uhuru wa kweli - GetValue

288

Transcript of uhuru wa kweli - GetValue

UHURU WA KWELI ii

Hakimiliki © Mwandishi

Baraka Shibanda

Simu: +255 767 495 842 | +255 768670143 |

+255 621054592

Baruapepe: [email protected]

Haki zote zimehifadhiwa!

Kitabu Kimefanyiwa Ubunifu na:

LD-Lamax Designs, +255 764 793 105

[email protected]

Haki zote za kitabu hiki zimehifadhiwa.

Hairuhusiwi kutoa nakala sehemu yoyote ya

kitabu hiki kwa namna yoyote bila idhini ya

mmiliki wa kitabu hiki, isipokuwa kwa kunukuu

kuliko ruhusiwa kisheria.

UHURU WA KWELI iii

YALIYOMO

SHUKRANI ------------------------------------------------------------------ ix

DIBAJI ----------------------------------------------------------------------- xiii

UTANGULIZI ---------------------------------------------------------------- xv

SURA YA KWANZA --------------------------------------------------------- 1

Kwanini iwe hivi? ------------------------------------------------------- 1

SURA YA PILI -------------------------------------------------------------- 21

Kwanini niuishi ukale ------------------------------------------------- 21

SURA YA TATU ------------------------------------------------------------ 61

Mbona sio asili yangu ------------------------------------------------ 61

SURA YA NNE ------------------------------------------------------------ 105

Sikuumbwa kwa kusudi hili ---------------------------------------- 105

SURA YA TANO ---------------------------------------------------------- 123

Nitasimama tena ----------------------------------------------------- 123

SURA YA SITA ------------------------------------------------------------ 171

Yesu Kristo alimaliza yote msalabani ---------------------------- 171

SURA YA SABA ----------------------------------------------------------- 189

Mimi si mfungwa tena ---------------------------------------------- 189

SURA YA NANE ---------------------------------------------------------- 205

Nimebarikiwa --------------------------------------------------------- 205

SURA YA TISA ------------------------------------------------------------ 223

Mimi ni mshindi ------------------------------------------------------ 223

UHURU WA KWELI iv

SURA YA KUMI----------------------------------------------------------- 243

Nitakiri hivi daima --------------------------------------------------- 243

HITIMISHO --------------------------------------------------------------- 265

KUHUSU MWANDISHI ------------------------------------------------- 267

UHURU WA KWELI v

VIFUPISHO

1 Falme: 1 Wafalme

1 Kor: 1 Wakorintho

1 Pet: 1 Petro

1 Samw: 1 Samweli

1 Timo: 1 Timotheo

1 Yoh: 1 Yohana

2 Kor: 2 Wakorintho

2 Yoh: 2 Yohana

3 Yoh: 3 Yohana

Ayu: Ayubu

BHND: Biblia ya Habari Njema

CCT: Christian Council of Tanzania

Dan: Daniel

Ebr: Waebrania

Efe: Waefeso

Filip: Wafilipi

UHURU WA KWELI vi

Gal: Wagalatia

Hes: Hesabu

Hos: Hosea

Isa: Isaya

KJV: King James Version

Kol: Wakolosai

Kut: Kutoka

Luk: Luka Mtakatifu

Mark: Marko Mtakatifu

Mat: Matendo ya Mitume

Math: Mathayo Mtakatifu

Mhu: Mhubiri

Mwa: Mwanzo

NEN: Biblia ya NENO

NIV: New International Version

Rum: Warumi

Tit: Tito

UHURU WA KWELI vii

TPT: The Passion Translation

UDOM: University of Dodoma

Ufu: Ufunuo

USCF: University Students Christian Fellowship

Yak: Yakobo

Yer: Yeremia

Yoh: Yohana Mtakatifu

Zab: Zaburi

UHURU WA KWELI viii

UHURU WA KWELI ix

SHUKRANI

angu nianze huduma hii ya uandishi sikuweza kupiga

hata hatua moja bila Mungu, Roho Mtakatifu.

Namshukuru sana Roho Mtakatifu rafiki yangu kwa

kuniwezesha kwa kiwango kikubwa kisichoelezeka hasa

pale nilipochoka, na kutaka kuahirisha kazi hii. Roho

Mtakatifu amekuwa akinipa msukumo mkubwa sana,

usioelezeka, kwa sababu kuna wakati hali yangu ya ndani

ilichoka. Kwa neema yake niliweza kuandika, hata katika

hali hiyo hiyo ya kuchoka. Kusudi niweze kutimiza ule

utumishi nilioitiwa katika kuhubiri na kufundisha kwa njia

ya uandishi tangu mwaka 2015.

Aidha napenda kuwashukuru sana hawa wafuatao; Apostle

Shemeji Melayeki amenisaidia sana kwa kiwango kikubwa

tangu nilipomwomba kunisaidia kuhariri kitabu hiki na

kuniandikia dibaji. Hakusita kunikubali na kufanya kazi hii,

bila kujali kuwa hatuna ukaribu sana wa mawasiliano na

kutofahamiana. Apostle Shemeji Melayeki amekuwa ni

mtumishi ambaye Mungu amekuwa akimtumia kwa

kiwango kikubwa sana hasa katika nchi ya Tanzania.

Amekuwa akifundisha ufunuo wa neno la kweli juu neema

ya Mungu na kujitambua hali tukijua tumezaliwa mara ya

pili (tumeokoka) na sisi ni nani katika Yesu Kristo. Nami

T

UHURU WA KWELI x

nimalize kwa kusema Apostle Shemeji Melayeki

umebarikiwa sana.

Bila kusahau katika kila huduma kuna watu nyuma yake

wanaoibeba kama ilivyo kawaida. Huduma ya injili ya Kristo

ni bure kutolewa kwa mataifa yote lakini kupelekwa

inapelekwa kwa gharama kubwa sana. Inawezekana hata

hiki kitabu kisingeweza kukufikia mkononi mwako

kukisoma leo hii pasipo msaada wa kifedha kutoka kwa

hawa wafuatao. Tumpe Sanjala, Eliasi Mlwafu, Charles

Mwaipaja, napenda kusema Mungu amewabariki sana.

Zaidi sana niwashukuru wazazi wangu ambao walinisaidia

kunijengea msingi wa kusimama imara katika kumtumikia

Mungu. Bwana Fredy Ambindwile Shibanda na Bi Bupe

Amoni Sanjala Mungu amewabariki sana. Bwana Yesu

amekwisha walipa kwa huduma njema sana.

Asanteni sana LD-Lamax Designs kwa kupangilia kitabu hiki

kuwa katika mfumo unaoweza kusomeka kirahisi na

kuifanya huduma hii kuwa na mvuto kwa wasomaji wote.

Pia nipende kuwashukuru watumishi mbalimbali ambao

wamekuwa wakinitia moyo, kunishauri na kuniombea au

kujifunza kutoka kwao katika huduma hii ili niweze

kufanikisha huduma hii. Ninakushukuru sana Shukuru

Sanga, Baraka Maliaki, Clintoni Sanga, Mwl Samweli

Mkumbo, Mwl Aliko Mwalulili, Mwl Tuntufye Mwakyembe.

UHURU WA KWELI xi

Pia nathamini kuwezeshwa kwa maombi na ushauri na timu

yangu yote ya huduma ya Udhihirisho wa Nguvu za Mungu

(Godly Power Manifestation Ministry [GPM]). Mimi nikiwa

kama Mwanzilishi wa huduma hii na kupewa maono haya

tangu tarehe 12 ya Mwezi Januari Mwaka 2017. Nimeona

kutiwa moyo sana na hawa ndugu zangu, tupo timu kubwa

kiasi ambacho siwezi kuwataja wote kwa majina. Mungu

awabariki sana sana na neema ya Kristo iendelee

kuwahifadhi.

Ninamshukuru baba yangu mlezi wa kiroho Mchungaji

Nelson Shoo amekuwa akinisaidia kiroho tangu nimfahamu

namshukuru sana. Namshukuru baba Mchungaji mlezi wa

USCF-CCT UDOM Chaplaincy, Mchungaji Timothy Erasto

Chimeledya amefanyika baraka sana tangu nimfahamu.

Kwa mara ya kwanza alinishauri kwa kiwango kikubwa

katika uandishi wa kitabu cha YAJUE MAISHA na kitabu cha

KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU. Kwakweli asingenitia moyo

katika hatua za awali za uandishi wa vitabu huenda leo hii

usingeweza kukiona kitabu hiki mikononi mwako. Mungu

amekubariki sana baba Erasto Timothy Chimeledya neema

ya Mungu iendelee kukuhifadhi katika huduma hii ya

ushauri.

UHURU WA KWELI xii

UHURU WA KWELI xiii

DIBAJI

azi aliyoifanya Yesu Kristo kwa mateso yake, kufa,

kufufuka na kuingia katika utukufu wake ni kazi ya

heshima sana. Huo ndio ukombozi kamili wa

mwanadamu. Hapo ndipo adui yetu mkubwa aliposhindwa

yaani dhambi na matokeo yake. Ndiyo maana mitume wa

Yesu Kristo walihubiri kwa nguvu sana habari za ufufuo wa

Yesu Kristo wakisisitiza matokeo yake; yaani toba iletayo

ondoleo la dhambi ikiwekwa muhuri na ubatizo wa Roho

Mtakatifu. Haya mambo mazuri mno.

Baraka Shibanda anatumia lugha rahisi kabisa kuelezea

umuhimu wa kazi ya Yesu na matokeo yake kwenye maisha

ya mwamini kwa namna ambayo ataona uhalisia wa maisha

ya ushindi ndani yake Kristo.

Ninaamini wakati unasoma kwa utulivu mkubwa utaona

ukisogea hatua katika kudhihirisha kazi ya msalaba wa Yesu

Kristo na kutembea katika uhalisia wa UHURU WA KWELI

ndani ya Yesu Kristo.

Apostle Shemeji Melayeki

Bachelor degree in Agricultural Economics

Email: [email protected]

Simu: +255763965297, +255714548565

K

UHURU WA KWELI xiv

Mwanzilishi wa huduma ya Global Family Gathering

Ministries

Dar-es-salaam, Tanzania

UHURU WA KWELI xv

UTANGULIZI

atazamio ya Mungu Baba yetu juu ya ulimwengu

hususani duniani ilikuwa ni kuifanya dunia iliyojaa

amani, upendo na furaha. Mambo haya yamekuwa ni ndoto

si kwa wasiomwamini Kristo tu bali kwa waaminio pia.

Kiuhalisia amani, upendo na furaha zilitakiwa kuwa

chemichemi zinazotokea kwa wote wanaomwamini Kristo

na kuiathiri dunia ili iweze kufurika amani, upendo na

furaha. Kinyume chake idadi kubwa ya waaminio

wamekuwa ndio watu wanaoonekana kuwa ni watu wenye

shida, misukosuko, matatizo yaliyowapelekea kuwa na

huzuni, maisha ya kufeli na kukata tamaa.

Haikutarajiwa kuwa maisha ya kushindwa ni utambulisho

kwa wale wanaomwamini Kristo. Ingawa wapo idadi kubwa

ya wasiomwamini Kristo pia wanaishi maisha ya kushindwa.

Je, Ni kweli Mungu anafurahia wanadamu kuteseka? Au

Mungu anataka wanadamu waishi maisha ya kushindwa?

La hasha! Luka anaandika katika kitabu chake, Luka sura ya

pili kuanzia mstari wa tisa. Malaika anawatokea katika

utukufu wa Bwana na kuwaambia. “Nawaletea habari

njema ya furaha kuu kwa watu wote. Maana leo katika mji

wa Daudi amezaliwa , kwaajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo

Bwana”

M

UHURU WA KWELI xvi

Neno mwokozi ni nomino ambayo kitenzi cheke ni okoa.

Katika lugha ya kigiriki neno okoa linatafsiriwa kama “sozo”.

Neno hili limebeba mambo matatu uponyaji, ukombozi na

ustawi (mafanikio kamilifu). Kwa hiyo wakati malaika

anapeleka taarifa wachungaji kuwa katika mji wa Daudi

amezaliwa mwokozi ambaye ni Kristo Bwana. Maana yake

Kristo amezaliwa ulimwenguni kwaajili ya kuleta uponyaji,

ukombozi na ustawi (mafanikio kamilifu). Baada ya malaika

kutoa taarifa hiyo mara walikuwepo malaika, wingi wa jeshi

la mbinguni, wakimsifu Mungu, na kusema;

“Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa

watu aliowaridhia” [Luk 2:14]

Maana yake Mungu alikusudia kwa mara nyingine dunia

yote iwe ni dunia yenye amani, upendo na furaha. Ukomo

wa mateso, huzuni, uchungu, kukataliwa na kushindwa

ulitatuliwa baada ya mwokozi Yesu Kristo kuja duniani. Hii

ni neema kubwa na ya ajabu mno ambayo akili ya

kibinadamu haiwezi kueleza kwa kiwango cha utoshelevu.

Katika kitabu cha Yohana 8:32, Yesu alikuwa anawaambia

Wayahudi waliomwamini Yesu kuwa;

“tena mtaifahamu kweli, na hiyo kweli itawaweka huru”

[Yoh 8:32]

Yesu alipowaambia Wayahudi tena waliomwamini kwa

lugha nyingine waliookoka. Walichanganyikiwa wakasema

UHURU WA KWELI xvii

mbona hatujawahi kuwa watumwa wakati wote na sisi tu

uzao wa Ibrahimu? Yesu anawaaambia katika mstari wa

thelathini na sita;

“Basi Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli”

[Yoh 8: 36]

Kumbe walikuwa wanamwamini Yesu Kristo lakini bado

walikuwa wamefungwa. Yesu aliwaambia hakuna namna

wanaweza kufunguliwa kuwa huru pasipokukaa katika neno

lake [neno la Kristo] (Yoh 8:30). Neno la Kristo ndio

linapelekea kuijua kweli na kuwa huru kweli kweli.

Kitabu hiki UHURU WA KWELI ni kitabu kinachomueleza na

kumfunua Kristo kama mkombozi kutusaidia kuwa huru

kupitia neema yake aliyoifunua katika yeye ili kutusaidia

kuponywa, kufunguliwa na kuwa na mafanikio kamili. Yesu

alikuja kusuluhisha chanzo cha matatizo yote. Wako watu

waliosongwa na ulevi mbaya (bad addictions) wa aina mbali

mbali (unywaji wa pombe, kuvuta bangi, kuangalia picha na

mikanda ya uchi). Wengine wamekuwa na mitazamo hasi

iliyotokana na imani potofu inayopelekea kujitahidi kwa

juhudi zao katika kulitimiza kusudi la Mungu. Katika

huduma, kazi, vipawa na karama walizopewa. Lakini

mambo haya yote tunaweza kuyafikia kwa neema ya Kristo.

UHURU WA KWELI xviii

Kitabu hiki kitakusaidia kupata ufahamu juu ya

mambo yafuatayo:-Kumsaidia mtu aliyeathirika na

ulevi mbaya (bad addictions) wa aina zote

ulioshindikana kupitia neema ya Kristo.

Kuwa na mtazamo sahihi ambao utapelekea kuwa

na imani itakayokusaidia kudhihirisha uponyaji,

ustawi (mafanikio) na kuishi maisha ya kimbingu

ukiwa duniani kupitia neema ya Kristo.

Kuwa na ufahamu juu ya kuwa na udhihirisho kamili

juu ya huduma, kazi, kipawa na karama zilizoko

ndani yako kupitia neema ya Kristo.

Namna ya kulitimiza kusudi la Mungu kikamilifu

kupitia neema ya Kristo.

Kwa Neema ya Roho Mtakatifu nakukaribisha tuweze

kujifunza UHURU WA KWELI katika Kristo Yesu ili tuweze

kufikia uponyaji, ukombozi na mafanikio kamilifu kama

Mungu alivyokusudia katika maisha yetu.

UMEBARIKIWA.

UHURU WA KWELI 1

SURA YA KWANZA

KWANINI IWE HIVI?

wanini iwe hivi ni swali ambalo linawatesa watu wengi

wakiwa wamefika katika hali ya kujidharau kujiona

hawafai kutokana na vile wanavyovifanya kwenye maisha

yao. Watu wengi wanapofikia hatua hii ya kujidharau huwa

wanaamua kuendelea kufanya makosa zaidi. Wengine

hukosa tumaini kabisa na kuamua kufia dhambini kwa

sababu wanaona haiwezekani kabisa kuwa watu wema

tena (watakatifu). Wakati mwingine kuona haifai kuokoka

na kurudia hali yao ya kawaida waliyokuwa nayo hapo

awali.

Kwanini iwe hivi?

Ni swali ambalo limewatesa watu wengi kiasi ambacho

wengine imewapelekea kukosa mwelekeo zaidi. Aidha kwa

kuendelea kufanya makosa zaidi, wengine wamechukua

maamuzi ya kujinyonga kwa sababu wanaona hawafai

kabisa uwepo wao katika jamii kutokana na tabia mbaya

walizo nazo. Inaweza ikawa ni ulevi wa matumizi ya

madawa ya kulevya, ulevi wa uzinzi, wizi, ujambazi.

K

UHURU WA KWELI 2

Ulevi ni nini? (What is addiction)

Ni kitendo kinachofanyika kwa kujirudia bila kujitambua.

Kuwa na msukumo usiotarajiwa wa kujirudia rudia, ambao

unaweza kuleta madhara ya kisaikolojia, kiafya, kitabia hata

kiuchumi pia. Hali hii imepoteza uwezo binafsi wa watu na

kujikuta wakifanya mambo ambayo hawakutaka kufanya

kabisa.

Tuangalie mifano ya hawa watu wawili Yuda Iskariote

mwanafunzi wa Yesu na Petro mwanafunzi wa Yesu

waliokuwa na swali la namna hii; kwanini iwe hivi? Lakini

kila mmoja alichukua maamuzi tofauti;

Mfano wa Yuda, alivyojinyonga;

“Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, alipoona yakuwa

amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa

makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha,

akasema, Nalikosa niliposaliti damu isiyo na hatia.

Wakasema, Basi haya yatupasani sisi? Yaangalie haya

wewe mwenyewe. Akavitupa vile vipande katika hekalu,

akaondoka, akaenda kujinyonga” [Math 27:3-5]

Yuda alikutana na wakati mgumu sana kwenye maisha

yake, alijikuta alivyomsaliti Yesu haikuwa tarajio lake

akajikuta amechanganyikiwa. Huenda na yeye alijiuliza

UHURU WA KWELI 3

swali la namna hii kwanini iwe hivi? Kwanini nimemsaliti

mwana wa Adamu? Hatimaye ushawishi wa Shetani

alimwingia akaenda kujinyonga, lakini unafikiri mtazamo

wa Yesu juu ya kujinyonga kwa Yuda unautazamaje? Yesu

alipenda kujinyonga kwa Yuda? La hasha Yesu mwenyewe

aliwahi kusema maneno haya;

“Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi, wapate

kutubu” [Luk 5:32]

Kama Yesu alikuja kwa waliopotea, alikuja kuhakikisha watu

wanabadili mitazamo yao na kugeuka katika njia mbaya.

Kama Yesu alikuja kwa wenye dhambi maana yake hakuna

ulevi, majuto, dhambi au majuto yasiyo sameheka mbele ya

Bwana Yesu. Mtazamo wa Yesu kwa Yuda ilikuwa ni kutubu

na sio kujinyonga.

Mfano wa Petro alivyotubu;

“Na Petro alikuwa chini behewani; akaja mmoja wa vijakazi

wa Kuhani mkuu, akamwona Petro akikota moto;

akamkazia macho, akasema, Wewe nawe ulikuwapo

pamoja na yule Mnazareti, Yesu. Akakana, akasema, Sijui

wala sisikii unayoyasema wewe. Akatoka nje hata

ukumbini; jogoo akawika. Na yule kijakazi akamwona tena

akaanza tena kuwaambia wale waliosimama pale, Huyu ni

mmoja wao. Akakana tena. Kitambo kidogo tena wale

UHURU WA KWELI 4

waliosimama pale wakamwambia Petro, Hakika u mmoja

wao, kwakuwa u Mgalilaya wewe. Akaanza kulaani

kuapiza, Simjui mtu huyu mnayemnena. Na mara jogoo

akawika mara ya pili. Petro akalikumbuka lile neno

aliloambiwa na Yesu, Kabla ya kuwika jogoo mara mbili,

utanikana mara tatu. Na alipofikiri, akalia” [Mark 14: 66-

72]

Swali la kujiuliza kati ya Yuda na Petro ni nani ambaye

alikuwa amekosea zaidi?

Yuda alimsaliti Yesu lakini Petro alimkana Yesu mara tatu

wazi wazi. Nakwambia Petro alistahili ajinyonge kama

alivyofanya Yuda lakini Petro alirudi kutubu huku akilia kwa

machozi. Hakuna uovu usio sameheka kwa Bwana, hakuna

ulevi usiosameheka, hata kama wanadamu wote watasema

haufai kabisa umeoza kwa dhambi huwezi kurudi kwa Yesu

kumtumikia. Yesu bado anakuita na bado anakuhitaji

kwaajili ya ufalme wake. Petro huenda naye alijiuliza swali

kwanini iwe hivi? Lakini alijua yupo mkombozi wake, lipo

tumaini lake, akatubu. Petro hakujali watu watasemaje

baada ya kutubu kwa sababu alimkana Yesu wazi wazi

mbele yao, bali aliangalia neema ya msamaha wa Kristo

maishani mwake, alitubu na kusamehewa.

UHURU WA KWELI 5

Unaweza ukawa na matendo maovu ambayo watu

wakasema haufai tena, hutakiwi tena kutubu. Unaweza

ukawa unafanya dhambi ya sirini na imekutesa huenda

hakuna mtu anayejua ikafika mahali mpaka ikakulevya.

Inawezekana Shetani anaachilia mashitaka kwenye nafsi

yako kwamba haufai tena huwezi tena kusimama, huwezi

tena kumtumikia Mungu. Yesu alishachukua udhaifu wako

wote, alibeba uovu wako wote, alishanyang’anya hati ya

mashitaka kwa Shetani akaigongomelea msalabani.

Haleluyaa! Anachokushitaki Shetani leo kuwa huwezi

kurudi tena kwa Mungu, huwezi kumtumikia Mungu.

Anachokwambia Shetani leo kuwa umefanya dhambi sana

haufai kabisa kuwa mototo wa Mungu, haufai hata

kumsogelea Mungu ni kwa sababu hujajua tu kuwa Yesu

alikufia msalabani. Moja ya kitu kilichomfanya Kristo afe

msalabani ilikuwa ni kunyang’anya hati ya mashitaka

ambayo Shetani anakushitaki leo.

Kama ni hivyo ni wakati wako sasa wa kusimama na

kumwambia Shetani asikushitaki tena rudi kumtumikia

Mungu amua kutubu (kugeuka). Umebeba kusudi la

Mungu, umebeba majibu ya vizazi vingi, usikubali

kukandamizwa na Shetani kifikra kuwa hauwezi kurudi kwa

Baba. Mungu anakutegemea sana kuujenga ufalme wake

ndio maana Shetani hataki urudi anajua utakuwa hasara

kwenye ufalme wake.

UHURU WA KWELI 6

Jiulize swali kwanini iwe hivi? Jiulize kwanini umtumikie

Shetani?

Mwambie Shetani asikutaabishe tena! Kwa sababu

alishapondwa kichwa na uzao wa mwanamke (Yesu Kristo

wa Nazareti). Kupitia huyo majuto hayapo tena,

kudharauliwa hakupo tena, hukumu haipo tena, mateso

hayapo tena. Swali kwanini iwe hivi? Yesu amelijibu

msalabani kuwa hakuna mzigo mzito usio sameheka kwake.

Kiri namna hiyo ili uweze kutoka mahali ulipo uanze kuishi

maisha ya ushindi na utakatifu. Kwa maana kwa moyo mtu

huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata

wokovu (Rum 10:10).

Fuatisha sala hii kwa Imani;

“Bwana Yesu asante kwa neema na upendo wako, wewe

uliyejifanya mwenye dhambi ili nipate haki. Wewe

uliyejifanya mwenye dhambi ili niwe mtakatifu, wewe

uliyedharaulika ukaaibika ili niheshimike, wewe uliyejifanya

maskini ili niwe tajiri.Wewe uliyekuwa dhaifu ili mimi

nitukuzwe najua unafahamu hali yangu mbaya

iliyonikamata. Baba nakutazama wewe ili unisaidie kutoka

kwenye vifungo hivi, nisaidie kutoka kwenye huu ulevi

(….taja tatizo lako unalotaka kutoka….). Asante Bwana Yesu

kwasababu kwa damu yako ulinisamehe pale msalabani.

UHURU WA KWELI 7

Kama katika kuchekwa na maumivu makali ulisamehe

naomba nisamehe pia. Nakiri kutembea kwa upya katika

maisha yangu na kuishi maisha ya ushindi. Asante

kwasababu umenifanya kuwa mmoja katika familia ya

Mungu Mtakatifu mwenye uweza wote.” Amen

Ukiwa umetamka sala hii umeshaingia kwenye familia ya

watakatifu (umeokoka). Nifuatilie kwenye email au namba

za simu zilizoko mwanzoni mwa kitabu kuna zawadi yako

nimekuandalia. Umebarikiwa sana.

Ulevi wa ugonjwa wa mwanamke aliyekuwa akitokwa

damu miaka kumi na miwili jinsi ulivyoponywa.

“Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda

wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali

zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu

yoyote, alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi

lake; mara hiyo kutokwa damu kwake kulikoma. Yesu

akasema, Ni nani aliyenigusa? Basi, watu wote walipokana,

Petro alimwambia, Bwana mkubwa, makutano haya

wanakuzunguka na kukusonga. Yesu akasema, Mtu

alinigusa, maana naona ya kuwa nguvu zimenitoka. Yule

mwanamke, alipoona ya kuwa hawezi kusitirika akaja

akitetemeka, akaanguka mbele yake, akamweleza mbele

ya watu wote sababu yake ya kumgusa, na jinsi

UHURU WA KWELI 8

alivyoponywa mara. Akamwambia Binti, imani yako

imekuponya; enenda zako na amani.” [Luk 8: 43-48]

Mama huyu aliyetokwa damu kwa miaka kumi na miwili,

alikuwa amedharauliwa na jamii kutokana na ugonjwa

wake, pia alikuwa ameugua ugonjwa ambao ulimtesa kiasi

cha kumlevya, hali hiyo ilimpelekea kuona ni sehemu ya

maisha yake. Katika jamii ya Waebrania ilikuwa ni

utamaduni, mtu aliyekuwa akitokwa damu alihesabiwa

kuwa ni najisi. Watu wa namna hii hawakuruhusiwa

kushiriki ibada wala maeneo yenye mikusanyiko kwahiyo

walikuwa wanatengwa kabisa. Mama huyu alikuwa

akitafuta msaada kwa waganga wa kienyeji, mali zake zote

ziliishia huko lakini ndani yake baada ya kuona hali yake

mbaya huenda alijiuliza moyoni mwake swali hili kwanini

iwe hivi? Nimetokwa damu mwaka wa kumi na mbili sasa,

mali zangu zote zimeishia kwa waganga wa kienyeji, jamii

yangu imenitenga. Huenda alilia kwa uchungu hali mbaya

anayoipitia, Kwanini iwe hivi? Akaazimia moyoni mwake

mimi nitakwenda kwa Yesu, nikashike upindo wa vazi lake

tu ili nipone.

Na alipokwenda kwa imani ulevi wake wote wa ugonjwa

uliomtesa miaka kumi na miwili ulimtoka. Najisikia

kumtukuza Mungu kwaajili ya hili, hakuna ulevi

unaoshindikana kwa Bwana. Ukimtwika fadhaa yako yeye

UHURU WA KWELI 9

anakubebe mzigo wake na kukupa nira yake iliyonyepesi

kuibeba (1Pet 5:7, Zab 55:22, Math 11:28-30) anaibadili

huzuni kuwa furaha kwenye maisha yako. Hakuna mzigo

usioweza kupumzishwa kwa Bwana, hakuna ulevi usioweza

kuachwa kwa Mungu aliye hai, upindo tu wa Yesu unaweza

kukusaidia kutoka kwenye hali mbaya iliyoshindikana

kwenye maisha yako. Ni zamu yako sasa jiandae kiri

umefunguliwa kupitia damu ya Mwanakondoo (Yesu Kristo)

msalabani.

Mwanamke mjane wa Serepta jinsi alivyopokea muujiza

wa kuzidishwa kiuchumi maradufu juu ya ulevi wa hali

yake mbaya ya kiuchumi.

“Basi, akaondoka, akaenda Sarepta, hata alipofika langoni

pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni;

akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo

chomboni nipate kunywa. Alipokuwa akienda kuleta,

akamwita akasema, niletee, nakuomba, kipande cha mkate

mkononi mwako. Naye akasema kama BWANA, Mungu

wako aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na

mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili

niingie nijipikie mimi na mwanangu, tuule tukafe. Eliya

akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye kama

ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate; kisha ujifanyie

nafsi yako na mwanao. Kwa kuwa BWANA, Mungu wa

UHURU WA KWELI 10

Israeli, asema hivi, Lile pipa la unga halitapunguka, wala ile

chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile BWANA

atakapoleta mvua juu ya nchi. Basi akaenda, akafanya

kama alivyosema Eliya; nayeye mwenyewe, na Eliya, na

nyumba yake, wakala siku nyingi. Lile pipa la maji

halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawa

sawa na neno la BWANA alilonena kwa kinywa cha Eliya”

[1Falme 17: 10-16]

Mwanamke mjane alikuwa amekata tamaa na hali yake

mbaya ya uchumi kiasi cha kumlevya. Unajua kwenye

ufahamu wake alikuwa anawaza kufa tu! Hakuona tena

ladha ya kuendelea kuishi kwa sababu ya hali yake mbaya

ya kiuchumi. Huenda alijiuliza swali juu ya hali yake mbaya

ya kiuchumi, kwanini iwe hivi? Akaamua kufanya maamuzi

ya kusubiri kifo kutokana na hali yake ya uchumi iliyokuwa

mbaya mno.

Mtumishi wa Mungu Eliya alimwambia ukanifanyie kwanza

mkate, unajua nini Mungu alikuwa anatafuta kwa yule

mwanamke? Ni imani, ili amwezeshe kutoka kwenye hali

yake mbaya ya kiuchumi. Yule mwanamke pamoja na hali

yake mbaya alienda mbele ya mtumishi wa Mungu Eliya

huku akiwa amemfanyia mkate. Akasema, nitaenda hivi hivi

na hali yangu mbaya ya kiuchumi na Bwana, Mungu

akamzidisha maradufu. Hata sasa hakuna linaloshindikana

kwa Bwana, Mungu anakusubiri wewe uende kama ulivyo

UHURU WA KWELI 11

wewe muamini tu ili akufanye kuwa mpya na kubadilisha

historia ya maisha yako leo.

Ayubu alipoondokewa na mifugo yake, watumishi wake

na binti zake. Mke wake alipomsaliti na kuumwa ugonjwa

wa majipu. Baadaye kubarikiwa kwa baraka zaidi ya

mwanzo.

“Ilitukia siku moja hao wanawe na binti zake walipokuwa

wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao

mkubwa, mjumbe akamfikilia Ayubu na kumwambia, Hao

ng'ombe walikuwa wakilima, na punda walikuwa wakilisha

karibu nao; mara Waseba wakawashambulia,

wakawachukua wakaenda nao; naam, wamewaua hao

watumishi kwa makali ya upanga, mimi peke yangu

nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Huyo alipokuwa akali

akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Moto wa

Mungu umeanguka kutoka mbinguni na kuwateketeza

kondoo, na wale watumishi, na kuwaangamiza; mimi peke

yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Huyo

alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na

kusema, Wakaldayo walifanya vikosi vitatu,

wakawaangukia ngamia, wakaenda nao, naam,

wamewaua wale watumishi kwa makali ya upanga; mimi

peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Huyo

alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na

UHURU WA KWELI 12

kusema, Wanao na binti zako walikuwa wakila na kunywa

divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa; mara, tazama,

upepo wenye nguvu ukatoka pande za jangwani, ukaipiga

hiyo nyumba pembe zake nne, nayo ikawaangukia hao

vijana, nao wamekufa; na mimi peke yangu nimepona,

mimi tu, kukuletea habari. Ndipo Ayubu akainuka,

akalirarua joho lake, kisha akanyoa kichwa chake, na

kuanguka chini, na kusujudia; akasema, Mimi nilitoka

tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena

huko uchi vilevile; Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; jina

la Bwana na libarikiwe. Katika mambo hayo yote Ayubu

hakufanya dhambi, wala hakumwazia Mungu kwa

upumbavu. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana,

akampiga Ayubu na majipu mabaya tangu wayo wa mguu

hata utosi wa kichwa. Naye akashika kigae cha kujikunia;

akaketi majivuni. Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe

hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru

Mungu, ukafe. Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena

kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je!

Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na

mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya

dhambi kwa midomo yake.” [Ayu 1:13-22, 2:7-10]

Ayubu aliondokewa wafanya kazi wake, wanyama wake,

binti zake, kupigwa ugonjwa wa majipu. Ugonjwa wa Ayubu

ulimfanya ajikune kutoka uwayo wa miguu yake mpaka

utosini kiasi cha kumlevya. Mke wake alimshauri amwache

UHURU WA KWELI 13

Mungu na kumkufuru ili afe lakini Ayubu hakuwa tayari.

Baadae mke wake akamkimbia, lakini alisimamia imani yake

kwa Bwana. Kwa siku moja alitokewa na matatizo magumu

sana, lakini alitamka neno moja tu kwa ujasiri. “Bwana

alitoa na Bwana ametwaa jina la Bwana libarikiwe”. Hii ni

kwa sababu Ayubu alimtumaini Bwana hakuangalia hali

ngumu aliyopitia. Huenda alijisemea kwanini iwe hivi?

Lakini alipomtazama Bwana akaona faraja na baraka

kwenye maisha yake. Kwa sababu Ayubu alijua yote

yanayoonekana nje kwa mwilini hata yakipotea bado

yanaweza kurejea maradufu. Ayubu alijua baraka zake halisi

zinapatikana ndani yake ndio maana alimtumaini Bwana.

Na baadaye maandiko yanasema;

“Basi hivyo Bwana akaubarikia huo mwisho wa Ayubu zaidi

ya mwanzo wake; naye alikuwa na kondoo kumi na nne

elfu, na ngamia elfu sita, na jozi za ng'ombe elfu, na punda

wake elfu. Tena alikuwa na wana waume saba, na binti

watatu” [Ayu 42:12-13]

Pamoja na hali mbaya aliyokuwa nayo Ayubu hakumkufuru

Mungu alimtumaini Mungu na Mungu akambariki Ayubu

katika mwisho wake na mwisho wake ukawa wa baraka

kuliko mwanzo.

UHURU WA KWELI 14

Stephano aliyepigwa mawe mpaka kufa

“Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala

masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba

zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo. Ni yupi katika

manabii ambaye baba zenu hawakumwudhi? Nao

waliwaua wale waliotabiri habari za kuja kwake yule

Mwenye Haki; ambaye ninyi sasa mmekuwa wasaliti wake,

mkamwua; ninyi mlioipokea torati kwa agizo la malaika

msiishike. Basi waliposikia maneno haya, wakachomwa

mioyo, wakamsagia meno. Lakini yeye akijaa Roho

Mtakatifu, akakaza macho yake, akitazama mbinguni,

akauona utukufu wa Mungu, na Yesu akisimama upande

wa mkono wa kuume wa Mungu. Akasema, Tazama! Naona

mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama

mkono wa kuume wa Mungu. Wakapiga kelele kwa sauti

kuu, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja,

wakamtoa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao

mashahidi wakaweka nguo zao miguuni pa kijana mmoja

aliyeitwa Sauli. Wakampiga kwa mawe Stefano, naye

akiomba, akisema, Bwana Yesu, pokea roho yangu. Akapiga

magoti, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi

hii. Akiisha kusema haya akalala. Na Sauli alikuwa akiona

vema kwa kuuawa kwake.” [Mate 7:51-60]

UHURU WA KWELI 15

Katika eneo hili hatuoni Stephano akiwaombea laana

waliompiga kwa mawe. Tena hatuoni akielekeza macho

yake kwa wale waliokuwa wakimpiga kwa mawe. Katikati ya

maumivu makali Stephano alisamehe na kusema. “Tazama

naona mbingu zimefunguka na mwana wa Adamu

amesimama mkono wa kuume wa Mungu”. Kwa sababu

Stephano alijua tumaini lake liko mikononi mwa Mungu,

huenda Stephano alisema kwanini iwe hivi? Lakini Stephano

alikua yuko mtetezi wangu Yesu Kristo. Na Yesu yupo tayari

hata katika magumu unayopitia kukuvusha na

kukustahilisha, kukufanya kuwa mtakatifu na mwenye haki.

Yesu amponya mtu aliyekuwa na udhaifu wa kupooza

miaka thelathini na nane.

“Baada ya hayo palikuwa na sikukuu ya Wayahudi; naye

Yesu akakwea kwenda Yerusalemu. Na huko Yerusalemu

penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa

Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao matano. Ndani ya

hayo jamii kubwa ya wagonjwa walikuwa wamelala,

vipofu, viwete, nao waliopooza, [wakingoja maji yachemke.

Kwa maana kuna wakati ambapo malaika hushuka,

akaingia katika ile birika, akayatibua maji. Basi yeye

aliyeingia wa kwanza baada ya maji kutibuliwa, akapona

ugonjwa wote uliokuwa umempata. Na hapa palikuwa na

mtu, ambaye amekuwa hawezi muda wa miaka thelathini

UHURU WA KWELI 16

na minane. Yesu alipomwona huyu amelala, naye akijua ya

kuwa amekuwa hali hiyo siku nyingi, alimwambia, Wataka

kuwa mzima? Yule mgonjwa akamjibu, Bwana, mimi sina

mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa; ila wakati

ninapokuja mimi, mtu mwingine hushuka mbele yangu.

Yesu akamwambia, Simama, jitwike godoro lako, uende.

Mara yule mtu akawa mzima, akajitwika godoro lake,

akaenda. Nayo ilikuwa ni sabato siku hiyo.” [Yoh 5:1-9]

Huyu kiwete alikuwa amekaa birikani kwa mda wa miaka

thelathini na nane, ni rahisi sana kukata tamaa. Unaweza

ukawa na tatizo lakini huenda hujawahi kabisa kusubiri kwa

mda mrefu namna hii kama huyu mgonjwa. Huenda aliona

yeye ndio dunia nzima inamuonea, huenda alijiuliza swali

juu ya ugonjwa wake kwanini iwe hivi? Lakini alipokutana

na Mkuu Yesu Kristo alimwambia sina mtu wa kunitia

birikani, kwa sababu kuna watu hutangulia mbele yangu na

kuponywa. Fikiria ni kwa kiasi gani alikuwa ameathirika,

lakini Yesu alimwambia simama jitwike godoro lako uende,

na yule mtu akaponywa siku ile. Inawezekana kabisa

nawewe kunaeneo unaona giza ni tatizo la mda mrefu sana

na inawezekana umewategemea watu wakusaidie lakini

haijawezekana. Inawezekana umekuwa na matumaini

kuwa kiko kitu kitakusaidia kuvuka hapo lakini ni kwa mda

mrefu sasa haijawezekana. Yesu anasema huruma zake

UHURU WA KWELI 17

hazikomi yeye anampa kila mwenye kiu chemichemi ya maji

ya uzima wa milele bure. Kwa hiyo, ukimuamini na

kumwabudu yote yatakuwa yako (Luk 4:7, Ufu 21:6, 22:1,

22:17).

UHURU WA KWELI 18

Tathmini kupitia maswali kutoka katika Sura ya Kwanza

1: Kutokana na sura hii ulevi ni nini?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

2: Kwanini Yuda hakupaswa kujinyonga?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

………………………………………………………………………………

3: Namna gani ya kutoka kwenye ulevi wa aina zifuatazo?

(i)Ulevi wa ugonjwa uliokaa mda mrefu

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

(ii)Ulevi wa kupoteza mali, fedha na watu uliowapenda

UHURU WA KWELI 19

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

(iii)Ulevi wa kukataliwa na kupingwa katika

kazi/huduma/karama/kipawa ulichopewa na Mungu

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………...

(iv)Ulevi wa kudharauliwa na kukataliwa na jamii yako

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

UHURU WA KWELI 20

UHURU WA KWELI 21

SURA YA PILI

KWANINI NIUISHI UKALE

kale ni kawaida ya kuishi katika desturi, mila, mapokeo

au hali ya uzamani katika mazingira yaliyobadilika au

kuboreshwa zaidi. Ni kuishi kwenye mazoea ya hali ya ulevi

wa dhambi, kufeli, hali ngumu ya maisha. Nataka nikuulize

hili swali la msingi wewe uliyeshika kitabu hiki na kukisoma

tena kwa maandishi ya wino mzito, kwanini uishi ukale?

Unafikiri kwanini unaona huwezi kutoka kwenye shida uliyo

nayo? Kwanini unakaa kwenye ulevi wa kutojibiwa haja

yako kwa mda mrefu?

Inawezekana unaona umekufuru (umemkufuru

Mungu)

Inawezekana unakiri umeharibikiwa. Kwa hiyo,

huwezi kufanikiwa

Inawezekana unashuhudiwa huwezi kusamehewa

Inawezekana unashitakiwa ndani yako

(kuhukumiwa)

Kama nilivyo kuuliza swali kwa maandishi ya wino mzito

nataka nikujibu swali kwa maandishi ya wino mzito kuwa

inawezekana kuishi upya! Kutokea kwenye;

U

UHURU WA KWELI 22

Utimilifu wa kazi ya msalaba wa Kristo

Wingi wa neema ya Kristo

Upendo wa Kristo

Utimilifu wa kazi ya msalaba wa Kristo.

Ili kufikia kiwango cha utimilifu unaoutaka kwenye maisha

yako lazima uamini utimilifu wa kazi ya msalaba wa Kristo.

Jitihada za kutoka kwenye ulevi mbaya wa kiuchumi,

magonjwa, uzinzi, kukataliwa, kudharauliwa zinatakiwa

kujengwa kwenye msingi wa utimilifu wa kazi aliyoifanya

Kristo msalabani. Lifahamu jambo hili kuwa Kristo alijitahidi

kuitimiza sheria yote ili utoke katika hali ya utumwa wa

laana ya sheria na wa ulevi wa kila aina ambao Shetani

ameendelea kukushitaki kuwa huwezi kutoka. Shetani

anajua Kristo alichokifanya msalabani ndio maana anataka

kukukandamiza kifikra ili usiweze kutoka katika hali mbaya

uliyo nayo. Shetani alishabaki kuwa ni mshitaki wetu,

maandiko yanasema hivi;

“Mwe na kiasi na kukeshsa; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi,

kama simba aungurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta

mtu ammeze” [1Pet 5:8]

Shetani hawezi kuja kukusifia kwa jambo lolote jema

ulilofanya ndio maana ukifanya dhambi au kosa

UHURU WA KWELI 23

anakukandamiza zaidi na kukuwekea mzigo mzito moyoni

mwako. Kusudi lake ni kukumeza ili usiweze kusogea mbele

za Bwana wala kurejea kwa Bwana Yesu. Lengo la Shetani

kukukandamiza ufahamu sio ili urudi kwa Bwana lengo lake

uendelee kukaa kwenye hali ya dhambi uliyonayo ndio

maana ukikosea utaona ndani yako anaanza kukuhukumu.

Mfano;

Ukikosea utasikia wewe ni Mkristo wa namna gani

anafanya hivi na anaenda kanisani?

Wewe ni mtu wa namna gani? Yaani unajiita umeokoka

na unafanya hivi?

Ivi wewe ni mtumishi wa Mungu kweli?

Na hii ndio sababu kubwa ndani yako unaona umemkufuru

Mungu, unakiri umeharibikiwa, unashuhudiwa huwezi

kusamehewa, unashitakiwa umehukumiwa. Mpendwa

unatakiwa kujua Shetani anapigana vita zake kwa akili

sana, hakuna vita ngumu kama Shetani akiamua

kukugandamiza kiufahamu. Hasa katika Vita ya kutoka

kwenye hali mbaya/ulevi wa aina yoyote.

Ni lazima tujue namna ambavyo tunaweza kushinda nguvu

ya mashitaka ya Shetani kwenye maisha yetu kwa

kuendelea kutenda kwa haki kama vile Mungu

alivyotufanya wenye haki katika Yesu Kristo ili tuishi katika

haki yake. Ni mapenzi ya Mungu tuishi maisha ya utakatifu,

UHURU WA KWELI 24

ni mapenzi ya Mungu tuishi maisha yenye baraka na

mafanikio. Kwa kuwa tunaishi katika mwili yako makosa

huwa yanayotokea kwenye maisha yetu. Tatizo kubwa

linakuja ni pale ambapo umekosea na kushindwa kutoka

kwenye makosa/dhambi.

Ndio maana utaona kuna watumishi wa Mungu wengi

waliacha utumishi, kuna wengine walikuwa wanamcha

Mungu na wameokoka waliacha imani (wokovu). Kwa

sababu ya mashitaka ya Shetani juu ya yale waliyoyafanya.

Shetani utaona mara nyingi anawasemesha kwenye

fahamu zao kuwa huwezi kuendelea kumtumikia

Mungu/kumwabudu Mungu ni bora uache kumtumikia

Mungu. Vita ya namna hii huwezi kuishinda tu kwa kufanya

maombi ya kuvunja mapepo na majini ama mizimu,

pamoja na kufanya maombi ya mfungo nilazima utumie

silaha inayozidi silaha anayoitumia Shetani ili kumshinda.

Ndio maana Paulo aliwaambia Wakorintho hivi;

“Maana ingawa tunaenenda kwa jinsi ya mwili, hatufanyi

vita kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za

mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha

ngome) tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka,

kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila

fikra ipate kumtii Kristo” [2Kor 10:3-5]

Paulo alisisitiza sana kuwa pamoja na kwamba tunaenda

kwa jinsi ya mwili, vita zetu hazifanyiki kwa jinsi ya mwili

UHURU WA KWELI 25

yaani jitihada, juhudi za kimwili kutoka kwenye ulevi wa

aina yoyote. Nahimizwa na Roho Mtakatifu nirudie

kukuandikia mstari huu; {tukiangusha kila mawazo na kila

kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu} kazi ya

Shetani ambayo anaifanya kwa kasi kubwa, na imepoteza

wengi kwenye ulimwengu huu wa sasa wa kumuabudu

Mungu ni kuinua ufahamu kandamizi wenye mlengo wa

kupinga kazi kubwa aliyoifanya Mkuu Yesu Kristo

Msalabani.

(Namshukuru Mungu, Roho Mtakatifu kwasababu kitabu

hiki kimekufikia mkononi mwako, kupitia ufunuo huu

uwekwe huru, kifikra na kuishi maisha ya utakatifu, ustawi,

kuinuliwa na ushindi daima). Tunaweza kushinda vita hii ya

kupinga na fikra za Ibilisi kwa kuamini kazi kamilifu ya

msalaba aliyoifanya Kristo, hii itapelekea kuwa na mambo

yafuatayo:-

Kuwa na imani sahihi

Kuondokana na hukumu/hatia ya Shetani

Nguvu ya fikra chanya

Kuwa huru

Ili tuweze kuamini kazi kamilifu ya msalaba ni lazima tujue

yafuatayo:-

Msalaba ulikuwa na kazi gani

Aliyeubeba msalaba ni nani

UHURU WA KWELI 26

Kwanini Mungu alitumia njia ya msalaba tu ili

kumponda Shetani kichwa

Kwanini zilihitajika juhudi za Yesu kuikamilisha kazi ya

msalaba

Msalaba ulikuwa na kazi gani?

Napenda ufahamu kuwa msalaba kazi yake ilikuwa ni

kumkamilisha mwanadamu, kutoka agano la kale kuingia

agano jipya ambalo maandiko yanashuhudia kuwa ni agano

imara. Mwanadamu ambaye alikuwa anaonekana kwenye

agano la kale ni muasi, mwenye dhambi, mwenye laana,

asiye na haki, Kupitia Msalaba wa Kristo Yesu akamilishwe

na kuingizwa agano jipya kuwa mwanadamu mtakatifu,

mwenye baraka na mwenye haki, aliyetukuzwa asiye na

mawaa wala hatia (Rum 5:12-21, 8:29-30 Efe 1:3-6). Ni kwa

kazi ya msalaba tu! Mwanadamu anaweza kuwa mtakatifu,

mwenye baraka na haki ya Mungu. Natamani uelewe hili

kwa msisitizo wa Roho Mtakatifu kuwa,

Ukiingizwa kwenye agano jipya ni agano lilio bora zaidi,

kujisimamisha katikati ya maagano mawili (agano la kale

na agano jipya) matokeo yake ni kuwa na imani isiyo sahihi.

UHURU WA KWELI 27

Kuna wakati fulani ukiwauliza Wakristo tabia za Mungu ni

zipi, kumetokea mtafaruko mkubwa kwa Wakristo kujibu

tabia za Mungu kwa maoni tofauti tofauti. Utakuta

wengine wanakwambia Mungu anaghadhabu sana,

wengine wanasema anahuruma sana, wengine wanasema

kuna dhambi ukifanya hauwezi kusamehewa kabisa na

kutengwa na Mungu, kuna wengine wanasema hakuna

dhambi isiyosameheka.

Naomba leo ujue hili wazi kwamba Wakristo wengi

wanachanganya tabia halisi za Mungu kwa sababu hawajui

tabia halisi za Kristo. Kristo alikuja kuanzisha agano jipya,

kazi yake timilifu inapatikana kwenye utimilifu wa kazi ya

msalaba. Kupitia kazi hiyo utamfahamu Mungu jinsi alivyo

kwa sababu Yesu alisema; Mimi ndimi njia, na kweli, na

uzima mtu haji kwa Baba ila njia ya mimi (Yoh 14:6). Ukiwa

ni Mkristo unayesoma kitabu hiki naandika kwa maandishi

ya wino mzito kuwa “Ili ufahamu tabia za Mungu ni lazima

ufahamu tabia za Yesu Kristo”

Kristo alikuja kufunua tabia halisi za Mungu akiwa duniani.

Biblia inashuhudia kuwa yaliyokuwa yakifanyika agano la

kale ilikuwa ni kivuli cha mambo yanayokuja yaani

kuundwa kwa mfumo mpya (agano jipya). Maana yake

tunatakiwa kutembea katika mfumo mpya/agano jipya.

Utasikia mtu anakiri ameokoka lakini mtu huyo mwisho wa

siku ataka kutembea na mfumo wa sheria za agano la kale.

UHURU WA KWELI 28

Agano jipya ni kama mkataba mpya japokuwa agano jipya

la Kristo ni zaidi ya mkataba kwakuwa halina mwisho

tutatembea nalo mpaka mwisho wa ulimwengu huu (ni

agano la milele).

Mkataba wowote unaposainiwa huwa na kanuni za

kuufuata. Inawezekana wanaohusika ni watu wale wale

waliokuwa na mkataba wa mwanzo. Mkataba mpya

ukisainiwa ujue kuna mambo mapya yanawekwa na

tunatakiwa kutembea na mkataba huo. Kristo kufa

msalabani na kumwaga damu yake ilikuwa ni ishara ya

kuingia kwenye agano jipya ndio maana Paulo aliwaambia

Waebrania kuwa;

“Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza

kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na

kuchakaa ki karibu na kutoweka” [Ebr 8:13]

Na kupitia damu ya Yesu Kristo tuliingizwa ndani ya agano

jipya kwa sababu hakuna agano pasipo kumwaga damu.

Kupitia damu ya Yesu Kristo tuliingizwa kwenye agano jipya

lililobora (Ebr 9:22-28)

Kama tuko kwenye agano jipya la Kristo uwe na uhakika

kuna mambo yamebadilika. Biblia inashuhudia kwamba

agano jipya limelifanya lile agano la kwanza (agano la kale)

kuwa kukukuu na kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki

karibu na kutoweka. Sisi kama tuliookoka (Tulio ndani

UHURU WA KWELI 29

Kristo) yaani ndani ya agano jipya la Kristo lazima kuna

namna mpya ya kutembea nalo. Huwezi ukawa

umeanzisha mkataba mpya wenye namna mpya za

kutembea nazo wakati huo huo unataka kufuata kanuni za

zamani.

Mfano katika mkataba wa kwanza wa biashara katika

kampuni uliyoajiriwa uliokuwa nao ulikuwa unatakiwa

kutoa dola mia kila mwaka na kulipa dola kumi kila mwezi

ili kukamilisha miadi ya biashara mliyoweka na muajiri

wako. Inatokea kila mwezi unaotakiwa kurejesha dola kumi

kiwango chako cha kufanya marejesho hakifikii dola kumi

kwa mwezi. Wakati fulani unawasilisha dola 2, wakati

mwingine dola 1 wakati mwingine unashindwa kabisa

kuwasilisha marejesho ya dola katika kampuni. Inapofikia

wakati wa mwisho wa mwaka katika dola mia moja

unawasilisha dola saba tu katika kampuni.

Wakati mwingine miaka mingine hakuna marejesho yoyote

ya dola katika biashara. Muajiri wako anaamua kuweka

mkataba mpya na wewe na kukwambia deni lote la nyuma

nimekulipia nataka tuanzishe mkataba mpya na wewe.

Sasa hautalipia gharama yoyote ile ili kupata hisa

unazozihitaji kazi yako itakuwa ni kupanua mipaka ya

biashara na badala yake kampuni itawajibika kukulipa dola

mia kila mwezi na dola elfu moja kwa kazi tu ya kupanua

mipaka ya biashara ya kampuni. Hii ni ajabu sana! Hii ni

UHURU WA KWELI 30

habari njema! Lakini jambo la ajabu sana ni kwamba wewe

unataka uendelee na mkataba ule ule uliopita unataka

ulipie deni ambalo huwezi kulilipa na pia uendelee kufanya

marejesho kwenye kampuni badala ya ya wewe kulipwa na

kampuni.

Hivi ndivyo walivyo Wakristo wa sasa inasikitisha sana!

Yesu alipoangikwa msalabani alitangaza kuwekwa huru na

dhambi zetu zote na kulipa deni yote ya dhambi tuliyokuwa

tunadaiwa, akatufutia makosa yote na kila uovu. Kristo

alitutoa katika hali ya utumwa ya kulipa gharama ya

makosa yetu tunayofanya na kutufanya kuwa wafalme,

makuhani, matajiri. Lakini bado wewe unataka kulipa

gharama ya deni ambalo kwanza hukuweza kulilipa

mwanzo na bado unang’ang’ania kukaa kwenye utumwa

wa dhambi.

Inasikitisha sana, fikiri kama ni wewe uko kwenye nafasi ya

Yesu ni namna gani ungekuwa unajisikia. Naamini kati ya

mambo ambayo yanahuzunisha sana ni watu kuishi ndani

ya utumwa wakati kiuhalisia ni wafalme na kulipa gharama

ya dhambi, makosa na uovu wakati yalishalipiwa.

Hatutakiwi kabisa kuishi maisha waliyokuwa nayo agano la

kale maana sisi tumefanyika kuwa agano liliobora zaidi ya

agano lile la kwanza. Kwa Imeandikwa hivi;

UHURU WA KWELI 31

“basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano

lililo bora zaidi” [Ebr 7:22]

Agano alilolifanya Mungu kupitia Yesu Kristo ni bora kuliko

agano la kwanza (agano la kale). Kama sio bora huu mstari

usingeandikwa kwenye biblia kama vile ambavyo yako

mambo mengi yaliyotendeka na Yesu Kristo, mitume na

manabii na hayakuandikwa. Roho Mtakatifu kuuruhusu

huu mstari kupitia mtume wake Paulo kuuandika ni kwa

sababu alijua una matokeo makubwa.

Aliyebeba msalaba ni nani?

Kabla sijakwambia aliyebeba msalaba ni nani nataka ujue

maana ya msalaba.

Msalaba ni kujikana, kujikataa kujikinai.

“Akawaambia watu wote, Mtu ye yote atakaye kunifuata

na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku

anifuate” [Luk 9:23]

Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake kila mtu

abebe msalaba wake kwakuwa Yesu alikuwa hajafa bado

msalabani. Kwa lugha nyepesi walikuwa hawana uwezo wa

kuokoka. Lakini Petro alikuja kusema tumtwike Yeye (Yesu

UHURU WA KWELI 32

Kristo) fadhaa zenu zote maana hujishughulisha sana kwa

mambo yenu (2Pet 5:7).

Kwakuwa Kristo alikuwa alishateswa msalabani watu wote

walikuwa na uwezo wa kumtwika Kristo fadhaa zao zote.

Kwa maana rahisi kujikana ni kujikataa, Kristo alikufa

msalabani ili tusiendelee kukaa katika hali ya kukataliwa,

alikataliwa, alijikinai na kujikana Yeye ili mimi na wewe

tukubalike. Tusibebe laana yoyote wala aina yoyote ya

mateso.

Msalaba ni upatanisho

Msalaba huo unamstari wa ulalo na wima. Mstari wa ulalo

unaonyesha upatanisho kati ya watu na watu. Mstari wa

wima unaonyesha upatanisho kati ya wanadamu na

Mungu. Kristo alitupatanisha kwa njia ya msalaba.

Aliyebeba msalaba ni nani?

Aliyebeba msalaba ni Kristo. Wote tulioungwa na Kristo

hatutakiwi kubeba matatizo yetu, hata hivyo hatukuweza.

UHURU WA KWELI 33

Tunatakiwa tumbebeshe Kristo kwa sababu Yeye aliweza

kubeba matatizo yetu. Usijibebeshe matatizo yako kwa

sababu huwezi mtwike Kristo kwa sababu Yeye anaweza

kubeba ulevi wa uzinzi, wizi, hali mbaya ya uchumi, na kila

aina ya ulevi Yeye anaweza kubeba. Hakuna mwanadamu

anayeweza kushinda dhambi kwa nguvu zake, hakuna

mwanadamu anayeweza kushika sheria asivunje hata

moja. Kuishi kwa sheria ni kuishi chini ya laana huwezi

kuishi chini ya sheria ukabarikiwa vivyo hivyo huwezi kuishi

katika Kristo ukalaaniwa (Gal 3:13).

Dhambi hupata nguvu unapoamua kuishi kwa sheria,

Shetani ni furaha yake kukuona unaishi kwa sheria kwa

sababu mara zote hutumia sheria kukushitaki kuwa

umekosea na haufai kuendelea kuwa na uhusiano na

Mungu. Naomba uelewe sheria sio tu amri kumi za Mungu

sheria ni mfumo wa kanuni ambao mtu amejiwekea

zinazomuwekea kuishi kwa kiwango fulani ili kuweza

kufikia utakatifu, kukubalika mbele za Mungu au katika

mafanikio yoyote yale.

Kwa mfano unaweza kujiwekea mfumo wa maisha

kwamba ili nifanikiwe nilazima nifanye jambo fulani.

Kuweka kanuni fulani, mipango au mfumo wa kufuata ili

ufanikiwe ni jambo jema. Lakini hatutakiwi kuamini

kufanikiwa kupitia kanuni, mipango au mifumo ya maisha

tunayoishi. Kwa sababu kwa kufanya hivyo tutamzuia

UHURU WA KWELI 34

Mungu kufanya zaidi ya uwezo tulio nao. Haki ambayo ni

kibali cha mtu kusimama mbele za Mungu inaweza kuja

kwa matendo ya sheria lakini pia inaweza kuja kwa njia ya

Yesu Kristo, lakini biblia inatuhakikishia haki ya Kristo ni

bora zaidi kuliko haki zetu za matendo ya sheria (matendo

mema). Tunahesabiwa haki ya Mungu kwa njia ya imani

iliyo katika Kristo Yesu.

Yaani haki ya matendo ya sheria maana yake unapata kibali

cha kupokea vitu vya Mungu kwa sababu ya juhudi ya

kuishika sheria. Haki hii kuna vitu itakuzuia usivipate

kwenye maisha yako ndio maana Kristo alisema;

“Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo

haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe

katika ufalme wa mbinguni” [Math 5:20]

Yesu alikuwa anamaanisha kwamba ipo haki iliyozidi haki

ya waandishi na mafarisayo ambayo ni bora zaidi kuliko ya

waandishi na mafarisayo. Angalia aina ya haki waliyokuwa

nayo mafarisayo na waandishi ilikuwa ni haki ya matendo

ya sheria. Yaani kufunga mara mbili kwa juma, kuomba

kutoa zaka, kuwasaidia wahitaji nk. Mambo haya

niliyoyataja ni mambo mema sana na tunatakiwa

kuyafanya.

Tatizo wengi wanayofanya haya, wanafanya kama sheria

na sio kwa moyo wa kupenda. Yaani wanafanya

UHURU WA KWELI 35

wakitegemea malipo kutoka kwa Mungu kwa matendo yao

na wanayaishi hayo kwa imani wakitegemea kuwa

watakuwa watakatifu au watafanikiwa kwa sababu ya hayo

wanayoyafanya. Ndio maana waandishi na mafarisayo

walikuwa wanajivunia haki ya matendo yao ya sheria

wakasahau yupo Yesu anayeweza kuwakamilisha zaidi

kupata haki iliyo bora zaidi ya haki ya matendo yao ya

sheria. Ndio maana Yesu alitoa mfano huu;

“Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja

Farisayo, wapili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama

akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa

kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang’anyi,

wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi

nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato

yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali,

wala hakuthubutu kuinua macho yake mbinguni, bali

alijipiga piga kifua akisema, Ee Mungu uniwie radhi mimi

mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda

nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa

maana kila ajikwezaye atadhiliwa, na ajidhiliye

atakwezwa” [Luk 18:10-14]

Kumbe haki yetu inatakiwa izidi haki ya mafarisayo ambayo

ni ya matendo ya sheria.Fanya jambo jema katika maisha

yako na kuliishi lakini hiyo utambue kuwa sio sababu

inayokufanya kuwa mtakatifu sana,kufanikiwa, wala

UHURU WA KWELI 36

kuhesabiwa haki mbele za Mungu. Mungu anataka uamini

kufanikiwa katika Kristo Yesu zaidi ya kila jambo jema

unalolifanya.

Haki tunayotakiwa kuwa nayo inatakiwa izidi haki ya

mafarisayo ya matendo ya sheria ambayo hupatikana

kupitia Kristo Yesu.

Ndio maana Yesu aliendelea kuwaambia watu mmesikia

watu wa kale walivyoambiwa, usiue, na mtu akiua

itampasa hukumu. Bali mimi nawaambieni, kila

amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu

akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu

akimwapiza, itampasa jehanum ya moto. Maana yake Yesu

aliitimiliza sheria jinsi ilivyotakiwa kuwa na kuwaeleza

kuwa bila Yeye (Yesu Kristo) mtu hawezi kuitimiza sheria

inavyopaswa. Kwa sababu katika yeye kuna ukamilifu wa

sheria yaani Yeye ni kilele cha sheria ndio maana

tunatakiwa kuishi katika yeye (Yesu Kristo).

Kwa sababu sheria inakikomo, inakiwango chake cha

mwisho, juhudi au uwezo binafsi wa mwanadamu kumtii

Mungu unakikomo chake. Ndio maana maandiko

yanasema;

“Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye

ahesabiwe haki” [Rum 10:4]

UHURU WA KWELI 37

Maana yake tunahesabiwa haki iliyobora zaidi ya Kristo

Yesu kwa njia ya imani. Ukimuamini Kristo unahesabiwa

haki, haki hii haitokani na matendo ya sheria haki hii

inatokana na Mkuu Yesu Kristo. Kwakuwa Kristo aliitimiza

sheria yote pale msalabani ili usiishi tena ndani ya laana ya

dhambi, kukataliwa na mateso.

Kwanini Mungu alitumia njia ya Msalaba tu kumponda

Shetani kichwa?

Nikukumbushe habari hii kabla ya Yesu kuanza kuteswa

alipokuwa bustani ya Gethsemane, akawaambia wanafunzi

wake, Roho yangu inahuzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni

hapa mkeshe pamoja nami, alipoanguka kifulifuli, akaomba

akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee

kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako

yatendeke (Luk 22:40-42).

Maana yake ilikuwa ni mapenzi ya Mungu, Yesu Kristo kufa

msalabani. Kwenye mapenzi ya Mungu kuna ukamilifu,

ndio maana Yesu alisema sio kila aniambiaye Bwana,

Bwana atakayeingia katika ufalme wa mbinguni. Maana

yake mapenzi ya Mungu ni ukamilifu. Mungu alimtoa Yesu

kufa msalabani kwaajili ya kututoa kwenye laana na mizigo

ya dhambi, kila aina ya ulevi na kutuondoa kwenye laana

ya sheria. Nguvu ya dhambi ilikuwa ni sheria ndio maana

UHURU WA KWELI 38

Mungu aliamua kumwondoa mwanadamu kwenye huo

mfumo na kumwacha aishi tu kupitia Mwanawe mpendwa

Kristo Yesu. Ndio maana imeandikwa hivi;

“maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila

akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote” [Yak

2:10]

Sheria nguvu yake ilikuwa katika kukosea. Ikitokea

umekosea katika neno moja wema wote ulikuwa

unabatilika kuwa ubaya. Na huu ndio mfumo ambao

Shetani aliupenda kuuishi na ndio maana ukikosea anaanza

kukushitaki ndani yako. Ashukuriwe Mungu kwa sababu

alituondoa kwenye laana ya mashitaka ya Shetani kupitia

Kristo Yesu. Roho Mtakatifu alikuja kutushuhudia sheria

yake katika Kristo Yesu ambayo ndiyo inayotuweka huru

mbali na sheria ya dhambi na mauti na kutufanya kuwa

watakatifu kwa neema yake(Rum 8:2, Tit 2:11-12).

Tangu mwanzo wa kuumbwa kwa ulimwengu ilikuwa ni

mpango wa Mungu tuishi katika Kristo Yesu.

Katikati ya bustani ya Edeni kulikuwa na mti wa ujuzi wa

mema na mabaya pamoja na mti wa uzima. Mungu

alimkataza Adamu kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema

na mabaya ambao ulikuwa ni ishara ya matendo ya sheria

(Mwanz 2:17). Mungu alitaka mwanadamu aishi tu kupitia

mti wa uzima ambao ilikuwa ni picha ya Yesu Kristo. Ndio

UHURU WA KWELI 39

maana Mungu aliwazuia wasiiendee njia ya matunda ya

mti wa uzima (Kristo).

Mwanadamu alipokula matunda ya mti wa ujuzi wa mema

na mabaya (sheria). Mungu aliwafukuza bustanini kwa

sababu mwanadamu alichagua mfumo mwingine kabisa

wa kuishi tofauti na ule alioukusudia tangu mwanzo.

Katikati ya bustani kulikuwa na mti wa uzima. Swali la

kujiuliza kwanini Mungu asingewaruhusu kula mti wa

uzima ili waishi milele? (Mwa 3:22-24) Jibu ni jepesi kabisa

Mungu hakutaka kuchanganya maisha ya matendo ya

sheria na wakati huo huo kuishi katika Kristo. Mungu

alitaka mwanadamu aishi katika Kristo peke yake ambao ni

mti wa uzima.

Ndio maana wakati huu hatutakiwi kuishi kwa sheria tena,

bali tunatakiwa kuishi katika Kristo Yesu. Kibali zaidi ya

matendo ya sheria hupatikana kwa njia ya msalaba tu. Ili

tuweze kufanikiwa zaidi ya mema tunayoyafanya ni lazima

tuishi katika Yesu Kristo na neema ya msalaba.

Kwanini zilihitajika juhudi za Yesu kuikamilisha kazi ya

msalaba?

Kristo alijitahidi kufuata kila sheria na kanuni zote. Ili sisi

tusiishi tena chini ya laana ya sheria na torati. Iliandikwa

kuwa Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwakuwa

UHURU WA KWELI 40

alifanywa laana kwaajili yetu; maana imeandikwa,

Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti (Gal 3:13).

Ilibidi ajitahidi kutukomboa kutoka kwenye laana ya torati

na sheria ili sisi tuwe huru tuishi tu kupitia Yeye (Kristo).

Kwani Mungu anashida na torati au sheria?

Mungu hana shida na torati au sheria kama jinsi ambavyo

Biblia inaeleza kuwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya

(sheria) ni ishara ya sheria au torati. Kazi yake ilikuwa ni

moja tu kukuwezesha kujua mema na mabaya, na

kwakuwa mwanadamu alichagua mti wa ujuzi wa mema na

mabaya yaani kuishi kwa sheria. Mungu alimruhusu Musa

kuleta sheria kumi za Mungu. Ambazo hakuna hata mmoja

ambaye aliweza kuishi kwa hizo. Wengi walikuwa

wanafuata baadhi nyingine wanazivunja. Mpaka wakati

Kristo alipokuja kutukomboa hakuwepo hata mmoja

aliyeweza kuzifuata kikamilifu. Ambapo maandiko

yanasema ikiwa mtu ameishika sheria akajikwaa katika

neno moja amekosa juu ya yote. Maana yake tulikuwa tuko

chini ya laana na hukumu ya sheria.

Ndio maana Mafarisayo na Waandishi walikuwa

wanajitahidi kufuata sheria lakini bado hawakuweza kufikia

kiwango cha kukubalika na Mungu alikokuwa anahitaji.

Ndio maana Kristo (Mungu aliyehai), Elohim, Mungu

UHURU WA KWELI 41

anayeishi akaamua aje mwenyewe kusudi aitimize sheria

yote ili Yeye akae kwenye nafasi yetu na sisi tukae kwenye

nafasi yake. Kristo alipokuja ulimwenguni alijifanya hana

utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa mfano wa

wanadamu; akajinyenyekesha akawa mtii (mwenye juhudi)

hata mauti ya msalaba. Kwahiyo Kristo ilibidi ajitahidi

kutimiza sheria yote ili sisi tutembee ndani ya neema yake

na tuwezeshwe ndani ya neema yake.

Wingi wa neema ya Kristo Yesu.

Neema ni kustahilishwa kusiko stahili, kibali au mafanikio

unayoyapata pasipo kazi au matendo, juhudi au sheria.

Kristo alipokuja duniani alikuja akiwa na neema na kweli.

Maandiko yanasema hivi;

“Kwakuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na

kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo” [Yoh 1:17]

Kwa maana hiyo ukweli uko upande wa neema. Yesu

alipokuja alikuja kuachilia neema ili watu wajitosheleze

kwa neema yake. Watu wengi wanaamini katika neema

lakini hawaamini katika utoshelevu wa neema ya Kristo.

Wakristo wengi wanaamini katika kuchanganya neema ya

Kristo na matendo yao, sheria au kanuni. Wakati Kristo

alikuja kwaajili ya kumsaidia mwanadamu aondokane na

hali ya kutumainia juhudi binafsi ili kupokea uponyaji,

UHURU WA KWELI 42

imani au mafanikio. Kwa sababu kama ikiwa kwa neema

haiwi kwa matendo tena na kama ikiwa kwa matendo haiwi

neema tena (Rum 11:6).

Neema haiusishi matendo kabisa, inahusisha kwenye

kuwezeshwa zaidi kupitia utimilifu wa Kristo wa kile

alichokifanya pale msalabani. Ndugu yangu lazima uelewe

kwamba tuko kwenye agano la neema na sio agano la

matendo ya sheria (agano la kale). Na hii ndiyo

ilimsababisha Kristo kufa pale msalabani lengo lake ni

kukuweka huru kabisa na uhuru huu utaanza kuuona

kwenye maisha yako na mipaka yako kwenye maisha yako

itavunjika. Ukiambatana na imani hii utaanza kutawala

dhambi kwa sababu dhambi haitakuwa na uwezo wa

kukutawala, utaweza kutawala katika kila eneo kwenye

maisha yako (Rum 5:17, 6:14). Baada ya kuanza kuweka

imani hasa kwenye kile Kristo alichokifanya na sio

unachokifanya utaona matunda yake. Ndio maana Paulo

aliwaambia Wagalatia hivi;

“Siibatili neema ya Mungu; maana, ikiwa haki hupatikana

kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure” [Gal 2:21]

Maana yake haki yako inabatilishwa kwa matendo ya

sheria. Tukisema ili tupokee uponyaji, imani, msamaha wa

dhambi au mafanikio nilazima tufuate kanuni fulani

ambazo tumejiwekea tunaibatili neema ya Kristo na ile

Kristo kufa msalabani ilikuwa ni bure.

UHURU WA KWELI 43

Kuwa ndani ya agano la neema ni kutojihesabia kabisa

juhudi zako na kuhesabia hasa juhudi za Kristo alizozifanya

pale msalabani kwa ajili yetu.

Shetani hapendi kabisa kuona mtoto wa Mungu imani ya

kuamini utimilifu wa kazi aliyoifanya pale msalabani.

Shetani anapenda upewe haki, utakatifu, mafanikio kwa

kuangalia kile unachokifanya na sio utoshelevu wa neema

ya Kristo. Shetani anajua kufanya hivyo utakuwa

umejichorea mipaka mwenyewe ya kupokea zaidi katika

jambo lolote unalolitaka litokee kwenye maisha yako kwa

ukamilifu. Shetani anajua ukiamini utimilifu wa kazi ya

msalaba aliyoifanya Yesu Kristo huwezi kutimiza kusudi la

Mungu alilokuwekea ndani yako. Ukiamua leo kuanza

kuamini kuanzia saa hii kupitia ukamilifu wa kazi ya Kristo

msalabani utaanza kuona vifungo vyote kwenye maisha

yako vimefunguka kabisa.

Mipaka ya juhudi zako binafsi inavunjika na kuanzia hapo

utaanza kuona jinsi ambavyo unaanza kuakisi maisha ya

kimbingu ukiwa duniani. Shetani hapendi watoto wa

Mungu wawe na hii imani ndio maana katika makanisa

mengi unapoanza kufundisha habari ya neema watu

wanaanza kuwa na mashaka. Shetani anaweka hofu ndani

yao kwa sababu anajua ukiifahamu siri hii kwenye maisha

yako hautakuwa mtumwa tena katika kile unachokifanya,

UHURU WA KWELI 44

na utaanza kuona ustawi na mafanikio makubwa sana

kwenye maisha yako bila kutumia nguvu kabisa.

Kuwa ndani ya neema ni kuamini kupitia juhudi za Kristo

alizozifanya pale msalabani ni kamilifu kuliko kile chema

unachokifanya.

Kuwa ndani ya neema haimaanishi usifanye jambo lolote

kuhusu mafanikio yako, uponyaji wako au utakatifu. Kuwa

ndani ya neema ni kuacha kutumainia na kuamini kile

chema unachokifanya na kutumainia na kuamini zaidi kile

alichofanya Yesu msalabani. Kuwa na tabia njema ni jambo

jema sana lakini jua kuwa wewe ni Mtakatifu kwa sababu

ya kile alichofanya Yesu msalabani na si kwa sababu

yamatendo yako mema. Kiwango cha utakatifu ambao

Mungu aliutaka alikifunga kwa Yesu Kristo ndio maana

alitaka tuamini alichofanya Yesu Kristo, ili tutakapoamini

tuone matunda yake, matokeo yake katika macho ya damu

na nyama. Yesu Kristo ni Mungu aliyejifunua kwa umbo la

mwanadamu, alipoona matendo yetu yanatuchorea

mipaka katika viwango vya mafanikio tunavyotakiwa

kufika. Aliamua kushuka mwenyewe ili asimame kwenye

nafasi yetu kusudi yeye afanye kwa nafasi yetu ili kuondoa

mipaka iliyokuwa inatuzuia kwa kujitahidi ambako

hakukufaa kitu kuweza kufika pale Mungu mwenyewe

alitaka tufike.

UHURU WA KWELI 45

Mkuu Yesu Kristo aliamua kutimiza kila kitu ambacho

kilistahili tukifanye kwaajili yetu, na kwa namna hiyo

akatuondolea mipaka kabisa ya kufika tunakotakiwa kufika

bila juhudi wala jitihada binafsi. Kipindi hiki cha agano

jipya, yaani agano la neema huwezi jitetea tena kuwa

sijaweza fanya jambo fulani kwenye maisha yangu kwa

sababu nguvu, uwezo au juhudi zangu zilikuwa ndogo.

Kristo alifanya zaidi ya pale uwezo wako ulikoma kusudi

akufikishe kwa neema yake mwenyewe aliyoiachilia bure

pasipo kuangalia matendo yetu. Ndio maana maandiko

yanasema hivi;

“Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti ilitawala

kwasababu ya yule mmoja, zaidi sana wao wapokeao wingi

wa neema, na kile kipawa cha haki, watatawala katika

uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo” [Rum 5:17]

Adamu alipoasi tulihesabiwa ni wenye dhambi sio kwa

sababu tulifanya dhambi ila kwa sababu Adamu aliasi

tuliingizwa kwenye mkumbo wa dhambi na dhambi

ilitutawala. Ndio maana tunahesabiwa watakatifu sio kwa

sababu ya matendo yetu ila ni kwa sababu ya kumwamini

Yesu Kristo. Ndio maana hakuna mtu anayeweza kujisifu

kwa matendo mema aliyonayo na asiokoke kwa sababu

atahukumiwa sio kwasababu ya mema anayoyafanya ila

kwa sababu hakuliamini jina la mwa na pekee wa Mungu

UHURU WA KWELI 46

(Yesu Kristo) [Yoh 3:18]. Matokeo ya dhambi ni mauti

ilitawala sasa unaona ni kwa jinsi gani ilikuwa mbaya.

Hali hii ndiyo inasababisha kila mtu amhitaji Kristo kwenye

maisha yake, huwezi kusema mimi sina dhambi kwakuwa

sikufanya. Yupo aliyefanya ambaye ni Adamu akakufanya

na wewe kuwa mwenye dhambi ukweli huu huwezi

kuukwepa. Ashukuriwe Mungu kwa sababu imekuwa ni

ajabu sana kuwa kupitia Yesu Kristo tulipokea wingi wa

neema na kipawa cha haki tulivipokea ambavyo

havikutokana na juhudi ya matendo yetu. Sasa utaona ni

kwa jinsi gani Mungu ni mwenye haki. Sisi ambao

hatukustahili kuhesabiwa dhambi kwa sababu ya dhambi

ya Adamu ndio ambao hatukustahili kupokea wingi wa

neema na kipawa cha haki katika Kristo Yesu.

Neema tuliyoipokea ilikuwa kutusaidia kustahilishwa

tusivyostahili na kipawa cha haki ambayo ni zawadi

tuliyoipokea inayotupa ujasiri wa kusimama mbele za

Mungu ili vitusaidie kutawala. Jinsi gani Mungu alivyo

waajabu yaani kupitia wingi wa neema na kipawa cha haki

vitusaidie kutawala. Kama ni hivyo basi tunahitaji kuufunua

sana uzuri wa wingi wa neema ya Kristo na kipawa cha haki

kwa wingi kwa kujifunza na kuyajaza maarifa yake moyoni

mwetu ili tuweze kutawala na kufikia kiwango cha imani ,

utakatifu na mafanikio kama vile Mungu anataka ifikie

UHURU WA KWELI 47

katika utimilifu wake wa kimo katika kumjua Yeye (Kristo

Yesu).

Kuwa ndani ya neema sio dhamana ya kuishi maisha ya

dhambi, lakini ni nguvu inayotusaidia kuishi katika haki,

kiasi na utakatifu.

Naomba utambue hili kuwa ndani ya neema sio kuishi

maisha yasiyo na mwelekeo, maisha yenye dhambi au

maisha yasiyo na nidhamu. Kinachotufanya tuwe na

kiwango cha utakatifu, haki,kiasi na nidhamu binafsi ni

neema pekee. Huwezi kufikia kiwango cha utakatifu ambao

Mungu anautaka kama uko nje ya neema. Huwezi kuwa na

nidhamu katika maisha nje ya neema. Ukijihesabia

utakatifu kwa kile unachokifanya hautaweza kwa sababu

juhudi zako ni bure mbele za Mungu pasipo imani ya

ukamilifu wa kazi ya Kristo Msalabani. Lazima ujikabidhi

kwenye neema ya Kristo halafu yeye mwenyewe ataachilia

utakatifu, nidhamu, kiasi na haki ambayo unatakiwa kuwa

nayo ambayo hii sio kwa sababu ya juhudi zako, bali kwa

sababu ya juhudi za Kristo msalabani. Maandiko yanasema

hivi;

“Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa sababu

hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema” [Rum 6:14]

Tukiwa chini ya sheria ni rahisi kutawaliwa na dhambi.

Neema ya Kristo pekee ndiyo inayoweza kutusaidia

UHURU WA KWELI 48

kuitawala dhambi na kuishi katika utakatifu ambao Mungu

anautaka. Paulo aliandika hivi;

“Maana neema ya Mungu iwaokowayo wanadamu wote

imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa

za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa,

katika ulimwengu huu wa sasa; tukilitazamia tumaini lenye

baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu

mkuu na Mwokozi wetu” [Tit 2:11-13]

Neema ya kristo ipo kwaajili ya kutusaidia kuishi katika

utakatifu, haki na kiasi. Huwezi kuwa ndani ya neema hali

bado ukaendelea kuishi katika dhambi. Vivyo hivyo huwezi

kuwa na ndani ya neema na usistawi na kufanikiwa. Neema

inapokuwa nyingi kwako ndivyo kiwango cha kuwa na

uwezo wa kutenda mambo kinakuwa kikubwa na ndivyo

kiwango chako cha kutawala kinakuwa kikubwa. Ndio

maana neema ya Kristo Yesu inazidishwa katika kumjua

Yesu Kristo (2Petro 1:2 KJV) ili kuweza kufikia kiwango cha

utakatifu ambao Mungu anautaka ni kwa njia ya neema ya

Kristo na kumjua Yeye (Yesu Kristo).

Kipindi cha agano la kale watu walijitahidi kutenda

matendo mema kwa sheria lakini bado hawakuweza kufikia

kiwango cha utakatifu ambao Mungu anautaka. Ndio

maana Kristo aliamua kufa kwaajili yetu ali aachilie neema

ya Kristo itusaidie kufikia kiwango cha utakatifu ambao

Mungu anautaka. Ndio maana Paulo pamoja na kwamba

UHURU WA KWELI 49

alifanya kazi ya mhubiri wa injili kwa juhudi zote lakini

hakutumainia anachokifanya. Alitumainia zaidi neema ya

Kristo ndio maana aliwaambia Wagalatia hivi;

“Siibatili neema ya Mungu; maana, ikiwa haki hupatikana

kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure” [Gal 2:21]

Paulo pamoja na kuwa na juhudi na jitihada alizokuwa nazo

lakini bado hakutumainia juhudi na jitihada alizokuwa nazo

bado aliitumainia neema ya Yesu Kristo. Ndio maana

anasema siibatili neema ya Kristo, kwa sababu kuibatili

neema ya Kristo ni kumfanya kuwa Yesu Kristo alikufa

msalabani bure.

Kutembea ndani ya neema ya Kristo sio maisha ya uvivu,

uzembe au dhambi, bali ni maisha ya kukusaidia

kukamilisha kusudi la kuumbwa kwako kikamilifu.

Wa-Kristo wengi wanaamini kufikia kusudi la kuumbwa

kwao wanatakiwa kujitahidi sana, kujitesa na kupambana ili

waweze kufanikisha kusudi la kuumbwa kwao hapa duniani.

Haiwezekani kufikia kusudi la kuumbwa kwako kwa juhudi

zako, kujitesa, wala kupambana. Katika agano la kale kila

mmoja alijitahidi kuwa mtakatifu kwa matendo ya sheria

lakini bado hawakuweza. Ndio maana utawaona

Mafarisayo na Waandishi walikuwa wanajitahidi kufuata

sheria kwa juhudi sana lakini bado hawakuweza kufikia

utakatifu ambao Mungu aliutaka. Kwa maana hatuwezi

UHURU WA KWELI 50

kulifanya kusudi la Mungu kikamilifu, kuishi maisha ya

utakatifu ambao Mungu anautaka kwa matendo ya sheria.

Yesu Kristo alipokufa msalabani aliachilia wingi wa neema

na kipawa cha haki ili tuweze kutawala dhambi na kila kitu

tunachokihitaji.

Mungu anapenda tufanye kazi kwa juhudi zote, tujitahidi

kwa kadri tunavyoweza lakini tusitumainie uwezo wetu

binafsi, juhudi au jitihada tunazozifanya kwenye mafanikio

yetu ili tuweze kufikia Mungu anataka tufike. Mungu

anataka tuamini kwa asilimia zote kwenye neema yake tu

kwa sababu kupitia neema yake tunaweza kufika pale

ambapo Mungu anataka tufike au kufikia kiwango cha

mafanikio ambayo tulitamani kuona yanatokea kwenye

maisha yetu.

Upendo wa Kristo.

Paulo aliwaambia Warumi hivi:-

“Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki

au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?”

[Rum 8:35]

Paulo aliwaaambia Warumi ni jambo gani linaloweza

kututenga na upendo wa Kristo? Maana yake hakuna jambo

linaloweza kututenga na upendo wa kristo katika maisha

UHURU WA KWELI 51

yetu. Upendo wa Kristo uko pale pale, tuwe na shida au

adha upendo wa Kristo uko pale pale, tuwe na njaa au uchi

upendo wa Kristo uko pale pale, tuwe na hatari au upanga

upendo wa Kristo uko pale pale.

Tunatakiwa kujua upendo wa Kristo haupungui kwa sababu

ya shida au changamoto tunazokutana nazo. Chanzo cha

Kristo kuja ilikuwa kwa sababu ya upendo wake ndio maana

maandiko yanasema hivi;

“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata

akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye

asipotee, bali awe na uzima wa milele” [Yoh 3:16]

Jambo la muhimu kutambua ni kuwa Mungu aliufunua

upendo wake kupitia Kristo. Aliona mwanadamu

alivyokuwa anapata shida katika hali ya dhambi na maisha

aliyokuwa nayo. Ndio maana Kristo alitupenda kwanza,

akatuchagua na kutuweka ndani ya ufalme wake.

Haijalishi ni eneo gani gumu unapitia inawezekana ni uzinzi

ndio unaokutesa, inawezekana ni uongo, inawezekana ni

ugonjwa umekutesa kwa mda mrefu kiasi ambacho

umeupa jina kuwa ni ugonjwa wako. Upendo wa Kristo uko

pale pale bado Kristo anakuhitaji kwenye ufalme wake kwa

sababu wewe ni wathamani sana.

UHURU WA KWELI 52

Kuwa mtu wa kuathiriwa na upendo wa Ki-Mungu

Watu wengi ukiwaambia kuhusu kuishi upendo wa ki-

Mungu kwenye maisha yao wanafikiri hawawezi kuwa na

upendo kama wa Mungu kwa sababu ni wa Mungu. Kama

ingekuwa upendo wa ki-Mungu katika Kristo Yesu

haiwezekani isingeandikwa kuwa;

“mkaenende katika upendo, kama Kristo naye

alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwaajili yetu, sadaka na

dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato” [Efe 5:2]

Kwa hiyo, ni lazima tuwe na upendo kama alikuwa nao Yesu

Kristo ndio maana tumeagizwa kuenenda katika upendo

wake

Biblia katika agano jipya haitufundishi upendo wowote ule

isipokuwa upendo wa ki-Mungu. Upendo wa ki-Mungu

unaachilia ndani yako kwa njia mbili;

Kujifunza upendo wa Mungu kupitia Yesu Kristo

Upendo wa Mungu kumiminwa kwa njia ya Roho

Mtakatifu

UHURU WA KWELI 53

Kujifunza upendo wa Mungu kupitia Yesu Kristo.

Katika agano jipya Mungu ameudhihirisha upendo wa

Mungu kwenye maisha ya mwanadamu. Kwanza kwa

kumtoa mwanaye pekee. Maandiko yanasema

“Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili

auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika

yeye” [Yoh 3:17]

Kumbe Mungu alimtuma Mwana ulimwenguni ili asiwepo

wa kupotea. Siku zote Mungu anapenda ukae katika njia

sahihi. Mungu anapenda uishi katika afya njema na

mafanikio katika eneo ambalo unatamani ufanikiwe.

Upendo wa Mungu kumiminwa kwa njia ya Roho

Mtakatifu.

Paulo anasema hivi;

“na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu

limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho

Mtakatifu tuliyepewa sisi” [Rum 5:5]

Kwa hiyo, upendo wa ki-Mungu ili uweze kuwa sehemu ya

maisha yetu nilazima tujifunze kwa Roho Mtakatifu. Kwa

sababu maandiko yanasema pendo la Mungu limekwisha

kumiminwa ndani yetu.

UHURU WA KWELI 54

Tabia za Upendo wa ki-Mungu katika Yesu Kristo.

“Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo

hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti

mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili

yote. Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali

ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma;

yakiwapo maarifa, yatabatilika.” [1Kor 13:4-8]

Tuangalie mistari hii katika Biblia ya Habari Njema (BHND)

“Mwenye upendo huvumilia, hufadhili; mwenye upendo

hana wivu, hajidai, wala hajivuni. Mwenye upendo hakosi

adabu, hatafuti faida yake binafsi, wala hana wepesi wa

hasira; haweki kumbukumbu ya mabaya, hafurahii uovu,

bali hufurahia ukweli. Mwenye upendo huvumilia yote,

huamini yote, hustahimili yote. Upendo hauna kikomo

kamwe. Kama kuna vipaji vya kutangaza ujumbe wa

Mungu, hivyo vitatoweka siku moja; kama ni vipaji vya

kusema lugha ngeni, vitakoma; kama kuna elimu, nayo

itapita.”

UHURU WA KWELI 55

Tafsiri ya Biblia ya NENO (NEN), imeandikwa;

“Upendo huvumilia, upendo hufadhili, upendo hauoni wivu,

hauna majivuno, hauna kiburi. Haukosi kuwa na adabu,

hautafuti mambo yake, haukasiriki upesi, hauweki

kumbukumbu ya mabaya. Upendo haufurahii mabaya bali

hufurahi pamoja na kweli. Upendo huvumilia yote, huamini

yote, hutumaini yote, hustahimili yote. Upendo haushindwi

kamwe. Lakini ukiwepo unabii, utakoma; yakiwepo

maarifa, yatapita.”

Kutoka katika tafsiri hizi tunaweza kuorodhesha yafuatayo

kuhusu tabia za upendo;

Huvumilia

Hufadhili

Hauoni wivu

Haujidai (hauna majivuno)

Hauna kiburi

Haukosi kuwa na adabu

Hautafuti faida yake binafsi

Haukasiriki upesi

Hauweki kumbukumbu ya mabaya

Haufurahii mabaya

Hufurahia kweli (Neno la Kristo)

Huvumilia yote

UHURU WA KWELI 56

Huamini yote (Katika Kristo)

Hustahimili yote

Haushindwi (Hauna kikomo) kamwe

Upendo wa namna hii unakuja kwa kujifunza pendo la

Kristo kwetu. Tukiathirika na upendo wa Kristo tunaweza

kuathirika katika tabia na kuziishi hizi tabia. Ndio maana

Mtume Paulo anasema, “tukaenende (tukatende) kama

Kristo naye alivyotupenda na akajitoa kwaajili yetu, sadaka

na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato” (Efe

5:2). Ili tuweze kufanikiwa kuwa na upendo kama wa Yesu

Kristo ili tuenende nao nilazima tujifunze upendo wa Kristo

kwetu. Kubali kuathiriwa na upendo wa Kristo kuanzia sasa

ili uanze kukuathiri kwenye tabia zako.

UHURU WA KWELI 57

Tathmini kupitia maswali kutoka katika Sura ya Pili

1: Kutokana na surah ii ukale ni nini?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

2: Elezea kwa ufupi namna gani ya kutoka kwenye ukale

kupitia yafuatayo:-

(i)Utimilifu wa kazi ya msalaba wa Kristo

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

(ii)Wingi wa Neema ya Yesu Kristo

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

(iii)Upendo wa Yesu Kristo

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

3: Ukamilifu wa kazi ya msalaba wa Kristo unasaidia katika

mambo yafuatayo, yataje:-

UHURU WA KWELI 58

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

………………………………….......

(iii)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

(iv)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

4: Kuishi kwa Neema ya Kristo kunasaidia katika mambo

yafuatayo, yataje:-

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………....

(iii)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

(iv)……………………………………………………………………………………

………………………………………...

(v)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

UHURU WA KWELI 59

5: Elezea kwa ufupi namna gani ya kuathirka na upendo wa

Kristo?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………..

UHURU WA KWELI 60

UHURU WA KWELI 61

SURA YA TATU

MBONA SIO ASILI YANGU

sili inajumuisha tabia za kitu. Mwanadamu aliumbwa

kwa asili ya Mungu, Mungu aliposema na tumfanye

mtu kwa mfano wetu na kwa sura yetu. Mungu alitaka tuwe

na tabia kama za Mungu katika Maisha yetu. Tuwe

watakatifu kama alivyo Mungu (1Petro 1:16), tuwe na

mamlaka kama alivyokuwa Mungu, tuwe watawala kama

alivyo Mungu, tuwe wenye haki kama alivyo Mungu. Paulo

aliandika hivi;

“Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili

wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe

mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale

aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita,

hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao

akawatukuza.” [Rum 8:29-30]

Paulo aliwaaambia Warumi tangu asili Mungu alitujua na

alituita ili tufanane na Mwana wake (Yesu Kristo). Na

Mungu alivyotuita alituheasabia haki na kututukuza katika

Kristo Yesu (tuliookoka). Paulo anasema hivi katika

Waefeso;

A

UHURU WA KWELI 62

“Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo,

aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu

wa roho, ndani yake Kristo; kama vile alivyotuchagua katika

yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe

watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo.

Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe

kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na uradhi wa mapenzi

yake. Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo

ametuneemesha katika huyo Mpendwa.” [Efe 1:3-6]

Imeandikwa kuwa kabla ya misingi ya ulimwengu kuumbwa

Mungu kwa mapenzi yake mwenyewe. Alitubariki kwa

baraka zote za rohoni kupitia mwanawake Yesu Kristo ili

tuwe watakatifu watu wasio na hatia mbele za Mungu. Na

anasema ametuneemesha kwa neema yake katika huyo

mpendwa. Kutokana na Warumi 8:29-30 na Waefeso 1:3-6

maana yake ni kwamba kwa Mapenzi ya Mungu mwenyewe

pasipo kulazimishwa mtu au kitu chochote. Mungu

alituchagua kabla ya misingi ya ulimwengu kupitia mwana

wake Yesu Kristo ili tuwe watakatifu, wenye haki, watu

wasio na hatia na kututukuza kwa neema yake mwenyewe

kupitia mwana wake wa pekee.

Sio kwa juhudi zetu wala sio kwa matendo yetu kufanywa

watakatifu, wenye haki, tusio na hatia na kutukuzwa kwa

neema yake. Bali ni kwa mapenzi ya Mungu kupitia Yesu

Kristo. Mungu hakuhitaji juhudi zako, matendo yako wala

UHURU WA KWELI 63

uadilifu wako bali alituchagua yeye mwenyewe pasipo

madai ya matendo yetu.

Tuangalie mfano wa Yakobo na Esau.

“Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, maana

alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe

akachukua mimba. Watoto wakashindana tumboni

mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini?

Akaenda kumwuliza Bwana. Bwana akamwambia,Mataifa

mawili yamo tumboni mwako,Na kabila mbili za watu

watafarakana tangu tumboni mwako.Kabila moja litakuwa

hodari kuliko la pili,Na mkubwa atamtumikia mdogo. Siku

zake za kuzaa zilipotimia, tazama! Mapacha walikuwamo

tumboni mwake. Wa kwanza akatoka, naye alikuwa

mwekundu mwili wote kama vazi la nywele. Wakamwita

jina lake Esau.

Baadaye ndugu yake akatoka, na mkono wake unamshika

Esau kisigino. Akaitwa jina lake Yakobo. Isaka alikuwa

mwenye miaka sitini mkewe alipowazaa. Ikawa Isaka

alipokuwa mzee, na macho yake yamepofuka asione,

akamwita Esau, mwanawe mkubwa, akamwambia,

Mwanangu. Naye akamwitikia, Mimi hapa. Akasema,

Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee, wala sijui siku ya kufa

kwangu. Basi, nakuomba, chukua mata yako, podo lako na

UHURU WA KWELI 64

upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo;

ukanifanyie chakula kitamu namna ile niipendayo,

ukaniletee, ili nile; na roho yangu ikubariki, kabla sijafa.

Na Rebeka akasikia, Isaka aliposema na Esau mwanawe.

Basi Esau akaenda nyikani awinde mawindo, ayalete.

Rebeka akamwambia Yakobo mwanawe, akisema, Angalia,

nimemsikia baba yako akisema na Esau, ndugu yako,

akinena, Niletee mawindo, ukanifanyie chakula kitamu ili

nile, na kukubariki mbele za Bwana kabla ya kufa kwangu.

Basi, mwanangu, sikiliza sauti yangu kama

nitakavyokuagiza. Enenda sasa kundini ukanitwalie wana-

mbuzi wawili walio wema, nami nitawafanya chakula

kitamu kwa baba yako, namna ile aipendayo. Kisha

utampelekea baba yako, apate kula, ili akubariki kabla ya

kufa kwake.

Yakobo akamwambia Rebeka mamaye, Esau ndugu yangu

ni mtu mwenye malaika, na mimi ni mtu laini. Labda baba

yangu atanipapasa, nami nitakuwa machoni pake kama

mdanganyifu; nami nitaleta juu yangu laana wala si

mbaraka. Mamaye akamwambia, Laana yako na iwe juu

yangu, mwanangu, usikie sauti yangu tu, enenda ukaniletee

wana-mbuzi. Akaenda, akawatwaa, akamletea mamaye.

Mamaye akafanya chakula kitamu namna ile aliyopenda

babaye.

UHURU WA KWELI 65

Kisha Rebeka akatwaa mavazi mazuri ya Esau mwanawe

mkubwa, aliyokuwa nayo nyumbani, akamvika Yakobo

mwanawe mdogo. Na ngozi za wana-mbuzi akamvika

mikononi, na katika ulaini wa shingo yake. Naye akampa

Yakobo mwanawe mikononi mwake hicho chakula kitamu,

na mkate alioufanya. Akaja kwa baba yake, akasema,

Babangu. Akasema, Mimi hapa, U nani wewe, mwanangu?

Yakobo akamwambia babaye, Mimi ni Esau, mzaliwa wako

wa kwanza, nimefanya kama ulivyoniambia. Ondoka,

tafadhali, ukae kitako, ule mawindo yangu, ili roho yako

inibariki.

Isaka akamwuliza mwanawe, Imekuwaje umepata upesi

namna hii, mwanangu? Akasema, Kwa sababu Bwana,

Mungu wako, amenifanikisha. Isaka akamwambia Yakobo,

Karibu, tafadhali, ili nikupapase, mwanangu, nione

kwamba wewe ndiwe mwanangu Esau, ama siyo. Basi

Yakobo akamkaribia Isaka, babaye, naye akampapasa,

akasema, Sauti ni sauti ya Yakobo, lakini mikono ni mikono

ya Esau. Wala hakumtambua, kwa maana mikono yake

ilikuwa kama mikono ya Esau, ndugu yake, yenye malaika;

basi akambariki.

Akamwuliza, Wewe ndiwe kweli mwanangu Esau?

Akasema, Ndimi. Akasema, Niletee karibu nami nipate kula

mawindo ya mwanangu, ili roho yangu ikubariki.

Akamsogezea karibu, naye akala; kisha akamletea mvinyo,

UHURU WA KWELI 66

akanywa. Isaka, baba yake, akamwambia, Njoo karibu

sasa, ukanibusu, mwanangu. Akakaribia akambusu. Naye

akasikia harufu ya mavazi yake, akambariki akasema,

Tazama, harufu ya mwanangu Ni kama harufu ya shamba

alilolibariki Bwana.

Ikawa Isaka alipokwisha kumbariki Yakobo, na alipokuwa

Yakobo ndiyo kwanza ametoka mbele ya Isaka, baba yake,

mara Esau ndugu yake akaja kutoka katika kuwinda kwake.

Naye pia amefanya chakula kitamu akamletea babaye,

akamwambia baba yake. Babangu na aondoke, ale

mawindo ya mwanawe, ili roho yako inibariki. Isaka, baba

yake, akamwuliza, U nani wewe? Akasema, Mimi ni

mwanao, Esau, mzaliwa wako wa kwanza. Isaka

akatetemeka tetemeko kuu sana, akasema, Ni nani basi

yule aliyetwaa mawindo akaniletea? Nami nimekwisha kula

kabla hujaja wewe, nikambariki; naam, naye atabarikiwa.

Esau aliposikia maneno ya babaye, akalia kilio kikubwa cha

uchungu sana, akamwambia babaye, Nibariki na mimi,

mimi nami, Ee babangu. Akasema, Nduguyo amekuja kwa

hila, akauchukua mbaraka wako. Akasema, Je! Hakuitwa

Yakobo kwa haki, maana amejitia mahali pangu mara mbili

hizi? Alichukua haki yangu ya mzaliwa wa kwanza, na sasa

amechukua mbaraka wangu. Akasema, Je! Hukuniwekea

na mimi mbaraka? Isaka akajibu, akamwambia Esau,

Tazama, nimemfanya awe bwana wako, na ndugu zake

UHURU WA KWELI 67

wote nimempa kuwa watumishi wake; kwa nafaka na

mvinyo nimemtegemeza, nami nikufanyie nini sasa,

mwanangu?

Esau akamwambia babaye, Una mbaraka mmoja tu,

babangu? Unibariki mimi, mimi nami, Ee babangu. Esau

akapaza sauti yake, akalia. Isaka, baba yake, akajibu,

akamwambia,Angalia,penye manono ya nchi patakuwa

makao yako,Na penye umande wa mbingu unaotoka juu.

Kwa upanga wako wewe utaishi, nawe utamtumikia

nduguyo; Na itakuwa utakapoponyoka, Utalivunja kongwa

lake katika shingo yako. Esau akamchukia Yakobo kwa ajili

ya ule mbaraka babaye aliombarikia. Esau akasema moyoni

mwake, Siku za kumlilia baba yangu zinakaribia, ndipo

nitakapomwua ndugu yangu Yakobo. [Mwa 25:21-26, 27:1-

27, 30-41]

Katika mfano huu utagundua kwamba hakuna jambo baya

alilofanya Esau wala hakuna jambo jema alilofanya Yakobo.

Mungu alimpa mbaraka Yakobo kwa sababu alimchagua

kuwa mrithi wa baraka za baba yake Isaka. Hii ni kwa sababu

Mungu alimchagua Isaka tangu akiwa tumboni mwa mama

yake Rebeka kuwa Mrithi wa baraka za Isaka.

UHURU WA KWELI 68

Mungu ametufanya kuwa miungu duniani maana yake tuna

mamlaka kama aliyonayo Mungu kwenye maisha yetu.

Mungu ametufanya kuwa washindi kwa sababu tunatokana

na yeye, ndio maana maandiko yanashuhudia hivi;

“Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda

ulimwengu; na huku ndiko kuushindako ulimwengu, hiyo

imani yetu” [1Yoh 5:4]

Asili yetu ni kushinda kwenye maisha yetu. Mungu anataka

tutembee kama washindi, watakatifu, wenye haki, wenye

mamlaka, tunaomlingana Mungu. Yesu alipokuja duniani

alikuja kwaajili ya kurejesha ufalme wake. Ndio maana Yesu

alipoanza huduma yake kwa mara ya kwanza alianza kwa

kutamka hadharani kutubu na kuiamini injili. Imeandikwa;

“Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Habari Njema ya Mungu,

akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu

umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili” [Mark 1:14b-15]

Neno “tubuni” ni neno ambalo kwenye lugha mama, lugha

ya kiebrania limetumika neno “teshuvah” maana yake

geuka. Neno tubuni limetokana na neno la kigiriki

“metanoia” maana yake badili mtazamo. Neno “injili”

kwenye lugha ya kigiriki limetumika neno “eungalion”

maana yake “habari njema”. Maana yake Yesu aliposema

“tubuni na kuiamini Injili” alikuwa anamaanisha hivi

“geukeni, badilisheni mtazamo wenu na kuiamini habari

UHURU WA KWELI 69

njema.” Tafsiri ya biblia ya The Passion Translation (TPT)

imetumia neno “kuambatana” maana yake geukeni,

badilisheni mtazamo wenu na kuambata na injili.

Kama ni hivyo basi kumbe tunaweza kusema Kristo alikuwa

anasema geukeni, badilini mtazamo wenu. Ufalme wa

Mungu unahitaji watu waliogeuka na kuacha njia zao

mbaya walizokuwa nazo, ufalme unahitaji watu ambao

walishabadilisha mtazamo. Sio rahisi sana kutembea na

ufalme wa Mungu kama bado hujabadili mtazamo wako.

Ukijua mamlaka, utawala na mfumo mzima wa uongozi wa

ufalme wa Mungu kuna aina ya maisha huwezi kuishi tena.

Huwezi kuwa mtumwa wa dhambi (Yoh 8:34) wakati unajua

unatakiwa kutawala, ukijua kuwa ukiwa duniani unatakiwa

kutawala kila kitu.

Yesu hakuja duniani kwaajili tu ya watu kwenda mbinguni,

alikuja kurudisha kile mwanadamu alichopoteza kwenye

bustani ya Edeni ambacho ni ufalme wake (ufalme wa

Mungu).

Mwanadamu kwa mara ya kwanza, Mungu alimuumba kwa

kusudi la kutembea ndani ya ufalme wake. Ndio maana kwa

mara ya kwanza Mungu anasema hivi;

“Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa

sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa

UHURU WA KWELI 70

angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye

kutambaa kitambaacho juu ya nchi.” [Mwa 1:26]

Wakatawale maana yake Mungu alimpa utawala wa ufalme

wake ili audhihirishe hapa duniani. Kwa tafsiri nyepesi

Mungu alikuwa anasema; “kama jinsi tunavyotawala

mbinguni kwa mfano huo ndivyo ninavyowapa kutawala

duniani.” Kutawala inajumuisha kusimamia na kuongoza.

Kristo alikuja kwaajili ya kuurudisha ufalme wake hapa

duniani kwa sababu tuliupoteza. Ndio maana mifumo yetu

ya kufanikiwa iko tofauti kabisa na mifumo ya ulimwengu

huu. Ndio maana Yesu anasema;

“Mimi siombi kwamba awatoe katika ulimwengu; bali

awalinde na yule mwovu. Wao si wa ulimwengu, kama

mimi nisivyo wa ulimwengu.” [Yoh 17:15-16]

Kama Yesu alisema ninyi sio wa ulimwengu huu kama mimi

nisivyo wa uliomwengu huu. Maana yake ni kwamba yoyote

aliyeko ndani ya Kristo ameumbwa kwenye mfumo tofauti

kabisa wa kufanikiwa na watu wa mataifa. Mifumo yetu ya

kufanikiwa iko tofauti kabisa na mifumo ya ulimwengu huu.

Ndio maana hatutakiwi kuamini kwenye mafanikio kama

vile ulimwengu unavyoamini. Kwa mfano ulimwengu

unaamini kwenye kufanya kazi sana ndio ufanikiwe. Lakini

sivyo biblia inavyotufundisha kwa watoto tulioko ndani ya

ufalme wa Mungu. Ndio maana Yesu aliwaambia wanafunzi

wake;

UHURU WA KWELI 71

“Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au

Tuvae nini? Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa

sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji

hayo yote. Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki

yake; na hayo mtazidishiwa.” [Math 6:31-33]

Yesu alikuwa anawaonyeshja watu kipaumbele kwa yoyote

aliye katika ufalme (aliyeokoka) ni kuutafuta ufalme (kuishi

jinsi ufalme unavyotaka). Tafsiri ya Biblia ya Habari njema

inasema;

“Basi, msiwe na wasiwasi: ‘Tutakula nini, tutakunywa nini,

tutavaa nini’. Maana hayo yote yanahangaikiwa na watu

wasiomjua Mungu. Baba yenu wa mbinguni anajua

kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote. Bali, shughulikeni

kwanza juu ya ufalme wa Mungu na matakwa yake, na

hayo yote mtapewa kwa ziada.”

Kumbe tukiushughulikia kwanza ufalme wa Mungu baada

ya hapo kuhusu kula, kunywa na kuvaa haitakuwa shida.

Kama ni hivyo basi uwe na uhakika ukiuishi ufalme wa

Mungu kula, kunywa na kuvaa haitakuwa jambo

unaloliwaza kwenye ufahamu wako. Kwa sababu

utakapoanza kuishi kama ufalme unavyotaka kula, kunywa

na kuvaa vitakuwa kwenye maisha yako kwa kiwango cha

kujitosheleza. Mungu alitufanya kuwa watu wa tofauti sana

(tuliookoka) kiwango ambacho hatutakiwi kupambana

kabisa kuhusu kutafuta kula, kunywa au kuvaa.

UHURU WA KWELI 72

Kwa sababu hatutatofautiana na watu wa mataifa kwa

sababu na wao kwenye ufahamu wao hutafuta hayo hayo.

Kumbe kama ni hivyo basi ukweli ni kwamba kila kitu

tunachokihitaji kwenye maisha yetu yaani kula, kunywa,

kuvaa ni vitu vinavyopatikana kirahisi tukiutumikia kwanza

ufalme wa Mungu.

Balozi wa Tanzania anapokuwa nchi ya Marekani huwa

anakuwa ndani ya uangalizi wa nchi ya Tanzania. Nchi ya

Tanzania huwa inahakikisha analindwa, anatunzwa kwa kila

kitu; kuhusu kula kwake, kunywa kwake, kuvaa kwake,

kulala kwake, ulinzi wake. Hayo ni mambo ambayo

hayafikirii kabisa kwenye ufahamu wake kwa sababu ni

wajibu wa serikali ya Tanzania kumhudumia. Kazi aliyonayo

balozi wa Tanzania huko Marekani ni kuitangaza nchi na

kuionyesha nchi uzuri wake, utajiri wake, maeneo ya utalii.

Hiki ndicho kilichoko kwenye ufahamu wake.

Vivyo hivyo tunapokuwa ndani ya ufalme wa Mungu Mungu

anataka tuishi jinsi ufalme unavyotaka tuishi halafu hayo

mambo mengine ya chakula, mavazi na malazi ni wajibu wa

ufalme wa Mungu kutuhudumia. Tunaishi kwenye dunia

inayotuelekeza tufanye mambo mengi sana, kila mmoja

atakwambia fanya hivi na vile ili uweze kufanikiwa. Lakini

kanuni ya ki-Mugu ni nyepesi ishi kwanza ufalme halafu

hayo mengine utazidishiwa. Ndio maana Kristo

UHURU WA KWELI 73

aliwafundisha wanafunzi wake namna nzuri ya kuomba

aliwaambia;

“Basi ninyi saline hivi; Baba yetu uliyembinguni , Jina lako

litukuzwe, Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa

duniani kama huko mbinguni. Utupe leo riziki yetu.” [Math

6:9-11]

Maana yake kipaumbele cha kwanza ili uweze kupata riziki

ni ufalme wake. Huwezi kuanza kuona matokeo mazuri ya

ufalme kama hauishi ufalme. Ili uweze kuishi kwa ufanisi

ndani ya ufalme unahitaji kujibu maswali yafuatayo:-

Ufalme unakutambua wewe ni nani?

Ufalme unataka ufanye nini?

Ufalme umekupa uwezo gani?

Ufalme umeadhimia nini kwenye hatima yako?

Ufalme unakutambua wewe ni nani?

Kila mmoja wetu Mungu alimuumba akiwa amemuwekea

kitu cha kufanya (utambulisho). Utambulisho huu ndio

unaokutofautisha wewe na watu wengine wote duniani. Na

utofauti huu ndio unaokupa wewe uwezo wa kufanya kitu

ambacho ufalme wa Mungu umekuitia kukifanya katika

kizazi hiki. Mungu alimjua Yeremia ndio maana alimwambia

hivi Yeremia;

UHURU WA KWELI 74

“Kabla sijakuumba katika tumbonalikujua, na kabla

hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii

wa mataifa” [Yer 1:4]

Mungu alimtambua Yeremia kuwa yeye ni nani. Mungu

alimtakasa (alimtenga) maalumu kwaajili ya kumuweka

Yeremia kuwa nabii wa mataifa. Mungu akamuwekea

Yeremia muda, nyakati na majira (Mhu 3:1). Kila mmoja

ameumbwa akiwa amewekewa kitu cha kufanya

ulimwenguni tofauti na watu wote duniani. Watu wengi

hawaamini hili ndio maana wanaishi maisha yasiyokuwa na

nidhamu (kufanya jambo kwa wakati). Mungu hakutuumba

kukaa duniani milele ndio maana alituweka ulimwenguni

kwa wakati, kusudi na majira. Lengo lake tuwe majibu

katika huu ulimwengu. Kuna watu hawatavushwa maisha

yao kwa sababu wanakusubiri wewe tu ndio uje uwatoe

kwenye shida na changamoto zao. Sasa jiulize na jijibu

mwenyewe ufalme wa Mungu unakutambua wewe ni nani?

Ni rahisi kujibu hili swali ukiwa ndani ya ufalme yaani

kuokoka. Unapookoka unaingizwa kwenye ufalme wa

Mungu na hapo ni rahisi sana kupata majibu ya swali letu

kwa sababu utakuwa umezaliwa kutokata na Baba

(Mungu). Sura yako itamfanania Mungu kwa sababu Mungu

alituumba kwa mfano na kwa sura yake mwenyewe (Mwa

1:26)

UHURU WA KWELI 75

Tuangalie mfano wa Utawala wa Mungu

Makao makuu (Mbinguni)

Mungu (Baba, Mwana, Roho)[Mfalme]

Maeneo ya utekelezaji (Duniani)

Mwanadamu (Balozi)

Malaika (watumishi wa mwanadamu)

Dunia

Shetani

Ufalme unataka wewe ufanye nini?

Biblia inasema;

“Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla

hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii

wa mataifa” [Yer 1:4]

Mungu alimtambua Yeremia kama nabii wa Mataifa. Ndio

maana Mungu alimwambia Yeremia nakujiua vizuri kabisa

kuwa wewe ni nabii wa Mataifa kwa sababu ndivyo

nilivyokuumba. Tena alimwambia angalia nimekuweka leo

juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung’oa, na kubomoa, na

kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda. Muulize

Mungu amekuweka ufanye nini? Biblia inasema;

UHURU WA KWELI 76

“Kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni

Mungu, wala hapana mwingine, Mimi ni Mungu, wala

hapana aliye kama mimi. Nitangazaye mwisho tangu

mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka

bado; nikisema shauri langu litasimama, name nitatenda

mapenzi yangu yote” [Isa 46:9-10]

Kumbe Mungu anapokuweka ulimwenguni anafahamu

mwisho wako kabla ya Mwanzo wako. Anakuwekea muda

na nyakati katika kutekeleza kusudi lako. Tambua kusudi

lako leo.

Ufalme umekupa uwezo gani?

Lazima utambue ufalme umekupa uwezo gani ndani yako.

Uwezo aliouwekeza Mungu ndani yako ni ule wa kukusaidia

kutimiza lengo/kusudi la Mungu kwenye maisha yako.

Lazima utambue Mungu amewekeza mambo gani ndani

yako. Unaweza kutambua uwezo ulioko ndani yako kwa

kuangalia mambo yafuatayo:-

Unapenda kufanya mambo gani

Mungu anakutambua wewe ni nani

Ufalme wa Mungu unakutambua wewe nani

Hatima ya maisha yako ni nini

UHURU WA KWELI 77

Ufalme wa Mungu umeazimia nini kwenye hatima yako

Maandiko yanasema;

“Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila

kusudi chini ya mbingu” [Mhu 3:1]

Lazima utambue kuwa Mungu amekuumba kwa kusudi

maalumu akiwa amekuwekea muda, majira na nyakati za

kutimiza hilio kusudi. Nilazima utambue mwisho

wako/hatima yako kwa sababu hautaishi milele duniani

kutimiza hilo kusudi.Biblia inasema;

“Maana nayajua mawazo ninayo wawazia ninyi, asema

BWANA, ni mawazo ya amani wala si mabaya, kuwapa

ninyi, tumaini siku zenu za mwisho” [Yer 29:11]

Tafsiri ya biblia ya King James Version (KJV) Habari njema

inasema hivi;

“Maana naijua mipango niliyonayo kwa ajili yako, mipango

ya kukupatia utajiri na sio majanga, mipango ya kukupeleka

kwenye hatima yako na tumaini lako.”

Maana yake Mungu amekusudia kukufikisha kwenye

hatima yako. Watu wengi wanafikiri hatima zao ziko mbele

yao. Lakini hatima yako haiko mbele yako, hatima yako iko

ndani yako nilazima ujue hatima yako ni nini. Kwa kufanya

hivyo itakusaidia kuwa na hamasa ya kutaka kufika

UHURU WA KWELI 78

unakotakiwa kufika. Jitiishe chini ya Roho Mtakatifu ili

akuonyeshe hatima yako (kusudi lako).

Namna ya kuushirikisha ufalme wa Mungu kwenye

maisha yako kwa njia ya sadaka ili utende kazi kwa niaba

yako.

Ufalme wa Mungu.

Ni mfumo wa maisha wa kimbingu wenye utaratibu na

kanuni ambao unaweza kuratibiwa duniani kama mbinguni.

Ndio maana Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kuomba

kuhusu ufalme wa mbinguni hivi;

“Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako

litukuzwe, Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa

duniani kama huko mbinguni. Utupe leo riziki yetu

Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo

wadeni wetu. Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule

mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu,

hata milele. Amina” [Math 6:9-13]

Moja ya jambo muhimu sana kulifahamu ni kwamba Yesu

aliwafundisha wanafunzi wake kuomba ufalme wake kuja.

Yesu alijua ufalme wa Mungu (mfumo wa maisha wa

UHURU WA KWELI 79

kimbingu) unaweza pia kuwa dhahiri duniani. Na ufalme wa

Mungu ukiwa dhahiri duniani basi huwa unafurikisha na

mahitaji ya kila siku (kula, kunywa, kuvaa, ulinzi). Kuna

muhimu mkubwa wa kuushirikisha ufalme wa Mungu

wakati wote, unapoushirikisha ufalme wa Mungu moja kwa

moja unaruhusu ufalme wa Mungu kutenda kazi kwa niaba

yako.

Moja ya njia inayoweza kuushirikisha ufalme wa Mungu

kutenda kazi kwa aniaba yako ni sadaka. Sadaka inaweza

kutumika kuushirikisha ufalme wa Mungu kutenda kazi kwa

aniaba yako. Ufalme wa Mungu ukitenda kazi kwa aniaba

yako uwe na uhakika unakuondoa kwenye mfumo tegemezi

wa uchumi wa duniani na kukuweka kwenye uchumi wa

mfumo wa ufalme wa Mungu. Inawezekana ukawa

unafanya biashara ndogo, au kipato chako cha mshahara ni

kidogo lakini ukiamua kuuhusisha ufalme wa Mungu

kutenda kazi kwa aniaba yako.Unaweza ukawa na kipato

kidogo au mshahara mdogo lakini ukaweza kufanya mambo

makubwa zadi yasiyoendana na kipato chako au mshahara

wako. Sadaka ni njia nzuri ya kuuhusisha ufalme wa Mungu

kutenda kazi kwa aniaba yako.

UHURU WA KWELI 80

Sadaka ni nini?

Ni kitu chochote kinachotolewa madhabahuni kukusaidia

kuuhusisha ufalme wa Mungu kutenda kazi kwa aniaba

yako. Kuna sadaka za aina nyingi kuna sadaka ya mda,

sadaka ya mwili, sadaka mali au fedha. Vitu vyote hivi

unaweza kuvitumia kutenda kazi kwa aniaba yako. Katika

agano jipya watu walihimizwa kutoa sadaka kwa moyo wa

kupenda wala si kwa kulazimishwa. Tutaangalia aina moja

ya sadaka (sadaka ya fedha) jinsi inavyoweza kuuhusisha

ufalme wa Mungu kwa aniaba yako.

Zingatia yafuatayo kabla ya utoaji wako wa sadaka (ya

fedha) kabla ya kutoa;

i. Mungu anautazama moyo kabla ya utoaji wako wa

sadaka

Hakikisha unauelewa sahihi kwenye moyo wako kabla ya

utoaji wa sadaka. Mungu anautazama moyo kwanza ili

uweze kupata matokeo sahihi ya utoaji wa sadaka yako.

Biblia inatuonyesha kuwa kuna watu walikuwa na sadaka

nzuri lakini kwa sababu mioyo yao haikuwa na ufahamu

sahihi kuwa Mungu anahitaji nini. Mungu alikataa sadaka

zao na aliwakataa na wao wenyewe. Mfano Mfalme Sauli

Mungu alikataa sadaka yake na alimkataa yeye kukaa

UHURU WA KWELI 81

kwenye nafasi yake kwasababu hakuwa na utii. Samweli

alimwambi; kutii ni bora kuliko dhabihu (1Samw 15:22).

Kwahiyo ni muhimu moyo wako kuwa na ufahamu sahihi ili

sadaka yako iweze kuleta matokeo ndio maana

imeandikwa;

“Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana

wanadamu hutazama sura ya nje, bali Bwana huutazama

moyo” [1Samw 16:7b]

Katika utoaji wa sadaka katika kipindi tulichonacho cha

agano jipya, ni tofauti kabisa na utoaji wa sadaka wa kipindi

cha agano la kale. Na ili usiweze kuleta mgogoro na Mungu

katika utoaji wako wa sadaka lazima uzingatie yafutayo:-

Hatutoi sadaka ili tubarikiwe [tulishabarikiwa

kwa baraka zote za rohoni katika Kristo Yesu (Efe

1:3)]

Hatutoi sadaka ili tuwe wenye haki [sisi tayari

tumehesabiwa haki kwa kumwamini Yesu Kristo

(Rum 8:29-30, Rum 5:17, 2Kor 5:21)

Hatutoi sadaka ili tuwe na kibali mbele za Mungu

(Tulishapata kibali kwa kumwamini Yesu Kristo)

Hatutoi sadaka ili tuwe watakatifu au watu

wema (Tulishafanywa kuwa watakatifu watu

wema tusio na mawaa kwa kumwamini Yesu

Kristo)

UHURU WA KWELI 82

Hatutoi sadaka ili tuwe matajiri tulishafanywa

matajiri kwa kumwamini Yesu Kristo (2Kor 8:9)

Sadaka katika sura ya agano jipya inatolewa kwaajili ya

nini?

Tunatoa sadaka kwaajili ya yafuatayo:-

Tunatoa sadaka ili kuwatunza watumishi

Tunatoa sadaka kwaajili ya wahitaji (yatima,

wajane, wagonjwa, wasiojiweza)

Sadaka inatolewa kwaajili ya huduma ya injili

Kazi zote hizi za sadaka sio kazi yetu ni kazi ya Mungu

mwenyewe. Mungu mwenyewe anawajibika kuwatunza

watumishi, kuwatunza wahitaji na kushughulika na kazi

yake ya injili. Ukiwa umezaliwa mara ya pili (uliyeokoka)

hata usipotoa sadaka huwezi kulaaniwa kwa sababu tayari

Yesu Kristo alikuwa ni sadaka kamilifu ambayo ni sadaka

aliitoa Mungu inayomridhisha. Na aliitoa kwaajili yetu ili

kusudi Kristo afanyike laana kwa aniaba yetu. Hatubarikiwi

kwa sababu tunatoa sadaka tunabarikiwa kwa sababu ya

kile alichofanya Yesu Kristo msalabani kwaajili yetu. Kwa

sababu hiyo hakuna namna kilichobarikiwa kinaweza kuwa

laana. Ndio maana Mungu alimkatalia Balaamu kulaani

UHURU WA KWELI 83

wana wa Israeli kwasababu Mungu alikuwa tayari

ameshawabarikia (Hes 22:12).

Kwa maana hiyo haimaanishi kuwa hakuna haja ya kutoa

sadaka. Kila imani ina hatua zake, Mungu anatusisitiza kuwa

tumebarikiwa katika Kristo ili tusipambane kutafuta

kubarikiwa. Hata hivyo hakuna jambo sasa tunaweza

kufanya likazidi sadaka kamilifu ya Yesu Kristo iliyotolewa

kwaajili yetu. Ndio maana maandiko yanasema Yesu Kristo

alitolewa sadaka mara moja kwaajili ya dhambi zetu

(zilizopita, zilizopo na zijazo), na wokovu wetu. Neno hili

wokovu limetokana na neno la kigiriki “sozo” ambalo

lilikuwa na maana ya ukombozi, ustawi (mafanikio) na

uponyaji. Kwahiyo Kristo alitolewa sadaka kamili kwaajili ya

dhambi zetu kikamilifu, ustawi (mafanikio) kamili na

uponyaji kamili. Ndio maana imeandikwa;

“mkaenende katika upendo, kama Kristo naye

alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na

dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato” [Efe 5:2]

Kristo ni sadaka kamilifu iliyotolewa kutufanikisha katika

kila eneo kwenye maisha yetu. Ukitoa kitu chochote hali

kwamba unataka kubarikiwa au kufanikiwa lazima utaleta

mgogoro na Mungu, na kwa namna hiyo hautapata

matokeo sahihi.

UHURU WA KWELI 84

Kwanini ni muhimu sana kutoa sadaka kama tumesha

barikiwa?

Kumbuka nimekwambia kuwa sio kazi yako kuwatunza

watumishi ni kazi ya Mungu. Sio kazi yako kuwatunza

wahitaji ni kazi ya Mungu, sio kazi yako kuhudumia injili ni

kazi ya Mungu. Sasa ukianza kuhudumia watumishi,

kuwatunza wahitaji na kuendeleza kazi ya injili kwa sadaka

yako unasimama kwenye nafasi ya Mungu. Kwa namna hiyo

unakuwa umeuhusisha ufalme wa Mungu na kwa namna

hiyo ufalme wa Mungu utaanza kutenda kazi katika

unachokifanya kwa aniaba yako. Na kwa namna hiyo

utaanza kuona kula, kunywa, kuvaa, malazi, ulinzi na

mahitaji yako vikimiminwa kwenye maisha yako.

Imeandikwa hivi;

“Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa

kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme

mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; kwa

maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na

kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;

nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja

kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia. Ndipo wenye

haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona

una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha? Tena ni

lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi,

tukakuvika? Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au

UHURU WA KWELI 85

kifungoni, tukakujia? Na Mfalme atajibu, akiwaambia,

Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa

hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi” [Math

25:34-40]

Tuangalie jinsi mama mjane wa Serepta aliutumikia

ufalme wa Mungu na ufalme wa Mungu ukafanya katika

eneo la uchumi kwa niaba yake.

“Basi, akaondoka, akaenda Sarepta, hata alipofika langoni

pa mji, kumbe! Mwanamke mjane alikuwako akiokota kuni;

akamwita, akamwambia, Niletee, nakuomba, maji kidogo

chomboni nipate kunywa. Alipokuwa akienda kuleta,

akamwita akasema, niletee, nakuomba, kipande cha mkate

mkononi mwako. Naye akasema kama BWANA, Mungu

wako aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na

mafuta kidogo katika chupa; name ninaokota kuni mbili

niingie nijipikie mimi na mwanangu, tuule tukafe. Eliya

akamwambia, Usiogope; enenda ukafanye kama

ulivyosema; lakini unifanyie kwanza mkate; kisha ujifanyie

nafsi yako na mwanao. Kwa kuwa BWANA, Mungu wa

Israeli, asema hivi, Lile pipa la unga halitapunguka, wala ile

chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile BWANA

atakapoleta mvua juu ya nchi. Basi akaenda, akafanya

kama alivyosema Eliya; nayeye mwenyewe, na Eliya, na

nyumba yake, wakala siku nyingi. Lile pipa la maji

UHURU WA KWELI 86

halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawa

sawa na neno la BWANA alilonena kwa kinywa cha Eliya”

[1Falme 17: 10-16]

Mwanamke mjane alikuwa amekata tamaa na hali yake

mbaya ya uchumi kiasi cha kumlevya. Lakini alipoamua

kuutumikia ufalme wa Mungu ufalme wa Mungu

ulishughulikia uchumi wake. Kumbe unapohusika

kuwahudumia wahitaji kwa sadaka yako, watumishi wa

Mungu, huduma ya injili hayo yote unamfanyia Mungu, na

kwa namna hiyo unakuwa umeushirikisha ufalme wa

Mungu kutenda kazi kwa niaba yako.

Namna gani ya kuitumia sadaka kuuhusisha ufalme wa

Mungu kutenda kazi kwa niaba yako?

Tumia sadaka yako kama mbegu. Kumbuka unapotoa

sadaka yako moja kwa moja unauhusisha ufalme wa Mungu

kukusimamia na kutenda kazi kwa aniaba yako. Ni agizo la

Mungu tangu Mwanzo Mungu alipomuagiza Adamu kuilima

bustani katika kila mche Mungu aliweka na mbegu ndani

yake (Mwa 1:11-12). Hata baada ya gharika, bado Mungu

aliendelea kuweka utaratibu wa kupanda na kuvuna.

Imeandikwa;

UHURU WA KWELI 87

“Muda nchi idumupo, majira ya kupanda, na mavuno,

wakati wa baridi na wakati wa hari, wakati wa kaskazi na

wakati wa kusi, mchana na usiku, havitakoma” [Mwa 8:22]

Mungu aliamuru kuwa majira ya kupanda na kuvuna kuwa

havitakoma. Kupanda na kuvuna vipo katika muendelezo,

ndio maana ili uweze kuvuna lazima upande. Unaweza

kuanza kutumia fedha yako kupanda, ili uweze kuvuna.

Kumbuka mbegu ziko za aina nyingi, kila mbegu

inayopandwa inakusudi lake. Mbegu ya mahindi lazima

ilete mazao ya mahindi. Mbegu ya harage lazima izae

maharage, kadhalika pia katika mbegu nyingine. Kiwango,

ubora, shamba, wakati na kiasi cha mbegu ni msingi wa

kujua matokeo ya hiyo mbegu itakuwaje. Kabla hujapanda

mbegu lazima ukusudie upandaji wako wa mbegu, na kiasi

cha mbegu kiendane na matokeo unayoyatarajia. Ndio

maana imeandikwa;

“Kwa habari za kuwahudumia watakatifu sina haja ya

kuwaandikia. Maana najua utayari wenu, ninaojisifia kwa

ajili yenu kwa Wamakedonia, kwamba Akaya ilikuwa tayari

tangu mwaka mzima; na bidii yenu imewatia moyo wengi

wao. Lakini naliwatuma hao ndugu, ili kujisifu kwetu kwa

ajili yenu kusibatilike katika jambo hili; mpate kuwa tayari,

kama nilivyosema; kusudi, wakija Wamakedonia pamoja

nami, na kuwakuta hamjawa tayari, tusije tukatahayarika

sisi, (tusiseme ninyi), katika hali hiyo ya kutumaini. Basi

UHURU WA KWELI 88

naliona ya kuwa ni lazima niwaonye ndugu hawa

watangulie kufika kwenu, na kutengeneza mapema karama

yenu mliyoahidi tangu zamani, ili iwe tayari, na hivi iwe

kama kipawa, wala si kama kitu kitolewacho kwa unyimivu.

Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba;

apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu. Kila mtu na

atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni,

wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye

kwa moyo wa ukunjufu. Na Mungu aweza kuwajaza kila

neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna

siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema; kama

ilivyoandikwa, Ametapanya, amewapa maskini, Haki yake

yakaa milele Na yeye ampaye mbegu mwenye kupanda, na

mkate uwe chakula, atawapa mbegu za kupanda na

kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu” [2Kor

9:1-10]

Ilikuwa ni utaratibu wa kanisa la Korintho kuwatunza

watumishi, ndio mana Paulo anasema kwa habari ya

kuwahudumia watakatifu sina haja ya kuwaandikia. Paulo

anaendelea kusema apandaye haba atavuna haba,

apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu. Anasema na

kila mtu atende kama alivyokusudia moyoni mwake, maana

yake katika kupanda lazima uazimie matokeo unayoyataka

katika kupanda kwako. Ndio maana anasema yeye

apandaye mbegu atawapa mbegu na kuzizidisha naye

ataongeza mazo ya haki yenu. Kama vile Mungu

UHURU WA KWELI 89

anavyotujua kuwa sisi ni wenye haki wake vivyo hivyo

anasema katika kupanda atatuzidisha na kuongeza mazao

ya haki yetu.

Mambo ya kuambatanisha (kuzingatia) ili sadaka yako

iweze kuuhusisha ufalme wa Mungu kwa niaba yako

kikamilifu:

Imani

Usahihi wa sadaka kama mbegu

Mahali pa kutoa/kupanda (shamba/madhabahu)

Neno la Kristo

Wakati wa kutoa

ii. Toa sadaka yako kwa Imani.

Sadaka inapotolewa kama mbegu, imani ni sehemu ya kiini

cha mbegu. Ili uweze kupata matokeo nilazima unapoamua

kutoa sadaka yako kama mbegu itoe ukiwa umeunganisha

na imani ya kujua kuwa utapokea matokeo unayoyatarajia.

Biblia inatueleza kuwa;

“kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani” [Gal 3:11b]

UHURU WA KWELI 90

Maandiko yanaonyesha pia;

“Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye

akisita-sita, roho yangu haina furaha naye” [Ebr 10:38]

Pia maandiko yanaendelea kutuambia;

“Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana

mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye

yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao” [Ebr

11:6]

Ili uweze kupata matokeo unayoyatarajia katika utoaji wako

wa sadaka kama mbegu hakikisha unaambatanisha imani

yako katika utoaji wako wa hiyo sadaka. Kujua kuwa uko

katika hali ya imani katika utoaji wako wa sadaka ni rahisi.

Utajua uko katika imani unapotoa hiyo sadaka endapo

utaona tayari unachokitaka kutoka kwa Mungu kimefanyika

au kimetokea tayari hata kama hujakishuhudia kwa macho

ya damu na nyama. Unapotoa hiyo sadaka yako

unapoambatanisha na imani yaani kiini cha mbegu

unaruhusu matokeo ya upatikanaji wa matokeo wa hiyo

mbegu yawe halisi mwilini.

Kumbuka huwezi kutenganisha mbegu na kiini. Gamba la

mbegu ni sadaka yako unayoitoa imani ni kiini Kwahiyo ili

hiyo mbegu iote lazima uweze kuambatanisha vyote viwili.

UHURU WA KWELI 91

Kama hutafanya hivyo utakuwa umeharibu mbegu yako na

hutaona matokeo. Ni sawa sawa unataka kupanda mbegu

za mahindi halafu kabla hujapanda unaanza kuzitolea

mbegu viini. Uwe na uhakika hazitaota na utakuwa

umepoteza sadaka yako bure. Kwahiyo hakikisha unatoa

sadaka hiyo kwa imani.

Unaposhughulika na upandaji wako wa mbegu kwa njia ya

sadaka unauruhusu ufalme wa Mungu kutenda kazi kwa

aniaba yako (kushughulika na mahitaji yako). Kula, kunywa,

kuvaa, malazi, ulinzi, sasa unapoamua kutoa sadaka yako.

Inaweza kuwa unapata msukumo wa kupeleka sadaka yako

wahitaji (yatima, wajane, wagonjwa), watumishi, au

kwaajili ya huduma ya injili. Kwa namna hiyo ndivyo

unaugusa moyo wa Mungu na ukigusa moyo wa Mungu

moja kwa moja unakuwa umeuruhusu ufalme wa Mungu

kutenda kazi kwa aniaba yako.

Inawezekana unahitaji nyumba ya gharama fulani, gari ya

gharama fulani, unataka kufungua kampuni kwa gharama

fulani, unataka kufungua kiwanda, au jambo lolote

unalotaka kulianzisha. Hakikisha Unapotoa sadaka yako

kama mbegu adhimia kuwa ninapotoa hii sadaka kwaajili ya

ufalme wa Mungu. Ninatarajia hiki ninachokitaka

nimekipokea, inawezekana hauna uwezo kabisa wa kujenga

hiyo nyumba, kuwa hilo gari, kampuni au kiwanda cha

gharama unayohitaji. Ukitoa hiyo sadaka na ukaamini

UHURU WA KWELI 92

umeshapata matokeo unaruhusu kile kiini cha imani yako

katika hiyo mbegu kilete matokeo.

Usahihi wa sadaka kama mbegu.

Usahihi wa sadaka yako unatokana na muongozo wa Roho

Mtakatifu au msukumo wa matarajio unayoyataka

kuyaona. Kumbuka usahihi wa sadaka yako kama mbegu

hautokani tu na jinsi unavyoona inafaa bali pia kwa uongozi

wa Roho Mtakatifu. Ndio maana biblia inashuhudia kuwa;

“Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba

atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na

kuwakumbusha yote niliyowaambia” [Yoh 14:26]

Kwa kuwa sisi tulioamini Roho Mtakatifu yupo kutufundisha

ni muhimu kumsikiliza ushauri wake katika utoaji wa sadaka

ili tuweze kupata matokeo sahihi. Roho Mtakatifu anaweza

kukupa msukumo wa kutoa hiyo sadaka yako kwa wahitaji,

watumishi au huduma ya injili. Kumbuka kusikiliza juu ya

kiwango anachokwambia utoe. Kwa mfano unaweza ukawa

unapata msukumo wa kutoa sadaka kwa yatima. Lakini sasa

utajuaje kuwa hiki ndio kiwango sahihi cha kupeleka huko?

Utajua kwa kusikiliza ushauri anaokupa Roho Mtakatifu.

Kwa mfano Roho Mtakatifu anaweza kukwambia peleka

dola mia moja au dola hamsini. Aidha kama hujaelewa vizuri

namna ya kumsikiliza Roho Mtakatifu anaweza kuzungumza

UHURU WA KWELI 93

na wewe kwa ishara. Ishara rahisi sana anaitumia Roho

Mtakatifu ni amani. Ndio maana imeandikwa na amani ya

Kristo iamue mioyoni mwenu (Kol 3:15a).

Unapopata msukumo wa kupeleka sadaka yako kwa

yatima. Ukitaka kupeleka dola ishirini husikii amani, dola

hamsini husikii amani, mpaka unafikisha dola mia ndio

unajisikia amani. Ukiona hivyo ipeleke hiyo sadaka ni sahihi,

kwa sababu amani ya Kristo imeamua hivyo. Au kinyume

chake ni hivi unaweza ukawa unapeleka kiwango kikubwa

kuliko vile inavyotakiwa. Huenda unataka kupeleka dola

mia mbili unakosa amani kumbe Roho Mtakatifu anataka

upeleke dola mia moja hiyo nyingine aidha uifanyie kitu

kingine au upande mahali pengine. Ni muhimu kumsikiliza

Roho Mtakatifu, msukumo wa ndani na amani iliyo ndani

yako.

Kumbuka matokeo ya sadaka yako kama mbegu

yanategemea sana usahihi wa hiyo mbegu. Ndio maana

imeandikwa apandaye haba atavuna hapa apandaye kwa

ukarimu atavuna kwa ukarimu. Fikiria unashamba la heka

moja halafu unambegu sado moja. Uwe na uhakika utapata

matokeo ambayo hukuyatarajia , mazao yako yatakuwa

kwa uchache sana. Ushauri wa Roho Mtakatifu na amani ya

Kristo vinamchango mkubwa sana kukujulisha usahihi wa

sadaka unayotoa.

UHURU WA KWELI 94

iii. Mahali pa kutoa/kupanda (madhabahu/shamba)

Zingatia kuwa sio kila mbegu inaweza kuota mahali popote.

Kila mbegu ina mahali pake sahihi kwa kuota mbegu ya

mahindi sio katika kila udongo,ardhi au shamba inaota.

Kadhalika pia mbegu ya karanga na mbegu za aina nyingine

zinaota na kustawi vizuri katika eneo sahihi. Peleka sadaka

yako mahali ambapo unaelekezwa na Roho Mtakatifu

upeleke au mahali unapojisikia amani. Aidha wewe

mwenyewe unaweza kutamani kutoa sadaka yako. Ili

uweze kupanda hiyo mbegu mahali sahihi zingatia mambo

mawili ya msingi. Uhai wa madhabahu unayopelekea na

imani kuhusu hiyo madhabahu, Je! Imani ya hiyo

madhabahu unayotaka kupeleka wana imani na kupanda na

kuvuna? Au hiyo madhabahu ina uhai? Ukipeleka kwenye

madhabahu ambayo inakosa hivi vitu viwili sadaka yako

itapata shida sana kuota.

Kumbuka kuwa biblia inatueleza wazi kuwa chuma hunoa

chuma (Mith 27:17a). Fikiria unapeleka sadaka kwenye

madhabahu isiyoamini kuhusu ustawi wa sadaka yako. Hiyo

madhabahu moja kwa moja haina uhai na kwa namna hiyo

utakuwa unatoa sadaka yako kwenye shamba kame. Na

kwa namna hiyo sadaka yako kamambegu itakauka

haitaota, na kwa namna hiyo hautaona matokeo ya hiyo

sadaka. Kwa mfano unataka kutoa sadaka yako kwa

mtumishi fulani au kusapoti kazi ya injili fulani Je, huyo

UHURU WA KWELI 95

mtumishi au hiyo huduma ina imani juu ya ustawi wa hiyo

sadaka yako.

iv. Neno la Kristo.

Neno la Kristo ni ulinzi wa sadaka yako kama mbegu . Neno

la Kristo linasimamia ahadi ambayo imekwisha kuwako.

Kumbuka kila kitu Yesu Kristo alishafanya pale msalabani

kwa ajili yetu. Ili tuweze kuuishi huo uhalisia wa kupokea na

kuuishi katika macho ya damu na nyama lazima

tuambatanishe na neno lake. Ni sawa na kumwambia

Bwana kuwa hii sadaka siitoi kwa sababu inastahili kuliko

wewe. Ila kwa sababu ya kile umekifanya tayari kwenye

neno lako kwaajili yangu. Kumbuka imani yaani kiini cha

mbegu hakiwezi kustahimili pasipokuwa na neno.

Biblia inatueleza umuhimu mkubwa wa kuwa na neno la

Kristo tunapopanda. Tuangalie mfano huu;

“Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake; naye

alipokuwa akizipanda, nyingine zilianguka karibu na njia,

zikakanyagwa, ndege wa angani wakazila. Nyingine

zikaanguka penye mwamba; zilipoanza kumea zikakauka

kwa kukosa rutuba. Nyingine zikaanguka kati ya miiba, na

miiba ikamea pamoja nazo ikazisonga. Nyingine

UHURU WA KWELI 96

zikaanguka penye udongo mzuri; zikamea, zikazaa moja

kwa mia. Alipokuwa akinena hayo alipaza sauti akisema,

Mwenye masikio ya kusikilia, na asikie. Wanafunzi wake

wakamwuliza, Maana yake nini mfano huo? Akasema,

Ninyi mmepewa kuzijua siri za ufalme wa Mungu; bali

wengine kwa mifano, ili wakiona wasione, na wakisikia

wasielewe.

Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu.

Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi

akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na

kuokoka. Na wale penye mwamba ndio wale ambao

wasikiapo hulipokea lile neno kwa furaha; nao hawana

mizizi, huamini kitambo kidogo, na wakati wa kujaribiwa

hujitenga. Na zilizoanguka penye miiba ni wale waliosikia,

na katika kuenenda kwao husongwa na shughuli na mali,

na anasa za maisha haya, wasiivishe lo lote. Na zile penye

udongo mzuri, ndio wale ambao kwa unyofu na wema wa

mioyo yao hulisikia neno, na kulishika; kisha huzaa

matunda kwa kuvumilia” [Luk 8:5-15]

Biblia inaweka wazi kuwa kati ya moja ya siri za ufalme wa

Mungu ni kupanda na kuvuna. Baada ya Yesu kuulizwa na

Wanafunzi wake maana yake nini mfano huo? Yesu

akawajibu kuwa ninyi mmepewa kuzijua siri za ufalme wa

Mungu lakini wengine hawazijui ndio maana alisema nao

UHURU WA KWELI 97

kwa mifano kusudi wakiona wasione na wakisikia wasisikie.

Sasa tulio wana wa ufalme (tuliookoka) Mungu ametujalia

neema ya kuzijua siri za ufalme wa Mungu moja ya siri hizi

ni kupanda na kuvuna. Kupanda ndani ya ufalme wa Mungu

na kuvuna ndani ya ufalme wa Mungu. Na moja ya mhimili

anaotaja katika kupanda kwenye ufalme wa Mungu ni neno

la Mungu.

Ili uweze kuisimamia sadaka kama mbegu uliyopanda

lazima uweze kusimamia neno. Ambalo linakuhakikishia

uhalali wa kumiliki hicho ulichonacho katika Yesu Kristo ili

kiweze kuleta matokeo. Hii itakusaidia kuimwagilia mbegu

yako na kuipalilia mpaka ilete matokeo kwa hakika ulikuwa

unayatarajia. Yesu aliwafunulia wanafunzi wake juu ya

mambo yanayoweza kupoteza uhakika wa ile mbegu kuleta

matokeo. Yesu anaanza na kusema Shetani anaweza

kuliondoa lile neno lililoko ndani yako na kwa namna hiyo

anasababisha usiamini na kuokoka. Kwa mfano unaweza

ukawa umepanda sadaka yako na ulitarajia ilete matokeo,

huenda ulitamani baada ya miaka kadhaa, mwaka mmoja

au miezi au siku kadhaa. Baada ya hapo unaona bado huoni

matokeo, ikifika kwenye hiyo hali ni rahisi sana kukata tama

na kuona sadaka uliyotoa kama mbegu ulipoteza, na kwa

namna hiyo Shetani analiondoa lile neno la ahadi uliopandia

sadaka yako. Kwa sababu hiyo imani yako inaondoka na

kwa namna hiyo tayari ile mbegu inakuwa imeshaharibika,

kwahiyo huwezi kuona matokeo.

UHURU WA KWELI 98

Kwahiyo, ili usimpe nafasi ya kuondoa imani yako juu ya

sadaka kama mbegu uliyopanda kwa ajili ya matarajio

unayoyataka, kubali kuambatana na neno la Mungu bila

kujali matokeo uliyoyatarajia unaona yamechelewa. Yesu

anaendelea kusema kuna mambo mengi yanayosababisha

usiambatane na neno. Jambo lingine ni wale ambao

wanaamini kupitia neno na wanalipokea kwa furaha baada

ya muda kitambo kifupi wanajitenga. Lile neno linakuwa

halina mizizi wanashindwa kupata matokeo. Yesu anasema

wako wengine ambao wanalisikia neno lakini kwa sababu

wanasongwa na shughuli, mali na anasa wanashindwa

kuivisha. Hali hiyo inasababisha wanashindwa kupata

matokeo sahihi juu upandaji wao na wanashindwa kuivisha

kwa sababu wanasongwa na mambo ya duniani. Ni kama

vile unatoa sadaka yako halafu watu wengine wanaanza

kukusonga kuwa umepoteza sadaka yako ili usiamini na kwa

namna hiyo unashindwa kuivisha.

Katika ule mstari wa 15, Biblia Tafsiri ya Habari Njema

inasema hivi;

“Na zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ndio watu wale

wanaolisikia neno, wakalizingatia kwa moyo mwema na

wautii. Hao huvumilia mpaka wakazaa matunda”

UHURU WA KWELI 99

Tafsiri ya Biblia ya Neno inasema hivi:

“Lakini zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo mzuri ni

mfano wa wale ambao hulisikia neno la Mungu na kulishika

kwa moyo mnyoofu wa utii, nao kwa kuvumilia kwingi

huzaa matunda”

Biblia inatusisitiza sana kumbatana na neno, usijaribu hata

kidogo kuacha kuambatana na neno kwa sababu unaona

umechelewa kuona matokeo. Yesu alisema kwa wale

wanaolishika neno na kulizingatia kwa moyo mwema na wa

utii, huvumilia mpaka kuzaa kwingi matunda. Ukiambatana

na neno sawa sawa katika upandaji wa sadaka yako

ukalizingatia kwa uvumilivu lazima utapata matokeo.

Usiruhusu kitu chochote kikachangia katika kuififisha imani

yako kama ni Shetani, watu wanokuzunguka wanakukatisha

tama juu ya upandaji wa sadaka yako. Wakumbushe kwa

njia ya neno kuwa bado Mungu anaendelea kushughulika

na sadaka kama mbegu niliyoipanda kwake. Kwa uvumilivu

wako wa kusubiri na kuendelea kuipalilia sadaka yako na

kuimwagilia maji utaona kuzaa matunda kwingi sana kupitia

hiyo sadaka. Ndio imeandikwa;

“Maana kama vile mvua ishukavyo, na theluji, kutoka

mbinguni, wala hairudi huko; bali huinywesha ardhi, na

kuizalisha na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, na

mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu,

litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure, bali

UHURU WA KWELI 100

litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo

yale niliyolituma” [Isa 55:10-11]

Kumbuka kuambatana na neno katika utoaji wa sadaka

yako kama mbegu. Neno lilitoka katika kinywa cha Mungu

lazima litimize mapenzi ya Mungu na kutimiza yale neno

limetumwa.

v. Wakati wa kutoa sadaka.

Wakati wa kutoa sadaka yako ni wakati ambao umepewa

maelekezo na Roho Mtakatifu wa kupeleka, au wakati

unajisikia amani kupeleka, kumbuka wakati una umuhimu

sana katika kuchangia matokeo ya hiyo sadaka. Mfano

umeambiwa na Roho Mtakatifu wakati huu peleka sadaka

kiasi fulani kwa yule mjane. Ujue ni wakati sahihi wa

kupeleka, huenda huo muda ndio wakati huyo mjane

anauhitaji na hiyo sadaka. Ukiwa na utii ndani yako wa

kutoa wakati huo unaruhusu sadaka yako kuleta matokeo.

Sio kila mbegu inayopandwa hata kama ni sahihi na

imepandwa kwenye shamba sahihi inaota kila wakati. Ndio

maana mbegu nyingi zinapandwa wakati wa masika kusudi

ziweze kuota kwa urahisi. Zingatia kutoa sadaka yako kwa

wakati ili uweze kupata matokeo inavyostahili. Ikiwa Roho

Mtakatifu au amani ya kristo inakuongoza kupeleka wakati

huo, zingatia kutoa wakati huo ili upate matokeo chanya.

UHURU WA KWELI 101

Tathmini kupitia maswali kutoka katika Sura ya Tatu

1: Kutokana na sura hii, asili ni nini?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

2: Yesu alikuja ili kuturejesha kwenye asili yetu. Taja hiyo

asili

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

3: Namna gani ya kuishi ndani ya Ufalme wa Mungu?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

4: Ili uweze kuishi ndani ya ufalme wa Mungu kwa ufanisi

unahitaji mambo yafuatayo:-

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

UHURU WA KWELI 102

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………....

(iii)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

(iv)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

5: Taja jambo linaloweza kuuhusisha ufalme wa Mungu

kwa vitendo

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

6: Taja vipaumbele ambavyo Mungu anaviangalia kabla ya

utoaji wako wa sadaka

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………....

(iii)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

(iv)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

UHURU WA KWELI 103

(v)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

(vi)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

7: Taja sababu za utoaji wa sadaka katika sura ya agano

jipya

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

(iii)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

8: Kwanini ni muhimu kutoa sadaka tuliobarikiwa katika

Kristo Yesu?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

9: Taja viambatanishi vya utoaji wa sadaka yako kama

mbegu katika sura ya agano jipya uli uweze kupata

matokeo sahihi

UHURU WA KWELI 104

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

(iii)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

(iv)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

(v)………………………………………………………………………………………

………………………………………

UHURU WA KWELI 105

SURA YA NNE

SIKUUMBWA KWA KUSUDI HILI

ungu alimuumba mwanadamu ili aweze kutawala

kila kitu duniani, ndio maana maandiko yanasema;

“Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa

sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa

angani na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye

kutambaa kitambaacho juu ya nchi” [Mwa 1:26]

Baada ya anguko mwanadamu yaani baada ya Adamu

kumwasi Mungu utawala ulichukuliwa na Shetani. Tangia

hapo mwanadamu aliishi ndani ya utumwa na kutawaliwa

na dhambi. Ashukuriwe Mungu ambaye alimtuma Mwana

wake wa pekee ili aje aurudishe utawala tuliopoteza

bustani ya Edeni ndio maana sentesi ya Kwanza kuisema

Yesu ilikuwa ni kwa habari ya ufalme. Marko aliandika hivi;

“Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Habari Njema ya Mungu,

akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu

umekaribia, tubuni na kuiamini injili” [Mark 1:14b-15]

Maana yake jambo la kwanza lililomleta Kristo ilikuwa ni

kurejesha ufalme wa Mungu. Yesu anasema katika

kuurejesha ufalme wake kuna kanuni mbili za kuufuata;

M

UHURU WA KWELI 106

Kutubu

Kuiamini injili

Kutubu na injili vikiambatana vinairejesha ufalme. Kutubu

kunabadilisha mtazamo lakini injili inamuokoa mtu. Ndio

maana Paulo alisema kwa ujasiri kwamba;

“siionei haya injili, kwasababu ni uweza wa Mungu uuletao

wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza na kwa

Myunani pia” [Rum1:16]

Ni injili pekee inayoweza kuleta ukombozi bila injili watu

wanaendelea kutenda dhambi, bila injili watu wanaishi

maisha ya umaskini, bila injili watu wanaishi maisha ya

utumwa.

Injili ni habari njema ya neema ya Yesu Kristo. Neema ni

upako wa msaada usiostahili, kibali cha kukubalika pasipo

kustahili. Paulo alishuhudia kuwa alikuwa akiihubiri habari

njema ya neema ya Mungu. Maandiko yanasema;

“Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa ni kitu cha thamani

kwangu kama kumaliza mwendo wangu wa huduma ile

niliyoipokea kwa Bwana Yesu, kuishuhudia habari njema ya

neema ya Mungu” [Mate 20:24]

Kumbe injili ni habari njema ya neema ya Mungu. Hakuna

mahali injili inashindwa kumtoa mtu. Ukiona kuna mahali

mtu anahubiriwa anashindwa kutoka ujue hiyo sio injili ni

UHURU WA KWELI 107

fundisho tu. Neema ya Mungu hakuna mahali ambapo

inafeli, ina nguvu ya kutawala dhambi, utumwa, umaskini.

Ukiwa ndani ya neema ya Mungu utatawala hakuna jambo

litashindikana kwenye maisha yako. Ndio maana Paulo

alishangaa sana kuona Wagalatia wameacha injili ya neema

ya Mungu na kugeukia injili ya namna nyingine. Maandiko

yanasema;

“Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye

aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya

namna nyingine” [Gal 1:6]

Wagalatia walihubiriwa injili ya neema ya Kristo lakini

wakarudi nyuma na kuanza kufuata mafundisho ya

matendo ya sheria. Paulo aliendelea kuwasisitiza Wagalatia

kuwa; “Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao

na kutaka kuigeuza injili ya Kristo. Lakini ijapokuwa sisi au

malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yoyote

isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe”

Anakazia alichoongea kwa msisitizo kuwa; Kama

tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye

yote akiwahubiri ninyi injili yoyote isipokuwa hiyo

mliyoipokea, na alaaniwe. Paulo anasema kwanini mtu

asipoihubiri injili ya neema ya Kristo alaaniwe. Paulo

anasema hivi;

UHURU WA KWELI 108

“Kwa maana, ndugu zangu injili hiyo niliyowahubiri,

nawajulisha ya kuwa siyo ya namna ya kibinadamu. Kwa

kuwa sikuipokea kwa mwanadamu wala sikufundishwa na

mwanadamu, bali kwa ufunuo wa Yesu Kristo” [Gal 1:6-12]

Kumbe injili ya neema ya Kristo haikuja kwa mafundisho ya

mwanadamu yoyote ndio maana Paulo anasema ni injili

aliyofunuliwa na Yesu Kristo. Injili isiyo ya matendo ya

sheria, ni injili ya kuitegemea na kuiamini neema ya Yesu

Kristo. Ndio maana Paulo aliwaambia Warumi siionei haya

injili kwasababu ni uweza wa Mungu uletao wokovu.

Neema ya Mungu haitegemei matendo ya mtu bali utendaji

wa Yesu Kristo na kazi aliyoifanya pale msalabani kwaajili

yetu. Paulo anasema hivi;

“Lakini ikiwa kwa neema haiwi kwa matendo tena, au hapo

isingekuwa neema” [Rum 11:6]

Kumbe neema ikiwa ni kwa matendo ni batili, neema

haihesabiwi kwa matendo kabisa, ikiwa inahesabiwa kwa

matendo ni ujira sio neema. Ujira ni mshahara anaoupata

mtu kutokana na kazi aliyoifanya. Neema ni zawadi

tuliyoipokea kutoka kwa Mungu iliyoachiliwa kwa njia ya

Yesu Kristo kupitia kazi yake aliyoifanya msalabani. Yohana

alishuhudia kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa,

neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo (Yoh

1:17).

UHURU WA KWELI 109

Ndio maana Paulo alikuwakumbusha Waefeso kuwa ni

neema ya Yesu Kristo ndiyo iliyotuokoa. Imeandikwa hivi;

“Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani;

ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha

Mungu; wala si kwa matendo mtu awaye yote asije

akajisifu” [Efe 2:8-9]

Wokovu tuliopewa kwa njia ya Yesu Kristo ni zawadi.

Zawadi ni jambo lolote unalopewa sio kwa sababu

umeomba au kwa sababu umefanya kwa juhudi zako.

Zawadi yoyote inayotolewa na mtu anakupa sio kwa sababu

ulifanya jambo fulani bali anakua ameamua kukupa bure.

Wokovu tulioupokea ulikuwa ni kwa neema. Hakuna

mwanadamu aliyestahili kuupokea kwa sababu wote

tulikuwa tumekosea kwa sababu ya mtenda dhambi mmoja

(Adamu). Ndio maana aliwaombea watu kwa neno la

neema ya Mungu, anasema hivi;

“Basi sasa nawaweka katika mikono ya Mungu, na kwa

neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa

urithi pamoja nao wote waliotakaswa” [Mate 20:32]

Neno la neema ya Mungu linaweza kuwajenga watu na

kuwapa urithi pamoja. Neno la neema ya Mungu linapojaa

ndani ya mioyo ya Mungu linajenga imani inayowasaidia

watu katika kuwajenga kuwapa urithi ulio katika Kristo

Yesu. Kama Paulo alivyowaandikia Warumi kuwa ili muweze

UHURU WA KWELI 110

kuwa na imani ya kuwajenga nilazima kusikia neno la Kristo;

imeandikwa ; Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia

huja kwa neno la Kristo (Rum 10:17). Kumbe hatuhitaji

kujijenga imani ndani yetu isipokuwa ni imani ya kusikia

neno la Kristo ambayo ni neema yake. Neema ya Kristo

inafunua urithi tulio nao ndani ya Kristo matendo ya sheria

yanafunua nafsi ya mtu mwenyewe. Ndio maana Paulo

anasema hiyo neema haikutokana na nafsi zetu.

Neema ya Mungu inataka wakati wote kumfunua Kristo

alilotenda msalabani kwaajili yetu. Nafsi zetu zinapenda

tujifunue wenyewe kwa ubora wa kazi zetu. Yesu alipokufa

msalabani ilikuwa ni mbadala wa sisi wenyewe. Yesu

anataka nafsi zetu zijazwe na picha yake ili tunapojitazama

tumuone yeye. Kwa hakika kuna mambo hatuwezi

kuyapokea au kuyafikia bila neema yake. Matendo yetu

mema yanashindwa kabisa kufikia kiwango cha kukubaliwa

na Mungu na kufikia kiwango ambacho Mungu anataka.

Ndio maana Kristo ilibidi afe msalabani ili tufanyike warithi

wa mambo yote aliyokuwa nayo kwaajili yetu. Waebrania

aliandika hivi;

“Maana agano la urithi lilipo, lazima iwepo mauti yake

aliyeifanya. Kwa maana agano la urithi lina nguvu

palipotukia kufa kwa mtu; kwakuwa halina nguvu kabisa,

akiwa yu hai yeye aliyelifanya” [Ebr 9:16-17]

UHURU WA KWELI 111

Na sisi tulifanyika kuwa warithi halali kwa sababu ya uzao

halali wa ahadi aliyopewa baba yetu Ibrahimu kupitia Yesu

Kristo.

“Na kwa kuwa ninyi ni wa Kristo, basi mmekuwa uzao wa

Ibrahimu, na warithio sawa sawa na ahadi” [Gal 3:29]

Neno la neema ya Kristo linaachilia kibali cha kuwa warithi

halali wa mambo yote aliyotupigania Kristo msalabani.

Mambo hayo ni kama vile:-

Kuishinda dhambi na kuitawala (Rum 6:14)

Kushinda umaskini (2 Kor 8:9)

Kushinda magonjwa (1 Pet 2:24)

Kufanywa wenye haki (2Kor 5:21)

Kufanywa washindi (Rum 8:37)

Kubarikiwa (Efe 1:3)

Tumefanyika wenye haki kwa sababu ya neema ya Kristo

Yesu.

Haki ni kibali cha kusimama mbele za Mungu. Agano la kale

liliwapa watu wachache kibali cha kusimama mbele za

Mungu, na ilikuwa kwa sheria. Hakuna mwanadamu yoyote

aliyekuwa anaruhusiwa kuingia kupeleka haja zake kwa

Mungu isipokuwa kuhani mkuu.

UHURU WA KWELI 112

Biblia inashuhudia kwamba; Lakini katika hema hiyo ya pili

kuhani mkuu huingia peke yake, mara moja kila mwaka;

wala si pasipo damu, atoayo kwaajili ya nafsi yake na kwa

dhambi za kutokujua za hao watu. Roho Mtakatifu

akionyesha neno hili, ya kwamba njia ya kupaingia

patakatifu ilikuwa haijadhihirishwa bado, hapo hema ya

kwanza ilipokuwa ingali ikisimama; Lakini Kristo akiisha

kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo mema

yatakayokuwapo, kwa hema iliyokubwa na kamilifu zaidi,

isiyofanyika kwa mikono, maana yake isiyo ya ulimwengu

huu, wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu

yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu,

akiisha kupata ukombozi wa milele (Rum 9:7-8, 11-12).

Yesu alipokufa msalabani aliachilia uhuru wa kila mmoja wa

kupaingia patakatifu pa patakatifu ambapo aliruhusiwa

kuhani mkuu wa kipindi cha agano la kale. Yesu ambaye ni

kuhani mkuu, mjumbe wa agano jipya, kupitia Yeye

aliachilia kibali cha kuingia patakatifu pa patakatifu, yaani

kibali cha kusimama mbele za Mungu. Ndio maana Mungu

alimtambulisha Yesu katika maeneo mawili eneo la kwanza

ni katika mto Yordani na eneo la pili ni katika mlima mrefu

alipoenda kuomba na Petro, Yakobo na Yohana (math 17:1-

5). Katika maeneo yote sauti ilisikika kutoka mbinguni

ikisema;

UHURU WA KWELI 113

“Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa

naye; msikieni yeye” [Math 3:16-17, 17:5]

Mstari huu katika Tafsriri ya biblia ya KJV ametumia neno

“well pleased” yaani niko radhi naye. Mungu akituona

anamuona Kristo ndani yetu na kwa huyo tunapata haki ya

kusogea mbele za Mungu na kuzungumza naye.

Pazia la hekalu lilipasuka vipande viwili kwa ishara ya

kuonyesha kuwa kila mmoja ana uhuru wa kupaingia

patakatifu pa patakatifu na kuwa na haki ya kusema na

Mungu. Maandiko yanasema;

“Naye Yesu akiisha kuipaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa

roho yake. Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande

viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba

ikapasuka” [Math 27:50-51]

Kupasuka kwa pazia la hekalu kuliashiria uhuru wa kila

mmoja kumfikia Mungu. Katika agano la kale ilikuwa

haiwezekani kabisa mwenye dhambi kukubaliwa mbele za

Mungu na kusamehewa. Katika agano jipya Mungu

anamtafuta mtu aliye mwovu, mwenye dhambi ili amfanye

mtakatifu. Agano la kale lilikuwa haliruhusu kabisa mtu

aliye mwovu, mwenye dhambi kuingia hata kwenye

nyumba ya ibada.

Ilikuwa ni kujitaksa kwanza kabla ya kusogelea uwepo wa

Mungu. Ndio maana kuhani mkuu wa agano la kale ilikuwa

UHURU WA KWELI 114

ni lazima ajitakase kwanza kabla hajaingia patakatifu pa

patakatifu. Agano jipya tumepewa neema kila mmoja

anaweza kumwendea Mungu jinsi alivyo na Mungu

mwenyewe akamfanya kuwa mtakatifu hi ni neema ya

ajabu sana.

Baada ya Yesu kufa msalabani aliamua kuwa radhi na

yoyote aliamua kumkubali Yesu Kristo na kumwamini. Hata

kama ni mwenye dhambi anafanywa kuwa mtakatifu

kupitia Kristo, hata kama hana haki anafanywa kuwa

mwenye haki kupitia Yesu Kristo. Agano la kale msamaha

wa dhambi ulikuwa wa mda, kufanywa mwenye haki ni kwa

mda tu. Sadaka za wanyama zilikuwa hazina uwezo wa

kuindoa dhambi moja kwa moja. Ilitakiwa kila mwaka

itolewe sadaka, lakini kupitia Yesu Kristo mara moja tu

tulifanywa kuwa wenye haki mbele za Mungu (1Pet 3:18,

Ebr 9:28). Paulo aliandika kuwa;

“Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa

kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.

Basi tu wajumbe kwaajili ya Kristo, kana kwamba Mungu

anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwaajili ya

Kristo mpatanishwe na Mungu. Yeye asiyejua dhambi

alimfanya kuwa dhambi kwaajili yetu, ili sisi tupate kuwa

haki ya Mungu katika Yeye” [2Kor 17, 21]

UHURU WA KWELI 115

Tulikuwa wenye dhambi kwaajili yetu alifanyika mwenye

dhambi ili sisi tufanywe kuwa wenye haki. Upendo wake

kwetu ni wa ajabu sana ndio maana alipozibeba dhambi za

ulimwengu mzima. Mungu hakutaka kabisa hata kuwa naye

karibu, wala kumtazama kwa sababu Mungu anachukia

dhambi. Maandiko yanashuhudia kuwa; Na kama saa tisa,

Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Elo, Eloi, lama

sabakthani? Yaani Mungu wangu, Mungu wangu, mbona

umeniacha? (Math 27:46)

Kama vile Mungu alivyokuwa yuko radhi na mwanawe

Mpendwa Yesu Kristo. Kila anayemwamini anahesabiwa

haki katika mambo yote asiyoweza kuhesabiwa haki kwa

torati ya Musa. Kama maandiko yanavyosema kuwa;

“Basi, na ijulikane kwenu, ndugu zangu, ya kuwa kwa huyo

mnahubiriwa msamaha wadhambi; na kwa yeye kila

amwaminiye huhesabiwa haki katika mambo yale yote

asiyoweza kuhesabiwa haki kwa torati ya Musa” [Mate

13:38-39]

Torati maana yake ni sheria, Wayahudi waliishi kwa sheria

tu katika kipindi cha agano la kale vitabu rejea vinaonyesha

kuwa kulikuwa na sheria zaidi ya mia sita ambazo walikuwa

ni lazima wayafuate. Kuna makosa yalikuwa hayawezi

kusamehewa kabisa adhabu yake ilikuwa ni kifo. Biblia

inashuhdia kuwa Mwanamke aliyezini na mwanaume

alitakiwa kupigwa mawe mpaka kufa.

UHURU WA KWELI 116

“Waandishi na Mafarisayo walimkamata mwanamke

aliyekuwa amezini na mwanamke biblia inasema;

Waandishi na Mafarisayo wakamleta mwanamke

aliyefumaniwa na uzinzi, wakamweka katikati.

Wakamwambia Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa

alipokuwa akizini. Basi katika torati, Musa alituamuru

kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe

wasemaje? Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili

wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama,

akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao walipozidi

kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi

miongoni mwenu na awe wa kwanza kumtupia jiwe.

Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi.

Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka

mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho

wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke

amesimama katikati.

Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke,

akamwambia Mwanamke, wako wapi wale washitaki

wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia?

Akamwambia hakuna Bwana. Yesu akamwambia wala

mimi sikuhukumu. Enenda zako wala usitende dhambi

tena” (Yoh 8:3-11).

UHURU WA KWELI 117

Yesu hakuwa na shida na sheria alitaka kutenda haki katika

sheria ndio maana aliwaambia yoyote asiye na dhambi awe

wa kwanza kumpiga mawe mwanamke huyu. Jambo

lililosababisha Yesu kuwaambia wanafunzi wake yoyote

asiyekuwa na haki iliyozidi haki ya Waandishi na Mafarisayo

ni kwasababu ya unafiki wa Mafarisayo. Maandiko

yanashuhudia kuwa Waandishi na Mafarisayo walikuwa

wakiwatwika watu mzigo mzito wa sheria hali wao

wenyewe walikuwa hawawezi kuzifuata (Math 23:23).

Napenda neno alitamka Yesu kwa yule mwanamke baada

ya wale washitaki wake kumwacha, Yesu alimwambia;

“Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende

dhambi tena”. Kazi ya sheria ni hukumu, Yesu

hakumhukumu bali alimsamehe dhambi zake na

kumwambia asitende dhambi tena. Kumbe tukiwa ndani ya

Kristo tunapewa zawadi ya kutohukumiwa

kinachotupelekea kutofanya dhambi tena. Kumbe sheria

haiwezi kumsaidia mtu asitende dhambi bali ni Kristo ndiye

anayeweza Kumsaidia mwanadamu asitende dhambi na

kufanywa mwenye haki. Biblia inasema;

“Basi tena, kama kwa kosa moja watu wote

waliohukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki

watu wote walihesabiwa haki yenye uzima. Kwa sababu

kama kwa kuasi mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika

hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja

UHURU WA KWELI 118

watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki” [Rum

5:18-19].

Kwa sababu ya utii wa Yesu Kristo tuliingizwa katika hali ya

wenye haki. Ndio maana Yesu bado anakuita, hata ukiwa

ulifanya ubaya kiasi gani bado anasema anakupenda, bado

anasema anakuhitaji katika ufalme wake. Paulo aliyekuwa

Sauli wakati wa nyuma aliwauwa watu wengi, maelfu ya

watu waliokuwa wakimshuhudia Yesu Kristo. Yesu

alimhitaji Sauli kwenye ufalme wake alimsamehe na

kumfanya kuwa mtume wa watu wa Mataifa, ambaye

alibatizwa kuwa Paulo. Leo hii tunasoma vitabu yake zaidi

ya nusu ya vitabu vya agano jipya kaandika yeye. Haki

tuliyopewa ilikuwa kwa sababu ya juhudi ya Yesu Kristo

msalabani sio kwa sababu yetu sisi wenyewe.

Tunahesabiwa haki ya Mungu kwa njia ya imani kwa neema

yake. Matendo yetu yalishindwa kufikia kiwango cha haki

au utakatifu aliokuwa anautaka Mungu. Ndio maana

Mungu alimtoa Mwanawe wa pekee Yesu Kristo ili kupitia

yeye tupewe haki yake kwa njia ya neema yake. Ndio maana

maandiko yanasema;

“Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria;

inashuhudiwa na torati na manabii; ni haki ya Mungu iliyo

kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio.

Maana hakuna tofauti; kwa sababu wote wamefanya

dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;

UHURU WA KWELI 119

wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya

ukombozi ulio katika Kristo Yesu” [Rum 3:21-24]

Haki ya Mungu ipatikanayo kwa njia ya imani ya Yesu Kristo

inaachilia amani ipitayo akili zetu na kutuweka huru. Paulo

anasema;

“Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na

mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu

Kristo ambaye kwa yeye tumepata kwa njia ya imani

kuifikia neema hii ambayo mnasimama ndani yake; na

kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu” [Rum 5:1-2]

Haki ya matendo ya sheria ni haki inayopatikana kwa

matendo mazuri ya mtu binafsi, yaani unahesabiwa haki

kutokana na kile unachokifanya. Haki ya pili ni haki ambayo

unahesabiwa sio tu kwa sababu ya matendo mazuri/mema

unayoyafanya bali kwa sababu ya Kristo. Haki hii tunaipokea

kwa njia ya imani ya Yesu Kristo. Ndio maana Paulo

aliwaambia aliwaambia Wagalatia mmetengwa na Kristo

mnaotaka kuhesabiwa haki kwa matendo ya sheria. Haki ya

matendo ya sheria imepunguka, haiwezi kufikisha matakwa

ya Mungu kwenye maisha yetu. Mungu mwenyewe anataka

tuishi kwa haki ya Yesu Kristo ambayo inapatikana kwa njia

ya imani. Maandiko yanasema;

“Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa

sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema. Maana

UHURU WA KWELI 120

sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya

imani” [Gal 5:4-5]

Kuishi kwa haki ya matendo ya sheria ni sawa na kusema

Yesu Kristo alikufa bure msalabani, haki ya Mungu haiwezi

kunisaidia jambo lolote kwenye maisha yangu. Ndio maana

Paulo aliwasisitiza sana Wagalatia kuishi kupitia haki

ipatikanayo kwa njia ya imani. Paulo anasema;

“siibatili neema ya Mungu; maana, ikiwa haki hupatikana

kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure” [Gal 5:21]

Haki ya Mungu inapatikana kwa njia ya imani ya Yesu Kristo,

matendo yetu mazuri mbele za Mungu yanaonekana ni deni

(Rum 4:4). Mbele za Mungu matendo yetu mazuri biblia

inashuhudia kuwa ni mafu (Ebr 9:14). Ili tukubalike mbele

za Mungu na matendo yetu mema yawe hai mbele za

Mungu nilazima tukubali kumwani Yesu Kristo aliyekufa

kwaajili yetu akafanyika mwenye dhambi ili sisi tuwe haki

ya Mungu (2Kor 5:21).

UHURU WA KWELI 121

Tathmini kupitia maswali kutoka katika Sura ya Nne

1: Ufalme wa Mungu unarejeshwa kwa viambatanishi

muhimu viwili, vitaje?

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

2: Injili ni nini?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

3: Neno la Neema Ya Kristo linaachilia kibali cha kuwa

warithi halali wa mambo yote aliyotupigania Yesu Kristo

msalabani. Yataje

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

(iii)……………………………………………………………………………………

…………………………………………

UHURU WA KWELI 122

(iv)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

(v)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

(vi)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

UHURU WA KWELI 123

SURA YA TANO

NITASIMAMA TENA

akumbuka mtumishi wa Mungu mmoja aliyekuwa na

kansa ya tumbo, kwa vile alivyokuwa mtumishi

mkubwa, walienda watumishi mbali mbali wakubwa

na maarufu kumuombea. Kwa kipindi kirefu aliweza

kuombewa bila kupata matokeo yoyote, kwa kadri

walivyomuombea ndivyo hali ilizidi kuwa mbaya.

Alipokwenda hospitali hakuweza kupatiwa matibabu hali

ilikuwa mbaya sana. Madaktari walithibitisha kuwa kansa

yake imefikia hatua ya mwisho kwa hiyo asingeweza

kupona. Akapewa maelekezo ya kumsaidia kutunza

ugonjwa wake ili usimuue kwa kasi. Huku nafsi yake ikiwa

imejaa majonzi na huzuni, akawa akifikiri kuhusu huduma

yake.

Anasema ndani yake hakuwa anashuhudiwa kazi ya

huduma yake ameimaliza. Lakini pia kutokana na maelezo

ya madaktari maana yake alikuwa anahesabiwa siku za

kufa. Mbele yake anaona giza mwanga hakuna, tumaini

limepotea, hawezi tena kutumika, hawezi tena kuwa na

uwezo wa kuruka ruka akihubiri injili kama alivyokuwa

akifanya.

N

UHURU WA KWELI 124

Ni miezi minne sasa bado Mungu alimuacha hai yuko

kitandani, kitanda kilikuwa rafiki yake kama mbinguni na

Mungu visivyoweza kutenganishwa. Siku alizokuwa

zimehesabiwa kuwa hai zilipita, akawa akiishi kwa neema.

Amefika mahali hawezi kutembea, hukaa kwa msaada, kula

kwa msaada, nafsi yake ikainama mwisho anauona

umekaribia.

Akaanza kupanga utaratibu wa kuwaachia urithi kwa mke

wake na watoto, na kuwapa ushauri. Akiwa anafanya hivyo

ndani yake anashuhudiwa kazi yake bado hajamaliza.

Akaandika urithi na kuwatia moyo watoto wake kuishi

katika utauwa na kumtafuta Mungu. Ndugu zake waliokuwa

mbali walianza kusogea karibu kumsalimia. Sio kwa lengo la

kumsalimia kama walivyokuwa wakisema bali kuepusha

usumbufu kuwa akifariki wasipate shida kusafiri kwenda

kwenye mazishi yake.

Siku moja akiwa kitandani huku moyo wake ukiwa na

maswali, akawaza moyoni mwake ivi kweli Mungu

ameshindwa kuniponya na hii kansa? Akasema nitaenda

kuangalia kwenye biblia Mwanzo mpaka ufunuo ili nione

kama kweli Mungu ameniandikia kufa na huu ugonjwa.

Akawa akisoma kwa shida anatafuta uthibitisho wa

kujiridhisha kuwa hawezi kupona. Akajisemea moyoni kama

nikikuta Mungu ameandika nitakufa kwa ugonjwa

nitakubaliana naye la kama si hivyo sitakubali kufa.

UHURU WA KWELI 125

Akawa akisoma na kuipitia biblia kuangalia mahali

palipoandikwa kuwa atakufa kwa ugonjwa. Hakuona mahali

popote, alipoendelea kusoma akakuta mahali

pameandikwa;

“Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili

wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe

hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake

mliponywa” [1Pet 2:24]

Andiko hili lilimtia moyo akasema sina sababu ya kufa kwa

sababu nilishalipiwa deni la dhambi. Mimi ni mwenye haki,

akaendelea kujisemea moyoni mwake kwa kupigwa kwake

mliponywa. Siku zikapita, wiki zikapita hadi mwezi ukapita,

lakini bado hali yake iliendelea kuwa mbaya. Akasema

moyoni mwake sitajali mimi nataka kufa kupitia hili andiko.

Siku zikaendelea kupita, wiki ukafika mpaka mwezi wa pili

ulifika bila kuona matokeo.

Siku moja usiku akiwa amelala kitandani, aliwaona watu

wamekuja wakiwa wamevaa mavazi meupe ya kidaktari

wakiwa wameshika visu na vyombo vya upasuaji. Akiwa

usingizini akawa anaona wanamvua nguo ya juu wanaanza

kunyofoa nyama kwenye ule uvimbe (kansa). Anasema

ilikuwa ni kama mda wa dakika tano wale watu wakapotea.

Aliposhtuka usingizini anaona kweli kabisa vifungo vya shati

lake vimefunguliwa, na anaona kwenye tumbo lake hakuna

mahali penye maumivu kama vile hajawahi kuumwa kabisa.

UHURU WA KWELI 126

Akapiga kelele kwa nguvu huku akisema nimepona!

nimepona! Ameni haleluya

Ugonjwa ulikuwa hauponyeki, madaktari walisema

amechelewa hawezi kupona, watumishi wakubwa na

maarufu walimuombea lakini hakupona. Bado alimuamini

Mungu na alipokea uponyaji. Hii inaonyesha wazi haijalishi

ni changamoto gani ngumu unapitia lakini bado Mungu

anaweza kukusimamisha.

Moja ya vitu vimekuwa changamoto kubwa sana hasa

katika kizazi hiki ni kuziishi changamoto zao na mambo

yaliyopita. Paulo alisema hivi;

“Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha

kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo

nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele” [Filip 3:13]

Paulo alijua kuwa huko nyuma aliwahi kuwatesa watumishi

wa Mungu kwa kuwauwa na kupinga wokovu. Kiasi

ambacho alikuwa akifikiria makosa yake, Lakini alifika

mahali akaacha kufikiria mambo yote yaliyopita kwenye

maisha yake na kusema “natenda neno moja tu

nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo

mbele”. Kwa sababu alijua mambo yaliyofanyika nyuma

hayana nafasi ya kuamua hatima yake.

UHURU WA KWELI 127

Kuwa na changamoto katika maisha bado hakukuzuii wewe

kuishi vile unavyotakiwa kuishi. Unaweza kuwa na

changamoto, unashida, uchumi wako sio mzuri,

changamoto kwenye ndoa yako na mahali popote pale

lakini bado ukaendelea kuishi vile unavyotakiwa kuishi.

Wakati wote Mungu yuko tayari kushughulika na

changamoto zako hata kama zinaoneka ni ngumu kiasi gani,

hata kama zinaonekana hazitatuliki. Angalia maagizo

ambayo Mungu aliwapa wana wa Israeli;

Wakasafiri kutoka mlima wa Hori kwa njia ya Bahari ya

Shamu; ili kuizunguka nchi ya Edomu, watu wakafa moyo

kwa sababu ya ile njia. Watu wakamnung'unikia Mungu, na

Musa, Mbona mmetupandisha huku kutoka nchi ya Misri, ili

tufe jangwani? Maana hapana chakula, wala hapana maji,

na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu. Bwana akatuma

nyoka za moto kati ya watu, wakawauma, watu wengi

wakafa. Watu wakamwendea Musa, wakasema,

Tumefanya dhambi kwa sababu tumemnung'unikia Mungu,

na wewe; utuombee kwa Bwana, atuondolee nyoka hawa.

Basi Musa akawaombea watu. Bwana akamwambia Musa,

Jifanyie nyoka ya shaba, ukaiweke juu ya mti, na itakuwa

kila mtu aliyeumwa, aitazamapo ataishi. Musa akafanya

nyoka ya shaba, akaiweka juu ya mti, hata ikiwa nyoka

amemwuma mtu, alipoitazama ile nyoka ya shaba, akaishi.

[Hes 21:4-9]

UHURU WA KWELI 128

Wana wa Israeli walikuwa katika safari kuelekea Misri

walifika mahali wakachoka. Wakataka kufuata njia zao kwa

sababu walichoka na ile njia, wakamnung’unikia Musa.

Mungu akatuma nyoka za moto zikawauma watu wengi

wakafa, wakarudi kwa Musa. Kumwambia awaombee kwa

Mungu wawaondolee nyoka, Musa akawaombea kwa

Mungu. Mungu akamwambia Musa jifanyie nyoka wa shaba

na kila atakayemwona ataishi. Musa alipoifanya ile nyoka

ya shaba na kila aliyeitazama ile nyoka ya shaba aliishi.

Inawezekana kuna watu nyoka zilikuwa zikiwauma lakini

kila aliyeitazama nyoka ya shaba aliishi.

Nyoka ya shaba ilikuwa ni lugha ya picha inamuwakilisha

Yesu Kristo katika agano jipya aliyeinuliwa mtini kwa sababu

ya makosa yetu na dhambi zetu. Kristo anashuhudia kuwa

alikuja kuzivunja kazi za yule adui mwovu Shetani. Pia

anasema alikuja kushughulikia maisha yetu tena maisha

tele. Imeandikwa;

“Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja

ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.” [Yoh 10:10]

Shetani kazi yake ni kuiba kuchinja na kuharibu, lakini

ashukuriwe Yesu alikuja ili tuwe na uzima KJV anasema ili

wawe na maisha tena maisha tele. Maana yake tukiishi

katika Kristo tunaweza kusimama tena, Bwana atatuinua na

kutuweka mahali tunapostahili. Kama ni hivyo basi hatuna

budi kuishi katika Kristo maana yeye ndiye mwenye maisha

UHURU WA KWELI 129

na yeye ndiye anayeweza kutusimamisha wakati wote

kwenye maisha yetu. Paulo aliandika hivi;

“tena alikufa kwa ajili ya wote, ili walio hai wasiwe hai tena

kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye

aliyekufa akafufuka kwa ajili yao.” [2Kor 5:15]

Tafsiri ya Biblia ya Habari Njema anasema hivi;

“Alikuja kwaajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi

kwaajili yao wenyewe, bali kwaajili yake yeye aliyekufa,

akafufuliwa kwaajili yao”

Biblia inashuhudia kuwa tunatakiwa kuishi kwaajili yake

yeye aliyekufa na kufufuliwa kwaajili yetu yaani Yesu Kristo.

Kwanini tunatakiwa kuishi katika Kristo Yesu?

Tangu mwanzo haikuwa mpango wa Mungu tuishi

kwaajili yetu, bali tuishi katika yeye (Yesu Kristo).

Roho zetu zimeathiriwa kwa zawadi, vipawa,

huduma na kazi ambavyo haviwezi kujidhihirisha

kuwa halisi katika macho ya damu na nyama kwa

nguvu zetu bali kwa msaada wake mwenyewe (Yesu

Kristo).

Hakuna jambo tutalifanya sisi wenyewe likawa ni

bora mbele za Mungu bila neema ya Kristo.

UHURU WA KWELI 130

Lolote tutakalolifanya kwa juhudi zetu, hata kama

limefikia kiwango cha mwisho cha juhudi zetu bado

litaonekana liko chini ya kiwango mbele za Mungu

pasipo neema ya Mungu.

Kufanya jambo lolote sisi wenyewe bila kupitia kwa

Yesu Kristo ni sawa na kusema sihitaji msaada wako

Mungu.

Kufanya jambo lolote sisi wenyewe bila neema ya

Kristo ni kuishi maisha ya kuchanganyikiwa, msongo

wa mawazo na maisha ya kufeli.

Kufanya sisi wenyewe bila neema ya Kristo ni sawa

kusema sihitaji msaada wako mkombozi (Yesu

Kristo). Ni kukataa kazi kamilifu ya Kristo iliyofanyika

pale msalabani.

Kufanya sisi wenyewe ni kujizuia sisi halisi

kujidhihirisha katika macho ya damu na nyama.

Tangu mwanzo haikuwa mpango wa Mungu tuishi kwaajili

yetu, bali tuishi katika yeye (Yesu Kristo).

Yesu Kristo alikuwepo tangu mwanzo kwenye uumbaji,

japokuwa biblia imemuelezea kwa lugha ya picha. Kwa

maana nyepesi ni kwamba alikuwepo lakini alikuwa

hajajifunua.

UHURU WA KWELI 131

i. Yesu ni nuru.

Mungu wakati anaumba dunia alisema na Iwe nuru. Kama

ilivyoandikwa;

“Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru” [Mwa 1:3]

Ile nuru iliyotokea ikaangaza duniani. Ikaangaza mchana na

usiku alikuwa ni Yesu Kristo.

Yesu Kristo aliye nuru aliwaongoza wana wa Israeli mchana

na usiku kwa mfano wa nguzo. Maandiko yanasema;

“Bwana naye akawatangulia mchana ndani ya wingu

mfano wa nguzo, ili awaongoze njia; na usiku, nadi ya moto

mfano wa nguzo, ili kuwapa nuru; wapate kusafiri mchana

na usiku” [Kut 13:21]

Yesu ndiye aliwaongoza Wana wa Israeli mchana na usiku

kwa mfano wa nguzo. Yesu ndiye aliyeachilia nuru wakiwa

jangwani na kuwaongoza.

Daudi alishuhudia kuwa Bwana ni nuru. Imeandikwa kuwa;

“Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope

nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?”

[Zab 27:1]

Daudi alisema hakuna wa kumhofu kwa sababu Bwana

yaani Yesu Kristo ni nuru yake na wokovu wake.

UHURU WA KWELI 132

Katika Isaya iliandikwa kuwa Bwana ni nuru. Imeandikwa;

“Jua halitakuwa nuru yako tena wakati wa mchana, Wala

mwezi hautakupa nuru kwa mwangaza wake; Bali Bwana

atakuwa nuru ya milele kwako, Na Mungu wako atakuwa

utukufu wako” [Isa 60:19]

Katika Isaya iliandikwa kuwa jua halitakuwa nuru wala

mwenzi. Alisema Bwana atakuwa nuru ya milele na

utukufu.

Yohana anashuhudia kwamba Yohana mbatizaji alikuja ili

aishuhudie ile nuru yaani Yesu Kristo. Imeandikwa;

“Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote

wapate kuamini kwa yeye” [Yoh 1:7]

Yesu alisema mwenyewe kuwa ni nuru ya ulimwengu na

yoyote anayemfuata hatakwenda gizani. Biblia inasemsa;

Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya

ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe,

bali atakuwa na nuru ya uzima” [Yoh 8:12]

Yesu alirudia tena kusema mda aliopo ulimwenguni yeye ni

Nuru ya ulimwengu. Imeandikwa;

“Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu”

[Yoh 9:5]

UHURU WA KWELI 133

Kwa mara ya tatu Yesu alirudia kesema mimi ni nuru ya

ulimwengu na anayemwamini asikae gizani.

“Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu

aniaminiye mimi asikae gizani” [Yoh 12:46]

Yohana alifunuliwa kuwa nuru na taa ya mbinguni ni

Mwanakondoo yaani Yesu Kristo.

“Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa

maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni

Mwana-Kondoo” [Ufu 21:23]

ii. Yesu ni Neno.

Neno la uumbaji lililokuwa likitoka kinywani mwa Mungu.

Neno la uumbaji alikuwa ni Yesu Kristo, yaani Yesu Kristo

ndiye aliyekuwa akiumba. Imeandikwa;

“Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako

kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo

alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala

pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani

yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru

ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.

Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake

Yohana. Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru,

UHURU WA KWELI 134

wote wapate kuamini kwa yeye. Huyo hakuwa ile nuru, bali

alikuja ili aishuhudie ile nuru. Kulikuwako Nuru halisi,

amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu.

Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata

kuwako, wala ulimwengu haukumtambua. Alikuja kwake,

wala walio wake hawakumpokea. Bali wote waliompokea

aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale

waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa

mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa

Mungu. Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi

tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee

atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.” [Yoh 1: 1-14]

Yohana anashuhudia kwamba hapo mwanzo palikuwa na

Neno ambaye alikuwa Mungu. Huyo neno alifanyika mwili,

tukauona utukufu wake kama wa Mwana pekee yaani Yesu

Kristo.

iii. Yesu ni Mti wa Uzima.

Mti uliopandwa katikati ya bustani ya Edeni alikuwa ni Yesu

Kristo. Biblia inashuhudia kwamba;

UHURU WA KWELI 135

“Bwana Mungu akachipusha katika ardhi kila mti

unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa

uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na

mabaya” [Mwa 2:9]

Katikati ya bustani kulikuwa na mti wa uzima na mti wa ujuzi

wa mema na mabaya. Mti wa uzima alikuwa ni Yesu Kristo

japokuwa umezungumziwa kwa lugha ya picha. Lakini pia

katikati ya bustani kulikuwa na mti wa ujuzi wa mema na

mabaya ilikuwa ni sheria za Musa zimezungumzwa kwa

lugha ya picha. Shetani alipokuwa anawadanganya Adamu

na Hawa, unaweza kufikiri alisema uongo mkubwa kumbe

ni kidogo. Shetani alianza kwa kuwadanganya Adamu na

Hawa halafu baadaye akaanza kuwaambia ukweli. Biblia

inashuhudia kwamba;

“Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, kwa

maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula

matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi

mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya” [Mwa

3:4-5]

Kumbe Shetani aliwadanganya Adamu na Hawa kuwa

hamtakufa. Huu ni uongo kwa sababu Mungu aliwaagiza

Adamu na Hawa kuwa wakila matunda ya mti wa ujuzi wa

mema na mabaya msiyale wala kuyagusa msije mkafa (Mwa

3:3). Shetani alivyosema hamtakufa aliwadanganya.

Baadae Shetani akaendelea kuwaeleza ukweli kwamba siku

UHURU WA KWELI 136

mtakayokula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya

ulioko katikati mtafumbuliwa macho (maana yake mtakuwa

na ufahamu). Mkijua mema na mabaya, yaani mtaujua

wema na ubaya, na hiki ndicho kilichowatokea Adamu na

Hawa baada ya kula tunda. Biblia inashuhudia kwamba;

“Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula,

wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa,

basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na

mumewe, naye akala. Wakafumbuliwa macho wote wawili

wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini,

wakajifanyia nguo” [Mwa 3:6-7]

Kumbe Adamu na Hawa walipokula tunda ni kweli

walifumbuliwa macho wote wawili. Wakajikuta wako uchi,

kumbuka Mungu aliwaumba tangu mwanzo Alipomuumba

Adamu (Mwa 2:7) na Hawa (Mwa 2:21-23). Walikuwa

hawana ufahamu kuwa wako uchi, walianza kupata

ufahamu wa kujua kukaa uchi ni kubaya baada ya kula

tunda.

Mungu hakutaka Adamu na Hawa waishi kwa kujua mema

na mabaya (kuishi kwa sheria) bali waishi katika yeye.

Walipokula matunda ya ujuzi wa mema na mabaya Mungu

aliwafukuza katika bustani ya Edeni. Jambo la kushangaza

Mungu aliwazuia Adamu na Hawa wasiirudie njia

inayoiendea mti wa uzima (yaani Yesu Kristo). Kwa sababu

UHURU WA KWELI 137

Mungu hakutaka waishi kwa kuchanganya ujuzi wa mema

na mabaya na wakati huo huo kuishi katika Kristo Yesu.

Yesu ni mti wa uzima.

Yohana alionyeshwa maono kuwa Yesu Kristo ni mti wa

uzima. Imeandikwa;

“Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza

na wa mwisho. Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri

kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango

yake. Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na

wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye

uongo na kuufanya. Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu

kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi

ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye

kung'aa ya asubuhi” [Ufu 22:13-16]

Yesu Kristo alisema yeye ni Alfa na Omega, ukisoma tafsiri

ya biblia ya King James Version (KJV). Anasema

wamebarikiwa wote wanaofanya amri zake na wana haki

katika mti wa uzima yaani Yesu Kristo. Ukiwa ndani ya Kristo

unakuwa na haki ya kuingia katika milango ya mji ule yaani

mbinguni. Baadae anasema ni mimi Yesu niliye shina na

mzao wa Daudi nyota yenye kung’aa asubuhi.

Yohana alifunuliwa kuwa Yesu ni mti wa uzima ulioko

katikati ya bustani ya Mungu. Biblia inasema;

UHURU WA KWELI 138

“Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho

ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula

matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu”

[Ufu 2:7]

Mti wa ujuzi wa mema na mabaya ni sheria ya Musa.

Japokuwa wapo watumishi wa Mungu waliweza kuujua

ubaya kabla ya sheria kumi za Musa. Kwa mfano Yusufu

aligundua kuwa uzinzi ni ubaya mkubwa kwa Mungu na

alikataa kulala na mke wa Potifa (Mwanz 39:9b). Maana

yake ni neema pekee inayoweza kukusaidia kushinda

dhambi. Mti wa ujuzi wa mema na mabaya ulikuwa

unazungumziwa kwa lugha ya picha kuwa ni sheria za Musa.

Kwa sababu ya tabia za sheria za Musa zilivyokuwa

ziliwekwa ziliwekwa ili watu waweze kujua mema na

mabaya.

Tuangalie ngazi tatu za sheria [lakini Mungu anataka tuishi

kwa sheria yake (sheria ya Mungu)].

UHURU WA KWELI 139

i. Ngazi ya kwanza ya sheria (sheria ya Musa)

Sheria Kumi za Mungu.

Imeandikwa;

“Mungu akanena maneno haya yote akasema, Mimi ni

Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri,

katika nyumba ya utumwa. Usiwe na miungu mingine ila

mimi. Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu

cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani,

wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala

kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni

Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba

zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami

nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri

zangu.

Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu wako, maana Bwana

hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.

Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi,

utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni Sabato ya

Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe,

wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako,

wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala

mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana, kwa siku sita

Bwana alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote

vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo Bwana

UHURU WA KWELI 140

akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa. Waheshimu baba

yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika

nchi upewayo na Bwana, Mungu wako. Usiue. Usizini.

Usiibe. Usimshuhudie jirani yako uongo. Usiitamani

nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako;

wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe

wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani

yako. [Kut 20:1-17]

Mti wa ujuzi wa mema na mabaya uliokuwa

unazungumziwa zilikuwa ni sheria kumi za Mungu, kwa

sababu ya tabia zake kwa mfano usizini, kinyume cha

kutozini ni kuzini. Sheria zilikuwa zinaeleza ubaya na wema

kwa wakati mmoja, sheria hizi zilitolewa ili watu wajue

mema na mabaya.

Ndio maana Paulo anasema hivi;

“kwa sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki

mbele zake kwa matendo ya sheria; kwa maana kutambua

dhambi huja kwa njia ya sheria. Lakini sasa, haki ya Mungu

imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na

manabii; ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika

Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti;

kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na

utukufu wa Mungu; wanahesabiwa haki bure kwa neema

yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; ambaye

Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya

UHURU WA KWELI 141

imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake ,kwa sababu

ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote

zilzotangulia kufanywa. apate kuonyesha haki yake wakati

huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye

amwaminiye Yesu.

Ku wapi, basi, kujisifu? Kumefungiwa nje. Kwa sheria ya

namna gani? Kwa sheria ya matendo? La! Bali kwa sheria

ya imani. Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa

haki kwa imani pasipo matendo ya sheria. Au je! Mungu ni

Mungu wa Wayahudi tu? Siye Mungu wa Mataifa pia?

Naam, ni Mungu wa Mataifa pia; kama kwa kweli Mungu

ni mmoja, atakayewahesabia haki wale waliotahiriwa

katika imani, nao wale wasiotahiriwa atawahesabia haki

kwa njia ya imani iyo hiyo. Basi, je! Twaibatilisha sheria kwa

imani hiyo? Hasha! Kinyume cha hayo twaithibitisha sheria.

[Rum 3:20-31]

Paulo anathibitisha kwamba hakuna mwanadamu mwenye

mwili atakayehesabiwa haki wa matendo ya sheria. Halafu

anatoa sababu ya matendo ya sheria (sheria za Musa) kuwa

kutambua dhambi au kuwa na maarifa ya dhambi kama KJV

alivyosema. Sheria za Musa zilikuja kwaajili ya kujua mema

na mabaya, yaani wema na ubaya ulijulikana kwa sheria za

Musa na biblia inaeleza wazi hakuna atakaye hesabiwa haki

kwa sababu ya hizo sheria bali kwa njia ya Kumwamini Yesu

UHURU WA KWELI 142

Kristo. Paulo anaendelea kusema hiyo haki ya Mungu

ipatikanayo kwa njia ya sheria inashuhudiwa na torati yaani

sheria (KJV) na manabii. Kuwa haki ya Mungu hupatikana

kwa imani ya Yesu Kristo. Maana yake sheria na manabii

zinakubali kuwa kwa imani ya Yesu Kristo tunahesabiwa

haki. Paulo anasema sasa ku wapi kujisifu? Kwa sababu

kujisifu kwa matendo ya sheria kumefungiwa nje (KJV

anasema kumeondolewa) yaani hakuna awezaye kujisifia

kwa sababu ya matendo ya sheria (matendo meama). Lakini

kila mtu ana uhuru wa kujisifia kwa sheria ya imani yaani

Sheria ya kumwamini Yesu Kristo. Paulo anamalizia kwa

kusema kinyume cha kuwa na sheria ya imani yaani kutaka

kuhesabiwa haki kwa matendo ya sheria, ni kuifanya sheria

ya imani sio kitu bali sheria ya matendo ya sheria ambayo

hatuwezi kuhesabiwa haki ya Mungukwa hiyo.

Ndio maana Paulo aliwaandikia Wagalatia hivi;

“hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa

matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi

tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya

Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo

ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki”

[Gal 2:16]

UHURU WA KWELI 143

Paulo anaendelea kusisitiza kwamba hakuna mwenye mwili

atakayeweza kuhesabiwa haki kwa matendo ya sheria. Bali

tunahesabiwa haki kwa njia ya imani ya Yesu Kristo

tunahesabiwa haki. Paulo anaendelea kusisitiza kuwa wale

walio wa matendo ya sheria wako chini ya laana.

Imeandikwa;

“Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako

chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu

asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha

torati, ayafanye” [Gal 3:10]

Maana yake kila mtu anayeishi kwa matendo ya sheria yuko

chini ya laana. Yaani kuishi kwa matendo ya sheria hali

kwamba umekataa kumwamini Yesu Kristo na kukubali

kuipokea haki yake kwa imani na kuishi kwa matendo yako

mema (matendo ya sheria) uko chini ya laana. Ndio maana

Luka alishuhudia kwamba;

“Basi na ijulikane kwenu, ndugu zangu, ya kuwa kwa huyo

mnahubiriwa msamaha wa dhambi; na kwa yeye kila

amwaminiye huhesabiwa haki katika mambo yale yote

asiyoweza kuhesabiwa haki kwa torati ya Musa” [Mat

13:38-39]

Luka alisema kwa Yesu Kristo tunahubiriwa msamaha wa

dhambi na kwa yeye tunahesabiwa haki katika mambo

tusiyoweza kuhesabiwa haki kwa sheria ya Musa. Ndio

UHURU WA KWELI 144

maana Paulo alisema mmeanguka katika hali ya neema

mnaotaka kuhesabiwa haki kwa matendo ya sheria (Gal

5:4).

Je tutende dhambi hali tukijua tunahesabiwa haki kwa

imani ya Yesu Kristo?

La hasha! Paulo alijibu swali linaloendana na hili. Biblia

inasema;

“Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi

kuwa nyingi? Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena

katika dhambi? Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa

katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi

tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti

yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia

ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika

upya wa uzima” [Rum 6:1-5]

Paulo anasema sisi tuliobatizwa katika Yesu Kristo tulizikwa

na Yesu Kristo katika mauti yake. Maana yake tuliifia

dhambi na ndio maana Yesu Kristo alivyofufuka tulifufuka

pamoja naye. Na kwa namna hiyo tulihesabiwa haki pamoja

naye ili kusudi tuenende katika upya wa maisha (KJV

anasema).

UHURU WA KWELI 145

Mungu anataka tuishi katika Yesu Kristo peke yake.

Mungu anataka tuishi katika yeye (Yesu Kristo). Adamu na

Hawa walipokula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya

(sheria za Musa). Mungu hakutaka waende kula matunda

ya mti wa uzima (Yesu Kristo). Imeandikwa;

“Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama

mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije

akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa

uzima, akala, akaishi milele; kwa hiyo Bwana Mungu

akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo

katika hiyo alitwaliwa. Basi akamfukuza huyo mtu,

akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya

Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda

njia ya mti wa uzima” [Mwa 3:22-24]

Mwanadamu alipokula matunda ya mti wa ujuzi wa mema

na mabaya (sheria za Musa) alikuwa amejichafua kiasi

ambacho Mungu hakutaka auendee mti wa uzima (Yesu

Kristo), kwa sababu sio mfumo wa maisha ambao Mungu

aliukusudia, yaani mfumo wa kuishi kwa sheria na kuishi

katika Yesu Kristo. Mungu alikusudia watu waishi katika

yeye tu yaani Yesu Kristo . Hii ndiyo sababu baada ya

anguko la Adamu na Hawa Mungu aliandaa mpango wa

kumwondoa mwanadamu kutoka kuishi maisha ya

matendo ya sheria, na kuanza kuishi maisha katika Yesu

Kristo (2 Kor 5:14-15).

UHURU WA KWELI 146

(ii) Ngazi ya pili ya sheria

Yesu aliongezea ukali katika sheria za Musa. Lakini alisema

hata katika hizo hamjakamilishwa bado. Mathayo 5:17-48

17:Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii;

la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.

Yesu hakuja kuitangua torati, au kuivunja torati bali alikuja

kuitimiliza torati, Mungu hana shida na sheria wala hakuna

shida yoyote katika sheria za Mungu. Yeye Mungu hakutaka

tuishi kwa torati, bali kwa neema. Sheria ni nzuri, ni takatifu

na ni kamilifu lakini huwezi kuwa mkamilifu au mtakatifu

kwa kuishi kwa matendo ya sheria. Bali kwa kuishi katika

yeye (2Kor 5:15), kwa sababu ukiishi katika yeye unakuwa

mkamilifu na mtakatifu kwa njia ya imani.

Sheria ya Musa ilikuwa haijatimilika lakini Yesu alikuja

kuitimiliza kwa njia ya neema na kweli. Yohana aliandika

kuwa; torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli

zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo. Maana yake neema na

kweli zilikuja kuitimiliza sheria ya Musa. Ukiishi kwa sheria

ya Musa pamoja na kwamba ni nzuri, kamilifu na takatifu,

lakini bado mbele za Mungu haitakufanya uwe mkamilifu au

mtakatifu. Utahesabiwa kuwa mkamilifu na mtakatifu kwa

kuishi kwa neema na kweli yaani neno la Mungu katika Yesu

Kristo.

UHURU WA KWELI 147

18: Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi

zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati

haitaoondoka ,hata yote yatimie.

Yesu anaendelea kusisitiza kuwa hata mbingu na nchi

zitakapoondoka hakuna torati itakayoondolewa hata yote

yatimie. Yesu hakuja kuvunja sheria bali kuitimiliza kwa

neema na kweli.

19: Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi

zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo

kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda

na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa

mbinguni.

Anaendelea kusema yoyote atakayevunja amri hizo zilizo

ndogo, na kuwafundisha watu hivyo ataitwa mdogo kabisa

katika ufalme wa mbinguni. Atakayezitenda na kuzifundisha

ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni. Nilazima

uzitende kwa ukamilifu na kuzifundisha. Yesu anasisitiza

kuwa hakuja kuvunja sheria bali kuitimiliza sheria.

20: Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo

haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe

katika ufalme wa mbinguni.

UHURU WA KWELI 148

Yesu anasema haki yenu isipozidi haki ya Waandishi na

Mafarisayo hamtaingia kamwe katika ufalme wa Mbinguni.

Haki ya Waandishi na Mafarisayo ilikuwa ni ya matendo ya

sheria. Waandishi na Mafarisayo waliamini kuwa haki ya

matendo ya sheria ndiyo itakayowapa kibali cha kuingia

mbinguni pamoja na kwamba wanamkataa Yesu Kristo.

Yesu aliweka wazi kuwa haki yenu nilazima izidi haki ya

waandishi na Mafarisayo, ambayo hiyo haki haipatikani kwa

matendo ya sheria bali kwa imani ya Yesu Kristo. Paulo

aliwaambia Warumi; Lakini mtu afanyaye kazi, ujira wake

hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni (Rum 4:4)

Maana yake mara zote jambo unalolifanyia kazi sio neema

tena bali ni deni. Mungu akitazama juhudi zako binafsi

halafu haoni ukimuishia Yesu Kristo kazi yako ni bure mbele

zake. Waandishi na Mafarisayo waliamini kwa matendo ya

sheria tu wanahesabiwa haki mbele za Mungu. Hawakujua

kumbe matendo yao ya sheria hayawezi kuwakamilisha

asipokuwepo Yesu Kristo. Ndio maana Yesu alitoa mfano

huu;

“Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni

wenye haki, wakiwadharau wengine wote. Watu wawili

walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja Farisayo, wa pili

mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama akiomba hivi

moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si

kama watu wengine, wanyang'anyi, wadhalimu, wazinzi,

UHURU WA KWELI 149

wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi nafunga mara mbili

kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote. Lakini

yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu

hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua

akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.

Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake

amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye

atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa” [Luk 18:9-14]

Maombi yana nguvu sana ya kuleta majibu, sadaka na fungu

la kumi likitolewa kwa imani linaleta matokeo makubwa

sana kwenye maisha ya mtu. Kibinadamu Farisayo alikuwa

yuko sawa ni Mtakatifu na anastahili kuhesabiwa haki lakini

shida ilikuwa kwenye eneo la imani alikoweka Farisayo,

Farisayo aliamini matendo yake ya sheria yanaweza

kumkamilisha. Kufunga na kutoa zaka akasahau kwamba

akifanya hayo yote bila kuweka imani yake kwa Mungu

atakuwa anafanya kazi bure. Yaani mbele za Mungu

atakuwa anadeni kama ilivyoandikwa katika Warumi 4:4.

Je tusifunge na kuomba hali tukijua tumeshahesabiwa

haki kwa imani na sio matendo ya sheria?

Hapana! Nilazima tufunge na kuomba kwa sababu kufunga

na kuomba ni mpango halisi wa Mungu kwa mwanadamu.

Fahamu kwamba jambo lolote unalolifanya, likiwekewa

UHURU WA KWELI 150

imani hilo kuwa ndio linalokuleta majibu. Tambua kwamba

Mungu analihesabu kuwa ni tendo la sheria. Ukiamini

kwamba mpaka niombe au nifunge ndio nitapata majibu,

au maombi yangu na kufunga yanajitosheleza mbele za

Mungu kunipatia haki au ninachokihitaji. Ukajifungia kuwa

sheria na ukajiwekea kuwa huo ndio msimamo wako, kuwa

bila kufanya hivyo huwezi kupata unachokitaka kwa

Mungu.

Jua kwamba imani yako iko katika matendo yako na sio kwa

Mungu. Hivi ndivyo huyu Farisayo alikuwa akiishi, sadaka

inaweza kuuhusisha ufalme wa Mungu kutenda kazi kwa

aniaba yako. Vivyo hivyo maombi, kufunga na matendo

mema havina shida kuvifanya, shida inaanzia pale

utakapoanza kuyaamini hayo kuwa kwa hayo pekee

yanakufanya kuwa mwenye haki mbele za Mungu na kuwa

mwongozo wa maisha yako, na sio katika imani ndani ya

Yesu Kristo, hapo jicho la Mungu linaona unafanya matendo

ya sheria. Hiki ndicho kilikuwa kimemsababisha Farisayo

asihesabiwe haki.

Fikiria kama Farisayo angeenda mbele za Mungu kuomba

kwa unyenyekevu. Na kumwambia Mungu pamoja na

kwamba ninafunga, pamoja na kwamba ninatoa zaka katika

mapato yangu yote. Bado ninaamini wewe ndiye

unayeweza kunisaidia na kunipa baraka na kuniwezesha.

Naamini Farisayo angehesabiwa haki kuliko Mtoza ushuru.

UHURU WA KWELI 151

Ni muhimu sana kufanya kwa juhudi zote matendo mema,

lakini ni muhimu zaidi kufanya kwa juhudi huku imani yetu

ikiwa mbele za Mungu. Yesu Kristo aliyekufa kwaajili yetu

kwa juhudi zake ili sisi tupate kibali, neema na haki kwaajili

yake.

21: Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu

akiua, itampasa hukumu.

22: Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake

hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake,

itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum

ya moto.

23: Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku

ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,

24: iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako,

upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka

yako.

25: Patana na mshitaki wako upesi, wakati uwapo pamoja

naye njiani; yule mshitaki asije akakupeleka kwa kadhi, na

kadhi akakupeleka kwa askari, ukatupwa gerezani.

26: Amin, nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe

kulipa senti ya mwisho.

UHURU WA KWELI 152

27: Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;

28: lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye

mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye

moyoni mwake.

29: Jicho lako la kuume likikukosesha, ling'oe ulitupe mbali

nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee

wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.

30: Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe

mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja

kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.

31: Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati

ya talaka;

32: lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe,

isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi;

na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.

33: Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape

uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;

34: lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa

mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu;

35: wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu

yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa

Mfalme mkuu.

UHURU WA KWELI 153

36: Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya

unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi.

37: Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa

kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu.

38: Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino

kwa jino;

39: Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu;

lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.

40: Na mtu atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako,

mwachie na joho pia.

41: Na mtu atakayekulazimisha mwendo wa maili moja,

nenda naye mbili.

42: Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe

kisogo.

43: Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na,

Umchukie adui yako;

44: lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu,

waombeeni wanaowaudhi,

45: ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni;

maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema,

huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

UHURU WA KWELI 154

46: Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata

thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi

yayo hayo?

47: Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani

la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama

hayo?

Yesu aliongeza ukali wa sheria ya Musa, pamoja na sheria

zilizokuwa zimeandikwa katika kitabu cha torati, lakini bado

hizo sheria zote alizozitaja zilikuwa haziwezi kutukamilisha.

Katika mstari wa mwisho katika sura hii ya tano Yesu

anamalizia kwa kusema;

48: Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa

mbinguni alivyo mkamilifu.

Yesu anasema mtakuwa wakamilifu kama Baba yenu wa

mbinguni alivyo mkamilifu. Huu ni wakati ujao ndio maana

anasema mtakuwa wakamilifu, ingekuwa kwa hizo sheria

alizooneza makali zingekuwa ni kamilifu basi angesema;

Hata sasa mmekuwa wakamilifu kwa hizo sheria, lakini kwa

sababu hata hizo haziwezi kutukamilisha kuwa wakamilifu

na watakatifu ndio maana akasema mtakuwa wakamilifu.

UHURU WA KWELI 155

(iii) Ngazi ya tatu ya Sheria (sheria ya Mungu kamilifu)

Yesu Kristo ni sheria iliyokamilifu. Warumi 10:1-4

1: Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua

yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.

Paulo aliwaombea watu waokolewe. Kwasababu alijua

wokovu unapatikana bure kwa njia ya imani ya Yesu Kristo.

2: Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa

ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa.

Paulo alisema wanajuhudi katika Mungu lakini si katika

maarifa. Kama lilivyo kanisa la sasa wanajuhudi katika

Mungu lakini si katika maarifa. Na ndio maana Mungu

anawakataa watu wasikae katika nafasi ya ukuhani

(uongozi). Hosea aliandika hivi;

“Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa

kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa

wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau

sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto

wako” [Hos 4:6]

UHURU WA KWELI 156

Kumbe kwa kukosa maarifa watu wanaangamizwa, na

Mungu anawaondoa katika nafasi ya ukuhani (uongozi)

kwake, kwa sababu ya kusahau sheria ya Mungu, Mungu

naye anasema atawasahau watoto wako.

3: Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na

wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini

ya haki ya Mungu.

Paulo anaendelea kusema; hawaijui haki ya Mungu,

wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe. Tafsiri ya biblia ya

King James Version (KJV) anasema; Kwa maana ni wajinga

wa haki ya Mungu. Kwa sababu ni wajinga wa haki ya

Mungu, wanaenda kujitafutia haki zao wenyewe na

kuzipeleka mbele za Mungu. Wakifikiri watahesabiwa haki

kwa hizo, lakini kumbe sivyo Mungu anavyoitazama haki.

4: Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye

ahesabiwe haki.

Paulo anathibitisha kuwa Yesu Kristo ni mwisho wa sheria.

Tafsiri ya biblia ya New International Version anasema; Kwa

maana Yesu Kristo ni kilele cha sheria. Pasipo yeye huwezi

kuhesabiwa haki. Ndio maana Mungu anataka uishi kwa

kumtegemea yeye na kumwamini yeye, Ameni Haleluya.

UHURU WA KWELI 157

Katika yeye kuna kuhesabiwa haki, utakatifu, kuto kuwa na

hatia, kutukuzwa, ni wafalme, kubarikiwa (Rum 8:29-30, Efe

1:3-6, 1:21, 2:6). Sheria nyingine si kitu kama haumtumainii

Yesu Kristo na hauishi katika yeye, Paulo alisema hivi;

“Namshukuru Mungu kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi

kama ni hivyo kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu”

[Rum 7:25a]

Paulo anasema anamshukuru Mungu kwa Yesu Kristo na

kuitumikia sheria ya Mungu. Ipatikanayo kwa njia ya imani

ya Yesu Kristo. Ndio maana imeandikwa hivi katika Biblia ya

Habari Njema;

“Alikufa kwaajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi

kwaajili yao wenyewe, bali kwaajili yake yeye aliyekufa,

akafufuliwa kwaajili yao” [2Kor 5:15]

Kumbe hatutakiwi kuishi kwaajili yetu tena bali kwaajili ya

Yesu Kristo aliyekufa kwaajili yetu na kufufuka kwaajili yetu.

Juhudi zetu, maarifa yetu, uwezo wetu binafsi

hautatusaidia kitu bila msaada wa Yesu Kristo na kuamini

kikamilifu kazi aliyoifanya pale msalabani kwaajili yetu.

Ndio maana Marko aliandika hivi;

UHURU WA KWELI 158

“nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote,

na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa

nguvu zako zote” [Mark 12:30]

Ukisoma Tafsiri ya KJV anasema Kumpenda Bwana Mungu

wako kwa moyo wako wote na nafsi yako yote na akili yako

yote hii ndiyo sheria ya kwanza. Sheria yetu ya kwanza

nilazima tumwamini Yesu Kristo kwaajili ya kile

alichokifanya pale msalabani kwaajili yetu kikamilifu.

Roho zetu zimeathiriwa kwa zawadi, vipawa, huduma na

kazi ambavyo haviwezi kujidhihirisha kuwa halisi katika

macho ya damu na nyama kwa nguvu zetu bali kwa

msaada wake mwenyewe (Yesu Kristo).

Mungu, Roho Mtakatifu alishaachilia zawadi, vipawa,

karama, huduma na kazi kwa njia ya imani kupitia Yesu

Kristo, ambavyo hivyo navyo tulivyopewa haviwezi

kujidhihirisha kikamilifu bila msaada wake mwenyewe, ndio

maana Yesu Kristo aliwaambia wanafunzi wake;

“Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu

nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi

ninyi hamwezi kufanya neno lo lote” [Yoh 15:5]

Ili tuweze kuwa dhahiri katika macho ya damu na nyama

tunahitaji sana msaada wa Mungu. Ili tuweze kufanikisha

UHURU WA KWELI 159

tunachokihitaji, na kila tulichoitiwa kukifanya, kwa sababu

bila Yesu Kristo hatuwezi kufanya jambo lolote. Katika

ulimwengu wa roho kwa imani kupitia Yesu Kristo kila

tunachotakiwa kuwa nacho kila mmoja kwa nafasi yake na

kusudi ansapewa. Kiwango cha kujifunua kwa hicho

ulichopewa kuwa sehemu yako, kutategemeana na

kiwango cha kumtegemea yeye na kuishi katika yeye (Yesu

Kristo). Neema na kweli zilikuja kupitia Kristo (Yoh 1:17) ili

kusudi zitufundishe kuishi katika yeye, ili kutuwezesha

kuishi kwa haki, kiasi, na utakatifu kupitia neema yake (Tit

2:11-12).

Ni kusudi la Mungu sasa kukuona umekuwa kufikia utimilifu

wa Kristo na kuwa dhahiri katika macho ya damu na nyama

kama alivyo Yesu Kristo. Imeandikwa katika Waefeso 4:13-

16

13: hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na

kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu

mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu

wa Kristo

Kiu ya Mungu kama alivyotuchagua tangu asili ili tuwe kama

Mwana wake wa pekee yaani Yesu Kristo (Rum 8:29-30).

Mungu anataka ili tuweze kuwa watu wakamilifu nilazima

tuwe na maarifa kupitia mwana wake wa pekee Yesu Kristo,

UHURU WA KWELI 160

ili tuwe na kimo, cheo au kiwango sawa cha utimilifu kama

Yesu Kristo alivyo.

14: ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na

huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya

watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.

Kumbe kinyume na kuwa na ufahamu wa kumjua Mwana

wa Mungu yaani Yesu Kristo ni kuwa kama mtoto mchanga

na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, hila, ujanja na

udanganyifu, suluhisho la hili ni kumjua sana mwana wa

Mungu.

15: Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata

tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo.

Tukiishika kweli yaani neno la Mungu na upendo wake na

kumfikia Yesu Kristo katika yote. Maana yake maisha yetu,

ufahamu wetu, baraka zetu, huduma, vipawa na kazi zetu

ziendane na jinsi Yesu Krsto alivyo.

16: Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na

kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya

UHURU WA KWELI 161

utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate

kujijenga wenyewe katika upendo.

Kupitia karama, huduma, zawadi na kazi tulizopewa kila

mmoja kwa kusudi lake, tukiunganishwa na msaada wa kila

mmoja kwa nafasi yake. Mungu anataka tuwe hivyo ili

kuukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo wa

Yesu Kristo. Kumbe basi ni muhimu kumjua Kristo ili tusiwe

kama watoto wachanga, bali tukue tufikie kimo kama Yesu

Kristo alivyo. Ili tuweze kuukuza mwili wa Kristo katika

upendo kila mmoja akisimama kwa nafasi yake katika

kusudi alilopewa.

Hakuna jambo tutalifanya sisi wenyewe likawa ni bora

mbele za Mungu bila neema yake

Tuangalie kisa cha mfalme Sauli;

Wakati huo Samweli akamwambia Sauli, Bwana alinipeleka

nikutie mafuta, uwe mfalme wa watu wake Israeli; basi

sasa, isikilize sauti na maneno ya Bwana. Bwana wa

majeshi asema hivi, Nimeyatia moyoni mwangu mambo

hayo Amaleki waliyowatenda Israeli, jinsi walivyowapinga

njiani, hapo walipopanda kutoka Misri. Basi sasa enda

ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo

navyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na

UHURU WA KWELI 162

mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng'ombe na kondoo,

ngamia na punda.

Ndipo Sauli akawaita watu, akawahesabu huko Telemu,

askari waliopanda farasi mia mbili elfu, na watu wa Yuda

kumi elfu. Sauli akaufikilia mji wa Amaleki, akauvizia

bondeni. Sauli akawaambia Wakeni, Haya! Enendeni zenu,

mkashuke ili kujitenga na Waamaleki, nisije

nikawaangamiza ninyi pamoja nao; maana mliwatendea

wana wa Israeli mema, walipopanda kutoka Misri. Basi hao

Wakeni wakaondoka, wakajitenga na Waamaleki. Sauli

akawapiga Waamaleki, toka Havila uendapo Shuri,

unaokabili Misri.

Akamkamata Agagi, mfalme wa Waamaleki, yu hai,

akawaangamiza hao watu wote kwa upanga. Lakini Sauli

na watu wake wakamwacha Agagi hai, na katika kondoo

walio wazuri, na ng'ombe, na vinono, na wana-kondoo, na

cho chote kilicho chema, wala hawakukubali

kuwaangamiza; bali cho chote kilichokuwa kibaya na

kibovu, ndicho walichokiangamiza kabisa. Ndipo neno la

Bwana likamjia Samweli, kusema, Najuta kwa sababu

nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma,

asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli

akasikitika, akamlilia Bwana usiku kucha.

Samweli akaondoka asubuhi na mapema ili aonane na

Sauli; Samweli akaambiwa ya kwamba, Sauli alifika

UHURU WA KWELI 163

Karmeli, na tazama, akajisimamishia ukumbusho,

akageuka, akapita, akatelemkia Gilgali. Samweli

akamwendea Sauli; naye Sauli akamwambia, Ubarikiwe na

Bwana, nimeitimiza amri ya Bwana. Samweli akasema,

Maana yake nini, basi, hiki kilio cha kondoo masikioni

mwangu, na huu mlio wa ng'ombe ninaousikia? Sauli

akasema, Wamewaleta kutoka kwa Waamaleki; maana

watu waliwaacha hai kondoo na ng'ombe walio wazuri, ili

wawatoe dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, nao

waliosalia tumewaangamiza kabisa.

Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Ngoja, nami

nitakuambia neno aliloniambia Bwana usiku huu. Naye

akamwambia, Haya, sema. Basi Samweli akasema, Ingawa

ulikuwa mdogo machoni pako mwenyewe, je! Hukufanywa

kuwa kichwa cha kabila za Israeli? Naye Bwana akakutia

mafuta uwe mfalme wa Israeli. Kisha Bwana akakutuma

safarini, akasema, Enenda ukawaangamize kabisa wale

Waamaleki wenye dhambi, upigane nao hata

watakapoangamia. Mbona, basi, hukuitii sauti ya Bwana,

bali ukazirukia nyara ukafanya yaliyo maovu machoni pa

Bwana?

Sauli akamwambia Samweli, Hakika mimi nimeitii sauti ya

Bwana, nami nimemleta Agagi, mfalme wa Waamaleki,

tena nimewaangamiza Waamaleki kabisa. Ila watu

waliteka nyara, kondoo na ng'ombe walio wazuri, katika

UHURU WA KWELI 164

vitu vilivyowekwa wakfu, kusudi wavitoe dhabihu kwa

Bwana, Mungu wako, huko Gilgali. Naye Samweli akasema,

je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu

Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora

kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu. Kwani

kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri

na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye

naye amekukataa wewe usiwe mfalme.

Ndipo Sauli akamwambia Samweli, Nimefanya dhambi;

maana nimeihalifu amri ya Bwana, pia na maneno yako;

kwa sababu naliwaogopa wale watu, nikaitii sauti yao. Basi

sasa, nakuomba, unisamehe dhambi yangu; rudi pamoja

nami, nipate kumwabudu Bwana. Samweli akasema,

Sitarudi pamoja nawe; kwa sababu umelikataa neno la

Bwana, Bwana naye amekukataa wewe, usiwe mfalme wa

Israeli. Naye Samweli alipogeuka, aende zake, Sauli

akaushika upindo wa vazi lake, nalo likararuka. Basi

Samweli akamwambia, Leo Bwana amekurarulia ufalme wa

Israeli, naye amempa jirani yako, aliye mwema kuliko

wewe. Tena Yeye aliye Nguvu za Israeli hatanena uongo,

wala hataona majuto; maana siye mwanadamu, hata

ajute. Akasema, Nimekosa; lakini uniheshimu sasa,

nakuomba, mbele ya wazee wa watu wangu, na mbele ya

Israeli, rudi pamoja nami, nimwabudu Bwana, Mungu

wako. Basi Samweli akarudi na kuandamana na Sauli; naye

Sauli akamwabudu Bwana. [1Samw 15:1-31]

UHURU WA KWELI 165

Sauli alipewa maagizo na Bwana aende kuwapiga

Waameleki na kuviharibu vitu vyote na kuangamiza kila

mwanaume na mwanamke,mtoto, ng’ombe, na kondoo na

ngamia na punda. Sauli akakiuka agizo la Bwana akawaua

Waameleki lakini akamwacha hai mfalme Agagi wa

Waameleki, kondoo walio wazuri, ng’ombe vinono, na

kondoo na kila kilichokuwa chema. Lengo la Sauli lilikuwa ni

kumtolea Bwana dhabihu (sadaka), akafikiri Mungu

anapenda sana sadaka. Mungu akasema ninajuta kwakuwa

nimemtawaza Sauli kuwa Mfalme juu Israeli, Mungu

akamkataa Sauli asiwe Mfalme juu ya Israeli. Samweli

akamwambia Sauli kutii ni bora kuliko dhabihu (sadaka) na

kusikia kuliko mafuta ya beberu.

Tujiulize swali la Msingi, kwani Sauli alifanya kosa gani

mpaka Mungu aseme najuta nimemtawaza kuwa mfalme

juu ya Israeli?

Sauli alifikiri kwa kufanya mambo ambayo anafikiri Mungu

yanampendeza sana yaani kutoa dhabihu (sadaka) bila

kuishi vile Mungu anavyompa maelekezo ataonekana kuwa

bora mbele za Mungu. Kumbe mbele za Mungu aliona

amefanya kosa kubwa, yaani amefanya dhambi wakati

kiuhalisia Mungu anajifunua sana ukimtolea sadaka lakini

kwa sababu Sauli alienda kinyume na maelekezo ilikuwa

dambi kwake.

UHURU WA KWELI 166

Watu wengi wanapenda kuishi kwa miongozo ya kwao,

wanaigilizia kwa watu wengine walifanikiwaje baada ya

hapo wanaanza kuishi kwenye maisha ya watu wengine.

Wakati wote wanaishi maisha ya kufeli kwa sababu

hawataki kumuishia Mungu (Yesu Kristo). Sisi tulio katika

agano jipya tumepewa agizo la kuwa na maarifa ya ki-

Mungu, ili tumfananie Yesu Kristo ili tuishi kwa utimilifu

kama Yesu Kristo (2Kor 5:15). Nje ya kumuishia Kristo ni

kuishi maisha ya majuto, dhambi, kufeli, msongo wa

mawazo na kuchanganyikiwa. Kinyume cha kumuishia

Kristo hakuna jambo jema utafanya mbele za Mungu

litakuwa bora, mpaka umejizatiti kuishi sawa sawa kuishi

katika Kristo.

Lolote tutakalolifanya kwa juhudi zetu, hata kama

limefikia kiwango cha mwisho cha juhudi zetu bado

litaonekana liko chini ya kiwango mbele za Mungu.

“Watu wawili walipanda kwenda hekaluni kusali, mmoja

Farisayo, wa pili mtoza ushuru. Yule Farisayo akasimama

akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa

kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang'anyi,

wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. Mimi

nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato

yangu yote. Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala

hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali

UHURU WA KWELI 167

alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi

mwenye dhambi. Nawaambia, huyu alishuka kwenda

nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa

maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye

atakwezwa” [Luk 18:10-14]

Kibinadamu Farisayo alikuwa na haki ya kuhesabiwa haki

kuliko Mtoza ushuru, lakini kosa la Farisayo lilikuwa ni

kutumaninia juhudi zake na uwezo wake kuhesabiwa haki.

Kama ilivyokuwa kanuni Mafarisayo walimkataa Yesu

walifikiri kwa juhudi zao ndio wanahesabiwa haki pasipo

kuishi katika Kristo. Ni vyema kufanya kila jambo kwa juhudi

lakini tusitumainie juhudi zetu bali tuishi katika Kristo na

kuamini ukamilifu wa kazi yake aliyoifanya kwaajili yetu.

Kufanya jambo lolote sisi wenyewe bila kupitia kwa Yesu

Kristo ni sawa na kusema sihitaji msaada wako Mungu.

Mungu alimtoa Mwana wake wa pekee, ili awe mbadala

wetu, Mungu kwa mapenzi yake mwenyewe aliamua

kumtoa Kristo. Ili aje kutusaidia na Kristo kusimama kwenye

nafasi yetu na sisi tukae kwenye nafasi yetu. Yesu Kristo

hakuwa na hatia lakini alifanyika mwenye hatia kwaajili

yetu, Yesu Kristo alikuwa mtakatifu lakini alifanyika

mwenye dhambi kwaajili yetu. Yesu Kristo alikuwa mwenye

UHURU WA KWELI 168

haki lakini alifanyika asiye na haki ili sisi tuwe wenye haki

katika yeye. Imeandikwa;

“Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani

mwake. Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano;

alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye

ahukumuye kwa haki. Yeye mwenyewe alizichukua dhambi

zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo

ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa

kwake mliponywa. Kwa maana mlikuwa mnapotea kama

kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi

wa roho zenu” [1Petr 2:22-25]

Kama Kristo alikufa kwaajili yako akafanyika mwenye

dhambi ili uwe mtakatifu, na mwenye haki. Kutafuta

utakatifu wako binafsi na haki yako ni kumfedhehi Mwana

wa Adamu na kuikanyaga damu yake, ni sawa na kusema

Yesu Kristo alikufa bure, hakuna alilonisaidia, au

hakunisaidia kikamilifu. Ndio maana unataka kujitahidi

wewe mwenyewe binafsi, ni sawa na kumwambia Mungu

sihitaji msaada wako. Ukiamua kuishi kwa juhudi zako yeye

atakuacha ujiishie mwenyewe na mwisho wake utakuwa ni

mtu wa kushindwa na kufeli. Kubali kuanza kuishi katika

Kristo ili uwe mtoshelevu na mkamilifu mbele za Mungu.

UHURU WA KWELI 169

Tathmini kupitia maswali kutoka katika Sura ya Tano

1: Kutoka katika sura hii namna gani ya kuambatana na

neno la Mungu ili uweze kupata matokeo?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

2: Taja sababu saba kwanini tuishi katika Yesu Kristo?

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

(iii)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

(iv)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

(v)………………………………………………………………………………………

……………………………………....

(vi)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

UHURU WA KWELI 170

(vii)……………………………………………………………………………………

…………………………………………

3: Tofautisha kati ya kuishi kwa sheria na kuishi kwa neema

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

4: Kutokana na ulivyojifunza katika sura hii, taja ngazi tatu

za sheria

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

(iii)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

5: Taja sheria iliyokamilifu (Mungu anayoiangalia)

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

UHURU WA KWELI 171

SURA YA SITA

YESU KRISTO ALIMALIZA YOTE MSALABANI

“Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema,

imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake” [Yoh

19:30]

Biblia inaposema roho yake biblia ya kigiriki imetumia

maneno “ekpneo” na ekpsucho”. Maana yake kutoa pumzi

nje. Baada ya Yesu kutoa pumzi nje alipumzika.Yesu

alipopumzika ndiko tunapotakiwa kuanzia. Maandiko

yanasema;

“Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu

yake, na kutufanya kuwa ufalme, makuhani kwa Mungu

naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una yeye hata milele na

milele.Amina” [Ufu 1:5]

Katika mstari huu tafsiri ya biblia ya kiingereza KJV

inaonyesha kuwa tulioshwa kwa damu yake kupitia damu

yake tulifanywa kuwa wafalme na makuhani. Yesu

alikamilisha kila alichotakiwa kukifanya kupitia msalaba

wake. Msalaba wa Kristo ni hatima ya mambo yote

yaliyokuwa yakitutesa. Ndio maana Paulo ameandika;

UHURU WA KWELI 172

“Maana Kristo hakunituma ili nibatize, bali niihubiri Habari

Njema; wala si kwa hekima ya maneno, msalaba wa Kristo

usije ukabatilika. Kwa sababu neno la msalaba kwao

wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu

ya Mungu” [1Kor 1:17-18]

Msalaba ilikuwa ni hatima ya Yesu Kristo kuja katika

ulimwengu huu, ndio maana pasipo Kristo sisi ni bure,

pasipo msalaba hakuna chochote ambacho kimebadilika.

Pasipo Kristo ni kuibatili neema ya Kristo ndio maana kuishi

nje ya neema ni kuibatili neema ya Kristo. Ndio maana

Paulo aliandika kuwa msalaba kwao wanaopotea ni upuzi

bali sisi tunaokolewa ni nguvu ya Mungu.

Ndio maana Paulo aliwaandikia Wagalatia;

“Lakini mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu cho chote ila

msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo

ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa

ulimwengu” [Gal 6:14]

Paulo anasema haonei fahari juu ya kitu chochote ila

msalaba wa Bwana Yesu Kristo. Msalaba wa Kristo

unaonyesha upatanisho kati ya Mungu na wanadamu na

upatanisho wa wanadamu kwa wanadamu. Msalaba wa

Kristo ni kiwakilishi cha upendo wa Mungu katika maisha

yetu; ndio maana imeandikwa;

UHURU WA KWELI 173

“Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani,

vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa; ili kila

mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye. Kwa

maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa

Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali

awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma

Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali

ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye

hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa

sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu” [Yoh

3:14-18]

Yesu Kristo kutolewa msalabani, ilikuwa ni kiwakilishi cha

upendo wa Mungu kwenye maisha yetu. Mungu

alimuhukumu Yesu msalabani kwa aniaba yetu, tulistahili

adhabu sisi, tulistahili kuteswa sisi, tulistahili kufa sisi.

Mungu alimtoa sadaka Mwana wake wa pekee Yesu Kristo

ili sisi tuwe huru, katka maisha (dhambi, magonjwa,

vifungo) (Rum 5:17). Hukumu ya Mungu iliishia msalabani

hakuna namna aliyemwamini Yesu Kristo atahukumiwa bali

ambaye hajamini hukumu yake imekwisha tolewa.

Imeandikwa;

“Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa sababu

hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema” [Rum 6:14]

Dhambi haina nguvu tena ya kututawala kwa sababu Yesu

Kristo aliikomesha na kuishinda pale msalabani. Mauti na

UHURU WA KWELI 174

kuzimu nguvu yake imeshindwa kwa sababu ya Yesu Kristo.

Tulitakiwa kuhukumiwa adhabu kali sana lakini Yesu

alihukumiwa na alipewa hiyo adhabu kusudi kila

anayemwamini Yeye asihukumiwe. Ndio maana Paulo

aliwaandikia Warumi;

“Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika

Kristo Yesu. Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio

katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya

dhambi na mauti. Maana yale yasiyowezekana kwa sheria,

kwa vile ilivyokuwa dhaifu kwa sababu ya mwili, Mungu,

kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe katika mfano wa

mwili ulio wa dhambi, na kwa sababu ya dhambi,

aliihukumu dhambi katika mwili; Kwa maana wale

waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale

waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho. Kwa kuwa nia ya

mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani. [Rum

8:1-6]

Kila aliyeko ndani ya Yesu Kristo hawezi kuhukumiwa, kwa

sababu Mungu alimtuma mwanawe mwenye mfano wa

mwili wa dhambi. Ili aihukumu dhambi katika mwili yake,

ndio maana kila anayemwamini yeye ahukumiwi kwa

sababu Mungu alimhukumu Yesu Kristo kwa aniaba yetu.

Ndio maana msalaba wa Kristo kwao wanaopotea ni upuzi

bali msalaba ni nguvu ya Mungu kwetu sisi. Kwa njia ya

yeye (Yesu Kristo) kupitia damu yake na jina lake

UHURU WA KWELI 175

tulitakaswa na kuondolewa dhambi zetu; Ndio maana Yesu

aliwaambia Wanafunzi wake;

“Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na

maandiko. Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba

Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba

mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na

ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. [Luk 24:46-

47]

Yesu aliwaambia Wanafunzi wake kwa jina lake watu

watahubiriwa toba ya ondoleo la dhambi. Petro naye

alitekeleza ujumbe huo alioambiwa na Bwana Yesu wa

kuhubiri toba ya ondoleo la dhambi kwa imani ya jina la

Yesu.

“Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa

jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi

mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu” [Mat 2:38]

Luka pia alihubiri ya kuwa hata manabii wanashuhudia ya

kuwa kwa jina la Yesu kila anayemwamini hupata ondoleo

la dhambi.

“Akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudia ya kuwa huyu

ndiye aliyeamriwa na Mungu awe Mhukumu wa walio hai

na wafu. Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba

kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi”

[Mat 10:42-43]

UHURU WA KWELI 176

Ndio maana Yesu Kristo kupitia mwili wake msalabani

aliuondoa uadui kati yetu na Mungu ili atufanye kuwa watu

wapya ndani ya nafsi yake na kutufanyia amani.

Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo

sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili

kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya

amani. [Gal 2:16]

Kupitia nafsi ya Yesu Kristo kupitia damu ya msalaba wake

alivipatanisha vitu vyote. Vitu vyote vilivyo juu ya nchi na

vilivyo mbinguni. Kwa sababu hiyo mimi na wewe tumepata

upatanisho.

Kwa kuwa katika yeye ilipendeza utimilifu wote ukae; na

kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake akiisha

kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye,

ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni. [Kol

1:19-20]

Yesu Kristo alinyenyekea mpaka mauti ya msalaba,

kwasababu kupitia msalaba ilikuwa ni ukamilifu wa kazi

iliyomleta duniani. Alihakikisha anafikia msalabani ili

kuhitimisha kiliochomleta duniani kwaajili ya ukombozi.

UHURU WA KWELI 177

“tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu,

alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya

msalaba” [Filip 2:8]

Ndio maana hakuna hati ya mashitaka tena, hukumu wala

uadui akaondoa vyote visiwepo tena, akavigogomelea

msalabani. Ndio maana alivua enzi yake na mamlaka

akashuka kuja kwetu KJV anasema akaviweka wazi na

kuvishangilia kupitia huo msalaba;

akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa

hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo

tena, akaigongomea msalabani; akiisha kuzivua enzi na

mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri,

akizishangilia katika msalaba huo. [Kol 2:14-15]

Kristo aliidharau aibu yake, ndio maana aliustahimili

msalaba kusudi aikamilishe kazi yake na kumaliza kazi yote

iliyomleta. Paulo anaendelea kusema; Tumezungukwa na

wingu kubwa la mashahidi namna hii tupige mbio na

kuweka kando kila mzigo mzito tukimtazama Yesu Kristo.

“Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa

la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito,

na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa

saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza

imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele

UHURU WA KWELI 178

yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi

mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu” [Ebr 12:1-2]

Na kwasababu hiyo ndio maana Petro aliandika;

“Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili

awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa

zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa

mambo yenu” [1Pet 5:6-7]

Mtwike Yesu Kristo fadhaa zako, uwe unachangamoto ya

kiuchumi, kudharauliwa kukataliwa, msongo wa mawazo.

Mtwike Yesu Kristo msalabani baada ya hapo kuwa huru.

Ikiwezekana andika shida yako kwenye diary mkabidhi Yesu

aishughulikie hiyo shida yako. Shetani akikukumbusha

kuwa mbona Mungu wako anachelewa kukujibu? Wewe

muonyeshe mahali ulipoandika. Mwambie Mungu

anashughulikia, mwambie Mungu analifanyia kazi.

Mwambie kwa sababu Yesu alimaliza yote msalabani

kwaajili yangu majibu yangu yapo karibu sana, na asubuhi

yangu ipo mlangoni. Usikubali Shetani akukandamize

ufahamu wangu, usikubali Shetani ukukumbushe jinsi

ulivyofeli. Mwambie Yesu wangu alishafaulu na alifanikiwa

pale msalabani kwaajili yangu kwahiyo sitafeli tena.

UHURU WA KWELI 179

Mshinde Shetani kwa neno la ushuhuda na damu ya

Mwanakondoo (Yesu Kristo) Msalabani.

Ndio maana imeandikwa;

“Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa

wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka

ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa

ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu,

mchana na usiku. Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-

Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao” [Ufu 12:10-11a]

Kazi ya Shetani usiku na mchana ni kukushitaki,

kukuhukumu, kukulaghai, kukuonyesha kushindwa na

kufeli. Hakuna namna tunaweza kumshinda Shetani zaidi

kushuhudia neno na damu ya Mwanakondoo. Yesu Kristo

aliyekufa kwaajili yetu akachukua udhaifu wetu na

masikitiko yetu. Kumbe Shetani kumshinda ni rahisi sana

tumia mambo mawili kumshinda; neno la ushuhuda na

damu ya Yesu Kristo. Ndio maana Yesu alimshinda Shetani

kwa neno la ushuhuda; imeandikwa;

“Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka

Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini

nyikani, akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu;

hata zilipotimia, aliona njaa. Ibilisi akamwambia, Ukiwa

ndiwe Mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate. Yesu

akamjibu, Imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate

UHURU WA KWELI 180

tu. Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za

ulimwengu kwa dakika moja. Ibilisi akamwambia, Nitakupa

wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi

mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo. Basi,

wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako.

Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana

Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. Akamwongoza

mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu,

akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe

chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake

wakulinde; na ya kwamba,mikononi mwao watakuchukua,

Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. Yesu akajibu

akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.

Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha akaenda zake

kwa muda” [Luk 4:1-13]

Shetani hawezi kukwambia wewe unanguvu kiasi gani

katika Kristo, wala hawezi kukwambia wewe ni nani katika

Yesu Kristo. Mshinde kwa neno la ushuhuda wa Yesu Kristo,

akikwambia na wewe unamaisha yamechoka umechakaa.

Mwambie imeandikwa katika Yesu Kristo nimebarikiwa kwa

baraka zote katika ulimwengu wa roho (Efe 1:3). Kwahiyo

subiri udhihiridsho wa baraka zangu ziko njiani, akikwambia

unajiita mtakatifu wewe! Umesahau ulivyozini! umesahau

ulivyoiba! umesahau ulivyodanganya! Umesahau ulivyo

laghai! Mwambie imeandikwa mimi ni Mtakatifu (Rum

UHURU WA KWELI 181

8:29-30, Efe 1:3-6), sina mawaa wala hatia katika Kristo

Yesu Kristo alilipia gharama ya haya yote unayonishitaki

miaka elfu mbili iliyopita, na kwasababu hiyo kwa neema

yake sitarudia tena, kwa sababu Yesu Kristo hata sasa

anaishi ndani yangu.

Damu ya Mwanakondoo (Yesu Kristo).

Kisha nikaona katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi

juu ya kile kiti cha enzi kitabu kilichoandikwa ndani na

nyuma, kimetiwa muhuri saba. Nikaona malaika mwenye

nguvu akihubiri kwa sauti kuu, N'nani astahiliye kukifungua

kitabu, na kuzivunja muhuri zake? Wala hapakuwa na mtu

mbinguni, wala juu ya nchi, wala chini ya nchi, aliyeweza

kukifungua hicho kitabu, wala kukitazama. Nami nikalia

sana kwa kuwa hapakuonekana mtu astahiliye kukifungua

hicho kitabu, wala kukitazama. Na mmojawapo wa wale

wazee akaniambia, Usilie; tazama, Simba aliye wa kabila ya

Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile

kitabu, na zile muhuri zake saba.

Nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale wenye uhai

wanne, na katikati ya wale wazee, Mwana-Kondoo

amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye

pembe saba na macho saba, ambazo ni Roho saba za

Mungu zilizotumwa katika dunia yote. Akaja, akakitwaa kile

UHURU WA KWELI 182

kitabu katika mkono wa kuume wake yeye aliyeketi juu ya

kile kiti cha enzi. Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye

uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka

mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na

vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni

maombi ya watakatifu.

Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe

kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa

kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako

watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,

ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu;

nao wanamiliki juu ya nchi. Nikaona nikasikia sauti ya

malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale

wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu

kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu, wakisema kwa sauti

kuu, Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea

uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu

na baraka.

Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya

nchi ya juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake,

nalivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na

uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na yeye Mwana-

Kondoo, hata milele na milele. Na wale wenye uhai wanne

wakasema, Amina. Na wale wazee wakaanguka,

wakasujudu. [Ufu 5:1-14]

UHURU WA KWELI 183

Mwanakondoo (Yesu Kristo) mzee wa siku yeye aliyeshinda

alikubali kufungua kile kitabu na muhuri zake. Alipokitwaa

kile kitabu wenye uhai wane na wale wazee ishirini na nne

walianguka wakasujudu mbele zake. Wakisema unastahili

kukichukua kile kitabu na kuzifungua mihuri zake, sauti za

malaika wengi zilisikika. Kwa hesabu yao ni ilikuwa elfu

kumi mara elfu kumi mara elfu wakisema unastahili

Mwanakondoo kwa damu yako. Uliwanunua watu wa kila

kabila, lugha na jamaa na taifa, na kupitia damu yako (yaani

wale waliomwamini) uliwafanya kuwa wafalme, makuhani,

wakamtukuza milele yote mwanakondoo (Yesu Kristo).

Ndio maana kupitia damu yake tuliokolewa. Ndio maana

Paulo aliandika;

“Lakini Kristo akiisha kuja, aliye kuhani mkuu wa mambo

mema yatakayokuwapo, kwa hema iliyo kubwa na kamilifu

zaidi, isiyofanyika kwa mikono, maana yake, isiyo ya

ulimwengu huu, wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali

kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika

Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele. Kwa

maana, ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya

ndama ya ng'ombe waliyonyunyiziwa wenye uchafu

hutakasa hata kuusafisha mwili; basi si zaidi damu yake

Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi

yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa,

UHURU WA KWELI 184

itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate

kumwabudu Mungu aliye hai?” [Ebr 9:11-14]

Yesu alijitoa nafsi yake na kupitia damu yake tulitakaswa na

kuwa watu tusio na uchafu wala mawaa.

Yohana aliandikia makanisa saba kuwa tulioshwa kwa

damu ya Yesu;

“Yohana, kwa yale makanisa saba yaliyoko Asia; Neema na

iwe kwenu na amani, zitokazo kwake yeye aliyeko na

aliyekuwako na atakayekuja; na zitokazo kwa roho saba

walioko mbele ya kiti chake cha enzi; tena zitokazo kwa

Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza

wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye

atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake”

[Ufu 1:4-5]

Yesu aliyemzaliwa wa kwanza na mkuu wa wafalme wa

dunia alitupenda na kutuosha dhambi zetu, ndio maana

tunatakiwa kwenda nuruni kwasababu damu ya Yesu

ilitusafisha dhambi zetu;

“bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru,

twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana

wake, yatusafisha dhambi yote” [1Yoh 1:7]

UHURU WA KWELI 185

Petro aliandika tulikombolewa si kwa vitu viharibikavyo,

fedha wala dhahabu. Bali kwa damu ya thamani ya

Mwanakondoo (Yesu Kristo) asiye na hila wala mawaa.

“Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu

viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika

mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu; bali

kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na

ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo” [1Pet 1:18-19

Kupitia damu ya Yesu tulipata neema ya kupaingia

patakatifu kwa ujasiri bila hofu na uwoga. Yesu alibadili

historia pale msalabani na kupitia Yeye tukafanyika wana

ndio maana tunapoenda kwa Mungu tunaenda kwa Baba

yetu kuongea naye,

“Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia

patakatifu kwa damu ya Yesu” [Ebr 10:19]

Yesu aliingia patakatifu kupitia damu yake mara moja na

kuupata ukombozi wa milele;

“wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake

mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha

kupata ukombozi wa milele” [Ebr 9:12]

Ukombozi huu ni ukombozi usiohusisha mchango wowote

kutoka kwako. Ulijitosheleza na hivyo wewe ni nafasi yako

UHURU WA KWELI 186

kuamini na kuambatana na hii kweli ili iwe halisi kwenye

macho ya damu na nyama.

UHURU WA KWELI 187

Tathmini kupitia maswali kutoka katika Sura ya Sita

1: Taja maana ya haya maneno ya kigiriki “ekpneo na

ekpsucho”

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

2: Taja mfumo wa maisha unaopelekea kuto tawaliwa na

dhambi

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

3: Namna gani ya kushinda hila/uongo wa Shetani. Taja

mambo mawili

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

UHURU WA KWELI 188

UHURU WA KWELI 189

SURA YA SABA

MIMI SI MFUNGWA TENA

Maandiko yanasema;

“Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana

amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema;

amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo,

kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa

habari za kufunguliwa kwao” [Isa 61:1]

Isaya alitabiri ujio wa Yesu Kristo mpakwa mafuta (Masihi

wa Bwana) kuwa atakuja kuwahubiri; wanyenyekevu habari

njema, kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia

mateka uhuru wao na waliofungwa habari za kufunguliwa

kwao. Maneno haya aliyotabiri Isaya yalitimia Yesu

alipokuja duniani. Yesu alipokwenda Nazareti alipewa

kitabu cha nabii Isaya kukisoma. Imeandikwa;

“Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia

mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma

kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu

kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, Na

kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa. Akakifunga

chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote

waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.

UHURU WA KWELI 190

Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia

masikioni mwenu” [Luk 4:18-21]

Yesu alithibitisha kuwa alikuja kuwatangazia wafungwa

kufunguliwa kwao, vipofu kuona tena na kuwaacha huru

waliofungwa. Na kuwaambia wote kuwa maneno haya

yametimia masikioni mwenu. Yesu ilikuwa ni desturi yake

kila mahali alipopita aliwafungua watu waliokuwa

wamekamatwa na kuteswa na ibilisi. Imeandikwa;

“habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta

kwa Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na

huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na

Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye. Nasi tu

mashahidi wa mambo yote aliyoyatenda katika nchi ya

Wayahudi na katika Yerusalemu; ambaye walimwua

wakamtundika mtini. Huyo Mungu alimfufua siku ya tatu,

akamjalia kudhihirika, si kwa watu wote, bali kwa

mashahidi waliokuwa wamekwisha kuchaguliwa na

Mungu, ndio sisi, tuliokula na kunywa pamoja naye baada

ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu. Akatuagiza

tuwahubiri watu na kushuhudia ya kuwa huyu ndiye

aliyeamriwa na Mungu awe Mhukumu wa walio hai na

wafu. Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa

jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi

[Mate 10:38-43]

UHURU WA KWELI 191

Katika uweza wa nguvu za Roho Mtakatifu Yesu Kristo

alikuwa akitenda kazi na kuwaponya wote walioonewa na

Ibilisi, Mungu alikuwa akitenda kazi pamoja naye. Luka

anathibitisha kuwa walitumwa kuwa mashahidi wa mambo

yote aliyoyatenda katika Wayahudi na Yerusalemu kwamba

aliuawa na kutundikwa mtini (msalabani), na kushuhudia ya

kwamba kwa jina lake Yesu kila aaminiye apate ondoleo la

dhambi. Dhambi haziondolewi kwa kulia kwa machozi

dhambi zinaondolewa kwa kuamini jina la Yesu na

kumwamini mwana wa Mungu. Imeandikwa;

“Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa

jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi

mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu” [Mate 2:38]

Petro aliwaambia tubuni mkabatizwe kwa jina lake Yesu

Kristo Mpate ondoleo la dhambi na kupokea kipawa cha

Roho Mtakatifu. Maana yake kwa kuliamini jina la Yesu

watu wanapata ondoleo la dhambi. Luka pia aliandika kuwa

kwa kuamini jina la Yesu tunapata ondoleo la dhambi;

“Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo

atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote

watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la

dhambi, kuanza tangu Yerusalemu” [Luk 24:45-46]

UHURU WA KWELI 192

Luka aliandika kuwa iliandikwa kuwa Kristo atateswa na

kufufuka siku ya tatu na mataifa yote watahubiriwa kwa jina

lake toba ya ondoleo la dhambi.

Toba sio kulia kwa machozi juu ya makosa uliyofanya;

toba ni kubadili mtazamo na kugeuka.

Neno toba katika biblia ya kigiriki limetumika neno

“metanoia” maana yake badili mtazamo katika lugha mama

ya kiebrania limetumika neno “teshuvah” maana yake

geuka. Kulia kwa machozi ukiwa umefanya kosa sio toba

toba ni kubadili mtazamo na kugeuka. Unaweza ukalia lakini

bado ukawa hujabadili mtazamo na haujageuka. Ndio

maana kuna idadi ya watu wengi ambao wanaenda mbele

za Mungu wanalia na kuomba msamaha juu ya makosa yao

lakini baada ya mda wanarudia makosa yale yale. Tafsiri

nyepesi ni kwamba hawakutubu, toba halisi inahusisha

kugeuzwa nia ya ndani kwa kubadili mtazamo na matokeo

yake yatakuwa ni kugeuka. Ndio maana imeandikwa;

“Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa

kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya

Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu” [Rum

12:2]

Nia ya ndani ikibadilishwa inapelekea kujua mapenzi ya

Mungu na ukamilifu. Nia ya ndani inageuzwa kwa kulisikia

UHURU WA KWELI 193

neno la Kristo na ufunuo kutoka kwake. Neno la Kristo

likikaa ndani linapelekea kujua mapenzi ya Mungu na

ukamilifu. Paulo anaandika kuwa;

“Bali ninyi, sivyo mlivyojifunza Kristo; ikiwa mlimsikia

mkafundishwa katika yeye, kama kweli ilivyo katika Yesu,

mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani,

unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya; na

mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; mkavae utu mpya,

ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu

wa kweli” [Efe 4:20-24]

Ukijifunza katika Yesu Kristo nilazima uuvue utu wa zamani

na tama zake yaani uongo, wizi, uzinzi, kuabudu miungu

mingine, husuda, fitina na mwenendo mzima wa utu wa

zamani. Vyote hivi vinaondolewa kwa kujifunza katika Yesu

Kristo kweli yake na ufunuo wa Yesu Kristo ndio maana

imeandikwa;

“Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi;

mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika

ufunuo wake Yesu Kristo” [1 Pet 1:13]

Kupitia ufunuo wa Yesu Kristo neema inafunuliwa

inayopelekea kugeuzwa nia na kufikia kiasi (uwezo wa

kujizuia) na utimilifu. Utimilifu unapatikana kwa kujifunza,

kukaa darasani na kulisikia neno la Kristo (Efe 4:13).

UHURU WA KWELI 194

Yesu Kristo alituweka huru na kila aina ya vizuizi na

vifungo.

Maandiko yanasema;

“Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo

kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo. Kwa

maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote

tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha

kati kilichotutenga” [Efe 2:14]

Tafsiri ya Biblia ya NENO (NEN) inasema hivi;

“Lakini sasa katika Kristo Yesu, ninyi ambao hapo kwanza

mlukuwa mbali na Mungu, sasa mmeletwa karibu kwa njia

ya damu ya Kristo. Kwa maana yeye mwenyewe ndiye

amani yetu, aliyetufanya sisi tuliokuwa wawili, yaani,

Wayahudi na watu wa Mataifa, tuwe wamoja kwa kuvunja

kizuizi na kubomoa ule ukuta wa uadui uliokuwa kati yetu”

Yesu Kristo kupitia damu yake alitufanya kuwa wamoja na

kuvunja vizuizi vyote vilivyokuwa vimetutenga kati yetu.

Yesu Kristo kwa njia ya msalaba alituacha huru na kubomoa

kila vizuizi na vifungo vilivyokuwa vimetutenga kati yetu sisi

wanadamu na Mungu. Imeandikwa;

UHURU WA KWELI 195

“Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa

roho yake. Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande

viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba

ikapasuka” [Math 27:50-51]

Pazia la hekalu lilipasuka vipande viwili kuashiria kuwa tuko

huru kupaingia patakatifu pa patakatifu. Hakuna kizuizi tena

katika Yesu Kristo kila aliye na Yesu Kristo amekuwa na

uhuru kweli kweli sasa anaweza kupaingia patakatifu. Ndio

maana Yesu Kristo baada ya kufa alienda kuzimu

kunyang’anya funguo za mamlaka na kuzimu alizokuwa

nazo Shetani;

“Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu

aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu,

akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na

aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata

milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za

kuzimu” [Ufu 1:17-18]

Yesu anazo funguo za mauti na kuzimu na aliishinda mauti

na kuzimu kutuacha huru na gereza la dhambi na mauti.

Imeandikwa;

“Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo

Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti”

[Rum 8:2]

UHURU WA KWELI 196

Kwa njia ya Msalaba wa Yesu Kristo tuliachwa huru mbali na

sheria ya dhambi na mauti. Paulo anasema;

“Bali kwa ajili ya ndugu za uongo walioingizwa kwa siri;

ambao waliingia kwa siri ili kuupeleleza uhuru wetu tulio

nao katika Kristo Yesu, ili watutie utumwani; ambao hata

saa moja hatukujitia chini yao, ili kwamba kweli ya Injili ikae

pamoja nanyi” [Gal 2:4-5]

Paulo anaeleza kuwa wako watu ambao hawakubali kujitia

chini yao lengo lao lilikuwa ni kuwatia utumwani. Lengo lao

lilikuwa kuwaweka utumwani kwa kuipotosha kweli ya injili

ya Yesu Kristo. Ndio maana Paulo anasema tulikataa kujitia

chini yao kusudi kweli ya injili ikae pamoja naye. Maana

yake kweli ya injili ikihubiriwa watu wanawekwa huru,

yoyote anayeijua kweli ya injili hawi mtumwa. Injili ya kweli

inayomuweka mtu huru ni kupitia neno la Kristo, ndio

maana Yesu Kristo alisema;

“Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini,

Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi

wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli

itawaweka huru” [Yoh 8:31-32]

Kupitia neno la Yesu Kristo watu wanawekwa huru kweli

kweli. Yesu alikuwa anawaambia Wayahudi na walioamini

kuwa kaeni katika neno. Kwa sababu wakikaa katika neno la

Yesu Kristo waijua kweli na hiyo kweli itawaweka huru.

UHURU WA KWELI 197

Kwahiyo kupitia Kristo na neno lake tu awekwa huru ukiwa

na Kristo unakuwa huru ukikaa katika neno lake (kujifunza)

unakuwa na kutoka kuwa mototo mchanga ili uwe mtu

mzima. Kusudi ufikiri kama Kristo, unene kama Kristo na

utende kama Yesu Kristo. Ndio maana imeandikwa;

“Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”

[Yoh 8:36]

Kupitia Yesu Kristo tunakuwa huru, huwezi ukawa ndani ya

Kristo ukawa na vifungo, magonjwa, laana, mikosi. Ukiona

umeamini halafu nafsi yako au Shetani anakwambia wewe

ni mfungwa ujue huo ni uongo. Uongo tunautambua kwa

kulijua neno la Kristo kila kilicho kinyume na neno la Kristo

ni uongo, kwahiyo usisite kuupinga huo uongo. Ndio maana

imeandikwa;

1: Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye

mkulima.

2: Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi

lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa.

3: Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno

nililowaambia.

UHURU WA KWELI 198

4: Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi

lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu;

kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.

Yesu anasema Baba ni mkulima (Mungu Baba), Yesu ni

mzabibu na sisi ni matawi, Yesu anasisitiza kuwa sisi

tumekuwa safi katika lile neno alilotuambia. Neno hilo ni hili

anasema; tukae ndani yake Kristo ndiyo maana anasema

pasipo Yeye sisi hatuwezi kuzaa kwahiyo nilazima tukae

ndani yake.

5: Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu

nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi

ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.

Kila anayekaa ndani ya Yesu Kristo huzaa sana pasipo Yesu

Kristo sisi hatuwezi kufanya neno lolote.

6: Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na

kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni

yakateketea.

Yesu anasema na mtu asipokaa ndani yake

(asipoamini/asipozaliwa mara ya pili/asipookoka) hutupwa

nje na kutupwa motoni yaani katika jehanamu ya moto

7: Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa

ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa [Yoh

15:1-7]

UHURU WA KWELI 199

Tukikaa ndani yake kwa maana ya kumwamini na tukilishika

neno la Yesu Kristo. Kila lolote tutakaloomba tutatendewa.

Tunajibiwa maombi kwa kumwamini Kristo na kulishika

neno la Kristo. Ukienda mbele za Mungu ili upokee majibu

ya maombi yako nilazima tuwe na neno la Yesu Kristo na

tuimwamini Yesu Kristo tukalishika neno lake tunakuwa

huru kweli kweli. Ndio maana Yesu aliwaombea wanafunzi

wake kuwa;

“Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli” [Yoh

17:17]

Kwahiyo neno la Kristo linatutakasa na kutuweka huru kwa

njia ya imani ya Yesu Kristo. Kwahiyo tukiijua kweli ya neno

la Mungu tunafanyika huru kweli kweli. Kwa sababu hakuna

jambo lolote litatusumbua kwenye maisha yetu katika kila

eneo. Ndio maana tunapaswa kulifuata neno la kweli ya

Yesu Kristo. Maandiko yako wazi kwa sababu kila kitu

tulichokuwa tunakihitaji kwaajili yetu Kristo alishamaliza.

Katika eneo la uchumi, afya, amani, furaha Yesu alimaliza na

kutupigania pale msalabani;

i. Katika eneo la uchumi imeandikwa;

“Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi

alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili

UHURU WA KWELI 200

kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake”

[2Kor 8:9]

Kwasababu ya Kristo aliyekuwa tajiri lakini akafanyika

maskini kwaajili yetu ili kupitia umaskini wake sisi tupate

kuwa matajiri. Ni jukumu letu kuambatana na hili neno na

kuliamini na kuliishi.

ii. Katika eneo la afya imeandikwa;

“Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili

wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe

hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa

[1Pet 2:24]

Kupigwa kwa Yesu kilikuwa chanzo cha sisi kupokea

uponyaji. Tunatakiwa kuambatana na hili neno kuliamini na

kuliishi. Ugonjwa ukija wewe sema Yesu alikufa kwaajili

yangu bila kujali hali ya nje. Ukishikilia baada yam da

uponyaji utakuwa juu yako.

iii. Katika eneo la amani imeandikwa;

“Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo

yenu na nia zenu katika Kristo Yesu” [Filip 4:7]

UHURU WA KWELI 201

Katika Yesu Kristo kuna amani ipitayo akili zote. Kupitia hiyo

amani inatuhifadhi mioyo yetu na nia zetu. Ndio maana

Yesu aliwaambia wanafunzi wake;

“Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo

mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni

mwenu, wala msiwe na woga” [Yoh 14:27]

Amani ya Kristo inatupa ujasiri na sio uwoga, amani ya

Kristo inatuhifadhi katika nia zetu na mioyo yetu.

iv. Katika eneo la furaha imeandikwa;

“Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini”

[Filip 4:4]

Katika Bwana Yesu tunakuwa na furaha suku zote.

Inawezekana kuwa na furaha siku zote katika Yesu Kristo.

Kama ingekuwa haiwezekani isingeandikwa. Ndio maana

Luka aliandika; Kwa maana ndani yake tunaishi,

tunakwenda, na kuwa na uhai wetu (Mate 17:28a)

“Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo

simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la

utumwa” [Gal 5:1]

UHURU WA KWELI 202

Biblia ya Habari Njema inasema hivi;

“Kristo alitupa uhuru, akataka tubaki huru. Basi, simameni

imara wala msikubali tena kuwa chini ya nira ya utumwa”

Katika Yesu Kristo tunakuwa huru, Yesu anataka tuwe huru

ndio maana anasema tusimame wala tusikubali kuwa chini

ya nira ya utumwa. Sisi sio watumwa kabisa ndani ya Yesu

Kristo tuko huru kabisa ndani yake. Amen Haleluya!

UHURU WA KWELI 203

Tathmini kupitia maswali kutoka katika Sura ya Saba

1: Kwanini wewe uliyeamini(uliyeokoka) uko huru (sio

mfungwa)?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

2: Eleza kwa ufupi maana halisi ya toba

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

3: Yesu alimaliza kila kitu kinachohusu maisha yetu pale

msalabani. Taja baadhi ya maandiko yanayoonyesha

ushahidi kuwa Yesu Kristo alimaliza pale msalabani katika

maeneo yafuatayo:-

(i)Katika eneo la uchumi

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

UHURU WA KWELI 204

(ii)Katika eneo la afya

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

(iii)Katika eneo la amani

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

(iv)Katika eneo la furaha

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

UHURU WA KWELI 205

SURA YA NANE

NIMEBARIKIWA

Maandiko yanasema;

“Mungu akamwambia Balaamu, Usiende pamoja nao; wala

usiwalaani watu hawa, maana wamebarikiwa” [Hes 22:12]

Ilikuwa ni mpango wa Mungu tangu mwanzo tubarikiwe

kupitia Yesu Kristo. Mungu alimbarikia Ibrahimu ili kusudi

atakayemwamini Mwana wake wa pekee Yesu Kristo.

Ahesabiwe baraka ya Ibrahimu kwa njia ya imani.

“Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama,

kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake

katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo

kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya

mwanawe. Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-

yire,kama watu wasemavyo hata leo,Katika mlima wa

BWANA itapatikana. Malaika wa Bwana akamwita

Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni akasema, Nimeapa

kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno

hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee, katika

kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao

wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko

pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao; na

UHURU WA KWELI 206

katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa

sababu umetii sauti yangu” [Mwa 22:13-18]

Ibrahimu alipoamua kumtoa mwana wake wa pekee Isaka,

bila kumzuilia. Mungu akaapa kuwa atambariki na

kuuzidisha uzao wake, kama nyota za mbinguni na kama

mchanga wa baharini. Mungu alimuahidi Ibrahimu kupitia

baraka alizobarikiwa mataifa yote ya dunia yatabarikiwa.

Mungu alituingiza kupokea baraka ya Ibrahimu kwa njia ya

kumwamini Yesu Kristo. Ndio maana imeandikwa;

“Basi, tusemeje juu ya Ibrahimu, baba yetu kwa jinsi ya

mwili?” [Rum 4:1]

Kumbe sisi tumefanyika watoto wa Ibrahimu kwa jinsi ya

mwili kwa njia ya imani ya Yesu Kristo. Ndio maana Paulo

aliandika;

“Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa

Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi” [Gal 3:29]

Kumbe sisi tumefanyika kuwa uzao wa Ibrahimu yaani

watoto wa Ibrahimu kwa jinsi ya mwili njia ya imani ya

kumwamini Yesu Kristo. Kwa sababu hiyo sisi ni warithi

sawa sawa na ahadi ya Ibrahimu.Kama vile Mungu

alivyomuahidi Ibrahimu kuwa uzao wako utakuwa kama

nyota za mbinguni na mchanga ulioko pwani. Sisi ni zao lake

UHURU WA KWELI 207

tuliofanywa kupitia imani ya Yesu Kristo. Kwa sababu hiyo

tuna haki ya kumiliki na kuwa warithi halali wa baraka

alizobarikiwa Ibrahimu na uzao wake. Ndio maana biblia

inasema;

“Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa

alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa,

Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; ili kwamba

baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo,

tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani” [Gal 3:14]

Kristo alifanyika laana ili atukomboe tusikae chini ya laana

na kwa njia ya imani katika yeye sisi tuliomwamini Yesu

Kristo tumebarikiwa sawa sawa na baraka ya Ibrahimu.

Kwasababu hiyo tunatakiwa kukiri wakati wote sisi ni

wabarikiwa na si walaaniwa kwa jina la Yesu Kristo.

Tumebarikiwa kwa kumwamini Yesu Kristo na kwa namna

hiyo hamna mtu yoyote anayeweza kutulaani.

Usikubali mtu yoyote anayekwambia umelaaniwa wakati

umemwamini Yesu Kristo. Mpuuzie kabisa hakuna namna

wewe uliyebarikiwa unaweza kuwa laana tena. Laana zote

alizibeba Yesu Kristo, laana za matendo ya sheria alizibeba.

Mimi na wewe kwakuwa hatuishi tena chini ya sheria bali

tunaishi katika Yesu Kristo hatulaaniwi.Ndio maana

imeandikwa;

UHURU WA KWELI 208

“Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa

alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa,

Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti” [Gal 3:13]

Laana zote alizibeba Kristo msalabani na kwasababu hiyo

mimi na wewe tuliomwamini Yesu Kristo hatuwezi kuwa

laana tena.

Sisi hatumo katika giza tena bali tupo katika nuru

Hakuna mtu awaye yoyote anaweza kuturudisha kwenye

giza tena. Hakuna namna yoyote inayoweza kumfanya

aliyemwamni Yesu Kristo kurudi gizani tena. Ndio maana

Paulo anaandika kuwa;

9: Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa

takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza

fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika

nuru yake ya ajabu

Sisi ni mzao mteule, tumeteuliwa na Mungu kwa njia ya

imani. Tumefanyika kuwa kuhani wa kifalme, tumefanyika

kuwa taifa takatifu na kuwa chini ya milki ya Mungu. Mungu

katutangazia fadhili zake ili tutoke gizani tuingie katika nuru

UHURU WA KWELI 209

yake ya ajabu biblia ya Habari njema anasema alitutoa

gizani na kutuingiza katika mwanga wake mkuu.

10: ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la

Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata

rehema.

Petro anaendelea kuthibitisha kuwa hatukuwa taifa, lakini

kwa kumwamini Yesu Kristo tumekuwa taifa la Mungu na

tumepata rehema kwa imani ya Yesu Kristo.

11: Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni

tamaa za mwili zipiganazo na roho.

Anaendelea kusema sisi kama wasafiri katika hii dunia

tuziepuke tama za mwili zipinganazo na roho. Kwasababu

sisi sio wa ulimwenguni humu kama wasafiri tunatakiwa

kuachana na tamaa za mwilini.

12: Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo

huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo

matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.

[1Pet 2:9-12]

UHURU WA KWELI 210

Petro anaendelea kusema kuwa watu wa mataifa

(wasiookoka) watutazamapo wayatazamapo matendo yetu

mazuri wamtukuze Mungu wetu. Imeandikwa;

“Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa

kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa

mapya” [2Kor 5:17]

Yesu Kristo ndiye aliyetufanya kuwa wapya; alituondoa

gizani na kututoa katika kongwa la utumwa tuliokuwa

tumebebeshwa akatufanya kuwa huru kweli kweli. Kama ni

hivyo basi tunatakiwa kutembea kama jinsi tulivyoitwa

kuwa katika yeye (Yesu Kristo). Ndio maana Paulo

aliwakumbusha kanisa la Korintho kuhusu wito wao katika

Yesu Kristo waliposahau na kuanza kuishi kama watu wa

mataifa;

“Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake

athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya

watakatifu? Au hamjui ya kwamba watakatifu

watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu

utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo

ndogo? Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si

zaidi sana mambo ya maisha haya? Basi, mkiwa na mahali

panapohukumiwa mambo ya maisha haya, mwawaweka

kuwa waamuzi hao waliohesabiwa kuwa si kitu; katika

UHURU WA KWELI 211

kanisa? Nasema hayo nipate kuwatahayarisha. Je! Ndivyo,

kwamba kwenu hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima,

awezaye kukata maneno ya ndugu zake? Bali

mwashitakiana, ndugu kwa ndugu, tena mbele yao

wasioamini.

Basi imekuwa upungufu kwenu kabisa kwamba

mnashitakiana ninyi kwa ninyi. Maana si afadhali

kudhulumiwa? Maana si afadhali kunyang'anywa mali

zenu? Bali kinyume cha hayo ninyi wenyewe mwadhulumu

watu na kunyang'anya mali zao; naam, hata za ndugu zenu.

Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa

Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme

wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala

wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala

walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi. Na baadhi

yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini

mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana

Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu” [1Kor 6:1-11]

Kanisa la Korintho lilipoteza sura na picha katika mwenendo

katika wito walioitiwa katika Kristo Yesu. Kanisa la Korintho

walikuwa wakishitakiana wao kwa wao tenambele ya wasio

amini. Kanisa la Korintho walikuwa waasherati, waabudu

sanamu, wazinzi, walevi, wanyang’anyi, watukanaji, ilifika

mahali mpaka wakawa wanafanya ufiraji na ulawiti. Paulo

aliwakumbusha kuwa Hamjui kuwa Watakatifu

UHURU WA KWELI 212

watauhukumu ulimwengu na malaika? Aliwakumbusha

kuwa hamjui mlipokuwa watu wa mataifa kabla hamjaamini

mlikuwa watu wa matendo ya namna hiyo? Paulo

anaendelea kusema hamjui kuwa mlipoamini mlioshwa,

mlitakaswa, mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu

Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.

Paulo aliwaambia mtu aliyekiumbe kipya, aliyemwamini

Yesu Kristo kama alivyokuoshwa rohoni, walivyotakaswa na

kuhesabiwa haki kwa imani ya jina la Bwana Yesu Kristo na

katika Roho wa Mungu haifai kuenenda kama watu wa

mataifa. Kumbe kila aliyeamini katika jina la Bwana Yesu

anaoshwa, anatakaswa na kuhesabiwa haki. Paulo kwa

neema ya Mungu aliweza kulirekebisha kanisa la Korintho

kwa kuwaelekeza kilichotokea baada ya wao kuamini

(kuokoka). Paulo alijua kutofautisha kati ya mtu wa asili na

mtu aliyeamini na kufanywa kuwa kiumbe kipya. Alijua

hakuna namna ambavyo watu walianza kuufuata utu wa

kale wanaweza kugeuzwa nia zao. Ni kwa kuwaambia tu

jinsi walivyo katika Yesu Kristo na si vinginevyo.

Ukiendelea kusoma sura hii mpaka ule mstari wa ishirini

bado Paulo alikuwa anawaeleza Wakorintho waliokolewa

vipi katika Yesu Kristo. Sura ya 11 Paulo anawapa ushauri

namna ya kuepukana na matendo ya utu wa zamani (mtu

asiyeokoka). Wewe ukiwa kama mtumishi wa Mungu

unayetumika katika eneo lolote inawezekana ukawa ni

UHURU WA KWELI 213

Mchungaji, Mwalimu, Mwinjilisti, Nabii, Mtume kumbuka

kulikumbusha kundi unalolihudumia hasa walioamini. Kuwa

wao ni wakina nani katika Yesu Kristo. Kwa sababu

ukiwaambia watu jinsi wasivyo katika Kristo Yesu, aidha

kwa kuwaambia ni wenye dhambi, hawafai, hawana haki, ni

machangudoa, wametoka nuruni na kurudi gizani

kwasababu ya matendo yao ya mtu wa kale. Unawavika

kongwa zito ambalo kutoka kwake haiwezekani kwa sababu

unakuwa unawakumbusha mtu mwingine kabisa jinsi

wasivyo katika Yesu Kristo. Paulo aliweza kulirekebisha lile

kanisa la Korintho kwa neema ya Mungu kwa

kuwakumbusha wao ni wa kina nani katika Yesu Kristo

hakuongezea kile alichokuwa anakiona kwa mtazamo wake.

Paulo angeweza kuwaambia Wakorintho ninyi ni walawiti,

waasherati, wazinzi, wafiraji, wanyang’anyi, msio na haki

kwa sababu ya matendo yenu ya mtu wa kale. Aliwaambia

wao ni wakina nani katika Kristo wao ni wa kina nani na kwa

namna hiyo ile kweli ilitenda kazi na kwa neema ya Mungu

wakabadilika. Kumbuka kuwa hakuna kitu kinachoweza

kumuweka mtu huru isipokuwa kweli na kweli ni neno la

Kristo.Kinyume na hapo utakuwa unahuduma kinyume na

agizo la Bwana Yesu. Sisi ni watumishi wa Mungu katika

Kristo Yesu tulioitwa kuhudumu katika mwili wa Kristo

tunapohudumu kinyume na wito tulioitiwa katika Kristo

hatulijengi kanisa bali tunalibomoa kwa mikono yetu huku

tukijiita ni watumishi wa Mungu. Ndio maana Yohana

UHURU WA KWELI 214

anatukumbusha sisi tulioitwa katika Kristo Yesu tunapaswa

kudumu katika mafundisho ya Yesu Kristo imeandikwa;

“Kila apitaye cheo, wala asidumu katika mafundisho ya

Kristo, yeye hana Mungu. Yeye adumuye katika mafundisho

hayo, huyo ana Baba na Mwana pia. Mtu akija kwenu, naye

haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu,

wala msimpe salamu. Maana yeye ampaye salamu

azishiriki kazi zake mbovu. [2Yoh 1:9-11]

Kama imeandikwa kuwa asiyedumu katika mafundisho ya

Kristo hana Mungu je si zaidi sana yule asiyefundisha

mafundisho ya Kristo? Yohana anasema mtu asiyeleta

mafundisho ya Kristo hapaswi kukaribishwa nyumbani na

wala hapaswi kupewa salamu. Kumpa salamu ni kushiriki

kazi zake mbovu, inawezekana kwa kujua au kutokujua

umehubiri au umewafundisha watu kinyume na habari

njrma ya neema ya Kristo.

Kama ile aliyopewa Paulo hiyo huduma kutoka kwa Bwana

Yesu, lakini sasa umejua anza kuhubiri injili ya neema ya

Yesu Kristo (Mat 20:24) ili watu wasibadili tu matendo yao

kuwa halisi katika Yesu Kristo zaidi sana wageuzwe nia zao

na kufanana na Kristo kikamilifu kama ilivyokuwa kusudi la

Mungu tangu asili (Rum 8:29-30). Waeleze watu jinsi

walivyogeuzwa kutoka gizani kwenda nuruni na kuwaambia

kweli jinsi ambavyo haiwezekani kurudi tena gizani.

UHURU WA KWELI 215

Waeleze watu uhalisia wao wajitambue wao ni wakina nani

katika Yesu Kristo.

Mungu anamtazama kila aliyeamini (aliyeokoka kama

Yesu Kristo).

Mungu akikutazama wewe uliyeokoka umefanana na Kristo

kwa asilimia miamoja. Ile thamani ambayo Mungu amempa

Yesu Kristo kama alivyomfanya kuwa mzaliwa wa kwanza

kwa ndugu wengi (yaani kuwa kaka yetu sisi tulimwamini)

[Rum 8:29-30]. Kwa namna hiyo kila alichokifanya Yesu

Kristo na wewe pia ulikuwepo ndani yake.

Kumbuka biblia inatueleza kuwa Kristo alidharauliwa,

alitukanwa, alifedheheshwa, alipigwa mijeledi, alipata aibu

tulikuwa ndani yake. Alipokataliwa tulikuwa ndani yake,

alipoteswa, hata alipochoka, hata alipokuwa anaonekana

hana thamani. Alipoibeba hiyo hukumu tulikuwa ndani

yake, alipokufa tulikuwa ndani yake, hata alipofufuka

tulikuwa ndani yake. Sisi tulishiriki mateso ya Yesu kwa

imani na hata Kristo alipokwenda kuzimu kunyang’anya

funguo za mauti na kuzimu tulikuwa ndani yake. Alipopaa

mbinguni na kuketi mkono wa kuume tulikuwa ndani yake,

hata sasa tuko ndani yake.

Kama ni hivyo basi hatuna sababu ya kulipia gharama mara

mbili, hakuna namna tunatakiwa tena kulipia gharama ya

UHURU WA KWELI 216

dhambi tulizolipa gharama katika Kristo Yesu. Kulipia

gharama ya kutoka kwenye vifungo, magonjwa, umaskini,

upweke, kukataliwa vyote tulilipia pale msalabani katika

Kristo Yesu. Mungu hawezi kuwa mwenye haki

kukuhukumu mara mbili kulipia gharama ya dhambi

uliyoifanya pale katika bustanini ulupokuwa ndani ya

Adamu (mtu wa kale aliyeasi). Hakuna namna tena

unatakiwa kulipia gharama ya ugonjwa na umaskini ulionao

tulilipia pale msalabani katika Kristo Yesu. Ninakushauri

ndugu yangu unayesoma kitabu hiki najua viko vitabu vingi

sana hapa duniani lakini kwakuwa umepata neema ya

kusoma kitabu hiki basi Mungu amekusudia, kwa neema

yake na ufunuo ulioko katika kitabu hiki juu ya neema ya

Yesu Kristo uweze kuwekwa huru kweli kweli.

Usikubali kulipa gharama mara mbili.

Ni mfumo wa dunia hii ndio unaotusisitiza kuwa ili uweze

kufikia kiwango fulani cha mafanikio unatakiwa

kupambana. Na wakati mwingine tumekewa utaratibu na

kanuni na miongozo ya kufanikiwa kiuchumi, kiroho. Na

tukaamini hivyo na kuweka kuwa ni muongozo wa maisha

yetu. Kiufupi ulimwengu huu umetutengenezea mfumo wa

kulipia gharama zaidi kupata vitu. Kuliko kufurahia zawadi

tulizopokea baada ya kulipia gharama ya mateso tuliyopata

katika Yesu Kristo. Biblia inateleza kwamba;

UHURU WA KWELI 217

“Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.

Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli” [Yoh

17:16-17]

Yesu aliposema wao si wa ulimwengu huu kama nisivyo wa

ulimwengu huu hakuwa anamaanisha kuwa hatutakiwi

kuishi katika huu ulimwengu. Ukisoma sura hii ya kumi na

saba mstari wa kumi na tano. Yesu aliomba mwenyewe

kuwa mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu bali

uwalinde na yule mwovu. Yesu anaposema wao si wa

ulimwengu huu anamaanisha kuwa mfumo wetu wa

maisha uko tofauti kabisa na mfumo wa huu ulimwengu.

Kwasababu hiyo hatupaswi kuenenda sawa sawa na mfumo

wa ulimwengu huu katika kila eneo. Kiuchumi

tumetofautiana sana na mfumo wa uchumi wa nyumbani

kwetu (mbinguni). Ndio maana Yesu aliwafundisha

wanafunzi wake kuomba ufalme wa Mungu kuja duniani

(Math 6:9). Lengo ni kwamba ukija uwasaidie kuishi sawa

sawa na ufalme wa Mungu unavyokusudia.

Tatizo linaanzia pale ambapo tunataka kuishi kwa kufuata

kanuni za ulimwengu kiuchumi, kiroho na katika kila eneo.

Kwa bahati mbaya mfumo wa ulimwengu umekuwa na

msukumo mkubwa kutushawishi. Kiasi ambacho tukaanza

kuchukua mifumo yao tukaihalalisha kwetu tulioamini,

tukaiishi na kuiweka kuwa miongozo ya maisha yetu.

Tukabadili sura ya kanisa kama jinsi linavyotakiwa kuwa

UHURU WA KWELI 218

kama jinsi Kristo alivyo, kanisa likageuzwa kuwa na sura ya

vyama vya siasa. Na kwa namna hiyo kanisa limeshindwa

kuvuka kiuchumi, na kiroho limekuwa kama watu

waliotelekezwa na Baba yao. Kwa sababu tunataka kuishi

kulingana na mifumo ya ulimwengu huu. Na kama

umeamini (umeokoka) sio rahisi kabisa kufanikiwa

kwasababu mfumo wa uchumi wa ulimwengu huu uko

tofauti kabisa na mfumo wa ufalme wa Mungu. Kwa hiyo

kila utakapokuwa unafanya sawa sawa na mfumo wa huu

ulimwengu utakuwa unakukataa. Sababu sio kuwa huwezi

kufanikiwa sababu hujataka kuambatana na mfumo halisi

wa ufalme wa Mungu kama jinsi ulivyo.

Kumbuka sisi ni wa agano jipya kila tunachokifanya ni

muhimu kuambatana na agano letu. Kama utakuwa ni mtu

uliyefanywa katika agano jipya ukataka kuishi katika agano

la kale. Hautafurahia kabisa alichofanya Yesu Kristo kwaajili

yako utabaki kufeli siku hadi siku. Lazima ukubali

kuambatana na injili ya Yesu Kristo na kuambatana na

ufalme wa Mungu ili kusudi uone matoeo. Mfano Wakristo

wengi wamekuwa wakiamini usemi huu kuwa “asiyefanya

kazi na asile” na kwa namna hiyo watu wamekuwa

wakijitesa kwa shughuli nyingi na kuona hamna mtu yoyote

anaweza akawasaidia isipokuwa kwa kazi wanazozifanya.

Wakati huo biblia kwamba;

UHURU WA KWELI 219

“Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, bali anamwamini yeye

ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake

mtu huyo imehesabiwa kuwa haki” [Rum 4:5}

Ukianza ule mstari wan ne unaeleza wazi kuwa mtu

afanyaye kazi ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema bali ni

deni. Mstari huu wa tano biblia inaeleza kuwa yule

asiyefanya kazi na anamwamini yeye yaani Yesu Kristo mtu

huyo imehesabiwa kuwa ni haki. Hii mistari haimaanishi

kuwa usifanye kazi, hii mistari inaonyesha kuwa imani yako

unaiweka wapi unapofanya kazi. Maana ulimwengu huu

unataka tutumikie kazi tuamini kuwa kazi ndiyo

inayotufanya tufanikiwe. Lakini biblia inatuambia kuwa

tukimwamini hata tukiwa bado hatujafanya kazi

tunahesabiwa haki. Kwahiyo shida haipo kwenye kufanya

kazi shida ipo kwenye imani yaani unaamini nini kazi au

unamwamini Yesu Kristo. Na kwa namna hiyo ukihamisha

imani yako kutoka kwenye kazi ukamwamini Yesu ambaye

alihakikisha anakufa kwaajili yako. Ili wewe usiwe mtumwa

wa kazi bali ufurahie neema ya kazi aliyoifanya msalabani

kwaajili yako.

Na ukianza kuamini namna hiyo utaanza kuona kila

unachokifanya, hakitaendeshwa na mfumo wa ulimwengu

huu bali ufalme wa Mungu. Kumbuka ufalme wa Mungu

unapoanza kutenda kazi kwaajili yako uwe na uhakika.

Mafanikio kwenye maisha yako yatafurika kwa sababu

UHURU WA KWELI 220

umeamua kukubali kwa kuamini kitu ambacho Yesu Kristo

amefanya kwenye maisha yako. Usikubali kulipia gharama

mara mbili kila kitu unachohitaji ulilipia pale msalabani

katika Yesu Kristo. Kubaliana na huu ukweli ambatana nao,

amini uanze kufurahia zawadi ya wokovu kwenye maisha

yako leo.

UHURU WA KWELI 221

Tathmini kupitia maswali kutoka katika Sura ya Nane

1: Kwanini tumebarikiwa katika Kristo Yesu?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

2: Ni nani aliyetukomboa kutoka katika laana?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

3: Kwanini aliyebarikiwa hawezi kulaaniwa?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………4:

Kwanini aliyeamini (aliyeokoka) hawezi kutoka nuruni

kurudi gizani?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

5: Kwanini Mungu anatufananisha na Yesu Kristo?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

UHURU WA KWELI 222

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

6: Kwanini usikubali kulipa gharama mara mbili?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

UHURU WA KWELI 223

SURA YA TISA

MIMI NI MSHINDI

atika waandishi katika biblia Paulo alikuwa ni miongoni

mwa watu walioifunua siri ya ushindi kwenye maisha

yao, kwasababu alijua siri ya ushindi kwenye maisha

yao haitegemeani na nguvu alizo nazo, ujuzi au maarifa

aliyo nayo. Kwasababu aliamini uwezo wake alio nao, nguvu

na maarifa si kitu mbele za Mungu katika Yesu Kristo. Paulo

anashuhudia kwamba;

“Kama ilivyoandikwa ya kwamba, kwa ajili yako tunauawa

mchana kutwa, tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa

kuchinjwa. Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na

zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda” [Rum 8:37]

Paulo alizungumza kwa lugha ya falsafa kuwa tunauawa

mchana kutwa. Kimsingi sio kwamba tunauawa mchana

kutwa bali ni kwamba sisi si wa ulimwengu huu ambao

Kristo anashuhudia kuwa; Kama mngekuwa wa ulimwengu,

ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake lakini

kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua

katika ulimwengu, kwasababu hiyo ulimwengu huwachukia

(Yoh 15:19).

K

UHURU WA KWELI 224

Ndio maana ulimwengu unatafuta kila namna ya kutuchinja

kama ilivyoandikwa tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa

kuchinjwa. Ndio maana usiku na mchana Shetani haachi

kutufuatilia kama jinsi Yohana alivyoandika kuwa;

“Kwahiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao huko. Ole

wan chi nabahari! Kwa maana yule ibilisi ameshuka kwenu

mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati

mchache tu” [Ufu 12:12]

Ili kuhakikisha anaharibu kusudi la Mungu kama

alivyotuchagua katika kizazi hiki. Ndio maana ulimwengu

unatuchukia, Shetani anapigana na sisi kwa sababu anajua

jinsi tulivyo. Tuko tofauti na yeye ndio maana imeandikwa;

Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake;

basi ufalme wake utasimamaje? (Math 12:26). Kwa hiyo

tunapigana na Shetani kwa sababu hayuko upande wetu.

Ndio maana sisi tuliompokea Kristo katika eneo la

mafanikio katika eneo lolote lile tunakutana na vita kubwa

isiyo ya kawaida inaweza kuwa vita ya uchumi, vita ya

huduma na katika kila eneo kwenye maisha yetu ya kiroho

na kimwili. Shetani anajua ana mda mchache ndio maana

anapambana tusiachilie kusudi la Mungu katika ulimwengu

huu kama alivyotuchagua. Ashukuriwe Mungu kwasababu

neno la Mungu linashuhudia kuwa lakini katika mambo

UHURU WA KWELI 225

hayo yote tunashinda na zaidi ya kushinda kwa yeye

aliyetupenda yaani Yesu Kristo.

Katika maeneo napenda kumuelewa Paulo kama jinsi Roho

Mtakatifu alivyomfunulia kuandika mstari huu bila kuweka

hali ya kutegemea huo ushindi kutoka kwetu binafsi. Bali ni

kuwa na ushindi huo kwa sababu ya yeye aliyetupenda

(Yesu Kristo). Kwa hiyo ushindi wetu hautokani na hali

tulizo nazo, iwe ni umaskini, magonjwa, udhaifu wa aina

yoyote hayajaorodheshwa.

Ingekuwa sababu ya kushindwa kwetu ni umaskini basi

Paulo angesema hauwezi kushinda kama wewe ni maskini.

Kama ingekuwa ni ugonjwa au udhaifu wowote ulio nao

Paulo angesema kwa sababu ya ugonjwa au udhaifu ulio

nao hauwezi kushinda. Lakini Paulo anaweza msisitizo

katika kumtaja yeye aliyetupenda yaani Yesu Kristo

tunashinda na zaidi ya kushinda.

Tafsiri nyepesi ya andiko hili maana yake ni nini? Maana

yake ni kwamba hatushindi na zaidi ya kushinda kwasababu

ya jinsi tunavyoshindana. Bali ni kwasababu ya jinsi

ambavyo Yesu Kristo alitupigania na alishinda na zaidi ya

kushinda pale msalabani. Jamani hii ni ajabu sana, hii ni

habari njema! Kumbe! Kushinda kwetu ugonjwa sio kwa

sababu ninapigana mimi. Ila ni kwasababu yake Yesu Kristo

UHURU WA KWELI 226

aliyepigana kwaajili yangu akashinda na zaidi ya kushinda

kama maandiko yanavyoshuhudia kuwa; Bali alijeruhiwa

kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya

amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi

tumepona (Isa 53:5).

Kumbe hatushindi na zaidi ya kushinda umaskini kwa

sababu tunapigana sisi bali ni kwa sababu Yesu Kristo

alipigana na umaskini na kwa neema yake Bwana wetu Yesu

Kristo alifanyika maskini ili kwamba sisi tupate kuwa

matajiri kwa umaskini wake (2Kor 8:9).

Ushindi na zaidi ya ushindi tulio nao katika Yesu Kristo ni

ushindi ambao upo kwa namna ya rohoni. Kwa tafsiri

nyingine naweza kusema kuwa ni ushindi ambao uko rohoni

lakini haujadhihirishwa kwa namna mwilini. Kazi yetu ni

moja ni kuudhihirisha ushindi tulio nao rohoni kwa namna

mwilini.

Kwa maneno mengine ni kwamba kuna namna ambavyo

tunatakiwa kuwa na imani ya kushinda na zaidi ya kushinda

ili imani tuliyo nayo iweze kujifunua mwilini. Ili tuweze kuwa

na imani ya aina yoyote lazima tujue imani inahitaji nini, ili

tuweze tuweze kutembea nayo.

UHURU WA KWELI 227

Maandiko yanasema hivi;

“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni

bayana ya mambo yasiyoonekana” [Ebr 11:1]

Mstari huu tafsiri ya biblia ya kiingereza King James Version

(KJV) katika neno bayana ya mambo yasiyoonekana

ametumia neno “the evidence of things not seen”. Maana

yake ni uhalisia wa vitu ambavyo bado havijaonekana kwa

namna ya mwilini. Kwahiyo ikiwa wewe ni mgonjwa na

mwili unalalamika kabisa unaumwa, haibadilishi ukweli

kuwa wewe ni mzima. Kama wewe ni maskini huna hata

dola moja mfukoni haibadilishi kwamba wewe ni tajiri.

Kadhalika katika maeneo mengine unapopitia shida, taabu

au changamoto yoyote ile haibadilishi ukweli kuwa hiyo

taabu, shida au changamoto ilisha isha.

Jiepushe kuwa na imani ya kuamini ushindi wako

kutokana na hali ya mazingira inavyoonekana nje [au

ulimwengu wa mwili].

Unaweza kuamia kuanzia sasa katika changamoto ya aina

yoyote ile inayoonekana mwilini. Kuitafutia majibu ya

kiroho na kuacha kuishi kutokana na mazingira ya nje. Mara

zote mwili na roho zimepingana. Ndio maana Paulo

aliwaandikia wagalatia kuwa; Kwa sababu mwili hutamani

ukishindana na roho, na roho ikishindana na mwili; kwa

UHURU WA KWELI 228

maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka

(Gal 5:17).

Siku zote mwili utakwambia hicho unachokiamini hakiwezi

kuwa, mwili utakupa uthibibisho kuwa huoni maumivu ya

uvimbe unao usikia. Mwili utakwambia huoni jinsi ulivyo

maskini huna hata dola moja mfukoni, hata jana usiku

umelala njaa. Siku zote mwili utakupinga kuwa haiwezekani

hicho unachokiamini rohoni kikawa halisi.

Kuna namna nzuri ya kuushinda mwili wako usiwe na nguvu

ya kushinda kile unachokiamini rohoni. Paulo aliandika hivi

kwa Wakolosai;

“Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi” [Kol 3:2]

Katika mstari huu Biblia tafsiri ya King James Version (KJV)

kwenye neno yafikirini yaliyo juu ametumia neno “set your

affection on things above”. Maana yake lenga ufahamu

wako kuathiriwa na mambo yaliyo juu. Tafsiri ya biblia ya

The Passion Translation (TPT) Anasema mstari huu namna

hii. Nimetafsiri kwa lugha ya Kiswahili hivi;

“Ndio, sherehekea hazina za ulimwengu wa roho na ujijaze

mawazo, ya uhalisia wa ulimwengu wa roho, na sio

uharibifu wa ulimwengu wa mwili”

Mara zote mawazo ya ulimwengu wa mwili ni kutaka

kutuonyesha kuwa uhalisia wa hazina za mbinguni sio kweli.

UHURU WA KWELI 229

Kwa kuangalia hali ya wakati huo unayopitia, Lakini biblia ya

TPT inatuhakikishia kuwa; tusherehekee hazina za

ulimwengu wa roho na kuachana na uharibifu wa

ulimwengu wa mwili kwasababu hazina za ulimwenmgu wa

roho ni halisi. Ulimwengu wa mwili una uharibifu mwingi,

lakini ashukuriwe Mungu tukienenda katika roho uharibifu

huu hautatupata. Kwa namna ambavyo unafikiri na

kutafakari hazina halisi za mbinguni na kuishi kuwa sehemu

yako ya maisha. Bila kuangalia mazingira ya nje ndivyo

unavyojiweka kwenye nafasi ya kupokea katika ulimwengu

wa mwili mambo ambayo yako rohoni.

Kwahiyo ukitaka udhihirisho wa neno la Mungu ambalo ni

kweli kama Yohana alivyoandika kuwa; “Uwatakase kwa ile

kweli; neno lako ndiyo kweli” (Yoh 17:17). Nilazima kuliishi

hilo neno. Jambo lolote nje ya neno la Mungu ni uongo, siku

zote Shetani anapenda tuamini uongo wake. Neno la

Mungu likisema wewe ni mshindi na zaidi ya kushinda

Shetani anakwambia umeshindwa na zaidi ya kushindwa.

Neno la Mungu linapokwambia wewe ni tajiri, Shetani

anasema wewe ni maskini, neno la Mungu likisema

umepona Shetani anasema unaumwa bado kwani huoni

uvimbe au maumivu uliyonayo, huoni hospitali

wamekwambia una ugonjwa bado. Ndivyo Shetani

anapenda ujione.

UHURU WA KWELI 230

Jambo la muhimu ni kuacha kuamini uongo wa Shetani na

kuishi uhalisia wa ulimwengu wa roho kupitia neno lake.

Hata Shetani akisema wewe ni maskini bado, wewe ni

mgonjwa, akisema huwezi kufanikiwa katika jambo hili

usimzingatie. Kwa kuwa na imani hiyo ndio mwanzo wa

udhihirisho wa ulimwengu wa roho kupitia neno la Mungu

kwenye maisha yako.

Tuangalie mfano huu;

Basi Nebukadreza akatoa amri kwa hasira na ghadhabu,

waletwe hao Shadraka, na Meshaki, na Abednego. Basi

wakawaleta watu hao mbele ya mfalme. Nebukadreza

akajibu, akawaambia, Enyi Shadraka, na Meshaki na

Abedinego, je! Ni kwa makusudi hata hamtumikii mungu

wangu wala kuisujudia sanamu ya dhahabu

niliyoisimamisha? Basi sasa, kama mkiwa tayari wakati

mktakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na

zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma,

kuanguka na kuisujudia sanamu niliyoishimamisha, ni

vema; bali msipoisujudia, mtatupwa saa hiyo hiyo katika

tanuru iwakayo moto; naye ni nani Mungu yule atakaye

waokoa ninyi na mikono yangu? Ndipo Shadraka, na

Meshaki, na Abedinego, wakajibu, wakamwambia mfalme,

Ee Nebukadreza, hamna haja ya kukujibu katika neno hili.

UHURU WA KWELI 231

Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza

kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na

mkono wako, Ee mfalme. Bali kama si hivyo, ujue, Ee

mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako,

wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.

Ndipo Nebukadreza akajaa ghadhab, na sura ya uso wake

ikabadilika juu ya Shadraka, Meshaki, na Abedinego, basi

akatoa amri watie moto ile tanuru mara saba kuliko desturi

yake kutiwa moto. Kisha akawaamuru baadhi ya watu

mashujaa wa jeshi lake kuwafunga Shadraka, Meshaki, na

Abedinego, na kuwatupa katika ile tanuru iliyokuwa

ikiwaka moto. Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa

suruali zao, na kanzu zao, na mavazi yao mengine,

wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.

Basi kwasababu amri ya mfalme ilikuwa ni kali, na ile

tanuru ilikuwa ina moto sana, mwako wa ule moto

ukawaua wale watu walio washika Shadraka, na Meshaki,

na Abednego. Na watu hao watatu, Shadraka, na Meshaki,

na Abednego, wakaanguka, hali wamefungwa, kati kati ya

ile tanuru iliyokuwa inawaka moto. Ndipo Nebukadreza

akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia

mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali

wamefungwa, kati kati ya moto? Wakajibu wakamwambia

mfalme, Kweli, Ee mfalme. Akajibu, akasema, Tazama,

mimi naona watu wane, nao wamefunguliwa, wanatembea

katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wan

UHURU WA KWELI 232

ne ni mfano wa mwana wa miungu. Kisha Nebukadreza

akaukaribia mdomo wa ile tanuru iliyokuwa inawaka moto.

Akanena akasema, Enyi Shadraka, na Meshaki na

Abedinego, watumishi wa Mungu aliyejuu, tokeni, mje

huku. Ndipo Shadraka, na Meshaki na Abedinego wakatoka

katika ule moto. Na maamiri, na manaibu, na maliwali, na

mawaziri, waliokuwa wamekusanyika pamoja,

hawakuwaona watu hao, ya kuwa ule moto ulikuwa hauna

nguvu juu ya miili yao, wala nywele za vichwa vyao

hazikuteketea, wala suruali zao hazikubadilika, wala harufu

ya moto haikuwapata hata kidogo. [Dan 3:13-27]

Shadraka, Meshaki na Abedinego waliamua kutozingatia ni

kitu gani mfalme anawa amrisha ambacho sio sahihi.

Waliamua kuishi uhalisia wa neno la Mungu kama Daudi

alivyoandika kuwa;

“Huwafanya malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake

kuwa moto wa miali” [Zab 104:4]

Shadraka, Meshaki na Abedinego walijua siri huu kuwa

Mungu anawafanya watumishi wake kuwa miali ya moto.

Ndio maana hawakukubali kuitumikia miungu ya mfalme

Nebukadreza. Ile imani ya kuokolewa katika moto

ikajifunua kuwa halisi kwenye tanuru la moto. Watu

waliowashika Shadraka, Meshaki na Abedinego kwa

UHURU WA KWELI 233

muwako tu wa ule moto uliwaua lakini Shadraka, Meshaki

na Abednego haukuwa na nguvu juu ya miili yao, nywele za

vichwa vyao, hata harufu ya moto haikuwapata. Huyu ni

Mungu mwenye uweza wote, huyu ni Mungu aliyeziumba

mbingu na nchi.

Hii ndio maana ya halisi ya kuwa kwa imani kila jambo

lisilowezekana linaweza kuwezekana. Ebu tujifunze kwa

hwa watumishi Shadraka, Meshaki na Abedinego kama

Mungu aliwatetea katikati ya jaribu gumu na zito namna

kwa imani zao. Je si zaidi sana Mungu kujifunua kwenye

ugonjwa ulio nao, si zaidi sana Mungu kujifunua katika

umaskini ulio nao. Ni rahisi sana ndio maana Yesu

aliwaaambia Wanafunzi wake;

“Yesu akawaambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake

aaminiye” [Mark 9:23]

Kwa imani hufanya bonde kuwa mlima mrefu na mlima

mrefu kuwa bonde. Kwa imani palipopotoka pananyooka

na palipoparuza panasawazishwa. Kwa imani bahari huwa

nchi kavu na nchi kavu huwa bahari yenye kina kirefu.

Kuanzia sasa anza kufurahia uhalisia wa hazina iliyoko

katika ulimwengu wa roho kupitia neno la Mungu hakuna

jambo litakalo shindikana kwenye maisha yako.

UHURU WA KWELI 234

Biblia inakiri kuwa sisi tumebarikiwa sio kwa sababu yetu

bali kwasababu ya Yesu Kristo aliyekufa msalabani

kwaajili yetu.

Yohana alimwandikia mpenzi wake Gayo hivi;

“Mzee kwa Gayo mpenzi, nimpendaye katika kweli. Mpenzi

naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya

yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo” [3 Yoh 1:1-2]

Mstari huu kwa tafsiri ya biblia ya The Passion Translation

(TPT) imetafsiriwa hivi;

“Mpenzi naomba ufanikiwe katika kila njia na uendelee

kufurahia afya njema kama nafsi yako ifanikiwavyo”

Maana yake ni kwamba baraka ni jambo la rohoni, sio

jambo ambalo liko mwilini. Ndio maana Yohana alitaka

mpenzi wake Gayo afanikiwe kama alivyofanikiwa katika

ulimwengu wa roho katika kila njia na afya yake. Kwasababu

yoyote aliye ndani ya Kristo kila baraka iko pamoja naye.

Paulo aliandika hivi;

“Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo,

aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu

wa roho, ndani yake Kristo; 6: Na usifiwe utukufu wa neema

yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa.”

[Efe 1: 3, 6]

UHURU WA KWELI 235

Kumbe Mungu alishatubariki baraka zote katika ulimwengu

wa roho. Hatukubarikiwi baraka za mambo madogo

yanayohesabika, bali ametubariki kwa baraka zote katika

ulimwengu wa roho. Pia ametuneemesha yaani kupewa

upako wa msaada tusio stahili na kibali cha kukubalika

tusivyostahili katika Mpendwa yaani Yesu Kristo.

Baraka ni nguvu ya upako inayomsaidia mtu kufanikiwa

kimwili. Au ni maneno mazuri au mambo mazuri

yanayotamkwa juu ya mtu yanayotarajiwa yatokee katika

maisha ya mtu. Biblia inaposema tumebarikiwa maana yake

tumepewa nguvu ya upako ya kutusaidia kufanikiwa mwilini

kabisa.

Tuangalie maandiko mengine yanayoonyesha uhalisia wa

jinsi tulivyo katika Kristo Yesu.

Paulo anasema hivi;

“Macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito

wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wake katika

watakatifu jinsi ulivyo; na ubora wa ukuu wa uweza wake

ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa

nguvu za uweza wake; aliotenda katika Kristo alipomfufua

katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika

ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na

mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala

UHURU WA KWELI 236

si ulimwenguni hum utu, bali katika ule ujao pia” [Efe 1:18-

21]

Maandiko yanaposema na utajiri wa utukufu wake katika

watakatifu jinsi ulivyo. Anamaanisha kuufunua uzuri wa

utajiri wa baraka zilizoko ndani yetu katika macho ya damu

na nyama. Ua lina kikonyo chenye rangi ya kijani pamoja na

uzuri wa rangi inayojidhihirisha nje ya kikonyo cha hilo ua.

Uzuri wa ua unaoneka kwenye udhihirisho wa rangi

iliyojitokeza nje. Ua lisipotoa nje udhihirisho wa rangi ubora

wake unakuwa umepunguka. Kama Paulo alivyosema

Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo

anamaanisha udhihirisho wa baraka tulizonazo katika

ulimwengu wa roho kuwa dhahiri katika ulimwengu wa

mwili. Kwa maana hiyo basi Mungu hawezi kupokea

utukufu wake pasipo udhihirisho wa baraka hizo kujifunua

katika macho ya damu na nyama.

Biblia inashuhudia kuwa katika uweza wa nguvu zake katika

Kristo Yesu kama tulivyoketishwa pamoja naye katika

ulimwengu wa roho kwa jinsi tulivyofufuliwa pamoja naye

(Efe 2:6). Tuliwekwa juu sana kuliko ufalme wote, na

mamlaka, na nguvu na usultani na kila jina linalotajwa

katika ulimwengu huu na ule ujao pia. Lakini pamoja na

hayo yote tuliyopewa kwenye ulimwengu wa roho

UHURU WA KWELI 237

yatakuwa bure kama yasipojifunua na kwa dhahiri katika

macho ya damu na nyama.

Paulo aliwaandikia Warumi hivi;

“Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti ilitawala

kwasababu ya yule mmoja, zaidi sana wao wapokeao wingi

wa neema na kile kipawa cha haki watatawala katika

uzima kwa yule mmoja, Kristo Yesu” [Rum 5:16-17]

Kumbe hatuhitaji kuomba neema ya Kristo wala kuomba

kipawa (zawadi) cha haki. Kwa sababu ni vitu tulivyo navyo.

Biblia inaposema kutawala maana yake ni mkakati wa

kisheria unaotusaidia sisi tulioamini (tuliookoka) kutawala

kisheria. Maana yake tumepewa wingi wa neema na kipawa

cha haki ili vitusaidie kutawala katika maisha. Kutawala

dhambi, kutawala umaskini, kutawala changamoto za kila

aina kwenye maisha yetu.

Kwanini baraka tulizobarikiwa hazijidhihirishi mwilini?

Ni kwasababu ya vita ya Shetani. Watoto wa Mungu wengi

hawafanikiwi kwa sababu ya vita za shetani. Shetani

asingependa kabisa yoyote anayemwamini Kristo

alichobarikiwa kwenye ulimwengu wa roho kiwe dhahiri

katika ulimwengu wa mwili. Ndio maana anatumia hila

yaani udanganyifu, uongo au ulaghai.Hila au kitu

UHURU WA KWELI 238

kinachoonekana ni chema au kina wema lakini nyuma yake

au ndani yake kimebeba maangamizi makubwa sana.

Maandiko yanasema hivi;

“Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika

uweza wa nguvu zake.Vaeni silaha zote za Mungu, mpate

kuweza kuzipinga hila za Shetani” [Efe 6:10-11]

Kama ni hivyo basi kumbe Shetani anapokuja kupigana vita

na wewe ili udhihirisho wa baraka, utajiri, ufalme na yote

tuliyopewa katika ulimwengu wa roho usijidhihirishe

anatumia hila. Kwa tafsiri nyepesi ni kwamba Shetani

anatumia hila ili kutucheleweshea udhihirisho wa baraka

tulizo nazo au zisitokee kabisa.

Shetani alitumia hila kumdanganya Adamu na hawa

kwenye bustani ya Edeni na kupitia hao tukaingizwa

kwenye laana ya mauti na kuondolewa ufalme. Kwasababu

hiyo tukaondolewa kwenye nafasi ya utawala kama vile

Mungu alivyotuagiza kutawala samaki wa baharini, ndege

wa angani, wanyama kila chenye kutambaa nan chi yote pia

(Mwa 1:26), tukamuuzia Shetani utawala tuliokuwa nao

tukawa watumwa na kuwekwa nafasi ya mwisho katika

ngazi ya utawala. Ashukuriwe Mungu kwasababu alishuka

mwenyewe (Yesu Kristo) kuja kurejesha utawala uliopotea

ili tuendelee kumiliki na kutawala.

UHURU WA KWELI 239

Tuangalie hila aliyotumia Shetani kumdanganya Hawa

kwenye bustani ya Edeni.

Musa aliandika;

“Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula,

wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa,

basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na

mumewe, naye akala” [Mwa 3:6]

Kumbe Shetani hakwenda na majeshi ya farasi, wala

hakwenda na mkuki kwenye bustani ya Edeni bali alitumia

hila ya kumdanganya kwa maneno ya uongo kama Paulo

alivyoshuhudia kuwa;

“Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa

kwa hila yake, asije akawaharibu fikra zenu, mkauacha

unyofu na usafi wa Kristo” [2Kor 11:3]

Shetani anapigana vita zake kwa akili sana. Ndio maana

anatumia hila ili kutudanganya kwenye fikra zetu na

kuharibu mpango wa Mungu kwenye maisha yetu. Kwa

sababu najua kusudi la Mungu ni kutaka kuona baraka zake

na ahadi zake zinajidhihirisha kwenye maisha yetu. Ndio

maana maandiko yanasema;

“Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita

kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili,

bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome)

UHURU WA KWELI 240

tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho

juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikra ipate

kumtii Kristo” [2Kor 10: 3-5]

Kumbe kazi ya Shetani ni kutuambia uongo kwenye fikra

zetu ili tuamini uongo wake. Ili kile ambacho ni halisi Mungu

amekiahidi kisitokee kwenye maisha yetu. Ndio maana

tunatakiwa kuziteka fikra zetu zipate kumtii Kristo.

Kwasababu tukiunganishwa mawazo yetu katika Kristo Yesu

na kumtazama wakati wote tutaakisi uweza wake, ukuu

wake, utajiri wake na ufalme ndani yake na kuwa hivyo

halisi katika maisha yetu ya mwilini.

UHURU WA KWELI 241

Tathmini kupitia maswali kutoka katika Sura ya Tisa

1: Ni nani aliyetupa kushinda?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………...

2: Kwanini aliyeokoka hawezi kushindwa?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

3: Kwanini ushindi wetu hautokani na hali yetu ya nje/

mazingira yanayoonekana kwa macho ya damu na nyama?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

4: Elezea kwa ufupi, uhalisia tulionano katika Kristo Yesu

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

UHURU WA KWELI 242

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

5: Taja sababu moja, inayosababisha baraka tulizobarikiwa

katika ulimwengu wa roho zijidhihirishe mwilini.

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

UHURU WA KWELI 243

SURA YA KUMI

NITAKIRI HIVI DAIMA

“Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa

chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani

tulihubirilo. Kwasababu ukimkiri Yesu kwa Kinywa chako ya

kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu

alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo

mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata

kupata wokovu” [Rum 10:8-10]

Mdomo ni mtaji wa ukiri, mdomo ni silaha ambayo

ikitumika vizuri inabadilisha hali ya maisha ya mtu. Mdomo

kwa lugha ya kiingereza yaani “mouth” limetokana na lugha

ya kigiriki “stoma” maana yake “the edge of a” maana yake

“makali ya”.Maana yake mdomo ni kibebeo cha maneno

yanayotoka katika ulimi wako. Kwahiyo basi kupitia mtaji

wa mdomo na utaamua uwe mtu mkuu au uwe mtumwa.

Yakobo aliandika kwamba;

“Tena angalieni merikebu; ingawa ni kubwa kama nini, na

kuchukuliwa na pepo kali, zageuzwa na usukani mdogo

sana, ko kote anakoazimia kwenda nahodha. Vivyo hivyo

ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu.

UHURU WA KWELI 244

Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa

sana. Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi,

umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote

unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao

huwashwa moto na jehanum. Maana kila aina ya

wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu

vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa

na wanadamu. Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu

usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti. Kwa huo twamhimidi

Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu

waliofanywa kwa mfano wa Mungu. Katika kinywa kile kile

hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo

kuwa hivyo. Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji

matamu na maji machungu? Ndugu zangu, Je! Mtini

waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika

chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu”

[Yak 3: 4-12]

Yakobo ameufananisha ulimi na usukani mdogo wa meli,

ndio maana anasema ijapokuwa ni usukani mdogo lakini

nahodha anaweza kuelekeza meli nzima kupitia huo

usukani mdogo. Kupitia ulimi unaweza kubariki au kulaani

maisha yako au maisha ya wengine. Yakobo anaendelea

kusema haifai katika kinywa chako kutoka baraka na laana,

anaendelea kusema chemichemi haiwezi kutoa maji

UHURU WA KWELI 245

matamu na maji machungu. Maana yake ikitokea kwenye

kinywa chako kunatoka maneno ya baraka na laana basi

ujue kunashida mahali. Tumepewa nafasi ya kusimamia

baraka tu yaani kutamka kwa mdomo kupitia ulimi maneno

ya baraka.

Ndio maana Yesu aliwakataza Yakobo na Yohana kutamka

maneno ya kuua. Biblia inasema;

“Yesu akamwambia, Msimkataze, kwa kuwa yeye ambaye

si kinyume chenu yu upande wenu. Ikawa, siku za kupaa

kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake

kwenda Yerusalemu; akatuma wajumbe kutangulia mbele

ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha

Wasamaria, ili kumtengenezea mahali. Lakini wenyeji

hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake

kwenda Yerusalemu. Wanafunzi wake Yakobo na Yohana

walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto

ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye

alivyofanya]? Akawageukia, akawakanya. [Akasema,

Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.] Kwa maana

Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali

kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine” [Luk

9:50-56]

Yakobo na Yohana walifikiri wako sahihi kutaka kutamka

maneno ya kuua kwa kualika moto ushuke kutoka

mbinguni. Lakini Yesu Kristo anawaambia hamjui roho

UHURU WA KWELI 246

mliyonayo, Mwana wa Adamu hakuja kuangamiza roho za

watu bali kuokoa. Kwahiyo haijalishi ni jambo gani baya

unakutana nalo tamka kwenye mdomo wako baraka tu na

sio laana. Uwe umeumizwa, uwe umefadhaishwa, uwe uko

katika hali ngumu bado hutakiwi kukiri laana kwenye

maisha yako au kwenye maisha ya wengine.

Maeneo tunayotakiwa kukiri wakati wote kwenye maisha

yetu kupitia imani ya Yesu Kristo;

Nitakiri mimi nimebarikiwa

Nitakiri mimi ni mrithi

Nitakiri mimi ni mfalme

Nitakiri mimi nimeponywa

Nitakiri mimi ni mshindi

Paulo aliwaandikia hivi Wakorintho;

“Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri

yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao

kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya

Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.

Maana hatuwaandikii ninyi neno, ila yale msomayo, au

kuyakiri; nami nataraji ya kuwa mtayakiri hayo hata

mwisho” [2Kor 1:12-13]

UHURU WA KWELI 247

Paulo aliwaambia Wakorintho kuwa tunawaandikieni hayo

kwasababu ninatarajia mtayakiri hayo hata mwisho.

Nitakiri mimi nimebarikiwa

Ilikuwa ni mpango wa Mungu tangu mwanzo tubarikiwe

kupitia Yesu Kristo. Mungu alimbarikia Ibrahimu ili kusudi

atakayemwamini Mwana wake wa pekee Yesu Kristo.

Ahesabiwe baraka ya Ibrahimu kwa njia ya imani.

“Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama,

kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake

katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo

kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya

mwanawe. Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-

yire,kama watu wasemavyo hata leo,Katika mlima wa

BWANA itapatikana. Malaika wa Bwana akamwita

Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni akasema, Nimeapa

kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno

hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee, katika

kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao

wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko

pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao; na

katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa

sababu umetii sauti yangu [Mwanz 22:13-18]

UHURU WA KWELI 248

Ibrahimu alipoamua kumtoa mwana wake wa pekee Isaka,

bila kumzuilia. Mungu akaapa kuwa atambariki na

kuuzidisha uzao wake, kama nyota za mbinguni na kama

mchanga wa baharini. Mungu alimuahidi Ibrahimu kupitia

baraka alizobarikiwa mataifa yote ya dunia yatabarikiwa.

Mungu alituingiza kupokea baraka ya Ibrahimu kwa njia ya

kumwamini Yesu Kristo. Ndio maana imeandikwa;

“Basi, tusemeje juu ya Ibrahimu, baba yetu kwa jinsi ya

mwili?” [Rum 4:1]

Kumbe sisi tumefanyika watoto wa Ibrahimu kwa jinsi ya

mwili kwa njia ya imani ya Yesu Kristo. Ndio maana Paulo

aliandika;

“Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa

Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi” [Gal 3:29]

Kumbe sisi tumefanyika kuwa uzao wa Ibrahimu yaani

watoto wa Ibrahimu kwa jinsi ya mwili njia ya imani ya

kumwamini Yesu Kristo. Kwasababu hiyo sisi ni warithi sawa

sawa na ahadi ya Ibrahimu. Kama vile Mungu alivyomuahidi

Ibrahimu kuwa uzao wako utakuwa kama nyota za

mbinguni na mchanga ulioko pwani. Sisi ni zao lake

tuliofanywa kupitia imani ya Yesu Kristo. Kwasababu hiyo

tuna haki ya kumiliki na kuwa warithi halali wa baraka

alizobarikiwa Ibrahimu na uzao wake. Ndio maana biblia

inasema;

UHURU WA KWELI 249

“Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa

alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa,

Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; ili kwamba

baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo,

tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani” [Gal 3:14]

Kristo alifanyika laana ili atukomboe tusikae chini ya laana

na kwa njia ya imani katika yeye sisi tuliomwamini Yesu

Kristo tumebarikiwa sawa sawa na baraka ya Ibrahimu. Kwa

sababu hiyo tunatakiwa kukiri wakati wote sisi ni

wabarikiwa na si walaaniwa kwa jina la Yesu Kristo.

Nitakiri mimi ni mrithi

Kupitia Yesu Kristo tulifanyika wana na Warithi kwa njia ya

Imani.

“Lakini nasema ya kuwa mrithi, wakati wote awapo mtoto,

hana tofauti na mtumwa, angawa ni bwana wa yote; bali

yu chini ya mawakili na watunzaji, hata wakati uliokwisha

kuamriwa na baba. Kadhalika na sisi, tulipokuwa watoto,

tulikuwa tukitumikishwa na kawaida za kwanza za dunia.

Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma

Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa

chini ya sheria, kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya

sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana. Na kwa

kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa

UHURU WA KWELI 250

Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba” [Gal

4:1-6]

Kabla hatujamjua Yesu Kristo tulikuwa kama watoto, lakini

Kristo alipokufa kwaajili yetu alitufanya tuwe wana cheo

cha wana kilitupa nafasi ya kuwa warithi. Ili tuweze kuwa

wana nilazima tuwe na ufahamu kuhusu Yesu Kristo.

Ukiokoka unafanyika mwana ili uwe uanze kuwa mwana

halisi lazima uwe na ufahamu kupitia Yesu Kristo (Efe 4:13).

Kumbe unaweza kuwa mtoto mchanga katika Kristo pia

unaweza kuwa mwana katika Kristo. Mtoto mchanga katika

Kristo ni yule aliye katika Kristo (aliyeokoka) lakini hajui haki

zake kupitia Yesu Kristo. Mwana katika Kristo ni yule

aliyekatika Kristo (aliyeokoka) na anajua haki zake katika

Yesu Kristo. Ndio maana Paulo aliwaambia Wakorintho;

“Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama

na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye

tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo.

Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa

mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi, kwa

maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana,

ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya

mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?”

[1Kor 3:1-3]

UHURU WA KWELI 251

Wakorintho walikuwa ni watu wa tabia za mwilini, akili ya

mwilini ndio maana Paulo aliwaambia kama kwenu kuna

fitina ninyi si watu wa mwilini? Ndio maana mnaenenda

kwa jinsi ya kibinadamu, ndio maana Paulo aliwaambia

Waefeso wazidi kumfahamu sana Mwana wa Mungu. Ili

waweze kufikia kimo na utimilifu wa Kristo (Efe 4:13),

kwasababu alijua bila kumfahamu sana Mwana wa Mungu

ni rahisi kutekwa na mapokeo ya wanadamu. Ndio maana

Paulo aliwaambia Wakolosai;

“Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure

na madanganyo matupu, kwa jinsi ya mapokeo ya

wanadamu, kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya

ulimwengu, wala si kwa jinsi ya Kristo” [Kol 2:8]

“Ee Timotheo, ilinde hiyo amana; ujiepushe na maneno

yasiyo ya dini, yasiyo na maana, na mshindano ya elimu

iitwayo elimu kwa uongo; ambayo wengine wanaikiri hiyo

wameikosa Imani. Neema na iwe pamoja nanyi” [1Timo

6:21]

Kwa hiyo, kumbe kuna mafundisho yanayofundishwa kwa

mapokeo ya wanadamu na mengine ni yale yanafundishwa

kwa jinsi ya Kristo. Mafundisho yanayoweza kukukuza

kufikia kimo na utimilifu wa Kristo ni yale yanayofundishwa

UHURU WA KWELI 252

kwa jinsi ya Kristo na sio mapokeo. Ndio maana maandiko

yansema tunatakiwa kumjua sana Mwana wa Mungu ili

tufikie kimo na utimilifu wa Kristo ili tusiwe watoto

wachanga. Tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila

upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukifuata njia

za udanganyifu (Efe 4:14).

Ndio maana Paulo alimsisitiza motto wake Timotheo kuwa;

mtu yoyote akifundisha elimu nyingine, wala hayakubali

maneno yenye uzima wa Bwana wetu Yesu Kristo. Wala

mafundisho yenye utauwa basi mtu huyo hafahamu neno

lolote (1Tim 6:3-4). Ndio maana akamkumbusha kuwa kwa

sababu ya watu kusikiliza elimu ya mapokeo, elimu isiyo ya

Kristo. Ndio maana Paulo alimsihi Timotheo alipokuwa

anakwenda Makedonia. Awakataze wengine wasifundishe

elimu nyingine na wala wasiangalie hadithi zisio na ukomo

ambazo hazileti imani katika Mungu (1Timo 1:3-4).

Tumefanyika kuwa wana wa Mungu kupitia kifo cha Yesu

Kristo pale msalabani.

“Na kwa sababu hii ni mjumbe wa agano jipya, ili, mauti

ikiisha kufanyika kwa kukomboa makosa yaliyokuwa chini

ya agano la kwanza, hao walioitwa waipokee ahadi ya

urithi wa milele. Maana agano la urithi lilipo, lazima iwepo

mauti yake aliyelifanya. Kwa maana agano la urithi lina

UHURU WA KWELI 253

nguvu palipotukia kufa kwa mtu; kwa kuwa halina nguvu

kabisa, akiwa yu hai yeye aliyelifanya” [Ebr 9: 15-17]

Kupitia kifo cha Yesu Kristo pale msalabani tulifanyika

warithi kupitia ile mauti yake na kuingizwa kwenye agano la

urithi wa kila alichokifanya Yesu Kristo kwaajili yetu.

Tunatakiwa kukiri wakati wote kwenye maisha yetu kuwa ni

warithi halali kupitia agano la kifo alilolifanya Yesu Kristo

pale msalabani.

Nitakiri mimi ni mfalme.

“macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito

wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika

watakatifu jinsi ulivyo; na ubora wa ukuu wa uweza wake

ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa

nguvu za uweza wake; aliotenda katika Kristo alipomfufua

katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika

ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na

mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala

si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia” [Efe 1:18-

21]

“Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye

katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu” [Efe 2:6]

UHURU WA KWELI 254

Sisi tuaminio tulifufuliwa pamoja na Kristo, tukaketishwa

katika ulimwengu wa roho na kuwekwa juu sana kuliko

ufalme wote, mamlaka, nguvu na usultani.

Tumefanyikakuwa wafalme kupitia kufa kwake na

kufufuliwa kwake.

Kifo cha Yesu msalabani ilikuwa ni mwanzo wa kutawala

kwetu tunayemwamini.

“Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema,

imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake” [Yoh

19:30]

Biblia inaposema roho yake biblia ya kigiriki imetumia

maneno “ekpneo” na ekpsucho”. Maana yake kutoa pumzi

nje. Baada ya Yesu kutoa pumzi nje alipumzika.Yesu

alipopumzika ndiko tunapotakiwa kuanzia. Maandiko

yanasema;

“Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu

yake, na kutufanya kuwa ufalme, makuhani kwa Mungu

naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una yeye hata milele na

milele.Amina” [Ufu 1:5b-6]

KJV anasema tulifanywa kuwa wafalme. Yaani kupitia damu

ya Yesu Kristo tulifanywa kuwa wafalme. Kama ni hivyobasi

tunatakiwa kukiri kila wakati kuwa sisi ni wafalme kupitia

UHURU WA KWELI 255

Yesu Kristo. Kifo cha Yesu Kristo msalabani ilikuwa ni

mwanzo wakutawala, alipopumzika, ulikuwa ni mwanzo wa

kutawala kwetu. Mfalme mara zote huwa ni mtu

aliyepumzika, hana msongo wa mawazo, hapambani,wala

hana mashaka lakini kila anachokitaka anakipata. Sio kwa

sababu anatafuta ila kwa sababu ya nafasi yake kinachompa

nafasi hiyo ni kiti alichokalia cha ufalme. Watu wengine

watamtumikia, au mazingira ili mradi apate anachokitaka

hiyo ndiyo kanuni ya mfalme. Unahitaji kutambua kuwa

wewe ni mfalme katika Kristo Yesu.

Mfalme:- Ni mtawala katika nchi huru inayojitegemea,

asiyechaguliwa na mtu yoyote, anayerithi nafasi kwa njia

ya uzo halali.

Mungu alitufanya kuwa wafalme halali kwa uzao kipitia

Yesu Kristo kwa njia ya kurithi ambaye ni uzao wa

kifalme.Ndio maana imeandikwa;

“Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa

takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza

fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika

nuru yake ya ajabu” [1Pet 2:9]

UHURU WA KWELI 256

Tabia za mfalme;

Anatoa amri

Ni mtu wa maamuzi

Anaishi kwa uadilifu

Anaunda na kuhamasisha ubunifu kwa wengine

Anaacha urithi kwa wengine

Anabariki maisha ya wengine

Nitakiri mimi ni mfalme katika Kristo Yesu kila wakati.

Nitakiri mimi nimeponywa

Isaya alitabiri kabla ya Yesu kufa msalsabani kuwa;

“Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa

maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na

kwa kupigwa kwake sisi tumepona” [Isa 53:5]

Petro aliandika katika Waraka wake wa kwanza kuwa;

“Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili

wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe

hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake

mliponywa” [1Pet 2:24]

UHURU WA KWELI 257

Yesu Kristo kwa kupigwa kwake tuliponywa, na adhabu ya

amani ya Yesu Kristo ilikuwa juu yake. Alibeba dhambi zetu

na kuachilia haki kwaajili yetu, haki ya uponyaji ni mali yetu

kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. Yesu alipopigwa

mijeledi tulikuwako ndani yake na kwa kupigwa kwake sisi

tukahesabiwa kuwa ni wazima. Hatuna haja ya kujiumiza

tena kwa sababu sadaka ilikwisha kutolewa (sadaka ya

Mwana kondoo) ili kusudi tufanyike wazima.

Tunatakiwa kumla Yesu Kristo mwili wake akiwa

ameokwa na sio mbichi

Tuangalie maelekezo waliyopewa Wana wa Israeli kuhusu

kumla Mwanakondoo;

Bwana akanena na Musa na Haruni katika nchi ya Misri,

akawaambia, Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi

kwenu; utakuwa ni mwezi wa kwanza wa mwaka kwenu.

Semeni na mkutano wote wa Israeli, mkawaambie, Siku ya

kumi ya mwezi huu kila mtu atatwaa mwana-kondoo, kwa

hesabu ya nyumba ya baba zao, mwana-kondoo kwa watu

wa nyumba moja; na ikiwa watu wa nyumba ni wachache

kwa mwana-kondoo, basi yeye na jirani yake aliye karibu na

nyumba yake na watwae mwana-kondoo mmoja, kwa

kadiri ya hesabu ya watu; kwa kadiri ya ulaji wa kila mtu,

UHURU WA KWELI 258

ndivyo mtakavyofanya hesabu yenu kwa yule mwana-

kondoo.

Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume wa mwaka

mmoja; mtamtwaa katika kondoo au katika mbuzi. Nanyi

mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na

kusanyiko lote la mkutano wa Israeli watamchinja jioni. Nao

watatwaa baadhi ya damu yake na kuitia katika miimo

miwili na katika kizingiti cha juu, katika zile nyumba

watakazomla. Watakula nyama yake usiku ule ule,

imeokwa motoni, pamoja na mkate usiotiwa chachu; tena

pamoja na mboga zenye uchungu.

Msiile mbichi, wala ya kutokoswa majini, bali imeokwa

motoni; kichwa chake pamoja na miguu yake, na nyama

zake za ndani. Wala msisaze kitu chake cho chote hata

asubuhi, bali kitu kitakachosalia hata asubuhi mtakichoma

kwa moto. Tena mtamla hivi; mtakuwa mmefungwa viuno

vyenu, mmevaa viatu vyenu miguuni, na fimbo zenu

mikononi mwenu; nanyi mtamla kwa haraka; ni pasaka ya

Bwana. Maana nitapita kati ya nchi ya Misri usiku huo, nami

nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri,

wa mwanadamu na wa mnyama; nami nitafanya hukumu

juu ya miungu yote ya Misri; Mimi ndimi Bwana.

Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba

mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, nitapita juu

yenu, lisiwapate pigo lo lote likawaharibu, nitakapoipiga

UHURU WA KWELI 259

nchi ya Misri. Na siku hii itakuwa ukumbusho kwenu, nanyi

mtaifanya iwe sikukuu kwa Bwana; mtaifanya iwe sikukuu

katika vizazi vyenu vyote, kwa amri ya milele [Kut 12:1-14]

Wana wa Israeli walipewa maelekezo ya kumla

Mwanakondoo akiwa ameokwa motoni. Pamoja na kichwa

chake, miguu yake na nyama zake za ndani. Wana wa Israeli

waliambiwa wasisaze kitu chochote. Wana wa Israeli

ilikuwa inawakilisha aliyeamini (aliyeokoka),

Mwanakondoo alikuwa anamuwakilisha Yesu Kristo. Wana

Wa Israeli waliambiwa wamle mwanakondoo akiwa

ameokwa pamoja na kichwa chake, miguu yake na nyama

za ndani. Alikuwa anazungumziwa Yesu Kristo kuwa

unatakiwa kumuangalia Kristo msalabani akiwa

amehukumiwa kwa ghadhabu kuu. Akiwa ameteseka kwa

kiwango cha mwisho kwaajili yako, na kwa namna hiyo

ukiona hivyo uzima utakuwa unaachiliwa kuanzia kichwani.

Kama unamatatizo au ugonjwa wa ubongo, miguuni kama

unamatatizo ya miguuni, nyama za ndani NIV amesema

viungo vya ndani. Maana yake maini, figo, mapafu, moyo,

kongosho, utumbo, tumbo, bandama. Vyote utaponywa

kwa kuangalia adhabu na mateso makuu aliponing’inizwa

pale msalabani. Kama wana wa Israeli walivyopewa

maelekezo ya kula kila kitu akiwa ameokwa. Na sisi pia

tunatakiwa kumla Yesu Kristo kila kitu, na utakapokuwa na

ugonjwa wa kichwa, miguu, viuongo vya ndani. Yaani iwe ni

UHURU WA KWELI 260

figo, mapafu, moyo, kongosho, utumbo, tumbo, bandama

vyote vitaponywa kupitia adhabu aliyoipata Yesu Kristo

msalabani.

Wakati mwingine umeshindwa kupona sio kwasababu

haujaponywa ila kwa sababu hujajua Yesu Kristo

alichofanya kwaajili yako. Ukimtazama Yesu Kristo halisi na

mateso yake huhitaji kujiumiza wewe ili uponywe kwa

imani tu. Utaanza kuona ugonjwa uliokamata kongosho

yaani kisukari, uwe ni ugonjwa wa moyo yaani shinikizo la

damu, iwe ni kansa ya ini, iwe ni kansa ya mapafu. Kupitia

Yesu Kristo uponyaji utaachiliwa tena sasa hivi, unahitaji

kumwamini Yesu Kristo kikamilifu ili upokee uponyaji wako

sasa. Kiri kuanzia sasa kwa kupigwa kwa Yesu Kristo

uliponywa. Ameni haleluya!

Nitakiri mimi ni mshindi.

Sasa tumebakiwa kukiri kuwa ni washindi, tulishapiganiwa

na Mungu vita zote zinazohusu maisha yetu. Ndio maana

Daudi alimwambia Goliati hivi;

“Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana

haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya

Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu” [1Samw

17:47]

UHURU WA KWELI 261

Kama Daudi alikuwa katika kipindi cha agano la kale alikiri

kuwa vita si vyake ni vya Bwana. Maana yake aliamini yeye

mwenyewe hawezi kupigana akashinda bali Bwana

anaweza kumpigania akashinda. Daudi alimshinda yule

mfilisti (Goliati) kwa sababu Bwana alimpigania je si zaidi

sana wewe uliye katika agano jipya? Habari njema hi hii

kwamba; wewe uliye katika agano jipya ulishapiganiwa

tayari na Yesu Kristo. Na ulishashinda miaka elfu mbili

iliyopita. Wewe unatakiwa kuamini kuwa ulishashinda na

kukiri ushindi ulionao. Paulo anathibitisha hili

alipowaandikia Warumi;

“Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki

au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?

Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya

kushinda, kwa yeye aliyetupenda” [Rum 8:35, 37]

Kumbe tulishashinda katika yeye kiri kuwa wewe ni mshindi

wakati wote kwenye maisha yako. Bila kujali unanjaa au

umeshiba, bila kujaliunadhiki au la, bila kujali upo kwenye

hatari au upanga. Kiri mimi ni mshindi, Ameni Haleluya!

UHURU WA KWELI 262

Tathmini kupitia maswali kutoka katika Sura ya Kumi

1: Kwanini tunatakiwa kukiri kwa mdomo wakati wote

tuliyokirimiwa katika Kristo Yesu?

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

……………………………………

2: Taaja maana yam domo kwa kigiriki

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………...

3: Taja maeneo matano tunayotakiwa kukiri wakati wote

katika Kristo Yesu

(i)………………………………………………………………………………………

…………………………………………

(ii)………………………………………………………………………………………

……………………………………....

(iii)……………………………………………………………………………………

…………………………………………

UHURU WA KWELI 263

(iv)……………………………………………………………………………………

………………………………………….

(v)………………………………………………………………………………………

……………………………………….

UHURU WA KWELI 264

UHURU WA KWELI 265

HITIMISHO

ujua wewe ni nani katika Yesu Kristo ni muhimu sana,

ili uweze kuanza kuona udhihirisho wa uhalisia ulio nao.

Ukijua haki zako katika Kristo Yesu sio rahisi kuishi

maisha yasiyo na haki. Kujua baraka zako, utakatifu, imani

na utimilifu ni muhimu sana. Kuanzia sasa nakushauri

kuambatana na injili ya neema ya Kristo. Maana hii ndiyo

injili ambayo Bwana Yesu alitutuma tuihubiri kwa mataifa

yote, na ndiyo injili inayokujulisha wewe ni nani katika Yesu

Kristo. Biblia imeandika kuwa;

“Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema imekwisha.

Akainama kichwa akaisalimu royo yake” [Yoh 19:30]

Kama Yesu Kristo alisema imekwisha pale msalabani. Basi

ujue alimaliza kila kitu kinachohusiana na maisha yetu pale

msalabani na uwe na uhakika hakuna kitu ambacho Yesu

Kristo hakufanya kinachohusiana na maisha yako. Kama ni

hivyo basi hali tukijua hivyo hatuna sababu ya kujitafutia

mambo yetu wenyewe. Muhimu ni kuwa tujitambue sisi ni

wa kina nani katika yeye. Ili tufurahie ile zawadi ya wokovu

kutoka kwake.

Tujue uhalisia wetu kupitia injili yake na neno lake Yesu

Kristo na kwa namna hiyo nakushauri kusoma vitabu

vinavyokusaidia kujua wewe ni nani katika Yesu Kristo.

K

UHURU WA KWELI 266

Sikiliza kwa wingi CD, nyimbo, mahubiri mafundisho

yanayokusaidia kujua wewe ni nani katika Yesu Kristo. Soma

sana vitabu vinavyokusaidia kujua wewe ni nani katika Yesu

Kristo. Kwa namna hiyo nafsi yako ikigeuzwa huku nje

kuuona uhalisia wako ndani ya Yesu Kristo haitakuwa shida.

Utaona uhalisia wako wa jinsi ulivyo katika Kristo Yesu. Zile

baraka zote ulizipokea katika Yesu Kristo, haki yako

uliyopewa zawadi, utakatifu na kutukuzwa utaanza

kuvishuhudia kwenye maisha yako halisi ya mwilini.

Natamani siku kuona ukishuhudia kuwa neno la Kristo

limebadilisha maisha yako kabisa na umekuwa hodari

katika Bwana. Bwana wa mbinguni amekubariki sana.

UHURU WA KWELI 267

KUHUSU MWANDISHI

araka Fredy Shibanda ni Mtumishi wa Mungu ambaye

Mungu amempa huduma ya Uinjilisti na Ualimu.

Alihitimu kidato cha nne mwaka 2013 katika shule ya

Sekondari Chanji iliyoko mkoa wa Rukwa-Tanzania. Baada

ya hapo mnamo mwaka 2014-2016 alifanikiwa kuchaguliwa

kujiunga na masomo ya kidato cha tano na sita katika Shule

ya wavulana Songea (Songea boys). Iliyoko Mkoa wa

Ruvuma, wilaya ya Songea, Tanzania.

Baada ya hapo alifanikiwa kujiunga na masomo katika chuo

kikuu cha Dodoma (UDOM), Dodoma-Tanzania. Kuanzia

mwaka 2016 mpaka mwaka 2019 alifanikiwa alihitimu

masomo yake ya Stahahada katika utaalamu wa maabara

ya afya.

Baraka Fredy Shibanda pia ni mwanzilishi na kiongozi mkuu

wa huduma ya Udhihirisho wa Mungu (Godly Power

Manifestastion Ministry) [GPM]. Aliyoianzisha mnamo

mwaka 2017, inayolenga kuhubiri injili na kufundisha neno

la Kristo katika nchi ya Tanzania na duniani kote. Huduma

hii inaendeshwa na misheni kutoka kitabu cha Matendo ya

Mitume Sura ya kwanza mstari wa nane. Inayosema,

“Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho

Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika

B

UHURU WA KWELI 268

Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata

mwisho wa nchi”

Pia huduma hii imekuwa ikiwatunza watoto yatima na kila

wenye uhitaji angalau mara moja kwa mwaka. Kufanya

mikutano na semina za mara kwa mara ili kuweza kuifikishia

dunia habari njema. Kuanzia Tanzania, nje ya nchi na

duniani kote kwa watu wote waliookoka na wasiookoka.

Pia ni Mwinjilisti na Mwalimu.

Anapatikana katika mitandao ya kijamii ifuatayo:-

YouTube: GPM Ministry

Facebook: Evangelist and Teacher Baraka Shibanda

Twitter: Evangelist and Teacher Baraka Shibanda

Instagram: Evangelist and Teacher Baraka Shibanda

UHURU WA KWELI 269

VITABU VINGINE KUTOKA KWAKE:

UHURU WA KWELI 270

Unaweza kuvipata siku hii ya leo ili uweze kukua zaidi

kiakili na kiroho.

Simu: +255 767 495 842 | +255 768670143 | +255

621054592