Matambiko Katika Jamii yA Wasambaa

75
SURA YA KWANZA UTANGULIZI WA UTAFITI 1.1Utangulizi Utafiti huu ulihusu nafasi ya matambiko katika jamii ya wasambaa wanaoishi mkoani Tanga katika wilaya ya Lushoto na ile ya Korogwe. Utafiti huu ulijikita zaidi katika wilaya ya Lushoto hususani katika Tarafa ya Mtae na katika kata ya Rangwi. Utafiti huu umegawanyika katika sehemu tano; sura ya kwanza ambayo imehusisha dhana na maana mbalimbali, usuli wa utafiti, historia ya wasambaa, tatizo la utafiti, malengo ya utafiti, maswali ya utafiti, umuhimu wa utafiti, mipaka ya utafiti, nadharia ya utafiti na hitimisho. Sura ya pili imehusisha mapitio ya machapisho mbalimbali, sura ya tatu imehusisha mbinu za ukusanyaji wa data, vyanzo vya data na taarifa, sampuli na 1

Transcript of Matambiko Katika Jamii yA Wasambaa

SURA YA KWANZA

UTANGULIZI WA UTAFITI

1.1Utangulizi

Utafiti huu ulihusu nafasi ya matambiko katika jamii ya

wasambaa wanaoishi mkoani Tanga katika wilaya ya Lushoto

na ile ya Korogwe. Utafiti huu ulijikita zaidi katika

wilaya ya Lushoto hususani katika Tarafa ya Mtae na

katika kata ya Rangwi.

Utafiti huu umegawanyika katika sehemu tano; sura ya

kwanza ambayo imehusisha dhana na maana mbalimbali, usuli

wa utafiti, historia ya wasambaa, tatizo la utafiti,

malengo ya utafiti, maswali ya utafiti, umuhimu wa

utafiti, mipaka ya utafiti, nadharia ya utafiti na

hitimisho. Sura ya pili imehusisha mapitio ya machapisho

mbalimbali, sura ya tatu imehusisha mbinu za ukusanyaji

wa data, vyanzo vya data na taarifa, sampuli na

1

usampulishaji. Sura ya nne imehusisha uchambuzi wa data

na sura ya tano imehusisha muhtasari wa utafiti na

hitimisho.

1.1.2 Dhana ya Matambiko

Masebo, J. A. (2007), anasema, tambiko ni sadaka inayotolewa kwa

mwenyezi mungu, miungu au mahoka, mizimu na pepo kwao

binafsi au kupitia kwa mwenyezi mungu wakati wa kusalia

miungu.

Kitula, K. na Catherine, N. M. K (2010) wanasema, neno

matambiko linatokana na imani kuwa mababu waliofariki

wana uwezo wa kuona matendo ya watoto na wajukuu wao

walio hai. Inadhaniwa kuwa wanapokasirika watoto hupata

matatizo ya magonjwa, vifo na mabalaa mengine. Ili kupoza

hasira zao huko walikolala basi hupikwa pombe na vyakula

vinavyokwenda kumwagwa makaburini au kuliwa na waganga

ambapo vitendo hivyo ndio matambiko.

Wikipedia, kamusi elezo huru, wanasema, Kila kabila lina

aina ya matambiko linayofanya kulingana na mila zake na

aina ya matatizo.

2

Makabila ya maeneo ya Tanga, Pwani na Morogoro hufanya

matambiko yao makaburini, kwenye miti mikubwa, milimani,

mapangoni, ziwani, baharini, makaburini na porini na

kupeana majina maalum ya mababu na kuvaa kago (alama)

mikononi. Kwa wasambaa wale wanaohusika na shughuli ya

utekelezaji wa matambiko huwa wamevalia nguo maalumu

maarufu kama kaniki (hizi ni nguo kama kanga lakini

zinakuwa nyeusi). Wasambaa hushikamana na mila au

desturi, ngoma za mashetani, mizuka na vinyamkera vyao

kama alama ya kuwaheshimu na kuwaenzi mababu zao wa kale.

Kamusi ya karne ya 21 (2011) wanasema, tambiko ni sadaka

au ada inayotolewa kwa mwenyezi mungu, miungu, pepo au

mizimu moja kwa moja au kwa mungu kupitia kwa miungu.

Yapo matambiko yaliyotolewa na wazee maarufu waliopewa

jukumu hilo. Matatizo yaliyoshindikana kwa mababu zetu

yalipelekwa kwa miungu ili iwasaidie kuyatatua.

Assumpta, K.M. (2011) amebainisha baadhi ya sifa za

matambiko ambazo ni kama ifuatavyo;

3

I. Matambiko ni sanaa inayotendeka.

II. Matambiko hayatolewi na mtu yeyote bali na wazee

maarufu walioteuliwa na jamii husika.

III. Matambiko hufanywa mahali maalumu kama vile chini ya

mti mkubwa, makaburini, mapangoni, milimani, mtoni,

njia panda au hata porini kutegemeana na jamii

husika.

IV. Matambiko yaliandamana na sala na ni utanzu wa

maigizo ambao unaendelea kufa.

Masebo, J. A (2013) anasema matambiko yana umuhimu na

hasara katika jamii kama ifuatavyo;

Umuhimu wa tambiko

Matambiko hujenga imani kama chombo cha kutatulia matatizo ya

jamii husika.

Tambiko husaidia kuendeleza mila na desturi za jamii husika

Tambiko husaidia kujenga na kuimarisha mahusiaano miongoni

mwa wanajamii

Matambiko huiongoza jamii katika mapambano dhidi ya matatizo

mbalimbali yanayoikabili jamii.

4

Hasara ya matambiko

Matambiko hujenga dhana potofu katika jamii kwa kuamini

nguvu fulani bila kuwa na uhakika au uthibitisho wa

kisayansi

Matambiko huleta hasara kubwa kwa jamii husika kwani

kafara, sadaka, za matambiko inahitaji wanyama/vyakula

ambavyo watu hutumia pesa nyingi kuvipata vitu hivyo.

Matambiko huwafanya watu kuishi kwa wasiwasi mkubwa kwani

panapotokea tatizo na uwezo wa kufanya tambiko haupo

wanajamii hao hupatwa na hofu maishani kwa kushindwa

kutimiza yale wanayodhani wazee/mahoka wanahitaji

kufanyiwa.

Masebo, J. A (2013) anasema matambiko yana wahusika

maalumu na madhari/mahali maalumu kama ifuatavyo;

Wahusika

Hawa ni wale wazee maarufu walioteuliwa na jamii kuendeleza

shughuli za matambiko, si kila mtu katika jamii anaweza kufanya

tambiko.

5

Mandhari/Mahali

Tambiko linaweza kufanyika porini/msituni, njia panda, kwenye

miti mikubwa, kwenye mawe makubwa, makaburini, mapangoni,

mtoni, ziwani, baharini, kwenywe nyumba maalumu na mahali

popote kutegemeana na aina ya tambiko.

1.2 Usuli wa utafiti

1.2.1Historia ya wasambaa

Kirama, Kh. (1953) anasema, jamii ya wasambaa inapatikana

katika milima ya usambara kaskazini mashariki mwa

Tanzania.Wasambaa ni jina ambalo limetokana na neno

kusambaa. Inasemekana kwamba jamii hii asili yao ni Kenya

na walikuja katika milima ya usambara kukimbia vita baina

yao na wamasai wakiwa wanagombea malisho ya wanyama wao

na hatimaye wakajikuta wanavuka mbuga ya mkomazi na

kusambaa katika milima ya usambara na hatimaye ikawa

chimbuko la jina wasambaa kwa maaana ya kwamba wamesambaa

katika milima. Ambapo kwa sababu walisambaa karibu katika

kila safu nayo ikaitwa milima ya usambara. Kwa asili

wasambaa wapo katika aina zaidi ya kumi lakini wote

6

husikilizana kwa lugha moja-Kisambaa ambao ni; wasambaa

washee, wahea, wanango, ntandaa, wakijewa, wagamo,

wang’hwasho na wakilindi.

Wikipedia, kamusi elezo huru wanasema wasambaa ni kabila

kutoka eneo la Milima ya Usambara, kaskazini-mashariki ya

nchi ya Tanzania, mwaka 2001 idadi ya Wasambaa

ilikadiriwa kuwa 664,000. Wasambaa kama wanavyojulikana

sana wanaishi kwenye milima ya usambara na lugha yao

kubwa ni kisambaa. Wasambaa wamegawanyika katika koo

mbalimbali ndani ya jamii zao ambazo ndio utambulisho

wao. Koo au ukoo ni jambo la muhimu sana katika maeneo ya

usambaa kwani wanajamii wa kisambaa wanatambuana kwa

majina ya ukoo. Alama maarufu ya koo za kisambaa ni

majina yanayoanza na SHE kama, Shemboko, Shekiango,

Shekimwei, Sheiza, Shembilu, Shekinyashi, Sheshe,

Shedodo, Shekalage, Shekifu n.k koo nyingi za kisambaa

zinajulikana kwa kuanza na majina hayo na Lugha yao ni

Kisambaa.

7

Kirama, Kh. (1953) Chakula, kwa wasambaa chakula chao cha

asili ni ugali wa mhogo (bada) kwa maharage pamoja na

ugali wa mahindi kwa kweme au mbegu za maboga. Mavazi kwa

watu wa awali walikuwa wanavaa nguo ambazo zinatokana na

maganda ya miti ambayo yanasuguliwa na mafuta ya samli

mpaka yanakuwa laini na kuwa tayari kuvaliwa.Vazi hilo

linavaliwa na wanaume na wanawake lakini linakuwa na

majina tofauti kwa wanaume zinaitwa “UKOPA” na kwa

wanawake zinaitwa “VINGUNGU”Imani, wasambaa wanaamini juu

ya Mungu wa kweli ambaye ni Mungu wa juu/mbinguni na

duniani ndiye haswa wanayemuabudu. Lakini pia wanaamini

juu ya miungu, mashetani, mizimu na ndio haswa pia

wanaitambikia. Pia Wasambaa wanaamini mambo ya

kishirikina na uchawi. Shughuli za uzalishaji mali

wasambaa hujishughulisha zaidi na kilimo na ufugaji kama

shughuli zao kubwa. Katika kilimo hulima mazao ya aina

mbalimbali kama vile mihogo, mahindi, maharage, viazi

ambapo mazao hayo hutumika kama chakula chao kikuu, kwa

wasambaa kukosekana kwa mihogo na mahindi ni ishara ya

8

njaa. Kuoa na kuolewa mwanaume anayetaka kuoa humtuma

mshenga kwa wazazi wa msichana kueleza nia yake. Wazazi

wakikubali kwa kutambua umuhimu wa familia kama kuongeza

uzao wanakaa kifamilia, kisha watamtuma mjumbe, ambako

wanakula pamoja na kutajiwa mahari kulingana na utaratibu

wa kisambaa kuwataka upande wa kiume wapange siku ya

kwenda ‘kupiga hodi’ kwa mwanamke, siku hii ndipo

wataambiwa rasmi kwamba wamepata binti. Siku hiyo upande

wakike wataandaa chakula maalamu kwa wageni. Utawala

wasambaa wanauongozi ulio imara na wakuheshimiwa sana na

kiongozi wao anajulikana kama zumbe. Elimu wasambaa kama

makabila mengine wana elimu ya jando na unyago ambapo

vijana wakifikia umri stahili wanaingia jandoni na

sherehe kubwa hufanyika. Ngoma wasambaa wana ngoma yao

maarufu sana ambayo hujulikana kama mdumange ngoma hii

hupigwa katika shunghuli mbalimbali za kijamii. Kifo kwa

wasambaa wanaimani kuwa mtu mwema akifa kuna ishara

zinatokea kama mvua kubwa na mtu huyo anaenda mahali

pazuri ambapo wanaamini ni peponi lakini kwa mtu muovu

9

kuna ishara mbaya kama kaburi kuwa gumu katika uchimbaji,

kukutana na mwamba ndani ya kaburi, kutokea nyoka na

mambo kama hayo.

Wikipedia, kamusi elezo huru, wanasema, wasambaa ni

miongoni mwa makabila ambayo watu wake wamesoma. Wasambaa

pia ni kabila la watu wanaopenda haki yaani hawapendi

kuonewa wala kumuonea mtu.Wasambaa ni watu wa ushirikiano

sana na waonapo au kusikia mtu yeyote ana tatizo wapo

tayari kumsaidia. Kisiasa ni watu makini sana katika

kutawala na wana ushawishi mkubwa sana kwani walio wengi

wana busara na wanajua kusikiliza mambo kwa umakini pia

ni waadilifu sana na wanasimamia sheria na taratibu.

Katika utafiti huu mtafiti aliangalia wasambaa kwa ujumla

wao hivyo historia ya wasambaa itaegemea wasambaa kwa

ujumla wao. Kipindi kirefu sasa tangia miaka ya nyuma,

wataalamu mbalimbali walijitokeza na kujaribu kuangalia

na kufanya tafiti juu ya matambiko kama kipengele

kimojawapo cha fasihi simulizi. Wataalamu hao waliweza

10

kuangalia matambiko katika baadhi ya makabila na

waliangalia mambo mbalimbali zaidi ya matambiko

yanayofanywa baada ya kutokea ajali au mtu kunusurika

kufa.

Japo tafiti hizo mbalimbali zimeweza kufanyika na

kufanikiwa kwa kiasi chake, lakini bado kiu ya hadhira

haikuweza kukatwa kwa kuwa hakuna tafiti ambazo

zimeengalia kwa kina mambo kadha wa kadha yanayopatikana

katika dhana ya matambiko kama vile; vifaa vitumikavyo

wakati wa matambiko, wahusika wa matambiko, mandhari na

mambo mengine mengi ambayo katika utafiti huu mtafiti

amejaribu kupitia kwa kina mambo hayo muhimu.

1.3 Tatizo la utafiti

Tafiti mbalimbali zilishafanywa juu ya matambiko lakini

tafiti hizo zilijikita zaidi katika matambiko ya jamii

nyingine za kaskazini mashariki mwa Tanzania kama jamii

ya wachaga, wapare na wameru, hata hivyo tafiti ambazo

zishafanywa katika kabila la wasambaa zimejikita zaidi

11

katika asili ya aina fulani tu ya wasambaa wakilindi

ambapo kulingana na Khalidi Kirama (1953) anasema asili

ya wasambaa wakilindi ni handeni na wanatokana na mtu

aliyefahamika kama Mbegha. Mtafiti katika utafiti huu

alijikita zaidi kuangalia/kutafiti juu ya nafasi ya

matambiko katika jamii ya wasambaa, mazingira ambayo

matambiko hufanywa katika jamii ya wasambaa, vifaa

ambavyo vinatumika au ni maalumu katika kufanya matambiko

na mambo mengine yanayoendana na zoezi zima la matambiko

ambapo kwa hakika watafiti waliotangulia hawajawahi au

kufikia kuchunguza mambo kama hayo au hata kufanya

utafiti wa kina.

1.4 Malengo ya utafiti

Utafiti huu ulikuwa na malengo ya aina mbili, lengo kuu

moja na malengo mahsusi matatu

12

1.4.1 Lengo kuu

Kuchunguza nafasi ya matambiko katika jamii ya wasambaa

1.4.2 malengo mahsusi

I. Kuchunguza dhima/umuhimu wa matambiko katika kukuza

fasihi ya jamii ya wasambaa.

II. Kuchunguza vipindi, mazingira ambayo matambiko

hutekelezwa katika jamii ya wasambaa.

III. Kuchunguza na kubaini vifaa vinavyotumika katika

kutekeleza zoezi zima la matambiko katika jamii ya

wasambaa.

1.5 Maswali ya Utafiti

I. Matambiko yana dhima/umuhimu gani katika jamii ya

wasambaa?

II. Matambiko hufanywa vipindi na mazingira gani katika

jamii ya wasambaa?

III. Vifaa gani hutumika katika kutekeleza zoezi la

matambiko katika jamii ya wasambaa?

13

1.6 Umuhimu wa Utafiti

Utafiti huu ni muhimu kitaaluma kwa jamii wasambaa kwa

ujumla kwa sababu matambiko ni kipengele muhimu cha

fasihi simulizi kwani hutunza na kukuza historia ya jamii

ya wasambaa, wakiwa wanajua walikotoka walipo na

wanakoenda. Kwa kuwa matambiko hushughulikia maswala

kadha wa kadha yanayoikumba jamii husika kiimani na hata

kiitikadi.

1.7 Mipaka ya Utafiti

Utafiti huu ulijikita zaidi katika kuangalia kwa kina juu

ya nafasi ya matambiko katika kukuza fasihi simulizi ya

jamii ya wasambaa, vipindi na mazingira ambayo matambiko

hutekelezwa, wahusika pamoja na vifaa ambavyo hutumiwa

katika kukamilisha jambo hilo.

1.8 Nadharia ya Utafiti

14

TUKI (2009:63) wanasema nadharia ni taratibu, kanuni na

misingi ambayo imejengwa katika muundo wa kimawazo kwa

madhumuni ya kutumiwa kama kielelezo cha kuelezea jambo.

Kulingana na Massamba na wenzake.

1.8.1 Uhalisia Mazingaombwe/Uhalisia Ajabu (Magical

Realist Theory)

TUKI (2009) wanasema hii ni dhana iliyobuniwa na msanii

wa ujerumani Franz Roh, katika kitabu chake Nach-

expressionnism, magischer realismus. Probleme der neusten

europaischer malalerei. Dhana hii huhusishwa na waandishi

wa marekani ya kusini au hata nchi zinazoitwa ulimwengu

wa tatu na hutambulishwa na sifa mbalimbali. Sifa hizi ni

za kuyaelezea matukio ya kifantasia au ya ajabu au

kichawi kwa namna ya moja kwa moja kwa namna inayofanana

na yaonekana kama ya kawaida tu. Mpaka uliopo kati ya

mambo yanayoweza kupatikana katika ulimwengu halisi na

yasiyowezakana huwa madogo sana. Sababu hasa ya matumizi

ya mtindo huu ni kuonesha kuwa matukio ya aina hii

15

hupatikana katika maisha ya kawaida katika jamii

zinazohusika. Nadharia hii inasisitiza kuwa fasihi

haiwezi kujitenga na hali halisi ya maisha ya watu katika

jamii ambamo fasihi imeundwa na kutumika. Waandishi

wanaoandika katika msingi huu hushikilia kuwa mtizamo wao

wakiuhalisia unawakilisha msimamo wa jamii zao. Yaani

mambo yanayotekelezwa kama ya ajabu na kichawi ni sehemu

ya mwonoulimwengu wa jamii hizo.

Msingi mkubwa wa nadharia hii ni usimulizi unaosimulia

mambo au matukio kama yanavyotokea katika ulimwengu

halisi au unaokaribia na uhalisia, mwandishi anapaswa

kuyamulika na kuyaakisi maisha katika nyanja zote

kijamii, kiuchumi, kiutamaduni na kisiasa. Uhalisia

unaongoza na kusisitiza uwasilishaji wa maisha ya jamii

kwa uaminifu na usanifu mkubwa, uhalisia unapinga na

kukataa aina yoyote ya majaribio. Nadharia hii itasaidia

kwa kiasi kikubwa katika utafiti huu kwa kuwa matambiko

yanazungumzia jamii na watu ambao kwa hakika waliishi na

ni halisi pia yanazungumzia maisha halisi ya mwanadamu

16

hususani muafrika. Nadharia hii kimsingi inahusika sana

na jamii ambazo zimechelewa hususani jamii nyingi za

Afrika na Tanzania kwa ujumla. Jamii ya wasambaa ni jamii

ambayo kimsingi bado inaegemea sana mambo haya ya

matambiko hivyo nadharia hii itakuwa kama mwanga katika

utafiti huu kwani mambo ya matambiko ni mambo ya ajabu

ajabu.

Zamora (1995) Nadharia ya uhalisia mazingaombwe ilianza

mnamo mwaka wa 1925 na muasisi wake alikuwa mhakiki wa

sanaa wa Kijerumani aliyeitwa Franz Roh.Dhana ya Roh ya

nach-expressionism, magischer realism ikitafsiriwa katika

lugha ya Kiswahili inaashiria hali ya ajabu au

mazingaombwe. Uhalisia ajabu unaeleza miujiza iliyomo

kwenye uyakinifu wa kila siku.

Mbatiah, M. (2002:60) anafafanua uhalisia ajabu hivi,

istilahi hii inatumiwa kuelezea mkondo wa uandishi ambapo

mazingira, matendo na matukio ya kifantasia husawiriwa

kwa kuiga mtindo wa uhalisia yaani kuyaeleza mambo kwa

17

njia ya moja kwa moja kana kwamba ni mambo ya kawaida.

Wasanii wanaotumia mkondo huu hudhamiria kuonesha kuwa

ingawa mambo yanayoshughulikiwa ni ya kiajabuajabu

hutokea katika maisha ya kawaida ya jamii husika. Katika

uhalisia wa ajabu ndoto na uhalisia vinachanganywa.

Nadharia hii itasaidia sana kwa shughuli za matambiko na

zenyewe ni za kimazingahobwe kwani watekelezaji

wanawasiliana na viumbe ambao hawaonekani na hakuna

ushahidi wa kisayansi ya kuthibitisha mawasiliano hayo

japo kuna uhalisia lakini kwa kiasi fulani.

Njogu na Wafula (2007) wanaeleza Uhalisia ulitokana na

matatizo yaliyokuwa yanawakabili watu, matatizo hayo

yaliwafanya watu kuanza kushutumu ulimbwende na matamanio

ya kilimbwende yalikuwa ya kiusingizini (kinjozi) zaidi

yakilinganishwa na shida na matatizo yaliyokuwa

yanawakabili watu. Walimbwende wao walitunga mambo ya

usingizini na waliishi ndotoni. Katika msingi huu

matatizo yanayokabili jamii ya wasambaa na

18

yanayosababisha kufanyika kwa matambiko ni mambo halisia

kabisa ila wanaopewa jukumu la kuyatatua au kuleta ahueni

dhidi ya matatizo hayo hapo ndio uhalisia wa ajabu

unapokuja.

Wamitila, K.W (2002) anasema dhana ya uhalisia huelezea

aina ya mitizamo au tapo la kifasihi ambako kazi ya

kifasihi zinachukuliwa kama zilivyohifadhiwa au kuakisi

sifa za kimsingi zinazohusishwa na uhalisia.

1.9 Hitimisho

Kwa kuhitimisha, sura ya kwanza iliweza kuangalia,

utangulizi, historia ya kabila la wasambaa, dhana ya

matambiko kama ilivyotafsiriwa na wataalamu mbalimbali.

Vilevile ndani ya sura ya kwanza kuna usuli wa utafiti,

tatizo la utafiti, malengo ya utafiti, maswali ya

utafiti, umuhimu wa utafiti, mipaka ya utafiti na

nadharia ya utafiti ambayo ndiyo iliyomuongoza mtafiti

katika utafiti huu.

19

SURA YA PILI

MAPITIO YA MACHAPISHO MBALIMBALI

2.1 Utangulizi

Sura hii ilimuongoza mtafiti katika kukusanya data

zinazoendana na mada tafitiwa. Pia sura hii ilijumuisha

machapisho au mapitio mbalimbali ya kazi za waandishi

wengine zinazoendana na mada ya utafiti ili kujua

matambiko hususani katika jamii ya wasambaa kama

inavyooneshwa na wataalamu mbalimbali katika sura hii.

2.2 Mapitio ya Machapisho Mbalimbali

20

Masebo, J. A. (2007) anasema, tambiko ni sadaka inayotolewa kwa

mwenyezi mungu, miungu au mahoka, mizimu, pepo kwao binafsi

au kupitia kwa Mwenyezi Mungu wakati wa kusalia miungu.

Matambiko ni sanaa kwa kuwa shughuli zenyewe zinakuwa na

ufundi wa aina fulani. Zinatendeka mahali maalumu na

wanaohusika wanakuwa watu wa umri fulani na maalumu. dhana

ya matambiko inatumiwa kuhusiana na jamii nyingi za kiafrika

kuelezea shughuli za utoaji wa kafara na sadaka. Matambiko

yalikuwa na umuhimu na uzito mkubwa katika jamii za kijadi

kuliko jamii za siku hizi. Katika jamii ya wasambaa matambiko

bado yalichukuliwa kuwa na umuhimu mkubwa sana kama ilivyo

katika jamii nyingine. Kwa mfano Miaka ya 1993 katika jamii

ya wasambaa hususani jimboni Mlalo palitokea mafuriko,

mafuriko hayo yalileta maafa makubwa kwani watu

walipoteza maisha, mali, nyumba hata mashamba

yaliharibiwa vibaya! Jamii ile ilihusianisha tukio/janga

lile na kukasirika kwa miungu/mizimu/ mababu zao juu ya

kusahau masuala ya kutambika kwa zumbe mkuu kimweri au

kudharau mambo ya matambiko. Lakini jamii ile ya wasambaa

mpaka leo panapotokea njaa, ukame, vifo na hata ajali

lazima wakatambike kwa zumbe wakiwa wanapeleka kondoo,

21

vyakula vya aina mbalimbali kwa ajili ya kukamilisha

zoezi hilo la kuomba msamaha kwa mababu waliotangulia.

Ilipozama MV Bukoba viongozi wetu badala ya kutafiti

chanzo cha tatizo waliwakusanya wazee kufanya matambiko,

pengine ilikuwa mbinu ya kuwapumbaza watu wasihoji uzembe

uliosababisha ajali hiyo mbaya! Lakini tunaona kuwa sio

jamii hii ya wasambaa tu hata jamii nyingine na serikali

kwa ujumla.

Wamitila, K. W. (2002) anasema, dhana ya matambiko

inatumiwa kuhusiana na jamii nyingi za kiafrika kuelezea shughuli

za utoaji wa kafara na sadaka. Matambiko yalikuwa na umuhimu

na uzito mkubwa katika jamii za kijadi kuliko jamii za siku hizi.

Kimsingi tambiko ni sanaa kwa kuwa shughuli zenyewe zilikuwa

na ufundi wa aina fulani. Zilitendeka mahali maalumu na

waliohusika walikuwa watu wa umri fulani na maalumu. Jamii ya

wasambaa bado wanashiriki kwa ndani sana mambo haya ya

matambiko na kuna sehemu maalumu za kufanya shughuli hizo za

utoaji sadaka.

Kitula, K. na Catherine, N. M. K. (2010) wanasema, neno

Matambiko linatokana na imani kuwa mababu waliofariki

wana uwezo wa kuona matendo ya watoto na wajukuu wao

22

walio hai. Kadhalika inadhaniwa kuwa mababu hao

waliotangulia, wanapokasirika wakiwa katika dunia ya wafu

(kuzimu) watoto waliowaacha duniani hupatwa na matatizo

kama vile magonjwa, vifo au mabalaa mengine. Katika

kupoza hasira zao huko "walikolala" basi hupikwa pombe na

vyakula vinavyokwenda kumwagwa makaburini au kuliwa na

waganga. Kimsingi itikadi za ushirikina ndizo haswa

zinazozua shughuli za miviga, matumizi fulani ya lugha

kama vile methali, hadithi na nyimbo. Iwapo imani hizi

zisingekuwepo shughuli za miviga kama miviga na matambiko

hazingekuwepo. Watu hufanya matambiko sababu wanaamini

jambo fulani lilitendeka au kutokea hasa yale mabaya

sharti yapatiwe suluhisho. Matatizo hayo ni kama; vifo

hususani vile vya kutatanisha, vita, njaa, magonjwa,

ajali, kukosa/kupata watoto, ukame na hata mafuriko.

Katika baadhi ya makabila likiwepo kabila la wasambaa

hata viapo hufanywa kwa kuwataja mababu moja kwa moja au

kwa ishara, huko alikolala yaani huyo anayesema

anathibitisha akimshuhudia babu, baba (mahoka) yake

23

aliyekufa kuwa akisemacho ni sahihi! Utekelezaji wa

matambiko huandamana na mihanga ya pombe, vyakula, kafara

ya damu hususani ya wanyama ili kuilaza mizimu

iliyochachamalia familia, koo na hata jamii fulani.

Masebo, J. A (2013) anasema, matambiko yana umuhimu na

hasara katika jamii kama ifuatavyo;

2.2.1 Umuhimu wa tambiko

I. Matambiko hujenga imani kama chombo cha kutatulia

matatizo ya jamii husika.

II. Tambiko husaidia kuendeleza mila na desturi za jamii husika

III. Tambiko husaidia kujenga na kuimarisha mahusiano

miongoni mwa wanajami

IV. Matambiko huiongoza jamii katika mapambano dhidi ya

matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii.

2.2.2 Hasara ya matambiko

I. Matambiko hujenga dhana potofu katika jamii kwa

kuamini nguvu Fulani bila kuwa na uhakika au

uthibitisho wa kisayansi.

II. Matambiko huleta hasara kubwa kwa jamii husika,

kwani kafara, sadaka, za matambiko inahitaji

24

wanyama/vyakula ambavyo watu hutumia pesa nyingi

kuvipata vitu hivyo.

III. Matambiko huwafanya watu kuishi kwa wasiwasi mkubwa

kwani panapotokea tatizo na uwezo wa kufanya tambiko

haupo wanajamii hao hupatwa na hofu maishani kwa

kushindwa kutimiza yale wanayodhani wazee/mahoka

wanahitaji kufanyiwa.

Katika jamii ya wasambaa matambiko yana faida kadhalika

yana hasara kama ambavyo Masebo, J. A. (2013)

alivyofafanua.

Masebo, J. A (2013) anasema, matambiko yana wahusika

maalumu na mandhari/mahali maalumu kama ifuatavyo;

2.2.3 Wahusika

Hawa ni wale wazee maarufu walioteuliwa na jamii kuendeleza

shughuli za matambiko, si kila mtu katika jamii anaweza kufanya

tambiko.

2.2.4 Mandhari/Mahali

25

Tambiko linaweza kufanyika porini, njia panda, makaburini,

mapangoni, mtoni, ziwani na kwenye miti mikubwa na mahali

popote kutegemeana na aina ya tambiko. Katika jamii ya wasambaa

matambiko yanafanywa na watu maalumu pia katika mazingira

maalumu kama ambavyo wataalamu mbalimbali

walivyofafanua/kueleza.

Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) (2010) wanasema

tambiko ni kitendo cha mtu au jamii kutekeleza ada

maalumu kutuliza mashetani au mizimu. Pia matambiko yana

husiana sana na ushirikina ambapo ushirikina ni tabia ya

kuamini uwezo wa kiumbe kingine juu yako badala ya ule wa

Mwenyezi Mungu. Kimsingi matambiko yanaandamana na mambo

ya uganga hivyo ushirikina unahusiana sana na mambo ya

matambiko. Ni dhahiri kabisa ushirikina unahusiana sana

na mambo ya uganga na matambiko na katika jamii ya

wasambaa haya mambo na ibada hizi ziko na zinahusiana kwa

karibu sana kwa kuangalia vitendo vya mazoezi hayo.

M’nganuth, T. K. (2007/2008) anasema kila palipotokea

janga/tatizo lolote palikuwa na haja ya kufanya tambiko.

Muafrika katika asili yake aliamini Mungu/miungu, mizimu

26

na mahoka. Nyimbo mbalimbali za kumsihi mungu

ziliambatana na na tambiko. Nyimbo za matambiko

zinapatikana kwa wingi katika miviga kama vile shughuli

za kaya pia katika ngoma za pugwa kwa waswahili na jamii

nyingine. Katika jamii ya wameru suala la matambiko

linaenda pamoja na nyimbo maalumu ambazo huibwa wakati

tambiko fulani likitekelezwa.

Mfano;

Wimbo ufuatao ni wa Kimeru ambao uliimbwa wakati wa kutoa

tambiko/sadaka hasa baada ya kipindi kirefu cha kiangazi

kuomba neema fulani kwa Mungu/miungu, mahoka, pepo na

hata mizimu.

Ingwe muningu baba

Jukia iromba rietu

Tukikwerncaga

I ii murungu twingirue kiao

Turi baku

Twingirue kiao turi baku

Kiiru kiiru turi baku

27

Tafsiri-kiswahili

Ewe mungu baba

Pokea dua zetu

Tunakusihi

Sisi jumuiya ya watu wa meru

Ewe mungu baba tuhurumie

Sisi ni wako

Ewe mungu sisi ni wako.

Nyimbo za aina hii zilipatikana kwa wingi katika miviga

kama vile shughuli za kawaida za kaya kadhalika katika

ngoma za mashetani/pungwa katika jamii ya wasambaa na

jamii nyingine zinazifanana na hizo.

2.3 Hitimisho

Wataalamu mbalimbali na waandishi nguli wa mambo ya

fasihi wamefanya tafiti mbalimbali kuchunguza dhama ya

matambiko. Dhana hiyo ndiyo inayotoa mwanga kwa wasomaji

kuelewa maana ya matambiko. Lakini wataalamu hao

hawajawahi kuangalia matambiko katika jamii ya wasambaa

hususani katika mambo kama; sababu za kufanya matambiko,

mazingira ya matambiko, vifaa na hata umuhimu wa

28

matambiko. Utafiti huu ulijaribu kuambaa kwa kina katika

kila kipengele ili kutoa picha halisi ya matambiko katika

jamii husika.

SURA YA TATU

MBINU ZA UTAFITI

3.1 Utangulizi

29

Sura hii iliwasilisha mbinu mbalimbali zilizotumika

kumsaidia mtafiti katika kukamilisha utafiti wake, mbinu

alizotumia mtafiti katika kukusanya data ambazo kwa namna

moja ama nyingine zitajibu maswali ya utafiti huu, mbinu

za utafiti, eneo la utafiti, vyanzo vya data, njia za

ukusanyaji data, sampuli na usampulishaji, vifaa vya

ukusanyaji data na uchanganuzi wa data.

Utafiti huu ulihusu nafasi ya matambiko katika kabila la

Wasambaa linalopatikana mkoa wa Tanga hususani katika

safu za milima ya usambara.

3.2 Mbinu za Ukusanyaji Data

3.2.1 Hojaji

Mtafiti alitumia mbinu hii ili kuweza kupata data

mbalimbali zinazohusu matambiko katika kabila la

Wasambaa. Baadhi ya maswali mtafiti aliyouliza yalikuwa

kama ifuatavyo;

30

I. Matambiko yana umuhimu gani katika jamii ya

wasambaa?

II. Matambiko hufanywa vipindi na mazingira gani?

III. Vifaa gani hutumika katika kutekeleza zoezi la

matambiko?

3.2.2 DodosoMtafiti ametumia mbinu ya kuuliza maswali katika

maandishi na kuwapatia wanajamii wa Rangwi ili kupata

data anazozihitaji. Watu waliotakiwa kujibu maswali hayo

ni watu wote wazee kwa vijana wanaoishi katika kata ya

Rangwi.

3.3 Vyanzo vya Data na Taarifa

Kamusi ya Kiswahili Sanifu (2004:59) ilieleza kuwa data

ni taarifa au takwimu inayotumiwa kuelezea au

kuthibitisha hoja fulani. Taarifa ni habari inayotolewa

ili kujulisha jambo fulani (uk 388). Ili mtafiti kuweza

kukamilisha utafiti wake alitumia vyanzo mbalimbali vya

31

data kama vile vitabu, majarida, makala, magazeti na

hotuba mbalimbali.

3.3.1 Data za Msingi

Kothari (1992:95) anasema, data za msingi ni zile data

zilizokusanywa kwa mara ya kwanza na hivyo ni data

halisi. Kwa msingi huo data za msingi zilizokusanywa

kupitia mahojiano na wazee mashuhuri ambao ni wasambaa

wanaoishi maeneo ya katika tarafa ya Mtae katika kata ya

Rangwi.

3.3.2. Data Fuatizi

Kothari (1992:95) anasema data fuatizi ni zile data

ambazo tayari zilikwishakusanywa na watafiti wengine ama

kuandikwa kama ripoti, makala. Data za namna hii ni

muhimu kwa sababu ndizo zilikazothibitisha data za msingi

za utafiti na kuupa mashiko utafiti huu.

3.4. Sampuli na Usampulishaji

32

Sampuli yetu katika utafiti huu ni wasambaa wa jamii ya

Lushoto wa tarafa ya Mtae katika kata ya Rangwi. Mtafiti

alitumia usampulishaji nasibu katika kukusanya data

ambapo kila kipengele kilichofaa kwa kutoa taarifa kuhusu

nafasi ya matambiko katika jamii ya wasambaa ili

kurahisisha uchukuaji wa data.

Sampuli nasibu imependekezwa kutumika kwa sababu ndiyo

njia inayofaa na kumpa mtafiti uhuru wa kuchagua nukuu

ilikayofaa kutumika kama data katika utafiti huu.

3.5. Mbinu za Uchambuzi wa Data

Data zilichambuliwa katika mkabala wa kimaelezo yaani

mkabala usio wa kiidadi au kitakwimu. Hii ni kwa sababu

utafiti huu haukuhusisha takwimu, data zilipangwa

kulingana na malengo na maswali ya utafiti ili

uchanganuzi wa data hizo uendane na malengo ya utafiti.

Data zote zilipewa msimbo wa nukuu na zilichambuliwa kila

moja ili kuweka utafiti huu katika mtiririko na mpangilio

wenye upatanifu. Data zote zilizoambatanishwa kama msimbo

33

wa nukuu zilichambuliwa kila moja na nafasi yake ili

kurahisisha uchakataji wa data. Data fuatizi zilinukuliwa

pale ilipobidi ili kuthibitisha data za msingi.

3.6. Vifaa vya Ukusanyaji wa Data

Vifaa vilivyotumika katika ukusanyaji wa data maktabani

ni kalamu, penseli na karatasi kwa ajili ya kunukuu data

za msingi, data fuatizi na vipengele vinginevyo muhimu.

Kompyuta ilitumika kwa ajili ya kufanya mawasiliano ya

kimtandao (barua pepe, na hata mitandao mingine ya

kijamii) pia ilitumika katika kupitia vitabu na mapitio

yaliyokuwa hayapatikani maktabani. Mtafiti alitumia

kompyuta na kinyonyi data (flashi) kwa ajili ya uchapaji,

unyonyaji data na utunzaji wa kumbukumbu za utafiti huu.

3.7 Eneo la Utafiti

3.7.1 Uwandani

Utafiti huu ulifanyika katika mkoa wa Tanga wilayani

Lushoto katika tarafa ya Mtae katika kata ya Rangwi

34

kijijini Emao ambako wakilindi ndio asili yao. Eneo la

Rangwi lilichaguliwa kutokana na ukweli wa kuwepo wazee

wengi ambao kwa kina wanajua maana ya matambiko, jinsi

yanavyofanywa, sababu, umuhimu kila kitu ambacho

kinahusiana na matambiko wanakijua lakini pamoja na hayo

yote walio wengi ni wasambaa ambao haswa ndio utafiti huu

uliwagusia sana. Pia mtafiti ni mzaliwa wa mazingira ya

usambara hivyo ni rahisi kupata data katika mazingira

halisi ya jamii anamoishi mtafiti ili kujua jamii yake

ilikuwa wapi na inaelekea wapi.

3.7.2Maktabani

Lakini pia mtafiti amefanya utafiti wa maktabani. Utafiti

umefanyika katika maktaba ya Chuo Kikuu Kishiriki cha

Jordan tawi la Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino

kilichopo mkoani Morogoro, maktaba ya mkoa wa Morogoro na

katika mtandao (internet). Maktaba hizo zimetumiwa na

mtafiti kwa kuwa data zote muhimu zinapatikana katika

maktaba hizo, ikiwa ni pamoja na vitabu na matini

35

mbalimbali zinapatikana humo. Maktaba hizo zimeteuliwa na

mtafiti kwani ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha

Jordan na ni mkazi wa Morogoro na ni rahisi kwake kufika

katika maeneo aliyoyateua, hii imemrahisishia mtafiti

ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama za utafiti.

3.8 Hitimisho

Katika sura hii mtafiti aliangalia eneo la utafiti ambalo

mtafiti alitapitia kwa madhumuni ya kukamilisha utafiti

huu. Vilevile mtafiti aliangalia mbinu za ukusanyaji wa

data, vifaa vilivyotumika katika kukamilisha utafiti huu

pamoja na sampuli mbalimbali za utafiti huu wa nafasi ya

matambiko katika jamii ya wasambaa.

36

SURA YA NNE

UCHAMBUZI WA DATA

4.1 Utangulizi

Sura hii inahusu uchambuzi na uwasilishaji wa data

zilizokusanywa kwa kuzingatia nadharia ya uhalisia

mazingaombwe. Katika tasnifu hii mchakato umelenga

kuchambua malengo ya utafiti ili kuweza kuchakata data

vizuri. Malengo ya utafiti ndiyo zana iliyomsaidia

mtafiti kujibu maswali ya utafiti, katika kufanikisha

utafiti huu mtafiti alitumia njia kuu tatu ambazo ni;

njia ya kuwahoji wenyeji wa mkoa wa Tanga hususani katika

wilaya ya Lushoto tarafa ya Mtae katika kata ya Rangwi,

njia ya watafitiwa kujibu maswali ya dodoso na mwisho

njia ya kutembelea maktaba na maeneo ya asili ambayo yapo

37

katika kata ya Rangwi (data za msingi na data fuatizi)

lengo ni kufanikisha kazi hii pamoja na kuonesha nafasi

ya matambiko katika jamii ya wasambaa.

Katika utafiti huu mtafiti ameonesha mchango wa washiriki

wa utafiti huu kwa kuzingatia jinsia, elimu, umri.

JINSIA IDADI ASILIMIA

WANAWAKE 10 40%

WANAUME 15 60%

JUMLA 25 100%

Kielelezo Na. 1 Jinsia ya washiriki

Kielelezo hapo juu kinaonesha idadi ya washiriki katika

utafiti kuwa idadi ya wanaume wanaoshiriki katika

shughuli za matambiko ni kubwa sana ukilinganisha na

idadi ya wanawake katika jamii ya wasambaa ambapo ni

dhahiri kabisa kuwa wanaume ndio watendaji wakuu katika

utekelezaji wa matambiko.

Miaka Idadi Asilimia

38

18-24 3 12%

25-35 2 8%

36-45 5 20%

56-60 5 20%

60-zaidi 10 40%

Jumla 25 100%

Kielelezo Na. 2 Umri wa washiriki

Katika kielelezo hapo juu, tunaona kuwa washiriki wenye

umri zaidi ya 60 ndio walio wengi na hawa ndio washiriki

wakubwa katika kutekeleza matambiko katika koo nyingi za

wasambaa kundi hili husaidiwa kwa karibu mno kwa lengo la

kurithisha kazi hiyo na kundi la miaka 56-59 na kwa kiasi

kidogo kundi la miaka 36-45. Kundi la miaka 25-35 pamoja

na 18-24 wao walitoa mawazo yao tu juu ya matambiko

katika jamii ya wasambaa.

Kiwango Idadi Asilimia

39

Wasiosoma 1 4%

Msingi 15 60%

Sekondari 6 24%

Chuo 3 12%

Jumla 25 100%

Kielelezo Na. 3 Kiwango cha elimu ya wahusika

Kielelezo hapo juu kinaonesha viwango vya elimu ambapo

kundi kubwa inaonesha ni la wale waliopata elimu ya

msingi wakifuatiwa na wale waliobahatika kupata elimu ya

sekondari na chuo na mwisho kabisa ambao hawajasoma.

Je? Kuna mavazi maalumu katika kutekeleza shughuli za

matambiko katika jamii ya wasambaa

Majibu Idadi Asilimia

Ndiyo 25 100%

Hapana _ _

Hawajui _ _

Jumla 25 100%

Kielelezo Na 4 Uwepo wa mavazi maalumu katika matambiko;

40

Kielelezo hapo juu kinaonesha kuwa washiriki wote 25 sawa

na asilimia 100 wamekiri kuwa kuna mavazi maalumu ambayo

hutumika katika kutekeleza shughuli za matambiko katika

jamiii ya wasambaa ambayo ni kaniki (kanga yenye rangi

nyeusi), vitambaa vyeupe na nyeusi pamoja na shanga za

rangi mbalimbali.

Majibu Idadi Asilimia

Ndiyo 20 80%

Hapana 2 8%

Hawajui 3 12%

Jumla 25 100%

Kielelezo Na. 5 Je, matambiko yana msaada wowote katika

matatizo ya wasambaa?

Katika kielelezo hapo juu, asilimia 80 ya washiriki

wamekiri kuwa matambiko yana msaada mkubwa mno katika

jamii ya wasambaa kwa sababu wanapotambikia mizimu yao

matatizo husika hupungua ama kutoweka kabisa mfano watu

hupona magonjwa, waliopotea wanaonekana, walioenda mbali

41

na nyumbani kwa muda mrefu bila mawasiliano hurudi mara

matambiko yanapofanywa.

Kimsingi kabla ya kuangalia suala lenyewe linalobeba kazi

hii ni vizuri kuangalia mambo muhimu yanayohusu kabila

hili la wasambaa kama; historia fupi ya kabila la

wasambaa, maelezo mafupi ya matambiko katika kabila la

wasambaa pamoja na chimbuko la matambiko katika kabila

hili.

4.2 Maelezo Mafupi Kuhusu Matambiko Katika Jamii ya

Wasambaa

Katika mahojiano na mtafitiwa mzee Matimua R. K anasema

katika jamii ya wasambaa matambiko ni njia ya

kumuunganisha mwanadamu na muumba wao kwa kumtolea mungu

sadaka na shukrani. Kulingana na maelezo ya wasambaa

walioshiriki katika utafiti huu wanadai kuwa matambiko ni

sehemu ya maisha yao katika kupambana na changamoto za

kimaisha. Na pale itokeapo jamii imeingia katika magumu

ya aina yeyote basi kimbilio linaloaminika kuleta utulivu

42

juu ya tatizo husika ni matambiko tu. Kwa wasambaa kuna

sala mbalimbali ambazo kwa hakika wanajamii huzitumia

katika nyakati tofauti tofauti ili kuomba Baraka kwa

mungu wanayemuamini ambapo amepewa majina kama Zumbe

Mnkhalamo (Mungu wa neema), Zumbe Tate (Mungu Baba)

ambapo katika sala zao huanza kumtaja yeye akifuatiwa na

majina ya watu waliotangulia kuanzia mkubwa mpaka mdogo

na ndipo hutaja nia zao zote na kuzikabidhi kwa miungu

yao.

Katika kipindi hiki ambapo jamii ya wasambaa ina

mchanganyiko wa dini yaani dini ya Kikristo na Kiislamu

matambiko bado yana nafasi kubwa kwa sababu ndani ya

jamii hii bado matambiko yanafanyika katika namna mpya.

Kwa wakristo walio wengi wanafanya misa za kuombea

marehemu wao (kumbukumbu) ambapo katika familia ama koo

hufanya ibada hizo lakini ndani yake kuna matambiko

yanafanyika kwa usiri mkubwa kwa sababu dini haziruhusu

matambiko. Kwa wakristo ibada za kuombea wafu zinaenda

sambamba na uikaji wa vyakula pamoja na uchinjaji wa

43

wanyama ambako vyakula hivyo huliwa na watu walioalikwa

katika shughuli hizo. Kwa upande wa waislamu hakuna

tofauti sana na wakristo kwani ibada za kuwaombea wafu

hufanywa sambamba na uchinjaji wa wanyama na upikaji wa

vyakula. Kimsingi matambiko yapo na yanaendelea ila

yanaenda kuvaa sura na jina lingine katika jamii ya

wasambaa.

Kulingana na Zamora, P. na Faris, W. B. (2005)

wakimrejelea Haen, D. wanasema kwamba uhalisia

mazingaombwe unabuni ulimwengu mbadala kwa hiyo

unarekebisha makosa ambayo uhalisia wetu unayategemea ili

kuwepo. Na ndio maana jamii ya wasambaa kwao matambiko ni

sehemu ya maisha yao kwa sababu wao wanaamini kuwa, kuna

ulimwengu mwingine baada ya maisha ya hapa duniani kufika

mwisho. Ambapo wao wanaamini kuna ulimwengu wa kuzimu

ambapo wanajamii waliotenda mema baada ya kufa roho zao

huenda huko kuzimu na wanajamii ambao matendo yao

hayakuwa mazuri roho zao hazifiki huko ila hutangatanga

duniani. Na ndio maana wasambaa hufanya matambiko ili

44

kurekebisha pale walipokosea ili mizimu iwawie radhi na

kuishi kwa amani kwa sababu wanaamini roho za mizimu zipo

katika ulimwengu mbadala na huu tuishio, na mizimu

wanafuatilia kazi/shughuli zetu za kila siku.

4.3 Chimbuko la Matambiko Katika Jamii ya Wasambaa.

Kwa mujibu wa mzee Imamu Abdi Kaniki katika mahojiano na

mtafiti wa tasnifu hii alidai kuwa matambiko katika jamii

ya wasambaa yameanza zamani sana enzi za mababu na mababu

Kirama, Kh. (1953) Katika kitabu chake cha Habari za

wakilindi amebainisha kuwa jamii ya wasambaa hususani

wakilindi ambao aliwazungumzia sana amesema walikuwa

wanatambika kwa miungu yao kuomba mambo mbalimbali hata

pale wanapoenda kinyume na maagizo ya mababu zao

(miungu). Pamoja na haya yote jamii ya wasambaa kama

ilivyo kwa jamii nyingine za kiafrika inaonesha kuwa

walianza matambiko zamani sana katika harakati za

mwanadamu kutafuta suluhu ya mambo ambayo kwa uwazi

yalikuwa nje ya uwezo wake kama vile ukame, vifo,

45

mafuriko, vimbunga na hata radi. Matambiko yalifanywa ili

kuomba msaada kwa mungu ili kupata ahueni juu ya shida

husika. Hivyo ni ukweli kuwa matambiko yalikuwepo tangia

zamani katika jamii ya wasambaa na sio suala ambalo

wameiga kutoka nje.

Chanady (1985) anasema kwamba uhalisia ajabu unahusu

matukio yasiyo ya kawaida, ya kiujiza au chochote kilicho

kinyume cha uhalisia wa kawaida. Katika hali hii kwa

sababu matukio yanayohitaji matambiko mengi yanatokea

katika hali ya ujabu kama vimbunga, radi, mafuriko na

vifo vya kutatanisha.

Wikipedia (2014) wanasema jamii ya Wasambaa, Wabondei,

Wasegeju, Wazigua na Wadigo za Mkoa wa Tanga zimeanza

kutambika kwa ajili ya mizimu yao katika mapango maarufu

sana ya Amboni tangia karne ya kumi na sita, hii

inadhihisha kwamba matambiko yalianza siku nyingi mno

katika jamii ya wasambaa.

4.4. Umuhimu wa Matambiko Katika Jamii ya Wasambaa

46

Matambiko yana nafasi na umuhimu mkubwa sana katika jamii

ya kabila la wasambaa, mtafiti aliweza kuhojiana na

wanajami 25 ambapo wanaume walikuwa 15 na wanawake 10

ambapo miongoni mwa watafitiwa 19 wamekiri matambiko yana

umuhimu wa kuwa sawa na asilimia 79 na washiriki 3 sawa

na asilimia 9.5 wamesema matambiko hayana umuhimu na

washiriki 3 wamesema hawajui chochote sawa na asilimia

9.5 kama inavyooneshwa katika kielelezo kifuatacho.

Majibu Idadi Asilimia

Ndio 19 76%

Hapana 3 12%

Hawajui 3 12%

Jumla 25 100%

Kielelezo Na. 6 Umuhimu wa matambiko

Matokeo yanabainisha baadhi ya umuhimu wa matambiko

katika jamii ya wasambaa wanaoishi kaskazini mwa Tanzania

kama ifuatavyo;

i.Matambiko hujenga imani

47

ii.Matambiko husaidia kuendeleza mila na desturi

iii.Matambiko hujenga mahusiaano mema

iv.Matambiko huiongoza jamii katika mapambano na matatizo

4.4.1 Matambiko Hujenga Imani

Matambiko hujenga imani kama chombo cha kutatulia matatizo ya

kijamii katika jamii husika katika misingi ya kwamba inapotokea

janga kwa mfano mafuriko, ukame, njaa, ajali, magojwa na

kufanywa matambiko katika namna mbalimbali kutegemeana na

tatizo wanajamii washakuwa na imani kwamba baada ya kufanya

hivyo lazima patakuwa na ahueni juu ya tatizo lao kama tu

wametekeleza kama wahenga wanavyotaka kwani wanahusianisha

matatizo na kuchukia kwa mababu waliotangulia.

Strecher (1999) anafafanua uhalisia ajabu kama kile kinachotendeka

wakati ambapo ukweli wa ndani wa mandhari ya juu unapoingiliwa

na kitu ambacho ni cha kiajabu sana kuaminika. Matambiko katika

jamii ya wasambaa huwajengea imani ya ajabu sana wanajamii

husika kutokana na mambo ya ajabu ambayo yanatokea na

yanayofanywa wakati wa matambiko na matokeo yake.

4.4.2 Matambiko Husaidia Kuendeleza Mila na Desturi

Matambiko husaidia kuendeleza mila na desturi za jamii ya

wasambaa kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Matambiko yana

umuhimu mkubwa sana kwa sababu yenyewe ni kama njia ya

kuwafundisha wanajamii jinsi ya kutatua matatizo yao kijamii.

48

kwa jinsi hiyo mila na desturi za jamii husika huendelea kutoka

kizazi kimoja hadi kingine kwa sababu wakati wa matambiko

katika jamii ya wasambaa huhusisha wake kwa wanaume, wazee

na vijana ambapo vijana huona jinsi wazee maalumu

wanavyofanya, hivyo hata kesho hawapo nao wameshajua taratibu

za kufuata katika kutunza na kuendeleza mila na desturi za kabila

la wasambaa.

Louis, P. (2005) anasema uhalisia ajabu unapaswa kueleweka kwa

kadiri fulani kama mkabala wa kuuwakilisha uhalisia kwa kukiuka

mipaka kati ya dhana, vitu au hali. Katika jamii ya wasambaa ni

ukweli kabisa kuwa matambiko ni chombo kikubwa cha kuendeleza

mila na desturi za jamii hii. Matambiko huvuka mipaka ya dunia

hii na kusogea mbali na kufikia upeo wa juu wa dunia nyingine

ambayo kwao wanaamini ni kuzimu yaani sehemu maalumu

zinakoishi roho za watu waliokufa hususani za wale waliotenda

mambo mema. Na wasambaa wana imani kuwa matatizo ni

matokeo ya kuchukia kwa mizimu.

4.4.3 Matambiko Hujenga Mahusiano Mema

Matambiko katika jamii ya wasambaa husaidia kujenga na

kuimarisha mahusiano mema miongoni mwa wanajamii. Katika

jamii ya wasambaa ikitokea wanajamii wamepishana kuna mambo

ya kufanya ili kuwaleta katika hali ya uelewano, ambapo hufanya

viapo maalumu ili yule aliyemkosea mwenzake iwe kwa makusudi

au kwa bahati mbaya asirudie tena na kwa kiapo hicho wanajamii

waliokoseana wanaahidi mbele ya wazee kwamba

49

hawamesameheana na hakuna mwenye kinyongo na mwenzake

baada ya hapo anachinjwa kondoo kama kosa ni kubwa na kula

pamoja ikiwa ni ishara ya kupatana na baadhi ya nyama na uchafu

uliokuwa tumboni mwa mnyama huyo huzikwa ikiwa ni ishara ya

kuzika tofauti zao na kuanza maisha mapya. Na ikitokea miongoni

mwa mmoja akamkosea mwenzake anadhurika hata kufa. Kwa jinsi

hiyo jamii kupitia matambiko panakuwa na mshikamano chanya.

Kulingana na Hean, D. T. (2005) anaelezea uhalisia mazingaombwe

kwa kuchukua michoro iliyo na uhalisia kama picha ya kamera

lakini iliyoibua hisia kwa kuchanganya uhalisia na ukosefu wa

uhalisia. Ambapo katika jamii ya wasambaa, kwa kukoseana

miongoni mwa wanajamii katika hali ya kibinadamu, ambapo hali

hiyo ni ya kawaida au ina uhalisia kabisa ila njia ya kuelewana au

kuwaleta pamoja wanajamii haina uhalisia kuanzia matendo

yenyewe ya kuwapatanisha kwani wanahusishwa viumbe ambao

hawapo katika uhalisia na hata dunia wanayoishi hatuijui kabisa.

Hatimaye wanajamii waliokoseana katika hali ya uhalisia hupata

hofu ya ajabu na kuelewana na kuheshimiana katika hali ya

kiajabuajabu. Na ndio maana mmoja wapo anapomkosea mwenzake

kwa mara nyingine tena kwa makusudi anapata madhara makubwa

ikiwa hata kufa katika hali isiyo ya kawaida.

4.4.4 Matambiko Huiongoza Jamii Katika Kupambana na

Matatizo

50

Matambiko huiongoza jamii katika mapambano dhidi ya matatizo

mbalimbali yanayoikabili jamii husika. Katika jamii ya wasambaa

kuna matatizo mbalimbali ambayo yanaitatiza jamii hii kwa mfano

ukame, mafuriko, njaa, ajali na mambo mengine mengi kwa

kupitia matambiko jamii huongozwa katika kupambana nayo kwani

inapotokea ukame na pengine wanajamii wanatumia vibaya

rasilimali zilizopo kama misitu kwa kupitia matambiko wanapata

ujumbe juu ya kutunza misitu au hata kutumia mito kwa shughuli

maalumu na sio shughuli ambazo ni za kuharibu mazingiza kwani

kwa kufanya hivyo wahenga wanakasirika na kuwaletea matatizo

hayo kama adhabu.

Njogu na Wafula (2007) wanaeleza Uhalisia ulitokana na

matatizo yaliyokuwa yanawakabili watu, matatizo hayo

yaliwafanya watu kuanza kushutumu ulimbwende na matamanio

ya kilimbwende yalikuwa ya kiusingizini (kinjozi) zaidi

yakilinganishwa na shida na matatizo yaliyokuwa

yanawakabili watu. Hapa wasambaa nao walikuwa

wanakabiliana na matatizo yao ya kawaida kwa kutafuta

suluhu kutoka kwa mizimu, miungu yao ambayo kiuhalisia

nguvu hizo hazina nguvu ila kiajabuajabu mizimu na miungu

ina nguvu sana hususani katika kutatua matatizo.

51

4.5. Athari za Matambiko Katika Jamii ya Wasambaa

Mtafiti alipenda kujua kama kuna hasara ama athari zozote

zinazoweza kusababishwa na utekelezaji wa matambiko. Kutokana

na majibu ya watafitiwa zipo hasara nyingi ambazo hutokea pindi

matambiko yanapofanywa washiriki walio wengi wamekiri kuwepo

kwa hasara hususani pindi matambiko yanapofanywa kwani

huhitaji pesa na wanyama. Ambapo watafitiwa 20 sawa na asilimia

80 wamekiri kuwepo kwa hasara, watafitiwa 4 sawa na asilimia 16

wamesema hakuna hasara yeyote kwani sadaka kwa miungu yao

hawaoni uwepo wa hasara na mtafitiwa 1 sawa na asilimia 4

amesema hajui uwepo au kutokuwepo kwa hasara.

Majibu Idadi Asilimia

Ndiyo 20 80%

Hapana 4 16%

Hawajui 1 4%

Jumla 25 100%

Kielelezo Na. 6 Athari za matambiko

Hasara zilizoanishwa na watafitiwa ni kama ifuatavyo;

I. Matambiko hujenga dhana potofu

II. Matambiko huleta hasara kubwa kwa jamii

III. Matambiko huwafanya watu kuishi kwa wasiwasi mkubwa

52

4.5.1 Matambiko Hujenga Dhana Potofu

Matambiko hujenga dhana potofu katika jamii kwa kuamini

nguvu fulani bila ya kuwa na uthibitisho wa kisayansi.

Matambiko hufanywa kwa kuamini miungu, mahoka, na mababu

waliotangulia ambapo wanajamii hujenga imani imara kabisa

kuwa wao ndio kila kitu na hata pale litokeapo tatizo

huhusianisha na kuwakasirisha na hivyo wanalazimika

kuwafanyia tambiko ama ibada kubwa za kishetani ambapo

huenda sambamba na upikaji wa vyakula na uchinjaji wa

wanyama jambo ambalo sio sahihi.

Marquez, G. (1925) yeye anachukulia uhalisia ajabu

kwamba, mambo yanayoelezewa kuwa ya kiajabu na kichawi ni

sehemu ya mwonoulimwengu wa jamii hizo. Wasambaa wao

wanaamini juu ya matambiko hata kama wachache huyaona

kama dhana potofu, wao wanichukulia kama sehumu ya maisha

yao. Mambo mengi yanayofanyika wakati wa matambiko

huhusiana sana na shughuli za kichawi, kuanzia vitendo na

53

hata nyimbo za matambiko hazina tofauti na zile za

kichawi.

4.5.2 Matambiko Huleta Hasara Kubwa kwa Jamii.

Matambiko huleta hasara kubwa kwa jamii husika kwani

kafara, sadaka za matambiko zinahitaji wanyama na vyakula

ambavyo wanajamii hutumia pesa nyingi kuvipata kwa

kuamini kuwa kwa kufanya hivyo hasira zao zitatulia na

mambo yataenda vizuri katika jamii husika jambo ambalo ni

kuongeza majukumu yasiyo ya lazima. Ambapo baadhi ya

vyakula na nyama huwekwa makaburini, mapangoni, mtoni,

baharini wakiamini waliotangulia (miungu, mahoka, mizimu)

watakula jambo ambalo kimsingi halina ushahidi kisayansi.

Robert, R. P.J. (1949) katika kitabu chake cha “Beliefs

in spirits” anasema mizimu ni viumbe ama roho za watu

waliokufa. Iwapo mtu atakufa katika hali nzuri bari roho

yake itaenda katika kijiji cha wafu kiitwacho kuzimu. Na

ikiwa mtu atakuwa katika hali ambayo sio nzuri roho yake

haifiki katika kijiji hicho bali hutangantanga mapangoni,

54

msituni, ziwani, mtoni, mabondeni na hata mashambani na

roho hizi huweza hata kuwadhuru watu wazima. Kutokana na

maelezo hayo walio hai hufanya matambiko makubwa

kutokomeza roho hizo ambazo huwasumbua mara kwa mara na

kukwamisha shughuli za kawaida za kibinadamu.

4.5.3 Matambiko Huwafanya Watu Kuishi kwa Wasiwasi Mkubwa

Matambiko huwafanya watu kuishi kwa wasiwasi mkubwa

kwani panapotokea tatizo na uwezo wa kufanya tambiko

haupo wanajamii husika hupwatwa na hofu kubwa maishani

kwa kushindwa kutimiza yale wanayodhani wazee, mahoka

wanahitaji kufanyiwa.

4.6. Mazingira Ambapo Matambiko Hufanyika

Katika mahojiano na mtafitiwa Ndg. Mngazija K.A anasema

matambiko katika jamii ya wasambaa hufanywa katika

mazingira maalumu sana na tulivu. Maeneo hayo ni lazima

ufikapo hapo uwe na utulivu na nidhamu ya hali ya juu

kulingana na viashiria vyake kwani katika jamii ya

wasambaa huchukuliwa kama maeneo matakatifu kulingana na

55

imani ya jamii husika. Katika jamii ya wasambaa miungu

yao inasadikiwa kuwa huishi katika mazingira kama mtoni,

mapangoni, juu ya milima mikubwa, kwenye misitu mikubwa,

kwenye majabali makubwa, kwenye nyumba maluumu (nyumba za

duara zilizoezekwa kwa majani ya migomba) pamoja na

makaburini. Katika maeneo ya usambaani wasambaa mara

nyingi huenda kutambika kwa zumbe Kimweri ambapo pana

mazingira mbalimbali ambayo yanasadifu matambiko

kulingana na tatizo husika. Pia kuna milima mbali mbali

kama Mlima Mzoghoti ambao upo eneo la Rangwi, masitu wa

Kideghe ambao upo katika kata ya Rangwi katika kijiji cha

Goka pamoja na mito mbalimbali.

Wamitila (2008) anadai kuwa uhalisiaajabu ni kuwepo

matukio ambayo ni vigumu kuyaeleza katika misingi wa

uhalisia wa kawaida katika jamii. Katika jamii ya

wasambaa mazingira ambayo matambiko hufanywa ni ya ajabu

japo yapo katika uhalisia wa kawaida na vigumu kuyaelezea

katika msingi wa kawaida. Kwa mfano vinyumba vya mizuka

ambavyo hutumika sana katika kufanyia shughuli kadha wa

56

kadha za matambiko na kiganga. Ambapo katika vinyumba

hivyo huwekwa vyakula, pesa na hata damu wakiamini mizimu

na mizuka huchukua kama sadaka yao kwao.

4.7. Vyakula Ambavyo Hutumika katika Kutekeleza Matambiko

Katika mahojiano na Mama Mahemedi anasema, Mtambiko

katika jamii ya wasambaa yanahitaji maandalizi makubwa

sana ya vyakula kwani huhusisha vyakula mbalimbali

kulingana na uhitaji wa waliotangulia na hata pengine

vyakula ambavyo wahenga walikuwa wanavipendelea. Mara

nyingi sana huwa wanapika makande yasio na maharage,

wali, nyama, maziwa, maji, asali, pombe nazi, pamoja na

matunda mbalimbali kama vile ndizi na mananasi. Vyakula

hivi kikishapikwa huwekwa kwenye vyombo maalumu na

kupelekwa maeneo husika kama makaburini, njia panda,

mapangoni, milimani na hata kumwagwa mtoni wakiamini kuwa

waliotangulia watakula na kupokea sadaka yao na

kuwasamehe pale walipokosea au kuwajalia neema kadha wa

kadha kulingana na mahitaji yao.

57

4.8. Wanyama Wanaotumia Katika Matambiko Katika Jamii ya

Wasambaa.

Mzee Abdi Shekalaghe anasema matambiko ni suala takatiku

sana katika jamii ya wasambaa na linatekeleza kwa

kuhusisha wanyama maalumu kulingana na maaono ya wazee

kutoka kwa wahenga. Wanyama hao ni kama ng’ombe, mbuzi,

kondoo na kuku kulingana na uzito wa tatizo. Katika jambo

hili wanyama hao wanaandaliwa vizuri na husemewa maneno

mbalimbali na maalumu ambapo hufikia hatua mnyama husika

hata awe dume la ng’ombe hulala peke yake na kuchinjwa

bila kuleta fujo ya aina yeyote na katika mchakato wa

kupasua wazee husika huwa wanachunguza baadhi ya mambo

kwenye tumbo la mnyama husika na kung’amua iwapo ombi lao

limepokelewa au la.

Rio (1999) anadai kwamba uhalisiaajabu unahusu matukio

yasiyo ya kawaida au jambo lililo kinyume na uhalisia wa

kawaida. Katika jamii ya wasambaa ni jambo la ajabu

machoni pa watu ambapo Ng’ombe dume anasemewa maneno ya

58

ajabu mpaka analala mwenyewe bila ya kushikwa na watu

tayari kwa kuchinjwa. Katika uhalisia wa kawaida hakuna

jambo kama hilo na haliwezekani. Jambo kama hilo ni la

ajabu mno, hapo inathibitishwa kuwa matambiko yana nguvu

na nafasi kubwa katika jamii ya wasambaa.

4.9. Mambo Yanayosababisha Utekelezaji wa Matambiko

katika Kabila la Wasambaa

Katika mahojiano na watafitiwa Bw na Bi Mashanga

(wataalamu wa matambiko katika ukoo wa Kaniki) wanasema

kama ilivyo kila jamii ina utaratibu wa kufanya mambo na

mahitaji, matatizo pia hutofautiana hivyo katika jamii ya

wasambaa kuna sababu mbalimbali ambazo huwasukuma

wasambaa kufanya matambiko. Wasambaa hawafanyi matambiko

kama sherehe za kidini au kama burudani bali kama sehemu

maalumu kabisa ya kujiweka karibu na miungu yao

wanayoiamini wakiwa na nia moja tu ya kuiabudu sambamba

na kutoa sadaka za makafara kwa miungu yao na mizimu

wanayoamini ina nguvu. Katika mahojiano kati ya mtafiti

59

na wahusika kadha wa kadha katika nyakati tofauti

waibainisha sababu mbalimbali ambazo kwazo lazima

wanajamii watambike. Nazo ni kama ifuatavyo;

I. Taratibu za kikoo pengine kila mwisho wa mwaka

lazima watoe sadaka kwa wazee wao waliotangulia.

II. Ukame unaosababisha watu kukosa chakula maji kwa

muda mrefu kwa wanajamii pamoja na mifugo yao.

III. Mafuriko mfano mwaka 1993 katika jimbo la mlalo

yalitokea mafuriko watu wengi walipoteza maisha na

mali nyingi.

IV. Upotevu wa mali kama ng’ombe wengi mara nyingi

wasambaa wanaamini kuwa mali inapotokea katika

mazingira yasiyoeleweka basi kuna jambo haliko sawa

hivyo matambiko hayakwepeki.

V. Kupotea kwa mtu katika jamii ya wasambaa inapotokea

mtu amepota katika mazingira ya kutatanisha hapo

wanapata ishara kuwa wamekosea mahali Fulani hivyo

lazima wakatoe sadaka.

60

VI. Kumbukumbu ya waliotangulia (wafu waishio kuzimu),

Koo nyingi kulingana na magumu wanayokutana nayo

wameamua kuweka siku maalumu ya kufanya ibada hizo

ili kuepukana na adhabu mabalimbali hususani pale

wanaposahau kufanya matambiko au ibada hizo.

VII. Mahitaji ya Baraka mbalimbali kulingana na baraka

ambazo wasambaa wanaamini ni kwa neema ya miiungu

mizimu wanayoitambikia basi itokeapo mwanafamilia

amepata kile anachoamini ni Baraka hana budi kwenda

kufanya tambiko.

VIII. Katika jamii ya wasambaa itokeapo ajali miongoni mwa

wanaukoo wao wanachukulia ni adhabu kutoka kwa

waliotangulia hivyo ili kuwatuliza ni lazima kufanya

tambikoili kuwanususu na mambo kama hayo.

IX. Mara nyingi vifo vya kutatanisha huwapa hofu watu

wengi kadhalika katika jamii ya wasambaa vifo

ambavyo chanzo chake hakipo wazi ni lazima watu

warudi nyuma na kutafakari pale walipokosea na

kufanya tambiko.

61

X. Magonjwa katika jamii ya wasambaa magonjwa ya

mlipuko pia huhusianishwa na kukosea wahenga hivyo

itokeapo magojwa ya aina hii kama tauni ambayo

iliathiri sana watu wa jamii ile matambiko

yalifanywa ili kuomba radhi.

XI. Shukrani za Baraka walizopata, Baraka mbalimbali

kama kunusurika kufa, kupata motto, kufaulu masoma,

kujenga nyumba,kununua gari na mambo kama hayo

matambiko hufanywa ili kufungua njia kwa wanajamii

hao.

4.10. Muda Ambao Matambiko Hufanywa

Mzee Kaniki, A.I anasema matambiko katika jamii ya

wasambaa hufanywa katika vipindi maalumu kwani jamii ina

mambo ambayo ni ya msimu na mengine ni ya dharula.

Ngwatu, H.M anasema kabla ya mvua za vuli wanajamii

hujipanga kwa ajili ya matambiko ili kupata Baraka au

kufunguliwa njia kwa ajili ya shughuli za kilimo ambapo

baada ya hapo wazee kwa kushirikiana na wataalamu wa

62

mambo ya matambiko huandaa maji maalumu ambayo ni

mchanganyiko wa udongo, maji, unga wa nafaka mbalimbali

baada ya kuomba mambo kadha wa kadha vijana hutumwa

kwenda kunyunyiza maji hayo maalumu shambani (hande)

ambapo hakuna mwanajamii anayeruhusiwa kuanza kufanya

shughuli zozote za kilimo mpaka vijana wapiti au kumaliza

shughuli hiyo muhimu na baada ya vijana hao kumaliza ni

lazima watu wakae siku tatu ama nne ili maombi yao

yafike. Lengo ni kuomba Baraka, msamaha kwa miungu na

mizimu pamoja na kuwaondolea nuksi mbalimbali kunzia

nyumbani mpaka mashambani na hata katika shughuli zao

zote katika msimu huo, hapo wanajamii wanakuwa wamepata

ruhusa ya kuanza kuandaa mashamba tayari kwa msimu wa

kilimo. Kadhalika baada ya mavuno matambiko pia hufanywa

kwa lengo la kutoa shukrani kwa miuungu hao.

Matambiko pia hufanywa muda wowote patokeapo dharula kama

magonjwa ya mlipuko, ajali na mambo kama hayo ambayo

hutokea bila taarifa.

63

4.11. Uhalisia Mazingaombwe/Uhalisia Ajabu wa Nafasi ya Matambiko Katika Jamii ya Wasambaa

TUKI (2009) wanasema hii ni dhana iliyobuniwa na msanii

wa ujerumani Franz Roh, katika kitabu chake Nach-

expressionnism, magischer realismus.Probleme der neusten

europaischer malalerei. Dhana hii huhusishwa na waandishi

wa marekani ya kusini au hata nchi zinazoitwa ulimwengu

wa tatu na hutambulishwa na sifa mbalimbali. Sifa hizi ni

za kuyaelezea matukio ya kifantasia au ya ajabu au

kichawi kwa namna ya moja kwa moja kwa namna inayofanana

yaonekana kama ya kawaida tu. Mpaka uliopo kati ya mambo

yanayoweza kupatikana katika ulimwengu halisi na

yasiyowezakana huwa madogo sana. Sababu hasa ya matumizi

ya mtindo huu ni kuonesha kuwa matukio ya aina hii

hupatikana katika maisha ya kawaida katika jamii

zinazohusika. Nadharia hii inasisitiza kuwa fasihi

haiwezi kujitenga na hali halisi ya maisha ya watu katika

jamii ambamo fasihi imeundwa na kutumika.Waandishi

wanaoandika katika msingi huu hushikilia kuwa mtizamo wao

64

wakiuhalisia unawakilisha msimamo wa jamii zao. Yaani

mambo yanayotekelezwa kama ya ajabu na kichawi ni sehemu

ya mwonoulimwengu wa jamii hizo. Mtazamo huu umemuongoza

mtafiti wa tasnia hii kung’amua kuwa matambiko katika

jamii ya wasambaa kwamba hufanywa kwa sababu matatizo au

changamoto mbalimbali yanakuwepo ndani ya jamii ya

wasambaa na matambiko katika hatua za utekelezaji wake

panakuwepo na uhalisia mkubwa kwa sababu vitu

vinavyotumika ni vya asili mno na uajabu au mazingaobwe

ni zile ishara kubwa zitokeazo mfano alama zionekanazo

katika tumbo la mnyama husika, mnyama kulala peke yake na

kuchinjwa, radi na mvua kubwa baada ya tambiko ikiwa ni

ishara ya kupokelewa kwa sadaka husika, kwa kututia

nadharia hii mtafiti ametazama nafasi ya matambiko katika

jamii ya wasambaa.

4.12. Hitimisho

Katika sura hii mtafiti amejikita katika kuchambua data

mbalimbali zilizopatikana na zinazohusu nafasi ya

65

matambiko katika jamii ya wasambaa. Mtafiti ameangalia

pia vipindi ambavyo matambiko hufanywa, vifaa vitumikavyo

katika zoezi la matambiko katika jamii ya wasambaa,

wahusika, vyakula vinavyotumika pamoja na mavazi

yanayotumika huku akiongozwa na nadharia ya uhalisia wa

mazingaobwe. Nadharia hii uhalisia mazingaobwe/uhalisia

ajabu (Magical Realist theory) imekuwa msaada mkubwa

katika kukamilisha utafiti huu kwani mtafiti ameweza

kubaini umuhimu, hasara, sababu pamoja na namna ambavyo

matambiko hufanywa katika jamii ya wasambaa. Vizazi vya

leo vinaenda kusahau na kuacha utanzu huu muhimu wa

fasihi simulizi hivyo mtafiti aliliona hilo na ndio

sababu kuu iliyomsukuma kufanya utafiti huu ili kutunza

na kuiendeleza fasihi ya wasambaa.

SURA YA TANO

HITIMISHO MUHTASARI NA MAPENDEKEZO

66

5.1Utangulizi

Tunapoongelea juu ya nafasi ya matambiko katika jamii ya

wasambaa, hapa tunaangalia na kubainisha umuhimu wa

matambiko, hasara za matambiko, wahusika wa matambiko

pamoja na mandhari au eneo matambiko yanapofanyika.

Mtafiti katika sura ya nne alichambua na

kubainishaumuhimu wa matambiko, hasara za matambiko,

wahusika wa matambiko pamoja na mandhari.

Vilevile mtafiti amechambua na kubainisha kwa kina

vipindi, mambo yanayosababisha kufanyika matambiko, vifaa

vinavyotumika katika matambiko, vyakula vinavyotumika

katika matambiko, miungu/mizimu inayotambikiwa, wanyama

watumikao, mavazi pamoja na msaada unaopatikana kwa

kufanya matambiko.

5.2 Muhtasari

Tasnifu hii imechunguza nafasi ya matambiko katika jamii

ya wasambaa inayopatikana kaskazini mashariki mwa

67

Tanzania, mkoani Tanga wilaya ya Lushoto katika tarafa ya

Mtae, kata ya Rangwi na kijiji cha Emao.

Sura ya kwanza inahusu utangulizi wa jumla ambao ulianza

kuelezea dhana ya Matambiko kwa kurejelea wataalam

mbalimbali, usuli wa utafiti, tatizo la utafiti. Malengo

ya utafiti, maswali ya utafiti, mipaka ya utafiti,

umuhimu wa utafiti pamoja na Nadharia ya utafiti

iliyomwongoza mtafiti katika kukamilisha utafiti wake.

Sura ya Pili inahusu mapitio ya machapisho mbalimbali

ambapo uchambuzi, tahakiki na tafiti mbalimbali

zimezofanywa na wataalam tofauti tofauti zilipitiwa

kutoka maktabani na mtandaoni, Mtafiti amewasoma wataalam

hao na kuweza kupata mwanga halisi na kuweza kufanya

utafiti huu, aidha kwa kurejelea nukuu mbalimbali katika

sehemu zinazohitajika bila kuongeza maneno ili

kukamilisha utafiti huu.

Sura ya Tatu inahusu mbinu za utafiti ambazo mtafiti

amezitumia katika utafiti huu, katika sura hii mbinu za

68

utafiti kama vile maktabani, uwandani na mtandaoni

zilitumika, sampuli na usampulishaji ziliweza kutumika

katika kukusanya data kwa kutumia vifaa maalumu kama vile

shajara, kalamu, kompyuta, kinyonyi na penseli katika

kunukuu data za msingi na data fuatizi katika kukamilisha

utafiti huu.

Sura ya nne inahusu uwakilishi na uchambuzi wa data. Hapa

data zilizokusanywa zimechakatwa kwa kuzingatia Nadharia

husika iliyomwongoza Mtafiti katika utafiti huu kwa lengo

la kuonyesha nafasi ya matambiko katika jamii ya wasambaa

umuhimu wake na hasara zake.

Sura ya tano ndiyo sura ya mwisho katika tasnifu hii,

sura hii inahusu utangulizi ambao ulieleza kwa kifupi

sura ya nne ilihusu nini pamoja na sura yenyewe

inazungumzia nini. Pia Mtafiti ameangalia muhtasari wa

tasnifu hii, Mchango mpya wa utafiti huu pamoja na

Mapendekezo mengine ya utafiti. Mtafiti katika sura hii

69

amebainisha maeneo mbalimbali ya kufanyiwa utafiti na

wanazuoni wengine katika hatua mbalimbali za kataaluma.

5.3 Mchango Mpya wa Utafiti Huu.

Utafiti huu umefanikiwa katika kubainisha nafasi ya

matambiko katika jamii ya wasambaa, umuhimu, hasara,

vipindi, mazingira, vyakula vitumi kavvyo na ujumbe

unaopatikana katika matambiko kwa jamii ya wasambaa na

wale ambao sio wasambaa. Hivyo basi Utafiti huu utakuwa

na umuhimu mkubwa katika tansinia hii ya nafasi ya

matambiko katika jamii ya wasambaa kwa kuwa umeweza

kubainisha umuhimu, hasara, wanyama watumikao, mavazi

yatumikayo mazingira yanayotumika pamoja na ujumbe ambapo

umeweza kuwapa mwanga wasambaa na hata wale ambao sio

wasambaa. Pia Utafiti huu utaamsha hisia za wasomaji na

kuchochea wanafasihi kuchunguza namna matambiko

yanavyoweza kutumika katika kufikisha ujumbe kwa jamii.

Aidha Utafiti huu utatoa mwanga kwa watafiti wengine

70

ambao watajikita katika suala zima la nafasi ya matambiko

katika jamii ya wasambaa mkoani Tanga.

5.4 Mapendekezo

Matambiko yana nafasi kubwa katika jamii ya kitanzania

kwani hutumika kuakisi masuala mbalimbali kwenye jamii

katika nyanja za kijamii, kiitikadi, kisiasa na kiuchumi

kama zilivyo tanzu nyingine za kifasihi. Hivyo mtafiti

anapendekeza tafiti zijazo zichunguze matambiko kwa

ujumla, ikiwa ni pamoja na kubaini aina nyingine za

matambiko. Pendekezo lingine kwa tafiti zijazo ziangalie

pia matambiko nje na ndani ya nchi yetu kwa lengo la

kukuza na kutunza fasihi ya jamii za kitanzania.

5.5 Matokeo ya Utafiti

Mtafiti alitimiza lengo la utafiti wake kwani kupitia

nafasi ya matambiko katika kabila la wasambaa, mtafiti

aliweza kuonesha umuhimu wa utafiti huu kwa wasomaji wa

tasnifu hii na jami ya wasambaa kwa ujumla. Kupitia

nadharia ya Uhalisia wa mazingaombwe, mtafiti ameweza

71

kuchambua matambiko katika kabila la wasambaa jinsi

yanavyofanywa, mazingira, wahusika, umuhimu na hata

athari zake.

Mambo hayo ndiyo yaliyomsukuma mtafiti kuweza kufanyia

utafiti wake na kuonesha jinsi umuhimu wa matambiko,

athari za matambiko, vyakula ambavyo hutumika katika

matambiko, wanyama wanaotumika katika matambiko ya

wasambaa.

5.6 Hitimisho

Katika sura hii ya Tano Mtafiti ameweza kuangalia

muhtasari wa mada kupitia sura zote tano, Mchango mpya wa

Utafiti huu pamoja na Mapendekezo kuhusu tafiti zijazo.

Ni matumaini ya mtafiti kuwa kazii hii ni mwanzo na

muendelezo wa kazi nyingine nyingi.

Marejeo

72

Assumpta, K.M. (2011) Fani ya Fasihi Simulizi kwa Shule za Upili,

Oxford university press.

Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) (2010) Kamusi ya Kiswahili

( toleo jipya) Oxford University Nairobi

Kamusi ya Karne ya 21 (2011) Longhorn Publishers (T) Ltd,

Nairobi. Kenya.

Kamusi ya Kiswahili Sanifu (2004) Oxford University Press.

Kenya.

Kirama, Kh. (1953) Habari za Wakilindi, Vuga Press

Kitula, K.- Catherine, N.M.K (2010) Misingi ya Fasihi Simulizi,

Kenya litearure Bereau.

Kothari, C. R. (1991) Research Methodology. Methods and Techning,

(2rd Edition). Wiley Eastern Limited. New Delh.

Masebo, J. A. (2007) Nadharia ya Fasihi Kidato cha Tano na Sita,Nyambari Nyangwine publishers.

Materu, B. L. (1982) Tanzu za Fasihi Simulizi Mulika namba 19,

Taasisi ya uchunguzi wa Kiswahili chuo kikuu cha Dar es

Saalam.

Mulokozi M. M. (1996) Fasihi ya Kiswahili OSW. Chuo kikuu cha

Dar es Salaam

Salimu, K. B.(1992) Kamusi ya Maana na Matumizi. Oxford univeritypress Nairobi, Dar es Salaam na Kampala.

73

Taasisi ya uchunguzi wa kiswahili (2008) Kamusi ya Kiswahili Sanifu,Nairobi, Kenya, University press, East Afrika L.t.d

Mng’anuth, K. T. (2007/2008) Fasihi Simulizi na Utamaduni,

Autolitho Ltd Nairobi Kenya.

TUKI (2004) Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Oxford University Press

TUKI (2009:63) Nadharia za Uhakiki wa Kazi za Fasihi, Oxford University

Press

TUMI (1988) Kiswahili kwa Shule za Sekondari; Chuo kikuu cha Dar

es Salaam

Wafula, R. M - Kimani, N. (2007) Nadharia ya Uhakiki wa Fasihi.

Jomo Kenyata Foundation. Nairobi.

Wamitila, K.W. (2008) Kanzi ya Fasihi, Misingi ya Uchanganuzi wa

Fasihi, Nairobi, Public Vide Muwa Publisher Limited.

Wamitila, K.W. (2006) Fasihi Istilahi na Nadharia, Nairobi

Phoenix publisher Ltd.

Wamitila, K.W. (2006) Uhakiki wa Fasihi Msingi na Vipengele Vyake,

Nairobi Phoenix publisher Ltd.

Wamitila, K.W.(2003) Kamusi ya Fasihi, Istilahi na Nadharia. EnglishPress Nairobi.

Wikipedia, Kamusi elezo huru, (2013) “Historia ya

Wasambaa”, http://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=washambaa&oldid=

889928 jamii (21/12/2013 saa 07:58)

74

Wikipedia, Kamusi elezo huru, (2013 “Milima ya Usambara,

http://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=milima ya usambara&oldid=

889928 jamii (09/02/2013 saa 10:56)

Wikipedia, Kamusi elezo huru, (2013) “Tarafa ya Mtae”,

http://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=mtae&oldid=451923jamii

(10/03/2014) (saa 15:53)

Wikipedia, Kamusi elezo huru, (2014) “Fasihi Simulizi ya

Kiafrika”, http://chomboz.blog.com/p/maisha.html (07/03/2014 saa

10:56)

Wikipedia, Kamusi elezo huru, (2014) “Matambiko na

Ushirikina”, [email protected] (10/02/2014) (saa

15:53)

75