Huzuni katika nyimbo za taarab za waimbaji Bi Fatma Issa na ...

88
The University of Dodoma University of Dodoma Institutional Repository http://repository.udom.ac.tz Humanities Master Dissertations 2016 Huzuni katika nyimbo za taarab za waimbaji Bi Fatma Issa na Shakila Said Rashid, Zeyana Omar Chuo Kikuu cha Dodoma Rashid, Z. O. (2016). Huzuni katika nyimbo za taarab za waimbaji Bi Fatma Issa na Shakila Said (Tasnifu shahada ya uzamili). Chuo Kikuu cha Dodoma, Dodoma. http://hdl.handle.net/20.500.12661/850 Downloaded from UDOM Institutional Repository at The University of Dodoma, an open access institutional repository.

Transcript of Huzuni katika nyimbo za taarab za waimbaji Bi Fatma Issa na ...

The University of Dodoma

University of Dodoma Institutional Repository http://repository.udom.ac.tz

Humanities Master Dissertations

2016

Huzuni katika nyimbo za taarab za

waimbaji Bi Fatma Issa na Shakila Said

Rashid, Zeyana Omar

Chuo Kikuu cha Dodoma

Rashid, Z. O. (2016). Huzuni katika nyimbo za taarab za waimbaji Bi Fatma Issa na Shakila

Said (Tasnifu shahada ya uzamili). Chuo Kikuu cha Dodoma, Dodoma.

http://hdl.handle.net/20.500.12661/850

Downloaded from UDOM Institutional Repository at The University of Dodoma, an open access institutional repository.

HUZUNI KATIKA NYIMBO ZA TAARAB ZA WAIMBAJI BI

FATMA ISSA NA SHAKILA SAID

Na

Zeyana Omar Rashid

Tasnifu Iliyowasilishwa kwa Ajili ya Kukamilisha Mahitaji ya Shahada ya Uzamili

ya Sayansi ya Jamii katika Fasihi ya Kiswahili Chuo Kikuu cha Dodoma

Chuo Kikuu cha Dodoma

Oktoba, 2016

i

ITHIBATI

Aliyetia saini hapa chini anathibitisha kuwa ameisoma tasnifu hii iitwaayo “Huzuni

katika nyimbo za taarab za waimbaji Bi Fatma Issa na Shakila Said”, na

kupendekeza ikubaliwe na Chuo Kikuu cha Dodoma kwa ajili ya kukamilisha

masharti ya Shahada ya Uzamili katika Fasihi ya Kiswahili ya Chuo Kikuu cha

Dodoma.

…………………………………

Dkt. Muhammed Seif Khatib

(Msimamizi)

Tarehe…………………………

ii

IKIRARI

NA

HAKI MILIKI

Mimi Zeyana Omar ninathibitisha kuwa tasnifu hii ni kazi yangu halisi na haijawahi

kuwasilishwa na haitawasilishwa katika chuo kikuu kingine kwa ajili ya shahada

yoyote.

Saini……………………

Hairuhusiwi kunakili, kutafsiri, kupiga chapa au kuiga sehemu yoyote ya tasnifu hii

bila ya ruhusa ya mwandishi au Chuo Kikuu cha Dodoma

iii

SHUKURANI

Kwanza kabisa, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa

kunijaalia uzima na afya njema katika kipindi chote cha kukamilisha utafiti huu. Pili,

ninamshukuru msimamizi wa utafiti huu, Dkt Muhammed Seif Khatib ambaye

alikuwa mwongozaji wa kazi hii na alifanya juhudi kubwa kuhakikisha kuwa utafiti

huu unamalizika katika hali ya ubora zaidi. Mwenyezi Mungu amlipe ujira mwema,

Amina.

Aidha, nawashukuru walimu wangu wote walionifundisha kozi za Fasihi ya

Kiswahili ambao kwa kiasi kikubwa waliweza kupanua uelewa wangu ulionisaidia

kukamilisha utafiti. Tatu, nawashukuru wazazi wangu Bi Fatma Almasi na Bwana

Omar Rashid ambao mbali na kunileya na kunipatia elimu, walifanya kazi kubwa ya

kuhakikisha kuwa namaliza masomo yangu kwa mafanikio mkubwa. Mwenyezi

Mungu awape umri mrefu na wenye afya njema katika maisha yao. Vilevile

ninawashukuru ndugu zangu Rukaiyya Omar, Tauhida Omar na Ali Omar kwa

kuonesha upendo wao wa dhati kwangu na kumlea mtoto wangu katika misingi bora

wakati nikiwa masomoni. Nitakuwa mwizi wa fadhila iwapo sikumshukuru mume

wangu mpenzi Bwana Mbarouk Nassor kwa kunivumilia pale nilipomwacha na

upweke lakini bado kaendelea kunidhihirishia upendo wake kwangu katika kipindi

hicho kigumu.

Nne, ninawashukuru walimu na wanafunzi wenzangu, Mabwana Kassim Simai,

Makame Pandu, Khamis Saleh, pamoja na Mabibi Zuleikha Abdallah, Bushura

Khamis na Salama Omar kwa mashirikiano na kubadilishana mawazo juu ya tafiti

zetu.

iv

TABARUKU

Ninaitabaruku tasnifu hii kwa mume wangu mpenzi, Bw Mbarouk N Mbarouk na

watoto wangu Ak-thar Mbarouk na Afnaan Mbarouk kwa kunijali katika kipindi

chote cha masomo yangu. Ipokeeni kazi hii kama zawadi katika maisha yenu.

Nawapenda nyote.

v

IKISIRI

Utafiti huu uliongozwa na malengo matatu ambayo yaliweza kusaidia na kubainisha

huzuni katika nyimbo za taarab za waimbaji Fatma na Shakila. Tafiti, makala, vitabu

na maoni ya wadau mbalimbali kuhusiana na suala zima la taarab asilia yalisaidia

kuchunguza dhamira pamoja na sababu mbalimbali zilizowasukuma wasanii wateule

kutunga na kuimba nyimbo za huzuni.

Utafiti huu ulifanyika uwandani na maktabani na kutumia mbinu ya usaili, udodosaji

na ushuhudiaji katika kukusanya data. Maeneo yaliyotumika katika ukusanyaji wa

data za nyimbo za taarab ni studio za Zenji FM na Coconut FM katika mkoa wa

Mjini Magharibi Unguja. Data zilichambuliwa kwa kuongozwa na nadharia ya

uhalisia ambayo imeongozwa na misingi yake mikuu miwili ambayo ni ushabihi

ukweli na msingi wa kimhakati. Nadharia hii ya uhalisia iliyotumika ilisaidia

kufanunua sababu zinazowasukuma wasanii kutunga nyimbo hizo, athari na hata

dhamira za nyimbo hizo.

Matokeo ya utafiti huu yameonesha kuwa huzuni humfika kila mtu katika jamii na ni

jambo lisiloweza kuepukika kwa mwanadamu yoyote yule. Nyimbo za huzuni

hutungwa kutokana na matukio mbalimbali ambayo yanawafika watu katika jamii.

Matukio hayo yaweza kuwa ya kijamii, kisiasa, na hata kiuchumi. Lakini katika

utafiti huu imedhihirika kuwa mara nyingi huzuni hutokea kutokana sababu za

kijamii kama vile kusalitiwa, kufiwa, ubinafsi, kukosa bahati na mengineyo. Ingawa

tafsiri ya awali na mawazo ya watu wengi ilionesha kuwa taarab ni muziki wa furaha

na ramsa, utafiti huu umebainisha kuwa sio kila nyimbo ya taarab ni ya furaha.

vi

YALIYOMO

ITHIBATI ...................................................................................................................... i

IKIRARI NA HAKI MILIKI ....................................................................................... ii

SHUKURANI ............................................................................................................. iii

TABARUKU ............................................................................................................... iv

IKISIRI ......................................................................................................................... v

YALIYOMO ............................................................................................................... vi

ORODHA YA VIELELEZO NA PICHA .................................................................. ix

SURA YA KWANZA ................................................................................................. 1

1.1 Utangulizi ............................................................................................................... 1

1.2 Usuli wa Tatizo ...................................................................................................... 1

1.3 Tamko la Utafiti ..................................................................................................... 3

1.4 Wasifu wa Fatma Issa Juma ................................................................................... 3

1.5 Malengo ya Utafiti ............................................................................................... 15

1.5.1 Lengo Kuu ......................................................................................................... 15

1.5.2 Malengo Mahsusi .............................................................................................. 15

1.6 Maswali ya Utafiti ................................................................................................ 15

1.7 Manufaa ya Utafiti ............................................................................................... 15

1.8 Nadharia ya Utafiti ............................................................................................... 15

1.9 Hitimisho .............................................................................................................. 16

SURA YA PILI: MAPITIO YA MAANDIKO ...................................................... 17

2.1 Utangulizi ............................................................................................................. 17

2.2 Chimbuko la Taarab Zanzibar .............................................................................. 17

2.3 Maandiko Yahusuyo Taarab ................................................................................ 19

2.4 Pengo la utafiti ..................................................................................................... 24

2.5 Hitimisho .............................................................................................................. 24

SURA YA TATU: USANIFU NA MBINU ZA KUKUSANYIA DATA ............. 25

3.1 Utangulizi ............................................................................................................. 25

3.2 Mpango wa utafiti ................................................................................................ 25

3.3 Eneo la utafiti ....................................................................................................... 25

vii

3.4 Walengwa wa Utafiti ............................................................................................ 25

3.4.1 Jamii ya Watafitiwa ........................................................................................... 26

3.4.2 Usampulishaji na Sampuli Iliyotumika ............................................................. 26

3.5 Ukusanyaji wa Data ............................................................................................. 27

3.5.1 Njia za ukusanyaji wa data ................................................................................ 27

3.5.2 Usaili ................................................................................................................. 27

3.5.3 Dodoso .............................................................................................................. 27

3.5.4 Ushuhudiaji ....................................................................................................... 27

3.6 Zana za kukusanyia data ...................................................................................... 28

3.6.1 Kamera .............................................................................................................. 28

3.6.2 Simu .................................................................................................................. 28

3.6.3 Daftari na kalamu .............................................................................................. 28

3.6.4 Ngamizi ............................................................................................................. 28

3.7 Mchakato wa Ukusanyaji Data na Uthabiti wake ................................................ 28

3.8 Mipaka ya Utafiti ................................................................................................. 29

3.9 Vikwazo vya Utafiti na Utatuzi wake .................................................................. 29

SURA YA NNE: UWASILISHAJI, UCHAMBUZI NA MATOKEO YA

MJADALA WA UTAFITI ...................................................................................... 30

4.1 Utangulizi ............................................................................................................. 30

4.2 Dhana ya Huzuni .................................................................................................. 30

4.3 Nyimbo za huzuni za waimbaji wateule .............................................................. 31

4.4 Sababu za Kutunga Nyimbo Za Huzuni ............................................................... 37

4.4.1 Usaliti ................................................................................................................ 37

4.4.1.1 Usaliti wa mume na mke ................................................................................ 37

4.4.2 Msiba ................................................................................................................. 39

4.4.3 Maliwazo na Ufariji .......................................................................................... 40

4.4.4 Choyo na Husuda .............................................................................................. 41

4.4.5 Ufitini na uchongezi .......................................................................................... 43

4.4.6 Huzuni na hali halisi ya maisha ......................................................................... 44

4.4.7 Huzuni na majuto .............................................................................................. 46

4.4.8 Huzuni na bahati ................................................................................................ 48

4.5 Dhamira ya Huzuni katika Nyimbo za taarab na tija zake ................................... 50

viii

4.5.1 Kupanua dhana ya Taarab ................................................................................. 50

4.5.2 Kuelimisha ........................................................................................................ 50

4.5.3 Kuliwaza ............................................................................................................ 51

4.5.4 Kuzindua ........................................................................................................... 52

4.5.5 Kurekebika tabia ............................................................................................... 53

4.5.6 Ujenzi wa hisia na huruma ................................................................................ 53

4.5.7 Kuonesha ujasiri ................................................................................................ 55

4.6 Athari zinazopatika katika Nyimbo za Huzuni .................................................... 56

4.6.1 Athari Chanya ................................................................................................... 56

4.6.1.1 Kuifanya jamii kujua matatizo yake ............................................................... 56

4.6.1.2 Kufariji na kuliwaza ....................................................................................... 56

4.6.1.3 Kugusa nafsi ya msikilizaji ............................................................................ 56

4.6.2 Athari hasi za Nyimbo za Huzuni ..................................................................... 57

4.6.3 Tofauti ya Fatma na Shakila .............................................................................. 57

4.6.4 Mfanano wa Fatma na Shakila .......................................................................... 58

4.7 Hitimisho .............................................................................................................. 59

SURA YA TANO: MUHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO .......... 60

5.1 Utangulizi ............................................................................................................. 60

5.2 Muhtasari wa Tasnifu ........................................................................................... 60

5.3 Utoshelevu wa Nadharia Iliyotumika ................................................................... 61

5.4 Mambo Mapya Yanayoibuliwa na Tasnifu Hii .................................................... 62

5.5 Mapendekezo wa Tafiti Zijazo ............................................................................. 62

5.6 Maoni ya Mtafiti juu ya Utafiti Huu .................................................................... 63

MAREJELEO ........................................................................................................... 64

VIAMBATISHO ....................................................................................................... 66

A: Mwongozo wa usaili kwa wataalamu wa Fasihi. .................................................. 66

B: Dodoso kwa wanfunzi waliotafiti taarab asilia...................................................... 67

C: Nyimbo za waimbaji wateule Zilizotumika katika kazi hii ................................... 69

D: Picha mbali mbali zinazohusiana na utafiti ........................................................... 76

ix

ORODHA YA VIELELEZO NA PICHA

Shakila akifanya biashara nyumbani kwake Charambe (Utafiti, 2016)

Mtafiti akimuhaji bi Shakila huko yumbani kwake Charambe Dar es Salaam.

(Utafiti, 2016)

Mtafiti akimuhoji bi Fatma huko nyumbani kwake Kwa Alamsha, Zanzibar.

(Utafiti, 2016)

1

SURA YA KWANZA

1.1 Utangulizi

Fasihi simulizi ina vipera vyake muhimu katika jamii. Taarab ikiwa kipera cha fasihi

simulizi imejidhihisha kuwa na jukumu la kuelimisha, kuburudisha na kuhuzunisha

kupitia mashairi na muziki wake. Sura hii imejadili kuhusu usuli wa tatizo, tamko la

utafiti, wasifu wa waimbaji teule, malengo ya utafiti, maswali ya utafiti, manufaa ya

utafiti, nadharia ya utafiti na hitimisho.

1.2 Usuli wa Tatizo

Neno taarab limefasiriwa na wataalamu mbalimbali na kuweza kutoa maana yenye

kukaribiana. Kwa mujibu wa Rais mstaafu wa Tanzania Mzee Mwinyi, akinukuu

kamusi ya „Al- Maurid‟ anasema, “Taarab ni furaha iliyokithiri, raha iliyoje, starehe,

staladhi, tafrija, muziki, kuimba au kughani” (Khatib, 2014:1)

Pia, kwa mujibu wa kamusi ya Kiarabu na Kiingereza Al- Faraidal- Durriyya neno la

taarab lililokaririwa na Khatib (2014: 1) linanyambulika na kuwa „tariba, Yatrib, au

Taraba, maneno yote hayo yanamaanisha furaha. Kamusi jengine la A Learner‟s

Arabic- English Dictionary inaeleza kuwa neno, “Taarab lina maana ya kutiwa

hamasa, kuwa na furaha, kusherehekea karamu, kuimba, au kupiga muziki”. (Khatib,

2014: 1)

Nae Andanega (2002) anasema kuwa; “neno taarab linahusiana na aina ya ngoma

inayoitwa tarabu na pia na neno la Kiurdu- Kihindi tarabu, maana yake ni furaha”

(Andanega, 2002: 109).

Kutokana na tafsiri ya maana zote hizo, taarab ina maana ni ile hali ya upigaji muziki

kwa „furaha‟. Taarab hupigwa katika shughuli mbalimbali za kijamii ambapo watu

2

huburudika kwa kupitia mashairi yake. Hata hivyo, tatizo lililojitokeza na

kushangaza ni kuwa tafsiri zote hizo zinaelekeza taarab kimaana katika furaha na

ramsa tu na kusahau kuwa taarab huweza kubeba dhamira za simanzi au hata tanzia.

Zipo nyimbo nyingi ambazo mashairi yake hubeba hali ya jitimai, maafa au majonzi

ambayo yanawakumba wanadamu katika maisha yao ya kila siku. Taarab haimo

katika ombwe, kwa hivyo mashairi yake lazima hugusa maisha ya watu katika jamii.

Kihistoria, wakati taarab inaatikwa Zanzibar katika kasri ya Sultan, nyimbo nyingi

zilizoimbwa wakati huo zilikuwa ni za kumsifu na kumtukuza Sultani aliyepo

madarakani. Nyimbo za kuombea dua juu ya mapenzi ya Sultani na Malkia wake;

kumsifu muumba na maumbile ya ulimwengu na nyimbo nyengine za mikasa za

kumfanya Sultani atabasamu na acheke nazo hazikukosa (Khatib: 2014- 4). Kadri

siku zilivyozidi kuyoyoma na kubadilika kwa mifumo ya kiutawala Zanzibar,

nyimbo za taarab nazo zikabadilika na zikawa nazo ni zenye kubeba hisia tofauti

kama vile kupashana, kupalilia mapenzi baina ya watu wawili, kejeli au za simanzi.

Ni dhahiri kuwa katika maendeleo ya muziki wa taarab hivi sasa, nyimbo za huzuni

nazo zimeibuka kila pembe mithili ya uyoga. Hali hii ya kwenda sambamba kwa

nyimbo za furaha na huzuni zimekuwa ni sehemu ya maisha ya mwanadamu.

Ongezeko hili la nyimbo za huzuni katika tasnia ya muziki wa taarab haliendani

kabisa na dhamira na lengo halisi la asilia la uanzishwaji wa muziki wa taarab.

Wakati ule wa zamani wa watawala wa kisultani ndani ya kasir, taarab ilikusudiwa

kuwapa furaha na starehe tabaka tawala ikiwa ni sehemu ya burudani wakati wa

mapumziko yao. Haikutarajiwa Sultan awe na huzuni, kwani yeye hupewa kila kitu

atakacho. Taarab baada ya kutoka nje ya majengo ya Sultani na kuwa muziki wa

makabwela, tanzia na huzuni, haziachi kuwepo katika maisha yao halisi.

3

1.3 Tamko la Utafiti

Muziki wa taarab unapendwa sana na kwa sasa umeweza kupaa sana katika anga za

mwambao wa Afrika Mashariki na baadhi ya nchi jirani. Taarab hii imezigusa nyoyo

za watu kwa mashairi yake yanavyoakisi hali halisi ya maisha na utamu wa muziki

wake. Hivyo, sasa zipo nyimbo nyingi ambazo zinazungumzia maudhui na dhamira

ambazo zimekuwa za kudumu katika tasnia ya ushairi wa taarab kwa miaka nenda

miaka rudi. Hata hivyo, nyimbo zenye kuakisi mapenzi ya kusifu zipo nyingi na

zimeziteka nyoyo za watu wengi. Maisha ya binadamu ya uhalisia hayaogelei raha na

furaha tu, yapo mambo kadha yanayomsibu mtu na humpa huzuni na jitimai. Hivyo

zipo nyimbo nyingi zinazobeba dhamira za huzuni ambapo wasanii wa taarab

hutumia usanii wao kwa lengo la kuakisi hisia zao juu ya maafa ambayo yanatokezea

katika maisha yao au jamii inayowazunguka. Licha ya kuwepo kwa tafiti nyingi

ambazo hueleza mambo mbalimbali yatokeayo katika jamii, lakini hakuna utafiti

uliofanywa kuchunguza dhamira na sababu zinazowasukuma wasanii katika miaka

ya karibu kutunga na kuimba nyimbo za huzuni katika taarab. Kwasababu hiyo,

mtafiti wa kazi hii imechunguza nyimbo za huzuni zilizoimbwa na wasanii wateule

Fatma Issa na Shakila Said kwa azma ya kuzibaini sababu za kuibuka nyimbo za

huzuni katika jamii kinyume na lengo la asili la kuasisi taarab.

1.4 Wasifu wa Fatma Issa Juma

Fatma Issa Juma ni mwimbaji, mtia sauti na mshairi wa taarab asilia. Amezaliwa

Kianga Wilaya ya Magharibi „A‟mwezi wa Oktoba mwaka 1957. Fatma ni mtoto wa

pili kati ya watoto wanne wa mzee Issa Juma. Mtoto wa kwanza ni mvulana ambaye

anaitwa Juma Isa Juma aliyezaliwa mwaka 1954, akifuatiwa na ndugu zake

Mwajuma 1966, Pili Issa Juma na kitinda mimba Mwatima Issa Juma. Akiwa mtoto

wa miaka mitatu, Fatma pamoja na wazazi wake walihama Kianga na kuhamia mjini

4

katika mtaa wa Rahaleo. Mama yake Fatma anaitwa Ajuza na yeye pia alikuwa ni

mwimbaji wa taarab katika mwaka 1963 akiwa na kikundi kilichojulikana kwa jina la

African Social Light. Katika shughuli zake za uimbaji, Ajuza alikuwa akimchukuwa

mtoto wake Fatma tarabuni. Huko ndiko alikoanza Fatma kuathiriwa na uimbaji

akiwa na umri mdogo sana.

Kama ilivyo kawaida ya watoto wa Kiislamu, Fatma alipelekwa madrasa katika

mwaka 1962. Alipokuwa katika madrasa, alishriki kuimba kasida akiwa na umri

mdogo sana. Aliporudi chuoni (madrasa) Fatma alikuwa akizikariri na kuziimba

nyimbo ambazo alizisikia katika kikundi cha mama yake. Hapo ndipo mama yake

alipokigundua kipaji cha mtoto wake.Kipaji cha Fatma kiliimarishwa zaidi pale

Fatma alipokwenda katika shughuli ya mama yake mdogo.Huko kulikuwepo Taarab

ya Kidumbaki. Midundo ya Kidumbaki ilimwingia Fatma ndani ya moyo na bila

kujijua. Alianza kutoa vipande vya nyimbo ambazo alikuwa akizisikia katika

kikundi cha mama yake. Mbali na kukariri nyimbo za mama yake lakini pia aliweza

kutunga beti za nyimbo katika shughuli hiyo. Anakumbuka mila na desturi za

Waswahili pale inapotokezea yeye kuimba ubeti mzuri katika taarab baadhi ya wazee

humrushia mchele kama ni ishara ya kumpongeza au kutema mate chini kuonesha

ishara ya kumwondelea husda.

Fatma alisoma katika skuli ya msingi Kidutani (Agakhan). Baadaye alihamishwa

katika skuli ya Kidutani kubwa ambayo sasa inajulikana kama Taasisi ya Kiswahili

na Lugha za Kigeni na kumalizia katika skuli ya Haileselasie. Skuli zote hizo zipo

katika Mkoa wa Mjini Magharibi.

Fatma aliolewa mwaka 1971 na bwana Saaduni Makanjira, ni mwenyeji wa Pongwe

na Fuoni. Fatma aliolewa akiwa bado mwanafunzi wa darasa la kumi. Katika mwaka

5

1972 alijifungua mtoto wake wa mwanzo ambaye anaitwa Mrisho. Baadaye

aliachana na Saaduni na kukaa ujane. Katika kipindi cha ujane alibahatika kuzaa

watoto kumi, lakini waliobahatika kuwa hai ni watoto watatu tu ambao ni Hamdani

Abdallah aliyezaliwa mwaka 1976, Rahma mwaka 1980 na Afuwa mwaka 1982.

Kati ya watoto hawa ni Hamdani pekee ndiye aliyerithi kipaji cha mama yake lakini

yeye amejikita katika muziki wa rumba na anaishi huko Muscat, Oman.

Fatma kutokana na kupenda sana muziki wa taarab na kubanwa na harakati za ndoa,

aliacha kusoma na kujishughulisha na muziki wa taarab. Mnamo mwaka 1973 mama

yake Ajuza alimpeleka katika kikundi cha Culture Musical Club cha Zanzibar.

Mwaka 1976 aliacha rasmi shughuli za uimbaji na kushughulikia kulea watoto wake.

Katika mwaka 1977 Fatma alishindwa kujizuia kutoshiriki katika taarab, alirudi tena

katika uwanja wa taarab. Mwaka 1977 uliokuwa ndiyo mwaka iliyozaliwa

CCM.Yeye alipangiwa kuimba nyimbo ya chama kipya hiki. Hiyo ilikuwa ni nyimbo

yake ya mwanzo kumtoa ukumbini. Baadaye kikundi cha Culture kilisafiri nje ya

Zanzibar kwa muda wa miezi sita hivi yeye hakushirikishwa. Fatma ikambidi

kwenda kikundi cha taarab cha Kidongochekundu katika mwaka 1978. Katika

kikundi cha taarab Kidongochekundu huko alitunga nyimbo yeye mwenyewe na

kuimba nyimbo nyingine ambazo aliyojizolea umaarufu mkubwa. Nyimbo

iliyomkosha uso ilijulikana kwa jina la „Wali mtamu na Muhogo Vilevile‟ .

Katika mwaka 1985, Fatma alirudi tena Culture.Baada ya kurudi tena Culture

alipewa nyimbo kuimba jambo lilomfanya wasanii wenzake kumuonea gere. Baadhi

ya nyimbo alizopewa kuimba katika Cultureni kama; „Mbuzi‟, „Kiwe‟, „Maafa‟ na

kadhalika. Hasada na choyo cha wenzake kilikuwa kikubwa, kwasababu hiyo,

ilimfanya atunge wimbo mwenyewe kujitetea. Alitunga wimbo wake wa mwanzo

6

ndani ya Culture inaitwa „Bugudha sitaki‟. Baadaye akatunga „Haya Maumbile

Yangu‟ wimbo ambayo ilipata washabiki wengi sana hadi leo. Alikuwa na kawaida

Fatma ya kutunga wimbo kila baada ya mwaka. Mwaka uliofata akatunga wimbo

nyengine iitwayo „Kunionya Sikatai‟.Alipotunga wimbo huu munkari wa mahasimu

zake ukapungua. Baadaye akatunga nyimbo nyengine ziitwazo “Hivyo ndivyo ilivyo

Dunia”na“Fitina”. Kupitia nyimbo hizi, Fatma alizidi kung‟ara na kufahamika

katika kila pembe ya mji wa Zanzibar na Dar es Salaam.

Mnamo mwaka 1990, Fatma akajiunga na kikundi cha sanaa cha Jeshini akiwa

mkufunzi wa taarab, akiwafundisha waimbaji chipukizi kuimba. Mbali ya kuwa

mwalimu katika kikundi hicho pia aliweza kutunga nyimbo tatu ambazo ni Hasama,

Ewe Nuru Yangu na nyingine. Fatma hakudumu katika kikundi hiki kutokana na

mgogoro uliokuwepo wa wasanii kati ya Jeshi na wasanii raia. Kutokana na mgogoro

huo wasanii raia wote waliondolewa katika kikundi hicho.

Baadaye Fatma aliitwa na Maryam Hamdan na kumuomba ajiunge na kikundi cha

mumewe cha Twinkling Star. Katika kikundi hiki aliimba na kurikodi nyimbo ya

„Hachochoeki‟ na „Nimehifadhika‟. Fatma hakudumu katika kikundi hiki kwasababu

uongozi waCulture ulimtaka tena arudi katika kikundi na ndipo hapo aliporudi na

kuimba nyimbo nyingi ambazo nyingine hakutunga yeye.

Mnamo mwaka 1994, msanii John Komba alimtaka kujiunga na kikundi cha

TanzaniaOne Theatre (T.O.T) kwa lengo la kumsaidia katika shughuli za uimbaji na

utungaji. Baada ya muda mfupi zilianza tafrani na mashaka katika kikundi hicho.

Baada ya miezi mitano Fatma ikatokea bahati ya kwenda Ujerumani na wasanii

wenzake wa kikundi cha Culture. Akiwa safarini, Fatma alipokea barua ya kumtaka

awe mkufunzi wa kikundi kipya kilichoanzishwa na Wizara ya Habari Utamaduni na

7

Michezo ya Serikali ya Zanzibar. Alikubali na kukitumikia kikundi hicho cha Sanaa.

Kama anavyosema yeye mwenyewe Fatma, “sina bahati nimejawa na mikosi”. Baada

ya muda mfupi ndani ya kikundi hiki, zilianza fitina na majungu kupitia waimbaji

wenzake. Baada ya kutokea kwa sitofahamu hizo ndipo alipotunga nyimbo zifuatazo;

Tenda na wewe Usifiwe, Mtachoka Vyenu Visa, na Huniwezi. Nyimbo nyengine tatu

ni Kheri Adui Shetani Kama Adui Kiumbe, Nenda Utakako, Hukusingiziwa. Baadaye

alihamia katika kikundi cha JKU akiwa mkufunzi na huko nako aliimba wimbo wa

„Kwa Mola Hakuna Kubwa‟. Kama ilivyo imekuwa ada ya kuwa, akiwepo katika

kikundi chochote kile lazima fitina na majungu yatokee na ndipo hapo alipoachana

na kikundi hiki. Baadaye alijiunga na kikundi cha Chuo cha Mafunzo (Magereza) na

akaimba nyimbo ya „Sitojali Kuchukiwa‟. Wimbo mwingine ambayo anatarajia

kuizindua hivi karibuni inaitwa „Maskini wa Bahati Tajiri wa Mikosi.

Siku zote “Waridi huchanua waridi” ndiyo hivyo kilivyo kwa kipaji cha Fatma

kwani ni urithi kutoka kwa wazazi wake wote wawili. Mama yake alikuwa ni

mwimbaji katika kikundi cha (Afican Light). Katika maisha yake Fatma anavutiwa na

kuwashabikia sana waimbaji wawili ambao ni Sabah Salum na Rukia Ramadhan wa

Zanzibar.

8

Picha namba 1: Mwimbaji wa Taarab bibi Rukia Ramadhan akiimba katika moja ya

shughuli iliyofanyika katika ukumbi wa Ngome Kongwe, Zanzibar

(Chanzo: Utafiti, juni 8, 2016)

Chanzo: www.bing.com/images/search?q=images of rukia ramadhan

Nyimbo zote ambazo yeye Fatma alizitunga na kutia muziki mwenyewe ni miongoni

mwa masahibu yaliyomkuta mwenyewe katika maisha yake. Kwa sasa Fatma ana

matatizo ya miguu na anapoimba hukaa kitako kutokana na maradhi hayo. 1

1.4 Wasifu wa Shakila Said

Picha namba 2: Mwimbaji wa Taarab bibi Shakila Said akiwa jukwaani (Chanzo:

Utafiti, juni 13, 2016)

Chanzo: www.bing.com/images/search?q=images of shakila said

1 Mahojiano kati ya mtafiti na msanii nyumbani kuhusu maisha yake yamefanyika kwake Kwa

Alamsha, tarehe 22/ 11/ 2015

9

Kuzaliwa na Ukoo Wake

Mzee (2013) anadai kuwa Tatu ndilo jina lake alilopewa Shakila lakini kutokana na

mahojiano yetu na msanii huko nyumbani kwake Charambe Dar es Salaam tarehe

12/3/2016 anasema kuwa Shakila ndilo jina sahihi alilopewa na wazazi wake na siyo

Tatu kama ilivyobainishwa na Mzee. Shakila alizaliwa mwaka 1947 katika Kitongoji

cha Malindi, Kata ya Pangani Mashariki, Wilaya ya Pangani Mkoa wa Tanga. Baba

yake mzazi ni Said Hamisi Dobi, mkulima mwenye asili ya Kiomboi Singida katika

kabila la Wanyiramba. Mama mzazi wa Shakila aliitwa Khadija Mohammed

Chatungwi wa kabila la Mnguu kutoka Mkoa wa Morogoro. Shakila alikuwa ni

mtoto wa kwanza kwa mama yake na mtoto wa pili kwa baba yake. Alitanguliwa

kuzaliwa na dada yake, Fatma ambaye ni mtoto wa mke wa kwanza kwa Said huku

akifuatiwa na ndugu zake ambao ni Salimu, Bijuma, Kirimbati na Kitinda mimba

wao Zanana.

Kama ilivyo kawaida ya Waislamu wote, mtoto lazima asome madrasa. Wazazi wa

Shakila nao hawakuwa nyuma kufanikisha suala hili. Mnamo mwaka 1953 Shakila

alipelekwa madrasa ya mwalimu Awadhi, Pangani, Tanga kupata elimu ya Kur-ani.

Shakila alisoma kwa juhudi zake zote na kuhitimu juzuu zote thelathimi akiwa katika

umri mdogo. Madrasa ni kitovu cha elimu ya Uisilamu. Katika madrasa huadhimisha

kila mwaka uzawa wa Mtume (s.a.w). Katika hafla hizo Shakila alikuwa kinara wa

kughani kasida mbalimbali katika shughuli hizo na ndiyo sababu iliyomsaidia hadi

leo kughani mashairi yake katika maonesho tofauti. Alipofikia umri wa kuanza shule,

wazazi wake walimpeleka shule ili aweze kuelimika na kufuta ujinga. Mwaka 1956,

Shakila alianza kusoma elimu ya msingi katika shule ya msingi huko Kimba,

Pangani. Alipofika darasa la nne, Shakila aliacha kusoma na kuendelea madrasa na

mara alipohitimu, alifungua madrasa yake na kuwasomesha watu wazima.

10

Mwanadamu hupitia vipindi tofauti vya maisha hususan katika suala la ndoa. Hivyo,

ndivyo ilivyomtokea Shakila katika maisha yake ya ndoa kwani ameweza kuolewa

mara kadhaa na waume wanne tofauti katika nyakati tofauti. Kwa mujibu wa Mzee

(2013), Shakila aliolewa kwa mara ya kwanza akiwa katika umri mdogo ingawa

hakuweka bayana umri huo. Aliolewa mwaka 1960 na mume aitwaye Waziri Ayuob

ambaye alifanikiwa kupata naye mtoto mmoja wa kiume anayeitwa Waziri

aliyezaliwa mwaka 1963. Kwa vile mume huyu alikuwa chaguo la wazee wake na

siyo lake hakukaa naye sana na hatimaye aliachika.

Katika utamaduni wa Kiislamu, si vizuri sana na wala haipendezi mwanamke kukaa

ujane, Shakila aliolewa kwa mara ya pili na mume ambaye alimpenda na kumridhia

yeye mwenyewe. Mwaka 1968 aliolewa na Khatib Akida ambaye alikuwa mutribu

mwenzake wa taarab na ndiye aliyempa msukumo Shakila katika uimbaji wake.

Bwana huyu alizaa naye watoto wanne.Wa kwanza ni mvulana aitwaye Hamad 1969,

na wasichana watatu ambao ni Lucky alikufa 1972, Mwanahawa mwaka 1973 na

Maembe mwaka 1975. Kifo cha mumewe Akida kilipotokea ndicho

kilichowatenganisha.

Baada ya kukaa eda ya miezi minne na siku kumi Shakila aliolewa na mume wa tatu

aliyeitwa Kibwana Salehe Mkali. Aliishi naye kwa muda wa miaka minane. Bwana

huyu alizaa naye watoto watano ambao ni Hadija 1978, Bijaa 1980, Mape 1986,

Bachu 1988 na Mgeni 1990.

Baada ya kuachana na Mkali, Shakila aliolewa ma mume wa nne aliyeitwa Saaduni

Amiri ambaye alizaa naye mtoto mmoja aitwaye Shani 1993. Kati ya watoto 12

aliozaa Shakila, Mape pekee ndiye aliyerithi kipaji cha kuimba. Aliimbia Dar

11

Modern Taarabna sasa amehama katika kikundi hicho na wanajitegemea yeye na

mama yake. Shakila hivi sasa hana mume baada ya kuachana na mumewe Saaduni.

Nyota njema huonekana asubuhi na ndivyo hivyo ilivyojidhihirisha kwa kipaji cha

Shakila. Alianza kupenda kuimba kupitia michezo mbalimbali ambayo wakiicheza

na watoto wenziwe utotoni. Lakini kipaji hiki kiligundulika rasmi kwake Shakila

alipokuwa darasa la tatu mwaka 1958 wakati alipochaguliwa na walimu wake

kumburudisha hayati Mwalimu J. K. Nyerere, aliyekuwa mwasisi wa TANU na Rais

wa kwanza wa Tanganyika na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipotembelea

Wilaya ya Pangani mwaka 1958. Katika tukio hilo, Shakila alionesha kipaji chake

mbele ya viongozi na watu waliohudhuria kwa kuimba bila ya haya katika ngoma

iitwayo Msanja.Umahiri wa Shakila uliwapagaisha watazamaji na kutojizuia katika

sehemu walizokaa huku nderemo na vifijo vikitawala katika ukumbi hii ilitokana na

mvuto wa sauti yake pamoja na ustadi wake wa kucheza (Mzee, 2013).

Kila mwimbaji huwa na mtu au mutribu ambaye humvutia na kumuathiri ndani ya

moyo wake. Shakila alivutiwa sana na uimbaji na sauti nzuri ya marehemu Ummu

Kulthum wa Misri (1904- 1975) na marehemu Siti binti Saad (1888-1950), mwimbaji

wa zamani wa taarab asilia Zanzibar.

Picha namba 3: Mwimbaji wa zamani wa Taarab asilia Marehemu bibi Siti binti

Saad akiwa katika shughuli ya kutoa burudani (Chanzo: Utafiti,

juni 8, 2016)

Chanzo: www.bing.com/images/search?q=images of siti bint saad

12

Picha namba 4: Mwimbaji wa zamani wa nyimbo za Kiarabu bibi

Ummukulthoum (Chanzo: Utafiti, juni 13, 2016)

Chanzo: www.bing.com/images/search?q=images of ummukulthoum

Mnamo mwaka 1961Shakila alijiunga na kikundi cha kwanza cha taarab kilichoitwa

Black Star. Katika kikundi hiki Shakila alikuwa mwimbaji na mtunzi, mumewe

Khatib Akida mume wa pili akiwa mpigaji wa tashkota. Katika kikundi hiki Shakila

aliimba nyimbo nyingi na kutokana na ustadi wake wa kuimba na alijikumbia sifa

kemkem kutokana na sauti yake nyororo anapoghani. Alivuma zaidi pale nyimbo

zake na zile alizoshirikishwa zilipoanza kurekodiwa katika Redio Tanzania Dar es

Salaam (RTD). Baadhi ya nyimbo hizo ni Mpenzi Amini (1962), Pilipili Usoila

Yakuwashiani? (1962), Majuto Yamenipata Kukosana na Mpenzi (1963), Kitumbili

Namba Moja na Kitumbili Namba Mbili (1965).

Nyimbo nyengine ni Hujui Alacho Kuku (1968), Jongoo Wacha Makuu (1969), na

Akukataye Hakwambii Toka (1969), Mapenzi ni Kama Donda. Kikundi hiki

kilijizolea umaarufu siku hadi siku na hivyo kukodiwa katika harusi na sherehe

mbalimbali za kiserikali na binafsi. Baadaye kikundi hiki kiligawanyika kutokana na

matatizo ya uongozi katika matumizi ya fedha.

13

Mnamo mwaka 1970, kilianzishwa kikundi kingine cha Taarab kilichoitwa Lucky

Star maarufu kama Nyota Njema. Makao makuu ya kikundi hiki yalikuwa barabara

ya 13 mjini Tanga. Shakila na mumewe pamoja na watribu wengine kutoka Black

Star wakajiunga katika kikundi hiki. Kutokana na mialiko mbalimbali hasa ya nje

Shakila aliweza kupata umaarufu zaidi kutokana na kipaji chake cha kuimba.

Kwa mujibu wa Mzee (2013), Shakila alikuwa ni mwimbaji mkuu katika kikundi cha

Lucky Star. Nyimbo zake zilipendwa sana kutokana na maudhui yake na pia

zinaburudisha kutokana na uzuri wa sauti yake. Baadhi ya nyimbo alizotungwa na

kushirikishwa akiwa katika kikundi cha Lucky Star ni Sina Tabasamu (1971), Hali

ya Masikitiko (1971), Mapenzi Yamepungua (1972), La Mateso Penzi (1972),

Mapenzi Yako ni Chumo (1972) na Chumo Jema ni Ibada (1972). Nyimbo nyengine

ni Karibu Mwenge Karibu (1973), Ninauliza Wenzangu Nini Dawa ya Mapenzi

(1974), Wachuma Mali Huli Yakuhadaa Dunia (1974), Mapenzi Yanacheka (1975),

na Viva Frelimo (1975). Alidumu katika kikundi hiki mpaka alipofiwa na mumewe

Akida.

Kutokana na suala la kuimba kuwa limo ndani ya damu yake, Shakila hakutaka

kuacha muziki wa taarab. Katika mahojiano na mtafiti nyumbani kwake Shakila

amebainisha kuwa amejiunga na JKT mwaka 1980 na kutumikia Jeshi hilo kwa muda

wa miaka thelathini, kinyume na maelezo ya Mzee (2013) na kwamba Shakila

alijiunga na JKT mwaka 2001akiwa mwalimu katika kikundi hicho namwimbaji.

Makao makuu ya kikundi hiki yapo Mgulani Dar es Salaam. Katika kikundi hiki

Shakila alizidi kung‟ara ndani na nje ya Afrika Mashariki na aliendelea kutunga,

kuimba na kuwafundisha waimbaji chipukizi nyimbo mbalimbali. Baadhi ya nyimbo

hizo alizotunga ni kama Baba Musa Tulizana (1986), Kiyanga Yanga (2002),

14

Kitanda (2003), Mzigo (2005), Kobe Nakutuma (2008), Uliza Kwanza (2012),

Usishindane na Fupa (2012)na Naita Tanga.

Kwa mujibu wa Shakila katika mahojiano yetu ya (tarehe 12. 3. 2016) huko

nyumbani kwake Charambe amesema kuwa, ametunga na kuimba nyimbo nyingi

ambazo pia ametia muziki mwenyewe. Baadhi ya nyimbo hizo ni kama vile Naita

Tanga ambayo ameiimba kwa lugha ya Kizigua, Mzigo, Mapenzi Yamepungua,

Mapenzi ni Kama Donda, Kobe Kamwambie Mwewe na kadhalika. Sababu

iliyompelekea kutunga nyimbo hizo ni matatizo ya kimapenzi ambayo yamemkuta

yeye mwenyewe katika maisha yake.

Kutokana na juhudi za Shakila katika uimbaji na utunzi, kila kikundi alichojiunga

alikifanya kipate umaarufu mkubwa. Hivyo, aliweza kupata mialiko mbali mbali ya

binafsi na ya kiserikali. Katika mialiko hiyo alifanya maonesho katika nchi za Ufini,

Misri, Swiden, Ujerumani, Ufaransa na Denmark.

“Chanda chema huvikwa pete”, huu ni usemi maarufu uliozoeleka kutumika katika

jamii ya Waswahili. Mara nyingi mtu akifanya vizuri hupewa zawadi ambayo

aghlabu hataisahau katika maisha yake. Hivyo ndivyo ilivyo kwa Shakila kwani

kupitia tasnia ya muziki wa taarab amejizolea tuzo tofauti tofauti. Baadhi ya tuzo

hizo ni tuzo ya Zeze ya mwaka 2000, iliyotolewa na Mfuko wa Utamaduni Tanzania

(Tanzania Cultural Fund). Tuzo nyingine alizopata ni ile2 ya mwimbaji mkongwe wa

Taarab kupitia Tuzo za Muziki za Kilimanjaro (Kilimanjaro Tanzania Music Award).

Shakila amestaafu kuimba Taarab mwaka 2009, na hivi sasa ni Mwenyekiti wa

Chama cha Waimbaji wa Taarab Tanzania (Mzee: 2013).

2 Mahojiano kati ya mtafiti na msanii nyumbani kwake Charambe, Dar-es-Salaam, tarehe 12/ 3/ 2016

(Shakila Said alifariki tarehe 19/08/2016, saa tatu usiku Hospitali ya Temeke)

15

1.5 Malengo ya Utafiti

1.5.1 Lengo Kuu

Utafiti huu ulilenga kuchunguza dhamira za nyimbo za huzuni katika taarab.

1.5.2 Malengo Mahsusi

a) Kubainisha baadhi ya nyimbo za huzuni za waimbaji wateule.

b) Kubainisha sababu zilizopelekea kutungwa kwa nyimbo hizo, na;

c) Kutathmini jamii ilivyopokea dhamira na athari za nyimbo hizo.

1.6 Maswali ya Utafiti

Utafiti huu uliongozwa na maswali yafuatayo:

a) Ni zipi nyimbo za huzuni za Bi Fatma Issa na Shakila Said?

b) Ni sababu gani mahasusi zilizopelekea kutungwa kwa nyimbo hizo?

c) Jamii imezipokeaje dhamira na athari za nyimbo za huzuni za waimbaji hao?

1.7 Manufaa ya Utafiti

Tasnifu hii imekuwa chachu ya kuwawezesha wasomaji kujua dhamira na sababu ya

kutungwa kwa nyimbo zenye za taarab zenye maudhui ya huzuni katika jamii. Pia,

utafiti huu umeuwezesha jamii kugundua nafasi na mchango wa nyimbo za huzuni

katika jamii. Aidha, umesaidia kuondosha dhana kuwa nyimbo hizo za taarab ni za

furaha na ramsa tu na sivyo vyenginevyo.

1.8 Nadharia ya Utafiti

Utafiti huu umeongozwa na nadharia ya uhalisia. Hivyo, ukusanyaji wa data,

uchambuzi na uwasilishaji wa data hizo uliongozwa na nadharia hiyo. Nadharia hii

ilizuka baada ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia baada ya watu wengi kuathirika na

madhara ya vita hivi. Athari hizo ni kama vile umasikini, njaa, vifo, mporomoko wa

16

uchumi na kadhalika. Nadharia hii iliasisiwa na mwanafalsafa Hegel katika miaka ya

1980 ya karne ya ishirini. Nadharia hii imeweza kuhusishwa na kazi ya kifasihi za

Kiswahili, na imebainisha misingi mikuu miwili ambayo inaweza kutumika katika

kuongoza uatafiti huu. Misingi hiyo ni;

a) Msingi wa kimhakati. Huu ni msingi ambao unaeleza matukio kama

yalivyo katika maisha ya kila siku bila ya kubadilisha kitu hata kimoja.

b) Msingi wa ushabihi ukweli. Huu ni msingi ambao unakaribia kueleza

matukio kama yalivyo bila ya kuongeza au kupunguza.

Kwa vile nadharia hii imeelezea matukio kama yalivyo katika jamii, nyimbo za

huzuni ni mojawapo ya kazi ambazo zinaakisi hali halisi inayoikumba jamii kila

siku. Huzuni ni sehemu ya matukio ambayo humtokea kila mtu katika maisha ya kila

siku. Hakuna mtu anayeweza kukwepa si masikini si tajiri. Nadharia hii imesaidia

kubainisha jinsi gani wasikilizaji na watazamaji kuweza kuguswa na nyimbo hizo

ambazo zinabeba maudhui ya huzuni. Aidha, imesaidia kutambua sababu

zinazowasukuma wasanii kutunga mashairi yenye huzuni na masikitiko katika jamii

zao. Kwa vile hali ya huzuni huwasonenesha wanajamii kwa kiasi kikubwa katika

jamii, nadharia hii ya uhalisia imeongoza na kuufanikisha utafiti huu kwa muda

muafaka.

1.9 Hitimisho

Katika sura hii ya kwanza utafiti umeangalia utangulizi, usuli wa tatizo, tamko la

utafiti, wasifu wa wasanii teule ambao ni Shakila na Fatma, malengo ya utafiti,

maswali ya utafiti na manufaa ya utafiti. Aidha, sura hii ilifafanua nadharia

iliyotumika katika utafiti huu ambayo niNadharia ya Uhalisia na misyake mikuuni

msingi wa kimhakati na ushabihi ukweli. Sura inayofuata itazungumzia mapitio ya

maandiko.

17

SURA YA PILI

MAPITIO YA MAANDIKO

2.1 Utangulizi

Sura hii imefafanua maandiko mbalimbali yanayohusiana na mada hii. Maandiko

hayo yamegawika katika sehemu kuu tatu. Kwanza ni maandiko yanayohusiana na

chimbuko la taarab. Pili, maandiko ya tafiti mbalimbali yanayohusina na taarab na

hatimaye makala mbalimbali zinazohusiana na taarab.

2.2 Chimbuko la Taarab Zanzibar

Kila jambo au kitu ambacho hutokea katika ulimwengu huu huwa na asili na chanzo

katika kuibuka kwake. Waandishi wengi wameandika vitabu, majarida na makala

kuelezea chimbuko, historia na maendeleo ya taarab Zanzibar. Kati ya hao ni Khatib

(2014), Mgana (1991) na kadhalika. Khatib (2014) katika Taarab Zanzibar, anaeleza

juu ya asili na vipindi mbalimbali vilivyopitia Taarab huko Zanzibar kama vile

kipindi cha ukoloni na ubepari na hadi baada ya Mapinduzi. Pia anaendelea kuelezea

kuwa lengo la Taarab la asili ni kuliwaza, kubembeleza, kukumbusha, kumithilisha,

kufurahisha na kupoza moyo. Lengo lingine ni, kusuuza nyoyo za watu waliojinamia

kwa huzuni na masaibu mbalimbali yanayowafika wanadamu.

Inaaminika kuwa taarab Zanzibar ilianza katika kipindi cha Sultan Seyyid Barghash

(1870-1888) (Khatib 2014, Mgana 1991). Mfalme huyu inasemekana alikuwa ni mtu

mwenye kupenda starehe na anasa, hivyo muziki wa taarab ukawa unapigwa katika

kasri yake ya Beit-el-Ajaib. Mapema Sultan Seyyid Barghash (1870- 1888) aliagiza

watu waliokuwa wajuzi kutoka Misri kuja kumpigia muziki huo. Baadaye alimpeleka

mtu maalum huko Misri aliyeitwa Muhammed Ibrahim, ili apate kufundishwa stadi

hii ya muziki wa taarab (Khatib: 2014-1-2). Aliporudi mutribu huyu Misri alikuwa

18

tayari ameshajua kuimba na kutambua kuzitumia ala za taarab. Inaaminika nyimbo

za taarab wakati huo zilikuwa za Kiarab kitupu.Kikundi maalum cha taarab ya Sultan

kikaanzishwa. Sanaa hii ilieendelea kumstarehesha Sultan na aila yake hata baada ya

kifo cha Seyyid Barghash. Alipoingia katika utawala naye sultan Khalifa bin Haroub

(1911-1960), aliidumisha na kuipalilia sanaa hii ya taarab kwa lengo la

kumstarehesha yeye mwenyewe kwa kumwondolea mawazo na machofu ambayo

yamkabili katika mwili, akili na moyo wake.

Picha namba 5: Mtawala wa Zanzibar Sultan Seyyid Barghash (1870-1888)

(Chanzo: Utafiti, juni 14, 2016)

Chanzo: www.bing.com/images/search?q=images of seyyid barghash

Hivyo, taarab ilikua na kuendelea hata baada ya kuondoka kwa mifumo ya kisultani

kiutawala.Vikundi vya watu binafsi vilianzishwa mapema sana. Vikundi vya

mwanzo ambavyo vilioanzishwa ni pamoja na; Naad Akhwan Safaa mwaka 1905,

Mwaka 1908 ilifatiwa na Naad Shuub1910 (Khatib: 2014). Vikundi vyengine

vilianzishwa mwaka 1945 Royal Air Force, 1945 Nuru- l-Uyunn, 1945 Sahib el Ari,

1945 Navy, 1945 Banati,1955 Michenzani 1957 Miembeni 1964 Kwa Alamsha 1964

Culture1964 1985 Wardah el Baidha 1986 Mila na Utamaduni 1986 Polisi 1986

19

Jeshi 1989 Ilyas& The Twinkling Star na mwaka 1989 Bwawani Musical Club.

(IssaMgana: 1991). Taarab ya vikundi vyote hivyo vilifata mtindo wa taarab asilia.

Baadaye vikundi vifuatavyo vikafata mtindo wa taarab ya kisasa vikiwemo East

Afican Melody; Tanzania One Theater (TOT); Zanzibar Stars, Dar-es-Salaam

Modern Taarab na vyenginevyo. Kadri siku zilivyoendelea kusonga mbele, muziki

wa taarab uliweza kupokea mabadiliko makubwa katika utumiaji wake wa vyombo

vyake vya asili na hata kucheza katika majukwaa. Hali hii ilichangiwa sana na suala

usasa wa matumizi ya vyombo vya elektroniki vitumiavyo umeme kuanza kutumika.

Vifaa ambavyo vikitumika katika muziki wa taarab wa asili kama vile Udi, Violin,

Dumbaki na Dafu vimeanza kuachwa. Wapo wanaoamini kuwa uasili wa taarab

asilia na utamu wake umeanza kupotea. Sababu kuu ni mabadiliko ya vyombo na

kuingiza uchezaji jukwaani. Sanaa ya Taarab kama zilivyo sanaa nyingine huenda na

wakati na pia huvuka mipaka na kuenea sehemu nyingi (Khatib, 2014).

2.3 Maandiko Yahusuyo Taarab

Muziki wa Taarab kwa kiasi kikubwa umeweza kuenea kwa kasi sana kutokana na

mahadhi na mashairi yake kuwakonga na kuwasuuza mioyo ya walio wengi. Wapo

wataalamu wengi sana ambao wametoa mchango wa kitaaluma ikiwemo katika suala

hili ikiwemo kuweza kupembua ni kwa jinsi gani muziki huo wa taarab unaweza

kuleta tija kwa wanajamii. Yapo maandiko mengi ya kiutafiti na makala yaliyojadili

taarab katika mielekeo tofauti. Wapo watafiti ambao wamezungumzia kuhusiana na

kipengele cha maudhui ya taarab lakini wametofautiana kwa kiasi katika tafiti hizo

zao.

20

Alawiy (2007) alifanya utafiti wake juu ya“Nyimbo za mafumbo za taarab

zinavyochangiakudumisha maadili ya jamii ya Wazanzibari”. Katika utafiti wake huo

alieleza kuwa nyimbo za taarab zimechangia sana katika kuendeleza na kukuza

maadili ya Wazanzibari. Pia alielezea kuwa asilimia kubwa ya nyimbo za taarab

zinalinda mila na desturi pamoja na heshima ya jamii, akihusisha utamaduni wa

Wazanzibar ambao hutumia lugha yenye staha na stara.

Saleh (1980) alifanya utafiti juu ya “Maudhui ya nyimbo za taarab za Unguja”. Yeye

alibaini kuwa lugha ndiyo kipengele muhimu kinachosaidia jamii kupata maudhui

hayo kwa urahisi zaidi. Saleh kwa upande wa fani anaeleza kuwa baadhi ya nyimbo

za taarab hutumia lugha nzito yenye mafumbo ndani yake ambayo si rahisi kwa

mtazamaji na msikilizaji kuupata ujumbe uliokusudiwa kwa haraka.

Mtafiti mwengine aliyeshughulikia nyimbo za Taarab ni Thabit (2007) ambaye

alitafiti juu ya “Nyimbo za taarab katika jamii ya Zanzibar”. Matokeo ya utafiti

wake yanaonesha kwamba maudhui ya nyimbo za taarab yana umuhimu katika

kusaidia kujenga malezi na maadili mema katika jamii ya Wazanzibar.

Alhabib (2012) katika utafiti wake wa matumizi ya “lugha katika nyimbo za taarab”

anabainisha kwamba lugha ya nyimbo za taarab imejaa mafumbo, sitiari, ishara,

taswira na picha na hivyo kuwa kivutio kwa wasikilizaji wake.

Broughton na wenzake (2000) kama alivyonukuliwa na Khamis (2012:20) wanadai

kwamba, kimaudhui, nyimbo za taarab zinalenga ziadi kwenye mapenzi. Nyimbo

hizi hutumia fani ya mafumbo na sitiari zaidi ambazo huwafanya watu waso na

uelewa na ujuzi wa sanaa hii kutoelewa maudhui ya nyimbo hizo. Hata hivyo,

21

wameona kuwa kuna baadhi ya nyimbo za siasa ambazo zinaeleweka kwa vile

hazitumii mafumbo.

Katika mwelekeo wa fani katika taarab, mengi yamefanyiwa utafiti.

Mzee (2013) amefanya utafiti kuhusu “Maudhui katika Nyimbo za Taarab za Bi.

Shakila” Kwake yeye alihusisha na fani ameona kwamba matumizi ya lugha yana

mchango mkubwa katika kuibua dhamira mbali mbali. Hivyo nyimbo hizo hutumia

vipengele mbali mbali vikiwemo vya tamathali za semi, methali na mafumbo ili

kuweza kufikisha ujumbe uliokusudiwa kwa hadhira. Mzee anaendelea kwa

kubainisha kuwa vipengele vya lugha vinaweza kuficha lugha ya karaha na matusi

katika kufikisha maudhui hayo. Hivyo, vinaweza kuadilisha, kuionya na kuikosoa

jamii bila ya kuleta mfarakano miongoni mwa jamii. Aidha kuhusu maudhui

(dhamira) yaliyomo katika nyimbo za Bi Shakila kwake yeye anaona kuwa

yanasawiri hali halisi ya maisha yaliyopo katika jamii.

Naye Hamisi (2012) alifanya utafiti juu ya “Matumizi ya Taswira na Mafumbo

katika Nyimbo za Mapenzi na Taarab Asilia.” Anaeleza kwamba taarab, hasa ile

asilia imedhamiriwa kuadilisha jamii. Katika kufanikisha suala hilo, wasanii

hutumia lugha yenye staha na ile aliyojengwa kwa namna inayobeba na

kuzungumzia masuala mazito badala ya kutumia lugha ya wazi isiyoficha hata yale

yasiyotakiwa kutamkwa na au kusikika hadharani. Yeye anaona kuwa yapo maneno

ambayo kwa mujibu wa mila na desturi za jamii ya Waswahili hayapaswi kutamkwa

wazi wazi. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kufanya hivyo ni sawa na kubomoa

badala ya kujenga maadili ya jamii.

22

Watafiti wengine wamejadili taarab na maendeleo yake katika mwelekeo tofauti ya

kifani na maudhui. Mbali ya wataalamu hawa kuhusisha taarab na dhima yake ya

kimaudhui na kifani, wengine wameangalia katika njanja tofauti.

Mzee (2011) alifanyia utafiti juu ya “Nyimbo za taarab asilia za Zanzibar”, katika

uchunguzi wake amezungumzia jinsi taarab zinavyokuwa na zinavyoendeshwa

katika harakati mbalimbali za maisha zikiwemo sherehe za harusi, matamasha,

kwenye shughuli za kisiasa na hata za biashara. Pia alielezea jinsi ya taarab asilia

inavyolinda utamaduni wa Mswahili.

Farhan (1992:4) amefanya utafiti juu ya “Historia ya nyimbo za taarab”. Yeye

ameeleza kuwa wakati wa kipindi cha miaka ya arubaini mpaka sitini nyimbo za

taarab zaidi zilikuwa zinazungumzia maswali ya mapenzi. Lakini kadri miaka

ilivyosonga mbele maudhui ya mapenzi yanabadilika kulingana na mabadiliko ya

jamii.

Ndungo na Wafula (1993) katika makala yao wamezungumzia kuhusiana na chanzo

na maendeleo ya taarab katika jamii ya Waswahili. Kwa ufupi sana wameeleza

muundo wa taarab ulivyokuwa.

Igobwa (2007) katika makala yake ya “Taarab na Chakacha”anadai kwamba taarab

inachukuliwa kama shughuli ya kijamii. Igobwa akimnukuu Ntarangwi (2003:149)

anaelezakuwa muziki wa taarab huwa unapigwa kwenye harusi za Waswahili kwa

kuwafurahisha waliokusanyika huku ukitumia mashairi ya Kiswahili yenye mvuto.

Anaeleza kuwa nyimbo hizi huwa zinatungwa upya katika onesho kutokana na

mchango wa wasikilizaji.

23

Khatib (1982) katika makala yake ya, Tarabu ni fasihi simulizi?, ameona kuwa

tarabu ni muziki wenye kupigwa na kuchanganywa na nyimbo ambao utaweza

kukidhi vitabia vya sanaa ya fasihi simulizi. Anaendelea kufafanua kuwa vitabia

hivyo vya taarabu na vile vya kazi nyengine ya fasihi simulizi kadiri vinavyoachana

au kukaribiana. Pia amehitimisha kwa kueleza kuwa tarabu asilia ina utendaji wenye

mipaka na ufinyu ukilinganisha na utendaji wa tanzu zingine za fasihi simulizi.

Zeid (2016), amebainisha kuwa taarabu asilia ni tarabu ambayo ina heshima na

inajali utu wa mtu kwani mtu anaposimama juu ya jukwaa huwa anajiheshimu na

kutulia na kuimba kwa staha zaidi na vile vile hutumia lugha ya mafumbo ambayo

inataka ujuzi kufumbua fumbo lilokusudiwa. Kuhusu tarabu ya sasa ni tarabu

ambayo inajali maslahi mtu tu nasi vyenginevyo. Mawazo yake yanashabihiana na

yale ya Shakila ambapo amesema kuwa “Waimbaji wa sasa wanaimba kwa lengo la

kujipatia kipato fulani na wala haina lengo la kuwaburudisha jamii nzima”.3

Imebainika kuwa watafiti wengi wamefanya tafiti zao katika maeneo tofauti

kuhusiana na suala zima la taarab. Wamegusia chimbuko la taarab asilia na mipasho,

maudhui, fani na maeneo mengine. Hata hivyo kazi zote hizo hazijajikita kuongelea

taarab na kuwa kiasili, katika chimbuko lake, ni muziki wa raha na ramsa. Na

kwamba sasa dhana ya kuongelea huzuni na simanzi sio ngeni na ni sehemu ya

mabadiliko katika tasnia hii. Katika muktadha huu hakuna aliyejadili juu ya taarab

imegeuka kuwemo dhamira za huzuni. Utafiti huu umeliziba pengo hilo.

3 Mazungumzo ya mtafiti na Shakila Charambe, tarehe 12/ 3/ 2016

24

2.4 Pengo la utafiti

Kulikuwepo na pengo kubwa katika dhamira za nyimbo za taarab asilia na za mtindo

wa kisasa na kuamini kuwa taarab kidhamira ni za furaha, bashasha na vicheko. Hata

lengo la kuanzishwa muziki huu ulikuwa ni kutoa maudhui yanayobebwa na muziki

wa furaha tu. Hakuna kazi ya utafiti iliyatanabahisha hilo. Utafiti huu umetoa

muelekeo mpya.

2.5 Hitimisho

Katika sura hii mjadala ulijikita katika maandiko mbalimbali yanayolandana na

malengo ya utafiti huu. Utafiti huu uliangalia maandiko yenye maana taarab na

chimbuko lake. Aidha, maandiko yaliangaliwa na mabadiliko ya kidhamira kutoka

mtazamo wa kiasili kuiona taarab ni muziki wa furaha na kuwa sasa muziki wa

majonzi, simanzi na huzuni. Sura inayofuata itazungumzia usanifu na mbinu za

kukusanyia data.

25

SURA YA TATU

USANIFU NA MBINU ZA KUKUSANYIA DATA

3.1 Utangulizi

Sura ya tatu imefafanua mpango wa jumla wa utafiti huu, mbinu zilizotumika

kukusanyia data na zana na vifaa vya utafiti vilivyotumiwa. Utafiti umebainisha

jamii ya watafitiwa, eneo la utafiti, mchakato mzima wa ukusanyaji ulivyokwenda

uchambuzi wa data, ikiwemo uhalali wake na uthabiti wa matokeo ya utafiti.

3.2 Mpango wa utafiti

Utafiti huu mchakato wake ni wa kitaamuli kwa vile ulionekana kuwa ni bora zaidi

na ulitumia njia ya maelezo katika uchambuzi wa data. Utafiti ulifanyika uwandani

na maktabani. Mtafiti alitumia njia ya uwandani zaidi kuliko maktabani kutokana na

uhalisia wa utafiti wenyewe. Hii ni kwasababu wahojiwa walikuwa wametawanyika

sehemu mbalimbali kama vile mitaani, katika vituo vya redioni na mashuleni. Utafiti

huu pia uliongozwa na nadharia ya uhalisia ambayo ililingana na matakwa ya utafiti

huu.

3.3 Eneo la utafiti

Utafiti huu ulifanyika katika kisiwa cha Unguja katika Wilaya ya Mjini na viunga

vyake. Maeneo haya yaliteuliwa kwa kuangalia vigezo thabiti ambavyo upatikanaji

wa data ulikuwa ni rahisi. Eneo la mji wa Unguja ni sehemu yenye wadau na

wapenzi wa muziki wa taarab ambao kwa kiasi kikubwa wanafuatilia kwa karibu

sana nyimbo za Shakila na Fatma.

3.4 Walengwa wa Utafiti

Walengwa wa utafiti huu waligawanyika katika maeneo makuu mawili ambayo

ndiyo yenye jamii ya watafitiwa na sampuli ya utafiti.

26

3.4.1 Jamii ya Watafitiwa

Walengwa wa utafiti huu walikuwa ni wapenzi wa nyimbo za taarab za Shakila na

Fatma wengine ni waendeshaji wa vipindi vya taarab vya redio, waimbaji wa nyimbo

zenyewe ambao walishirikishwa. Hata watafiti wa kazi za taarab walihusishwa.

Mgawanyiko wa makundi ulikuwa kama ufuatao;

a) Wapenzi mbalimbali wa tasnia ya taarab asilia hasa wa nyimbo za Shakila na

Fatma;

b) Watangazaji wa redio wa nyimbo za taarab asilia,

c) Wasanii wateule wa muziki wa taarab ambao ni Shakila na Fatma.

d) Wanafunzi walioshughulikia na taarab asilia katika tafiti zao.

3.4.2 Usampulishaji na Sampuli Iliyotumika

Kwa mujibu wa Kothari (2003), sampuli nzuri ni ile iliyo ndogo, jumui na

itakayomuwezesha mtafiti kuidhibiti. Kombo (2006) anaona: “Kusampulisha ni

mchakato wa kuchagua idadi ya wawakilishi wenye tabia sawa na walengwa wa

utafiti”. Kutokana na mawazo ya wataalamu hao, kwa hivyo sampuli hii

imeyazingatia hayo na iliteua na kuchagua wawakilishi ambao walitumika katika

kazi husika. Hivyo, kwa utafiti huu, sampuli ilichaguliwa kwa kuzingatia mbinu ya

usampulishaji lengwa ili kupata uwakilishi halisi. Makundi ya sampuli halisi

yalikuwa kama hivi ifuatavyo;

a) Washabiki kumi wa tasnia ya muziki wa taarab asilia.

b) Watangazaji watano wa muziki wa taarab;

c) Wanataaluma kumi na tano waliofanya tafiti za taarab;

d) Wasanii wawili teule ambao ni Shakila na Fatma.

27

3.5 Ukusanyaji wa Data

Kipengele hiki kinaelezea njia na zana mbalimbali ambazo zimetumika katika

ukusanyaji wa data.

3.5.1 Njia za ukusanyaji wa data

Mtafiti alitumia data za awali kupitia njia ya usaili, ushuhudiaji na udodosaji. Mbinu

hizi zilifanya utafiti huu kuwa halisi zaidi kwani mtafiti alipata kushiriki kikamilifu

katika maonesho kadhaa ya taarab. Pia mtafiti alipata muda wa kuona CD na

kusikiliza nyimbo za waimbaji wateule.

3.5.2 Usaili

Mtafiti alitumia mbinu ya usaili kwa washabiki na wapenzi wa muziki wa taarab

hususan nyimbo za Shakila na Fatma na hata kwa watangazaji wa vipindi vya taarab

asilia katika redio. Mtafiti alitumia njia hii ili kupata taarifa hata kwa wale wote

ambao hawajui kusoma na kuandika. Kwa upande wa watangazaji wa redio mbinu

hii ilimsaidia mtafiti kubadilishana mawazo nao ana kwa ana ili kupata taarifa za

undani na maoni yao kuhusiana na taarab asilia.

3.5.3 Dodoso

Mtafiti alitumia dodoso wakati wa kukusanyia data. Dodoso zilitumika kwa wale

wenye uwezo wa kusoma na kuandika. Mbinu hii ilitumika kuwahoji wanafunzi

ambao wamefanya tafiti zao kuhusiana na taarab asilia ili kupata maoni na mawazo

yao kuhusu utafiti huu.

3.5.4 Ushuhudiaji

Mtafiti alitumia mbinu hii kwa kushiriki baadhi ya maonesho ambayo yalitendeka

katika majukwaa mbalimbali ili kuona jinsi gani nyimbo hizo zinavyoathiri au kuteka

nyoyo za watu.

28

3.6 Zana za kukusanyia data

Mtafiti atatumia zana tofauti ili kukamilisha utafiti. Zana hizo ni pamoja na;

3.6.1 Kamera

Kamera ilitumiwa na mtafiti kupiga picha sehemu ambazo zitaonesha waimbaji na

pale waimbaji wakiwa jukwaani. Pia ilitumika picha kupiga nao waimbaji hawa

wateule na makundi mengine ya watafitiwa.

3.6.2 Simu

Mtafiti alitumia simu kwa ajili ya mawasiliano na ukusanyaji wa data na pia kwa ajili

ya kurekodi na kupiga picha.

3.6.3 Daftari na kalamu

Mtafiti alitumia daftari na kalamu katika ukusanyaji wa data ili kuandika taarifa

muhimu zinazohusiana na utafiti na kutunza kumbukumbu muhimu kutoka kwa

wasailiwa.

3.6.4 Ngamizi

Mtafiti alitumia ngamizi katika kuchapa na kuangalia baadhi ya taarifa katika tovoti

mbali mbali.

3.7 Mchakato wa Ukusanyaji Data na Uthabiti wake

Utafiti huu ulifuata taratibu sahihi zipasazo kufuatwa na mtafiti. Mtafiti aliomba

ridhaa kwa uongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma pamoja na kupata kibali katika

Ofisi ya Makamu wa Pili wa Raisi wa Zanzibar ambaye ndiye mtoa kibali kisheria

kwa upande wa Tanzania Zanzibar ili kupata uhalali wa kuingia sehemu mbalimbali

kukusanya data. Aidha, tahadhari ilichukuliwa katika kuhakikisha kuwa taarifa zote

zinazotoka kwa wahojiwa zimekuwa siri. Data za uwandani zimekusanywa kwa njia

29

ya usaili, dodoso na ushuhudiaji. Mwongozo wa usaili utatumika kuwahoji wasanii

teule pamoja na wadau wa muziki wa taarab. Pia, walihojiwa wataalamu wa fasihi

hususan wa fasihi simulizi kwa njia ya ushuhudiaji. Mtafiti pia alitembelea maonesho

mbalimbali ya taarab na kuangalia na kusikiliza CD za nyimbo za waimbaji wateule.

3.8 Mipaka ya Utafiti

Utafiti huu ulijikita zaidi katika kuchunguza namna ya mashairi ya taarab ya huzuni

yanavyojitokeza katika nyimbo za taarab hasa za Shakila na Fatma. Nyimbo

nyengine zote za waimbaji hao ambazo hazihusiani na huzuni hazikushughulikiwa

katika utafiti huu. Pia utafiti haikujadili muziki au tuni za waimbaji wateule.

3.9 Vikwazo vya Utafiti na Utatuzi wake

Mtafiti alipata vikwazo pale baadhi ya wahojiwa kutokuwa tayari kutoa majibu ya

maswali ya mtafiti, na kukataa kuchukuliwa picha zao. Mtafiti alifanya jitihada ya

kuondoa dhana potofu za wahojiwa kwa kuwaelimisha juu ya malengo ya utafiti na

baadae walikubali. Hali ya kupungukiwa fedha za kuendesha mchakato wa utafiti

kwa vile waimbaji wanaishi Zanzibar na Dar es Salaam ulijitokeza. Katika hili

mtafiti ilimbidi atafute kwa wahisani mbalimbali. Jambo ambalo lilifanikiwa na

kufanikisha mchakato huu.

3.10 Hitimisho

Sura hii imejadili mambo mbalimbali ikiwemo mpango wa utafiti, eneo la utafiti,

walengwa wa utafiti, ukusanyaji wa data, mipaka ya utafiti na vikwazo vya utafiti na

utatuzi wake ambavyo vyote vimefafanuliwa kwa kina katika sura hii.

30

SURA YA NNE

UWASILISHAJI, UCHAMBUZI NA MATOKEO YA MJADALA WA

UTAFITI

4.1 Utangulizi

Sura hii imejadili kwa kina matokeo ya utafiti. Mjadala huo umegawanywa katika

sehemu kuu tatu kwa kuzingatia maswali na malengo ya utafiti huu. Sehemu ya

kwanza imefafanua sababu zilizowashawishi kutunga nyimbo zenye maudhui ya

huzuni. Sehemu ya pili imefafanua dhamira za nyimbo zenyewe na athari zake hasi

na chanya. Sehemu ya tatu na ya mwisho imelinganisha tofauti na mfanano kati ya

waimbaji wateule Fatma na Shakila. Hivyo, katika kila sehemu ya sura hii data

ziliwasilishwa kwa njia ya maelezo na kuongozwa na nadharia teule ya Uhalisia

ambayo husawiri hali halisi ya maisha ya mwanadamu katika maisha yake ya kila

siku.

4.2 Dhana ya Huzuni

Huzuni kama dhana ngeni katika muziki wa taarabkwa mwanadamu ni ile hali ya

masikitiko, majonzi, jitimai au simanzi ambayo mtu huipata ndani ya nafsi yake.

Huzuni huwa na visababishi kadhaa katika jamii. Hali hizo ni kama vile matokeo ya

misiba, maradhi, usaliti na kadhalika. Dhana ya huzuni katika maisha mwanadamu si

ngeni masikioni mwa walio wengi, kwani hali hii hujitotokeza mara kwa mara katika

maisha halisi ya watu kila siku. Mwanadamu hupatwa na huzuni kupitia mambo

mbalimbali anayotendewa au yalomsibu. Huzuni humfika mtu yeyote lakini kila mtu

huwa na namna yake ya kuipokea au kuikabili. Mwengine humfika akanyamaza

asitake mwengine ajue. Huweza mtu ikampata akasononeka nayo na mwishowe

kumuathiri. Wale wachache wenye vipaji wakiwemo washairi na waimbaji

31

hawaifutiki huzuni ikawatesa, bali huitoa hadharani kama dukuduku kwa njia ya

sanaa. Watu wa aina hii aghlabu huzuni haiwaumizi.

4.3 Nyimbo za huzuni za waimbaji wateule

1. KHERI ADUI SHETANI KAMA ADUI KIUMBE

Tutahadhari adui kiumbe, daima asikusibu Mungu akuepushie

Ujue si mzuri hata chembe, huwa hataki sababu mashakani akutiye

Hata kuchoka hachoki kwa kila pembe, na wala haoni tabu hasarani aingiye

Hata kama kitu huna masikini hambe, basi atakusulubu maisha uyajutiye

Adui umuonapo mkimbiye, kheri adui shetani kama adui kiumbe

Malipo ni duniyani, akhera hwenda hisabu viumbe

Kwa kweli wanalingana mfitini na hasidi, chanzo chake huwa choyo shoti

uwatambuliye

Tena wengi wapo hufanya juhudi, huzua yaliyo siyo ili wakuvurugiye

Huwa mkarimu kwao na hujitahidi, hakosi kisingizio mwema adui hanaye

Japo mwenyewe chako kakubariki wadudi, watakwendea mbio hadi lao

litimiye

Mja mwanadamu kufikiri na kuhisi, ndio hasa tarajio liburi simfnyiye

Maana wivu chuki hasada binafsi, huambatana na choyo husuda akuonee

Na kufanyiana hayo yake nafsi, roho mbovu alonayo yataka ajaliwaye

Mpewa hapokonyeki hapana dadisi, mtengenezaji hayo mola ndiye atoaye

Mjue hana kosa apewaye, kheri adui shetani kama adui kiumbe

Malipo ni duniani, akhera hwenda hesabu viumbe

Ni yeye mwenye uwezo mshirika hana, kwake hakuna lawama huwapa

wamuombaye

Wewe uonavyo mengineyo huna, nawe usikate tama muombe akujaliye

32

Kuchukuwa kwa kuwana si uungwana, ni tabia mbaya jama ziwacheni

mtubiye

Huu si wakati tena wakufatanafatana, yapo mengi yalazima ya thawabu

jichumiye

Mja mwishowe akusaidiye, kheri adui shetani kama adui kiumbe

Malipo ni duniani, akhera hwenda hesabu viumbe

KIITIKIO

Imani imewasakama wakiona yakwendea

Imani zimewahama rohoni wanaumiya

Lo! Po! Yasini mate chini ninatema

Kunusuru ya jaliya nahizi tabia mbaya

Mwimbaji: Fatma Isa

2. ASOKASORO HAKUNA

Hicho kilonichukiya maovu kunikataza, ikiwa nnakoseya wajibu kuniongoza

Ikiwa nnakosea wajibuweni kuniongoza, wala sioni vibaya mimi kunielekeza

Kinachonipa udhia, ni kule kuniapiza

Aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Asokasoro hakuna, aloumbwa na muweza

Mwenye lile hili hana, ndio shani yake azza

Tabia kutolingana, sijambo lakushangaza

Kinachonikera sana, nisonalo kupakaza

La msingi niiteeni, na wala sitopuuza

Sikatai nambieni, wallahi tawasikiza

Mengine msinidhani, yakuwa nitawabeza

Name tawashukuruni, kwa vile mmenifunza

33

Kama kosa nimefanya, na iwe nimeteleza

Dogo msilipe mwanya, likaja likatatiza

Mukawa mwayakusanya, nyinyi mnoendeleza

Hivyo sitokaa kimya, lazima tawaeleza

Kiitikio

Kunisema sichukui

Kusengenya haifai

Ni hekima njema rai

Kunionya sikati

Mwimbaji: Fatma Isa

3. HAYA MAUMBILE YANGU

Ubinafsi na choyo, nyoyoni vyawasumbuwa

Kutwa kazi yenu hiyo, zimewajaa shakawa

Kufanya niyapendayo, kwangu kosa limekuwa

Hilo haliwezekani, na wala halitokuwa

Leo nakuelezeni, muache kunichunguwa

Msijitie shidani, haya nimejaaliwa

Kwani hasa jambo gani, nyie lakulaumiwa

Kama baya kwenu nyie, kwangu nnaona sawa

Nawambia msikie, msio fahamikiwa

Fedhehani msingiye, kukaa kujizuzuwa

Lilobaki mnachie, sitaki kulaumiwa

Wengi wamenihasimu, na thamani kunitoa

Mwapita kumwaga sumu, kila ovu kutupiwa

34

Bure mnanituhumu, yafitina kuyagawa

Nami ni mwanadamu, si vyema kulaumiwa

Kiitikio

Nami ni mja mwezeni

Hata mkinichukiya

Aibu yangu ndo yenu

Kama mtafikiriya

Mwimbaji: Fatma Isa

4. AKUKATAAYE HAKWAMBII TOKA

Akukataaye, hakwambii toka

Huona mamboye, yamebadilika

Waweza ukae, huwezi ondoka

Nipende kwa dhati, au nikataye

Usinidhihaki, la kweli nambiye

Kama hunitaki, kheri nituliye

Watu hutendana, zaidi ya hayo

Wakatukanana, kupita mifano

Mwisho hupatana, yakesha maneno

Mwimbaji: Shakila Said

5. MAPENZI YAMEPUNGUA

Nilipokuwa na pendo, na ikawa twapendana

Hukuwa navyo vishindo, wala hatukupigana

Umebadilika mwendo, ni kheri tukaachana

35

Duniani wengi wapo, wapenzi kila aina

Usidhani peke yako, uzuri mnapitana

Sina haja pendo lako, dunia hii pana

Kiitikio

Mapenzi yamepunguwa mimi nimeshayaona

Kila nikiyachunguza hakwishi kuoneana

Mapenzi yamenguwa.

Mwimbaji: Shakila Said

6. MAPENZI NI KAMA DONDA

Nimechoka vumiliya, leo nawapasuliya

Nimekuwa siku hizi, kila siku ninaliya

Nanyi hamuniulizi, kipi ninacoliliya

Ni kama donda mapenzi, leo nawaelezeya

Waweza funga pumzi, kuzimu ukaingiya

Wala hayana mjunzi, yoyote humuelemeya

Nimempenda fulani, jina sitowatajiya

Alikuwa msikizi, kila ninalomwambiya

Alikuwa mtimizi, yote nilohitajiya

Kiitikio

Mapenzi ni kama donda

Yaingiapo moyoni

Nimechoka vumiliya

Leo nawapasuliya.

Mwimbaji: Shakila Said

36

7. KIFO CHA MAHABA

Kifo cha mahaba, ni cha idhilali

Hakina haiba, wala afadhali

Bali tajikaba, nifilie mbali

Kufa kwa mahaba, nia adhabu kali

Leo ni msiba, usio mithali

Kesho ni adhaba, mbele ya jalali

Ewe mahabuba, niepushe hili

Niwewe twabiba, hapana wa pili

Hapanda jaziba, tajiua kweli

Mwimbaji: Shakila Said

8 NENDA UTAKAKO

Nenda utakaponenda nenda hujazuiliwax2

Japokua nakupenda kwa hilo siyoumbuax2

Katu mm sitojali zako inda ulichoweka chuku

Kwapwani sitokuganda kwako nikajizuzua

Wapowengi mdhubuti mapenzi wanoyajuax2

Wanaopend kwa dhati wenyehdhi namurua

Kamwe sijiombei umauti kwa wewe sitojiuwa

Name nishajidhatiti lolote utoamuwa

Unavuma nje wavuma kipanga waallahi sikukutambua

Unataka sikuyapinga ari pia ilikuwa

Kama mboni yamachoni nnavokuenga mamlaka yote umepewa

Kumbe vile ni mjinga hujui kusaminia

Nalia na moyo wangu weweulonisumbua

Kwakukwachia pendo langu si ila yangukuchungua

37

Tena nenda niko radhi roho yangu wala sitolaumiwa

Katambe na ulimwengu mimi hutonikomoa

KIITIKIO

Nenda utakako mwanakwenda usojua kupenda

Baki hukohuko ewe nunda ucnitoeroho bure

Pendo halitaki pupa nakwambia ukijua

Mara moja hukutupa watu wasikutambue

Daima asosikia madhila kujitakia

Tena wala usirudi tena nenda nakusabiliya

Endelea nawako ujana mwisho utajijutia

Na Yule ng‟ombe nimchezeeeee

4.4 Sababu za Kutunga Nyimbo Za Huzuni

4.4.1 Usaliti

Huzuni yeyote kwa binadamu huwa na sababu. Ukiacha sababu ya kimaumbile kama

kifo, nyingi ya sababu ni matendo ya mtu kwa mwengine. Usaliti lina asili ya neno

„salata‟ yenye maana usaliti au ujeuri. Usaliti katika mapenzi ni tendo la

kumdanganya mpenzi wake mtu. Usaliti ni ile hali ya mtu kutojiaminisha kwa

mwenza au kumwendea kinyume juu ya mambo ambayo hayatakiwi kufanyiana

katika maisha. Usaliti hujitokeza katika maisha ya kila siku kutokana na matendo na

vituko tofauti. Tuone aina ya usaliti na aina ya watu wanaosalitiana. Mwenye

kusalitiwa hukumbwa na simanzi na huzuni.

4.4.1.1 Usaliti wa mume na mke

Usaliti wa mume na mke katika jamii zetu siyo jambo geni katika macho na masikio

ya watu wanaoishi katika jamii. Huyaona matukio haya kila mara katika maisha yao

38

ya kila siku. Usaliti sasa umezoeleka sana katika jamii zetu. Wakati mwengine usaliti

humtarajii mtu kwendea kinyume na mambo ambayo wahusika wamekubaliana

katika masuala ya biashara au siasa. Katika familia, mume au mke huweza kufanya

kitendo cha ndoa nje ya ndoa huu nao usaliti. Hali hii hupelekea kuzuka kwa

migogoro na mitafaruku katika ndoa. Yote haya hujiri kutokana na mmoja kati ya

wapenzi wawili au wote wawili kukosa uaminifu kwa mwenziwe katika maisha yao

ya kila siku. Mshairi na mwimbaji mmoja aliyefikwa na masaibu hayo ametunga

wimbo wa “Nenda Utakako”kuelezea yaliyomkuta.Moja ya beti ya shairi lake

anamruhusu mpenzi ende atakako kisa amesalitiwa. Hata hivyo, anakiri kuwa bado

anampenda sana mpenzi wake hivyo lakini anashindwa kuvumilia inda zake.Wimbo

huu ndani yake unaonesha jinsi ya usaliti ulivyojitokeza kwake. Naye Fatma anatoa

dukuduku lake;

Nenda nenda utakapo nenda nenda hujazuiliwa

Japo kuwa nakupendakwa hilo sitoumbuwa

Katu mimi sitojali zako inda ulichoweka chukuwa

Kwapani sitokuganda kwako nikajizuzuwa

Hali hii ya usaliti wa kimapenzi inajitokeza pia kwa msanii mwengine. Si mwengine

ila ni Shakila katika wimbo wake wa “Mapenzi Yamepungua”. Shairi linasema;

Ulipokuwa na pendo Naikawa twapendana

Hukuwa navyo vishindo Wala hatukupigana

Umebadilika mwendo Ni kheri tukaachana

Duniani wengi wapo Wapenzi kila namna

Ulidhani peke yakoUzuri unapitana

Sina haja pendo lako Dunia hii pana

39

Beti zote hizo mbili zinaonesha jinsi mmoja ya mpenzi anavyoweza kubadili

mwenendo wake wa kuwa na mwengine kwa kificho. Shairi la pili linaonesha kuwa

hapo awali Shakila alikuwa na mume ambaye alimkinai, alimuamini na alimpenda

sana. Awali ya pendo lao mume hakuwa na visa na hawakudiriki kupigana. Shakila

anaamini kuwa katika dunia hii wapo wengi awezaye kumpenda na hayupo yeye

pekee yake. Wazuri kupita mpenzi wake wa zamani pia wapo. Dunia ina nafasi

atapata mwengine ampendaye. Katika muktadha huu usaliti kati ya mume na mke ni

jambo ambalo limeenea duniani kote hasa katika wakati huu wa maendeleo ya

sayansi na teknolojia na utandawazi. Matokeo ya hayo yote ni muhusika kukumbwa

na huzuni na majonzi kama ile iliyooneshwa na washairi na waimbaji wa nyimbo

Nenda Utakako na Mapenzi Yamepungua.

4.4.2 Msiba

Msiba ni ile hali ya mtu kuondokewa na mwenza wake au mtu wake wa karibu sana.

Hali hii ikijitokeza, mwanadamu hawezi kuizuia.Mungu huwa tayari ameshalipanga

limtokezee mja wake. Kuondokewa na mpendwa wake kwa kuaga dunia moyo

hujawa na huzuni na simanzi ambazo ni vigumu kuizuia.Wimbo wa “Mapenzi ni

kama Donda”ulioimbwa na Shakila ni wimbo unaonesha ni kwa jinsi gani Shakila

alivyoumia baada ya mumewe kufikwa na mauti na kumuacha yeye akiwa mpweke

mwenye simanzi katika maisha yake. Shairi laomboleza;

Ni kamadonda mapenzi leo nawaelezea

Waweza funga pumzikuzimu ukaingia

Wala hayana mjuzi yoyote humuelemea

Hapa mshairi ametumia jazanda ya donda katika wimbo wake kufananisha ni kwa

jinsi gani anavyoumia ndani ya mtima wake baada ya kuondokewa na mumewe

ambaye amemzoea na aliyekuwa akimtumikia na kumtunza katika shida zake zote.

40

Jazanda ya dondani jeraha kubwa ambalo huleta maumivu makali katika mwili.

Jeraha huleta homa na wakati mwengine husababisha mauti lisipotibiwa. Pia msanii

ametumia jazanda ya kuzimu pahala kunakoaminiwa hukaa watu waliokufa. Yeye

kumfika msiba huo anajiona mwenye kuzibwa pumzi na huenda donda la mapenzi

humfikisha yeye huko. Kutokana na hali hiyo, msanii ametumia jazanda hiyo

kuonesha uchungu, simanzi na jitimai kutoka katika sakafu ya moyo wake pale

anapomkumbuka mume wake ambaye hayupo katika ulimwengu huu na hutamwona

tena. Muziki wa taarab umetumika hapa kama daraja ya kuiwasilisha huzuni za

muathirika kwa umma.

4.4.3 Maliwazo na Ufariji

Imebainika kuwa baadhi ya wasikilizaji wanapozisikiliza nyimbo za taarab za asilia

zenye maudhui ya huzuni na majonzi nao wao huguswa kwa hisia nzito kutokana na

kukumbuka hali ambayo hata wao imewakuta. Mmoja ya washabiki wa nyimbo hizi

zikiwemo nyimbo za mwimbaji Fatma anasema, anapozisikia nyimbo za huzuni

hukumbuka mambo ambayo yanayowasibu watu kadhaa katika jamii yake.

Anaposikiliza nyimbo hizo wakati mwengine hujikuta anatokwa na machozi kama

vile yeye ndiye yaliyomfika masahibu ndani ya moyo wake. Nyimbo

inayomuhuzunisha zaidi ni ile isemayo Haya Maumbile Yanguiliyoimbwa na

kutungwa naFatmaIssa. Kutokana na muziki wake, mashairi yake na hata uimbaji

wake wenye naghama basi hujikuta mshabiki huyu Fatma Ali ni mateka.

Hububujikwa na machozi bila ya kujijuwa. Beti zifuatazo za shairi lake limejaa hisia,

simanzi na sonono;

Ubinafsinachoyo nyoyoni vyawasumbua

Kutwa kazi yenu hiyo imewajaa shakawa

Kwangu yepi muonayo mageni msoyayajuwa

Kufanya niyapendayo kwangu koslimekuwa

41

Hili haliwezekani na wala halitokuwa

Leo nakuelezeni muachkunichunguwa

Msijitie shidani haya nimejaaliwa

Kwani hasa jambo gani mie lakulaumiwa

Wapo walonihasimu wengi nathamani kunitowa

Nawambia msikie msiofahamikiwa

Fedhehani msingie kukaa kujisumbuwa

Lilobaki mnachie sitaki kulaumiwa

Haya Maumbile Yanguni nyimbo iliyotungwa, kuweka sauti na kuimbwa na Fatma

Issa. Nyimbo hii huwahuzunisha na kuwasikitisha watu wengi kutokana na mlio wa

vinanda unavyoyayatika na tungo ya mashairi yake yanavyosisimuwa. Mwimbaji

anawatolea uvivu waivu na mahasimu wake kwa kuwapasha kinagaubaga.

Anawalaumu kwa ubinafsi wao na choyo na hufika kumchukia.Fatma anahoji

walimwengu kuwa hayo anayoyatenda kwa kupenda mwenyewe imekuwa kosa?

Halikuwahi kutendwa? Kwa kuwa hayo ni majaaliwa yake kwanini atolewe thamani

na kuhasimiwa na kulaumiwa na wenzake? Hataki kulaumiwa, aachwe! Fundo la

moyo lenye masikitiko linalobainishwa kupitia beti za nyimbo ya taarab.

4.4.4 Choyo na Husuda

Nyimbo nyingi za taarab kwa kawaida zikiwemo za huzuni hutungwa kutokana na

matakwa ya mtunzi mwenyewe binafsi. Hata hivyo hutokea washairi kuombwa

kuwatungia wengine lakini baada ya nyimbo kutungwa huwa ya wote. Msanii

huimba nyimbo kwa kuiweka tayari jamii, kuitia hamu na kwamba mtu yeyote

anaweza kuihusisha na jambo lililomsibu. Hivyo, msanii huichora taswira ya huzuni

ili kuitaka hadhira imuunge mkono. Hali ya choyo na husuda inamwathiri mwimbaji

na mshairi Fatma. Choyo ni ubahili na ni roho mbaya ambayo mja huijenga ndani ya

42

nafsi yake dhidi ya mwengine. Husda ni kijicho ambacho mtu huonesha kwa

kumwonea gere mwengine. Yote mawili haya, hatimaye huleta madhara kwa

mlengwa husika. Utafiti huu uliohusisha na nyimbo za taarab asilia zinazoimbwa

zimeenda sambamba na matukio ambayo yanakumba jamii katika suala hili la choyo

na husda. Mara nyingi choyo na husuda husababisha madhara kwa wanajamii

ikihusisha mitafaruku na migogoro. Fatma, mtunzi na mwimbaji, akiwa mtunzi

amebainisha kuwa baadhi ya wasanii wenzake wanamwonea choyo na kuwa na

husuda kutokana na kipaji chake cha kuimba ambacho yeye anaamini kuwa

amejaaliwa na Mola wake. Mara kadhaa wasanii wenzake hukaa vipembeni

kumsema na kumkebehi na hata kumfitinisha kwa mkuu wake wa kazi. Kadhia hiyo

ndiyo iliyomfanya atunge wimbo waAsokasoro Hakuna.Wimbo huo unasema;

Kile kilonichukiza maovu kunikataza

Ikiwa nnapotea wajibu kuniongoza

Wala sioni vibaya mimi kunielekeza

Kinachonipa udhia ni kule kuniapiza

Asokasoro hakuna aloumbwa na muweza

Mwaenye lile hili hana ndio shani yake azza

Tabia kutolingana sijambo la kushangaza

Kinachonikera sana nisonalo kupakaza

Kunisema sichukui

Kusengenya haifai

Ni hekima njema rai

Kunionya sikatai

43

Hizi ni baadhi ya beti ambazo zinaonesha jinsi gani msanii anavyochukizwa na suala

zima la husuda na choyo ambacho watribu wenzake humfanyia kwa lengo la

kutimiza ubaya wao. Mwimbaji analalamikia waovu wake na wale wanaomwonea

choyo na kumwekea husuda. Anaamini kuwa yeye kama binadamu si mkamilifu

hakosi ila wala kasoro. Hata hivyo, anawanyooshea kidole wenzake kuwa hata wao

hawakosi ila, hivyo anakataa kusengenywa lakini anakubali kuonywa. Anachukizwa

na kuapizwa, kusingiziwa yaso ya ukweli lakini yuradhi kukatazwa maovu na

kuelekezwa. Muziki wa taarab umemsaidia mtunzi na mwimbaji kwa huzuni kutoa

dukuduku lake.

4.4.5 Ufitini na uchongezi

Fitina na kuchongeana, ni ile hali ya kuchonganisha watu au kufanya wasielewane.

Mara nyingi fitina hutokea pale neema ikimfika mtu mmoja na yule anayekosa

hufitini. Katika jamii za Waswahili fitina hujichomoza katika masuala tofauti ya

kijamii. Kwa mfano, mwanamke anapojaaliwa kupata mume, watu wa karibu wa

yule mume au mke hutia fitina kwa kumzulia maovu ambayo kwayo yana lengo la

kufitinisha kwa kutotaka afanikiwe katika ndoa yake. Hata katika sehemu za kazi

napo huzuka fitina ambazo mara nyingi huathiri shughuli za kazi. Ingawa jambo la

kutiliana fitina limezoeleka katika mitaa, vijiji na ndani ya jamii zetu, lakini jambo

hili pia hujitokeza katika vikundi vya sanaa. Mfano bayana na hai umemtokea msanii

Fatma. Nyimbo ya Fitina iliyoimbwa na Fatma inaonesha jinsi gani watu

wanavyotiliana chonza na fitina kati yake na mpenziwe. Mashairi anaeleza chimbuko

la fitina hiyo;

Chanzo chake hata tukazoeana

Kufika kunipa vyakekwa moyo bila khiyana

44

Wasiwasi sina kwake napokea kwa mapana

Dhamira na lengo lake kuja kutia fitina

Sema namshasema khabari tunapeana

Za ulimwengu mzima mengi tunaaambizana

Kumbe nia kunichuma anielewe bayana

Karudi kiguu nyuma kenda kuzusha fitina

Kitu kilichonipoza ni kule kumshiba sana

Bila ya kumchunguza tukawa tumevaana

Yale yanayotutaza kukaa kuelezana

Mwisho wake yake jazauhasidinafitina

Hizi ni baadhi ya beti ambazo zinaonesha jinsi gani utiliaji wa fitina ulivyoshamiri na

kuota mizizi dhidi ya mshairi. Msanii anaonesha alivyokuwa naye mpenzi wake wa

karibu na ambaye wamekinaiana na kushibana na kupeana yale ya moyoni. Pia,

amefadhiliwa kwa mengi hata amekuja kubaini kuwa alikuwa akimchuma na

akimwendea kinyume kwa kuyasema yao ya siri kwa wengine. Lililomponza ni kule

kumuamini bila ya kiasi na kuacha kumchunguza. Malipo yake ni kumuhasidi na

kumfitini. Fitina na choyo aliyofanyiwa na wenzake imeibua simanzi kubwa kwake.

Hali hiyo imeifanya nyimbo hii iwe ya huzuni.

4.4.6 Huzuni na hali halisi ya maisha

Utafiti huu umebaini kuwa, wapo baadhi ya watu ambao walisikiliza nyimbo hizi za

huzuni hapo zamani na bila ya kutambua nyimbo hizi zina mchango katika jamii.

Watu hawa walikuwa wamezoweya kusikiliza nyimbo za furaha pekee. Hii ni

kwasababu na kuwa jambo ambalo linazungumziwa la huzuni huwa halijamgusa bali

akisikiliza nyimbo kwa lengo la kujiburudisha tu. Bwana Ali wa skuli ya Nyuki

45

4anasema kuwa hapo zamani nyimbo za huzuni alikuwa hazitilii manani sana

kwasbabu alikuwa anamwona mwimbaji ni mtu mwenye kusikitika tu kwa hiyo hapo

kwake yeye hakuona faida yoyote ya hizi nyimbo. Lakini kwa kadri siku

zilivyoendelea kusonga mbele na yeye binafsi kukabiliwa na matatizo mbalimbali

katika jamii ndipo anapojenga taswira kuwa kumbe nyimbo hizi zilikuwa zikionesha

hali halisi ya maisha ya mwanadamu. Akitolea mfano nyimbo ya Asokasoro

Hakunani wimbo ambao umeimbwa zamani lakini kwasasa ndiyo wimbo anauelewa

lengo na dhamira yake katika jamii. Hivyo, kutokana na hali hiyo mtafiti amebaini

kuwa nyimbo za huzuni huweka kumbukumbu akilini mwa msikilizaji. Asokasoroni

wimbo uliotungwa na kuimbwa na Fatma ambao mashairi yake humkumbusha Ali

vitu vingi ambavyo hapo awali hakuvitambua. Baadhi ya beti za nyimbo zinasema

hivi;

Wala sioni vibaya mimi kunielekeza

Kinachonipa udhia ni kule kuniapiza

Asokasoro hakuna aloumbwa na muweza

Mwaenye lile hili hana ndio shani yake azza

Tabia kutolingana sijambo la kushangaza

Kinachonikera sana nisonalo kupakaza

Kunisema sichukui

Kusengenya haifai

Ni hekima njema rai

Kunionya sikatai

4 Ali Khatib ni mwalimu wa skuli ya nyuki niliyezungumza naye tarehe 22/4/2016

46

Wimbo huu anapousikiliza humkumbusha mbali sana na kwa kuwajuwa

walimwengu walivyokuwa na tabia ya kusengenyana na kupakaza uovu ambao hata

wakati mwingine haupo katika ulimwengu huu. Hivyo, mwimbaji anadhihirisha

huzuni zake kwa kusema kuwa si jambo jema kukaa na kuanza kumsengenya na

kumsema, jambo la msingi ni kukaa na kumwita na kumuonya kwa mambo yote

ambayo mja anahisi kuwa si mazuri na hiyo ndiyo itakuwa ni njema. Nadharia ya

uhalisia meakisi utafiti huu kwa msingi wake wa umhakati kwa kusadifiana na

maisha ya kila siku ya jamii, kwani masuala ya kuoneana choyo, kusengenyana

yametawala jamii zetu kiasi ambacho wasanii hutumia kalamu zao kuionya jamii juu

ya matendo hayo maovu.

4.4.7 Huzuni na majuto

Nyimbo za huzuni zinapotungwa na wasanii hutunga baada ya wao kutendewa

ghiliba ambazo nyingine huwa za kimapenzi. Wengine hukata tamaa ya kuwa na

mpenzi huyo tena. Shakila katika wimbo wake waAkukatae Hakwambii Toka, yeye

mwenyewe akiwa mwimbaji amebainisha jinsi gani anavyoonesha majuto juu ya

yule ambaye alikuwa akimpenda kwa dhati katika maisha yake. Hata hivyo, mpenzi

huyo hakuonesha mapenzi ya dhati kwake. Hali hiyo ilimpelekea Shakila kuwa na

majuto ndani ya moyo wake. Mwimbaji anaamini kuwa huyu mpenzi wake

anamfanyia vitimbi vinavyoonesha kuwa amemchoka na vinaashiria kumkataa. Hata

hivyo linalobainika ni kuwa hamwambii waziwazi kama hamtaki bali humfanyia

ishara, vitendo na vituko vya kumkataa. Shakila analalamika kwa kuimba;

Nipendekwa dhati au nikataye

Usinidhihaki la kweli nambiye

Kama hunitaki kheri nituliye

Kheri nituliye kama hunitaki kheri nitulie

47

Katika ubeti huu anaonesha jinsi gani mpenzi wake alivyokuwa hamjali na

hamthamini katika maisha yake. Hivyo, msanii Shakila anaamuwa kubadilisha nia

yake na kuaamua bora abaki peke yake kuliko kumng‟ang‟ania mtu ambaye hana

habari naye. Mwimbaji anampa masharti mpenzi wake kuwa ampende kikweli na

kwa dhati kama hawezi amwambiye waziwazi kama hamtaki na asimdhihaki.

Mwimbaji Fatma kwa upande wake na kwasababu ya mashaka kama hayo na yeye

ameamua katika nyimbo nyengine anaonesha majuto yake kwa mpenzi wake ambaye

alimthamini na kumsabilia hapo awali kila kitu katika maisha yake. Lakini

mwishowe huyu mpenzi alimfanyia vituko ambavyo hakuvitegemea. Mpenzi wake

huyo alikuwa akibadilisha wanawake wa kila aina. Ndipo hapo Fatma aliposhindwa

kuvumilia akaamua atunge na aimbe yeye mwenyewe nyimbo ya Nenda

Utakapo.Wimbo huu unaonesha jinsi ya mume asivyothamini mapenzi ya mke

ambaye anampenda. Kwa machungu na huzuni tele, Fatma anaghani;

Unavuma mja wavuma kipanga wallahi sikukutambuwa

Unayataka sikupinga maridhiya nilikuwa

Kama mboni ya macho nnavyokuenga mamlaka yote umepewa

Kumbe vile nimjinga hujui kuthaminiwa

Nalia na moyo wangu wewe ulonisumbuwa

Kukwachia pendo langu si ila yangu kuchunguwa

Tena nenda niko radhi roho yangu wala sitolaumiwa

Katambe na ulimwengu mimi hutonikomowa

Beti hizi mbili zinaonesha jinsi msanii anavyoujitia moyo wake kwa kumpenda mtu

ambaye hana utu wala uungwana. Mwimbaji ameonesha huzuni zake kwa

kumfananaisha mpenzi wake na ukwere wa kipanga ndege apendaye kunyaka

vifaranga vya kuku sawa na “wasichana”. Alimridhia kwa kila kitu na kumuenzi

48

kama mboni ya macho yake. Alimsabilia kila kitu chake, kwa kufanya hivyo

alimwona mjinga. Kwa vituko hivyo yupo tayari kuachana naye ili atambe na

wanawake wengine waliojaa ulimwenguni.

4.4.8 Huzuni na bahati

Licha ya kila mtu katika jamii kujaribu kufanya mengi sana yenye kupendeza na

kuleta tija lakini watatokea watu wachache tu watakaosifu na kukujali lakini kwa

wengine watakudhihaki na kukudharau. Na wakati mwengine mtu hata afanye kitu

kizuri cha namna gani, hakitathaminiwa, badala yake atachukiza na kubandikwa ila

katika jamii husika. Yote haya yanajiri kwasababu ya mtu kukosa bahati katika jamii.

Utafiti huu umebaini kuwa nyimbo ambazo Fatma amezitunga na kuziimba yeye

mwenyewe zimejikita katika kumkosesha bahati. Jambo hili amelidhihirisha katika

mahojiano kati ya msanii huyu na matafiti huko nyumbani kwake (tarehe

22/11/2015) mtaa wa Kwa Alamsha Zanzibar. Alieleza kuwa yeye binafsi ni mtu

ambaye hana bahati hata kidogo kwani kila kikundi anachojiunga nacho huzuka

migogoro katika kipindi kifupi tu anapokaa katika kikundi hicho. Kwa matokeo hayo

ndipo yeye alipojiaminisha kuwa yeye hana bahati ya kupendwa na wasanii

wenzake. Yeye anaamini kinachomponza ni kipaji chake cha kuimba. Hali hii ndiyo

inayompa hamu na shauku ya kutunga nyimbo nyingi yeye mwenyewe binafsi.

Yawezekana ukosefu wa bahati kama huo upo kwa watu wengine. Kwake yeye hili

limepalilia kipaji chake. Wimbo waSijali Kuchukiwa, uliotungwa na yeye Fatma

ambao unaonesha jinsi ambavyo Fatma anavyochukiwa na watribu wenzake. Ingawa

yeye anajitahidi kukaa nao kwa wema na hisani, haiwi nusura kwake ya kupata

bahati. Fatma kwa huzuni analalama;

Sitoyalipiza katu hayo unayonitendea

Kuvumiliya si kitu mitihani ya duniya

49

Ninange kwa kila mtu na ubaya kunitiya

Kitachokulipa ni utu uovu sitokufanyia

Kinyume siendi siendi kuntu hata ukinichukiya

Rohoni mwangu siweki kitu japo nishayazoeya

Kama nimekukosea mie yailahi ndiye hakimu

Na kama unanioneya ni yeye atohukumu

Hukumu hukumu hakimu hukumu

Ongeza kunifisidi kwa kisa na kila mambo

Tukana niite hasidi ukioniona vikumbo

Kustahmili nazidi subira ndo zangu nyimbo

Japo wanikera hadi sitokujibu kwa fumbo

Madhali Mungu shahidi kwako siongezi jambo

Hakimu wa haki wadudi yatakwisha majigambo

Bahati yangu miye kwa binaadamu mbaya

Hata niwafanyie nini kwa binaadamu mbaya

Ni wabebe mgongoni kwa binaadamu mbaya

Ni wape cha mvunguni kwa binaadamu mbaya

Hawana shukurani

Hizi ni beti ambazo Fatma anaonesha jinsi alivyokuwa hana bahati kwa wenzake.

Kila kukicha wenzake humsakama na kumsema vibaya katika jamii. Mwimbaji

analidhihirisha hili pale anaposema kuwa hatolipiza kisasi abadani kwa ubaya wote

ambao wenzake wanayomfanyia. Wala rohoni mwake yeye haweki fundo kwani

yote hayo ameshayazowea kumfika katika ulimwengu na kwake hakuna geni hata

moja. Anaamini kuwa yote hayo ni miongoni mwa mitihani tu ya duniya. Anaendela

kulalamika kuwa hata afanye hisani na awabebe mgongoni basi malipo yake ni

50

majungu tu na fitina. Yeye anamwachia Mungu amlipiye na yeye atazidi kuvuta

subira.

4.5 Dhamira ya Huzuni katika Nyimbo za taarab na tija zake

Katika kulijadili suala hili wahojiwa wengi wametoa maoni tofauti.Wahojiwa wapo

kutoka makundi tofauti. Wapo wale watangazaji wa vipindi vya redio za taarab asilia

na walimu wa somo la Fasihi.

4.5.1 Kupanua dhana ya Taarab

Sanaa ya fasihi kwa kiasi kikubwa imetajirika kutokana na muziki huu wa taarab

kukua na hasa katika kipengele cha dhana ya taarab ya asili kuwa taarab ni furaha.

Kiasili nyimbo zilizotungwa zilikuwa ni za furaha tu na zilikuwa zikitungwa kwa

madhumuni ya kustarehesha watawala. Miaka nenda miaka rudi, taarab imekua na

kubeba maudhui ya furaha, ramsa, huzuni na majonzi. Kutokana na hali hiyo,

wasanii wamepata uhuru wa kutunga nyimbo zenye maudhui wanayoyataka wao

wenyewe na kuanzia hapo ziliibuka nyimbo za huzuni katika jamii zetu. Nyimbo

hizo za huzuni zimeonesha matatizo mbalimbali ya kijamii yenye kuhusisha na

mambo mengine ya majonzi, jitimai na simanzi.

4.5.2 Kuelimisha

Wapo wahojiwa wanaoamini kuwa nyimbo zenye kubeba maudhui ya huzuni huwa

zinaelimisha jamii kwa kiasi kikubwa sana. Hawa huamini kuwa msanii

anapoiwasilisha nyimbo yake, jamii hupata ujumbe na sababu la tokeo lenyewe.

Kupitia dhamira za nyimbo hizi jamii hupata uelewa wa matukio na sababu zake.

Hivyo, kupitia nyimbo hizi jamii huweza kuepukana kwa namna moja ama nyengine

na mambo maovu ambayo yapo kinyume na silka na tamaduni za Waswahili. Jamii

hufunzwa kuepukana na husuda, choyo na fitina. Usaliti wa kimapenzi unaobebwa

51

na chuki zisizo na msingi, huweza kuepukwa. Haya hujiri kutoka na na nyimbo

ambazo zinaimbwa kwakuwa zinatoa elimu juu ya athari ya mambo hayo ambayo

hayapendezi katika jamii. Hivyo, ingawa nyimbo hizo hutungwa kuelezea masahibu

yaliyomfika mtu lakini pia huelimisha jamii kuachana na mambo hayo yasiyo na

msingi katika jamii. Tunaona nyimbo Mapenzi Yamepungua, msanii amefaulu

kuonesha mume ambaye haijali ndoa yake na aendaye kinyume na mkewe. Kupitia

nyimbo hii, jamii inaelimika kuwa makini katika ndoa na kuachana na mambo

ambayo hayaleti faida yoyote katika maisha yenu.

4.5.3 Kuliwaza

Kupitia nyimbo za huzuni wanajamii wanaliwazika kutokana na mashairi, vinanda

vinavyotumika na sauti ya mwimbaji ya masikitiko kupitia nyimbo hizo. Nyimbo

nyingine za taarab ni za mahadhi na mashairi ya majonzi, ziimbwapo huleta huzuni

kwa jamii na iimbwapo huleta faraja. Faraja huwapa nguvu kutekeleza majukumu

kwani mashairi ya nyimbo hizo huzungumzia matatizo yanayoikumba jamii yao. Bw.

Ali Nahoda wa Coconut FM na Bi.Fatma Mohamed wa Zenji FM wote hao ni

watangazaji wa vipindi vya taarab asilia wao wanapozisikiliza nyimbo za huzuni

hasa nyimbo ya Fatma Issa ya Asokasoro Hakuna nyoyo zao wenyewe huliwazika

kwani katika nyimbo hiyo mwimbaji na mtungaji huyu amegusia hali halisi ya

maisha. Moja ya beti ya kibwagizo cha nyimbo hiyo kinasema;

Kunisema sichukuwi

Kusengenya haifai

Ni hekima njema rai

Kunionya sikatai

52

Hapa Fatma anaiasa jamii yake kuwa mtu anapofanya kosa ni vizuri kumwita na

kumwambia kwa njia ya hekima kabisa bila ya kukaa vipembeni na kumsengenya

kwa maneno mabaya. Kupitia beti hii, wote Bw. Ali na Bi. Fatma, 5wameridhika

kwa maoni yake anavyoielekeza na kushauri namna bora ya kuishi bila ya kuoneana

choyo na kusengenyana.

4.5.4 Kuzindua

Miongoni mwa dhamira ya nyimbo za huzuni ni kuizindua jamii kwa yale mambo

ambayo yametendwa kwa siri na ambayo hayajulikani. Wahojiwa katika utafiti huu

wamesema kuwa kupitia nyimbo za huzuni jamii hupata kuyajuwa na kuelewa

mambo tofauti ambayo yapo kinyume na utamaduni, silka na desturi za maisha.

Mambo hayo yanayosababishwa na udhaifu wa binaadamu uliomo ndani ya moyo

wake. Ili jamii iondokane na tabia hizo ziendazo kinyume na desturi na mwenendo

mwema wa jamii, nyimbo hizi hubainika kuwa ni funzo. Hivyo basi, jamii inaposikia

jambo hilo mwimbaji ameliimbiya, watu hutanabahi na kuliona kosa na kupata

uelewa. Mfano mzuri ni wa nyimbo ya Kheri Adui Shetani Kama Adui Kiumbe

ambayo msanii anaonesha kuwa bora mwanadamu kuwa na uadui tena bila ya

kificho na shetani kuliko na mwanadamu mwenzake katika dunia. Kiumbe huyu

mwanadamu akikusudia lake hufanya kila mbinu ili amtiye ubayani mtu ili apate

achukize katika jamii. Likifanikiwa hili ataridhika na kufurahia kuona kiumbe

mwenziwe anateseka, kudhalilika na anaadhirika katika ulimwengu huu.

5 Fatma Ali Mohd ni mtangazaji wa Zenji FM na Ali Nahoda ni mtangazaji wa Coconut FM

nilozungumza nao tarehe 22/4/2016 huko Mombasa na Migombani Zanzibar

53

4.5.5 Kurekebika tabia

Kupitia nyimbo za huzuni za taarab, jamii inapata manufaa makubwa kutokana na

kuwa nyimbo hizi huirekebisha jamii kwa kuona chimbuko la tatizo, athari na

matokeo yake na suluhisho. Nyimbo huweza kuifanya jamii ibadilike na kuachana na

mambo ambayo hayapaswi kufanywa na mwanadamu baada ya kuonekana madhara

yake. Nyimbo hizi hukemea husuda na mambo mengine yakiwemo choyo na maovu

mengine. Mfano wa nyimbo za huzuni ambazo zinashajiisha watu kutooneana choyo

na gere bali mtu afanye bidii ili aweze kufanikiwa na mambo yake ni kama vile;

Haya maumbile YangunaAsokasoro Hakuna nyimboiliotungwa na kuimbwa na

Fatma. Nyimbo ya aina hizi zinakataza tabia ya husuda na kuoneana maya na

humtaka mtu atafute njia mbadala ambayo itamwezesha kufanikiwa katika maisha

yake. Pia, kupitia wimbo waMapenzi Yamepunguaulioimbwa na kutungwa na

Shakila, mwimbaji anawasihi wawili wapendanao wawe na mapenzi ya kweli ili

waweze kupiga hatua za kimaendeleo katika jamii. Wasia unaotolewa ni kuwa si

busara wala si hekima mpenzi mmoja kumdanganya mpenzi mwingine.

4.5.6 Ujenzi wa hisia na huruma

Tumeona kuwa nyimbo hizi za huzuni za taarab jinsi zinavyoweza kuteka hisia za

huruma kwa wasikilizaji. Waimbaji wanapowasilisha kazi zao hudhihirishiwa tatizo

wanalolizungumzia mbele ya hadhira ambayo wao huliona kama ni la kwao. Hapo

ndipo mtu baada ya kusikia nyimbo inamjia huruma, majonzi na simanzi kwa

kumuhurumiya yule aliyepatwa na hilo tatizo akiamini mwimbaji mbele yake ndiye

muhanga. Kwa mfano Bw. Ali 6anasema kuwa anapoisikiliza nyimbo ya Mapenzi ni

Kama Donda moyo wake hupatwa na mshituko na majonzi na kumuhurumia mtu

6 Bwana Ali Haji wa skuli ya Faraja niliyezungumza naye tarehe 6/4/2016 huko skuli ya Sekondari

Faraja Zanzibar

54

huyu ambaye amefanyiwa ukatili ambao haustahili kufanyiwa mwanadamu.

Mwimbaji Shakila, kwa madaha, jinsi anavyonung‟unika katika nyimbo yake hii,

huuvaa uhusika wa muhanga na kujihisi kama yeye ndiye mwenye jeraha limtesalo

kimapenzi. Hivyo, kupitia nyimbo hizi za huzuni mtu hukumbuka matukio tofauti

ambayo labda yalimkuta yeye au mtu mwingine ambaye huleta simanzi na majonzi.

Kwa mtu anaposalitiwa kwa kawaida huwa ana majonzi ya muda mrefu ambayo kwa

mara moja hayawezi kusahaulika tena kwa muda mfupi. Kwa hiyo, mara anaposikia

nyimbo ambayo msanii naye amesalitiwa huliona lile tatizo lilomfika kuwa siyo la

peke yake bali ni humfika kila mtu ambaye bado anavuta pumzi katika ulimwengu

huu. Matokeo yake mtu huyo huliwazika na kujiona kuwa bado ni mtu duni na dunia

haijamtenga bali ipo pamoja naye. Hata hivyo kwa mtu ambaye pia hajapatwa na

tatizo kubwa, humuhurumia yule mtu ambaye amefikwa na tatizo, yeye humgusa

ndani ya moyo wake.

Kwa mfano, Amina tunamwona asemavyo kuwa anapoisikiliza nyimbo ya Fatma Isa

ya Asokasoro Hakuna hupatwa na simanzi kubwa ndani ya moyo wake na huamini

kuwa kweli mwanadamu hapendelei kuona mtu anapata neema yoyote katika dunia

bali hujipendelea yeye binafsi tu. Amina7 anaungama kuwa hata akiisikiliza nyimbo

ya Shakila ya Macho Yanacheka Moyo Unalia ambaye akivuta taswira ya viungo

viwili hivi vya macho na moyo “macho kuwa yanacheka na moyo unalia” ambavyo

havina uhai lakini vimepewa ubinaadamu na vina mvuto mkubwa na hisia kali katika

moyo. Nyimbo hii humuathiri sana yeye. Pamoja na hayo atharia ya uhalisia

inaonekana kusibu katika utafiti huu kwa kutumia msingi wa pili wa ushabihi ukweli

pale msanii anapovipa uhai vitu visivyo uhai na msikilizaji kuvipokea kwa hisia

7 Amina Ali ni mwalimu wa skuli ya Faraja ambaye nimezungumza naye tarehe 23/ 4 /2016 hapo

skuli ya Faraja Zanzibar

55

zinazokaribia ukweli. Kwa mfano anaposema „macho yanacheka‟ kiuhalisia si kweli

lakini kwa dhamira ya ndani utaona kuwa macho yanacheka.

4.5.7 Kuonesha ujasiri

Wahojiwa wengine katika utafiti huu wamebainisha kuwa miongoni mwa nyimbo za

huzuni, zaonesha ujasiri kwa upande mmoja na ukatili wa watu katika jamii kwa

upande wa pili. Mtu aliyetendwa uovu huweza kustahmili matukio ya kikatili

ambayo yanamkumba katika mazingira magumu. Hata hivyo, muathirika huyo

huchukua maamuzi magumu na ya kijasiri ya kumkwamuwa kutoka katika janga.

Kwa hivyo, msanii anapoimba nyimbo yake kuhusu masaibu yaliyomkuta huwa

anaitaka jamii kutonyongeka na mambo ambayo yaathiri maisha yao. Msikilizaji na

mtazamaji anatakiwa awe jasiri na shujaa wa kutoa maamuzi yanayostahiki ili kukata

minyororo ya kifungo ambacho hakina manufaa yoyote. Yashauriwa mtu

anapotendewa na mpenzi wake ubaya anapaswa afikiri njia mbadala ambayo itaweza

kumkwamuwa katika hali aliyonayo. Fatma, 8mwimbaji na mtunzi alipofikwa na

matatizo hayo alipata ujasiri wa kumfukuza mume ambaye alikuwa akimwendea

kinyume kila siku na hatimaye akaamua kuachana naye na kukaa peke yake bila

mpenzi. Baada ya kuona kuwa yeye yamemkuta mambo kama hayo na akaamini

kuwa hata katika jamii matukio kama hayo hayakosekani hivyo, akaamuwa kutunga

nyimbo ya Nenda Utakapo ili kuwahamasisha jamii kujenga ujasiri na kupiga moyo

konde.

8 Mazungumzo yangu na Fatma Issa tarehe 22/11/2015 nyumbani kwake Kwa Alamsha Zanzibar

56

4.6 Athari zinazopatika katika Nyimbo za Huzuni

Ama kwa hakika hakuna kitu hata kimoja katika ulimwengu huu kikakosa athari

katika jamii. Athari hizo zitatofautiana kutokana na mitazamo ya mtu binafsi na jamii

husika. Utafiti huu umegundua athari zifuatazo;

4.6.1 Athari Chanya

4.6.1.1 Kuifanya jamii kujua matatizo yake

Mara nyingi wanajamii hukumbwa na matatizo mbalimbali ambayo huwatweza

walio wengi. Msanii anapotunga nyimbo yake hufikiri kuwa lile tatizo

analoliwasilisha ni lake peke yake, ukweli ni kuwa wenye matatizo kama hayo wapo

wengi. Lakini pale nyimbo hiyo inavyotoka na kupokelewa watu wengine

hutanabahi kuwa tatizo lile siyo lake peke yake. Hubainika kumbe nyimbo hiyo

huwagusa wengi na huzuni hiyo hufikwa na masaibu au matatizo kama hayo watu

kadha wa kadha. Kwa mantiki hii nyimbo hubaki kuwa ni mali ya kila aipendaye.

4.6.1.2 Kufariji na kuliwaza

Kutokana na uhalisi wa matukio tofauti ambayo yanaikuta jamii na maafa

mbalimbali yanayotokea, nyimbo hizi huwafariji na kuliwaza watu ambao

wamekutwa na matatizo hayo katika jamii. Bila ya kupata faraja na maliwazo hayo

kutoka nyimbo hizi, baadhi ya watu wangebaki kulia na kuyayatika kwa kukosa

maliwazo. Hali ingetokea mwanadamu asingefanya shughuli zake za kimaendeleo na

dunia ingedumaa.

4.6.1.3 Kugusa nafsi ya msikilizaji

Mara nyingine mtu ambaye anasikiliza nyimbo ambayo tukio lake limemgusa hufikia

hatua ya kulia kwa kutokwa na machozi kutokana na uhalisi wa tukio husika. Kwa

mfano mtangazaji waZenji Bi Fatma Ali anasema kuwa mara nyingi anaposikiliza

57

nyimbo za Fatma hujikuta analia bila sababu kutokana na mashairi yake

yanavyomuingia ndani ya moyo wake na kuhisi kuwa lile tatizo analolizungumzia na

yeye linamhusu.

4.6.2 Athari hasi za Nyimbo za Huzuni

Katika kipengele hiki wapo wahojiwa ambao hawapati athari yoyote wanaposikiliza

nyimbo hizo bali wamesema kuwa hakuna athari yoyote wanayoipata, kwao nyimbo

hizo ni sehemu ya kupata burudani tu katika moyo wao. Kwa mfano Nahoda

mtangazaji waCoconut FM anasema kuwa anapozisikiliza nyimbo hizo huwa hapati

athari yoyote licha ya kuburudika tu ndani ya moyo wake na kuamini kuwa matukio

mabaya kama hayo siyo vizuri kufanyiana walimwengu.

4.6.3 Tofauti ya Fatma na Shakila

Ni ukweli usiopingika kuwa panapotokea wasanii stadi wawili wa uimbaji taarab

lazima zitakuwepo tofauti ambazo zinaweza kutofautisha kati ya mwimbaji mmoja

na mwengine. Jambo hili hutokea kwasababu ya vionjo mbalimbali vinavyotumika

katika kujenga kazi zao. Kwa kiasi kikubwa Fatma anaposimama jukwaani huteka

nyoyo za wengi pale anapowasilisha kazi yake jukwaani na mashairi ya nyimbo yake

hugusa moja kwa moja matukio ambayo yapo katika jamii. Vile vile vyombo vya

taarab vitumikavyo na ucharazaji wake vina utofauti mkubwa pale aimbapo Fatma.

Nyimbo zake hutumia vyombo vya asilia kama vile fidla, udi, qanuni na nai jambo

ambalo huufanya muziki uonekane wa kipekee na kiasilia zaidi.

Uimbaji wa Shakila ni tofauti kwani yeye nyimbo zake hutumia vyombo vya kisasa

kama vile gita, organ, accordion na kadhalika. Hivyo, kupitia utofauti huu wa

vinanda na mtindo wa muziki, uimbaji wa Fatma unaonekana kuwa ni bora kuliko

ule wa Shakila. Pia kuna tofauti nyingine kati ya uimbaji wa Fatma na Shakila,

58

kupitia suala zima la mitindo ya mahadhi ya nyimbo zao. Kwa mwimbaji Fatma,

anapoimba nyimbo zake husisimua nafsi ya hadhira yake kutokana na kuimba kwake

kwa naghama, masikitiko na huzuni kubwa. Hali hii huifanya hadhira ishiriki moja

kwa moja katika tukio la huzuni analolizungumzia. Shakila kwa upande wake,

nyimbo zake nyingi zimebeba maudhui ya mapenzi yasiyo na huzuni nzito. Lakini

Fatma nyimbo zake za mapenzi zinazungumzia matukio ya majonzi yanayoisibu

jamii. Fatma ameimba nyimbo zake katika hali mbili, za kumpenda mwenza wake na

maafa yaliyomkuta dhidi ya watribu wenzake waliokuwa hawampendi yeye apate

neema.

Amekuwa Fatma kama anavyoamini, akikosa bahati katika maisha yake. Anaamini

kuwa popote endapo na kushiriki sanaa hii ya taarab huwa hawapakosi fitina na

ubinafsi ambao husababishwa na wasanii wenzake katika kikundi chao. Yeye

anaamini inatokana na kipaji chake cha kuimba na kutunga nyimbo mbalimbali

zenye mvuto, na kwa hivyo, mafanikio yake wenzake hupatwa na choyo ambacho

inayoambatana na husuda. Yeye anaamini kuwa ustadi wake umemsababishia

madhara makubwa na sasa anayo itikadi kuwa, kwa vile anapoimba hukaa juu ya kiti

kutokana na maradhi ya miguu jambo analoliamini kuwa wenzake wamemfanyia

ushirikina. Kiumri Shakila ana umri wa miaka 69 na Fatma miaka 59. Wamepitana

kwa miaka kumi.

4.6.4 Mfanano wa Fatma na Shakila

Shakila na Fatma wote waimbaji na wote ni wanawake. Wote ni washairi na waweka

muziki katika nyimbo ingawa wote hawapigi chombo chochote. Wote ni waimbaji

wa taarabu asilia ambao huimba nyimbo zenye maudhui ya huzuni na pia huimba

nyimbo za furaha. Yawezekana hili ni sadfa pale mfumo wa maisha wa jamii ya

59

Tanga na Zanzibar kufanana kwani wote ni watu wa mwambao na pia ni Waisilamu.

Wote katika maisha wamekatishwa masomo yao ya shule ili waolewe. Wameolewa

wote na waume tofauti na kuzaa nao watoto wengi. Wote hivi sasa ni wajane na

maisha yao kiuchumi si mazuri. Wote wanaendelea na kuimba lakini nyota zao za

umaarufu zinafifia. Maumbo yao yakimbilia uzee na makunyuzi ya nyuso zao

zimepunguza haiba zao.

Tukihusisha matokeo ya utafiti huu na nadharia, ya uhalisia tutaona kwamba

nadharia hii jukwaani imesawiri yale yaliyomo katika utafiti huu kwani masaibu

yaliyowapata wasanii hawa ni mambo ambayo wanawake wengi yanawakuta katika

jamii zetu.

4.7 Hitimisho

Katika sura hii, matokeo ya utafiti yamewasilishwa na kuchambuliwa kulingana na

maswali ya utafiti. Maswali hayo yameakisi malengo ya utafiti yaliyokusudiwa.

Mjadala umegawanyika katika sehemu kuu tatu. Kwanza imechambuliwa sababu za

kutungwa kwa nyimbo za huzuni. Katika mjadala huo mtafiti ameonesha kuwa zipo

sababu mbali mbali ambazo zinazowasukuma wasanii hao kutunga nyimbo hizo.

Miongoni mwa sababu hizo ni matukio ambayo yanawakuta wasanii hao binafsi

katika harakati zao za kila siku. Pia, yapo matukio yatokanayo katika jamii ambayo

husababishwa kutungwa nyimbo. Sehemu ya pili imejadiliwa kwa kina dhamira za

nyimbo za huzuni pamoja na athari zake. Dhamira hizo ni kuelimisha, kuliwaza,

kuzindua, kurekebika tabia, ujenzi wa hisia na huruma na kuonesha ujasiri.Dhamira

mbalimbali ambazo zinakwenda sambamba na maisha halisi ya mwanadamu.

Sehemu ya tatu ya sura imeeleza jinsi washairi na waimbaji hawa walivyofanana na

kutofautiana kimaisha, kiumbaji na kitabia na kiwasifu.

60

SURA YA TANO

MUHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO

5.1 Utangulizi

Sura hii inawasilisha muhtasari na hitimisho la tasnifu hii. Kadhalika, sehemu hii

imetoa maoni kadhaa yaliyopatikana kutokana na utafiti huu. Aidha, sura hii

imeelezea jinsi nadharia ilivyosibu na kutoa mapendekezo kwa tafiti zijazo.

5.2 Muhtasari wa Tasnifu

Utafiti huu uliangalia juu ya nyimbo za huzuni za waimbaji Shakila na Fatma

ambayo ililifafanua nyimbo teule za huzuni za waimbaji hawa sababu, zilizopelekea

kutungwa kwa nyimbo hizo na tathmini juu ya jamii inavyozipokea nyimbo hizo za

huzuni.Tasnifu hii imegawika katika sura tano, ambapo kila sura imeeleza mawazo

yake makuu kwa muhtasari.

Sura ya kwanza imetoa mwelekeo wa tasnifu hii kwa kuanza na utangulizi, usuli wa

tatizo, tamko la utafiti, historia ya wasanii teule ambao ni Shakila na Fatma, malengo

ya utafiti, maswali ya utafiti na manufaa ya utafiti. Aidha, sura hii ilifafanua nadharia

iliyotumika katika utafiti huu ambayo niNadharia ya Uhalisia na misingi yake mikuu

ni msingi wa kimhakati na ushabihi ukweli.

Sura ya pili imefafanua maandiko yaendayo sambamba na utafiti huu. Sura hii

imeeleza maandiko mbalimbali yanayolandana na utafiti huu.Utafiti huu uliangalia

maandiko yanayofafanua chimbuko la taarab. Aidha, maandiko yahusuyo taarab

yaliangaliwa, na hatimaye utafiti huu ulionesha pengo la utafiti ambalo lilitoa

mwanya kwa mtafiti kuliziba pengo hilo.

Sura ya tatu imeeleza mbinu na vifaa vilivyotumika katika utafiti huu. Sura hii

inabainisha muongozo kamili wa utafiti ulivyokuwa, aina ya kundi lililohitajika kwa

ajili ya kutoa majawabu juu ya maswali ya utafiti pamoja namna data

61

zilivyokusanywa na kuchambuliwa kwa kuongozwa na nadharia iliyochaguliwa

ambayo ni nadharia ya uhalisia.

Sura ya nne imeonesha namna data zilivyowasilishwa na kutafsiriwa. Aidha,

malengo na maswali ya utafiti ambayo yalijibika na kugawika katika sehemu tatu

kuu. Kwanza, kuorodhesha baadhi ya nyimbo za huzuni za waimbaji wateule, pili

kubainisha sababu zilizopelekea kutungwa kwa nyimbo hizo, na kutathmini jamii

ilivyopokea nyimbo hizo za taarab na athari zake.

Sura ya tano inahusu hitimisho la utafiti huu kwa ujumla wake ikijengwa na

muhtasari wa kazi, matokeo ya utafiti, utoshelevu wa nadharia, pamoja na

mapendekezo juu ya tafiti zijazo.

5.3 Utoshelevu wa Nadharia Iliyotumika

Nadharia ya Uhalisia ndiyo iliyotumika katika kukusanya data na uchambuzi wake.

Nadharia hii imebeba mambo makuu mawili ambayo ni msingi wa kimhakati na

ushabihi ukweli. Msingi wa mwanzo, ni msingi wa kimhakati. Huu ni msingi ambao

husawiri matukio kama yalivyo katika jamii kwani tumeona ya kuwa nyimbo

ambazo zimetungwa huelezea matukio ambayo yanawafika wanajamii katika maisha

yao ya kila siku. Hivyo, nadharia hii imekwenda sambamba na matukio yote ambayo

yanamfika mwanadamu katika uhai wake. Msingi wa pili, ni ushabihi ukweli. Msingi

huu huelezea namna matukio yanavyokaribia kuelezea ukweli huo. Hivyo kutokana

na mnasaba huo tunaona kuwa nadharia hii ya Uhalisia imesawiri matukio yote

ambayo yanamtokezea mwanadamu katika maisha yake. Kwani mara nyingi msanii

anapotunga kazi yake huelezea ambayo yapo katika jamii, hivyo hata huzuni nayo

ipo katika jamii na huweza kumfika kila mtu iwe kwa siri au dhahiri.

62

5.4 Mambo Mapya Yanayoibuliwa na Tasnifu Hii

Mambo mapya yaliyomo katika tasnifu hii ni haya yafuatayo:

Dhana ya asili n maana ya taarab kuwa ni furaha na ramsa imepitwa na wakati.

Taarab sasa ni muziki wa furaha na huzuni.

Utafiti umebaini pia kuwa jamii inazichukulia nyimbo za huzuni katika mitazamo

tofauti. Wako wanaoangalia yaliyomo ndani ya nyimbo husika na kuyaakisi katika

mazingira halisi yalivyo katika maisha yetu ya kila siku kwa mfano usaliti, misiba,

choyo na ubinafsi. Na wapenzi wengi wa nyimbo za aina hii ni wale ambao

wameguswa na mikasa inayofanana na mashairi yaliyomo katika nyimbo hizi. Hata

hivyo katika nyimbo hizo wapo waliokuwa wanaoangalia sauti za waimbaji na

mtiririko wa vinanda kwa ajili ya kuburudika tu bila kuangalia maudhui ya ndani ya

nyimbo husika.

Pili, ni umahiri wa wasanii katika kuwasilisha hisia zao kwa kutumia vipaji viwili

kwa wakati mmoja, yaani kutunga na kuimba. Katika utafiti huu, msanii Bi Fatma

Issa anaoneka kutunga nyimbo kama vile ya Ubinafsi na Choyo na kuiimba

mwenyewe hii ni kutokana na kuguswa na majaribu ya waja moja kwa moja

yaliyokuwa yakimsibu kutoka kwa watu tofauti.

Mwisho, katika jambo la kusikitisha sana ni kuwa wasanii wote hawa wawili pamoja

na kutumia vipaji vyao kuelimisha na kuburudisha jamii bado kazi zao hii

hazikuwabadilisha maisha yao kuwa bora zaidi na kuziona thamani ya vipaji vyao.

5.5 Mapendekezo wa Tafiti Zijazo

Kukamilika kwa tasnifu hii haimaanishi ya kwamba ni mwiko kwa wengine kutafiti

katika kipengele hiki cha fasihi ikiwemo taarab. Hii ni kwa sababu utafiti huu

63

ulikuwa na malengo na mipaka yake. Hivyo, bado kuna maeneo kadhaa ambayo

yanatakiwa yafanyiwe kazi na watafiti wengine. Maeneo yanayopendekezwa ni:-

Mosi, katika muziki wa taarab kuna tofauti ya utungaji na uwasilishaji wa nyimbo za

taarab asilia na taarab ya kisasa, ni vyema kwa watafiti wajao kulinganisha na

kutofautisha uwasilishaji wa taarab hizi.

Pili, tukiangalia matokeo ya utafiti yalivyoonesha kubeba hadhi kubwaya wasanii

hawa lakini hatima yake maisha yao yalikuwa duni sana. Ipo haja ya kufanyiwa

utafiti wa kina juu ya sababu zinazopelekea wasanii hawa wakongwe wa muziki wa

taarab asilia kutonufaika na kazi yao.

Tatu, kiuhalisia imeonekana taarab asilia imepotea kwa kasi hivyo, ipo haja ya

kuchunguza sababu zilizopelekea wasanii wa taarab ya sasa kuhamia zaidi kwenye

taarab ya kisasa na kuiacha taarab asilia.

5.6 Maoni ya Mtafiti juu ya Utafiti Huu

Kutokana na matokeo ya utafiti huu napendekeza maoni yafuatayo kushughulikiwa

ili kuisaidia jamii:-

Mosi, kuwalazimisha wasanii wote wa taarab kujisajili katika haki miliki ili kuweza

kunufaika na kazi zao zinapotumika katika sehemu mbali mbali kama vile kwenye

kumbi za starehe, redio na televisheni ili wanufaike na kazi zao na ziwafaye sasa na

wanapostaafu shughuli hizo.

Pili, kuandaa makongamano yenye lengo la kujadili namna ya kuimarisha na

kurithisha kizazi kijacho sanaa ya taarab asilia kwenye utungaji na uwasilishaji na

wakati huo huo taarab ya kisasa iimarishwe zote, kwani zina umuhimu kwa jamii.

64

MAREJELEO

Alawiy, Z. (2007), “Nyimbo za Mafumbo za Taarab zinavyochangia kudumisha

maadili yajamii ya wazanzibar”, Ripoti ya utafiti kwa ajili ya Shahada

Chuo Kikuu Suza, (haijachapishwa).

Alhabib, E.A (2012) „Matumizi ya Lugha katika Nyimbo za Taarab‟.Tasnifu ya

Umahiri katika Kiswahili, Chuo Kikuu Huria Tanzania.

Andanega A.A.S (2002) “Bahari ya Elimu ya Ushairi”. Ndanda Mission Press,

Mtwara.

Fargion, J. T. (2014), Taarab Music in Zanzibar in Twentieth Century: A story of old

is gold, Ashgate Publishing Limited.

Far-han, I. (1992), Introduction of Taarab Music in Zanzibar.Makala iliyowasilishwa

katika International Conference on the history of Zanzibar (14-16,

Desemba).

Igobwa, E.S (2007), Taarab and Chakacha in East Africa: Transformation,

appreciation and Adaptation of two Popular Music Genres of Kenyan

coast, conference on music in the world of islam – Assah 8-13 August 1-

8

Juma, M. (2012) „Taarab Asilia‟. Tanzania Daima 13/7/2011

Khamis, A.M. (2012). Matumizi ya Taswira katika Nyimbo za Mapenzi za Taarab

asilia yaZanzibar. Tasnifu ya Umahiri katika kiswahili. Chuo kikuu cha

Dar es salaam.

Khatib, M. (2014), “Taarab Zanzibar”.Oxfrord university Press, Dar es Salaam.

Khatib, M.S (1982) „Taarab ni fasihi simulizi? Makala ya semina za Tuki Dar es

salaam. Taasisi ya Taaluma za Kiswahili, uk 3

Kombo, D. Na tromp, d. (2006), Proposal and Thesis Writing, An Introduction,

paulines publications Africa.

Kothari, C. (2003), Research Methodology and Techniques, New international, (p)

ltd New Delhi.

65

Lange, S. (2000). Muungano and TOT: Rivals on the Urban Cultural Scene.

Mashindano / competitive music performance in east africa, mhariri ni

frank Gunderson and Gregory f.b. Dar es Salaam : Mkuki na Nyota

Publishers, uk. 67-85

Mgana, I. (1991), Jukwaa la Taarab Zanzibar.Hakapaino, Helsiniki Medi Africa.

Msokile, M. (1981), Nafasi ya Nyimbo za fasihi Simulizi katika jamii.Iliyoandikwa

katika makala za fasihi Simulizi.Chuo kikuu cha Dar-es-salaam.

Msokile, M. (1992), Kunga za fasihi na Lugha. Educationa publishers and

distributers.Dar-es-salaam.

Mulokozi, M. (1990), Tanzu za fasihi simulizi.Mulika toleo la 21.Chuo kikuu cha

Dar-es-Salaam.

Mzee F.A (2013), Maudhui katika Nyimbo za Taarab za bi Shakila. Tasnifu ya

Uzamili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (haijachapishwa).

Ntarangwi, M (2001) „a socio – historical and contextual analysis of popular musical

performance among the swahili of mombasa kenya. Cultural analysis

2001: 2:1-37 University of California, Los Angeles.

Ponera, A.S., (2014), Utangulizi wa Nadharia ya Fasihi Linganishi, Karljamer print

technology, Dar es salaam, Tanzania.

Saleh, S.S. (1980), „Nyimbo za taarab Unguja‟ Lugha Yetu namba 37. Jarida la

BAKIZA.

Senkoro, F.E.M.K (1987), Fasihi na jamii, Press and Publicity Center, Dar es salaam.

Thabit, W (2007), “Nafasi ya Maudhui ya Nyimbo za Taarab katika jamii ya

Zanzibar ya leo”.Ripoti ya utafiti ya shahada chuo kikuu cha Suza,

(haijachapishwa).

Wamitila, k.w. (2004), Kichocheo cha fasihi simulizi na andishi. Nairobi focus

publication ltd.

Zeid, O (2016) Mabadiliko ya Taarab Asilia. (Mahojiano na mtafiti).

66

VIAMBATISHO

A: Mwongozo wa usaili kwa wataalamu wa Fasihi.

1) Unafahamu nini kuhusu dhana ya huzuni?

2) Ni zipi nyimbo za huzuni ambazo unazifahamu?

3) Je ni kwa kiasi gani nyimbo hizo zinaweza kuathiri jamii?

4) Je wewe unafurahishwa na nyimbo hizo? Ikiwa ndio/ hapana kwanini

5) Ziko aina ngapi za huzuni?

6) Kwa maoni yako unahisi ni sababu zipi zinazowasukuma wasanii kutunga

nyimbo hizo?

7) Je upo umuhimu wowote wa kutunga nyimbo zenye maudhui ya huzuni?

67

B: Dodoso kwa wanfunzi waliotafiti taarab asilia

1) Unafahamu nini kuhusu dhana ya huzuni

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

………………………

2) Taja sababu mbili zinazowasukuma wasanii kutunga nyimbo zenye maudhui

ya huzuni.

a) ……………………………………

b) …………………………………….

3) Ni kwa vipi nyimbo za huzuni zinaathiri jamii.

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

………………………..

4) Ni mazingira yepi ambayo yanasababisha utokeaji wa huzuni katika

nyimbo hizo.

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

……………………

4) Ni miktadha gani inayopelekea huzuni katika jamii?

…………………………………………………………………………………

………………………………………………………………………………..

68

5) Taja dhima za nyimbo za huzuni unazozijua ambazo zinajitokeza katika

nyimbo za taarab.

…………………………………………………………………………………

………………………………………………………………………………….

………………………………………………………………………………….

…………………………………………………………………………………

6) Je ipo haja ya wasanii kutunga nyimbo ambazo zinabeba maudhui ya huzuni?

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………….

7) Toa maoni yako kuhusu nyimbo hizo.

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

…………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………….

69

C: Nyimbo za waimbaji wateule Zilizotumika katika kazi hii

2. KHERI ADUI SHETANI KAMA ADUI KIUMBE

Tutahadhari adui kiumbe, daima asikusibu Mungu akuepushie

Ujue si mzuri hata chembe, huwa hataki sababu mashakani akutiye

Hata kuchoka hachoki kwa kila pembe, na wala haoni tabu hasarani aingiye

Hata kama kitu huna masikini hambe, basi atakusulubu maisha uyajutiye

Adui umuonapo mkimbiye, kheri adui shetani kama adui kiumbe

Malipo ni duniyani, akhera hwenda hisabu viumbe

Kwa kweli wanalingana mfitini na hasidi, chanzo chake huwa choyo shoti

uwatambuliye

Tena wengi wapo hufanya juhudi, huzua yaliyo siyo ili wakuvurugiye

Huwa mkarimu kwao na hujitahidi, hakosi kisingizio mwema adui hanaye

Japo mwenyewe chako kakubariki wadudi, watakwendea mbio hadi lao

litimiye

Mja mwanadamu kufikiri na kuhisi, ndio hasa tarajio liburi simfnyiye

Maana wivu chuki hasada binafsi, huambatana na choyo husuda akuonee

Na kufanyiana hayo yake nafsi, roho mbovu alonayo yataka ajaliwaye

Mpewa hapokonyeki hapana dadisi, mtengenezaji hayo mola ndiye atoaye

Mjue hana kosa apewaye, kheri adui shetani kama adui kiumbe

Malipo ni duniani, akhera hwenda hesabu viumbe

Ni yeye mwenye uwezo mshirika hana, kwake hakuna lawama huwapa

wamuombaye

Wewe uonavyo mengineyo huna, nawe usikate tama muombe akujaliye

Kuchukuwa kwa kuwana si uungwana, ni tabia mbaya jama ziwacheni

mtubiye

Huu si wakati tena wakufatanafatana, yapo mengi yalazima ya thawabu

jichumiye

70

Mja mwishowe akusaidiye, kheri adui shetani kama adui kiumbe

Malipo ni duniani, akhera hwenda hesabu viumbe

KIITIKIO

Imani imewasakama wakiona yakwendea

Imani zimewahama rohoni wanaumiya

Lo! Po! Yasini mate chini ninatema

Kunusuru ya jaliya nahizi tabia mbaya

Mwimbaji: Fatma Isa

2. ASOKASORO HAKUNA

Hicho kilonichukiya maovu kunikataza, ikiwa nnakoseya wajibu kuniongoza

Ikiwa nnakosea wajibuweni kuniongoza, wala sioni vibaya mimi kunielekeza

Kinachonipa udhia, ni kule kuniapiza

Aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Asokasoro hakuna, aloumbwa na muweza

Mwenye lile hili hana, ndio shani yake azza

Tabia kutolingana, sijambo lakushangaza

Kinachonikera sana, nisonalo kupakaza

La msingi niiteeni, na wala sitopuuza

Sikatai nambieni, wallahi tawasikiza

Mengine msinidhani, yakuwa nitawabeza

Name tawashukuruni, kwa vile mmenifunza

Kama kosa nimefanya, na iwe nimeteleza

Dogo msilipe mwanya, likaja likatatiza

Mukawa mwayakusanya, nyinyi mnoendeleza

71

Hivyo sitokaa kimya, lazima tawaeleza

Kiitikio

Kunisema sichukui

Kusengenya haifai

Ni hekima njema rai

Kunionya sikati

Mwimbaji: Fatma Isa

3. HAYA MAUMBILE YANGU

Ubinafsi na choyo, nyoyoni vyawasumbuwa

Kutwa kazi yenu hiyo, zimewajaa shakawa

Kufanya niyapendayo, kwangu kosa limekuwa

Hilo haliwezekani, na wala halitokuwa

Leo nakuelezeni, muache kunichunguwa

Msijitie shidani, haya nimejaaliwa

Kwani hasa jambo gani, nyie lakulaumiwa

Kama baya kwenu nyie, kwangu nnaona sawa

Nawambia msikie, msio fahamikiwa

Fedhehani msingiye, kukaa kujizuzuwa

Lilobaki mnachie, sitaki kulaumiwa

Wengi wamenihasimu, na thamani kunitoa

Mwapita kumwaga sumu, kila ovu kutupiwa

Bure mnanituhumu, yafitina kuyagawa

Nami ni mwanadamu, si vyema kulaumiwa

72

Kiitikio

Nami ni mja mwezeni

Hata mkinichukiya

Aibu yangu ndo yenu

Kama mtafikiriya

Mwimbaji: Fatma Isa

4. AKUKATAAYE HAKWAMBII TOKA

Akukataaye, hakwambii toka

Huona mamboye, yamebadilika

Waweza ukae, huwezi ondoka

Nipende kwa dhati, au nikataye

Usinidhihaki, la kweli nambiye

Kama hunitaki, kheri nituliye

Watu hutendana, zaidi ya hayo

Wakatukanana, kupita mifano

Mwisho hupatana, yakesha maneno

Mwimbaji: Shakila Said

5. MAPENZI YAMEPUNGUA

Nilipokuwa na pendo, na ikawa twapendana

Hukuwa navyo vishindo, wala hatukupigana

Umebadilika mwendo, ni kheri tukaachana

Duniani wengi wapo, wapenzi kila aina

Usidhani peke yako, uzuri mnapitana

Sina haja pendo lako, dunia hii pana

73

Kiitikio

Mapenzi yamepunguwa mimi nimeshayaona

Kila nikiyachunguza hakwishi kuoneana

Mapenzi yamenguwa.

Mwimbaji: Shakila Said

6. MAPENZI NI KAMA DONDA

Nimechoka vumiliya, leo nawapasuliya

Nimekuwa siku hizi, kila siku ninaliya

Nanyi hamuniulizi, kipi ninacoliliya

Ni kama donda mapenzi, leo nawaelezeya

Waweza funga pumzi, kuzimu ukaingiya

Wala hayana mjunzi, yoyote humuelemeya

Nimempenda fulani, jina sitowatajiya

Alikuwa msikizi, kila ninalomwambiya

Alikuwa mtimizi, yote nilohitajiya

Kiitikio

Mapenzi ni kama donda

Yaingiapo moyoni

Nimechoka vumiliya

Leo nawapasuliya.

Mwimbaji: Shakila Said

7. KIFO CHA MAHABA

Kifo cha mahaba, ni cha idhilali

Hakina haiba, wala afadhali

74

Bali tajikaba, nifilie mbali

Kufa kwa mahaba, nia adhabu kali

Leo ni msiba, usio mithali

Kesho ni adhaba, mbele ya jalali

Ewe mahabuba, niepushe hili

Niwewe twabiba, hapana wa pili

Hapanda jaziba, tajiua kweli

Mwimbaji: Shakila Said

8 NENDA UTAKAKO

Nenda utakaponenda nenda hujazuiliwax2

Japokua nakupenda kwa hilo siyoumbuax2

Katu mm sitojali zako inda ulichoweka chuku

Kwapwani sitokuganda kwako nikajizuzua

Wapowengi mdhubuti mapenzi wanoyajuax2

Wanaopend kwa dhati wenyehdhi namurua

Kamwe sijiombei umauti kwa wewe sitojiuwa

Name nishajidhatiti lolote utoamuwa

Unavuma nje wavuma kipanga waallahi sikukutambua

Unataka sikuyapinga ari pia ilikuwa

Kama mboni yamachoni nnavokuenga mamlaka yote umepewa

Kumbe vile ni mjinga hujui kusaminia

Nalia na moyo wangu weweulonisumbua

Kwakukwachia pendo langu si ila yangukuchungua

Tena nenda niko radhi roho yangu wala sitolaumiwa

75

Katambe na ulimwengu mimi hutonikomoa

KIITIKIO

Nenda utakako mwanakwenda usojua kupenda

Baki hukohuko ewe nunda ucnitoeroho bure

Pendo halitaki pupa nakwambia ukijua

Mara moja hukutupa watu wasikutambue

Daima asosikia madhila kujitakia

Tena wala usirudi tena nenda nakusabiliya

Endelea nawako ujana mwisho utajijutia

Na Yule ng‟ombe nimchezeeeee

76

Picha namba 6: Mtafiti akimuhoji bibi Shakila Said huko nyumbani

kwake Charambe Dar es Salaam. (Utafiti, 2016)

D: Picha mbali mbali zinazohusiana na utafiti

77

Picha namba 7: Mtafiti akimuhoji bibi Fatma Issa huko nyumbani kwake

Kwa Alamsha, Zanzibar. (Utafiti, 2016)