahamu matukio ya mchakato wa kujiua, sababu za mitanziko

ya wahusika kujiua katika jamii, pamoja na athari za miktadha mbalimbali ya maisha

ya jamii anayopitia mhusika katika maisha yake, ambayo huweza kusababisha

mhusika kufikia maamuzi ya kujiua. Kufahamika kwa matukio, sababu na athari za

miktadha hiyo kutawezesha jamii kupata elimu juu ya masuala ya kujiua, na hivyo

kupunguza tatizo hilo.

Pili, kwa kuwa uchambuzi ambao umefanyika umeonesha mtagusano wa kitaaluma

kwa kuzishikamanisha nyuga za Afya, Saikolojia, Sosholojia, na Fasihi, mwingiliano

huo wa kitaaluma utaongeza ufahamu zaidi kwa watafiti wengine kutambua kuwa

matatizo ya kisosholojia, kama lilivyo la kujiua, yanaweza pia kushughulikiwa katika

11

uga wa Fasihi na nyuga nyinginezo za kitaaluma, na hivyo kupatiwa masuluhisho

kwa haraka na kwa ufanisi zaidi.

Tatu, inatarajiwa kuwa tasinifu hii italeta manufaa kinadharia na kiuhakiki. Kwa

upande wa nadharia, licha ya kuendeleza nadharia ya kidhanaishi ambayo

imezoeleka katika uhakiki na uchambuzi wa kazi za Euphrase Kezilahabi, pia utafiti

huu umetumia nadharia nyingine, ambayo ni Sosholojia ya Kifasihi. Kabla ya

kufanyika kwa utafiti huu, kulingana na upeo wa mtafiti, nadharia hii ilikuwa

haijawahi kutumika katika uhakiki wa riwaya teule za Euphrase Kezilahabi. Aidha,

tasinifu hii imependekeza nadharia nyingine zinazofaa katika uhakiki wa kazi zenye

mwelekeo wa kidhanaishi. Nadharia hizo ni pamoja na: nadharia ya korasi, nadharia

ya usimulizi, nadharia ya simiotiki, nadharia ya uhalisia, na nadharia ya Saikolojia

changanuzi. Kutumiwa kwa nadharia hizo katika uhakiki wa kazi za Euphrase

Kezilahabi, kutasaidia kubainisha mambo mengine yanayosawiriwa katika kazi hizo

katika kuihakiki jamii.

Nne, matokeo ya utafiti huu yanatarajiwa kuwa na faida kwa watafiti wengine, kwani

yataongeza hamasa ya kufanyika kwa tafiti nyingine zenye mwelekeo wa kuzihakiki

jamii katika nyanja mbalimbali. Kichocheo cha kufanyika kwa tafiti hizo ni pamoja

na mapendekezo yaliyotolewa katika tasinifu hii.

Tano, matokeo ya utafiti huu yanatarajiwa kuwa chanzo kimojawapo cha taarifa kwa

watafiti na wasomaji wengine wanaochunguza na kutafiti kazi mbalimbali za Fasihi

kwa kutumia nadharia ya Kisosholojia na nadharia ya Kidhanaishi kwa kuhusianisha

na jamii za Kitanzania. Aidha, watafiti na wasomaji hao wataweza kupata maarifa

yanayohusiana na taaluma nyingine kama vile Saikolojia, Sosholojia, Afya, pamoja

na Sayansi za Jamii kwa jumla.

1.8 Mawanda ya Utafiti

Utafiti huu ulihusu usawiri wa mchakato wa kujiua katika riwaya teule za Euphrase

Kezilahabi tu, ambazo ni Rosa Mistika, Kichwamaji, na Dunia Uwanja wa Fujo na

kama ni mwangwi wa mtanziko wa kijamii au la. Tunatambua kuwa ni vigumu

kuchunguza dhana hii ya kujiua katika riwaya zote za Kiswahili au jamii nzima ya

Watanzania kutokana na suala la muda na rasilimali. Hata hivyo, tunaamini kuwa

matokeo ya utafiti huu yameweza kuakisi matukio ya mchakato wa kujiua

12

yanayosawiriwa katika kazi za Fasihi kwa jumla. Hii ni kwa sababu: Mosi, kazi zote

za fasihi zinachota malighafi kutoka katika jamii; hivyo, yaliyomo katika riwaya

teule yametosha kuwakilisha yale yaliyomo katika riwaya nyingine, ambazo

hazikushughulikiwa na utafiti huu. Pili, jamii ya mwandishi wa riwaya teule inafaa

kuwakilisha jamii nyingine za Tanzania kwa kuhusianisha matukio na miktadha ya

kijamii inayopatikana katika jamii hiyo. Tatu, kwa kuwa data zilizotumika katika

utafiti huu zilipatikana kutoka katika makundi mbalimbali ya watafitiwa, tunaamini

kuwa makundi hayo yalisaidia katika upatikanaji wa data wakilishi kwa jamii pana

ya Watanzania. Hii inatokana na ukweli kwamba matukio ya watu kujiua

yanajitokeza pia katika jamii nyingine za Watanzania.

Hivyo, katika kuchambua usawiri wa mchakato wa kujiua katika riwaya teule za

Euphrase Kezilahabi tulichunguza kama kujiua huko ni mwangwi wa mtanziko wa

kijamii au la. Hata hivyo, pale ambapo mifano mingine nje ya kazi hizo teule

imetumika, mifano hiyo isichukuliwe kama data za msingi, bali kutumika kwake

kulilenga kujenga na kuthibitisha au kuwezesha hoja mbalimbali kuwa madhubuti na

kueleweka zaidi.

1.9 Muhtasari wa Sura ya Kwanza

Sura hii ya kwanza imeweka msingi wa utafiti huu kwa kujadili vipengele vya

utangulizi kuhusu lengo la utafiti wetu. Vipengele muhimu vilivyoshughulikiwa ni

ufafanuzi wa dhana muhimu, usuli wa tatizo la utafiti, tamko la utafiti, na malengo

ya utafiti. Vipengele vingine ni maswali ya utafiti, manufaa ya matokeo ya utafiti, na

mipaka ya utafiti. Vipengele hivi vilimpa mtafiti mwanga na mwelekeo wa kufanya

utafiti ili kubaini ni nini hasa alikusudia kufanya, na ni nini matokeo ya utafiti wake.

Kupitia vipengele hivi, mtafiti alibaini kuwa tatizo la watu kujiua ni kubwa katika

jamii zetu na linaendelea kuziathiri jamii zote duniani. Kutokana na hilo, alibainisha

kwa ufupi umuhimu wa kufanyika kwa utafiti huu kwa kueleza kuwa jamii inatakiwa

kushirikiana na kuchukua jitihada za pamoja ili kulishughulikia kwa kina tatizo hili.

Sura inayofuata inahusu mapitio ya maandiko mbalimbali yaliyowezesha mwanya

wa utafiti huu kubainishwa. Aidha, inajadili viunzi vya nadharia zilizomwongoza

mtafiti na kuwezesha matokeo ya utafiti huu kupatikana.

13

SURA YA PILI

MAPITIO YA MAANDIKO NA KIUNZI CHA NADHARIA

2.1 Utangulizi

Sura hii inahusu mambo makuu mawili. Jambo la kwanza, ni mapitio ya maandiko

mbalimbali kuhusiana na mada yetu. Jambo la pili, ni ufafanuzi wa viunzi vya

nadharia zilizotumika katika mchakato mzima wa ukusanyaji na uchambuzi wa data.

2.2 Mapitio ya Maandiko

Katika sehemu hii, tumepitia maandiko mbalimbali yanayohusiana na mada yetu.

Mapitio hayo yamegawanywa katika sehemu tatu, ambazo ni: mapitio ya maandiko

kuhusu kazi za Kezilahabi kwa jumla, mapitio kuhusu mchakato wa kujiua katika

riwaya teule za Kezilahabi, na mapitio kuhusu dhana ya kujiua kwa mitazamo ya nje

ya Fasihi. Sehemu hii inahitimishwa kwa kufafanua mwanya uliokusudiwa kuzibwa

kupitia tasinifu hii.

2.2.1 Mapitio Kuhusu Kazi za Kezilahabi kwa Jumla

Ziko tafiti na tahakiki mbalimbali kuhusu kazi za Kezilahabi, hususani riwaya,

ambapo kila mtafiti na mhakiki amefanya utafiti wake kulingana na malengo

yaliyomsukuma kufanya hivyo. Miongoni mwa wataalamu waliohakiki kazi za

Kezilahabi ni Mulokozi (1983, 2010); Senkoro (1982, 2007 & 2011), Musau (1985),

Mlacha (1985), Madumulla (1993), na Mbatiah (1998).

Mulokozi (1983) anaeleza dhamira ya uhusiano wa mtu binafsi na jamii. Pia,

anafafanua tatizo la mtu kutengwa au kubaguliwa na jamii yake. Anaeleza kuwa,

ingawa mtu binafsi ana hiari ya kufanya fujo zake, lakini hana nguvu mbele ya jamii,

na kwamba anapogombana nayo, yeye ndiye atakayeumia, kwani fujo ya mtu binafsi

huhanikizwa na fujo ya jamii au taifa. Anaendelea kueleza kuwa katika riwaya ya

Dunia Uwanja wa Fujo, kuna wahusika waliotengwa na jamii kutokana na matendo

yao. Kwa mfano, Mugala kutokana na uchawi1, Makoroboi kwa sababu ya wizi,

vijana wazinzi kwa sababu ya kuzini hadharani na kuvunja miiko ya jamii, Dennis

1 Ufundi wa kutumia dawa au vitabu maalumu vya uganga ili kuleta madhara kwa

viumbe (TUKI, 2014).

14

kwa sababu ya usomi, utajiri wake, na kazi ya upelelezi, na Tumaini kwa sababu ya

uzinzi, kazi ya upelelezi, na hatimaye ubepari wake. Anaeleza zaidi kuwa Tumaini,

ambaye ni mhusika mkuu alichukiwa na kijiji kizima kwa kuharibu mabinti za watu,

kwa kuwatia mimba, pamoja na fedheha ya wazazi wake kutokana na tabia za

uchawi. Kutokana na hilo, aliamua kuhama pale kijijini na kukimbilia mjini, kwani

aliona hawezi kushinda vita vyake dhidi ya kijiji. Hata hivyo, pamoja na kwamba

andiko hilo halielezi moja kwa moja kuhusu usawiri wa mchakato wa kujiua kama ni

mwangwi wa mtanziko wa kijamii au la, bado lilikuwa muhimu katika utafiti huu.

Hii ni kwa sababu linabainisha baadhi ya mambo na matukio kama vile mtu

kujitenga kijamii au kutengwa na jamii ambayo humletea mtu upweke na msongo wa

mawazo, hatimaye, huweza kusababisha mtu huyo kujiua.

Naye Musau (1985), kupitia riwaya za Rosa Mistika, Kichwamaji, na Dunia Uwanja

wa Fujo, alishughulikia suala la maana ya maisha. Anamwona Kezilahabi kama mtu

aliyekata tamaa. Anafafanua kuwa dunia ni uwanja wa fujo na mahala pasipo na

furaha. Utafiti huo wa Musau ulikuwa na umuhimu mkubwa sana katika utafiti huu.

Hii ni kwa sababu umesaidia na kumpa mwanga mtafiti wa kuyafahamu masuala ya

furaha, sababu za kukata tamaa ya maisha, na namna yanavyowaathiri wahusika

katika kazi hizi. Hata hivyo, utafiti huo bado hauelezi lolote kuhusu usawiri wa

mchakato wa kujiua katika kazi hizo, na kama ni mwangwi wa mtanziko wa kijamii

au la. Tasinifu hii ilipata nafasi ya kulishughulikia suala hilo kwa kina.

Mbatiah (1998) anaeleza kuwa kazi za Euphrase Kezilahabi zinaweza kugawanywa

katika vipindi viwili: yaani, kipindi cha kwanza zilipoandikwa riwaya za awali

ambazo ni: Rosa Mistika, Kichwamaji, Dunia Uwanja wa Fujo, na Gamba la Nyoka.

Anaeleza kuwa katika riwaya hizi zote kuna sifa nyingi za kimaudhui na kimtindo

zinazolingana. Anaongeza kuwa riwaya hizo ni za kiuhalisia kwa sababu zinaelezea

maisha halisi ya Watanzania baada ya uhuru na Azimio la Arusha. Katika uchambuzi

wake, anaegemea kwenye nadharia ya Udhanaishi na anaeleza kuwa Rosa Mistika

aliathiriwa na mazingira yaliyomlea. Anaichambua zaidi riwaya ya Rosa Mistika na

anaona kuwa imetawaliwa na hisia ya kicheko cha uchungu, kwa sababu mwandishi

anaicheka jamii yake kwa kushindwa kuwalea watoto wake wa kike. Aidha, katika

Kichwamaji, mwandishi anajadili masuala kama vile kifo, furaha, maisha na uwepo

wa Mungu. Kutokana na hilo, tunapata falsafa kuhusu dhana ya ‗kichwamaji‘ kuwa

15

ni ishara ya ukosefu wa mawazo mwafaka katika muktadha wa jamii, ambayo ni

alama ya mkengeuko. Katika Dunia Uwanja wa Fujo tunapata mwendelezo wa

mjadala kuhusu tatizo la maisha kama lilivyoanza kujadiliwa katika Kichwamaji.

Hapa tunaelezwa kuwa maisha ya mwanadamu ni vurumai ambayo huletwa

ulimwenguni na watu fulani katika nyakati mbalimbali za kihistoria. Andiko hili

lilikuwa muhimu kwa utafiti wetu kwa sababu lilitupa taswira ya wahusika

wanaochunguzwa katika utafiti huu. Pia, lilimpa mtafiti welewa zaidi kuhusu

nadharia ya Udhanaishi, ambayo ni mojawapo ya nadharia alizozitumia katika utafiti

wake.

Katika kipindi cha pili, Mbatiah anaziangalia riwaya za Euphrase Kezilahabi ambazo

ni Nagona na Mzingile. Katika uchunguzi wake, anadai kuwa riwaya hizi si za

kiuhalisia, kwani zimejikita katika udhanaishi na zinaelezea kitendawili kuhusu

maisha ya mwanadamu na nafasi yake ulimwenguni. Anafafanua zaidi kuwa riwaya

hizi zinamtoa msomaji katika mazingira halisi ya kiulimwengu aliyoyazoea na

kumpeleka kwenye ulimwengu wa kindoto baina ya kifo na uhai, baina ya kuwa

macho na kuwa na usingizi, na msomaji anasafiri kifikra kwa kuutalii ulimwengu ili

kujua ukweli wake. Anaendelea kueleza kuwa mwanadamu hawezi kupata fanaka na

furaha maishani mwake kwa sababu ulimwengu ni mbovu na haumjali; na kwamba,

juhudi anazofanya ili kujiendeleza apate furaha daima ni za kumletea maangamizi.

Andiko hili la Mbatiah limekuwa na umuhimu mkubwa katika tasinifu hii kwa

sababu linadokeza baadhi ya mihimili ya nadharia ya Udhanaishi, ambayo ni

mojawapo ya nadharia zilizozitumia katika utafiti wetu. Mihimili hiyo ni pamoja na

kutafuta uhuru binafsi, uwezo wa mtu wa kujifikiria na kujiamulia mambo yake,

pamoja na wajibu wake katika ulimwengu. Msingi mwingine ni kukengeuka kwa

misingi ya jamii husika, kukata tamaa na mauti. Mihimili hii ni muhimu katika utafiti

wetu kwani ndiyo iliyoitumika katika kubaini matukio ya wahusika kujiua na sababu

za mitanziko yao. Pia, andiko hilo linaeleza kuhusu falsafa ya maana ya maisha na

mitazamo ya jamii katika kazi teule, na hivyo kubainisha chanzo cha baadhi ya

wahusika kujiua, ambacho ni kipengele cha msingi kilichokusudiwa kushughulikiwa

katika utafiti huu.

Nao Wamitila (1999) na Senkoro (2006) walihakiki na kutoa maana za majina katika

riwaya za Kezilahabi. Wamitila anaona kuwa majina mengi aliyoyatumia

16

yanaendana na mazingira ya Ukerewe, mahali alikokulia Kezilahabi. Anafafanua

zaidi kwamba, wakati mwingine, majina huweza kutumika kama ploti na motifu.

Katika Rosa Mistika jina la Rosa Mistika lenye maana ya ‗waridi lenye fumbo‘

linamfanya msomaji ajiulize maswali yanayoibua ploti. Wamitila anaendelea

kufafanua kuwa jina lenyewe ni rahisi kueleweka, lakini linamwachia msomaji

taharuki. Anakwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa Kezilahabi ametumia kejeli

katika baadhi ya majina ya wahusika, kama vile, Deogratias katika Rosa Mistika

linalotokana na neno la Kigriki lenye maana ya ‗Asante Mungu‘, lakini tabia za

mhusika haziendani kabisa na jina hilo kutokana na kukosa maadili. Andiko hilo

limekuwa na umuhimu, kwa kuwa lilimhamasisha kufahamu taharuki inayoibuliwa

na msomaji kutokana na jina la mhusika Rosa, ambaye baadaye aliamua kujiua. Hata

hivyo, andiko hilo halikuwa na lengo tulilolishughulikia katika tasinifu yetu. Hivyo,

kutupatia mwanya wa kulishughulikia kwa kina katika utafiti uliofanyika.

Kwa upande wake, Senkoro (2006) alitafiti masuala ya Fasihi ya Kiswahili ya

Majaribio kama makutano ya Fasihi Simulizi na Fasihi Andishi katika riwaya ya

Rosa Mistika. Anabainisha kuwa, mara kwa mara, wahusika katika Fasihi simulizi

huwakilisha pande kuu mbili: wa wema au haki na wa ubaya au uonevu. Anaendelea

kueleza kuwa, katika riwaya hii, kuna majina ya wahusika ambao tabia zao

hazibadiliki tangu mwanzo hadi mwisho wa riwaya. Akitolea mfano wa jina la Rosa

Mistika, anaeleza kuwa hili ni jina jingine la Bikira Maria likiwakilisha ua waridi

lenye fumbo. Anaona kuwa jina hili ni lile la ua moja wakati Flora (ambalo ni jina la

mdogo wake Rosa Mistika) maana yake ya asili ni mimea, na hivyo hili si la ua moja

wala mmea mmoja tu, bali mimea yote. Anadai kwamba, bila shaka, mwandishi

alitutaka tumwone Rosa Mistika kuwa yu dhaifu sana kama ua moja tu

alinganishwapo na Flora, ambaye anawakilisha mimea yote. Maelezo haya

yanatupatia picha kuwa, inawezekana ndiyo maana hata baada ya vifo vya wazazi

wake, pamoja na kile cha Rosa, Flora aliweza kustahimili kwa kuwalea wadogo

zake, wakati Rosa alichukua maamuzi ya kujiua. Hivyo, kwa kuwa utafiti huo

unadokeza juu ya maisha ya Rosa Mistika ambaye ni mhusika aliyejiua, uliacha

mwanya wa kuyafuatilia maisha yake kwa undani kwa lengo la kubaini mchakato wa

matukio ya kujiua kwake na sababu za mitanziko yake.

17

Aidha, Diegner (2002) alichunguza riwaya za Kezilahabi kwa kujikita katika

kipengele cha sitiari kama inavyoelezwa katika taaluma ya Fasihi. Anaeleza kwamba

riwaya hizi zimebeba falsafa ya udhanaishi na zina mfuatano wa maudhui ambayo ni

ya kihalisi kulingana na mazingira, ikiwa ni pamoja na yale yanayoelezwa ndani

yake. Anaongeza kuwa tunaweza kuzigawa kazi za Euphrase Kezilahabi katika

vipindi viwili: kipindi cha kwanza ambapo mwandishi alishughulikia masuala mazito

ya kijamii kwa kutumia mtindo wa lugha nyepesi kwa wasomaji wake. Anaongeza

kuwa kipindi hiki ni cha Rosa Mistika, Kichwamaji, Dunia Uwanja wa Fujo, na

Gamba la Nyoka. Anabainisha kwamba mandhari aliyotumia mwandishi ni ya

Ukerewe, Mkoani Mwanza, ambapo hata uumbaji wa wahusika wake unafanana.

Mtafiti huyu anaeleza kuwa Kezilahabi anashughulishwa sana na suala la maana ya

maisha na kumtafuta Mungu. Anafafanua zaidi kuwa yote haya yanajitokeza kwa

njia ya istiara. Kipindi cha pili ni wakati zilipoandikwa Nagona na Mzingile. Riwaya

hizi ni tofauti na zile za mwanzo kutokana na kutumia lugha ya kiishara na kitaswira,

na hivyo kutoeleweka kwa urahisi. Hata hivyo, pamoja na ufafanuzi mzuri

uliofanywa na mtafiti huyo, bado suala la kujiua halikushughulikiwa kwa undani

katika utafiti wake, bali limedokezwa tu. Hii ni kwa sababu utafiti huo umezibainisha

riwaya hizo kuwa ni za kidhanaishi tu, pasipo kuelezea kwa kina suala la kujiua.

Hivyo, utafiti huo uliacha mwanya uliouzibwa katika utafiti wetu.

Flavian (2012) alichunguza suala la usimulizi katika riwaya ya Dunia Uwanja wa

Fujo. Anafafanua kuwa tahakiki zilizofanywa kuhusiana na kazi za Kezilahabi

zinajaribu kueleza masuala mbalimbali ya kijamii kama vile falsafa, dhamira, istiara,

na motifu. Anaona kuwa kazi hizi zinaonekana kukamilika kutokana na mbinu za

usimulizi ambazo wahakiki wengine hawakuzishughulikia kwa undani. Pia, anaeleza

namna mwandishi anavyoyasuka matukio, na kumfanya msomaji asafiri na

mwandishi, huku akiwafuatilia wahusika na maudhui wanayoyabeba. Anatolea

ufafanuzi wa Wamitila (1997) anayeeleza kwa ufupi tu kuwa, usimulizi wa riwaya ya

Dunia Uwanja wa Fujo, una athari kubwa kama zilivyo taswira na ishara. Ijapokuwa

utafiti huo haubainishi wala kudokeza lolote juu ya masuala ya usawiri wa mchakato

wa kujiua, bado mawazo yake yametumika kama kianzio cha kuchunguza maisha ya

baadhi ya wahusika na maudhui wanayobeba, ikiwa ni pamoja na hatima zao. Haya

yote yamechangia katika ukamilifu wa tasinifu hii.

18

Naye Ponera (2014) alichunguza jinsi ufutuhi unavyojitokeza katika nathari za

Kiswahili, hususani katika nathari za Shaaban Robert na Euphrase Kezilahabi.

Anaona kuwa nathari hizo zimeundwa kwa kutumia ufutuhi kama mbinu mojawapo

ya kibunilizi. Akifafanua kipengele kimojawapo cha ufutuhi ambacho ni furaha,

anaeleza kuwa furaha ni kionjo cha kisaikolojia ambacho huhusu hali ya ukunjufu

wa moyo na bashasha ambayo, aghalabu, hutokana na ridhiko la moyo au nafsi.

Utafiti huo umekuwa na mchango katika utafiti huu, kwa sababu suala la furaha na

uhusiano wake na matukio ya kujiua limeshughulikiwa kwa kina.

Kwa upande mwingine, Chuachua (2016) alichunguza namna maarifa ya Wabantu

yanavyojitokeza katika riwaya za Shaaban Robert na Euphrase Kezilahabi. Katika

uchunguzi wake, alijikita katika vipengele kama vile, uchawi, tambiko, imani au

fikra kuhusu roho na kifo na moyo. Vipengele vingine ni Mungu, mwanya, uzazi,

utoaji majina, uganga na ardhi. Utafiti huo unahitimisha kuwa kazi hizo

zinawasilisha maarifa halisi ya Wabantu yakiegemea katika misingi ya kiontolojia2.

Ni wazi kwamba utafiti huo unataja baadhi ya vipengele ambavyo vimechunguzwa

katika utafiti huu. Vipengele hivyo ni pamoja na suala la kifo na majina ya wahusika.

Kwa jumla, katika utafiti huu andiko hilo lilimwongezea maarifa mtafiti, hususani

katika kuchunguza dhana ya kifo, na baadhi ya majina ya wahusika kwa lengo la

kubaini sifa na uhusika wao.

2.2.2 Mapitio Kuhusu Mchakato wa Kujiua katika Riwaya za Kezilahabi

Katika kupitia na kuchunguza maandiko kuhusiana na suala la wahusika kujiua,

hususani katika kazi za Kezilahabi, ni maandiko machache sana tuliyofanikiwa

kuyapata. Miongoni mwa maandiko hayo ni: Mulokozi (1983, 2010), Mlacha (1985),

Madumulla (1993), Senkoro (1996), Wamitila (2008), Sakkos (2008), na Fuluge

(2013). Kwa jumla, watafiti hao wanaeleza kuwa, kazi za Kezilahabi zimefungamana

na matukio ya kujiua.

2 Ni maarifa, mtazamo na imani ya jamii kuhusu maisha na kuwapo kwake, na kuhusu ulimwengu

kwa jumla. Ontolojia hujaribu kujibu maswali yafuatayo: Binadamu ni nani au ni nini? Asili ya

binadamu ni nini? Asili ya ulimwengu ni nini? Asili ya mwanamume/mwanamke ni nini? Lengo na

hatima ya maisha ni nini? Je, kuna mamlaka nje ya ulimwengu inayotawala maisha na jaala ya

mwanadamu? Binadamu anahusianaje na ulimwengu na vilivyomo? Wakati ni nini; binadamu

anahusianaje nao? Mauti ni nini? Je, kuna maisha baada ya kufa? (Mulokozi, 2017:343).

19

Mulokozi (1983, 2010) alitafiti maandiko ya Kezilahabi kwa kuangalia maudhui

katika Rosa Mistika, Kichwamaji na Dunia Uwanja wa Fujo. Katika Rosa Mistika,

anaonesha athari ya maisha ya Seminari ambayo mwandishi amekulia, pamoja na

uhasama dhidi ya malezi na maisha hayo. Anaona kuwa kuna dalili za mtazamo wa

kukata tamaa katika kutafakari maisha ambazo zinajitokeza katika riwaya hii. Katika

Kichwamaji, alishughulikia zaidi suala la falsafa na maana ya maisha, kuwapo au

kutokuwapo kwa Mungu na athari za wakoloni. Katika riwaya ya Dunia Uwanja wa

Fujo, ameonesha dhamira mbalimbali zinazojitokeza ambazo ni pamoja na ndoa,

malezi, uchawi na mazingaombwe, kuwapo kwa maisha, maana yake na kiini cha

riwaya, na mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi katika jamii. Anamchukua mtu katika

hatua zote za maisha yake: uzazi na ujana, malezi, ndoa, uzee hadi kifo.

Kwa jumla, Mulokozi anazichambua kazi za Kezilahabi kwa kuzihusisha kwa kiasi

kikubwa na udhanaishi, huku akiwaona wahusika waliojengwa katika kazi hizi kuwa

wamekata tamaa. Mulokozi anakwenda mbali zaidi kwa kusema kuwa kujiua huko

kwa kukata tamaa pia ni njia ya kukimbia matatizo, njia ambayo haifai. Utafiti huo

umekuwa na umuhimu mkubwa sana katika utafiti wetu kwa sababu unadokeza suala

la maisha ya wahusika na makuzi yao, ambapo kwa upande wetu tumeyachunguza

kama sehemu ya michakato ya kijamii. Hata hivyo, utafiti huo unatofautiana na

utafiti wetu, kwani mtafiti huyo alichunguza maudhui katika riwaya hizo, huku

akihusisha na nadharia ya udhanaishi. Kwa upande wa utafiti wetu, tumeshughulikia

usawiri wa mchakato wa kujiua katika riwaya teule kwa kuuhusisha na mwangwi wa

mtanziko wa kijamii. Aidha, kwa upande wa nadharia, tumetumia nadharia ya

Udhanaishi na Sosholojia ya Kifasihi.

Mlacha (1985) aliangalia udhanaishi unaojitokeza katika nathari za Kezilahabi.

Alibainisha matukio kama vile ulevi, kujiua na kuua ambayo yanaashiria

kuchanganyikiwa kwa akili. Kulingana na mwelekeo wa malengo yake, andiko hili

halijatoa ufafanuzi wa kutosha kuhusu nini husababisha mtu kuchanganyikiwa, bali

linadokeza baadhi tu ya vipengele vya udhanaishi na kuishia kueleza kuwa matukio

hayo huashiria kuchanganyikiwa kwa akili. Hivyo, utafiti huo ulikuwa muhimu kwa

mtafiti katika kuchunguza usawiri wa vipengele vingine vya kidhanaishi na namna

vinavyohusiana na dhana ya kujiua katika riwaya teule za Kezilahabi. Aidha, utafiti

umechunguza matukio yanayounda mchakato wa kujiua, pamoja na namna athari za

20

miktadha ya maisha ya jamii inavyochangia katika kumwathiri mhusika kiasi cha

kufikia hatua ya kujiua kama ilivyowatokea wahusika katika riwaya teule.

Madumulla (1993) alitafiti namna wahusika katika nathari za Kezilahabi, kama vile

Rosa Mistika, Kichwamaji, Gamba la Nyoka, Cha Mnyonge Utakitapika Hadharani

na Mayai Waziri wa Maradhi, wanavyojiua. Katika utafiti wake, anaona kwamba

Kezilahabi ana upungufu wa kisanii katika kutafuta suluhu za matatizo yawapatayo

wahusika wake. Anabainisha upungufu wa mwandishi huyo kwamba unatokana na

namna anavyoumba wahusika wake wanaoamua kujiua kwa lengo la kuyakwepa

matatizo ya kijamii. Anaongeza kwamba kujiua hakumalizi tatizo la jamii, bali

pengine humaliza kwa kiasi fulani matatizo ya aliyejiua na kuyahamishia matatizo

hayo kwa wanaobaki hai. Mtafiti huyo amefanikiwa kubainisha aina ya wahusika

wanaopatikana katika kazi za Kezilahabi, huku akidokeza tu kuhusu udhaifu wa

mwandishi huyu. Hatimaye, anatoa hitimisho la jumla kuhusu mwandishi huyu

anavyowaumba wahusika hao wanaojiua pasipo kutoa suluhisho la nini kifanyike.

Hivyo, utafiti huo haujakidhi maswali yote kuhusu matukio ya wahusika kujiua na

mitanziko inayosababisha kujiua kwao. Kutokana na andiko hilo kushindwa

kubainisha matukio na sababu za mitanziko ya wahusika, utafiti huu umeshughulikia

masuala hayo kwa kina na kuziba mwanya uliokuwa umeachwa na andiko hilo.

Aidha, Senkoro (1996) amezichambua kazi za Kezilahabi kwa jicho la kidhanaishi

kwa kuchunguza maana ya maisha. Anasema kuwa uchotarishaji katika kazi za

mwandishi huyu ulianzia katika zile riwaya za mwanzo, yaani Rosa Mistika,

Kichwamaji, na Dunia Uwanja wa Fujo. Anaona kuwa kazi hizi zinajishughulisha

na suala la maana ya maisha kwa kutumia mazingira ya vijijini na miji ya Tanzania,

lakini kwa jicho la udhanaishi. Kimsingi, udhanaishi huyaona maisha kuwa ni kitu

kisichokuwa na maana. Hii ndiyo sababu wahusika wa Kezilahabi kama vile

Kazimoto wa Kichwamaji, Rosa Mistika na Charles wa Rosa Mistika, mwishoni

wanaamua kuwa maisha hayana maana; kwa hiyo, ama wanaamua kujiua (Kazimoto

na Rosa) au wanaamua kujitenga na uwongo wa maisha hayo kwa kugeuka kuwa

buruda (Charles). Makala yake hiyo imetalii kwa kiasi kikubwa udhanaishi

unaojitokeza katika kazi za Kezilahabi. Inaeleza kuwa Kezilahabi alifanya majaribio

na falsafa ya udhanaishi, akionesha kuwa maisha hayana maana, kwani mtu

anazaliwa ili afe. Kwa Kezilahabi, maisha ni fumbo sawa na Rosa alivyo ua waridi

21

lenye fumbo. Hata hivyo, pamoja na kutalii sana katika suala la udhanaishi, bado

uhakiki wake unaacha mwanya wa utafiti, kwa sababu hauelezi lolote kuhusu usawiri

wa mchakato wa kujiua katika riwaya hizo, na kama ni mwangwi wa mtanziko wa

kijamii, au la. Pia, haudokezi lolote kuhusu matukio ya mchakato wa kujiua na

namna yanavyosawiriwa katika riwaya hizo.

Sakkos (2008) alihakiki riwaya ya Kichwamaji kwa kutumia nadharia ya Udhanaishi

na ile ya Ufeministi ili kubaini nadharia inayofaa katika kuchambua riwaya hii.

Anaeleza habari za Kazimoto kwenda kuomba kazi kwa Mkuu wa Wilaya ambaye

pia ni rafiki yake wa utotoni. Baada ya kunyimwa kazi, anajiona kama mtu

aliyetengwa na kila mtu katika jamii yake. Inaelezwa mikasa aliyoipitia Kazimoto

baada ya kifo cha dada yake (Rukia), mama yake, na mkewe (Sabina) kumzalia

mtoto mwenye kichwa kikubwa. Kutokana na majanga yote hayo, Kazimoto alikosa

tumaini na kuamua kujiua. Kazi hii ni muhimu, kwa kuwa imempa mtafiti mwanga

wa kuyamulika kwa kina maisha ya Kazimoto na kubainisha sababu za za kujiua

kwake.

Kwa upande wake, Wamitila (2008) amehakiki riwaya ya Rosa Mistika, Kichwamaji,

Dunia Uwanja wa Fujo, na Gamba la Nyoka. Katika uhakiki wake, anaeleza kuwa

kazi hizi, zimefungamana na matukio ya vifo. Vilevile, anaeleza kuwa kazi hizi

zimeangalia maana ya maisha, nafasi ya Mungu katika ulimwengu, nafasi ya mtu

binafsi dhidi ya jamii, na dhana ya furaha na kifo. Anaona kuwa Kezilahabi

ameathiriwa na waandishi wa kidhanaishi kama vile Martin Heidegger (1889),

Friedrich Nietzche (1844), Samuel Beckett (1975), Albert Camus (1913) na

wengineo walioandika kazi zao zilizobobea katika falsafa hii. Ni wazi kuwa kazi

hiyo imekuwa mwanga katika utafiti huu, kwani inadokeza baadhi ya sifa za

udhanaishi, pamoja na sifa za mwandishi. Hata hivyo, kazi hiyo haielezi kwa kina

kuhusiana na matukio ya kujiua pamoja na athari za miktadha ya kijamii

inayosawiriwa katika mchakato wa mtu kujiua. Hivyo, utafiti huu ulikusudia

kuchunguza usawiri wa mchakato wa kujiua katika riwaya teule za Euphrase

Kezilahabi kwa kuuhusisha na uhalisi katika jamii.

22

2.2.3 Mapitio Kuhusu Dhana ya Kujiua kwa Mitazamo ya Nje ya Fasihi

Kama ilivyoelezwa hapo awali, tatizo la kujiua, kwa kiasi kikubwa, limefanyiwa

utafiti katika nyanja za sosholojia, saikolojia na afya. Hapa chini tunadokeza kazi

chache zinazohusu suala hilo la kujiua.

Durkheim (1979) anahusisha tatizo la kujiua na suala la kujitenga kijamii.

Anafafanua kuwa suala la kujiua linatokana na kujitenga kijamii na linaonekana zaidi

vijijini, ikilinganishwa na mijini. Anaongeza kuwa mtu anayepanga kujiua

anapobaini kuwa ametengwa kutokana na mabadiliko ya kijamii, kihisia, au

kiuchumi, huchanganyikiwa na huweza kujiua. Licha ya kuwa kazi hiyo ni ya

kisosholojia, na kwamba inadokeza mojawapo ya sababu zinazoweza kusababisha

mtu kujiua, bado haielezi kwa kina kuhusu matukio ya mchakato wa kujiua na

sababu za mitanziko ya wahusika inayoweza kusababisha mtu kujiua. Hata hivyo,

kazi hiyo imekuwa na umuhimu katika utafiti wetu, kwani ilimpa mtafiti maarifa ya

awali katika kuchunguza na kubainisha matukio ya mchakato wa kujiua na sababu za

mitanziko ya wahusika zinazosababisha mtu kujiua.

Maltsberger (1993) katika utafiti wake anaona kuwa kujiua kuna uhusiano na

masuala ya ndoto. Anaeleza kwamba ndoto hutufundisha mambo yasiyo ya hiari

kuhusu suala la kujiua ambalo linahusishwa na dalili za mtu kukosa uvumilivu.

Anaongeza kwamba, mara nyingi, mgonjwa aotaye ndoto za kutaka kujiua huwa na

lengo la kutaka kulipa kisasi kwa yaliyompata. Pia, hukusudia kumwadhibu

aliyemsababishia matatizo, mfadhaiko na huzuni aliyo nayo, na/au kuanza maisha

mapya tofauti na yale anayopitia, ili kujitenga na dunia aliyopo. Maelezo haya

yanabainisha wazi kwamba suala la kujiua ni la kimchakato, na siyo la ghafla. Kazi

hiyo ilikuwa muhimu katika utafiti huu, kwani imemsaidia mtafiti kufahamu

mchakato wa matukio yanayohusiana na masuala ya kujiua na namna

yanavyosawiriwa katika riwaya teule.

Ndosi na wenzake (2004) wanabainisha kuwa kujiua ni chanzo cha pili au cha tatu

cha vifo vinavyowapata vijana baada ya vile vinavyotokana na ajali. Wanaongeza

kuwa, kwa kila jaribio moja la mtu kujiua, kuna majaribio mengine manane ya watu

kutaka kujiua. Baadhi ya sababu zinazobainishwa katika kazi hiyo ni matatizo ya

akili ambayo humsababishia mhusika kupata msongo wa mawazo, na kutumia

23

madawa ya kulevya na vilevi vingine. Sababu nyingine ni migogoro ya kijamii na

wahusika kuugua kwa muda mrefu. Kazi hii ni muhimu, kwani imempa mtafiti

mwanga wa kuyajua baadhi ya matukio ya kujiua, pamoja na sababu za mtu kujiua.

Hata hivyo, kwa kuwa haielezi kwa uwazi kuhusu matukio ya mchakato wa kujiua

na sababu za mitanziko ya wahusika, iliacha mwanya kwa utafiti kushughulikia

masuala hayo kwa kina.

Glucksman na Kramer (2017) wanabainisha kwamba kujiua kunatokana na sababu

mbalimbali, zikiwamo za kitabia, kijamii, kibaiolojia na kiutamaduni. Wanaendelea

kufafanua kuwa ni vigumu kubainisha wazi na kumtambua mtu anayepanga kujiua.

Watafiti hawa wanaona kwamba suala la ndoto na majaribio ya kutaka kujiua

kutokana na huzuni au mfadhaiko wa mawazo ni chanzo kimojawapo kikubwa

kinachoweza kusababisha mtu kujiua. Wanaelezea zaidi kwamba kuna tofauti kubwa

baina ya wagonjwa wenye mfadhaiko na dalili za kujiua, na wale walio na

mfadhaiko, lakini hawana dalili za kutaka kujiua. Glucksman na Kramer (2017:17)

wanayashadidia zaidi kwa kusema:

…the manifest dream content of depressed, non-suicidal patients

differs from that of depressed, suicidal patients. The dream

imagery of depressed, suicidal patients contains themes of death,

dying, violence, and depature. The dream imagery of depressed,

non-suicidal patients contains themes of rejection, helplessness,

hopelessness, humiliation, failure and loss.

…mambo yanayodhihirika kwenye ndoto za wagonjwa wenye

mfadhaiko wasiokusudia kujiua ni tofauti na yale ya wagonjwa

wa mfadhaiko wanaokusudia kujiua. Taswira ya ndoto kwa

wagonjwa wa mfadhaiko na wanaokusudia kujiua huwa na

mawazo ya kifo, kufa, vurugu, na kutoweka. Taswira ya ndoto

kwa wagonjwa wa mfadhaiko wasiokusudia kujiua hubeba

mawazo ya kukataliwa, kukosa msaada, kukosa tumaini

kutothaminiwa/kunyanyapaliwa, kushindwa na kuchanganyikiwa

(Tafsiri ya Mtafiti).

Utafiti wa wataalamu hawa umetupa picha kwamba kuna uhusiano baina ya ndoto na

kujiua, na kwamba anayepanga kujiua hupitia mchakato na mlolongo wa matatizo

ambayo, hatimaye, humsababisha kuwaza kuutoa uhai wake kwa kujiua. Hata hivyo,

licha ya kuwa utafiti huo hauelezi kwa kina kuhusu usawiri wa mchakato wa kujiua

kama ni mwangwi wa mtanziko wa kijamii, au la, umesaidia katika kubainisha

24

baadhi ya matukio anayopitia mhusika kabla ya kuchukua uamuzi wa kujiua katika

riwaya teule za Euphrase Kezilahabi.

2.2.4 Mwanya Uliotakiwa Kuzibwa na Utafiti

Baada ya kupitia maandiko mbalimbali kuhusiana na mada yetu, tulibaini mwanya

ambao ulileta msukumo wa kufanyika kwa utafiti huu. Mwanya huo unajitokeza kwa

nia kuu tatu ambazo ni:

Mosi, watafiti wengi katika mapitio ya Kiswahili hawakubainisha kwa kina matukio

ya mchakato wa kujiua, sababu za mitanziko ya wahusika, na miktadha ya maisha ya

jamii inayosawiriwa katika mchakato wa kujiua. Matukio ya kujiua katika tafiti hizo

yametazamwa kama kitendo tu cha kukata tamaa kwa wahusika; na kwamba, huo ni

udhaifu wa mwandishi katika kuumba wahusika wenye kukata tamaa.

Pili, watafiti mbalimbali wamechunguza tatizo la kujiua katika kazi za Kezilahabi

kwa jicho la kidhanaishi. Wamebainisha kuwa wahusika katika kazi hizo hujiua

kutokana na kukata tamaa. Hata hivyo, tafiti zao hazikuhusisha nadharia hiyo ya

Udhanaishi na ile ya Sosholojia ya Kifasihi ili kubaini namna mchakato wa kujiua

unavyohusiana na kuathiriwa na miktadha ya kijamii. Aidha, katika kazi za

mwandishi huyu, mchakato wa matukio ya kujiua, sababu za mitanziko ya wahusika,

pamoja na tathmini ya uhusiano wa matukio ya mchakato wa kujiua na vichocheo

vya matukio ya kujiua katika jamii, haikushughulikiwa kwa kina.

Tatu, matukio ya watu kujiua, kwa kiasi kikubwa, yamekuwa yakitazamwa kwa

jicho la kisosholojia, kisaikolojia na kiafya, pasipo kuhusishwa na Fasihi (Ndosi na

wenzake, 2004; Shirika la Afya Duniani, 2018; na Habari Leo, 2018). Katika

mapitio yetu, tulibaini kuwa tafiti nyingi za kifasihi zilizolishughulikia tatizo hili la

kujiua, zimejikita zaidi katika matini zenyewe pasipo kuchunguza hali halisi ya tatizo

hili katika jamii. Kutokana na hilo, palikuwa na haja ya kufanyika utafiti wenye

mwelekeo huo ili kulishughulikia kifasihi, huku tukihusisha na data halisi

zinazopatikana katika jamii mahususi.

2.3 Viunzi vya Nadharia

Utafiti huu uliongozwa na nadharia mbili, ambazo ni: Nadharia ya Udhanaishi na

Nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi. Misingi ya nadharia hizi ndiyo iliyomwongoza

25

mtafiti katika mchakato wote wa ukusanyaji wa data, uchambuzi na uwasilishaji

wake.

2.3.1 Nadharia ya Udhanaishi

Udhanaishi ni harakati au hali ya kukata tamaa inayoendana na kuyaona maisha

kuwa ni kitu kisichokuwa na maana. Hufungamana na kukata tamaa, ulevi, na hata

kujiua. Camus (1984) anauelezea udhanaishi kuwa ni falsafa inayoshughulikia

masuala mbalimbali kuhusu maisha. Anaugawa katika mitazamo miwili: mosi,

maisha kama ombwe, yaani mahali patupu, na kwamba maisha hayana faida yoyote.

Pili, kujiua kama suluhisho la matatizo anayopitia au anayokabiliana nayo binadamu

duniani kwa kuamini kwamba hakuna maisha baada ya kifo. Wamitila (2003)

anauelezea udhanaishi kuwa ni maono au mtazamo unaohusiana na hali na maisha ya

binadamu, nafasi na majukumu yake ulimwenguni na uhusiano wake na Mungu. Nao

Wafula na Njogu (2007) wanauelezea Udhanaishi kuwa ni falsafa inayotokana na

‗utamaushi‘, yaani kutokuwa na furaha, na kukosa tumaini katika maisha kulingana

na namna yalivyo.

Wataalamu wengi wanaamini kwamba falsafa ya udhanaishi inatokana na mawazo

ya mwanatheolojia Soren Kierkegaard (1813 - 1855) kutoka Denmark. Katika vitabu

vyake vya Fear and Trembling (1843), The Concept of Dread (1844), na Sickness

unto Death (1849), Kierkgaard anashikilia kwamba mtu ni kikaragosi cha nguvu

zilizomuumba na za kijamii. Kwa jumla, wadhanaishi huyaona maisha ya mtu kuwa

ni ya kitanzia na hayana maana, kwa kuwa mwisho wa mwanadamu ni kifo.

2.3.1.1 Misingi ya Nadharia ya Udhanaishi

Misingi ya nadharia hii ni pamoja na:

a) Kujadili matatizo halisi yanayomkumba binadamu na kukwepa imani ya

kinjozi juu ya maana ya maisha;

b) Kutoamini kuhusu uwepo wa Mungu anayedaiwa kwamba ndiye muumba wa

ulimwengu, ambao kimsingi, haumjali binadamu huyu;

c) Kutafuta uhuru binafsi, uwezo wa mtu wa kujifikiria na kujiamulia mambo

yake, pamoja na wajibu wake katika ulimwengu; na

d) Kukengeuka kwa misingi ya jamii husika, kukata tamaa na mauti. Aidha,

kukumbwa na fadhaa, mashaka, pekecho na uchovu.

26

2.3.1.2 Nadharia ya Udhanaishi Ilivyotumika

Nadharia hii ilikuwa mwongozo katika kufikiwa kwa lengo la kwanza, lililokusudia

kubainisha usawiri wa matukio yanayounda mchakato wa kujiua katika riwaya teule

za Euphrase Kezilahabi. Vilevile, ilimwongoza mtafiti katika kupatikana kwa

matokeo ya lengo la pili, lililohusiana na kuchunguza sababu za mitanziko ya

wahusika zinazosawiriwa katika riwaya teule. Pia, ilisaidiana na nadharia ya

Sosholojia ya Kifasihi katika kumwongoza mtafiti ili kupatikana kwa matokeo ya

lengo la tatu. Hii ilitokana na misingi ya nadharia ya Udhanaishi kushindwa

kutosheleza mahitaji ya malengo yote matatu ya utafiti huu. Lengo hilo lilikuwa ni

kutathmini uhusiano wa matukio ya mchakato wa kujiua yanayosawiriwa katika

riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii. Kwa jumla, misingi ya

nadharia hizi mbili ilikamilishana kwa sababu ilimwongoza mtafiti katika mchakato

wake wa kupata matokeo ya utafiti wake kwa lengo hilo la tatu.

2.3.2 Nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi

Nadharia nyingine iliyotumika katika utafiti huu ni ile ya Sosholojia ya Kifasihi.

Kwa mujibu wa Coser (1963), nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi iliasisiwa na

Charles Taylor (1822 - 1917) na George Lukacs (1885 - 1971). Katika ufafanuzi

wake, Lukacs anaona kuwa masuala mbalimbali ya kijamii yanayohusiana na

uumbaji wa kazi za Fasihi, kwa kiasi kikubwa, hutegemea jinsi mwandishi

anavyofungamana na maisha ya jamii husika. Anaongeza kuwa, badala ya

kumithilisha au kufananisha hali ya maisha, Fasihi na sanaa zinapaswa kuwa ‗picha

ya uhalisi,‘ ijapokuwa picha hiyo hukiuka misingi ya uigaji wa moja kwa moja wa

uhalisi. Hii ina maana kuwa ni vigumu kuitenga kazi ya Fasihi na jamii, ambayo

kwayo kazi hiyo imechipuzwa. Kwa msingi huo, ni wazi kwamba Nadharia ya

Sosholojia ya Kifasihi ni kitengo muhimu sana cha uchunguzi ambacho humulika

mahusiano yaliyopo baina ya kazi halisi ya sanaa, umma, muundo wa jamii, na

namna kazi hiyo inavyojitokeza na kutathminiwa kuhusiana na uzuri na udhaifu

wake. Vilevile, nadharia hii huelezea sababu za kuibuka kwa kazi fulani ya sanaa

yenye umbo fulani la kijamii, ikiwamo namna fikra za mwandishi zinavyoongozwa

na mila, desturi na maisha ya jamii yake. Kimsingi, nadharia hii huchunguza jinsi

mtunzi wa kazi fulani ya kifasihi anavyoathiriwa na tabaka lake, itikadi yake ya

kijamii, mazingira ya kiuchumi ya kazi yake, na hali ya jamii yake anayoilenga.

27

Coser (1963) anaeleza kuwa, Fasihi ni zao la jamii na hufungamana na maisha halisi

ya jamii husika katika kila nyanja. Kuhusiana na suala la utamaduni, anaeleza kuwa

dhana hii ni ngumu kuielezea kwa sababu ni dhana changamani sana. Hii inatokana

na kuhusisha ndani yake masuala ya imani, mila, desturi, itikadi, maadili, sheria,

elimu, pamoja na mazoea anayokuwa nayo mtu akiwa ni sehemu ya jamii. Kwa

msingi huo, ni wazi kwamba mawazo haya ya Coser yanadhihirisha kuwa Fasihi

hufungamana na historia, fikra, pamoja na mitazamo na imani ya jamii husika.

Vipengele hivi ni muhimu katika utafiti wetu, kwani kwa namna moja ama nyingine,

tumevishughulikia katika utafiti wetu tulipokuwa tunachunguza usawiri wa

mchakato wa kujiua katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi ili kubaini kama ni

mwangwi wa mtanziko wa kijamii au la.

Kwa upande wake, Mungah (1999) anaeleza kuwa mtu anayesifika kama mmoja wa

waasisi wa nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi ni Hippolyte Taine (1828 – 1893).

Anaeleza zaidi kuwa Taine katika kitabu chake cha History of English Literature

(1863), alichunguza kazi ya Kifasihi kama taswira ya kijiografia, kiutamaduni na

kimazingira inayochimbuka kutoka katika jamii husika. Anaongeza kuwa kazi ya

kifasihi inatakiwa kuchukuliwa kama taarifa ya kweli inayohusu maisha halisi ya

watu. Kimsingi, nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi huiweka kazi ya Fasihi katika

ulimwengu wa jamii na kuelezea uhusiano uliopo baina yake. Hutawaliwa na imani

kuwa kuna uhusiano baina ya Fasihi na jamii, ambapo, kutokana na uhusiano huo,

kazi hiyo huweza kuandikwa.

Vilevile, Mungah (k.h.j) anaelezea zaidi kuwa Taine anadai kwamba kazi yoyote ya

fasihi, kama vile riwaya, ni kioo ambacho husawiri vipengele vyote vya maisha ya

jamii husika. Anatilia mkazo kuwa, kwa hakika, fasihi haiwezi kutengwa na

miktadha ya maisha ya binadamu katika harakati zake za maisha. Kipengele hiki

kinachoihusu Fasihi na jamii, pamoja na maisha ya jamii kwa jumla kilikuwa

muhimu sana katika utafiti wetu. Hii ni kwa sababu kimeshughulikiwa tulipokuwa

tunatathmini uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua katika

riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii.

28

2.3.2.1 Misingi ya Nadharia ya Kisosholojia

Misingi ya nadharia hii imejengwa katika mawazo kwamba:

a) Binadamu ni uti wa mgongo wa ulimwengu pamoja na sanaa kwa jumla. Hivyo,

kazi yoyote ya Fasihi ni taswira ya kijiografia, kimazingira na kitamaduni,

ambamo kazi hiyo imezuka. Kwa msingi huo, kazi hiyo haipaswi kutenganishwa

na muktadha, kwa kuwa mara nyingi hufungamana na historia ya jamii;

b) Fasihi ni dhihirisho la ujumi na ubunifu wa jamii katika kupambana na mazingira

yake, na hivyo, haiwezi kutengwa na harakati za binadamu zinazoongoza maisha

yake;

c) Usuluhishi wa migororo unaosawiriwa ndani ya Fasihi, kama vile katika msuko

wa matukio, unaficha tu migongano anuwai ya kijamii ambayo haijasuluhishwa.

Hivyo, una dhima ya kiitikadi;

d) Mhakiki hawezi kuhakiki kazi yoyote ya Fasihi bila kuzingatia miktadha yake ya

mazingira na maisha ya mwandishi. Siyo kazi tu ya fasihi inayochunguzwa, bali

pia na vipengele vilivyo nje ya kazi hiyo.

2.3.2.2 Nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi Ilivyotumika

Nadharia hii imekuwa na umuhimu mkubwa katika utafiti huu, kwani imetuongoza

katika kufikiwa kwa lengo la tatu, lililolenga kutathmini uhusiano baina ya usawiri

wa matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya

kujiua katika jamii. Kulingana na Narizvi (1982) uhusiano baina ya Fasihi na jamii ni

suala muhimu sana katika uchunguzi unaohusu masuala ya binadamu. Anaongeza

kuwa uhusiano huo husawiriwa kwa kuchunguza namna kazi husika

inavyofungamana na jamii. Ili kudhihirisha kuwa Fasihi ni zao la jamii, Escarpit

(1971), kama alivyonukuliwa na Mungah (keshatajwa), anaeleza kwamba bila msingi

wa kijamii, ukweli wa Fasihi hubadilishwa sawa na wa ramani isiyo na vitu vya

kimaumbile. Maelezo haya ya Escarpit yanalandana na mhimili mmojawapo wa

nadharia hii unaodai kwamba Sosholojia ya Kifasihi pia hushughulikia mamlaka na

nguvu fulani za kijamii. Kwa muktadha wa utafiti huu, mamlaka ni uwezo wa

kuamua na kufuatilia mwenendo na tabia za watu wengine kulingana na matakwa ya

huyo mwenye mamlaka. Mamlaka hayo yanaweza kuwa ni ya kisheria, mila na

desturi, au mamlaka ya kihaiba. Kwa mantiki hiyo, uchunguzi kuhusu jamii ya

mwandishi, umetusaidia tulipokuwa tunafanya tathmini ya uhusiano baina ya

29

usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya

matukio ya kujiua katika jamii.

Kipengele kingine muhimu katika nadharia hii ambacho tumekitumia katika utafiti

wetu ni kile kinachosisitiza kwamba mhakiki hawezi kuhakiki kazi ya Fasihi pasipo

kuzingatia miktadha inayomhusu mwandishi. Hii ina maana kuwa kinachotakiwa

kuchunguzwa si kazi za mwandishi pekee, bali ni pamoja na vipengele vingine

ambavyo viko nje ya kazi. Pia, inatakiwa kuchunguza maisha ya jamii

yaliyosababisha kupatikana kwa kazi husika. Mazingira hayo ni kama vile ya kisiasa,

kiuchumi, kiutamaduni, na kijamii.

2.4 Muhtasari wa Sura ya Pili

Sura hii imebainisha mapitio mbalimbali yanayohusiana na mada ya utafiti wetu ili

kupata msingi wa hoja za utafiti wetu. Kilichobainika ni kwamba, kwa kiasi

kikubwa, wataalamu na wahakiki wengi wa kazi za Euphrase Kezilahabi

wamezichambua na kuzihakiki kazi hizo kwa jicho la kidhanaishi. Aidha, kwa upeo

wa mtafiti, hakuna utafiti uliofanyika kuhusiana na riwaya teule uliotumia nadharia

ya Sosholojia ya Kifasihi pamoja na ile ya Udhanaishi kwa pamoja. Zaidi mapitio ya

maandiko ya wataalamu mbalimbali yalibaini kuwa wahakiki na watafiti wengi wa

Fasihi ya Kiswahili hawajalishughulikia kwa kina tatizo la watu kujiua katika jamii.

Pia, sura hii imejadili nadharia zilizomwongoza mtafiti katika kujenga hoja na

kukamilisha utafiti wake. Nadharia hizo ni Udhanaishi na Sosholojia ya Kifasihi.

Imebainishwa kwamba, misingi ya nadharia hizi imekamilishana ili kuweza kufikiwa

na kupatikana kwa matokeo ya utafiti kulingana na malengo yaliyokusudiwa. Sura ya

Tatu inahusu methodolojia na njia za utafiti.

30

SURA YA TATU

METHODOLOJIA YA UTAFITI

3.1 Utangulizi

Sura hii inaeleza namna utafiti huu ulivyosanifiwa na kufanyika hadi kukamilika

kwake. Vipengele vilivyoshughulikiwa katika sehemu hii ni usanifu wa utafiti,

mkabala wa utafiti, eneo la utafiti, walengwa wa utafiti, na ukusanyaji wa data.

Vipengele vingine ni mchakato wa ukusanyaji data, mbinu za uchambuzi wa data,

maadili na itikeli za utafiti, pamoja na uhalali na uthabiti wa data.

3.2 Usanifu wa Utafiti

Kwa mujibu wa Kothari (2004), usanifu wa utafiti ni uamuzi kuhusu nini, wapi, lini,

kwa kiwango gani na namna gani utafiti utafanyika. Hii ina maana kuwa usanifu wa

utafiti ni mpangilio maalumu wa kanuni za kukusanya data na uchanganuzi wake ili

kufikia uyakinifu wa malengo ya utafiti kwa kuzingatia muda, mahali pa utafiti, na

hali ya uchumi uliopo katika kukamilisha mada ya utafiti. Usanifu wa utafiti wetu

ulikuwa ni wa kifenomenolojia. Fenomenolojia hujishughulisha na maisha ya

binadamu na namna ya kuufahamu ulimwengu kulingana na uzoefu wa maisha ya

watu hao kuhusiana na hali au jambo fulani linalofanyiwa utafiti (Brentano, 1995;

Schram, 2003; Van Manen, 2014). Usanifu wa kifenomenolojia hujikita katika

ufafanuzi wa taarifa ambazo, kimsingi, hukusanywa na kuchambuliwa kwa njia ya

maelezo yenye kuakisi mtazamo wa wahojiwa kuhusiana na jambo husika. Nguzo

kuu ya fenomenolojia ni uzoefu au tajiriba za maisha alizonazo mtu kuhusu hali au

jambo fulani katika maisha yake kulingana na mazingira aliyopo (Chuachua, 2016).

Data za kifenomenolojia hukusanywa kwa njia mbalimbali, ikiwa ni pamoja na

mapitio ya maandiko, mahojiano, ushuhudiaji, pamoja na majadiliano katika vikundi.

Shabaha kubwa ya kutumia usanifu wa kifenomenolojia ilikuwa kupata maelezo ya

kina kutoka kwa watafitiwa kuhusu uzoefu na uelewa wao juu ya usawiri wa

mchakato wa kujiua katika jamii, hususani jamii ya mwandishi wa riwaya teule.

Aidha, kupitia usanifu huu, mtafiti aliweza kubainishiwa matukio yanayounda

mchakato wa kujiua, sababu za mitanziko ya kujiua kwa wahusika na kutathmini

uhusiano uliopo baina ya usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya

teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii. Vilevile, usanifu huu

31

ulimwongoza mtafiti katika kubainisha athari za miktadha ya jamii inavyomwathiri

mhusika hadi kufikia maamuzi ya kujiua kwake.

3.3 Mkabala wa Utafiti

Utafiti huu ulitumia mkabala wa kitaamuli katika ukusanyaji, uchanganuzi wa data,

pamoja na utoaji wa matokeo. Mkabala wa kitaamuli ni ule ambao data zake

hazielezwi na kufafanuliwa kwa kutumia namba (au takwimu). Hii haina maana

kuwa takwimu na namba hazitumiki kabisa, isipokuwa kinachosemwa hapa ni kuwa

hutumia maneno kuwasilisha na kujadili data za utafiti (Enon, 1998; Merriam &

Tisdell, 2016). Ponera (2016:116) anafafanua zaidi kwa kusema:

Utaamuli ni aina mojawapo ya mikabala ya kufanyia utafiti,

ambao hutumia zaidi tafakuri katika kuhusisha taarifa

mbalimbali za kitafiti. Kisha kutoa ufafanuzi kwa kuzingatia

misingi ya nadharia husika, pamoja na ithibati bayana,

zipatikanazo ama maskanini (uwandani) au katika matini.

Utafiti huu umetumia mkabala wa kitaamuli kwa sababu:

a) Mkabala wa kitaamuli una sifa ya kupokea fasili zinazotofautiana kwa tukio

lilelile moja, kwa sababu una sifa ya kuruhusu mitazamo mbalimbali ya watu

kulingana na uzoefu wao;

b) Mkabala huu una sifa ya kuruhusu sampuli ndogo kutumika kwa kuwa muda

mwingi hutumika katika kukusanya data za kimaelezo baina ya mtafiti na

watafitiwa;

c) Mbinu zilizotumika katika kukusanya data ni nusu funge. Hii ina maana

kuwa, pamoja na kuwapo kwa maswali mbalimbali yaliyokuwa

yameandaliwa ili kuongoza mahojiano, mtafiti alikuwa na uhuru wa kuuliza

maswali mengine ya nyongeza na fuatizi kwa watafitiwa wake. Aidha,

watafitiwa nao walikuwa na uhuru wa kujieleza kwa kina na kutoa maoni yao

kuhusu dhana na maswali yaliyoulizwa;

d) Malengo na maswali ya utafiti huu yalikusudia kuchunguza tabia, hali,

mitazamo na uzoefu wa watafitiwa kuhusu usawiri wa matukio ya mchakato

wa kujiua kwa kuhusisha na maisha yao halisi ya kila siku;

e) Utafiti huu ulihusisha uchambuzi wa data za maktabani kwa kujikita katika

riwaya teule na magazeti. Uchambuzi huo ulifafanuliwa kwa njia ya maelezo

na siyo namba au takwimu;

32

f) Utafiti ulijikita katika ufafanuzi wa matukio mbalimbali ya kujiua kwa

wahusika, sababu za mitanziko ya wahusika kama zinavyosawiriwa katika

riwaya teule, pamoja na tathmini ya uhusiano baina ya matukio ya mchakato

wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika

jamii.

Mkabala huu, basi, ulifaa kutumika katika utafiti huu kwa sababu data zilizopatikana

uwandani na maktabani zilihakikiwa, kuchanganuliwa na kufafanuliwa kwa njia ya

maelezo zaidi na siyo kwa njia ya takwimu. Lengo lake lilikuwa kupata matokeo ya

malengo mahususi kwa kuhusianisha na maswali ya utafiti yaliyokusudiwa kujibiwa.

Kimsingi, malengo ya utafiti huu hayakuhitaji data ama takwimu za kimahesabu.

Kwa maana hiyo, pale ambapo namba na idadi zilitumika, hazikutumika kama

mkabala wa kiidadi, bali kwa lengo la kutoa ufafanuzi tu.

3.4 Eneo la Utafiti

Utafiti huu ulifanyika maktabani na uwandani. Maeneo yaliyohusishwa katika

upatikanaji wa data ni Dodoma, Mwanza na Dar es Salaam. Dodoma ni eneo ambalo

mtafiti alikusudia kupata nyaraka mbalimbali zinazohusiana na mada ya utafiti wake

yakiwamo magazeti, kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma, pamoja na Maktaba ya Mkoa

huo. Nyaraka hizo zilikuwa mahususi kwa ajili ya kupata data za kimaktaba hususani

zile za magazetini ambazo zilihitajika zaidi kwa ajili ya lengo la tatu. Aidha,

alilitumia eneo hilo la Dodoma katika kufanya mahojiano na baadhi ya wataalamu

wa Fasihi, wataalamu wa Saikolojia, pamoja na wataalamu wa magonjwa ya akili ili

kupata data za uwandani ambazo zilikuwa mahususi kwa ajili ya lengo la tatu.

Mtafiti alikuwa na uhakika wa kuwapata watafitiwa hao kwa urahisi kutokana na

kuwapo kwa Chuo Kikuu cha Dodoma ambacho kina wataalamu wengi wa Fasihi na

Saikolojia. Vilevile, Mkoani Dodoma kuna hospitali maalumu ya magonjwa ya akili

iitwayo Mirembe na kuna madaktari bingwa wa magonjwa ya akili, ambapo mtafiti

aliweza kupata data za lengo la tatu zinazobainisha uhusiano wa magonjwa ya akili

na masuala ya kujiua.

Kwa upande wa Mkoa wa Mwanza, mtafiti alilitumia eneo hilo kwa lengo la kupata

data za uwandani kutoka katika jamii ya mwandishi. Data hizo ni zile zilizohusu

matukio ya mchakato wa kujiua kwa wahusika, pamoja na miktadha mbalimbali ya

33

kijamii juu ya usawiri wa mchakato wa kujiua. Mkoa wa Mwanza ulichaguliwa kama

mojawapo ya eneo la utafiti kwa sababu ndiko alikozaliwa mwandishi wa riwaya

teule. Aidha, riwaya hizo, kwa kiasi kikubwa, zinasawiri mandhari na matukio

yanayohusu mkoa huo. Kutokana na hilo, mtafiti alikuwa na uhakika wa kuwapata

kwa urahisi watafitiwa wake, hususani wale wa kabila la Wakerewe na Wakara

wanaopatikana katika kata ya Namagondo, kijiji cha Namagondo. Watafitiwa

wengine waliolengwa na utafiti huu kwa upande wa Mwanza ni viongozi wa dini,

viongozi wa serikali na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama. Kimsingi, data

zilizokusudiwa kupatikana katika Mkoa huo wa Mwanza, zilikuwa mahususi kwa

ajili ya lengo la tatu la utafiti wetu. Lengo hilo lilimtaka mtafiti kufanya tathmini ya

uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na

vichocheo vya mchakato wa kujiua katika jamii.

Vilevile, mtafiti alifanya utafiti katika Mkoa wa Dar es Salaam kwa sababu ya

kuwapo kwa maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam iitwayo Maktaba ya Dkt.

Wilbert Chagula na Makavazi ya Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI). Lengo

la kuchagua eneo hili lilikuwa kufanya mapitio ya nyaraka na maandiko mbalimbali

kuhusiana na utafiti wake. Maktaba hiyo ilitumika kwa kuwa, ikilinganishwa na

maktaba nyingine, hii ni kongwe zaidi. Hivyo, mtafiti alikuwa na uhakika wa kupata

maandiko mengi kutokana na tafiti na tahakiki nyingi kufanyika katika Chuo hicho

kikongwe hapa nchini. Aidha, eneo hili lilitumika katika kuwapata wataalamu wa

Fasihi na wahakiki wa kazi za Fasihi zikiwamo za Euphrase Kezilahabi. Kwa kiasi

kikubwa, data zilizolengwa kupatikana katika Mkoa wa Dar es Salaam zilikuwa ni za

kimaktaba. Data nyingine zilizopatikana kutoka kwa watafitiwa zililenga kushadidia

na kujaliza data za msingi za kimaktaba.

Kwa jumla, maeneo hayo, mbali na kuteuliwa kutokana na sababu zilizoelezwa, kwa

upande mwingine, yaliteuliwa ili kuwakilisha maeneo mengine ya Tanzania yenye

matukio ya kujiua. Uwakilishi huo unatokana na kutumia watafitiwa kutoka maeneo

tofauti, wenye umri na tajiriba tofauti, ambao waliweza kutoa mawazo yao kuhusiana

na matukio ya mchakato wa kujiua.

34

3.5 Walengwa wa Utafiti

Hii ni jamii iliyokusudiwa kutafitiwa na mtafiti ili iweze kutoa taarifa mbalimbali

kuhusiana na malengo ya utafiti wake. Kwa msingi huo, walengwa wa utafiti huu

waligawanywa katika makundi mawili. Kundi la kwanza, ni wango la utafiti, kwa

maana ya jamii ya watafitiwa kwa jumla. Kundi la pili, ni sampuli iliyoshughulikiwa,

ikiwa ni pamoja na usampulishaji wake.

3.5.1 Wango la Utafiti

Wango la utafiti ni jumla ya watu, vitu au elementi zote ambazo mtafiti amekusudia

kuvitumia katika utafiti wake ili kupata sampuli inayohitajika kulingana na mahitaji

ya utafiti wake. Wango la utafiti huu lilijumuisha:

a) Riwaya zilizoandikwa na Euphrase Kezilahabi: Hizi zilisaidia kuyabainisha

matukio mbalimbali ya mchakato wa kujiua kwa wahusika. Aidha, zilisaidia

katika kubainisha sababu za mitanziko ya wahusika, pamoja na kutathmini

uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya

teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii;

b) Taarifa za matukio ya kujiua kutoka katika vyanzo mbalimbali vya habari

yakiwamo magazeti na televisheni: Hizi zilisaidia kupatikana kwa matukio

halisi yanayohusu kujiua yanayozikumba jamii zetu. Data hizi zilitusaidia

zaidi katika kufanya tathmini ya uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya

mchakato wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua

katika jamii;

c) Wataalamu na wahakiki mbalimbali waliozisoma au kuzihakiki kazi

mbalimbali za Fasihi ya Kiswahili: Kwa jumla, hawa walisaidia katika

upatikanaji wa taarifa za matukio ya kujiua katika riwaya za Kiswahili. Pia,

walitoa maoni na mitazamo yao kuhusu matukio hayo ya kujiua;

d) Jamii ya mwandishi wa riwaya teule: Hii ilisaidia kutoa taarifa kuhusu jamii

yao pamoja na matukio ya kujiua kwa wahusika. Taarifa hiyo ilikuwa

mahususi kwa ajili ya lengo la tatu;

e) Viongozi wa dini: Hawa walisaidia kutoa mtazamo wao kuhusu matukio ya

kujiua kwa misingi ya dini wanazoziongoza;

f) Viongozi wa serikali: Hawa walisaidia katika upatikanaji wa data za lengo la

tatu, ambapo walieleza jitihada zinazofanywa na serikali katika kutoa elimu

kuhusu matukio ya watu kujiua;

35

g) Wanasaikolojia: Walitoa sababu za kisaikolojia za watu kufikia maamuzi ya

kujiua; na

h) Wataalamu wa magonjwa ya akili: Kundi hili lilisaidia kutoa ufafanuzi

kuhusu matukio ya watu kujiua, pamoja na uhusiano uliopo baina ya

magonjwa ya akili na matukio ya kujiua.

Taarifa zilizopatikana kutoka katika makundi hayo zilisaidia kujibu maswali ya

utafiti wetu na kuwezesha upatikanaji na ukamilifu wa tasinifu hii.

3.5.1.1 Usampulishaji

Usampulishaji ni mchakato wa kupata sampuli kutoka kwenye wango la utafiti. Hii

ni mbinu ya uteuzi wa sampuli, yaani mwongozo unaotumika katika kuteua kundi

dogo kutoka katika sampuli kuu ili kuwa kiwakilishi cha sampuli hiyo katika kutoa

data zinazohitajika katika utafiti husika (Babbie, 1999). Ufafanuzi huu una maana

kuwa usampulishaji ni mbinu ya kiufundi anayoitumia mtafiti katika kuchagua

wawakilishi wake kutoka katika sampuli kubwa ili kuwakilisha wango lote. Utafiti

huu ulitumia usampulishaji lengwa ili kupata sampuli ya watafitiwa.

Enon (1995) na Newman (2007) wanaeleza kuwa usampulishaji lengwa ni mbinu ya

usampulishaji ambapo mtafiti huchagua sampuli anayoihitaji kutokana na sifa za

watafitiwa alizozikusudia kwa kuzingatia malengo mahususi ya utafiti wake. Mbinu

hii hujikita katika matarajio kwamba mtafiti anataka kugundua, kuelewa au kupata

ufafanuzi kuhusu jambo fulani kulingana na vigezo alivyojiwekea. Vigezo hivyo

huakisi moja kwa moja lengo kuu la utafiti na huongoza katika mchakato wa

upatikanaji wa data zinazohitajika. Hii ni pamoja na kueleza umuhimu wa vigezo

hivyo katika utafiti husika. Mbinu hii ya usampulishaji lengwa ilimsaidia mtafiti

kuwapata watafitiwa wenye sifa zilizolengwa katika utafiti wake na namna

walivyokidhi haja na malengo ya utafiti wake. Hivyo, utafiti huu ulitumia

usampulishaji lengwa wa aina tatu kama zilivyoainishwa na Meriam & Tisdell

(2016):

a) Usampulishaji lengwa wa kipekee: Aina hii ilichaguliwa kwa kuzingatia sifa

za kipekee za sampuli zilizokidhi malengo ya utafiti wetu;

b) Usampulishaji tajwa au wa kupokezana: Katika aina hii ya usampulishaji,

watafitiwa wachache mahususi walifanyiwa mahojiano kuhusu mchakato wa

36

kujiua, kisha nao waliweza kuwataja watafitiwa wengine wenye ufahamu

kuhusiana na matukio ya mchakato wa kujiua hususani katika riwaya za

Euphrase Kezilahabi;

c) Usampulishaji wa kutegemea fursa: Mtafiti aliitumia aina hii ya

usampulishaji kuwapata watafitiwa, ambao kimsingi walihitajika sana ili

kutoa taarifa kuhusu utafiti, lakini kutokana na majukumu yao ya kazi,

ilikuwa vigumu kuwapata kwa urahisi. Hali hiyo ilimlazimu mtafiti

kuwafanyia mahojiano mara tu ilipopatikana fursa ya kufanya hivyo, huku

akizingatia suala la gharama na mahali.

3.5.1.2 Sampuli ya Utafiti

Sampuli ni sehemu ndogo ya kundi lengwa iliyochaguliwa kushiriki katika kutoa

data za utafiti (Gay, 1987; Kothari, 2009). Kipengele hiki ni muhimu sana katika

suala la utafiti kwa sababu humsaidia na kumpa mtafiti mwelekeo katika kupanga

muda na gharama za utafiti wake. Cohen na Lawrence (2000) na Bryman (2004)

wanaeleza kuwa uteuzi wa sampuli ni mchakato muhimu ambao humsaidia mtafiti

katika kuchagua kikundi cha vitu au watu kwa lengo la kutumiwa katika utafiti wake.

Sampuli hiyo hutumika kama kiwakilisho cha kundi zima litakalotafitiwa kwa

sababu si rahisi kulifanyia utafiti kundi zima. Sampuli ya utafiti wetu iliteuliwa kwa

kuzingatia mada ya utafiti, malengo na maswali ya utafiti, na ukubwa wa jamii ya

watafitiwa. Kwa hiyo, katika utafiti wetu, sampuli lengwa iliyotumika ina jumla ya

watoa taarifa thelathini na sita (36) ambao wamegawanyika katika makundi

yafuatayo:

a) Riwaya teule tatu (3) za Euphrase Kezilahabi, ambazo ni: Rosa Mistika,

Kichwamaji, na Dunia Uwanja wa Fujo. Riwaya hizi ziliteuliwa kutokana na

uchunguzi wa awali uliofanywa na mtafiti kuonesha kuwa zina sifa za

kipekee zinazoendana na mada na malengo ya utafiti wake. Sifa hizo ni

pamoja na uwezo wa kutoa data za kutosheleza utafiti wake, kwa sababu ni

za kihalisia na zina matukio yanayohusu kujiua kwa baadhi ya wahusika

wake. Riwaya nyingine za mwandishi huyu kama vile Nagona (1990) na

Mzingile (2011) si za kiuhalisia na hazina matukio ya kujiua, bali zinaelezea

zaidi kuhusu falsafa ya maisha kwa namna ya kiuhalisiajabu;

37

b) Magazeti matano (5) ya matoleo mbalimbali yenye taarifa za matukio ya

kujiua kwa miaka minne mfululizo, yaani 2016 hadi 2019. Mtafiti aliamua

kufuatilia matukio ya kujiua kwa miaka minne mfululizo ili kupata uwiano

wa utokeaji wa matukio hayo. Magazeti yaliyochaguliwa ni Habari Leo,

Mtanzania, Mwananchi, Nipashe, na Tanzania Daima. Haya yalichaguliwa

miongoni mwa mengi kutokana na upekee wake, kwa sababu hutoa taarifa za

kiuchunguzi na huchapishwa kila siku. Pia, mtafiti alibaini kuwa yalikuwa na

data za matukio ya kujiua zilizokuwa zinahitajika katika utafiti wake.

Vyombo vingine vya habari vilivyotoa data ni vinne (4), yaani ―Global TV on

line‖, ―Azam TV‖, Televisheni ya Afrika Mashariki (EATV), na ―BBC

Swahili‖. Hivi vilichaguliwa kwa kutegemeana na fursa, kwani matukio ya

kujiua yalitangazwa mtafiti akiwa anafuatilia taarifa mbalimbali za habari;

c) Wataalamu na wahakiki saba (7) wa kazi za Fasihi: Kati ya hao wanne (4)

walipatikana Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, mmoja (1) Chuo Kikuu cha

Dodoma, na wawili (2) walipatikana Dar es Salaam na Dodoma kwa

kutegemeana na fursa. Upatikanaji wa wataalamu na wahakiki hawa

ulizingatia nafasi yao kitaaluma, ukongwe wao katika kufundisha somo la

Kiswahili, pamoja na kujihusisha kwao na masuala mbalimbali ya utafiti wa

Kiswahili. Idadi hiyo ya wataalamu ilifikiwa baada ya kupatikana kwa data

muhimu zilizokuwa zinahitajika kulingana na malengo ya utafiti huu.

Wataalamu hawa walisaidia kutoa data kuhusu mwandishi wa riwaya teule na

mtazamo wao juu ya matukio yanayounda mchakato wa kujiua katika riwaya

teule;

d) Watafitiwa kumi (10) (watu wazima kuanzia miaka arobaini na kuendelea na

vijana wenye umri kati ya miaka kumi na mitano hadi arobaini), kutoka

katika Mkoa wa Mwanza, Wilaya ya Ukerewe. Upatikanaji wa watafitiwa

hawa ulizingatia uzoefu wao wa kuishi katika eneo husika na namna

wanavyomfahamu Euphrase Kezilahabi, au kazi zake, au familia yake. Aidha,

mtafiti aliomba ridhaa kutoka mamlaka ya eneo husika ili iweze kumsaidia

kuwapata watafitiwa wenye sifa zinazohitajika. Mgawanyo wake ulikuwa

kama ifuatavyo: wanaume 2, wanawake 3, vijana wa kiume 2, na vijana wa

kike 3. Mgawanyo wa idadi unaozingatia uwakilishi wa kijinsia ulilenga

kupata ulinganifu wa mitazamo kutoka jinsi hizo kuhusu usawiri wa

38

mchakato wa kujiua, na fursa ya upatikanaji wao. Watafitiwa hawa

walichaguliwa kwa sababu wanaishi katika eneo ambalo mwandishi wa

riwaya teule alizaliwa, na pia kazi zake kwa kiasi kikubwa zinasawiri eneo

hilo. Hivyo, idadi hiyo ilitosha kutoa data wakilishi zinazohusu matukio ya

mchakato wa kujiua na athari za miktadha ya maisha ya jamii iliyomwibua

mwandishi wa riwaya teule kulingana na uzoefu wao;

e) Viongozi wawili (2) wa dini kutoka Mkoa wa Mwanza. Upatikanaji wa

viongozi hawa ulizingatia nafasi na majukumu yao ya uongozi katika

kuihudumia jamii. Viongozi wote wawili waliopatikana walitoka katika dini

ya Kikristo. Hatukufanikiwa kuwapata viongozi wa dini ya Kiislamu

kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu. Hata hivyo, data

zilizotolewa na viongozi wa dini ya Kikristo, zilitosheleza mahitaji ya data

zilizokuwa zinahitajika katika kukamilika kwa utafiti huu;

f) Watafitiwa wengine watano (5) walikuwa ni wataalamu wa masuala ya

Saikolojia na magonjwa ya akili kutoka katika Mkoa wa Dodoma.

Upatikanaji wa wataalamu hawa pia ulizingatia nafasi yao kitaaluma, na

ukongwe wao katika masuala ya kutoa nasaha na katika kuhudumia

wagonjwa wa akili. Hawa waligawanywa katika makundi kama ifuatavyo:

wataalamu wa Saikolojia wawili (2) - mwanaume mmoja (1) na mwanamke

mmoja (1); na wataalamu wa magonjwa ya akili watatu (3) - wanaume

wawili (2), na mwanamke mmoja (1). Mgawanyo wa idadi unaozingatia

uwakilishi huo kijinsia ulikusudia kupata ulinganifu wa mitazamo kutoka

jinsi hizo kuhusu usawiri wa mchakato wa kujiua. Kundi hili la wataalamu

wa Saikolojia na magonjwa ya akili lilichaguliwa ili kusaidia kufafanua

kitaalamu kuhusu, uhusiano wa masuala ya kiakili na kisaikolojia, namna

yanavyohusika katika mchakato mzima wa mtu kujiua. Pia, lilisaidia

kubainisha mazingira, dalili za mtu anayekusudia kujiua, na tahadhari

zinazotakiwa kuchukuliwa ili kumsaidia mtu mwenye dalili za kutaka kujiua.

3.6 Ukusanyaji wa Data

Ukusanyaji wa data katika utafiti wowote ule unahusu kukusanya taarifa mahususi,

zinazokusudiwa kutoa au kupinga uhalisi wa mambo fulani (Kombo na Tromp, 2006).

39

3.6.1 Njia za Ukusanyaji wa Data

Data za utafiti huu zilikusanywa kwa kutumia mbinu kuu mbili: usomaji na uchambuzi

makini wa matini teule (riwaya, magazeti na ufuatiliaji wa taarifa za habari), na

mahojiano.

3.6.1.1 Usomaji na Uchambuzi Makini wa Matini

Mtafiti alikwenda maktabani ambako alizisoma na kuzichambua kwa makini riwaya

teule (Rosa Mistika, Kichwamaji, na Dunia Uwanja wa Fujo), magazeti teule

(Habari Leo, Mtanzania, Mwananchi, Nipashe, na Tanzania Daima), na ufuatiliaji

wa taarifa mbalimbali za habari. Alifanya hivyo ili kupata data msingi, yaani data

halisi zilizokusanywa kwa mara ya kwanza na ambazo zilihitajika kulingana na

malengo ya utafiti wake. Katika hatua hiyo, aliweza kubainisha data za matukio ya

mchakato wa kujiua yanayosawiriwa katika riwaya teule, katika magazeti teule, na

taarifa mbalimbali za habari. Pia, alitumia mbinu hiyo katika kupata data kuhusu

sababu za mitanziko ya wahusika zinazosawiriwa katika riwaya teule. Vilevile,

mbinu hii ilimsaidia kupata data kuhusu matukio ya mchakato wa kujiua

yanayosawiriwa katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika

jamii.

Kwa msingi huo, data zilizopatikana kutokana na usomaji na uchambuzi makini wa

matini zilikuwa mahususi katika kupima malengo yote matatu ya utafiti huu.

Mwongozo wa usomaji na uchambuzi wa matini ulitumika katika kufanikisha mbinu

hii. Pia, vifaa kama vile kompyuta pakatwa, shajara, kinyonyi, simu ya mkononi, na

kalamu vilitumika katika kurekodi, kutunzia data na kuandikia taarifa zilizopatikana

maktabani.

3.6.1.2 Mahojiano

Drake na Linda (2011) wanaeleza kuwa mahojiano ni majibizano ya ana kwa ana

yanayohusisha watu wawili au zaidi, yenye lengo la kukusanya taarifa au maoni

yanayohusu mada fulani. Pia, mahojiano hayo yanaweza kuwa ya simu au barua

pepe. Utafiti huu ulitumia mbinu ya mahojiano nusu funge, kwa kuwa licha ya

kuwapo kwa maswali yaliyoongoza mahojiano baina ya mtafiti na watafitiwa, mtafiti

na watafitiwa wake hawakufungwa na mwongozo huo. Mbinu hii ilitumika ili kupata

data za moja kwa moja kutoka kwa watafitiwa. Mtafiti alikuwa huru kuuliza maswali

40

mengine fuatizi mbali na yale yaliyomo katika mwongozo wa mahojiano kulingana

na muktadha wa watafitiwa wake. Aidha, watafitiwa nao walikuwa huru kueleza

zaidi ya kile kilichoandaliwa katika mwongozo wa mahojiano.

Mbinu ya mahojiano ilitumika kukusanya data za uwandani katika maeneo matatu ya

watafitiwa, kama ifuatavyo: Mosi, wataalamu na wahakiki waliowahi kutafiti au

kufanyia tahakiki riwaya za Kiswahili, hususani riwaya teule. Kundi hili lilihojiwa ili

liweze kutoa taarifa juu ya mwandishi wa riwaya teule na namna linavyofahamu

matukio ya mchakato wa kujiua yanayosawiriwa katika riwaya hizo, sababu za

mitanziko ya wahusika, pamoja na kutoa tathmini ya uhusiano baina ya usawiri wa

matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya

kujiua katika jamii. Watafitiwa hao walipatikana Dodoma na Dar es Salaam. Pili,

wataalamu wa saikolojia na wale wa magonjwa ya akili waliopatikana katika Mkoa

wa Dodoma. Kundi hili lilihojiwa ili kutoa ufafanuzi wa kitaalamu kuhusu uhusiano

uliopo baina ya masuala ya magonjwa ya akili na saikolojia katika mchakato wa mtu

kujiua. Pia, lilisaidia kubainisha mazingira na dalili za mtu anayekusudia kujiua.

Tatu, watafitiwa kutoka Mkoani Mwanza. Hawa walihojiwa ili kutoa taarifa

zinazohusiana na mwandishi wa riwaya teule na uzoefu wa maisha ya jamii ya

mwandishi huyo. Mtafiti alirekodi majibu katika shajara na kwenye kinasa sauti kwa

ajili ya uchambuzi. Kwa kiasi kikubwa, mbinu hii ilisaidia kupatikana data

zilizokuwa mahususi kwa ajili ya lengo la tatu la utafiti huu. Zana iliyotumika

sambamba na njia hii ni mwongozo wa mahojiano. Pia, vifaa kama vile shajara,

kinasa sauti, kamera, simu ya mkononi, na kalamu vilitumika katika kurekodi na

kutunzia data zilizopatikana uwandani.

3.6.2 Mchakato wa Ukusanyaji Data

Mchakato wa kukusanya data ni suala muhimu sana linalopaswa kuzingatiwa na

mtafiti ili kuthibitisha au kupinga uhalisi wa mambo fulani. Katika utafiti huu, taarifa

mbalimbali zilikusanywa maktabani na uwandani kwa kutumia vifaa mbalimbali

vilivyoandaliwa na mtafiti. Mtafiti alianza na mbinu ya usomaji na uchambuzi

makini wa matini teule ili kupata data msingi kwa ajili ya malengo yote matatu. Kwa

kuwa usomaji na uchambuzi huo wa matini teule kwa kiasi kikubwa ulifanyikia Dar

es Salaam na Dodoma, mtafiti alitumia muda huo pia kuwatafuta watafitiwa

41

kulingana na sampuli yake kwa ajili ya kupata data za uwandani. Muda wa miezi

miwili ulitumika katika kukamilisha mchakato huo.

Baada ya kukamilika kwa data za maktabani na za uwandani katika Mkoa wa Dar es

Salaam na Dodoma, mtafiti alikwenda jijini Mwanza ili kupata data nyingine za

uwandani kama ilivyobainishwa katika sampuli yake ya utafiti. Akiwa katika Mkoa

wa Mwanza, alifanya mahojiano na jamii ya mwandishi wa riwaya teule pamoja na

viongozi wa dini kuhusiana na usawiri wa mchakato wa kujiua. Hata hivyo, kutokana

na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wake, mtafiti hakufanikiwa kufanya mahojiano

na Mkuu wa Mkoa, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, na

Kamanda wa Polisi Wilaya ya Ukerewe. Kutokana na hilo, mtafiti aliamua kutumia

data zilizopatikana katika vyanzo mbalimbali vya habari yakiwamo magazeti na

televisheni ili kupata matokeo thabiti kulingana na malengo yake. Muda uliotumika

katika kukusanya data za uwandani Mkoani Mwanza ulikuwa mwezi mmoja. Katika

mchakato mzima wa ukusanyaji wa data, mwongozo wa usomaji na uchambuzi

makini wa matini ndio uliotumika ili kupata data za maktabani na mwongozo wa

mahojiano kwa data za uwandani.

3.7 Mbinu za Uchambuzi wa Data

Baada ya kukamilika kwa mchakato wa ukusanyaji wa data za utafiti, mtafiti

alizichambua data zake kwa kutumia mkabala wa kitaamuli. Mbinu iliyotumika

katika uchambuzi wa data ilikitwa katika mwegamo wa kimaudhui. Sababu za

kutumia uchambuzi wa kimaudhui ilikuwa ni kumwezesha mtafiti kuunganisha,

kuainisha, kulinganisha na kufafanua data zilizopatikana maktabani na zile za

uwandani ili kupata matokeo bora. Kwa mujibu wa Patton na Michael (2002)

uchambuzi wa data kitaamuli kwa kutumia mbinu ya kimaudhui ni mchakato wa

kuzibadilisha na kuzichakata data zilizokusanywa kwa njia ya maandishi na sauti na

kuzichuja kwa kuchukua taarifa muhimu na kuzipanga kulingana na namna

zinavyowiana kimaudhui. Nao Kombo na Tromp (2006) wanaeleza kuwa

uchanganuzi wa kimaudhui ni mbinu ya uchambuzi ambayo huziweka mada

kulingana na namna zinavyofanana na kuhusiana.

Katika utafiti huu, mtafiti alizichambua na kuzipanga data katika makundi kulingana

na malengo na maswali ya utafiti wake kama ifuatavyo: Kundi la kwanza lilihusu

42

data zilizobainisha matukio ya mchakato wa kujiua na namna yanavyosawiriwa

katika riwaya teule. Kundi la pili lilihusu data zilizolenga kuchunguza sababu za

mitanziko ya wahusika zinazosawiriwa katika riwaya teule. Na, kundi la tatu lilikuwa

na data zilizolenga kutathmini uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya mchakato

wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii. Data

za malengo hayo zilipatikana kwa mbinu ya usomaji na uchambuzi makini wa matini

maktabani na mahojiano baina ya mtafiti na watafitiwa uwandani. Baada ya

kuzipanga data hizo katika makundi, hatua iliyofuata ilikuwa ni kuzifafanua kwa

kutumia maelezo kulingana na malengo ya utafiti na kwa kuzingatia mwoano wa

kimaudhui, huku mtafiti akiongozwa na nadharia ya Udhanaishi na ile ya Sosholojia

ya Kifasihi ili kujibu maswali ya utafiti wake.

3.8 Itikeli za Utafiti

Itikeli ni dhana inayotumika kumaanisha usahihi wa matendo katika mahusiano ya

watu wa jamii fulani yaliyokubaliwa na jamii hiyo kuwa ndiyo sahihi au si sahihi

kwa kuzingatia matakwa ya jamii hiyo (Faustine, 2017). Utafiti huu ulizingatia

taratibu zote muhimu kabla ya kuanza kufanyika na wakati wa ufanyikaji wake.

Mtafiti alilazimika kuzingatia itikeli za utafiti, kuanzia hatua ya ukusanyaji wa data,

uchanganuzi wake, pamoja na uandishi wa matokeo ya utafiti. Mambo muhimu

aliyoyazingatia ni:

a) Kanuni na taratibu zote za utafiti za Chuo Kikuu cha Dodoma, ikiwa ni

pamoja na kuomba barua ya utambulisho, na vibali mbalimbali vilivyompa

ruhusa ya kufanya utafiti katika maeneo yaliyobainishwa katika sampuli yake

ya utafiti. Barua na vibali hivyo, aliviwasilisha katika mamlaka za maeneo

aliyoomba kufanyia utafiti, ambayo ni Dar es Salaam, Dodoma, na Mwanza

ili mamlaka hizo nazo zimpe ridhaa hiyo;

b) Kuwaomba ridhaa watafitiwa wake ili aweze kutimiza jukumu la kuhojiana

nao. Aidha, aliwaeleza na kuomba ridhaa yao ili awarekodi na kunukuu

taarifa walizozitoa kwa ajili ya kuzitumia katika utafiti wake;

c) Kuwafafanulia watafitiwa wake malengo na umuhimu wa utafiti huo na

kuwaeleza kwamba taarifa walizotoa zitakuwa ni siri baina yake na wao, na

kwamba zitatumika kwa shughuli ya utafiti lengwa tu;

43

d) Maadili na itikeli za jamii ya watafitiwa, ikiwa ni pamoja na kuvaa mavazi ya

heshima, na kuzingatia mila na desturi zao;

e) Kuwafafanulia watafitiwa haki yao ya msingi wakati wote wa utafiti, ikiwa ni

pamoja na kusitisha mahojiano palipokuwa na haja ya kufanya hivyo,

kufichwa kwa majina yao walipotaka iwe hivyo, uhuru wa kutoa taarifa na

kuuliza maswali na mengine ya namna hiyo.

3.9 Uhalali na Uthabiti wa Matokeo ya Utafiti

Ponera (2014) anaeleza kuwa uhalali wa utafiti maana yake ni hali ya utafiti kuwa na

uwezo wa kupima jambo au mambo yaliyotakiwa kupimwa au kutafitiwa tu. Kuhusu

uthabiti wa utafiti, anaeleza kuwa ni hali ya utafiti kutoa matokeo yanayowiana ikiwa

utafiti utafanyika katika wakati mwingine, mahali pengine, au na mtu mwingine. Hii

ina maana kuwa matokeo ya utafiti yanatakiwa kuthibitisha kile ambacho mtafiti

alikusudia kukipima kulingana na malengo na mipaka ya utafiti wake bila kuathiriwa

na mambo yaliyo nje ya malengo ya utafiti. Kwa mantiki hiyo, ili kuhakikisha kuwa

utafiti huu unakuwa na uhalali na thabiti, mtafiti alikwenda katika maeneo halisi ili

kupata data za uwandani, alitumia matini sahihi kulingana na sampuli ya utafiti

wake, alipata data kutoka katika vyanzo sahihi, pamoja na kutumia njia na mbinu

sahihi katika ukusanyaji na uchanganuzi wa data.

Kwa jumla, uhalali na uthabiti wa utafiti huu ulitokana na namna mtafiti

alivyohusisha mbinu, pamoja na utoshelevu wa njia za kukusanyia data za utafiti

wake. Pia, misingi ya nadharia zilizotumika ilimwongoza katika kuchanganua na

kufasiri data kulingana na malengo mahususi.

3.10 Muhtasari wa Sura ya Tatu

Sura hii imeshughulikia mbinu mbalimbali zilizomwongoza mtafiti katika mchakato

mzima wa ukusanyaji wa data na uchambuzi wake. Vipengele vilivyoshughulikiwa

ni usanifu wa utafiti, mkabala wa utafiti, eneo la utafiti, na walengwa wa utafiti.

Vipengele vingine ni mchakato wa ukusanyaji wa data, mbinu za uchambuzi wa

data, maadili na itikeli za utafiti, pamoja na uhalali na uthabiti wa data. Mbinu hizi

zilisaidia kupata matokeo ya utafiti ili kukamilisha uandishi wa tasinifu yetu. Sura

inayofuata inahusu uwasilishaji wa data na mjadala wa matokeo ya utafiti wetu.

44

SURA YA NNE

UWASILISHAJI WA DATA NA MJADALA WA MATOKEO YA UTAFITI

4.1 Utangulizi

Sura hii inawasilisha data na kujadili matokeo kulingana na malengo yaliyoongoza

utafiti wetu. Mjadala huo umegawanywa katika sehemu kuu tano. Sehemu ya

kwanza ni utangulizi wa jumla. Sehemu ya pili imebainisha na kujadili matukio

mbalimbali ya mchakato wa kujiua yanayosawiriwa katika riwaya teule za Euphrase

Kezilahabi. Sehemu ya tatu imechunguza sababu za mitanziko ya wahusika

zinazosawiriwa katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi. Sababu hizo zimewekwa

katika makundi manne, yaani sababu za kijamii, kiutamaduni, kiuchumi na kifalsafa.

Sehemu ya nne imetathmini uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya mchakato wa

kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii. Sehemu

ya tano inahitimisha kwa kutoa muhtasari wa jumla kuhusiana na mambo

yaliyojadiliwa katika sura nzima.

4.2 Matukio ya Mchakato wa Kujiua katika Riwaya Teule za Euphrase

Kezilahabi

Sehemu hii inawasilisha data na matokeo yanayohusiana na swali la kwanza la

utafiti lisemalo ‗Matukio yanayounda mchakato wa kujiua katika riwaya teule za

Euphrase Kezilahabi yana usawiri gani?‘ Sehemu yenyewe imegawanyika katika

vijisehemu sita. Mosi, muhtasari wa riwaya ya Rosa Mistika. Pili, matukio ya

mchakato wa kujiua katika riwaya ya Rosa Mistika. Tatu, muhtasari wa riwaya ya

Kichwamaji. Nne, matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya ya Kichwamaji.

Tano, muhtasari wa riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo. Sita, ni matukio ya mchakato

wa kujiua katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo. Kufahamika kwa matukio hayo

kunaweka bayana sababu za wahusika hao kujiua, mapito yao katika kupambana na

maisha, na mitazamo yao kuhusu dhana ya maisha.

Kwa jumla, matukio ya kujiua yanaweza kuwekwa katika makundi mawili, yaani,

kujiua kimwili na kujiua kiroho. Kujiua kimwili ni kitendo cha mhusika

kutenganisha mwili wake na roho na kuwa ndiyo hatima ya maisha yake hapa

duniani (Kubler-Ross, 1991). Kwa upande mwingine, kujiua kiroho ni kitendo cha

mtu kujitenga na Mungu kutokana na kutenda dhambi na hivyo kuyakosa maisha ya

milele (ufalme wa Mungu) (Luka 23:46; Rumi 6:23 katika Biblia Takatifu, 1997).

45

Mtazamo huu unahusiana zaidi na masuala ya kiimani (kidini). Kimsingi, katika

tamaduni nyingi duniani, hususani za Kiafrika, kujiua ni kitendo kisichokubalika

kijamii na kiimani. Utafiti huu umejikita zaidi katika kuchunguza matukio ya kujiua

kwa wahusika kimwili kwa kubainisha matukio hayo katika riwaya za Rosa Mistika,

Kichwamaji, na Dunia Uwanja wa Fujo.

4.2.1 Muhtasari wa Riwaya ya Rosa Mistika

Rosa Mistika (1971) ni riwaya ya kwanza kuandikwa miongoni mwa riwaya za

Euphrase Kezilahabi. Inajadili dhana ya maisha. Jambo hili linamshughulisha sana

mwandishi huyu katika takribani kazi zake zote. Alianza kuiandika alipokuwa

anasoma katika Seminari ya Mtakatifu Maria huko Nyegezi, Mwanza na

kuikamilisha akiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Mulokozi, 1983). Ilichapishwa

kwa mara ya kwanza mwaka 1971. Kwa kiasi kikubwa, inaelezea maisha ya mhusika

mkuu, Rosa Mistika, tangu utoto wake, matukio na misukosuko aliyopitia katika

maisha yake, hadi kuamua kujiua kwake. Wahusika wengine ni pamoja na Flora,

Zakaria, Regina, Deogratias, na Charles Lusato. Hawa wamesaidia sana katika

kuikamilisha riwaya hii, kwani wamemjenga mhusika mkuu katika mapito ya maisha

yake, hadi kufikia hatua ya kuyakana maisha yake kwa kujiua.

Mandhari yanayosawiriwa katika riwaya hii, kwa kiasi kikubwa, ni ya Ukerewe,

ambako ni chimbuko la mwandishi na, kwa kiasi kidogo, Morogoro na Mwanza.

Morogoro ndiko Rosa Mistika alikosomea mafunzo yake ya Ualimu, na Mwanza ni

eneo alilopangiwa kufanya kazi yake ya Ualimu. Tunakubaliana na fikra za

Mulokozi (k.h.j) kuwa riwaya hii inadhihirisha mambo makuu matatu, ambayo ni:

athari ya maisha ya Seminari kwa mwandishi, ujana na ubalehe wake, na dalili za

mtazamo wa kukata tamaa katika kutafakari maisha.

Msingi wa riwaya hii ni tukio la kujiua kwa mhusika mkuu, Rosa Mistika. Ijapokuwa

anaacha ujumbe kwamba kujiua kwake kunasababishwa na tukio la kuachwa

kimapenzi na mchumba wake Charles, utafiti umebaini kwamba tukio hili

halikumtokea ghafla, bali ni kilele tu cha matukio kadhaa aliyoyapitia katika maisha

yake. Uthibitisho wa hoja hii ni kwamba mwishoni mwa riwaya, Rosa Mistika,

akiwa mbele ya Mungu, anatakiwa kujibu mashtaka kutokana na kujiua huko;

ambapo, badala ya kumtaja Charles kuwa ndiye chanzo cha kufanya hivyo,

46

anaelekeza lawama zake kwa baba yake, Zakaria. Mashtaka hayo ni kama

yanavyoelezwa na mwandishi katika dondoo lifuatalo:

Mungu: Rosa kwa nini umejiua?

Rosa: Ee Mungu wangu. Haya yote yametokea kwa sababu ya

baba yangu.

Mungu: Rosa, ninakuuliza tena, kwa nini umejiua?

Rosa: Ee Mungu wangu. Haya yote yametokea kwa

sababu ya baba yangu.

Mungu: Zakaria una usemi gani kujitetea?

Zakaria: Ee Mungu wangu. Haya yote yametokea kwa

sababu ya ubaya na udhaifu wake mwenyewe.

Mungu: Rosa. Una ushahidi?

Rosa: Ndiyo, Bwana. Ulimwengu mzima.

Mungu: Na Zakaria?

Zakaria: Ulimwengu mzima, Bwana Mungu wangu

(uk. 98).

Katika dondoo hili, Mungu anamuuliza Rosa swali la msingi: ―Rosa, kwa nini

umejiua?‖ Swali hili lilikuwa kiini cha utafiti uliofanyika. Ili kuonesha uzito na

ukubwa wa tukio hili, swali hilohilo linaulizwa mara mbili. Hata hivyo, badala ya

kujibu kwamba amejiua kwa sababu ya kuachwa na Charles, kama anavyoeleza

katika barua yake kabla ya kujiua kwake, anaelekeza lawama zake kwa baba yake,

Zakaria. Anapojitetea, ―Ee Mungu wangu. Haya yote yametokea kwa sababu ya baba

yangu‖ anatudokeza kwamba kinachosababisha kujiua kwake siyo tukio la kuachwa

na Charles peke yake, bali kuna matukio mengine. Kwa msingi huo, jibu hili lilimpa

msukumo zaidi mtafiti wa kuona kwamba kumbe kujiua ni mchakato

unaofungamana na matukio mengi ndani yake.

Aidha, kwa kuwa jambo hili linasawiriwa katika kazi za Fasihi, ni uthibitisho kuwa

Fasihi ina uhusino na jamii. Kutokana na hilo, mtafiti alipata msukumo wa kufikiri

kwamba, inawezekana pia watu wanapojiua katika jamii zetu huwa hawajiui kwa

sababu ya jambo au tukio moja tu, bali huwa ni mchakato unaofungamana na

matukio mengi ndani yake. Kwa msingi huo, matokeo yanaonesha kuwa matukio ya

mchakato wa kujiua kwa Rosa Mistika katika riwaya hii ni: kupigwa na baba yake,

kuwachongea wasichana wenzake, kuota ndoto, na kusimamishwa shule,

kufumaniwa na kufukuzwa chuo. Matukio mengine ni kutoa mimba, kujitenga na

kutengwa na jamii yake, na kuachwa na mchumba wake. Matukio haya yamejadiliwa

kama ifuatavyo:

47

4.2.1.1 Kupigwa na Baba yake

Utafiti umebaini kwamba, hili ni tukio la kwanza kabisa linalounda mchakato wa

kujiua kwa Rosa Mistika katika riwaya hii. Imebainika kwamba, akiwa mwanafunzi

wa darasa la sita, alipata kipigo kikali kutoka kwa baba yake, Zakaria, mara tu baada

ya kugundulika kwamba amepokea barua ya mapenzi kutoka kwa Charles Lusato.

Huu ndio ulikuwa mwanzo wa kukata tamaa ya maisha yake, kumwogopa,

kumkasirikia na kumchukia baba yake, kuwachukia na kuwakasirikia wavulana, na

kukataa kuwa karibu nao. Mwandishi anaeleza kuwa baada ya Zakaria kubaini kuwa

Rosa amepokea barua hiyo, alichafuka na kumwita:

Rosa alikuja hali shuka ikiteremka chini. Kabla hajasema

lolote alipigwa na kuanguka chini. Alijaribu kuamka na

kukimbia lakini shuka ilimtegatega na kumwangusha chini

tena. Alikuwa sasa mikononi mwa baba yake. ―Lete hiyo

barua iko wapi? Pamoja na shilingi ulizopewa. Unafikiri sisi

hapa maskini?‖ Rosa alipigwa tena na tena, makofi

yalikwenda mfululizo hata damu ikamtoka puani na mdomoni.

Alilia, ―baba nihurumie, sitarudia tena, nimekoma.‖ Rosa

alinyang‘anywa shuka (uk. 6).

Kinachobainika katika dondoo hili ni kwamba, Rosa hapewi nafasi ya kujitetea na

kueleza ukweli wa jambo hilo, badala yake anashushiwa kipigo kikali, kiasi cha

kumwacha akiwa nusu uchi. Matokeo yake ni kwamba tukio hili linamjengea chuki

dhidi ya baba yake kutokana na vitisho vyake vya kumbana na kumnyima uhuru kwa

kumchunga sana. Pia, linamfanya ajihisi kuwa hapendwi na hana usalama wowote,

kwani kipigo hicho kinatia pengo kubwa katika ujenzi wa maisha yake. Imebainika

kwamba baada ya kipigo hicho, Zakaria huku akiwa na fimbo mkononi, anaongozana

naye hadi chumba cha watoto hali akiunguruma na kusema: ―Lazima uonyeshe barua

hiyo! Unataka kuniletea umalaya wa mama yako hapa!‖ (uk. 7). Kauli hii ya dharau

na udhalilishaji dhidi ya mwanamke, inamjengea Rosa mtazamo wa kuona kuwa

kumbe mwanamke ni kiumbe duni na kisichokuwa na thamani yoyote mbele ya

mwanamume. Matokeo yake, anashindwa kuelewa maana ya maisha, na hivyo,

anaanza kukata tamaa kwa kuyaona kuwa hayana maana.

Mwandishi anathibitisha jambo hili anapoeleza kwamba kutokana na kubanwa na

Zakaria, Rosa anashindwa kujitetea na kujiokoa, hivyo analazimika kuonesha barua

na pesa alizopewa na Charles. Mwandishi anaeleza kwamba:

48

Rosa, akiwa na haya nyingi, alichukua mfuko wake wa

madaftari, na katika daftari la Jiografia alitoa barua hiyo

pamoja na shilingi tano. Alimpa baba shilingi hizo; lakini ile

barua aliikunjakunja na kuitupia mdomoni. Alijaribu kuitafuna

lakini babake alimkaba koo. Rosa hakuitema. Zakaria alikaza

mkono. Macho ya Rosa yalianza kuwa mekundu, ulimi

ulimtoka na barua ilianguka chini. Ilikuwa na utelezi kama

kuku aliyetapikwa na chatu. Zakaria aliiokota mara moja.

―Sema nani amekupa barua hii!‖ ―Charles,‖ Rosa alitamka

kwa shida (uk. 7).

Tukio hili la kikatili linafanywa na baba dhidi ya mtoto wake wa kike, ambaye yuko

katika hatua za balehe. Pambano hili linatokea Rosa akiwa hana welewa wa kutosha

kuhusu ulimwengu huo mpya wa mapenzi, huku akikabiliwa na mabadiliko kadhaa

yanayoendelea kutokea katika maisha yake kimwili na kiakili. Ni wakati huu

ambapo anahitaji kupewa mwanga na miongozo mbalimbali kuhusiana na suala la

maisha yake, na namna ya kuzikabili changamoto zilizoko mbele yake. Badala

yake, licha ya kupewa kipigo kikali na cha kikatili kiasi hicho, analazimishwa

kuongozana na baba yake hadi nyumbani kwa Ndalo, mjomba wake Charles. Huko,

Zakaria anampa Charles onyo na maneno makali na mazito. Anamwambia:

―Charles! Tangu leo ukome kutembea na binti yangu. Chukua

vishilingi vyako (alimtupia shilingi tano). Unafikiri sisi ni

maskini tusio na mikono!‖ Rosa alilia karibu usiku kucha (uk.

8).

Matokeo yanaonesha kuwa malezi haya ya vitisho, ukali na ukatili wa Zakaria

yanamfanya Rosa awachukie wanaume na kujitenga nao kabisa. Kwa wakati huu,

anashindwa kuelewa kwamba kuwachukia wanaume siyo suluhisho la maisha yake,

bali ni mtihani mgumu anaokabiliana nao ili kuwaelewa. Badala ya wazazi wake

(Zakaria) kuwa watu wa kwanza kumwelekeza ili aufalu mtihani huo, wao

wanakuwa kitisho zaidi kwake. Hili linadokezwa na mwandishi anaposema:

Hivi ndivyo Rosa alivyolelewa; hivyo ndivyo alivyotunzwa;

hivyo ndivyo alivyochungwa na baba yake. Tangu siku hiyo

alikoma kutembea na mvulana yeyote. Na Zakaria alipojua

hayo alifurahi sana. Alijidai kwamba yeye alifahamu jinsi ya

kulea binti zake – hasa alipokuwa amekunywa kidogo.

Hakufahamu kuwa Rosa alikuwa katika rika baya, na kwamba

ukali ulikuwa haufai; hakufahamu kuwa mabinti wanahitaji

uhuru fulani kutoka kwa baba zao; hakufahamu kwamba kwa

kumpiga bintiye alikuwa akiingilia utawala usio wake, na

49

kwamba kuhusu maoni ya ndoa yake alifahamu kidogo sana;

na hakufahamu kwamba Rosa alihitaji kuwafahamu wavulana.

Kwa hiyo, kutokana na malezi ya namna hii, Rosa alianza

kuwaangalia wavulana kama watu wasiopaswa kuandamana

nao, au hata kuzungumza nao (uk. 9).

Dondoo hili linaonesha kuwa malezi ya kunyimwa uhuru, ukali, vitisho na ukatili wa

Zakaria dhidi ya binti yake, ndiyo yanayojenga chuki na uhasama baina yao. Ni

kweli kwamba katika jamii kuna miiko na maadili mbalimbali yanayotakiwa

kufuatwa na kuzingatiwa. Hata hivyo, kutokana na kufungwa na sheria, taratibu na

miiko ya jamii, watu hulazimika kukengeuka misingi hiyo na kutafuta uhuru katika

kujiamulia mambo yao. Mambo haya ndiyo yanayozingatiwa sana katika nadharia ya

Udhanaishi, kwani mtu hutafuta uhuru binafsi na uwezo wa kujifikiria na kujiamulia

mambo yake mwenyewe. Pia, mtu huyo huwa na wajibu wake katika ulimwengu.

Utafiti ulibaini kwamba malezi ya ukali, ukatili na vitisho kwa mtoto hayafai, kwa

sababu humjengea nidhamu ya woga na husababisha akengeuke misingi ya malezi

aliyopewa kwa kutafuta uhuru binafsi. Kinachotakiwa ni kumwonya, kumwelekeza

na kumfunza namna ya kuishi na kukabiliana na changamoto mbalimbali za kimaisha

zitokanazo na mazingira yake. Kama inavyojitokeza kwa Rosa Mistika, utafiti

umebaini kwamba kutokana na msichana huyo kukosa mwongozo imara wa namna

ya kuwafahamu na kukabiliana na changamoto zitokanazo na wanaume,

anapotambua kwamba kuna uzuri ndani yao, anazidisha chuki kwa baba yake. Hata

uhusiano wake na baba yake unabadilika baada ya kutambua ukweli kwamba chanzo

cha matatizo yake ni malezi kutoka kwa baba yake. Matokeo yake ni kwamba

uhusiano wao unageuka na kuwa uadui, huku akipinga waziwazi mfumo wa malezi

ya baba yake. Hii inajidhihirisha kupitia majibizano makali baina yake na Zakaria

anaposema kwamba: ―Rosa, tangu leo wewe si mwanangu‖, ambapo Rosa naye bila

kusita anamjibu baba yake kwamba: ―Tangu leo, wewe si baba yangu.‖ (uk. 58).

Mazonge na mikatale ya jamii yake inamsukuma kuutafuta uhuru binafsi alioukosa

kwa muda mrefu. Hata hivyo, uhuru huo kama unavyoelezwa katika msingi wa tatu

wa nadharia ya Udhanaishi, siyo kamili, bali ni wa kuogofya. Hii inatokana na

ukweli kwamba mwanadamu hata akiupata uhuru huo, huweza kuutumia vibaya na

baadaye humletea madhara. Matokeo yanaonesha kuwa tukio la kupigwa kwa Rosa

linasababisha autafute uhuru wake ambao unakuwa chanzo cha mchakato wa kujiua

50

kwake, kutokana na kuutumia vibaya. Hili linathibitishwa na Rosa mwenyewe

kupitia kalamu ya mwandishi anaposema:

―Sasa ninakufa: ninakufa sasa. Maisha yangu yalikuwa

magumu. Sasa nimeona wazi kwamba malezi yangu ndiyo

yalikuwa chanzo cha taabu. Malezi. Siyo malezi ya mama,

lakini malezi ya baba yangu. Kweli baba alinichunga.

Nilichungwa kama msichana wa jela. Nilipopata uhuru,

nilishindwa kuutumia. Deogratias, Thomas, Charles – wote

hao nimewapoteza. Kwa heri Flora, kwa heri Honorata, kwa

heri Stella, kwa herini Sperantia, Emmanuel kwa herini! Baba

na mama samahani kama nimefanya vibaya.‖ Juu ya kitanda

alikuwa amelala Rosa. Alikuwa amekufa (kur. 91 – 92).

Ni wazi kwamba Rosa anamlalamikia Zakaria na siyo mama yake, kutokana na suala

la malezi aliyopewa. Anaona kuwa mchakato wa kujiua kwake unatokana na ukatili

wa baba yake kwa kumlea kama mfungwa. Malezi hayo ndiyo yanayosababisha

kupigwa sana na kuwa ndilo tukio la kwanza la mchakato wa kujiua kwake. Hili

linasababisha akengeuke misingi ya malezi ya baba yake. Matokeo yake, kama

inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi, anaamua kujitafutia uhuru binafsi. Hata

hivyo, uhuru huo unamwingiza katika mateso kiasi cha kuyaona maisha kama kitu

kisichokuwa na thamani kwake. Hivyo, anajilaumu kwa kuutumia uhuru huo vibaya

na kuyachukia malezi mabaya aliyopata kutoka kwa baba yake.

4.2.1.2 Kuwachongea Wasichana Wenzake

Matokeo yanaonesha kwamba tukio hili ni kiini cha mabadiliko ya tabia ya Rosa

aliyotoka nayo nyumbani kwao na ndilo linalomwingiza zaidi katika mchakato wa

kujiua kwake. Hii ni baada ya kuwataja wanafunzi wenzake wa shule ya sekondari

ya Rosary waliotoroka usiku na kwenda kulala mjini. Kufahamika kwa tukio hilo

kunasababisha wasichana hao wanapewe adhabu ya kusomba magari mia ya

mchanga. Wanapobaini kuwa Rosa ndiye aliyewachongea kwa mkuu wao wa shule,

wanaamua kumchania madaftari yake na kumchomea mashuka yake yote. Pia,

wanamwandikia ujumbe wa vitisho na kuuweka kwenye dawati lake. Kitendo hicho

kinasababisha Rosa azidi kuchukiwa na wasichana wenzake. Hali hiyo inamfanya

aishi maisha ya upweke na kukosa amani na furaha. Ujumbe huo unasema:

―Kumbe ndiyo maana uko mnyamavu namna hii! Ulifikiri

tutafukuzwa! Utakatifu wako uko wapi?‖ Wasichana

walikoma kumsumbua Rosa lakini chuki haikwisha. Rosa

51

alichukiwa sana. Alipojaribu kukaa na kuongea na wenziwe

walimkimbia na kumwacha peke yake. Rosa alikonda.

Alimaliza darasa la tisa kwa shida sana (uk. 29).

Katika dondoo hili, imebaini kwamba tukio la Rosa kutengwa na wenzake linampa

wakati mgumu pale shuleni na linamkondesha sana. Ifahamike kwamba Rosa

anaingia na kuanza masomo katika shule hiyo akiwa na tabia nzuri iliyojengwa

kutokana na malezi makali na ya ufungwa aliyoyapata kutoka kwa baba yake.

Imebainika kwamba katika malezi hayo, amejifunza kwamba mtu akifanya mambo

mabaya huadhibiwa, na akifanya mazuri ikiwa ni pamoja na kusema ukweli

hupongezwa. Hata hivyo, anashangaa kuona kwamba baada ya kusema ukweli

kuhusu wasichana waliotoroka kwenda kucheza disko, uongozi wa shule

haumpongezi kama alivyotarajia. Badala yake anachukiwa na kutengwa na

wanafunzi wenzake, wakiwemo wasichana hao. Kitendo hicho kinamkatisha tamaa

na kuamua kukengeuka misingi ya malezi aliyojengewa na baba yake. Matokeo yake

anaamua kujiingiza katika vitendo viovu kama wanavyofanya wasichana wenzake.

Mabadiliko ya tabia yake yanazidi kuchochewa na maneno ya vijana wawili wa

shule ya sekondari ya Bwiru. Rosa mwenyewe anawasikia wakimzungumzia na

kudai kwamba inawezekana yeye ni kilema kutokana na ukimya wake na kushindwa

kujihusisha na masuala ya wavulana (uk. 29). Maneno hayo yanamletea maumivu

makali, yanamkata maini na kumsumbua sana moyoni mwake (uk. 30). Yanakuwa

kichocheo cha kuanza kujihoji kutokana na malezi aliyopewa na baba yake.

Mwandishi anaendelea kujenga wazo lake kwa kusema: ―Hata alipokuwa kitandani,

maneno haya yaliendelea kuzunguka kichwani mwake. Alikata shauri. Alikata shauri

kwenda kucheza dansi‖ (uk. 30). Baada ya kuanza maisha ya kwenda kucheza dansi,

anaanza kupata hisia tofauti, hasa baada ya kucheza na Deogratias. Kitendo hicho

kinasababisha mgongano wa mawazo yanayomfanya ajiulize maswali haya:

Kama nikifanya urafiki na wavulana baba yangu atafahamu?

Yeye yuko Ukerewe, mimi niko Usukuma, baba anakaa

akinichunga anafikiri yeye atanioa? (uk. 32).

Dondoo hili linaonesha kwamba, ijapokuwa Rosa alitoka kwenye malezi ya baba

yake akiwa na tabia nzuri, tabia hiyo ilianza kubadilika alipokumbana na mazingira

ya sekondari, ambayo ni tofauti na yale ya nyumbani kwake. Matokeo yanaonesha

kwamba kumbe tabia hiyo ilikuwa ni ya woga uliotokana na kufungwa na sheria

52

kandamizi za baba yake zilizomnyima uhuru wa kufanya mambo yake kama kiumbe

razini. Mtafiti anaamini kwamba iwapo Rosa angepewa uhuru wake tangu mwanzo,

angejua namna ya kuutumia kwa kuchagua na kufikiri lipi la kufanya na lipi la

kuacha. Maelezo haya yanaungwa mkono na Kipacha (2019) anayeeleza kwamba:

Rosa anaamua kubadilika kitabia baada ya wanafunzi wenzake

kumtusi na kumwita kilema kwa kukataa vishawishi vya

kujiingiza katika tabia ya ufuska. Hata hivyo, anapoamua

kuendana na tabia za wanajamii waliomzunguka, anatumbukia

katika mtego wa kushutumiwa kwa tabia yake ya ufuska na

ulevi kupindukia. Rosa anapitia kipindi cha utambuzi kuwa,

mifumo ya uthamani ya kitamaduni na kimaadili

inayomzunguka haina mantiki wala haimsaidii; na yote ni ya

kidanganyifu. Hivyo, anaamua kuitupilia mbali na kuchukua

mkondo wake kwa kukata minyororo iliyokuwa ikimfunga

kama msichana, mwanamke na mwanajamii (kur. 423 - 424).

Kwa jumla, utafiti umebaini kwamba kitendo cha Rosa cha kuwachongea wasichana

wenzake kwa Mkuu wa shule, ndicho kinachokuwa chanzo cha mabadiliko ya tabia

yake kwa kukengeuka misingi ya malezi ya baba yake. Matokeo yake, anaamua

kukata tamaa baada ya kubaini kwamba kitendo cha yeye kuwa na tabia nzuri ndicho

kinachosababisha wenzake wamchukie na kujitenga naye. Hatimaye, anabaini

kwamba kuwa na tabia nzuri hakumsaidii lolote, bali kunamwangamiza. Anaamua

kufanya lolote analotaka kwa sababu alipofanya aliyoyataka baba yake hakupata

faida, na anapofanya kinachotakiwa na mfumo wa shule yake, bado hapati faida.

Mabadiliko hayo ndiyo yanayomwingiza katika mchakato wa matukio ya kujiua

kwake.

4.2.1.3 Kuota Ndoto

Tukio lingine la mchakato wa kujiua kwa Rosa ni ndoto mbili alizoota mara tu baada

ya kurudi kutoka kwenye disko. Ndoto hizo zinaonesha mabadiliko ya kimwili ya

Rosa na mwanzo wa kuingia katika mahusiano ya kimapenzi. Kwa mfano, katika

ndoto yake ya pili, anaona kuwa yuko na kijana mrefu, mwembamba na mwenye

ndevu nyingi, huku akimtazama kwa huruma. Mambo anayoota katika ndoto hiyo,

hatimaye, yanamtokea baadaye kama inavyosawiriwa katika ukurasa wa 75, pale

anapojiwa na Charles, akiwa chumbani kwake huko Mwanza na kukabidhiwa barua

ya kumwomba wawe wachumba. Mwandishi akisimulia ndoto hizo, anasema:

53

Baada ya muda usingizi ulimchukua. Alimwona baba yake

akitembea barabarani na mbwa. Mbwa huyo alikuwa

amefungwa kamba shingoni. Mbwa aliona mbuzi. Alikata

kamba na kukimbia. Alimrarua mbuzi vipande… Rosa aliamka,

alilala, na usingizi ulimchukua tena. Aliona kijana mwembamba

mwenye ndevu nyingi akimtazama kwa macho yenye huruma.

Rosa alipomwona alimkimbilia na kumkumbatia akisema kwa

sauti, lazima unioe, ukinikataa wewe maisha yangu

yamekwisha; sina tumaini tena! Rosa alitokwa na machozi.

Mvulana alimbusu na kumwambia: ―Nitakujibu baadaye kwa

barua; lakini unafikiri baada ya ku… Thereza alikuwa bado

hajaelewa Rosa alipomrukia na kumkumbatia. Waliangushana

kitandani. Rosa alianza kumbusu, lakini tamaa yake haikuweza

kupungua. Rosa alihitaji ule mkwaruzokwaruzo wa aina ya

pekee. Mkwaruzokwaruzo wa ndevu na manyoya ya tumboni.

Zaidi ya hayo, moto ulikuwa ukiwaka upande wa Kusini lakini

wao walikuwa wakizimisha upande wa Kaskazini (kur. 32 –

33).

Katika dondoo hilo, mwandishi anapoelezea kuhusiana na ndoto ya kwanza ya Rosa

kwamba anamwona baba yake akiwa amemshikilia mbwa aliyefungwa, analenga

kutoa taswira kuhusu maisha ya Rosa kwa jumla. Mbwa analinganishwa na Rosa,

ambapo, mara nyingi, mbwa huwa hapewi uhuru wa kutosha ili asiwarukie na

kuwadhuru watu. Hivyo, dawa ya mbwa huyo huwa ni kufungwa minyororo ili asiwe

na uhuru wa kutosha na kufanya atakavyo. Hivyo ndivyo inavyomtokea Rosa. Kama

ilivyo kwa mbwa, Rosa naye ananyimwa uhuru wa kufanya atakayo kutokana na

kufungwa na sheria, pamoja na malezi makali ya baba yake.

Ifahamike kwamba, mambo haya yanamtokea Rosa akiwa katika hatua nyingine za

mabadiliko ya kimwili na anahitaji mwongozo wa maisha yake na namna ya

kuyakabili. Imebainika kwamba ndoto anazoota zinachochewa na tukio la yeye

kwenda disko na kucheza muziki kwa mara ya kwanza, huku akiwa amekumbatiana

na kupapasana na mwanamume anayeitwa Deogratias. Ndoto hizi zinaamsha hisia na

hamu yake ya kufanya mapenzi, kiasi cha kuamka na kwenda kumkumbatia Thereza,

msichana mwenzake, kwa lengo la kutimiza na kuondoa hisia hizo. Kipacha (2019)

anaeleza kwamba Rosa anaamua kuvunja maadili kwa kujaribu kufanya mapenzi ya

jinsia moja na rafiki yake, Thereza, huku akimbusu, lakini tamaa yake haikuweza

kupungua. Utafiti umebaini kuwa baada ya tukio hili, Rosa anaamua kujiingiza rasmi

katika mapenzi na kuwa na mahusiano na wavulana wengi kwa wakati mmoja.

Mwandishi anasema:

54

Rosa alianza mapenzi. Alianza mapenzi lakini aliyaendea

haraka sana kama mbwa aliyekata kamba. Aliona mvulana

mmoja au wawili walikuwa hawamtoshi kwa urafiki. Mwaka

huo huo aliwakubalia wavulana watano (uk. 33).

Kutokana na dondoo hilo imebainika kuwa, kitendo cha Rosa kuyaendea mapenzi

kwa pupa, kinamfanya asiwe na tahadhari ya namna ya kuutumia uhuru alioutafuta

kwa nguvu. Matokeo yake, anajitapa na kujiona kwamba yu mshindi kwa hayo

anayoyafanya, huku akidai kwamba anawaendesha wavulana kama mtu aendeshaye

punda. Anasema:

Unafahamu, Thereza, siku hizi ninawachezea wavulana kama

mtu aendeshaye punda. Vuta kamba mkono wa kulia na punda

atakata kona: vuta mkono wa kushoto, pia atakata kona. Punda

hafahamu aendapo isipokuwa mwendeshaji tu. Ndivyo hivyo

ninavyowachezea wavulana siku hizi (uk. 33).

Hii ina maana kwamba, Rosa haoni tofauti ya wavulana hao anaowachezea na

kuwaendesha awalinganishapo na baba yake mzazi. Anakusudia kusema kwamba,

anamwendesha baba yake kwa sababu naye ni mwanaume sawa na wavulana hao, na

kwamba, anao uwezo na uhuru wa kumchezea mvulana au mwanaume yeyote baada

ya kuupata uhuru wake. Anaamua kuyafanya yote haya kama njia ya kumkomesha

baba yake kutokana na malezi ya kikatili aliyompa.

Kama inavyoelezwa katika msingi wa tatu wa nadharia ya Udhanaishi, Rosa anafikia

hatua ya kuutafuta uhuru wake binafsi na uwezo wa kujifikiria na kujiamulia mambo

yake. Anakata kamba na minyororo aliyofungwa na baba yake kwa muda mrefu

kama inavyosawiriwa katika ndoto ya kwanza. Anaamua kukengeuka misingi ya

malezi aliyowekewa na baba yake kwa kutoendelea kutii vigezo vya jamii kwa

jumla. Ndiyo maana mwishoni mwa riwaya hii, kigezo kimojawapo kikuu, ambacho

ni Mungu, kinajitokeza na kuendesha kesi juu ya uasi wa Rosa na tukio la kujiua

kwake. Hapa Mungu anataka kumwonesha binadamu kuwa mwisho wa maisha hapa

duniani kila mmoja atabainishiwa ukweli halisi wa namna anavyoishi. Mwandishi

ametumia ndoto ili kuendeleza wazo la malezi aliyoyapata Rosa ambayo ni ya

kukandamizwa na kuwekewa mikatale na makatazo mengi (Wafula, 2007). Ndoto

hizi zinabeba maana maalumu kwa kuwa zinaelezea maisha halisi ya mhusika Rosa

Mistika, kwa kufichua athari ya tajiriba za utotoni katika makuzi ya maisha yake.

55

Kwa hiyo, utafiti umebaini kwamba ndoto zote mbili za Rosa zinachangia na

kuchochea kwa kiasi kikubwa katika mchakato wake wa kujiua. Hii ni kwa sababu,

ndoto ya kwanza, inamsukuma katika kuasi sheria na kanuni za malezi aliyolelewa

na baba yake kwa kutafuta uhuru wake binafsi kama inavyoelezwa katika nadharia

ya Udhanaishi. Hata hivyo, imebainika kuwa uhuru huo anautumia vibaya na

unamwingiza katika mtanziko wa maisha yake. Hii ni baada ya kukiuka miiko na

maadili ya malezi aliyopewa na wazazi wake. Ndoto ya pili inamwingiza katika

mahusiano ya kimapenzi na Charles, ambapo baada ya penzi hilo kuvurugika, Rosa

anachukua maamuzi ya kujiua.

4.2.1.4 Kusimamishwa Shule, Kufumaniwa na Kufukuzwa Chuo

Kubadilika kwa tabia ya Rosa akiwa katika shule ya sekondari ya Rosary na

kukengeuka misingi ya malezi aliyopewa na baba yake, kunasababisha matokeo yake

mtihani kuwa mabaya. Hili linamfanya azidi kuchukiwa na kutengwa siyo tu na

marafiki zake pale shuleni, bali hata na walimu wake. Matokeo yake ni kwamba

Mkuu wa shule anaamua kumsimamisha masomo na kumrudisha nyumbani kwao,

huku akilazimika kurudi kwa ajili ya kufanya mtihani wake wa mwisho. Mwandishi

anasema:

Sista John alimsimamisha Rosa masomo kutokana na tabia

yake kubadilika na kuwa na wanaume tofauti. Alisimamishwa

masomo na kulazimika kuja kufanya mtihani wake wa

Cambridge. Rosa alilia. Rosa alikwenda nyumbani (uk. 35).

Matokeo yanaonesha kuwa tukio hili linazidi kumwingiza Rosa katika mchakato wa

kujiua kwake, kwani anazidi kukata tamaa na kuyachukia maisha yake kwa kukosa

matumaini ya kuwa na maisha bora na mazuri ya hapo baadaye. Hata hivyo, anapata

matumaini kidogo anaporudi na kufanya mtihani wake wa mwisho, ambapo anapata

ufaulu mdogo unaomsaidia kwenda kusomea mafunzo ya Ualimu huko Morogoro

(uk. 37).

Utafiti umebaini kuwa akiwa Chuoni Morogoro, Rosa kama kawaida yake

anaendelea na tabia yake ya umalaya hadi kufikia hatua ya kupewa jina la

‗laboratory‘, yaani sehemu ya kufanyia majaribio, huku akiufurahia zaidi uhuru

mpya alioupata, akiwa mbali na malezi ya baba yake. Hata hivyo, anapoamua

kuanzisha mahusiano ya kimapenzi na Mkuu wake wa chuo, Bwana Thomas,

56

mapenzi yao hayadumu, kwani anafumaniwa na mke wa Mkuu huyo wakiwa ndani

ya nyumba yao. Rosa akiwa katika dimbwi hilo la mapenzi, anashtukia kumwona

mke wa Thomas akiwa na shoka mkononi mwake. Kisha, anaambiwa:

―Leo utanitambua! Unataka kuniletea hapa umalaya wako!‖

Rosa alijaribu kukimbia. Alishikwa na yule mwanamke. Rosa

aliangushwa chini. Yule mwanamke alimwinamia. Rosa

alitiwa jino. Palepale uso wa Rosa ulienea damu. Yule

mwanamke alionekana akitema kitu fulani chini. Rosa alilia.

Mwalimu alimtoa mke wake juu ya Rosa. Rosa alikimbia.

Kabla hajawahi kutoka redio ilimpata mgongoni. Ilianguka

chini na kupasuka (uk. 55).

Kutokana na dondoo hilo, imebainika kuwa tukio hili linakuwa sababu za

kumwondoa Rosa katika furaha aliyokuwa nayo muda mfupi kabla ya kufumaniwa.

Hivyo, anakosa mwelekeo kwa kuzidiwa nguvu na mke wa Thomas kutokana na

kipigo kizito, kinachomsababishia maumivu makali na ya kutokwa na damu.

Anapata maumivu zaidi anapogundua kwamba kipigo hicho kinamsababishia kilema

cha maisha kutokana na kung‘atwa sikio lake na mke wa Thomas na sura yake

kuharibiwa vibaya. Mwandishi anaeleza kwamba:

Rosa alipofika chumbani alijifungia humohumo kwa ufunguo.

Alikimbilia kioo. Alipojiangalia ndani ya kioo hakuweza

kuamini kwamba hiyo ilikuwa kweli sura yake. Alilia kwa

sauti. Alililia sikio lake. Yule mwanamke alimuuma sikio na

kutoa sikio lote la nje. Alianza kusikia maumivu makali (uk.

55).

Utafiti umebaini kuwa tukio la kufumaniwa na kupigwa kwa Rosa, linachangia sana

katika mchakato wa kujiua kwake, kwani linamjengea chuki akilini mwake dhidi ya

wanaume na maisha yake kwa jumla. Matokeo yanaonesha kwamba kitendo cha

kujifungia ndani akiwa na maumivu makali, huku akiijutia hali mbaya aliyo nayo, ni

usawiri wa tukio litakalompata baadaye, ambapo atajifungia chumbani kwake kabla

ya kuchukua uamuzi wa kujiua. Inaelezwa kwamba:

Rosa alipofika chumbani mwake alijitupa kitandani. Mambo

mengi yalimzunguka kichwani mwake. ―Rosa,‖ alisikia sauti

moyoni mwake ikimwita. Ilikuwa sauti kama ya mtu

anayetaka kufa. Ilikuwa sauti hafifu sana. Rosa peke yake

aliweza kuisikia. Rosa peke yake aliweza kuitambua (uk. 55).

57

Taswira inayosawiriwa katika dondoo hili, haitofautiani na ile inayompata katika

tukio halisi la kujiua kwake. Katika kipengele cha 4.4.3 kinachoelezea uhusiano wa

njia zinazotumika katika kujiua, imefafanuliwa kuwa wataalamu wa magonjwa ya

akili wanaeleza kwamba mtu anayetaka kujiua husikia sauti ikimwita na kumhimiza

kutekeleza kitendo hicho, pasipo kurudi nyuma wala kughairi uamuzi wake. Bila

shaka, sauti anayoisikia Rosa kwa wakati huo ni ya kifo inayotokana na maumivu ya

kuondolewa kwa sikio lake na kipigo kikali kutoka kwa mke wa Thomas. Hivyo,

anaingia katika mchakato wa kujiua kutokana na kukata tamaa ya maisha na kukosa

furaha na matumaini kwa namna maisha yanavyomwendea.

Hatimaye, mabadiliko ya uongozi wa Mkuu mpya wa chuo yanafanyika. Bwana

Thomas anaondolewa na kuletwa mkuu mwingine, Bwana Albert. Mabadiliko haya

yanakuwa mwiba mchungu kwa Rosa, kwani uongozi huo haufurahishwi na

mwenendo wa tabia yake na unaamua kumfukuza chuo. Tunaambiwa:

… Baada ya mkutano wake na wanafunzi, Bwana Albert

alikuwa amekuja kumwambia Rosa apange vitu vyake

sandukuni; kwamba amefukuzwa kabisa. Kwa namna fulani

alimwonea huruma; lakini alipaswa kufuata sheria. Rosa

alisikia uchungu wa kufukuzwa shule (kur. 67).

Kutokana na nukuu hii, imebainika kuwa Rosa anapoipokea barua ya kufukuzwa

kwake, haoni tena sababu ya kuendelea kuishi. Matokeo yake ni kwamba, anaingia

katika mchakato wa kujiua ili kuyakomesha maisha yake ya taabu. Hata hivyo,

imebainika kuwa uamuzi huo haumtokei kwa ghafla, bali analikabili tukio hilo hatua

kwa hatua. Mosi, anaonekana akipokea barua ya kufukuzwa chuo, halafu anafuatilia

kinachoendelea baina ya Mkuu wa Chuo na wanafunzi wake pale mistarini, kisha

anapanga njia ya kujiua kwake na kuandaa kifaa cha kujiulia. Yote haya yanamtokea

kutokana na kukata tamaa kwa kuchoshwa na mazonge mengi yanayomkabili na

kukosa matumaini ya kupata cheti cha ualimu anaousomea. Hata hivyo, akiwa katika

kilele cha kutimiza azma yake, anaokolewa na Mkuu wa Chuo mwenyewe, baada ya

kuingia ghafla chumbani kwa Rosa kwa lengo la kumhimiza afungashe mizigo yake

na kuondoka chuoni hapo. Hili linamfanya Mkuu huyo amwonea huruma na

kubatilisha uamuzi wake baada ya kushauriana na walimu wenzake. Kisha, Rosa

anaendelea na masomo yake, huku akiwa na chuki dhidi ya maisha kutokana na

matukio mengi anayokumbana nayo.

58

4.2.1.5 Kutoa Mimba

Tukio lingine la mchakato wa kujiua kwa Rosa ni la kutoa mimba mara kwa mara

kutokana na tabia yake ya umalaya. Vitendo hivi vinaanza akiwa katika shule ya

Sekondari ya Rosary na vinaendelea akiwa Chuo cha Ualimu Morogoro. Mwandishi

anaeleza:

Rosa akiwa Morogoro TTC aliendeleza tabia yake ya kufanya

mapenzi. Alilazwa hospitali mahututi kwa kutoa mimba ya

miezi miwili. Rosa alikaa hospitali muda wa majuma mawili.

Rosa alipona. Aliendelea na mchezo wake. Katika majuma

mawili yaliyofuata, Rosa alikonda sana. Vijana walikuwa

wakimzungumzia yeye katika vikundi; hata yeye mwenyewe

alifahamu. Alianza kuwa anaviziavizia vikundi hivyo ili

afahamu wanasema nini juu yake (uk. 45).

Kupitia katika dondoo hili, imebainika kwamba licha ya kulazwa hospitalini na

kunusurika kufa, Rosa anaendelea na mchezo huo wa kutoa mimba. Haoni thamani

ya viumbe hao wasiokuwa na hatia. Ama kweli, mazoea hujenga tabia, na sikio la

kufa halisikii dawa, kwani ielezwa kwamba akiwa mwaka wa pili wa masomo yake

huko Morogoro, alirudia tena kutoa mimba, kama anavyoeleza mwandishi

anaposema: Mwandishi anasema:

Rosa alitoa tena mimba alipoingia katika mwaka wake wa

pili. Wengine walisema kwamba ilikuwa mimba yake ya tatu;

wengine walisema kwamba ilikuwa ya nne. Tukio hilo la

kutoa mimba lilisababisha Rosa kuchukiwa na walimu

wote… (uk. 52).

Utafiti umebaini kwamba matukio ya kutoa mimba mara kwa mara yanasababisha

maisha ya Rosa kuwa ya mashaka, ya upweke na ya kuchukiwa na kila mtu kwa

sababu ya kukosa marafiki. Matokeo yake, anaishi maisha ya kuviziavizia kwa

kukosa mtu wa karibu wa kumpa taarifa ya mambo yanayoendelea hapo chuoni

kumhusu yeye. Haya yanampata kutokana na kukiuka wosia wa mama yake, kwani

kabla ya kwenda shuleni aliambiwa:

… Jambo moja hasa ningependa kukutahadharisha: wavulana

wakorofi. Huenda wakakutaka mapenzi, na nia yao ikiwa ni

kukupa mimba itakayokukatisha masomo yako. Daima

wakwepe hao. Na iwapo utakuwa mpumbavu ukapata mimba

usiitoe. Tunasikia kwamba siku hizi wasichana wengi

wanaosoma wanafanya hivyo ili wapate kuendelea na masomo

59

yao. Wanapenda masomo zaidi kuliko watoto wao. Hata hivyo

ni wauaji (uk. 11).

Dondoo hili linaonesha namna Rosa anavyoamua kukengeuka maadili na misingi ya

utu aliyoelezwa na mama yake kabla ya kwenda shule. Badala yake, anatoa mimba

nyingi na kumsababishia matatizo mengi. Matokeo yake ni kwamba matukio hayo

yanasababisha aishi maisha ya upweke na ya kuchukiwa na kila mtu pale chuoni.

Haya yanazidi kumwingiza katika mchakato wa kujiua kwake kutokana na kukata

tamaa ya maisha.

Aidha, utafiti umebaini kuwa Rosa anafikia uamuzi huo wa kukata tamaa kutokana

na wazazi wake kushindwa kumwandaa kuingia katika maisha ya utu uzima, ikiwa

ni pamoja na namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha yake. Hii

ni kwa sababu, wanamlea katika hali ya upweke kwa kumweka mbali na wavulana,

ambao kimsingi, ni sehemu ya jamii yake. Matokeo yake ni kwamba,

anapobadilisha mazingira ya nyumbani kwake na kwenda mazingira mengine mbali

na wazazi wake, anabaini kuwa mazingira hayo yamezungukwa na wavulana. Hali

hiyo, ndiyo inayomsukuma kuanza kujitambua kuwa, yeye ni nani, na hivyo,

anaanza kuwatambua vijana wa kiume. Matokeo yanaonesha kuwa, akiwa katika

mazingira hayo anabaini kuwa, wavulana ni binadamu kama walivyo binadamu

wengine na wala si wabaya kama alivyolazimishwa na wazazi wake kuwa, hawa ni

watu wabaya. Aidha, anabaini kuwa wavulana wana uwezo wa kumpenda, kwani

mapenzi anayopata kutoka kwao, yanakuwa fidia ya mapenzi aliyokosa kutoka kwa

wazazi wake, hususani Zakaria. Hata hivyo, kwa upande mwingine mapenzi haya

haya ndiyo yanayomponza kwa sababu yanamfanya aharibike na kumkatisha tamaa

ya maisha yake kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi. Kutokana na

maumivu ya kuachwa na mpenzi wake, anakosa uvumilivu na anaamua kujiua.

4.2.1.6 Kujitenga na Kutengwa na Jamii yake

Kujitenga au kutengwa na jamii husababisha mtu kuwa na upweke3, ambao ni

miongoni mwa dalili za mchakato wa mtu anayetaka kujiua. Mara nyingi mtu huyo

hukwepa mwingiliano na watu wengine na kubaki mwenyewe, huku akitafakari na

3 Hali ya kiumbe kukaa bila ya kushirikiana na wengine (BAKITA, 2017).

60

kupima kama uamuzi anaotaka kuuchukua ni sahihi au la. Mtu huyo anapoachwa

katika hali hiyo kwa muda mrefu, huweza kumsababishia msongo wa mawazo,

ambao humkatisha tamaa na hata kufikia hatua ya kuchukua maamuzi ya kujiua.

Kujitenga kwa Rosa baada ya kukumbwa na matukio mengi akiwa katika Chuo cha

Ualimu Morogoro ni uthibitisho wa hoja hii, kama anavyoeleza mwandishi:

Rosa alikata shauri. Kwa sasa alikaa kimya. Moyoni alikuwa

amevurugika kama mtu aliyetaka kutapika. Kwa sasa

hapakuwa na mtu aliyefahamu mawazo yake (uk. 58).

Dondoo hili linathibitisha kwamba mtu anapojitenga na jamii yake, huweza kupata

msongo wa mawazo, ambao huchangia katika mchakato wa kujiua kwake. Kulingana

na utafiti huu, imebainika kuwa mtu anapofikia hatua hiyo, hutakiwa kushauriwa

mapema ili asijiingize katika fikra hizo, kwani anapokosa mtu wa karibu wa

kumweleza matatizo yake, hujiona kama hana thamani na ndipo huamua kujiua. Hii

ni kwa sababu msongo wa mawazo ni tatizo la kisaikolojia, ambalo humweka

mhusika katika hali ya hofu au wasiwasi kutokana na kuzidiwa na mawazo kwa

kukosa jibu la kitu kilichoko mbele yake au kichwani mwake (Freud, 1900; Ndosi na

wenzake, 2004; Glucksman & Kramer, 2017). Matokeo yanaonesha kuwa, watu

wengi hufikia uamuzi wa kujiua kwa sababu ya kukaa kimya na kuyakumbatia

matatizo mbalimbali wanayoyapitia.

Vilevile, imebainika kuwa mchakato wa kujiua kwa Rosa unatokana na kitendo cha

kutengwa na jamii yake, akiwamo baba yake, walimu wake, wanafunzi wenzake,

pamoja na mchumba wake, Charles. Kwa mfano, anaumizwa na maneno ya baba

yake anaposema: ―Rosa ndiye nani? Malaya hajawa mgeni wangu wala mtoto

wangu.‖ (uk. 57). Maneno haya yanamkatisha Rosa tamaa na yanamsumbua sana

moyoni mwake. Hali hiyo inasababisha aamue kukengeuka misingi ya jamii kwa

kumtamkia baba yake maneno mazito aliyokuwa ameyatunza moyoni mwake kwa

muda mrefu. Anasema: ―Kila wakati unatuchunga. Unafikiri utatuoa wewe!‖ (uk.

58). Mwandishi anaeleza kuwa, kimsingi, maneno haya yalitakiwa kusemwa na Rosa

siku ile ya kwanza alipopigwa na baba yake, baada ya kukutwa na barua ya mapenzi

iliyotoka kwa Charles. Matokeo yanaonesha kuwa, kitendo cha Rosa kumtukana

baba yake kutokana na kauli yake hiyo kinachochea hasira zaidi dhidi yake.

Kutokana na hilo, Zakaria anaamua kumtamkia maneno mabaya, ambapo Rosa naye

61

bila kusita, anamrudishia baba yake maneno kama hayo. Kupitia kalamu ya

mwandishi, Zakaria anasema: ―Rosa, tangu leo wewe si mtoto wangu.‖ Kwa upande

wake, Rosa naye anadakiza bila kukawia kwamba: ―Tangu leo wewe si baba yangu.‖

(uk. 58).

Kwa jumla, matokeo yanaonesha kuwa suala la kutengwa na kujitenga kijamii

huweza kusababisha mtu kupata msongo wa mawazo, ambao ni chanzo kikubwa cha

sonona. Aidha, msongo huo wa mawazo huweza kusababisha mhusika kukata tamaa

kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi. Hali hiyo huweza hata

kumsukuma mhusika kufikia hatua ya kuchukua maamuzi ya kujiua kama

ilivyotokea kwa Rosa Mistika.

4.2.1.7 Kuachwa na Mchumba Wake

Katika tukio hili, imebainika kuwa Rosa Mistika anachukua maamuzi ya kujiua

muda mfupi tu, baada ya kupokea barua ya kuachwa kimapenzi na mchumba wake,

Charles. Hili linatokea muda mfupi mara tu, baada ya Charles na Rosa kukubaliana

kutoka Mwanza kwenda nyumbani kwao, Ukerewe, kwa lengo la kuwajulisha

wazazi wao, kuhusiana na suala la uchumba wao. Hata hivyo, wanapokaribia kufika

Ukerewe, Charles anampa Rosa barua, ambapo:

Rosa kabla ya kuisoma alianza kuibusu. Alifungua kwa

makini. Mikono yake ilikuwa ikitetemeka. Mwishowe barua

ilifunguliwa. Mle ndani mlikuwa na kipande kidogo cha

karatasi ngumu, aina ya zile zitumikazo kuwekea sementi.

Rosa hakuamini alichokiona. Alijikaza. Alisoma ile barua; Ha!

Rosa, kweli wewe ulikuwa bikira! Unafikiri baada ya

kufahamu kwamba ulichezewa sana huko Morogoro, na baada

ya mimi mwenyewe kuona bonde la ufa na kuliona lile sikio,

unafikiri mimi ninaweza kukuoa! Ha! Dada yangu, sahau.

Haiwezekani hata kwa mizinga! Hata kama ukiwa wa bure!

(uk. 90).

Matokeo yanaonesha kuwa, mara tu baada ya Rosa kusoma barua hiyo, hakuamini

alichokiona ndani yake. Furaha yake aliyokuwa nayo muda mfupi kabla ya kufungua

barua hiyo, iligeuka na kuwa maumivu makali kwake. Mwandishi anaeleza kuwa

kabla ya kuanza kuisoma barua hiyo, alikwenda chumbani kwake upesiupesi ili aone

kilichokuwa kimeandikwa. Anafafanua zaidi kuwa, kabla ya kuisoma, alianza

kuibusu huku akiwa na furaha tele. Hata hivyo, furaha yake ilitoweka kutokana na

62

ndoto ya matamanio yake kupotea. Hatimaye, ujumbe ulikuwamo ndani ya barua

hiyo, unasababisha Rosa kuchukua uamuzi wa kujiua. Hii ni baada ya kugundua

kwamba, ndoto yake ya kuolewa na Charles haiwezi kutimia kama alivyotarajia.

Utafiti umebaini kuwa, kitendo cha Charles kuandika barua hiyo kwenye karatasi

ngumu kililenga kuonesha dharau kwa Rosa, na kwamba, baada ya kugundua

kwamba hakuwa bikira, hakuwa na thamani tena kwake na alimwona kama

takataka. Hali hii ndiyo iliyousukuma mbele mchakato wake wa kujiua kwa kuona

kuwa maisha yake hayakuwa na maana tena. Zaidi ya hayo, karatasi hiyo ngumu ni

ishara kuwa Rosa baada ya kusoma ujumbe huo atachukua uamuzi mgumu wa

kukatisha maisha yake. Haya yanasawiriwa na mwandishi anapoeleza mambo

yanayotokea mara tu, baada ya Rosa kuisoma barua hiyo. Anasema:

Rosa alipomaliza kusoma kichwa kilimwanga. Aliona

kizunguzungu. Jasho lilimtoka. Machozi yalimteremka mpaka

kifuani. Rosa aliona ulimwengu wote ulimwonea huruma,

lakini sasa aliona kama kwamba ulimwengu wote ulikuwa

ukimchekelea. Kuishi aliona hawezi. Aliona ni fedheha.

Alitafuta chupa. Aliona chupa iliyokuwa na mafuta ya nywele

ndani yake. Bila shaka yalikuwa mafuta ya nywele ya

Sperantia. Rosa aliyamwaga chini. Alichukua ile chupa na

kuisagasaga juu ya jiwe. Baada ya kuisaga aliweka ule

ungaunga wa vipande vya chupa ndani ya glasi. Aliweka maji

(uk. 90).

Maelezo haya ni uthibitisho kuwa tukio la kujiua siyo la ghafla kama ambavyo huwa

linatazamwa na watu mara wasikiapo kuwa mtu fulani amejiua, bali ni mchakato.

Suala hili pia, linathibitishwa na mwandishi anapoeleza kuwa:

Rosa alifikiri kwanza kabla ya kunywa. Alitubu dhambi zake.

Alitafuta karatasi nzuri sana halafu aljichanja mkononi na

wembe. Damu ilitoka. Kwa damu hiyo aliandika maneno

fulani juu ya karatasi. Alipomaliza kuandika maneno yake

Rosa alivuta hasira yake. Alifikiri juu ya maisha. Mara moja

alikunywa yale maji. Alilala juu ya kitanda cha Honorata.

Palepale damu ilianza kumtoka mdomoni. Vile vipande vya

chupa vilimkatakata kooni. Rosa alitema mate. Aliona damu.

―Asante. Kifo njoo upesi,‖ alisema. Baada ya muda mfupi

Rosa alisikia maumivu makali sana tumboni. Muda mrefu

haukupita Rosa alijiona anaanza kupoteza fahamu. Alianza

kuona kitu kama moshi mbele yake. Alisema maneno yake ya

mwisho. Hapakuwa na mtu yeyote aliyesikia isipokuwa

manyigu yaliyokuwa yamejenga paani (uk. 91).

63

Kama inavyojidhihirisha katika msingi wa nne wa nadharia ya Udhanaishi, Rosa

anaamua kukengeuka misingi ya jamii kwa kufanya tukio ambalo halikubaliki katika

jamii. Anaamua kukata tamaa na kuyaondoa maisha yake kwa kujiua. Anakifurahia

na kukiita kifo chake cha maumivu, huku akitokwa na damu pasipo kujuta wala

kuonesha nia ya kuahirisha tukio hilo. Huu ndio unakuwa mwisho wa maisha yake

baada ya kupitia misukosuko na matukio mengi katika maisha yake. Haoni tena

sababu ya kuendelea kuishi. Anaamua kujiua kama suluhisho la kuyakomesha

maisha ambayo ni kama adhabu kwake. Anaridhika kwamba kufa kwake, ndio uhuru

wake.

Utafiti umebaini kwamba tukio hili la kujiua halimtokei ghafla, kwani kabla ya

kuchukua uamuzi huo, anafanya kwanza maandalizi. Maandalizi hayo ni pamoja na

kutafuta karatasi na kuandika ujumbe, kutafuta na kupanga njia anayokusudia

kuitumia katika kufikia azma hiyo, kuandaa chupa, kuisagasaga, na hatimaye,

kufanya kitendo chenyewe. Hii inadhihirisha kwamba kujiua ni mchakato, na wala

siyo kitendo cha ghafla. Aidha, imebainika kuwa mchakato huo ni wa namna mbili:

mchakato kwa mawanda mapana ya maisha ya mtu anayejiua, na mawanda finyu ya

wakati au siku yenyewe ya kujiua.

Mawanda haya ndiyo yaliyomsaidia mtafiti kubaini kwamba wakati mwingine

mchakato huo huweza kuwa wa muda mrefu na wakati mwingine wa muda mfupi

kutegemeana na aina ya tukio au jambo linalomsibu mhusika kwa wakati huo.

Matokeo yanaonesha kuwa mchakato huo unajitokeza hata katika kitendo chenyewe

cha kufa, yaani baada ya kunywa vipande hivyo vya chupa, tukio la kufa halitokei

mara moja. Anaanza kutema mate na kuona damu ikimtoka, anakiita kifo kimjie

upesi, anasikia maumivu makali tumboni, anapoteza fahamu na kuona kitu kama

moshi mbele yake, kisha anasema maneno yake ya mwisho. Huu ni uthibitisho

kwamba kujiua ni mchakato na siyo tendo la ghafla. Maelezo hayo yanaungwa

mkono na Ilomo4 anayesema kuwa:

4 Mahojiano baina ya mtafiti na Bw. Flavian Ilomo Oktoba 2, 2019. Yalifanyika

katika viunga vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambako anafundisha masomo ya

Fasihi.

64

Kujiua kwa Rosa Mistika hakukutokea ghafla bali mchakato

wake ulianza na suala la malezi ambayo, aliyapata nyumbani

kwake. Malezi hayo hayakumwandaa kwa maisha mengine ya

nje ya nyumbani kwake. Hata watu waliomwahidi kuwa naye,

baadaye walimtenga. Jamii yake ilimgeuka na kumwita

malaya. Kwa hiyo, anafikia hatua ya kuona kwamba hakuna

anayeweza kutatua matatizo yake. Hivyo, anaona kuwa

suluhisho lake ni kujiua.

Vilevile, maelezo haya yanaungwa mkono na Ponera5, ambapo katika ufafanuzi

wake anaeleza kuwa:

Ni kweli kwamba kujiua ni mchakato na siyo kitendo cha

ghafla. Nakupongeza kwamba unaliangalia suala la kujiua

kama mchakato na siyo kama tukio. Ungefanya kosa kubwa

sana kama ungefanya utafiti wako kwa kulichunguza suala hilo

kama tukio. Kwa hakika kujiua siyo tukio na hata kufa

kwenyewe kwa namna yoyote ile, siyo tukio bali ni mchakato.

Tunakufa polepole sana kama anavyoeleza Kezilahabi

mwenyewe katika Kichwamaji (uk.186) . Anasema tunakufa

polepole, hatufi mara moja. Nakupongeza kwa kuwa wewe

unafanya utafiti kuhusu mchakato wa kujiua. Unalipa uzito

suala lenyewe la kifo kwamba ni mchakato na siyo tukio. Watu

wanapoishi, wanakabiliana na mazonge mengi ya maisha yao

pamoja na watu wanaoamiliana nao. Hivyo, katika hali hiyo,

inafika hatua kwamba mazonge hayo yanatakiwa yafike

mwisho. Hatimaye, wengine huamua kujiua au kujiondoa.

Hivyo, hatua hiyo huwa ni kukamilisha tu matukio mengi

anayokuwa amepitia mhusika kabla ya tukio hilo. Mchakato wa

kujiua katika riwaya teule umesawiriwa vizuri sana. Kwamba,

watu hao, hawakurupuki tu na kujiua, bali mwandishi

anawapitisha katika hekaheka, matatizo, miiba, konakona na

hemwahemwa hadi kufika mahali mtu anaamua kusema, sasa

basi, inatosha.

Kwa jumla, imebainika kuwa maelezo ya Ponera na Ilomo katika madondoo hayo,

yanaunga mkono hoja iliyokwisha kuelezwa na mtafiti kwamba kujiua ni mchakato,

na siyo tukio la ghafla. Mfano mzuri wa mchakato huo ni tukio la kujiua kwa Rosa

Mistika kama linavyosawiriwa kupitia ujumbe aliouacha kabla ya kujiua kwake.

Fikra hizo hazikumjia mara moja, bali zinajitokeza mara kadhaa akiwa Morogoro na

5 Mahojiano baina ya mtafiti na Dkt. Athumani S. Ponera yalifanyika kwa njia ya

simu Februali 17, 2020. Dkt. Athumani S. Ponera ni Mhadhiri Mwandamizi wa

Fasihi, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.

65

Mwanza. Imebainika kuwa, akiwa Mwanza anaamua kuachana na tabia yake ya

mwanzo ya umalaya na anabadilika, hadi anapoamua kujiingiza tena katika mapenzi

kwa kumkubalia Charles, huku akiahidi kwamba, akishindwana naye, huo ndio

utakuwa mwisho wa maisha yake. Anasema:

Kijana huyu lazima anioe; nikimkataa huyu basi maisha yangu

yamekwisha; sina tumaini tena. Alikata shauri kupiga mshale

wake wa mwisho. Mshale huu ukienda pembeni, basi jitu

maisha – litaniua, Rosa aliwaza moyoni. Rosa alikumbuka

jinsi alivyopigwa na baba yake; alikumbuka alivyopelekwa

nyumbani kwa Ndalo usiku… Kadri alivyopata nuru ndivyo

mapenzi yake yalivyoongezeka. Rosa aliona kwamba huyo

ndiye alikuwa mume aliyeandikiwa na Mungu tangu awali.

Rosa alikubali ombi la Charles la kutaka wawe wachumba.

Alimjibu kwa barua (uk. 76).

Ndoto yake ya kuolewa na Charles inaposhindikana, jitu maisha linamuua kama

alivyojisemea mwenyewe. Inaelezwa kwamba, wakati wa kuosha maiti yake,

karatasi safi sana iliyoandikwa na Rosa kwa kutumia damu aliyojichanja mkononi

kwa kutumia kiwembe, ilikutwa ndani ya kwapa lake. Juu ilikuwa imeandikwa jina

la Charles. Waliisoma:

Charles mimi nilikupenda. Ninakupenda hata sasa. Charles

ninajiua kwa ajili yako. Lakini kwa kuwa ninakupenda,

ninakwambia siri moja kubwa uzingatie. Charles kuoa bikira

ni bahati tu wala si kitu cha kutafuta: ukimwonja mchumba

wako kabla ya ndoa si bikira tena, hata kama alikuwa (uk. 93).

Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa, kitendo cha Rosa kuandika ujumbe katika

karatasi nzuri, tofauti na ile iliyotumiwa na Charles, ni ishara kuwa anaamua kufa

huku akiwa na mapenzi ya dhati kwake na anamthamini. Hii inatokana na kauli yake

mwenyewe anaposema: ―Charles mimi nilikupenda. Ninakupenda hata sasa.‖ Kwa

upande mwingine, kutumiwa kwa karatasi hiyo nyeupe kuna lengo la kuusaili

uadilifu na usafi wa maisha ya Charles. Hii inatokana na kitendo chake cha

kumhukumu Rosa kuwa ni mtu mwovu na asiyekuwa na thamani yoyote ya kuolewa

naye, kwa sababu ya kutokuwa na ubikira (uk. 90). Kutokana na hilo, imebainika

kuwa Rosa anaamua kumwachia ujumbe unaodokeza ugumu wa kuupata ubikira

anaoutafuta kwa sababu, wenye kuwaharibu wasichana na kuwaondolea ubikira wao

ni watu kama yeye. Anayabainisha haya anaposema: ―… ukimwonja mchumba wako

kabla ya ndoa si bikira tena, hata kama alikuwa.‖ Maneno haya yanamshitaki Charles

66

kuwa, na yeye yumo katika kuondoa na kuharibu ubikira wa wasichana.

Kulithibitisha hili, mwandishi anaonesha namna Charles anavyotaka kumwonja Rosa

kwa kufanya naye mapenzi, kabla ya kumwoa. Anasema:

… siku moja wakiwa katika hali hii, Charles alimwangusha

Rosa juu ya kitanda. Charles alikuwa katika hali mbaya. Rosa

alikuwa amefumba macho: alikuwa naye amekwisha. Charles

alifunga milango na madirisha. Rosa alikuwa bado amelala juu

ya kitanda akipumua kama njiwa. Charles alianza kumbusu;

waligeuzana huku na huko juu ya kitanda. Charles alianza

kuvuta gauni la Rosa juu polepole sana. Rosa alihisi mkono wa

Charles ukimgusa. Ulikuwa umefika mbali mara wazo

lilipomjia Rosa kichwani. Alishika mkono huo na kuurudisha

polepole (uk. 78).

Dondoo hili linathibitisha kuwa, ijapokuwa Charles anamwona Rosa kama mtu

mwovu na asiyekuwa na thamani kwake, naye pia ni mwovu kama alivyo Rosa.

Uovu wa Charles unajidhihirisha pia kutokana na kitendo anachotaka kumfanyia

Rosa, yaani kutaka kufanya naye mapenzi kabla ya kumwoa. Pia, utafiti umebaini

kuwa, Charles ana uzoefu wa kuwafanyia kitendo kama hicho wasichana wengine.

Hii ni kutokana na namna anavyofanya maandalizi kabla ya kumwingilia Rosa

kimwili. Maandalizi hayo ni pamoja na kufunga milango na madirisha, kulivuta na

kulipandisha gauni la Rosa juu, na kuingiza mkono katika sehemu nyeti za Rosa.

Hata hivyo, Charles anapolazimisha kufanya kitendo hicho, anasababisha Rosa

kusema uongo kwamba yeye ni bikira. Anasema:

―… Charles siyo leo.‖

―Mpaka lini?‖

―Mpaka siku tutakayooana. Afadhali tungoje siku yenyewe.‖

―Haiwezekani.‖

―Vumilia kidogo muda umekaribia. Ninakuomba usiniharibu

kabla ya muda. Charles – mimi ni bikira.‖

Rosa alitamka maneno ya mwisho kwa shida na kusitasita.

Charles aliposikia maneno haya alikufa ganzi. Hakuwa na

hamu tena ya kumpapasapapasa Rosa (uk. 78).

Ikumbukwe kwamba Rosa anaposema kuwa yeye ni bikira, tayari Charles ana taarifa

nyingi zinazohusiana na umalaya wake, alizozipata kutoka kwa marafiki zake hata

kabla ya kumwomba Rosa uchumba. Kutokana na hilo, utafiti umebaini kwamba

kitendo cha Rosa kumdanyanya Charles kuwa yeye ni bikira, kinatokana na matakwa

ya jamii yake, ya kuwataka mabinti kuolewa wakiwa na ubikira. Hii ni kwa sababu

67

katika utamaduni wa Mwafrika, suala la kutunza ubikira hadi wakati wa kuolewa lina

hadhi na thamani kubwa. Aidha, wasichana ambao hutunza ubikira wao hadi hatua

ya kuolewa kwao, hutambuliwa na kupewa heshima kubwa kwa kuwa na msimamo

imara katika kutunza maadili ya jamii zao. Hata hivyo, matokeo yanaonesha kuwa

ijapokuwa jamii hizo zinataka mabikira, bado zinaonesha udhaifu mkubwa katika

kuwashughulikia na kuwachukulia hatua watu wenye tabia mbaya kama za Charles,

wanaowaharibu mabinti zao. Hatuoni zikiwakemea na kuwachukulia hatua kali

wanaume wanaowahitaji mabikira, ilihali wao wenyewe ndio wanaowaharibia

mabinti hao ubikira wao.

Kwa jumla, utafiti umebaini kuwa haya ni miongoni mwa matukio ya mchakato wa

kujiua kwa Rosa yanayosawiriwa katika riwaya hii. Tasinifu hii inaonesha kuwa,

ijapokuwa matukio haya yanamhusu Rosa, kimsingi msichana huyu ametumiwa na

mwandishi kama kiwakilishi tu cha wasichana wengi wanaoishi katika nchi ya

Tanzania, Afrika ya Mashariki, Afrika, na ulimwengu mzima. Mwandishi amejaribu

kuonesha kwamba kuharibika kwa Rosa Mistika kunatokana na athari za kijamii na

mazingira anayoishi. Anakusudia kuifikishia jamii elimu ya sosholojia kwamba

jukumu la kulea mtoto si la baba na mama peke yao, bali ni la asasi mbalimbali,

ambapo asasi hizo huweza kumwathiri mtoto tangu akiwa mdogo hadi anapokuwa

mtu mzima. Matokeo yanaonesha kuwa asasi ya kwanza, ambayo ni familia, inaibua

hisia za huzuni kutokana na malezi ya Rosa, kwa namna anavyolelewa na baba yake.

imebainika kuwa Zakaria anamlea Rosa kwa mkono wa chuma na kumnyima

mapenzi, usalama na huruma. Pia, anamchunga kama kuku achungavyo vifaranga

vyake na kumkosesha uhuru wa kujiamulia mambo yake. Baadaye, Rosa anapopata

uhuru, anashindwa kuutumia. Matokeo yake anakufa kifo cha maumivu makali, huku

akikifurahia kwa sababu huo kwake, ndio uhuru aliokuwa anautafuta kama suluhisho

la taabu zake.

Hivyo, kulingana na nadharia ya Udhanaishi utafiti umebaini kwamba, ulimwengu

ndio unakuwa chanzo cha kuharibu maisha ya Rosa kwa kushindwa kumweleza

bayana kosa lake. Hii inatokana na ukweli kwamba mabadiliko ya tabia yake

yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na mazingira yanayomlea na kumkuza. Mwandishi

anaeleza kuwa, ―Rosa alikuwa msichana mzuri, mrefu kiasi, mnyenyekevu na

mnyamavu…‖ (uk. 4). Tabia hiyo nzuri ya Rosa Mistika inaharibiwa na mazingira

68

kama anavyoeleza Madumulla (2009) kwamba Kezilahabi anamuunda Rosa Mistika

kama fumbo linalokuja duniani kama bikira, lakini linachafuliwa na ulimwengu wa

misukosuko au dunia ya ―ubatili mtupu‖. Hii ina maana kwamba, ijapokuwa Rosa

alizaliwa bila hatia, lakini mazingira yake ndiyo yanayomharibia maisha yake.

Mfano mzuri ni Zakaria anayemnyima fursa ya kujifahamu na kuwafahamu watu

wengine, Sista John anayesababisha nguo na vitabu vyake kuchomwa moto,

Mwalimu Thomas anayesababisha Rosa kuondolewa sikio lake, pamoja na Charles

anayemlewesha, na kisha, kumbaka.

4.2.2 Muhtasari wa Riwaya ya Kichwamaji

Kichwamaji (1974) ni riwaya ya pili kuandikwa na Euphrase Kezilahabi na

imetumika katika kupata data za msingi za utafiti huu. Riwaya hii iliandikwa na

kuchapishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1974. Inasimulia kwa undani maisha ya

wahusika wawili, ambao ni Kazimoto na Manase. Vijana hawa baada ya kujipatia

elimu ya Kimagharibi, wanashindwa kueleweka vizuri kwa jamii kutokana na

matendo yao. Elimu ya Magharibi inawakengeusha na inakuwa sababu ya wao

kutazamwa tofauti na kizazi cha wazee na jamii kwa jumla.

Sakkos (2008) anaeleza kuwa Kichwamaji ni riwaya ya kwanza ya kidhanaishi katika

Kiswahili. Anafafanua zaidi kwamba katika riwaya hii, mwandishi anayachambua na

kuyasawiri maisha ya jamii yake kwa kina, huku akiegemea katika falsafa ya

Udhanaishi. Falsafa hii inatilia mkazo katika kuchunguza tajiriba ya mtu binafsi

katika kupambana na safari yake ya maisha. Sakkos anaongeza kuwa katika riwaya

hii, mwanadamu amesawiriwa kama kiumbe dhaifu, kinachoishi maisha magumu,

yaliyotawaliwa na vurugu na yasiyo na maana katika ulimwengu usiokuwa na

maana.

Kwa kiasi kikubwa, masimulizi na maudhui ya riwaya hii yanasawiri na kuelezea

maisha ya mhusika mkuu, Kazimoto, tangu akiwa mtoto mpaka anapoamua

kujisababishia kifo chake kwa kujiua. Mwandishi anaeleza kwamba kutokana na

Kazimoto kuwa na elimu ya Chuo Kikuu, anaamua kwenda kwa Mkuu wa Wilaya,

ambaye ni rafiki yake waliyekua pamoja, aitwaye Manase, kwa lengo la kuomba

kazi. Huko anafanikiwa kuonana naye, lakini anakataliwa. Baada ya hapo, Kazimoto

anaamua kurudi kijijini kwake akiwa na sononeko moyoni mwake. Anapokuwa

69

kijijini kwake, jamii pia inaonekana kujitenga na kuwa mbali naye. Pia, akiwa katika

hali hiyo ya mtanziko, anaumizwa sana kwa kitendo cha dada yake, Rukia, kutiwa

mimba na Manase. Kutokana na tukio hilo, anadhamiria kulipa kisasi kwa Manase,

pamoja na familia yake. Baada ya hapo, Kazimoto anapitia mikasa na matukio

mbalimbali yanayomsukuma na kumweka katika dimbwi la tafakuri kuhusu dhana na

maana ya maisha. Hatimaye, anayaona maisha kama adhabu, hali inayomsukuma

zaidi kutafakari na kuona kuwa hakuna Mungu.

Katika riwaya hii mwandishi anayasawiri na kuyapa uzito matatizo na matukio ya

kijamii, pamoja na mustakabali wake. Ili kumsawiri vyema Kazimoto, mwandishi

anaunda masimulizi yanayohusisha maisha ya wahusika wengine kama vile Sabina,

Pili, Vumilia, Moyokonde, Rukia, na Kabenga, ili kumjenga mhusika mkuu,

Kazimoto. Hatimaye, Kazimoto naye anafuata nyayo za Rosa Mistika. Anaamua

kujiua kwa kujipiga risasi kutokana na msongo wa mawazo, baada ya kupitia na

kukumbwa na matukio mengi katika maisha yake. Hapa tunabainisha baadhi ya

matukio ya mchakato wa kujiua kwake, ambayo ni: kunyimwa kazi, Rukia kutiwa

mimba, vifo vya Rukia na mama yake na kifo cha Kalia. Matukio mengine ni kifo

cha mtoto wake, kuugua ugonjwa wa ajabu, na kujitenga kijamii. Matukio haya

yamejadiliwa kama ifuatavyo:

4.2.2.1 Tukio la Kunyimwa Kazi

Matokeo yanaonesha kuwa mchakato wa kujiua kwa Kazimoto unaanza na tukio la

kwenda ofisini kwa Mkuu wa Wilaya, Manase, kwa lengo la kuomba kazi ya muda.

Huyu ni mtu anayefahamiana naye kwa muda mrefu kutokana kukua pamoja na

kusoma shule na Chuo Kikuu wakiwa pamoja. Imebainika kuwa, Kazimoto akiwa

ofisini hapo, kabla ya kuingia ndani na kuonana na Mkuu wa Wilaya, anapanga

foleni miongoni mwa watu wengi wanaokusudia kumwona kiongozi huyo. Hata

hivyo, licha ya kufahamiana naye, Kazimoto anapofanikiwa kuingia ofisini humo,

anakumbana na changamoto kwani hapokelewi vizuri, bali anadharauliwa na

kutolewa nje kwa madai kuwa, hana adabu. Badala yake anaambiwa aingie tena

mwishoni mara tu watakapomalizika watu wote walioko kwenye foleni.

Kudharauliwa na kutothaminiwa huko, ndiko kunakoanza kujenga chuki na mtazamo

hasi kuhusu thamani na maana ya maisha yake. Mazungumzo yafuatayo baina ya

Kazimoto na Manase yanalisawiri vizuri jambo hili:

70

―Habari za asubuhi,‖ nilimsabahi.

―Asante, keti kitini.‖

―Mimi nilikuwa na shida kidogo.‖

―Ndiyo kusema sasa huna.‖

―Nina shida,‖ nilijisahihisha ili kumpendeza. ―Natafuta kazi ya

muda. Miezi mitatu hivi.‖

―Wewe nani?‖ Nilikasirika kidogo, lakini hasira yangu

niliimeza kwa kuuma meno. ―Mimi Kazimoto, mwanafunzi

wa Chuo Kikuu – Dar es Salaam.‖

―Huko ndiko mnakofunzwa jinsi ya kuwasabahi wakubwa

namna hiyo.‖

―Mimi ninatafuta kazi.‖

―Hata mimi nilipokuwa Makerere nilikuwa nikiwaheshimu

watu. Au kwa kuwa umesoma Chuo Kikuu unafikiri u mtu

tofauti.‖

―Kusoma Chuo Kikuu siyo dhambi,‖ nilimjibu. ―Lakini mimi

hayo hayakunileta hapa. Mimi ninatafuta kazi.‖

―Huna adabu! Kaa nje kwanza, unanichelewesha kazi bure.

Utaingia humu mtu wa mwisho (uk. 4).

Kinachobainika katika dondoo hili ni hasira ya Kazimoto kutokana na kiburi, dharau

na udhalilishaji anaofanyiwa na Manase. Anakasirika zaidi anaposhuhudia upendeleo

wa wazi unaofanywa na kiongozi huyo, kwani anawasikiliza kwa makini na kuwapa

kazi watu wa jinsia ya kike, wakiwemo Vumilia, Pili, na Salima, na kuwanyima wale

wa jinsia ya kiume, akiwamo yeye. Sambamba na hilo, anakasirishwa na tabia ya

Manase ya kutumia ofisi hiyo ya umma kama sehemu ya kupangia mipango na

vitendo vyake vya umalaya na wasichana hao, huku watu wengi wakiwa kwenye

foleni wakisubiri kuingia. Hata hivyo, Kazimoto anapoingia kwa mara ya pili, baada

ya kusubiri kwa muda mrefu, anaambiwa kuwa muda umekwisha na kutakiwa kurudi

kesho yake. Majadiliano yafuatayo baina yao, yanadhihirisha jambo hili:

―Samahani, ninataka kufunga ofisi. Saa nane na nusu sasa.

Utarudi kesho.‖ Nilimtazama machoni kwa mshangao.

―Kazimoto, fika kesho asubuhi.‖

―Mimi niliendelea kumkazia macho.‖

―Bwana Manase,‖ nilimwita.

―Ndiyo, unanifahamu; lakini sasa nimo kazini.‖

―Ndiyo.‖

―Manase,‖ nilimwita tena.

―Kazimoto,‖ aliniita (uk. 7).

Dondoo hili, linaonesha kiburi cha kiongozi huyu na namna anavyokiuka maadili na

misingi ya kazi yake, huku akitoa huduma kwa upendeleo na kuwanyanyasa watu

wake. Jambo hili linamkasirisha, linamuumiza, linamsumbua na kumuudhi sana

71

Kazimoto. Ndiyo maana anapoambiwa muda umekwisha, anaendelea kusimama

palepale, huku akimtazama kwa muda (uk. 7). Matokeo yake, anaamua kwenda

kunywa pombe nyingi ili alewe upesi kama njia ya kuyasahau mambo hayo. Kitendo

hicho cha kwenda kunywa pombe ni dalili mojawapo ya kukata tamaa ya maisha

kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi. Matokeo yake ni kwamba hasira

hii inapomzidi, anapanga kwenda ofisini kwa Manase kesho yake ili akamchome

visu. Mwandishi anaeleza kwamba:

Wazo la kufika tu ofisini nimchome Manase visu vya tumboni

lilinijia tena kichwani. ―Huenda nami nikanyongwa,‖ nilisema

moyoni. ―Sitapata faida yoyote isipokuwa kuwaacha wazazi

wangu taabuni. Jambo la maana ni kujaribu kumpa Manase

maisha magumu hapa duniani. Nisipoweza basi nitajilipiza

kisasi kwa njia nyingine.‖ (uk. 15).

Kinachojitokeza katika dondoo hili ni kwamba Kazimoto anaamua kuachana na

uamuzi wa kwenda kumchoma visu Manase kwa kuhofia madhara makubwa

yanayoweza kumpata. Anaachana na kitendo hicho, huku akiwa na kinyongo moyoni

mwake kutokana na Manase kumtia mimba dada yake, Rukia, (uk. 16). Hili

linathibitishwa na Kazimoto mwenyewe, baada ya kuamua kumuuliza Manase

kuhusu tukio hilo la kinyama (kur. 16 – 17). Matokeo ya kuuliza swali hilo,

yanasababisha apoteze na kunyimwa kazi ya kuhesabu ng‘ombe, aliyokuwa

amepewa na Manase muda huo huo. Mwandishi anaeleza kuwa, Manase akiwa na

hasira kali alimnyang‘anya Kazimoto karatasi yake na kumtamkia waziwazi kuwa:

―Sasa hata kazi hupati…‖ (uk. 17).

Utafiti umebaini kuwa tukio hili la kunyimwa kazi linaunda mchakato wa kujiua

kwake, kwani kitendo cha Kazimoto kupanga kumchoma visu Mkuu wa Wilaya ni

dalili ya kukata tamaa ya maisha yake. Suala hili kama linavyoelezwa katika

nadharia ya Udhanaishi, linamtokea akiwa katika harakati za kuutafuta uhuru wake

binafsi na uwezo wa kujifikiria na kujiamulia mambo yake mwenyewe. Hali hiyo

ndiyo inayosababisha akengeuke misingi ya maisha ya jamii yake na kupanga

kumuua kiongozi huyo wa Serikali. Kutokana na hilo, tumebaini kwamba iwapo

kitendo hicho kingefanikiwa, huo ungekuwa mwisho wa maisha yake ama kwa

kujiua mwenyewe au kwa kuuawa na nguvu ya umma. Hivyo, tukio hili la kunyimwa

72

kazi kwa Kazimoto, linajenga chuki na visasi moyoni mwake na linakuwa chanzo

kimojawapo cha mchakato wa kujiua kwake.

4.2.2.2 Rukia Kutiwa Mimba

Hili ni tukio lingine la mchakato wa kujiua kwa Kazimoto ambapo dada yake, Rukia

anatiwa mimba na Manase, wakiwa wanaishi pamoja huko Dar es Salaam. Haya

yanatokea baada ya Kazimoto kumwomba Manase, ambaye ni mtu wake wa karibu

na rafiki waliyesoma pamoja, kukaa na Rukia ili aendelee na masomo yake ya darasa

la tisa. Matokeo yake, Manase anautumia mwanya huo kumwingilia Rukia kwa

nguvu na kumtia mimba. Tukio hili linamkasirisha sana Kazimoto, kiasi cha

kumfanya ayachukie maisha yake, kumchukia Manase na kujenga uhasama dhidi

yake. Anakasirishwa zaidi na uongo wa Manase, anayedai kwamba Rukia ndiye

aliyemlazimisha kufanya naye mapenzi kutokana na umalaya wake. Haya

yanabainishwa katika mazungumzo baina ya Kazimoto na Manase kama ifuatavyo:

―Manase.‖ Nilimwita. Alinitazama. ―Jambo gani ulifanya?‖

Nilimuuliza hali nikimtazama usoni. Mara moja sura

ilimgeuka. Nilimwona anafungua mdomo polepole.

―Kazimoto, huelewi vizuri hadithi yenyewe.‖

―Halikuwa kosa langu.‖

―Ni kosa la nani?‖

―Hakika Rukia mchokozi sana. Yeye ndiye alinianza.‖

―Alikuanzaje?‖

―Unaona. Siku moja nilipokuwa nimelala usingizi nilisikia

mtu anagonga mlango wangu. ‗Nani huyo!‘ Nilisema kwa

sauti. ‗Ni mimi Rukia, fungua mlango!‘ ‗Kuna nini?‘

Nilimuuliza. ‗Wewe fungua mlango tu!‘ Nilipofungua mlango

aliingia chumbani mwangu; alilala juu ya kitanda changu. Sasa

wewe fikiri Kazimoto, mwanaume kama wewe ungefanya

nini?‖ … Bila shaka utakubalina nami kwamba Rukia alikuwa

malaya tangu alipoota maziwa (kur. 16 – 17).

Dondoo hili linabainisha uongo wa wazi wa Manase wa kumsingizia Rukia kwamba,

ndiye aliyemchokoza na kusababisha kufanya naye mapenzi. Aidha, kauli hii,

inaonesha namna wanaume wanavyowalaghai watoto wa kike kimapenzi, ambapo

mara tu wafanikiwapo katika nia yao ovu, huwakataa na kuwadharau. Kitendo cha

Manase kumwita Rukia malaya, ndicho kinachomkasirisha zaidi Kazimoto,

kinamkatisha tamaa ya maisha na kujenga chuki na visasi dhidi yake. Mwandishi

anabainisha majadiliano baina yao kama ifuatavyo:

73

―Unamwita malaya!‖ Nilisema kwa hasira.

―Ndiyo.‖

―Hebu sema tena!‖

―Rukia ni malaya. Kama umekasirika na jambo lililotokea kwa

bahati mbaya unaweza kufanya jambo lolote upendalo! Sijali

sasa!‖ Alisema kwa hasira. ―Sasa hata kazi hupati!‖ Karatasi

nilinyang‘anywa.

―Tutaona!‖ Alimwambia kwa hasira kubwa (uk. 17).

Katika dondoo hili, Kazimoto anakasirishwa na kitendo cha Manase cha

kumdhalilisha Rukia kwa kumwita malaya. Anapolitamka kwa hasira neno ―tutaona‖

ni dalili ya kukata tamaa kwake na kwamba yuko tayari kwa lolote linalomjia mbele

yake. Kukata tamaa huku ndiko kunakomwingiza katika mchakato wa kujiua

kutokana na kusongwa na mawazo mengi yanayotokana na tukio hili. Anazidisha

chuki kwa Manase anapopewa ujumbe na Rukia kwamba hayuko tayari kuendelea

kuishi na Manase na kwamba ataacha shule, iwapo hatatafutiwa sehemu nyingine ya

kuishi kutokana na vitendo anavyofanyiwa na Manase. Anasema:

―Sijui Manase ni mtu wa namna gani. … Kaka usiponitafutia

mahali pengine pa kukaa mimi nitarudi nyumbani. Heri

kuacha shule!‖ (uk. 19).

Kazimoto anazidi kuchanganyikiwa anapobaini kwamba Rukia amekata tamaa, hana

furaha na uvumilivu wake wa kuendelea na shule umekwisha. Kabla ya kuufanyia

kazi ujumbe huo, anasongwa zaidi na mawazo anapopokea barua inayoeleza matukio

na mapito yote ya Rukia. Katika barua hiyo, Rukia anasema:

Kaka mpendwa,

Moyo wangu siku hizi hauna raha. Lakini leo nimechukua

kalamu ili nikueleze mambo yote. Nimeona kwamba siwezi

kuwa nakuficha wewe mambo, hali mambo yenyewe sasa

hayawezi kufichika. Wewe ukiwa ndiye kaka yangu na ndiye

uliyenitafutia nafasi hii ya shule ninakupa heshima. Fahamu

kuwa mambo haya sijapata kumweleza mtu mwingine

isipokuwa wewe peke yako.

Kaka, uliponileta hapa nilikaa kwa raha kwa muda wa juma

moja tu. Baada ya juma hilo, niliona Manase anaanza

kunitazama kwa njia ya ajabu. Baada ya majuma mawili

mambo yalizidi kuwa mabaya, kwani nilipokuwa naoga siku

moja niliona jicho lake kwenye tundu la ufunguo. Mwishowe

aliniambia wazi alichokuwa anataka. Nilimwambia: Manase!

Kaka yangu akifahamu litakuwa jambo la aibu sana! Lakini

yeye alijibu kwamba wewe ni mwanaume kama yeye. Alifika

74

hatua ya kutumia nguvu! Na kweli alitumia nguvu bila utashi

wangu. Kaka, sitaki kukupotezea muda wako wa kujifunza kwa

kusoma barua ndefu. Mimi maisha yangu yameharibika. Shule

nimekwishaacha. Jambo ambalo limenisikitisha sana ni hili

lifuatalo: Jana usiku, Manase alirejea nyumbani mlevi.

Alikuwa na tikiti ya basi. Baada ya kunitukana kwa maneno

ambayo siwezi kukuandikia, alianza kupanga vitu vyangu

sandukuni. Leo atanisindikiza hadi kituo cha basi. Kaka,

machozi yananilengalenga, sijui nitasema nini kwa baba na

mama. Usifike kuja kuniaga kwenye kituo cha basi nisije

nikazimia.

Sina mengi,

Nduguyo,

Rukia Mafuru (kur. 19 - 20).

Kutokana na barua hii, imebainika kwamba Kazimoto anazidi kuchanganyikiwa na

kuongeza chuki na hasira mara tu, anapopata taarifa kwamba Rukia amekuwa akiishi

maisha ya taabu na mateso kwa muda mrefu, lakini hakutaka kuitoa siri hiyo

mapema. Matokeo ya usiri na uvumilivu wake huo, ndiyo yanayosababisha atiwe

mimba na kuvuruga maisha yake ya baadaye. Hapo ndipo Kazimoto anapobaini

kuwa, Rukia ameamua kuandika barua hiyo, baada ya kukosa furaha na matumaini

kwa kuona kwamba maisha yake sasa, hayana maana yoyote.

Kwa kuzingatia msingi wa kwanza wa nadharia ya Udhanaishi unaojadili matatizo

halisi yanayomkumba binadamu utafiti umebaini kwamba, watu wengi hujiua

kutokana na kuzidiwa na maumivu makali wayapatayo. Maumivu hayo

husababishwa na mrundikano wa mambo ambayo huwa wanayashikilia katika mioyo

yao, pasipokuwashirikisha watu wao wa karibu. Hili ndilo linalomtokea Kazimoto,

kwani mara tu baada ya kupata barua hiyo, anapatwa na msongo wa mawazo na

hasira yake inazidi kufura. Hafurahishwi na kiburi cha Manase cha kumdhalilisha na

kumnyanyasa dada yake kwa kumwita malaya, huku akimwambia kwamba

Kazimoto ni mwanaume kama yeye. Hali hiyo inasababisha ashindwe kuhudhuria

masomo kwa muda wa siku moja kutokana na kichwa chake kuvurugika. Tukio la

Rukia kutiwa mimba linamsababishia msongo wa mawazo unaomweka katika

mchakato wa kujiua kwake. Hii ni kwa sababu yeye ndiye aliyemwomba Manase

akae na Rukia. Hivyo, anajiona kuwa anastahili kubebeshwa lawama za uharibifu

huo.

75

4.2.2.3 Vifo vya Rukia na Mama Yake

Tukio lingine la mchakato wa kujiua kwa Kazimoto linatokana na vifo vya dada

yake, Rukia, pamoja na mama yake. Kama ilivyokwisha kuelezwa hapo awali,

matokeo yanaonesha kuwa tukio la kutiwa mimba kwa Rukia linapokelewa kwa

masikitiko makubwa na Kazimoto pamoja na familia ya mzee Mafuru, ambaye ni

baba yake Kazimoto. Kwa mfano, mama yake anapopata taarifa hii, anasononeka

sana moyoni mwake; na kama ilivyo kwa Rukia, wote wawili wanakataa kula kwa

muda mrefu. Hata Kazimoto anaporejea nyumbani kutoka Chuo, anawakuta wakiwa

katika hali hiyo, huku wakilia muda wote kwa masikitiko makubwa. Hali hii

inamsababishia maumivu moyoni mwake na inaendeleza chuki na msongo wa

mawazo. Anaumia na kusononeka zaidi anapofanya jitihada za kumbembeleza Rukia

ili ale chakula, lakini jitihada hizo zinashindikana. Kuhusiana na suala hili,

mwandishi anaeleza namna Kazimoto anavyombembeleza Rukia. Anasema:

―Rukia,‖ nilimwita polepole. ―Rukia,‖ niliita tena.

Hakuniitikia. Nilijaribu tena. ―Rukia, jaribu kula chakula

kidogo.‖ Hakuniitikia. Badala yake alianza kulia kwa kelele

(uk. 37).

Katika nukuu hii, mwandishi anajaribu kuisawiri hali aliyo nayo Rukia kutokana na

kitendo hicho cha kutiwa mimba pasipo ridhaa yake. Hali hiyo halimtokei Rukia

peke yake, bali hata mama yake anakuwa katika wakati mgumu kutokana na hali

aliyo nayo binti yake. Utafiti umebaini kwamba, muda mfupi baadaye, mama yake,

huku akiwa amejaa uchungu, anamwambia Kazimoto mambo yanayowasibu yeye

pamoja na Rukia. Anamweleza kuwa vijana wa siku hizi wanaangamiza maisha ya

wazazi na kwamba, kutokana na hilo, yeye hatakuwa na muda mrefu wa kuishi kwa

sababu atakufa pamoja na binti yake. Anasema:

―Kazimoto,‖ mama alisema. ―Kazimoto, tuache tupumzike,

tuache tulie. Huu ni ugonjwa umeletwa na vijana na

utatumaliza sisi kina mama wenye mabinti. Ninajiona kwamba

nitakwenda pamoja na binti yangu‖ (uk. 37).

Maneno haya yanazidi kumuumiza Kazimoto, kwa sababu hapendi kuwaona Rukia

na mama yake wakiendelea kulia na kuumia kiasi hicho. Anashindwa kuvumilia na

kuamua kuondoka, huku akiwaacha wote wawili wanalia wakiwa wamekumbatiana.

Imebainika kuwa, akiwa katika maumivu na sononeko hilo, mama yake huyu

76

anaendeleza mgomo wa kula kwa madai kwamba atakula mara tu atakapojifungua

binti yake. Jambo hili linathibitishwa na mwandishi anaposema: Saa sita, chakula

kilipoletwa, tulisikia kwamba mama alikataa kula mpaka binti yake atakapojifungua

(uk. 76).

Kazimoto anazidi kuumia, kwani kitendo cha Rukia na mama yake kukataa kula

kinasababisha afya zao kuzorota na kudhoofu sana. Matokeo yake, Rukia anakosa

nguvu wakati wa kujifungua na kusababisha kifo chake. Mazungumzo baina ya Tuza

na Kazimoto yanathibitisha jambo hili kama ifuatavyo:

―Kazimoto,‖ Tuza alisema, ―ndugu yako amekufa kwa sababu

amekosa nguvu; alikuwa hajala vizuri kwa muda mrefu

uliopita.‖

―Hayo usemayo ni kweli,‖ nilimwambia.

―Amekufa akitaja jina lako,‖

―Alisema nini kuhusu jina langu?‖

―Alikulilia; akikuomba umsamehe kwa yale yote yaliyotokea

kwake. Amekuomba usisikitike sana. Hata yeye alikuwa haoni

tena maana ya kuishi.‖

―Ndiyo hayo aliyosema?‖

―Nimesahau jambo moja. Amesema kwamba, maadam yeye

akitoweka kama yalivyokwisha kutimia, anakutakia uhusiano

mzuri na Manase. Yeye amemsamehe ni zamu yako

kumsamehe‖ (uk. 83).

Matokeo yanaonesha kuwa, Kazimoto anapoipokea taarifa ya kifo cha dada yake,

anapata uchungu, majonzi, masikitiko na maumivu yasiyomithilika. Hii ni kwa

sababu mama yake pia, anakufa muda mfupi baada ya kifo cha Rukia. Kauli yake

aliyoisema mara tu, baada ya Rukia kupata mimba kwamba atakufa pamoja na binti

yake, kutokana na ugonjwa ulioletwa na vijana, kuwaua akina mama wenye mabinti,

inatimia. Kifo hiki kinatokea muda mfupi mara tu baada ya Kazimoto kupata taarifa

ya kifo cha Rukia, ambapo anaitwa na baba yake, Mzee Mafuru na kuambiwa

kwamba mama yake amezimia, huku akimwagiwa maji kichwani (uk. 82). Kifo cha

mama yake kinatokana na uchungu na maumivu makali anayoyapata anaposhuhudia

kaburi la mtoto wake. Mwandishi anaeleza namna kifo hicho kinavyotokea.

Anasema:

Wakati wa kuchimba kaburi, mama alikuwa ndani ya nyumba

akizungumza mambo ambayo yalikuwa hayaeleweki. Lakini

kaburi lilipokwisha, Tuza na Tegemea walimshika na

77

kumsaidia kutoka nje ili aone binti yake akizikwa. Alipofika tu

mlangoni na kuona shimo lililokuwa limechimbwa tayari

kumzika binti yake alilia kwa sauti ya juu sana. ―Rukia!

Rukiaa!‖ hali akionyesha kwa mkono wake kaburini. Halafu

alianza kulia kwa namna ya pekee. ―Kichwa! Kichwa!‖

alitotoma na kuanguka chini. Wakati alipobebwa kupelekwa

kitandani alikuwa amekwisha kufa (uk. 85).

Katika dondoo hili tunabaini hisia za huzuni, masikitiko na majonzi yanayoibuliwa

na kuikumba familia ya mzee Mafuru. Maumivu na masikitiko ya mama yake

Kazimoto kutokana na kifo cha Rukia, yanamsonga na kusababisha kifo chake.

Tukio hili linasababisha Kazimoto kusongwa sana na mawazo na kutamka maneno

ya masikitiko na ya kuhuzunisha yanayoonesha wazi kwamba tukio hili ni mojawapo

ya matukio ya mchakato wa kujiua kwake. Tunaelezwa kuwa:

Huo ndio ulikuwa mwisho wa mama yangu. Nilikuwa siwezi

kumwona tena maishani. Nilikuwa siwezi kusikia tena sauti

yake. Mola alimnyima ile furaha kubwa wapatayo kina mama

wakati mtoto wao anapooa. Huo ndio ulikuwa mwisho wa

mama aliyempenda binti yake wa pekee kama pumzi na

mwanadamu. Alikuwa amenyang‘anywa pumzi yake.

Niliyakumbuka tena maneno yake, ―Kazimoto, tuache

tupumzike, tuache tulie. Huu ni ugonjwa umeletwa na vijana,

na utatumaliza sisi kina mama wenye mabinti. Ninajiona

nitakwenda na binti yangu‖ (uk. 85).

Ni kweli kwamba kauli ya mama yake inatimia, kwani anakwenda pamoja na binti

yake. Utafiti umebaini kwamba vifo hivi vinatokea kutokana na wahusika hao

kuyaona maisha kuwa hayana maana, kama inavyoelezwa katika nadharia ya

Udhanaishi. Kitendo cha kukataa kula muda wote ni uthibitisho kwamba, kwao

maisha hayakuwa na maana na walikuwa tayari kufa muda wowote. Hili

linathibitishwa na kauli ya Rukia aliyomwambia Tuza kabla ya kufa kwake kwamba,

―… Hata yeye alikuwa haoni tena maana ya kuishi…‖ (uk. 83).

Matokeo yanaonesha kuwa tafiti mbalimbali, ikiwamo ile ya Kubller-Rose (1991)

zinabainisha kuwa, kufikiri na kupenda kuongelea masuala ya kifo na kujiua ni dalili

mojawapo ya mtu kujiua. Hili linajitokeza kwa Kazimoto, ambaye, baada ya kifo cha

Rukia na kile cha mama yake, anatumia muda wake mwingi kuwaza juu ya tukio

hili. Huu ni mchakato wa kujiua, kwani hata katika ujumbe anaouacha kuhusu kujiua

kwake, anaongelea kuhusu suala la kifo. Mwandishi anaeleza kuwa, baada ya vifo

78

vya ndugu zake hao, Kazimoto alianza kufikiri jinsi kifo chake kitakavyokuwa.

Anasema:

―Usiku nilianza kufikiri juu ya kifo. Nilifikiri jinsi kifo changu

kitakavyonijia – kwa ugonjwa, kwa ajali au kwa

kukatwakatwa na wezi? Labda kwa uzee au kwa sumu!

Huenda nikajiua mwenyewe! Nilikumbuka ndoto ya Kalia.

Niliwakumbuka wale ng‘ombe, sisimizi, nyuki, na mengine

mengi niliyoyaona huko machungani. Niliona kwamba adhabu

kubwa ya mwanadamu ni maisha yenyewe. Nilimkumbuka

mlevi mmoja niliyemkuta akipiga mti mweleka mpaka

akaumia mwenyewe. Maisha ndiyo yaliyokuwa yakimsumbua,

wala siyo pombe. Wakati huo usiku niliyaona maisha chanzo

cha yote.‖ (uk. 84).

Dondoo hili linamwonesha Kazimoto akiwa katika kina cha tafakuri kuhusu kifo na

namna kitakavyomjia. Nadharia ya Udhanaishi inafafanua kuwa maisha ya mtu ni ya

kitanzia na hayana maana, kwani mwisho wa mwanadamu ni kifo. Pia, inamwona

binadamu kama kiumbe anayeteseka na anayeishi katika ulimwengu usiomjali;

aliyezungukwa na mateso na ubwege na anayeshindwa kukabiliana au kupatana

vyema na uhalisi huo. Haya ndiyo yanayoonekana kumsumbua sana Kazimoto

kutokana na matatizo mengi anayokabiliana nayo. Katika tafakuri yake, anaona kuwa

binadamu amepewa adhabu ya kuyatunza maisha yake. Hata hivyo, anaeleza kuwa

maisha yenyewe siyo rahisi, kwani ni adhabu kubwa kuyatunza kwa sababu huwa

hayashibishwi wala kuridhishwa. Zaidi ya hayo, huyo aliyetoa adhabu ya kuyatunza

maisha hayo, huyachukua wakati wowote aupendao.

Hatimaye, matokeo yanaonesha kuwa, baada ya Kazimoto kufikiri kuhusu kifo kwa

muda mrefu, anaamua kutamka waziwazi kuwa mwisho wa mwanadamu utaletwa na

mwanadamu mwenyewe. Hii inaonesha kuwa tukio la vifo vya Rukia pamoja na

mama yake, pia ni mojawapo ya matukio yanayomsukuma katika mchakato wa

kujiua kwake.

4.2.2.4 Kifo cha Kalia

Tukio la kuuawa kwa Kalia, ambaye ni mdogo wake Kazimoto, nalo linachangia

kwa kiasi kikubwa katika mchakato wa kujiua kwa Kazimoto. Hii inatokana na

ukweli kwamba mambo mengi anayoyafanya yanamwathiri Kalia na kusababisha

tabia yake kubadilika. Miongoni mwa mambo hayo ni kumtuma mara kwa mara

79

kwenda kumwitia wasichana wake, na wakati mwingine kufanya vitendo vya ufuska

mbele yake. Kalia anapochoshwa na mwenendo wa Kazimoto, anaamua kukengeuka

na kumtamkia waziwazi kwamba naye anahitaji kuwa na mwanamke (uk. 73).

Mabadiliko ya tabia na mwenendo wake, yanamsababishia Kazimoto msongo wa

mawazo unaomwingiza katika mchakato wa kujiua kwake. Hii ni baada ya Kalia

kuuawa na wananchi kutokana na tabia yake ya umalaya iliyochangiwa kwa kiasi

kikubwa na mwenendo mbaya aliouiga kutoka kwa Kazimoto.

Matokeo yanaonesha kuwa tukio la kwanza linaloonesha mabadiliko ya tabia ya

Kalia linashuhudiwa na Kazimoto mwenyewe, ambapo Kalia anaamua kumtoroka

Kazimoto na kutaka kumbaka msichana mdogo, akiwa machungani. Hata hivyo,

msichana huyo anaokolewa na Kazimoto kabla ya kufanyiwa kitendo kibaya na

Kalia kama inavyobainishwa katika dondoo hili:

… alikuwa amekwishavutwa mpaka majanini. Niliona tu

majani yakitingishika. Niliweka kitabu changu mkononi halafu

nilishuka. Nilikimbia mara moja kwenda kumwokoa huyu

msichana, wakati huu nikihisi kwamba alikuwa ameshikwa na

chatu. Nilipofika pale mahali sikujua la kufanya. Msichana

alikuwa amelala kifudifudi akilia. Macho ya Kalia

yalipokutana na yangu aliona kwamba tendo alilofanya

halikunifurahisha (uk. 80).

Dondoo hili linaonesha namna Kazimoto alivyochukizwa na kusononeshwa sana na

tukio hili la Kalia, la kutaka kumbaka msichana huyo. Hili linasababisha Kazimoto

asikitike na kujilaumu kwamba kwa kuwa yeye ndiye chanzo cha mabadiliko ya

tabia ya Kalia, basi anastahili kuwajibika kwa hilo. Majibizano baina yake na Kalia

ni uthibitisho kwamba kuharibika kwa tabia ya Kalia, kunatokana na matendo maovu

aliyoyaiga kutoka kwa Kazimoto:

―Kalia, kwa nini umefanya hivi?‖ Nilimuuliza. Alinyamaza.

―Umefanya, umefurahi, lete mkono nikupe heko,‖

nilimwambia.

Alicheka kidogo wakati nikimsogelea. Nilipomsogelea

nilimpa vibao viwili vitatu akaanguka chini.

―Mbona wewe huwa unafanya. Mimi sijasema lolote hata kwa

baba. Leo mimi nafanya unanipiga. Kwa nini? Unanionea tu.

Unafikiri mimi mjinga kuwa natazama tu?‖ Alipomaliza

kusema hivi aliinuka kwenda nyumbani (uk. 80).

80

Katika dondoo hili, Kazimoto anashitakiwa na dhamiri yake anapobaini kuwa

mabadiliko ya tabia ya Kalia yanatokana na matendo yake maovu. Maneno ya Kalia

kwamba ―mbona wewe huwa unafanya‖, ndiyo yanayomzindua na kubaini kwamba,

kumbe yeye ndiye chanzo cha mkengeuko huo. Kalia anathibitisha ule usemi

usemao, mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu. Kazimoto anatoa kibanzi

katika jicho la Kalia wakati kwenye jicho lake kuna boriti. Hatimaye, anaanza kuona

ubaya na udhaifu wake wote ndani ya Kalia. Hii inamfanya aukumbuke msemo

usemao, mkuki humuua yule aliyeufua. Tabia na mwenendo wake mbaya ndio

unaomwingiza katika mchakato wa kujiua kwake kutokana na msongo wa mawazo

anaoupata. Hii ni baada ya kutambua kwamba, yeye ndiye sababu ya kifo cha Kalia.

Anasema:

Huu ndio ulikuwa mwisho wa nunda mla watu (Kalia).

Mwisho wake uliendelea kunisumbua moyoni; kifo chake

kilihusika sana na matendo yangu. Ilikuwa kama kwamba

mimi mwenyewe nilimuua mdogo wangu (uk. 114).

Dondoo hili linabainisha wazi mchakato wa kujiua kwa Kazimoto, kwani kifo cha

Kalia kinampa msongo wa mawazo na maumivu makali moyoni mwake. Maneno

haya ndiyo anayoyarudia katika ujumbe anaouandika kabla ya kujiua kwake.

Anatamka kuwa yeye ndiye aliyemuua mdogo wake, ingawa hakumgusa. Kazimoto

anayatamka maneno haya, mara tu baada ya Kabenga kuleta taarifa kwamba mwili

wa Kalia umekutwa ukielea majini. Baada ya taarifa hiyo, miji ya Mafuru na

Kabenga inaamua kwenda kuuchukua. Mwandishi anaeleza hivi:

Mji wetu na Kabenga tulikwenda kubeba maiti na kuleta

nyumbani. Kalia alikuwa amechomwa mikuki miwili, mmoja

tumboni, na mwingine kifuani. Ilikuwa kazi bure kueleza

polisi, baba hakutaka. Kila mtu kijijini alifikiri kifo

kilichompata kilikuwa cha haki na kwamba angeishi angeleta

maafa mengi zaidi (uk. 114).

Dondoo hili linaonesha tukio lingine gumu linalompata Kazimoto na kusababisha

ajielekezee lawama kwa kusababisha kifo cha mdogo wake. Ni kweli kwamba

hakumgusa kwa kumchoma mikuki hiyo, lakini ni wazi kwamba ndiye aliyemchoma

Kalia mikuki mingi zaidi ya hiyo miwili iliyokutwa mwilini mwake, kutokana na

tabia na mwenendo wake mbaya.

81

4.2.2.5 Kifo cha Mtoto Wake

Kufiwa na mtoto wake ni tukio lingine la mchakato wa kujiua kwa Kazimoto. Tukio

hili linatokea kwa sababu ya Sabina, ambaye ni mke wa Kazimoto kucheleweshwa

kupata huduma akiwa katika uchungu wa kujifungua, wakati huo daktari

akimhudumia mgonjwa mwingine. Mlolongo wa matukio yanayompata Kazimoto

unazidi kumpa msongo wa mawazo na kumchanganya kifikra. Mkanganyiko huo

anaupata mara tu baada ya kuwasili hospitalini, ambako anaelezwa na Yaya namna

mambo yalivyotokea:

―Poleni sana Kazimoto, mtoto wako amerudi. Hakuweza

kuishi. Wakati wa kujifungua ulipofika daktari alikuwa

akifanya upasuaji kwa mtu mwingine. Mke wako alipata shida

ya kuweza kupitisha kichwa cha mtoto ambacho kilikuwa

kikubwa kupita kiasi. Daktari alichelewa kufika. Alipokuja

mtoto alizaliwa lakini aliishi kwa muda wa saa moja tu.

Tulifanya tuliloweza ili kuokoa maisha yake, lakini kwa kuwa

hakuzaliwa ili apate kuishi, alirudi (uk. 179).

Dondoo hili linaonesha kuwa maelezo yanayotolewa na Yaya, yanamuumiza zaidi

Kazimoto, kwani yanamthibitishia na kuweka bayana kuhusu kifo cha mtoto wake

huyo. Maelezo hayo yanaonesha wazi kwamba licha ya mtoto huyo kuwa na kichwa

kikubwa, huenda angeweza kupona iwapo daktari angemhudumia mapema.

Maumivu yake yanazidi anapoingia katika chumba kimojawapo na kuwakuta Tuza

na Sabina wakiwa wanalia. Kilio chao kinazidi mara wanapomwona Kazimoto

anaingia. Kazimoto kupitia kwa mwandishi anaeleza:

―Nilikaa juu ya kitanda. Niliweka mkono wangu ndani ya

mkono wa mke wangu ambaye sasa alilia kwa kwikwi.

Sikuweza kusema neno lolote isipokuwa kusikitika kwa

unyamavu‖ (uk. 179).

Kitendo cha Kazimoto kukaa kimya bila kusema jambo lolote kinadhihirisha namna

alivyokuwa na maumivu ya ndani juu ya tukio hilo. Katika hali ya kawaida, ni vema

mtu kusema kitu kilichomo moyoni kuliko kukaa nacho, huku akiumia ndani kwa

ndani. Hili ndilo linalompata Kazimoto, kwani anaamua kukaa kimya. Zaidi ya hayo,

hata walimu wenzake alioongozana nao kwenda hospitalini, wanaporuhusiwa

kuingia ndani, nao wanaamua kukaa kimya. Kuhusu hili, mwandishi anasema:

82

―Waliingia. Wao pia walinyamaza baada ya kuyaona mambo

yalivyokuwa kwa macho yao wenyewe. Nani atamuuliza nani?

Na nani atasema nini? Chumba chote kilikuwa kimya

isipokuwa kwikwi za Tuza na mke wangu. Tulikesha

chumbani humo pamoja nao huzuni ilitawala chumba kizima‖

(uk. 179).

Dondoo hili linaonesha namna tukio hili linavyomchanganya Kazimoto, na hajui la

kufanya. Majonzi ya kufiwa na mtoto wake, yanamsukuma na kumzamisha katika

tafakuri ya kina kuhusu ukatili wa Mungu dhidi yake. Anaona kuwa mateso hayo

yote yangeweza kuepukwa iwapo Mungu angemwonea huruma. Anasema:

―Nilianza tena kufikiri juu ya Mungu. Kama kweli alikuwapo

kwa nini aliweza kufanya ukatili mkubwa kama huo.

Matumaini yetu yote; kazi na taabu tuliyopata – yote hayo

chini! Sikuona maana ya kuishi‖ (uk. 180).

Kinachobainika katika dondoo hili ni kwamba Kazimoto anatafakari kuhusu nafasi

ya Mungu katika mahangaiko yake. Kama inavyoeleza nadharia ya Udhanaishi,

anaonesha dalili za wazi za kukana nafasi na uwepo wa Mungu kwa madai kwamba

hamjali, ambapo hata ulimwengu wenyewe, nao pia hauko upande wake. Anaposema

kuwa haoni sababu ya kuishi ni dalili ya kukata tamaa. Hili ndilo analoandika pia

katika ujumbe anaouacha kabla ya kuamua kujiua kwake. Anasema kuwa anaamua

kujiua kwa kuwa haoni sababu ya kuendelea kuishi na kuzaa kizazi kibaya. Anakata

tamaa ya maisha kwa kuona kwamba hayana maana. Haya yanathibitishwa katika

majadiliano baina yake na Sabina kama ifuatavyo:

―Mimi nimekata tamaa,‖ nilimwambia mke wangu.

―Tamaa ya nini?‖ aliniuliza kwa sauti yenye masikitiko mengi.

―Ya kuishi – kupata watoto.‖

―Mimi nina matumaini bado. Mungu ni mkubwa; Anafahamu

kila kitu. Atatuwekea kitu kikubwa na kizuri zaidi.

Anatujaribu kwa mateso ili kuona utulivu wetu. Bwana‘ngu

inafaa tuvumilie. Tukubali na tupokee lolote lile

linaloporomoshwa na Mungu juu ya maisha yetu. Yeye ndiye

anafahamu mabaya na mazuri.‖

―Mimi siwezi kuishi tena,‖ nilimwambia.

―Kwa nini?‖

―Ulimwengu si pahala pa kuishi.‖

―Unataka kwenda kuishi wapi?‖

―Ninataka kwenda kuishi mahali ambapo ninaweza kuishi bila

kufikiri na bila kujua kwamba ninaishi‖ (uk. 180).

83

Majadiliano haya yanabainisha kwa uwazi namna Kazimoto na Sabina

wanavyotofautiana kimtazamo kuhusu Mungu na namna ya kuzikabili changamoto

zao. Wakati Kazimoto anaonesha kuwa maisha hayana maana na kuamini kwamba

ulimwenguni si mahali pazuri na salama pa kuishi, Sabina kwa upande wake bado

anaweka matumaini yake kwa Mungu. Kama inavyoelezwa katika nadharia ya

Udhanaishi, Kazimoto haamini kuhusu uwepo wa Mungu, anayedaiwa kwamba

ndiye muumba wa ulimwengu, ambao kimsingi kwa yeye anaona kuwa haumjali.

Matokeo yanaonesha kuwa kutofautiana kwao kimtazamo ndiko kunakozidi

kumsukuma Kazimoto katika mchakato wa kujiua anaposema ―mimi siwezi kuishi

tena.‖ Kauli hii inaonesha kwamba Kazimoto haoni tena thamani na maana ya

maisha yake. Kinachoonekana ni kwamba, kwa wakati huu yuko katika msongo wa

mawazo kutokana na tukio la kufiwa na mtoto wake. Kwa wakati huu, hapaswi

kuendelea kubishana na kuachwa peke yake, bali anahitaji kupata msaada wa karibu

kutoka kwa wataalamu wa saikolojia na magonjwa ya akili wa namna ya kulikubali

tukio hilo. Anapodai kwamba anataka kwenda mahali ambako hataweza hata kufikiri

na kujua kama anaishi, anaonesha kwamba yuko katika mchakato wa kujiua.

4.2.2.6 Kazimoto Kuugua Ugonjwa wa Ajabu

Tukio lingine la mchakato wa kujiua kwa Kazimoto ni la kuambukizwa ugonjwa wa

ajabu, baada ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na msichana anayeitwa Pili. Tabia

ya umalaya wa msichana huyu inasababisha Kazimoto kuambukizwa ugonjwa wa

huo wa ajabu, na hivyo, kuharibu kizazi chake. Kazimoto anapobaini kwamba tatizo

hili ndilo chanzo cha kifo cha mtoto wake, na kuzaliwa akiwa na kichwa kikubwa,

anakata tamaa ya maisha. Anapatwa na msongo wa mawazo unaomtesa sana na,

hatimaye, anaamua kujiua ili asiendelee kuzaa kizazi kibaya kama anavyoeleza

mwenyewe katika ujumbe anaouacha kabla ya tukio la kujiua kwake (uk. 195).

Ifahamike kwamba, Kazimoto na Pili wamekuwa katika mahusiano hayo kabla na

hata baada ya Kazimoto kufunga ndoa na Sabina. Hata hivyo, kwa muda wote huo,

Kazimoto hakujua kama ameambukizwa ugonjwa wa ajabu, hadi alipomwona mtoto

mwenye kichwa kikubwa katika familia ya Manase na Salima. Hatimaye, inabainika

kwamba familia hiyo pia, ina majonzi na masikitiko kutokana na kupata mtoto

mwenye kichwa kikubwa. Hii ni baada ya Manase kumwambukiza mke wake

ugonjwa huo wa ajabu alioupata kwa malaya, Pili. Jambo hili linampa msukumo

84

Kazimoto naye kumweleza Manase kinagaubaga kuwa, amekuwa katika mahusiano

ya kimapenzi na Pili, kabla na hata baada ya ndoa. Anaongeza kuwa, pamoja na yote

hayo, bado yeye na mke wake hawajisikii kuumwa chochote, kama ielezwavyo:

Manase alieleza kwamba ugonjwa huo ulikuwa hauwezi

kutambulika kwa urahisi. Alisema kwamba ugonjwa huo

unaingia ndani ya damu na kukaa bila kumdhuru mhusika.

Baada ya miaka kumi na minne hivi au zaidi unaanza

kumdhuru mhusika, lakini kabla yake ni vigumu kuusikia (uk.

192).

Maelezo haya yanasababisha Kazimoto kupata majonzi. Hii ni baada ya kuambiwa

kwamba ugonjwa huo huwa unaharibu kizazi kimoja hadi kingine. Pia, anakatishwa

tamaa zaidi anapoambiwa kuwa, daktari mwenye uwezo wa kutibu ugonjwa huo,

alifariki wiki moja tu iliyopita na hakuna mwingine wa kumsaidia. Yafuatayo ni

majadiliano baina ya Kazimoto na Manase:

―Daktari huyo alikupa dawa?‖ nilimuuliza.

―Ndiyo, alinipa.‖

―Ninaweza kumwona hata mimi?‖

―Bahati mbaya sana, Kazimoto, huyo daktari alikufa juma

lililopita, na watu waliopelekwa kusafisha nyumba yake ili

mwingine aingie walichoma vidonge vyote hivyo bila

kufahamu. Sasa hapatikani tena daktari ye yote.‖

―Wewe mwenyewe hukubakiza vidonge fulani?‖

―Bahati mbaya sana, Kazimoto, vyote vimekwisha.‖

Tulinyamaza kwa muda.

"Kazimoto,‖ Manase aliniita.

―Manase,‖ nilimwitikia.

―Maisha yangu yamekuwa magumu sana. Siwezi kutoka nje

ya nyumba hii isipokuwa wakati wa kazi. Nilikuwa nataka

kununua gari jipya lakini mke wangu amenizuia. Amesema

hataki kuona gari la kuchukulia malaya nyumbani kwake. Gari

lililolala hapo nje halikuharibika lenyewe. Lilichomwa na mke

wangu.‖

―Mimi maisha yangu yamekuwa magumu zaidi; dawa…

dawa,‖ nilimwambia (kur. 192 - 193).

Kinachobainika katika majadiliano haya ni kwamba wote wawili, Manase na

Kazimoto, wako katika msongo wa mawazo, kutokana na tukio hilo la

kuambukizwa ugonjwa wa ajabu. Tatizo hili linazidi kumweka Kazimoto katika

mchakato wa kujiua, kwani licha ya kusababisha mtoto wake kufa, hata huyo daktari

wa kumtibu anakosekana. Mtazamo wa Manase kuhusu kizazi chao kijacho kwamba

85

ni cha watoto wenye vichwa vikubwa, unazidi kumkatisha tamaa Kazimoto. Kwa

mantiki hiyo, haoni tena sababu ya kuendelea kuishi. Majadiliano yao ni kama

ifuatavyo:

―Unafikiri nini juu ya kizazi kijacho?‖ nilimuuliza.

Manase aliinama. Alifikiri. Halafu aliinua kichwa chake.

―Sijui,‖ alisema, ―lakini naona watoto wetu wanakuja na

vichwa vikubwa. Sijui kunaweza kuwa na nini ndani ya

vichwa hivyo.‖ Manase alitingisha kichwa chake kwa huzuni.

―Hata mimi naogopa,‖ nilisema.

Tulinyamaza kwa muda kila mmoja kati yetu akitazama

sakafuni.

―Kazimoto,‖ aliniita.

―Manase,‖ nilimwitikia.

―Kamwone mke wako, nami nikamwone wangu. Ulimwengu

unaozea mikononi mwetu. Mikono yangu naiona michafu‖

(uk. 193).

Mazungumzo haya yanaonesha kwamba Kazimoto hayuko tayari kuendelea kupata

aibu kwa kuzaa watoto wenye vichwa vikubwa. Dalili za kujitenga na ulimwengu

zinajitokeza anapomwambia Manase kwamba kila mmoja aende akamwone mke

wake. Ujumbe tunaoupata hapa ni kwamba Kazimoto anataka kila mmoja awe tayari

kuibeba aibu inayomkabili, inayotokana na tabia yake ya umalaya na kuambukiza

vizazi vyao ugonjwa wa ajabu. Tukio hili linamzamisha katika fikra kuhusu maana

ya maisha. Kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi, anakata tamaa kwa

kukengeuka misingi ya jamii na kujitenga. Haya yanamwingiza katika mchakato wa

kujiua kwake kwa kuona kwamba ulimwengu unamwozea katika mikono yake

michafu kutokana na uovu wake.

4.2.2.7 Kujitenga Kijamii

Kujitenga kijamii ni hali nyingine ya mchakato wa kujiua kwa Kazimoto. Jambo hili

linaanza kujitokeza akiwa nyumbani kwa Manase. Hii ni baada ya kubaini kwamba

tabia yake ya umalaya ya kutembea na wasichana wengi akiwamo Pili, ndicho

chanzo cha kifo cha mtoto wake. Kujitenga huko kunamwingiza zaidi katika

mchakato wa kujiua kwa sababu anaanza kuishi maisha ya upweke, tofauti na maisha

yake ya kawaida aliyoyazoea. Hivyo, anaamua kukaa kimya na kujitenga na Sabina

muda wote wakiwa safarini. Tabia hii inaendelea hadi wanapofika nyumbani kwao.

Mambo haya yanathibitishwa kupitia kwa Kazimoto mwenyewe, anaposema:

86

Njiani sikuzungumza na Sabina maneno mengi. Kila mmoja

alikuwa akiwaza yake. Tulipofika shuleni tuliomba ufunguo

wa nyumba yetu kutoka kwa mwalimu aliyekuwa akitutunzia

nyumba. Tulifungua na kuingia ndani kimya kama kwamba

tulikuwa tukiingia kaburini. Nyumba ilionekana kuwa tofauti

kabisa. Tulipoingia ndani tulikaa juu ya kochi, kupumzika

kidogo. Tulikaa kimya. Tukawa tunaogopa kutazamana (uk.

194).

Utafiti umebaini kuwa, kujitenga kwa Kazimoto kunamweka katika mchakato wa

kujiua kwa sababu ya kusongwa na mawazo mengi, ambayo hana namna ya

kuyatatua. Mjadala anaouanzisha baina yake na Sabina baada ya kimya cha muda

mrefu, ndio unaoonesha kwamba kujitenga huko kunamsukuma katika mchakato wa

kujiua kwake kutokana na kukata tamaa ya maisha. Hali hiyo kama inavyofafanuliwa

katika nadharia ya Udhanaishi, ndiyo inayosababisha akengeuke misingi ya jamii

yake kwani anazama katika fikra nzito juu ya dhana ya maisha. Majadiliano

yafuatayo yanathibitisha jambo hili:

―Mke wangu,‖ nilimwita.

―Bwanangu,‖ aliitikia.

―Sijui kwa nini ninaishi.‖

―Nimechoka na maswali yako ya kijinga,‖ alisema.

―Huwezi kuishi kama watu wengine?‖ Wewe nani?‖

―Mimi sijijui,‖ nilimwambia.

―Hakika sikufahamu kwamba wewe ni kichwamaji namna hii!

Sikufahamu! (kur. 194 - 195).

Dondoo hili linaonesha dhahiri kwamba Kazimoto yuko katika mgongano wa

mawazo, ambapo haoni sababu ya kuendelea kuishi. Hata hivyo, kutokana na

kukosekana kwa elimu ya saikolojia, imebainika kuwa mtu anayemweleza matatizo

yake haelewi na hamsaidii, bali anamwita Kichwamaji, yaani mtu asiyekuwa na akili

au kichwa wazi, huku akiendelea kulia hadi macho yake kuwa mekundu na kuamua

kwenda kulala. Matokeo yake ni kwamba kitendo cha kumwacha Kazimoto peke

yake, kinamwongezea upweke na mwanya wa kuendelea kufikiria kuhusu maisha na

kuzidi kujitenga nayo. Kazimoto mwenyewe anasema:

―Nilisimama pale dirishani kwa muda mrefu nikifikiri.

Nilifikiri furaha; ilikuwa imetawaliwa sana na huzuni. Salima

ambaye siku moja alitwambia kwamba kwa jambo lile alikuwa

haoni tofauti yetu na ng‘ombe, yeye mwenyewe hana raha

sasa. Wakati nilipokuwa nikifikiri juu ya maisha nilisikia kitu

fulani kama sauti ikiniita‖ ―Kazimoto!‖ Sauti ilisikika

87

polepole. ―Naam,‖ nilijibu kimoyomoyo. Nilikwenda ndani ya

chumba cha kulala. Sabina alikuwa amejifunika shuka akilia

kwa kwikwi. Nilichukua kitu fulani. Nilikuwa sifahamu jambo

nililokuwa ninafanya, isipokuwa nguvu fulani zilikuwa

zikiniongoza – sauti! Sauti! (uk. 195).

Kinachobainishwa katika tasinifu hii ni kwamba mtu anayepanga kujiua huwa katika

hali ya mtanziko. Husikia sauti ikimwita na kumhimiza kutekeleza kitendo cha

kujiua na kwamba kama atachelewa, basi watu wengine watakuja na kumuua kabla

ya yeye mwenyewe kufanya hivyo. Sauti ya namna ndiyo inayomsukuma Kazimoto

kuingia katika mchakato wa kujiua kwake, kwani anaingia ndani na kuchukua silaha

pasipo kutambua tendo analokusudia kulifanya.

Wakati mchakato huu ukiendelea, Sabina akiwa amelala huku akilia kwa uchungu

kutokana na kauli ya mume wake kwamba haoni sababu ya kuendelea kuishi,

Kazimoto anaamua kuutumia mwanya huo kujiua kwa kujipiga risasi. Matokeo yake

ni kwamba Sabina anakuwa mtu wa kwanza kushuhudia kichwa cha mumewe

kikivuja damu, huku bastola ikiwa pembeni. Kikaratasi kidogo anachokiona juu ya

meza kinabainisha sababu ya kujiua kwake. Kilikuwa na ujumbe ufuatao:

Nimejiua. Siwezi kuendelea kuzaa kizazi kibaya. Pia sikuona

tofauti kati yangu na mdudu au mnyama. Akili! Akili! Akili ni

nini? Pia nikiwa duniani sikupata kukutana hata siku moja na

mtu anayeamini kwamba kuna Mungu. Watu wanaoogopa

kufa na kwenda motoni hao nimewaona, tena wengi sana. Mtu

ye yote asilaumiwe kwa kifo changu. Mimi, kabla ya kufa,

ninaungama mbele ya ulimwengu kwamba nilimwua mdogo

wangu ingawa sikumgusa (uk. 195).

Ujumbe huu ni uthibitisho tosha kwamba mara nyingi kujiua hakutokei ghafla, bali

ni mchakato ambao humtokea mhusika baada ya kukabiliwa na matukio mengi

maishani mwake. Mwandishi kupitia kwa mhusika wake Manase, anathibitisha suala

hili anaposema:

Ukweli ni kwamba sisi wanadamu tunakufa polepole. Watu

wengi wanafikiri kwamba kifo kinakuja mara moja. Hili ni

jambo la uongo. Tangu mwanadamu anapozaliwa anaanza

kufa polepole ingawa yeye anajiona yu sawa. Siku zake

zinakatwa moja moja. Kaburi ni hatua yetu ya mwisho.

Kazimoto, tunapoishi tunakufa polepole. Kwa hiyo, ―kufa ni

kuishi.‖ (uk. 186).

88

Kwa mujibu wa Kezilahabi, kufa na kuishi ni hali zinazoingiliana, kwani aliye hai

huenda pia amekufa. Kauli hii inalenga kuthibitisha kwamba kujiua siyo tukio la

ghafla, bali ni mchakato. Hii ni kwa sababu mtu anayepanga kujiua hudhamiria na

hufanya maandalizi kadhaa kabla ya kufikia uamuzi huo. Hata hivyo, kwa kuwa

mchakato huo hufanywa na mhusika mwenyewe kimya kimya, mara nyingi jamii

isikiapo kuwa mtu fulani amejiua, hulipokea suala hilo kwa mshtuko na huliona

kama ni tukio la ghafla. Hili linathibitishwa na mwandishi wa riwaya hii anaposema

kuwa ―Wengi waliosikia juu ya kifo cha Kazimoto walistuka sana‖ (uk. 195).

Matokeo yanaonesha kuwa, kujiua kwa Kazimoto kunatokana na kukata tamaa ya

maisha na kutotambua nafasi ya Mungu kama inavyoelezwa katika msingi wa pili wa

nadharia ya Udhanaishi. Anaondoka na msimamo walio nao wadhanaishi wanaokana

kuhusu uwapo wa Mungu kwa madai kwamba woga ndio unaowasukuma watu

kuamini kuhusu Mungu. Aidha, anaeleza kuwa hajaona watu wakiwa na imani ya

kweli kuhusu Mungu, bali waoga ndio wengi kwa sababu huogopa adhabu ya moto.

Utafiti huu, basi, umebaini kwamba kujiua kwa Kazimoto kunatokana na mchakato

wa matukio mbalimbali anayoyapitia katika maisha yake. Matukio hayo ndiyo

yanayompa msongo wa mawazo na kusababisha akate tamaa kwa kuona kwamba

maisha kwake hayana maana tena. Hatimaye, anaamua kujiua kama suluhisho la

matatizo na taabu nyingi alizozipitia katika maisha yake.

4.2.3 Muhtasari wa Riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo

Dunia Uwanja wa Fujo (1975) ni riwaya ya tatu ya Euphrase Kezilahabi katika

mfululizo wa kazi zake. Ilichapishwa mwaka 1975. Riwaya hii pia, imetumika katika

utafiti huu kwa kumpatia mtafiti data za msingi. Kwa kiasi fulani, inaendeleza

mjadala kuhusu tatizo la maisha ya binadamu, maana yake, pamoja na kusudi lake,

mjadala unaoanza katika Kichwamaji (Mbatiah, 1998). Mulokozi (1983) anafafanua

kuwa katika riwaya hii mwandishi analitazama tatizo la maisha kwa viwango viwili.

Mosi, kwa kiwango cha jamii. Katika kiwango hiki, anashughulikia tatizo la maisha

katika ngazi tatu, yaani, ngazi ya familia, ngazi ya kijiji na ngazi ya taifa. Pili, kwa

kiwango cha mtu binafsi. Hapa anabainisha kuwa mara nyingi kanuni na miiko ya

jamii huweza kumfunga mtu binafsi na hata kuingilia uhuru na matamanio yake.

89

Riwaya hii, kwa kiasi kikubwa, inasimulia na kueleza kuhusu maisha ya mhusika

mkuu, Tumaini, tangu akiwa mtoto hadi kuuawa kwake. Mulokozi (k.h.j) anadokeza

kuwa matendo na tabia ya Tumaini inatokana na sababu kuu tatu. Mosi, malezi

mabaya. Huyu ni mtoto pekee katika familia ya Kapinga na Muyango, anayelelewa

kwa kudekezwa na kuengwaengwa. Pili, urithi mkubwa wa shilingi elfu hamsini

anaoachiwa na wazazi wake. Hela hiyo anaitumia kwa anasa na uasherati. Tatu, aibu

inayotokana na wazazi wake kugeuzwa vizuu kutokana na uchawi wa Mugala. Kama

ilivyo kwa riwaya nyingine zilizotangulia, mhusika mkuu, Tumaini, amejengwa na

wahusika wengine wanaosaidia kusogeza mbele dhamira za mwandishi katika

kufanikisha maudhui yake. Riwaya hii inabainisha kuwa maisha ya mwanadamu ni

vurumai inayotokana na mwanadamu huyo kuitafuta furaha maishani mwake.

Vurumai hizi, kwa kifupi, huletwa ulimwenguni na watu fulani, ambao, hujitokeza

katika nyakati mbalimbali za historia ya maisha ya binadamu huyo.

Aidha, imebainika kuwa katika riwaya hii mwandishi anaishughulikia na kuibua

migogoro, matatizo, pamoja na mikinzano mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na hata

ya kifalsafa katika jamii ya Tanzania, hususani, baada ya kutangazwa kwa Azimio la

Arusha. Pia, anaisawiria taswira ya maisha ya mwanadamu kama kiumbe kilicho

dhaifu na kisichoweza kuudhibiti ulimwengu wake, kuufanya ukitumikie na

kumletea furaha katika maisha yake. Matokeo yanaonesha kuwa jitihada za Tumaini

kuisaka furaha hiyo zinashindikana kutokana na kuandamwa na matukio na

mitanziko kadha wa kadha kuhusu mali na mashamba yake, ambayo sasa yanatakiwa

kutaifishwa. Kitendo hicho kinamkatisha tamaa. Hivyo, anaamua kumuua Mkuu wa

Wilaya akiwa mkutanoni akiwahutubia wananchi. Hata hivyo, nguvu ya dola

inafanikiwa kumtia Tumaini hatiani. Hatimaye, naye anauawa kwa kunyongwa

kutokana na kosa hilo la mauaji. Yafuatayo ni matukio ya mchakato wa kujiua

yanayosawiriwa katika riwaya hii: matukio ya aibu na fedheha, na tukio la Tumaini

kumuua Mkuu wa Wilaya.

4.2.3.1 Matukio ya Aibu na Fedheha

Matokeo yanaonesha kuwa, chanzo kimojawapo cha mchakato wa kujiua ni matukio

ya aibu na fedheha yanayompata mhusika au jamii yake. Mhusika au watu wake wa

karibu huamua kujiua ili kukwepa aibu, dharau na fedheha kutokana na kushindwa

kufanya au kutimiza jambo binafsi au la kijamii. Katika riwaya hii, tukio mojawapo

90

la aibu na fedheha linamhusu Kapinga. Hili linasababishwa na kitendo chake cha

kukosa nguvu za kufanya tendo la ndoa kwa takribani siku tatu, mara tu baada ya

kufunga harusi yake. Aibu na fedheha hii haimpati yeye peke yake, bali inawapata

pia, wazazi wake. Tukio hili linasababisha mama yake mzazi kushindwa kuvumilia

aibu hiyo kwa sababu ya umati mkubwa wa watu kumzomea, huku Kapinga

akiendelea kuhangaika ndani. Ili kuikwepa aibu hii, mama yake anaamua kuchukua

uamuzi wa kutaka kujiua, lakini anashikwa na kuokolewa. Mwandishi anasema:

―… Kapinga alikata tamaa. Alitoka nje kwenda kumwambia

kaka yake kwamba alishindwa. Rudi tena! Kaka yake

alimsukumia ndani ya nyumba kwa ghadhabu. Kapinga alirudi

ndani. Alijaribu tena lakini hakuweza. Usiku huo ngoma

hazikuchezwa, kwani arusi ilikuwa bado kuthibitishwa kwa

kitendo.‖ Kesho yake watu walikuwa wakiwazomea wazazi

wake. ―Mama yake nusura ajiue kama asingalishikwa‖ (uk.

10).

Kinachobainika katika dondoo hili ni kwamba tukio la kutaka kujiua kwa mama yake

Kapinga, halitokei ghafla, bali ni mchakato unaomtokea baada ya kuvumilia kwa

muda mrefu. Kutokana na hilo, anaamua kukata tamaa baada ya kubaini kwamba

Kapinga mwenyewe amekata tamaa na kukiri kwamba jambo hilo ni gumu kwake na

hawezi kufanikiwa. Hata jitihada zinazofanywa na bibi arusi za kuvunja sheria za

jamii yake ili kumsaidia Kapinga kwa kuhofia suala la usalama wa ndoa yake,

zinashindikana. Mwandishi anaeleza kwamba:

Alijitahidi kumsaidia bwana wake. Akiwa amevaa shanga

nyingi sana kiunoni, alimchomachoma Kapinga kwa matiti

kifuani; alimtekenya tumboni, mgongoni na kisogoni lakini

Kapinga alikuwa baridi, alikuwa akiguna tu. Bibi arusi

alitokwa na machozi. ―Kapinga! Kapinga kweli nirudi kwetu!‖

Alilia. Kapinga ingawa jasho lilikuwa limemtoka, alishindwa.

Alinyang‘anywa mwanamke. Kesho yake bibi arusi alirudi

kwao. Kapinga aliaibisha kijiji kizima (uk. 10).

Dondoo hili linaonesha kwamba kukatishwa tamaa huko hakutokei kwa Kapinga na

ndugu zake peke yao, bali hata mke wake anakumbwa na jambo hili. Ama kweli

sikio la kufa halisikii dawa, na kisicho riziki hakiliki, kwani licha ya mwanamke

huyo kumpa vionjo na manjonjo yote, Kapinga anashindwa kutimiza jukumu lake.

Hivyo, mama yake naye anaamua kukata tamaa kwa kutaka kujiua ili kuikwepa aibu

91

na fedheha hiyo. Furaha ya kumpokea mwali wake inapotea, kwani kabla ya kufikia

maamuzi ya kutaka kujiua inaelezwa hivi:

―… siku ambayo Kapinga alimleta bibi arusi nyumbani kwa

shangwe kubwa, vijana na wageni wengi walikuwapo. Kimila,

usiku ulipowadia, Kapinga aliambiwa kuingia ndani ya

nyumba baada ya bibi arusi kuoshwa vizuri na kupakwa

mafuta. Kapinga alipofika kitandani alimkuta bibi – arusi

tayari kwa ajili yake – amejifunika kanga moja (kur. 9 - 10).

Tunachokibaini ni kwamba ujio wa bibi arusi huyu unampa furaha ya muda mfupi

mama yake Kapinga, lakini furaha hiyo inageuka na kuwa majonzi na masikitiko

kutokana na Kapinga kushindwa kufanya tendo la ndoa. Jamii yake inapomcheka na

kumzomea, inachochea na kumpa msukumo mama yake kukata tamaa na kutaka

kujiua kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi. Kwa msingi huo, matukio

ya aibu na fedheha ni chanzo kimojawapo cha mchakato wa kujiua kama

inavyotokea kwa mama yake Kapinga.

Tukio lingine la aibu na fedheha ni la mwanasiasa kumwaibisha na kumvunjia

heshima Tumaini mbele za watu mkutanoni. Katika hali ya kawaida, kila mtu

anastahili kuheshimiwa na kuthaminiwa utu wake. Tukio la kumsema vibaya

Tumaini hadharani linalofanywa na mwanasiasa huyo, linamkasirisha sana Tumaini

na linamjengea chuki inayomsukuma na kumchochea kuingia katika mchakato wa

kujiua. Mwanasiasa huyo, kupitia kalamu ya mwandishi, anasema:

―… lakini wanyonyaji wapo. Kwa mfano, mnamwona huyu!

Ebu simama Bwana watu wakuone!‖ Tumaini alisimama na

watu walimzomea. Mwanasiasa aliendelea, ―haya ndiyo

manyonyaji haya!‖ Watu walimcheka na kumzomea. Tumaini

alikaa (uk. 117).

Kitendo cha kudhalilishwa na kuitwa mnyonyaji, siyo tu kwamba kinasababisha

Tumaini kuchekwa na kuzomewa na watu, bali pia kinamvunjia heshima, utu na

thamani yake katika jamii. Ifahamike kwamba utajiri wake haukutokana na

kuwanyonya watu kama anavyodai mwanasiasa huyo, bali unatokana na jitihada

zake za kufanya kazi kwa bidii baada ya kuanzisha mashamba makubwa. Kutokana

na kudhalilishwa huko, Tumaini haoni tena faida ya kuendelea kupambana na

kufanya kazi kwa bidii, badala yake anakata tamaa kwa kusongwa na mawazo

mengi. Mwandishi anasema:

92

Tumaini aliporudi nyumbani kichwa kilikuwa kikimwanga

kwa sababu ya mambo yaliyotokea kwake mkutanoni.

Tumaini alijiona mtu mkubwa; na maneno ya mwanasiasa

kuhusu kitambi chake yalimuudhi sana. Aliona udhia sana

kuambiwa maneno kama hayo mbele ya wafanyakazi wake wa

shambani na mbele ya watu waliokuwa wakimheshimu na

kumwita mzee. Hakuona kwa nini mwanasiasa yule

alimchagua yeye tu kati ya watu wote wenye vitambi

waliokuwako mkutanoni (uk. 119).

Mwandishi anaeleza namna Tumaini alivyosongwa na mawazo mara tu baada ya

kurudi nyumbani kwake, akitokea mkutanoni. Kitendo cha kudhalilishwa mbele ya

wafanyakazi wake pamoja na watu wengine mkutanoni, kinamfanya akate tamaa ya

maisha. Mchakato wa kujiua kwake unaongezeka akiwa chumbani kwake, kwani

anakosa usingizi na kubaki akizungukazunguka, huku mawazo yakimzunguka

kichwani mwake. Tumaini, kupitia kalamu ya wandishi, anasema:

―Siwezi kutukanwa na mwanasiasa anayetegemea kura yangu!

Haiwezekani! Kuniambia mimi, ―Mnaliona hilo; haya ndiyo

manyonyaji haya!‖ Mimi Tumaini! Mimi sikumkataza

kunenepa! Na hata hivyo ninakula jasho langu. Tabu

niliyopata zamani imenifunza jinsi ya kutafuta pesa. Nilikata

shauri kufanya kazi; nikawa nashinda shambani asubuhi na

jioni. Na sasa nimepata mali. Halafu huyu mwanasiasa

ananiita mnyonyaji! Mali niliyoisumbukia mwenyewe wakati

watu wengine wanashinda kwenye kangara! Haiwezekani!

Potelea mbali vijiji vyao vya ujamaa ambavyo vimerudisha

nyuma maendeleo ya watu wengi. Haiwezekani!‖ (uk. 120).

Kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi, Tumaini anakosa furaha na

anakata tamaa ya maisha kwa kuyaona kuwa hayana maana yoyote. Ithibati ya hali

hiyo ni kauli yake kwamba: ―Haiwezekani! Potelea mbali vijiji vyao vya ujamaa,

ambavyo vimerudisha nyuma maendeleo ya watu wengi. Haiwezekani!‖ Kauli hiyo

inaonesha kuna kitu anakusudia kufanya kutokana na msongo wa mawazo alio nao.

Kitu hicho, kwa muktadha wa tasinifu yetu, ni mchakato wa kujiua kwake au

kuhatarisha maisha ya huyo aliyemtia aibu na fedheha.

4.2.3.2 Tukio la Tumaini Kumuua Mkuu wa Wilaya

Tukio lingine la mchakato wa kujiua linatokana na kitendo cha Tumaini kumuua

Mkuu wa Wilaya. Tukio hilo nalo halitokei ghafla, bali linaambatana na matukio

kadhaa anayoyapitia Tumaini, yanayomkatisha tamaa na kumsababishia msongo wa

93

mawazo. Tukio hili linatokea mara tu baada ya kupokea barua kutoka kwa Mkuu wa

Wilaya, ikidai kwamba Serikali imetaifisha mashamba yake yote ili kujenga kijiji

cha Ujamaa. Jambo hili linamuumiza na kumkatisha tamaa. Mazungumzo baina yake

na mke wake, mama Bahati, ni uthibitisho wa jambo hili:

―Mama Bahati, hawa wanasiasa wanajua sasa kuwatania

wenzao. Eti wananiambia nijiunge nao! Eti baada ya kuchukua

mashamba yangu nijiunge nao! Siyo utani huo kitu gani?‖ …

mimi naona afadhali tuonyeshane nao. Watashinda. Lakini

nitakuwa nimewafunza somo.

―Somo gani?‖ Aliuliza mama Bahati.

―Kwamba Ujamaa ni ndoto!‖ Alijibu Tumaini kwa haraka na

kwa msisitizo (kur. 126 - 127).

Hapa dalili za wazi za mchakato wa kujiua kwa Tumaini zinajidhihirisha. Ukweli

wake ni kwamba anapanga kupambana na nguvu ya dola, huku akitambua dhahiri

kuwa, hana uwezo huo. Hata hivyo, licha ya kuufahamu ukweli huo, bado anaamua

kumuua Mkuu wa Wilaya wakati akihutubia wananchi. Mwandishi anaelezea kuwa:

… kelele za watu zilikuwa hazijatulia mlio wa bunduki

uliposikika. Hapo hapo Mkuu wa Wilaya alitotoma chini

akaanguka. Mlio wa pili ulisikika pale pale. Tumaini ambaye

alikuwa akijaribu kutoroka alianguka chini. … Askari

walimzunguka Tumaini. Akiwa amelala chini, mitutu kama

sita ya bunduki ilikuwa imelenga kichwa chake, akaambiwa

asijitingishe. Askari wengine walimbeba Mkuu wa Wilaya

upesi upesi, akaingizwa ndani ya gari kupelekwa hospitali (uk.

128).

Dondoo hili linabainisha namna Tumaini anavyokengeuka misingi ya jamii kwa

kukata tamaa na kusababisha kifo. Kama inavyoelezwa katika nadharia ya

Udhanaishi, anakumbwa na fadhaa, mashaka, pekecho na uchovu. Anaamini

kwamba, mwisho wa mwanadamu ni mauti. Kitendo anachokifanya ni uthibitisho wa

mchakato wa kujiua au kuuawa kwake. Hata hivyo, anakamatwa na askari mara tu

baada ya kutenda tukio hili wakati akitafuta mwanya wa kutoroka. Muda mfupi

baadaye, taarifa ya tukio la kuuawa kwa Mkuu wa Wilaya inasambaa na kusomwa

katika vyombo vya habari, huku ikieleza kwamba ameuawa na jambazi wakati

akihutubia wananchi kuhusu vijiji vya ujamaa, na kwamba, jambazi hilo

limekatamtwa.

94

Hatimaye, Tumaini anaamua kukiri kosa lake na kuhukumiwa kunyongwa baada ya

mwaka mmoja. Hata hivyo, kabla ya kufanyiwa kitendo hicho, anaelekeza lawama

zake kwa Dennis kwa madai kwamba ushauri wake wa kumtaka afanye kazi kwa

bidii, ndio uliosababisha aingie katika matatizo hayo. Anayasema haya mara tu,

baada ya kutembelewa na Dennis huko gerezani, wakati akisubiria kunyongwa:

―Dennis, unayakumbuka maneno uliyoniambia siku ya kwanza

tulipokutana hapa Shinyanga?‖

―Sikumbuki vizuri. Zamani sana.‖ Dennis alisema.

―Muda mrefu umepita. Lakini nitakukumbusha. Ulisema

kwamba dunia uwanja wa fujo, kwamba kila mtu lazima

atumie kichwa chake ajitahidi, afanye kazi kwa bidi ili apate

kujiendeleza.‖

―Ninayakumbuka sana maneno hayo,‖ Dennis alisema.

―Mimi nimefanya fujo hiyo: nimeweza kuwa tajiri. Lakini sasa

niko wapi?‖ … Dennis, sasa nitazame. Nitakufa kama

ng‘ombe. Nitatupwa pembeni kama gunia zee niliwe na

mchwa.‖ … Mimi nilifuata maoni yako. Nilikuwa tajiri.

Lakini kwa utajiri nilioupata nimelazimika kuua. Sikuweza

kuvumilia.

―Lakini hukulazimika kuua, Tumaini! Kwa nini uliua!‖

―Mali yangu, Dennis. Mali ambayo kwa muda mrefu

nilisumbukia… Ulikuwa wakati mbaya kwangu, Dennis.

Wakati nilipokuwa tu naanza kuchanua. Sikuweza kuvumilia

kukatwa kama ua la njiani lichumwavyo na msafiri

asiyejulikana‖ (kur. 129 - 130).

Ifahamike kwamba, Dennis alipomwambia Tumaini kuwa dunia uwanja wa fujo,

alimaanisha kwamba, kila mtu lazima atumie kichwa chake na ajitahidi kufanya kazi

kwa bidii ili apate kujiendeleza. Hata hivyo, Tumaini anapofanya jitihada za kutafuta

mali kwa bidii na kutajirika, anakutana na vikwazo vya jamii, kwani anashindwa

kutambua kwamba mtu hupata utu wake awapo katika jamii. Matokeo yake, kanuni

za jamii zinamfunga na kuingilia matakwa yake na shughuli zake za kujinufaisha,

kujiendeleza na kujitafutia furaha. Ndiyo maana, Dennis anamwambia Tumaini

kwamba hakupaswa kuua, bali kuvumilia. Hii ni kwa sababu anaishi katika jamii,

ambapo nguvu za mtu binafsi mara zote huwa haziwezi kushindana na nguvu za

jamii. Salamu anazompa Dennis kumpelekea mke na watoto wake ni uthibitisho

kwamba anakifurahia kifo chake. Anasema:

―Ukirudi. Waambie nitawakumbuka daima. Waambie

nitakufa. Lakini nitakufa kiume. Sitatoa hata chozi moja.

Waambie sina masikitiko kwa jambo nililolitenda. Nitakufa na

95

heshima yangu. Kama nilifanya kosa vizazi vitaamua (uk.

130).

Hivi ndivyo Tumaini alivyoingia katika mchakato wa kifo chake. Ni kweli katika

hali ya kawaida hakujiua kama ilivyotokea kwa Kazimoto na Rosa Mistika. Hata

hivyo, utafiti umebaini kwamba anapitia matukio yote ya mchakato wa kujiua kama

vile kukata tamaa, kupata msongo wa mawazo na kukubaliana na lolote linaloweza

kumtokea. Tunalithibitisha hili kutokana na kauli yake kwamba atakufa kiume,

hatatoa hata chozi moja, hana masikitiko kwa jambo alilotenda na kwamba atakufa

na heshima yake. Hivyo, kwa kuwa anajua madhara yatakayompata baada ya tukio la

kumuua Mkuu wa Wilaya, basi tunahitimisha kwamba Tumaini alijiua kwa sababu

alijisababishia kifo chake.

Kwa jumla, mjadala katika sehemu hii ulilenga kubainisha usawiri wa matukio

yanayounda mchakato wa kujiua katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi. Kabla

ya kubainisha matukio hayo, muhtasari wa riwaya teule umetolewa. Baada ya hapo,

ubainishaji wa matukio hayo umefanyika kwa mfuatano kwa kuanza na riwaya ya

Rosa Mistika, Kichwamaji, na Dunia Uwanja wa Fujo. Mjadala umebainisha

kwamba matukio yanayosawiriwa katika riwaya hizo, ndiyo yanayounda mchakato

wa kujiua kwa wahusika. Aidha, mjadala umeonesha kwamba wahusika hao kabla ya

kuchukua uamuzi wa kujiua kwao, wanapitia matukio na changamoto nyingi

zinazowakatisha tamaa ya maisha ambapo mwishowe wanachukua maamuzi ya

kujiua. Wahusika waliojadiliwa kwa kina ni Rosa Mistika, Kazimoto, mama yake

Kapinga na Tumaini.

Katika ubainishaji wa usawiri wa matukio hayo ya mchakato wa kujiua katika riwaya

hizo, mtafiti ameongozwa na nadharia ya Udhanaishi. Nadharia hii imemwongoza

katika kubainisha kwamba mtu hufikia uamuzi wa kujiua, kutokana na kukata tamaa

ya maisha kwa kuyaona kuwa hayana maana. Aidha, imemwongoza katika kueleza

kwamba binadamu hutafuta uhuru wake kwa kutetea ubinafsi wake; na hufikia hatua

ya juu kabisa ya ubinafsi huo, yaani kujiua. Hivyo, hulazimika kukengeuka misingi

na kanuni zinazoiongoza jamii ili kujitafutia uhuru huo.

Sehemu inayofuata inawasilisha data kuhusu sababu za mitanziko ya wahusika

zinazosawiriwa katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi.

96

4.3 Sababu za Mitanziko ya Wahusika katika Riwaya Teule za Euphrase

Kezilahabi

Sehemu hii inajadili sababu za mitanziko ya wahusika zinazosawiriwa katika riwaya

teule za Euphrase Kezilahabi. Sababu hizo zimegawanywa katika makundi makuu

manne, ambayo ni sababu za kijamii, kiutamaduni, kiuchumi na kifalsafa. Mwisho,

kuna sehemu inayotoa muhtasari wa jumla kuhusiana na mjadala uliofanyika.

4.3.1 Sababu za Kijamii

Kulingana na TUKI (2014), jamii ni mkusanyiko wa vitu au watu wenye asili au

kitovu kimoja. Kwa kuwa Fasihi huwakilisha maisha, basi katika sehemu hii,

tunajadili sababu ambazo zina uhusiano wa moja kwa moja na maisha ya kila siku ya

jamii. Sababu hizo ni mahusiano ya kimapenzi na mfumo wa malezi.

4.3.1.1 Mahusiano ya Kimapenzi

Mahusiano ya kimapenzi ni sababu kubwa inayochangia watu wengi kuingia katika

mitanziko. Hali hii huwapata zaidi vijana ambao huwa katika rika la kubalehe,

ambapo hupitia changamoto mbalimbali za kimaisha. Wengi wao hujaribu kufanya

mambo mengi na makubwa ili kufikia matarajio na matamanio yao. Inapotokea kuwa

matarajio na matamanio hayo hayakufikiwa, huweza kukumbwa na msongo wa

mawazo, na hivyo, kujikuta katika hali ya kushindwa kuelewa nini kifanyike. Mara

nyingi, msongo huo wa mawazo huweza kusababisha mhusika kufikia hatua ya

kukata tamaa, na hata kuchukua uamuzi wa kujiua, hasa pale anapokosa ushauri na

miongozo sahihi. Kipengele hiki kinajikita katika mahusiano ya kimapenzi baina ya

mvulana na msichana.

Katika riwaya ya Rosa Mistika, suala la mahusiano ya kimapenzi linajitokeza kwa

kiasi kikubwa na linasababisha wahusika kuingia katika mitanziko ya kimaisha. Kwa

mfano, Rosa Mistika anajiingiza katika mtanziko wa mahusiano ya kimapenzi na

watu mbalimbali. Hatimaye, anaamua kujiua baada ya kukosa jibu sahihi juu ya

maisha yake. Mtanziko huo anaanza kuupata akiwa darasa la sita, mara tu baada ya

kuandikiwa barua ya mapenzi na Charles (uk.8). Barua yenyewe ni hii ifuatayo:

97

Namagondo,

P.O.Box Mpenzi,

Ukerewe.

Mpenzi Rosa Mistika

Ewe ua waridi lenye fumbo! Ewe dada wa makao yangu uliye

kitulizo changu! Fungua macho uone makala hii fupi ya

mapenzi. Nakuota kila siku wakati wa usiku, sipati usingizi

kwa ajili yako. Kuvumilia nimeshindwa. Tafadhali unijibu

upesi. Nakutakia ushindi mzuri katika mtihani wako.

Wako katika mapenzi na matumaini,

Charles Lusato.

Barua hii fupi na yenye maneno machache, imebeba ujumbe unaoibua na kuchochea

hisia, msisimko na fikra nzito ndani ya moyo wa Rosa Mistika, zinazomwingiza

katika mahusiano ya kimapenzi na Charles. Hata hivyo, mahusiano yenyewe

hayadumu, kwani yanaingia dosari mara tu baada ya Zakaria, baba yake Rosa, kupata

taarifa kuhusiana na barua hiyo. Zakaria hafanyi uchunguzi, badala yake, anampa

Rosa kipigo kikali kinachomfanya ajutie, ajilaumu na kujishuku kwa kuona kuwa

hapendwi, na hana usalama.

Utafiti umebaini kuwa kipigo hicho kinamsababishia Rosa mtanziko, ambapo

anatakiwa kuchagua ama kukubaliana na kutii sheria ngumu, kali, kandamizi na

zinazomnyima uhuru, kutoka kwa baba yake, ama kuzitupilia mbali na kuendelea na

mahusiano ya kimapenzi na Charles. Kukosekana kwa uhuru wa kujiamulia mambo

yake mwenyewe, kunamkatisha tamaa ya mapenzi na kumsababishia woga wa

maisha yake. Hali hiyo inasababisha amkasirikie na kumwogopa sana baba yake

pamoja na kuwakasirikia na kuwaogopa wavulana. Hatimaye, anaamua kumtii baba

yake, huku akiingiwa na chuki na kinyongo dhidi ya Charles na wanaume wengine

kwa jumla. Hivyo, kitendo cha Rosa kujiingiza katika mahusiano ya kimapenzi

kinachojidhihirisha ndani ya barua hii kinasababisha mtanziko kwake, kwani

kinampa wakati mgumu wa kufikiri uamuzi wa kuuchukua na kuufuata.

Pia, Rosa anapata mitanziko zaidi anapotoka katika sheria ngumu za kunyimwa

uhuru kutoka kwa Zakaria. Hii ni kwa sababu anakumbana na sheria nyingine ngumu

za masista katika shule ya Sekondari ya Rosary. Uvumilivu wake wa kuendelea

kufungwa katika minyororo hiyo ya ukandamizaji unamwishia na kuamua kujitafutia

uhuru wake binafsi. Matokeo yake ni kwamba anaanza kuiga tabia za wasichana

98

wenzake kwa kutoroka usiku na kwenda kucheza dansi. Msukumo huu anaupata

baada ya kuumizwa na maneno ya wavulana wawili wa shule ya sekondari ya Bwiru

wanaomjadili na kumwita kilema kwa sababu hana uhusiano na wavulana.

Mwandishi anasema:

Hata alipokuwa kitandani, maneno haya yaliendelea

kuzunguka kichwani mwake. Alikata shauri. Alikata shauri

kwenda kucheza dansi (uk. 30).

Imebainika kwamba msuguano wa mawazo anaoupata kuhusiana na suala hili la

mapenzi unamweka katika mtanziko, kwani anapata wakati mgumu wa kuamua

jambo lipi alifanye na lipi asilifanye.

Kitendo cha kuamua kwenda kucheza dansi kinamsababishia mtanziko, kwa kuwa

kinachangia sana katika mabadiliko yake kitabia. Pia, kinaibua hisia kali za mapenzi

anazozipata mara tu baada ya kucheza dansi na Deogratias. Tukio hili ndilo

linalosababisha aingie katika mgongano wa mawazo zaidi na kuanza kujiuliza

maswali yanayoumiza akili yake. Kupitia kwa mwandishi anasema:

Kama nikifanya urafiki na wavulana baba yangu atafahamu?

Yeye yuko Ukerewe, mimi niko Usukuma, baba anakaa

akinichunga anafikiri atanioa? (uk. 32).

Matokeo yanaonesha kuwa uamuzi anaouchukua wa kujiingiza na kuanza mapenzi

kwa madai kwamba baba yake yuko mbali na hamwoni, unampa wakati mgumu

zaidi anapobaini kwamba kunyimwa uhuru huko kumemcheleweshea mambo mazuri

ambayo hakuyafahamu kabla. Hivyo, anaamua kujiingiza katika bahari ya mapenzi

kwa pupa, pasipo kufanya maandalizi ya kutosha. Tabia na mwenendo wake sasa

vinatawaliwa na kukumbwa na nguvu ya mazingira yake mapya, tofauti na yale

aliyoyazoea. Mbatiah (1998) anaeleza kuwa Rosa anaamua kutumbukia katika bahari

iliyochafuka ya mapenzi bila kujua kuogelea. Haya yanajitokeza akiwa katika shule

ya Rosary. Mwandishi anasema:

Rosa sasa alianza mapenzi. Alianza mapenzi lakini aliyaendea

haraka sana kama mbwa aliyekata kamba. Aliona mvulana

mmoja au wawili hawamtoshi kwa urafiki. Mwaka huo huo

aliwakubalia wavulana watano (uk. 33).

99

Kutokana na dondoo hili tumebaini kwamba, uhuru anaojitafutia anautumia vibaya

na unamzamisha katika bahari ya mapenzi, ambayo haikati na wala haimalizi hamu

yake ya mapenzi. Kitendo cha kucheza dansi na kukumbatiana na Deogratias

kinamwamshia hisia kali za mapenzi zinazomweka katika mtanziko. Hali hiyo

inamfanya ashindwe kupata jibu sahihi la mtu, yaani mwanaume wa kuweza

kumaliza na kutatua tatizo lake. Badala yake, anavunja maadili ya jamii yake na

kwenda kwa msichana mwenzake, Thereza, na kutaka kumbaka. Mwandishi

analithibitisha jambo hili anaposema:

… Thereza alikuwa bado hajaelewa Rosa alipomrukia na

kumkumbatia. Waliangushana kitandani. Rosa alianza

kumbusu, lakini tamaa yake haikuweza kupungua. Rosa

alihitaji ule mkwaruzokwaruzo wa aina ya pekee.

Mkwaruzokwaruzo wa ndevu na manyoya ya tumboni. Zaidi

ya hayo, moto ulikuwa ukiwaka upande wa Kusini lakini wao

walikuwa wakizimisha upande wa Kaskazini (kur. 32 – 33).

Kitendo cha Rosa kwenda na kumparamia msichana mwenzake na kutaka kumaliza

hisia zake kinathibitisha kwamba yuko katika mtanziko. Ndiyo maana anashindwa

kupata jibu sahihi la uamuzi anaouchukua. Jambo hili linazidi kumtatiza na kumpa

wakati mgumu zaidi. Hii ni kwa sababu Thereza anashindwa kummalizia hamu na

hisia zake za mapenzi na kusababisha azidi kuchanganyikiwa. Yote haya yanampata

kutokana na kukengeuka misingi ya malezi na maadili aliyoyapata kutoka kwa

wazazi wake kwa kutafuta uhuru wake mwenyewe kama isemavyo nadharia ya

Udhanaishi. Uhuru huo ndio unaomwingiza katika mtanziko, kwani anaposhindwa

kutimiza na kumaliza hisia zake kwa Thereza, anaamua kufanya mapenzi na

wanaume wengi. Hata hivyo, bado hawamalizi kiu yake na kuzidi kumzamisha

katika bahari hiyo, ambayo kwa wakati huo, hajui urefu wa kina chake.

Kutokana na kuendekeza na kuendeleza tabia yake ya umalaya, mtanziko wa

mahusiano ya kimapenzi haumtokei akiwa katika shule ya Rosary pekee, bali hata

akiwa katika Chuo cha Ualimu Morogoro. Matokeo yanaonesha kuwa akiwa huko

pia, anajiingiza katika mahusino ya kimapenzi na watu wengi, akiwemo Mkuu wa

Chuo hicho, Bwana Thomas. Matokeo yake, Rosa anazidi kupatwa na masaibu ya

kimapenzi anapofumaniwa na mke wa Thomas, akiwa ndani ya nyumba ya Mkuu

huyo wa Chuo, huku akiwa katika ulimwengu wa mapenzi (uk. 54). Imebainika

kuwa tukio hili linazidi kumweka katika mtanziko zaidi anapoona kuwa, thamani

100

yake inazidi kupungua baada ya kuumizwa na mwanamke huyo, kwa kukatwa sikio

lake. Mwandishi anaeleza kuwa Rosa alilia na kulililia sikio lake kutokana na

maumivu makali aliyoyapata (uk. 55). Inaelezwa kwamba mambo mengi

yalimzunguka kichwani mwake, kiasi cha kusikia sauti hafifu sana kama ya mtu

anayekufa, ikimwita moyoni mwake. Sauti hiyo haisikiki kwa kila mtu, bali ni Rosa

peke yake ndiye anayeisikia na kuitambua. Matokeo yake, anajikuta katika wakati

mgumu wa kuamua jambo la kufanya, kutokana na mvutano na mvurugiko wa fikra

anaokabiliana nao. Mvutano na mvurugiko huo wa fikra, ndio unaosababisha

baadaye, afikie hatua ya kukata tamaa ya maisha na kukengeuka misingi ya malezi

aliyoipata kwa baba yake.

Sambamba na hilo, tumebaini kwamba baada ya kufanikiwa kuhitimu mafunzo yake

ya Ualimu huko Morogoro, Rosa anapangiwa kazi ya kufundisha katika shule ya

Msingi Nyakabungo, Mkoani Mwanza. Akiwa huko, anaamua kuachana na tabia ya

umalaya na kuchagua maisha ya ndoa, ili kupata utulivu wa maisha. Hatimaye,

anafanikiwa kumpata Charles Lusato, mpenzi wake wa zamani aliyesababisha

apigwe sana na baba yake, baada ya kumwandikia barua ya mapenzi akiwa darasa la

sita. Hata hivyo, anapopata matumaini mapya ya kuishi na kijana huyo, ndoto zake

zinapotea baada ya Charles kufichuliwa siri ya maisha ya umalaya wa Rosa.

Matokeo yake ni kwamba Charles anapobaini kuwa Rosa hana bikira, anamkataa na

anamwacha. Kitendo hicho cha kukataliwa kinamsababishia mtanziko, kwani

anapata ugumu wa kuamua jambo sahihi la kufanya. Hali hiyo inamkatisha tamaa ya

kuendelea kuishi na kufikia hatua ya kuchukua maamuzi ya kujiua huku akiacha

ujumbe unaoelekeza lawama zake kwa Charles, kwamba anajiua kwa ajili yake (uk.

93).

Hali hii inathibitisha kwamba kuvurugika kwa mahusiano kimapenzi huweza

kumsababishia mhusika mtanziko. Hali hiyo hutokea pale ambapo mhusika hujikuta

katika wakati mgumu wa kuamua jambo la kufanya kwa sababu uamuzi wowote

huwa na athari mbaya kwake. Kutokana na mitanziko hiyo, wahusika wengine

huweza hata kuchukua maamuzi ya kujiua. Hili ndilo linalomtokea Rosa, kwani

anafikia uamuzi huo baada ya kukata tamaa kwa kuona kwamba maisha hayana

maana tena kwake. Anapanga kuchukua uamuzi huo kama suluhisho la maisha yake

ili asiendelee kuumizwa tena na masuala ya mahusiano ya kimapenzi. Hii

101

inatudhihirishia kuwa, haoni sababu ya kuendelea kuishi, kama inavyoeleza adharia

ya Udhanaishi kwa sababu maisha yake yamekosa matumaini.

Vilevile, mtanziko unaotokana na mahusiano ya kimapenzi unajitokeza katika riwaya

ya Kichwamaji. Baadhi ya wahusika wanaokumbwa na mtanziko huo ni: Rukia,

Sabina, Kazimoto, Manase, Vumilia, na Moyokonde.

Utafiti umebaini kwamba Rukia anapatwa na mtanziko kwa kushindwa kujua hatima

ya maisha yake ya shule kutokana na vitendo vinavyohusiana na mapenzi,

anavyofanyiwa na Manase. Anazidi kutatizika anapobaini kwamba mahusiano hayo

yanamsababishia mimba pasipo matarajio yake. Barua anayomwandikia kaka yake,

Kazimoto, inaonesha wazi kwamba yuko katika mtanziko. Barua hiyo inasema:

Kaka mpendwa,

Moyo wangu siku hizi hauna raha. Lakini leo nimechukua

kalamu ili nikueleze mambo yote. Nimeona kwamba siwezi

kuwa nakuficha wewe mambo, hali mambo yenyewe sasa

hayawezi kufichika. Wewe ukiwa ndiye kaka yangu na ndiye

uliyenitafutia nafasi hii ya shule ninakupa heshima. Fahamu

kuwa mambo haya sijapata kumweleza mtu mwingine

isipokuwa wewe peke yako.

Kaka, uliponileta hapa nilikaa kwa raha kwa muda wa juma

moja tu. Baada ya juma hilo, niliona Manase anaanza

kunitazama kwa njia ya ajabu. Baada ya majuma mawili

mambo yalizidi kuwa mabaya, kwani nilipokuwa naoga siku

moja niliona jicho lake kwenye tundu la ufunguo. Mwishowe

aliniambia wazi alichokuwa anataka. Nilimwambia: Manase!

Kaka yangu akifahamu litakuwa jambo la aibu sana! Lakini

yeye alijibu kwamba wewe ni mwanamume kama yeye. Alifika

hatua ya kutumia nguvu! Na kweli alitumia nguvu bila utashi

wangu. Kaka, sitaki kukupotezea muda wako wa kujifunza kwa

kusoma barua ndefu. Mimi maisha yangu yameharibika. Shule

nimekwishaacha. Jambo ambalo limenisikitisha sana ni hili

lifuatalo: Jana usiku, Manase alirejea nyumbani mlevi.

Alikuwa na tikiti ya basi. Baada ya kunitukana kwa maneno

ambayo siwezi kukuandikia, alianza kupanga vitu vyangu

sandukuni. Leo atanisindikiza hadi kituo cha basi. Kaka,

machozi yananilengalenga, sijui nitasema nini kwa baba na

mama. Usifike kuja kuniaga kwenye kituo cha basi nisije

nikazimia.

Sina mengi,

Nduguyo,

Rukia Mafuru (kur. 19 - 20).

102

Barua hii inadhihirisha wazi kwamba masaibu anayoyapata Rukia katika maisha

yake, yanamsababishia mtanziko kutokana na kushindwa kupata majibu sahihi ya

mambo hayo. Uamuzi wake wa kumwandikia kaka yake barua, na maneno yaliyomo

ndani ya barua hiyo ni uthibitisho kwamba, uvumilivu wake wa kuendelea kuishi na

Manase umemwishia, na hayuko tayari tena kuendelea na shule. Udhaifu na uduni

wa maisha ya familia yake unakuwa chanzo cha kuingia katika mtego wa kuishi na

Manase na kumsababishia matatizo kwa kutiwa mimba, ambayo hakuitarajia. Tukio

hili, kama inavyoelezwa katika Udhanaishi, linasawiri picha halisi ya mwanadamu

ambaye ni kiumbe dhaifu kinachoishi maisha yasiyo na maana, katika ulimwengu

usio na maana.

Matokeo yake, anapata msongo wa mawazo unaomsababishia kifo chake kwa kukosa

nguvu za kusukuma mtoto wakati wa kujifungua. Hii ni baada ya kukaa muda mrefu

bila kula chakula kwa sababu ya mtanziko aliokuwa nao. Suala hili, kama

lilivyokwisha kujadiliwa katika kipengele cha 4.2.2.3 kinachohusu vifo vya Rukia na

mama yake hapo awali, linathibitishwa kupitia mazungumzo baina ya Tuza na

Kazimoto (uk. 83).

Hivyo, ni kweli kwamba Rukia anakufa kwa sababu ya mtanziko unaotokana na

kukosa mapenzi ya dhati kutoka kwa mtu aliyemtia mimba, yaani Manase. Uamuzi

wake wa kukataa kula kwa muda mrefu na kukosa nguvu za kusukuma mtoto wakati

wa kujifungua ni uthibitisho kwamba, haoni sababu ya kuendelea kuishi kutokana na

kuathiriwa na suala la mahusiano ya kimapenzi. Kwa hiyo, anachagua kufa kama

njia ya kuyakwepa matatizo hayo, kwa kuwa haoni tena sababu ya kuendelea kuishi.

Hivyo basi, matokeo ya utafiti yamebaini kuwa mahusiano ya kimapenzi ni sababu

mojawapo ya mtu kupata mtanziko, kwa kuwa humpa wakati mgumu wa kuamua la

kufanya pale anaposongwa na mawazo. Mtanziko huo wakati mwingine husababisha

mtu kuchukua maamuzi ya kujiua kutokana na kukata tamaa ya maisha kama

inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi.

Vilevile, mahusiano ya kimapenzi yanajitokeza kwa Sabina na yanamsababishia

mtanziko. Hii ni baada ya kudanganywa na mvulana aliyewekeana naye ahadi

kwamba wataoana. Suala hili linamweka katika wakati mgumu, kwani linasababisha

aonekane na kutazamwa tofauti na jamii yake. Miongoni mwa watu wenye mtazamo

103

tofauti dhidi yake ni Kazimoto. Huyu, anahoji sababu za Sabina kutopenda kuolewa,

licha ya uzuri alio nao. Hata hivyo, majibu ya Sabina yaliyojaa masikitiko, huzuni,

maumivu na majonzi aliyo nayo moyoni mwake, yanathibitisha mtanziko alionao juu

ya jambo hili. Anasema:

―Kazimoto,‖ alianza kuzungumza. ―Kama ungefahamu taabu

ambayo nimekwishapata usingeniambia vile. Mimi nimo

katika huzuni. Usifikiri kwamba mimi sipendi kuolewa au

kwamba mimi sipendi wanaume. Kazimoto, ni vigumu kupata

wanaume. Nilikuwa na mchumba wangu. Kijana huyo

nilimpenda kweli na nilimpa moyo wangu wote, lakini siku

moja niliona picha yake gazetini ameoa msichana mwingine.

Ninawaombea maisha mazuri. Nilipata kijana mwingine,

nilitaka kumfanya mchumba, lakini nilipokataa mambo

aliyokuwa akipenda, yeye alinitukana kwamba nilikuwa

sifahamu mapenzi na kwamba sikuwa mchangamfu. Tangu

siku hiyo sijapata kumwona tena kijana huyo (uk. 103).

Dondoo hili linaonesha kwamba suala la ulaghai na udanganyifu katika mapenzi

limekuwa likisababisha mitanziko kwa watu wengi. Sabina ni mfano mzuri wa watu

hao, kwani licha ya kuendelea na shughuli zake za kijamii za kila siku, maisha yake

yanatawaliwa na maumivu na huzuni kubwa kutokana na kushindwa kujua hatima ya

maisha yake.

Mtanziko mwingine wa mahusiano ya kimapezi unaomkumba Sabina unatokana na

kubanwa na misingi na kanuni za jamii yake, ambapo, licha ya kuwa na hamu ya

kutaka kuolewa, utamaduni haumpi nafasi ya kumtongoza mwanaume amtakaye.

Hali hii inamweka katika wakati mgumu, kwani anabaki akisubiria mtu aje

pasipokuwa na uhakika wa kumpata. Ushahidi wa hili unatokana na maelezo ya

Sabina mwenyewe, anayeeleza kuwa, endapo atatokea mwanamume ambaye

ataamua kuomba uchumba kwake, atampenda na kumheshimu sana. Hii inaonesha

wazi kuwa vikwazo vya kijamii vinamzuia kumtafuta mwanamume amtakaye, hivyo

kusubiri kudra za Mungu. Anasema:

―… Lakini naona kwamba siwezi kuishi bila mume. Nikipata

mchumba sasa sijui nitampendaje! Nitamng‘ang‘ania kufa na

kupona. Siku ya kuolewa nafikiri bwana wangu nitakuwa

namlisha kwa mikono yangu mwenyewe‖ (uk. 104).

104

Ni wazi kwamba, watu wengi katika jamii zetu wana mitanziko inayotokana na

mahusiano ya kimapenzi. Hali hiyo inapozidi, huweza kusababisha msongo wa

mawazo, ambapo wengine huweza hata kujiua kutokana na kukata tamaa ya maisha

kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi.

Tasinifu hii imebaini kwamba watu wengi wana mitanziko ya mahusiano ya

kimapenzi inayotokana na sababu na visingizio mbalimbali. Miongoni mwa sababu

au visingizio hivyo ni umri, msimamo wa kiimani, udanganyifu na kukata tamaa ya

maisha. Watu wa namna hii wanahitaji kufarijiwa na kupata ushauri wa kisaikolojia.

Kufanyika kwa mambo kama hayo kutawaondoa katika msongo wa mawazo, na hata

kujisikia kuwa wao pia, ni sehemu ya jamii.

Vilevile, matokeo ya utafiti yamebaini kuwapo kwa wahusika wengine

wanaokumbwa na mtanziko wa mahusiano ya kimapenzi katika riwaya hii ya

Kichwamaji. Wahusika hao ni pamoja na Kazimoto, Manase, Vumilia, na

Moyokonde. Kwa upande wa Kazimoto na Manase, pamoja na mambo mengine,

imebainika kuwa mtanziko wao pia, unatokana na wote wawili kuwa na mahusiano

ya kimapenzi na msichana malaya anayeitwa Pili, ambapo anawaambukiza ugonjwa

wa zinaa. Nao, Kazimoto na Manase, kutokana na tabia yao ya uzinzi na umalaya,

wanawaambukiza ugonjwa huo wake zao. Athari za ugonjwa huo zinasababisha

wake zao kuzaa watoto wenye vichwa vikubwa. Matokeo yake ni kwamba kila

mmoja wao anaingia katika mgogoro na mafarakano na mwenzi wake kwa

kusababisha janga hilo. Imebainika kuwa, hatimaye, mgogoro huo unasababisha

mtanziko kwa familia zote mbili, na unamsukuma Kazimoto kuamua kujiua kama

inavyoeleza nadharia ya Udhanaishi kutokana na kukata tamaa ya maisha.

Kuhusiana na familia ya Manase, matokeo yanaonesha kuwa, Salima, ambaye ni

mke wa Manase, anaamua kulichoma moto gari la Manase ili asiendelee kulitumia

katika masuala ya anasa. Vilevile, Manase anapotaka kununua gari jipya, Salima

hakubaliani na uamuzi huo. Hivyo, Manase anakuwa ni mtu wa kukaa ndani muda

wote kutokana na kukata tamaa ya maisha na kukosa majibu ya mambo

yanayomkabili (uk. 193). Hii inaonesha kwamba yuko katika mtanziko na unampa

wakati mgumu wa kujua maisha yake ya baadaye yatakavyokuwa. Imebainika

kwamba mara nyingi mtu akiwa katika hali kama hiyo, huweza hata kuchukua

105

maamuzi ya kujiua kutokana na kukata tamaa ya maisha kama ielezavyo katika

nadharia ya Udhanaishi.

Vilevile, mahusiano ya kimapenzi yanamsababishia Kazimoto mtanziko kutokana na

mtoto wake kufariki. Suala hili linaongeza simanzi na majonzi katika familia yake.

Tukio hili linamweka katika mtanziko, kwa sababu linamwingiza katika fikra nzito

na kumtafakarisha sana kuhusu maisha, pamoja na kizazi kijacho. Mahusiano ya

kimapenzi anayoyafanya na Pili na kumsababishia ugonjwa wa ajabu, ndiyo

yanayomzamisha katika mtanziko huu. Kwa kurejelea nadharia ya Udhanaishi,

imebainika kuwa hali hiyo ya mtanziko inamweka na kumzamisha katika dimbwi la

fikra, kwa sababu hajui maisha yake baadaye yatakavyokuwa. Hatimaye, anaamua

kujiua kwa madai kwamba haoni sababu ya kuendelea kuzaa kizazi kibaya (uk. 195).

Pia, kabla ya kujiua kwake anabainisha wazi kwamba, yeye ndiye aliyesababisha

kifo cha mdogo wake, Kalia, ingawa hakumgusa. Haya yanatokana na vitendo vyake

vya kujihusisha na masuala ya mapenzi, ambapo tabia yake hiyo inasababisha Kalia

kuuawa baada ya kuiga vitendo na tabia yake.

Aidha, Kazimoto anapata mtanziko mwingine unaotokana na mahusiano ya

kimapenzi baina yake na Sabina. Mtanziko huu unasababishwa na Mzee Fungameza

kutokana na kitendo chake cha kumshawishi Kazimoto kuachana na mpango wake

wa kumwoa Sabina kwa madai kwamba, jamii yake ina asili ya magonjwa na

uchawi. Suala hili linampa Kazimoto wakati mgumu wa kuamua hatima ya

mahusiano yake na Sabina, ikizingatiwa kwamba Mzee Fungameza ni baba mkubwa

wa Sabina. Anasema:

… ingawa Sabina ni jamaa yangu, bado ninaona kwamba

lisingekuwa jambo zuri wewe kumwoa… Sabina – nikwambie

mtoto wangu – ni tunda baya na nisingependa wewe ulile.

Tukitazama katika ukoo wao kwa makini, hasa jamii yao

utaona kwamba ulikuwa na sifa mbaya tangu zamani. Babu

yake wa pili – ninyi hamkumwona – alikuwa mgonjwa wa

ukoma. Alikufa bila vidole vya mikono na miguu. Nyanya

yake – nyinyi hamkumkuta anaishi – alikuwa mchawi wa

kustaajabisha. Alikufa macho mekundu kama umeme.

Ukimtazama vizuri Sabina utaona kwamba anaweza kurithi

mambo haya mawili. Ukitazama vizuri mwili wake, utaweza

kudadisi kwamba anaweza kupata ukoma katika miaka yake

ya uzee. Na hali ya unyamavu aliyonayo inaonyesha wazi

106

kwamba amekwishafahamu siri za watu wengi. Yaani siri za

usiku (kur. 146 - 147).

Katika dondoo hili, Mzee Fungameza, siyo tu kwamba anaisema vibaya jamii ya

Sabina kwa masuala ya uchawi na magonjwa, bali pia anamnasibisha Sabina na

masuala hayo. Kutokana na hilo, anazidi kumweka Kazimoto katika mtanziko

anapoelezea mambo yanayodaiwa kufanywa na Sabina akiwa Tabora. Anasema:

… huko Tabora, mtoto wangu, ndiko tunda lilikoozea. Jambo

huenda likakushangaza, Sabina aliwahi kuchukuliwa na

kutunzwa kama kimada. Akaishi na jambazi fulani kwa miaka

miwili. Lile jambazi baada ya kumtafuna, lilimwacha na kuoa

msichana mwingine wa kwao huko – sijui wapi… Lakini hili

pia ni jambo dogo, labda jambo ambalo siwezi kumsamehe ni

lile la kutoa mimba mara mbili. Mimba hizi alizitoa alipokuwa

Tabora. Kama ataweza kuzaa tena sijui… (kur. 145 - 146).

Ifahamike kwamba uongo na ulaghai huu unafanywa na Mzee Fungameza wakati

Kazimoto akiwa katika mchakato wa kufunga ndoa na Sabina. Katika hali ya

kawaida, maneno haya siyo tu kwamba yanamkatisha tamaa Kazimoto, bali pia

yanampa wakati mgumu wa namna ya kulikabili jambo hili. Ushauri unaotolewa na

Mzee Mafuru, ambaye ni baba yake Kazimoto, kwamba ajihadhari na watu wenye

nia mbaya, kwa sababu wanaweza kuvunja uchumba wa watu, kwa kiasi fulani

unamwondoa Kazimoto katika mtanziko huo, kwani unamsaidia kubaini hila za

Mzee Fungameza (uk. 147). Pia, anatiwa moyo na kuendelea na mchakato wake wa

kumwoa Sabina, baada ya Sabina mwenyewe kumwomba asisikilize maneno ya

watu, kwa sababu si kila mtu hupenda watu wafanikiwe. Anasema:

Kazimoto, wewe sasa ni mtu mzima. Sidhani kwamba

unaweza kushtushwa na mambo kama haya. Jambo

linalotupendeza sisi haliwezi kumpendeza kila mtu. (uk.

148).

Ni kweli kwamba mahusiano ya mapenzi baina ya Kazimoto na Sabina

yanasababisha mtanziko kwa Kazimoto kutokana na changamoto zinazojitokeza

katika mchakato wa kuoana kwao. Hata hivyo, mtanziko huo unaondoka baada ya

kubaini hila, uongo na ulaghai wa Mzee Fungameza. Jambo muhimu lialopaswa

kufahamika ni kwamba mtu akiwa katika mtanziko, huwa na wakati mgumu wa

kuamua la kufanya. Hali hiyo husababisha hata kuchukua maamuzi ya kujiua

kutokana na kukata tamaa kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi.

107

Sababu ya mtanziko wa mahusiano ya mapenzi pia inajitokeza kwa Vumilia na

mumewe, Moyokonde. Watu hawa, licha ya kuwa na maisha magumu kutokana na

hali yao duni ya kipato, wanaamua kuishi kwa kupendana na kuvumiliana. Tegemea

ambaye ni mama yake Vumilia, akiwa na Kazimoto baada ya kumtafuta Vumilia

kwa muda mrefu, hatimaye, wanafanikiwa kumpata huko Mabatini, Mwanza akiwa

anaishi na Moyokonde kama mke na mume. Kutokana na mazingira hayo, Tegemea

anakata shauri la kuondoka na binti yake. Kauli hiyo inasababisha mtanziko kwa

wote wawili, Vumilia na Moyokonde. Kwa upande wake, Moyokonde anamweleza

Tegemea kwamba, kutokana na mapenzi ya dhati aliyonayo kwa mke wake, Vumilia,

hawezi kuishi pasipo kuwa naye. Anaongeza kuwa, iwapo uamuzi wake ni kuondoka

pamoja na Vumilia, basi akubali kuondoka nao wote wawili, kwa sababu akiachwa

peke yake, yuko tayari hata kufa kwa ajili yake. Mazungumzo baina ya Moyokonde

na Tegemea yanabainisha jambo hili:

―Tukuchukue wewe tukupeleke wapi?‖

―Hata kama ni kuniua,‖ alijibu Moyokonde.

―Nimekuja kumchukua binti yangu, na kesho nasafiri naye.‖

Moyokonde aliinama kwa masikitiko. Aliinua kichwa.

―Hata kama mnataka kumchukua, afadhali mngoje ajifungue,

kwa sababu sasa ni mjamzito.‖

―Mimi nitamchukua mtoto wangu tu. Mtoto wako

atakayezaliwa tutakurudishia.‖

―Hapana. Wewe ni mtu mzima mwenzangu. Mimi nilikuwa

sijapata mtoto maishani. Kumchukua Vumilia sasa ni

kuchukua maisha yangu. Mwanizika kaburini bila nguo.‖ (uk.

174).

Majadiliano haya yanaonesha namna Moyokonde anavyopata wakati mgumu

kutokana na Tegemea kutaka kumnyang‘anya na kuondoka na binti yake. Suala hili

la mahusiano ya mapenzi halimpi wakati mgumu Moyokonde pekee, bali hata

Vumilia mwenyewe anapata ugumu wa kuamua ama akubaliane na matakwa ya

mama yake au akatae na kuendelea kuishi na mumewe. Hatimaye, anachukua

uamuzi mgumu na kumweleza mama yake waziwazi kuwa hayuko tayari kuondoka

naye, bali kubaki na Moyokonde (uk. 174). Msimamo huu wa Vumilia unamsukuma

mama yake kuridhishwa na upendo uliopo baina yao. Kutokana na hilo, anaamua

kuwaondolea mtanziko huo kwa kuwapa baraka zake ili waendelee kuishi pamoja

kama mume na mke (uk. 174). Hivyo, ni wazi kwamba mahusiano ya kimapenzi

huweza kusababisha mitanziko kwa wahusika, hususani pale ambapo mahusiano

108

hayo yatakumbwa na vikwazo mbalimbali. Mtanziko huo huweza hata kusababisha

mhusika kuchukua maamuzi ya kujiua kutokana na kukata tamaa ya maisha kama

inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi, hususani pale anapokuwa haoni

mwanga wa maisha yake ya baadaye. Maelezo ya Moyokonde kwamba yuko tayari

hata kufa iwapo mama yake Vumilia ataamua kuondoka na mtoto wake, ni ithibati

juu ya jambo hili.

Katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo, mtanziko wa mahusiano ya kimapenzi pia,

unajitokeza kwa wahusika mbalimbali. Miongoni mwao ni Leonila, Anastasia, Vera,

na Dennis. Matokeo yanaonesha kuwa wahusika hawa walipitia changamoto nyingi

za kimahusiano, kiasi cha kupata wakati mgumu wa kuamua kuhusu hatima ya

mahusiano na maisha yao kwa jumla.

Mtanziko wa mahusiano ya mapenzi kwa Leonila unatokana na hila na udanganyifu

wa Tumaini unaomwingiza katika mahusiano ya kimapenzi. Tumaini anamhadaa

Mugala, ambaye ni bibi yake Leonila, kwa kumpa ugoro na pipi ili amfanyie mpango

wa kuwa na mahusiano na mjukuu wake. Kwa kuwa Mugala huwa analala nyumba

moja na wajukuu zake, anakubaliana na ulaghai wa Tumaini. Anatengeneza

mazingira ya kumruhusu Leonila kwenda kulala kwa Tumaini usiku kwa siri (kur. 18

- 19). Tumaini anapomkuta Leonila akiwa na bikira yake, anampongeza na anampa

shilingi kumi zaidi. Mahusiano yao yanaendelea vizuri kwa muda mrefu. Matokeo

yake, Leonila anapata mimba na kusababisha mgogoro na mafarakano katika familia

ya Kasala, ambaye ni baba yake Leonila.

Hata hivyo, licha ya Tumaini kukiri kwamba alimkuta Leonila akiwa bikira, Leonila

anapopata mimba, Tumaini anamgeuka na kumkataa kwamba mimba hiyo siyo yake,

na kamwe hawezi kumwoa. Anasema: ―Mimi siwezi kumwoa Leonila, mimba si

yangu. Hata kama akizaa, mtoto wake mnaweza kumtupia mbwa‖ (uk. 26). Badala

yake, Tumaini anaanzisha mahusiano ya kimapenzi na Anastasia na kusababisha

Leonila kuwa na wakati mgumu, kwa sababu licha ya Tumaini kuikataa mimba hiyo,

anakataa hata kumwoa (uk. 26). Hivyo, hii ni ithibati kwamba mahusiano ya

kimapenzi ni sababu mojawapo ya watu kupata mitanziko katika maisha yao,

ambapo wengine huamua hata kujiua kutokana na kukata tamaa ya maisha kama

inavyoeleza nadharia ya Udhanaishi.

109

Kwa upande wa Anastasia matokeo yanaonesha kuwa, naye anakumbwa na mtanziko

unaotokana na mahusiano ya kimapenzi kwa kutakiwa, ama akubaliane na matakwa

ya wazazi wake ya kuolewa na Mzee Tembo, au akubaliane na ulaghai wa Tumaini

na kutoroka naye. Jambo hili linatokea mara tu baada ya Mzee Tembo kufiwa na

mke wake, ambaye ni dada yake, Anastasia. Hivyo, Anastasia mwenye umri wa

miaka kumi na sita tu, analazimishwa na wazazi wake kuolewa na Mzee Tembo

mwenye umri wa miaka hamsini, ili aweze kuwatunza watoto walioachwa na

marehemu dada yake. Kutokana na hilo, anajikuta akishindwa kupata maamuzi

sahihi ya nini cha kufanya ikizingatiwa kwamba, yuko katika mahusiano ya

kimapenzi na Tumaini. Zaidi ya hayo, tayari Tumaini amepanga kumtorosha ili

kumwepusha na balaa hilo. Ifahamike kwamba, msukumo wa wazazi wa Anastasia

wa kumlazimisha aolewe na Mzee Tembo, haukuwa kwa ajili ya kwenda kuwalea

watoto walioachwa na dada yake tu, bali pia, ni kwa sababu ya mali nyingi alizo

nazo mzee huyo. Mazungumzo baina ya Mzee Tembo na wazazi wa Anastasia

yanaonesha furaha yao kwake na wanampa nafasi ya kuongea na Anastasia,

ijapokuwa yeye mwenyewe hapendi. Haya yanabainishwa katika mazungumzo baina

yao kama ifuatayo:

―Ninashukuru sana kwa wema wako. Ninafurahi sana kama

ningeweza kumchukua upesi. Watoto wa dada yake

wanasumbuka sana.‖

―Ndiyo maana nilikwambia ufike upesi. Sisi tu tayari kukupa

binti yetu huyu kwa sababu ya wema wako uliotutendea.

Hatutaki kuomba mahari makubwa sana. Ng‘ombe watatu,

mbuzi wawili na shilingi mia nne zatosha.‖

―Baba mkwe, asante sana, asante sana,‖ Tembo alisema kwa

unyenyekevu akipiga makofi polepole.

―Basi, ukazungumze naye. Bukehele! Njoo hapa nikutume!

Wewe nenda jikoni‖ (uk. 39).

Dondoo hili linaonesha namna wazazi wa Anastasia wanavyomgawa binti yao kama

zawadi kwa Mzee Tembo kwa kigezo cha wema alio nao, pasipo ridhaa ya

mwolewaji. Hii inasababisha mtanziko kwa Anastasia, kwani hata anapoambiwa

akae ndani ili azungumze na Mzee Tembo, yeye anakataa na kukimbilia nje huku

akilia na kumwacha peke yake ndani. Kitendo hiki kinamuudhi sana baba yake na

anamlazimisha arudi ndani ili azungumze na mchumba wake. Kauli ya baba yake

inasema: ―Rudi ndani! Unaogopa wanaume!‖ Baba yake alifoka (uk. 40). Kauli hii

inazidi kumweka Anastasia katika mtanziko. Hatimaye, anachagua kuwasaliti wazazi

110

wake na kuamua kutoroka na Tumaini ili kukomesha utamaduni wa wazazi wa

kuwachagulia watoto wao wachumba na kuwalazimisha kuoa au kuolewa na watu

wasiochaguo lao na wasiowataka. Tumaini analielezea suala hili anaposema:

―Anastasia, usilie. Lazima tuwaonyeshe wazee kwamba

mpango wa zamani wa kugawa mabinti wapendavyo wao,

umekwisha. Huu ni ulimwengu wa ndoa za mapenzi; siyo tena

ulimwengu wa kugawa mabinti kama zawadi kwa watu

wasiowapenda… (kur. 42 - 43).

Dondoo hili linaonesha kwamba mahusiano ya kimapenzi yanamsababishia

Anastasia mtanziko, kwa kuwa yanampa wakati mgumu wa kuamua jambo sahihi la

kufanya kwa wakati huo. Kulingana na utamaduni wa jamii yake, kitendo cha

kuwatoroka wazazi wake, siyo tu kwamba kinawadhalilisha, bali pia kinawaletea

aibu mbele ya watu. Mwandishi anaeleza kwamba kitendo hiki kinamkasirisha sana

baba yake, kwa sababu kinatokea huku jamaa zake wakiwa wamekwishakusanyika

kwa ajili ya arusi. Matokeo yake, jamaa za Mulele wanaanza kudharau na

kutawanyika, huku wakisema:

Watu wasiofahamu kulea binti zao matokeo yao haya haya.

Lakini watu wengine walimtetea Anastasia kwamba alifanya

vizuri kutoroka. Tumaini aliposikia habari hizi alicheka

moyoni (uk. 53).

Hapa tunaona kuwa, Tumaini anafanikiwa kumtorosha Anastasia na kwenda naye

kuanza maisha mapya kama mke na mume huko Shinyanga. Hili linafanikiwa baada

ya kumshawishi Anastasia kuwalaghai wazazi wake kwamba anataka kwenda kijiji

cha Lutare kuangalia ngoma. Baada ya kumalizika kwa mchezo huo, ndipo

anapoamua kutoroka na Tumaini. Kwa kurejelea nadharia ya Udhanaishi, matokeo

yanaonesha kuwa Anastasia anaamua kufanya hivyo kama njia ya kuusaka uhuru

wake binafsi kwa kufanya yale anayoona yanafaa dhidi ya mikatale ya jamii,

inayomkandamiza na kumnyima uhuru wake.

Kwa jumla, utafiti umebaini kwamba mahusiano ya kimapenzi, husababisha watu

wengi kuwa na mitanziko. Suala hilo huwaweka katika hali ya kutatiza, kukanganya

au kuhangaisha. Aidha, huwapa wakati mgumu wa kuchagua la kufanya kutokana na

mkinzano wa mawazo waupatao. Hii ni kwa sababu uamuzi wowote wapangao

kuchukua, huwa na madhara kwao. Hili linathibitishwa katika gazeti la Mtanzania la

111

Novemba 30, 2019 linaloeleza kuwa, sababu mojawapo ya watu kujiua ni msongo

wa mawazo unaotokana na mahusiano ya kimapenzi. Haya ndiyo yanayojitokeza pia,

kwa wahusika Rosa Mistika, Rukia, Sabina, Kazimoto, Manase, Vumilia,

Moyokonde, Leonila, na Anastasia kama tulivyojadili katika sehemu hii.

4.3.1.2 Mfumo wa Malezi

Mfumo wa malezi na namna watoto wanavyolelewa katika jamii huweza

kusababisha mitanziko kwa wahusika. Malezi ni mchakato wa kumtunza na

kumsaidia mtoto, tangu kuzaliwa hadi utu uzima, kwa kuhusisha maumbile, hisia,

jamii na uwezo wa kiakili. Mchakato huo hulenga kumkuza na kumfundisha mtoto

kabla au baada ya kuzaliwa hadi anapofikia umri wa utu uzima ili kufuata tabia na

mwenendo unaostahiki. Kwa mujibu wa BAKITA (2017), malezi ni mafundisho

mazuri yanayotolewa na mzazi au mlezi katika makuzi ya mtoto. Katika jamii nyingi

za Kiafrika, mfumo wa malezi hupitia michakato mbalimbali. Hatimaye, mifumo

hiyo humtoa mhusika katika hali ya utoto na kuwa mtu mzima anayetambua wajibu

wake. Kutokana na hilo, ni jukumu la wazazi na walezi kuhakikisha kuwa mtoto

anaandaliwa mapema na kutambua mambo yote muhimu kama binadamu mkamilifu.

Katika riwaya teule, mwandishi anabainisha ugumu uliopo kuhusiana na suala la

malezi ya watoto, hususani wa kike. Anaona kuwa, malezi ayapatayo mtu akiwa

mtoto mdogo, huwa na athari kubwa sana katika maisha yake ya baadaye. Hii ina

maana kuwa, endapo mtoto atalelewa maisha ya ukali, manyanyaso, ukatili, mateso,

vitisho na masimango, bila shaka mambo hayo yataweza kujidhihirisha kwenye

maisha yake ya baadaye. Aidha, kama atapata malezi ya kudekezwa, ya upendo,

furaha, na kuthaminiwa, anaweza kusawiriwa hivyo hivyo maishani mwake. Kwa

mantiki hiyo, wazazi au walezi wanapotofautiana katika misimamo ya namna ya

kuwalea watoto wao, huwaweka watoto hao kwenye mitanziko ya maisha yao ya

baadaye kama inavyojitokeza katika riwaya teule zilizotumika katika utafiti huu.

Katika riwaya ya Rosa Mistika, tumebaini kuwa malezi aliyopata Rosa kutoka kwa

wazazi wake, hususani kutoka kwa Zakaria, yanamsababishia mtanziko katika

maisha yake. Hii inatokana na kunyimwa uhuru wa kuchangamana na wavulana

kutokana na kulelewa katika hali ya ukali, ukatili, kubanwa na kuchungwa sana.

Musau (1995) anaeleza kuwa Zakaria anaamini kuwa hayo ni malezi bora ambayo

112

ufanisi wake utaonekana pale binti huyo atakapomletea mahari baba yake, baada ya

kuolewa. Hata hivyo, imebainika kwamba malezi ya namna hiyo yanasababisha Rosa

kutofahamu namna ya kukabiliana na matatizo yanayotokana na maisha ya kisasa nje

ya kijiji chao, na mbali na jicho la baba yake. Matokeo yake, akiwa katika shule ya

sekondari ya Rosary, anapata mtanziko pale anapofikiria kukengeuka misingi ya

malezi aliyojengewa na baba yake. Hili linathibitishwa kupitia kauli yake,

anaposema:

Kama nikifanya urafiki na wavulana baba yangu atafahamu?

Yeye yuko Ukerewe, mimi niko Usukuma, baba anakaa

akinichunga anafikiri atanioa? (uk. 32).

Kinachobainika kupitia kauli hii ni kwamba, Rosa hakurupuki tu na kukengeuka

misingi ya malezi aliyojengewa na baba yake, bali anasongwa na mawazo

yanayompa wakati mgumu wa kufikia uamuzi anaopanga kuuchukua. Hata hivyo,

anapobaini kuwa malezi hayo ndicho chanzo cha matatizo yake, anamchukia baba

yake na kujibizana naye hadharani. Zakaria anamkana Rosa kuwa si mtoto wake na

wakati huohuo Rosa naye, anamkana Zakaria kuwa si baba yake (uk. 58).

Utafiti umebaini kuwa kitendo cha Rosa kujibizana na baba yake, ni ishara ya wazi

ya kupinga mfumo wa malezi ya baba yake. Anafikia hatua hii kutokana na Zakaria

kumbana katika suala la malezi na kumnyima uhuru. Hivyo, anaamua kuutafuta kwa

nguvu kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi, ili kupata mwanga na

kujitimizia haja ya matamanio yake. Mwandishi analisawiri jambo hili anaposema:

Maisha ya binadamu ni kama mti. Mti unahitaji maji, hewa na

mwanga. Kama mti ukinyimwa mwanga wa kutosha na miti

mingine, utarefuka. Utajaribu kupita miti yote ili upate

mwanga. Zakaria aliwanyima binti zake mwanga wakati ule

walipokuwa wakiuhitaji sana. Aliwapiga; aliwakataza

kuzungumza na mvulana yeyote. Nao kama mti walijaribu

kujirefusha ili wapate mwanga, na walirefuka kweli; kiasi cha

kutoweza kuonywa na mtu yeyote (uk. 47).

Ni kweli kwamba Rosa anakosa mwanga na njia sahihi kwa sababu ya kunyimwa

uhuru, pamoja na vitisho vingi anavyofanyiwa na baba yake. Kitendo hicho

kinamuumiza sana na kinamjengea chuki moyoni mwake, dhidi ya baba yake.

Matokeo yake anafikia hatua ya kukengeuka misingi ya jamii na kukata tamaa ya

maisha kwa kuamua kuutafuta uhuru wake kwa nguvu kama inayoelezwa katika

113

nadharia ya Udhanaishi. Anayathibitisha haya katika mazungumzo yake na Charles

wakiwa huko Mwanza. Anasema:

―Charles, tendo la baba limeniumiza kuliko unavyofahamu.

Ah Charles, kama tu wazazi wangalifahamu kwamba tendo lao

moja linaweza kuharibu maisha ya watoto wao wangejua

ugumu wa madaraka yao na uangalifu uwapasao (uk. 77).

Maneno hayo ni uthibitisho tosha kwamba Rosa yuko katika mtanziko unaotokana na

malezi kutoka kwa baba yake. Mtanziko huo unasababisha achukue uamuzi wa

kujiua, kama anavyoeleza mwenyewe kabla ya kuchukua uamuzi huo, huku

akielekeza lawama zake kwa Zakaria. Anasema:

―Sasa ninakufa: ninakufa sasa. Maisha yangu yalikuwa

magumu. Sasa nimeona wazi kwamba malezi yangu ndiyo

yalikuwa chanzo cha taabu. Malezi. Siyo malezi ya mama,

lakini malezi ya baba yangu. Kweli baba alinichunga.

Nilichungwa kama msichana wa jela. Nilipopata uhuru,

nilishindwa kuutumia… Baba na mama, samahani kama

nimefanya vibaya.‖ (uk. 91).

Rosa anaposema kwamba maisha yake yalikuwa magumu, na kwamba, malezi ya

baba yake ndiyo sababu ya taabu zake, anakusudia kuthibitisha kwamba aina ya

malezi anayoyapata mhusika huweza kumsababishia mtanziko, ambao pia, huweza

kusababisha mtu kujiua kutokana na kukata tamaa kama inavyoelezwa katika

nadharia ya Idhanaishi. Ndiyo maana, Rosa anamwelekezea lawama baba yake

kutokana na aina ya malezi aliyompa, na kumkosesha mwanga wa namna ya

kuzikabili changamoto za maisha yake.

Suala hili la malezi linasawiriwa pia katika maiti ya Rosa, ambapo uso wake

unaonekana kama wa mtu anayetabasamu, ijapokuwa amekufa kwa maumivu

makali. Mwandishi anasema:

Uso wa Rosa ulionekana kama wa mtu anayetabasamu.

Ingawa alikufa kwa maumivu aliweza kufunga na kufumba

mdomo na macho yake vizuri. … siri ya malezi (uk. 93).

Uso wa Rosa unabeba siri ya maisha yake yaliyogubikwa na madhila yatokanayo na

malezi na matendo mabaya aliyoyapitia. Tabasamu lake ni ishara kwamba anaicheka

jamii yake, kutokana na malezi mabaya kwa watoto wao, hususani, wa kike. Kauli

114

hii inaungwa mkono na Mbatiah (1998) anayeeleza kuwa riwaya hii ya Rosa Mistika,

imetawaliwa na kicheko cha uchungu. Anaongeza kuwa mwandishi anaicheka jamii

yake kwa kushindwa kuwalea watoto wake, hususani watoto wa kike. Anaenda mbali

zaidi kuwa malezi haya mabovu yanakiangamiza kizazi kizima cha watoto wa kike.

Kwa msingi huo basi, ni wazi kwamba Rosa anawakilisha maisha ya vijana wengi

katika jamii, ambao maisha yao kwa jumla yameathiriwa kutokana na mifumo ya

malezi wanayoyapitia katika jamii zao. Aidha, uso huo unaonesha kwamba Rosa

anakifurahia kifo chake, kwa sababu maisha yake hayakuwa na maana tena. Ndiyo

maana ameamua kujiua kuliko kuendelea kuishi. Kulingana na nadharia ya

Udhanaishi, kwake huo ndio uhuru aliokuwa anautafuta kwa muda mrefu, ijapokuwa

uhuru huo ndio ulioyaangamiza maisha yake.

Kwa jumla, utafiti umebaini kwamba kitendo cha kuwabana na kuwanyima uhuru

watoto kwa kuwawekea sheria ngumu na kandamizi, si kigezo madhubuti cha

kuwajengea tabia njema kwao. Kitendo hicho kama inavyoeleza nadharia ya

Udhanaishi, husababisha watoto hao kukengeuka misingi ya malezi wayapatayo na

kuamua kutafuta uhuru wao binafsi na uwezo wa kujifikiria na kujiamulia mambo

yao wenyewe. Hivyo, wazazi na jamii kwa jumla wanatakiwa kuwaeleza watoto wao

ukweli ulivyo kuhusu changamoto za maisha yao. Kitendo cha kuwazuia na

kuwabana wasione mwanga wa mambo yatokeayo ulimwenguni husababisha

mivutano baina yao na wazazi wao, na ndipo hufikia uamuzi wa kuutafuta uhuru wao

kwa nguvu. Mfano mzuri wa kulithibitisha hili ni Rosa Mistika anayejaribu kuutafuta

uhuru wake. Anafanya hivyo ili kuondokana na mfumo wa malezi kandamizi wa

kufungwa na minyororo, uliokita mizizi katika familia ya Zakaria na jamii kwa

jumla. Hata hivyo, uhuru huo unamsababishia matatizo mengi, likiwamo suala la

mapenzi, na hivyo kumpa wakati mgumu wa kuamua na kuchagua la kufanya.

Hatimaye, anachagua kujiua, huku akilalamikia suala la malezi makali, kutoka kwa

baba yake.

Katika riwaya ya Kichwamaji, mitanziko inayosababishwa na suala la malezi,

inasawiriwa pia, hususani kwa vijana. Mitanziko hiyo inatokana na mabadiliko

makubwa ya kitabia kwa vijana, yanayosababishwa na aina ya malezi wanayoyapitia.

Kukosekana kwa malezi bora kunachangia kwa kiasi kikubwa vijana wengi wa

kiume kuwapatia mimba wasichana, wengi wao wakiwa katika umri mdogo.

115

Matokeo yake, wengine hukumbwa na mitanziko kutokana na kushindwa kupata njia

ya kukabiliana na matatizo wanayoyapata. Matilda analithibitisha hili anaposema:

―Haya yote ni sawa,‖ Matilda alisema, lakini nionavyo mimi

sababu yenyewe hasa ni kwamba malezi ya watoto wa siku

hizi yamelegea sana. Wakati mimi nilipokuwa kama wao

ilikuwa mwiko kukutwa na kaka nimesimama na mvulana

yeyote; siku hizi kaka anaweza kumletea ndugu yake barua

kutoka kwa mvulana mwenziwe. Maana yake nini? Wengine

wanaweza kushikana viunoni dansini – kaka na dada! (uk. 58).

Katika nukuu hiyo, Matilda anaonekana kukasirishwa na kitendo cha kulegea kwa

malezi ambako hakutokei kwa vijana wa kiume pekee, bali hata kwa vijana wa kike.

Kulegea huko ndiko kunakosababisha kuharibika kwa vijana, hususani wa kike, na

kuwasababishia mitanziko kutokana na kukosa njia madhubuti za kutatua na

kukabiliana na mitanziko hiyo. Maelezo ya Matilda, yanaungwa mkono na kijana

mwingine anayeona kuwa, kuporomoka kwa malezi ya vijana wa siku hizi,

kunatokana na vijana wengi kuwa na dharau. Anasema:

Sababu kubwa ilikuwa vijana wa siku hizi wanadharau wazazi

wao. Dharau hii imeletwa na elimu. Wanafikiri kwamba

mawazo yote ya wazee ni ya kijadi (uk. 58).

Utafiti umebaini kwamba mabadiliko katika malezi ya vijana wa siku hizi, kwa kiasi

kikubwa yamechangiwa na mwingiliano wa tamaduni, hususani zile za Kimagharibi.

Athari kubwa imetokana na mfumo wa elimu itolewayo kwa vijana hao. Vijana

wengi wa kiume wamekuwa wakiwalaghai na kusababisha mitanziko kwa mabinti

kwa kuwatia mimba na wakati mwingine kuzikataa. Vitendo hivyo vimekuwa

vikiwasababishia mabinti wengi mitanziko katika maisha yao, ambapo wengi wao

hufikia hata uamuzi wa kujiua kutokana na kukata tamaa kama inavyoelezwa katika

nadharia ya Udhanaishi. Manase ni mfano mzuri wa vijana wenye kiburi cha elimu

itokanayo na athari hizo za Kimagharibi. Kutokana na kiburi hicho, anamtia mimba

Rukia na kuikataa kwa kusingizia kwamba alikuwa malaya tangu alipoota maziwa

(uk. 17). Kitendo hiki kinasababisha Rukia kupata mtanziko na baadaye kuchangia

katika tukio la kifo chake.

Kitendo kingine cha vijana wa kiume kuwatia mimba watoto wa kike

kinachohusishwa na mabadiliko ya malezi ya vijana wa siku hizi, kinasawiriwa

116

katika mazungumzo baina ya Kazimoto na wenzake nyumbani kwa Kamata. Jambo

kubwa linalokusudiwa kuibuliwa na mwandishi ni namna watoto wa kike

wanavyopata mimba na, wakati mwingine, kushindwa kumbainisha mhusika wake.

Haya yanajidhihirisha katika majadiliano baina yao, kama ifuatavyo:

―Nasikia binti Kasembe ana mimba ya miezi saba,‖ mmoja

kati yao alisema.

―Mama yake anasema ni mitano.‖

―Mimi nasikia saba na ametiwa mimba hiyo na kijana fulani

mchafumchafu. Sijui wasichana hawana macho?‖

―Msichana alikuwa darasa la kumi na mbili na ametiwa mimba

na kilevi kama sisi.‖

―Wazazi wa msichana huyu wamekataa kumkubalia kijana

huyo kumwoa binti yao.‖ (uk. 57).

Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba vitendo vya vijana wa kiume kuwahadaa na

kuwatia mimba watoto wa kike, vimeshamiri sana katika jamii zetu. Wengi wao

wakishafanikiwa kukipata wanachokitafuta, huwakana na kuwasingizia mambo

mengi, kama vile umalaya, kutokuwa na sifa ya kutembea nao, na nyinginezo. Hali

hiyo ya kukataliwa, husababisha mitanziko kwa wasichana hao. Wengine hukata

tamaa n ahata kujiua kama ielezwavyo katika nadharia ya Udhanaishi. Suala hili

linaungwa mkono na Msigala6 anayeeleza kwamba:

Wasichana wengi wana msongo wa mawazo unaotokana na

athari za mahusiano ya kimapenzi. Hata hivyo, suala la

kuachwa katika mapenzi ni safari tu kwa sababu atakuja

mwingine. Hivyo, wasichana hao wanapaswa kuwa

wavumilivu. Ukizidiwa tafuta mtu mweleze shida yako kwa

sababu kadiri unavyomwelezea mtu shida hiyo, ndivyo

unavyozitema zile sumu.

Vilevile, utafiti umebaini kwamba wakati mwingine wasichana hao huweza hata

kutoa mimba hizo, huwatupa watoto wao, na mara nyingine huchukua maamuzi ya

kujiua, kutokana na kukata tamaa ya maisha kwa kuyaona kuwa hayana maana tena

6 Mahojiano baina ya mtafiti na Bw. Selestino Helman Msigala Septemba 30, 2019.

Yalifanyika Ofisini kwa mtafitiwa, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambako

anafundisha masomo ya Fasihi.

117

kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi. Haya yote hutokea pale

wanapopitia wakati mgumu na kukosa majibu sahihi ya uamuzi wa kuchukua.

Aidha, kwa kuwa vijana wengi wamekuwa wakijiingiza katika vitendo hivyo pasipo

kujiandaa vema, matokeo yanaonesha kwamba wamekuwa wakisababisha watoto

wengi kutowafahamu baba zao, hivyo kupata malezi ya upande mmoja tu, yaani

upande wa mama. Matokeo yake, jamii imekuwa ikishuhudia migongano, migogoro

na kukosekana kwa maelewano baina ya mama na watoto hao, pale wanapotaka

kujua baba zao waliko. Mwandishi analisawiria suala hili kupitia kwa Vumilia,

anayemtaka mama yake amwambie ukweli kuhusu mahali aliko baba yake.

Mwandishi anasema:

Vumilia alikuwa hajapata kumwona baba yake. Jambo hili

lilimfanya apoteze wachumba, kwani wengi walimwita mtoto

wa vichakani. Hili halikuwa kosa lake. Lawama yote

ilimwendea Tegemea mama yake. Tegemea alipokuwa bado

mwanamwari alifanya kazi ya umalaya. Alikuwa ametembelea

miji mingi ya mwambao, Mombasa hadi Mtwara. Katika

kurandaranda kwake alizaa watoto kadhaa, lakini wote hao

walichukuliwa na baba zao (uk. 68).

Matokeo yanaonesha kwamba, matukio kama haya ya vijana kuwatia mimba

wasichana na kusababisha watoto kupata malezi ya upande mmoja, yamekithiri

katika jamii zetu. Jamii imefikia hata kuwaita ombaomba au watoto wa mitaani.

Hivyo, kutokana na watoto hao kukosa malezi thabiti, maisha ya wengi wao

yamekuwa ni ya kukatisha tamaa, yasiyo na matumaini, na yaliyokosa mwanga.

Aidha, imebainika kuwa watoto wanapotaka kujua baba zao waliko na mama

kushindwa kutoa majibu sahihi, huweza kusababisha migogoro na mizozo baina yao

na wazazi wao. Mfano mzuri ni Vumilia anayemwelekezea lawama mama yake,

Tegemea, kwa kushindwa kumwonesha baba yake na kusababisha mtanziko katika

maisha yake kutokana na kukosa malezi ya baba yake. Inaelezwa kwamba:

Wakati huu Vumilia aliinua uso wake kwa mara ya kwanza.

Alimtazama mama yake, halafu alinitazama mimi (Kazimoto).

―Kati yenu hakuna anayenipenda,‖ alisema. ―Maisha yangu

yaliharibika tangu zamani wakati huo hamkusema lolote.

Imekuwaje kwamba leo mmeota kuja kunitafuta na

kunichukua! Mwili nilionao ni wangu; moyo nilionao ni

wangu. Niacheni nife na masumbuko. Na nitakapokufa

118

ninawaombeni mpige ngoma, mkatangaze kote kijijini

kwamba mbwa wa masikini amelamba mchanga‖ (uk. 166).

Mwandishi anaeleza kuwa maneno haya yaliwakata maini wote wawili, yaani

Tegemea na Kazimoto. Kilichokibainika hapa ni kwamba Vumilia anaamua

kuyasema haya kwa uchungu, kwa sababu mama yake hakumpa mwongozo upasao

juu ya maisha yake kutokana na kushindwa kumwambia ukweli kuhusu mahali aliko

baba yake. Kwa upande wa Kazimoto, yeye analaumiwa kwa kuwa ni miongoni

mwa watu waliomharibia maisha yake kwa kumchezea kingono. Utafiti umebaini

kwamba hata pale ambapo Tegemea anamng‘ang‘ania Vumilia kwa kutaka

kuondoka naye, Vumilia anakataa na kusema:

―Mimi sitaki maneno mengi,‖ Vumilia anasema, ―Ninataka

kukuuliza swali moja ambalo ulikataa kunijibu tangu zamani.

Je, baba ni nani?‖ Tegemea alinyamaza. ―Basi fahamu

kwamba maisha yangu yalianzia hapo kuharibika. Kutofahamu

nani baba yangu.‖ (uk. 167).

Huu ni ukweli mchungu kwa Tegemea. Vumilia anaamua kumpasulia jipu ambalo

kwa wakati huo limekwishakuiva, baada ya kuteseka nalo kwa muda mrefu, yaani

kutaka kumjua baba yake mzazi. Hadi kufikia hatua hii, ni wazi kwamba Vumilia

amekuwa katika mtanziko mkubwa unaotokana na tatizo la malezi ya upande mmoja

tu wa mama yake, pasipo kumjua baba yake. Hili linamwia vigumu Tegemea

kuendelea kuhoji ubaya wa Vumilia wa kupata mimba na kuishi na Moyokonde

pasipo ridhaa ya wazazi wake, kwa sababu naye amezaliwa katika mazingira yasiyo

rasmi na pasipo kumjua baba yake mzazi. Hali hii inaonesha kwamba, ijapokuwa

Vumilia hafikii hatua ya kuchukua maamuzi ya kujiua kutokana na kukatishwa

tamaa na namna alivyolelewa, ukweli ni kwamba mtu akiwa katika mtanziko,

huweza kujiua kwa kuyaona maisha hayana maana kama ielezwavyo katika nadharia

ya Udhanaishi.

Utafiti umebaini kwamba aina ya malezi wapewayo watoto wetu ni mojawapo ya

masuala yanayosababisha mitanziko katika jamii. Hii ni kutokana na vijana wengi

kukengeuka misingi na kanuni za jamii husika. Hali hiyo inatokana na vijana wengi

kukengeushwa na elimu ya kimagharibi na kuharibiwa na uozo ulioletwa na

mabadiliko ya kijamii, kutokana na kumomonyoka kwa mfumo wa kimaadili wa

kijadi (Mbatiah, 1998). Mfano mzuri ni Manase na Kazimoto ambao ni wasomi wa

119

Chuo Kikuu lakini wanashindwa kufikia matarajio ya maisha yao; badala yake, kwa

sababu ya umalaya wao, wanakiambukiza kizazi chao ugonjwa wa zinaa walioupata

kutoka kwa Pili. Matokeo yake, wanazaa kizazi kibaya na kusababisha mitanziko

kwao wenyewe na kwa familia zao. Kutokana na mitanziko hiyo, Kazimoto anaamua

kujiua kutokana na kukata tamaa na kwa kuona kuwa, huo ndio uhuru kwake kama

ielezavyo nadharia ya Udhanaishi.

Katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo, imebaini kwamba kutofautiana kwa

mitazamo ya wazazi katika malezi huweza kusababisha mitanziko kwa watoto wao.

Hii ni kwa sababu watoto hao hupata wakati mgumu wa kujua upande sahihi wa

kuegemea, kutokana na kujengewa tabia tofauti na wazazi wao. Kutokana na hilo,

mwandishi anaibua mitazamo mikuu miwili inayojitokeza katika riwaya hii

kuhusiana na suala la malezi ya watoto. Mtazamo wa kwanza, ni malezi ya

kuwadekeza, kuwaengaenga na kuwatimizia watoto kila wanachohitaji. Malezi ya

namna hii tunayapata kwa Tumaini kutoka kwa wazazi wake — Kapinga na

Muyango. Mtazamo wa pili, ni malezi ya ukali, vitisho, ukatili, kuwachunga na

kuwafuatilia sana. Mfano mzuri ni familia ya Kasala na Mungere. Matokeo

yanaonesha kwamba kutofautiana kwa mitazamo ya namna ya kuwalea watoto,

ndiko kunakosababisha mitanziko katika makuzi na malezi yao, kwani mabadiliko

yao kitabia hujengeka kadiri wanavyopewa aina fulani ya malezi.

Mwandishi anasawiria aina ya malezi anayoyapata Tumaini kutoka kwa wazazi

wake, hususani baba yake, yanavyochangia katika kuharibika kwa tabia yake.

Anasema:

… alikuwa bado mtoto mdogo, alitunzwa vizuri. Alitafutiwa

mvulana mdogo wa kumtunza kwa mshahara. Tumaini alikua

kwa kuengwa. Alinunuliwa vijigari vidogo vidogo vingi; kila

alicholilia alipewa. … Muyango alipokuwa akifanya kosa la

kumpenda Tumaini kupita kiasi, Kapinga alifanya kosa la

kujali sana Tumaini atarithi nini. … Hivyo basi, ndivyo

Tumaini alivyotunzwa; ndivyo alivyokua … Tumaini

alipokuwa akipigwa na walimu alizoea kuwatukana

―Washenzi ninyi! Baba hajapata kunipiga! Mna haki gani

ninyi ya kunipiga!‖ (kur. 11 - 12).

Dondoo hili linaonesha namna wazazi wa Tumaini wanavyotofautiana kimtazamo

katika kumlea mtoto wao. Kutofautiana huko ndiko kunakosababisha Tumaini kuwa

120

na tabia mbaya kiasi cha kuwadharau na kuwatukana hata walimu wake kwa madai

kwamba, hata baba yake mwenyewe huwa hampigi. Kauli hii inatopa picha kwamba,

kuharibika au kujengeka kwa tabia ya mtoto huchangiwa sana na malezi ayapatayo

kutoka kwa wazazi wake. Malezi hayo, wakati mwingine, husababisha mkinzano wa

mawazo ambayo humpa wakati mgumu mhusika wa kuchagua la kufanya na

humkatisha tamaa. Muyango anathibitisha kutofautiana na Kapinga katika suala la

malezi ya Tumaini, hususani katika suala la urithi wa mali, anapomwambia Tumaini

hivi:

… funguo hizo hapo mezani. Utalifungua sanduku la

marehemu baba yako, na humo utakuta kitabu kidogo cha

benki. Hizo zote ni pesa zako. Lakini ninaogopa kwamba

zitakuangamiza. Kumbuka kwamba mwanadamu harithi pesa;

mwanadamu hurithi hekima na busara ya babu. Mimi

mwenyewe nilitaka tukuachie nusu, na nusu nyingine

tuwapatie yatima. Watoto wote yatima ni watoto wangu.

Lakini baba yako alikataa. Nilimwambia, ―Kapinga, ni vibaya

mtoto kurithi pesa nyingi; afadhali mjengee nyumba ya kukaa

arithi. Apande mibuyu na michungwa ambayo ataendelea

kutunza kwa jasho. Ni vizuri mtoto kurithi vitu kama hivyo,

licha ya hekima na kumrithisha mtoto ni kumvisha taji la

uovu.‖ Baba yako alikataa kabisa; na kwa kuwa nilishindwa

kugeuza mawazo ya baba yako alipokuwa mzima, siwezi sasa

geuza tamshi lake. Pesa hizo zote ni zako (kur. 14 - 15).

Kitendo cha Kapinga kumwachia urithi mkubwa Tumaini kinamjengea mwenendo

na tabia mbaya kutokana na kiburi cha urithi wa mali hizo. Hali hii inampa wakati

mgumu wa ama kuuzingatia na kuufuata wosia anaopewa na mama yake, au

kuegemea upande wa malezi ya baba yake. Hatimaye, anaamua kufuata aina ya

malezi aliyopewa na baba yake na kujiingiza katika vitendo vya anasa. Anaamua

hata kuacha shule na kujiingiza katika vitendo vya kuwaharibu wasichana kwa

kutembea nao ovyo, na wengine kuwatia mimba (kur. 21 - 22).

Aidha, kiburi chake kinamweka katika wakati mgumu na kusababisha kuchukiwa na

watu wote kijijini hapo kutokana na mwenendo na tabia yake mbaya. Kutokana na

hilo, anaamua kutoroka na Anastasia na kukimbilia Shinyanga (uk. 53). Akiwa huko,

anaendelea na tabia yake mbaya ya umalaya, ambapo anajiingiza katika mahusiano

ya kimapenzi na malaya, Hadija, na kusababisha ugomvi baina yake na Anastasia.

121

Ugomvi huo unazidi kumpa wakati mgumu kutokana na mkinzano wa mawazo

anaoupata, hususani baada ya Hadija kumpiga risasi Anastasia (uk. 84).

Pia, Tumaini anazidi kutatizika na kukosa uamuzi sahihi wa jambo la kufanya

anapoishiwa na mali hiyo, huku akikabiliwa na hali ngumu ya maisha ambayo

hajawahi kuyapitia. Mtanziko huo unamsukuma hadi kwa Dennis, ambako anaomba

kibarua kinachomwingiza katika mtego wa majambazi, ambapo anapigwa na

kutupwa karibu na hospitali ya Shinyanga. Kitendo hiki kinazidi kumtatiza na

kumfanya ayachukie maisha, kama anavyosema yeye mwenyewe kuwa:

―Msizungumzie tena juu ya maisha. Msizungumzie juu ya kitu chochote kile. Maisha

yangu yameharibika‖ (uk. 97).

Hivyo, utafiti umebaini kuwa malezi mabaya anayoyapata Tumaini kutoka kwa baba

yake ni sababu mojawapo ya mtanziko wake. Kauli yake ya huzuni, masikitiko na

majuto anayoitoa, huku akiwa na maisha magumu, tofauti na maisha yake ya awali,

ni uthibitisho wa jambo hili. Kuhusiana na hali hiyo, mtafiti anaona kuwa Kapinga,

ndiye anayestahili lawama hizi kwa kumpa Tumaini malezi mabaya, ikiwa ni pamoja

na kumvisha taji la uovu wa mali ya urithi mkubwa, pasipo kumwandaa kwanza na

kumsababishia mtanziko katika maisha yake. Kwa kujiegemeza katika nadharia ya

Udhanaishi, imebainika kwamba Tumaini anakata tamaa ya maisha kutokana na

mtanziko unaomkabili. Hii inasababisha ashindwe kuona mwanga katika maisha

yake ya baadaye. Mtanziko huo, ndio unaomsukuma katika hatua ya kuyaona maisha

kutokuwa na maana na kukifurahia kifo chake.

Vilevile, imebainika kuwa mwandishi anasawiria aina nyingine ya malezi

inayojitokeza katika riwaya hii, ambayo ni ya ukali na vitisho. Malezi ya namna hii

ambayo ni ya kuwanyima uhuru, kuwabana na kuwachunga sana watoto, wanayapata

Leonila na wenzake kutoka kwa baba yao, Kasala. Malezi haya, siyo tu kwamba

yanawanyima watoto uhuru wao, bali yanawajengea pia mienendo na tabia ya hofu

na woga kama isawiriwavyo katika nadharia ya Udhanaishi. Mambo haya

yanawasababishia mitanziko katika maisha yao. Kauli anayoambiwa Leonila na

mama yake baada ya kubainika kwamba ana mimba ni uthibitisho wa jambo hili.

Anasema:

122

Leonila, baba yako atakuwa mkali kama simba aliyepigwa

mkuki mguuni. Hakika jambo ulilotenda si la busara. Baba

yako atakurarua vipandevipande… (uk. 6).

Maelezo haya yanasawiri tabia ya ukali wa Kasala katika kuwalea watoto wake.

Jambo muhimu ni kwamba jamii inatakiwa kuhakiki ni aina gani ya malezi

yanayofaa kutolewa kwa watoto, na nani anatakiwa kuwajibika katika suala hilo.

Matokeo yanaonesha kuwa watoto hawatakiwi kupewa malezi ya ukali, vitisho,

ukatili, na ya kuegemea upande mmoja, bali jamii nzima inatakiwa kushirikiana

katika suala hili la malezi. Hii inatokana na ukweli kwamba maelezo ya mama yake

Leonila yanaibua wazo linaloonesha kwamba mtu mmoja tu, ambaye ni Kasala,

ndiye aliyeachiwa jukumu la kuwalea na kuwadhibiti watoto wake. Mama huyu

haoneshi dalili za waziwazi za kukichukia kitendo hicho, badala yake, anasubiri

hatua zitakazochukuliwa na Kasala. Mwandishi anaelezea suala la malezi ya Kasala

kwa watoto wake kama ifuatavyo:

―... ilikuwa vigumu sana kuwapata wasichana hawa (Leonila

na Aurelia) kwa sababu baba yao – Kasala – aliwatunza kama

maji ndani ya mtungi. Siku moja alimpiga Leonila mpaka

akazirai kwa sababu ya kukawia sana kisimani. Lakini mtungi

wa Kasala ulikuwa na tundu kubwa. Maji yaliweza kupita.

Tundu liliwekwa na Mugala – mama yake.‖ (uk. 17).

Katika dondoo hili, mwandishi anakusudia kuionesha jamii kuwa malezi ya vitisho,

ukali, ukatili, na ya kuwanyima uhuru watoto, mara nyingi, siyo msingi wa

mwenendo na tabia njema kwao. Pia, suala la malezi halipaswi kuwa la mtu mmoja

pekee, bali jamii nzima inatakiwa kushirikiana. Sambamba na hilo, mwandishi

anaonesha kuwa, licha ya ukali wa Kasala, bado malezi yake yanaingia dosari

kutokana na kukosekana kwa ushirikiano katika familia yake. Utafiti umebaini kuwa

Mugala, ambaye ni mama yake Kasala, ndiye anayesababisha Leonila kupata mimba

baada ya Tumaini kumhonga ugoro na pipi, kisha, kumfanyia mpango wa kuingia

katika mahusiano ya kimapenzi naye kwa siri (kur. 19 - 20).

Hivyo, malezi ya Kasala na ya Mugala yanampa Leonila wakati mgumu wa kuamua

la kufanya kutokana na mkinzano wa mawazo anaoupata, yaani kufuata malezi ya

baba yake, au ya bibi yake. Hata hivyo, msukumo wa malezi ya bibi yake

unamwingiza katika mtanziko zaidi, inapobainika kwamba Tumaini amemtia mimba.

123

Kitendo hiki kinasababisha Kasala kukasirika na kumpa kipigo kikali. Inaelezwa

kuwa:

Kasala alichukua kamba. Alimfunga Leonila kuambatana na

mti wa mchungwa. Leonila alijaribu kukataa; lakini baada ya

muda alikuwa amefungwa tayari akingojea adhabu yake.

Kasala alikwenda kuchukua fimbo ndani ya nyumba. Kasala

alirudi, fimbo mkononi. Alimtandika Leonila fimbo mbili

matakoni (kur. 21 - 22).

Utafiti umebaini kuwa, malezi ni mojawapo ya sababu zinazochangia katika

mitanziko ya wahusika. Hii ni kutokana na kukosekana kwa uwiano mzuri wa namna

ya kuwalea. Hii ina maana kwamba watoto hawatakiwi kulelewa katika hali ya ukali,

vitisho na kuwanyima sana uhuru, kwa sababu kufanya hivyo, siyo kigezo thabiti cha

kudhibiti tabia na mienendo yao. Aidha, hawatakiwi kudekezwa na kuengwaengwa,

kwani huo pia, siyo msingi bora wa malezi, na huweza kuchangia katika kuziharibu

tabia zao na kuwasababishia mitanziko. Suala la muhimu ni kwamba, kutokana na

mwingiliano wa tamaduni, pamoja na mabadiliko ya kijamii na ya kiwakati, malezi

yanatakiwa kwenda sambamba na mabadiliko hayo pasipokuathiri utamaduni halisi

wa jamii husika. Hivyo, jamii inatakiwa kushirikiana na kuungana katika suala hili ili

kuepusha mitanziko kwa watoto wetu. Mitanziko hiyo mara nyingi huweza

kuwasukuma wahusika katika hatua ya kukata tamaa na hata kujiua kama

inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi.

4.3.2 Sababu za Kiutamaduni

Utamaduni ni uzoefu wa kimaisha wa watu fulani unaohusisha michakato ya kijamii,

ambayo huiwezesha jamii hiyo kujielezea na kujitambulisha, pamoja na kufanya

shughuli za kila siku. Kila jamii ina utamaduni, mila na desturi zake ambazo

hutumiwa kama mojawapo ya utambulisho wake. BAKITA (2017) linaeleza kwamba

utamaduni ni mwenendo wa maisha unaohusisha asili, mila, desturi, jadi au itikadi

unaotawala katika jamii fulani; mtindo wa jumla wa maisha ya jamii fulani. Mbiti

(1969) anaeleza kuwa Waafrika wanaamini katika mila na desturi zao, ambazo

hujidhihirisha kwa njia mbalimbali, kama vile vyakula, utoaji majina, dini, nyimbo,

ngoma zao na kadhalika. Katika utafiti huu imebainika kuwa, miongoni mwa

vipengele vya utamaduni wa Kiafrika vinavyoweza kusababisha mitanziko kwa

124

wahusika ni masuala ya mila na desturi, masuala ya dini na tatizo kuhusu ndoa na

uzazi. Vipengele hivi vimejadiliwa kwa kina kama ifuatavyo:

4.3.2.1 Suala la Mila na Desturi

Miongoni mwa vipengele vya kiutamaduni vilivyojadiliwa katika sehemu hii, ni

masuala ya mila na desturi. Vipengele hivi vimejadiliwa kwa namna tatu: urithi wa

mali, utoaji wa mahari, na utani. Kuhusiana na suala la urithi wa mali za marehemu,

usiozingatia usawa na miongozo sahihi ya ugawanyaji wake, utafiti umebaini kuwa,

jambo hili huweza kusababisha mitanziko na mafarakano makubwa katika jamii.

Suala hili linajitokeza katika riwaya ya Rosa Mistika, ambapo ndugu wa Zakaria

wanaamua kugawana mali zake mara tu, baada ya kifo chake. Kitendo hiki

kinasababisha mtanziko kwa watoto wake, kwa sababu ndugu hao hawazingatii

wosia aliouacha kabla ya kifo chake, kwamba mali zote ni za mke wake, Regina,

pamoja na watoto wake. Mwandishi anaeleza:

Lakini Zakaria alikuwa mwalimu. Alifahamu kwamba

matatizo yatatokea kuhusu urithi wa mali yake. Jamaa hawa

baada ya kukosa funguo za kufungulia masanduku,

waliyapasua kwa shoka. Mle ndani walikuta shilingi hamsini

ndani ya bahasha iliyokuwa imeandikwa jina la Regina juu.

Katika sanduku jingine walikuta kijibarua kidogo, nacho

kilieleza habari yote kuhusu watu watakaorithi vitu. Zakaria

aliandika zamani (uk. 96).

Utafiti umebaini kuwa, licha ya Zakaria kuacha wosia unaonesha warithi wa mali

zake, ndugu zake hao wanaugomea kwa madai kwamba haukuandikwa naye.

Matokeo yake, wanaendelea na mpango wao wa kugawana mali hizo na kusababisha

mtanziko kwa watoto wa marehemu. Mwandishi analithibitisha hili anaposema:

Hawa jamaa walirithi. Walirithi hawa jamaa. Walirithi,

walirithi. Jamaa waligawana vitu. Walirithi kila kila

kilichokuwa ndani ya nyumba. Walirithi michungwa na

miembe. Walirithi migomba yote. Walirithi paka na mbwa.

Walirithi majani yaliyokuwa juu ya paa, na miti yote

iliyofanya nyumba isimame. Walirithi mashamba yote.

Walirithi kuku; walirithi hata mbolea ya ng‘ombe. Walirithi.

Hawa jamaa walirithi. Lakini hapakuwa na mtu mmoja

aliyeweza kusema atamchukua mtoto fulani amtunze. Badala

yake walimdai John alipe mahari ili pia wagawane (uk. 96).

125

Kitendo kinachofanywa na ndugu wa Zakaria kinawakera, kinawakanganya na

kuwachanganya sana watoto wake, kwa kuwa wanapata wakati mgumu na hawajui

jambo la kufanya. Hii ni kwa sababu hawahusishwi kabisa katika mgao huo na kila

wanachogusa wanaambiwa siyo mali yao. Matokeo yake wanaachwa katika

mtanziko, kwa sababu hakuna hata mmoja miongoni mwa ndugu hao, anayetaka

wajadili namna ya kuwalea. Mwandishi wa riwaya hii pia, anaonesha kukerwa na

kitendo hicho. Ndiyo maana analirudiarudia neno ‗walirithi‘.

Hata hivyo, utafiti umebaini kuwa pamoja na mitanziko hiyo, si kila mhusika

anayeipitia huchukua maamuzi ya kujiua, bali wengine huistahimili na kuendelea na

maisha yao kama kawaida. Mfano mzuri ni Flora, ambaye ni mdogo wake Rosa

Mistika. Matokeo yanaonesha kuwa, msichana huyu licha ya kupitia changamoto

nyingi katika maisha yake, zilizomsababishia mitanziko mbalimbali, bado

anaendelea kupambana na maisha yake na hachukui maamuzi ya kujiua kama ilivyo

kwa dada yake, Rosa Mistika. Hii inaonesha kwamba wahusika wengine, kama vile

Rosa Mistika huamua kujiua kutokana na udhaifu wao wenyewe, kama anavyoeleza

Zakaria katika ukurasa wa 98, anapotoa sababu za kujiua kwa Rosa Mistika.

Aidha, katika kulielezea zaidi suala hili la urithi katika jamii ya Wakerewe, Bununja7

anasema:

Katika jamii yetu masuala ya urithi hususani miaka ya nyuma

lilikuwa jambo la kawaida sana. Urithi huo ulikuwa ni wa

mwanamke mjane kurithiwa na jamaa za marehemu na urithi

wa mali za marehemu. Kwa upande wa kurithi wajane, suala

hilo kwa sasa limepungua sana. Hii ni kwa sababu mara nyingi

mwanamke mjane apatapo taarifa ya kurithiwa na jamaa hao,

hukimbia na kuiacha nyumba yake. Kwa upande wa mali za

marehemu, hizi zilirithiwa na jamaa za marehemu pamoja na

watoto wa kiume wa marehemu. Kwa Wakerewe mke wa

marehemu na watoto wa kike hawakurithi chochote. Jamii

hiyo iliwachukulia kuwa, wao ni wapita njia na kwamba

wataondoka na kwenda kuishi sehemu nyingine baada ya

kuolewa. Aidha, mali nyingi za marehemu zilirithiwa na

7 Mahojiano baina ya mtafiti na Bi. Rozina Mugabe Bununja Desemba 18, 2019.

Yalifanyika katika Kijiji cha Namagondo kisiwani Ukerewe. Bi. Rozina Mugabe

Bununja ni mwalimu wa Shule ya Msingi Mwitongo iliyoko katika kata ya

Namagondo.

126

ndugu wa marehemu na mara nyingi suala hili lilizusha

ugomvi mkubwa katika familia na ukoo kwa jumla. Watoto

wa kiume walirithi mashamba na baadhi ya mali za

marehemu. Ili kutatua suala hili, mara nyingi mzee wa ukoo

alihusika katika kulishughulikia na kulitafutia ufumbuzi.

Kwa mujibu wa Bununja, masuala ya urithi katika jamii ya Wakerewe, hususani

urithi wa mali bado yapo. Mara nyingi ndugu wa waliofiwa, hung‘ang‘ania mali

zilizoachwa na marehemu. Jambo hili husababisha mizozo na migogoro katika

familia na ukoo wa marehemu. Mizozo na migogoro hiyo mara nyingi ndiyo

husababisha mitanziko kwa wahusika na kwa jamii kwa jumla. Jambo muhimu hapa

ni kwamba kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi, wakati mwingine

mitanziko hiyo husababisha wahusika kukata tamaa na hata kuamua kujiua.

Tofauti na inavyosawiriwa katika riwaya ya Rosa Mistika, ambapo ndugu wa Zakaria

wanarithi mali zote za marehemu na kusababisha mtanziko kwa watoto wake,

ijapokuwa wao hawajiua, suala hili la urithi wa mali linasawiriwa kwa namna tofauti

katika riwaya ya Kichwamaji. Katika riwaya hii, mwandishi anaonesha kuwa suala la

urithi wa mali likizingatiwa na kufanyika vizuri, siyo lazima liwe sababu ya

mitanziko katika jamii, bali mali hiyo inaweza kutumika katika kutatua matatizo

makubwa yanayomkumba mhusika. Kwa mfano, Kamata anaitumia mali ya urithi

kulipia mahari kubwa aliyopangiwa na wazazi wa Matilda, inayolenga kumkomoa

kwa sababu, wazazi hao, hawapendi binti yao aolewe na Kamata. Mwandishi

anasema:

Mwishowe wazazi wake walikubali, lakini moyoni kitu fulani

kilikuwa bado kikiwachoma. Kwa kutaka kumkatisha tamaa

Kamata walidai mahari kubwa sana. Kamata alikuwa tayari

kulipa, kwani baba yake alipofariki alimwachia pesa nyingi

kutokana na kazi ya uvuvi‖ (kur. 47 - 48).

Katika dondoo hili, mwandishi anakusudia kueleza kuwa mali ya urithi siyo haramu,

bali uharamu wake unatokea pale ambapo mhusika huamua kuitumia ovyo tofauti na

utaratibu. Hili linathibitishwa na mwandishi kupitia kwa Kamata, ambaye licha ya

kurithi pesa nyingi, pesa hiyo haikumtumbukiza katika anasa, bali aliitunza na

hatimaye, ilimsaidia katika majukumu mengine ya kijamii, likiwamo suala la kulipia

mahari. Hivyo, kulingana na utafiti huu imebainika kuwa mali ya urithi inaweza

kusababisha mitanziko na hata kumfanya mhusika akate tamaa na kuamua kujiua

127

kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi. Kwa upande mwingine, mali

hiyo inaweza kutumika katika kutatua matatizo mbalimbali na kumwepusha mhusika

na mitanziko katika maisha yake.

Pia, suala la urithi wa mali linajitokeza katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo.

Jambo kubwa linalojadiliwa ni kwamba suala la urithi lisipowekewa misingi imara,

huweza kumletea mrithi matatizo makubwa, na hata kumsababishia mtanziko.

Mwandishi anaelezea namna wazazi wa Tumaini wanavyomrithisha mtoto wao pesa

nyingi pasipo kumwachia miongozo imara ya namna ya kuitumia. Matokeo yake

Tumaini anaitumia pesa hiyo kwa anasa na kusababisha migongano na migogoro

baina yake na jamii yake kama inavyoelezwa katika ukurasa wa 14 na 15.

Matokeo yanaonesha kuwa Tumaini mwenyewe akiwa katika mazungumzo na

Dennis na mama Resi, anakiri kwamba pesa za urithi alizoachiwa na wazazi wake,

ndizo zilizomharibia maisha yake na kumsababishia mtanziko. Mama Resi kwa

upande wake, anaona kwamba urithi wa Kiafrika haufai kwa sababu huwaacha

watoto wa marehemu bila kitu chochote na huwasababishia mitanziko. Haya

yanabainishwa katika mazungumzo yao kama ifuatavyo:

―Mimi ninafahamu kitu kilichokufanya ukawa na maneno

mengi namna hii,‖ Dennis alisema.

―Ni kitu gani?‖ Tumaini aliuliza.

―Pesa za urithi ndizo zimekufanya ukawa na maneno mengi

namna hiyo. Zamani ulikuwa mnyamavu ajabu.

―Wewe unafikiri nini juu ya urithi?‖ Tumaini aliuliza.

―Urithi wa Kiafrika haufai,‖ Mama Resi alidakia. ―Mtu akifa

jamii za marehemu wanachukua mali yote na kuwaacha

watoto bila kitu chochote.‖

―Mimi pesa zangu zimo benkini. Na atakayerithi ni mtoto

wangu, au labda watoto wangu,‖ Dennis alisema.

―Dennis,‖ Tumaini alisema, ―ninashangaa kuona kwamba

mawazo yako yanapingana. Mara unasema kwamba pesa za

urithi ndizo zinaniharibu, mara kwamba watoto wako ndio

watarithi kila kitu.‖

―Wewe Tumaini zimekuharibu kwa sababu ulikuwa peke yako

na pesa ulizorithi zilikuwa nyingi,‖ Dennis alijibu.

―Hata mimi ninafikiri hivyo,‖ Mama Resi aliingia ndani.

―Hata mimi nakubali kwamba pesa za urithi ndizo

zimeniharibia maisha yangu…‖ (uk. 80).

128

Dondoo hili linaonesha namna pesa za urithi zilivyo na madhara na zinavyoweza

kusababisha mtanziko kwa mhusika. Hata hivyo, tasinifu hii inaona kuwa madhara

hayo yanaweza kutokea iwapo pesa hizo hazitatumika kwa umakini na kwa

uangalifu. Mfano mzuri ni Tumaini ambaye baada ya kukengeuka maagizo na

miongozo aliyopewa na mama yake ya namna ya kuitumia pesa hiyo, anakata tamaa

ya maisha yake kutokana na mtanziko anaoupata. Mtanziko huo ndio unaomsukuma

katika mchakato wa kujiua kwake kutokana na kukata tamaa ya maisha kwa kuyaona

kuwa, hayana maana kama ielezwavyo katika nadharia ya Udhanaishi.

Ulipaji wa mahari ni suala lingine linalosawiriwa na mwandishi katika riwaya teule,

ambalo huweza kusababisha mtanziko kwa wahusika. Mtanziko huo huwapata

kutokana na wazazi wa mwolewaji kupanga mahari kubwa, hasa pale wanapotaka

kumkomoa mwoaji. Kwa mujibu wa TUKI (2014), mahari ni mali au fedha

inayotolewa na mwanamume kupewa mwanamke au wazazi wa mwanamke

anayetaka kumwoa. Kulingana na mila na desturi nyingi za Kiafrika, ikiwamo

Tanzania, hususani kwa jamii zinazofuata mfumo dume, mtoto wa kike kabla ya

kuolewa, hulazimika kulipiwa mahari. Jukumu la ulipaji wa mahari hiyo huwa ni la

jamaa wa mwoaji au mwanaume na hulazimika kulipa mahari hiyo kwa kuzingatia

makubaliano ya familia ya mwolewaji. Mahari hiyo hutolewa kama ishara ya

shukrani au zawadi kwa wazazi wa binti anayeolewa. Pia, huwa ni amana kwa

wazazi na ukoo mzima wa binti anayeolewa. Mahari hiyo huhusisha vitu mbalimbali,

ikiwa ni pamoja na wanyama, vifaa vya kazi, pamoja na hela. Wakati wa utoaji wa

mahari hiyo, watu teule wa ukoo hualikwa kushiriki katika kikao cha kuamua

kiwango cha mahari inayotakiwa kutolewa. Kuwapo kwa watu hao ni muhimu ili

maamuzi yanayoafikiwa yasitawaliwe na tamaa za kibinafsi (Wango, 2009). Kwa

msingi huo, kiwango hicho mara nyingi huwa si cha juu sana bali huendana na

uwezo wa aila husika.

Reed (1975) anaeleza kuwa desturi ya kulipa mahari ilianza pale jamii za jadi

zilipoanza kufuga mifugo, hususani ng‘ombe. Wakati huu, wanaume walikuwa na

hamu kubwa ya kutambuliwa kama baba wa watoto wa wake zao. Anaongeza kuwa,

baada ya muda, wanawake walianza kuwa chini ya mamlaka ya wanaume. Kwa hiyo,

wanaume pia, walianza kumiliki watoto waliozaliwa na wake waliowalipia mahari.

Kutokana na hilo, mume alilazimika kumlinda na kumdhibiti mke wake ili amzalie

129

watoto alio na uhakika nao kuwa ni damu yake na wawe warithi halali. Hivyo,

kulingana na mila na desturi za Kitanzania na Kiafrika, kwa upana wake, tendo la

ulipaji wa mahari ndilo linalohalalisha ndoa yoyote itakayofungwa. Hata hivyo,

tendo hili lisipofanyika kwa uangalifu, huweza kusababisha mitanziko kwa

wahusika, kama anavyobainisha mwandishi wa riwaya teule.

Katika riwaya ya Kichwamaji, mwandishi anabainisha namna suala la mahari

linavyosababisha mtanziko katika familia ya Mzee Mafuru. Mtanziko huo

unasababishwa na familia ya Kabenga kupanga mahari kubwa inayotakiwa kulipwa

kabla ya Kazimoto kuanza kuishi na Sabina. Suala hili halisababishi mtanziko kwa

familia ya Mzee Mafuru pekee, bali hata kwa Sabina mwenyewe. Mazungumzo

baina ya Kazimoto na Sabina yanathibitisha jambo hili:

―Unafahamu wazazi wetu walikwenda kuandikisha vitu vya

mahari. Mpaka sasa bado hawajakubaliana ingawa

wameandikisha mbele ya padre. Nilipofika hapa ndilo lilikuwa

jambo la kwanza kuambiwa. Baba yako amedai mahari

ambayo nilikuwa sijapata kusikia. Baba pia mkaidi. Amesema

hata kama ninaweza kutoa hawezi kuniruhusu nitoe na nikuoe

wewe kwa mahari kama hayo, kama kwamba kuna uadui kati

yetu na ninyi. Kabenga ni mtu ambaye tunasikilizana sana

naye, hasa katika siku chache zilizopita. Hatuoni kwa nini

atudai mahari makubwa namna hiyo. Ndoa ni uungwana siyo

uadui.‖

―Baba ameomba kiasi gani?‖

―Ameomba shilingi elfu moja; ng‘ombe watatu, dume na jike

wawili; mbuzi watano; visu vinne, kinu, nafikiri vilevile na

mchi wake, na kitanda.‖

―Kweli, baba hawezi kudai hayo yote kama kwamba ananiuza.

Kwani anafikiri anaweza kutajirika siku moja! Mahari ni

mazuri lakini lazima yakadiriwe. Mahari yanapoteza maana

kama wazazi wakianza kupata wazo la faida vichwani

mwao…‖ (kur. 142 - 143).

Kinachoonekana katika majadiliano haya ni kwamba Kazimoto na Sabina wako

katika mtanziko unaotokana na Kabenga kupanga mahari kubwa. Suala hili linawapa

wakati mgumu ikizingatiwa kwamba Mzee Mafuru naye, licha ya kuwa anatoka

katika utamaduni sawa na Kabenga, hayuko tayari kulipa kiasi hicho cha mahari,

ijapokuwa anao uwezo wa kufanya hivyo. Sabina, kwa upande wake, haoni sababu

ya baba yake kupanga mahari kubwa, kwa kuwa suala la mahari halitakiwi hulenga

katika kuwapa faida wazazi.

130

Ifahamike kwamba katika jamii nyingi za Kiafrika, kushindwa kulipa au kukamilisha

mahari huweza kusababisha mhusika kunyimwa ridhaa ya kukaa na binti huyo, au

kuzuiliwa kabisa kuendelea na michakato mingine ya ndoa. Itokeapo hivyo,

wahusika huwa katika mitanziko na huweza hata kupata msongo wa mawazo. Hali

hiyo huweza hata kusababisha wengine kukata tamaa na hata kujiua kama

inavyoeleza nadharia ya Udhanaishi, kwa sababu hukosa matumaini na mwanga wa

maisha yao ya baadaye. Matokeo yanaonesha kuwa suala hili linampata Moyokonde

na linamsababishia mtanziko, ambapo kutokana na kushindwa kulipa mahari ili

kuhalalisha ndoa yake na Vumilia, mama yake Vumilia anaamuru mtoto wake

asiendelee kuishi naye. Hili linajitokeza katika mazungumzo baina ya mama yake

Vumilia na Moyokonde, kama ifuatavyo:

―Wewe ndiye umemwoa binti yangu?‖ Alimuuliza

Moyokonde.

―Ndiyo.‖ Moyokonde alijibu kwa unyenyekevu.

―Ulifika nyumbani kuleta posa?‖

―Hapana.‖

―Unafikiri Vumilia ameanguka kutoka angani?‖

―Hapana.‖

―Basi fahamu kwamba Vumilia alizaliwa. Ukifahamu hivyo

fahamu pia kwamba mama yake amekuja sasa kumchukua.‖

―Kusema haki sasa Vumilia nimekwisha mpenda, vile

kwamba siwezi kuishi bila yeye. Kama mkitaka kumchukua

basi nichukueni na mimi.‖ (uk. 173).

Majadiliano haya yanaonesha jinsi Moyokonde anavyopata mtanziko anapoambiwa

kwamba hapaswi kuendelea kuishi na Vumilia. Yote hayo yanatokana na

Moyokonde kukiuka mila na desturi za jamii kwa kushindwa kulipa mahari na kuishi

na Vumilia pasipo ridhaa ya wazazi wake. Hivyo, huu ni uthibitisho kwamba

kushindwa kukamilisha utaratibu wa mahari huweza kusababisha mtanziko kwa

wahusika. Matokeo yanaonesha kuwa, wakati mwingine, mitanziko husababisha

mhusika kukata tamaa ya kuishi na hata kufikia maamuzi ya kujiua kama

inavyoelezwa katika msingi wa nne wa nadharia ya Udhanaishi.

Vilevile, tatizo hili la mahari linajitokeza katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo.

Humu mwandishi anamwonesha Mulele, ambaye ni baba yake Anastasia,

akimlazimisha bintiye, Anastazia, kuolewa na Mzee Tembo. Imebainika kuwa

Mulele anampangia Mzee Tembo mahari, huku akionesha kama anafanya takrima

131

kwake kwa sababu ya wema alio anao. Suala hili linamsababishia mtanziko

Anastasia, kwani licha ya mzee huyu kuwa na umri wa miaka hamsini na yeye miaka

kumi na sita tu, vilevile hampendi. Jambo hili linabainishwa kama ifuatavyo:

―… Tembo alifika nyumbani kwa Mulele ili kufanya mpango

wa mahari na kuweka siku ya arusi…‖

―… Ndiyo maana nilikwambia ufike upesi. Sisi tu tayari

kukupa binti yetu huyu kwa sababu ya wema wako

uliotutendea. Hatutaki kuomba mahari makubwa sana.

Ng‘ombe watatu, mbuzi wawili na shilingi mia nne zatosha.‖

―Baba mkwe, asante sana, asante sana,‖ Tembo alisema kwa

unyenyekevu akipiga makofi polepole…‖ (uk. 39).

Kitendo cha Mulele kumtoa Anastasia kwa Mzee Tembo kama takrima na

kumpangia mahari pasipo ridhaa yake, kinazidi kumpa wakati mgumu Anastasia.

Matokeo yake, anaamua kukubaliana na ulaghai wa Tumaini na kutoroka naye.

Anapanga kwenda kuishi pamoja naye huko Shinyanga kama njia ya kuusaka uhuru

wake binafsi kama inavyoelezwa katika msingi wa tatu wa nadharia ya Udhanaishi.

Hii ni baada ya kushindwa kuvumilia mazonge na mikatale ya jamii yake

inayomlazimisha kufanya mambo pasipo ridhaa yake. Matokeo yanaonesha kuwa,

mara nyingi ndoa za kulazimishwa na wazazi au walezi ni chanzo komojawapo cha

mitanziko kwa wahusika na husababisha hata kujiua kutokana na kulazimishwa

kuishi na watu wasiowataka.

Kipengele kingine cha mila na desturi kinachojadiliwa na mwandishi katika riwaya

teule ni utani. Kipengele hiki pia huweza kusababisha mitanziko kwa wahusika

katika maisha yao kama taratibu zake zitakiukwa. TUKI (2014) inaeleza kuwa utani

ni taratibu za kimila ambazo zinawafanya watu kuambiana au kutendeana jambo

lolote bila ya chuki. Kwa upande wake, Mulokozi (2017) anaeleza kuwa mila ya

utani imeenea sana katika makabila mengi ya Afrika Mashariki. Aghalabu, watani

wanapokutana hutaniana kwa maneno (na hata vitendo), huku wakizingatia masharti

yanayotawala uhusiano wao wa kiutani. Anabainisha michepuo ya utani kuwa ni:

utani wa mababu au mabibi na wajukuu, utani wa mashemeji, utani wa makabila au

ya kiukoo, utani wa wanarika, na utani wa marafiki. Anaongeza kuwa kila mojawapo

kati ya michepuo hii huwa na kanuni zake, miktadha yake na mipaka yake katika

jamii zinazohusika.

132

Mara nyingi, utani huonesha uhusiano uliopo baina ya wahusika ambapo watendaji

humithilisha hali na maisha ya wahusika hao. Maelezo haya yanafanana na yale ya

Sengo (2009) anayeeleza kuwa, utani ni uhusiano wa kijamii uliojengeka baina ya

pande mbili, wenye lengo la kufurahisha, kufunza, kukosoa na kukuza uhusiano kwa

kuzingatia mila na desturi za jamii husika. Wanjala (2013) anakazia maelezo hayo

kwamba, malumbano ya watani ni maneno ya kufanyiana mzaha au dhihaka kwa

kueleza mwenendo au utaratibu wa maisha ya jamii husika. Kwa kawaida utani

huambatana na ubadilishanaji wa maneno au misemo ambayo wakati mwingine,

huonekana kama kero au matusi. Hata hivyo, mwandishi wa riwaya teule anabainisha

kuwa, utani huweza kusababisha mtanziko kwa wahusika kwa kuwa, si kila mtu

hupenda kutaniwa. Hii ni kwa sababu, mara nyingi, utani huambatana na mizaha,

kejeli na maudhi kwa kutegemeana na tukio lililopo. Kutokana na hilo, baadhi ya

watu hukosa uvumilivu na huzua migogoro, na hatimaye, huweza hata kusababisha

mhusika kukata tamaa na kujiua kama ielezwavyo katika nadharia ya Udhanaishi.

Katika riwaya ya Rosa Mistika, suala hili linasawiriwa kupitia tabia ya Zakaria, ya

kupenda utani na mizaha. Hii inasababisha mtanziko katika jamii yake kwa kuwa

utani huo, anaufanya mbele ya watu wengi kwenye msiba wa Ndalo. Zakaria

anawatania watu hao kwa kusema:

―Watu wote mliopo hapa, mnatafuta nini! Mnafikiri hapa kuna

arusi! Ondokeni hapa! Ndalo amekwisha kufa kesho ataoza!

Sitaki kusikia mtu akilia bwe! Bwe! Hapa!‖ (uk. 89).

Utani huu unafanywa na Zakaria kwenye msiba wa mtani wake Ndalo, huku akijua

dhahiri kwamba jamii hiyo iko katika majonzi, uchungu na maumivu makali kwa

kuondokewa na ndugu yao. Katika hali ya kawaida, maneno anayoyatamka yanakera

na kuudhi, hasa anaposema, ―Ndalo amekwisha kufa kesho ataoza.‖ Mwandishi

anaeleza kwamba, katika utani huo, Zakaria anavua hadi kofia yake kichwani, akiwa

amepanda juu ya kaburi na kuanza kusema:

―Uhuru wananchi! Wananchi uhuru…! Mimi, nikiwa hapa

kama mwenyekiti wa walevi, ni…‖ Zakaria hakumaliza

maneno yake kitu kama fimbo ndefu iliposimama wima juu ya

kifua chake (uk. 89).

133

Ni kweli kwamba jamii nyingi hutaniana kwa lengo la kuburudisha, kutambulisha

asili na utamaduni wa jamii fulani, pamoja na kurithisha mila na desturi za jamii.

Hata hivyo, baadhi ya watu huchukizwa na kitendo hicho kwa kuwa huambatana na

mizaha, kejeli, ubadilishanaji wa maneno na matusi makali pamoja na kukashifu.

Hili ndilo linalomtokea mtu anayemchoma mkuki Zakaria na kusababisha kifo

chake, kwani maneno yake yanathibitisha hasira kali aliyo nayo dhidi yake.

Mwandishi anaeleza kuwa baada ya Zakaria kutupiwa mshale huo, mtu mmoja

alisikika akiapa, huku akitamka majina ya mababu akisema: ―Kwa jina la Mkaka na

Kamera! Nimemuua mbwa! Mtu hawezi kudharau mji wa watu namna hii!‖ (uk. 90).

Baada ya tukio hili, ndipo inapobainika kuwa:

Zakaria alikuwa mtani wao (mtani wa ukoo wa akina Ndalo).

Na kufuatana na desturi ya Wakerewe, mtani anaweza

kumtania mtani wake wakati wowote na mahali popote

isipokuwa mahakamani. Anaweza pia kuchukua chochote

kisichozidi thamani ya mbuzi mmoja. Mtani hapaswi

kuhamaki wakati huu. Na hivyo ndivyo Zakaria alivyowatania

watani zake (uk. 90).

Kinachobainika kutokana na dondoo hili ni kwamba, kitendo kinachofanywa na

muuaji wa Zakaria kinaleta mtanziko kwa jamii, kwa sababu utani anaoufanya

Zakaria ni sehemu ya utamaduni wa jamii yake. Ndiyo maana kuuawa kwake

kunasababisha mkinzano wa mawazo, kwa kuwa haieleweki iwapo jamii nzima

inakubali na kuelewa umuhimu wa utani au la. Matokeo yake jamii hiyo inabaki

katika mtanziko, kwani hata baada ya Zakaria kuuawa, hatuoni nguvu na hatua

zozote zikichukuliwa dhidi ya mhusika wa kitendo hiki. Badala yake, jamii inazidi

kutatizwa na kukanganywa linapotokea tukio lingine la mke wa Zakaria kufa ghafla,

mara tu anaposhuhudia kifo cha mume wake (uk. 90). Mkanganyiko huu unaiweka

jamii katika wakati mgumu kwa sababu inashindwa kuamua na kujua jambo la

kufanya kutokana na mambo yanayotokea. Tunaambiwa:

Katika kijiji cha Namagondo maafa kama haya yalikuwa bado

hayajatokea hata siku moja. Watu wanne kufa siku moja! Na

wote majirani! Na watatu wakiwa wa mji mmoja! Kijiji kizima

kilijaa masikitiko (uk. 92).

Maelezo haya yanaonesha namna suala la utani linavyosababisha jamii hiyo kuwa

katika mtanziko, kwani siyo tu kwamba linasababisha kifo cha Zakaria, bali

134

linasababisha pia, kifo cha mke wake, Regina. Hii inathibitisha kuwa, wakati

mwingine, mitanziko husababisha mtu kuchanganyikiwa na kupata mshituko, ambao

husababisha mhusika kujiua au kufa kama ilivyomtokea Regina, mara tu baada ya

kifo cha Zakaria.

Vilevile, suala la utani linajitokeza katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo.

Mwandishi anaonesha kuwa, ijapokuwa utani ni sehemu ya maisha ya jamii, si kila

mtu hupenda kutaniwa au kutaniana. Hii ina maana kwamba utani huweza

kusababisha mkinzano wa mawazo, kutokana na watu wengine kukosa uvumilivu wa

mambo. Hili linajitokeza katika riwaya hii, ambapo Kasala anashindwa kuvumilia

utani unaofanywa na Makaranga na kusababisha ugomvi baina yao. Mazungumzo

yafuatayo yanasawiri jambo hili:

―…haya ni mambo ya waliosoma!‖ Kasala alijitetea.

―Sisi mambo ya Kizungu hatuyafahamu, ndiyo maana mke wa

Makaranga alikojoa ndani ya motakaa.‖

―…Mimi sitaki maneno ya kijinga kama hayo!‖ Alifoka.

―Kama wewe una akili mbona Tumaini alimpa mimba binti

yako! Tena alikuwa akilala ndani ya nyumba yako! Ndiyo

maana mama yako alikuwa mchawi!‖

―Unataka tupigane!‖ Kasala aliamka. ―Mimi sijataja jina la

mama yako! Unataka tupigane!‖

―Nani anakuogopa!‖ Makaranga alisema. Waliamka wote ili

wapigane. (uk. 36).

Dondoo hili linaonesha namna utani unavyosababisha mgongano wa mawazo kati ya

Kasala na Makaranga kutokana na Makaranga kuvuka mipaka ya utani wao. Kitendo

cha kumtania Kasala kwa kumtaja mama yake kutokana na uchawi wake,

kinamsababishia mtanziko. Matokeo yake, anachukua uamuzi mgumu wa kutaka

kupigana naye. Kinachojitokeza hapa ni kwamba, licha ya kuwapo kwa umuhimu

wa suala la utani katika jamii, ni wazi kwamba si kila mtu hupenda utani. Hii ni kwa

sababu utani una mipaka yake. Utafiti umebaini kwamba, endapo mipaka na

mazingira ya utani hayatazingatiwa, utani huo huweza kugeuka na kusababisha

mitanziko kwa wahusika. Hali hiyo, huweza hata kusababisha mizozo na migororo,

ambayo pia, huweza kuwa chanzo cha watu kukata tamaa na hata kujiua kama

inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi.

135

Aidha, matokeo yanaonesha kuwa suala la utani kama linavyoelezwa na mwandishi

katika riwaya teule, bado lipo katika jamii yake na ni miongoni mwa vipengele

muhimu vya mila na desturi za jamii hiyo. Pia, imebainika kwamba suala hili ni

miongoni mwa mambo yanayoweza kusababisha mtanziko kwa wahusika, kwa kuwa

wengine kushindwa kuistahimili hali hiyo, na huweza hata kuchukua maamuzi ya

kujiua. Akithibitisha kuhusu kuwapo kwa suala la utani katika jamii ya mwandishi,

Nagane8 anasema:

Kwa sisi Wakerewe, suala la utani ni la muda mrefu sana.

Huwa tunataniana tukiwa humuhumu kisiwani. Mara nyingi

huwa tunataniana na wenzetu kutoka kisiwa cha Ukara. Katika

jamii yetu utani uko katika kila ukoo. Utani huo hufanyika

katika misiba au sherehe mbalimbali. Wakati mwingine,

watani huweza kuchukua nyama ya mbuzi au ya ng‘ombe na

kumwachia mtani wao nyama kidogo tu kwa ajili ya

kuwapikia watu waliokuja kwenye tukio husika. Hata hivyo,

akishachukua mtani mmoja, basi mwingine huwa hachukui

tena.

Kwa jumla, matokeo yanaonesha kwamba suala la utani bado lipo katika makabila

mengi ya Tanzania na unathaminiwa sana. Hii inatokana na ukweli kwamba, pamoja

na mambo mengine, utani husaidia kujenga umoja na mshikamano, udugu, na huibua

mambo mazuri na maovu yaliyopo katika jamii. Hata hivyo, matokeo yanaonesha

kwamba jamii inatakiwa kuelimishwa zaidi juu ya suala hili. Hii ni kwa sababu kama

haitakuwa na welewa wa kutosha, suala hili linaweza kusababisha mitanziko ambayo

wakati mwingine huwa chanzo cha mafarakano katika jamii. Pia, mitanziko hiyo

huweza kusababisha wahusika kujiua au hata kuwaua wenzao kama ilivyotokea kwa

jamii ya Zakaria.

4.3.2.2 Suala la Dini

Dini ni mfumo wa imani wa kuabudu na kuheshimu Muumba. Asasi hii hutawala

mfumo wa maisha ya mtu katika idara zake, kwa kuwa humwekea misingi muhimu

ya maisha. Hii inatokana na kuwa na nguvu kubwa kuliko asasi nyingine za kiitikadi,

8 Maelezo haya yalitolewa na Mzee Pantaleo Vicent Tilibuzya Nagane katika

mahojiano na mtafiti Desemba 18, 2019. Yalifanyika katika Kijiji cha Namagondo

kisiwani Ukerewe. Mzee Pantaleo Tilibuzya Vicent Nagane ni kaka mkubwa wa

Euphrase Kezilahabi.

136

kwa sababu huathiri fikra za watu. Kwa mujibu wa TUKI (2017), dini ni imani

inayohusiana na mambo ya kiroho, kwamba kuna muumba, ambaye aliuumba

ulimwengu huu na kwamba ndiye mtawala wa kila kilichomo. Mbiti (1969)

anafafanua kuwa, pamoja na ujio wa dini za Kikristo na Kiislamu, Waafrika wana

dini zao za jadi. Katika ufafanuzi wake kuhusu dini za jadi, Awolalu (1976)

anasema:

… tunapozungumzia dini za jadi ya Kiafrika tunamaanisha

imani na desturi ya dini ya asili ya Waafrika. Ni dini ambayo

inatokana na kushikilia imani za mababu wa Waafrika wa leo,

na inayoabudiwa nyakati hizi kwa namna na vivuli tofauti vya

uzito, na idadi kubwa ya Waafrika, wakiwamo wale wanaodai

kuwa ni Waislamu au Wakristo.

Waafrika huamini katika miungu yao, na kwamba jambo fulani likitokea vinginevyo

hutazamwa kama ni laana au mwiko. Kutokana na hilo, wengi wao wanapokumbwa

na majanga mazito hukimbilia katika dini zao za jadi ama dini za kigeni kwa imani

kuwa hii ndiyo asasi yenye ulinzi kamili. Kwa hiyo, dini za jadi ni imani za mababu

ambazo zinafuata miiko na maadili halisi ya taifa au kabila fulani. Matokeo

yanaonesha kuwa dini huweza kumsababishia mhusika mtanziko, hasa pale

anaposhikilia sana misingi ya imani yake na kuibua mitazamo inayokinzana baina

yake na jamii inayomzunguka.

Suala hili linajitokeza katika riwaya ya Kichwamaji na linasababisha mtanziko kwa

Sabina, kwa kuwa inamfanya aonekane mtu tofauti kulingana na mitazamo ya

kawaida ya jamii yake. Hii inatokana na msimamo wake wa kushikilia sana misingi

ya dini yake ya Kiprotestanti. Kutokana na hilo, vijana wenzake wanamwogopa na

kumtenga. Kitendo hiki kinampa wakati mgumu wa kujua hatima ya maisha yake.

Anashindwa hata kupata mtu wa kuwa naye katika mahusiano ya kimapenzi. Hii ni

kwa sababu kila mtu anamwogopa kwa namna alivyo. Jambo hili linasababisha

akose mwelekeo wa maisha yake ya baadaye, na anakata tamaa ya maisha kama

isawirivyo nadharia ya Udhanaishi. Mwandishi anathibitisha hili anaposema:

Sabina alikuwa anaogopwa na vijana wengi kutokana na

msimamo wake kwa kuwa alikuwa Mprotestanti halisi. Dini

ilimkaa sana moyoni. Wale waliomnyemelea aliwajibu kwa

misemo ya Biblia. Kweli watu waovu huogopa wacha-Mungu.

137

―Msichana mcha Mungu huyo utamwezaje?‖ Vijana

walijiuliza (uk. 101).

Ni kweli kwamba, mara nyingi, mtu aliyeshikilia sana misingi ya dini au imani yake,

hutazamwa kwa namna tofauti na watu wasiokuwa na misingi hiyo. Msimamo wa

Sabina kuhusu dini yake, ndio unaomsababishia mtanziko. Hali hiyo ya mtanziko

huweza kusababisha mhusika kujiona hafai na hastahili, hususani kwa wale ambao

huwa tofauti na msimamo wake. Msimamo huo humfanya pia, ashindwe kujua

maisha yake ya baadaye yatakavyokuwa, kwani hukata tamaa na huweza hata kujiua

kama isawirivyo nadharia ya Udhanaishi. Hii husababishwa na mhusika kutengwa

na jamii kama anavyothibitisha Sabaina anapoulizwa na Kazimoto, ni kwa nini

hapendi kuolewa, licha ya uzuri wake alionao:

―Kazimoto,‖ alianza kuzungumza. ―Kama ungefahamu taabu

ambazo nimekwishapata usingeniambia vile. Mimi nimo

katika huzuni. Usifikiri kwamba mimi sipendi kuolewa au

kwamba sipendi wanaume. Kazimoto, ni vigumu kupata

wanaume. Nilikuwa na mchumba wangu. Kijana huyo

nilimpenda kweli na nilimpa moyo wangu wote, lakini siku

moja niliona picha yake gazetini ameoa msichana mwingine.

Ninawaombea maisha mazuri. Nilipata kijana mwingine,

nilitaka kumfanya mchumba, lakini nilipokataa mambo

aliyokuwa anapenda, yeye alinitukana kwamba nilikuwa

sifahamu mapenzi na kwamba sikuwa mchangamfu. Tangu

siku hiyo sijapata kumwona tena kijana huyo. Tangu hapo

sijapata tena kijana mwenye nia.‖ (uk. 103).

Katika dondoo hili, utafiti umebaini mawili yanayomtatiza Sabina, licha ya kuwa na

hamu ya kuolewa. Mosi, udanganyifu wa vijana wengi wa kiume kuhusiana na suala

la mapenzi. Pili, ni msimamo wa dini yake, unaosababisha atengwe na vijana

wenzake na kukosa mtu wa kuolewa naye. Kitendo cha kukimbiwa na mchumba

wake kinatokana na msimamo wake wa dini unaomfanya atofautiane naye

anapomwomba afanye naye tendo la ndoa. Misingi na minyororo ya dini yake

inamnyima uhuru wa kukubaliana na kufanya kile anachokihitaji, ijapokuwa naye

ana uhitaji sawa na kijana huyo. Tunalithibitisha hili kupitia maneno ya Sabina

mwenyewe anaposema kuwa, alitamani kuishi na mwanamume, lakini hakubahatika

kumpata. Hii inaonesha kwamba Sabina yuko katika mtanziko wa muda mrefu na

amekata tamaa ya maisha yake kutokana na kukumbwa na hofu na mashaka kama

138

ielezavyo nadharia ya Udhanaishi juu ya maisha yake ya baadaye. Madai yake ni

kwamba siku atakayompata, hatathubutu kumpoteza. Anasema:

―… Lakini naona kwamba siwezi kuishi bila mume. Nikipata

mchumba sasa sijui nitampendaje! Nitamng‘ang‘ania kufa na

kupona. Siku ya kuolewa nafikiri bwana wangu nitakuwa

namlisha kwa mikono yangu mwenyewe.‖ (uk. 104).

Kinachojitokeza katika dondoo hili ni mtanziko alio nao Sabina kwa sababu ya

kufuata sana misingi ya dini na kusababisha aogopwe na kukosa wanaume. Kitendo

hicho kinasababisha akate tamaa na kuamua kuikata minyororo hiyo ya dini ili

kuutafuta uhuru binafsi kama inavyoelezwa katika Udhanaishi. Anapanga kumpa

nafasi mtu yeyote anayetaka kuwa naye katika mahusiano ya mapenzi. Hatimaye,

misingi hiyo inabomolewa kwa urahisi sana na Kazimoto, ambapo, anaanza kufanya

naye mapenzi kabla hata ya kufunga naye ndoa (uk. 104). Matokeo yanaonesha

kwamba mtu akiwa katika mtanziko, huweza kupata msongo wa mawazo, ambao

huathiri uwezo wa akili na hata kumsababisha achukue maamuzi magumu likiwamo

suala la kujiua.

Mtafiti anaamini kwamba dini ni asasi muhimu sana katika kujenga maadili ya mtu

na jamii kwa jumla. Hata hivyo, anaona kuwa misingi ya dini haitakiwi kumtenga

mtu na jamii yake, kiasi cha kusababisha aogopwe na kushindwa kufungamana nayo.

Utafiti umebaini kuwa maumivu anayoyapata Sabina kiasi cha kuogopwa na vijana

wengi, yanaonesha namna dini ilivyomweka katika mtanziko wa maisha yake.

Ndiyo maana Kazimoto anapomgusa tu, anapewa kile anachokihitaji, tofauti na

msimamo wake wa awali. Hii ni baada ya Sabina kuamua kukengeuka misingi ya

dini yake na kujitafutia uhuru binafsi wa kujiamulia mambo yake mwenyewe kama

inavyoelezwa katika msingi wa tatu wa nadharia ya Udhanaishi. Mtafiti anaona

kuwa, iwapo Sabina angebaki katika hali hiyo pasipokubadilika, angeweza hata

kupata msongo wa mawazo, ambao ungemweka katika upweke, na hatimaye,

angeweza hata kujiua au kuishi kwa kuyavumilia maumivu

4.3.2.3 Tatizo la Ndoa na Uzazi

Matatizo yatokanayo na migogoro ya ndoa na masuala ya uzazi husababisha

mitanziko katika jamii. Mitanziko hiyo hutokea pale ambapo wahusika hushindwa au

kukosa uwezo wa kuzaa, kuzaa watoto wa jinsia fulani, au kulazimishwa kuingia

139

katika mahusiano ya ndoa na watu wasiowataka. Kwa mujibu wa TUKI (2014), ndoa

ni makubaliano rasmi ya mwanamke na mwanamume kuishi pamoja kama mume na

mke. Katika jamii nyingi za Kiafrika, heshima ya ndoa hukamilika pale wanandoa

wanapopata watoto, hususani wa kiume. Aidha, ndoa huchukuliwa kama sehemu ya

faraja kwa mtu aliyefikia umri wa utu uzima.

Kimsingi, Waafrika huthamini sana watoto. Pia, thamani ya mwanamke wa Kiafrika

hupatikana kutokana na kuwa na uwezo wa kuzaa watoto, tena wengi (Temples,

1959; Wiredu, 1980; Magesa, 1999; na Mbiti, 2011). Hivyo, mwanamke mwenye

uwezo wa kuzaa huthaminiwa na kupendwa sana kwenye ndoa, ikilinganishwa na

mwanamke asiyekuwa na uwezo wa kuzaa. Kulingana na Thatiah (2018), kutoweza

kuwa na watoto huchukuliwa kuwa ni balaa na nuksi. Hii ni kwa sababu watoto

huchukuliwa kuwa baraka katika ndoa na jamii kwa jumla. Kwa mantiki hiyo, iwapo

ndoa haikubarikiwa kupata watoto kutokana na utasa au kutokuwa na uwezo wa

ujauzito, shauri hilo mara nyingi, huzungumzwa na wanaukoo ili kutafuta suluhisho.

De Beavoir (1985) anaeleza kuwa asasi ya ndoa inampa mwanamke majukumu

mawili muhimu, ambayo ni: kuzaa watoto na kuhakikisha kuwa anamtimizia mume

wake mahitaji ya kimapenzi, pamoja na kuangalia nyumba yake. Maelezo ya

mtaalamu huyu yanaonesha namna suala la ndoa na uzazi lilivyo muhimu katika

maisha.

Imebainika kuwa mtazamo wa jamii nyingi za Kiafrika ni kwamba, tatizo la kukosa

watoto au kuzaa watoto wa jinsia fulani tu, husababishwa na mwanamke hata kama

tatizo hilo litakuwa linatokana na mwanamume mwenyewe. Mambo hayo

yanapotokea, huiweka ndoa husika katika mtanziko, na hata kusababisha wakati

mwingine kuwa na migogoro na wakati mwingine ndoa hizo kuvunjika, kama

anavyoeleza Euphrase Kezilahabi katika riwaya teule.

Katika riwaya ya Rosa Mistika, mtanziko wa ndoa unaojitokeza ni baina ya Zakaria

na Regina. Mtanziko huu unahusishwa na kitendo cha Regina kuzaa watoto wa kike

tu. Kitendo hiki kinaiweka ndoa hiyo katika mtanziko, kwani Zakaria anapanga

kumwacha iwapo ataendelea kuzaa watoto wa kike. Kutokana na hilo, Regina

anakosa amani na kujiona kama mwanamke ambaye hajakamilika kwa kutokuwa na

mamlaka katika familia yake. Hii inatokana na mtazamo wa jamii nyingi za Kiafrika

140

kumchukulia mtoto wa kike kama kiumbe duni na kisichokuwa na nafasi na thamani

kubwa, kilinganishwapo na mtoto wa kiume. Mwandishi analisawiri suala hili

anaposema:

Lakini Regina tangu aolewe hakuwa na raha: alikuwa

akisumbuliwa na kuteswa na mumewe kwa kosa lisilo lake.

Regina alikuwa na watoto watano wasichana; wote wazuri

kama yeye. Matumaini yake ya kukaa pamoja na watoto hao

kama alivyoambiwa na bwanake yalikaa katika mimba ya

miezi mitano aliyokuwa nayo sasa… siyo mimba peke yake

iliyomfanya Regina asimwache bwanake; ilikuwa pia na moyo

aliokuwa nao juu ya watoto wake. Hakutaka kuachana na

watoto hao; bila yeye, mumewe alikuwa hawezi kuwatunza.

Mawazo yake yalikuwa juu ya furaha ya watoto wake katika

maisha yao ya baadaye (uk. 3).

Katika dondoo hili, tunapata mitanziko mikuu mitatu aliyonayo Regina. Mosi, hali

yake ya ndoa itakavyokuwa iwapo atazaa mtoto mwingine wa kike, tofauti na

matakwa ya mumewe. Jambo hili linampa wakati mgumu, linamtesa na kumkosesha

furaha, kwani hajui matokeo yake yatakuwaje. Pili, anatatizwa na kukanganywa na

hali ya watoto wake itakavyokuwa, kwani atashindwa kutimiza jukumu lake la

malezi. Kulingana na tamaduni nyingi za Kiafrika, jukumu la malezi ya mtoto ni la

mama. Hili linajidhihirisha kupitia misemo mbalimbali ikiwemo methali isemayo:

Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu. Ndiyo maana hata mtoto

anapofanya makosa, mara nyingi lawama nyingi huelekezwa kwa mama yake. Tatu,

ni kukosa furaha katika maisha yake kwa kosa lisilo lake, kwani, licha ya kumzalia

Zakaria watoto watano wa kike, bado anaonekana kutokuwa na thamani kwake

kutokana na kukosa mtoto wa kiume.

Matokeo yanaonesha kuwa mambo haya matatu, ndiyo yanayomweka Regina katika

mtanziko na yanamnyima uhuru wa kuamua la kufanya mbele ya Zakaria. Pia,

yanamkatisha tamaa ya maisha kama isawiriwavyo katika nadharia ya Udhanaishi,

na hajui maisha yake ya baadaye yatakavyokuwa. Hii inamaana kwamba, ijapokuwa

Regina haoneshi dalili za wazi za kujiua, ukweli ni kwamba yuko katika mtanziko na

ana msongo wa mawazo, ambayo ni dalili mojawapo inayoweza kusababisha

mhusika kujiua. Kimsingi, Regina anaonekana kutokuwa na furaha katika maisha

yake kutokana na vitendo anavyofanyiwa na Zakaria.

141

Ponera (2010) anaeleza kuwa furaha ni kionjo cha kisaikolojia ambacho huhusu hali

ya ukunjufu wa moyo na bashasha, ambayo aghalabu, hutokana na ridhiko la moyo

au nafsi. Aidha, anamnukuu Shaaban Robert (1954) anayeelezea dhana hiyo ya

furaha kwa kusema:

… Furaha ya kweli huja kwa akili yetu wenyewe. Twaweza

kuhuzunika hata wakati tumekaa juu ya mlima wa dhahabu na

kufurahi hata kama hatuna senti moja ya shaba mfukoni

mwetu. Nadhani kwamba furaha ya kweli huja si wakati

tuwapo matajiri au maskini; lakini ni wakati tuwezapo

kutimiza haja na faraja zetu zipasazo katika maisha yetu. Kwa

hiyo, furaha na akili au ya moyo ndiyo furaha ya kweli, tukiwa

matajiri au maskini, mjini au vijijini (uk. 13).

Ni wazi kwamba maisha ya Regina yanakosa furaha kutokana na kutokuwa na

utulivu wa moyo na akili kunakosababishwa na manyanyaso, masimango pamoja na

kipigo cha mara kwa mara kutoka kwa mumewe. Kwa hali hiyo, imebainika kuwa

kukosekana kwa furaha katika ndoa ni sababu mojawapo ya mtu kuwa katika

mtanziko kama ilivyo kwa Regina. Hata hivyo, matokeo yanaonesha kuwa pamoja

na mtanziko huo, Regina hachukui maamuzi ya haraka ya kujiua, ijapokuwa

anaonesha dalili za kukata tamaa ya maisha kama isawiriwavyo katika nadharia ya

Udhanaishi. Hii ni kwa sababu mtanziko humweka mtu katika njia panda na

hulazimika kuchagua la kufanya, ambapo kila uamuzi auchukuao mhusika huwa na

madhara kwake. Hii inayakinisha hoja iliyokwisha kuelezwa hapo awali kuwa,

mtanziko huweza kusababisha mhusika kujiua au kuendelea kuishi katika hali ya

kukata tamaa lakini kwa uvumilivu.

Hata hivyo, matokeo yanaonesha kuwa mtanziko wake unaanza kupungua mara tu,

baada ya kujifungua mtoto wa kiume na kutimiza ndoto na matamanio ya muda

mrefu ya mume wake. Suala hili linamfanya Zakaria anafurahi na kumpongeza

Regina kwa kumzalia mtoto wa kiume. Hii inasaidia kurejesha kidogo amani na

furaha katika familia yake. Anasema:

―Regina! Sasa mji huu umekuwa wako.‖ ...

Usiku huo Zakaria aliimba aleluya karibu usiku kucha. Kesho

yake alikwenda posta. Mke wake alishangaa kumwona jioni

anarudi na vitu vyote alivyokuwa ametaja. Alianza kupata

sauti. Alianza kuzungumza kwa furaha. Hata watu wa kijijini

waliona ajabu... (kur. 24 – 25).

142

Matokeo yanaonesha kuwa kuzaliwa kwa mtoto huyu wa kiume kunaikamilisha ndoa

ya Zakaria na Regina, kwani kwa Waafrika, kuzaa watoto wa kiume ni fahari kubwa

na jambo linalopewa heri na baraka zote. Furaha ya Zakaria inajidhihirisha pia,

katika maana ya jina la Emmanuel analopewa mtoto huyu. Senkoro (2006) anaeleza

kuwa katika dini ya Kikristo, Emmanuel ni jina lingine la Yesu Kristo, likiwa na

maana ya ―Mungu yu pamoja nasi‖. Imebainika kuwa jina hili lina heshima kubwa

kwa Wakristo. Hii ni kwa sababu huchukuliwa kuwa ni jina la mwana pekee wa

Mungu. Huyu, alitumwa na Mungu baba kuja duniani kuleta wokovu na ukombozi

kwa kuwapatanisha wanadamu na Mungu. Ushahidi wa hoja hii unapatikana katika

Biblia Takatifu, ambapo, katika utabiri wake, Isaya anasema: ―Tazama, Bikira

atachukua mimba, naye atamzaa mwana, nao watamwita jina lake Emmanuel, yaani

Mungu pamoja nasi‖ (Isaya 8: 8, 10; Mathayo 1: 23). Akielezea zaidi kuhusiana na

jina hilo, Ngassa9 anasema kuwa:

Emmanuel ni jina lenye asili ya Kilatini, yaani ―Mungu

pamoja nasi‖. Jina hili lina fundisho kubwa sana katika imani

ya Kikristo, kwani linamtambulisha Yesu kama Mungu kati

yetu. Ndiyo maana tunasema, Yesu ni Mungu na, kwa hakika,

suala hili linahitaji imani kubwa sana ili kulielewa. Ni Mungu

aliyetwaa mwili, kwani hapo mwanzo alikuwapo hata kabla ya

kuumbwa kwa ulimwengu, lakini siyo katika hali ya

kibinadamu au kimwili. Hii ni teolojia ya umwilisho

inayoonesha kwamba huyo aliyekuwapo anatwaa mwili.

Kwa msingi huu, ni dhahiri kuwa mwandishi analitumia jina hili kwa makusudi ili

kuonesha umuhimu na thamani ya mtoto huyo anayechukuliwa kama mkombozi na

mpatanishi kati ya Zakaria na Regina. Hii ni kwa sababu kuzaliwa kwa Emmanuel

anayetumiwa na mwandishi katika riwaya yake, kunamwezesha Regina kuendelea

kuishi pamoja na familia yake. Tunaambiwa kuwa matumaini yake ya kukaa pamoja

na watoto hao kama alivyoambiwa na bwanake yalikaa katika mimba ya miezi

mitano aliyokuwa nayo sasa (uk.3). Hatimaye, mimba hiyo ndiyo inayowezesha

9 Mahojiano baina ya mtafiti na Padre Ibrahimu Ngassa, yalifanyika Desemba 17,

2019 katika viunga vya Seminari ya Mtakatifu Maria huko Nyegezi. Hapa ndipo

aliposomea pia, Euphrase Kezilahabi, mwandishi wa riwaya teule. Padre Ibrahimu

Ngassa ni mlezi wa wanafunzi wanaoandaliwa kuwa Mapadre.

143

kuzaliwa kwa mtoto wa kiume na kupewa jina la Emmanuel kama ishara ya kuleta

upatanisho baina ya Zakaria na Regina. Hii inaonesha kuwa, ijapokuwa Regina

alikuwa katika mtanziko uliomkosesha furaha na ulimfanya awe msongo wa

mawazo, ambao ungeweza hata kusababisha ajiue, mtoto huyu anasaidia kuuondoa

mtanziko huo. Aidha, anasaidia kumwondoa Regina katika hali ya kukata tamaa

kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi, badala yake anakuwa huru

kuendelea kuishi kwa furaha na utulivu pamoja na watoto wake. Huu ni uthibitisho

kuwa suala la ndoa na uzazi huweza kusababisha mtanziko kwa mhusika, ambao

humpa wakati mgumu wa kuamua jambo la kufanya, kwani wakati mwingine

humsukuma mhusika katika ukingo na fikra za kujiua.

Ifahamike kwamba, kabla ya kuzaliwa kwa Emmanuel, Zakaria alimfokea Regina

kwa kumtolea kauli mbaya, za maudhi, kashifa, lawama na manyanyaso. Haya

yalimkosesha furaha katika maisha yake yote. Yalimfanya akate tamaa na kuyaona

maisha hayana maana kama inavyoelezwa katika Nadharia ya Udhanaishi. Kwa

mfano, kauli anayoitoa Zakaria baada ya kuwafukuza na kuwakimbiza vijana

wanaojifanya wanataka kununua mayai, inathibitisha mojawapo ya kauli hizo mbaya.

Mwandishi anasema:

Wale vijana walikimbia bila kuangalia nyuma. Walifikiri

bado anawafuata. Zakaria aliwasikia kwa mbali

wakimtukana.

Mshenzi, utaoza na binti zako!‖

Zakaria hakuwajibu lolote. Regina na Rosa walikuwa

wamenyamaza tu.

―Mshenzi, unanizalia wasichana tu! Unaniletea taabu

nyumbani bure tu!‖ Zakaria alifoka. Regina hakujibu;

aliogopa kumdhihaki... (uk. 23).

Regina anaamua kukaa kimya ili kumtunzia heshima mumewe na kuepusha

mitanziko zaidi katika ndoa yake. Aidha, kukaa kimya huko kunaonesha hulka

waliyonayo wanawake wengi ya uvumilivu na utii kwa waume zao. Maoni ya mtafiti

kuhusiana na ukimya wa Regina ni kwamba, yawezekana anafanya hivyo kwa

kuogopa kumdhihaki na kumdhalilisha mumewe kutokana na ujinga wake wa

kuelekeza lawama kwake, kwa kitendo cha kumzalia watoto wa kike tu, wakati

kibaiolojia, anayeamua jinsia ya mtoto ni mwanaume, na wala siyo mwanamke

(Taylor na wenzake, 1995; Allan, 2003; Mwaniki & Geoffrey, 2009). Kwa hiyo,

144

mtafiti anaona kuwa Zakaria, ndiye anayestahili lawama zote kwa kumzalisha

mkewe watoto wa kike mara zote na kusababisha mtanziko katika familia yake.

Mtanziko huo unamkatisha tamaa na anayaona maisha hayana maana kama

inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi Hata hivyo, matokeo yanaonesha kuwa,

ijapokuwa mtanziko huweza kusababisha msongo wa mawazo na kumkatisha tamaa

ya maisha mhusika na hata kujiua, Regina anaonesha ujasiri na uvumilivu na

hachukui maamuzi ya kujiua.

Katika riwaya hii, pia, mtanziko unaosababishwa na uzazi na ndoa unajitokeza baina

ya Ndalo na Bigeyo. Wanandoa hawa wanajikuta katika mkinzano wa mawazo na

kupata wakati mgumu kutokana na kuhangaika kwa muda mrefu wakitafuta watoto

pasipo mafanikio. Hali hii inasababisha ndoa yao kukosa furaha na amani, kwa

sababu kwa asili, uimara wa ndoa na ufahari wa Mwafrika huonekana kwa kuzaa

watoto, tena wengi. Pia, imebainika kuwa uzazi ndiyo njia ya uzima wa milele, na

ugumba ni laana mbaya kuliko zote, kwa kuwa huondoa thamani ya mtu duniani.

Methali ya Kibantu inayosema: ―Nyumba ya mgumba haina matanga‖ ni uthibitisho

kwamba mgumba hana thamani katika jamii, kwa sababu ya kukosa uzazi. Hoja hii

inaungwa mkono na Shaaban Robert (2013) anayeeleza mtazamo wa Waafrika

kuhusiana na watu wasiokuwa na uwezo wa kuzaa na athari zake, anaposema:

Ustawi uliofanyika katika nchi hii tangu mwanzo wa ufalme

wangu, umeniletea heshima. Lakini ugumba umemeza

heshima na utasa umetia wimbi fahari ya Malkia. Sina mtoto

wa kurithi kiti changu cha ufalme, kutoa mashauri ya hekima

barazani kama mababu zake (uk. 3).

Mwandishi anaonesha thamani na heshima inayotokana na uzazi ambao huwezesha

kupatikana watoto wa kurithi hata kiti cha ufalme. Anaonesha mtanziko aupatao mtu

asiyekuwa na uzazi, ambapo hata heshima yake hutoweka mbele ya jamii, kwa

sababu hutazamwa kama mtu ambaye hajakamilika bado. Hii inatokana na ukweli

kwamba mtu anapooa au kuolewa, matarajio ya jamii yake huwa ni kumwona

mwanamke akiwa mjamzito mapema iwezekanavyo. Chuachua (2016) anaeleza

kuwa, kwa kawaida, minong‘ono huanza baada ya mwaka mmoja au miezi michache

tu, tangu kufunga ndoa, endapo hakuna dalili za kupatikana kwa mtoto. Matokeo

yanaonesha kuwa, minong‘ono hiyo husababisha wahusika kupata mitanziko na

hujiona kama watu duni na wasiokuwa na thamani katika jamii. Kutokana na hilo,

145

imebainika kwamba wengine hufikia hatua ya kukata tamaa na huyaona maisha

hayana maana tena kwao kama isemavyo nadharia ya Udhanaishi. Hivyo, huamua

kujiua ili kuikwepa aibu na fedhea kutoka kwa jamii inayowazunguka. Ifuatayo ni

taarifa inayothibitisha kuwa mtanziko wa ndoa na uzazi huweza kusababisha

mhusika kujiua kama inavyoripotiwa na (https://www.eatv.tv/news/current-affairs/).

Taarifa hiyo inasema:

Askari polisi wa Kituo cha Polisi, Wilaya ya Kahama, H.1363

PC Gideon Clement (miaka 30), Mkazi wa Muleba, Mkoani

Bukoba, amejiua kwa kujipiga risasi shingoni Alhamis, April

4, 2019 majira ya saa moja na nusu asubuhi akiwa kwenye

lindo mjini Kahama. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga,

ACP Richard abuwao, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo,

ambapo amesema sababu za askari huyu kujiua, ni kutokana

na kutofanikiwa kupata mtoto, licha ya kuishi kwenye ndoa na

mkewe kwa kipindi cha miaka mitano. Kamanda huyo

ameeleza kuwa sababu hizo, zilibainishwa katika ujumbe

alioutuma kwa mke wake. Ujumbe huo ulisema kwamba hana

sababu za kuendelea kuishi kwa kuwa hajajaliwa kupata mtoto

na amekaa katika ndoa na mke wake, ambapo jana yake

alilalamikia sana jambo hilo na alianza kuonesha dalili kwa

kumtumia mkewe ujumbe wa simu akieleza kuhusu mali zake,

vikiwamo viwanja (www. Eatv.tv).

Hapa taarifa hii inatoa ithibati juu ya umuhimu wa suala la ndoa na uzazi katika

jamii, na namna linavyopewa kipaumbele. Aidha, taarifa hii inaonesha namna

mhusika anavyoweza kupata mtanziko na kukata tamaa ya kuendelea kuishi kama

inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi kutokana na kukosa uzazi, na hivyo,

kuamua kujiua. Utafiti umebaini kuwa, hili ni tukio moja tu miongoni mwa mengi

yanayotokea katika jamii yanayowapata wahusika kutokana na mitanziko ya ndoa na

kukosa uwezo wa kuzaa.

Kwa upande wake, Mbiti (1969) anaeleza kuwa suala la kuoa na kuolewa kwa

Mwafrika, si hiari, bali ni la lazima. Anafafanua zaidi kwa kusema:

… therefore, it is a duty, religious and ontological for everyone

to get married; and if a man has no children or only

daughters, he finds another wife so that through her, children

(or sons) may be born who would survive him and keep him

(with the other living dead of the family) in personal

immortality (pg. 26).

146

… kwa hiyo ni jukumu la kidini na kijamii, kwa kila mmoja

kuoa au kuolewa; na kama mwanaume hana mtoto au ana

watoto wa kike pekee, atafute mke mwingine, ili kupitia

kwake, watoto (wa kiume) waweze kuzaliwa, ambao

wataendeleza ukoo wake na kumweka (pamoja na wafu

wengine katika familia) katika dhana ya uhuishwaji (uk. 26)

(Tafsiri ya Mtafiti).

Maelezo haya yanatoa picha kwamba ndoa haiwezi kukamilika mpaka mwanamke

anapoonesha kuwa na uwezo wa kuzaa. Pia, mtazamo wa Mbiti unaonesha kwamba

tatizo la kutozaa au kupata watoto wa jinsia moja husababishwa na mwanamke.

Ndiyo maana anaona kwamba mwanaume akibaini tatizo hili, anapaswa kutoka nje

ya ndoa yake na kutafuta mwanamke mwingine wa kuzaa naye watoto wa kiume.

Mawazo ya Mbiti hayatofautiani sana na ya Faustine (2017) anayeeleza kuwa, katika

jamii za Kiafrika wanandoa wasiobahatika kupata watoto, huwa hawathaminiwi

katika jamii. Aidha, mara nyingi, ndoa zao huwa hazidumu; au mwanaume huamua

kuoa mke mwingine ili kupata watoto. Hali hiyo ya kutodumu kwa ndoa hizo,

husababisha wahusika kuwa katika mitanziko, na wengine huishi kwa woga, hofu na

wasiwasi kama ielezwavyo katika nadharia ya Udhanaishi. Aidha, wengine huamua

kujiua kama suluhisho la mitanziko hiyo.

Mawazo ya Mbiti na Faustine yanaeleza mambo halisi, kwani mitazamo hiyo ndiyo

iliyoshamiri katika jamii zetu. Hata hivyo, utafiti huu unaona kuwa kushamiri kwa

mitazamo hiyo ni mwendelezo tu wa mfumo dume wa kumkandamiza mwanamke.

Mfumo huu mara zote humtazama mwanamke kama kiumbe duni na kisichokuwa na

thamani na uwezo wa kufanya lolote. Ukweli ni kwamba wanandoa wanapokosa

uzazi, wote wawili hupata mtanziko ambao huwaondolea thamani yao katika jamii.

Hivyo, hufanya jitihada mbalimbali kama vile kwenda kwa waganga wa jadi au

kutumia madawa ya asili kabla ya kwenda hospitalini, ili kupewa dawa za

kufanikisha tatizo lao (Kitereza, 1980). Hufanya hivyo kwa kuamini kuwa, uganga

ndilo suluhisho la matatizo mengi yanayomsibu mtu, likiwamo tatizo la uzazi.

Tatizo hili la uzazi ndilo linalowakumba pia, Ndalo na Bigeyo katika riwaya ya Rosa

Mistika. Wao, wanahangaika na kwenda kwa waganga mbalimbali, huku wakipoteza

pesa nyingi ili kutafuta dawa ya uzazi. Mahangaiko yao yanatokana na mtanziko

walionao wote wawili kutokana na kukosa watoto na kukosa thamani katika jamii.

Mwandishi anasema:

147

Ndalo pamoja na Bigeyo walikuwa wanakula nyama ya kuku

hali wanakimbia kuzunguka nyumba. Ndalo na mkewe

walikuwa wanasumbuliwa na jambo moja – uzazi. Walikuwa

wamekwishapoteza fedha nyingi kutafuta dawa ya uzazi.

Mwaka mmoja walikwenda nchi za mbali kuitafuta. Walirudi

na nusu debe la mizizi ya miti. Mizizi ilikwisha na wala

hapakuwa na alama yoyote ya Bigeyo kupata mimba. Mwaka

uliofuata walikwenda pengine. Huko walimkuta mganga

mmoja wa kienyeji aliyewaambia kwamba Bigeyo alikuwa

hazai kwa sababu alipokuwa bado msichana alikataa

kuwabeba wadogo zake mgongoni. Dawa ya uzazi sasa

ilikuwa lazima kupata mkojo wa wadogo zake ajimwagie

mgongoni. Lakini jambo hili halikuwa rahisi; wadogo zake

sasa walikuwa watu wazima. Waliporudi nyumbani, haukupita

muda mrefu mdogo wake akamtembelea. Bigeyo alifurahi

sana. Wakati wa kulala ulipofika alimpelekea mdogo wake

kopo. Alimwambia kwamba katika kijiji hicho ilikuwa hatari

kutoka nje wakati wa usiku. Alimwambia akojoe ndani ya

kopo. Asubuhi na mapema Bigeyo alichukua lile kopo na

kwenda kujimwagia mgongoni. Mwaka ulipita. Bigeyo

alipokuwa anashiba sana mumewe alimuuliza kama amepata

mimba. Miaka miwili ilipita; hapakuwa na alama yoyote kwa

Bigeyo kuchukua mimba…. Mwishowe, walikata shauri

kwenda Kaskazini, huko walimkuta mganga mwingine

aliyewaambia wale nyama ya kuku mweupe wakikimbia

kuzunguka nyumba ili kutakasa mji (kur. 17 - 18).

Dondoo hili linaonesha umuhimu wa uzazi, na namna unavyowapa wakati mgumu

Ndalo na Bigeyo. Furaha ya ndoa yao inakosekana kwa sababu ya kukosa uwezo wa

kupata watoto. Wanahangaika huku na kule ili kulinda heshima yao, kwani uzazi ni

njia pekee ya kumletea mtu heshima na thamani katika kuendeleza familia na ukoo

wake. Hatimaye, uvumilivu wao unafika mwisho. Kama inavyoeleza katika nadharia

ya Udhanaishi, wanakata tamaa kutokana na maisha yao ya kukosa matumaini ya

kufanikiwa. Kiashiria cha wazi cha kukata tamaa huko ni kauli ya Bigeyo (uk. 18)

kwamba kitendo cha wao kukosa watoto ni laana. Hata hivyo, matokeo yanaonesha

kuwa, pamoja na mtanziko wa ndoa na uzazi wanaoupata, Ndalo na Bigeyo

hawachukui maamuzi ya kujiua, bali wanaendelea kuishi kwa uvumilivu, huku

wakiwa wamekata tamaa.

4.3.3 Sababu za Kiuchumi

Miongoni mwa matatizo ya kiuchumi yanayosababisha mtanziko ni umaskini, hali

ngumu ya maisha, na ukosefu wa kazi. BAKITA (2017) linaeleza kuwa uchumi ni

mfumo wa uzalishaji mali wa nchi kwa shughuli za biashara, viwanda na kilimo,

148

pamoja na matumizi ya mali hizo. Kwa maneno mengine, uchumi ni jumla ya

shughuli zote za binadamu zinazolenga kutosheleza mahitaji yao. Unajumuisha njia

za uzalishaji, usambazaji, ugawaji na matumizi ya bidhaa na huduma. Hali ya

uchumi inapokuwa mbaya, huweza kusababisha mtu au taifa kushindwa

kujitosheleza katika mahitaji yake, na hata kusababisha mtanziko wa namna ya

kuyaendesha maisha kwa jumla. Mwandishi wa riwaya teule anabainisha namna

sababu za kiuchumi zinavyoweza kuwa chanzo cha mitanziko kwa wahusika.

Katika riwaya ya Rosa Mistika, umaskini na hali ngumu ya maisha katika familia ya

Zakaria vinasababisha mtanziko kwa Rosa na mama yake, Regina. Hali hiyo

inawatokea mara tu baada ya Rosa kufaulu masomo yake ya darasa la saba na

kutakiwa kwenda kujiunga na sekondari ya Rosary. Barua inayoonesha mahitaji

anayotakiwa kwenda nayo shuleni, inazidi kumweka katika wakati mgumu zaidi

anapojibiwa na Zakaria kwamba hana hela hiyo (uk. 9). Uduni wa maisha yao

unasababisha Rosa kuchelewa kuripoti shuleni kwa muda wa mwezi mmoja. Suala

hili linachangiwa pia na kitendo cha Zakaria kuiba fedha iliyoandaliwa kwa lengo

hilo na kwenda kuitumia katika masuala ya ulevi (uk. 11). Mwandishi anaeleza

kuwa:

Zakaria alikuwa mwalimu zamani, lakini alifukuzwa kazi kwa

sababu ya ulevi. Jirani zake walisema alijali pombe kuliko

watoto. … Sasa watoto walikuwa shuleni, heko kwa mama

yao (uk. 11).

Zakaria anaonesha kutowapenda wala kuwajali watoto wake. Hataki kuwalipia ada

ya shule kwa madai ya kukosa pesa, lakini siku zote anazo za kunywea pombe.

Kitendo cha kuiba fedha iliyoandaliwa kwa ajili ya ada ya Rosa kinawasababishia

mtanziko Rosa na mama yake, kwani wanapata wakati mgumu wa namna ya

kulitatua tatizo hili (uk. 16). Wanapoamua kubuni biashara ya kuuza mihogo

(udaga), hawafanikiwi kwa sababu ya kukosekana kwa wanunuzi. Ugumu

wanaoupata kutokana na kushindikana kwa biashara hiyo unawasukuma kubuni

biashara nyingine, ambayo ni ya kuuza pombe ya mihogo iitwayo mapuya.

Hatimaye, wanafanikiwa kupata pesa hiyo (uk. 18).

Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa umaskini na hali ngumu ya maisha hukatisha

tamaa na huweza kumsababishia mhusika mtanziko. Hii ni kwa sababu mtu huyo

149

hujikuta katika wakati mgumu na hushindwa kujua la kufanya. Matokeo yake,

huweza hata kujiingiza katika vitendo vya ulevi kama njia ya kuondoa msongo wa

mawazo unaokuwa unamkabili. Suala hili linasawiriwa na mwandishi anapoelezea

hali ngumu ya maisha ya Zakaria. Kutokana na hali hiyo anashindwa hata kujenga

nyumba ya maana na kuamua kuishi maisha ya ulevi. Mwandishi anasema:

Zakaria alikuwa ameshindwa hata kujenga nyumba ya maana.

Katika nyumba alimokuwa akilala sasa pamoja na watoto

wake, nyota zilikuwa zikiwashangilia kila siku usiku. Tangu

Ijumaa mpaka Jumapili Zakaria alikuwa anakwenda kunywa,

na siku nyingine za juma alijifanya mgonjwa kitandani (uk. 6).

Kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi, dondoo hili linaonesha namna

Zakaria alivyokata tamaa na kuamua kujiingiza katika vitendo vya ulevi. Hii ni

kutokana na umaskini na hali ngumu ya maisha yake. Mambo haya yanamweka

katika mtanziko na kushindwa kupata majibu sahihi ya maisha yake. Mwandishi

anaeleza zaidi kuhusu umaskini na hali ngumu ya Zakaria, anaposema, ―… usiku huo

mvua ilinyesha kwa wingi sana. Lo! Nyumba ilikuwa kama mti. Ilivuja

kustaajabisha…‖ (uk. 13). Imebainika kwamba mambo haya yanachangiwa na tabia

yake ya kuendekeza ulevi na uvivu kwa visingizio vya kuumwa. Hatimaye, anajikuta

katika mtanziko unaomkatisha tamaa ya maisha yake. Hata hivyo, hachukui

maamuzi ya kujiua kama iwatokeavyo watu wengine, ambao husukumwa katika

hatua ya kujiua kama suluhisho la kumaliza matatizo yao, wanapokuwa katika hali

kama hiyo.

Hii ndiyo picha halisi ya maisha ya familia ya Zakaria, anayoisawiri mwandishi wa

riwaya hii. Mateso, mahangaiko na maumivu ya familia hii yanasababishwa na tabia

ya Zakaria ya kutumia pesa zake nyingi katika ulevi. Anashindwa kuwajibika na

kutimiza majukumu yake kama baba wa familia. Mtafiti anaamini kuwa, kama

angeitumia pesa hiyo kwa uangalifu, angeweza hata kujenga nyumba nzuri ya kuishi

na familia yake. Hata hivyo, matokeo yanaonesha kwamba kwa jamii ya Wakerewe

150

kama zilivyo jamii nyingine za Tanzania, kwao suala la unywaji wa pombe ni jambo

la kifahari. Hili linathibitishwa na Kadala10

kama ifuatavyo:

Wakerewe wana kawaida ya kunywa pombe na huwa

wanalewa sana. Kwa Wakerewe pombe ni jambo la kawaida

na halina uzito wala makatazo yoyote. Ndiyo maana hata

katika riwaya ya Rosa Mistika, mwandishi mwenyewe

ametusawiria kwamba pombe imetumika kama nyenzo ya

kupatia uchumi ili watoto (Rosa Mistika) waende shule au

wasome.

Matokeo yanaonesha kwamba katika jamii nyingi za Kiafrika, pombe huchukuliwa

kama kiburudisho na kitu cha fahari na heshima kubwa miongoni mwao. Hata

hivyo, unywaji usio wa kistaarabu na unaozidi kiwango, humpoteza na kumharibu

mtu na, wakati mwingine, huweza hata kumfanya kuwa mtumwa wake. Mambo

haya, ndiyo yanayojitokeza kwa Zakaria, kwani anashindwa hata kutimiza

majukumu ya kuilea familia yake, kwa sababu ya unywaji wa pombe unaozidi

kipimo. Anajali pombe kuliko familia yake. Mbali na hilo, anathubutu hata kuiba

pesa iliyoandaliwa kwa ajili ya Rosa kwenda shule. Matokeo yake, anaitumia pesa

hiyo katika ulevi na nyingine anawanunulia marafiki zake pombe (kur. 18 - 19). Kwa

kufanya hivyo, anaisababishia mitanziko familia yake na kuikosesha amani, furaha

na upendo.

Vilevile, masuala ya umaskini na hali ngumu ya maisha yanajitokeza katika riwaya

ya Kichwamaji. Humu yanasababisha mtanziko katika familia ya Mzee Mafuru.

Umaskini wa familia hii unakuwa ndicho chanzo cha mtanziko wa Rukia kutokana

na familia hii kumwomba Manase aishi naye ili kuendelea na masomo yake. Hii ni

baada ya kukosa mahali pa kuishi. Kitendo hiki kinamsababishia mtanziko kutokana

na usumbufu wa Manase wa kumtaka kimapenzi. Hili linathibitishwa na Rukia

mwenyewe katika ujumbe anaomwandikia kaka yake, Kazimoto (uk. 19).

10 Mahojiano baina ya mtafiti na Dkt. Ramadhani Thomas Kadala Oktoba 1, 2019.

Yalifanyika katika viunga vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Dkt. Ramadhani

Thomas Kadala ni Mhadhiri wa Fasihi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

151

Nadharia ya Udhanaishi inatilia mkazo harakati au hali ya kukata tamaa, ambapo

huendana na kuyaona maisha kuwa ni kitu kisichokuwa na maana. Hili ndilo

tunaloliona kwa Rukia ambaye anaonekana kukata tamaa kutokana na mtanziko

unaotokana na vitendo anavyofanyiwa na Manase. Hatimaye, anajikuta katika wakati

mgumu anapobaini kuwa, ametiwa mimba pasipo ridhaa yake.

Kitendo hiki kinasababisha familia yote ya Mzee Mafuru kuwa katika mtanziko,

mara tu inapopata taarifa kwamba Rukia kuacha shule, baada ya kupata mimba.

Matokeo yake, kinasababisha Kazimoto kufikia hatua ya kutoa kauli inayoonesha

namna anavyotatizika juu ya suala hili. Anasema, ―Kulikokuwa na mwanga sasa

giza! Manase ana kiburi namna gani! Mimi ni mwanamume kama yeye!‖ (uk. 20).

Matokeo yanaonesha kuwa, hata mama yake anakumbwa na mtanziko kutokana na

tatizo hili. Kauli anayomweleza Kazimoto kwamba, ―… tuache tupumzike, tuache

tulie. Huu ni ugonjwa umeletwa na vijana na utatumaliza sisi kina mama wenye

mabinti…‖ (uk. 37), inathibitisha suala hili.

Kauli hii nzito na yenye masikitiko makubwa ndani yake, inatolewa na mama yake

Rukia, huku akilengwalengwa na machozi, kutokana na mtanziko alio nao baada ya

Rukia kutiwa mimba. Suala hili linamkosesha furaha na kumkatisha tamaa ya

maisha. Anakosa matumaini katika maisha na kuyakatia tamaa. Anaelekea kujutia

umaskini na hali ngumu ya maisha yake, inayosababisha mtanziko kutokana na

kumpeleka Rukia kuishi na Manase na kumsababishia tatizo hili.

Aidha, umaskini na hali ngumu ya maisha ya familia ya Mzee Mafuru, vinasababisha

mtanziko kwa Kazimoto ambaye anashindwa kuendelea na masomo yake akiwa

darasa la kumi kutokana na kukosa pesa. Hili linatokea mara tu baada ya kutoka

hospitalini alikokaa kwa muda wa mwaka mmoja kutokana na kuumwa ugonjwa wa

kifua kikuu. Mambo yanazidi kumwendea vibaya anaposhindwa kutimiza ndoto yake

ya kumaliza shule mwaka huo na kulazimika kutafuta kibarua. Anaeleza hivi:

Nilipotoka hospitalini nilikuwa na nia ya kusoma kufa na

kupona, lakini mwaka huo baba akashindwa kulipa ada ya

shule; shule nikaacha, nikatafuta kazi. Manase akawa sasa

miaka miwili mbele yangu (uk. 10).

152

Ni wazi kwamba hali hii ya umaskini inampa wakati mgumu Kazimoto, kwa sababu

anashindwa kutimiza malengo yake. Hivyo, nalazimika kuacha shule kwa muda ili

akatafute kazi ya kumwezesha kupata fedha kwa ajili ya kuendelea na masomo yake

ya chuo. Yote haya yanatokea kwa sababu ya umaskini na hali ngumu ya maisha ya

familia ya Mzee Mafuru.

Pia, umaskini na hali ngumu ya maisha vinamsababishia mtanziko Moyokonde

kutokana na kitendo cha Tegemea, ambaye ni mama yake Vumilia, kutaka kuondoka

na mwanaye, kwa sababu ya umaskini wake. Uamuzi huu unakuja baada ya Tegemea

kuwakuta Vumilia na Moyokonde wakiishi katika kijumba kidogo cha mabati, huku

Vumilia akiwa mjamzito. Mwandishi anaeleza:

Nyumba hii ilikuwa na vyumba viwili: cha kulala na cha

maongezi. Paa lilikuwa karibu, vile kwamba nilikaribia

kuligusa kwa kichwa. Madebe yalikuwa na matundu mengi na

nilishangaa kama kweli waliweza kulala humo wakati wa

mvua. Katika chumba cha maongezi niliona viti viwili vya

kuegemea; mtungi wa maji na kabati dogo ambamo niliona

sahani na vikombe vya chai (uk. 165).

Picha inayochorwa na mwandishi katika dondoo hili ni ya umaskini na maisha

magumu waliyo nayo Moyokonde na Vumilia. Kuishi katika nyumba ya namna hiyo

kunatokana na kukosa kipato na uwezo wa kugharamia nyumba nzuri na yenye

hadhi. Pia, afya zao dhaifu zinadhihirisha hali ya umaskini na ngumu waliyo nayo.

Mahojiano baina ya Tegemea na Vumilia yanatupa picha ya maisha wanayoishi

Vumilia na Moyokonde.

―Ulikuwa mgonjwa? Kwa nini umekonda namna hii?‖

Tegemea aliuliza. Vumilia hakujibu. ―Ulikuwa hupati chakula

cha kutosha?‖ Vumilia aliendelea kunyamaza. ―Husemi!

Mtoto huyu namna gani! Umekuwaje? Ulikuwa mgonjwa?‖

―Hapana,‖ Vumilia alijibu.

―Nimesikia umeolewa?‖ Tegemea aliuliza tena. Vumilia

alinyamaza.

―Labda wanakusingizia?‖ Tegemea aliendelea.

―Nimeolewa,‖ alijibu.

―… Unapenda kukaa naye?‖ Vumilia alinyamaza. ―Vumilia

huwezi kusumbuka hivi.‖ Tegemea alisema. ―Nimekuja

kukuchukua twende Ukerewe. Nyumbani kwetu huwezi

kukuta watu wanasumbuka hivi. Huwezi kukuta mtu anaishi

katika nyumba kama hii japokuwa ni shamba. Hivi nani

alikufukuza?‖ (uk. 165).

153

Hapa, Tegemea anakerwa sana na maisha wanayoishi Vumilia na Moyokonde. Azma

yake ya kutaka kuondoka na Vumilia kwenda naye Ukerewe inamtatiza na

kumkanganya Moyokonde, kwani anapata wakati mgumu kwa kuwa hajui la

kufanya. Anadiriki hata kulisema suala linaloleta aibu na fedheha kwa kutaka

Tegemea aondoke nao wote wawili ili akawatunze. Kama inavyoelezwa katika

nadharia ya Udhanaishi, hali hii inaonesha kuwa, amekata tamaa ya maisha kutokana

na mtanziko alio nao. Kutokana na mtanziko huo, Moyokonde anamweleza Tegemea

kuwa, yuko tayari hata kufa kama ataachwa peke yake pasipo kuishi na mke wake

Vumilia. Haya yanajitokeza katika majadiliano baina yake na Tegemea kama

ifuatavyo:

―…Mimi nitamchukua mtoto wangu tu. Mtoto wako

atakayezaliwa tutakurudishia.‖

―Hapana. Wewe ni mtu mzima mwenzangu. Mimi nilikuwa

sijapata mtoto maishani. Kumchukua Vumilia sasa ni

kuchukua maisha yangu. Mwanizika kaburini bila nguo.‖

―Lakini kama unampenda, mbona umekwishashindwa

kumlisha? Mtoto wangu hakuwa mwembamba namna hii. Na

kwa nini mnaishi katika nyumba ya kuku. Siwezi kumwacha

mtoto wangu humu.‖

―Mimi ninakubali kwamba ni maskini. Lakini hata maskini pia

hupenda. Isipokuwa siwezi kuwazuia kama mmekata shauri

kuninyang‘anya mwenzangu. Muulizeni mwenzangu.

Akikubali, basi mimi sina la kusema.‖ (uk. 174).

Majibu yanayotolewa na Moyokonde katika majadiliano haya yanaonesha namna

alivyo na wakati mgumu kutokana na mkinzano wa mawazo alio nao. Anakiri hali

yake ya umaskini kwa masikitiko makubwa yanayomfanya Tegemea amwonee

huruma kutokana na hali aliyo nayo. Kauli yake kwamba hawezi kuwazuia kama

wamekata shauri kumnyang‘anya mwenzake inaonesha wazi kuwa amekata tamaa,

na hana namna nyingine ya kufanya. Hii inadhihirisha kuwa umaskini na hali ngumu

ya maisha huweza kusababisha mtanziko. Pia, humkosesha mtu uhuru wa kujiamulia

mambo yake kama inavyoelezwa katika msingi wa tatu wa nadharia ya Udhanaishi.

Hili linathibitishwa kupitia kwa Moyokonde ambaye anafikia hatua ya kuwaeleza

Tegemea na Kazimoto kwamba, hana la kufanya kama wao wameamua

kumnyang‘anya mwenzake, yaani Vumilia. Hii inaonesha kuwa amekosa uhuru wa

kupanga na kujiamulia mambo yake mwenyewe.

154

Vilevile, tumebaini kuwa ukosefu wa ajira au kufukuzwa kazi ni tatizo lingine

linaloweza kumsababishia mhusika mtanziko. Kuhusiana na hili ni kwamba,

inapotokea mtu aliyekuwa na kazi fulani akafukuzwa au kuachishwa kazi hiyo, au

mtu anapotafuta kazi kwa muda mrefu na kuikosa, huweza hupatwa na wakati

mgumu wa kufikiria namna atakavyojikimu kimaisha. Hali hiyo husababisha

mhusika kupata msongo wa mawazo na kukata tamaa. Kutokana na hilo, wengine

huamua kujiingiza katika matukio ya ulevi wa pombe na matumizi ya madawa ya

kulevya kama njia ya kuondoa msongo wao wa mawazo. Pia, wengine huamua hata

kujiua kama njia ya kutanzua mtanziko wao. Hufikia haua hiyo kutokana na kukata

tamaa kwa kuona kuwa maisha yao hayana maana tena kama inavyoeleza nadharia

ya Udhanaishi.

Pia, tatizo la kukosa kazi linasawiriwa katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo. Hili

linamkumba Tumaini mara tu baada ya kutumia ovyo na kumaliza pesa ya urithi

aliyokuwa nayo. Kutokana na hilo, anahangaika huku na huko kutafuta kazi, bila

mafanikio yoyote. Hatimaye, anaamua kwenda kwa Dennis kumweleza kuhusu tatizo

hilo. Yafuatayo ni majadiliano baina yao:

―Siku hizi niko katika hali mbaya sana. Nimejaribu kutafuta

kazi lakini sikufanikiwa. Nimekuja kuomba msaada wako,

maana ninyi mlioko juu mna nguvu zaidi.‖

―Kazi?‖ Dennis alisema hali ameweka mkono wake juu ya

shavu, alijifanya kufikiri.

―Ndiyo, kazi,‖ Tumaini alisema, ―isipokuwa isiwe kazi ya

kufagia barabara.‖

―… nitafurahi sana kama utaweza kunipa jibu lako leo au

kesho. Niko katika hali mbaya sana bwana.‖ (uk. 81).

Matokeo yanaonesha kuwa baada ya majadiliano haya, Dennis anaamua

kumshirikisha jambo hilo mke wake, Vera, ambaye kwa wakati huo ana chuki na

hampendi Tumaini kutokana na kuwa maarufu zaidi kumzidi mume wake. Hivyo,

anafurahishwa na kitendo chake cha kwenda kuomba kazi kwa mumewe kwa

kuamini kwamba tangu wakati huo, umaarufu wake utaisha na mume wake, ndiye

atayepata umaarufu zaidi na kumzidi yeye. Kwa hiyo, baada ya majadiliano yao

wanakubaliana kwamba, apewe kazi ya kupeleleza watu wapingao serikali katika

mabaa. Hivyo, Tumaini anakubali kufanya kazi hiyo, kwa kuwa hana namna

nyingine ya kufanya. Hata hivyo, kazi hiyo inamweka katika wakati mgumu na

155

kusababisha achukiwe sana na watu, hususani wenye mabaa, pamoja na wateja wao,

kwa sababu ya kuingilia na kugusa maslahi yao. Mwishowe, anajikuta akiingia

katika mgogoro na Vera, pamoja na mmiliki wa Africans’ Royal Bar. Hawa

wanamtafutia Tumaini majambazi ambao wanampiga na kumuumiza vibaya sana

(uk. 97). Tumaini anakumbwa na matatizo haya kwa sababu ya mitanziko aliyo nayo,

inayotokana na hali yake mbaya ya kiuchumi. Hii ni baada ya kuishiwa pesa yake ya

urithi na kukata tamaa ya maisha kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi.

Utafiti umebaini kwamba, ijapokuwa mtanziko huo wa kiuchumi haumsukumi

Tumaini moja kwa moja kwenye tukio la kujiua kwa wakati huo, ni wazi kwamba

huo ulikuwa ni sehemu ya mchakato wake wa kukata tamaa ya kuendelea kuishi

kutokana na namna maisha yalivyo.

4.3.4 Sababu za Kifalsafa

Mitazamo ya kifalsafa juu ya ukweli kuhusu maisha huweza kusababisha mitanziko

kwa wahusika, na hata kwa jamii kwa jumla. TUKI (2014) inaeleza kuwa falsafa ni

elimu ya asili, maana na sababu za mambo au vitu. Nayo, Wizara ya Elimu na

Utamaduni (1992) inafafanua kuwa falsafa ni taaluma inayojishughulisha na kutafuta

ukweli wa jambo kwa njia ya kutafakari. Mantiki iliyomo katika fasili hizo ni

kwamba falsafa ni taaluma au mtazamo unaochunguza matumizi ya dhana, kupima

hoja pamoja na mbinu za ujengaji hoja. Pia, hufanya uhakiki au tathmini na

kuthibitisha au kutoa ushahidi wa hoja zinazozungumzwa na nadharia mbalimbali

zinazohusu hali halisi ya maisha kwa kuzingatia imani, mila, Desturi, pamoja na

mienendo aliyo nayo binadamu. Katika riwaya teule, Euphrase Kezilahabi anaibua

vipengele vikuu vitatu juu ya mtazamo wa kifalsafa kuhusu maisha. Vipengele hivyo,

ambavyo ni dhana ya maisha, dhana ya kifo na dhana kuhusu Mungu, vinaibua

mjadala na kusababisha mtanziko kwa wahusika kama inavyojitokeza katika kazi

hizo.

4.3.4.1 Dhana ya Maisha

Dhana ya maisha ni swali linalowashughulisha na kuwatatiza watu wengi wakiwamo

Wanatheolojia, Wanasayansi na Wanafalsafa (Muller 1964; Lepp 1968 katika

Mungah 1999, na Freeman 1971). Majibu mbalimbali yanayopingana na hata

kutofautiana yamekuwa yakitolewa kuhusiana na swali hilo. Kwa upande wa dini,

suala hili limekuwa likihusishwa na masuala ya kidhanifu yanayodai kuwa, chanzo

156

cha maisha ni Mungu au nguvu zilizo nje ya fikra za binadamu. Haya

yanathibitishwa kupitia kitabu cha Mwanzo 1: 26 - 27 katika Biblia Takatifu, 1997).

Hoja hii inaungwa mkono na Jaspers (1883 – 1986) na Darwin (1809 – 1832)

wanaodai kuwa Mungu ana nafasi kubwa katika kuyafanya maisha ya mwanadamu

yawe kama yalivyo au yanavyoonekana. Kwa mtazamo wao, maisha ya mwanadamu

hupangwa na Mungu. Aidha, kwa msingi wa dini ya jadi ya Waafrika, maisha ni

mapito kutoka ulimwengu wa kawaida kuelekea ulimwengu wa mizimu. Kwa

upande wa Wanasayansi, hususani wale wa karne ya ishirini, wakiwamo Richard

Dawkins (1941) na David Haig (1955), majibu yao yamekuwa yakihusishwa na

masuala ya utafiti, yanayojikita katika mabadiliko ya mwanadamu.

Nao Wanafalsafa, hususani wadhanaishi, wamekuwa wakidai kuwa maisha hayana

maana, na wakati mwingine hayapo, kwa sababu ni ya kuwazika tu (Camus 1954;

Beckett, 1975). Pia, hudai kwamba hakuna Mungu kabisa kwani kama angekuwapo,

angeingilia kati na kutatua shida na matatizo yanayomkumba binadamu katika

maisha yake ya kila siku. Aidha, hudai kwamba kila jambo alifanyalo mwanadamu

katika ulimwengu wake, ni kutokana na asili yake tu ya kimaumbile, hivyo Mungu

hayupo. Wanaongeza kuwa kuamini katika nguvu za Mungu ni kupoteza muda wa

kufikiri na kufanya shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Kimsingi, kutofautiana kwa mitazamo kuhusu falsafa ya maisha kumesababisha

mtanziko mkubwa kwa binadamu; na wengine wameshindwa kabisa kuamini juu ya

dhana mbalimbali zinahohusiana na maisha kwa jumla. Euphrase Kezilahabi ni

miongoni mwa watu wenye mtanziko kuhusu dhana ya maisha. Anadhihirisha jambo

hili waziwazi katika kazi zake. Kwa mfano, katika dibaji ya diwani yake ya Kichomi

(1974: xv) anasema: ―Wazo moja hasa lilinisumbua. Jambo lenyewe lilikuwa ni

swali linalohusu maana ya maisha. Swali hili liliukera sana moyo wangu.‖ Nukuu hii

inaonesha namna Kezilahabi anavyopata wakati mgumu na kukanganywa na dhana

ya maisha, kwa kuwa hata chanzo chake chenyewe hakieleweki. Mtazamo wake

kuhusu maana ya maisha kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi

unamkatisha tamaa. Hapa anawatumia wahusika kama vile Rosa Mistika, Kazimoto,

Manase, na Tumaini katika kazi zake kuendeleza mtanziko wake kwa kuyaona

maisha kama kitu kisichokuwa na maana.

157

Katika riwaya ya Kichwamaji, dhana ya maisha inasababisha mtanziko kwa Manase

na Kazimoto. Hawa wanapata mkinzano wa mawazo wa namna ya kuielewa maana

halisi ya maisha kwa jumla. Mtanziko huo unasababisha wayaone maisha kama kitu

kisichokuwa na maana, kwa kuwa hata binadamu mwenyewe anachukuliwa kama

kiumbe dhaifu na duni, na kinachoishi katika ulimwengu usiomjali. Hoja hii

inaungwa mkono na Mbatiah (1998) anayeeleza kuwa maisha ya mwanadamu

hayana maana yoyote, ni batili, ya kuudhi na ya kutatanisha. Haya ndiyo

yanayojitokeza katika nyumba ya Manase, ambapo watu wanaoishi ndani ya nyumba

hiyo, hawaoni tena thamani ya maisha. Wanayafananisha na ngozi ya simba

iliyotundikwa ndani ya nyumba hiyo. Manase anayabainisha haya anaposema:

―… mtu yeyote aonaye ngozi hii atafikiri juu ya maisha yake

lakini kwa kuwa haoni kitu tena kwa sababu ya woga,

polepole ataanza kuona kwamba maisha yake hayana maana.

Mnyama kama huyu anaweza kutunyang‘anya maisha haya

kwa urahisi sana. Kazimoto, kwa ufupi ni kwamba watu

wanaoishi katika nyumba hii hawaoni tena maana ya maisha.‖

(uk. 188).

Katika dondoo hili, Manase anadokeza hali ya kukanganya inayoikumba nyumba

yake, kiasi cha kufikia hatua ya kukata tamaa juu ya maisha. Kama inavyoelezwa

katika nadharia ya Udhanaishi, matatizo yanayoikumba nyumba yake yanakatisha

tamaa na kufikia wakati wa kuona kuwa maisha hayana maana tena. Pia, anaichora

picha ya maisha ya binadamu yalivyo magumu kwa kuhusisha na mistari iliyomo

katika picha mojawapo, iliyotundikwa ndani ya nyumba yake. Anafafanua kuwa:

―Katika picha hii utaona mistari inakwenda juu na mingine

inashuka chini; halafu mingine inatoka pembeni na

kuchanganyika katikati mfano wa mtego. Picha hii inaonyesha

jinsi maisha ya binadamu yalivyo magumu. Ukitazama vizuri

unaweza kuona picha ya mwanadamu ameshikwa katika

mtego huu kama samaki. Inaonyesha kwamba matatizo ya

binadamu magumu na hayawezi kutafutiwa jawabu kwa

urahisi. Mwanadamu kama samaki, atajaribu kujikakamua

lakini kazi bure.‖ (uk. 188).

Kuhusiana na dondoo hili tumebaini kuwa, maisha ya binadamu yanasawiriwa kama

mateso na yanasababisha mtanziko kwake, kutokana na kushikwa katika mtego kama

samaki. Anapata wakati mgumu wa kuyaelewa na kuyatunza kwa sababu ya

kupotoshwa na kuangamizwa katika kutafuta furaha. Hali hiyo ya ugumu wa maisha

158

yake ndiyo inayosababisha ayaone kama kitu kisichokuwa na maana na

kumsababishia mtanziko. Mtanziko huo unamkosesha furaha kiasi cha kuyaona

maisha yake kama adhabu inayoshinda mambo mengine yote anayokumbana nayo.

Hii inatokana na ukweli kwamba binadamu hana uwezo wa kuyaendesha na

kuyapanga maisha yake, ambayo hayajulikani mwanzo na mwisho wake. Maelezo

haya yanalandana na ya Mbatiah (1998) anayeelezea maisha ya binadamu kama

fumbo linalohitaji jitihada kubwa ili kulifumbua.

Pia, dhana ya maisha inamsababishia mtanziko Kazimoto. Huyu anafikia hatua ya

kuyaona maisha kuwa hayana maana. Hii ni kutokana na kupitia matatizo mengi

yanayompa wakati mgumu, hasa anaposaili maisha na maana yake, kama

inavyojitokeza katika majadiliano yafuatayo baina yake na Sabina.

―Mke wangu,‖ nilimwita.

―Bwana‘ngu,‖ aliitikia.

―Sijui kwa nini ninaishi.‖

―Nimechoka na maswali yako ya kijinga,‖ alisema.

―Huwezi kuishi kama watu wengine?‖ Wewe nani?‖

―Mimi sijijui,‖ nilimwambia.

―Hakika sikufahamu kwamba wewe ni kichwamaji namna hii!

Sikufahamu! (uk. 194 - 195).

Kutokana na dondoo hili, tunapata sababu mahususi zinazotufanya tuelewe ni kwa

nini Kazimoto anapata mtanziko kuhusu maisha yake. Anayaona maisha kuwa ni

adhabu na tanzia kali, ambapo anashindwa kupata njia sahihi ya kujinasua nayo.

Maswali anayohojiana na mkewe yanaonesha namna alivyokumbwa na fadhaa,

mashaka, pekecho na uchovu wa maisha kama inavyoelezwa katika msingi wa nne

wa nadharia ya Udhanaishi. Yote haya yanatokana na mtanziko kuhusiana na dhana

ya maisha unaomsukuma katika hatua ya kujiua kama suluhisho la kumaliza matatizo

yake.

Katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo, dhana ya maisha pia inajitokeza na

inasababisha mtanziko kwa Tumaini. Matatizo anayopitia katika maisha yake,

yanamfanya atafakari kwa kina juu ya dhana hii. Tafakuri hiyo inamweka katika

mkinzano wa mawazo kiasi cha kukosa majibu sahihi ya nini hasa maana ya maisha.

Matokeo yake, anafikia hatua ya kukata tamaa kwa kuona kwamba kumbe maisha

hayana maana. Hii ni kwa sababu hayampi furaha anayoihitaji baada ya kuhangaika

159

kwa muda mrefu akitafuta mali. Furaha ya muda mfupi anayoipata baada ya kujipatia

mali zake inatoweka. Hii ni baada ya kuambiwa kwamba mali hizo pamoja na

mashamba yake yanataifishwa kutokana na sera ya vijiji vya ujamaa. Hali hiyo

inamkatisha tamaa na kuona kuwa furaha ni wazo tu; ni kitu kisichoweza kupatikana,

kwani kuendelea kuitafuta ni namna ya kujitafutia maangamizo. Hili linabainishwa

kupitia mazungumzo baina yake na Dennis anapomwambia:

Tumaini la furaha ni wazo tu ambalo linaweza kusukuma

mwanadamu mbele ili kumwangamiza ama kumwendeleza.

Lakini hatalishika mkononi (uk. 163).

Dondoo hili linaonesha kwamba furaha ni wazo tu, na wala siyo hali ambayo

mwanadamu ataifikia. Hii ni kwa sababu hakuna mtu aliyewahi kufikia kiwango cha

juu kabisa cha furaha katika maisha yake. Hoja hii inaungwa mkono na Camus

(1954) anayedai kwamba furaha ya kudumu, kamwe, haiwezi kupatikana katika

maisha ya binadamu. Dhana ya maisha ya binadamu kutokuwa na furaha inaelezwa

pia na Kezilahabi kwamba:

Mwanadamu ni kiumbe ambaye amejaribu kutafuta njia nyingi

zitakazomwezesha kupata furaha. Kwa kuwa ameshindwa

kupata furaha hapa duniani amejenga kichwani mwake kitu

kama mbingu, yaani mahali anapotegemea kupata furaha

baada ya kufa (uk. 123).

Hivyo, dhana ya maisha inasababisha mtanziko kwa Tumaini, kwa kuwa anakosa

furaha; na anayaona hayana maana tena kwake. Kutokana na hilo, anaamua

kupambana na nguvu ya jamii, huku akijua kabisa kwamba, kamwe, mtu binafsi

hawezi kushindana na nguvu hizo. Anasema, ―…mimi naona afadhali tuonyeshane

nao. Watanishinda. Lakini nitakuwa nimewafunza somo…‖ (uk. 127). Kauli hii

inaonesha dhahiri kwamba amekata tamaa, na anaamua tu kupambana na nguvu

ambayo, kamwe, hawezi kuishinda. Suala hili la mtu binafsi kushindana na nguvu za

umma, linaelezwa na Mulokozi (1983) kwamba kanuni za jamii wakati mwingine

humfunga mtu binafsi na kuingilia matakwa yake na shughuli zake za kujinufaisha,

kujiendeleza, na kujitafutia furaha. Hata hivyo, anaeleza kuwa katika hilo, ni wazi

kwamba mtu binafsi, kamwe hawezi kushindana na nguvu ya umma.

Hili ndilo linaloshuhudiwa kwa Tumaini kwani, ijapokuwa anafanikiwa kumuua

Mkuu wa Wilaya matokeo yanakuwa mabaya kwake kwa sababu anaishia gerezani,

160

ambapo katika ukurasa wa 129, mwandishi anaonesha kuwa, Tumaini pia anauawa

kwa kunyongwa (uk. 129). Yote haya yanampata kutokana na mtanziko aliokuwa

nao kuhusu suala la maisha na namna yalivyo. Hivyo, maisha ya Tumaini yanaishia

katika kutokuwa na maana kama inavyoeleza nadharia ya Udhanaishi.

4.3.4.2 Dhana ya Kifo

Dhana ya kifo imemshughulisha binadamu kwa muda mrefu kiasi cha kumpumbaza

kwa karne nyingi, na kumsababishia mtanziko katika maisha yake. Mtanziko huo

unatokana na mkanganyiko anaoupata katika kuielewa dhana hiyo. Hii inatokana na

kuwapo kwa mitazamo mbalimbali ya kuachana miongoni mwa watu kuhusu dhana

hii. Baadhi ya watu huamini kwamba kuna maisha baada ya kifo, na wengine hudai

kwamba hakuna maisha baada ya kifo. Kwa mfano, Temples (1959) anaeleza kuwa,

fikra kuhusu uhai na kifo ni masuala yanayowashughulisha sana Waafrika. Hii

inatokana na kuamini kwao kwamba kifo ni matokeo ya laana inayotokana na

kupungua kwa nguvu-hai. Nao, Marealle (2002) na Mbiti (2011) wanaeleza kuwa,

Waafrika huamini kwamba kifo siyo mwisho wa maisha na kuwapo kwa mtu.

Wanafafanua zaidi kwamba, kwa Waafrika kifo ni mwanzo tu wa maisha mengine ya

mtu katika ulimwengu wa wafu hai. Naye, Menkiti (1984) anakubaliana na mawazo

ya Mbiti na anafafanua kuhusu mila na desturi za Waafrika. Anaeleza kuwa

Waafrika wanaamini kwamba kifo siyo mwisho wa uhai bali ni mwanzo tu wa

maisha menngine. Anasema:

Following John Mbiti, we can call the inhabitants of the ancestral

community by the name of the living dead. For the ancenstral dead

are not dead in the world of spirits nor are they dead in the memory of

the living men and women who continue to remember them, and who

incessantly ask their help through various acts of libation and

sacrificial offering. (uk. 174).

Kwa kufuatia mawazo ya John Mbiti, tunaweza kuwaita wakazi wa

jumuiya ya wahenga kwa jina la wafu wanaoishi. Wahenga hao

hawajafa katika ulimwengu wa kiroho, kadhalika hawajafa katika

kumbukumbu za waliohai, wake kwa waume, ambao wanaendelea

kuwakumbuka na huendelea kuomba msaada wao kupitia matendo

mbalimbali ya matambiko na kutoa sadaka. (Tafsiri ya mtafiti)

Katika andiko hili, Menkiti amefafanua juu ya imani za Waafrika katika kifo,

ambapo anaona kuwa mtu akifa anaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine wa

kiroho. Hii ina maana kuwa mwili ndio unaotengana na roho lakini roho inaendelea

161

kuwepo na kuwatembelea walio hai. Fikra hizi zinashabihiana kwa kiasi kikubwa na

Stumph na Fierser (2008) ambao wanaona kuwa roho ya binadamu ni muunganiko

wa mwili na roho.

Matokeo yanaonesha kuwa, kwa Waafrika mtazamo kuhusu maisha baada ya kifo

unakitwa katika dhana kuwa mtu anapokufa, hurudi duniani kwa kuzaliwa upya

ndani ya ukoo huo, au katika mazingira tofauti na yale aliyokulia. Hoja hii inaungwa

mkono na Faustine11

anaposema kuwa:

Imani ya Waafrika juu ya dhana hiyo ni kwamba kifo si

mwisho wa maisha, bali ni mwanzo tu wa maisha mapya

katika ulimwengu mwingine tofauti na waliouzoea.

Wanaamini kuwa mtu akifa bado huendelea kujidhihirisha

katika jamii kwa njia mbalimbali kama vile, majina, ndoto,

maono, na wakati mwingine, kwa kumwingia mtu na kumtia

wazimu.

Kwa upande wake, Mpalanzi (2019) anaeleza kwamba, misingi ya ontolojia ya

Kiafrika inazingatia imani kuwa baada ya kifo, roho za watu waliokufa huendelea

kuishi ulimwenguni. Anafafanua zaidi kuwa, kulingana na ontolojia hiyo, nafsi ya

mtu imejengwa na elementi mbili za msingi, ambazo ni mwili na roho, ambapo

wakati wa kuzaliwa mtu, mwili na roho huungana. Roho hiyo huendelea kuwapo

katika mwili wa mtu katika kuishi kwake. Baada ya mwili kufa, roho huendelea

kuwapo ulimwenguni na kuungana na miili mingine. Naye, Mihanjo (2004)

anafafanua dhana hii kuwa:

… roho ya binadamu hutoka katika ulimwengu wa roho. Roho

hiyo hushiriki katika akili na mawazo ya jumla na huunganishwa

na mwili, lakini huwa si kitu kimoja na mwili. Hata hivyo, baada

ya kifo, roho haifi. Kwa sababu hiyo, roho hutoka katika mwili

mmoja na kuingia mwili mwingine. Hii ni kwa sababu roho ni

kitu ambacho hakina umbisho. Hivyo, roho ni kitu ambacho

hakiwezi kuharibika…

11 Mahojiano baina ya mtafiti na Dkt. Stella Faustine Novemba 9, 2019. Yalifanyika

katika viunga vya Chuo Kikuu cha Dodoma. Dkt. Stella Faustine ni Mhadhiri wa

Fasihi, Chuo Kikuu cha Dodoma.

162

Katika dondoo hili, kama ilivyo kwa Faustine (keshatajwa) na Mpalanzi

(keshatajwa), matokeo yanaonesha kuwa Mihanjo pia, anakubaliana na hoja

inayoeleza kuwa, Waafrika wanaamini kwamba kuna maisha baada ya kifo. Hii ina

maana kwamba kwa asili Waafrika hulichukulia suala la kifo katika hali ya thamani

kubwa sana. Pia, huamini kwamba kifo ndiyo njia inayomfanya mwanadamu aingie

katika sehemu mpya ya maisha yake katika awamu nyingine. Vilevile, huamini kuwa

mtu hufa mwili tu na roho yake hubaki hai. Hivyo, jamaa zake huendelea

kuwasiliana naye kwa njia mbalimbali kama vile kufanya matambiko. Hii ina maana

kwamba tofauti na Wanyama wengine, Waafrika huamini kwamba hakuna kifo kwa

mwanadamu. Wao huamini kuwa, kifo ni badiliko la kiasili ambapo mtu hubadili tu

mahali pake pa kuishi. Kwa hiyo, matokeo yanaonesha kuwa kwa jumla, kifo kwa

Waafrika hutazamwa kama mchakato wa kuhama kutoka katika ulimwengu halisi na

kwenda ulimwengu dhahania.

Aidha, utafiti umebaini kwamba dini za kigeni zinaamini kuhusu kuwapo kwa

maisha ya kiroho baada ya kifo. Imebainika kwamba kulingana na imani ya dini

hizo, mtu aliyeishi hapa duniani bila dhambi, atakapokufa ataishi maisha mengine

yaliyo bora zaidi katika ulimwengu wa kiroho. Mpalanzi (2019) analielezea hili kwa

kurejelea katika Kurani na Biblia. Anafafanua kuwa Kurani inatetea hoja ya kuwapo

kwa maisha baada ya kifo na kwamba mtazamo huo, unatetewa na kauli ya Allah

anaposema: ―Kila kilicho juu ya ardhi ni chenye kufa‖ (taz. Surat Al-Rahman, aya ya

27). Kwa kuzingatia mtazamo huo, ni dhahiri kwamba Uislamu unaamini maneno ya

Allah yanayosema kuwa: ―Kila nafsi itaonja mauti.‖ (taz. Surat Anbiya, aya ya 35).

Hii ni kwa sababu kwa desturi, hakuna uhai usiokuwa na mauti. Hivyo, Uislamu

unaamini kuwa siku ya kufufuka, mfu atarudishiwa uhai wake na kuhukumiwa

kutokana na matendo yake aliyoyafanya hapa duniani. Kuhusiana na hili wao

huamini kwamba watenda mema watakwenda mbinguni, na waovu watakwenda

motoni kuadhibiwa kutokana na kushindwa kumtii Mungu na Mtume wake.

Hali kadhalika, suala la kifo na maisha baada ya kifo linaelezwa katika imani ya dini

ya Kikristo. Kwa mfano, Biblia Takatifu inafundisha kuhusu theolojia ya imani ya

kuwapo kwa maisha baada ya kifo. Hapa tutatoa mifano michache, katika (Luk. 16:

19 – 31), ambapo katika kifungu hicho kuna kisa kinachohusu mtu tajiri na maskini

Lazaro. Inaelezwa kwamba watu hawa walipokufa, tajiri alikwenda kuzimu na

163

Lazaro akaenda mbinguni au paradiso. Pia, katika Injili ya Yohana, Yesu anasema:

―Mimi ndiye ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi ajapokufa, atakuwa anaishi‖

(Yoh. 11: 23 – 27). Mifano hii michache inaonesha kuwa kundi hili kama ilivyo kwa

Waafrika na kwa Waislamu, nalo linaamini kuwa mtu akifa hupumzika tu kaburini

akisubiri ufufuo wa Yesu, na kwamba baada ya hapo maisha yake yataendelea tena.

Maandiko hayo yanasema: ―… nao waliokufa watafufuliwa kwanza. Kisha, sisi tulio

hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao‖ (1Thes. 4: 13 – 18) katika Biblia Takatifu,

(1997).

Kwa jumla, matokeo yanaonesha kwamba suala la kuwapo kwa maisha baada ya

kifo, lilikuwapo tangu enzi na lilikuwa na msingi wa imani za kijadi za Waafrika.

Kutokana na maelezo hayo imebainika kwamba suala hili limeendelea kupewa

msukumo mpya na dini za kigeni, yaani dini zilizoletwa na wakoloni kwa mwavuli

wa Umisionari. Hata hivyo, utafiti umebaini kwamba ujio wa dini hizo, pamoja na

jitihada za kujaribu kuidhoofisha imani ya Waafrika kuhusu suala la kifo na maisha

baada ya kifo, haitofautiani na mtazamo uliojengeka katika imani hiyo ya dini za

kigeni.

Kwa upande mwingine, Kipacha (2019) anaelezea mtazamo wa wadhanaishi kama

vile Nietzsche (1844) na Kezilahabi (1944), wanaoonesha mawazo tofauti juu ya

dhana ya kifo. Wao wanapinga suala la kuwapo kwa maisha baada ya kifo na

kuwako kwa uwili wa mwili na roho. Hoja hii inaungwa mkono na Kahigi na

Mulokozi (1979) katika Mnenuka (2011) wanapoeleza kuwa, maisha ya binadamu

yanaanza na kuishia hapahapa duniani. Wanafafanua zaidi kuwa, kama ilivyo kwa

viumbe vingine, baada ya kufa binadamu huoza na kuwa udongo, na huo ndio

unakuwa mwisho wa historia ya maisha ya binadamu huyo. Hii ni sawa na kusema

kuwa maisha ya mwanadamu hupotea kama moto unavyopotea ukizimika. Kwa

upande mwingine, Mulokozi (2017) anaona kuwa pamoja na kuwapo kwa fikra za

maisha baada ya kifo, maisha hayo ni dhahania kwa kuwa maisha halisi ni ya hapa

duniani. Anafafanua zaidi kuwa, hakuna pepo wala jehanamu na wala hakuna tunzo

wala adhabu baada ya kufa. Kwamba mtu hutunzwa au kuadhibiwa awapo hapahapa

duniani. Hivyo, mwanadamu akifa ndio mwisho wa maisha yaliyo halisi. Kwa hiyo,

utafiti umebaini kwamba kuwapo kwa mitazamo inayoachana juu ya dhana ya kifo,

ndiko kunakosababisha mtanziko miongoni mwa wahusika katika riwaya teule.

164

Mitanziko hiyo huweza kusababisha wengine kuchukua maamuzi ya kujiua kama

suluhisho la maisha yao.

Katika riwaya ya Kichwamaji, utafiti umebaini kuwa dhana ya kifo inasababisha

mtanziko kwa Kazimoto. Anajikuta katika mkinzano wa mawazo anapoambiwa na

Kalia kwamba mtu akifa, huendelea kuishi, kwa kuwa kufa ni kubadilika hali. Kalia

anayasema haya wakati akimsimulia Kazimoto kuhusu ndoto yake aliyoota akijikuta

yuko Mbinguni, huku akiwa na watu wengine waliokwisha kufa, lakini wakiwa hai.

Anasema:

―… Hata! mara fulani fulani Mungu mpenzi alikuwa

anaturuhusu kuja ulimwenguni. Tuliwaona watu, lakini wao

walikuwa hawawezi kutuona. Halafu tulirudi. Tulipokuwa

tunafika mahali fulani mara hali yetu iligeuka tulikuwa

tumezoea kuiita ―kupokelewa na Mungu mpenzi.‖ ―Bado

sijaelewa, yaani mlikuwa mnatembea kwa miguu?‖

―Hapana, tulikuwa tunakwenda tu, hali yetu ilizoea kugeuka

na tukajiona mbinguni tena.‖ (uk. 75).

Dondoo hili linaonesha namna Kazimoto anavyopata wakati mgumu kuelewa dhana

ya kifo. Hii inatokana na mtazamo alio nao kwamba mtu akifa hawezi kuendelea

kuwa hai tena. Anasema: ―Mimi naamini kila kitu kilicho na mwanzo kina mwisho.

Na kifo ndio mwisho kwa mwili wa binadamu, roho inabaki lakini haigeuki tena‖

(uk. 123). Hivyo, kutofautiana kwa mtazamo wake na Kalia kunamfanya ashindwe

kupata majibu sahihi kuhusiana na dhana hii ya kifo. Tunaelezwa kwamba, baada ya

majadiliano yao, Kazimoto anajikuta katika mtanziko, huku akifikiria mambo kama

vile: Mosi, kwamba kufa ni kugeuka hali. Pili, kwamba waliokufa tuko karibu nao,

lakini hatuwezi kuwaona kwa sababu hali yetu haijageuka (uk. 75). Udadisi na

mkanganyiko anaoupata juu ya dhana ya kifo unamweka katika mtanziko kutokana

na mkinzano wa mawazo anaoupata.

Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa mtanziko wa Kazimoto hauishii katika

majadiliano yake na Kalia pekee, bali anatatizwa pia na dhana hii baada ya

kukumbwa na matatizo ya kufiwa na dada yake, Rukia. Hapa anaikumbuka ndoto ya

Kalia na inamfanya azidi kutatizika. Kutokana na ndoto hiyo anajikuta akizama

katika tafakuri nzito kuhusiana na namna kifo chake kitakavyomjia. Anaeleza hivi:

165

―Usiku nilianza kufikiri juu ya kifo. Nilifikiri jinsi kifo changu

kitakavyonijia - kwa ugonjwa, kwa ajali au kwa kukatwakatwa

na wezi? Labda kwa uzee au kwa sumu! Huenda nikajiua

mwenyewe! Niliikumbuka ndoto ya Kalia. Niliwakumbuka

wale ng‘ombe, sisimizi, nyuki na mengine mengi niliyoyaona

huko machungani. Niliona kwamba adhabu kubwa ya

mwanadamu ni maisha yenyewe. Nilikumbuka mlevi mmoja

niliyemkuta akipiga mti mweleka mpaka akaumia mwenyewe.

Maisha ndiyo yaliyokuwa yakimsumbua, wala siyo pombe.

Wakati huo usiku niliyaona maisha kuwa chanzo cha yote.‖

―Hii ni adhabu ambayo kila mwanadamu amepewa kutunza

maisha yake. Maisha ambayo hayashibishwi wala

kuridhishwa. Zaidi ya hayo mwenye nguvu anatunyang‘anya

wakati wote bila hata kutuarifu.‖ (uk. 84).

Katika dondoo hili, tunaona namna Kazimoto anavyopata wakati mgumu katika

kuitafakari dhana ya kifo. Anakatishwa tamaa na dhana yenyewe, kwani, licha ya

kushindwa kueleweka kwake, bado mwanadamu hana hiari na uamuzi juu ya kifo

chenyewe. Anafikia hatua ya kuona kwamba: ―Mwisho wa mwanadamu utaletwa na

mwanadamu mwenyewe‖ (kur. 84 - 85). Kauli hii siyo tu kwamba inaonesha kukata

tamaa kwake katika kutafakari juu ya kifo kama inavyoelezwa katika nadharia ya

Udhanaishi, bali inaonesha pia, namna dhana yenyewe inavyomweka katika

mtanziko.

Vilevile, dhana ya kifo inamsababishia mtanziko Kazimoto, hususani, anapoihusisha

na mtazamo wa wazee walioishi hapo zamani. Kinachomsumbua zaidi ni namna

wazee hao walivyoyatazama maisha ya mtu baada ya kufa. Kutofautiana kwake na

wazee hao kimtazamo juu ya dhana hiyo kunampa wakati mgumu kwa kuwa, hapati

jibu sahihi kuhusiana na jambo hilo. Hili linathibitishwa katika majadiliano baina

yake na Manase kama ifuatavyo:

―Zamani wazee wetu walikuwa wakiamini kwamba mtu

alikufa na kuzaliwa tena. Yaani, kulikuwa na hali kama ya

duara. Lakini mimi nimeanza kuamini kwamba hali yenyewe

ni mstari usio na mwisho. Ni hali ya kwenda mbele bila kurudi

nyuma.‖

―Ninaamini kwamba kufa ni kugeuka hali. Kama kufa ni

kugeuka hali ninaamini kuwa kuna kugeuka na kugeuka na

kugeuka. Ndiyo maana ya mstari usio na mwisho. Kwa hiyo

sioni kwa nini mbingu iwepo baada ya kufa ambayo ni hatua

moja tu, na labda ya kwanza katika kugeuka kwa viumbe.

Kwa nini isiwepo baada ya hatua ya pili?‖

166

―Mimi ninaamini kila kitu kilicho na mwanzo kina mwisho.

Na kifo ndio mwisho kwa mwili wa binadamu, roho inabaki

lakini haigeuki tena. Kwani huo mstari usio na mwisho

ulianzaje? Kama una mwanzo basi utakuwa na mwisho.‖

―Tunaweza kusema kwamba mstari huo una mwanzo, lakini

mwisho wake haujulikani. Kifo siyo mwisho wa binadamu, ni

tukio fulani katika mfululizo wa kugeuka kwa viumbe.‖ (uk.

123).

Kwa kuzingatia ujumbe uliomo katika dondoo hili tumebaini kuwa, mwandishi

anaonesha namna dhana ya kifo inavyosababisha mtanziko kwa Kazimoto. Hii

inatokana na mtazamo wake kuhusiana na dhana hiyo, kutofautiana na ule wa wazee

wanaoamini kuwa, kifo ni mwanzo wa maisha mapya. Kazimoto kwa upande wake

anatofautiana nao, kwa sababu anaona kuwa kifo ndio mwisho wa maisha ya

mwanadamu hapa duniani. Mkinzano huu wa mawazo, ndio unaompa wakati mgumu

wa kuielewa dhana ya kifo. Matokeo yake ni kwamba mtanziko huo unamsukuma

katika kufikia maamuzi ya kujiua kwake.

4.3.4.3 Dhana Kuhusu Mungu

Dhana ya kuwako au kutokuwako kwa Mungu imeishughulisha akili ya mwanadamu

tangu kuumbwa kwa ulimwengu huu hadi sasa, na ni miongoni mwa sababu za

mitanziko ya wahusika katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi. Hii inatokana na

ugumu uliopo katika kuielewa na kuielezea dhana hii, kwa sababu inahusiana na

mambo ya asili, pamoja na ukweli wa maarifa. Hoja hii inaungwa mkono na

Chuachua (2016) anayeeleza kuwa Mungu ni mojawapo ya dhana ngumu za

kifalsafa, na kwamba inaweza kuelezeka kiontolojia. Hii ni kwa sababu, Mungu

anasawiriwa na kuelezwa na jamii mbalimbali duniani kote kuwa, ni mwanzo wa

kuwapo na kuendelea kwa vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana. Falsafa ya

Kiafrika inadhihirisha kuwa jamii za Kibantu huamini kuhusu uwepo wa Mungu.

Inaeleza kuwa, hata kabla ya majilio ya wageni kutoka nje ya bara hili la Afrika,

Wabantu walikuwa na Mungu wao waliyemwamini, waliyehusiana na kushirikiana

naye katika shughuli zao za kila siku. Kwa mtazamo wa kiontolojia, Mungu

anasawiriwa na kuelezwa na jamii mbalimbali duniani kote kuwa ni mwanzo wa

kuwapo na kuendelea kwa vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana.

Chuachua (k.h.j) anaelezea mtazamo wa Idowu (1973) kuhusu Mungu kwamba:

Katika utamaduni wa Kiafrika, Mungu ndiye kiumbe mkuu na kibainishi cha dini

167

yao. Pia, ni mtawala, muumbaji wa dunia, na chanzo cha kuwapo kwake. Anaongeza

kuwa, katika utamaduni wa Kiafrika, Mungu ni halisi zaidi ya vitu vyote na hutajwa

mara nyingi katika sala, hususani wakati wa matatizo. Mawazo ya Idowu

hayatofautiani na ya Temples (1959) anayedai kwamba dhana kuhusu Mungu

inapoelezwa kwa mtazamo wa Kiafrika, yafaa ieleweke kwamba Mungu ni nguvu

kuu kuliko nguvu zote, na ni chanzo cha kuwapo kwa kila kitu ulimwenguni.

Kwa upande mwingine, Mbiti (1995) anabainisha namna jamii za Kiafrika

zinavyoielezea dhana kuhusu Mungu. Anaeleza kuwa, kwa Wazulu na

Wanyarwanda, Mungu hujulikana kama ni ―Mwenye Hekima‖, kwa Waakan ni

―Mjua Yote au Mwona Yote‖, Wayoruba huamini kwamba ―Mungu pekee ndiye

aliye na busara, na ndiye huamua mwelekeo wa moyo wa mtu‖ na ndiye huona yale

yote yaliyomo moyoni mwa mtu. Wakikuyu wao huamini kuwa Mungu hana baba

wala mama, pia hana mke wala watoto. Aidha, Mungu siyo mtoto wala mzee, na

kamwe huwa habadiliki. Aonekanavyo leo, ndivyo alivyokuwa jana na juzi. Kwa

mtazamo wa Mbiti, Mungu ana umri mkubwa kuliko dhana ya nyakati za zamani; na

kwamba yupo nje ya uumbaji wake. Pia, hadhi yake inaupita huo uumbaji wake.

Kwa maneno mengine, kwa kila hali, Mungu ana hadhi ya juu sana kupita vitu na

viumbe vyote alivyoviumba.

Kwa jumla, katika kujibu swali la Mungu ni nani, Katekisimu ya Kanisa Katoliki

(1998) inasema: ―Mungu ni muumba wa mbingu na dunia, muumba wa watu na vitu

vyote na ni Baba mwema.‖ Katika fundisho hilo la kanisa Katoliki, Mungu

anaelezwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi na Baba mwema wa wanadamu.

Kimsingi, katika dini ya Kikristo, Mungu anaitwa majina mengine kama vile

Mwenyezi, Mwenye Enzi, Bwana, Yehova, na Yahwe. Kwa upande wake, Mpalanzi

(2019) anaeleza kuwa, kwa mujibu wa dini ya Kiislamu, kuna majina 99 ya

kumrejelea Mungu. Baadhi ya majina hayo ni Allah, Al Rahman, Rabuka, na Maliki.

Anafafanua zaidi kwamba kwa kawaida majina hayo huwa na maana ya ndani ya

kuelezea sifa na tabia zake. Kwa mfano, katika Kurani Tukufu, Mungu anaelezwa

katika sura ya 40 (Al Ghafir). Aya ya 64 inasema:

Ni Mwenyezi Mungu aliyekufanyieni ardhi kuwa ni pahala pa

kukaa na mbingu kuwa dari. Na atakutieni sura, na akazifanya

nzuri sura zenu, na akakuruzukuni vitu vizuri. Huyo ndiye

168

Mwenyezi Mungu Mola wenu Mlezi. Basi ametukuka

Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Nukuu hii inaonesha dhahiri kuwa Mungu ndiye muumba wa binadamu na vitu vyote

vya duniani na mbinguni. Pia, ni Mtukufu na mtunzaji wa watu na vitu vyote

alivyoviumba. Hivyo, utafiti umebaini kuwa mitazamo ya kidini na ya watu

mbalimbali kuhusiana na dhana waliyo nayo juu ya Mungu, ndiyo inayosababisha

pia, wahusika katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi kupata mitanziko juu ya

dhana hiyo, na wengine kujiua kwa kuona kuwa hakuna Mungu.

Katika riwaya ya Kichwamaji, dhana kuhusu Mungu inasababisha mtanziko kwa

Kazimoto kutokana na madai yake kwamba hakuna Mungu. Hoja hii inamweka

katika wakati mgumu, kwa sababu mtazamo wake unakinzana na mawazo ya wazee

anaojadiliana nao, kiasi cha kuvuruga hata mazungumzo baina yao. Kutokana na

mkinzano huo, mzee mmoja miongoni mwao anaamua kuondoka, huku akitupatupa

mikono yake juu kuonesha kuwa hakubaliani na fikra za Kazimoto. Anasema:

―Mnazungumza na mwehu!‖ Alisema kwa kelele. ―A!

Anasema kwamba hakuna Mungu. Hakuna Mungu! Mtoto wa

nani? Mababu na mababu wamekwenda; wamechukuliwa na

nani? Bangi!‖ (uk. 51).

Hapa mwandishi anaonesha kuwa suala la kuamini juu ya uwepo wa Mungu ni

gumu, kwani kuna mitazamo inayotofautiana juu ya dhana hii. Kutofautiana huko

ndiko kunakosababisha Kazimoto akose jibu sahihi kuhusiana na kuwapo au

kutokuwapo kwa Mungu. Mtanziko wake hauishii katika majadiliano na wazee hao

pekee, bali unajitokeza pia katika majadiliano baina yake na Kalia. Mtanziko huo

anaupata kutokana na namna Kalia anavyoisimulia ndoto yake inayoelezea kuhusu

Mungu. Maelezo yake yanamkanganya Kazimoto na anashindwa kuelewa vizuri

kuhusiana na Mungu anayeelezwa na Kalia. Hili linabainishwa kupitia majadiliano

yao kama ifuatavyo:

―Ulivyoona wewe mbingu iko mbali na dunia?‖

―Hata! Mara fulani fulani Mungu mpenzi alikuwa anaturuhusu

kuja ulimwenguni. Tuliwaona watu, lakini wao walikuwa

hawawezi kutuona. Halafu tulirudi. Tulipokuwa tunafika

mahali fulani mara hali yetu iligeuka tukajiona mbinguni tena.

Hali ya kugeuka tulikuwa tumezoea kuiita kupokelewa na

Mungu Mpenzi.‖

169

―Bado sijakuelewa, yaani mlikuwa mkitembea kwa miguu?‖

―Hapana, tulikuwa tunakwenda tu, hali yetu ilizoea kugeuka

na tukajiona mbinguni tena.‖

―Mlikuwa mnakwenda tu namna gani?‖

―Kwa nini huelewi?‖

―Kwa nini kila mara unasema Mungu Mpenzi?‖

―Kwa sababu tulipokuwa mbinguni tuliona kwamba Mungu

anatupenda vile kwamba tuliona vigumu kumkosea kwa

sababu ya aibu kubwa.‖ (uk. 74).

Majadiliano haya yanaonesha namna Kazimoto anavyopata mtanziko kuhusu dhana

ya Mungu, kwani licha ya kupewa ufafanuzi wa kutosha, bado anaonekana kuwa

mgumu kuielewa. Kutofautiana kwake kimtazamo na namna Kalia anavyoielezea

dhana hiyo inayohusu Mungu, ndiko kunakompa wakati mgumu wa kuielewa dhana

hii. Hii ni kwa sababu haamini kuhusu kuwapo kwa Mungu anayedaiwa kwamba,

ndiye muumba wa ulimwengu kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi.

Vilevile, mtanziko wa Kazimoto kuhusiana na dhana ya Mungu unajitokeza katika

majadiliano baina yake na Manase. Maelezo ya Manase kwamba Mungu hawezi

kufahamika kwa kutumia akili za kawaida yanampa Kazimoto wakati mgumu na

anakosa jibu sahihi kuhusu dhana ya Mungu. Kwa Kazimoto, maelezo ya Manase

yanaonekana ni kama imani ya kinjozi tu, juu ya maana halisi ya maisha kwa

kuyahusha na Mungu kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi.

Majadiliano yafuatayo yanabainisha mtanziko wake juu ya dhana hii:

―Unafikiri nini juu ya watu wasioamini kwamba Mungu

yupo?‖

―Ni wajinga,‖ Manase alisema mara moja.

―Hivi wewe unafikiri mtu asiyeamini Mungu ni mtu gani?‖

Nilimuuliza.

―Ni mtu ambaye anataka kumfahamu Mungu kwa kutumia

kichwa chake. Mungu hawezi kueleweka kwa akili.‖

―Hapo ndipo sikubaliani nawe. Mtu asiyeamini Mungu ni mtu

asiyeamua kuwako kwa Mungu kwa kutumia milango ya

fahamu peke yake. Licha ya milango ya fahamu mtu

asiyeamini Mungu anatumia akili zake. Mimi naona kwamba

bongo pia zaweza kukosea.‖

―Ndiyo, lakini milango ya fahamu ni zaidi. Ndiyo maana

ninasema kwamba lazima vyote viwili viafikiane. Na ndivyo

mtu asiyeamini Mungu afanyavyo. Milango ya fahamu ipo

kusaidiana na ubongo, lakini bongo lazima zikuchukue nafasi

kwanza baada ya kuafikiana.‖

170

―Sioni kwa nini umeingiza ndani mambo ya milango ya

fahamu?‖ Aliuliza.

―Unaona, Manase; mwanadamu ameamua kwamba kuna

Mungu kwa sababu ya hali yake ya woga iletwayo na milango

ya fahamu. Kwa hiyo mtu anayeamini kwamba Mungu yupo

ni yule aamuaye kwa kufuata milango ya fahamu zake. Kwake

fahamu zinatawala bongo.‖

―Kama ni vile basi, ninaona kwamba awezaye kutueleza vizuri

zaidi juu ya jambo hili la Mungu ni yule ambaye fahamu zake

zinakubaliana na bongo. Hakuna kinachochukua nafasi ya

kwanza.‖ Kazimoto aliendelea:

―Woga umeleta Mungu,‖ niliendelea kufikiri, ―Na woga

umeletwa na mambo yote yanayomzunguka mwanadamu. Na

ujasiri je unaleta nini? Nafikiri unaleta kutoamini Mungu.

Ujasiri umeletwa na juhudi ya mwanadamu katika kuyashinda

mambo mabaya. Kwa hiyo sayansi inaweza kutusaidia

kuelewa jambo hili ingawa ni polepole (kur. 124 - 125).

Pia, Kazimoto anaonekana kuwa ni mfuasi mzuri wa nadharia ya Udhanaishi,

ambayo haiamini kuhusu uwapo wa Mungu anayedaiwa kuwa ndiye muumba wa

ulimwengu kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi. Mazungumzo baina

yake na Manase yanaonesha namna anavyopata mtanziko katika kuamini kuhusu

uwapo wa Mungu. Kauli ya Manase kwamba wasioamini Mungu ni wajinga, kwa

sababu hutumia vichwa vyao tu ili kumwelewa, inampa wakati mgumu zaidi.

Anatofautiana naye kimtazamo kuhusiana na dhana ya Mungu kutokana na fikra

zake kwamba wanaofikiri kuwa kuna Mungu ni waoga. Hii ni kwa sababu

husukumwa tu, na milango yao ya fahamu kuamini na kufikiri hivyo. Mkinzano wa

mawazo baina yake na Manase unasababisha mtanziko na anakosa jibu sahihi la

kumfanya aamini iwapo kuna Mungu au la. Matokeo yanaonesha kuwa,

mkanganyiko anaoupata Kazimoto kuhusu kuwapo au kutokuwapo kwa Mungu, ndio

unaochangia katika mchakato wa baadaye wa kujiua kwake.

Aidha, dhana kuhusu Mungu inasababisha mtanziko kwa Kazimoto kutokana na

kupitia changamoto mbalimbali katika maisha yake. Changamoto hizo zinampa

wakati mgumu kiasi cha kuhoji nafasi ya Mungu katika maisha yake, ambaye haoni

wala hamtatulii matatizo yake kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi.

Kitendo cha kufiwa na mtoto wake kinampa msukumo zaidi wa kutafakari juu ya

Mungu. Mwandishi kupitia kinywa cha Kazimoto anasema:

171

―Nilianza tena kufikiri juu ya Mungu. Kama kweli alikuwapo

sikuona kwa nini aliweza kufanya ukatili mkubwa kama huo.

Matumaini yetu yote; kazi na taabu tuliyopata yote hayo chini!

Sikuona maana ya maisha.‖ (uk. 180).

Msingi wa kwanza wa nadharia ya Udhanaishi unajadili matatizo halisi

yanayomkumba binadamu, kiasi cha kumkatisha tamaa na hata kusababisha mauti.

Hili ndilo linalompata Kazimoto, kwani anakata tamaa kuhusu maisha kwa kuwa,

haoni tena thamani na nafasi ya Mungu kwake. Anafikia hatua hii kutokana na

mtanziko alio nao kuhusu dhana ya Mungu. Matokeo yake anapanga kuchukua hatua

ya kwenda mahali atakakoishi bila kufikiri wala kujua kwamba anaishi. Kulingana

na utafiti huu, uamuzi huo ni mchakato wake wa kujiua. Suala hili kama

lilivyojadiliwa katika kipengele cha 4.2.2.3, linasawiriwa kupitia majadiliano baina

yake na Sabina (uk. 180).

Majadiliano hayo ni uthibitisho wa wazi kwamba, dhana kuhusu Mungu

inamsababishia Kazimoto mtanziko na anakata tamaa ya maisha kama inavyoelezwa

katika nadharia ya Udhanaishi. Haamini kuhusu uwapo wa Mungu anayedaiwa

kwamba ndiye muumba wa ulimwengu. Hii ni kwa sababu uwapo huo kimsingi

haumjali, bali unampa wakati mgumu kwa sababu ya kupitia changamoto nyingi

katika maisha yake. Kutokana na hilo, anajikuta katika wakati mgumu wa kufanya

uchaguzi wa ama kuendelea kuishi, au kuondoka duniani na kwenda mahali ambako

ataishi bila kufikiri na kuishi pasipo kujua kama anaishi. Hivyo, utafiti umebaini

kwamba mtanziko alio nao Kazimoto kuhusu kuwapo au kutokuwapo kwa Mungu,

ndio unampa msukumo wa kujitafutia uhuru wake kwa nguvu kama inavyoelezwa

katika nadharia ya Udhanaishi na kumwingiza katika mchakato wa kujiua kwake. Hii

ni kwa sababu haoni na haamini kuhusu kuwapo kwa Mungu.

Vilevile, dhana kuhusu Mungu inajitokeza katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo.

Humu inasababisha mtanziko kwa Tembo na wenzake. Hawa wanapata wakati

mgumu kuelewa kuhusu Mungu kutokana na vitendo vinavyohusiana na Mungu,

vinavyofanywa kanisani. Mjadala huo unabainishwa na mwandishi kama ifuatavyo:

―Lakini mimi jambo moja linanishangaza. Siku moja niliingia

kanisani nikaona watu wanapewa vijidudu fulani mdomoni,

hivi ni nini?‖

172

―Mimi zamani nilifikiri ni shilingi. Lakini nilisikia

wanavitafuna,‖ mtu mmoja alisema.

―Wanasema kuna Mungu‖ mwingine aliongeza.

―Ha! Ha!‖ watu walicheka.

―Mbona mtoto wangu Dennis alikaleta nyumbani

tukakachoma kakaungua! Mungu wao yukoje? Kasala alisema.

―Mtoto wangu,‖ Mulele alisema, ―Alipokuwa karibu kupewa

vijitu hivyo alizoea kunung‘unika kwamba mapadre wachoyo

wanakula kipande kikubwa kuliko wengine.‖ (uk. 37).

Kutokana na dondoo hili, tunabaini namna dhana kuhusu Mungu inavyosababisha

mtanziko kwa Tembo na wenzake. Kauli ya mmoja wao kwamba ―… Wanasema

kuna Mungu‖ ni uthibitisho wa wazi kwamba watu hawa hawaielewi vizuri dhana

hiyo inayohusiana na Mungu. Utafititafiti umebaini kwamba, Wakristo, hususani wa

dhehebu la Katoliki, wana desturi ya kula chakula hicho kinachowatatiza Tembo na

wenzake. Kanisa hilo huamini kuwa katika maumbo ya mkate na divai, ndimo

anamopatikana Yesu Kristo, ambaye ni mwana wa Mungu na Mungu kweli. Hili

linathibitishwa katika Biblia Takatifu (1997). Tunaelezwa kuwa:

Nao walipokuwa wakila, Yesu alitwaa mkate, akabariki,

akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, ―Twaeni, mle;

huu ndio mwili wangu.‖ Akakitwaa kikombe, akashukuru,

akawapa, akisema, ―nyweeni nyote katika hiki; kwa maana hii

ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi

kwa ondoleo la dhambi…‖ (Mathayo 26: 26 - 29; Marko 14:

22 - 24; Luka 22: 17 - 20).

Kitendo hiki cha kula mwili wa Yesu, ndicho kinachosababisha mtanziko kwa

Tembo na wenzake. Hii ni kwa sababu, katika hali ya kawaida kinachoonekana

katika macho yao ya kawaida ni mkate halisi, lakini maelezo yanayotolewa yanadai

kuwa, huo ni mwili wa Yesu. Aidha, inaelezwa kwamba tukio la kuugeuza mkate

kuwa mwili wa Yesu, na divai kuwa damu yake, lilifanywa na Yesu mwenyewe

alipokula karamu ya mwisho pamoja na wanafunzi wake. Tukio hili lilifanyika siku

moja kabla ya kufa kifo cha mateso na cha aibu msalabani. Hivyo, kumbukumbu

hiyo hufanyika kupitia mkate na divai, ambavyo kwa imani yao, hugeuzwa na kuwa

mwili na damu ya Yesu. Kwa msingi huo, tukio hili hupewa heshima na thamani

kubwa, kwani mara nyingi waumini hao wapokeapo mwili na damu hiyo, wakati

mwingine hulazimika kupiga magoti na kusali kwa utulivu. Kwa muktadha huo,

dhana hii ni ngumu kueleweka hata kwa baadhi ya madhehebu ya dini, yenye

mtazamo tofauti juu ya imani hiyo.

173

Aidha, katika mafundisho ya imani ya Kikristo, inaaminika kwamba Mungu ni

mmoja, lakini amegawanyika katika nafsi tatu; Mosi, Mungu Baba ambaye ndiye

muumbaji wa mbingu na dunia (Mwanzo 1: 1- 31 katika Biblia Takatifu, 1997). Pili,

Mungu Mwana, yaani Yesu Kristo, ambaye ndiye aliyetumwa na Mungu Baba kuja

duniani kuwakomboa wanadamu kutokana na dhambi zao (Mathayo 3: 16 - 17 katika

Biblia Takatifu, 1997). Na, tatu, Mungu Roho Mtakatifu, ambaye huwaimarisha

waumini kwa kuwafundisha na kuwakumbusha mafundisho ya Yesu (Yohana 20: 19

- 23 katika Biblia Takatifu, 1997). Waumini hao hukiri fumbo hili wanaposali sala ya

Kanuni ya Imani inayosema:

Nasadiki kwa Mungu mmoja, Baba Mwenyezi, Muumba

mbingu na nchi, na vitu vyote vinavyoonekana na

visivyoonekana. Nasadiki kwa Bwana mmoja Yesu Kristo,

Mwana wa pekee wa Mungu, aliyezaliwa kwa Baba tangu

milele yote. Mungu aliyetoka kwa Mungu, mwanga kwa

mwanga, Mungu kweli kwa Mungu kweli. Aliyezaliwa bila

kuumbwa, mwenye Umungu mmoja na baba, ambaye vitu

vyote vimeumbwa naye. Ameshuka toka mbinguni kwa ajili

yetu sisi wanadamu, na kwa ajili ya wokovu wetu; akapata

mwili kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, kwake yeye Bikira

Maria, akawa mwanadamu. Akateswa kwa mamlaka ya

Ponsyo Pilato, akasulubiwa, akafa akazikwa, akashukia

kuzimu, akafufuka siku ya tatu, kama ilivyoandikwa. Akapaa

mbinguni, amekaa kuume kwa Baba, atakuja tena kwa

utukufu, kuwahukumu wazima na wafu, nao ufalme wake

hautakuwa na mwisho. Nasadiki kwa Roho Mtakatifu Bwana

mleta uzima, atokaye kwa Baba na Mwana, anayeabudiwa na

kutukuzwa, pamoja na Baba na Mwana, aliyenenwa kwa

vinywa vya Manabii. Nasadiki kwa kanisa moja Takatifu

Katoliki la Mitume, naungama ubatizo mmoja, kwa

maondoleo ya dhambi. Nangojea na ufufuko wa wafu na

uzima wa milele ijayo. Amina (Misale ya Waumini, 1993:

424).

Kwa hakika, dhana kuhusu Mungu ni ngumu kueleweka na inasababisha mtanziko

kwa Tembo na wenzake. Matokeo yake wanajikuta katika wakati mgumu wa kupata

jibu sahihi kuhusiana na dhana hiyo kutokana na mkinzano wa mawazo,

unaowakanganya na kuwatatiza. Wanakosa jibu sahihi kuhusu Mungu anayepatikana

katika umbo la mkate, na ndiyo maaana wanacheka, huku wakikejeli na kuonesha

dharau juu ya chakula hicho. Hivyo, kwa kuzingatia nadharia ya Udhanaishi katika

msingi unaopinga kuhusu kuwapo kwa Mungu, imebainika kwamba dhana hii ni

ngumu kueleweka na inawaweka Tembo na wenzake katika mtanziko.

174

Kwa jumla, sehemu hii imejadili sababu mbalimbali za mitanziko ya wahusika kama

zinavyosawiriwa katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi. Sababu hizo

zimegawanywa katika makundi makuu manne, yaani sababu za kijamii, kiutamaduni,

kiuchumi na kifalsafa. Kuhusiana na sababu za kijamii, tumejadili suala la mfumo

wa malezi na mahusiano ya kimapenzi. Katika kipengele cha mfumo wa malezi,

tumeeleza kwamba ili kujenga maadili na misingi bora ya maisha ya watoto, suala

hili linatakiwa kuwa ni jukumu la jamii nzima. Kwa upande wa mahusiano ya

kimapenzi, tumeeleza kuwa hili ni janga, kwa kuwa linasababisha mitanziko na hata

kuwakengeusha wahusika kwa kukiuka misingi na maadili ya jamii. Matokeo yake ni

kwamba wengine hufikia hata hatua ya kuchukua maamuzi ya kujiua kutokana na

kukata tamaa ya kuendelea kuishi.

Kuhusiana na sababu za kiutamaduni tumeeleza kwamba jamii inatakiwa kuenzi na

kudumisha mila na desturi zake. Hata hivyo, ili kuepusha mitanziko kwa wahusika,

imeelezwa kwamba suala hili linatakiwa kufanyika kwa umakini na kwa kuzingatia

miktadha inayotawala na kuongoza jamii husika. Kwa upande wa sababu za

kiuchumi, mambo makubwa yaliyojadiliwa ni umaskini na hali ngumu ya maisha, na

suala la ukosefu wa kazi. Tumebaini kuwa mambo haya husababisha mitanziko kwa

wahusika, kwani huwapa wakati mgumu pale wanaposhindwa kutatua matatizo yao,

kutokana na kuwa katika hali duni za maisha. Vilevile, tumebaini sababu za

kifalsafa. Hizi zimegawanywa katika sehemu kuu tatu; yaani mtanziko kuhusu dhana

ya maisha, dhana ya kifo na dhana kuhusu Mungu. Kuhusiana na masuala haya

matokeo yanaonesha kwamba, kuna mkanganyiko mkubwa wa namna ya kuzielewa

dhana hizi. Hii ni kutokana na kuwapo kwa mitazamo inayotofautiana miongoni

mwa jamii juu ya dhana hizo. Mjadala wetu umeongozwa na nadharia ya

Udhanaishi.

Hatimaye, utafiti umebaini kuwa mitanziko inayowapata wahusika huwaweka katika

hali ngumu ya kuamua jambo la kufanya. Wahusika hao hujikuta wakiwa katika njia

panda, kwani hukabiliwa na wakati mgumu kuhusu uamuzi wa kuchukua. Hii ni kwa

sababu kila uamuzi wapangao kuuchukua, huwa na madhara kwao. Kutokana na hali

hiyo, mara nyingi husukumwa katika kutafuta njia itakayoonekana ni bora kwao na

inayoweza kuonekana kama njia ya kumaliza matatizo yanayokuwa yanawakabili.

Hivyo, mara nyingi husukumwa katika kuchukua maamuzi ya kujiua.

175

Baada ya mjadala huu unaoonesha sababu za mitanziko ya wahusika katika riwaya

teule za Euphrase Kezilahabi, sehemu inayofuata inatathmini uhusiano uliopo baina

usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya

matukio ya kujiua katika jamii.

4.4 Uhusiano wa Mchakato wa Kujiua katika Fasihi na Uhalisi katika Jamii

Katika sehemu hii, tunafanya tathmini ya uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya

mchakato wa kujiua katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi na vichocheo vya

matukio ya kujiua katika jamii. Tathmini hii inafanyika ili kubaini iwapo matukio ya

mchakato wa kujiua yanayosawiriwa katika riwaya teule yanaakisi matukio halisi ya

kujiua katika jamii zetu. Msukumo wa kufanya tathmini hii unatokana na mjadala

tuliofanya katika lengo la kwanza la utafiti hii. Katika lengo hilo, tulibainisha usawiri

wa matukio yanayounda mchakato wa kujiua katika riwaya teule za Euphrase

Kezilahabi. Hivyo, tathmini hii inafanyika ili kuthibitisha kuwa mwandishi wa kazi

za fasihi ni zao la jamii inayomzaa na kumkuza. Pia, huandika kazi kwa kuakisi

mambo halisi yanayotokea katika jamii yake kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na

kijamii.

Sambamba na hilo, katika utafiti huu matukio ya mchakato wa kujiua

yaliyobainishwa na kujadiliwa katika sehemu ya 4.2 yanawahusu wahusika wakuu

watatu. Nao ni Rosa Mistika katika riwaya ya Rosa Mistika, Kazimoto katika riwaya

ya Kichwamaji na Tumaini katika riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo. Katika mjadala

huo tulibainisha kuwa changamoto mbalimbali za kimaisha zilizowakumba wahusika

hao, zilichangia na kuwafikisha katika hatima ya maisha yao ya kujiua au

kujisababishia kifo.

Katika sehemu hii, tunatathmini uhusiano wa matukio ya mchakato wa kujiua katika

riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii. Uhusiano huo

tunautathmini kwa namna kuu mbili: Mosi, uhusiano wa sababu za matukio ya kujiua

zinazoibuliwa na mwandishi katika riwaya teule na vichocheo vya kujiua kwa

wahusika katika jamii zetu. Pili, uhusiano wa njia za kujiua zinazojichomoza katika

riwaya teule na katika maisha halisi ya jamii zetu.

176

4.4.1 Uhusiano wa Sababu za Matukio ya Kujiua

Katika kuchunguza uhusiano wa sababu za matukio ya kujiua, tunatathmini kile

kilichoibuliwa na mwandishi katika riwaya teule kwa kuhusianisha na vichocheo vya

kujiua katika maisha halisi ya jamii zetu. Utafiti huu umebaini kuwa, mara nyingi

mtu hufikia uamuzi wa kujiua kutokana na kuathiriwa kisaikolojia kiasi cha kukata

tamaa na kuona kama dunia imemkataa na kwamba hawezi kuishi tena. Imebainika

kwamba mtu huyo huamini kwamba, suluhisho lake ni kujiua. Kulingana na tasinifu

hii, kuathirika kisaikolojia ni kufanya mambo tofauti na tabia au haiba iliyozoeleka

kwa mhusika. Kuathirika huko huweza kusababisha mhusika kujiona hana thamani

tena katika jamii yake. Hali hiyo humkatisha tamaa na husababisha aingiwe na

mawazo ya kujidhuru. Matokeo yanaonesha kwamba mawazo hayo huanza na hisia,

kisha hufuatiwa na kitendo chenyewe cha kujiua. Maelezo haya yanaungwa mkono

na Nsolezi12

anayedai kuwa:

Kujiua huanza na hali ya hisia ambapo mhusika kushindwa

kujizuia kutokana na janga au tatizo analokuwa anakabiliana

nalo. Mtu hufikia hatua ya kujiua kutokana na sababu

zinazotibua hisia au kupatwa na matukio ya kuumiza sana,

kiasi cha kuona kwamba hana sababu ya kuendelea kuishi

tena. Sababu hizo ni kama vile kukataliwa na familia yake,

jamii yake, mpenzi wake na kufiwa na mtu au watu wake wa

karibu. Mvurugiko wa kisaikolojia na mtikisiko wa kihisia,

ndio husababisha mtu kujiua. Hata hivyo, si rahisi sana

kuelewa kiasi cha mtikisiko na mvurugiko huo. Suala lililo

bayana ni kwamba kuna uhusiano mkubwa baina ya kujiua na

masuala ya kisaikolojia.

Kwa upande wake, Kubller-Ross (1991) anadai kuwa mtu hufikia uamuzi wa kujiua

baada ya kushindwa kuipokea hali, tukio au jambo fulani zito linalomsumbua na

kumuumiza. Mtaalamu huyo anafafanua hatua tano apitiazo mtu aliyekumbwa na

tatizo kubwa ambalo huweza kumsababisha achukue uamuzi wa kujiua. Hatua hizo

ni: kukataa au kujikana, kupandwa na hamaki au hasira, kukosa jibu sahihi la tatizo

linalomkumba au linalomkabili, kupatwa na mfadhaiko au sonona, na mwisho ni

12 Mahojiano baina ya mtafiti na Dkt. Florentina Nsolezi yalifanyika katika viunga

vya Chuo Kikuu cha Dodoma Novemba 30, 2019. Dkt. Florentina Nsolezi ni

Mhadhiri wa Saikolojia katika Idara ya Elimu ya Saikolojia na Mafunzo ya Mitaala,

Chuo Kikuu cha Dodoma.

177

kushindwa kukubaliana na hali au tukio lenyewe. Kwa kuzingatia hatua hizo,

imebainika kuwa mtu huamua kujiua kutokana na kukataa au kushindwa kulipokea

na kulikubali tatizo au jambo linalokuwa linamkabili. Hali hiyo humkatisha tamaa na

kuchukulia kwamba kujiua kwake, ndilo suluhisho pekee la tatizo lake. Hoja hii

inaungwa mkono na Kano13

anayedai kuwa:

Suala la kujiua ni la kisaikolojia na linauhusiano mkubwa na

aina ya tabia aliyonayo mhusika. Kimsingi, kuna aina mbili za

watu; yaani wandani (introvert) na wasondani (extrovert).

Mara nyingi wanaofikia hatua ya kujiua ni wandani kwa

sababu wana tabia ya kuyakumbatia mambo kutokana na tabia

ya ukimya wao. Aidha, kutokana na tabia yao ya hushindwa

kuwashirikisha matatizo yao watu wao wa karibu, hubaki

wakinung‘unikia na kuumia mioyoni mwao. Matokeo yake,

huweza kufanya hukumu ndani kwa ndani kwa kuchukua hatua

ya kujiua, kutokana na kupata msongo wa mawazo. Wasondani

ni wa wazi, hupenda kuongea na mara nyingi wanapopatwa na

madhila au matatizo, huwashirikisha watu wao wa karibu

ambao huwasaidia katika kuyatatua au kuwapa ushauri wa

namna ya kukabiliana nayo.

Kwa jumla, utafiti umebaini kuwa kuna uhusiano mkubwa baina ya kujiua na

masuala ya kisaikolojia. Hii ni kwa sababu kabla ya kufikia uamuzi wake, mhusika

hupata mvurugiko wa kisaikolojia, ambao humsukuma kufanya kitendo hicho.

Mvurugiko huo husababisha mhusika kupata mtikisiko wa akili, ambao humsukuma

kufanya kitendo cha kujiua kwa kuamini kwamba, hilo ndilo suluhisho la matatizo

yanayomkabili. Matokeo yanaonesha kuwa mhusika hufikia hatua hiyo kutokana na

kukata tamaa, kujiona mpweke, kuwa na tabia ya kuzungumzia masuala ya kujiua,

kupatwa na sonona pamoja na magonjwa mengine ya akili. Mambo haya pia

yamebainishwa na mwandishi wa riwaya teule katika kazi zake kwa kuwa,

ameandika kazi hizo kwa kuyamulika masuala yaliyomo ndani ya jamii yake. Huu ni

13 Mahojiano baina ya mtafiti na Dkt. Erasto Kano yalifanyika katika viunga vya

Chuo Kikuu cha Dodoma Januari 18, 2020. Dkt. Erasto Kano ni Mhadhiri wa

Saikolojia katika Idara ya Elimu ya Saikolojia na Mafunzo ya Mitaala, Chuo Kikuu

cha Dodoma.

178

uthibitisho kuwa, kuna uhusiano mkubwa baina ya sababu za matukio ya kujiua

yanayosawiriwa katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika

jamii. Matukio hayo yanatokana na athari katika masuala ya mapenzi, magonjwa ya

akili na athari katika malezi. Masuala mengine ni mizozo na migogoro ya kifamilia,

vifo vya wapendwa wao, ukosefu wa kazi na matatizo kazini pamoja na changamoto

mbalimbali za maisha.

4.4.1.1 Kujiua Kunakosababishwa na Athari za Mahusiano ya Kimapenzi

Changamoto mbalimbali zitokanazo na athari za mahusiano ya kimapenzi ni

miongoni mwa vichocheo vinavyosababisha watu wengi kujiua. Baadhi ya

changamoto hizo ni mafarakano baina ya wapenzi hao, kushindwa kutimiziana ahadi

za makubaliano yao, kukataliwa, kuachwa na kutelekezwa, na kusalitiana. Matokeo

yanaonesha kuwa mara nyingi wahusika wanapokumbwa na changamoto hizi,

huweza kuathirika kisaikolojia na hata kufikia hatua ya kukata tamaa kwa kuona

kuwa, hawana thamani tena katika jamii. Kutokana na hilo, huweza hata kuchukua

uamuzi wa kujiua kama suluhisho la matatizo yao. Utafiti umebaini kuwa, matukio

ya kujiua yanayotokana na athari za mahusiano ya kimapenzi yanayosawiriwa katika

riwaya teule yanalandana na vichocheo vya matukio ya namna hiyo yanayojitokeza

katika maisha halisi ya jamii zetu. Hii ni kwa sababu kazi za Fasihi ni zao la maisha

halisi ya jamii.

Kwa mfano, katika riwaya ya Rosa Mistika, mwandishi anabainisha athari

zitokanazo na mahusiano ya kimapenzi zinazoweza kusababisha mtu kujiua, hasa

pale wahusika wanaposhindwa kutimiziana na kufikia makubaliano ya malengo na

mipango yao. Suala hili linasawiriwa kupitia kwa mhusika mkuu Rosa Mistika

anayechukua uamuzi wa kujiua. Hii ni baada ya kukataliwa na kuachwa na mchumba

wake Charles. Ifahamike tu kwamba kabla ya kuchukuliwa kwa uamuzi huo, Rosa

anadharauliwa, anachukiwa na kulaumiwa sana na jamii yake kutokana na tabia na

mwenendo wake mbaya wa kujihusisha na kufanya mapenzi ovyo. Jamii hiyo

inathubutu hata kumpa majina kama vile ―kahaba‖, ―malaya‖, ―lab‖, ―mwasherati‖,

―mzinzi‖, na ―mvunja ndoa za watu.‖ Majina haya siyo tu kwamba yanamfanya

aonekane hafai katika jamii yake, bali yanaathiri pia fikra na mtazamo wake

kuhusiana na suala la maisha. Matokeo yake ni kwamba, anafikia uamuzi wa

kuyaona maisha kama upuuzi, ikizingatiwa kwamba miongoni mwa watu wanaotoa

179

shutuma na lawama hizo ni baba yake mzazi, Zakaria, na mchumba wake, Charles.

Zaidi ya hayo, anasikitishwa sana na kitendo cha Charles kuwa miongoni mwa watu

wanaomsimanga na kumlaumu kwa madai ya kukosa bikra, ilhali yeye mwenyewe ni

miongoni mwa watu wenye tabia za kuwaharibia mabinti bikra zao. Kutokana na

hilo, anapata msukumo wa kujiua ili kuyakomesha maisha yake ya taabu na

misukosuko, huku akimwachia Charles ujumbe ulioandikwa kwa wino wa damu.

Ujumbe huo unasema:

… Charles ninajiua kwa ajili yako. Lakini kwa kuwa

ninakupenda, ninakwambia siri moja kubwa uzingatie. Charles

kuoa bikira ni bahati tu wala si kitu cha kutafuta: ukimwonja

mchumba wako kabla ya ndoa si bikira tena, hata kama

alikuwa (uk. 93).

Kwa hakika, ujumbe huo siyo tu kwamba unasikitisha, bali unaibua simanzi na

masononeko kwa Charles mwenyewe na kwa jamii kwa jumla. Aidha, taswira

inayojitokeza tumfikiriapo Rosa akiwa katika hatua ya kuandika ujumbe huo

tulioudondoa, ni ya mtu mwenye masikitiko, aliyekosa matumaini, na anayeyajutia

maisha yake. Anakata tamaa na kukengeuka misingi ya jamii yake. Kama

inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi, haoni tena faida ya kuishi na anatamani

kifo kimchukue haraka. Kipacha (2019) anaeleza kwamba Rosa aliona hakuna

sababu ya kuendelea kuishi katika hali ya maumivu yaliyogubikwa na mkururo wa

usaliti, uonevu, uongo na ukandamizwaji, tangu ngazi ya familia, ujirani, kwenye

taasisi za kishule na jamii kwa jumla. Anafafanua zaidi kuwa, aliamua kufikia

hitimisho hilo kwa kuona kwamba hakuna sababu ya kuendelea kuishi kwa

kusalitiwa. Hivyo, alichagua kujiua kama njia mojawapo ya suluhisho la matatizo

yake.

Matokeo yanaonesha kwamba kitendo cha Rosa kubakwa na kudhalilishwa na

mchumba wake, Charles, ndicho kinachompa nguvu na msukumo wa kuchukua

uamuzi wa kujiua kwake. Anaamua kufanya hivyo kama njia ya kujikomboa na

kujitoa katika mauvivu makali ya kisaikolojia na kiontolojia, yanayoyagandamiza

maisha yake. Anakufa huku akitabasamu kwa sababu ya ugumu wa maisha yake

unaohusishwa na suala la mahusiano ya kimapenzi. Hivyo, anaamua kukiita kifo

hicho kimjie kwa haraka, huku akikifurahia kwa kusema: ―Asante, kifo njoo upesi‖

(uk. 91). Kauli hii inafanana na maelezo ya Camus (1954) anayedai kuwa,

180

madhumuni ya maisha siyo kuishi kwa furaha, bali kufa ukiwa mwenye furaha.

Suala hili ndilo linalomtokea Rosa Mistika, kwani kama inavyoelezwa katika msingi

wa tatu wa nadharia ya Udhanaishi, anautafuta uhuru wake binafsi kwa kukifurahia

kifo ambacho kwake, ndilo suluhisho la maisha yake.

Katika utafiti huu tumebaini kwamba masuala ya watu kupishana katika mapenzi

kama yanavyosawiriwa katika riwaya teule, yamekuwa yakiripotiwa pia mara kwa

mara katika jamii zetu. Tukio mojawapo la namna hiyo lilitokea huko Bukoba tarehe

17.12.2018 na kuripotiwa katika gazeti la Habari Leo la Desemba 19, 2018. Katika

tukio hilo lenye kichwa cha habari kisemacho: ―Amuua Mpenzi Wake Akidai

Amemsaliti, Naye Ajiua‖ inaelezwa kwamba:

Mwalimu Karoli Domisian alimuua mpenzi wake aitwaye

Regina Temu kwa kumnyonga na tai. Baada ya hapo, naye

aliamua kujiua kwa kujinyonga kwa kutumia kamba ya

manila, ambapo kabla ya kujiua kwake aliacha ujumbe

unaobainisha kuwa, alifikia uamuzi huo kutokana na mpenzi

wake huyo kumsaliti katika masuala ya mahusiano ya

kimapenzi (kur. 1 – 2).

Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa, hili ni miongoni mwa matukio mengi

yanayohusiana na masuala ya mapenzi yanayozikumba jamii zetu. Matukio kama

haya yamekuwa na athari kubwa na yanasababisha watu kujiua au hata kuwaua

wenzi wao. Daniel Marandu, ambaye ni mtaalamu wa Saikolojia kama

anavyoripotiwa katika gazeti la Mtanzania la Novemba 30, 2019, anathibitisha kuwa

matukio haya ni mengi na yameshamiri katika jamii zetu. Katika ufafanuzi wake,

anabainisha sababu mojawapo ya watu kujiua kuwa ni msongo wa mawazo

unaotokana na mahusiano ya kimapenzi. Anasema:

Hii ―stress‖ (msongo wa mawazo) ni mbaya zaidi bora ya

kufiwa na mzazi, unaweza kulia siku mbili ukasahau, lakini ya

mapenzi ni tofauti. Wengi wao, wanajikatia tamaa na

kujinyonga… Watu wasitafute ―solution‖ (njia au ufumbuzi)

ya kudumu kwa tatizo ambalo ni ―temporary‖ (la muda),

kuachwa katika mapenzi ni safari tu kwa sababu atakuja

mwingine. Hivyo, watu wanapaswa kuwa wavumilivu.

Ukizidiwa tafuta mtu mweleze shida yako kwa sababu

unavyomwelezea mtu unatema zile sumu. Kwa hali ilivyo

sasa, misawajiko ya mahusiano ya kimapenzi imekuwa ni

chachu kubwa ya watu kujinyonga kwa sababu wengi,

wamereplace mapenzi na pesa. Hivyo, mtu mwingine

181

hushindwa kujizuia pale anaposikia kuwa, mpenzi wake ana

mahusiano na mtu mwingine (kur. 1 - 2).

Maelezo haya yanaonesha kuwa watu wengi wana msongo wa mawazo unaotokana

na athari za mahusiano ya kimapenzi. Kutokana na hali hiyo, Marandu anawashauri

watu wanaokumbwa na matukio ya aina hiyo, kutafuta mtu wa karibu au wataalamu

wa masuala ya saikolojia na magonjwa ya akili, wanaoweza kuwapa ushauri juu ya

mambo hayo.

4.4.1.2 Kujiua Kunakosababishwa na Athari katika Malezi na Migogoro ya

Kifamilia

Kutofautiana katika suala la malezi ya watoto baina ya wazazi au walezi pamoja na

migogoro ya kifamilia, ni miongoni mwa sababu zinazochochea watu kufikia

maamuzi ya kujiua. Katika hali ya kawaida, kila mtu bila kujali hali aliyo nayo,

anahitaji na anastahili kuheshimiwa na kuthaminiwa utu wake. Halikadhalika, watoto

nao wana haki zao za msingi wanazohitaji kuzipata kutoka kwa wazazi au walezi

wao. Hata hivyo, wazazi au walezi wanapotumia mamlaka yao kwa kuwanyanyasa,

kuwakandamiza, kuwasema vibaya, kuwapiga na hata kuwabana na kuwanyima sana

uhuru wao, huweza kusababisha watoto hao kukengeuka misingi ya malezi yao. Hii

inatokana na ukweli kwamba malezi ya namna hiyo huwaathiri kisaikolojia na

kuwafanya wajitathmini walivyo. Matokeo yake, baadhi yao hufikia uamuzi wa

kujiona kuwa hawafai na hawastahili kuendelea kuishi. Hivyo, kama inavyoelezwa

katika msingi wa nne wa nadharia ya Udhanaishi, wengine huchukua uamuzi wa

kujiua kama suluhisho la matatizo yanayokuwa yanawakabili.

Suala hili limesawiriwa vyema katika riwaya ya Rosa Mistika. Katika riwaya hii,

mwandishi anamtumia Rosa Mistika kama kipaza sauti chake kwa kulalamika na

kuhoji aina ya malezi yanayopaswa kutolewa kwa watoto. Utafiti umebaini kwamba,

Rosa Mistika anachukizwa na kulalamikia malezi ya ukali, vitisho, ukatili, na

kunyimwa uhuru kutoka kwa baba yake, Zakaria, pamoja na masista wa sekondari ya

Rosary. Hali hiyo inamsukuma mwandishi kujaribu kuudodosa uwezo na nafasi ya

fikra za wazazi na dini kuhusu suala la malezi ya watoto, hususani wa kike.

Anazisuta fikra za kuwalea watoto kwa kuwanyima uhuru wao kama anavyofanyiwa

Rosa Mistika, huku Zakaria akijisifu kwamba anajua kuwalea mabinti zake (uk. 9).

182

Matokeo yanaonesha kwamba uhusiano wa Rosa na baba yake ulibadilika baada ya

kutambua ukweli kuwa, chanzo cha matatizo yake ni malezi kutoka kwa baba yake.

Matatizo hayo yalizusha mgogoro wa kimalezi kama unavyojidhirisha kupitia

majibizano baina yao. Hapo ndipo Rosa anafikia hatua ya kumtamkia baba yake

maneno makali aliyoyatunza moyoni mwake kwa muda mrefu. Anasema: ―Kila

wakati unatuchunga. Unafikiri utatuoa wewe!‖ (uk. 58). Kauli hii inaonesha kwamba

uhusiano wao umevurugika na umegeuka kuwa uadui baina yao.

Kutokana na hilo, utafiti umebaini mkengeuko wa wazi wa kimalezi, kwa kuwa Rosa

hakubaliani tena na aina ya malezi anayoyapata kutoka kwa baba yake. Athari za

kisaikolojia zitokanazo na malezi ya ukali, ya kukandamizwa, kubanwa na

kunyimwa uhuru wa kufanya mambo yake, zinajidhihirisha waziwazi. Haoni tena

umuhimu wa kumsikiliza na kuzingatia malezi ya baba yake, aliyoyavumilia kwa

muda mrefu. Matokeo yake, malezi hayo yanakuwa chanzo cha mgogoro baina yake

na baba yake kiasi cha kujenga chuki na uadui dhidi yake. Hii ni baada ya kubaini

kwamba alinyimwa uhuru wake, na hivyo kulazimika kuutafuta kwa nguvu kama

inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi. Mwandishi anathibitisha hili

anaposema kuwa:

Maisha ya binadamu ni kama mti. Mti unahitaji maji, hewa na

mwanga. Kama mti ukinyimwa mwanga wa kutosha na miti

mingine, utarefuka. Utajaribu kupita miti yote ili upate

mwanga. Zakaria aliwanyima binti zake mwanga wakati ule

walipokuwa wakiuhitaji sana. Aliwapiga; aliwakataza

kuzungumza na mvulana yeyote. Nao kama mti walijaribu

kujirefusha ili wapate mwanga, na walirefuka kweli; kiasi cha

kutoweza kuonywa na mtu yeyote (uk. 47).

Dondoo hili linaonesha sababu za wazi za kuathirika kisaikolojia kwa Rosa. Matokeo

yake anaamua kuutafuta uhuru wake kwa nguvu. Hata hivyo, anautumia uhuru huo

vibaya kwa kujitumbukiza katika bahari ya mapenzi kiasi cha kuparamia wanaume

wengi, bila kuchukua tahadhari. Tabia yake inaanza kubadilika akiwa katika shule ya

sekondari ya Rosary. Hii ni baada ya kutoka katika mikono ya baba yake; na tabia hii

inaota mizizi akiwa katika Chuo cha Ualimu Morogoro. Mabadiliko hayo ya kitabia

yanaendelea hata baada ya kumaliza mafunzo yake ya ualimu. Matokeo yake,

anafikia maamuzi ya kujiua kutokana na kushindwa kuhimili mgogoro wa nafsi na

maumivu makali ya kuachwa na mpenzi wake, Charles (uk. 93).

183

Matokeo yake ni kwamba, tukio hilo linamwibulia kesi na analazimika kutoa sababu

za kujiua kwake. Hata hivyo, badala ya kueleza kuwa sababu za kujiua kwake ni

Charles kama alivyoeleza katika ujumbe wake kabla ya kujiua, anaelekeza lawama

hizo kwa Zakaria. Anamlalamikia kuwa, yeye ndiye chanzo cha kuharibika kwa

maisha yake kutokana na aina ya malezi aliyompa (uk. 98). Hii inatupa picha

kwamba katika jamii zetu, wapo wazazi na walezi wenye tabia kama ya Zakaria.

Hawa huwalea watoto wao kwa mkono wa chuma, huku wakiwabana na

kukandamiza uhuru na haki zao za msingi. Hata hivyo, utafiti huu haukusudii

kusema kuwa watoto wanatakiwa kuachwa na kufanya lolote walitakalo, bali

unaeleza kuwa wazazi na walezi wanatakiwa kutambua kwamba, watoto nao wana

haki zao za msingi. Hivyo, wanatakiwa kupewa nafasi ya kusikilizwa ili kuweza

kubaini hisia, matamanio na matarajio yao ya baadaye. Kitendo cha kuwabana sana

na kuwapa malezi ya ukali na vitisho, huweza kuwaathiri kisaikolojia. Pia,

kuchochea na kusababisha migogoro na mizozo baina yao na wazazi au na walezi

wao. Kulingana na nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi mizozo na migogoro hiyo

husawiriwa ndani ya fasihi ili kuficha mambo anuwai ya kijamii ambayo

hayajasuluhishwa. Kushindwa kusuluhishwa kwa migogoro hiyo ndiko husababisha

wengine hushindwa kuvumilia mateso na manyanyaso wayapitiayo. Hivyo, huamua

kuchukua maamuzi ya kujiua kama ilivyotokea kwa Rosa Mistika.

Jambo lililo dhahiri ni kwamba matukio ya watu kujiua yakihusishwa na masuala ya

malezi, kama ilivyomtokea Rosa Mistika, yapo na yamekuwa yakitokea mara kwa

mara katika jamii zetu. Wakati mwingine kujiua huko kumekuwa kukisababishwa na

malezi ya kikatili kutoka kwa wazazi au na walezi wao au kwa kulelewa na watu

wengine tu pasipo kuwatambua wazazi wao halisi. Kwa mfano, katika gazeti la

Mtanzania la Februari 22, 2019, kuna taarifa inayoeleza kwamba:

Tarehe 19 Februari, 2019, Jasmini Ngoye (miaka 18)

mwanafunzi wa Sekondari ya Lupanga Manispaa ya

Morogoro, alijiua kwa kujipiga risasi, ambapo kabla ya kujiua

kwake aliacha ujumbe unaoeleza kuwa, yeye ni mtoto

asiyewajua wazazi wake na asiyejua mahali alikozaliwa (kur.

1 – 2).

Tukio la namna hii kama inavyosawiriwa katika riwaya ya Rosa Mistika,

linathibitisha kuwa katika jamii zetu kuna matukio mengi ya watu kujiua

184

yanayohusishwa na aina ya malezi wayapatayo kutoka kwa wazazi au walezi wao.

Kitendo cha Jasmini kulalamika kuwa, alikuwa hawajui wazazi wake wala mahali

alikozaliwa, kinaleta picha kwamba hakuridhishwa na aina ya malezi aliyokuwa

anayapata kutoka kwa walezi wake. Hii inaonesha kwamba alitamani kulelewa na

wazazi wake kama wangekuwepo. Hali hiyo ndiyo iliyomwathiri kisaikolojia kiasi

cha kuongelea na kutabiri juu ya kifo chake kabla ya kuchukua uamuzi wa kujiua.

Sambamba na suala la malezi katika riwaya ya Rosa Mistika, utafiti umebaini

kuwapo kwa migogoro na mizozo ya mara kwa mara baina ya Zakaria na Regina.

Migogoro hiyo ijapokuwa haiwahusu watoto wao moja kwa moja, ukweli ni kwamba

kwa kiasi kikubwa wanapoiona na kuishuhudia huwaathiri kisaikolojia. Hii ni kwa

sababu mara nyingi migogoro na mizozo hiyo itokeapo, huwafanya wanafamilia hao

kuwa na woga na hofu. Pia, huwa ni chanzo cha kukosekana kwa amani, utulivu na

maelewano baina yao (uk. 3). Katika sehemu hiyo mwandishi anaonesha namna

Regina anavyoivumilia migogoro na mizozo inayotokea mara kwa mara katika

familia yake.

Kama inavyoelezwa katika msingi wa tatu wa nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi,

mwandishi anaonesha kwamba usuluhishi wa migogoro unaosawiriwa ndani ya

fasihi na namna anavyoyasuka matukio yake, unaficha tu migongano anuwai ya

kijamii ambayo haijasuluhishwa. Anaonesha kuwa si kila mtu anaweza kuwa na

uvumilivu kama huo wa Regina, kwa kuwa wengine huamua kujiua kama njia ya

kuyakwepa matatizo hayo. Hii ni kwa sababu maisha ya namna hiyo, siyo tu kwamba

huwakosesha furaha, bali huwakatisha tamaa ya kuendelea kuishi kama

inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi. Mfano mzuri ni Rosa Mistika ambaye

haoni sababu ya kuendelea kuvumilia maumivu ya kisaikolojia anayoyapata kutoka

kwa baba yake; hivyo, anaamua kujiua. Anachukua uamuzi huo kutokana na

migogoro ya mara kwa mara baina yake na baba yake, na baada ya kushuhudia

migogoro na mizozo ya muda mrefu anayofanyiwa mama yake.

Matokeo yanaonesha kuwa, kuna uhusiano baina ya migogoro na mizozo

inayosawiriwa katika riwaya ya Rosa Mistika na vichocheo vya migogoro ya namna

hiyo, inayotokea katika mazingira halisi ya maisha ya jamii. Migogoro na mizozo

hiyo kwa kiasi kikubwa, ndiyo huchochea watu kujiua hasa pale wanaposhindwa

185

kuvumiliana. Kwa mfano, katika gazeti la Mwananchi la Februari 19, 2018

linaripotiwa tukio la kujiua kwa mwalimu Respicius Kazimbaya (46) wa shule ya

msingi Dutumi, mtaa wa Kambitano, Kata ya Lukobe Mkoani Morogoro. Taarifa

hiyo inaeleza kuwa:

Tukio hilo lilitokea Februari 17, 2018 kutokana na migogoro

na mizozo ya kifamilia na kwamba mwalimu huyo, alichukua

uamuzi wa kumuua mkewe, Scrinda Andrew Magumba (42),

kwa kumkatakata mapanga kichwani na shingoni. Pia,

alimchomachoma sehemu mbalimbali za mwili wake kwa

kutumia kitu chenye ncha kali. Kisha, siku moja baada ya

tukio hilo, mwili wa mwalimu huyo, ulikutwa ukining‘inia

kwenye mti wa mwembe, akiwa amejinyonga kwa kutumia

kitenge. Akithibitisha kutokea kwa tukio hili, Kamanda wa

Polisi Mkoa wa Mororogo Ulrich Matei alisema kuwa, taarifa

za awali zilibaini kwamba, ugomvi wao ulitokana na

mwanaume huyo kutaka kuuza nyumba yao, iliyoko Lukobe

Manispaa ya Morogoro. Jambo hilo, lilipingwa vikali na mke

wa mwalimu huyo kiasi cha kuzusha mgogoro, uliosababisha

kutokea kwa vifo hivyo (uk. 4).

Utafiti umebaini kuwa, hili ni tukio mojawapo miongoni mwa matukio mengi

yanayotokana na migogoro na mizozo ya kifamilia, yanayozikumba jamii zetu.

Migogoro na mizozo hiyo inahusiana sana na ile inayosawiriwa katika riwaya ya

Rosa Mistika, kama ilivyokwisha kujadiliwa hapo awali katika kipengele hiki. Kwa

mantiki hiyo, mwandishi anaibua migogoro na mizozo hiyo ili kuipa jamii yake

mwanga wa kuyajadili matatizo halisi, yanayomkumba binadamu huyo. Haya ndiyo

yanayojadiliwa katika nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi kwani huyasawiri mambo

mbalimbali yanayoikumba jamii kulingana na mazingira halisi ya maisha yake.

4.4.1.3 Kujiua Kunakosababishwa na Athari za Magonjwa

Magonjwa sugu au kuugua kwa muda mrefu ni miongoni mwa sababu za matukio ya

watu kujiua. Watu hao hukata tamaa ya kuendelea kuishi kutokana na kuathirika

kisaikolojia kiasi cha kushindwa kuendelea kuvumilia mateso au maumivu

wayapatayo. Wengine huchukua uamuzi wa kujiua kutokana na msongo wa mawazo

usababishwao na vitendo vya unyanyapaa na unyanyasaji wafanyiwavyo na watu

wanaowauguza au kuwahudumia. Pia, kutokana na maradhi yao, wengine hufikia

hatua ya kujihisi kwamba wao ni kero kwa familia au kwa jamii, na kwamba,

hawana umuhimu kutokana na kutohitajika kwao tena.

186

Suala hili linasawiriwa katika riwaya ya Kichwamaji kupitia kwa Kazimoto

anayeamua kujiua baada ya kuugua ugonjwa mbaya wa zinaa ulioathiri kizazi chake.

Mwandishi anaeleza kwamba ugonjwa huo aliupata baada ya kufanya mapenzi na

msichana malaya, aitwaye Pili. Kisha, Kazimoto naye, alimwambukiza mke wake

Sabina, ambapo kutokana na athari za ugonjwa huo, alizaa mtoto mwenye kichwa

kikubwa. Kitendo hicho, kilisababisha Kazimoto kupata msongo wa mawazo na

kufikia hatua ya kujiua ili asiendelee kuzaa kizazi kibaya. Hili linathibitishwa na

yeye mwenyewe anaposema kuwa: ―Nimejiua. Siwezi kuendelea kuzaa kizazi

kibaya‖ (uk. 195). Kauli hii inathibitisha kuwa, magonjwa sugu au kuugua kwa muda

mrefu humwathiri mtu kisaikolojia. Pia, huweza kusababisha akengeuke misingi ya

jamii yake na hata kukata tamaa ya maisha na kujiua kama inavyoelezwa katika

msingi wa nne wa nadharia ya Udhanaishi.

Kama inavyosawiriwa katika riwaya ya Kichwamaji, matukio ya watu kujiua

kutokana na magonjwa sugu au kuugua kwa muda mrefu ni mengi na yamekuwa

yakitokea mara kwa mara katika jamii zetu. Gazeti la Nipashe la Desemba 27, 2018,

lenye kichwa cha habari kisemacho, ―Ajinyonga hadi kufa kwa kuchoka kusumbua

familia‖ ni uthibitisho wa kuwapo kwa matukio haya. Taarifa hiyo inaeleza kuwa,

Awetu Makunula (44), mkazi wa Nakayaya Wilayani Tunduru, Mkoani Ruvuma,

alijinyonga hadi kufa kwa madai ya kuchoka kusumbua familia kutokana na hali ya

familia yake. Inaelezwa kwamba Makunula alikutwa akining‘inia juu ya mti wa

mkorosho, jirani na nyumba ya wazazi wake. Akielezea kuhusiana na maisha ya

mkewe, Salumu Namtikwe anasema:

Tulikuwa tumelala wote lakini ilipofika majira ya saa kumi na

moja alfajiri, aliniaga kuwa anatoka nje kufagia uwanja wa

nyumba kwani anataka kuwahi kwenda shambani. Mimi

nikaendelea kulala. Baada ya muda mfupi kupita, nilipata

taarifa kuwa, mke wangu amejinyonga hadi kufa, baada ya

kujining‘iniza katika mti uliopo jirani na nyumbani kwa

wazazi wake. Baada ya kupata taarifa hizo, nilikwenda eneo la

tukio na kumtambua marehemu. Kwa muda mrefu sasa mke

wangu alikuwa akisumbuliwa mara kwa mara na maradhi

mbalimbali. Jambo hilo, lilimfanya aishi maisha ya unyonge,

ya kukosa amani na matumaini, na ya kukatisha tamaa (kur. 3

- 4).

187

Kutokana na tukio hilo ni dhahiri kwamba kujiua kwa Makunula ni mojawapo ya

matukio mengi yanayotokea katika jamii zetu, yanayosababishwa na athari za

magonjwa mbalimbali. Athari hizo kama zinavyosawiriwa kwa Kazimoto katika

riwaya ya Kichwamaji, ndizo zinazosawiriwa pia, katika jamii zetu kutokana na

matukio mengi ya kujiua yanayoripotiwa mara kwa mara. Hii inaonesha kwamba

kuna kulandana kwa ujitokezaji wa matukio ya kujiua yanayosababishwa na athari za

magonjwa mbalimbali katika riwaya teule na katika jamii zetu. Mwandishi wa

riwaya ya Kichwamaji anapotupa picha ya ugonjwa wa ajabu wa Kazimoto, analenga

kuthibitisha kuwa, Fasihi ni dhihirisho la ujumi na ubunifu wa jamii katika

kupambana na mazingira yake. Kutokana na hilo, kama inavyofafanuliwa katika

msingi wa pili wa nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi, kamwe haiwezi kutengwa na

harakati za binadamu zinazoongoza maisha yake.

Kwa jumla, sababu za matukio ya watu kujiua katika jamii zetu ziko nyingi. Hata

hivyo, kwa kuwa katika sehemu hii tulikusudia kutathmini uhusiano wa matukio ya

kujiua, yanayosawiriwa katika riwaya teule na vichocheo vya matukio hayo katika

jamii, kipengele hiki kimetathmini uhusiano wa sababu za kutokea kwa matukio

hayo. Katika kufanya hivyo tumebaini kwamba kuna sababu kuu tatu za matukio ya

kujiua yanayosawiriwa katika riwaya teule yenye uhusiano na vichocheo vya

matukio ya kujiua katika jamii. Matukio hayo ni: kujiua kunakosababishwa na athari

za mahusiano ya kimapenzi, kujiua kunakosababishwa na athari katika malezi na

migogoro ya kifamilia, na kujiua kunakosababishwa na athari za magonjwa.

4.4.2 Uhusiano wa Njia Zinazotumika katika Kujiua

Katika lengo la kwanza la utafiti tulibainisha kuwa, mara nyingi tukio la mtu kujiua

huwa halimtokei ghafla, bali ni mchakato ambao kwa kawaida huchukua muda

mrefu hadi kukamilika kwake. Katika lengo hilo pia, tulieleza kuwa mtu huamua

kujiua kutokana na sababu fulani, ambayo humfikisha katika kiwango cha juu kabisa

cha ubinafsi wake au upeo wa mwisho wa kufikiri kwake. Kutokana na hilo, mtu

huyo huchukua uamuzi wa kujiua kama suluhisho la matatizo yanayomkabili kwa

wakati huo. Hata hivyo, utafiti umebaini kuwa, mazingira aliyokulia mhusika au

jamii inayomkuza na kumlea, huwa na athari kubwa inayoweza kumfikisha mtu huyo

katika hatima ya maisha yake. Pia, mazingira hayo humpa mhusika msukumo wa

kufikiria na hata kuchagua njia anayoona inafaa katika kutimiza matakwa yake. Hii

188

ni kwa sababu mazingira hayo, ndiyo huwezesha mhusika kubaini njia rahisi ya

upatikanaji wa nyenzo za kumsaidia katika kufikia uamuzi anaokuwa ameuchukua.

Hivyo, matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa njia za kujiua zinazosawiriwa katika

riwaya teule, zina uhusiano na njia zinazotumiwa na wahusika katika mazingira

halisi. Miongoni mwa njia hizo ni kujiua kwa kujinyonga, kujipiga risasi, kujichoma

kisu na kwa kutumia sumu.

4.4.2.1 Kujiua kwa Kujinyonga

Kwa mujibu wa BAKITA (2017), kujinyonga ni kitendo cha kujifunga kamba au kitu

chochote kinachoweza kufunga shingoni, aghalabu kwa lengo la kujitoa uhai. Watu

wengi wamekatisha na kupoteza maisha yao kwa kutumia njia hii. Mwandishi wa

riwaya ya Rosa Mistika anaeleza kuwa, hata Rosa Mistika kabla ya kuamua na

kufikiria njia nyingine ya kuitumia katika kujiua kwake, njia hii ya kujinyonga ndiyo

iliyomjia kwanza akilini mwake. Anaeleza kuwa:

Rosa akiwa chumbani mwake, alisikia makofi yakipigwa.

Moyoni mwake alifikiri kwamba wanafunzi walikuwa

wakishangilia kufukuzwa kwake. Akiwa chumbani mwake

Rosa hakuweza kuona ulimwengu. Alitafuta kamba akakosa.

Alichukua mkanda wa gauni lake, aliona haufai (kur. 65 - 66).

Kutokana na nukuu hii, tunabaini namna mazingira aliyomo mhusika

yanavyochangia na kumsaidia katika kuchagua njia ya kujiua kwake. Mwandishi

anaibua mazingira aliyomo Rosa, na ambayo anayatumia katika kutafuta na kupanga

njia anayoiona kuwa rahisi kwake katika kutekeleza kusudio lake la kujiua. Njia ya

kujinyonga ndiyo inayomjia kwa haraka zaidi na anataja vifaa ambavyo ni rahisi

zaidi kupatikana katika mazingira aliyomo — kamba pamoja na mkanda wa gauni

lake. Hii inadhihirisha kwamba, mazingira kama inavyofafanuliwa katika nadharia

ya Sosholojia ya Kifasihi yana athari kubwa kwa mtu anayepanga kujiua. Hii ni kwa

sababu humpa msukumo wa kuamua ni njia gani aitumie katika kutimiza kusudio

lake.

Hata hivyo, ifahamike tu kwamba kabla ya mhusika kuchukua uamuzi wa kujiua,

huwa katika mahangaiko na mfadhaiko unaotokana na mvurugiko wa kisaikolojia.

Aidha, kutokana na ukubwa na ugumu wa suala lenyewe la kujiua, mhusika hujaribu

kutafuta kila njia ili kurahisisha na kufanikisha tukio hilo. Hili ndilo linalomtokea pia

189

Rosa Mistika, kwani anaposhindwa kufanikisha tukio lake la kujiua kwa kujinyonga,

anatafuta njia nyingine inayompa msukumo zaidi wa kutaka kutekeleza kitendo

hicho (uk. 66). Kama inavyoeleza nadharia ya Udhanaishi, anafanya jitihada zote

hizi ili kutafuta uhuru wake binafsi na uwezo wake wa kujifikiria na kujiamulia

mambo yake mwenyewe. Jitihada hizo zinamfanya akate tamaa ya maisha na

kukengeuka misingi ya jamii yake kwa kufanya tukio la kujiua, ambalo kwa hakika

halikubaliki katika jamii yake.

Kwa hiyo, kutokana na mwandishi kutusawiria mazingira na njia za kujiua kwa

Rosa, utafiti huu ulifanyika katika jamii ya mwandishi ili kubaini kuhusu kuwapo au

kutokuwapo kwa matukio ya kujiua pamoja na njia zitumiwazo na wahusika katika

kujiua kwao. Matokeo yanaonesha kwamba katika jamii hiyo, kuna uhusiano wa

matukio na njia za kujiua zinazotumiwa na wahusika kama zinavyosawiriwa katika

riwaya teule. Hili linathibitishwa na Kalogosi14

anayeeleza kuwa:

Matukio ya watu kujiua katika kisiwa chetu cha Ukerewe

hususani, hapa Namagondo, yamekuwa yakiripotiwa mara

kwa mara. Wengine hujinyonga na wengine hujiua kwa

kujitupa katika ziwa au mito. Kwa mfano, mto Nabili

unaoanzia Kazilankanda ni miongoni mwa mito mikubwa

katika jamii ya Wakerewe, ambapo watu wengi hujiua kwa

kujirusha humo. Hufanya hivyo ili kukwepa aibu itokanayo na

mambo mabaya na ya aibu. Mambo hayo ni kama vile:

kukutwa akifanya mapenzi na mke au mume wa mtu,

kudharauliwa na kushindwa kutimiza majukumu mbalimbali

ya kifamilia. Katika jamii ya Wakerewe, matukio ya kujiua

hutokea zaidi kwa wanaume. Aidha, vijana ndio hujiua zaidi

kutokana na masuala ya mahusiano ya kimapenzi na migogoro

ya kifamilia.

Maelezo ya Kalogosi yanathibitisha na kutupa picha halisi ya mambo yanayotokea

katika jamii ya mwandishi na yale yaliyoandikwa katika riwaya teule. Aidha, njia za

14 Mahojiano baina ya mtafiti na Mch. Charles Bita Kalogosi Desemba 18, 2019.

Yalifanyika katika Kijiji cha Namagondo katika kisiwa cha Ukerewe. Mch. Charles

Bita Kalogosi ni Mchungaji katika Kanisa Jipya la Mitume katika kijiji cha

Namagondo.

190

kujiua kwa wahusika zinazoelezwa na mwandishi katika kazi zake, ndizo

zinazoonekana kutumiwa pia na wahusika wanaochukua uamuzi wa kujiua katika

jamii yake. Kulingana na nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi, kazi yoyote ya fasihi

huzuka kutokana na taswira ya kijiografia, kimazingira na kiutamaduni. Hili

linathibitishwa na Kezilahabi mwenyewe anaposema:

Mimi hupendelea zaidi kutumia mandhari halisi. Ukitazama

kwa uangalifu maandishi ya Kiswahili, waandishi ambao

wamefanikiwa ni wale ambao wameweka wahusika wao chini

ya mazingira wanayoyaelewa na hasa yale ya kabila lao. Mimi

mwenyewe niandikapo riwaya zangu nahakikisha kuwa

wahusika wangu wanakulia na kukomaa Ukerewe Kisiwani na

baada ya hapo ninaweza kuwafanya watembee na kukaa mijini

Tanzania nzima (Kezilahabi, 2003).

Hoja ya Kezilahabi kwamba uandishi wake huzingatia mandhari halisi ya maisha

aliyokulia inatupa picha ya kuona kuwa, ubunifu wake katika kuumba wahusika

wake, na namna anavyosuka matukio yake, anahusianisha na maisha halisi ya jamii

yake. Hii inatokana na ukweli kwamba Fasihi ni dhihirisho la ujumi na ubunifu wa

jamii katika kupambana na mazingira yake kama inavyofafanuliwa katika nadharia

ya Sosholojia ya Kifasihi.

Kwa upande mwingine, Simbe15

anaelezea sababu za matukio mengi ya kujiua

kuwakumba zaidi wanaume tofauti na wanawake. Anasema:

Kinachosababisha waanaume wengi hufikia hatua ya kumaliza

au kujiua kabisa tofauti na wanawake, ambao hujaribu kujiua

pasipo kumaliza ni sababu za kimaumbile. Katika mchakato

wote wa kujiua kwamba atamaliza au hatamaliza,

hutegemeana na hali yake ya akili au historia ya magonjwa ya

akili. Hii ni kwa sababu asilimia 90 ya watu wanaojiua, huwa

na tatizo au magonjwa ya akili.

15 Mahojiano baina ya mtafiti na Dkt. Gema Peter Simbe Novemba 29, 2019.

Yalifanyika katika viunga vya Hospitali ya Magonjwa ya Akili Mirembe. Dkt. Gema

Peter Simbe ni Daktari Bingwa wa Afya na Magonjwa ya Akili ya Watoto na Vijana

katika hospitali hiyo.

191

Kwa hiyo, utafiti umebaini kuwa mwandishi wa riwaya teule aliamua kuyasawiri

mazingira yenye uhusiano na yale ya jamii yake ili kudhihirisha kuwa, kazi yoyote

ya fasihi ni taswira ya kijografia, kimazingira na kitamaduni ya jamii husika. Pia,

kazi hiyo hufungamana na historia ya jamii husika, kama inavyoelezwa katika

nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi.

Utafiti umebaini kuwa matukio ya watu kujiua kwa kujinyonga, yameshamiri katika

jamii zetu na yamekuwa yakiripotiwa mara kwa mara katika vyombo mbalimbali

vya habari. Suala hili kama linavyoripotiwa katika gazeti la Habari Leo la Novemba

5, 2018, linathibitishwa na DCP Adriane Magayane ambaye ni Naibu Kamishina wa

Polisi kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, (IGP) Simon Sirro. Katika

taarifa hiyo, Magayane anaeleza kuwa, vitendo vya watu kujiua kwa kujinyonga

vinaongoza nchini, vikifuatiwa na matumizi ya sumu, risasi na kwa kutumia visu.

Anasema:

Watu 262 kati ya 333 waliojiua nchini katika kipindi cha

mwaka 2016 hadi Juni 2018, walijinyonga wakifuatiwa na

watu 67 waliojiua kwa sumu. Aidha, katika kipindi cha Januari

2018 hadi Juni mwaka 2018, mikoa iliyoripoti matukio mengi

ya kujiua ni Mwanza matukio 29, Mbeya 18, Dodoma 11,

Tabora 11 na Shinyanga matukio 8 (kur. 1 – 2).

Aidha, takwimu hizo za kipolisi zinabainisha kwamba katika mwaka 2016 pekee,

watu 131 walijiua. Kati ya hao watu 101 walijiua kwa kujinyonga na watu 30 kwa

kutumia sumu. Mwaka 2017 watu 88 walijiua; kati yao, 71 walijiua kwa kujinyonga,

16 kwa kutumia sumu na mmoja kwa risasi. Pia, katika kipindi cha Januari 2018 hadi

Juni 2018 matukio ya watu kujinyonga yaliongezeka kutoka 71 mwaka 2017 hadi 90

yakifuatiwa na matumizi ya sumu ambayo ni 21. DCP Magayane anaendelea kueleza

kuwa:

Katika kipindi hicho, wanaume waliongoza kwa kujiua kwa

matukio 283 sawa na asilimia 84.98, huku idadi ya wanawake

ikifikia 50 ambayo ni sawa na asilimia 15.02. Taarifa hiyo

inabainisha zaidi kuwa mwaka 2016 wanaume waliojiua

walikuwa 106, sawa na asilimia 80.92, huku wanawake

wakiwa 25, sawa na asilimia 19.08 wakati mwaka uliofuata wa

2017, wanaume waliojiua walikuwa 81, sawa na asilimia

92.05 na wanawake 7, sawa na asilimia 7.95 (uk. 2).

192

Kutokana na taarifa hizi, tunapata picha ya jumla kuwa, tatizo la watu kujiua katika

jamii zetu lipo na ni kubwa. Hivyo, jamii zetu zinatakiwa kuitikia wito wa Shirika la

Afya Duniani, uliotolewa katika vyombo mbalimbali vya habari, likiwemo gazeti la

Mtanzania la tarehe 25 Januari 2018. Wito huo unazitaka jamii zote duniani

kushirikiana katika kulikabili tatizo la watu kujiua. utafiti umebaini kwamba

miongoni mwa njia za kukabiliana na tatizo hili ni kutoa elimu kwa jamii ya namna

ya kuwatambua watu wenye dalili za kutaka kujiua. Aidha, jamii inatakiwa

kuwawahisha hospitalini wale wenye dalili au tatizo la akili. Pia, inatakiwa kuchukua

hatua mbalimbali za kutatua migogoro na matatizo yanayowakumba ili kuwaepusha

na msongo wa mawazo, ambao ni chanzo kikubwa cha watu kujiua.

Akizungumzia sababu za ongezeko la idadi ya watu kujinyonga nchini,

mwanasaikolojia Daniel Marandu kama anavyoripotiwa na gazeti la Mtanzania la

Novemba 30, 2019, anasema kuwa:

Hali hiyo inatokana na mfumo mzima wa maisha kubadilika,

likiwamo suala la upatikanaji wa fedha, ajira na mengineyo.

Unakuta mtu zamani watoto wake walikuwa wanasoma shule

za gharama lakini kutokana na hali ilivyo sasa, anashindwa

kumudu na kukata tamaa. Siku hizi watu wengi wanaachishwa

kazi kwa kupunguzwa katika makampuni mbalimbali pamoja

na wenye vyeti feki na kusababisha watu hao kukata tamaa ya

maisha. Utakuta mtu amefanya kazi miaka 55, lakini leo

anakuja kutumbuliwa kwa cheti feki. Hivyo, anajiona kuwa

hapati hata yale mafao yake ya miaka yote hiyo na mbele

haoni ‗future‘ hivyo anaona bora ajinyonge (uk. 3).

Mtaalamu huyu anatoa picha halisi ya matukio yanayosawiriwa katika jamii, kwani

ni kweli kwamba matukio ya watu kujiua kwa kujinyonga yamekuwa yakiongezeka

siku hadi siku kutokana na mihemko na misukosuko wanayopitia katika maisha yao.

Kujiua huko huchangiwa na mambo mengi, ambayo kwa kiasi kikubwa, huwaelemea

wahusika na kuwasababishia msongo wa mawazo hasa pale wanapokosa majibu

sahihi ya namna ya kukabiliana na changamoto zao za maisha. Tukio mojawapo

linalothibitisha kuwa matukio ya watu kujiua kwa kujinyonga yapo katika jamii,

lilitokea huko Bukoba tarehe 17.12.2018, kama lilivyofafanuliwa katika kipengele

cha 4.4.1.1.

193

Tukio lingine la namna hiyo, lilitokea mnamo tarehe 24.09.2018 katika Kijiji cha

Mwakiligiri kata ya Mhunduru wilaya ya Misungwi, Mkoani Mwanza, kama

linavyoripotiwa katika www.ippmedia.com. Taarifa hiyo inaeleza kwamba:

Ndugu Kwilokeje Boniface (35), alimuua mkewe, Shija

Chagula (30), kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni wivu

wa mapenzi. Mwanaume huyo alimpiga mkewe sehemu

mbalimbali za mwili wake na baada ya hapo naye kuamua

kujiua kwa kujinyonga. Kutokea kwa tukio hilo kulitokana na

Boniface kumtuhumu mke wake kuwa, alikuwa akitoka nje

ya ndoa yao. Hivyo, kabla ya tukio hilo Boniface alifagia

uwanja na kuondoka. Baada ya muda mfupi, alirudi

nyumbani na kubaini kuwapo kwa mataili ya baiskeli.

Kutokana na hilo, palizuka ugomvi baina yao na ndipo

alipoamua kumpiga mkewe na kumkaba hadi kufa.

Alipobaini kuwa mke wake alikuwa amefariki, ndipo na yeye

aliamua kujiua kwa kujinyonga.

Zaidi ya hayo, huko Tabora kituo cha Televisheni ya Afrika Mashariki

(https://www.eatv.tv/news/current-affairs/) kinaripoti matukio ya watu wawili

waliojiua kwa kujinyonga mnamo tarehe 31.12.2019. Watu hao ni Basili Stephen

Sungu (38) wa shule ya Ikongolo. Huyu alijinyonga katika dari ya chumba

alichokuwa amelala na mkewe, aitwaye Theresia Jumanne Ally (35). Taarifa hiyo

inaeleza zaidi kuwa, uchunguzi wa awali ulibaini kwamba, wanandoa hao walikuwa

na mizozo ya kifamilia na huenda ndiyo iliyosababisha Basili kuamua kujiua. Tukio

lingine lililotokea katika mtaa wa Juhudi katika Manispaa ya Tabora. Katika tukio

hilo, mjasiriamali ndugu James Albert (22), alikutwa akiwa amejinyonga kwenye

kenchi la sebule ya nyumba yake kwa kutumia mkanda wa begi.

Matokeo yanaonesha kwamba haya ni baadhi tu ya matukio ya watu kujiua kwa

kujinyonga, na yamebainishwa kama ithibati ya kushamiri kwake, yanayotokea katika

jamii zetu siku hadi siku. Aidha, tumebaini kuwa njia za kujiua zinazotumiwa na

wahusika katika riwaya teule zinahusiana na zile zinazotumiwa na wahusika

waliotajwa katika matukio yaliyobainishwa hapo awali katika kipengele hiki. Kwa

mfano, katika riwaya ya Rosa Mistika utafiti umebaini kuwa Rosa anaonekana

akihangaika kutafuta kamba, kisha mkanda wa begi ili aweze kufanikisha azma yake

yake ya kujiua. Vivyo hivyo, wahusika waliotajwa katika matukio yaliyoripotiwa

katika jamii, imebainika kwamba wametumia kamba au mkanda wa begi ili kutimiza

azma zao.

194

4.4.2.2 Kujiua kwa Kujipiga Risasi

Kujipiga risasi ni njia nyingine inayotumiwa na watu katika kuyaondoa maisha yao.

Mara nyingi wahusika huacha ujumbe unaobainisha sababu za kujiua kwao. Utafiti

umebaini kuwa, njia hii kwa namna inavyosawiriwa katika riwaya teule, ina

uhusiano mkubwa na matukio halisi yanayohusishwa na njia hii, yanayotokea katika

jamii. Kwa mfano, katika riwaya ya Kichwamaji mwandishi anabainisha namna

Kazimoto anavyoamua kujiua kwa kujipiga risasi, baada ya kupitia changamoto

mbalimbali za kimaisha. Miongoni mwa changamoto hizo ni vifo vya ndugu zake

ambao ni Rukia, mama yake, mtoto wake, pamoja na Kalia. Kabla ya kufikia uamuzi

huo, mwandishi anamchora Kazimoto akiwa katika kina cha tafakuri kuhusiana na

namna kifo chake kitakavyomjia. Anatafakari njia mbalimbali zinazoweza

kuyaangamiza maisha yake, ikiwamo hiyo ya kujiua (uk. 84).

Katika sehemu hiyo, mwandishi anaitafakarisha hadhira yake juu ya maisha, kifo na

hatima yake. Anamtumia mhusika wake Kazimoto kubainisha hali anayokuwa nayo

mtu mwenye dalili za kujiua. Kinachodhihirika bayana ni kwamba mtu huyo huwa

katika hali na tabia tofauti na ile iliyozoeleka. Huonesha dalili za kuyachukia maisha

na kuwaza mambo yahusianayo na kifo. Aidha, imebainika kwamba mtu huyo

husikia sauti tofauti zikimwita. Sauti hizo humwelekeza na kumpa msukumo wa

kufikiria kifo na namna anavyoweza kujiua. Hii ni kwa sababu, suala la kujiua lina

uhusiano mkubwa na magonjwa ya akili16

kama inavyofafanuliwa katika nukuu

inayosema kuwa:

Kuna uhusiano mkubwa baina ya kujiua na magonjwa ya akili.

Tafiti mbalimbali zinabainisha kwamba kuna baadhi ya

magonjwa ya akili ambapo mgonjwa husikia sauti za watu

wakimwelekeza au wakimhoji na kumlazimisha ajiue. Kwa

hiyo, anaposikia sauti hizo huzifuata na kutekeleza kitendo

hicho. Kwa msingi huo, watu wengi hujiua kwa sababu ya

kusikia sauti, kwani kusikia sauti na kupata msongo wa

mawazo ni sehemu ya magonjwa ya akili. Huwezi kujiua

16 Mahojiano baina ya mtafiti na Dkt. Enock Changarawe Novemba 27, 2019.

Yalifanyika katika viunga vya Hospitali ya Magonjwa ya Akili Mirembe. Dkt. Enock

Changarawe ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya akili katika hospitali hiyo.

195

kama si mgonjwa wa akili. Watu wengi hujiua kutokana na

msongo wa mawazo au mshituko wa jambo fulani, kukata

tamaa ghafla na kadhalika. Mtu mwenye shida ya magonjwa

(msongo wa mawazo) huweza kujiua kwa sababu ya kujiona

kwamba hana thamani duniani na anaona ni bora achukue

maamuzi ya kujiua. Msongo wa mawazo ni chanzo namba

mbili cha vifo vya vijana wenye umri kati ya miaka kumi na

tisa na ishirini na tisa (19 – 29). Kwa mujibu wa takwimu

zilizochapishwa na Shirika la Habari la Uingereza (BBC),

tarehe 30.10.2019, watu milioni mia nne hamsini (M. 450)

duniani wanakabiliwa na tatizo la msongo wa mawazo. Hali

hiyo husababisha wengi wao kupata tatizo la afya ya akili.

Baadhi ya watu hao hupata wakati mgumu wa kutafuta

matibabu kutokana na unyanyapaa unaohusishwa na tatizo la

afya ya akili. Kwa hiyo, ni dhahiri kwamba kuna uhusiano

mkubwa kati ya magonjwa ya akili na kujiua, ingawa wengi

wanaweza kuwa si wangonjwa wa akili wa muda mrefu bali

huweza kupata msongo wa mawazo wa ghafla na kujiua.

Kimsingi, kitendo cha kusikia sauti na kupata msongo wa mawazo, ni dalili

mojawapo ya magonjwa ya akili. Hii ina maana kwamba suala la mtu kujiua kama

lilivyoelezwa hapo awali, lina uhusiano mkubwa na masuala ya magonjwa ya akili.

Suala hili linaungwa mkono na Ng‘ambi17

anayesema kuwa:

Kuna baadhi ya magonjwa ya akili ambapo mgonjwa husikia

sauti za watu wakimhoji na kumtaka ajiue kabla watu wengine

hawajamuua. Mara nyingi mtu huyo hupata msukumo wa

kuzisikiliza na kuzifuata sauti hizo. Inajulikana kwamba

asilimia tisini ya watu wanaojiua huwa na matatizo ya akili na

asilimia chache zinazosalia hutokana na matatizo mengine.

Hata hivyo, ukiwaza vizuri utagundua kwamba mtu yeyote

anayejiua kwa wakati ule tendo hilo linapofanyika, hali yake ya

akili huwa si sawa. Ifahamike kwamba ugonjwa wowote ule ni

mkusanyiko wa dalili. Hivyo, kila mtu ana tatizo la akili,

ingawa viwango vinatofautiana. Magonjwa ya akili

yanayohusiana na sonona na msongo wa mawazo, huweza

kusababisha mtu kujiua.

17 Mahojiano baina ya mtafiti na Bw. Paschal John Ng‘ambi Novemba 29, 2019.

Yalifanyika katika viunga vya Hospitali ya Magonjwa ya Akili Mirembe. Bw.

Paschal John Ng‘ambi ni Muuguzi Kiongozi katika hospitali hiyo.

196

Maelezo haya yanaleta picha kuwa, binadamu au kiumbe kingine chochote kile

kinaweza kuumwa kiungo fulani katika mwili wake. Kuna watu wanaumwa moyo au

tumbo la uzazi au la kawaida. Hivyo, imebainika kuwa akili nayo inaweza kuumwa

kama ilivyo kwa kiungo kingine chochote. Akili ikiumwa ndipo mgonjwa huanza

kusikia sauti kama vile mtu anamwita na anajiona ni bora afe kwa sababu amepoteza

imani ya kuishi au kujisikia kutokuwa na amani ya kuishi. Hali hiyo ndiyo

iliyomkumba Kazimoto, kwani inaelezwa kuwa kabla ya kuchukua uamuzi wake wa

kujiua, alisikia sauti zikimwita pasipo kujua sauti hizo zinamaanisha nini na zinatoka

wapi. Anasema:

―Nilisimama pale dirishani kwa muda mrefu nikifikiri.

Nilifikiri furaha ilikuwa imetawaliwa sana na huzuni. Salima

ambaye siku moja alitwambia kwamba kwa jambo lile alikuwa

haoni tofauti yetu na ng‘ombe, yeye mwenyewe hana raha

sasa. Wakati nilipokuwa nikifikiri juu ya maisha nilisikia kitu

fulani kama sauti ikiniita‖ ―Kazimoto!‖ Sauti ilisikika

polepole. ―Naam,‖ nilijibu kimoyomoyo. Nilikwenda ndani ya

chumba cha kulala. Sabina alikuwa amejifunika shuka akilia

kwa kwikwi. Nilichukua kitu fulani. Nilikuwa sifahamu jambo

nililokuwa ninafanya, isipokuwa nguvu fulani zilikuwa

zikiniongoza – sauti! Sauti!‖ (uk. 195).

Kwa kuzingatia nukuu hii, matokeo yanaonesha kwamba tukio la mtu kujiua,

huambatana na mvurugiko wa akili yake. Ndiyo maana mwandishi anaeleza kuwa,

Kazimoto akiwa katika mchakato huo wa kujiua anashindwa kutambua kila

kinachomtokea katika maisha yake kwa wakati huo, bali anasukumwa na nguvu isiyo

ya kawaida inayomtaka atimize kusudio lake. Hivyo, ni dhahiri kuwa watu wengi

hujiua kwa kufuata na kusikiliza sauti, ambazo huwaelekeza kufanya tukio la kujiua.

Mwandishi anaonesha kuwa, hata Kazimoto kabla ya kuchukua uamuzi wake wa

kujiua, anatokewa na hali ya namna hiyo na anasikia sauti zikimpa msukumo wa

kufanya tendo hilo. Msukumo huo unamfikisha katika tukio halisi la kujiua kwa

kujipiga risasi huku akiacha ujumbe juu ya meza ukielezea sababu za kujiua kwake

(uk. 195).

Kujiua basi, ni jambo linaloelekeana sana na matendo na ni mchakato unaoambatana

na viashiria na tabia fulani anazoonesha mhusika, kabla ya kitendo chenyewe cha

kujiua. Kwa hiyo, kujiua ni matokeo ya tabia na vitendo hivyo. Mtu mwenye

ugonjwa wa akili huonesha hisia, fikra na tabia zisizokuwa za kawaida. Vilevile,

197

huweza kufanya matendo yasiyokuwa ya kawaida, ijapokuwa mwenyewe huwa

hatambui hali hiyo. Matokeo yanaonesha kuwa magonjwa mengi ya akili

husababishwa na vinasaba vya urithi, sababu za kisaikolojia pamoja na vichocheo

vingine vya kimazingira. Vichocheo hivyo ni kama vile matumizi ya madawa ya

kulevya, maisha magumu, kuzidisha mambo kama vile kusoma sana, mrundikano wa

mambo au matatizo ya kimaisha, pamoja na ulevi. Hata hivyo, imebainika kuwa

binadamu yeyote ana uwezekano wa kupata ugonjwa wa akili wakati wowote bila

kujali kama ni kijana au mzee.

Kwa jumla, utafiti umebaini kuwa matukio ya watu kujiua kwa kujipiga risasi,

yamekuwa yakiripotiwa mara kwa mara na vyombo vya habari katika jamii zetu.

Matukio haya yamekuwa yakihusishwa na masuala mbalimbali kama vile kusalitiana

katika mapenzi baina ya wapenzi au wanandoa pamoja na visasi mbalimbali. Hili

linathibitishwa katika gazeti la Habari Leo la Septemba 11, 2019. Taarifa hiyo inadai

kuwa: ―Watanzania 666 wamejiua kwa kipindi cha miaka minne kinachoanzia 2016

hadi 2019, ambapo kati ya hao, watu 5 wamejiua kwa kujipiga risasi.‖ (uk. 8).

Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime anathibitisha hili katika mazungumzo

yake na waandishi wa habari kwenye maandhimisho ya Siku ya Kupinga na Kuzuia

Kujiua, ambayo hufanyika kila mwaka Septemba 10.

Tukio lingine la kujiua kwa risasi lilitokea katika Mkoa wa Mwanza, Mei 25, 2018.

Taarifa ya tukio hilo, ilitolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Ahmed Msangi.

Alielezea tukio hilo kuwa:

Ndugu Maxmilliani Ngedere Tula (miaka 40), alimpiga risasi

mke wake aitwaye Teddy Patrick (miaka 38) kwa kutumia

bastola yenye namba BJ. 30666 yenye usajili 00103129, kisha

naye kujiua kwa kujipiga risasi. Anafafanua zaidi kuwa wote

wawili walikuwa wafanya biashara wa samaki. Anaongeza

kuwa tukio hilo lilitokea muda mfupi baada ya wanandoa hao

kurudi nyumbani wakitokea kwenye shughuli yao ya biashara.

Anaendelea kueleza kuwa, wanandoa hao wakati wakiwa

chumbani kwao, walisikika kama wanagombana ambapo

muda mfupi baadaye, ilisikika milio ya risasi kadhaa huko

chumbani kwao (Global Habari Tv on line Mei 26,2018).

Kutokea kwa tukio hili ni uthibitisho kwamba matukio ya kujiua kwa kutumia njia

mbalimbali yapo katika jamii zetu. Matukio haya kama ilivyoelezwa hapo awali,

198

huchangiwa sana na masuala mbalimbali ya kijamii, yanayofungamana na maisha ya

jamii husika. Hivyo, ni wazi kuwa kuna uhusiano wa njia za kujiua kwa wahusika,

zinazosawiriwa katika riwaya teule na zile zinazotumiwa na wahusika katika maisha

halisi ya jamii.

4.4.2.3 Kujiua kwa Kujichoma Kisu

Hii ni njia nyingine ya kujiua inayosawiriwa katika riwaya teule na katika jamii.

Utafiti umebaini kuwa, kuna uhusiano wa namna njia hii inavyosawiriwa na

wahusika katika riwaya teule na hali halisi ya watu kujiua katika jamii. Kwa mfano,

katika riwaya ya Rosa Mistika mwandishi anamwonesha Rosa Mistika akiwa katika

harakati za kujiua kwa kujichoma kisu, mara tu baada ya kupewa barua ya

kufukuzwa Chuo cha Ualimu Morogoro. Inaelezwa kwamba baada ya kupokea barua

hiyo, anaamua kulala kitandani akilia na kutokwa na machozi mengi, kiasi cha

kuweza kujaza kikombe cha chai, huku kichwa chake kikimwanga. Kilio hicho

kinasababisha amlalamikie na kumlaumu Mungu kwa madai kwamba, ndiye chanzo

cha mateso na mahangaiko yake (uk. 45). Matokea yake anaamua kukata tamaa

kwani haoni sababu ya kuendelea kuishi kama inavyoelezwa katika nadharia ya

Udhanaishi. Mwandishi analithibitisha hili anaposema:

… Mwishowe alikumbuka kwamba alikuwa na kisu kidogo

sandukuni. Alifungua sanduku upesiupesi ili akomeshe taabu

zake na hasira yake kushuka. Alikitoa. Alikikunjua. Rosa

alipasua gauni lake tumboni apate mahali pa kupitishia kisu.

Alifumba macho aliposikia kisu kinagusa tumbo lake. Rosa

alianza kukisukuma polepole ili kiingie tumboni mwake.

Ngozi ya juu ilikuwa imekwisha kwaruzwa aliposikia mkono

wake unashikwa. Rosa alikuwa mikononi mwa Albert (uk.

66).

Dondoo hili linamwonesha Rosa Mistika akiwa katika hali ya mahangaiko, mateso

na maumivu makali, yanayomkatisha tamaa ya maisha yake. Hali hiyo ndiyo

inayompa msukumo wa kufanya maamuzi ya kutaka kujiua kwa kisu pale

anapolazimishwa kuacha chuo na kurudi nyumbani bila ya cheti cha ualimu.

Kutokana na hilo, anaona kuwa maana ya maisha ni upuuzi mtupu. Hivyo, anaamua

kukengeuka misingi ya jamii yake kwa kutaka kufanya kitendo cha kujiua, ambacho

hakikubaliki na ni kinyume na maadili ya jamii yake.

199

Kwa jumla, katika kipengele hiki tumebaini kuwa kuna uhusiano wa njia hii ya watu

kujiua kwa kutumia visu kama inavyosawiriwa katika riwaya ya Rosa Mistika, na

matukio halisi ya kujiua katika jamii. Taarifa kuhusiana na suala hili, inathibitishwa

na gazeti la Habari Leo la Septemba 11, 2019. Inataja watu 219 waliojiua kwa

kujichoma visu kwa kipindi cha miaka minne kinachoanzia 2016 hadi 2019 na

kwamba idadi hiyo inafuatia, baada ya wale waliojiua kwa kujinyonga, ambao ni

367. Zaidi ya hilo, inabainisha wingi wa matukio ya watu kujichoma visu kwa

kipindi hicho cha miaka minne, ambapo kwa mwaka 2016 pekee, matukio hayo ni

131 (uk. 8). Hii ni idadi kubwa ikilinganishwa na miaka mingine.

4.4.2.4 Kujiua kwa Kutumia Sumu

Kujiua kwa kutumia sumu ni njia nyingine inayotumiwa na watu wengi katika

kuyakatisha na kuyafupisha maisha yao. Katika riwaya ya Kichwamaji suala hili

linajitokeza kupitia kwa Kazimoto anayetafakari njia inayoweza kuyaondoa maisha

yake. Miongoni mwa njia hizo ni sumu. Anasema:

―Usiku nilianza kufikiri juu ya kifo. Nilifikiri jinsi kifo changu

kitakavyonijia – kwa ugonjwa, kwa ajali au kwa

kukatwakatwa na wezi? Labda kwa uzee au kwa sumu! ….‖

(uk. 84).

Katika dondoo hili, mwandishi anabainisha njia kadhaa za kujiua, zinazomjia

Kazimoto akilini mwake, ikiwamo ya kutumia sumu. Kwa kufanya hivyo, anatupa

picha na kuthibitisha kuwa tendo la kujiua, huwa halimtokei mtu kwa ghafla bali

huwa ni mchakato wa muda mrefu au mfupi kutegemeana na sababu husika. Tafakuri

inayofanywa na Kazimoto inaonesha kuwa, mchakato wa kujiua kwake unachukua

muda mrefu, ndiyo maana anafikiria hata njia inayoweza kutumika katika kuyaondoa

maisha yake. Hii inatokana na ukweli kwamba kujiua huanza na sababu

inayohusishwa na tukio katika muktadha fulani, ambapo tukio lingine huweza

kutokea ghafla na kufanya mchakato huo, kuwa mfupi na wakati mwingine kuwa

mrefu. Hili linafafanuliwa na Ng‘ambi (keshatajwa) anaposema kuwa:

Kwa hakika, mpaka mtu anafikia tendo lenyewe la kujiua,

huwa anapitia hatua kadhaa. Hatua hizo ni kama vile,

matamanio ya kufa (death wish), mawazo ya kujiua (suicidal

ideas or thoughts), kujirudiarudia kwa viwango vya kufikiria

kujiua na kupanga kujiua pamoja na kuamua njia

atakayoitumia kufikia azma hiyo.

200

Hili ndilo linajitokeza pia kwa Kazimoto, kwani tukio la kujiua kwake halimtokei

ghafla, bali linachukua muda mrefu. Anafikia hatua ya kufikiria njia ya kuitumia

katika kujiua kwake kutokana na kukata tamaa ya maisha.

Kwa upande wa riwaya ya Rosa Mistika, kuna tukio moja tu la msichana mmoja

kumwekea Rosa sumu kwenye maji kwa lengo la kumdhuru. Tukio hilo linamtokea

Rosa akiwa katika shule ya Msingi Nyakabungo, Mkoani Mwanza, ambapo baada ya

kuchemsha maji hayo, yanabadilika rangi. Aidha, maji hayo yanapo mwagwa nje,

kesho yake, sehemu hiyo inageuka na kuwa kichuguu kikubwa (uk.72-73). Hii ina

maana kuwa sumu hiyo iliwekwa kwa makusudi katika maji hayo kwa lengo la

kuyaangamiza maisha ya Rosa Mistika. Kwa mantiki hiyo, ni dhahiri kuwa sumu ni

njia mojawapo inayotumiwa na watu katika kuyaondoa maisha yao au kuyaondoa na

kuyakatisha maisha ya watu wengine.

Nje ya fasihi, utafiti umebaini kuwapo kwa matukio ya watu kujiua kwa kutumia

sumu katika jamii. Gazeti la Habari Leo la Septemba 11, 2019, linabainisha matukio

ya watu waliojiua kwa kutumia sumu kwa kipindi cha mwaka 2016 hadi 2019 kuwa

ni watu 75. Matukio hayo ni kama ifuatavyo: ―Mwaka 2019 watu 8, mwaka 2018

watu 21, mwaka 2017 watu 16 na mwaka 2016 watu 30‖ (uk. 8). Taarifa hiyo

inabainisha sababu za watu hao kujiua kuwa, ni pamoja na masuala ya mahusiano ya

kimapenzi, ugomvi wa kifamilia, matatizo kazini na ugumu wa maisha. Inaongeza

kuwa msongo wa mawazo, ndio unaowasukuma zaidi watu kujiua kutokana na

kukosa watu wa kuwapa ushauri wa namna ya kukabiliana na vyanzo vyake.

Kutokana na hilo, imebainika kuwa matukio mengi ya watu kujiua kwa njia

mbalimbali ikiwamo ya kutumia sumu, yamekuwa yakiripotiwa mara kwa mara.

Aidha, tukio lingine la mtu kujiua kwa kutumia sumu liliripotiwa na kituo cha

televisheni cha Azam tarehe 30.4.2018. Taarifa hiyo inaeleza kuwa Maganiko Nunda

(42) mkazi wa Geita, aliamua kujiua kwa kunywa sumu tarehe 29.4.2018. Sababu ya

kujiua kwake inatajwa kuwa ni mgogoro baina yake na mkewe, Salome Josefu.

Akisimulia kuhusiana na mgogoro huo, Frank Maganiko, ambaye ni mtoto wa

marehemu, anadai kuwa kwa muda mrefu baba yake alikuwa ametofautiana na

mama yake. Kutokana na hilo, mama yake aliamua kuondoka hapo nyumbani siku

nne kabla ya tukio hilo kutokea. Frank anafafanua zaidi kuwa, mara kwa mara baba

201

yake alikuwa akitishia kwamba atajiua au kuua mmojawapo wa wanafamilia.

Hatimaye, azma yake ikatimia huku akiacha ujumbe unaobainisha sababu za

kuchukua uamuzi huo. Ujumbe huo unasema:

Mimi Maganiko C. Nunda,

Ndugu zangu, na jamii inayonizunguka, nawaomba nimechoka

na manyanyaso ninayoifanyia hii familia yangu, mke pamoja

na watoto mpaka sasa mama watoto wa familia hayupo.

Ukweli hapa mimi ni kikwazo cha kuisumbua familia, sana

sana mke wangu ninachomfanyia imefikia sehemu sasa hata

mimi mwenyewe kimeniumiza na sioni tena umuhimu wa

kuishi popote pale duniani.

Taarifa zaidi kuhusiana na tukio hilo inadai kuwa, kabla ya tukio hilo marehemu

alionekana akinywa pombe nyingi tofauti na hali yake ya kawaida. Kitendo hicho

kiliwashangaza watu wengi. Uchunguzi wa awali ulibaini kuwa, kulikuwa na

msuguano wa kutoelewana baina yake na mkewe. Kutokana na hilo, ndipo Maganiko

alipoamua kujiua. Hata hivyo, taarifa hiyo ilifafanua kuwa uchunguzi zaidi wa tukio

hilo, ulikuwa bado unaendelea ili kubaini hasa chanzo chake, ikiwa ni pamoja na

kubaini aina ya sumu aliyoitumia.

Kinachojitokeza kupitia tukio hilo ni kwamba jamii haina elimu ya kutosha

kuhusiana na dalili za mtu anayepanga kujiua. Hii inatokana na ukweli kwamba

mhusika alishaanza kuonesha dalili hizo kwa kuongelea masuala ya kujiua au kuua

mmojawapo wa wanafamilia, lakini hakuna aliyeshtuka na kuchukua hatua za

kumsaidia. Pia, kitendo cha mhusika kunywa pombe nyingi tofauti na hali yake ya

mazoea kilitosha kubaini kuwa, hakuwa katika hali yake ya kawaida. Matokeo yake

hata mke wake aliamua kujitenga naye kwa kumwacha peke yake, hadi alipokutwa

na mtoto wake akiwa amejiua. Alifikia hatua hiyo kutokana na kukosa msaada. Hali

hiyo ilisababisha akate tamaa kama inavyoelezwa katika nadharia ya Udhanaishi kwa

kuona kwamba maisha yake hayana maana tena na hana mahali pengine pa kuishi.

Kwa jumla, sehemu hii ilikusudia kufanya tathmini ya uhusiano baina ya usawiri wa

matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya

kujiua katika jamii. Uhusiano huo umechunguzwa kwa namna mbili. Mosi, uhusiano

wa sababu za matukio ya kujiua zinazosawiriwa katika riwaya teule na vichocheo

vya kujiua katika jamii. Pili, uhusiano wa njia za kujiua zinazosawiriwa katika

202

riwaya teule na katika mazingira halisi ya jamii. Tathmini hiyo inaonesha kuwa,

kuna uhusiano mkubwa baina ya sababu za matukio ya kujiua zinazosawiriwa katika

riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii kwa jumla. Hata

hivyo, licha ya kuwapo kwa uhusiano huo, utafiti umebaini kwamba matukio ya

kujiua katika riwaya teule, ni usawiri wa kisanaa wa mwandishi. Hii ina maana kuwa

mwandishi ameamua kuyasawiri matukio hayo kama nyenzo ya kupenyezea na

kupitishia falsafa yake ya Udhanaishi kama kipengele kimojawapo cha kifasihi.

Aidha, tumebaini kuwa kuna uhusiano baina ya njia za kujiua zinazosawiriwa katika

riwaya teule na zile zinazotumiwa na wahusika katika mazingira halisi ya jamii.

Hivyo, kwa kuwa dhima mojawapo ya fasihi ni kuimulika jamii na kusawiri kuhusu

kuwapo au kutokuwapo kwa jambo fulani, utafiti umebaini kwamba suala la kujiua

lipo katika jamii kama linavyosawiriwa katika riwaya teule.

Sambamba na hilo, tumebaini kuwa mwandishi haishii katika kulisawiri tu suala la

kujiua, bali anaihakiki jamii yake kwa kuchunguza mfumo wa maisha pamoja na

mchakato mzima wa mtu hadi kufikia hatua ya kujiua. Vilevile, tumeona kuwa kuna

uhusiano mkubwa kati ya kujiua na masuala ya magonjwa ya akili pamoja na athari

za kisaikolojia. Hii ina maana kwamba mtu hufikia hatua ya kujiua baada ya

kuathiriwa kiakili na kisaikolojia. Pamoja na hayo yote, tasinifu imebainisha kuwa

watu wengi hawana uelewa wa kutosha kuhusu dalili za mtu kujiua, licha ya kuwapo

kwa matukio mengi ya watu kujiua katika jamii. Kwa mantiki hiyo, mtafiti anaona

kuwa kama hazitachukuliwa jitihada za kutosha za kuielimisha jamii kuhusiana na

suala la watu kujiua, basi tatizo hili litaendelea kuzikumba na kuziathiri jamii zetu

siku hadi siku.

4.5 Muhtasari wa Sura ya Nne

Kwa jumla, sura hii ilijikita katika kujadili matukio ya mchakato wa kujiua

yanavyosawiriwa katika riwaya ya Rosa Mistika (1971), Kichwamaji (1974), na

Dunia Uwanja wa Fujo (1975). Pia, ilijadili sababu mbalimbali za mitanziko ya

wahusika kama zinavyosawiriwa katika riwaya hizo. Hatimaye, imehitimishwa kwa

kutathmini uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua katika

riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii.

203

Katika uchunguzi wetu tulibaini kwamba hizi ni riwaya za mwanzo kabisa za

kiuhalisia za Euphrase Kezilahabi. Nazo, zinajikita katika kushughulikia matatizo

halisi yanayozikumba jamii katika mazingira halisi, hususani mazingira ya

mwandishi. Vilevile, tulibaini kwamba riwaya hizi ni za kiuhalisia kwa sababu

zinaakisi hali halisi ya maisha ya jamii husika. Aidha, wahusika wake ni wa kawaida

kwani wanapatikana katika mazingira ya kawaida na wanasawiri tajiriba za maisha

ya jamii husika.

Sura inayofuata inawasilisha muhtasari wa matokeo ya tasinifu hii, mahitimisho

pamoja na mapendekezo ya maeneo yanayohitaji kutafitiwa zaidi.

204

SURA YA TANO

MUHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO

5.1 Utangulizi

Sura hii inawasilisha muhtasari wa matokeo ya utafiti, hitimisho, na mapendekezo ya

maeneo yanayohitaji utafiti zaidi.

5.2 Muhtasari wa Tasinifu Hii

Tasinifu hii ina jumla ya sura tano. Sura ya kwanza inajenga msingi wa utafiti kwa

kuanza na ufafanuzi wa dhana muhimu zilizotumika katika utafiti huu, usuli wa

tatizo la utafiti, tamko la utafiti, malengo ya utafiti, maswali ya utafiti, manufaa ya

matokeo ya utafiti, pamoja na mawanda ya utafiti. Lengo kuu la utafiti lilikuwa ni

kuchunguza usawiri wa mchakato wa kujiua katika riwaya teule za Euphrase

Kezilahabi na kuona kama kujiua huko ni mwangwi wa mtanziko wa kijamii au la.

Ili kufikiwa kwa lengo hili kuu, utafiti ulikuwa na malengo mahususi matatu: Mosi,

kubainisha usawiri wa matukio yanayounda mchakato wa kujiua katika riwaya teule

za Euphrase Kezilahabi; pili, kuchunguza sababu za mitanziko ya wahusika

zinazosawiriwa katika riwaya teule; na tatu, kutathmini uhusiano baina ya usawiri wa

matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya

kujiua katika jamii.

Sura ya pili inahusu mapitio ya maandiko na viunzi vya nadharia zilizotumika katika

utafiti huu. Misingi ya nadharia ya Udhanaishi na ile ya Sosholojia ya Kifasihi ndiyo

iliyomwongoza mtafiti, na hatimaye, kufikiwa kwa lengo kuu pamoja na malengo

mahususi. Maandiko yaliyopitiwa yaligawanywa kama ifuatavyo: Mosi, mapitio ya

maandiko kuhusu kazi za Euphrase Kezilahabi kwa jumla; pili, mapitio kuhusu

mchakato wa kujiua katika riwaya teule za Euphrase Kezilahabi; na tatu, mapitio

kuhusu dhana ya kujiua kwa mitazamo ya nje ya Fasihi. Baada ya kupitia maandiko

hayo, mianya mbalimbali ya kiutafiti ilibainishwa. Mianya hiyo ni pamoja na: tafiti

zilizotangulia kushindwa kubainisha kwa kina matukio ya mchakato wa kujiua,

sababu za mitanziko ya wahusika, na kutotathminiwa kwa uhusiano wa usawiri wa

matukio ya kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya kujiua katika jamii. Pia,

tulibaini kwamba tafiti nyingi zimefanywa kwa mwegamo wa nadharia moja tu ya

Udhanaishi pasipo kuhusisha na nadharia nyingine, ikiwamo ya Sosholojia ya

Kifasihi, ili kubaini uhusiano wa matukio ya kujiua katika riwaya na miktadha ya

205

maisha ya jamii. Vilevile, tafiti hizo zilifanywa kipwekepweke kwa jicho la

kisosholojia, kisaikolojia, na kiafya pasipo kuhusishwa na fasihi. Hali kadhalika,

utafiti huu umebaini kwamba tafiti nyingi za kifasihi zilizotangulia, zilishughulikia

tatizo la kujiua kwa kujikita katika matini pekee pasipo kuchunguza hali halisi katika

jamii.

Sura ya tatu imefafanua kwa kina namna utafiti huu ulivyofanyika. Vipengele

muhimu vilivyoshughulikiwa ni usanifu wa utafiti, mkabala wa utafiti, eneo la

utafiti, walengwa wa utafiti, na njia za ukusanyaji wa data. Vipengele vingine ni

mchakato wa ukusanyaji wa data, mbinu za uchambuzi wa data, maadili na itikeli za

utafiti, pamoja na uhalali na uthabiti wa data. Kwa jumla, data zilikusanywa kwa

kutumia mbinu kuu mbili, ambazo ni: usomaji na uchambuzi makini wa matini teule

pamoja na mahojiano na watafitiwa uwandani. Usanifu wa utafiti huu ni wa

kifenomenolojia, na mkabala wa uchanganuzi wa data ni wa kitaamuli. Mbinu

iliyotumika katika uchambuzi wa data ilikitwa katika mwegamo wa kimaudhui.

Mbinu hii ilimwezesha mtafiti kuunganisha, kuainisha, kulinganisha na kufafanua

data zilizopatikana maktabani na zile za uwandani, hivyo, kuwezesha upatikanaji wa

matokeo bora.

Sura ya nne ilihusu uwasilishaji wa data na mjadala wa matokeo ya utafiti. Sehemu

ya kwanza ilihusu ubainishaji wa usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua katika

riwaya teule za Euphrase Kezilahabi. Utafiti umebaini kwamba matukio ya mchakato

wa kujiua yameshamiri katika riwaya teule zote tatu. Katika riwaya ya Rosa Mistika,

matukio yaliyobainishwa yanamhusu mhusika mkuu, Rosa Mistika, ambayo ni:

kupigwa na baba yake, kuwachongea wasichana wenzake, kuota ndoto, na

kusimamishwa shule, kufumaniwa na kufukuzwa chuo. Matukio mengine ni kutoa

mimba, kujitenga na kutengwa na jamii yake, na kuachwa na mchumba wake,

Charles. Katika riwaya ya Kichwamaji, matukio yaliyobainishwa yanamhusu

mhusika mkuu, Kazimoto. Nayo ni: kunyimwa kazi, Rukia kutiwa mimba, vifo vya

Rukia na mama yake, na kifo cha Kalia. Matukio mengine ni kifo cha mtoto wake,

kuugua ugonjwa wa ajabu, na kujitenga kijamii. Katika riwaya ya Dunia Uwanja wa

Fujo, matukio ya mchakato wa kujiua yaliyobainishwa ni: matukio ya aibu na

fedheha, na tukio la Tumaini kumuua Mkuu wa Wilaya. Kwa jumla, matokeo ya

utafiti yanaonesha kuwa matukio yanayosawiriwa katika riwaya hizo, ndiyo

206

yaliyounda mchakato wa kujiua kwa wahusika. Vilevile, utafiti umebaini kwamba

wahusika hao kabla ya kuchukua uamuzi wa kujiua, walipitia changamoto nyingi

maishani mwao. Hatimaye, walikosa uvumilivu ambapo, walikata tamaa na

kuchukua uamuzi wa kujiua.

Sehemu ya pili, imejadili sababu za mitanziko ya wahusika zinazosawiriwa katika

riwaya teule za Euphrase Kezilahabi. Utafiti umebaini kwamba sababu mbalimbali

za kijamii, kiutamaduni, kiuchumi, na kifalsafa, kwa kiasi kikubwa, huchangia watu

kupata mitanziko ya kimaisha. Sababu za kijamii zilizobainishwa ni: mfumo wa

malezi na mahusiano ya kimapenzi. Kuhusiana na mfumo wa malezi, tumebaini

kwamba ili kujenga misingi bora na imara ya maisha ya watoto, jamii inatakiwa

kushikamana na kushirikiana katika jukumu zima la malezi. Kwa upande wa

mapenzi, tumebaini kwamba mahusiano ya kimapenzi ni janga linalosababisha

mifarakano na mitanziko katika jamii. Sababu za kiutamaduni zilizobainishwa ni:

urithi wa mali, mila na desturi, pamoja na masuala ya dini na elimu. Vilevile, utafiti

umebaini kwamba masuala haya yanatakiwa kufanyika kwa tahadhari kubwa ili

yasiwe chanzo cha mitanziko katika jamii. Kuhusiana na sababu za kiuchumi,

tumebaini kwamba, hizi huweza kusababisha mtu kukosa mwelekeo wa maisha na

hata kukata tamaa. Sababu zilizojadiliwa ni umaskini na hali ngumu ya maisha na

tatizo la ukosefu wa kazi. Pia, tasinifu inabainisha sababu za kifalsafa ambazo pia,

huweza kuwa chanzo cha mtu kupata mitanziko. Sababu hizo zimegawanywa katika

makundi matatu, ambayo ni: mtanziko kuhusu dhana ya maisha, dhana ya kifo, na

dhana kuhusu Mungu. Utafiti umebaini kwamba dhana ya maisha ni ngumu

kueleweka kutokana na kuwapo kwa mitazamo mbalimbali isiyofanana miongoni

mwa watu. Kuhusiana na suala la kifo na maisha baada ya kifo, nalo pia lina

mitazamo mbalimbali. Kwa upande mwingine, suala la kuwapo au kutokuwapo kwa

Mungu limezua mjadala mkubwa miongoni mwa watu. Mkanganyiko huo, ndio

husababisha mitanziko kwa wahusika.

Katika sehemu yetu ya tatu, tulifanya tathmini ya uhusiano baina ya usawiri wa

matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na vichocheo vya kujiua katika

jamii. Utafiti umebaini kwamba kuna uhusiano mkubwa baina ya matukio ya kujiua

yaliyomo katika riwaya teule na vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii kwa

jumla. Hata hivyo, utafiti umebaini kwamba kwa namna fulani mwandishi wa riwaya

207

teule, aliamua kuyasawiri matukio hayo katika riwaya zake kama mbinu ya kisanaa

ya kuipenyeza na kuipitisha falsafa yake ya Udhanaishi kama kipengele kimojawapo

cha kifasihi.

Hatimaye, sura ya tano imetoa muhtasari, hitimisho na mapendekezo kuhusu tafiti

zijazo. Imeanza na utangulizi wa mambo yaliyoelezwa katika sura hii na kufuatiwa

na muhtasari wa matokeo ya utafiti kwa jumla. Kisha, imetoa hitimisho la utafiti

linalojumuisha vipengele vitatu, ambavyo ni: utoshelevu wa nadharia zilizotumika,

mchango mpya wa utafiti huu, na mapendekezo kuhusu tafiti zijazo.

5.3 Hitimisho la Tasinifu Hii

Sehemu hii inalenga kutoa ufafanuzi wa maeneo makuu matatu, mbayo ni:

utoshelevu wa nadharia zilizotumika, mchango mpya unaotokana na utafiti, na

mapendekezo kuhusu tafiti zijazo.

5.3.1 Utoshelevu wa Nadharia Zilizotumika

Utafiti umetumia nadharia mbili, ambazo ni: Nadharia ya Udhanaishi na nadharia ya

Sosholojia ya Kifasihi. Misingi au mihimili ya nadharia hizi imemsaidia na

kumwongoza mtafiti katika mjadala wa utafiti wake. Nadharia ya Udhanaishi

ilimwongoza katika mjadala wa matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule

na sababu za mitanziko ya wahusika zinazosawiriwa katika riwaya teule za Euphrase

Kezilahabi. Nadharia hii ilikuwa mwafaka katika malengo hayo kwa sababu matukio

ya kujiua na sababu za mitanziko hutokana na mhusika kukata tamaa, kama

inavyobainishwa katika misingi ya nadharia hii. Mjadala wa lengo la tatu ulihusisha

misingi ya nadharia zote mbili. Hii ni kwa sababu lengo hili lilikusudia kutathmini

uhusiano baina ya usawiri wa matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na

vichocheo vya matukio ya kujiua katika jamii. Hivyo, misingi ya nadharia hizi

ilikamilishana, kwani tukio la mtu kukata tamaa na kujiua linahusishwa na misingi

ya nadharia ya Udhanaishi, na vichocheo vya kujiua huchangiwa na mazingira ya

kijamii kama inavyoelezwa katika nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi.

Hivyo, mtafiti anaamini kwamba, kwa kuwa nadharia hizo mbili zimejengana na

kukamilishana, matokeo ya utafiti huu yamekidhi haja na kutosheleza ubora na

uthabiti wa kile kilicholengwa. Hii ni kwa sababu matokeo yake yamekidhi kusudio

la mtafiti na anaamini kwamba matokeo haya yatakidhi hata haja na kiu za wasomaji

208

na jamii kwa jumla katika mambo mengi, ambayo hayakufahamika awali kabla ya

kufanyika kwa utafiti huu.

5.3.2 Mchango Mpya wa Matokeo ya Utafiti Huu

Utafiti una mchango mkubwa kwa jamii na taifa kwa jumla kama ifuatavyo:

5.3.2.1 Mchango wa Kijamii

Utafiti una mchango kwa jamii kwa sababu unaipa mwanga wa kutambua kuwa

matukio ya kujiua huwa hayamtokei ghafla, bali ni mchakato kwa anayejiua. Kama

ilivyofafanuliwa katika tasinifu hii, tofauti na tafiti mbalimbali zilizotangulia, kujiua

kulitazamwa kama tukio tu, hivyo kulifanya suala hilo kueleweka kwa mawanda

finyu. Utafiti huu umebaini kwamba kujiua husababishwa na mambo mengi ambayo

humzonga mhusika kabla ya kufikia kitendo chenyewe. Hivyo, matokeo ya utafiti

yataisaidia jamii kuyafahamu baadhi ya matukio ya mchakato wa kujiua, sababu za

mitanziko ya wahusika, na athari za miktadha mbalimbali anayopitia mhusika katika

maisha yake, ambayo huweza kusababisha kufikia maamuzi ya kujiua.

5.3.2.2 Mchango wa Kitaaluma

Mosi, utafiti unaleta mtagusano wa kitaaluma kwa kuzishikamanisha nyuga

mbalimbali zikiwamo za Afya, Saikolojia, Sosholojia, na Fasihi. Kutokana na

mwingiliano huo wa kitaaluma, jamii itaongeza na kupanua welewa zaidi kwamba

suala la kujiua ni mtambuka na linaweza kushughulikiwa na nyuga mbalimbali,

ikiwamo Fasihi.

Pili, ni mchango wa kinadharia na kiuchambuzi. Hii inatokana na ukweli kwamba

watafiti wengi waliozitafiti kazi za Euphrase Kezilahabi walijiegemeza zaidi katika

nadharia ya Udhanaishi. Hivyo, utafiti huu licha ya kuendeleza nadharia hiyo ya

Udhanaishi, pia umetumia nadharia nyingine ambayo ni Sosholojia ya Kifasihi.

Tumefanya hivyo ili kuonesha kuwa kuna nadharia nyingine zinazoweza ama

kusimama peke yake kushughulikia kazi za kidhanaishi au kwa kushirikiana na

nadharia yenyewe ya Udhanaishi katika kuhakiki kazi za Euphrase Kezilahabi.

Tatu, matokeo ya utafiti huu ni chanzo kimojawapo muhimu cha taarifa kwa watafiti

na wasomaji wengine wanaochunguza na kutafiti kazi za Fasihi zenye mwelekeo wa

kujiua. Aidha, kwa kuwa utafiti huu una mawanda ya kisaikolojia, kisosholojia na

209

kiafya, una mchango pia, kwa watafiti wa nyuga hizo, na siyo kwa uga wa Fasihi

peke yake.

5.3.2.3 Mchango wa Kisera

Matokeo ya utafiti huu yanaweza kutumiwa na watunga sera, pamoja na wakuuzaji

mitalaa ya elimu kulipatia uzito suala la kujiua na kuchukua hatua madhubuti za

kuielimisha jamii kuhusu namna ya kujiepusha nalo. Elimu hiyo ni pamoja na

kuzielewa dalili za mtu anayekusudia kuchukua uamuzi wa kujiua, namna ya

kuwasaidia watu wenye dalili hizo na kuepuka unyanyapaa. Kutekelezwa kwa jambo

hili kutaiepusha na kuikinga jamii na balaa hili.

5.3.3 Mapendekezo Kuhusu Tafiti Zijazo

Sehemu hii inatoa mapendekezo yanayotokana na mada ya utafiti uliofanyika kwa

ajili ya tafiti zijazo. Maeneo yanayopendekezwa hayakuwa sehemu ya malengo ya

utafiti wetu. Hata hivyo, kwa kuwa yanahitaji zaidi majibu ya kiutafiti, tunadhani

kwamba ipo haja ya kumakinikiwa na tafiti zijazo.

Pendekezo la kwanza linahusu haja ya kufanyika kwa utafiti kuhusu mchakato wa

kujiua katika jamii nyingine za Tanzania ili kubaini zaidi ukubwa wa tatizo hili

katika jamii kwa upana wake. Hii inatokana na ukweli kwamba kutokana na suala la

muda na rasilimali, utafiti huu haukuweza kuchunguza matukio ya mchakato wa

kujiua katika jamii zote za Tanzania, bali kwa kiasi kikubwa uliilenga jamii ya

mwandishi wa riwaya teule. Hata hivyo, mifano ya jamii nyingine imetolewa kama

ithibati tu ya kile kilichobainika katika jamii ya mwandishi. Hivyo, kwa kuwa

imethibitika kwamba matukio ya mchakato wa kujiua bado yapo katika jamii zetu,

kuna haja ya kufanya utafiti zaidi katika jamii nyingine za Tanzania. Hii itasaidia

kubaini iwapo matukio ya mchakato wa kujiua yaliyobainishwa katika utafiti huu,

yanafanana na kujiua kwa wahusika katika jamii nyingine za Tanzania.

Pendekezo la pili ni wito wa tafiti nyingi zaidi kufanyika katika tanzu nyingine za

Fasihi kama vile Ushairi, tamthiliya, na Fasihi Simulizi. Hii ni kwa sababu matokeo

ya tafiti hizo, yatazisaidia jamii zetu kuelewa mambo mbalimbali yanayozikumba,

likiwemo suala la kujiua. Pia, kueleweka kwa mambo hayo kutayapa uzito zaidi

matokeo ya utafiti huu kuhusu kuwapo kwa matukio ya kujiua pamoja na mazingira

na michakato ya mtu kujiua.

210

Pendekezo la tatu ni kwamba, kwa kuwa utafiti huu umelishughulikia suala la kujiua

kwa kuhusisha masuala ya kisaikolojia, kiafya, na kisosholojia; kuna haja ya suala

hili kutafitiwa pia, kwa kulihusisha na masuala ya Kiikolojia na Kijaala au Ujaala.

Katika mtazamo wa jumla, Ujaala ni hali ya kunasibisha kuwapo kwa viumbe

waliomo duniani, pamoja na hali au matukio yote yawakumbayo, na uwezo wa

Mungu. Hii ina maana kwamba hata uwezo wa kisanii pamoja na mambo

yamtokeayo binadamu, ya ustawi wake na anguko lake, hutokana na kani ya Mungu,

ambayo iko juu ya uwezo wake, huyo binadamu. Hivyo, matukio ya mchakato wa

kujiua yachunguzwe kwamba, hutokea kwa kuhusishwa na mipango ya Mungu,

yaani kwamba kujiua kwa mtu kuchunguzwe kama ni mpango wa Mungu.

Kwa upande wa Kiikolojia, utafiti ufanyike kwa kuhusisha mchakato wa kufa na

kujiua kama sehemu ya kutengeneza uwiano katika jamii kwa manufaa ya viumbe

wote na vizazi vyote. Hii ni kwa kuwa uhakiki wa Kiikolojia huchunguza uhusiano

uliopo kati ya fasihi na mazingira. Hivyo, kufanyika kwa utafiti wenye mwegamo

huo, kutasaidia kutetea na kupigania mazingira na kuinusuru dunia isiangamizwe na

uharibifu wa matendo ya mwanadamu. Aidha, kufanyika kwa utafiti kwa mtazamo

wa Kiikolojia, kutawezesha kuusaili mtazamo unaomwona binadamu kuwa kiini cha

ulimwengu, mlengwa wa kila jambo, mmiliki na mnufaika halali wa mazingira, na

maumbile yote. Kwa kufanya hivyo, utasaidia kumbainisha binadamu kama kiumbe

na zao mojawapo tu la maumbile; na kwamba hana haki kuwazidi viumbe wengine.

211

MAREJELEO

Adolf, G. (2019, Novemba 30). Ajinyonga Baada ya Kuamka na Kumkosa Mkewe

Kitandani. Mtanzania (uk. 3).

Allan, R. (2003). Senior Biology 2. New Zealand: Bio Zone International Ltd.

Awolalu, J. O. (1976). ―What is African Traditional Religion?‖ Studies in

Comparaetive Religion. 10 (2), (1 – 10).

Babbie, E. (1999). The Basics of Social Research. Belmont: Wadsworth Publishing

Company.

BAKITA, (2017). Kamusi Kuu ya Kiswahili ya BAKITA. Dar es Salaam: Longhorn

Publishers Ltd.

BAKIZA, (2010). Kamusi la Kiswahili Fasaha. Kenya: Oxford University Press,

East Africa Ltd.

Balisidya, M. L .Y. (1973). Fasihi ya Kiswahili. Mulika, (2: 12 – 17).

BBCswahili.com. (2018). Dira ya Dunia. Taarifa ya Habari za Dunia. Siku ya

Jumanne, tarehe 25.9.2018, Saa Tatu Usiku.

Brentano, F. (1995). Psychology from an Empirical Standpoint. London: Routledge.

Bryman, A. (2004). Social Research Methods. New York: Oxford University Press.

Camus, A. (1954). The Stranger. New York: Vintage Books.

Camus, A. (1984). The Myth of Sisyphus, and Other Essays. London: Penguin.

Chuachua, R. (2016). Falsafa ya Riwaya za Saaban Robert na Euphrase Kezilahabi

katika Muktadha wa Epistemolojia ya Kibantu. Tasinifu ya Shahada ya

Uzamivu katika Fasihi ya Kiswahili (Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha

Dodoma.

212

Cohen, L. na Lawrence, M. (2000). Research Methods in Education. London:

Routledge.

Coser, L. (1963). Sociology through Literature: An Introductory Reader. Prentice

Hall, Englewood Cliffs.

Cruswell, J. W. (2009). Research Design: Qualitative, Quantitative and Mixed

Method Approaches, (toleo la 3). London: Sage Publications.

Densin, N. K. na Lincoln, Y. S. (Wah.), (2000). Handbook of Qualitative Reseach.

London: Sage Publications.

Diegner, L. (2002). Allegories in Euphrase Kezilahabi‘s Early Novels. Swahili

Forum, (ix: 43 – 74).

Diegner, L. (2005). Intertextuality in the Contemporary Swahili Novel: Euphrase

Kezilahabi‘s Nagona and William Mkufya‘s Ziraili Na Zirani. Paper Presented

at 17th

Swahili Collequim in Bayreuty, Mei 21 - 23, 2004. AAP 51: 117 - 125

http://www.ifeas.uni-mainz.de/SwaFo/SF12Diegner.pdf, 10/12/2017, saa 5

Asubuhi.

Durkheim, E. (1979). Suicide: A Study in Sociology (Translated by J. A. Spaulding &

G. Simpson). New York: The Free Press. (Original Work Published in 1897).

Drake, P. and Linda, H. (2011). Practitioner Research at Doctoral Level:

Develioping Coherent Research Methodologies. New York: Routledge and

Taylor & Francis Group.

Enon, J. C. (1998). Education Research, Statistics and Measurement. Kampala

Uganda: Makerere University.

Ezra, F. (2019, Septemba 27). Watu 200 Hujiua Tanzania. Tanzania Daima (uk. 3).

Famila ya Maamkio Mapanda (1997). Biblia Takatifu. Jimbo la Bologna Italia:

Mediagraf, Noventa Padovana PD.

213

Faustine, S. (2017). Falsafa ya Waafrika na Ujenzi wa Mtindo wa Uhalisiajabu

katika Riwaya za Kiswahili. Tasinifu ya Shahada ya Uzamivu katika Fasihi ya

Kiswahili (Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Dodoma.

Faustine, S. (2019). Falsafa ya Waafrika kama Kijenzi cha Mtindo na Uhalisiajabu

katika Riwaya za Kiswahili. Koja la Taaluma za Insia, Wah. Ponera, A. S na

Z. A. Badru. Dar es Salaam: Karljamer Publishers Limited. Kur. 378 – 401.

Flavian, L. (2012). Usimulizi katika Riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo. Tasinifu ya

Digrii ya Uzamili (Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Dar es Salaam..

Freeman, E. (1971). The Theatre of Albert Camus (A Critical Study). London:

Methuen and Co. Uk. 5.

Freud, S. (1900). The Interpretation of Dreams. The Complete and Definitive Text,

Translated and Edited by James Strachey (2010). Basic Book Group. New

York: The Hogarth Press, Ltd.

Friedman, M. (1973). Burried Alive: The Biography of Janis Joplin. New York:

Morrow.

Fuluge, A. (2013). Dhana ya Kujiua katika Kazi za Kezilahabi. Tasinifu ya

Kukamilisha Mahitaji ya Masomo ya Umahiri katika Kiswahili

(Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Dodoma.

Gay, L. R. (1987). Educational Research: Competence for Analysisi and Application.

Ohio: Merril Publishing Company.

Glucksman, M. L na Kramer, M. (2017). Manifest Dream Content as Predictor of

Suicidality. Psychodynamic Psychiatry, 54(2), (175 – 185).

Hegel, G. W. F. (1956). The Philosophy of History (Tafsiri ya J. Sibree). New York:

Dover Publications Inc.

Hountondji, P. J. (1983). African Philosophy: Myth and Reality. London: Hutchinson

University Library for Africa.

214

Jimbo Kuu Katoliki la Songea (1998). Katekisimu Ndogo ya Kanisa Katoliki.

Peramiho: Peramiho Printing Press.

Karerega, B. D. & Shenk, D. W. (1980). Islam and Christianity. Nairobi: Uzima

Press.

Katare, E. R. (2007). Julius Kambarage Nyerere: Falsafa Zake na Dhana ya

Utakatifu. Dar es Salaam: Creative Prints Limited.

Kaufmann, W. (1976). Existentialism, Religion and Death. New York: Meridian.

Kezilahabi, E. (1971). Rosa Mistika. Dar es Salaam: East Africa Literature Bureau.

Kezilahabi, E. (1973). Dunia Uwanja wa Fujo. Dar es Salaam: East Africa Literature

Bureau.

Kezilahabi, E. (1974). Kichwamaji. DSM: EAPH.

Kezilahabi, E. (1979). Gamba la Nyoka. Arusha – Dar es Salaam: EAP.

Kezilahabi, E. (1985). Cha Mnyonge Utakitapika Hadharani: (Mzalendo, 7 Aprili

1992), Misingi ya Hadithi Fupi, (107 – 113).

Kezilahabi, E. (1985). African Philosophy and the Problem of Literary Interpretation.

Tasinifu ya Shahada ya Uzamivu (Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha

Wisconsin Madison.

Kezilahabi, E. (1990). Nagona. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press.

Kezilahabi, E. (2011). Mzingile. Nairobi: Vide – Muwa Publishers Limited.

Kezilahabi, E. (2003). Utunzi wa Riwaya na Hadithi Fupi, katika Makala za Semina

ya Kimataifa ya Waandishi wa Kiswahili III Fasihi. Taasisi ya Uchunguzi wa

Kiswahili. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, (203 – 231).

215

Kipacha, A. (2019). Kifo au Maisha ya Maumivu: Usomaji wa Rosa Mistika ya

Euphrase Kezilahabi kwa Jicho la Kikanushi. Katika Ponera, A. S & Badru, Z.

A. (Wah.), Koja la Taaluma za Insia: Kwa heshima ya Prof. Madumulla (422 -

434). Dar es Salaam: Karljamer Publishers Ltd.

Kitereza, A. (1980). Bwana Muyombokere na Bi. Bugonoka, Ntulanalwo na

Bulihwali, Juzuu ya I na II. Dar es Salaam: Tanzania Printing House.

Kitomari, S. (2018, Desemba 27). Ajinyonga hadi Kufa kwa Kuchoka Kusumbua

Familia. Nipashe (uk. 3).

Kombo, D. K. na Tromp, D. L. (2006). Proposal and Thesis Writing and

Introduction. Nairobi: Pauliness Publications.

Kothari, C. R. (2004). Research Methodology: Methods and Techniques. New Delhi:

New Age International Publishers.

Kothari, C. R. (2009). Research and Methodology: Methods and Techniques. New

Delhi: New Age International Publishing Ltd.

Lyimo, J. (2019, Februari 24). Watoto Wawili Marafiki Wajinyonga. Mwananchi

(uk. 4).

Kubler-Ross, E. (1991). On Death and Dying. New York: Macmillan Publishing Co.

Madumulla, J. S. (1993). Mwandishi wa Riwaya ya Kiswahili na Suala la Ukweli wa

Maisha. Fasihi, Uandishi na Uchapaji, ed by Mulokozi, M. M. & C. G.

Mung‘ong‘o. Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press, (141 – 153).

Madumulla, J. S. (2009). Riwaya ya Kiswahili: Nadharia, Historia, na Misingi ya

Uchambuzi. Dar es Salaam: Mture Educational Publishers Limited.

Magesa, L. (1977). African Religion: The Moral Traditionals of Abundant Life.

Nairobi: Pauline Publications Africa.

Magesa, N. J. (1999). Mbinu za Ndoa Visiwani Ukerewe. Dar es Salaam: Chuo

Kikuu cha Dar es Salaam.

216

Maltsberger, J. T. (1993). Dream and Suicide. Suicide and Life - Threatening

Behavior. Vol. 23 (1), The American Association of Suidology. New York:

Plenum.

Mason, M. (2011). The Sample Size and Saturation in PhD Studies Using Qualitative

Interviews. Forum: Qualitative Social Reseach, 11(3), (45 – 52).

Mbatiah, M. (1998). Mienendo Mipya katika Uandishi Mpya wa Kezilahabi: Nagona

na Mzingile. Mulika, (24: 1 – 11).

Mbiti, J. S. (1969). African Religions and Philosophy. London: Heinemann.

Mbiti, J. S. (1970). The Concept of God in Africa. London: S.P.C.K.

Mbiti, J. S. (2010). Introduction to African Religion. Kampala: East African

Educational Publishers Ltd.

Mbiti, J. S. (2011). African Religions and Philosophy. Kampala: East African

Educational Publishers Ltd.

Menkiti, I. (1984). Person and Community in African Traditional Thought. Katika R.

Wright (mhariri). African Philosophy, An Introduction of Lanham. MD:

University Press of America.

Merriam, S. B. & Tisdell, E. J. (2016). Qualitative Research: A Guide to Design and

Implementation. 4th

Edition. San Francisco. Jossey-Bass.

Mlaga, W. (2019). Euphrase Kezilahabi kama Mwanafalsafa Kamili: Mifano Kutoka

Riwaya ya Mzingile. Mulika Na. 37, Dar es Salaam: TUKI.

Mlacha, S. A. K. (1985). Wahusika katika Riwaya ya Kiswahili Tanzania. Mulika,

Na.17.

Mlacha, S. A. K. (1991). Point of View as Stylistic Device in Kiswahili Novels.

Kiswahili: Jarida la Uchunguzi wa Kiswahili, (58: 54 – 61).

217

Mlacha, S. A. K na Madumulla, J. S. (1991). Riwaya ya Kiswahili. Dar es Salaam:

Dar es Salaam University Press.

Mnenuka, A. J. (2011). Falsafa ya Maisha katika Ushairi wa Mugyabuso Mulokozi

na Shaaban Robert. Kioo cha Lugha, (9: 104 – 121).

Moustakas, C. (1994). Phenomenological Research Methods, Thousand Oaks, CA:

Sage.

Mpalanzi, L. E. (2019). Makutano kati ya Dini ya Jadi na za Kigeni: Mifano kutoka

Riwaya Teule za Kiswahili. Kioo cha Lugha, (17: 114 – 131).

Mphahlele, E. (1976). A Guide to Creative Writing. Nairobi: EALB.

Msangi, S. E. (2012). Taswira katika Riwaya za Euphrase Kezilahabi: Aina na

Sababu za Kutumiwa kwake katika Rosa Mistika, Nagona na Mzingile.

Tasinifu ya Kukamilisha Mahitaji ya Digrii ya Kwanza katika Sanaa na

Elimu (Haijachapishwa). Chuo cha Waislamu Morogoro.

Msokile, M. (1992). Misingi ya Hadithi Fupi. Dar es Salaam: Dar es Salaam

University Press.

Muhando, P. na Balisidya, N. (1976). Fasihi na Sanaa za Maonesho. Dar es Salaam:

TPH.

Muller, R. W. (1964). The Testament of Samuel Beckett. London: Faber and Faber.

Mulokozi, M. M. (1983). Dunia Uwanja wa Fujo (Mapitio ya Kitabu). Kiswahili:

Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili, 50(1), (1 – 12).

Mulokozi, M. M . (2010). ―A Survey of Kiswahili Literature: 1970 - 1980‖, Current

Research Interest: Kiswahili Language and Literature, Writing and Publishing.

University of Dar es Salaam. www.gap.urgent.be/Africafocus 18/11/2018 saa

9.20 usiku.

Mulokozi, M. M. (2017). Utangulizi wa Fasihi ya Kiswahili. Dar es Salaam:

KAUTTU.

218

Mungah, C. I. (1999). Dhana ya Maisha katika Novela Mbili za Euphrase

Kezilahabi: Nagona na Mzingile. Tasinifu ya Kutosheleza Baadhi ya Mahitaji

ya Shahada ya ―Masters of Arts‖ (Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Nairobi.

Mung‘ong‘o, C. G. (1977). Mirathi ya Hatari. Dar es Salaam: Mkuki na Nyota

Publishers Ltd.

Musau, P. M. (1985). Euphrase Kezilahabi: Mwandishi Aliyekata Tamaa. Tasinifu

ya MA (Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Nairobi.

Musau, P. M. (1995). Kezilahabi na Thomas Hardy Sarafu ya Pili? Kioo cha Lugha,

(1. Na. 2.

Mwandishi Wetu. (2017, Januari 25). Tanzania ya 27 Afrika Matukio ya Watu

Kujinyonga – WHO. Mtanzania (uk. 4).

Mwandishi Wetu. (2019, Septemba 11). Watanzania 666 Wajiua kwa Visu, Sumu,

Kujinyonga. Habari Leo (kur. 1: 8).

Mwaniki, J. M. & Geoffrey, G. G. (2009). Fundamental of Biology. Dar es Salaam:

Educational Publishers.

Narizvi, S. (1982). The Sociology of Literature of Politics. Australia: Edamund

Burke.

Neubeck, K. (1986). Social Problems: A Critical Perspective. New York: Random

House.

Ndosi, N. K, Mbonde, M. P, na Lyamuya, E. (2004). ―Profile of Suicide in Dar es

Salaam.‖ Dar es Salaam, East African Medical Journal, Vol. 81 No. 4, uk. 207

- 211.

Njogu, K. na Chimerah, R. (2008). Ufundishaji wa Fasihi: Nadharia na Mbinu.

Nairobi: Jommo Kenyatta Foundation.

219

Oriedo, H. E. (2000). Fani katika Riwaya za Shaaban Robert: Kusadikika, Utubora

Mkulima na Siku ya Watenzi Wote. Tasinifu ya Shahada ya Uzamivu

(Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Moi.

Patton, M. Q, na Michael, C. (2002). Qualitative Research Methodology: A Guide to

Using Medicine. London: Sans Frontieres.

Practorius, R. T. (2006). ―Suicide and Community Traumatic Events: Is there a

Connection?‖ Ph.D Thesis, The School of Human Resource Education and

Workforce Development, Texas University.

Ponera, A. S. (2014). Ufutuhi katika Nathari ya Kiswahili: Ulinganisho wa Nathari

za Shaaban Robert na Euphrase Kezilahabi. Tasinifu ya Shahada ya Uzamivu

ya Sayansi Jamii katika Fasihi ya Kiswahili (Haijachapishwa). Chuo Kikuu

cha Dodoma.

Ponera, A. S. (2016). Suala la Matumizi ya Nadharia kama Kiunzi cha Tafiti za

Kitaamuli: Mfano wa Matumizi ya Nadharia ya Ukanivali. Journal of

Humanities, 3 (116 – 129).

Ponera, A. S. (2019). Misingi ya Utafiti wa Kitaamuli na Uandishi wa Tasinifu.

Dodoma: Central Tanganyika Press.

Reed, E. (1975). Women’s Revolution: From Matriarchat Clan to Patriarchal

Family. New York: Path Finder Press, Inc.

Robert, S. (2013). Kufikirika. Dar es Salaam: Mkuki na Nyota Publishers.

Sabinus, J. (2018, Novemba 5). Wanaojinyonga Nchini Idadi Yao Inatisha. Habari

Leo (kur. 1 - 2).

Sakkos, T. (2008). ―Existentialism and Feminism in Kezilahabi‘s Novel

Kichwamaji.‖Swahili Forum, (15: 51 – 61).

Selden, R. na Wenzake (2005). A Reader Guide to Contemporary Theory. London:

Pearson Education Ltd.

220

Sengo, T. (2009). Utafiti wa Utani Ukwereni. Dar es Salaam: AERA Kiswahili

Researched Product.

Senkoro, F. E. M. K. (1977). Riwaya ya Kiswahili na Maendeleo ya Umma. Tasinifu

ya Uzamili (Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Senkoro, F. E. M. K. (1995). Euphrase Kezilahabi: Shaaban Robert wa Pili. Kioo cha

Lugha, Juzuu 1.

Senkoro, F. E. M. K. (1996/7). Nadharia ya Fasihi na Fasihi ya Kiswahili ya

Majaribio. Kioo cha Lugha 2.

Senkoro, F. E. M. K. (2006). Fasihi ya Kiswahili ya Majaribio: Makutano ya Fasihi

Andishi na Simulizi. Kioo cha Lugha, (4: 22 – 38).

Senkoro, F. E. M. K. (2007). Uhalisiamazingaombwe katika Fasihi ya Kiswahili:

Istilahi Mpya, Mtindo Mkongwe. Kioo cha Lugha, (5: 1 – 12).

Senkoro, F. E. M. K. (2011). Fasihi. Dar es Salaam: KAUTTU.

Schram, T. H. (2003). Conceptualizing Qualitative Inquiry. Upper Sanddle River,

NJ: Merrill Prentice Hall.

Sletteboe, W. (1997). Dilemma: A Concept Analysis, in Journal of Advanced

Nursing 26 (3), (449 – 454).

Sletteboe, W. (1987). Celebrities & Suicide: A Taxonomy and Analysis (1948 -

1983), American Sociological Review, 52(3), (401 – 412).

Taylor, D. J na wenzake. (1997). Biological Science. New York: Cambridge

University Press.

Temples, P. (1959). Bantu Philosophy. Paris: Presence Africaine.

Tiwari, P. & Ruhela, S. (2012). ―Social Isolation & Depression among Adolescent: A

Comparative Perspective‖, 2nd International Conference on Social Science

and Humanity IPEDR vol. 31, IACSIT Press, Amity University, Singapore.

221

TUKI. (2013). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Dar es Salaam: Oxford University Press.

TUKI. (2014). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Dar es Salaam: Oxford University Press.

Van Manen, M. (2014). Phenomenology of Practice: Meaning–giving Methods in

Phenomenological Research and Writing. Wulnut Creek, CA: Left Coast

Press.

Vasques, A. S. (1973). Art and Society. New York: Monthly Review Press.

Wafula, R. M na Njogu, K. (2007). Nadharia za Uhakiki wa Fasihi. Nairobi: The

Jomo Kenyatta Foundation.

Wellek, R. na Warren, A. (1949). Theory of Literature. London: Penguin Books Ltd.

Wamitila, K. W. (1997). What‘s in a Name: Towards Literary Onomastics in

Kiswahili Literature AAP 60: Swahili Forum VI, pp. 35 – 44.

Wamitila, K. W. (2002). Uhakiki wa Fasihi, Misingi na Vipengele Vyake. Nairobi:

Phoenix Publishers Limited.

Wamitila, K. W. (2003). Kamusi ya Fasihi: Istilahi na Nadharia. Nairobi: Focus

Books Publications Limited.

Wamitila, K. W. (2006). Uhakiki wa Fasihi, Misingi, na Vipengele Vyake. Nairobi:

Phoenix Publishers Ltd.

Wamitila, K. W. (2008). Kanzi ya Fasihi: Misingi ya Uchanganuzi wa Fasihi.

Nairobi: Vide Muwa Publishers Ltd.

Wanjala, F. S. (2013). Kitovu cha Fasihi Simulizi kwa Shule na Vyuo. Mwanza:

Serengeti Publishers Ltd.

Williams, R. M. (1970). American Society: A Sociological Interpretation. New York:

Random House.

222

Wiredu, K. (1980). Philosophy and African Culture. London: Cambridge University

Press.

Wizara ya Elimu na Utamaduni. (1992). Historia ya Falsafa ya Elimu. Dar es

salaam: National Printing Company.

WHO. (2018). Tanzania ya 27 Afrika Matukio ya Watu Kujinyonga: (Mtanzania, 25

Januari, 2018; uk. 4).

223

VIAMBATISHO

A: Vibali na Barua za Ruhusa kwa Ajili ya Utafiti

224

225

226

227

228

229

B. Miongozo ya Ukusanyaji wa Data

B.1 Mwongozo wa Usomaji na Uchambuzi makini wa Matini

Vyanzo vya Kusomwa Vipengele Sababu

Riwaya teule na vyanzo

mbalimbali vya taarifa

kama vile magazeti,

redio, na televisheni.

Matukio ya mchakato wa

kujiua na sababu za

mtanziko wa wahusika

katika riwaya teule

Kubainisha ujitokezaji

wa matukio ya mchakato

wa kujiua na kubaini

sababu za mitanziko ya

wahusika katika riwaya

teule.

Miktadha ya utokeaji wa

matukio ya mchakato wa

kujiua.

Kubainisha uhusiano wa

sababu za matukio ya

kujiua na njia za

wahusika kujiua.

B.2 Mwongozo wa Mahojiano

B.2.1 Mahojiano kwa Viongozi wa Dini

Jina langu ni Adria Fuluge, mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu katika Fasihi ya

Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dodoma. Mada ya utafiti ni: ―Usawiri wa Mchakato wa

Kujiua katika Riwaya Teule za Euphrase Kezilahabi: Ni Mwangwi wa

Mtanziko wa Kijamii?” Lengo la utafiti huu ni kuchunguza na kubaini matukio ya

mchakato wa kujiua katika riwaya teule, pamoja na miktadha ya utokeaji wake katika

jamii ya mwandishi. Kabla ya kuanza mahojiano haya, naomba kukujulisha kuwa

taarifa utakazotoa zitakuwa ni siri baina ya mtafiti na wewe, na zitatumika tu kwa

lengo la utafiti huu. Tafadhali, naomba ushirikiano wako katika mahojiano haya.

1. Tafadhali, unaweza kututajia jina lako na kutupa maelezo mafupi kuhusu

huduma za kiroho unazofanya katika jamii yako.

2. Kwa mtazamo wako, mchakato wa kujiua ni nini?

3. Kwa maoni yako na unavyofahamu, ni matukio gani husababisha watu

kujiua? Je, ni miktadha ya namna gani husababisha mtu kuchukua uamuzi wa

kujiua?

4. Katika vitabu vitakatifu na mafundisho ya dini yako, kujiua kunatazamwaje

na ni adhabu gani humpata anayejiua? Je, unadhani fikra za watu wanaojiua

kuhusu Mungu na maisha yao kwa jumla zikoje?

5. Kwa maoni yako, unafikiri kuna uhusiano gani baina ya matukio

yanayosababisha mhusika kujiua na miktadha (mazingira) ya jamii husika?

230

B.2.2 Mwongozo wa Mahojiano kwa Wananchi wa Ukerewe

Jina langu ni Adria Fuluge, mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu katika Fasihi ya

Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dodoma. Mada ya utafiti ni: ―Usawiri wa Mchakato wa

Kujiua katika Riwaya Teule za Euphrase Kezilahabi: Ni Mwangwi wa

Mtanziko wa Kijamii?” Lengo la utafiti huu ni kuchunguza na kubaini matukio ya

mchakato wa kujiua katika riwaya teule, pamoja na miktadha ya utokeaji wake katika

jamii ya mwandishi. Kabla ya kuanza mahojiano haya, naomba kukujulisha kuwa

taarifa utakazotoa zitakuwa ni siri baina ya mtafiti na wewe, na zitatumika tu kwa

lengo la utafiti huu. Tafadhali, naomba ushirikiano wako katika mahojiano haya.

1. Tafadhali unaweza kututajia jina na umri wako?

2. Unamfahamu Euphrase Kezilahabi? Kama ndiyo, elezea ni kwa vipi na kwa

namna gani?

3. Kuna madai kuwa jamii ya watu wanaoishi katika Mkoa wa Mwanza,

hususani katika kisiwa cha Ukerewe, ina tabia ya kujiua. Je, madai hayo yana

ukweli kiasi gani? Na kama ni kweli, ni watu wa rika na jinsia gani zaidi

wanaofanya mambo hayo?

4. Kama madai ya swali la tatu hapo juu ni ya kweli, je, ni miktadha/mazingira

gani husababisha kutokea kwa mambo hayo? Je, nini husababisha watu hao

kujiua? Na, je, kabla ya kujiua kwao, huonesha dalili gani au zipi?

5. Kama madai ya swali la nne hapo juu ni kweli, je, matukio hayo ya mchakato

wa kujiua hutokea wakati gani na katika miktadha au mazingira gani?

Hutumia mbinu gani katika kutimiza azma hiyo?

B.2.3 Mwongozo wa Mahojiano kwa Viongozi wa Serikali

Jina langu ni Adria Fuluge, mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu katika Fasihi ya

Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dodoma. Mada ya utafiti ni: ―Usawiri wa Mchakato wa

Kujiua katika Riwaya Teule za Euphrase Kezilahabi: Ni Mwangwi wa

Mtanziko wa Kijamii?” Lengo la utafiti huu ni kuchunguza na kubaini matukio ya

mchakato wa kujiua katika riwaya teule, pamoja na miktadha ya utokeaji wake katika

jamii ya mwandishi. Kabla ya kuanza mahojiano haya, naomba kukujulisha kuwa

taarifa utakazotoa zitakuwa ni siri baina ya mtafiti na wewe, na zitatumika tu kwa

lengo la utafiti huu. Tafadhali, naomba ushirikiano wako katika mahojiano haya.

231

1. Matukio ya watu kujiua yamekuwa yakiripotiwa mara kwa mara katika

vyombo vya habari hapa nchini. Je, hali ikoje katika Mkoa huu wa Mwanza?

2. Kulingana na unavyofahamu, ni kundi la rika na umri gani limekuwa

likihusishwa na mchakato wa kujiua mara kwa mara?

3. Kama tatizo hili lipo katika Mkoa huu wa Mwanza, je, wanaojiua zaidi ni

wale wanaotoka mjini au vijijini? Kiwango chao cha elimu kikoje?

4. Matukio ya mchakato wa kujiua hutokea zaidi wakati gani na katika miktadha

ya namna gani? Na, je, wanaojiua huacha ujumbe au taarifa yoyote

inayohusiana na tukio la mchakato huo wa kujiua?

5. Kwa nafasi yako ya uongozi serikalini, kuna jitihada gani katika kumaliza au

kutatua na kukabiliana na tatizo hili?

6. Ni miktadha ya namna gani ya kijamii ambayo huweza kusababisha mhusika

kujiua? Je, Serikali hukabiliana vipi na miktadha hiyo ili kupunguza au

kutokomeza matukio haya ya kujiua?

B.2.4 Mwongozo wa Mahojiano kwa Wataalamu wa Saikolojia na Magonjwa ya

Akili

Jina langu ni Adria Fuluge, mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu katika Fasihi ya

Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dodoma. Mada ya utafiti ni: ―Usawiri wa Mchakato wa

Kujiua katika Riwaya Teule za Euphrase Kezilahabi: Ni Mwangwi wa

Mtanziko wa Kijamii?” Lengo la utafiti huu ni kuchunguza na kubaini matukio ya

mchakato wa kujiua katika riwaya teule, pamoja na miktadha ya utokeaji wake katika

jamii ya mwandishi. Kabla ya kuanza mahojiano haya, naomba kukujulisha kuwa

taarifa utakazotoa zitakuwa ni siri baina ya mtafiti na wewe, na zitatumika tu kwa

lengo la utafiti huu. Tafadhali, naomba ushirikiano wako katika mahojiano haya.

1. Tafadhali, unaweza kututajia jina lako na kutupa maelezo mafupi kuhusu

huduma za kiafya unazofanya katika jamii yako.

2. Kwa mtazamo wako, kujiua ni nini na mchakato wa kujiua ni nini? Je, kuna

aina ngapi za kujiua?

3. Wewe ni mtaalamu wa saikolojia/magonjwa ya akili. Unadhani kuna

uhusiano gani baina ya masuala ya kisaikolojia/kiakili na mchakato wa

matukio ya kujiua?

4. Je, ni sababu na matukio ya namna gani husababisha mtu kujiua? Je, mtu

anayetaka kujiua huwa na tabia au dalili zipi?

232

5. Tafiti mbalimbali za kisaikolojia, kishosholojia na kiafya zimefanyika

kuhusiana na watu kujiua, lakini bado tatizo hili lipo katika jamii. Nini maoni

yako juu ya hili?

6. Kuna uhusiano gani baina ya magonjwa ya akili na mtu kujiua? Je, anayejiua

ni lazima awe na matatizo au magonjwa ya akili?

B.2.5 Mwongozo wa Mahojiano kwa Wataalamu na Wahakiki wa Kazi za

Fasihi

Jina langu ni Adria Fuluge, mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu katika Fasihi ya

Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dodoma. Mada ya utafiti ni: ―Usawiri wa Mchakato wa

Kujiua katika Riwaya Teule za Euphrase Kezilahabi: Ni Mwangwi wa

Mtanziko wa Kijamii?” Lengo la utafiti huu ni kuchunguza na kubaini matukio ya

mchakato wa kujiua katika riwaya teule, pamoja na miktadha ya utokeaji wake katika

jamii ya mwandishi. Kabla ya kuanza mahojiano haya, naomba kukujulisha kuwa

taarifa utakazotoa zitakuwa ni siri baina ya mtafiti na wewe, na zitatumika tu kwa

lengo la utafiti huu. Tafadhali, naomba ushirikiano wako katika mahojiano haya.

1. Kwa namna unavyomfahamu Kezilahabi kwa kupitia kazi zake au kwa

kuonana naye ana kwa ana, unaweza kumwelezeaje kitabia na maisha yake

kwa jumla?

2. Ni tukio au matukio gani ya kujiua yaliyomo katika kazi teule (Rosa Mistika,

Kichwamaji, na Dunia Uwanja wa Fujo) za Euphrase Kezilahabi

unayoyakumbuka? Je, matukio hayo yana maana gani katika mchakato wa

kujiua?

3. Kwa maoni yako, unaweza kuelezeaje kuhusu kuwapo au kutokuwapo kwa

uhusiano baina ya matukio ya mchakato wa kujiua katika riwaya teule na

miktadha ya jamii ya mwandishi?

4. Suala la kujiua linajitokeza sana katika muktadha wa kisosholojia, kiafya na

kisaikolojia, na tafiti nyingi zimefanywa kwa mwegamo huo. Je, Fasihi ina

nafasi gani katika mchakato wa kujiua?

5. Pamoja na tafiti mbalimbali kufanyika kuhusiana na tatizo la watu kujiua

katika jamii, bado tatizo hili lipo na linazikumba jamii nyingi duniani kote,

ikiwa ni pamoja na Tanzania kwa umahususi. Unadhani tatizo hili

linachangiwa na nini, na nini kifanyike?

233

C. Taarifa za Watafitiwa

Na Jina Shughuli

Afanyayo

Mahali pa

Mahojiano

Tarehe ya

Mahojiano

1 Dkt. Athumani

Salumu Ponera

Mhadhiri

Mwandamizi

Chuo cha

Kumbukumbu ya

Mwalimu Nyerere

17/2/2020

2 Dkt. Stella Faustine Mhadhiri Chuo Kikuu cha

Dodoma

9/11/2019

3 Dkt. Erasto Kano Mhadhiri Chuo Kikuu cha

Dodoma

18/1/2020

4 Dkt. Florentina

Nsolezi

Mhadhiri Chuo Kikuu cha

Dodoma

30/11/2019

5 Dkt. Rashid

Chuachua

Mh. Mbunge

Jimbo la Masasi

Jijini Dodoma 10/11/2019

6 Dkt. Enock

Changarawe

Daktari Bingwa

wa Magonjwa

ya Akili

Hospitali ya

Mirembe Dodoma

27/11/2019

7 Dkt. Gema Peter

Simbe

Daktari Bingwa

wa Magonjwa

ya Akili

Hospitali ya

Mirembe

29/11/2019

8 Dkt. Ramadhan

Thomas Kadala

Mhadhiri Chuo Kikuu cha

Dar es Salaam

1/10/2019

9 Dkt. Angelus

Mnenuka

Mhadhiri Chuo Kikuu cha

Dar es Salaam

1/10/2019

10 Pd. Ibrahim Ngassa Padre Viunga vya

Seminari ya

Mtakatifu Maria

Nyegezi Mwanza

17/12/2019

11 Bw. Flavian Ilomo Mhadhiri

Msaidizi

Chuo Kikuu cha

Dar es Salaam

2/10/2019

12 Bw. Selestino

Helman Msigala

Mhadhiri

Msaidizi

Chuo Kikuu cha

Dar es Salaam

30/9/2019

13 Bw. Paschal John

Ng‘ambi

Muuguzi

Kiongozi

Hospitali ya

Mirembe

29/11/2019

14 Bw. Edmund

Makaranga Tangi

Mkulima Namagondo,

Ukerewe

17/12/2019

15 Bw. Pantaleo Vicent

Tilibuzya Nagane

Mkulima Namagondo,

Ukerewe

17/12/2019

16 Bw. Angelo Msusa Mkulima Murutunguru,

Ukerewe

17/12/2019

17 Bi. Veneranda

Pantaleo

Muuguzi

Mstaafu

Namagondo,

Ukerewe

18/12/2019

234

18 Bi. Muyango

Mkokolo Mkama

Mkulima Namagondo,

Ukerewe

18/12/2019

19 Bi. Rozina Mugabe

Bununja

Mwalimu Namagondo,

Ukerewe

17/12/2019

20 Bi. Mungere

Mtesigwa

Mwalimu Namagondo,

Ukerewe

19/12/2019

21 Mch. Charles Bita

Kalogosi

Mchungaji Namagondo,

Ukerewe

8/12/2019

22 Bi. Regina Tanu Mwalimu S/M Nakasahenge,

Namagondo

18/12/2019

23 Bi. Aneth Benedicto Mkulima Namagondo,

Ukerewe

18/12/2019