silaha - KIPAJI APP
-
Upload
khangminh22 -
Category
Documents
-
view
1 -
download
0
Transcript of silaha - KIPAJI APP
Silaha za Adui Samuel Imori
i
SILAHA ANAZOZITUMIA
ADUI KUWAANGAMIZA
WATU WA MUNGU
ASKOFU SAMWEL IMORI.
Silaha za Adui Samuel Imori
ii
Haki Miliki@2018Samuel Imori
Mawasiliano;
+255765446611,+255715788219, +254707224495, +255 715 788 219
Email [email protected]
ISBN: - 978-9987-9995-6-9
Toleo la – Tano
Angalizo:-
Kitabu hiki ni mali halali ya Bishop Samwel Imori, ni makosa kunakili
au kutoa nakala za kitabu hiki bila idhini ya mwandishi. Nunua nakala
halisi ili kuinua huduma hii.
Kimechapishwa na
Truth Printing Company
0764 425 704/ 0652 383 590
Ubungo Dar es salaam Tanzania
Silaha za Adui Samuel Imori
1
YALIYOMO
UTANGULIZI: .............................................................................................. 2
SILAHA ANAZOTUMIA SHETANI KUWAANGAMIZIA
WANADAMU ............................................................................................... 5
Fedha ni nini? Biblia inaisemeaje fedha?. .............................................. 12
HITIMISHO ................................................................................................ 86
Silaha za Adui Samuel Imori
2
UTANGULIZI:-
Namshukuru Mungu aliyeniwezesha kukiandika kitabu hiki vipo
vitabu vingine vilivyo tangulia na ipo mistari mbalimbali katika
Biblia ilinifanya niandike hivyo vitabu vilivyotangulia,
Kipo kitabu cha
1. Vikwazo vya kuurithi uzima wa milele sehemu ya kwanza
2. Vikwazo vya kuurithi uzima wa milele sehemu ya pili
3. Kanisa ni nini?
4. Zijue huduma 5 katika kanisa
Baadhi ya mistari iliyonifanya niandike vitabu hivyo vilivyotangulia
ni hii hapa chini,
Luka13:24
Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba maana
nakwambia kwamba wengi watataka kuingia wasiweze.
Math7:22-23
Wengi watanambia sikuile Bwanabwana, hatukufanya unabii kwa
jina lako? Na kwajina lako kutoa pepo, nakwajina lako kufanya
miujiza mingi? Ndipo nitakapo waambia dhahiri sikuwajua ninyi
kamwe, ondokeni kwangu ninyi mtendao Maovu.
Silaha za Adui Samuel Imori
3
1kor9:26-27
Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, sikama asitaye, napigana
ngumi vivyo hivyo sikama Apigaye hewa, bali nautesa mwili wangu
na kuutumikisha, isiwe nikiisha kuwahubiri Wengine mwenyewe
mtu wa kukataliwa niwe.
Hiyo ndio mistari iliyonifanya nikae chini nakutafuta majibu:-
Kwamba wengi watataka kuingia katika uzima wa milele
lakini wasiweze, Nini kitawazuia na wanataka?
Kwamba wengi watajitetea kwamba walifanya miujiza mingi
kwa jina la Yesu lakini atawafukuza, maana yakewaende
wakaishi na mapepo waliokuwa wanayafukuza”fikiri hapo
kidogo”
Yakwamba mtumishi wa Mungu aliamua kuutesa mwili wake,
akaamua kuu tumikisha ili, Asije akaingiza wengine mbinguni
naye akakuta anakataliwa.
Mistari hiyo ndiyo ilionifanya nikae chini nitafute majibu, ndio vitabu
hivyo vine vikazaliwa.
Sikutaka kuishia hapo nilipo kutana na mstari ufuatao hapo chini-;
Hosea4:6a
“watu wangu wana anaangamizwa kwa kukosa maarifa
Mungu alimtumia mtumishi wake akatamka maneno hayo,ndugu
msomaji wangu wa Kitabu hiki usemi huo ni mgumu, sio wa
Silaha za Adui Samuel Imori
4
kawaida watuwangu wanaangamizwa ni watu wa Mungu maana
amewaita waziwazi kwamba “Watu wangu”
Nilishtuliwa na maneno hayo na ndipo nikakaa chini, nikatafuta
nikataka kujua kile kinachowaangamiza watu hawa wa Mungu, ndipo
kitabu hiki kikazaliwa.
Napendamno kumshukuru Mungu aliyenisaidia kukiandika, nakutakia
kila la kheri unapokisoma.
Kikafanyike msaada kwako wewe unayekisoma sasa na kwa
mwingine yeyote pia atakaye kisoma.
Katika Jina la Baba/Mwana na Roho mtakatifu,
Amen
Silaha za Adui Samuel Imori
5
SILAHA ANAZOTUMIA SHETANI KUWAANGAMIZIA
WANADAMU
Hosea4:6a
Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.
1kor 2:11
Shetani asije akapata kutushinda kwa maana hatukosi kuzijua hila
zake
Efeso 6:16
Zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani ambayo kwa hiyo mtaweza
kuizima mishale yote yenye moto ya Yule mwovu.
1thes 2:18
Kwahiyo tulitaka kuja kwenu naam mimi Paul, mara ya kwanza na
mara pili shetan akatuzuia.
Maandiko yote hapo juu yaliotangulia yanatosha kukutaarifu ya
kwamba tuko vitani na kwa kuwa tukovitani vema tujue tunapigana
na nani?
Na tukiisha jua tunayepigana naye tusiishie hapo tutafute kuzijua
silaha anazozitumia
Silaha za Adui Samuel Imori
6
Kwa upande wetu Mtume Paul alituandikia kwamba tuvae silaha zote
za Mungu ndipo tutaweza kupambana na huyo adui yetu tunaye
pambana naye.
Vita yetu tutashinda, lakini tusipojua silaha anazotumia, kwa
vyovyote atatushinda.
Neno la Mungu limetuambia hivi “watu wangu wanaangamizwa kwa
kukosa maarifa”
Kwa kukosa ujuzi, kukosa kuzijua silaha anazozitumia huyo adui yetu
Kama tunataka tushinde sharti tuzijue hila zake, tujue kwamba hana
mchezo, tujue anarusha mishale yenye moto ikimpata mtu
haimuumizi tuu bali humchoma pia ni mishale yenye moto.
Tumeendelea kuona waziwazi Mtume Paul akielezea vita hiyo kwa
kutamka kuwa walikuwa wamejipanga waende kwa wathesalonike
lakini, anasema waziwazi kwamba shetani akawazuia, akafanikiwa
kuwazuia
Mtume hatuambii kututishia wala hakuogopa kusema pengine
kwamba atadhalauliwa au pengine ataonekana hana nguvu hapana
alilielezea waziwazi jambo hili ili litusaidie kujipanga sawa sawa,
litusaidie kufikiri, na tuweze kutambua kwamba kama huyu adui yetu
hatutajua jinsi ya kumkabili,basi ni dhahiri kwamba atatuangamiza
kama yanenavyo maandiko yakwamba watu wa Mungu
tunaangamizwa kwa kukosa maarifa.
Maarifa haya yanayosemwa ni ujuzi wa jinsi ya kupigana na huyo
anayeitwa mwizi, au mwivi, Biblia inasema katika kitabu cha
Silaha za Adui Samuel Imori
7
Yohana 10:10
Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu, mimi nalikuja ili
wawe na uzima kisha wawe nao tele.
Tumelisikia jina la huyu adui yetu anaitwa mwivi, mwivi ni mtu Yule
anayechukua visivyo vyake, tena Akaitwa muuaji,mchinjaji, kwahiyo
kila anapotutembelea huwa anakuja atimize hayo ambayo ni majina
yake.
Huja ili aibe, achinje, aue, wakati mwingine kwa kutozielewa kazi
zake anatuumiza, kutokuelewa kwamba yeye ni, mwizi, mwuuaji.
Nilipokuwa na tafakari jambo hili la muuaji, nikalikuta andiko katika
Biblia linasema hivi, waulize wanyama nao watawafundisha.
Nilipousoma mstari huo ilinichukua muda kulitafakari hilo, tuusome
mstari huo kwanza ndipo tuendelee kujifunza
Ayubu 12:7
Lakini sasa waulize hao wanyama nao watakufundisha,na nyuni
wa aangani hao watakuambia.
Nilipoutafakari sana mstari huo, nilipata kuelewa kwamba wanyama
wanaoufahamu wa kuwajua maadui zao.
Nilimtazama sungura akifukuzwa na mbwa, hawezi kusimama, hata
akichoka namna gani, hawezi kusimama, tangu alipo zaliwa naamini
wazazi wake walimfundisha sungura kwamba mbwa ni adui yao, ni
muuaji wao,hana utani, akimkuta sungura anamla, kwamba mbwa
Silaha za Adui Samuel Imori
8
anapomkamata sungura niukweli usio pingika huwa analiwa, na kwa
mfano huo, wana wa Mungu wakifundishwa wakamjua vizuri huyo
wanayemwita shetani, wanayemwita ibilisi, huyowanayemwita
mpinzani wao, jina lake tumelisikia ni muuaji, yeye anapomwendea
mtu ni ili amuue wala hana utani, kama vile ambavyo mbwa
hanautani anapomkabili sungura nia yake huwa ni kumuua, nasi
tukielewa kuwa huyo anayeitwa mwizi, haji kwautani wala haji
kubahatisha yeye anakuja ili aue, nasi tukielewa vizuri tutajiponya, au
tutatafuta mbinu za kuweza kumkabili ndio maana imeandikwa
kwamba yeye atakayeshinda atapewa kuketi pamoja na Yesu, kama
yeye alivyoshinda.
Sikumoja nilikuwa nimealikwa Ibada mahali Fulani, vijana
walisimama kuimba, wimbo uliokua unaimbwa nilifuatilia yale
maneno waliyokuwa wakiyatamka, ya likuwa yanasema hivi, nita
nukuu machache
Wimbo ulikuwa unasema hivi;-
tutapita katikati yao, wakipita kwa chini tutapita kwa juu
Wakipita kwa juu tutapita kwa chini
Wakipita kushoto tutapita kulia
Wakipita kulia tutapita kushoto
Nliwaza sana nilipo yasikiliza hayo maneno, na waliokuwa wakiimba
ni wakristo, wanapambana na huyo adui yetu tulie mtaja hapo juu
yakwamba ni mwivi, huyo ambaye ni muuaji. Sasa nikajiuliza, hivi
Silaha za Adui Samuel Imori
9
hawa waimbaji wanasema, wapite kulia pindi wakigundua kuwa
muuaji huyu yupo kushoto, na wapite juu pindi wakigundua kuwa
muuaji yuko chini, mwisho wasiku wataitwa wameshinda au
wataitwa wamekwepa? hili swali lilinifanya nichukue muda wa
kutosha kujiuliza kama watu hawa wanaoitwa kanisa wanajifahamu
kuwa wao ni nani?
Ndio maana nikaandika kitabu kiitwacho“KANISA NI NINI”.
Jina mojawapo la kanisa ni askari, ukisoma utaelewa vizuri Askari
kazi yake sio kumkwepa adui kwa kupita kulia wakati yeye adui
akipita kushoto.
Nia yangu ya kukiandika kitabu hiki ni kuyafungua macho ya wale
wanaopigana vita na adui huyu anaeitwa ibilisi, shetani, mwizi, ndio
maana tumeona jambo muhimu ambalo lilifanya niandike kitabu hiki
kwamba “watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa”
Katika mstari huu tunasikia sauti ya Mungu ikisema watu wake
wanaangamizwa kwa kukosa maarifa
Wanaangamizwa na nani?
wamekosa maarifa ya kufanyaje?
Kwa vyovyote yupo anayewaangamiza na kwa vyovyote yapo
maarifa, au ujuzi ambao watu wake hawa wameyakosa, ambayo
wanatakiwa kufundishwa ili waepuke kuangamizwa.
Ni vizuri pia wafundishwe, vizuri kumhusu huyo mwizi, pamoja na
silaha anazozitumia, naomba Mungu atusaidie ili macho ya mioyo
Silaha za Adui Samuel Imori
10
yetu yatiwe nuru, tupate kuona yatupasayo kuyatenda katika sikuhizi
za kumalizia
Kama nilivyotangulia kusema kwamba jina mojawapo la kanisa ni
Askari
2 Tim 2:3
Ushiriki taabu pamoja nami kama askari mwema wa kristo Yesu.
Hakuna askari yeyote anayeweza kwenda vitani bila silaha, hawezi
kwenda mikono mitupu, lazima awe na silaha. Napenda uelewe kuwa
hata huyo anayeitwa mwizi au mwivi naye niaskari pia, nimesema
askari sharti awe na silaha, adui yetuyeye anazo silaha anazozitumia
katika vita.
Kabla hatujaendelea kujifunza napenda nikupe picha ya kile kinacho
fanyika ili huyo mwizi ampate mtu amwangamize, huwa anatumia
kitu kinachoitwa mtego, mfano mzuri wakujifunza ni kwa mvuvi
Wavuvi wengine hutumia ndoano, kwawale msioijua ndoano, ni
chuma kilichotengenezwa maalumu kwa kunasia samaki, lakini
mvuvi akirusha ndoano pekeyake kwenda kwenye maji, kamwe
samaki hawezi kukila chuma ,mpaka akifiche kile chuma na kitu
kinachitwa chambo, chambo ni ya mnyoo, anauvalisha kwenye
ndoano, samaki anapokuja haoni chuma ila anaona mnyoo, yeye
anaudaka na kuumeza ule mnyoo, akiisha meza ndio anasikia
kunaswa, mvuvi anachofanya anavuta ndoano inanasa Yule samaki,
mnyoo ule huwa umemaliza kazi yake, hapo samaki anajikuta tayari
Silaha za Adui Samuel Imori
11
yuko nje ya maji, ndoano memnasa Yule samaki tayari kwenda
kufanyika kitoweo
1Tim 2:24-26
Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi, balikuwa
mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu
akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana
Mungu awape kutubu na kuijua kweli, wapate tena fahamu zao
nakutoka katika mtego wa ibilisi, ambao hao wametegwa naye hata
kuyafanya mapenzi yake.
Mistari hiyo hapo juu inaelezea vizuri kwamba ibilisi anayo mitego,
nia yake ni kuwa nasa, kuwa kamata, wakristo kama vile mvuvi
anavyotumia mbinu za kumkamata samaki, kwa kutumia chambo
(mnyoo)
Vivyo hivyo huyu adui shetani naye anao ujuzi wa kuweza
kuwakamata wanadamu, anayo minyoo yake anayoivisha kwenye
ndoano yake ili awapate.
Shetani anayo minyoo yake anayoitumia kwasasa, au kwenye kitabu
hiki nitajikita kwenye mnyoo mmoja ambao umetumiwa na huyo adui
yetu kuwaangamiza watu wa Mungu.
Mnyoo huu unaitwa Fedha. (pesa)
Nimeeleza vizuri nilipotoa mfano wa mnyoo,mnyoo kama mnyoo
hauna tatizo lolote kwa wengine ni chakula kizuri sana, ukimwambia
Silaha za Adui Samuel Imori
12
mtu kuwa mnyoo, hata akikuuliza je waweza kutuambia ubaya wa
mnyoo ni nini?
Itakuwa vugumu kutamka ubaya wa mnyoo maana haupo, ila ukiuliza
idadi ya samaki waliokamatwa kwa kumeza ndoano iliyovalishwa
mnyoo, utakuta samakiwengi sana, mnyoo ulivalishwa juu ya ndoano,
samaki hakuona ndoano bali aliona mnyoo na akaumeza mnyoo ila
kumbe ndani ya ule mnyoo kulikuwa na ndoano.
Fuatana na mimi ninapokwenda kuuelezea mnyoo anaoutumia ibilisi
kuwaangamiza watu wa Mungu
“watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa”
Fedha ni nini? Biblia inaisemeaje fedha?.
Mhubiri 10:19
karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, na divai huyafurahisha
maisha, na fedha huleta jawabu la mambo yote.
Watu wengi wanapousoma mstari huo wanauchukua hivyo kwamba
ni jawabu la mambo yote.
Mtu akisema mambo yote ana maana gani?
Ukiuliza mambo yote maana yake nini?
Mtu anayeona karibu atasema mambo yote mazuri,nitakubaliana naye
kwa haraka haraka kwamba ni mambo yote mazuri, ukitaka kusafiri,
Silaha za Adui Samuel Imori
13
kula vizuri, kujenga nyumba nzuri, gari nzuri, chuo kizuri, yaani
chochote kizuri unacho kijua kuwa ni kizuri, unapopishana na
magari,unaweza ukalinganisha gari na gari kwa utofauti wa ubora
wake au gharama yake,unaingia hoteli ya bei juu,zingine unasikia
nyota tatu, nyota tano, n.k yote hayo inatajwa fedha,unaingia kwenye
ndege umakuta daraja la 1, la2, na la 3 yote hayo inatajwa fedha ndio
maana Biblia ikasema nijawabu.
Baada ya kukuonyesha uzuri kabisa wa fedha, nivizuri tuangalie
Biblia imesemeaje fedha, au imeizungumziaje-
1Tim 6:10
Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha,
ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani
nakujichoma kwa maumivu mengi.
Tumeanzia mstari huo unaosema vizuri waziwazi kwamba lipo shina
la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha(kuzipenda fedha)hapa
ndipo penye matatizo ndugu zangunimekuelekeza uzuri wa fedha,
jinsi inavyoweza kukufanyia mambo mazuri, kukusafirisha vizuri,
kukulisha vizuri, kukufanya ukanyage mahali ambako usingeweza
kabisa kukanyaga, fedha hiyo inakufanya utembelee gari ambayo
usingeweza kabisa kuitembelea bila fedha.
Nakwakuwa kila mtu anapenda vitu vizuri, asafiri vizuri, ale vizuri na
ukumbuke kinachosababisha hivyo vitu vizuri ni fedha na Biblia
imetuambia shina la mabaya yote ya kila namna ni kupenda fedha
Silaha za Adui Samuel Imori
14
Haikusema tusipende maisha mazuri, haikusema tusipende nyumba
nzuri,ila imesema tusipende fedha kwanini?
Kinacholeta mambo hayo yote yanayoitwa mazuri ni fedha.Na ili mtu
avipate hivyo, lazima aitafute fedha maana ndiyo inayoleta, na kama
fedha ndiyo inayoleta mambo mazuri inamlazimu mtu aipende na
kama akiipenda fedha, itamlazimu atafute kwa njia yeyote, hapo
ndipo unasikia wizi, unyanganyi, ujambazi, kutokuwa waaminifu,
ndio maana neno la Mungu limetuambia tusiipende fedha hiyo.
Ebr 13:8
Msiwe na tabia ya kupenda fedha, mwe radhi na vitu mlivyonavyo,
kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, sitakupungukia kabisa wala
sitakuacha kabisa.
Biblia inatueleza vizuri kwamba tabia ya kupenda fedha ni mbaya
sana, kama nilivyotangulia kusema kwamba mtu akiipenda fedha
ataitafuta kwa njia yeyote ile, iwe njia ya halali au iwe njia ya haramu
ilimradi tu anaipenda.
Neno la Mungu limetuambia kwamba Mungu wetu ametuahidi
kwamba hatatuacha kabisa, hatatupungukia kabisa, hii kauli ya neno
la Mungu kutuambia kabisa.Utakumbuka Bwana wetu Yesu akiwa
msalabani, alisema Baba mbona umeniacha?
Hakusema mbona umeniacha kabisa.
Silaha za Adui Samuel Imori
15
Hii inamaanisha kwamba Mungu wetu katika kutupitisha katika
masomo mbalimbali anaweza akatuacha katika masomo, ila
nikwamuda sio kabisa.
Isaya 54:7-8
Kwa kitambo kidogo nimekuacha, lakini kwa rehema nyingi
nitakukusanya.
Kwa ghadhabu ifurikayo nalikuficha uso wangu dakika moja lakini
kwa fadhili za milele nitakurehemu, asema Bwana mkombozi wako.
Hapo tumeendelea kuona kwamba kwa dakika moja Mungu aweza
kukuacha, lakini sio kabisa, kwa hiyo tunatakiwa kuwa wavumilivu
wakati tunapo pitia mambo magumu, tunapopitia taabu, mateso ya
aina yeyote, pengine nikupungukiwa, wengine nitaabu ya aina yeyote.
Zaburi 91:15
Ataniita nami nitamwitikia, nitakuwa pamoja naye taabuni,
nitamwokoa na kumtukuza.
Ndugu msomaji wangu hakuna mtu yeyote duniani awezaye kusema
kwamba anaipenda taabu, maana yake shida, mateso, hakuna mtu
ataipenda hali hiyo, lakini wale wanao safari kuelekea mbinguni
taabu kwao haiwafanyi wamwache Mungu, ila wata mwita Mungu
naye ameahidi kuwa pamoja nao katika taabu, ndipo awaokoe na
awatukuze. Kipindi hicho akiwepo taabuni hapo ndipo neno la
Mungu linasema atakaye vumilia mpaka mwisho ndiye ataokoka.
Mathayo 24:13
Silaha za Adui Samuel Imori
16
Lakini mwenye kuvumilia mpaka mwisho ndiye atakaye okoka.
Habari ya wokovu huu ambao Yesu aliuleta kuupata nirahisi tu,
nikumkiri Yesu na kumwamini unapata haki na wokovu.
Rumi 10:9-10
Kwa sababu ukimkiri Yesu kwa kinywa chako na kuamini moyoni
mwako kuwa Mungu alimufufua katika wafu utaokoka.
Hiyo ndio hatua anayopitia mtu anapata haki, na anapata wokovu,
ndio tukasoma hapo juu katika
Math 24:13
Kwamba atakaye vumilia mpaka mwisho ndiye ataokoka, kumbe
mtu anapookoka anatakiwa awe ameamua kutoka moyoni, vizuri
ajue kwamba ametoka katika utawala ule wa giza, amejiunga na
ufalme wa Mungu, mtu huyo atafahamu kwamba upande ule wa
pili unamtafuta ili umrudishe tena kwenye utumwana wengi
wamewezwa, nawakajikuta wanarudi kule walikotoka.
Wakati mwingine utajikuta unapitia hali ya kupungukiwa, unaweza
kupungukiwa vitu mbali mbali fedha ikiwa ni miongoni, hapo ndipo
Yule adui anapoweza kuleta kwako mnyoo (fedha) ili akunasie kama
mvuvi anavyo nasa samaki kwa kutumia mnyoo kama nilivyo eleza
hapo mwanzo
Filp 4:11-13
Silaha za Adui Samuel Imori
17
Sikwamba na sema hayo kwakuwa nina mahjitaji, maana
nimejifunza kuwa radhi na hali yeyote nilionayo, najua kudhikiwa,
tena najua kufanikiwa, katika hali yeyote na katika mambo yote,
nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na
kupungukiwa.
Mstari 13
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Mtume Paul anatufundisha waziwazi katika neno la Mungu, kwamba
amejifunza kuwa na hali iwayoyote, alijifunza njaa,shibe akahitimu
ndipo alipomalizia mstari 13, watu wengi wanakariri mstari huo
unaosema kuwa anayaweza mamboyote katika yeye aliyekuwa
anamtia nguvu.
Utakumbuka kule mwanzo katika kitabu cha mhubiri, tumesoma
unaosema”fedha ni jawabu la mambo yote”. Ndipo nikakumbuka
Biblia inaposema mambo yote,wengi wanatazama mazuri tu wala
hawaelewi kuwa nipamoja na mabaya yote, Paul nalieleza vizuri
akiwafundisha wafilipi akasema alikuwa amefundishwa kushiba,
kuona njaa, alikuwa amefundishwa kupungukiwa na akawa
amefundishwa kuwa navyo au kufanikiwa, ndipo akafikia uamuzi
huo yakwamba anayaweza mamboyote katika Yesu kristo, hii ni
kusema nini? akiwa na njaa bado ataendelea kuwa na Yesu, akishiba
bado shibe haitambadilisha amwache Yesu.
Hayo yote ni mafundisho ambayo sharti tuyapitie tunapofundishwa na
Mungu wetu.
Silaha za Adui Samuel Imori
18
Zab 30:6-8
Nami nilipofanikiwa nalisema, sitaondoshwa milele.Bwana, kwa
radhi yako wewe uliuimarisha mlima wangu. Uliuficha usowako,
nami nika fadhaika. Ee Bwana nalikulilia wewe, Naam, kwa
Bwana naliomba dua .
Ninaendelea kukuonyesha jinsi mafanikio yanayoletwa na kile
tulichokiona kikiitwa fedha, tumeona mtumishi wa Mungu Daud
akisema alipofanikiwa alisema hataondoshwa milele, hapo unaweza
ukaiona silaha nyingine inayojitokeza inaitwa “kiburi”anatamka
mdomoni mwake kuwa hataondoshwa, kwa lugha nyingine
atatamalaki wazi, ataishi milele. Mtu akitamka ati hataondoshwa
milele unaona wazi wazi kiburi na kiburi kinamfanya mtu asiendelee
kujifunza.
1kor 8:2
Mtu akidhani ya kuwa anajua neno hajui neno lolotebado, kama
impasavyo kujua.
Hii inatukumbusha kwamba tusichoke kujifunza, tusichoke kuongeza
elimu. Nakumbuka kunamsemo usemao”Elimu haina mwisho”
Mungu atusaidie kuendelea kuwa wanafunzi wa Yesu.
2YOH 1:9
Kila apitaye cheo wala asidumu katika mafundisho ya kristo, yeye
hana Mungu, yeye adumuye katika mafundisho hayo huyo ana
Baba na Mwana pia.
Silaha za Adui Samuel Imori
19
Haya yote ni mafundisho mazito kwamba mwanadamu sikuzote,
analo la kujifunza hakuna anayeweza kusema sasa nimemaliza
kujifunza , mmoja asema elimu ni bahari haimaliziki
Ukiwa wazi kuendelea kujifunza hautafikia kusema kama alivyo
sema mmoja kwamba alipofanikiwa alisema hataondoshwa milele,
alitakiwa aendelee kujifunza kwamba anapita katika dunia hii, na
akijua hilo mafanikio yasinge mlemaza kama yanavyo lemaza
wengine. Na mtu akishindwa kuelewa hivyo hatajiandaa nani rahisi
kiburi kumpata akadhani hatakufa,ebu tuone
Zab 89:47-48
Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wakudumu kwa ubatili gani
umeiumba jamii ya wanadamu. Ni mwanamme gani atakaye ishi
asione mauti , atakaye jiokoa nafsi yake na mkono wa kuzimu
Mwandishi wa zaburi hiyo hapo juu alijua kuwa siyo wa kudumu
alijua anapita katika ulimwengu huu na mtu akijua hivyo, basi atakaa
mkao wa kupita, atajiandaa, wengi hawajui hivyo , kumbuka hata
zamani salaam walizopewa wafalme ni uishi milele ee mfalme, na
kweli walikuwa wanaitikia, lakini kwa uhalisia nani ataishi milele?
Nani atakayeishi asiione mauti?
Tena swali aliloliuliza ni hili, mwanamme gani ataishi asiione mauti?.
Hakusema ni mwanadamu gani ataishi asiione mauti, alisema ni
mwanamme gani atakayeishi asione mauti? Yupo mmoja ambaye
ataishi milele na milele
Silaha za Adui Samuel Imori
20
Uf 1:17-18
Nami nilipo mwona nalianguka miguuni pake kama mtu aliye kufa.
Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, usiogope,
mimi ni wakwanza na wa mwisho, na aliye hai, nami nalikuwa
nimekufa na tazama ni hai hata milele na milele.Nami ninazo
funguo za mauti na za kuzimu.
Maandiko hayo yanamsema Yesu mwokozi, mwana wa Mungu
mwokozi wa ulimwengu , aliye tumwa kuja ulimwenguni kuwaokoa
wanadamu kutoka katika dhambi zao. Hayo maandiko yanasema
anaishi milele na milele na yeyote atakaye mwamini atampa uzima
wa milele. Na mara unapompokea unakuwa na uwezo wa kufanyika
mwana wa Mungu.
Yoh 1:12
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa
Mungu ndio wale waliaminio jina lake.
Ukisha mwamini ukafanyika, kuwa mwana wa Mungu, hapondipo
tayari unakuwa umefanyika kuwa askari, kama nilivyo tangulia
kusema kuwa askari sharti awe na silaha, anatakiwa ajue vizuri
kuitumia silaha yake na pia nikasema kuwa upande wa pili wao pia
wanazo silaha wanazo zitumia kupigana vita, hapo itategemea ni
askari yupi aliye fundishwa vizuri, huyo ndiye atashinda, kumbuka
mstari wetu ulio kibeba kitabu hiki ni ule usemao
Hos 4:6a
Silaha za Adui Samuel Imori
21
“watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa”
Mwizi huyu anayeitwa shetani nimekueleza kuwa anaomnyoo wake
anaoutumia kuwavulia watu na kuwatoa katika eneo wanalotakiwa
kukaa.kama vile samaki alivyoweza kuishi nchi kavu anapotolewa
majini, ndivyo na adui yetu anavyo watoa watu wa Mungu, walio
fanyika watoto wa Mungu kwenye eneo lao na ndipo
anapowaangamiza kama yanenavyyo maandiko.
Napenda tuendelee kuona mnyoo anaoutumia ambao nimekwambia
ni pesa, tutaendelea kuangalia Biblia ilivyoisemea pesa
Luka 16:14
Basi mafarisayo ambao wenyewe ni wapenda fedha, waliyasikia
hayo yote wakamdhihaki
Napenda tuangalie vizuri mstari huo, kumbuka Biblia imetuonya
kwamba tusiipende fedha ,madhara yake ni makubwa kama mtu
ataipenda fedha,
Mafarisayo walikuwa wanaipenda fedha na Yesu alipowahubiria,
mahubiri yake hayakuwafaa mafarisayo , kinyume chake
walimdhihaki, nini klichofanya wamdhihaki? Jibu ni rahsi sana –
walikuwa wanapenda fedha, unaona dhihaka ikazaliwa.
Silaha za Adui Samuel Imori
22
Yesu alikuwa ametuhubiri nini?
Luka 16:13
hakuna mtumishi awezaye kutumikia mabwana wawili kwa maana,
ama atamchukia huyu na kumpenda huyu, ama atashikamana na
huyo na kumdharau huyu, hamwezi kumtumikia Mungu na mali.
Biblia imesemea fedha kuwa ni bwana ikasema jinsi ilivyo vigumu
mtu kuwatumikia mabwana wawili Ooh! Kumbe Mungu ni Bwana na
Pesa ni bwana, unaweza ukaona cheo kingine cha fedha ni bwana;
naamini unaelewa maana ya bwana, Mheshimiwa, Mkubwa, Mzito,
wa Thamani, wa maana. Tunaendelea kuona jinsi Biblia ilivyotaja
fedha
Marko 14:11
Nao waliposikia walifurahi, wakaahidi kumpa fedha akatafuta njia
ya kumsaliti wakati wa kufaa.
Biblia inasema waliposikia walifurahi kwani walikuwa wamesikia
nini,
Marko 14:10
Yuda Iskariote, Yule mmoja katika wale Thenashala akaenda zake
kwa wakuu wa makuhani, apate kumsaliti kwao,
nadhani jibu tumelipata Yuda alenda akawaeleza kwamba yuko
tayari kumsaliti kwao, yaani kuwaonesha Yesu ili wamuue. Nao
waliposikia kwamba wamepata mtu atakayewaonesha wakafurahi na
Silaha za Adui Samuel Imori
23
waahidi kumlipa fedha kwa kazi hiyo, hapo unalo la kujifunza,
tunajifunza nini?
Yuda alitamanai apate fedha kwa njia ambayo aliona itamletea fedha
ni kumsaliti Mwokozi na ndivyo alivyofanya, na kweli aliipata, lakini
Biblia inatuambia kwamba mwisho wa siku alijuta kwa tendo hilo
hata fedha zile alizirudisha kwao wale waliompa nao walizikataa pia
mwishowe zikatupwa, mwisho wake utakumbuka kwamba
alijinyonga hakuweza kutubu dhambi hiyo ya usaliti na alifanya
hivyo ilia pate fedha.
Napenda tuendelee kutembelea Biblia kwa kuona baadhi ya mistari
inavyoongelea fedha
Mathayo 21:12
Yesu akaingia ndani ya hekalu akawafukuza wote waliokuwa
wakiuza na kununua hekaluni, akazipindua meza za wabadilisha
fedha na viti vyao waliokuwa wakiuza njiwa.
Hekalu ni mahali inapofanyika ibada na walikuwemo watu humo
wakifanya biashara, hapa tunajifunza nini? Tunajifunza kuheshimu
nyumba ya ibada, nyumba hiyo inatakiwa iheshimiwe Mungu wetu ni
mtakatifu, wao wale wamwabuduo wanatakiwa wamwabudu katika
Roho na Kweli. Na kwakuwa Mungu wetu hana upendeleo ndivyo
tunatakiwa tusiwapendelee watu katika hali zao, Yesu wetu
alipokuwepo duniani hakuwapendelea watu wenye vyeo wala wenye
fedha
Silaha za Adui Samuel Imori
24
Mathayo 22:15-16
Ndipo mafarisayo wakaenda zao wakafanya shauri jinsi ya kumtega
kwa maneno wakatuma kwake wanafunzi wao pamoja na
maherodi, wakasema mwalimu twajua ya kwamba wewe ni mtu wa
kweli na njia ya Mungu waifundisha katika kweli wala hujali cheo
cha mtu awaye yeyote kwa maana hutazami sura za watu
Mistari hiyo hapo juu inatundisha nini? Yesu alitufundisha jinsi ya
kuwa watu wa kweli, utakumbuka hata msemo wa kawaida wa
Kiswahli; “msema kweli ni mpenzi wa Mungu”, lakini utakumbuka
neno la Mungu linasema siku za mwisho watu hawataipenda kweli,
wataikataa na hilo ndilo linaendelea leo, Mtume Paulo alimwasa
mototo wake wa kiroho kuhusu siku hizo za mwisho
2 Timotheo 4:1-5
Nakuagiza mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu,
atakayewahukumu walio hai na waliokufa, kwa kufunuliwa kwake
na kwa ufalme wake, lihubiri neno, uwe tayari wakati ukufaao na
wakati usiokufaa,karipa,kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na
mafundisho, maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho
yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia
waalimu makundi makundi kwa kuwa wana masikio ya utafiti, nao
watajiepusha wasisikie yaliyo kweli na kuzigeukia hadithi za uongo,
bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya fanya
kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako.
Silaha za Adui Samuel Imori
25
Mtume Paulo aliziona siku za mwisho ambazo ndizo tulizonazo leo,
watu hawataki kweli watu wanataka maneno sio Neno, unajua
maneno hayambadilishi mtu, neno la Mungu ndilo peeke linaloweza
kumbadilisha mtu, mpaka afanane na Yesu, yeye Bwana Yesu
tumesikia kuwa hakujali cheo cha mtu wala sura ya mtu yeyote.
Anaposema cheo hapo anasema fedha, maana ukisikia mtu kapanda
cheo, hapo ujue inatamkwa fedha na ukisikia hakutazama sura ya
mtu, anamaanisha nini? Nilikuwa nimetembelea nchi moja na
nilipokuwa huko nilitamani kwenda ibadani, mwenyeji wangu
aliniuliza swali hili”ungependa kusali katika kanisa la mchungaji
kabila gani? nilishangaa kwa swali hilo, akaendelea kusema waumini
wao wahuko wanakwenda kushiriki ibada ya mchungaji kabila
yao,unaona hao walikuwa wanatazama sura, kabila n.k.siku moja
naikumbuka, nilikuwa safarini jumamosi usiku gari yetu
ilituharibikia,jumapili ikatukuta na ilionekana tutakaa pale jumapili
yote, jumatatu spare itakapokuwa imeletwa ,na tulitembea kwa mguu
kidogo tukaingia mjini, Mungu bariki tukakuta kanisa,nilifurahi sana.
Vyombo vilisikika vikiimba kwa uzuri kabisa, naukumbuka wimbo
niliousikia ni huu;-
“nyimbo na tuziimbe tena, za alivyotupenda mbele, kwa bei ya
dhamani sana mbinguni huonana milele.”
Nilifurahi sana, nilienda nikaingia, nikakuta watu wachache, viti
vingi,nikaelewa kuwa bado wataendelea kuja. Niliingia nikanyoosha
moja kwa moja nikaenda kwenye viti vile vya mbele,sio kwa
wachungaji,viti vya mbele kwa wakristo nilipofika nilikaa, kama
ilivyo kawaida nilimshukuru Mungu, nikamaliza nikakaa sawa, mara
Silaha za Adui Samuel Imori
26
alikuja shemasi kwangu, akanisalimia, akaniomba niinuke nimfuate,
nilitii, alinitangulia kuelekea nyuma ya kanisa, akanionyesha kiti cha
nyuma kidogo kutoka kile nilicho kuwa nimekaa, akaniambii kaa
hapa, sikupapenda nilitamani nikae pale mbele niwezekumsikiliza
mhubiri vizuri, nikamuuliza kwanini unaniweka huku akanambia viti
vile nivya watu maalumu, wale wanao toa sadaka kuanzia 20,000/=
niwatu wazito, nilishangaa, nilikaa nikatulia kweli walianza
kuingia,walikuwa wazito ukiwatazama hata mavazi yao tu, nilisema
kweli hawa niwa 20,000/=ndipo nilipo elewa kile Yakobo
alichokiandika. Ndugu zangu imani ya Bwana wetu yesu kristo,
bwana wa utukufu, msiwe nayo kwa kupendelea watu, maana
nikiingia katika sinagogi lenu mtu mwenye pete ya dhahabu, na
mavazi mazuri kasha akiingia na maskini, mwenye mavazi mabovu
nanyi mkimstahi Yule aliye vaa mavazi, mazuri na kumwambia keti
wewe hapa mahali pazuri na kumwambia Yule masikini simama
wewe pale, au keti miguuni pangu, je hamkufanya hitilafu mioyoni
mwenu mkawa waamuzi wenye mawazo mabovu? ndugu zangu
wapenzi sikilizeni je Mungu hakuwachagua masikini wa dunia wawe
matajiri wa imani na warithi wa ufalme alio waahidia wampendao,
bali ninyi mmemvunjia heshima maskini, je matajiri hawawaonei na
kuwavuta mbele ya viti vya hukumu? Neno la Mungu wetu linasema
kwamba Mungu hana upendeleo, inakuwaje watu wake wanakuwa na
upendeleo, wanapendelea watu kwa kuwatazama sura zao, jinsia
zao,vyeo vyao ,urefu wao, udogo wao, utu uzima wao. Haifai kuwa
hivyo, Mungu atusaidie.Tunaendelea kuitembelea Biblia
ikitufundisha kuhusu fedha ambayo nimesema kwamba ni munyoo
ambao shetani anautumia, kama vile mvuvi anavyotumia mnyoo
kumnasa samaki.Nimesema mnyoo kama mnyoo hauna tatizo,wala
Silaha za Adui Samuel Imori
27
sio mbaya, ila ukimuuliza samaki au ukitafuta idadi ya samaki
walio vuliwa kwasababu walikula au walimeza mnyoo ni wengi mno,
fedha nayo kama fedha haina tatizo, wala fedha sio mbaya, wala
haina ubaya wowote ninzuri, lakini ukiuliza idadi ya watu
walioangamizwa na adui kwakutumia fedha ni wengi mno, na
tutaendelea kuangalia ili tupate kujifunza neno linalosema, yale
yaliyofunuliwa ni yetu ili tuyafanye pamoja na watoto wetu.
Kumb 29:29
Mambo ya siri niya Bwana, Mungu wetu; lakini mambo
yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu mileleili tuyafanye
maneno yote ya sharia hii.
Ndugu msomaji wangu mahali pale ambapo Biblia imekaa kimya
nasi tunapaswa kukaa kimya, pale ambapo imeongea ikatuelekeza
twapaswa kufanya vivyo hivyo au vile inavyo tuelekeza, vingine tuta
ongeza au tutapunguza na tukifanya hivyo, yenyewe inajisemea au
inajilinda kwa vile inavyo kataza.
Mith 30:5-6
Kila neno la Mungu limehakikishwa yeye ni ngao yao
wamwaminio, usiongeze neno katika maneno yake; asije
akakulaumu, ukaonekana umwongo.
.watu wengi wamelaumiwa na Mungu na wameonekana waongo pale
walipo punguza neno la Mungu na wengine wameonekana waongo na
Mungu amewalaumu pale pale walipo liongeza neno la Mungu.
Silaha za Adui Samuel Imori
28
Kumb 4:2
Msiliongeze neno ni waamurulo, wala msilipunguze,mpate
kuzishika amri za Bwana Mungu wenu niwaamuruzo.
Yapo mambo ambayo Mungu amewaamuru wanadamu, ni juu yao
kuyafanya au kuto kuyafanya, yote hayo yapo kwenye uwezo wa
mwanadamu, Mungu wetu hamlazimishi mtu,amempa uhuru wa
kuchagua.
UF 22:18-19
Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu
hiki, mtu yeyote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo
yalioandikwa katika kitabu hiki,na mtu yeyote akiondoa lolote
katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea
sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji
mtakatifu,ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki.
Nimetangulia kukwambia ya kwamba Biblia haikuachwa tu bila
ulinzi, maana kila mtu angeingia tuu apunguze jambo, angeingia tu
aongeze jambo, lakini Mungu akaweka ulinzi, na inatulazimu tutii,
tufanye vile inatuagiza. Tunaendelea kuangalia inazungumzia nini
kuhusu fedha, kumbuka mstari muhimu ulio tufikisha hapa ni
Hosea 4:6a
“watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa”
Silaha za Adui Samuel Imori
29
Yoh 2:14-16
Akaona pale hekaluni watu waliokuwa wakiuza ng’ombe na
kondoo na njiwa na wenye kuvunja fedha wameketi,akafanya
kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na
ng’ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha,akazipindua
meza zao akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, yaondoeni
haya,msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara.
Mungu atusaidie tuone kile Bwana wetu Yesu alichofanya, na
watuwengi wameshidwa kuelewa alichokifanya, neno la Mungu
linasema sisi ni hekalu la Bwana, ni nyumba ya Mungu, Mungu wetu
anatamani akae katika hekalu lake, ambalo ndilo sisi, yaani kanisa,
nakama ndivyo tunatakiwa kulisafisha liwe safi, vinginevyo hatakaa,
meza zilizomo zinatakiwa kupinduliwa, njiwa waliomo, fedha zinazo
badilishwa humo zinatakiwa kumwagwa
Gal 5:19
Bali matendo ya mwili ni dhahiri ndio haya, uasherati, uchafu,
ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira,
fitina faraka, unafiki, uzushi, husuda, ulevi, ulafi na mambo ya
nayofanana na hayo, katika hayo na waambia mapema kama
nilivyokwisha kuwaambia ya kwamba watu watendao mambo ya
jinsi hiyo hawata urithi ufalme wa Mungu.
Msomaji wangu tume muona Yesu akipindua meza alizozikuta
hekaluni hakukubaliana biashara ziendelee kwenye nyumba ya Baba
yake, na nimekuelezea kwamba nyumba ya Mungu sio ile ya
Silaha za Adui Samuel Imori
30
matofali, ni mioyo yetu ndio hii inaitwa kanisa, linatakiwa liwe safi
lisiwe na hila, lisiwe na doa lolote ndio kazi Yesu aliokuja kuifanya
chini ya jua.
Efeso 5:25-27
Enyi waume wapendeni wake zenu kama kristo naye alivyo lipenda
kanisa,akajitoa kwaajili yake,ili makusudi alitakase na kulisafisha
kwa maji katika neno,apate kujiletea kanisa tukufu,lisilo na
ila,wala kunyanzi wala lolote kama hayo;bali liwe takatifu lisilo na
mawaa.
Katika kitabu changu cha” kanisa ni nini”,nimeeleza vizuri kanisa ni
nini, watu wengi kwakuto kujua,wanajitahidi sana kuwa watakatifu
wakati wanapokuwa kwenye nyumba ya ibada pale wanatembea kwa
upole sana ,ukiwauliza ni kwanini wanafanya hivyo,wanasema ni
kwasababu wapo kanisani, maana wamepotoka hapo,utashangaa
wakiwa mbali na nyumba ya ibada wanaweza wakaongea
vyovyote,wakatenda vyovyote,akiwa mbali na nyumba ya ibada
anaweza akanywa kilevi, lakini akiwa katika nyumba ya ibada kamwe
hawezi kunywa kilevi, ukimuuliza atakwambia nyumba ya ibada
sharti iheshimiwe, hawajui yakwamba wao ndio nyumba ya Mungu
ya ibada, kwamba wao ndio kanisa, ndio hekalu la Mungu,na hekalu
linatakiwa liwe safi kama tulivyo tangulia kuona hapo juu.
1Kor 6:19-20
Au hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho mtakatifu aliye
ndani yenu, mliye pewa na Mungu? wala ninyi sio mali yenu
Silaha za Adui Samuel Imori
31
wenyewe,maana mlinunuliwa kwa thamani, sasa basi mtukuzeni
Mungu katika miili yenu.
Msomaji wangu tunatakiwa tuwe tayari wakati wowote,tuwe safi siku
zote sio jumapili, au jumamosi peke yake, ni siku zote.sikumoja
wanafunzi wa Bwana Yesu walimuuliza awaambie atakuja
lini.Walitamani wajue mpaka siku, lakini Yesu alisema hata yeye
hajui siku hiyo,a liwaambia dalili za kuja kwake, soma hapa chini
Math 24:36
Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna ajuaye, hata malaika
walio mbinguni, ila Baba peke yake
Mstari huo unanifanya niwaze sana, Mungu wetu ni waajabu ukweli
unabaki pale pale,kamaYesu angewaambia siku ya kuja na saa ya
kuja kulinyakuwa kanisa, naamini watuwengi sana wangeweza
kwenda naye,wangejiandaa muda ambao wangejua siku zimebaki
chache na saa chache, ndio wange kusanyika tayari kwa safari ya
mbinguni tayari kwa unyakuo. Fikiri kidogo ingekuwaje, nyumba za
ibada zisingetosha sikuhiyo.Wengine wangekuja imebaki siku moja,
wengine mpaka ingebaki saa moja, wengine hata dakika 10au5.
Haingekuwa na maana, wala wala wasingekuwa wanampenda
Mungu, bali wange kuja tukwa kuwa muda huo umefika, mpaka
Bwana Yesu anasema hakuna aijuaye hata malaika, hata mwana pia
ila Baba pekeyake, japo alijitahidi kuzitaja dalili za kuonyesha
kwamba siku hiyo imekaribia, na sasa tunaziona zikitimia moja baada
ya nyingine. Na mtumishi wa Mungu Paul pia aliona vyema
amuelezee kijana wake siku hizo za kumalizia atazijuaje
Silaha za Adui Samuel Imori
32
2Tim 3:1-7
Lakini fahamu neno hili ya kuwa siku za mwisho kutakuwako
nyakati za hatari, maana watu watakuwa wenye kujipenda
wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi,
wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio
safi, wasio wapenda wakwao, wasio taka kufanya suluhu,
wasingiziaji, wasio jizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti,
wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda
Mungu, wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake, hao
nao ujiepushe nao.Kwamaana katika hao wamo wale wajiingizao
katika nyumba za watu, na kuchukua mateka, wanawake wajinga
wenye mizigo ya dhambi, walio chukuliwa na tama za namna
nyingi, wakijifunza sikuzote,ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa
ile kweli.
Msomaji wangu mpendwa unayesoma kitabu hiki, yawezekana bado
ulikuwa hauja zijua dalili za kurudi kwa Yesu kulinyakuwa kanisa,
alisema atatokea kama mwizi, mwizi hatoi taarifa ya lini anakuja
kuiba, mwizi anakuja ghafla na ndivyo Bwana wetu atakuja ghafla
kulichukua kanisa, kulinyakua, siku ambayo itakuwa ya kutisha,
sikuhiyo vitatokea vifo vya kutisha, fikiri kidogo,mtu atakuwa ndani
ya bus na dereva ameokoka,kanisa likinyakuliwa,dereva nae ata
nyakuliwa, ataliacha bus liendelee pamoja na wasafiri litaishia wapi?
fikiri kidogo ndege itakuwa angani ,wakati huo pailot atakuwa
ameokoka, atanyakuliwa, ndege hiyo itakuwa na abiria fikiri kidogo
mwisho wake utakuwa ni wapi? pengine itakuwa ni treni, dereva
wake ameokoka, ananyakuliwa , treni inabaki inaendelea na
Silaha za Adui Samuel Imori
33
safari,ukweli ni kwamba itakuwa siku ya kutisha, ndio maana
unashauriwa uwe mtakatifu siku zote, masaa yote na dakika zote,
ndio maana Bwana Yesu akasema watu wake wakeshe ,wawe macho,
wawe tayari, wakae mkao wa kuondoka.Mtume Paul
alimtahadharisha mtoto wake kwa kumuelezea atakavyo utambua
wakati huo utakapokuwa umefika, ebu zipitie dalili hizo zote moja
baada ya nyingine uzitafakari kwa undani, sitazielezea kila moja ila
ile moja inayo husu fedha, akaisema”watu watapenda
fedha”.Msomaji wangu, nilielezea hapo mwanzoni kwamba neno la
Mungu linatukataza kuzipenda fedha, nikaelezea kwamba fedha kama
fedha haina tatizo ila tatizo ni kuipenda ,nikasema nikasema ikitokea
ukakubwa na roho hiyo ya kuipenda fedha, utaitafuta kwa hali yoyote
hata ya aibu utaipokea.
1Tim 3:8
Vyivyo hivyo mashemasi nao wawe wastahivi si wenye kauli mbili,
si watu wa kutumia mvinyo sana, si watu wanaotamani fedha ya
aibu.
1Pt 5:2
Lichungeni kundi la Mungu lililokwenu, na kulisimamia, si kwa
kulazimishwa bali kwa hiari kama Mungu atakavyo, sikwakutaka
fedha ya aibu bali kwa moyo
Mdo 24:26
Pamoja na hayo alitaraji kwamba atapewa fedha na Paul, kwa hiyo
alimwita mara nyingi akaongea naye.
Silaha za Adui Samuel Imori
34
Neno la Mungu halikubaliani na rushwa lakini utakubaliana na mimi
kwamba rushwa imeuwa wengi, hata watumishi wa Mungu,
wanapofikia mahali pakusimama kidete kuipinga, rushwa
wanaharibiwa na wanaotoa. Mtumishi wa Mungu Paul hakukubaliana
na rushwa, yeye alikuwa tayari kusimama katika kweli
Mdo 20:33
Sikutamani fedha wala dhahabu, wala mavazi ya mtu.
Hili limekuwa tatizo kubwa katika siku zetu tulizonazo, watumishi
wengi wa Mungu wametamani mali za washirika wao, wametamani
fedha za washirika wao, wametamani nyumba, mavazi ya washirika
wao bila aibu wengine wamewaomba mali, wazi wazi wamegeuka
omba omba.
Mdo 8:18-20
Hata Simon alipoona ya kuwa watu wanapewa roho mtakatifu kwa
kuwekewa mikono ya mitume akataka kuwapa fedha akisema,
nipeni na mimi uwezo huu, ili kila mtu nitakaye mweka mkono
wangu apokee roho mtakatifu, lakini Petro akamwambia fedha
yako naipotelee mbali pamoja nawe kwa kuwa umedhania ya kuwa
karama ya Mungu ya patikana kwa mali, huna fungu wala huna
sehemu katika jambo hili, kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za
Mungu.Basi tubia uovu wako huu ukamwombe Bwana ili kama
yamkini usamehewe fikira hii ya moyo wako, kwamaana nakuona
ukatika uchungu kama nyongo, na tena ukatika kifungo cha uovu,
Silaha za Adui Samuel Imori
35
Simion akajibu akasema.Niombeeni ninyi kwa Bwana, yasinifikilie
mambo hayo mliyosema hata moja.
Msomaji wangu unawezaukaona fedha inavyo weza kumfikisha mtu
aliye nayo, Simioni alisukumwa kwa ndani ampe mtume fedha, lakini
kwakuwa mtume wa Mungu wakweli alikuwa na macho ya rohoni,
hakuikubali fedha ile, macho yake yalifunguka, akaona uovu katika
moyo wa Simioni, akaona vifungo vya uchungu kama nyongo, wala
fedha zake hazikumsaidia, ndivyo ilivyo hata leo, wako watu
wamewaweka wachungaji mifukoni hata wange tenda dhambi
hawasemwiwengine mpaka wana vilabu vya pombe, lakini bado
niwatu wenye vyeo makanisani.Hawaguswi, hawaonywi,
hawakemewi, Petro akamwambia Simioni apotelee mbali na fedha
yake, kwa kuwa alidhani kwamba ufalme wa Mungu unapatikana
kwa mali, kama wengi wanavyodhani kwamba wanapokuwa na fedha
ni wa muhimu sana kuliko wengine wale wasio na fedha, kwa njia
hiyo wakadhani kwamba waweza wakafanya lolote na wasifanywe
lolote, Mungu atusaidie, atuhurumie, atupe macho ya rohoni,
tuwafungue watu waone, kama alivyo funguliwa Simioni na akahitaji
maombi, naamini alipata rehema, akaelewa yakwamba fedha haiwezi
kununua uzima wa milele, fedha haiwezi kununua ufalme wa Mungu,
vitu hivyo havilinganishi na chochote chini ya jua. Msomaji wangu
wa kitabu hiki kumbuka yakwamba kila andiko lenye pumzi ya
Mungu lafaakwa mafundisho na kuwaonya wanadamu.
2Tim3:16
Kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa mafundisho, na kwa
kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kuwa
Silaha za Adui Samuel Imori
36
adibisha katika haki ili mtu wa Mungu awe kamili,amekamilishwa
apate kutenda kila tendo jema.
Nimeelezea jinsi Biblia inavyoongelea fedha, inavyoelezea, nikasema
fedha kama fedha sio mbaya wala haina ubaya wowote, ila fedha
hiyo kama mtu akiipenda, matokeo yake hayawi mazuri.
1Tim6:17-19
walio matajiri wa ulimwengu wa sasauwaagize wasijivune, wala
wasiutumainie utajiri usio yakini, bali wa mtumaini Mungu
atupaye vitu vyote kwa wingi ili tuvitumie kwa furaha,
watendemema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari
kutoa malizao, washirikiane na wengine kwa moyo, huku
wakijiwekea akiba iwe msingi mzuri kwa wakati ujao, ili wapate
uzima ulio kweli kweli.
Biblia inayo mambo mengi yakumfundisha mwanadamu aliyeubwa
kwa mfano wa Mungu. Maandiko hayo yanapeleka ujumbe kwa
matajiri wa ulimwengu huu kwamba waagizwe wasijivune,
auwasiringe, wasiuumainie utajiri wao, wasiutegemee utajiri,
wasiishie hapo wakaridhika na hali hiyo, bali wamtafute Mungu,
ufahamu wao uende zaidi ya huo utajiri wao wasidhani wataishi
milele, kama mmoja aliyefanikiwa akatamka kuwa hataona mauti.
Zab 30:6
Nami nilipofanikiwa nalisema sitaondoshwa milele.
Silaha za Adui Samuel Imori
37
Nakumbuka wakati Mungu alipokuwa amekusudia kuwabariki watu
wake, alipotaka kuongeza mali, walizokuwa nazo alitangulia
kuwaonya, kuwatahadharisha akawapelekea ujumbe
Kumb 8:11-20
Jihadharini usije ukamsahau Bwana Mungu wako kwakuto
kuzishika amri zake, na hukumu zake, na sharia zake,
ninazokuamuru leo,angalia utakapokuwa umekula na kushiba,na
kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake, na makundi yako ya
ng’ombe na kondoo yatakapo ongezeka, na fedha yako,na dhahabu
yako itakapoongezeka, na kilakitu ulichonacho kitakapoongezeka,
basi hapo moyowako usiinuke ukamsahau Bwana Mungu wako
aliyekutoa katika nchi ya misri, katika nchi ya utumwa,
aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka
za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji, aliyekutolea maji
kwenye mwamba mgumu, aliye kulisha jangwani kwa mana, wasio
ijua baba zako apate kukutweza, apate kukujaribu, ili kukutendea
mema mwisho wako.Hapo usiseme moyoni mwako nguvu zangu na
uwezo wa mkono wangu ndio ulionipatia utajiri huo,bali
utamkumbuka Bwana Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu
za kupata utajiri, ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako
kama hivi leo, lakini itakuwa, kama ukimsahau Bwana Mungu
wako na kuiandama miungu mingine, na kuitumikia na kuiabudu,
nawashuhudia leo ya kuwa mtaangamia bila shaka. Kama vile
mataifa yale ambayo Bwana anawaangamiza mbele yenu ndivyo
mtakavyo angamia, kwa sababu hamkutaka kuisikiliza sauti ya
Bwana Mungu wenu.
Silaha za Adui Samuel Imori
38
Kama nilivyotangulia kukuarifu kwamba fedha mara nyingi adui yetu
huitimia kama vile mvuvi anavyotumia mnyoo kumvua samaki, na
hapo juu tumeona vizuri Mungu wetu akiwapatia watu wake
maelekezo, anawaambia ya kwamba anaompango mzuri kabisa
kwaajili yao katika siku zao za usoni, siku zao za mwisho, ni mpango
wa kuwabariki, nimpango wa kuwainua, na kwakuwa anawapenda,
inamlazimu awatahadharishe mapema, amewajulisha waziwazi
kwamba chochote walichonacho kitaongezeka, ng’ombe, fedha,
dhahabu, n.k. Mungu wetu anatupenda sana na kwakuwa anatupenda
anajua alivyo tuumba, akatutengenezea mioyo na hakuacha
kututaarifu moyo ulivyo, katika kuelezea hali ya miili yetu alisema
hivi:-Mguuwako ukikukosesha uukate, mkono wako ukukukosesha
uukate, lakini alipofika kwenye moyo hakusema uukate, akasema
uulinde sana moyo kuliko kitu kingine chochote unachokilinda
hakutaka kuishia hapo alitoa sababu. Sababu aliyoitoa ni kwa kuwa
ndiko zinitoka chemichemi za uzima, hakusema uukate moyo,
hauwezi kukatwa. Katika kitabu change cha vikwazo vya kuurithi
uzima wa milele sehemu ya kwanza, nime uelezea moyo kirefu.
Mith 4:23
linda moyo wako kuliko vyote ulindavyo,maana ndiko zitokako
chemichemi za uzima.
Ni kwanini tunatakiwa kuulinda kuliko kiungo chochote?
Silaha za Adui Samuel Imori
39
Yer 17:9
moyo huwa ni mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa
kufisha nani awezaye kuujua.
Utakumbuka tumesikia Mungu akiwaelezea watu wake kwamba
watakapokuwa wamevuka, watakapokuwa wamefanikiwa kwa kila
kitu, mali zitakapoongezeka mioyo yao isiinuke, wakamsahau
Bwana, unaweza kusikia vile mafanikio yanavyoweza kusababisha
moyo wa mtu ukainuka, na ukamsahau Mungu aliye kuwezesha, aliye
kufanikisha kwenye hayo mafanikio.
Math 19:16-26
Na tazama mtu mmoja akamwendea akamwambia, mwalimu
nitende jambo gani jema ili nipate uzima wa milele? Akamwambia
kwani kuniuliza habari ya wema?Aliye mwema ni mmoja.Lakini
ukitaka kuingia katika uzima ishike amri:-Akamwambia zipi? Yesu
akasema ni hizi, usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo,
waheshimu baba yako na mama yako, nampende jirani yako kama
nafsi yako, Yule kijana akamwambia, haya yote nimeyashika,
nimepungukiwa na nini tena? Yesu akamwambia, ukitaka kuwa
mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape masikini,nawe
utakuwa na hazina mbinguni, kasha njoo unifuate, Yule kijana
aliposikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni,kwa sababu alikuwa
na mali nyingi, Yesu akawaambia wanafunzi wake,amini
nawaambieni yakwamba itakuwa shida kwa tajiri kuingia katika
ufalme wa mbinguni. Nawaambia tena, nirahisi zaidi ngamia
kupenya kwenye tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika
Silaha za Adui Samuel Imori
40
ufalme wa Mungu. Wanafunzi waliposikia walishangaa
mno,wakisema ninani basi awezaye kuokoka. Yesu akawakazia
macho, akawaambia kwa wanadamu hilo haliwezekani, bali kwa
Mungu yote yanawezekana.
Maelezo tuliyoyasoma hapo juu, umeona waziwazi kijana tajiri,
naamini alipokuja kwa Bwana Yesu alikuwa tayari kufanya lolote
ambalo Bwana angemweleza afanye, pengine angefika Bwana
amwambie atoe sadaka, au mchango, naamini angekuwa tayari, lakini
kile alichoagizwa kilimshinda,unaweza okaona jinsi mali inavyo
weza kukaa kwenye moyo wa mtu, ikautawala, akaipenda, kumbuka
tulisoma kwamba tusiipende, maana ukiipenda hautakubali kuiachia,
utaishikilia, itafanyika kama ndio kimbilo lako, Mungu hatapata
nafasi katika moyo wako, nyaraka zingine, zinasema kuwa kijana
baada ya kusikia hivyo, alikasirika, akakunja uso wake akaondoka.
Hakutaka tena kuendelea kumsikiliza Yesu akifundisha, hilo lilitosha
kumfukuza, akakosa amani, akaona jibu ni kuondoka, akaona hawezi
kuikosa mali, akaona vema akose mbimgu lakini abaki na mali. Hiyo
ndio hali ya matajiri wengi mioyo yao imewekwa kwenye mali,
ndiomaana mahali pengine imeandikwa hazina yako ilipo ndipo na
moyo wako ulipo.
Luk 12:16-21
Akawaambia mithali akisema, shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa
limezaa sana, akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema nifanyeje?
Maana sina pakuyaweka akiba mavuno yangu. Akasema nitafanya
hivi, nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa kubwa zaidi,
na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu, kisha
Silaha za Adui Samuel Imori
41
nitajiambia , ee nafsi yangu una vitu vyema vingi ulivyojiwekea
akiba kwa miaka mingi, pumzika basi, ule, unywe,ufurahi, lakini
Mungu akamwambia,mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka
roho yako,na vitu ulivyo jiwekea tayari vitakuwa vya nani? Ndivyo
alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.
Kama nilivyotangulia kusema kwamba yaliyofunuliwa kwetu niyetu
na watoto wetu tuyafanye, ukweli unabaki palepale kwamba duniani
ni mahali pa kupita, tukielekea mahali petu pa kudumu, mahali pa
milele. Mahali pa milele pa mwanadamu pameandaliwa, ni mahali
pawili tu , motoni na mbinguni pote hapo ni pa milele, hapa duniani
tunazo mali za hapa hapa duniani, hatutakwenda nazo mbinguni, na
utakumbuka anayetuchagulia pa kwenda kati yapawili sio Mungu
wala sio shetani ni kila mtu amepewa achague, amepewa uhuru huo,
hili ni jambo ambalo watu wengi hawajui, na wakajikuta
wanadanganywa kwamba wanaweza wakaombewa na wakawekwa
mahali pema peponi, ngoja tujifunze kidogo kuhusu hilo la
uchaguzi.Kitabu hiki kimekufikia kwa makusudi maalumu uweze
kuelewa kwamba umepewa uhuru huo wa kujichagulia mahali
utakapoishi milele na milele
Kumb 30:15-18
Angalia nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na
mabaya kwa hivi nikuagizavyo leo kumpenda Bwana Mungu wako,
kuenenda katika njia zake, na kushika maagizo yake na amri zake
na hukumu zake, upate kuwa hai na kuongezeka, Bwana Mungu
wako apate kukubarikia katika nchi uingiayo kuimiliki. Lakini
Silaha za Adui Samuel Imori
42
moyo wako ukikengeuka, usipotaka kusikia, lakini ukavutwa kando
kwenda kuabudu miungu mingine, na kuitumikia, nawahubiri hivi
leo hakika mtaangamia, hamtazifanya siku zenu kuwa nyingi juu
ya nchi, uivukiayo Yordani, uingie kuimiliki.
Mungu wetu hamlazimishi mtu kumtii ila kama tulivyosoma hapo
juu, amemuwekea uchaguzi mbele yake, achague aidha amtii au
asimtii, napenda nikufungue macho, katika dunia hii wapo miungu
wengi, mmoja wapo ni shetani, anajulikana kama mungu wa dunia hii
na kwa kuwa miungu wako wengi twapaswa kuwa makini na unajua
miungu inapenda kuabudiwa, watu wanaiabudu pengine bila kujua,
wakidhani ndiyo Mungu wa kweli lakini Mungu wa kweli, wa pekee
yupo yeye ambaye ndiye muumba mbingu na nchi, ndiye aliepanga
mahali ambapo watu wataishi milele na milele ndiye huyo ninaye
sema habari zake nawakati alipokuwa anampatia mwanadamu nafasi
ya kuchagua,aliweka nchi iwe shahidi,aliweka anga liwe shahidi, kwa
hiyo mwanadamu anapochagua vibaya au vizuri mashahidi wapo.
Kumb 30:19
Nazishuhudia mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa
nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, Baraka na laana, basi
chagua uzima, ili uwe hai wewe na uzao wako, kumpenda Bwana
Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushika maneno yake kwani hiyo
ndio uzima wako, na wingi wa siku zako,upate kukaa katika nchi
Bwana aliyowaapia baba zako, Ibrahim na Isaka na Yakobo kuwa
atawapa.
Silaha za Adui Samuel Imori
43
Nimesema kwamba Mungu wetu anatupenda kwa sababu alituumba
kwa mfano wake, anatupenda upeo, hapendi mtu yeyote apotee ndio
maana akatuwekea mbele yetu tuchague, bado akatushauri kuwa
chagueni uzima, yaani kumtii, yaani kumheshimu yeye.Hata
alipoandaa moto wa milele ambao waliomkataa wataishi milele,
aliweka utaratibu wa jinsi watakavyotupwa humo, mwanadamu
atakuwa wa mwisho kabisa kutupiwa humo kwenye moto wa milele
(Jehanam) hii inatuonyesha wazi wazi kwamba Mungu hakupenda
mwanadamu aishi motoni milele, ebu tuangalie mpango wa kutupwa
humo motoni utakuwaje, naandika hii kwasababu wapo watu
wasemao ya kwamba hakuna jehanam,kwamba hakuna moto wa
milele.
Uf 19:20
Yule mnyama akakamatwa, na Yule nabii wa uongo pamoja naye,
yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo
aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama,
nao walioisujudia sanamu yake, hao wawili wakatupwa wangali hai
katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti.
Kama nilivyosema wapo watu wanadanganya watu ya kwamba
hakuna ziwa la moto, Biblia imetamka wazi wazi kuwa hao watajwa
hapo juu ndio watakao tangulia. Nani tena atafuata? tuendelee
kujifunza.
Uf 20:10
Silaha za Adui Samuel Imori
44
Na Yule ibilisi mwenye kuwadanganya, atatupwa kwenye ziwa la
moto na kibiriti, alimo Yule mnyama na Yule nabii wa uongo, nao
watateswa mchana na usiku hata milele na milele.
Tunaendelea kumwona shetani akiwafuata katika huo moto wa
milele, na baada ya hayo, nani tena atafuata?
Uf 20:14
Mauti na kuzimu Zikatupwa katika lile ziwa la moto.Hii ndio mauti
ya pili, yaani hilo ziwa la moto.
Mauti ni nini? mauti ni kifo, ni roho inayombeba mwanadamu,
tunaposema mtu amekufa, huwa amechukuliwa na roho inayoitwa
mauti, hiyo roho ikiisha kumchukua mtu inampeleka mahali
panapoitwa kuzimu, kuzimu ni wapi? Ni mahali ambapo roho zisizo
na Mungu zinatunzwa zikingojea kutupwa katika ziwa lile la moto
tulilolisoma hapo juu kwa hiyo huyo mauti na huyo kuzimu,
watatupwa kwa pamoja katika hiloziwa la moto wa milele na milele,
inaitwa ziwa la moto
Nani tena atafuata? nimeendelea tena kukuelezea habari ya ziwa la
moto wa milele na milele,tumeendelea kumsikia Mungu katika neno
lake, akitushauri tuchague kumcha yeye, na tukichagua kumcha yeye,
tutakuwa tumeepuka hilo ziwa la moto wa milele na milele.Nani tena
atafuata?
Uf 20:15
Silaha za Adui Samuel Imori
45
Na iwapo mtu yeyote hakuoenekana ameandikwa katika kitabu cha
uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.
Hapo ndipo tumeona mwanadamu akiwa wa mwisho kutupwa humo
katika lile ziwa la moto wa milele na milele, tumeona ushahidi ya
kwamba Mungu alimpenda mwanadamu, hakutaka mtuyeyote apotee
bali wawe na uzima wa milele, hakuna kitu kingine chochote
ambacho Mungu alikipatia kichague pakukaa milele na milele,
isipokuwa mwanadamu peke yake kama tulivyoona katika maandiko,
ya kwamba iwapo mtu yeyote ataonekana hakuandikwa katika kitabu
cha uzima, atatupwa katika lile ziwa la moto, waweza kuwa na swali
hili kwamba mtu anaandikwaje katika kitabu cha uzima?
Yoh 3:16
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa
mwanawake wa pekee, ili kilamtu amwaminiye asipotee, bali awe
na uzima wa milele na milele.
Nimeendelea kukuonyesha jinsi Mungu alivyompenda mtu, hata
akamtoa mwana wake wa pekee (YESU) ili azichukue dhambi zao, ili
wasamehewe, waiepuke jehanam ya moto wa milele na milele.
Yoh 5:24
Amini amini nawaambia, yeye alisikiaye neno langu na kumwamini
yeye aliyenipeleka yunauzima wa milele, wala haingii hukumuni,
bali amepita kutoka mautini na kuingia uzimani.
Silaha za Adui Samuel Imori
46
Yawezekana ulikuwa na maswali kwamba jina la mtu linaandikwaje
katika kitabu cha uzima? Neno la Mungu linatufundisha wazi wazi ya
kwamba ukiamua kumpokea Bwana Yesu katika moyo wako na
ukamkiri kwa kinywa chako ya kwamba Mungu alimfufua katika
wafu,unapokea wokovu, na tayari unafanyika kuwa mwana wa
Mungu, na tayari unakuwa umechagua uzima, tayari unakuwa
umechagua kuishi mbinguni milele, tayari unakuwa umeiepuka ile
jehanam tulioisoma, kwamba jina lake lingine ni ziwa la moto wa
milele na milele.Baada yakuona yakwamba mahali palipotengwa ili
wanadamu wakae milele ni sehemu mbili, mbinguni milele na milele,
sehemu ya pili ni motoni milele na milele nia hasa ya adui yetu
ambae ni shetani angependa aende na wanadamu wote kwenye ziwa
la moto, ndio maana anajitahidi kuwavuta, kuwarubuni na hawezi
akawarubuni tu watakatifu, kumbuka nimekuelezea mapema vile
ambavyo mvuvi anajitahidi kuwavuna samaki, vile asivyo wakamata
kwa ndoano tupu, yeye hutumia chambo, mnyoo, nikasema mnyoo
kama mnyoo hauna tatizo, wala hauna ugomvi na samaki, nichakula
kizuri kwa samaki, lakini mnyoo huo huo mvuvi anapouchukua,
anautumia kuivishia ndoano, na samaki anapoona anafikiri kwamba
ni chakula, kumbe kimegeuka si chakula tena bali ni chambo, hatajina
linabadilika, linatoka kuwa mnyoo linakuwa chambo.
Kwa mfano huo huo wa jina kubadilika hata fedha nayo inayo tabia
hiyohiyo ya majina kubadilika.Mtu anapoambiwa atoe mali ili aweze
kupewa mke, bado ni fedha ileile lakini inageuka na kuitwa
mahali.Mtu akiomba fedha ilia toe huduma Fulani, katika ofisi Fulani,
ni fedha tena anaitaja idadi, lakini hapo inajificha inajisema, rushwa,
chai, kitu kidogo ukipeleka mototo shule unaambiwa fedha kiasi gani
Silaha za Adui Samuel Imori
47
unatakiwa ulipe, ukiisha itoa inaitwa ada, karo.Ukitaka kusafiri,
unaenda stand, utaombwa fedha, lakini utasikia jina linabadilika
wanasema nauli, hiyo ni mifano michache tu jinsi fedha inavyoweza
kujigeuza geuza, kulingana na hali ya mahali hapo, tutaendelea
kuiangalia fedha jinsi Biblia inavyoiongelea
Yak 5:1-6
Haya basi ,enyi matajiri lieni,mkapige yowe kwa sababu ya
mashaka yenu yanayowajia, mali zenu zimeozi na mavazi yenu
yameliwa na nondo, dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu,
na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto,
mmejiwekea akiba katika siku za mwisho, angalieni ujira wa
wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila,
unapiga kelele na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa
BWANA wa majeshi, mmefanya anasa katika dunia na
kujifurahisha kwa tama, mmejilisha kwa tama, mmejilisha kwa
mioyo yenu kama siku ya machinjo, mmehukumu mwenye haki,
mkamwuua wala hashindani nanyi.
Utakumbuka kule mwanzoni neno la Mungu lilituambia kwamba
fedha ni jawabu la mambo yote, na nikakwambia nijawabu la mambo
yote kwenda kulia na kwenda kushoto.Mtu mzuri akiwa na fedha basi
fedha hiyo inamfanya apate majibu ya mambo yake yote anayotaka
ayatimize.Mtu mbaya naye pia anapokuwa na fedha zitamfanya apate
majibu ya mambo yake yote anayotaka ayatimize.Neno la Mungu
limewaelekeza katika kitabu cha Yakobo, kwamba matajiri walie
sikulia tu hakutoshi wapige yoe.Ameendelea kusema dhahabu zao na
fedha zao zimeingia kutu, hili ni neno gumu, ameeleza jinsi matajiri
Silaha za Adui Samuel Imori
48
wanavyoshindwa kuwalipa watu wanaowafanyia kazi,wanaishia tu
kulia kwa Mungu na akasema kilio chao kimefika kwa Mungu,
akaendelea kuonyesha jinsi mwenye haki anavyoonewa na tajiri,
anaumizwa, hajibu chochote, hana ubavu wa kumjibu tajiri,
tumeendelea kuwaona matajiri vile wanavyoweza kuutumia utajiri
wao vibaya, wakawa wamemkasirisha Mungu, wameua wenye haki
wengi, yatima wengi, wajane wengi ,wengine kwakuwa wanazo
fedha wanatoa rushwa, wanafanikiwa kuwafunga watu wasiona hatia
ili tu kwa kuwa hawana fedha, hapo ndipo fedha inaweza ikamfikisha
mtu, akawa apate jawabu la mambo yote.
Uf 3:17-19
Kwakuwa wasema mimi ni tajiri, nimejitajirisha wala sina haja ya
kitu, nawe hujui yakwamba wewe umnyonge, na mwenye mashaka,
na maskini, na kipofu na uchi, nakupa shauri ununue kwangu
dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi
meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako, isionekana na dawa ya
macho ya kujipaka macho yako, upatekuona, wote niwapendao
mimi nawakemea na kuwarudi, basi uwena bidii ukatubu.
Neno la Mungu linatufundisha nini katika mistari hiyo hapo juu?
kumbuka tumesoma kwamba matajiri walie tena wapige yowe, na
hapo tunaambiwa kunawatu wanaodai ni matajiri, na kweli ni matajiri
wa mali za dunia, Biblia ina wataka, inawapa ushauri, wanunue
dhahabu iliyosafishwa kwa moto, hii dhahabu iliyosafishwa ni
nini?anasema akisha inunua ndipo atakuwa tajiri, lakini hataki anadai
yeye tayari ni tajiri,
Silaha za Adui Samuel Imori
49
Akaendelea kumwelezea kwamba anunue mavazi meupe apate kuvaa
ili aibu ya uchi wake isionekane, kwa lugha nyingine yuko uchi,
akaendelea kumwambia anunue dawa ya kupaka macho yake yapate
kuona kwa lugha nyingine haoni. Mungu wetu anaendelea kutusaidia
ili tupate kuelewa kilicho mbele yetu, tuweze kukaa mkao
unaotakiwa, neno la Mungu linatukumbusha wazi kwamba mtu
ambaye ni tajiri katika ulimwengu huu, anayo magari, majumba na
mengine yote tunayoyafahamu, halafu hana Mungu, huyo mtu ni
maskini wa kutupwa,Yesu akamwambia Yule mtu aliyejitajirisha,
akavunja maghala madogo, akajenga makubwa, kisha akaiambia nafsi
yake ikae sasa ile, ifurahi,akifikiri ndio amefika, lakini neno la
Mungu likamjia likamwambia hivi:-“mpumbavu”likamwambia leo
hii wanaitaka roho yako, je mali hiyo ulijiwekea itakuwa ya nani?
Mistari hii ninayokupa hapa watu wengi hawapendi kusikia, lakini ni
ukweli usiopingika, mwanadamu aliandikiwa, ili kumkumbusha ya
kwamba anapita, anaelekea mahalipale alipopachagua, mstari
ulionifanya niwaze sana na kuendelea kutafuta kinacho waangamiza
watu wa Mungu ni ule ambao Mungu alimtumia mtumishi wake nabii
Hosea.
Hosea 4:65
“watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa”
Mungu wetu hapendi tuangamizwe ndio maana aliamua kutuma
watuishi wake ili wawasaidie watu wake wasiangamizwe, akawatoa
wengine mitume/manabii/wainjilisti/wachungaji/na waalimu.Baada
Silaha za Adui Samuel Imori
50
yakuwa amewatoa hao, kusudi wasaidiane, hao tena wanawapoteza
watu wake, na bado Mungu hajanyamaza anapiga kelele akisema
hivi.
Isaya9:16
Kwamaana wawaongozao watu hawa ndio wawakoseshao, na hao
walioongozwa na watuhao wameangamia.
Nimeendelea kurudia rudia kusema, jinsi Mungu wetu
anavyotupenda, jinsi asivyopenda tuangamie ndio maana akamleta
Yesu mwokozi.Naye akajitoa kwaajili yetu akatufia msalabani,
akaimwaga damu yake takatifu, akaifanya kazi ya ukombozi,
akatamka katika kinywa chake akiwa msalabani, maneno
kadhaa.Nivema tujifunze kutokana na hayo maneno aliyoyatamka
aliwaombea maadui zake akiwepo msalabani, alimkabidhi mama
yake kwa Yohana ili amtunze, alisikika akitamka waziwazi kwamba
”imekwisha” nimeyachukua hayo mambo matatu aliyoyasema akiwa
msalabani, ili yatufundishe, yatufungue tupate kujua tunavyotakiwa
kutumia vinywa vyetu na mida yetu tuliopewa na Mungu
kuishi.Sikumoja nilimuuliza kijana mmoja swali, naye alinijibu vizuri
kwa kulingana na uelewa wake.
Swali lilikuwa hivi: Yesu alikuja kufanya nini duniani?
Jibu: alikuja kutuokoa kwa kuimwaga damu yake msalabani.
Swali: je nihilotu pekeyake?au kuna jambo lingine?
Jibu: nadhani ni hilo tu,sidhani kamalipo jambo lingine.
Silaha za Adui Samuel Imori
51
Yawezekana hata wewe unalijua hilo jibu moja, zuri kabisa la kweli,
lakini kama ungeulizwa uitaje kazi nyingine au sababu nyingine
tofauti na hiyo ya kumwaga damu.Ungepata jibu la kujibu? au na
wewe ungejibu kama Yule kijana alivyonijibu kwamba hajui kazi
nyingine aliokuja kufanya duniani?
Yesu kristo alipokuja duniani alijisema wazi wazi kwamba ametoka
kwa Baba yaani Mungu, watu hawakumwamini, lakini alisema kweli,
akajielezea wazi wazi kwamba yeye ndiye njia kweli na uzima”
Yoh 14:6
Yesu akamwambia, mimi ndimi njia na kweli na uzima, mtu haji
kwa Baba ila kwa njia ya mimi.
Alikuwa anasemaje hapo? anasema wazi wazi kwamba mtu akitaka
afike kwa Baba yake, ambaye ndiye Mungu, muumba mbingu na
nchi, amtazame vile anavyotembea, vile anavyofanya naye afanye,
vile anavyosema naye aseme hivyo atafika, na kwa njia hiyo,
mtumishi wa Mungu Petro akatuandikia hivi:-
1Pt 2:21-23
Kwasababu ndiyo mliyoitiwa, maana kristo naye aliteswa kwaajili
yenu akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.Yeye hakutenda
dhambi wala hila haikuonekana kinywani mwake, yeye
alipotukanwa hakurudisha matukano alipoteswa hakuogofya, bali
alijikabidhi kwake ahukumuye kwa haki.
Silaha za Adui Samuel Imori
52
Nimechagua mambo matatu aliyo yatamka alipokuwa msalabani,
alikuwa ameyafundisha katika mafundisho yake, sasa akayaweka
kwenye vitendo.
Math 5:38-48
Mmesikia kwamba imenenwa jicho kwa jicho na jino kwa jino,
lakini mimi nawaambia, msishindane na mwovu, lakini mtu
akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili, na mtu atakaye
kushtaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia, na mtu
atakayekulazimisha mwendo wa maili moja nenda naye
mbili.Akuombaye mpe, naye atakaye kukopa kwako usimpe kisogo,
mmesikia kwamba imenenwa umpende jirani yako na umchukie
adui yako, lakini mimi nawaambia wapendeni adui zenu,
waombeeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye
mbinguni, maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema,
huwanyeshea mvua wenye haki na wasiohaki, maana mkiwapenda
wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? hata watoza ushuru
je hawafanyi yayo hayo? Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu,
mwatenda tendo gani la ziada? hata watu wa mataifa je! Nao
hawafanyi kama hayo? Basi ninyi mtakuwa wakamilifu kama Baba
yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.
Nimetangulia kukuelezea kwamba Yesu alikuja duniani kutuonyesha
jinsi ya kutembea kuelekea kwa Baba yake, ndipo sa akasema “mimi
ndiye njia kweli na uzima”
Silaha za Adui Samuel Imori
53
Alifundisha jinsi ya kuwatendea maadui zetu, naye akawaombea
maadui walio mtukana msalabani ndipo alipofungua mdomo wake sio
kuwalaani, bali kuwaombea kwa Baba yake, ndipo akasema, “Baba
uwasamehe” Baada ya kuwa amewaombea maadui zake akatimiza
kile alichokuwa amekifundisha kumhusu adui.Alijua anaondoka, na
alikuwa anamheshimu mama yake, sio kumheshimu tu tunaona
alikuwa anamtunza, alitii neno la Mungu.
Waheshimu baba yako na mama yako.
Na sasa muda wake ulikuwa umefika tayari yuko msalabani,
hangeendelea tena kumhudumia mama yake, akamkabidhi kwa
Yohana, aliyekuwa mwanafunzi wake, aliyempenda.
Yoh 19:25-27
Na penye msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mama yake
Yesu, na umbu la mama ye mariamu wa kiopa, na Mariamu
Magdalena, basi Yesu alipomuona mama yake, nayule mwanafunzi
aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake “Mama
tazama mwanao”, kisha akamwambia Yule mwanafunzi, tazama
mama yako, na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua
nyumbani kwake.
Waheshimu baba yako na mama yako ni amri ambayo Mungu
aliwapa wanadamu, akaendelea kusema kuwa ukiwaheshimu utapata
heri, na utaishi miaka mingi, Yesu alimuheshimu mzazi wake
hakutaka kumwacha hewani, siku tulizonazo wapo watu wengi
hawajali, hawaheshimu wazazi wao. Nikukumbushe tu kuwa wapo
Silaha za Adui Samuel Imori
54
wazazi wa aina mbili; wa kimwili na wa kiroho, wote ni wazazi
tunatakiwa kuwaheshimu kama tunataka tupate heri, kama tunataka
tuishi miaka mingi katika nchi tuliyopewa. Msomaji wangu bado
hujachelewa yawezekana wazazi wako wangali hai hawajatoka
ulimwenguni, nenda watafute kabla hawajaondoka, wakubariki,
mmoja akasema nenda wakutemee mate
Jambo la mwisho alilotamka ni “imekwisha” akiwa na maana
“nimemaliza” alikuwa anatangaza wazi kwamba amemaliza, aliijua
kazi iliyo mleta, ndio maana alisema imekwisha, alijua Baba yake
alimtuma kuja kufanya nini ,na huyo ndio ametutuma, kama tunataka
kuifurahisha mbingu sharti tujue tumetumwa kufanya nini, sharti
tujue ni nini kinaifurahisha mbingu, sikumoja wanafunzi wa Yesu
walirudi wanafurahi sana, wanashangilia, wakisema
“pepo wanatutii”
Yesu akawakataza kwamba hilo siyo la kufurahia, ila la kufurahia ni
hili”majina yenu yameandikwa mbinguni”yawezekana mimi na wewe
tunafurahia miujiza inayotendeka, mapepo yanavyotutii, magari
tunayoyaendesha, majumba makubwa tulio ya jenga, mavyeo
makubwa tulionayo, mapesa tuliojikusanyia, wakristo tulio
wakusanya, lakini isikie sauti ya Mungu inasema msifurahie hayo
Lk 10:20
Bali furahini yakwamba majina yenu yameandikwa mbinguni.
Silaha za Adui Samuel Imori
55
Ni hatari kubwa, na upumbavu mkubwa, kama tutafurahia hayo na
huku majina yetu hayapo huko mbinguni.Yawezekana tukafurahia
hayo yote kumbe majina ama hayajaandikwa ama yamefutwa.
Uf 3:5
Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta
kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake
mbele za Baba yangu, na mbele za malaika zake.
Yesu anatueleza jinsi tutakavyofanya majina yetu asiyafute ni pale
tutakaposhinda, tutakaposhinda nini? anasema yeye ashindaye, tuone
ashindaye nini?
Yoh 16:33
Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu,
ulimwenguni mnayodhiki, lakini jipeni moyo, mimi nimeushinda
ulimwengu.
Ndugu yangu mpendwa, ulimwengu unaendelea kuwavuta wanadamu
ili uende nao kubaya, kule katika lile ziwa la moto tulilolisoma hapo
mwanzoni.Yeye mwenyewe alitufundisha namna ya kutembea,
namna ya kutamka, mpaka akatamka “imekwisha”bado tutaendelea
kumsikiliza kutufundisha jinsi ya kutamka. Math 9:13
Lakini nendeni mkajifunze maana yake maneno haya, nataka
rehema, wala si sadaka, kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali
wenye dhambi.
Silaha za Adui Samuel Imori
56
Yesu kristo mwana wa Mungu aliyekuja akaishi kama mwanadamu
hapa duniani, alizijua sadaka, ndio maana anatamka wazi wazi ya
kwamba lengo lake, kusudi lake siyo sadaka, siyo fedha, kuhubiri
kwake siyo ni ili apate fedha, alilijua neno la Mungu, maana tulisoma
kwamba
“Msiwe na tabia yakupenda fedha”
Hapa anaonyesha wazi wazi kwamba lolote analolifanya sio kwa
sababu apate fedha, yaani fedha sio kipaumbele, ila kipaumbele ni
kuwatafuta wanadamu waliopotea awarudisha kwa muumba wao,
ndio maana akawaambia waende wajifunze, wasije wakamdhania
kwamba anatafuta fedha kutoka kwao.
2Kor12-14
Tazama hii ni mara yatatu ya mimi kuwa tayari kuja kwenu,wala
sitawalemea, maana, sivitafuti vitu vyenu bali nawatafuta ninyi,
maana haiwapasi watoto kuweka akiba kwa wazazi, bali wazazi kwa
watoto.
Bwana wetu Yesu kristo alitumwa na Baba yake, alipomaliza kazi
yake naye akawatuma watumishi wake, nao wanatamka wazi wazi
kwamba hawatafuti vitu, ya kwamba vitu sio kipaumbele, magari,
majumba, vyeo n.k bali wanatafuta roho za watu, ni rehema, maana
yake huruma, na wengi wametumbukia wakaingia kutaka mapato ya
aibu kama tulivyoona huko nyuma.
Silaha za Adui Samuel Imori
57
Math 12:7
Lakini kama mngalijua maana yake nini maneno haya, nataka
rehema, wala si sadaka, msingali walaumu wasio na hatia.
Bwana wetu aliendelea kusisitiza kwamba wapo watu wanalaumiwa
bila sababu yoyote, na akasema kusudi lake la kuja, la kuhubiri,
kusudi lake la kuombea wagonjwa, siyo fedha, hapana, ni huruma, na
msaada, ni kuzipata roho zao sio vitu vyao na wanafunzi wake pia
tunapaswa kufuata nyayo zake alizozipitia na hiyo ndio njia ya
kwenda kwa Baba yake, ambaye ndiye Mungu wa kweli.
Filp 3:17-19
Ndugu zangu, mnifuate mimi mkawatazame wao waendao kwa
kufuata mfano tulio wapa ninyi, maana wengi huenenda, ambao
nimewaambieni mara nyingi habari zao, kuwa niadui za msalaba
wa kristo, mwisho wao ni uharibifu muungu wao ni tumbo, utukufu
wao ukatika fedheha yao, waniao mambo ya duniani.Kwa maana
sisi wenyeji wetu uko mbinguni, kutoka huko tena tunamtazamia
mwokozi, Bwana wetu Yesu kristo atakaye ubadili mwili wetu wa
unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza
ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini
yake.
Mtumishi wa Mungu Paul alikuwa anawaonya ndugu zetu wafilipi
kwa machozi, maana walikuwapo watu ambao walikuwa wanadai
kwamba wana mtumikia Mungu. Kumbe walikuwa ni maadui wa
msalaba hawakutaka shida yeyote, walikuwa wanaye mungu wao
Silaha za Adui Samuel Imori
58
akawaelezea wazi wazi kwamba mungu wao alikuwa ndugu aitwaye
“tumbo”, wengi hata siku zetu tulizonazo Mungu tumbo
amewaendesha watu sana,wanamtumikia, na hana malipo atakayo
walipa, neno la Mungu linasema hivi” vyakula ni kwa tumbo”lakini
vyote vitatoweshwa, ndugu yangu mpendwa, haujachelewa bado
yawezekana ulikuwa una mtumikia muungu tumbo, waweza badilika,
naukampata Mungu wa kweli, muumba mbingu na nchi.Yeye
aliewapa wanadamu wachague watakapoishi milele. Zaburi49:16-
17
Usiogope mtu atakapopata utajiri, na fahari ya nyumba yake
itakapozidi, maana atakapokufa hatachukua chochote.
Mpendwa msomaji wangu, neno la Mungu ni kweli, na sisi tu
mashahidi kwamba tumewaona majiri wengi walio wahi kuwepo
chini ya jua, na mwisho wao walikufa, lakini ukweli unabaki pale
pale ya kwamba hawakuchukua kitu chochote, hata kimoja, kinyume
chake walifunikwa nguo moja tu, shuka nyeupe, jina la shuka hiyo ni
sanda, mmoja akasema ni nguo pekee yenye bei rahisi kuliko nguo
zote, baada ya kufunikwa nguo hiyo, wengine ndio imetoka hivyo,
wengine wanawekwa kwenye sanduku, kisha kaburi huchibwa na
mwili wa mtu huyo hushushwa mle ndani ndani, analazwa humo,
watu wamemzunguka, wapo wanaolia kiliokweli maana alikuwa
msaada kwao, wapo ambao wanalia ila ni kwa sababu wengine nao
wanalia, lakini kiuhalisia wanashukuru kimoyo moyo kwa kuwa
jamaa alikuwa ni kero kwao, wengine wanajipanga ni nini
watachukua, ndio maana unaona hawaishii hapo kumweka kaburini,
wanaleta nondo, wanaleta smenti. Huo ndio una kuwa mwisho wa
Silaha za Adui Samuel Imori
59
mtu huyo ama amesha fika kwa Mungu atakakokaa milele na milele.
Ama ameshafika kuzimu atakakokaa milele na milele, kama
nilivyokwisha kukuelezea kwamba Mungu wetu alitupatia tuchague,
bado tukiwa hai, lakini viongozi wetu wengine wakatudanganya, na
kweli tukadanganyika kwamba ukifa utaombewa, sasa unamsikia mtu
anaomba hivi
“ee Baba mpokee mtu huyo na umuweke mahali pema peponi”Huo ni
uongo mkubwa, niutapeli ni kuwadanganya wajinga, hakuna sala ya
jinsi hiyo chini ya jua, hakuna sala ya jinsi hiyo kama nilivyokwisha
kukuelezea yakwamba Yesu wetu ndiye njia na alipo kuja
alitufundisha mambo mengi moja wapo ni hilo la kuwaombea wafu,
hakusema popote kwamba mfu anaombewa, napenda tuone jinsi
alivyo lifundisha hilo
Lk 16:19-31
Akasema, palikuwa na mtu mmoja tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya
zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa, na masikini
mmoja jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda
vingi naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo
yalioanguka katika meza ya Yule tajiri hata mbwa wakaja
wakamlamba vidonda vyake, ikawa Yule masikini alikufa,
akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahim, Yule tajiri
naye akafa, akazikwa, basi kulekuzimu aliyainua macho yake
alipokuwa katika mateso akamwona Ibrahimu kwa mbali, na
Lazaro kifuani mwake, akalia akasema ee Baba Ibrahim,
nihurumie umtume Lazaro achovye ncha ya ya kidole chake
majini auburudishe ulimi wangu, kwa sababu ninateswa katika
Silaha za Adui Samuel Imori
60
moto huu, Ibrahim akasema, mwanangu kumbuka ya kwamba
wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na
Lazaro vivyo alipata mabaya, na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa,
na wewe unaumizwa, na zaidi ya hayo kati yetu sisi na ninyi
kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda
kwenu wasiweze, wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu,
akasema basi, baba yangu kwakuwa ninao ndugu watano ili
awashuhudie, wasije wao pia wakafka mahali hapa pa mateso,
Ibrahim akasema, wanao Musa na manabii, na wawasikilize wao.
Akasema la baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye
kwa wafu watatubu. Akawaambia wasipowasikia Musa na manabii,
hawata shawishiwa hata mtu akifufuka katika wafu.
Nilichotaka kukuonyesha hapa ni kuifahamu njia ya kwenda juu kwa
Mungu Baba wa Bwana wetu Yesu kristo, alituelezea kwamba
ukichelewa kuchagua pale utakapoishi milele baada ya kufa kwako,
basi utakuwa umechelewa na ujue usipo mchagua Yesu aliye njia ya
uzima, basi elewa umemchagua moto wa milele na milele, hakuna
mahali pengine tofauti ambapo watu wataishi milele na milele tofauti
na mbinguni au motoni. Ameeleza vizuri alikuwepo mtu tajiri,
akawepo na mwingine maskini Lazaro, wote walikufa, Lazaro
alichukuliwa mpaka mapumzikoni tajiri naye akafa, akaenda
matesoni alipokuwa huko alijaribu kutafuta msaada kwa Ibrahim,
tumeona haukupatikana tumeendelea kumuona akawahurumia ndugu
zake aliokuwa amewaacha duniani, bado haikusaidia chochote
akajulishwa kwamba mtu anapokufa mambo yake yameishia hapo,
yale unayoyasikia ati tumuombee marehemu, ule ni upumbavu,
kwanini nimeuita upumbavu? mpumbavu amesema hakuna Mungu,
Silaha za Adui Samuel Imori
61
hiyo ndio sifa ya mpumbavu, nimemwita mpumbavu kwasababu
kuombea wafu nisawa na kusema hakuna Mungu, maana ka kweli
unasema Mungu yupo basi ungemtafuta, ungemuuliza ili akuelekeze
namna ya kuwaombea watu wale ambao bado hawajafa, sasa
unasubiri mtu afe, hukumwonya aache dhambi zake alipokuwa hai,
ukaendelea hata kupokea sadaka zake za wizi, za rushwa, za dhuluma
na hukumwonya, hukumwambia vile Mungu wake anataka aishi,
akiisha kufa ndio unamwambia Mungu amweke mahali pema. Mahali
pema wapi? Mshahara wa dhambi ni mauti, naomba tulielewe hilo
kabla hatujafa tutengeneze maisha yetu na Yesu atuokoe tutakuwa
tumechagua uzima wa milele na milele.
Mith 14:20
Masikini huchukiwa hata na jirani yake bali tajiri ana marafiki
wengi.
Niukweli usiopingika ya kwamba masikini huchukiwa hata na jirani,
ila tajiri anamarafiki wengi, katika kitabu changu cha vikwazo vya
kuurithi uzima wa milele ni meelezea kirefu habari ya marafiki, Neno
linasema usimwamini rafiki, nikaandika aina saba za marafiki,
ukisoma utaelewa vizuri, sasa kama wewe ni tajiri, elewa hivyo unao
marafiki wengi, humo humo hata wasaliti wako wamopia, Yesu
alikuwa na wanafunzi kumina mbili msaliti alikuwemo mmoja basi
wakiwa ishirini na nne watakuwa wapo wasaliti wawili, sasa neno
limesema kwamba tajiri anao marafiki wengi, kwa vyovyote pia
wasaliti niwengi.
Silaha za Adui Samuel Imori
62
Mith 18:23
Masikini hutumia maombi bali tajiri hujibu kwa ukali.
Hawa wawili ni wanadamu wote pengine umri wao ni mmoja,
pengine elimu yao ni moja, pengine kabila laoni moja, pengine urefu
wao au ufupiwao ni mmoja, pengine wote wanao watoto na wake pia,
lakini sikia kwakuwa mmoja nitajiri anajibu kwa ukali, nini
kinamfanya ajibu kwa ukali? ”utajiri”, utajiri ni nini?ni fedha,Yule
mwingine ni masikini, ametumia maombi, nini kinamfanya atumie
maombi amekosa nini fedha. Napenda kurudia rudia baadhi ya
sentensi ili usisahau, nilikueleza kuwa nakuonyesha baadhi ya
misemo au mafundisho ambayo Biblia inasemea kuhusu fedha.
Mith 19:4
Utajiri huongeza rafiki wengi, bali masikini hutengwa na rafiki
yake.
Mungu wetu hakuacha kutu patia taarifa, leo wapo matajiri ambao
wana marafiki wengi, wanaweza wasijue ni kwanini wana marafiki
wengi, kumbe nikwaajili ya utajiri, hii inamaana kuwa utajiri ukiisha
tu, na marafiki hao wala hatawaona, hii inamaanisha kwamba, sio
marafiki wakweli, katika kitabu change cha vikwazo sehemu ya
kwanza nimeelezea vizuri sana kirefu kuhusu aina ya marafiki,
nikawaelezea kwamba wako aina saba, hao wote inabidi tujifunze, ili
tuweze kujihadhari na marafiki wabovu wasio wazuri wanaweza
kutuangamiza
Silaha za Adui Samuel Imori
63
Ay 34:19
Sembuse huyo asiyependelea nyuso za wakuu, wala hawajali
matajiri kuliko masikini kwani wote nikazi ya mikono yake.
Bwana wetu aliwataarifu wanadamu wazi wazi kwamba yeye
hapendelei mtu kwa kuwa ni tajiri, anasema wote ni mali yake yeye,
na hili linatuhakikishia kwamba kweli Yesu alitoka kwa Mungu,
twaweza kuwaona wakimtembelea na kumwambuia jinsi
walivyokuwa wamemchunguza na kumjua, hakujisema ila
walimsema hivi,
Math 22:15-16
Ndipo mafarisayo wakaenda zao, wakafanya shauri jinsi ya
kumtega kwa maneno, wakatuma watu kwake wanafunzi wao
pamoja na maherodi wakasema mwalimu twajua yakuwa wewe ni
mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli wala
hujali cheo cha mtu awaye yeyote kwa maana hutazami sura za
watu.
Watu hawa tumewasikia waziwazi wakimsalimia Yesu wakisema
jinsi alivyo lisema neno la Mungu katika kweli, bila unafiki, bila
kuficha ili mtu mwenyewe abaki kuamua, njia
Atakayeitembea wakamwambia kuwa wamemfahamu kwamba hajali
cheo cha mtu wala haangalii sura ya mtu awayoyoyote, laiti
watumishi wa Mungu wange mfanana, nao wangetambulikana kwa
jinsi hiyo, lakini tofauti kubwa ipo leo kati ya matajiri na masikini,
niombi langu Mungu atusaidie kwa njia ya Roho mtakatifu.
Silaha za Adui Samuel Imori
64
Yer 9:23-24
Bwana asema hivi,mwenye hekima asijisifu kwasababu ya hekima
yake,wala mwenye nguvu asijisifu kwasababu ya nguvu zake,wala
tajiri asijisifu kwaajili ya utajiri wake, bali ajisifuye na ajisifu
kwasababu hii ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijua, yakuwa
mimi ni Bwana, nitendaye mema, na hukumu, na haki katika nchi,
maana mimi napendezwa na mambo hayo asema Bwana.
Yaangalie vizuri maagizo hayo, Mungu wetu alipowatazama
wanadamu aliwaangalia akakuta wanajisifu, kila mmoja alikutwa
analo la kujisifia, wengine urefu wao, wengine unene wao, wengine
elimu yao ,wengine vyeo vyao, wengine nyumba zao, wengine
magari yao, ndipo akawahurumia wote, akawasaidia wapate kujua,
nikipi ambacho mtu anapaswa ajisifie, alikuta wengine wanajisifia
dini zao,wengine wanasema dini yetu ni kubwa ,wengine wanasema
dini yetu niya kwanza wengine niya pili n.k. yeye akawahurumia
akawaambia mtu yeyote akitaka kujisifia, kujisifu kutakakokuwa kwa
maana ni Yule aishie kunifahamu, anijue mimi, ajue mimi nataka
nini, ajue maagizo yangu kwa wanadamu, hivyo atakuwa kheri huyo
atakuwa amechagua fungu jema.
Yak 1:9-11
Lakini ndugu asiye na cheo afurahi kwa kuwa ametukuzwa, bali
tajiri kwakuwa ameshushwa, kwa maana kama ua la majani
atatoweka, maana jua huchomoza kwa hari, huya kausha majani,
ua lake hunyauka uzuri wa umbo lake hupotea, vivyo hivyo naye
tajiri atanyauka katika njia zake.
Silaha za Adui Samuel Imori
65
Neno la Mungu limeendelea kumsaidia tajiri ajifahamu, utajiri usije
ukamziba masikio, usije ukamziba macho yake asione,
akalinganishwa na majani, maua jinsi yanavyo weza kupendeza,
kumeremeta kwa rangi mbalimbali, na jinsi yanavyoweza kunukia
vizuri lakini jua likichomoza, likilipiga lile ua jani lake linainama na
kuanguka uzuri wake wote, unaishia hapo, harufu nzuri yote inaishia
hapondipo likafananishwa na tajiri aliyechanua, alie utegemea utajiri
wake, alie jisifia utajiri, bila kumtegemea Mungu ,utajiri aliojisifia,
asijisifie kumjua Mungu kama tulivyosoma hapo juu.
Mdo 5:1-11
Lakini mtu mmoja jina lake Anania, pamoja na Safira mkewe,
aliuza mali.Akazuia kwa siri sehemu ya thamani yake mkewe naye
akijua haya, akaleta fungu moja akaliweka miguuni pa mitume,
Petro akasema, Anania kwanini shetani akujaza moyo wako
kumwambia uongo Roho mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya
thamani ya kiwanja. Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? na
kilipokuwa kimeisha kuuzwa, thamani yake haikuwa uwezo wako?
Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia
uongo mwanadamu bali Mungu, Anania aliposikia maneno hayo
akaanguka akafa, hofu nyingi ikawapata watuwote walioyasikia
haya, vijana wakaondoka wakamtia katika sanda, wakamchukua
nje wakamzika, hata muda wa saa tatu baadae mkewe akaingia
naye hana habari ya hayo yaliotokea. Petro akamjibu, niambie
mlikiuza kiwanja kwa thamani hiyo? akasema ndio kwa thamani
hiyo, Petro akamwambia imekuwaje hata mkapatana kumjaribu
Silaha za Adui Samuel Imori
66
Roho wa Bwana? angalia miguu ya walio mzika mumeo iko
malangoni,nao watakuchukua nje wewe nawe, mara akaanguka
miguuni pake akafa wale vijana wakaingia, wakamkuta amekufa
wakamchukua nje, wakamzika pamoja na mumewe, hofu nyingi
ikawapata kanisa lote nawatu wote walioyasikia hayo.
Msomaji mpendwa, tumeendelea kuiona hiistoria ya mtu mmoja
aliyekuwa kanisani wakati wake
mtume Petro, mtu huyu walikaachini, wakashauriana na mke wake,
wakaamua kuuza mali yao ambayo ni kiwanja, baada ya kukiuza,
wakashauriana kwamba wapeleke sehemu tu ya fedha kanisani,
zingine wafiche na ndiyo walifanya lakini Roho wa Mungu ndani ya
mtume Petro aliuona ule udanganyifu, akamuuliza wazi aeleze fedha
waliouza kile kiwanja, Anania hakuwa na roho ya toba, aliendelea
kudanganya hata mbele ya mtumishi wa Mungu Petro, tunaona
matokeo yake alikufa, hakuweza kutubu, na mkewake pia aliendelea
kuficha wizi waliokuwa wameufanya, naye pia tunaona kile kilicho
mtokea,wote wakawa wameangamizwa, kwa kuwa walikosa maarifa,
waliipenda fedha, wakaificha, laiti wangekuwa wameitii sauti hiyo
iliyo waambia wasiipende fedha mwisho wao hawa watu wawili
haukuwa mzuri kama tulivyoona.Jambo hili litufundishe, na Roho
mtakatifu atusaidie, mioyo yetu iwe mioyo ya nyama, mioyo yenye
toba, mioyo iliyo tayari kumrudia Mungu pale tunapogundua
tumekosea, moyo wa Anania uliendelea kuwa mgumu na moyo wa
Safira mke wake pia wote wakakutwa namauti. Mioyo yetu
inatakiwa iwe mioyo ya nyama.
Mark 4:13- 20
Silaha za Adui Samuel Imori
67
Akawaambia hamjui mfano huu? basi mifano yote mtaitambuaje?
mpanzi huyo hulipanda neno, nao wakiisha kusiia mara huja
shetani akaliondoa lile neno lililopandwa mioyoni mwao, kadhalika
na hawa ndio wapandao penye miamba, ambao kwamba wakiisha
kulisikia lile neno, mara hulipokea kwa furaha , ila hawana mizizi
ndani yao, hali hudumu muda mchache, kasha ikitokea dhiki au
udhia kwa ajili ya lile neno mara hujikwaa, na hawa ndio wale
wapandwao penye miiba, ni watu walisikiao lile neno, na shughuli
za dunia na udanganyifu wa mali , na tama za mambo mengine
zikiingia hulisonga lile neno likawa halizai na hawa ndio
waliopandwa penye udongo ulio mzuri, ni watu wasikiao lile neno
na kulipokea, na kuzaa matunda, mmoja thelathini, mmoja sitini na
mmoja mia.
Katika habari za maandalio ya moyo, ili neno lipandwe
yanamtegemea muandaaji, kama tulivyoona ya kwamba ipo aina nne
ya mioyo, upo moyo ambao unaruhusu udanganyifu wa mali,
zinausonga unakuwa hauzai, hii yote inatufundisha tujikague,
tuiandae mioyo yetu vizuri, ili neno linapopandwa lipate kuzaa
matunda.
Mith 16:1
Maandalio ya moyo niya mwanadamu, bali jawabu la ulimi latoka
kwa Bwana.
Mungu atusaidie tuiandae mioyo yetu iwe mioyo inayo lipokea neno
la Mungu kwa unyenyekevu, na tuweze kulitii, tuweze kutenda vile
linavyo tuagiza. Hapo tutaitwa kheri, kama nilivyosema kwamba
Silaha za Adui Samuel Imori
68
yapo maandiko mengine ni magumu, hata watu hawayapendi
kuyasikia, lakini maadamu yameandikwa, ni kwa ajili ya
mwanadamu, ili ayafanye au yamuonye, yamwadhibishe awe mtu
mkamilifu.
Lk 6:24
Lakini olewenu ninyi mlio na mali kwa kuwa faraja yenu
mmekwishakuipata ole wenu ninyi ambao mmeshiba sasa, ole wenu
ninyi mnao cheka sasa, kwa kuwa mtaomboleza na kulia, ole wenu
ninyi watu wote watakapowasifu kwa kuwa baba zao walitenda
manabii wa uongo mambo kama hayo.
Neno linasemaje?Walio na mali tayari wamepata faraja, kumbe mali
inaleta faraja, hapo tunatakiwa tusiridhike na faraja ile ambayo mali
inaileta wale walioshiba wanaambiwa ole, maana yake tusije
tukashiba tukajisahau, mmoja alipo shiba alitamka kwamba
hataondoshwa pia wanaocheka sasa wanaambiwa ole wao, uwe
makini, unapocheka, jiulize nini kinakuchekesha? neno linasema kila
jambo lina majira, unapocheka ujue ipo siku utalia, kama utakumbuka
vizuri, nilikuelezea hivi Mungu alipokusudia kuwabariki watu wake
wakati alipo watoa misri, aliwapa anyo, akasema
”JIHADHARINI”alianza na jambo hilo, kasha akawaambia huko
mnakokwenda, ninao mpango mzuri kabisa, kuwabariki katika
sikuzenu za mwisho, malizenu zitaongezeka na chochote mlicho
nacho kitaongezeka, akawaambia muwe makini, mthibiti mioyo yenu
isije ikainuka, mkashikwa na kiburi, mkanisahau.Mwanadamu ni
mwepesi sana wa kusahau anapopata raha kidogo, ni mwepesi
kusahau alikotoka, anapotajirika tu nirahisi kujisahau na kwa sababu
Silaha za Adui Samuel Imori
69
hiyo basi Mungu alimtumia mhubiri, kuwakumbusha wanadamu
kama ambavyo nakumbusha leo hivi hakuna jambo la kudumu chini
ya jua, kila jambo wanalopitia wanadamu ni la muda, vile ambavyo
mwanadamu sio wakudumu,basi hata hali aina yoyote anayoipitia sio
ya kudumu, uwe umasikini,utajiri,kiwe kilio au kicheko n.k
Mh 3:1-9
Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati katika kila kusudi
chini ya mbingu:-
-wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa
-wakati wa kupanda na wakati wa kung’oa yalio pandwa
-wakati wa kuua na wakati wa kupoza
-wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga
-wakati wakulia na wakati wakucheka
-wakati wakuomboleza na wakati wa kucheza
-wakati wakutupa mawe na wakati wa kukusanya mawe
-wakati wakukumbatia na wakati wakuto kukumbatia
-wakati wakutafuta na wakati wa kupoteza.
-wakati wakueweka na wakati wa kupoteza
-wakati wa kurarua na wakati wa kushona
Silaha za Adui Samuel Imori
70
-wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia
-wakati wa kunyamaza na wakati wa kunena
-wakati wa vita na wakati wa amani
Je mtendaji anayo faida gani katika yale anayo jishughulisha nayo?
mistari hii yote kama utaisoma kwa utulivu, naamini utapata amani,
hutahangaika sana, maana imepangwa na mwenye kuumba
ulimwengu huu, ninachoomba ufananishe hivi, mchana una saa kumi
na mbili, maana yake nini? Mchana ukiisha pita umepita, lazima uje
usiku, na usiku ukiisha pita umepita,lazima uje mchana, napenda
tuendelee kujifunza kwamba lile alilolipanga Mungu ndilo
litakalotendeka, ndio maana Yesu alipokuwa anaomba ili kikombe
kimuepuke, alimpa Mungu nafasi ya kuingilia kati pale aliposema
hivi ”sikama nitakavyo, bali mapenzi yako yatimizwe” napenda
tujifunze kwamba hata kuku wote wangekusanyika,watangaze ngoma
waamuwe kwamba hawatawika, napenda nikwambie kutakucha
tuu.Wanaweza wakadhani hivi, kwa kuwa wanadamu wana wataja
taja wakati mwingine wanasema kabla ya majogoo tuondoke, hata
Bwana Yesu alitaja hivi:- Petro kabla ya kuwika jogoo utanikana
mara tatu, kwa hiyo jogoo anaweza dhani kwamba asipowika
hakutakucha, ndivyo ilivyo kwetu wanadamu kila jambo linamajira
yake, kwa maana hiyo basi, wakati wa kucheka unapofika, cheka
ukijua hautacheka milele, wakati wa kulia ukifika, lia ukijua hautalia
milele, wakati wa umaskini hauwezi kuwa masikini milele. Msomaji
wangu mpendwa usipoyaelewa haya, hali iwayoyote inaweza
ikakufanya ukakata tama, wapo waliowahi kuwa matajiri sana na leo
hawana kitu tena, wamebaki watu wa kawaida, wapo watu waliwahi
Silaha za Adui Samuel Imori
71
kuwa masikini mpaka wakafikia msemo usemao ati masikini wa
kutupwa, lakini leo watu hao nimatajiri wa kupindukia, na endelea
kukuonyesha vile fedha au mali zinavyoweza kutumiwa na adui yetu
zikafanyika mnyoo wa kumwangamiza mwanadamu kama
tulivyosoma kwenye maandiko kwamba,” Hos 4:6a watu wangu
wanaangamizwa kwa kukosa maarifa”
2Falme 5:20
Lakini Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu
akasema.Tazama Bwana wangu amemwachilia huyo Naamani
Mshami, asivipokee mikononimwake vile vitu alivyovileta, kama
Bwana aishivyo, mimi nitamfuata mbio nipokee kitu kwake.Basi
Gehazi akamfuata Naaman, naye Naaman alipomwona mtu
apigaye mbio anakuja mbio nyuma yake, alishuka garini amlaki,
akasema je niamani? akasema, amani, Bwana wangu amenituma
kusema tanzama, sasa hivi wamenijia, kutoka milimani mwa
Efraimu vijana wawili wawana wa manabii, uwape nakuomba
talanta mbili, akamshurutisha, akafunga talanta mbili za fedha
ndani ya mifuko miwili, na mavazi mawili, akawatwika watumishi
wake wawili, nao wakayachukua mbele yake, naye alipofika
kilimani, alivitwaa mikononi mwao, akaviweka nyumbani
akawaacha wale watu kuondoka nao wakaenda zao, lakini yeye
akaingia, akasimama mbele za bwana wake, Elisha
akamwambia,watoka wapi Gehazi? Akanena mtumwa wako
hakwenda mahali, akamwambia je moyo wangu haukwenda na
wewe, hapo alipogeuka Yule mtu katika gari ili akulaki? je huu
ndio wakati wa kupokea fedha na kupokea mavazi,na mashamba ya
Silaha za Adui Samuel Imori
72
mizeituni na mzabibu na kondoo na ng’ombe na watumwa na
wajakazi? Basi ukoma wa naaman utakushika wewe na wazao
wako hata milele naye akatoka usoni pake mwenye ukoma kama
theluji.
Msomaji wangu mpendwa, hapojuu tunayo mambo mengi mno
yakujifunza, huyo mtumishi wa Elisha, ambaye jina lake ni Gehazi,
yeye kama tulivyo msoma alikuwa ana mtumikia Elisha, na Elisha
alikuwa anamtumikia Mungu, sikumoja alikuja mgonjwa wa ukoma
kumtembelea ili amponye, kutoka nchi ya Sham, alipofika alimkuta
Gehazi akiwa mlinzi na mtumishi wa Mungu
Elisha alikuwa ndani, Naaman aliomba aonane na Elisha, kwa hiyo
Gehazi aliingia ndani kwa Elisha akampa taarifa kwamba yupo mtu
nje, mtu mkubwa mwenye cheo amefuatana na msafara wake ana
ukoma, anataka kukuona, mtumishi wa Mungu Elisha hakubabaishwa
na cheo hicho, wala hakubabaishwa na zawadi, (sadaka) alizokuwa
nazo, akampatia Gehazi maelezo alimwambia aende katika mto
Yordani akajichovye mara saba, halafu aende kwao Ushamini, Gehazi
akayapokea hayo maelekezo, akayapeleka kwa Naaman, Naaman
aliposikia hivyo hakupendezwa alionekana kulalamika,akisema
maneno yafuatayo:-mimi nilizanikwamba angenijali angenitetemekea
mm ebu tone vile alivyojibu katika maandiko.
2Falm 5:11
Lakini Naamani akakasirika akaondoka akasema.Tazama
nalidhani bila shaka atatoka kwangu na kusimama, na kuomba
kwa jina la Bwana Mungu wake, na kupitisha mkono wake mahali
Silaha za Adui Samuel Imori
73
penye ugonjwa, na kuniponya mimi mwenye ukoma, je abana na
farpari, mito ya dameski, si bora kuliko maji yote ya Israel, je
siwezi kujiosha ndani yake, na kuwa safi? akageuka akaondoka
kwa hasira.
Naaman alikuwa mgonjwa wa ukoma ameenda kwa mtumishi wa
Mungu Elisha ilia pate msaada, na Mtumishi wa Mungu
amemwelekeza mtumishi wake Gehazi ampatie maelekezo naye
amempatia maelekezo, lakini yamemkasirisha, ameamua kuondoka
na ukoma wake, alichodai ni kwamba Elisha hakutoka amshike
amwombee, utakumbuka nilikueleza jinsi watu walivyo msalimia
Bwana wetu Yesu, wewe umtu wa kweli, njia ya Mungu waifundisha
katika kweli, hujali cheo cha mtu awaeyeyote, hutazami sura za watu.
Math 22:15-16
Mtumishi wa Mungu Elisha, hakutishwa na cheo cha Naaman, kama
vile maandiko yanenavyo kwamba Bwana wetu Yesu hakujali cheo
cha mtu wala sura za watu msomaji wangu, mwisho tunaona Naaman
anakubali akaenda akajichovya katika mto Yordan, nyama ya mwili
wake ikawa laini, ukoma ukamwacha, alifurahi sana, alikuwa tayari
kukutana na Elisha ampatie sadaka, alipofika alimkuta Gehazi,
akamuelezea kwamba tayari ni mzima, na alikuwa anataka aingie
amuone Elisha, si kumuona tu na kumpatia fedha, napenda tuendelee
kujifunza kwake, utakumbuka imeandikwa kwamba tumejengwa
katika misingi ya mitume na manabii, Bwana Yesu akiwa jiwe kuu la
pembeni.
Silaha za Adui Samuel Imori
74
2Falm 5:15
Akamrudia Yule mtu wa Mungu, yeye na mafuatano yake yote,
akaja akasimama mbele yake akasema, sasa tazama, najua ya
kwamba hakuna Mungu duniani mwote ila katika Israel, basi
nakuomba upokee mbaraka kwa mtumwa wako, lakini akasema,
kama Bwana aishivyo ambae nimesimama mbele zake sipokei kitu,
akamshurutisha apokee lakini akakataa Naamani akasema kama
sivyo lakini mtumwa wako na apewe mzigo wa udongo wa baghala
wawili, kwa maana mtumwa wako hatatoa tena sadaka ya
kuteketezwa wala dhabihu kwa miungu mingine ila kwa Bwana,
jambo hili Bwana amwachilie mtumwa wako, bwana wangu
akiingia nyumbani mwa Rimoni ili aabudu humo naye akitegemea
mkononi mwangu, nami nikijiinama nyumbani mwa Rimoni hapo
ninapojiinama nyumbani mwa Rimoni, Bwana amwachilie
mtumwa wako jambo hili, akamwambia, enenda kwa amani basi
akamwondokea mbali kidogo.
Naamini umeyasikia majibizano ya Naaman na mtumishi wa Mungu
aliyejuu Elisha,alilazimishwa na Naaman achukue zawadi lakini
Elisha alikataa katakata, nikwanini alikataa mali, fedha, dhahabu?
nilikwambia kilajambo lina majira yake hata kupokea nako yako
majira yake, upo wakati wa kupokea na wakati wa kuto kupokea,
hivyo ndivyo tunatakiwa kufahamu, wakati mwingine utayapokea
mapato ya aibu, wakati mwingine utamuuza Yesu kama Yuda
alivyomuuza kwa vipande thelathini,wakati mwingine utamwombea
mtu atapona, naye atamanio alipie huo uponyaji, nawe kwakuwa
unaitamani pesa na utamwambia anatakiwa alipie kiasigani, naye
Silaha za Adui Samuel Imori
75
akitoka hapo atajua, atawaza, kwamba huyu Mungu thamani yake ni
vipande thelathini, mwishowake utakuwaje? Fuatilia mwisho wa yuda
ulivyokuwa,wala haukuwa mzuri, alimaliza vibaya.Haponapo
tumemuona Gehazi, akiwaza moyoni mwake jinsi ya kupokea ile mali
alioikataa Elisha, naona Gehazi hakujua alichokuwa anafanya pale
kwa Elisha, labda hakuwa ameambiwa kwamba yukopale kujifunza
namna ya kumtumikia Mungu, alitakiwa kuwa makini sana,
kumwangalia Elisha anavyotumika. Alikataa sadaka zile za Naaman,
naye alipaswa kuziepuka, lakini kwakuwa hakuelewa somo hilo,
akajaribiwa, akazikimbilia, akazipokea kwa kudanganya kwamba
ametumwa na Elisha, akasema uongo na kilichotokea ni kibaya sana,
utakumbuka kwamba Elisha alikuwa ametumika chini ya Elia kwa
muda mrefu bila kuchoka, mpaka akafaulu kuupata upako ulio
kuwepo ndani ya Elia, na Gehazi naye alikuwa ametumika kwa muda
chini ya Elisha akitegemea kuupata upako uliokuwepo ndani ya
Elisha, matokeo yake tumeyaona alipodanganya, akakimbilia fedha,
dhahabu, Elisha alijisikia vibaya sana, akakumbuka muda alioupoteza
kumfundisha, moyo wake ukataabika ikamlazimu auite ule ukoma wa
Naaman, nao ukatii wito ukaja akauweka kwa Gehazi aliyekuwa
mtumishi wake, msomaji wangu huo ndio ulikuwa mwisho wa
Gehazi, alianza vizuri ,aliona miujiza mingi aliyoitenda mtumishi wa
Mungu Elisha, akitumiwa na Mungu,lakini haikumsaidia, haikugeuza
moyo wake usitamani fedha kama tulivyosoma huko nyuma kwamba
tusiipende fedha, tumeiona fedha ikifanyika mnyoo wa kumvua
Gehazi. Kutoka kwenye eneo lake la kuishi, maana alikuwa
anamtumikia Elisha mtumishi wa Mungu aliye hai, yeye Gehazi
aliishia kuchuma ukoma. Mafundisho ya Mungu wetu ni mazuri
kuliko fedha, lakini watu wengi wanapenda fedha kuliko mafundisho
Silaha za Adui Samuel Imori
76
ya neno la Mungu, jipime wewe unapenda nini kati ya mafundisho ya
Mungu na fedha na dhahabu? kuwa muwazi unapojibu.
Mith 8:10
Pokea mafundisho yangu wala sio fedha, na maarifa kuliko
dhahabu safi.
Neno la Mungu wetu linatushauri tupokee mafundisho ya Mungu,
tupokee maarifa ili tusiangamie, kumbuka mstari ule mzito
Hosea 4:6a
Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.
Watu wengi kwa kupenda fedha na kuchukia mafundisho,
kilichofuata ni kukosa maarifa, na walipokosa maarifa, bila shaka
umesikia kilichofuata niwazi waliangamia.Wanadamu wanapenda
utajiri, lakini upo utajiri usio na mwisho ni utajiri gani huo?
Mith 8:18
Utajiri na heshima ziko kwangu, naam, utajiri udumuo na haki pia
Nimeendelea kukuonyesha, nabado tunaendelea kuuona, tukaona kila
jambo lina majira yake, tukauona hatautajiri na majira yake, aweza
mtu aliekuwa tajiri akawa masikini kama tulivyoona huko nyuma na
sasa tumekutana na utajiri ule udumuo, utajiri usio na mwisho, mimi
ningependa kuupata huo utajiri usio na mwisho utajiri udumuo milele
na milele ni upi huo?
Silaha za Adui Samuel Imori
77
Math 13:45-46
Tena ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara,
mwenye kutafuta lulu nzuri, naye alipoona lulu moja ya thamani
kubwa, alikwenda akauza alivyo navyo vyote, akainunua.
Napenda kuyarudia rudia mambo mengine ili yaweze kukaa, ili
yaweze kueleweka zaidi.Lulu ni aina ya madini yenye thamani sana,
Bwana akaitolea mfano yakwamba mfanya biashara mmoja
ilimlazimu afanye jambo aliloliona kwamba ni la muhimu sana
kwake, Yawezekana watu wengine hata wafanyabiashara wengine
waliokuwa wenzake hawakumwelewa kabisa, pengine walimbatiza
hata majina kadri walivyoona kwamba inafaa, tumesoma vizuri kuwa
alikuwa katika shughuli zake za kilasiku, akitafuta biashara zake,
alikuwa anatafuta lulu, siku moja akakutana na lulu ya thaman kubwa
tena moja tu, ilimlazimu afanye jambo alienda akauza vitu vyake
vyote alivyokuwa navyo vyoote, fedha alioipata, ilitosha anunulie ile
lulu moja tu kwa sababu ilikuwa ya thamani kubwa,
haikulimganishwa na kitu chochote alichokuwa nacho, ikabidi auze
vyooote. Nimemkumbuka kijana mmoja aliyeambiwa na Bwana Yesu
kwamba akitaka kuurithi uzima wa milele, aende akauze mali zake,
akiisha kuuza awagawie masikini halafu arudi aje kwa Bwana Yesu
apate kuurithi uzima wa milele, Biblia inasema kijana akakasirika
akaukunja uso wake akaondoka.Lakini mfanya biashara wa lulu
alifaulu. Alijinyenyekeza, akashuka, na huo ndio moyo wa Mungu,
ndivyo Yesu alivyotufundisha kwa mujibu wa maandiko yafuatayo
Silaha za Adui Samuel Imori
78
Filp 2:8
Tena alipoonekana ana umbo kama mwanadmu, alijinyenyekeza
akawa mtii hata mauti, naam mauti ya msalaba, kwahiyo tena
Mungu alimwadhimisha mno akamkirimia jina lile lipitalo kila
jina, ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni na
vya duniani, na vya chini ya nchi, na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu
Kristo ni Bwana kwa utukufu wa Mungu Baba.
Mwana wa Mungu alie toka mbinguni, yeye alijinyenyekeza akawa
mtii, mahali pengine tunasoma wazi wazi kwamba alionewa na
akanyenyekea wala hakufunua kinywa chake, hata nimeukumbuka
wimbo tuliokuwa tunaimba zamani, tuliimba hivi, nanukuu
“Yesu kristo alikuwa na uwezo wa kupiga,
Lakini yeye alipopigwa alinyamaza kimya,
Alikuwa na uwezo wa kusema,
Lakini yeye aliposemwa alinyamaza kimya”
Linganisha mistari hiyo, hii hapa chini
Mith 18-23
Masikini hutumia maombi, bali tajiri hujibu kwa ukali.
Maneno ya mungu ni magumu ndio maana Yesu akawataka wasitoke
yerusalemu, bali wamungoje Roho mtakatifu aje awasaidie.nikwanini
tajiri anajibu kwa ukali?kwanini asitumie maombi, kwanini
Silaha za Adui Samuel Imori
79
asinyamaze? nini kinamsukuma ajibu kwa ukali? nimali aliyonayo,
imo kwenye moyo imemfundisha kwamba yeye ni bora kuliko mtu
mwingine, hana muda wa kujibu kwa upole, bali hujibu kwa ukali,h
awezi kujinyenyekeza, mtu akishiindwa kujinyenyekeza huyo moja
kwa moja anaendeshwa na kiburi, kikubwa ndicho kilimfanya licifer
atupwe chini, kiburi kikiwa ndani ya mtu kinamfundisha kwamba
yeye nibora kuliko mtu mwingine yeyote kiburi kikimpata mtu, huyo
ataishia kuangamia tu, hapo ndipo Lucifer alipo ishia.Mnyoo
mwingine ambao shetani anautumia kummaliza mwanadamu, mtu wa
kiburi utamjua katika kauli zake, mwenendo wake. Muasisi wa kiburi
ni Lucifer, amewaambukiza wengi, wenzetu waliotutangulia
walikisemea sana sana, nitakupatia maandiko machache
yanayoongelea kiburi, yako mengi ila nitakupatia machache.
Mith 8:13
kumcha Bwana ni kuchukia uovu kiburi na majivuno, na njia
mbovu na kinywa cha ukaidi pia nakuchukia.
Zab 10:2
Kwa kiburi chake asiye haki, mnyonge anafuatiwa kwa ukali, na
wanaswe kwa hila zizohizo walizoziwaza
Zab 12:3
Bwana ataikata midomo yote ya kujipendekeza, nao ulimi unenao
maneno ya kiburi
Silaha za Adui Samuel Imori
80
Zab 18:27
Maana wewe utawaokoa watu wanaoonewa, na macho ya kiburi
utayathiri.
Zab 19:13
Umzuie mtumishiwako asitende mambo ya kiburi, yasinitawale
mimi, ndipo nitakapokuwa kamili name nitakuwa safi, sina kosa
lililokubwa.
Zab 31:18
Midomo ya uongo iwe na ububu imneneayo mwenye haki maneno
ya kiburi kwa majivuno na dharau.
Zab 31:23
Mpendeni Bwana, ninyi nyote mliowatauwa wake, Bwana
huwahifadhi waaminifu humlipa atendaye kiburi malipo tele.
Zab 56:2
Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, maana waletao vita
juu yangu kwa kiburi ni wengi.
ZAB 73:6
Hivyo kiburi kimekuwa mkufu shingoni mwake, jeuri huwavika
kama nguo
Zab 101:5
Silaha za Adui Samuel Imori
81
Amsingiziaye jirani yake kwa siri huyo nitamharibu, mwenye
macho ya kiburi na moyo wa majivuno, huyo sitavumilia naye.
Zab 119:85
Wenye kiburi wamenichimbia mashimo ambao hawaifuati sharia
yako
Zab 119:122
Uwe mdhamini wa mtumishi wako apate mema, wenye kiburi
wasinionee.
Mpendwa msomaji wangu, tumeendelea kuona jinsi watu wa Mungu
wanavyoangamizwa kwa kukosa maarifa, Mungu wetu hapendi mtu
yeyote apotee, anatupenda mno, haya nimeyaeleza jinsi aduii yetu
anavyo waangamiza watu wa Mungu, ziko njia mbalimbali
anazotumia, sitaweza kuzielezea zote, ila zile chache ambazo
nimejaliwa kuzielezea, naamini macho yako yamefunguliwa,
umeziona na kama umeziona naamini utachukua hatua ya kujiweka
vizuri ili Yule adui yetu asikunase, na wewe uliye naswa tayari kwa
kuwa hukujua, naamini haujachelewa maadam unapumua, waweza
kabisa ukaamua kumtii Mungu na ukampinga huyo adui yetu, naye
atakimbia na utakuwa umebaki salama.
Rum 16:17-20
Ndugu zangu nawasihi, waangalieni wale wafanyao fitina na
mambo ya kukwaza kinyume cha mafundisho mliojifunza,
mkajiepushe nao, kwa sababu waliohivyo hawamtumikii Bwana
Silaha za Adui Samuel Imori
82
wetu Kristo, bali matumbo yao wenyewe, na kwa maneno laini na
ya kujipendekeza waidanganya
mioyo ya watu wanyoofu, maana utii wenu umewafikilia watu wote,
basi nafurahi kwaajili yenu, lakni nataka ninyi kuwa wenye hekima
katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya naye
Mungu wa amani atamseta shetani chini ya miguu yenu
upesi.Neema ya Bwana wetu Yesu kristo na iwe pamoja nanyi
amen.
Luk 4:1-13
Na Yesu, hali amejaa Roho mtakatifu, alirudi kutoka Yordan,
akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani akijaribiwa
na ibilisi, na siku hizo alikuwa hali kitu, hata zilipotimia aliona
njaa, ibilisi akamwambia, ukiwa ndiwe mwana wa Mungu, liambie
jiwe hili liwe mkate Yesu akamjibu imeandikwa ya kwamba mtu
hataishi kwa mkate tu.Akampandisha juu, akamwonyesha milki
zote za ulimwengu kwa dakika moja,ibilisi akamwambia, nitakupa
wewe enzi hii yote na fahari yake kwa kuwa imo mikononi mwangu,
nami humpa yeyote kama nipendavyo, basi wewe ukisujudu mbele
yangu yopte yatakuwa yako. Yesu akajibu akamwambia,
imeandikwa msujudie Bwana Mungu, umwabudu yeye peke yake,
akamwongoza mpaka Yerusalemu akamuweka juu ya kilele cha
hekalu akamwambia, ukiwa ndiwe mwana wa Mungu jitupe chini,
kwamaana imeandikwa, atakuagizia malaika zake wakulinde, na ya
kwamba mikononi mwao watakuchukua usije ukajikwaa mguu
Silaha za Adui Samuel Imori
83
wako katika jiwe, Yesu akajibu akamwambia imenenwa usimjaribu
Bwana Mungu wako, basi alipomaliza kila jambo, ibilisi
akamwacha akaenda zake kwa muda.
Msomaji wangu mpendwa, Mungu wetu atusaidie tupate kuelewa,
tupate kufundishika, mwalimu wetu aliyekuja duniani kututolea damu
yake, yeye alitufundisha namna ya kuishi katika dunia hii, na kuufikia
ushindi, alikutana na adui yetu ibilisi na akahojiana nanaye, mwisho
akashinda alimjaribu kwa mambo yafuatayo” ibilisi akamwambia
ikiwa ndiwe mwana wa Mungu liambie jiwe hili liwe mkate, Yesu
akajibu imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate tu” “Ibilisi
akamwambia, nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwakuwa
imo mikononi mwangu, nami humpa yeyote kama nipendavyo, basi
wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako. Yesu akajibu
imeandikwa msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke
yake ukiwa ndiwe mwana wa Mungu jitupe chini, kwa maana
imeandikwa atakuagizia malaika zake wakulinde, mikononi mwao
watakuchukua usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.Yesu akajibu
akamwambia imeandikwa, usimjaribu Bwana Mungu wako.
Napenda tuyaangalie majaribu aliyomjaribu
1. Alikaa siku arobaini akaona njaa
Filp 4:11-13
Sikwamba nasema hayo kwakuwa nina mahitaji, maana
nimejifunza kuwa na radhi na hali yeyote nilionayo, najua
kudhiliwa, tena najua najua kufanikiwa, katika hali yoyote na
Silaha za Adui Samuel Imori
84
katika mamboYoyote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa
na vingi na kupungukiwa, nayaweza mambo Yote katika yeye
anitiaye nguvu.
2. Ibilisi akamwonyesha fahari, mali ya duniahii, yewye
hakuzitamani.
Filp 3:8
Naam zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa
ajili ya uzuri usio na kiasi.Wakumjua Kristo Bwana wangu, ambaye
kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote, Nikiyahesabu kuwa
kama mavi ili nipate kristo.
3. Ibilisi akamwambia ikiwa ndiwe mwana wa Mungu jitupe,
kwa mana imeandikwa atakuagizia malaika zake wakulinde
naya kwamba mikononi mwao watakuchukua, usije
ukajikwaa mguu wako katika jiwe
Ebr 10:26-29
Maana kama tukifanya dhambi kusudi, baada ya kuupokea ujuzi
ile kweli, haibaki tena Dhabihu kwa ajili ya dhambi, bali kuna
kutazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa Moto uliotayari
kuwa wao wapingao, mtu aliyedharau sharia ya musa hufa posipo
Huruma kwa neno la mashahidi wawili au watatu, mwaonaje?
haikumpasa adhabu Iliyo kubwa zaidi mtu Yule alie mkanyaga
mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya Agano aliyotakaswa
kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?
Silaha za Adui Samuel Imori
85
Msomaji wangu mpendwa tumemuona yule adui yetu ibilisi
akimwabia Bwana wetu Yesu kwamba ajitupe ”jitupe” maana yake
jirushe, hata kama ngazi zipo hakuna haja ya kutelemka polepole
kuzitumia, jitupe tu na Mungu atatuma malaika wakushike na,
wakusaidie usijikwae usiumie. Hii ni kusemaje, yapo mambo
ambayo neno la Mungu linatuelekeza jinsi ya kuyafanya, lakini
wakati mwingine tunakaidi, wakati mwingine tunaamua kutekeleza
mambo mbayo tunayajua wazi kabisa kwamba si sahihi, tunafanya
makusudi kabisa, ninaomba Mungu wetu mwenye huruma
atuhurumie, aturehemu, pale ilipotokea tukaanguka kwenye mtego
huo wa makusudi, mtego huo wakujitupa, tukajikuta yumejitupa ili
malaika watushike, wakati mwingine hawakutushika tukaangukia
pua maana tulifanya makusudi. Naomba uyatafakari majaribu hayo
yote ambayo Bwana wetu aliya pitia, na akashinda tumeona wazi
wazi njaa haikumsumbua, shibe haikumsumbua, fahari ya
ulimwengu huu haikumsumbua, kujirusha, kujiamulia kutenda
lolote lililo kinyume na Mungu hakufanya hivyo. Jikague
ujihakikishe ulivyo, wapi umeshindwa, wapi unatakiwa
uparekebishe, parekebishe maana bado ungali na muda wa kufanya
hivyo katika jina la Baba/Mwana na Roho mtakatifu Amen.
Silaha za Adui Samuel Imori
86
HITIMISHO
Nakushukuru sana wewe msomaji wangu mpendwa, kwa kutumia
muda wako kukisoma kitabu hiki , maana ningekiandika kasha
usikisome isingekuwa na maana. Naamini hauko vile ulivyokuwa
kabla hujakisoma, nakushauri umshirikishe mwingine Yule
umpendaye, ili naye akisome. Nakut akia ushindi katika safari
yako kwenda mbinguni, mahali utakapoishi milele na milele, mahali
ambapo hakuna kilio, wala mateso ya aina yeyote ile, kule ambapo
tutaishi na Baba yetu, muumba mbingu na nchi, niamaombi yangu
kwamba hautachoka katika safari hii, ambayo alituambia wazi
wazi, kwamba wale watakao shinda watavikwa mavazi meupe na
watapewa jina jipya.
Uf 2:17
Yeye aliye na sikio na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia
makanisa, yeye ashindaye nitampa baadhi ya le mana iliyofichwa,
nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya hilo limeandikwa JINA JIPYA
asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.
Uf 2:12
Yeye ashindaye nitamfanya nguzo katka hekalu la Mungu wangu
wala hatatoka humo tena kabisa, name nitaandika juu yake jina la
Mungu wangu na jina la mji wa Mungu wangu. Huo Yerusalem
mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu
mwenyewe lile JIPYA.
Silaha za Adui Samuel Imori
87
Msomaji wangu nakutakia safari njema iliyojaa ushindi, Mungu
akuwezeshe maneno haya usiyasikie tu, na ukaishia njiani, jitie
nguvu, uwena moyo mkuu, ufike ulipokee jiwe leupe lenye jina lako
“jipya”, nafurahia sana sana ninaposoma ya kwamba
.jina langu litakuwa jipya
.jina la Yesu litakuwa jipya
.jerusalemu itakuwa mpya
.nchi nayo itakuwa mpya
Ee Mungu tusaidie tuyaone mambo mapya, katika jina la YESU
Amen.