Methali za Kiswahili zilizoachwa: sababu na athari zake kwa ...

125
The University of Dodoma University of Dodoma Institutional Repository http://repository.udom.ac.tz Humanities Master Dissertations 2015 Methali za Kiswahili zilizoachwa: sababu na athari zake kwa jamii Juma, Aley Rashid Chuo Kikuu cha Dodoma Juma, A. R. (2015). Methali za Kiswahili zilizoachwa: sababu na athari zake kwa jamii. Dodoma: Chuo Kikuu cha Dodoma http://hdl.handle.net/20.500.12661/540 Downloaded from UDOM Institutional Repository at The University of Dodoma, an open access institutional repository.

Transcript of Methali za Kiswahili zilizoachwa: sababu na athari zake kwa ...

The University of Dodoma

University of Dodoma Institutional Repository http://repository.udom.ac.tz

Humanities Master Dissertations

2015

Methali za Kiswahili zilizoachwa: sababu

na athari zake kwa jamii

Juma, Aley Rashid

Chuo Kikuu cha Dodoma

Juma, A. R. (2015). Methali za Kiswahili zilizoachwa: sababu na athari zake kwa jamii.

Dodoma: Chuo Kikuu cha Dodoma

http://hdl.handle.net/20.500.12661/540

Downloaded from UDOM Institutional Repository at The University of Dodoma, an open access institutional repository.

METHALI ZA KISWAHILI ZILIZOACHWA: SABABU NA ATHARI ZAKE KWA

JAMII

Aley Rashid Juma

Tasnifu Iliyowasilishwa kwa Ajili ya kukamilisha Masharti ya Shahada ya

Uzamili ya Sayansi ya Jamii katika Fasihi ya Kiswahili

Chuo Kikuu cha Dodoma

Oktoba, 2015

i

ITHIBATI YA MSIMAMIZI

Aliyesaini hapo chini, anathibitisha kwamba, ameisoma tasnifu inayoitwa;

MethalizaKiswahili Zilizoachwa: Sababu na Athari zake kwa Jamii, na

amependekeza kwamba, inafaa ikubaliwe na Chuo Kikuu Cha Dodoma, kwa ajili

ya tunzo ya Shahada ya Uzamili katika Fasihi ya Kiswahili.

…………………………….

Profesa Frowin Paul Nyoni

(Msimamizi)

Tarehe ……………………..

ii

IKIRARI NA HAKIMILIKI

Mimi,Aley Rashid Juma, nathibitisha kuwa tasnifu hii ni kazi yangu halisi na kwamba

haijawahi kuwasilishwa na wala haitawasilishwa katika Chuo Kikuu kingine chochote,

kwa ajili ya utunuku wa Shahada yoyote ile.

Saini ……………………….

Tarehe …………………….

Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuzalisha, kunakili, wala kusambaza sehemu

yoyote ya tasnifu hii, kwa namna yoyote, bila ya kibali cha maandishi, kutoka kwa

mwandishi au Chuo Kikuu Cha Dodoma.

iii

TABARUKU

Natabaruku kuitolea hidaya tasnifu hii kwa hawa wafuatao:

Kwanza ni mpendwa mama yangu, Mwatima Vuai Mkanga. Yeye ndiye aliyenizaa

nakunilea kwa umakini mkubwa hadi kufikia ukubwani. Pia,ndiye mwalimu wangu wa

kwanza wa maadili, dini na mbinu za maisha yangu ya baadaye kwa jumla. Kila

nimuonapo huvuta hisia za mbali kwa kiasi gani alivyopata tabu kwa ulezi wa peke yake

bila ya kuwa naye karibu mfarijimume wake kwa kazi hiyo ngumu. Nakiri kuwa sina

cha kumlipa zaidi ya kuwa karibu naye, na kumuonesha mapenzi ya dhati kwa bawa la

huruma, ucheshi na msaada wa hali na mali, huku nikimuombea kwa Mwenyezimungu

ampe umri mrefu wenye afya na kheri nyingi, Amin.

Pili ni Baba yangu mzazi, Bwana Rashid Juma Ali. Kwa hakika alitamani sana

kuendelea na maisha katika hii dunia ili ashirikiane na mama katika kumlea mtoto wao

kwa huruma na mapenzi, lakini haikuwezekana, kwaniumri wake ulimalizika kwa

kutangulia mbele ya haki siku ishirini na tatu tu tokea kuzaliwa kwa mwanawe

mpendwa. Roho na nafsi yangu zinalitembelea kaburi lake kila siku ili kupata hisia za

mapenzi yake kwangu na yangu kwake kwa kumuomba Mwenyezimungu amsamehe

makosa yake, na amuweke mahali pema Peponi, Amin.

iv

SHUKURANI

Kwanza, namshukuru kwa dhati na kwa unyenyekevu wote Mwenyezimungu

aliyeniumba, kunikuza, kunipa afya, akili na fahamu na kisha akaniwezesha

kuikamilisha kazi hii muhimu na ya kihistoria katika maisha yangu.

Pili, napenda kumshukuru kwa dhati msimamizi wangu wa utafiti huu Profesa Frowin

Paul Nyoni ambaye amejaa busara, hekima na ucheshi katika kutoa maelekezo ya kazi

hii hadi pale ilipokamilika. Juhudi zake za kipekee sitazisahau maishani mwangu na

namuahidi kumuenzi kwa kufuata nyayo zake.

Tatu, nawashukuru wahadhiri wangu wote wa programya Shahada ya umahiri ambao ni

Dkt. Khatib, Prof. Madumulla,Dkt. Ponera, Dkt. SebondenaDkt. Songoyi. Maarifa yao

yalikuwa ndiyo msingi muhimu wa kazi hii ya utafiti katika Fasihi ya Kiswahili.

Nne, ninawashukuru kwa dhati wanafunzi wenzangu wote wa fani ya Fasihi ya

Kiswahili mwaka 2013/2015. Ushirikiano na msaada wao kwangu, ulisadifu vyema

katika kuyamudu masomo yangu na katika kuikamilisha kazi hii muhimu.

Tano, naishukuru pia familia yangu, mke wangu mpenzi Fatma Nassor Ali na watoto

wangu wapendwa Abdulhamid, Layla, Aisha, Abdulbasit na Latifah kwa heshima,

upendo na ustahamilivu wao mkubwa katika kipindi chote cha mimi kuwa mbali nao.

Shukrani zangu nyengine ni kwa muhisani wanguambaye alikuwa na kazi kubwa ya

kunipa moyo, ushauri na misaada ya hali na mali kila nilipokwama kwa muda wote wa

progam na kazi yangu hii ya utafiti.

Hao wote niliyowataja hapo juu, ndugu na wengineo ambao sikupata nafasi ya kuwataja

ama kuwaainisha hapa, nawashukuru kwa dhati, na kwa jumla, nawaombea kheri na

mafanikio katika maisha yao yote, Amin.

v

IKISIRI

Tasnifu hii inahusuMethali za Kiswahili Zilizoachwa: Sababu na Athari zakekwa

Jamii. Methali za Kiswahili zilizoachwa ni semi zenye muhutasari wa mawazo ya

busara kwa mkato zinazotokana na jamii ya Waswahiliambazo, kwa sasa

hazitumikitena. Methali hizo zilichunguzwa katika jamii ya Waswahili waishio Zanzibar

ambayo katika utafiti huu inajulikana kwa jina la jamii ya Wazanzibari.Utafiti ulilenga

kuzibainisha baadhi ya methali hizo, kuchunguza sababu na athari za kuachwa kwake

katika jamii hiyo.Sababu ya kuchunguza suala hilo ilitokana na mtafiti kubaini baadhi ya

methali hizo ambazo zilimvutia na kuona kuachwa kwake ni hasara kwani jamiiitapoteza

vitu muhimu. Hivyo, shabaha ya kufanya utafiti huu nikuibua upya matumizi ya methali

hizo ili jamii iweze kufaidika na hekima, falsafa, mafunzo na mvuto wake.

Mbinu zilizotumika kupata data ni udurusu wa maandiko, udodosaji, mahojiano na

mjadala wa kikundi. Jamii tafitiwa ni ya Wazanzibari kwa kuwa ndiko ulikofanywa

utafiti huu. Data zilizopatikana kutoka uwandani zilichanganywa na zile za

maktabani.Nadharia ya Uamilifu yenye msingi wa kuangalia kazi ya fasihi simulizi

ilitumika.

Matokeo ya utafiti yamebainikuwepokwa methali zilizoachwaambazo baadhi yake

zimeoneshwa katika tasnifu hii. Pia,zipozinazotumiwa sana,kwa wastani na kwa

nadra.Sababu za kuachwa methali hizo ni mvuvumko wa maendeleo ya sayansi na

teknolojia, ukosefu wa taasisi za kuzihifadhi na kuzirithisha, mabadiliko ya msamiati

uliotumika katika methali hizo, na kuibuka kwa methali nyingi mpya.Athari chanyakwa

jamii, ni kuondoka kwa msamiati mgumu usiotumika sasa,na kuiruhusu lugha kuwa na

mabadiliko chanya ya maendeleo ya sayansi na teknolojia. Kwa upande wa athari hasi ni

kufifia kwautamaduni wa Wazanzibari,jamii kuzikosa adili za methali hizo, na jamii

kukosa burudani itokanayo na methali hizo.Kwa matokeo hayo, utafiti huu ni muhimu

kwa walimu, wanafunzi, wataalamu, na jamii nzima ya Wazanzibari na Waswahili kwa

jumla.Tasnifu hiiina sura tano za ripoti ya utafiti,marejeleo pamoja na baadhi ya

viambatisho vya utafiti huu.

vi

YALIYOMO

ITHIBATI YA MSIMAMIZI ..............................................................................................

IKIRARI NA HAKIMILIKI ............................................................................................. ii

TABARUKU ................................................................................................................... iii

SHUKURANI ................................................................................................................... iv

YALIYOMO ..................................................................................................................... vi

SURA YA KWANZA ....................................................................................................... 1

UTANGULIZI ................................................................................................................... 1

1.1 Usuli wa Tatizo la Utafiti ............................................................................................. 1

1.2 Tamko la Tatizo la Utafiti ............................................................................................ 7

1.3 Malengo ya Utafiti ....................................................................................................... 8

1.4.1 Lengo la Jumla .......................................................................................................... 8

1.4.2 Malengo Mahususi .................................................................................................... 8

1.5Maswali ya Utafiti ......................................................................................................... 8

1.6Umuhimu wa Utafiti ..................................................................................................... 9

1.7Nadharia ya Uchanganuzi wa Data ............................................................................... 9

1.8Mipaka ya Utafiti ........................................................................................................ 12

1.9Muhutasari wa Sura ya Kwanza .................................................................................. 13

SURA YA PILI ................................................................................................................ 14

MAPITIO YA MAANDIKO ........................................................................................... 14

2.2 Mapitio ya Maandiko Kuhusu Fasihi Simulizi .......................................................... 14

2.3 Mapitio ya Maandiko Kuhusu Semi .......................................................................... 18

2.4Mapitio ya Maandiko Kuhusu Methali ....................................................................... 21

2.5Mapengo Yanayojitokeza Kutokana na Mapitio ya Maandiko................................... 32

2.6 Muhutasari wa Sura ya Pili ........................................................................................ 32

SURA YA TATU ............................................................................................................. 33

USANIFU NA MBINU ZA UTAFITI ............................................................................ 33

3.1 Utangulizi ................................................................................................................... 33

3.2 Mpango wa Utafiti ..................................................................................................... 33

vii

3.3 Eneo la Utafiti ............................................................................................................ 34

3.4 Walengwa wa Utafiti.................................................................................................. 34

3.4.1 Jamii Tafitiwa.......................................................................................................... 34

3.4.2 Aina na Dhana ya Usampulishaji ............................................................................ 35

3.5 Ukusanyaji wa Data ................................................................................................... 36

3.5.1 Njia na Zana za Ukusanyaji wa Data ...................................................................... 36

3.5.1.1Udurusu wa Kimaktaba ......................................................................................... 36

3.5.1.2 Mahojiano ............................................................................................................ 37

3.5.1.3 Mjadala wa Vikundi ............................................................................................. 37

3.5.1.4 Udodosaji ............................................................................................................. 37

3.5.1.5 Uchunguzi ............................................................................................................ 38

3.5.2 Zana za Kukusanyia Data........................................................................................ 38

3.5.3 Mchakato wa Ukusanyaji wa Data .......................................................................... 39

3.6 Uchanganuzi wa Data ................................................................................................ 40

3.7 Uhalali na Uthabiti wa Matokeo ya Utafiti ................................................................ 43

3.8 Itikeli za Utafiti .......................................................................................................... 43

3.9 Muhutasari wa Sura ya Tatu ...................................................................................... 44

SURA YA NNE ............................................................................................................... 45

UWASILISHAJI NA MJADALA WA MATOKEO YA UTAFITI ............................... 45

4.1 Utangulizi ................................................................................................................... 45

4.2 Methali za Kiswahili Zilizoachwa katika Jamii ya Wazanzibari ............................... 45

4.2.1 Miktadha ya Maisha ya Jamii ya Wazanzibari ....................................................... 45

4.2.1.1 Muktadha wa Kijografia na Kiuchumi ................................................................. 47

4.2.1.2 Muktadha wa Kiutamaduni .................................................................................. 48

4.2.1.3 Muktadha wa Kifasihi .......................................................................................... 50

4.2.2 Methali za Kiswahili Zilizoachwa .......................................................................... 52

Jeduwali la methali zilizoachwa katika jamii ya Waswahili Zanzibar ............................ 56

4.3 Sababu za Wazanzibari Kuacha Baadhi ya Methali za Kiswahili ............................. 70

4.3.1 Mvuvumko wa Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia ............................................ 71

4.3.2 Mabadiliko ya Msamiati Uliotumikakatika Methali hizo ....................................... 74

4.3.3 Kuwepo kwa Methali Nyingi Mpya ........................................................................ 76

viii

4.3.4 Ukosefu wa Taasisi za Kuzihifadhi na Kuzirithisha Methali.................................. 78

4.4 Athari za Kuachwa kwa Baadhi ya Methali za Kiswahili.......................................... 79

4.4.1 Tija Zilizopatikana .................................................................................................. 80

4.4.1.1 Kuondoka kwa Msamiati Mgumu (Usiotumika) ................................................. 80

4.4.1.2 Kuiruhusu Lugha Kulandana na Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia .............. 81

4.4.2 Madhara yanayopatikana ........................................................................................ 82

4.4.2.1Kufifia kwa Utamaduni wa Wazanzibari .............................................................. 82

4.4.2.2 Jamii Kuzikosa Adili za Methali .......................................................................... 83

4.4.2.3 Jamii Kukosa Burudani Inayotokana na Methali hizo ......................................... 84

4.5 Muhutasari wa Sura ya Nne ....................................................................................... 86

SURA YA TANO ............................................................................................................ 88

MUHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO ..................................................... 88

5.1 Utangulizi ................................................................................................................... 88

5.2 Muhutasari wa Tasnifu ............................................................................................... 88

5.3 Utoshelevu wa Nadharia Iliyotumika ........................................................................ 90

5.4 Mchango Mpya wa Utafiti ......................................................................................... 91

5.5 Maoni na Mapendekezo ya Mtafiti ............................................................................ 91

MAREJELEO .................................................................................................................. 93

VIAMBATISHO .............................................................................................................. 99

A: Barua za Ithibati ya Kufanyia Utafiti .......................................................................... 99

A1: Barua ya kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma............................................................... 99

A2: Kibali cha Ruhusa ya Kufanyia Utafiti Zanzibar. ................................................... 100

B: MIONGOZO YA USAILI, DODOSO NA UDURUSU WA MAKTABA .............. 101

B1: Mwongozo wa Hojaji kwa Wataalamu na Wazee wenye uzoefu ........................... 101

B2: Mwongozo wa Usaili kwa Wanafunzi wa Sekondari na Diploma ya Kiswahili .... 102

B3: Mwongozo wa Dodoso kwa Wakufunzi na Vyuo na Watu wa Mitaani ................. 103

B.4: Mwongozo wa Udurusu wa Maktaba ..................................................................... 105

C.2: Methali Zinazotumiwa kwa wastani katika Jamii ya Wazanzibari ........................ 110

C.3: Methali zinazotumiwa kwa nadra katika jamii ya Wazanzibari............................. 113

ix

VIFUPISHO VILIVYOTUMIKA

BAKIZA Baraza la Kiswahili la Zanzibar

UZ Zanzibar University

SUZA The State University of Zanzibar

TAKILUKI Taasisi ya Kiswahili na Lugha za Kigeni

TATAKI Taasisi ya Taaluma za Kiswahili

Bi Bibi

Bw. Bwana

Prof. Profesa

Dkt. Daktari

Na. Namba

1

SURA YA KWANZA

UTANGULIZI

Utafiti huu ulichunguza sababu na athari za kuachwa kwa baadhi ya methali za

Kiswahili, katika jamii ya Wazanzibari.Sura hii imeelezea vipengele vya usuli na tamko

la tatizo la utafiti, malengo na masuali ya utafiti.Vipengele vingine vilivyoelezewa

katika sura hii ninadharia, umuhimu pamoja na mipaka ya utafiti.

1.1 Usuli wa Tatizo la Utafiti

Jamii ya Waswahili wa Zanzibar, kama jamii za Waswahili wengine, imekuwa na

umuhimu mkubwa na fasihi simulizi ya Kiswahili. Wenyeji wa Zanzibar mara

nyingi wameshuhudia vikao vya mabibi na mababu wakiwasimulia hadithi murua

wajukuu zao (Othman na Yahya, 2004). Pia, wameshuhudia mara nyingi maghani ya

mashairi, ngoma, maigizo na semi zikitumika katika sherehe zao za arusi, jando na

unyago. Aidha, wamekuwa wakiwasikia watu wakiwasilisha ujumbe kwa kutumia

moja ya semi za Kiswahili. Hadi hii leo amali hizo zimekuwa zikiendelea kufanyika,

ingawa kwa sasa hivi zimekuwa zinapungua kwa kiasi kikubwa kutokana na sababu

mbalimbali.

Fasihi simulizi imegawika katika matawi kulingana na muundo, tabia, uwasilishwaji

na muktadha wa matumizi yake. Hakuna idadi iliyokwishakubalika na wataalamu

wote juu ya matawi hayo, lakini wataalamu wengi wamekaribiana katika

2

kuzibainisha aina hizo zinazoitwa tanzu za fasihi simulizi.Kwa mujibu wa Mulokozi

(1989), tanzu za fasihi simulizi ni sitana amezigawa kwa kuzingatia umbile na tabia

ya kazi inayohusika, pia kwa kuzingatia muktadha na namna ya uwasilishaji wake

kwa hadhira. Tanzu hizo ni mazungumzo, masimulizi, maigizo, ushairi, ngomezi

pamoja na semi. Kwa kuwa kila moja ya tanzu hizi ni pana na ina mambo mengi

ndani yake, ndio maana utafiti huu, ulijiegemeza katika utanzu mmoja peke yake,

ambao ni utanzu wa semi.

Mulokozi (1996) anaeleza kuwasemi ni tungo au kauli fupifupi za kisanaa ambazo

hubeba maana au mafunzo muhimu ya kijamii. Semi ni moja ya utanzu wa fasihi

simulizi unaojumuisha tanzu ndogondogo za lakabu, mafumbo, methali, misemo na

vitendawili. Naye Wamitila (2004), anazieleza semi kuwa ni kundi la tungo za fasihi

simulizi ambazo ni fupifupi na zina matumizi ya taswira, tamathali na ishara kwa

mapana. Ujumbe wake huwasilishwa kwa njia ya mkato, yenye mkokotezo na

kukumbukika haraka.Kwa kawaida, utanzu wa semi tofauti na tanzu nyengine za

fasihi simulizi, hutumika mara nyingi zaidi, takriban kila siku na katika kila aina ya

muktadha ndani ya jamii yoyote ile. Kila jamii moja huwa na semi zake, ingawa kwa

baadhi yake huwa na uhusiano mkubwa wa kimaana baina ya semi za jamii moja na

nyengine. Semi hutofautiana kutokana na lugha, utamaduni, itikadi na idili za jamii.

Jamii ya Waswahili nayo, inazo semi zao na ni wajuzi wa matumizi yake. Huzitumia

katika mazungumzo yao ya kawaida, nakatika sherehe zao mbalimbali. Mara nyingi

watunzi wa fasihi andishi ya Kiswahili, nao wamekuwa ni weledi wa kuzitumia semi

mbalimbali katika kazi zao. Kwa jamii ya Kiswahili, semi hutumiwa na walimu

3

wanapofundisha, viongozi wanapohutubia, wazazi wanapowaasa au kuwashajihisha

watoto wao, vile vile semi hutumiwa na hata watu kwa wapenzi wao au wagomvi

wao (Salum, 2007). Wote hao huzitumia semi hizo, kwa madhumuni mbalimbali

kama vile kuelimisha, kuburudisha, kuonya, kuasa, kukosoa na kuadabisha.

Kutokana na upana wa matumizi ya semi kwa jamii za Wazanzibari, ndio maana

maandishi ya semi yakawa yameenea katika sehemu mbalimbali za jamii yao. Katika

zama hizi, semi Zanzibar huandikwa kwenye kanga, magari, makawa, mikoba, kuta

za nyumba, mapazia, milangoni kwenye fulana na kadhalika (Mbaruk, 2011:10).

Wataalamu wamevibainishavipera vya semikuwa ni lakabu, mafumbo, methali,

misemo, nahau na vitendawili. Kutokana na upana wa utanzu wa semi, haikuwa

rahisi kwa mtafiti, kuvishughulikia vipera vyote na hivyo, utafiti huu ulijikita katika

kipera kimoja ambacho ni methali.

King‟ei (1998), anasema kuwamethali ni usemi mfupi, wenye maana pana, na busara

au hekima ulio na mizizi katika jamii fulani na unaoelimisha, kuasa au kukejeli watu

au vitendo fulani katika jamii lakini kwa njia iliyofumbwa na kuwekewa tasfida. Nao

Mulokozi (1996), na Njogu na Chimerah (1999) wanazieleza methali kuwa ni semi

fupifupi zinazoeleza kwa muhutasari fikra au mafunzo mazito yaliyotokana na

uzoefu wa kijamii. Mara nyingi mawazo hayo huelezwa kwa kutumia tamathali hasa

sitiari na mafumbo. Methali ni utanzu tegemezi ambao kutokea kwake kunategemea

fani nyengine za kushikamana nazo.Mifano ya fani hizo ni mazungumzo, hotuba au

majadiliano mazito katika miktadha maalum ya kijamii. Baadhi ya methali huwa ni

vielelezo au vifupisho vya hadithi fulani inayofahamika vizuri kwa jamii. Methali

nyingi zina muundo wa sehemu mbili, sehemu ya kwanza inayoanzisha wazo na ya

4

pili inayokamilisha au kulikanusha wazo hilo. Kwa mfano; Tamaa mbele mauti

nyuma, na Haraka haraka hainaBaraka. Hata hivyo, methali hazina ulazima wa

kuwa na muundo kama huo, kwani zipo zenye miundo tofauti na huo.

Kama ilivyo kwa kipera chochote cha fasihi simulizi, methali nazo asili yake ni jamii

husika. Hivyo, methali za Kiswahili chimbuko lake ni jamii ya Waswahili, ambapo

nyingi zao zimebuniwa kutokana na lugha ya Kiswahili na lugha za Kibantu. Hata

hivyo, baadhi ya methali za Kiswahili zina asili ya lugha za kigeni, hasa Kiingereza

na Kiarabu. Sifa za methali za Kiswahili kwanza ni kupokewa kutoka kizazi hadi

kizazi, pili ni uchache wa maneno na tatu ni kuwa na maana iliyokamili. Sifa

nyingine ni kuwa na maana za kifalsafa, maana na matumizi yake kutegemea

muktadha, na mara nyingi huwa na muundo wa swali na jibu. Kwa upande wa

dhima, methali za Kiswahili zina dhima ya kuonya, kuhimiza, kuliwaza, kutilia

mkazo jambo, kukejeli na kudhihaki. Dhima nyengine ni kuhifadhi utamaduni,

kushauri, kudumisha matumizi ya msamiati, kuelimisha na kuburudisha.

Jamii ya Waswahili inazo methali za Kiswahili nyingi sana. Inakadiriwa kuwa ni

zaidi ya methali elfu mbili na mia tano. Methali zimeanza kuwepo miaka mingi

iliyopita, kiasi cha kukadiriwa tokea kuanza kwa jamii ya Waswahili, na zimekuwa

zikirithiwa kutoka kizazi hadi kizazi. Methali zimekuwa zikibuniwa katika kila zama

ya maisha ya mwanadamu. Kubuniwa huko hutokana na mahitaji ya jamii kwa

mujibu wa idili za jamii husika. Kwa hivyo, jamii ya Waswahili imeshuhudia

methali za aina kwa aina zikitumika katika jamii yao, bila kumjua nani mwanzilishi

5

wake. Methali hizo, ni nzuri katika matamshi, mafunzo, hekima na falsafa, na

miundo yake.

Yapo maelezo mengi yaliyoelezwa kuhusu uzuri na umuhimu wa methali kwa jamii

ya Waswahili na hata jamii nyengine duniani.Katika maelezo hayo wapo

waliozifananisha methali na roho katika mwili (Finnegan, 1979).Wapo

waliozifananisha na viungo katika chakula (Mhilu, 2011).Pia,wapo waliozifananisha

na mafuta bora ya kupikia chakula. Wote hao wameeleza hayo kwa lengo la

kuonesha umuhimu wa methali katika jamii na kwa hakika methali ni muhimu katika

lugha ya jamii yoyote ulimwenguni ikiwemo ya Kiswahili. Pamoja na uzuri na

umuhimu huo wa methali katika jamii ya Waswahili, kwa muda mrefu sasa, baadhi

ya utajiri na urithi huo mwema, umekuwa ukiachwa kutumiwa katika jamii ya

Wazanzibari. Tatizo hili lilikuwepo tangu zamani, lakini limejitokeza zaidi katika

miaka ya elfu mbili na kuendelea hadi sasa. Kunamethali nyingi zilizokuwa zikitoa

mafunzo mema na zenye utajiri wa misamiati mizuri ya lugha zimeachwa kutumiwa

(Farsi, 1979: Hassan, 2013). Kwa mfano: “Mkataa chinjo hupata mtanda”, “Endapo

juu kipungu hafikilii mbinguni”, “Boi manda malipo yake parapanda”, “Sumu ya

huyu ni dawa ya mwengine”, “Utamu wa wazimu aujuaye mwendawazimu

mwenyewe” na nyengine nyingi. Methali hizo sasa hazisikiwi zikisemwa katika

mazungumzo ya kawaida, hazionekani kutumika katika maandishi, wala hazijulikani

na kizazi kilichopo, isipokuwa kwa sasa zimebakia katika kumbukumbu za wazee

wachache waliobaki hai katika mitaa au katika vitabu vichache vilivyotungwa

zamani.

6

Hali hii si nzuri na haifai kufumbiwa macho, kwani kuachwa moja kwa moja

zisitumike ni hasara kwa jamii, kwa sababu kwa mujibu wa Msuya(1979),fasihi

simulizi, zikiwemo semi na hasa methali, ni hazina kubwa ya hekima na falsafa

ambazo kwa kawaida huwa hazipatikani hata vitabuni. Kwa hivyo, hali hiyo

inaonesha wazi kuwa, kuna haja ya kulishughulikia suala la kuachwa kwa baadhi ya

methali za Kiswahili, katika matumizi ya jamii ya Waswahili ikiwemo ya

Wazanzibari. Kumekuwepo fununu kuwa sababu ya kuachwa kutumiwa fasihi

simulizi zikiwemo methali ni mtindo wa maisha, kwa maana kuwa binadamu na

viumbe wengine huwepo duniani kwa kipindi na kisha wakatoweka na kuja

wengine; na hivyo, methali nazo hufuata mkumbo huo. Maendeleo ya sayansi na

teknolojia yaliyoshamiri ulimwenguni hivi sasa ni sababu nyengine

inayofikiriwa.Pia,ni kutokana na dhana potofu kuwa fasihi simulizi ni sanaa ya watu

wajinga wasiojua kusoma, ambapo kwa sasa hali hiyo inatoweka kwa nguvu

(Khamis, 1983). Hata hivyo, hizi ni baadhi ya sababu zinazofikiriwa kijuujuu tu,na

hazina uhakika wowotekwani hadi hivi sasa haujafanywa utafili juu ya suala hili.

Umuhimu wa fasihi simulizi unaonekana wazi duniani kote hivi sasa. Hali hii

imesababisha uonekane pia na umuhimu wa kuzitunza tanzu zake. Hii ndio sababu

jamii nyingi zinashughulika katika kuzifanyia tafiti mbalimbali tanzu zao za fasihi

simulizi, kwa lengo la kuziimarisha na kuziwekea mustakabali mwema wa siku

zijazo (Khamis, 1983). Fasihi simulizi ya Kiswahili nayo inahitaji kufanyiwa tafiti

kama hizo, katika tanzu zake zote. Hadi sasa hakujakuwa na tafiti nyingi na za

kutosha zinazohusiana nayo. Hii ni kwa sababu mbali mbali zikiwemo za uchache

wa wataalamu na za kiuchumi. Tafiti zilizofanyika bado ni chache sana kuiwezesha

7

fasihi simulizi ya Kiswahili kuimarika katika nyanja za kitaaluma na kimaendeleo.

Kwa ajili hiyo, utafiti wowote wa fasihi simulizi ya Kiswahili kipindi hiki, utakuwa

ni muhimu katika kuisogeza kwenye lengo la juu, ikitarajiwa kuwa ni pamoja na

tafiti zinahusiana na methali za Kiswahili kama huu.

1.2 Tamko la Tatizo la Utafiti

Zimekuwepo baadhi ya tafiti zilizofanywa kuhusu semi kwa jumla au baadhi ya vipera

vyake zikiwemo methali, lakini tafiti zote hizo hazijagusia sababu wala athari za

kuachwa kutumiwa kwa methali hizo katika jamii ya Waswahili. Kwa mfano,

Madumulla (2005) amefanyia kuhusu methali na misemo katika jamii ya Wahehe.

Mulokozi (1985) ametafiti kuhusu fani na maudhui katika methali za Kiswahili. Hassan

(2013) utafiti wake ni kuhusu dhima ya methali katika kudumisha maadili, Uledi (2012)

amefanyia kuhusu muundo na lugha katika methali na vitendawili. Ndaro (2012)

ametafiti kuhusu fani katika methali za Kidigo. Mgulu (2011) utafiti wake ulihusu

usanaa katika Methali, na Simchimba (2012) alifanyia falsafa ya Ki-Afrika katika

Methali za Kiswahili. Hawa wote wamefanyia tafiti zao juu ya muundo, lugha, dhima,

au fani na maudhui ya methali; na hivyo, kutougusia upande wa athari au sababu za

kuachwa kutumika kwa methali katika jamii yoyote ile. Mbrouk (2011) amefanyia

utafiti juu ya athari za semi kwa jamii ya Wazanzibari, lakini amejikita katika semi

zinazotumika katika kanga peke yake; na hivyo, kuacha pengo katika sababu na athari za

methali zilizoachwa kutumika katika jamii hiyo. Kwa sababu hiyo, utafiti ulihitajika ili

zijulikane sababu za kuachwa kwa baadhi ya methali katika jamii ya Wazanzibari, ikiwa

ni pamoja na kubainisha athari inayoweza kuipata jamii hiyo kutokana na tatizo hilo. Hii

8

ndio maana utafiti huu ulijikita katika eneo hilo ili kupata ukweli juu ya methali za

Kiswahili zilizoachwa, sababu na athari zake kwa jamii ya Wazanzibari.

1.3 Malengo ya Utafiti

Utafiti huu uliongozwa na malengo yafuatayo;

1.3.1 Lengo la Jumla

Lengo kuu ni kuchunguza sababu na athari za kuachwa kwa baadhi ya methali za

Kiswahili katika Jamii ya Wazanzibari.

1.3.2 Malengo Mahususi

a) Kubainisha methali za Kiswahili zilizoachwa katika jamii ya Wazanzibari;

b) Kuchunguza sababu za kuachwa kwa baadhi ya Methali hizo katika jamii ya

Wazanzibari, na;

c) Kuchunguza athari za kuachwa kwa baadhi ya methali hizo kwa jamii ya

Wazanzibari.

1.4 Maswali ya Utafiti

a) Ni methali zipi za Kiswahili zilizoachwa kutumiwa katika jamii ya Wazanzibari?

b) Kuachwa kutumiwa kwa methali za Kiswahili katika jamii ya Wazanzibari

kunatokana na sababu zipi?

9

c) Kuna athari gani zinazotokana na kuachwa kwa baadhi ya methali za Kiswahili

katika jamii ya Wazanzibari?

1.5 Umuhimu wa Utafiti

Utafiti huu una umuhimu ufuatao; Kwanza, unatarajiwa kuwa chachu ya kufufua

upya matumizi ya methali nzuri zilizokuwa zimeshaachwa katika miaka hii. Hali hii

itaisaidia jamii ya Wazanzibari kuzikumbuka na kuzitumia methali za asili, na hivyo

kuhifadhi na kuendeleza utamaduni, falsafa na maadili mazuri ya jamii yao. Pili,

utafiti huu utasaidia kitaaluma katika matumizi ya marejeleo kwa wataalamu

mbalimbali wakiwemo walimu na wanafunzi wa ngazi zote. Tatu, utafiti umeweza

kuibua mianya mipya itakayowahamasisha watafiti wengine kuifanyia utafiti zaidi

fani hii ya fasihi simulizi ya Kiswahili zikiwemo methali.

1.6 Nadharia ya Uchanganuzi wa Data

Nadharia iliyotumika kuuongoza utafiti huu ni ya Uamilifu. Nadharia ya Uamilifu

(Utendajikazi) hushughulikia kazi ya fasihi simulizi inayofanywa katika mfumo wa

kijamii. Hii ni nadharia inayokiangalia kipande cha kazi ya fasihi simulizi kuwa ni

sehemu ya mfumo wa kijamii (na hivyo kuwa sehemu ya utamaduni wao). Fasihi

hiyo iwe inatupa jambo la msingi, kiasi kwamba kipande hicho cha kazi ya fasihi

simulizi hutekeleza jukumu maalum katika jamii husika. Katika nadharia ya

Uamilifu inaelezwa kuwa kila kitu hujengwa na vipengele kadhaa na kila kipengele

kinakuwa na utendakazi mahasusi kwa jamii. Hivyo, kwa mujibu wa nadharia hii,

10

fasihi simulizi huchukuliwa kama ni sehemu ya kazi inayofanywa na kipengele

hicho cha sanaa, katika mfumo wa utamaduni.

Nadharia hii imezungumziwa na wataalamu mbalimbali. Kwa mujibu wa Wallace na

Wolf (1980), nadharia ya uamilifu iliasisiwa na wanasosholojia. Miongoni mwa hao

ni Malinowski (1884 – 1942). Ambaye ameichukulia fasihi simulizi kulingana na

utendakazi wake katika jamii. Naye Emile Durkheim (1858 – 1917) aliutazama

uamilifu kuwa ni mfumo unaoeleza sababu mbalimbali na athari za matukio ya

kijamii kama vile migomo juu ya mambo mbalimbali. Wanasosholojia wengine

walioizungumzia nadharia hii na kuyaunga mkono maelezo ya wataalamu

waliowatangulia kama Wolf na wenziwe, ni Angusle Comte (1787 – 1857), Herbert

Spencer (1830 – 1917), na Vilfredo (1848 – 1923). Baada ya hapo nadharia hii

ikaendelezwa na wanaanthropolojia akiwemo Radcliffe Brown (1881 – 1955).

Okpewho, Leech na Firthwalikuja kuiendeleza fasili iliyotolewa na Malinowski

kuhusu nadharia ya uamilifu. Wataalamu hawa walisema kwamba, uamilifu ni kazi

ambayo kipande cha kazi cha fasihi simulizi, hufanya kazi katika mfumo wa jamii.

Fasili hiyo inatoa jambo la msingi kuwa tanzu za fasihi simulizi kama semi

zikiwemo methali, hutekeleza mahitaji au matakwa ya jamii husika. Kwa hivyo,

kutumika kwa nadharia ya uamilifu katika utafiti huu ni muhimu kwa sababu ya

kuubainisha utendakazi wa methali za Kiswahili ambazo ni sehemu ya semi.Kwa

upande mwengine, nadharia ya uamilifu imeelezewa kuwa ni utathmini wa uhusiano

uliopo kati ya sanaa simulizi na mahitaji ya kijamii, kwani kulingana na nadharia hii,

mwanafasihi anahitajika kuzingatia hatua zifuatazo:

11

a) Kuueleza utamaduni wa jamii inayotumia utanzu huo wa fasihi simulizi, hasa

katika miktadha inayotumika utanzu huo, ili kusaidia kufahamu umuhimu wa utanzu

huo katika miktadha ya utamaduni.

b) Kuuelezea utanzu huo wa fasihi simulizi anaoushughulikia ili kuonesha hali halisi

inayopatikana katika jamii hiyo.

c) Kuuelezea utanzu huo kama ni chombo kinachotumika mara kwa mara, na kama

ni sehemu ya utamaduni, kulingana na mahitaji ya jamii.

d) Kuuelezea utendakazi wa utanzu huo katika mfumo wa maisha na jamii hiyo kwa

jumla.

Ili kuweza kutekeleza jukumu hilo maalum katika jamii hiyo, nadharia hii huzingatia

mihimili mikuu ifuatayo:-

a) Uelezaji wa kipandekazi cha fasihi simulizi kama kazi ya sanaa iliyomo katika

jamii yenye jukumu linaloitikia matakwa ya jamii hiyo.

b) Uendelezwaji wa kipandekazi hicho cha fasihi simulizi katika jamii hiyo.

c) Utendajikazi wake wa jukumu au dhima ya kipandekazi hicho cha fasihi simulizi

katika jamii.

Kwa mujibu wa nadharia ya uamilifu, dhana ya utendakazi humaanisha lile jukumu

linalotekelezwa na utanzu wa fasihi simulizi katika utamaduni wa jamii fulani.

Kutokana na ufafanuzi huu, inaonekana wazi kuwa fasihi simulizi ina jukumu la

kukidhi matakwa ya jamii kwa mielekeo ya tabia na kawaida za wanajamii husika.

12

Nadharia ya uamilifu pia huzingatia kuwa, fasihi simulizi inao utendakazi maalum

katika mfumo wa jamii iliomo ndani yake. Utendakazi huu huwa ni sawa kwa tanzu

na vipera vyote vya fasihi simulizi ukiwemo utanzu wa semi ambamo ndani yake

kuna kipera cha methali kilichoshughulikiwa na utafiti huu.

Nadharia ya uamilifu imeweza kuuongoza vema utafiti huu kwani, katika utafiti huu

kilichunguzwa kipandekazi cha fasihi simulizi cha methali zilizoachwa katika

matumizi ambayo kwa sasa ni sehemu kamili ya utamaduni wa jamii za Waswahili.

Hivyo, katika utafiti huu kulielezwa kwa kina juu ya methali za Kiswahili ikiwa ni

sehemu ya semi katika fasihi simulizi sambamba na utamaduni wa Wazanzibari.

Aidha, kwa vile utafiti ulichunguza sababu na athari za kuachwa kwa methali hizo,

ile namna ya utendakazi wa jukumu au dhima ya methali katika jamii ya

Wazanzibari iliweza kuelezwa ipasavyo. Vilevile, uendelezwaji wa methali hizo

kama ni kipandekazi cha fasihi simulizi katika jamii ya Wazanzibari imeweza

kufafanuliwa ipasavyo.

1.7 Mipaka ya Utafiti

Utafiti huu ulijihusisha na methali za Kiswahili zilizoachwa. Aidha, utafiti ulijikita

katika kujua sababu na athari za kuachwa kwa methali hizo tu. Hivyo, methali

nyenginezo na maeneo mengine yanayohusiana na methali hizo kama vile muundo,

lugha na mengineyo hayakuhusishwa katika utafiti huu isipokuwa kwa kurejelea

pale ilipolazimika.

13

1.8 Muhutasari wa Sura ya Kwanza

Sura hii ilielezea juu ya usuli na tamko la tatizo la utafiti, lengo kuu la utafiti, malengo

mahususi, masuali ya utafiti, pamoja na nadharia ya utafiti, umuhimu na mipaka ya

utafiti huu. Kwa ujumla, sura ilianza na usuli wa tatizo la utafiti uliozungumzia fasihi

simulizi, umuhimu na matumizi yake semi pamoja na methali. Tamko la utafiti ambalo

ni kuchunguza sababu na athari za kuachwa kwa baadhi ya methali za Kiswahili

limebainishwa. Pia, vipengele vya nadharia, umuhimu na mipaka ya utafiti viliweza

kujadiliwa katika sura hii.

14

SURA YA PILI

MAPITIO YA MAANDIKO

Sura hii inaelezea juu ya maandiko yaliyopitiwa kuhusiana na utafiti huu. Maandiko

yalikuwa ni kuhusu fasihi simulizi na umuhimu wake, semi kwa ujumla, methali za

Kiswahili na kumalizia kwa kuonesha mapengo yaliyojitokeza kutokana na mapitio

ya maandiko hayo.

2.2 Mapitio ya Maandiko Kuhusu Fasihi Simulizi

Njogu na wenzake (2001) wameonesha umuhimu mkubwa wa fasihi simulizi katika

jamii ya Waswahili. Wakiainisha matumizi ya fasihi simulizi kuwa ni chombo cha

kuwasilishia maadili ya jamii husika, pamoja na kuiburudisha, wanasema:

Katika jamii zote fasihi simulizi imetumiwa kuwasilisha maadili na

mafungu kemkem kuhusu jamii husika. Pia, imetumika ili

kustarehesha na kuburudisha kwa namna inavyotumia lugha,

uigizaji, utendaji, taharuki na mbinu mbalimbali za simulizi. Fasihi

hujidhihirisha katika nyimbo na ngoma, mashairi, maigizo, ngano,

methali, na vitendawili. (uk.85).

Kutokana na maelezo hayo, ni wazi kuwa fasihi simulizi ina umuhimu mkubwa kwa

jamii yoyote ile ikiwemo ya Waswahili. Vilevile, nyenzo pekee yamawasiliano ya

kijamii ni lugha; lugha isiyotumia sanaa huwa haiwasilishi ujumbe mzuri na kwa

njia nzuri. Hivyo, fasihi simulizi ni njia nzuri ya kuwasilishia ujumbe kwa jamii na

kwa namna iliyobora zaidi. Aidha, wanatoa maelekezo juu ya njia bora za

ufundishaji wa lugha ya Kiswahili hasa upande wa fasihi simulizi na kuonesha

15

namna hadithi, methali na tanzu nyengine za fasihi simulizi zinavyoweza kuwa

chachu ya maendeleo ya jamii katika lugha. Pia, maelezo yao yametaja tanzu za

fasihi simulizi kuwa ni nyimbo, ngoma, mashairi, maigizo, ngano, methali na

vitendawili. Kazi hii ina mchango katika utafiti huu kwa kuonesha haja ya

kushughulikiwa kwa kutafitiwa fasihi simulizi ya Kiswahili katika tanzu zake zote

ikiwemo ya semi ambayo ndani yake methali za Kiswahili zinapatikana.

Haji (1992) anaieleza fasihi simulizi kuwa ni ile inayobuniwa bila ya kuandikwa.

Akifafanua zaidi, anasema kuwa msanii huyatoa mawazo yake kwa kutumia maneno

ya mdomo, yaani kwa kusimulia.Pia, amegusia juu ya chanzo cha fasihi simulizi

kuwa ni uwezo wa binadamu wa kuwasiliana kwa maneno (lugha); na kuwa, kwa

vile haifahamiki lugha ilianza lini,vilevile na fasihi nayo haifahamiki ilianza lini.

Ameonesha pia kuwa fasihi simlizi ni yenye kurithiwa kutoka kizazi hadi kizazi.

Akiainisha tanzu zake, amezitaja kuwa ni ngano, visasili, migani, tamthilia,

vitendawili, methali na ushairi. Dhima za fasihi simulizi amezitaja za kuburudisha,

kuidilisha, kuamsha na kudadisi. Kazi yake ina mchango katika utafiti huu kwa vile

maelezo yake yaliakisi zaidi kwa mifano ya fasihi simulizi inayotumiwa na jamii ya

Wazanzibarizikiwemo methali.

Msuya (1979) anaizingatia fasihi iwe simulizi au andishi kuwa ni sehemu ya

utamaduni wa jamii na hivyo kila jamii iwe kabila au taifa hainabudi kuwa na fasihi

yake. Anaiona fasihi kuwa ni chombo cha kuielezea na kuitazamia jamii

kiutamaduni, kiuchumi, kisiasa na kihistoria. Katika kuonesha umuhimu wake ndani

ya jamii mbalimbali, ameizungumzia fasihi simulizi kuwa ina hazina kubwa zaidi za

16

falsafa na misemo yenye nguvu kwa kuliwaza, kufunda, kusuta na kutia mori. Katika

kuonesha uhusiano wa fasihi simulizi na semi zikiwemo methali anasema kuwa

fasihi simulizi haitokamilika kama isipoonyesha methali na vitendawili.Vilevile,

ioneshe na misemo mingine ya kufumba kama nahau na tamathali za maneno yenye

mchomo na maliwazo.Katika kuonesha umuhimu wa misemo zikiwemo methali

amezielezea kuwa ni kioo cha kuwatazamia watu kwa jumla katika nyanja zote za

maisha yao iwe siasa, uchumi, utamaduni na historia. Pia, aligusia asili ya misemo

kuwa ni hadithi ndefu zilizofupishwa, na mambo mengine ya kweli yaliyotokea

katika historia ya maisha yao. Hata hivyo, ameonesha shaka yake kuwa, pamoja na

kuwa misemo (methali) ya kale iliyohifadhiwa hadi leo kuwa mingi, lakini ipo

misemo kadhaa ambayo hubadilika kwa kufuata wakati, mazingira na watu

wanaoitumia. Anaendelea kufafanua maana na matumizi ya methali kadhaa za jamii

ya Waparehukuakizihusisha na methali za Kiswahili zaidi ya mia moja na hamsini.

Kazi hii ina mchango mkubwa katika utafiti huu ingawa haikuhusiana na methali za

Kiswahili moja kwa moja.Maelezo ya Msuyayameusaidia utafitikugundua kuwapo

kwatatizo la kuachwa kwa baadhi ya methali katika jamii.Hata hivyo, Msuya

hakuonesha ni methali zipi zilizobadilishwa ama kuachwa nani sababu gani za

kuachwa kwake na hivyo kuacha pengo lililotoa mwanya wa utafiti huu kufanyika.

Haji (1983) ameilezea fasihi simulizi kuwa ni chombo muhimu cha kuhifadhi

utamaduni wa jamii. Ameelezea kuwa iwapo jamii inahitaji kuufufua utamaduni

wake, hainabudi kuvipa kipaumbele vipengele muhimu ikiwemo lugha. Kwa mujibu

wa maelezo yake anaona kuwa, lugha ikiwa ni chombo na kielelezo kimojawapo cha

jamii ni lazima iangaliwe kwa undani na mapana yake. Aidha, amesisitiza kuwa

17

kuiangalia lugha kwa upande wa maandishi pekee si busara kwani kudhani kuwa

kuimiliki sanaa ya uandishi ndio kigezo pekee cha ustaarabu, uhai na maendeleo ya

jamii ni dhana potofu, kwani maandishi hayana historia kubwa katika maisha ya

mwanadamu. Kazi yake ilitoa msukumo katika utafiti huu kwa kuithibitisha lugha

kuwa ni kpengele muhimu kinachostahiki kupewa kipaumbele katika suala zima la

kufufua utamaduni wa jamii. Hivyo, kuzishughulikia methali zilizoachwa katika

lugha ya Kiswahili ni moja ya hatua ya kuipa kipaumbele lugha.

Khamis (1983) anaanza kwa kuwakosoa wale wanaodhani kuwa fasihi simulizi

haina nafasi tena kwa jamii ya sasa hivi ilioingia katika maendeleo ya sayansi na

teknolojia. Ameeleza kuwa hoja zinazotolewa kuonesha kuwa fasihi simulizi inakufa

hazina mashiko; na kwamba, kamwe fasihi simulizi haiwezi kuvizwa kwa vile nayo

ni chombo cha maendeleo.Pia, ni kwa sababu ni chombo cha wanyonge ambao

hawawezi kukosekana katika jamii. Akizungumzia nafasi iliyopewa fasihi simulizi

ya Tanzania, ametaja kuwa ni uhuru uliopo wa kuibuni na kuitumia, kufundishwa

mashuleni na vyuoni, kutumika kwenye vyombo vya habari kama redio na

televisheni, na kuundwa kwa vikundi maalumu vya utamaduni vya binafsi na kitaifa.

Pia,ameyataja matatizo yanayoikabili fasihi simulizi ya Tanzania kuwa ni athari

zilizoachwa na wakoloni, uchunguzi na uhifadhi wake na muwamko mdogo wa

kisiasa,kuwepo kwa jamii yenye lugha nyingi na kutokuwepo inayofahamika na

kutumiwa na watu wote. Matatizo mengine ni ufundishaji wake mashuleni na

vyuoni, uchache wa vikundi vya utamaduni, kupewa nafasi ndogo na duni katika

vyombo vya habari, pamoja na uchache wa kazi zilizoandikwa kuhusiana na

nadharia ya fasihi simulizi. Kwa ujumla, kazi yake inatoa changamoto ya umuhimu

18

wa kushughulikiwa kwa karibu fasihi simulizi za jamii mbalimbali za Tanzania,

ikiwemo jamii ya Wazanzibari ambako utafiti huu umefanywa.

Mapitio haya yanayojadili fasihi simulizi kwa jumla yameonesha maana, aina,

umuhimu na matumizi yake katika jamii na kuwa ipo haja ya kuisimamia fasihi hiyo

hadi pale itakapoleta tija inayotarajiwa na jamii husika. Mapitio haya yameusaidia

utafiti huu kwa kiasi kikubwa kwa kuonesha mwanga kuhusu umuhimu na matumizi

ya fasihi simulizi katika jamii. Hali hii inaimarisha kuona kuwa utafiti wa

kushughulikia methali za Kiswahili kama ni sehemu ya kuishughulikia fasihi

simulizi ya Ki-Tanzania.

2.3 Mapitio ya Maandiko Kuhusu Semi

Mbarouk (2011) anaeleza kuwa mara zote semi hujitofautisha na lugha ya kawaida

kwa kutumia kwake sana lugha ya picha na ishara; na kwamba,hali hiyo huifanya

lugha iwe na ladha maalumu kwa msemaji na wasikilizaji. Anamnukuu Finnegan

(1970) ambaye anaonesha umuhimu mkubwa wa matumizi ya semi katika jamii hasa

za Waswahili. Katika kuonesha umuhimu huo, ameeleza kuwa ndio maana semi kwa

jamii ya Zanzibar hutumika katika sehemu rasmi na zisizorasmi.Na katika sehemu

zote hizo semi huwa zinatekeleza dhima yake kwa ukamilifu. Anataja baadhi ya

dhima za semi na kuzitolea mifano kuwa ni kutoa ushauri ama nasaha, kwa

mfano“Asiyesikia la mkuu, huvunjika guu”. Nyengine ni kutoa mafunzo ya

kiutendaji na ya kimaadili; kwa mfano“Muamini Mungu si Mtovu”. Kutumia kejeli

na vijembe; kwa mfano“Mchamaago hanyele huwenda akawiya papo”, dhima ya

19

kushawishi na kushambulia; kwa mfano“Akiba haiozi”. Kwa ujumla, kazi hii

imesaidia kiasi kikubwa katika utafiti huu, kwani katika mifano mingi ya semi

zilizotumiwa ni methali. Pia, methali hizo ni zile zinazotumiwa kila siku, na hivyo

kutoa mwanya katika kuzipambanua na zile zisizotumika kwa sasa.

Mulokozi (1996) anauelezea utanzu wa semi kuwa ni utungo wa kisanaa wenye

kubeba maana au mafumbo muhimu ya kijamii na kuuhusisha na fasihi

simulizi.Akiutofautishana tanzu nyengine, anasema kuwa semi huchukua kauli fupi

na kuziainisha kwa kuvitaja vipera vyake kuwa ni methali, vitendawili, mafumbo,

misimu, lakabu, na kauli-tauria. Pia, ameashiria baadhi ya sifa za semi kupitia fasili

yake kuwa ni za kisanaa na pia hubeba ujumbe, mafunzo au maana nzito kwa jamii.

Hivyo, semi ni muhimu kuwepo katika jamii.Hata hivyo, Mulokozi hakuainisha

mambo mengine yanayohusiana na semi kama vile maana ya semi za Kiswahili,

matumizi, historia, mitindo na miundo yake. Hivyo, ni maeneo muhimu kuyatafiti

kwa maendeleo na mustakabali wa semi za Kiswahili. Kazi hii imeusaidia utafiti huu

kwa kuziainisha methali kuwa ni miongoni mwa semi na hivyo zinabeba sifa

zilizotajwa hapo juu ikiwa ni pamoja methali za Kiswahili zilizoachwa ambazo

utafiti huu unazishughulikia.

Msuya (1979), anazungumzia semi na umuhimu wake pamoja na nafasi au dhima

yake katika jamii hasa zakale enzi za mababu. Akitolea mfano wa misemo ya

Kipare, anasema:

Misemo inayodumu inasikika Upareni mwote maana lugha ya

kipare ina utajiri mwingi sana na misemo ya methali, nahau,

20

tamathali za usemi na kadhalika. Utajiri huu unadhihirika kwa vile

mzee wa kipare akiwa ametulizana katika mazungumzo ya kijadi,

hawezi kuzungumza kwa dakika tatu tano hivi bila kubandika

methali au nahau au tamathali za maneno…Misemo yao huwa kioo

cha kuwatazamia kwa jumla, ikiwa kisiasa, kiutamaduni, kiuchumi,

kihistoria, na kadhalika. Misemo hiyo imejaa hekima na falsafa ya

juu kwa sababu ilitumika pindi walipotaka kuwaadhibu wadogo na

kuwatanabahisha wakubwa. (Bila shaka walipotenda

makosa)…Misemo ya kale ya kale iliyohifadhiwa hadi leo ni mingi,

ila mingine imebadilika kwa kufuata wakati, mazingira na watu

wanaoitumia. (uk. 9-11).

Msuya ametaja misemo mingi ya Kipare, na akaihusisha na misemo zaidi ya mia

moja na sitini ya Kiswahili katika kazi yake. Pia,amegusia falsafa ya misemo

mbalimbali na asili yake. Kazi hii iliusaidia utafiti huu kwa kuzihusisha semi na enzi

za kale; hivyo,inadhihirisha kuwa semi zikiwemo methali zimeanza zamani na jamii

hupokezana kutoka kizazi hadi kizazi kwa njia ya kurithishana. Utafiti huu unaona ni

muhimu jambo hilo kudumishwa na ndio maana ya kuamua kutafiti sababu za

kuachwa kwamethali hizo.

Kwa ujumla, mapitio hayo yanaonesha umuhimu wa utanzu huu wa fasihi simulizi

katika maisha ya kila siku ya mwanadamu na namna asivyoweza kuuepuka katika

matumizi. Hii inadhihirisha pia haja ya kuingia kwa undani zaidi kwa kuviangalia

vipera vya utanzu huu wa fasihi simulizi. Lakini kutokana na wingi wake, si rahisi

kwa utafiti mmoja kushughulikiwa vipera vyote vya semi na kwa msingi huo, ndio

maana utafiti ulikiangalia kipera kimoja tu cha semi ambacho ni cha methali.

21

2.4Mapitio ya Maandiko Kuhusu Methali

Hassan (2013) anaibainisha miktadha mbalimbali ambayo methali hutumika. Akiitaja

miktadha hiyo ni pamoja na muktadha wa pwani, wa shuleni, wa sokoni, muktadha wa

dini, wa shughuli za kazi na muktadha wa shughuli za kijamii. Mingine ni miktadha ya

kisiasa, mazungumzo ya vijana (vijiweni) na muktadha wa nyumbani. Pia, ameonesha

sababu kadhaa za methali kutofautiana baina ya jamii moja na nyingine. Anazitaja

baadhi yake kuwa ni tofauti ya kimatamshi inayosababishwa na tofauti ya lahaja,

kupanuka kwa eneo la watumiaji, na usanifishaji wa lugha. Akataja sababu ya kufanana

kwa methali baina ya jamii kuwa ni historia ya maisha ya watumiaji wa lugha

husika.Kwa mfano, watumiaji wa lugha ya Kiswahili wana asili moja ya lugha za Ki-

bantu. Akinukuu katika Jarida la Taasisi ya Elimu Tanzania(1988: 6), anasema:

Ingawa kumbukumbu za historia hazitoshi katika kufikia maamuzi

wa chimbuko halisi la lugha ya Kiswahili, ushahidi wa kiisimu

uliopo unaonesha dhahiri kuwa Kiswahili ni lugha ya Ki-bantu.

Amethibitisha pia kuwa methali hubeba maadili na falsafa ya jamii husika.Ameyataja

baadhi ya maadili, falsafa na mitazamo inayobebwa na methali kuwa ni heshima na utii

kwa wazee na wakubwa, upendo na ushirikiano, kufanyakazi kwa bidii, kumcha Mungu,

sitara, subira, utamaduni na jamii.

Hassan anamueleza Saidi (1976) kwa kusema kuwa ni mwandishi aliyekusanya methali

zaidi ya mia mbili zinazozungumzia maudhui mbalimbali na zinazotumika katika

miktadha tofauti ya kijamii. Hata hivyo, anasema mwandishi huyo hakutoa maelezo

yoyote yahusuyo methali hizo; lakini amemalizia kazi yake kwa kuweka mazoezi ya

kumtaka msomaji akamilishe methali alizopewa kama ni sehemu ya kupima ufahamu

22

wake juu ya mada ya methali iliyotolewa mifano. Yawezekana kuwa alikusudia

kuzikusanya tu na kumwacha msomaji au msikilizaji, aweze kuangalia ni ujumbe gani

unaopatikana katika methali hizo. Kwa upande mwengine, Saidi ameikumbusha jamii

baadhi ya methali ambazo zinaanza kutoweka ili jamii hiyo iweze kuzihifadhi kwa ajili

ya kizazi cha sasa na kinachokuja. Kwa kiasi kikubwa, licha ya Saidi kutozitolea

ufafanuzi wowote methali hizo, lakini kazi yake imetoa mchango wa kuionesha jamii

methali ambazo, kwa kiasi Fulani, zimeanza kusahaulika katika matumizi; na hivyo,

kuusaidia utafiti huu kuthibitisha hali ya kuachwa kwa baadhi ya methali za Kiswahili

katika jamii.

Mgulu (2011) ameonesha kuwa methali zina vyanzo vingi kwa sababu zinatumikia

vipengele vyote vya maisha ambayo yamekusanya mambo mengi yasiyo na

kikomo.Anaongeza kuwa vyanzo vya methali ni sawa na bahari isiyokuwa na kikomo.

Anavitaja baadhi ya vyanzo hivyo kuwa ni tanzu na vipera vya fasihi simulizi, ibada,

matambiko, tiba asilia, ujenzi wa maadili mema na shughuli za kiuchumi za jamii

husika. Vyanzo vingine alivyovieleza ni misiba na majanga kwa upande mmoja, na kwa

upande mwengine, ni furaha na sherehe za kijamii. Mgulu ameonesha pia hatua

zinazochukuliwa katika kuondosha uwelewa mbaya juu ya methali za Ki-Afrika ambazo

zimekuwa zikipotoshewa falsafa na ukweli wake na wataalamu kutoka nje kutokana na

kutozielewa vema lugha na tamaduni Ki-Afrika. Miongoni mwa hatua alizozitaja kuwa

zimeshaanzwa ni kuanzishwa kwa tovuti maalumu inayozitolea maelezo methali za

jamii za Ki-Afrika inayoitwa African Proverbs, sayings and stories website:

www.afriprov.org. Hatua nyengine ni kuanzishwa kwa mradi wa kukusanya wataalamu

na waandishi wazalendo waliochunguza na kukusanya methali za jamii zao kwa shabaha

23

ya kuzihifadhi. Kutokana na mradi huo, kutoka mwaka 1999 hadi mwaka 2004, vitabu

kumi na vitatu vinavyohusiana na methali viliweza kuandikwa. Kazi hii iliibua hamasa

ya mtafiti juu ya kuchunguza methali za Kiswahili zilizoachwa kwa matarajio kuwa ni

mchango mwengine mpya wa kuziendeleza, kuzitunza na kuzihifadhi za Kiswahili ikiwa

ni moja ya rasilimali ya Afrika.

Simiyu (2011) ameelezea maana, upatikanaji, ubunifu, umuhimu pamoja na matumizi ya

methali. Akizielezea methali anasema kuwa mara nyingi methali hutegemea na huwa na

uhusiano mkubwa na mazingira, muktadha na mila za jamii husika. Kupitia methali,

utamaduni wa jamii husika husawiriwa na kuakisiwa kwa namna ya pekee. Akielezea

upatikanaji wa methali anasema, aghalabu hupatikana kwa mapokeo kutoka kizazi hadi

kizazi, akiwa na maana ya kuwa vizazi hurithishana fasihi simulizi. Hata hivyo, anakiri

kuwa methali zinaendelea kubuniwa hata sasa kutokana na miktadha, wakati na mahitaji

ya jamii. Kimuundo, anaungana na wataalamu wengine walioona kuwa kwa kawaida,

methali, hasa za Kiswahili, huwa na sehemu mbili, sehemu inayoibua wazo na ile

inayolikamilisha wazo hilo.Kwa upande wa ubunifu wake, anagundua kuwa methali

hutumia lugha maalumu na teule kwa ustadi mkubwa. Lugha inayopambwa kwa sitiari,

nidaa, tashbiha, taswira, balagha, takriri, mchezo wa maneno, tamathali za semi, tanakali

sauti, pamoja na mbinu nyengine za kinudhumu. Pia, katika ufafanuzi huo anadokeza tu

muktadha wa methali na mazingira, ijapokuwa hakuhusisha na jamii maalumu.

Sambamba na hayo, anautaja wakati, pahala, na mwingiliano au kufananakwa matumizi

ya methali za jamii nyingi. Kazi yake imetoa wigo mkubwa wa umuhimu wa methali

katika jamii na kuusaidia utafiti huu katika kuona namna methali zinavyosheheni

24

matumizi ya tamathali za semi jambo linaloufanya uzikodolee macho zaidi methali

zilizoachwa iwapo zimekidhi hitaji hilo.

Madumulla (1995-2005) anaonesha kuwa methali hutokana na ujuzi, sheria na tabia za

jamii husika.Anasema: “A short sayings in common use expressing a well-known truth

or common fact ascertained by experience or observation”. Yaani; Methali semi fupifupi

zinazoelezea mambo ya kweli yanayotambulikana na wanajamii au ukweli uliozoeleka

ambao hutokana na uchunguzi wa tajriba za maisha (Tafsiri ya Mtafiti).Aidha,

amedokeza kuwepo kwa taaluma maalum inayoshughulikia kwa upana methali

mbalimbali za ulimwengu inayoitwa Perimiolojia1 na amedokeza historia ya

methali.Anamnukuu Roger Wescott ambaye anasema;

Proverbs were older than epic but more recent than riddles and

placed their dates at 5000 years ago for epic, 10,000 years for

proverbs and 15,000 years for riddles.’ (Madumulla, 2005:20).

Methali ni kongwe zaidi kuliko tenzi, lakini ni za karibuni koliko

vitendawili, kwani inakadiriwa kuwa tenzi zilianza miaka 5000

iliyopita, ambapo methali ni miaka 10,000 iliyopita na vitendawili

ni miaka 15,000 iliyopita.(Tafsiri ya Mtafiti)

Maelezo haya yanathibitisha kuwa methali zimeanza zamani na hivyo huwa ni zenye

kurithiwa kutoka kizazi hadi kizazi. Jambo hili liliusaidia utafiti huu kwa kuonesha haja

ya kushughulikiwa methali zilizoachwa kwa vile huenda urithi huo muhimu ukakatika

usiendelee iwapo hazitoshughulikiwa.

1 Kwa mujibu wa Madumulla (1995), Paremiolojia ni kitengo cha kitaaluma kinachoshughulikia kwa

upana zaidi methali mbalimbali za ulimwenguni.

25

Wamitila (2004) anaielezea maana ya methali na kuonesha umashuhuri wake katika

jamii zote duniani. Anasema utanzu wa methali ni mmojawapo wa tanzu za sanaa-

jadiiya ambazo hutambuliwa haraka kutokana na lugha yake, muundo, pamoja na

yaliyomo. Anauelezea ubunifu uliomo, anasema kuwa muundo wa methali hutumia

mbinu maalumu za lugha zilizojengwa kishairi zinazochangia kujenga kumbukumbu

katika akili za wanajamii. Kwa upande mwengine, Wamitila anaonesha vigezo

mbalimbali vinavyotumiwa na wataalamu katika uainishaji wa methali. Anavitaja

baadhi kuwa ni kigezo cha kiabjadi (Kialfabeti), kimuktadha (kidhamira), kiuamilifu

(utenda kazi), kimtindo au kimuundo, kigezo cha kimaana, pamoja na kigezo cha

kiisimu (kisarufi). Sambamba na vigezo vya uainishaji, ametaja pia baadhi ya sifa za

methali, kama vile umapokeo, matumizi, urudiaji, sifa za kisarufi na kisintakisia,

matumizi ya sitiari, sifa za kisemantiki mfano usambamba, takriri, pamoja na kweli

kinzani. Sifa nyingine ni vitambulishi vya kimaana, kwa mfano matumizi ya vikale

na visifa vya kisauti kama vile mizani, takriri konsonanti na takriri irabu. Mbali na

maelezo hayo, Wamitila katika kazi yake anaonesha dhana ya Umataifa2 wa methali

akitolea mfano methali za kiduruma na kigiriyama zinazotokana na lugha za

Kibantu, zenye uhusiano mkubwa na lugha ya Kiswahili. Pia, ameyataja majukumu

ya methali katika jamii kuwa ni ya kimaadili, kiumbuji, kielimu, ufupishaji, kuakisi

mtazamo wa jamii pamoja na majukumu ya kibalagha. Mwisho wa uchambuzi wake

anataja mifano ya methali katika Kiswahili, Kigiriyama, Kikamba, Kikuyu na

Kipokomo. Kwa ujumla, Wamitila ameonesha namna kipera hiki cha semi

kinavyoshughulikiwa kwa upana katika jamii mbalimbali duniani kupitia taaluma

2 Umataifa wa methali ni mwingiliano au mfanano unaojitokeza katika methali za jamii mbalimbali.

Mfanano huo hutokea kiumbo, kiasi cha kuonekana kama zimetafsiriwa kutoka lugha moja na kwenda

nyingine.

26

inayojulikana kama paremiolojia. Kazi yake iliusaidia utafiti huu kwa kuona upeo

wa umuhimu wa kuzishughulikia methali za Kiswahili ili nazo ziweze kutoa

mchango kwa jamii ya Waswahili na dunia kwa jumla.

Njogu na wenziwe (2001) wanaonesha namna methali na semi nyengine

zinavyoweza kufundishwa kwa wanafunzi katika skuli za sekondari na vyuo.

Wanasema ni muhimu kufundisha methali kwa kuanza kuieleza maana ya nje

inayotokana na maana za maneno yaliomo, kisha kuifafanua kwa kuielezea maana

yake ya ndani. Baadaye ni kutaja matumizi yake katika maisha ya kila siku na

wakaongezea kuwa inawezekana kuitungia kisa. Katika kazi yao, wamezitaja

methali zaidi ya mia moja na hamsini. Humo, wameonesha methali zinavyoweza

kugawika katika makundi mbalimbali ya hali zilizomo katika jamii. Miongoni mwa

makundi waliyoyataja ni pamoja na kundi la methali za zaraa, au kuhimiza na

kuonya. Kundi la methali zinazoonesha uhusiano baina ya watawala na watawaliwa.

Jengine ni la methali zinazoelemea upande wa sayansi. Methali zinazorejelea katika

ngoma, muziki, kucheza, kuimba, midundo na hata ala za miziki. Methali

zinazofungamana na ulimwengu na anga yake. Makundi mengine ni ya methali

zinazohusu elimu, magonjwa na matibabu, bahari, pwani na yalioko, jinsia na zile

zinazohusu ujenzi. Kazi hii imeusaidia utafiti katika kuonesha mawanda ya methali

na namna yalivyozivaa nyanja zote za maisha ya wanadamu katika jamii. Hali hiyo

inaonesha upeo wa matumizi ya methali katika jamii na kuuthibitisha umuhimu

wake.

27

King‟ei na Ndalu (1999) wanaonesha umuhimu na mfano mzuri wa kuzihifadhi

methali za Kiswahili. Mbali na kutoa maana pana, usuli, sifa pamoja na dhima za

methali za Kiswahili,pia wameorodhesha methali za Kiswahili zaidi ya elfu mbili na

mia tano.Hivyo,kuifanya kazi yao kuwa ni ya kwanza iliyodhihirisha utajiri mkubwa

wa jamii ya Waswahili kuhusu methali. Methali hizo wamezipanga kwa mpango wa

kialfabeti, na kila moja wameitolea maana yake ya juujuu (nje), makusudio (maana

ya ndani) na matumizi yake. Kazi hii iliufaidisha utafiti huu kwanza kwa kuonesha

wingi wa methali za Kiswahili.Jambo hili liliangaziwa kwa undani zaidi kwa

kuhusishwa na sababu za kuachwa kwa baadhi ya methali nyengine katika matumizi

ya kila siku katika jamii ya Wazanzibari.Ingawaje methali nyingi zimekuwa na

tofauti ndogo ya namna zinavyotamkwa na jamii ya Wazanzibari, kwa vile

zimeandikwa kwa matamshi ya lahaja ya kimtang‟ata nchini Kenya. Pili, ni kazi

iliyotumika katika kuzibainisha methali zilizoachwa katika jamii ya Wazanzibari.

Hata hivyo, kazi hii haijagusia sababu na athari za kuachwa huko kwa jamii.

Njogu na Chimerah (1999) wanazielezea methali kuwa ni muhutasari wa wazo la

busara kwa mkato na kuzihusisha na mashairi.Hii ni kwa sababu pamoja na ufupi

wake, ndani yake hubeba takriri, vina na hata mizani (katika baadhi ya methali). Pia,

wameonesha umuhimu wa methali kufundishwa mashuleni na kutoa miongozo

mizuri ya namna ya ufundishaji wake ili kuzidi kuzipa uhai wa kimatumizi ndani ya

jamii husika, hasa kwa vijana ambao wanahofiwa si waelewa wa matumizi ya

methali kwa vile nyingi zao hawazifahamu. Ufafanuzi wao ulitoa msukumo mpya

wa kuzishughulikia methali ikiwa ni pamoja na namna ya kuzifundisha. Jambo hilo

28

liliusaidia utafiti huu kwa kuzirudishia methali zilizoachwa uhai wake iwapo fikra ya

kuzifundisha itafanyiwakazi.

Mtesigwa (1989) anaonesha wingi wa methali zilizopo katika jamii za Ki-Afrika

kwa kusema kuwa Lugha za binadamu zina utajiri mkubwa wa methali.Utajiri huu

umeenea na kupindukia katika lugha za Kiafrika hususan katika eneo la lugha za

Kibantu Kusini mwa Ikweta, na pia lugha za Kinegro huko Afrika Magharibi.

Amezielezea maana na sifa za methali na kubainisha ukaribu wa methali na

vitendawili na kuwa tafauti zao hubainika kupitia mbinu, muundo, na malengo ya

umbo husika. Akitaja sifa za methali ameonesha kuwa ni lazima ziwe fupi, zitumie

lugha ya kisanaa, zitoe mafunzo kwa jamii, na zivutie wasikilizaji kwa kutumia

kikamilifu tamathali za semi. Kwa maelezo yake, anaona methali lazima zitumie

lugha ya tamathali ili ziweze kukidhi haja inayokusudiwa. Maelezo hayo yametoa

msukumo katika utafiti huu kwa kuona kuwa kuna haja kubwa ya kuzichunguza

methali zilizoachwa iwapo zimekidhi mahitaji hayo kikamilifu au ni moja ya sababu

iliyosababisha kuachwa kwa kukosa mvuto unaochochewa na matumizi ya tamathali

za semi.

Shariff (1988) anabainisha namna mabalimbali za matumizi ya lugha katika jamii ya

Waswahili.Anasema kuwa Kiswahili cha kawaida kina tungo za namna tatu za

matumizi ya lugha ambazo hujitokeza zaidi. Kwanza, kuna utumiaji wa lugha

uliyowazi; pili, kuna utumiaji wa misemo; na tatu, kuna lugha ya kimafumbo

itumiwayo mara nyingi zaidi kiasi cha kuwaona Waswahili kuwa ni watu

wanaopenda sana kutumia misemo na mafumbo katika mazungumzo yao. Aidha,

29

ameonesha maana ya misemo, asili na matumizi yake. Pia, ameonesha kuwa baadhi

ya misemo, hasa ya zamani husahauliwa na jamii. pia, mingine huendelea kubuniwa

kila leo.Anasema:

Misemo mingi ya lugha hii inatokana na hekima za wajuzi wenye

busara. Misemo mingi huwa imepokewa kutokana na wavyele kama

lugha yenyewe, kwa jumla ilivyo. Tunaweza kusema kuwa baadhi

ya misemo ya zamani imekwishasahauliwa, lakini ni kweli pia

kuwa misemo mipya hutungwa na wasemaji wa lugha waliohai,

kwani katika kila zama hakukosekani watu wenye busara na wenye

kutunga misemo yao wenyewe inayolingana na mawazo yao ya

hekima… Misemo aghalabu ni maelezo juu ya jambo au mambo

fulani kwa mukhtasari na kwa lugha ya kuvutia. (Uk. 80).

Msamiati wa misemo katika kazi hii umekusudiwa kujumuisha vipera vyote vya

utanzu wa semi ikiwemo misemo yenyewe, methali na vipera vyengine. Kazi yake

imeusaidia utafiti huu kugundua ukweli kuwa methali bado huendelea kubuniwa, na

hivyo, kuanza kufikiria kwamba huenda ikawa ni moja ya sababu za kuachwa baadhi

ya nyengine.

Haji (1983) anaonesha usanii wa hali ya juu unaopatikana katika methali na

vitendawili. Ameanza kwa kukanusha madai yasemayo kwamba fasihi simulizi si

fasihi kwa sababu ina kasoro ya sanaa. Anaona kuwa kuwafikiria wakulima na

wafanyakazi hawawezi kuwa wasanii wa kiwango cha juu ni kasoro za kifikra na

kwamba kutokujua kuandika si sababu ya kuifanya jamii hiyo isiweze kuwa na

fasihi. Hayo yote ni mawazo dhaifu yasiyo na mashiko yoyote. Akibainisha usanii

unaopatikana katika methali, ametolea mifano methali za“Asolijua chozi amtazame

aliaye”, “Kuzunguka mbuyu si dawa ya shetani”, na “Kuku wa masikini hatagi;

30

akitaga haangui; akiangua halei”. Katika mifano hii, kuna matumizi ya sitiari, lugha

ya picha, na urejeshi, ambavyo vimejikita vema katika methali hizo na nyingi

nyinginezo za Kiswahili. Mbali na mbinu hizo, Haji anabainisha mbinu nyengine za

kisanaa kuwa ni lugha ya kishairi, mapigo, na takriri. Anatolea mfano wa methali ya

“Mchezea chuma huchuma, kama hakuchuma, tumbo hunguruma”. Mbinu nyengine

za kisanii zilizomo katika methali za Kiswahili ni tash-hisi na utumiaji wa maneno

machache.Anatoa mifano ya matumizi ya mbinu hii katika methali zifuatazo: “Kizito

huonjwa”, “Kieleacho huzama” na “Ndugu mtambie, usimkalie”. Kazi hii

inaubainisha kwa undani zaidi usanii wa methali, na hivyo, kuufaidisha utafiti huu

kuona tafiti zinazohusiana na methali ni miongoni mwa tafiti za kifasihi. Kwa

upande mwengine ni kazi iliyoufaidisha utafiti kwa kuona kuwa ipo mitazamo

dhaifu ya baadhi ya watu juu ya fasihi simulizi na kuonesha kuwepo kwa haja ya

kulichunguza jambo hili kwani linaweza likawa ni sababu ya kuachwa kwa baadhi

ya methali au athari zake kwa jamii.

Finnegan (1979) anaziona methali kuwa ni hazina kubwa iliyomo katika lugha za

wanadamu. Anazichukulia methali kuwa ni utajiri uliomo ndani ya lugha hasa zile za

Ki-Afrika hususan lugha za Kibantu. Katika kuueleza umuhimu wa methali katika

lugha anasema methali ambazo hutumika kama lugha ni muhimu kwa uhai wa

binadamu ambapo bila ya kuwepo kwake lugha inaweza kubakia lakini itabakia

kama umbo lisilo nyama, damu na roho.Finnegan anaziona methali kuwa ni mfano

halisi wa sanaa ya maneno yalioteuliwa kwa umakini mkubwa ili kutunza kwanza,

picha halisi ya jambo fulani.Pili, ni kuipatanisha hali halisi hiyo na funzo au maadili

fulani yanayokusudiwa katika jamii husika. Mtaalamu huyu ametoa maana ya

31

methali, kuonesha baadhi ya miundo na matumizi yake katika jamii ambapo

imeusaidia utafiti huu kutambua mchango mkubwa wa methaliza Afrika zikiwemo

za Kiswahili ambazo sehemu yake utafiti huu unazishughulikia.

Farsy (1979) anawazindua watu juu ya suala la kuweka kumbukumbu za

kimaandishi katika tanzu za fasihi simulizi hasa hadithi, methali na vitendawili. Hii

ni kwa sababu bila ya kufanya hivyo, urithi huu mzuri husahauliwa, na hatimaye

kupotea kabisa; jambo ambalo halifai kuachwa litokee kutokana na umuhimu wake

katika jamii. Farsy anaeleza:

Sikuzote napenda kushughulika na Kiswahili na jambo hilo

limenitia bidii kuandika kila methali niliyosikia katika mazungumzo

yangu, na hasa katika mazungumzo yangu na wazee. Methali

zinafaa sana kwa mafundisho ya adili; kwa hiyo ni jambo la

muhimu kwa waalimu kujua methali nyingi kama inavyowezekana,

na kuzitumia sana katika mafundisho yao. (Uk.i)

Farsy pia amebainisha kuwa waswahili wana utajiri mkubwa wa hadithi, methali na

vitendawili vilivyokusanya mambo mengi ya imani na desturi, kiasi kwamba si

rahisi kwa mtu mmoja kukamilisha zoezi la kuzikusanya kwa ukamilifu. Pia,

ameeleza kusudio la kuwahamasisha watu kuandika ni kuepuka kupoteza hazina na

rasilimali hiyo kutokana na kusahauliwa na jamii kutokana na jamii hiyo kukabiliwa

na mambo mengine ya kisasa. Katika kazi yake amekusanya methali zaidi ya mia

tano za Kiswahili na kuzitolea maana zake kwa lugha ya Kiingereza. Aidha,

ameandika kwa kutumia utaratibu wa kiabjadi, hivyo kumpa wepesi msomaji

anayekusudia kutafuta methali maalumu. Kazi hii ni miongoni mwa hazina kubwa

zilizouwezesha utafiti huu kupata data halisi za methali zilizoachwa kutumiwa katika

jamii pamoja na baadhi ya sababu zake.

32

2.5Mapengo Yanayojitokeza Kutokana na Mapitio ya Maandiko

Kwa Wataalamu waliojadili methali za Kiswahiliwanakubalianakimawazo katika

vipengele vya maana, sifa, matumizi, na muundo, dhima katika jamii, matumizi

katika tamathali, pamoja na kubeba kwake ukweli na falsafa ya jamii husika. Hata

hivyo, kazi hizobado zinatuibulia mapengo yafuatayo: Mosi niubainifu wa methali

za Kiswahili zilizoachwa na jamii ya Wazanzibari.Pili, ni kutofahamika sababu za

kuachwa kwa methali hizo.Tatu ni kutofahamika athari za kuachwa baadhi ya

methali kwa jamii ya Wazanzibari. Hivyo, mtafiti aliamuakulifanyia utafiti suala hili

la kuachwa kwa baadhi ya methali za Kiswahili katika jamii ya Wazanzibari ili

kuuziba mwanya huo uliojitokeza.

2.6 Muhutasari wa Sura ya Pili

Sura hii ilielezea juu ya maandiko yaliyopitiwa kuhusiana na utafiti huu. Maandiko hayo

yalikuwa ni kuhusu fasihi simulizi na umuhimu wake, semi kwa ujumla na methali za

Kiswahili. Sura ikamalizia kwa kuonesha mapengo yaliyojitokeza kutokana na mapitio

ya maandiko hayo.Sura inayofuata imejadili juu ya usanifu na mbinu za utafiti.

33

SURA YA TATU

USANIFU NA MBINU ZA UTAFITI

3.1 Utangulizi

Sura hii imeelezea juu ya mbinu, vifaa na mambo mbalimbali yaliyohusishwa katika

utafiti huu. Sehemu imeeleza mbinu na vifaa vya utafiti, mpango wa utafiti na

walengwa wa utafiti. Aidha, sehemu hii imeonesha jamii ya watafitiwa, mbinu za

kupatia sampuli, eneo la utafiti, ukusanyaji na uchambuzi wa data, udhibiti na miiko

ya ukusanyaji wa data.

3.2 Mpango wa Utafiti

Utafiti ulifanyika maktabani na uwandani. Maktaba zilitumika kufanya mapitio ya

maandiko. Mambo yaliyohusishwa katika eneo hili, ni usomaji wa vitabu vya

taaluma ya utafiti, lugha, na fasihi. Pia, zilisomwa makala, magazeti, majarida, tafiti

zilizotangulia, pamoja na ripoti.Kwa upande wa uwandani, maeneo yaliyohusika na

ukusanyaji wa data kwa njia za uchunguzi, udodosaji, mijadala ya vikundi na

mahojiano ni katika vyuo vikuu vilivyopo Zanzibar ambavyo ni Chuo Kikuu cha

Taifa cha Zanzibar, Chuo Kikuu cha Zanzibar na Chuo Kikuu cha Elimu cha

Zanzibar.Mitaa minne kutoka Mkoa wa Mjini Magharibi ambayo ni Sogea na

Kikwajuni kwa Wilaya ya Mjini na Mwanakwerekwe na Fuoni kwa Wilaya ya

Magharibi. Eneo jengine ni katika taasisi za BAKIZA na TAKILUKI. Maeneo yote

haya yaliweza kufikiwa ipasavyo.

34

3.3 Eneo la Utafiti

Utafiti huu ulifanyika katika Mkoa wa Mjini Magharibi katika kisiwa cha Unguja.

Eneo hilo lilihusisha vyuo vikuu vitatu; Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar, Chuo

Kikuucha Zanzibar na Chuo Kikuucha Elimu cha Zanzibarili kupata Wakufunzi na

Wanafunzi wa fasihi ya Kiswahili. Pia, utafiti ulihusisha taasisi za BAKIZA na

TAKILUKI zinazohusiana na lugha ya Kiswahili na fasihi yake ili kupata wataalamu

wa lugha na fasihi ya Kiswahili. Vile vile ulihusisha mitaa ya Kiwajuni, Sogea,

Mwanakwerekwe na Fuonikwa ajili ya kupata wazungumzaji wa kawaida wa lugha

ya Kiswahili. Sababu yakuteuliwa eneo hilini kuwa katika Zanzibar ndio Mkoa

pekee wenye mchanganyiko wa watu kutoka sehemu zote za Zanzibar.Hii

ilirahisisha upatikanaji wa taarifa zilizokusudiwa. Aidha, ni maeneo yenye wazee

mashuhuri, watu wa kawaida na maskani wanamozungumza watu shughuli zao za

kiuchumi, siasa na utamaduni.Kwa upande wa maktabani maktaba nne zilihusishwa

katika utafiti huu ambazo ni maktaba za SUZA, UCEZ, UDOM pamoja na maktaba

kuu ya Zanzibar. Lengo la kwenda maktaba hizo ni kupata maandiko mbalimbali

yaliyohusiana na utafiti huu.

3.4 Walengwa wa Utafiti

3.4.1 Jamii Tafitiwa

Jamii tafitiwa ilihusisha makundi yafuatayo:

a) Wakufunzi na Wanafunzi wa lugha ya Kiswahili na fasihi katika vyuo vikuu.

35

c) Wazee wenye ufahamu na uzoefu wa matumizi ya methali katika mitaa.

d) Watu wa kawaida wanaozungumza lugha ya Kiswahili mitaani.

e) Wataalamu kutoka taasisi zinazohusiana na lugha ya Kiswahili na fasihi yake.

f) Methali za Kiswahili zinazotumiwa na jamii ya Waswahili wa Zanzibar.

g) Maandiko mbalimbali yahusuyo fasihi simulizi na semi kwa umashuhuri wake.

3.4.2 Aina na Dhana ya Usampulishaji

Sampuli hiyo ya walengwa ilipatikana kutokana na maumbile ya utafiti husika pamoja

na mkabala uliyouongoza utafiti wenyewe. Sampuli ilipatikana kwa kutumia njia ya

sampuli lengwa kwa kuwa ni mwafaka kwa utafiti wa kitaamuli kama huu. Kwa hivyo,

watafitiwa walichaguliwa kulingana na matakwa ya utafiti huu. Hivyo, kutokana na

makundi ya walengwa wa utafiti huu, jamii ya watafitiwa ilikuwa na watu mia moja na

ishiriniiliyogawanywa kama ifuatavyo:

a) Wakufunzi sita na Wanafunzi thalathini wa somo la fasihi ya Kiswahili kutoka

katika vyuo vikuu vilivyoteuliwa. Uzoefu wakusoma maandiko yanayohusu methali

utasaidia kugundua tofauti ya sasa na zamani katika matumizi ya methali.

b) Wazee sita wenye ufahamu na uzoefu wa matumizi ya methali kutoka katika

mitaa ya iliyoteuliwa. Watu hawa wanaaminika kuwa na kumbukumbu za methali

zilizoachwa.

c) Wazungumzaji wa kawaida thathini na mbili kutoka katika mitaaminne

ilioteuliwa. Lengo ni kupata uwelewa wao kuhusu methali zilizoachwa.

36

d) Wataalam wane wa lugha ya Kiswahili na fasihikutoka taasisi zilizoteuliwa. Watu

hawa wana uzoefu wa tafiti mbalimbali zinazohusiana na fasihi ya Kiswahili.

e) Wanafunzi ishirini na nne wa kadato cha sita,kumi wa Diploma wanaosoma fasihi

ya Kiswahili pamoja na walimu sita wa skuli ya sekondari wa somo la fasihi. Lengo

ni kuhakiki methali wasizozifahamu miongoni mwa zilizokusanywa kwa utafiti huu.

3.5 Ukusanyaji wa Data

Njia na zana mbali mbali zilitumika ili kurahisisha zoezi zima la ukusanyaji wa data

zinazohitajika katika utafiti huu. Njia na zana zilizotumika ni hizi zifuatazo:

3.5.1 Njia na Zana za Ukusanyaji wa Data

Katika utafiti huu njia zifuatazo ziliweza kutumika:

3.5.1.1Udurusu wa Kimaktaba

Udurusu ulifanyika katika maktaba nne za Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar,

Chuo Kikuu cha Dodoma, Chuo Kikuu cha Elimu cha Zanzibar pamoja na maktaba

kuuya Zanzibar. Katika maktaba hizo, vitabu vya taaluma ya utafiti, lugha, na fasihi

viliweza kupitiwa. Aidha, makala, majarida, tafiti zilizotangulia, ripoti na maandiko

mbalimbali yaliyosaidia kupata data zilizohitajiwa yalisomwa kupitia maktaba hizo.

Zana zilizotumika kwa njia hii ni daftari na kalamu kwa ajili ya kuandikia

kumbukumbu za maandishi muhimu yaliopatikana katika maandiko kama ni data za

utafiti.

37

3.5.1.2 Mahojiano

Mahojiano yalifanyika kwa Wazee sita wenye uwezo mzuri wa kuzifahamu na

kuzitumia methali kutoka mitaa minne iliyoteuliwa kutoka Mkoa wa Mjini

Magharibi. Pia, ilitumika kwa Wataalamu wanne kutoka taasisi za BAKIZA na

TAKILUKI. Mbinu hii iliwezesha kupatikana taarifa zilizosahihi kwa kiasi kikubwa.

Zana zilizotumika kwa njia hii ni daftari, kalamu, kamera ya picha jongefu pamoja

na muongozo wa usaili uliotayarishwa.

3.5.1.3 Mjadala wa Vikundi

Njia hii ilitumiwa katika utafiti huu kwa wanafunzi ishirini na nne wa kidato cha sita

skuli tatu za sekondari; Chukwani, Lumumba na Bembela, wanane kila skuli,

wanafunzi kumi wa Diploma chuo cha Ualimu Mazizini na kwa walimu sita wa

Kiswahili kutoka Skuli ya Mwembeladu. Zana zilizotumika katika njia hii ni daftari,

kalamu, simu yenye picha na kinasa sauti, orodha za methali na muongozo wa usaili.

3.5.1.4 Udodosaji

Njia hii ilitumiwa kwa Wakufunzi sita wawili kutoka kila Chuo, baina ya SUZA, UZ

na UCEZ na kwa Wanafunzi thalathini wa shahada ya kwanza wa fasihi ya

Kiswahili kumi kutoka kila chuo. Njia hii ilitumia za ya dodoso zilizogawiwa kwa

watafitiwa.

38

3.5.1.5 Uchunguzi

Njia hii ilitumika kwa kuhudhuria katika baadhi ya misiba na sherehe za arusi. Pia,

katika baraza za mazungumzo za vijana na wazee katika mitaa iliyoteuliwa. Sehemu

hizi mtafiti alichunguza matumizi ya methali za Kiswahili kwa ujumla wake katika

mazungumzo yao ya harakati za maisha yao. Zana ziliotumika katika njia ni shajara,

kalamu pamoja na simu yenye picha jongefu na mgando na kinasa sauti.

3.5.2 Zana za Kukusanyia Data

Zana zilizotumika katika utafiti huu ni za kuhifadhia sauti, picha na

maandishi.Miongoni mwa zana hizo ni shajara, daftari, kalamu, karatasi, kamera ya

picha jongefu, simu yenye picha jongefu na mgando na kinasa sauti. Zana hizo

zilitumiwa katika njia mbalimbali za kukusanyia data ambazo ni za mahojiano,

udodosaji, uchunguzi, mijadala ya vikundi na udurusu wa maktaba kama

zilivyoelezewa hapo juu.

Zana nyengine muhimu zilizotumika ni Kompyuta na flashi.Hizi ni

zanazilizotumiwa tokea mwanzo hadi mwisho wa utafiti huu. Zana hivi

zinategemeana katika kazi zake na zilihitajika sambamba. Katika utafiti huu

kompyuta na flashi zilitumika kuhifadhia mahunzi laini (soft copy) ya kazi zote

zilizohusiana na utafiti ikiwa ni pamoja na data za maktabani, uwandani pamoja na

ripoti nzima ya utafiti. Kwa upande wa kompyuta mbali na kuhifadhia data za utafiti

na ripoti, katika utafiti huu ilitumika kama ni sehemu ya maktaba ambapo mtafiti

alisoma vitabu na nyaraka zilizohusiana na utafiti zinazopatikana mtandaoni.

39

Pia,ilitumika kuchapishia mchanganuo wa data na ripoti ya utafiti. Kwa jumla,zana

hizizilitumika muda wote wa kazi ya utafiti na hata baada yake.

3.5.3 Mchakato wa Ukusanyaji wa Data

Mtafiti alitumia daftari na kalamu kukusanyia data za Maktabani. Kisha alitumia

shajara, daftari, kalamu, karatasi, kamera ya picha jongefu, simu yenye picha

jongefu na mgando na kinasa sauti kukusanyia data za Uwandani kupitia njia za

mahojiano, udodosaji, uchunguzi pamoja na mijadala ya vikundi.

Katika hatua ya kuzitafuta datahizo, njia na zana mbalimbali zilitumika. Moja ni njia

ya udurusu wa kimaktaba. Katika njia hii, kazi kama vile Swahili Sayings ya Farsi

(1958), Yatokanayo na Fasihi Simulizi ya Msuya (1979), Kamusi ya Methaliya

King‟ei na Ndalu (1989), na Tanzu za Lugha ya Njogu na wenzake, Nafasi yaFasihi

Simulizi katika Jamii ya Tanzania ya Khamis (1983), na Athari za Semi za

Kangakatika Jamii, ni miongoni mwa kazi zilizoupa utafiti huu utajiri mkubwa wa

kuzipata methali za Kiswahili, sababu pamoja athari zake kwa jumla.Njia nyengine

ziliyotumiwa kuzipata data za utafiti huu ni za mjadala wa vikundi,mahojiano na

dodosoambapo kwa njia hizo vilevile methali, sababu na athari nyingi zilipatikana.

Kwa mfano, katika mjadala na walimu wa somo la Kiswahili. Mtafiti aliweza

kukusanya zaidi ya methali mia moja na thalathini na sababu na athari kwa wastani.

Pia, methali zilikusanywa kupitia njia ya kisasa ya kutafuta katika mtandao nakupata

kurasa zilizo andikwa methali za Kiswahili. Kwa mfano, katika Blog ya Mwambao

ndani yake kuna methali za Kiswahili zilizoitwa za Mwambao mia tatu thamanini na

40

nne zilizotafsiriwa kwa lugha ya Kiingereza. Njia ya uchunguziilitumika katika

baadhi ya baraza za wazee, maskani za vijana, katika misiba na sherehe za harusina

kupata methali za Kiswahili. Kutokana na njia zote hizo, mtafiti alifanikiwa

kukusanya methali mia tano na ishirini na sita, sababu na athari zaidi ya ishirini kila

moja, kiwango ambacho kiliweza kutosheleza kuzibainisha methali zilizoachwa

miongoni mwazo, pia sababu na athari za msingi, kazi ambayo ndio iliyofanywa

baada ya hatua hiyo.

3.6 Uchanganuzi wa Data

Uchanganuzi pamoja na uwasilishaji wa matokeo ya data za utafiti huu ulifanywa

kwa umakini mkubwa kwa njia ya maelezo huku ikihusishwa kwa ukamilifu misingi

ya nadharia ya uamilifu iliyoteuliwa kuuongoza utafiti huu. Aidha, data zote

zilizopatikana maktabani na uwandani, zilichanganywa na kuchanganuliwa vyema

kwa mujibu wa malengo mahasusi ya utafiti. Uchanganuzi wa data ulikuwa kama

ifuatavyo:

Hatuazilizotumiwa katika kuzibainisha methali zilizoachwa ni hizi zifuatazo:

Kwanza ni mtafiti kuipitiya orodha ya methali zilizokusanywa. Kwa njia hii, methali

mojamoja ilifikiriwa iwapo inafahamika au la. Kila methali iliokumbukwa

iliwekewa alama na isiyokumbukwa iliachwa. Zoezi hilo lilibainisha methali

zinazojulikana na zile ambazo hazikumbukwi miongoni mwa zilizokusanywa. Hatua

ya pili ni kuzisikiliza methali ambazo hazikukumbukwa katika vikundi vya

majadiliano. Kila kikundi kilitakiwa kukumbuka methali wanazozifahamu huku

41

zikifuatiliwa kwa makini zile zisizokumbukwa katika hatua ya awali iwapo zitaweza

kutajwa katika vikundi. Hatua hii ilweza kuzibainisha zaidi methali zinazojulikana

na zisizokumbukwa miongoni mwa zile zilizotengwa hatua ya kwanza. Hata hivyo,

hatua hii haikuweza kuzipambanua wazi zile zilizoachwa kwani baadhi yake zimo

zilizoshuhudiwa kutumika katika sehemu tofauti za uchunguzi wa utafiti huu. Hivyo,

katika methali ambazo hazikutajwa zimo zilizoachwa kwa kutojulikana na zimo

zilizoachwa kwa kusahauliwa, jambo lililosababisha kuwepo kwa hatua nyengine ya

kuzipambanua aina mbili hizo.

Hatua ya tatu ni kwenda katika madarasa matatu ya wanafunzi wa kidato cha sita,

darasa la wanafunzi wa diploma na walimu wa Kiswahili. Katika hatua hii, methali

ilitajwa sehemu yake ya mwazo na kuwaachia wanafunzi waimalizie methali hiyo

sehemu ya mwisho. Kigezo cha mtafiti katika majaribio haya matano, ni kuwa kila

methali iliyoweza kukamilishwa ndio iliosahauliwa kutajwa katika jaribio la hatua

ya pili na iliowashinda kuijaza ndio isiyojulikana na hivyo kuwa ni miongoni mwa

zile zilizoachwa. Hatua hii ilizibainisha methali zilizosahauliwa na zilizoachwa.

Pamoja na ubainifu wa hatua hiyo, mtafiti alitaka kuhakikisha zaidi kuhusu methali

hizo kwa hatua ya mwisho ya kuzihakiki.Katika kuzihakiki methali zilizoachwa,

kwanza aliwapelekea watu maalum watano waliozipitia moja moja ili kubaini iwapo

zipo walizowahi kuzisikia zikisemwa mtaani, redioni au sehemu yoyote, au kuziona

katika maandishi au kuzikumbuka kwa namna yoyote ile. Pili, ni kwa ulinganisho

wa mtafiti katika mapitio ya maandiko ya baadhi ya kazi za miaka ya thamanini na

kurejea nyumba na zile miaka ya tisini hadi mwaka 2014. Na tatu ni katika

42

uchunguzi wa mazungumzo ya Wazanzibari katika baadhi ya baraza zao za

mazungumzo na katika baadhi ya shughuli zao za kijamii zilizohudhuriwa na mtafiti.

Katika hatua ya kuchanganua data zenye sababu za kuachwa kwa methali hizo,

kwanza ziliwekwa sababu zote zilizobainika kupitia udurusu wa maktaba katika

dodoso, mahojiano na mijadala ya vikundi ambapo mtafitiwa aliichunguza kila

sababu na kuikubali aliyoiona ndio na kuikataa aliyoiona sio hatua ambayo

ilizithibitisha baadhi na kuziondoa nyengine. Katika hatua nyengine watafitiwa hao

mbali na kutakiwa kukubali au kukataa sababu zilizopitia udurusu wa maktaba, pia

walipewa uhuru wa kutoa sababu wanazoziona ndizo na ambazo hazijatajwa. Kupitia

fursa hii sababu kadhaa zilitajwa ambazo zilichambuliwa na kuwekwa katika

mafungu stahiki.

Uchanganuzi wa data zilizolenga kupata athari, nazo zilikusanywa kupitia njia

zilizotajwa hapo juu ambapo mtafitiwa alitakiwa kutaja athari anazozijua yeye.

Watafitiwa walitoa athari nyingi ambazo katika uchambuzi wake athari

zinazolingana ziliwekwa kundi moja. Hatua hiyo ilikuzikusanya athari hizo katika

makundi na kuziondoa zile ambazo zilizoonnekana sio za msingi. Aidha, makundi ya

athari hizo yalichambuliwa kwa kina zaidi hatua iliyobainishakuwapomakundi

yaliyohusiana na mengine ambayo yaliunganishwa pamoja. Makundi hayo nayo

yalichanganuliwa ili kubaini ya athari zenye madhara na ya athari zenye tija kwa

jamii.

43

3.7 Uhalali na Uthabiti wa Matokeo ya Utafiti

Uhalali wa matokeo ya utafiti ni namna ya kuyafanya maotokeo ya utafiti yawe na

maelezo yenye vigezo vinavyopima mambo yaliyotakiwa kupimwa katika utafiti huo.

Ambapo, uthabiti wa utafiti ni namna utafitiunavyoweza kutoa matokeo yanayofanana

na tafiti nyingine za baadaye zinazolingana nao. Uhalali na uthabiti ni vipengele

vinavyohusiana na kutoshelezana katika utafiti.hivyo, ni vigumu kuwa na utafiti

wenye matokeo yaliyo thabiti lakini yasiwe na uhalali wa matokeo hayo (Kothari,

2009).

Kwa mujibu wa Ponera (2010), uhalali wa matokeo ya utafiti huthibitishwa kwa

mambo kama vile: Kwanza, ni kupitia kuyabainisha malengo ya utafiti pamoja na

mipaka yake. Pili, ni kupitia matumizi mazuri ya njia za kukusanyia data

yanayowezesha kupata data zinazotoa matokeo ya utafiti kwa kiwango cha uthabiti

kinachoridhisha. Tatu, ni kupitia matumizi ya lugha nyepesi na rahisi kufahamika

kwa watafitiwa juu ya kinachotafitiwa hali inayoyafanya majibu wanayoyatoa

yahusiane na yalingane na malengo ya utafiti husika. Hivyo basi, utafiti huu

uliofanywa pia ulijiegemeza katika misingi hii ili kuweza kujenga uhalali na uthabiti

wa matokeo yake. Hivyo, matokeo ya utafiti huu ni thabiti na halali.

3.8 Itikeli za Utafiti

Kwa mujibu wa Ponera (2010), itikeli za utafiti ni kanuni na mmiko yote ya kisheria,

kijamii na kiutamaduni inayopaswa kuzingatiwa na kufuaywa wakati wa ukusanyaji

44

wa data za uwandani. Katika ukusanyaji wa data za utafiti huu, kanuni ya kuchunga

miiko yote ya utafiti iliyohitajika zilifuatwa. Hivyo, masuala ya kupata vibali vya

ruhusa ya kufanya utafiti kutoka Chuo Kikii cha Dodoma, Serikali ya Mapinduzi

Zanzibarna sehemu nyengine zilizohusika yalifuatiliwa kabla kuanza kwa utafiti.

Aidha, masuala kama vile kutunza siri za taarifa, ridhaa ya watafitiwa pamoja na

kutoainisha majina yao yalizingatiwa kikamilifu. Hali hiyo, ilizingatiwa pia katika

uchukuaji wa picha na sauti kwa baadhi ya watafitiwa wa utafiti huu kwa kadri

ilivyowezekana, kwa ajili ya kuweka kumbukumbu nzuri za utafiti.

3.9 Muhutasari wa Sura ya Tatu

Sura ya tatu imeelezea juu ya mbinu, vifaa na mambo mbalimbali yaliyohusishwa na

kazi ya ukusanyaji na uchambuzi wa data. Aidha, imeeleza mbinu zilizotumika

katika utafiti huu ni udurusu wa maktaba, dodoso, mahojiano na mijadala ya vikundi.

Kwa upande wa vifaa vilivyotumika ni madaftari, kalamu, miongozo ya usaili,

kamera, na simu.Sura imeelezea mpango na walengwa wa utafiti. Pia, imeonesha

jamii ya watafitiwa, mbinu za kupatia sampuli, eneo la utafiti, ukusanyaji na

uchambuzi wa data, udhibiti na miiko ya ukusanyaji wa data. Sura ya nne inajadili

juu ya uwasilishaji na mjadala wa matokeo ya utafiti.

45

SURA YA NNE

UWASILISHAJI NA MJADALA WA MATOKEO YA UTAFITI

4.1 Utangulizi

Sura hii ina uchambuzi wa data za utafiti.Sura inaundwa na sehemu kubwa

nne.Sehemu ya kwanza inajadili juu ya methali zilizoachwa katika jamii ya

Wazanzibari. Sehemu ya pili inajadili sababu za jamii ya Wazanzibari kuacha baadhi

ya methali. Sehemu ya tatu inajadili athari za kuachwa kwa baadhi ya methali hizo.

Sura inamalizia kwa muhutasari wa matokeo ya mjadala huo.

4.2Methali za Kiswahili Zilizoachwa katika Jamii ya Wazanzibari

Nadharia iliyotumika katika utafiti huu inamtaka mtafitikuelezea utamaduni wa jamii

inayotumia utanzu wa fasihi simulizi unaotafitiwa ambao, katika utafiti huu ni methali

za Kiswahili zilizoachwa ili kusaidia kufahamu umuhimu wake kabla ya kuueleza na

kuuchunguza utendakazi wa utanzu husika. Hivyo, maelezo yanayofuta yanakusudiwa

kutekeleza hitaji hilo.

4.2.1 Miktadha ya Maisha ya Jamii ya Wazanzibari

Kwa mujibu wa Shariff na Mazrui (1994), Waswahili wameelezewa katika maana

mbalimbali kulingana na mielekeo ya watoaji wa maana hizo. Anasema baadhi

wamewaeleza Waswahili kwa kuwanasibisha na uafrika, baadhi wamewanasisha na

lugha na wengine wamewanasibisha na eneo la kijografia.Ananukuu baadhi ya maana

46

hizo anasema maana iliyotolewa katika Encyclopaedia Britanica kwa kiingeraza kuwa

Waswahili ni waliochanganya damu ambayo ni matokeo ya muda mrefu ya kuingiliana

kati ya Wanigro wa pwani na Waarabu pamoja na mchanganyiko wa damu ya watumwa

kutokana na takriban, makabila yote ya Afrika Mashariki.Pia, ananukuu maandishi ya

kale ya Mombasa yaliyoandikwa kiasi ya miaka mia mbili nyuma anasema kuwa

Waswahili ni jamii ya watu maalumu waliotafauti na Waarabu. Ni watu ambao

walikuwa washupavu katika kulinda usalama na uhuru wao, na mara kwa mara

wakiwagonganisha vichwa maadui zao ili kuutetea uhuru wao; na mas-ala ya

kuchanganya nasaba na Waarabu halikuwa ni jambo walilolitilia maanani. Kutokana na

maana mbalimbali kwa ujumla wake Waswahili ni mchanganyiko wa watu kutoka

makabila tofauti, ambao wametokea katika mwambao wa Afrika ya Mashariki na

wakawa wanatumia lugha ya Kiswahili katika kuwasiliana. Kwa ufahamu huo rangi,

kabila au wanakotokea ni vigezo vya ziada ambavyo kukubalika au kukatalika

kutatemea na muktadha wa maana inayotolewa.

Kwa vigezo vilivyotajwa hapo juu ni wazi kuwa watu wanaoishi katika visiwa vya

Zanzibar ni moja ya jamii ya Waswahili duniani. Hii ni kwa sababu Wazanzibari ni

mchanganyiko wa jamii nyingi zilizotoka sehemu mbalimbali zilizounganishwa pamoja

na utamaduni wenye kutumia lugha ya Kiswahili kama lugha yao kuu. Katika

kuthibitisha kuwa Wazanzibari ni jamii ya Waswahili, Shariff anasema “Katika wakati

huo Waswahili bado walikuwa wametawaliwa na Waarabu ambao hawakuifanya

Zanzibar kuwa ndio mji mkuu wa serikali mpaka ilipofikia mwaka 1832” (uk. 140).

Kwa hivyo, jamii ya Wazanzibari ni moja ya jamii za Waswahili duniani.

47

4.2.1.1 Muktadha wa Kijografia na Kiuchumi

Zanzibar ni visiwa viwili vikubwa vya Unguja na Pemba na vyengine vidogo kadhaa

vinavyovizunguka.Visiwa hivyo viko upande wa Mashariki wa Bara la Afrika.Kwa

upande wa Magharibi, vimepakana na mwambao wa Tanzania Bara, na sehemu

zilizobakia vimezungukwa na bahari ya Hindi. Visiwa vyengine vinavyoungana na

hivyo ni ambavyo ni Tumbatu, Uzi, Pungume, Vundwe, Bawe, Changuu na Misali kwa

upande wa Unguja. Kwa upande wa Pemba ni Kojani, Kisiwapanza, Maziwang‟ombe na

Fundo ambavyo baadhi yake sehemu ya jamii ya wazanzibariinaishi. Mji mkuu wa

visiwa hivyo ni Zanzibar uliopo eneo la Magharibi mwa kisiwa cha Unguja.

Kwa mujibu wa takwimu za Bodi ya Sensa ya watu na makaazi ya Zanzibar (2011),

wakaazi wa Zanzibar kwa sasa ni zaidi milioni moja na laki mbili. Wakaazi wengi wa

Unguja wanaishi sehemu za Kasikazini, Magharibi na Kati zenye ardhi nzuri ya kilimo.

Kwa upande wa Pemba, wakaazi wake wamesambaa takriban sehemu zote za kisiwa,

kwa vile eneo lote, isipokuwa sehemu chache ni lenye ardhi nzuri kwa kilimo. Shughuli

kuu za kiuchumi ni kilimo, biashara na uvuvi. Kwa upande wa kilimo, hulima karafuu,

mwani na viungo kama mazao ya biashara. Vile vile hulima mpunga, nafaka, muhogo,

migomba na vilimo vya maweni, kwa mazao ya chakula. Biashara za ndani na nje

zimeifanya Zanzibar kwa miaka kadhaa itambulikane kama ni kituo cha kibiashara tokea

zama za wakoloni.

48

4.2.1.2 Muktadha wa Kiutamaduni

Kwa mujibu wa Othman na Yahya (2004), Utamaduni ni jumla kuu inayokusanya

mambo yote ya asili yanayotendeka katika jamii hiyo. Mambo hayo ni kama vile lugha,

mila, itikadi, desturi, shughuli za kijamii kama harusi na misiba, ngoma, dini, malezi,

mavazi na hata tabia. Aidha, mazingira na historia nazo huchangia kwa kiasi kikubwa

mwelekeo wa utamaduni wa jamii husika uonekane kama hivyo ulivyo. Kwa kuwa kila

jamii duniani inao utamaduni wake, hivyo ndivyo ilivyo kwa jamii ya Wazanzibari yaani

wanao utamaduni wao. Wenyeji wa Zanzibar ni wahamiaji wa kale waliohama makwao

kwa sababu za kiuchumi na kuhamia Zanzibar. Baadhi ya wahamiaji hao walitoka nchi

za jirani na wengine nchi za mbali. Baadhi ya miji hiyo ni Somalia, Lamu, Mombasa,

Mzizima (Dar es salam), Yemen, Ngazija, Oman na Barahindi. Mchanganyiko wa jamii

zote hizi, dini na lugha inayowaunganisha wote ndizo zilizochangia kuujenga utamaduni

binafsi wa Mzanzibari na kuupa sura uliyonayo hivi sasa.

Kwa mujibu wa Al-Ismaily (1999), kiutamaduni, Zanzibar imeathiriwa zaidi na

utamaduni wa Kiislamu kwa vile wakaazi wake zaidi ya asilimia tisini na tano ni

wafuasi wa dini ya Uislamu. Hali hiyo, inaufanya utamaduni wao wa mavazi, shughuli

za kijamii kama arusi na mazishi, vyakula na mapisi, na maingiliano baina yao, ufanyike

kwa taratibu za kiislamu kwa kiasi kikubwa. Aidha, kitabia wanasifika sana na sifa za

upole, ukarimu, utulivu, upendo, ujamaa wa damu, na kushikamana na mafundisho ya

dini zao kwa kiasi kikubwa. Lugha kuu na rasmi ya wakaazi wa Zanzibar ni Kiswahili.

Kwa mujibu wa Khatib (1983), Zanzibar kuna lahaja kuu nne za Kiswahili ambazo ni

Kimakunduchi (Kikae) inayozungumzwa Kusini mwa kisiwa cha Unguja, Kitumbatu

49

inayozungumzwa kisiwani Tumbatu na maeneo ya Kaskazini ya Unguja, Kipemba

inayozungumzwa kisiwani Pemba, na Kiunguja inayozungumzwa Unguja Mjini na

maeneo ya Magharibi na ya Kati ya kisiwa cha Unguja. Kiunguja Mjini ndiyo lahaja

iliyosanifiwa na kurasimishwa kuwa ndio matamshi ya lugha kuu ya Kiswahili. Pamoja

na kuwa lugha kuu ya jamii ya Wazanzibari ni Kiswahili, jamii hiyo ina mchanganyiko

mkubwa wa watu wa makabila na mataifa mbalimbali duniani. Akiulezea utamaduni wa

Waswahili wa Zanzibar Sengo (1992) anasema:

Kazi kubwa ya kitaalamu juu ya utamaduni wa Kiswahili, ambayo

tunaijua hadi sasa ni tasnifu ya udaktari wa falsafa iliyoandikwa na

mwalimu Sengo kuhusu Sanaajadiiya ya Visiwani. Mwandishi

wake alivitalii visiwa vya Pemba na Zanzibar kwa utafiti wa kina na

kuibuka na hoja za kuueleza utamaduni wa Waswahili wa Visiwani

kwa kuheshimu utata uliosababishwa na Bahari ya Hindi.

Waswahili wenyewe wana michanganyiko, tangu ya maumbile,

damu, historia, asili, sababu, matukio, itikadi, imani n.k. Bahari ya

Hindi, historia ndefu ya Uislamu na lugha ya Kiswahili, ni baadhi

ya sababu kuu za kuwafanya Waswahili kujihisi wamoja kilugha,

kiutamaduni na kihisia. Uafrika asilia umepewa nafasi ya mwanzo

katika haki na hadhi ya Waswahili. Suala la ugozi lisitazamwe

kisiasa tu kwani kimaumbile watu tumepakwa rangi mbalimbali ili

tutambuane na tuelewane kirahisi katika kuendesha mambo yetu ya

kila siku maishani (uk. 12).

Kutokana na maelezo hayo ya Sengo, niwazi kuwa jamii ya Wazanzibari ni yenye

michanganyiko kadhaa ikiwemo ya itikadi, imani, damu na makabila. Aidha, kutokana

na lugha ya Kiswahili, watu hawa wameunganishwa na kujihisi ni wamoja katika

utamaduni wao uliochukuwa takriban kutoka katika kila kabila hasa Uafrika, Uarabu,

Uhindi na Ushirazi. Kwa hivyo, Wazanzibari ni jamii ya Waswahili yenye utamaduni

wake halisi unaozitofaisha na tamaduni za jamii nyengine za Waswahili.

50

4.2.1.3 Muktadha wa Kifasihi

Jamii ya Waswahili ya Zanzibar ina uhusiano mkubwa na fasihi ya Kiswahili iwe

andishi au simulizi. Kwa upande wa fasihi andishi kumetokea waandishi na wataalamu

wengi wa fasihi andishi ya Kiswahili ambao wameandika, kuhakiki, na kufanya tafiti

nyingi za Kiswahili. Mfano wa wanafasihi hao niSaid Ahmed Muhammed aliyeandika

Asali Chungu (1977), Kivuli Kinaishi (1990), na Sikate Tamaa (1980). Mwandishi

mwengine ni Shafi Adam Shafi aliyeandika Kasri ya Mwinyi Fuadi (1978), Kuli (1979)

na Vuta N’kuvute (1999). Muhammed Said Abdulla kwa upande wake ameandika

Mzimu wa Watu wa Kale (1960), Duniani kuna Watu (1976) naBwana Msa (1984).

Mohamed Suleiman Mohamed ameandika Kiu (1972), Nyota ya Rehema (19) na

Muhammed Seif Khatibu ameandika Fungate ya Uhuru (1988) naWasakatonge

(2003).Kazi zote hizo na nyengine nyingi, zinasifika sana kwa ufasaha wake wa lugha,

kiasi cha kuzifanya kuwa ni burudani na kigezo tosha cha maadili na utamaduni wa

jamii ya Waswahili wa Zanzibar pia kuziwezesha kutumika katika kufundishia fasihi

Mashuleni na Vyuoni.

Sambamba na fasihi andishi, fasihi simulizi nayo imetamalaki vyema katika fani zake

zote za hadithi, ushairi, maigizo, nyimbo pamoja na semi zikiwemo methali ndani yake.

Mara nyingi jamii imeshuhudiwa ikikaa katika mitaa na vijiji kwa nyakati tofauti na

hasa jioni, watoto na watu wazima wakisimuliana hadithi, vitendawili na kucheza

michezo mbali mbali. Nyimbo zinazoendana na aina ya ngoma zao kama taarabu asilia

na za kisasa, ngoma za kiutamaduni kama msewe na maumbwa nazo ni nyingi sana.

Kwa ujumla fani hii ya fasihi simulizi ndio mlezi wa wanajamii wote waswahili. Hii

imewafanya Waandishi nao waitumie kiasi kikubwa fasihi simulizi zikiwemo methali na

51

semi mbalimbali katika kazi zao. Hali hii, inathibitisha wingi wa kazi za fasihi simulizi

zinazotumiwa na jamii ya waswahili inayoishi Zanzibar. Akithibitisha wingi wa simulizi

hizo katika shairi lake la "Utamaduni Udumu," Maalim Haji Chum kama

alivyonukuliwa na Sengo (1992) anasema:

Kuna nyingi simulizi, ambazo zatia hamu

Za kale na siku hizi, kuzitunza ni muhimu

Tusiige upuuzi, ja kuabudu mizimu

Utamaduni udumu, vizazi hadi vizazi.

Methali na misemo mingine imo katika data ya mswada wa Maalim

Haji Chum. Misemo hii ni katika jumla ya mafumbo na vijembe

vya Kiswahili. Mifano: kuku mna wana halembewa bwe (kuku

mwenye watoto halengwi jiwe), kulya nguru si kazi, kazi kumosa

(kula nguru si kazi, kazi ni kumuosha) mdota asali hadoto umoja

(muonja asali haonji mara moja), si kiya mna kuche simba (si kila

mwenye makucha ni simba). Katika mafumbo yao, huwa wanasema

makubwa na mazito sana (uk.8).

Dondoo hili linathitisha kuwa simulizi hizo sio tu ni nyingi, bali pia ni zenye mafumbo

mazito na ambayo ndio hasa chem chem ya jamii za Waswahili ikiwemo ya Wazanzibari

kupenda kuzitumia simulizi zao hizo.

Kutokana na maelezo hayo kuhusu jamii ya Wazanzibari na utamaduni wake, utafiti

umebaini kuwa jamii ina uhusiano mkubwa na lugha ya Kiswahili. Hii ni kwa sababu

pamoja na kuwa Wazanzibari wana asili mbalimbali kama vile Makabila ya lugha za

Kibantu, Kiarabu, Kihindi na Kingazija, lakini wote hao hawatumii lugha hizo bali wote

hutumia lugha ya Kiswahili katika mawasiliano hata kama lafudhi zao zinawatofautisha.

Vilevile, utafiti umebaini kuwa jamii hii kama zilivyo jamii nyengine za Waswahili ina

matumizi makubwa ya methali za Kiswahili. Hili limethibitishwa katika uchunguzi

uliofanywa katika shughuli za kijamii katika sherehe na misiba pamoja baraza za

mazungumzo zilizohudhuriwa na mtafiti kwa vile, sehemu zote hizo methali zilikuwa

52

zikitumiwa. Kwa mfano, katika baraza moja ya mtaa3methali zifuatazo zilitumiwa:

“Mafahali wawili hawakai zizi moja”, “Hayawi hayawi, huwa”, na “La kuvunda halina

ubani”. Methali hizi zilikuwa zinasemwa na watazamaji wakati bao na karata

zinachezwa katika baraza hiyo. Hali hiyo ilibainika pia katika harusi na misiba. Kwa

hivyo, hali hiyo inabainisha kuwa Wazanzibari kutumia methali katika miktadha

mbalimbali ya maisha yao ni sehemu ya utamaduni wao.

C1: Methali hutumika hata katika mazungumzo ya kawaida katika Baraza za

mazunguzo. Mtafiti (aliyevaa shati ya njano anayeonekana uso) akiwa katika moja ya

Baraza hizo katika mtaa wa Sogea akifuatilia matumizi ya methali katika mazugumzo.

4.2.2 Methali za Kiswahili Zilizoachwa

Methali za Kiswahili zilizoachwa ni istilahi iliotumika katika utafiti huu, kuziwakilisha

methali maalumu. Methali hizo ni zile zilizokosa nafasi ya matumizi katika harakati za

kijamii kuanzia kipindi cha miaka ya tisiini hadi hivi sasa. Methali hizo, zilikuwa

mashuhuri sana na zikitumiwa katika jamii za Wazanzibari, lakini kwa sababu

zimeachwa kutumiwakwa sababu zisizofahamika, hivi sasa zimeshasahaulika na sehemu

3 Uchunguzi huo ulifanywa mtaa wa Sogea kwa Ayuba siku ya Jumatano tarehe 8/4/2015 saa 10:00 za

alasiri.

53

kubwa ya jamii ya wazee hawazikumbuki tena. Sio hivyo tu, bali utafiti umegundua

kuwa jamii ya vijana wao hawazifahamu kabisa. Methali hizo kwa sasa zimebakia katika

kumbukumbu za wazee wachache na katika baadhi ya vitabu vichache vilivyoandikwa

zamani. Methalihizo ambazo sasa jamii ya Wazanzibari haizitumii tena, ndio methali

zilizoachwa kwa mujibu wa utafiti huu.

Kuwepo kwa methali zilizoachwa kumethibitishwa kwa njia za udurusu wa maktaba,

mahojiano na dodoso. Kwa mfano, Farsi4 (1979) anaeleza wazi kuwa kutokana na

kuingizwa kwa elimu ya kisasa, na kizazi cha wazee kutoweka ambao ndio walionayo

fasihi simulizi, imani za nchini, vitendawili, methali na hadithi vinasahauliwa. Maelezo

yake yanathibitisha kuachwa methali pia yanaonesha kuwa tatizo hili limeanza zamani

kwa vile kipindi alicholizungumzia suala hili ni tokea miaka ya hamsini.Ingawa kwa

mujibu wa maelezo hayo suala la kuachwa kwa baadhi ya methalilimeanza zamani,

utafiti unaonesha kuwa bado linaendelea hadi sasa na katika miaka hii linaendelea kwa

kasi.Akiielezea kazi ya mwandishi Said iliyokusanya methali zaidi ya mia mbili za

Kiswahili, Hassan(2013) anasema kuwa mwandishi huyo kwa upande mwengine

anaikumbusha jamii baadhi ya methali ambazo zinaanza kutoweka ili (jamii hiyo) iweze

kuzikumbuka na hata kuzihifadhi kwa ajili ya kizazi cha sasa na cha baadaye.Aidha,

kupitia mahojianona wazee pamoja na watu wa makamo, nao wamekubaliana na ukweli

huo. Kwa mfano, wakati wa mahojiano na Bibi Asiya Miraji Khamis5 wa Kikwajuni

juualikirikuwa ni kweli siku hizi ziko methali zilizoachwa kutumiwa na kuongeza kuwa

4 Said Saleh Farsi ni mwandishi wa miaka ya khamsini aliyekusanya kazi mbali mbali za fasihi ya

Kiswahili Zanzibar. Miongoni mwa kazi zake ni Swahili Sayings 1 ya methali na Swahili Sayings2 ya

Vitendawili na kauli mbalimbali za kiitikadi walizonazo jamii ya waswahili Zanzibar. 5 Mahojiano hayo yalifanyika Ijumaa tarehe 03/02/2015 baina ya mtafiti na Bi Asiya. Bi Asiya ni

miongoni mwa wazee mashuhuri wenye ufahamu na ujuzi wa matemizi methali katika mazungumzo.

54

si methali tu, bali hadithi, vitenawili na hata maneno mengine ya zamani. Akitolea

mfano wa neno la kumkaribisha mgeni „starehe‟, ambalo kwa anahisi sasa halitumiki

kwani hajawahi kulisikia na lilikuwa ni neno la kawaida. Pia, maelezo yaSaid Ahmed6

kuwa baadhi ya kazi huwa zina muda maalumu, na unapopita zinaweza kuachwa, hivyo,

na kazi za fasihi simulizi zinaweza kuachwa na kutoweka kabisa kwa vile hazikuwa na

kumbukumbu ya kimaandishi. Kwa hivyo, kuachwa kwa baadhi ya methali za Kiswahili

katika jamii ya Wazanzibari nijambo lisiloshaka na hivyo kutoa mwanya kwa utafiti huu

kuzibainisha, ambapo matokeo halisi ya hatua zilizochukuliwa katika kuzibainisha

methali hizo ni haya yafuatayo:

Hatua ya kuipitiya orodha ya methali mia tano na ishirini na sita zilizokusanywa, utafiti

ulibaini methali mia tatu na hamsini ni zenye kujulikana kwa vile mtafiti alizikumbuka.

Kujulikana kwa methali hizo na mtafiti, kunathibitisha kuwa hizo ni methali

zinazoendelea kutumika hadi sasa katika jamii ya Wazanzibari. Methalimia moja na

sabini na sita zilizobakia ambazo mtafiti hakuzikumbuka,zilitengwa kwa hatua

inayofuata ambayo ni hatua ya kuzisikiliza kupitia vikundi vitano vya

majadilianovilivyotakiwa kutaja methali wanazozifahamu. Katika hatua hii,methali mia

tatu na kumi na saba zilikumbukwa na mia mbili na tisa hazikutajwa miongoni mwa

methali mia tano na ishirini na sita zilizokusanywa. Methali ambazo hazikutajwa

zilipambanuliwakati ya zilizosahauliwa na zilizoachwa.Kwa hatua hiyo, methali mia

moja na tano kati ya mia mbili na tisazilibainika kusahauliwa na mia moja na kumi tisa

zilizobakia ndizo zilizoachwa. Aidha, katika zoezi la kuzihakiki methalizilizoachwa,

6 Profesa Ahmed said Mohamed ni mtaalamu wa lugha ya Kiswahili na Mwandishi mashuhuri wa kazi za

fasihi andishi ya Kiswahili kutoka Zanzibar. Ameandika kazi nyingi za riwaya, tamthilia na ushairi.

Mahojiano kati yake na Mtafiti yalifanyika Jumatatu 9 /3/2015 katika ukumbi wa TAKILUKI.

55

matokeo yamebainisha kuwa methali thalathini na moja zinajulikana kwa vile

zilikumbukwa, na zilizobakia thamanini na nne, ndizo zilizothibiti kuwa ni miongoni

mwa methali nyingi za Kiswahili ambazo sasa jamii ya Wazanzibari haizitumii tena.

Kwa ujumla, utafiti umebaini kuwa,katika matumizi ya kawaidakwa jamii ya

Wazanzibari, methali hujigawa makundi manne. Kundi la kwanza ni la methali

maarufu sana. Hizi ni methali zinazotumiwa mara kwa mara. Utafiti ulibaini kuwa

watu wa rika zote wanazifahamu na kuzitumia takriban kila siku katika harakati za

maisha yao. Methali hizi zimebainika kuingia katika kundi hili kwa kule kupatikana

katika dodoso, vitabu na katika vikundi vyote vitano vya mijadala. Katika utafiti huu

methali mia mbili na kumi na nne ziliingia katika kundi hili. Kundi la pili, ni la

methali zinazofahamika kwa wastani. Hizi, ni zile ambazo zinatumiwa kwa wastani

katika jamii ya Wazanzibari. Katika mijadala ya vikundi, zilitajwa mara tatu au

mbilina hazikutajwa sana katika dodoso na pia hazikupatikana kwa wingi katika

vitabu vilivyotungwa miaka ya tisini hadi sasa. Methali mia moja na hamsini na tano

ziliingia kundi hili kati ya mia tano na ishirini na sita. Kundi la tatu ni la methali za

nadra. Methali hizi ni zile zinazotumiwa kwa uchache ambazo na zaidi hutumiwa na

wazee. Methali hizi hazikujulikana na vijana wengi pia zilipatikana kwa uchache

katika dodoso na zilitajwa katika kikundi kimoja tu kati ya vikundi

vitano.Methalisabini na tatu kati ya mia tano na ishirini na sita ziliingia kundi hili.

Na kundi la nne ni la methali zilizoachwa. Methali hizi,hazikupatikana katika dodoso

wala hazikutajwa katika vikundi vyote. Wanafunzi nao walipotajiwa sehemu ya

mwanzo hawakuweza kuzikamilisha. Hii nikuonesha kuwa methali hizi rika za

vijana na wanafunzi hawazifahamu kabisa. Methali hizi zilizopatikana katika vitabu

56

vya miaka ya hamsini na sitini, na kwa baadhi ya wazee katika mahojino. Methali

hizi hasa ndizo zilizokusudiwa kubainishwa katika utafiti huu ambapo ulibaini

methali thamanini na nne kati ya mia tano na ishirini na sita zilizochunguzwa

zimeachwa.

Methali za Kiswahili zilizothibiti kuwa zimeachwa katika jamii ya Waswahili ya

Zanzibar kwa mujibu wa utafiti huu ni hizi zifuatazo:

Jeduwali la methali zilizoachwa katika jamii ya Waswahili Zanzibar

Na. Methali

iliyoachwa

Etimolojia yake Maelezo ya jumla

kuhusu maana na

matumizi yake

1. Angakaanga,

tu chini ya

gae.

Asili ya methali hii ni

sehemu zenye

wafinyanzi.

Maana yake hata kama

atakaanga, sisi tupo

chini ya gae la

kukaangia (muhindi,

mtama).

Methali hii hutumika

wakati siri inapofichuka.

Maana yake ni kuwa

Hapana siri inayoweza

kufichika kwa watu hao

hata wasiijue.

2. Atangaye

sana na jua

hujua.

Asili yake katika taasisi

za elimu.

Anayehangaika na juwa

likampata katika

kujifunza jambo huweza

kilijua.

Hutumika katika

kushajihisha watu

wasivunjike moyo katika

kutafuta elimu.

Maana yake mtu

anayejishughulisha kwa

bidii kubwa hufanikiwa.

3. Atangazaye

mirimo si

mwana wa

ruwari.

Asili yake katika

shughuli za kiutawala.

Kuamrisha si lazima

kwa mwenye mamlaka

tu.

Ruwari(Liwali kiongozi)

Inatumika kuhimiza

utiifu kwa yoyote

anayetoa amri au

ushauri.

Maana yake ni kuwa

unapopewa amri

57

Mirimo (kazi,mashauri) usiidharau kwa

kuangalia aliyeitoa.

4. Avuliwaye

nguo

huchutama.

Asili yake kwa watu

wanaojiheshimu.

Mtu aliyevuliwa nguo

lazima achutame ili

ajisitiri.

Mtu anayefanya jambo

la aibu hana budi kuona

haya.

5. Boi manda

malipo yake

parapanda.

Asili yake enzi za

utumwa.

Boi manda (Mtumishi

wa hadhi ya chini)

Parapanda (zogo, kelele)

Hutimika wanapo

kuwepo watumishi

wanaonyanyaswa.

Watumishi wa hali za

chini hawathaminiwi.

6. Chombo cha

kuzama

hakina

usukani.

Asili yake sehemu

zenyepwani.

Maana yake chombo

kinachozama kwa

kuvuja maji hakiwezi

kuokolewa.

Hutumika wakati jambo

limeshaharibika sana.

Iwapo jambo limekiuka

mipaka na linazidi

kuzorota, si rahisi

kulirekebisha na hivyo

hapana haja ya

kuendelea kupoteza

muda kulishughulikia.

7. Dunia duara,

ukiichezea

utachera.

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Utachera (utasumbuka)

Mtu akijishughulisha

sana na mambo ya dunia

atahangaika na kupata

tabu bila ya mafaniko.

8. Endapo juu

kipungu

hafikii

mbinguni.

Asili yake ni sehemu

zenye viongozi

wanaojiona sana.

Kipungu (aina ya ndege

anyeruka juu sana)

Kadri anavyoruka juu

sana, hawezi kuzifikia

mbingu.

Hutumika anapotokea

mtu anayejiona kwa

cheo au mali.

Kujivuna si jambo jema

kawni mwisho wake ni

mtu kuharibikiwa.

9. Fungato

haliumizi

kuni.

Asili yake ni vijijini.

Mzigo uliofungwa

vyema haumuumizi

mbebaji.

Hutumiwa kwa

kuhimiza kusaidiana.

Jambo likiharibika kwa

mmoja tushirikiane

kulitengeneza.

10. Hakuna

nafsi tupu.

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Hutumika

kutahadharisha watu.

58

Hakuna mtu asiye na

mawazo katika akili

yaake.

Kila mtu ana mawazo

katika nafsi na hivyo

kumsikiliza ni muhimu,

huenda yakafaa.

11. Hasara

humfika

mwenye

mabezo.

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Mabezo (dharau, jeuri).

Anayepuuza ushauri

huishia kuhasirika.

Hutumika kuonyea tabia

mbaya ya dharau.

Inatuonya kutodharau

tunayoambiwa ili tuje

tukajuta.

12. Jina jema

hung‟ara

gizani.

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Jina la mtu mwema

husifiwa kila wakati.

Hutumiwa kuhimizia

kuwa wema katika jamii.

Inatuhimiza tuwe na

tabia njema ili tupate

utajo mwema.

13. Jogoo hulia

“uta wangu

ukule”.

Asili yake sehemu zenye

mifugo hasa ya kuku.

Uta wangu ukule (silaha

yangu iko mbali nami.

Hutumika kuwashutumu

wanaotoa visababu vya

uongo wanapokosa

kuwajibika.

Inatuasa tusiwe na tabia

ya kutowajibika kwa

kutegemea kutoa

dharura za uongo.

14. Joka la

mdimu

linalinda

watundao.

Asili yake sehemu za

kilimo cha matunda ya

viungo (ndimu, limao)

Nyoka aishiye mdimni

huwazuia wanaotaka

kuchuma ndimu.

Hutumika atokeapo mtu

anaewazuia wengine

jambo japo yeye hana

haja nalo.

Inatuasa tusiwe na tabia

ya uchoyo wa namna

hiyo.

15. Jungu bovu,

limekuwa

magae.

Asili yake sehemu zenye

wafinyanzi.

Jungu lililovunjika

huweza kuvunjika zaidi

hadi kubakia magae tu.

Hutumika atokeapo mtu

muovu akizidisha uovu

wake katika jamii.

Inatahadharisha kuwa

mtu akiwa muovu

huweza kuzidisha uovu

wake hasa asipokanywa.

16. Kanga hazai

ugenini.

Asili yake sehemu zenye

misitu yenye mawe.

Kanga (aina ya ndege

wa msituni kama kuku)

Hutumika kumtetea mtu

mgeni anaposhindwa

kufanya baadhi ya

mambo ugenini.

59

Kanga akihamishwa

kupelekwa ugenini

hushindwa kutaga

mayai.

Ugeni una shida zake,

hivyo ni vyema

kuwastahamilia wageni

wanaposhindwa kufanya

baadhi ya mambo.

17. Kikuu

pachika

kitakufaa

masika.

Asili yake sehemu zenye

vibanda vya mapaa ya

makuti, nyasi.

Kikuukuu usicho na haja

nacho kihifadhi,

kitakufaa kipindi cha

mvua za masika

Hutumika kushajihisha

uwekaji wa akiba.

Usidharau kilichotumika

usichokuwa na haja

nacho kwa muda huo. Ni

muhimu kukitunza

huenda kitakufaa

baadaye.

18. Kisokula

mlimwengu,

sera nale.

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Asichoweza kukila

binadamu hicho ni cha

shetani (ibilisi)

Hutumika kuwaasa watu

kuachana na mabaya.

Inatushauri kuachana na

mabaya kwani hayana

faida kwa wanadamu.

19. Kiwi cha

Yule, ni

chema cha

huyu; hata

ulimwengu

uwishe.

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Kibaya cha mtu hakiwi

chema kwa mwengine

daima.

Kitu kikiwa kibaya kwa

mmoja na muhali kuwa

chema kwa mwengine.

Inatuasa kutoshughulika

na vitu viso faida kwetu.

20. Koko haidari

mai.

Asili yake sehemu za

pwani.

Mbegu za mkoko

hazigusi maji ingawa

mkoko wenyewe umo

majini.

Hutumika kuonesha hali

ya kinyume na kawaida.

Mtu huweza kuishi

kwenye mazingira

mazuri au mabaya lakini

asiweze kuathiriwa

nayo.

Inatushajiisha kuwa

makini.

21. Kucha

Mungu si

kilemba

cheupe.

Asili yake katika

sehemu za ibada.

Kumwogopa Mungu ni

katika moyo na si kwa

kuvaa kilemba safi

kichwani.

Hutumika katika

kuwaaidhi watu kuwa

nan yoyo safi.

Inatufunza kuwa tabia

ya mtu kiimani na

vitendo vyake ndio

kipimo cha utu wake na

60

wala sio mavazi au

maneno yake matupu.

22. Kufa kwa

mdomo,

mate

hutawanyika

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Mtu anapokufa mate

hupotea kinywani

mwake.

Hutumika wakati

mambo Fulani

yanapoharibika kwa

kuondoka msimamizi.

Inatufunza kuwa makini

kukabili mambo ili

yasiharike kwa

kuondoka Yule

anayeyasimamia.

23. Kula

kutamu,

kulima

mavune.

Asili yake sehemu za

kilimo.

Mavune (Uchovu, tabu).

Kula chakula ni raha

lakini kukilima

shambani ni tabu sana.

Hutumika kushajihisha

watu kufanya juhudi au

kuwasuta wanaopenda

kula bure bila kufanya

kazi.

Si vema kutegea

kufanya kazi na kusubiri

kutumia bure.

24. Kutu kuu ni

la mgeni.

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Kutu kuu (makaribisho

mazuri).

Makaribisho mazuri na

ukarimu hufanyiwa

mgeni.

Hutumika kufunzia

ukarimu na ihsani kwa

wageni.

Inatuhimiza kuwafanyia

wema wageni ili

waweze kuwa na furaha

ijpokuwa wapo ugenini.

25. Kutwanga

nisile unga,

nazuia mchi

wangu

Asili yake ni katika

sehemu za vilimo vya

nafaka (mtama,

mpunga).

Ikiwa nitatwanga halafu

nikose japo sehemu ya

nnachotwanga, ntazuia

mchi wangu nisitwange.

Hutumika kuhimiza

malipo ya jasho la mtu

baada ya kufanya kazi.

Mtu anapokosa manufaa

ya mchango wake katika

jambo, huweza kuacha

kuchangia na huenda

likakosa kufanikiwa.

26. Lipitalo,

hupishwa.

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Jambo la mpito

huachiwa lipite.

Hutumika kuwaasa

wanaong‟ang‟ania

jambo la mpito

wasiloweza kulipata.

Inatuasa kutoshindana

na mambo ya kuzuka

tusiyoweza kuyapata.

61

27. Maafuu

hapatilizwi.

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Maafuu (mpungufu wa

akili).

Mtu mwenye akili

pungufu hapaswi

kuadhibiwa kwa

kukosea jambo.

Hutumika kuwaasa

wanaowatesa watu kwa

jambo wasiolielewa.

Inatuonya kutochukua

hatua kali kwa wale

wanaoshindwa kufanya

jambo kwa kutokuelewa.

28. Majumba

makubwa

husitiri

mambo

makubwa.

Asili yake katika

shughuli za kiutawala.

Mamlaka makubwa

huweza kufanya mambo

makubwa (mazuri au

mabaya) bila ya

kujulikana na wengi.

Hutumiwa

linapojitokeza jambo

kubwa lakushangaza

katika familia za

watukufu.

Inatutanabahisha kuwa

katika tawala au

majumba ya wakubwa

hufanyika mengi ila

huwa hayatangazwi.

29. Maneno

makali

hayavunji

mfupa.

Asili yake sehemu za

biashara ya nyama.

Maneno makali ya fitina

hayamuathiri mwenye

uwezo zaidi na makini.

Hutumika kuwashauri

watu wasishituliwe na

tetesi za watu fitina.

Maneno ya fitina na

uongo hayamuathiri mtu

makni asiyebabaika.

30. Mavi

usoyala,

wayawingia

ni kuku?

Asili yake sehemu zenye

mifugo hasa ya kuku.

Winga (fukuza)

Mtu hawezi kutumia

mavi yake kwa nini

awainge kuku

wanapoyala?

Hutumika kukanyia

tabia ya ubakhili.

Inatufunza tusiwe na

tabia ya ubakhili wa

kuwanyima wengine

hata vile tusivyovihitaji.

31. Mbinu

hufuata

mwendo.

Asili yake sehemu za

malezi ya maadili.

Mbinu za mikono

hufuata jinsi mtu

anavyokwenda.

Hutumika kuhimiza

kuwafuata wakubwa

wetu (wazazi, viongozi)

Inatufunza kuwa ni

vyema kwenda

sambamba na

wakumbwa wetu na si

vema kupingana nao.

32. Mchakacho

ujao,

haulengwi

na jiwe.

Asili yake sehemu za

ardhi za maweni,

mashamba.

Mchakacho (sauti za

majani

yanayokanyagwa)

Sauti za hatua ya kitu

Hutumika

kutahadharisha pupa ya

kufanya mambo.

Haifai kufanya jambo

kwa pupa kabla ya

kulijua lilivyo.

62

kinachokuja bila

kukijuahakirembewi

jiwe.

33. Mfa maji

hukamata

maji.

Asili yake sehemu zenye

maji (mito, maziwa,

bahari).

Anayekufa kwa maji

hachagui cha kukamata

kujiokolea.

Hutumika kuwanasihi

wenye shida kueleza

shida zao.

Mwenye tabu au shida

hutafuta kila aina ya

msaada ili kuitatua shida

yake.

34. Mgeni

hachomi

chaza mtaani

akanuka.

Asili yake sehemu zenye

bahari.

Mgeni achomapo chaza

ugenini hafikilii kunuka.

Hutumika mgeni

akiteleza kufanya jambo

baya.

Inatuhimiza kusamehe

wageni wanapokosea

kwani huwa hukosea

kwa bahati mbaya tu.

35. Mkata hana

kinyongo.

Asili yake sehemu za

kufunza maadili.

Mkata (Masikini)

Masikini siku zote huwa

haoneshi kuudhika

kwake.

Hutumika kumliwaza

mnyonge

anapokasirishwa.

Inatufunza kuwa

masikini ni mtu

anayebeba mengi ya

tabu na kuyastahamilia.

36. Mkata

hapendi

mwana

Asili yake sehemu

zenyejamii za masikini.

Masikini huwa hapendi

kuwa na mtoto kwa

kuchelea gharama.

Hutumika kuonesha

woga wa watu duni wa

kubeba gharama

wasizozimudu.

Inatuasa kutowatwisha

mizigo wasioimudu.

37. Mkataa

chinjo

hupata

mtanda

Asili yake sehemu za

mauzo ya vitoweo

(nyama).

Chinjo -nyama nzuri

Anayekataa nyama

iliyonona kwa kuchagua

kwake huishia na

ngumu.

Hutumika

kumtahadharisha mtu

anayechagua sana.

Mtu anayekataa cha

kupewa kwa kudhani

atakachochagua

mwenyewe ndio chema,

huambulia na kibaya

kwa kutoelewa vema.

38. Mkate

mkavu wa

nyumbani ni

bora kuliko

nyama

shuwa ya

Asili yake sehemu za

mifugo mauzo ya

nyama.

Nyama shuwa- nyama

laini, iliyonona.

Ni bora kula mkate usio

Hutumika kuhimiza

kuthamini maisha ya

nyumbani.

Mtu huridhika kuwa

kwao japo kuna dhiki

63

pengine. na kitoweo uliowenu

kula nyama iliyonona

lakini sio yenu.

kuliko kuwa ugenini

ijapo kuna mazuri zaidi.

39. Mkono

mmoja

hauchinji

ng‟ombe.

Asili yake sehemu za

machinjio ya wanyama.

Mkono mmoja peke

yake hauwezi kuchinja

ng‟ombe.

Hutumika kuhimiza

ushirikiano wa watu.

Ufanisi wa mambo

hauwi mzuri bila ya

kuwa na ushirikiano.

40. Mkosa

kitoweo

humangiria.

Asili yake sehemu zenye

jamii za masikini.

Humangiria – hukadiria

kwa umakini.

Aliyekosa kitoweo

hukitumia kwa uangalifu

sana kichache

kilichosalia.

Hutumika katika

kutahadharisha

matumizi ya fujo,

isirafu.

Inatufunza tusiwe na

matumizi mabaya ya

vitu tulivyojaaliwa

kuvipata kwa wasaa au

kwa tabu, tutahasirika.

41. Mla cha

uchungu na

tamu hakosi

Asili yake sehemu zenye

jamii za masikini.

Anayekula vyakula

vibaya, hatakosa

kubahatika kula na

vitamu.

Hutumika kuwaliwaza

waliofikwa na yale ya

kustahamiliwa.

Inatufunza kuwa

wastahamilivu wakati

wa dhiki ili kuipata

faraja ya baadaye.

42. Mla kwa

miwili hana

mwisho

mwema.

Asili yake sehemu za

kufunza maadili.

Anayekula kwa kutumia

mikono yote miwili

mwishowe hufikwa na

mabaya.

Hutumika kuwaasa watu

kuacha tama.

Mwenye tamaa ya

kutaka kufaidi kwa

kutumia hila na uongo

mwishowe hupata

hasara.

43. Mla mbuzi,

hulipa

ng‟ombe.

Asili yake sehemu za

mifugo mauzo ya

nyama.

Anayepewa mbuzi

humlipa kwa kutoa

ng‟ombe. Au

anayekamatwa kwa

kuiba mbuzi atalipishwa

kutoa fidia ya ng‟ombe.

Hutumika kuhamasisha

kushuru fadhila.

Mtu akitendewa wema

mdogo, hukumbuka na

kulipa kwa wema

mkubwa zaidi.Au

hutumika kuhadharisha

ubaya wa wizi.

Anayekamatwa kwa

wizi huishia kulipa fidia

ya kubwa zaidi ya

alichoiba.

64

44. Mlilala

handingwan

dingwa;

mwemacho

haambiwi

tule

Asili yake sehemu za

kufunza maadili.

Handingwandingwa –

hahisi njaa.

Aliyelala haumwi na

njaa, aliye macho

hasubiri kuitwa kula.

Hutumika atokeapo

mvivu anayelalamikia

njaa.

Inatufunza kutokuwa

wavivu kwa kudhani

hatutaumwa na njaa.

45. Mnyamaa

kadumbu

Asili yake ni lahaja ya

Kimakunduchi.

Aliyenyamaza ndiye

aliyeshinda.

Hutumika anpotokea

msemaji sana.

Inatufunza kuwa kusema

sana hakuna faida.

46. Mpemba

hakimbii

mvua ndogo

Asili yake na kisiwani

Pemba.

Mpemba hakmbii mvua

ndogo kwa kuzowea

kuona mvua kubwa.

Hutumika anapotishiwa

mwenye hali kubwa.

Mwenye kufikwa na

misukosuko mikubwa

hatishiki kwa midogo.

47. Msafiri

masikini

ajapokuwa

sultani

Asili yake sehemu zenye

utawala wa Kiarabu.

Msafiri ni sawa na

masikini hata kama ni

Mfalme.

Hutumika kuelezea

mwenye hali ya juu

anapokabili hali duni.

Mtu hubidi kuishi

maisha duni hata kama

alikuwa na hadhi kubwa

pale inapobidi.

48. Msasi

haogopi

mwiba

Asili yake ni sehemu

zenye misitu na usasi.

Anayewinda wanyama

msituni haogopi

kuchomwa na miiba.

Hutumika kuliwazia

panapotokea matatizo.

Inatufanza kuwa wajasiri

kukabiliana na matatizo

tukitarajia kupata

mafanikio.

49. Mshale

kwenda

msituni

haukupotea

Asili yake ni sehemu

zenye wawindaji

wanyama.

Mshale ulioelekezwa

msituni huwa

haukupotea bure.

Hutumika kuhimiza

uvumilivu.

Sio kila juhudi

zinazofanywa hutoa

matunda haraka,

huwenda ukachelewa.

50. Mtaka unda

haneni

Asili yake sehemu za

kufunza maadili.

Anayekusudia kutenda

jambo hana haja ya

kusema.

Hutumika kuhimiza

utendaji kuliko kusema.

Inatufunza tuwe

watendaji zaidi na

tusijisifu au kujitangaza.

51. Mteuzi

haishi tama

Asili yake sehemu za

kufunza maadili.

Anayependa kuchagua

huwa na tamaa siku

zote.

Hutumika kuasa kuwa

na tama.

Inatufunza tusipende

kuchagua huenda

tukapoteza fursa

muhimu.

65

52. Mtoto

msikivu hula

cha siri

Asili yake sehemu za

kufunza maadili.

Mtoto anayewasikiliza

wakubwa zake hupata

mpaka vya ndani.

Hutumika kushajihisha

utiifu kwa wakubwa.

Inatufunza kuwa

tunapofuata ushauri wa

wakubwa zetu, hupata

mafanikio tusioyatarajia.

53. Mtoto wa

mhunzi

akikosa

kufua,

huvukuta

Asili yake sehemu

zinazofuliwa vyuma.

Mhunzi – mfua vyuma.

Mtoto wa mfua vyuma

anapokosa kufua vyuma

mikono yake humuuma.

Hutumika kuonesha

athari ya kazi nzito.

Jambo lolote lenye

mazoweya kuliacha

linaleta matatizo.

54. Mtumi wa

kunga

haambiwi

maana.

Asili yake ni sehemu

baraza za wazee.

Kunga – jambo la siri.

Anayetumwa kupeleka

siri sehemu haambiwi

undani wa siri hiyo.

Hutumika kuhimiza

kufanya siri mambo

muhimu.

Inatufunza watu

tunapowatuma mambo

ya siri tusiwaeleze

makusudio ili siri

isifichuke.

55. Mvungu

mkeka.

Asili yake sehemu za

ndani katika nyumba.

Mvungu – chini ya

kitanda.

Sehemu ya chini ya

kitanda huwa kama

mkeka kwa kuhifadhia

vitu vingi vizuri.

Hutumika kuonesha

umuhimu wa kutunza

mambo.

Moyo wa mwanadamu

ni kama mvungu kwa

kuhifadhi siri nyingi.

56. Mvuvi

anajua

pweza alipo

Asili yake ni sehemu

zenye amali ya uvuvi.

Pweza – aina ya samaki.

Mvuvi wa pweza ndiye

anafahamu pweza

anamoishi.

Hutumika kuwaenzi

wenye ujuzi wa jambo.

Ukitaka kuelimika juu

ya jambo fulani

mwendee mwenye ujuzi

nalokwasababundiye

awezaye kutoa ushuri

sahihi juu ya jambo hilo.

57. Mwacha

asili ni

mjasiri.

Asili yake sehemu za

kufunza maadili.

Anayeacha utamaduni

wa kwao huwa ni mtu

mpuuzi.

Hutumika kuuenzi

utamaduni wa jamii.

Kuacha utamaduni wa

asili na kufuata wa

kigeni huwa nikama

utumwa asiye na kwao.

58. Mwamba na

wako

hukutuma

umwambie.

Asili yake ni sehemu za

kufunza maadili.

Anayemsema jamaa

yako mbele yako huwa

Hutumika kuhadharisha

tabia ya kusengenya.

Mwenye kufanya ubaya

bila kificho, huwa

66

anakutuma umwambie. hawachelei wale

wanaomuona.

59. Mwana maji

wa Kwale

kufa maji

mazowea.

Asili yake ni mwambao

wa pwani.

Kwale – mji ulioko

Pemba na Tanga.

Mkaazi wa Kwale kufa

kwa ajali ya maji si

jambo la kustaajabisha.

Hutumika kuasa tabia ya

kujigamba.

Si vema kufanya jambo

kwa kujiona hodari

kwani huweza

kuliharibu na hata

kujipata mwenyewe.

60. Mwana

mkuwa

nawe ni

mwenzio

kama wewe.

Asili yake ni sehemu za

kufunza maadili.

Mtoto anayelelewa nawe

naye ni mwenzio kama

ndugu yako wa

kuzaliwa.

Hutumika kuhimiza

uhusiano mwema.

Kuishi pamoja na mtu

wan je ya familia yako

kwa muda mrefu

kunajenga uhusiano

mwema wa kijamaa

kama ndugu wa

kuzaliwa pamoja.

61. Mwana wa

ndugu

kirugu,

mjukuu ni

mtu mbali

Asili yake ni sehemu za

kufunza maadili.

Kirugu – kipele

kinachouma.

Mtoto wa ndugu yako ni

mtu wako wa karibu

zaidi kwa kuwahudumia

kuliko mjukuu wako.

Hutumika kukumbusha

uhusiano wa jamaa wa

karibu.

Inatufunza kuwa jamaa

wa mtu wa karibu nao ni

muhimu kwa kuwajali

na kuwasaidia kama

mwanao na mjukuu

wako.

62. Mwekaji

kisasi

haambiwi

mwerevu.

Asili yake katika

mapambano.

Anayeweka kisasi cha

kutendewa uovu si

katika watu wenye

busara.

Hutumika kuhimiza

kusameheana na

kustahamiliana.

Inatufunza kuwa haifai

kulipizana kisasi

tunapokoseana na badala

yake tujenge tabia ya

kusameheana.

63. Mwenye

njaa hana

miiko.

Asili yake katika jamii

masikini.

Mtu mwenye njaa kali

huwa hachagui chakula.

Hutumika kuhimiza

kufanya kila aina ya

bidii ili kufanikiwa.

Ni muhimu kutumia

maarifa mbalimbali ili

kutosheleza mahitaji

yanayokabili.

64. Mwibaji na

watwana,

Asili yake ni sehemu

zenye utumwa na

Hutumika kuasa tabia

mbaya.

67

mlifi ni

mwungwana

ubwana.

Watwana – watu

wanaotumiliwa, Kilifi –

mji ulioko Kenya.

Mwizi wenziwe ni watu

wanaotumiliwa lakini

mtu wa Kilifi yeye ni

mtu mwenye heshima.

Muovu siku zote

hujulikana kwa tabia

yake ya kukaa na watu

wenye zinazolingana

naye. Na mwema na

hukaa na watu wema

wenziwe.

65. Mwili wa

mwenzio ni

kando ya

mwilio.

Asili yake ni sehemu za

kufunza maadili.

Mwenzako ni mtu wa

mbali na nafsi zenu ni

tofauti.

Hisia katika kupokea

mambo zinatofautiana.

Hutumika kuonesha

utofauti wa hisia za

watu.

Yanayompata mtu

mmoja (mema au

mabaya) athari yake ni

tofauti na kama

yangempata mtu

mwengine.

66. Mzika

pembe ndiye

mzua

pembe.

Asili yake sehemu zenye

imani za kishirikina

(kwenye waganga).

Anayeizika pembe ndiye

aijuaye ilipo na ndiye

awezaye kuizikua.

Hutumika kuonesha

umuhimu wa kumpata

muhusika katika kutatua

tatizo.

Mtatuzi bora tatizo ni

yule aliyesababisha

tatizo kwa vile

analifahamu vizuri.

67. Mzowea

kutwaa,

kutoa ni vita.

Asili yake ni sehemu za

kufunza maadili.

Aliyezowea kupewa kila

mara huona vigumu

kutoa yeye.

Hutumika aokeapo mtu

bahili na mwenye tamaa.

Inatufunza tusiwe na

tabia mbaya za uchoyo

na ubahili.

68. Mzungu wa

kula

hafundishwi

mwana.

Asili yake ni katika

kipindi cha ukoloni.

Mtoto hafundishwi

namna ya kula kwa vile

huweza kugundua

mwenyewe.

Hutumika kuonesha mtu

anavyoweza kujikimu.

Mtu hahitaji

kufundishwa jinsi ya

kujitosheleza haja zake

za msingi bali hubuni

njia mwenyewe hizo.

69. Ndege

mwigo hana

mazowea.

Asili yake sehemu za

ufugaji hasa ndege.

Ndege anayefanya

mambo kwa kuiga

wenziwe huwa hapati

kujifunza mwenyewe.

Hutumika atokeapo mtu

anayefanya mambo kwa

kufuata mkumbo.

Anayefanya jambo kwa

kuiga tu si kwa ujuzi

huwa hapati ujuzi huo na

huwa hafanikiwi.

70. Ndugu

chungu,

Asili yake ni sehemu za

ufinyanzi.

Hutumika kuonesha

umuhimu wa ndugu au

68

jirani

mkungu.

Mkungu – ufuniko wa

chungu.

Umuhimu wa ndugu

kwa mtu ni kama

chungu na jirani ni kama

mkungu.

jirani.

Inatufunza kuwathamini

ndugu na majirani lakini

si sawa kuwathamini

majirani zaidi kuliko

ndugu.

71. Ndugu mwui

afadhali

kuwa naye

Asili yake ni sehemu za

kufunza maadili.

Mui – mbaya.

Nduguyo mbaya ni bora

uwe naye kaliko

kumkosa.

Hutumika kuonesha

umuhimu wa kumuenzi

ndugu.

Hata kama ni mbaya,

ndugu ni vema kuwa

naye kwani anweza

kutatua matatizo yako

kuliko marafiki

wanaoweza kukukimbia.

72. Nimekupaka

wanja, wewe

wanipaka

pilipili?

Asili yake ni sehemu za

kilimo cha viungo.

Inakuwaje mimi

nikupake wanja wewe

unipake pilipili?

Hutumika kumsimanga

anayelipawema kwa

ubaya.

Inatuasa kuthamini

wema tuliotendewa kwa

kurejesha wema na sio

ubaya.

73. Njia ya siku

zote haina

alama.

Asili yake ni sehemu za

usafirishaji na biashara.

Njia ya kupitwa

kikawaida haihitaji

kuekewa alama kwani

haipotezi.

Hutumika kuonesha

umuhimu wa uzowefu.

Jambo linalofanywa

mara kwa mara husaidia

kufanywa vizuri na bila

ya taabu kubwa.

74. Nta si asali;

nalikuwa

nazo si

uchunga.

Asili yake ni sehemu za

kurina asali.

Nta – utomvu

unaoyashikilia mavuna

ya jumba la nyuki.

Nta si sawa na asali na

aliyekuwa nazo si sawa

na aliyenazo sasa.

Hutumika kumkashifu

anayejitapa kwa

alichokuwa nacho kabla.

Mtu hapaswi kuringia

vitu duni alivyovimiliki

zamani na sasa hanavyo,

huwa hakuna faida

yoyote.

75. Nyimbo ya

kufunzwa

haikeshi

ngoma.

Asiliyake ni sehemu

zenye utamaduni wa

ngoma.

Nyimbo ya kujifundishia

haitegemewi kukesheza

ngoma.

Hutumika kuonesha

ubaya wa kutegemea

vitu vya mpito.

Haifai kutegemea vitu

vya mpito ambavo

havidumu.

76. Paka

hakubali

kulala chali.

Asili yake ni sehemu

zenye mifugo ya

nyumbani.

Hutumika kuonesha

tabia ya werevu wa mtu.

Mtu mwerevu si rahisi

69

Paka hakubali kulala

chali kwa wepesi wake

wa kujigeuza haraka.

kuwezwa na matatizo

kwani anazo njia nyingi

za kutatua matatizo

yake.

77. Radhi ni

bora kuliko

mali.

Asili yake sehemu za

mafunzo ya maadili.

Radhi za (Mungu,

wazee, mke, mume) ni

bora kuliko kuwa na

mali nyingi bila ya

radhi.

Hutumika kuonesha

thamani ya kuridhiwa.

Inatufunza kushughulika

kutafuta radhi zaidi

kuliko mali kwani mali

bila ya radhi hainufaishi.

78. Radhi za

wazee ni

fimbo

maishani.

Asili yake sehemu za

mafunzo ya maadili.

Kukosa radhi za wazazi

ni adhabu kubwa ya

maisha.

Hutumika kuonesha

thamani ya wazee.

Mwenye radhi za wazee

husitirika na aliyezikosa

husumbukamaishani.

79. Shimo la

ulimi mkono

haufutiki.

Asili yake sehemu za

mafunzo ya maadili.

Ulimi unaweza kutoboa

shimo lisiweze kuzibwa

kwa mikono.

Hutumika kuhadharisha

madhara ya ulimi

unapotumiwa vibaya.

Inatufunza tuyafikirie

kwa makini

tunayoyanena kabla ili

yasije yakaleta madhara

makubwakwa jamii.

80. Simbiko

haisimbuki

ila kwa

msukosuko.

Asili yake ni sehemu za

bahari.

Simbiko – uzi wa

ndoana.

Fundo ya uzi wa ndoana

huwa haifunguki mpaka

kwa tabu au

kufunguliwa makusudi.

Hutumika kuonesha

umakini wa uhusiano.

Watu wenye uhusiano

wa dhati si rahisi

kuachana au kutengana

ila kwa uhasidi mkubwa

uliokusuduwa

kuwatenganisha

makusudi.

81. Tonga si

tuwi.

Asili yake sehemu zenye

minazi.

Ukubwa wa nazi sio

wingi wa tuwi.

Hutumika kulinganisha

maarifa ya vijana na

wazee.

Maarifa ya kijana

hayawezi kushinda yam

zee licha ya nguvu na

uzima alizonazo kijana.

82. Ukitaja

nyoka, shika

fimbo

mkononi.

Asili yake ni mazingira

ya mitaa yenye misitu.

Hutumika kuhadharisha

hatari.

Inatufunza tujiandae

kwa hatari inayotokea

ghafla wakati wowote.

83. Umekuwa Asili yake ni maeneo ya Hutumika kuhimiza

70

nguva,

huhimili

kishindo?

pwani.

Nguva – samaki

anyonyeshaye wanawe.

Huuwawa kwa wepesi

sana.

kuwa na ujasiri.

Inatufunza tusiwe dhaifu

bali tuwe wajasiri katika

kukabiliana na matatizo

yanayotukabili.

84. Waraka ni

nusu ya

kuonana.

Asili yake ni mazingira

ya kijamii.

Waraka – barua.

Kutumiana barua na

nusu ya watu kuonana.

Hutumika kuhimiza

kukumbukana.

Inatufunza kuwa ni

muhimu kwa waliombali

kukumbukana japo kwa

kuandikiana barua.

4.3Sababu za Wazanzibari Kuacha Baadhi ya Methali za Kiswahili

Sehemu hii inafafanua sababu mbalimbali ambazo utafiti huu umebaini kuwa ndizo

zinazosababisha kuachwa kwa baadhi ya methali za Kiswahili katika jamii ya

Wazanzibari. Katika hatua ya kwanza ya kuchanganua data zenye sababu za

kuachwa kwa methali hizo, utafiti umebaini sababu nane ambazo zilipendekezwa na

mtafiti kwa watafitiwa wake. Katika hatua ya kuyachambua majibu ya watafitiwa,

utafiti umebaini sababu tano ndizo zilizokubalika na jamii ya watafitiwa. Aidha,

katika hatua ya kuzichambua sababu walizozitoa watafitiwa binafsi, utafiti ulibaini

sababu nyingizinarejea katika zile sababu za awali zilizopendekezwa na

mtafiti.Sababu zilizobaki hazikuonekana kuwa ni sababu za msingi za tatizo hilo na

hivyo kuachwa.

Uchambuzi wa data za sababu za kuachwa methali ulitumia muhimili wa pili wa

nadharia ya uamilifu. Msingi huu unaangalia utendaji kazi wa jukumu la kipande

kazi hicho cha fasihi simulizi katika jamii ambapo utafiti ulibaini methali hizo

hazitekelezi dhima zake ipasavyo. Sababu ya msingi ya kushindwa kutekeleza dhima

zake ni kukosa nafasi ya matumizi katika jamii ya Wazanzibari, jambo

71

lililosababisha kuchunguza sababu za kutotumiwa na kugundulika mambo kadhaa

kuwa ndio yanayosababisha kuachwa kwa methali hizo.Kwa ujumla, utafiti

umegundua sababu kuu zifuatazo:

4.3.1 Mvuvumko wa Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia

Kwa mujibu wa Oxford Advanced Learners Dictionary of current English (2000),

Sayansi ni taaluma ya maumbile na mwenendo wa asili wa kiulimwengu unaotokana

na msingi wa ukweli unaoweza kuthibitishwa kwa kwa njia za majaribio. Teknolojia

ni utumiaji wa taaluma ya sayansi kimatendo katika kubuni na kutengenezazana na

mashine mpya (uk. 1051, 1230) (Tafsiri ya Mtafiti). Kutokana na fasili hizo,

inafahamika kwamba, Sayansi na teknolojia ni msamiati unaotumika kuwakilisha

taaluma ya kisasa inayotolewa kwa uchunguzi, majaribio, vipimo na kisha

kuthibitishwa kwa utafiti au uchunguzi na baadaye kutumika katika ubunifu na

utengenezaji wa zana, mitambo au mashine bora zinazorahisisha utendakazi na

kuleta mabadiliko ya haraka ya kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yanayotokana na

matumizi ya uvumbuzi huo wa kitaalamu.

Jamii nyingi zimekumbwa na mabadiliko ya aina hii. Hii ni kutokana na ukweli

kwamba mabadiliko ya aina hii kwa kiasi kikubwa yamerahisisha maisha ya

wanadamu katika shughuli zao nyingi za kimaisha. Sekta mbalimbali duniani leo

zimefikia kiwango cha hali ya juu kabisa kwa ufanisi. Kwa mfano, sekta ya viwanda,

biashara mfano huduma za kibenki, kilimo mfano zana za kilimo, kuvunia na

madawa. Pia, sekta ya elimu mfano matumizi ya kompyuta na vyuo vikuu vya

72

kimitandao, sekta ya afya mfano madawa na upasuaji wa haraka pamoja na sekta ya

habari mfano ujenzi wa vituo vya redio na televisheni na zana za kurushia

matangazo. Yote haya yamekuwa kwa kasi katika jamii za wanadamu kutokana na

wepesi wake wa utengenezaji na matumizi ya zana za kisasa ambapo hali hiyo

imekuja kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia yaliyofikiwa.

Hata hivyo, maendeleo haya ya sayansi na teknolojia pamoja na kuonekana kuwa ni

hatua muhimu ya kimaendeleo kwa upande mmoja, kwa upande mwengine imeleta

athari hasi katika sekta kadhaa. Hivyo, kama ilivyo kwa mambo mengi kuwa na

athari hasi na chanya, na ndivyo ilivyo kwa maendeleo hayo yanayotokana na

sayansi na teknolojia. Akithibitisha hali hiyo, Kitabuge (2011) anasema kuwa

ugunduzi katika suala la sayansi na teknolojia kwa kawaida huwa na manufaa na

madhara kwa viumbe, na kuongeza kuwa uchanya na uhasi wa athari hizo unaweza

kuonekana kwa kuangalia hali ya utendaji au awasilishaji wa fasihi simulizi ilivyo

sasa katika jamii. kwa mujibu wa maelezo haya, ni wazi kuwa pamoja na kuwa

fasihi simulizi imenufaika, bali pia imeathiriwakutokana na maendeleo hayo.

Sababu hii inaonekana kuwa wazi zaidikiasi cha kukubalika na jamii kubwa ya

watafitiwa. Hii ni kutokana na ukweli kuwa suala la maendeleo ya sayansi na

teknolojia limeathiri mfumo mzima wa maisha ya wanadamu, ikiwa ni pamoja na

lugha zao hasa upande wa fasihi.Khamis (1983) anathibitisha athari hasi mbaya

itokanayo na sayansi na teknolojia kwa kusema kuwa fasihi simulizi imevizwa kwa

maendeleo ya kiufundi na uvumbuzi wa mashine kadhaa, hasa za uchapaji na za

mawasiliano kama vile redio, teprikoda na televisheni. Yesaya (2011) anaonesha pia

73

athari hasi ya sayansi na teknolojia kupitia sekta ya habari katika fasihi simulizi ya

watoto anasema maendeleo ya teknolojia ya habari na mawasiliano ambayo

nimatokeo ya kukua na kuenea kwa sayansi na teknolojia duniani katika karne hii ya

ishirini na moja, yameathiri sana muundo wa nyimbo za watoto waishio mijini.

Maendeleo haya ya sayansi na teknolojia yaliyosababisha kutokea na kuenea kwa

vyombo vya habari na mawasiliano. Nyimbo nyingi za watoto waishio mijini

zimeathiriwa na maendeleo haya.Kutokana naugumu wa kuyaepuka na athari zake

kwa fasihi simulizi yote kwa jumla ni kubwa.

Katika jamii ya Wazanzibari maendeleo haya nayo yameshajikita vyema. Hali hiyo

imefanya mwenendo wa utamaduni wao kubadilika. Kwa mfano, hivi sasa vikao vya

wazee na vijana na watoto wao vimetoweka kutokana na elimu hii Farsi (1958).

Utamaduni wa kusikiliza methali, hadithi na vitendawili umetoweka. Nafasi ya vikao

hivyo, imechukuliwa na mshughuliko wa vijana katika elimu ya kisasa (sayansi na

teknolojia) kwa upande mmoja, na vyombo vya habari kama vile redio, simu, video

na televisheni kwa upande mwengine. Vyombo hivyo vyote vina uchache wa

kuwasilisha kazi za fasihi simulizi au kukosa kabisa. Kwa hivyo, kutokana na

kukosekana kwa njia hiyo ya asili, na uchache uliopo wa mawasilisho ya kazi za

fasihi simulizi, kazi hizo husahauliwa na hatimae kuachwa kama ilivyotokea kwa

methali hizo.

Ukichukua mfano wa methali; “Angakaanga, tu chini ya gae”, “Avuaye nguo

huchutama” na “Kutwanga nisile unga, nazuia mchi wangu”. Hizi ni methali ambazo

kwa wakati wake zilitumika sana na ni nzuri lugha na ujumbe wake. Ila mambo

74

yanayoelezwahivi sasa jamii ya waswahili ni nadra sana kuyatumia. Mambo kama

chungu kwa sasa mbadala wake ni sufuria ambayo haitoi gae. Pia ukaangaji wa

nafaka kama mtama ama mahindi ni nadra sana kwani sasa kuna mashine za kusagia.

Utamaduni kuvua nguo kwa kuchutama pia umetoweka baada ya ujenzi wa vyoo

vinavyositiri kwa uhakika kwani lengo ni kuepusha kukashifika kwa vile makaazi

halisi ya wakati huo mara nyingi hayakusitiri ipasavyo. Pia masuala ya kutwanga

kupembua unga wa makapi, matumizi ya vinu na michi vinatoweka katika jamii ya

Wazanzibari baada ya kuibuka vifaa kama blenda na mashine za kusagia. Hayo ni

mabadiliko yanayotokana na maendeleo hayo.

4.3.2Mabadiliko ya Msamiati Uliotumikakatika Methali hizo

Katika hali halisi, mambo mengi duniani hayakuwepo hapo kabla, baadae yametokea na

tena yatatoweka. Vilevile, kuna mambo kadhaa ambayo yapo leo lakini hayakuwepo

zamani. Hali hiyo, pia ndiyo inayomkabili mwanadamu na maisha yake hapa duniani.

Lakini hapa hoja ni kuwa, kwa vile binadamu hutoweka, vilevile na mambo yake pia

hufuata mwendo huo. Kwa hivyo, lugha nayo huwepo na baadae hutoweka. Ndio maana

leo kuna oradha ya lugha kadhaa zilizokuwa zinatumika hapo zamani, na hivi sasa

hazipo tena pia, kuna lugha nyingi zilizopo leo zamani hazikuwepo. Kwa hivyo, iwapo

lugha nzima huweza kutoweka, na sehemu ya lugha ni wepesi zaidi kutoweka. Bila

shaka, kuna uwezekano mkubwa wa vitu vya lugha kama hadithi, nyimbo na methali

vikawepo kwa wakati fulani na baadaye kutoweka. Hali hii ipo zaidikwa fasihi simulizi

ya Ki-Afrika ikiwemo ya Kiswahili ambayo ilihifadhiwa kupitia vifua vya watu kwa

muda mrefu kabla ya kuwepo kwa maandishi.

75

Kazi za fasihi simulizi huwa na uteuzi wa maneno maalumu yanayotumika katika

jamii. Uteuzi huu hufanywa kwa ufundi mkubwa. Mbali na uteuzi wa maneno hayo,

pia, mpangilio wake huwa kwa ufundi. Kwa sababu hiyo, ndio maana kazi hizo hasa

za fasihi simulizi huvutia usikivu wake na hupendwa kutumiwa na kila rika la

kijamii.Methali hutumia lugha maalumu na teule kwa ustadi mkubwa. Lugha yake

hupambwa kwa sitiari, nidaa, tashbiha, taswira, balagha, takriri, mchezo wa maneno,

tamathali za semi, tanakali sauti, pamoja na mbinu nyengine za kinudhumu (Simiyu,

2011). Pamoja na yote hayo, vitu hivyo huweza kubadilika ladha yake kwa tatizo la

kukosa matumizi ya baadhi ya misamiati iliyotumiwa katika methali hizo kwenye

jamii ya leo ya Wazanzibari.

Baadhi ya methali hizi zina misamiati ambayo kwa sasa jamii ya Wazanzibari

haiitumii tena. Hali hii,huwafanyavijana wasizifahamu methali hizo. Jambo hilo

huwafanya wazee wenye methali hizo nao waziache na kutumia zile zenye maneno

yanayoeleweka zaidi. Kwa mfano maneno kama vile, „humangiria‟, „Mkata‟ na

„handingwandingwa‟ katika methali; “Mkosa kitoweo humangiria”,

“Mlilalahandingwandingwa,mwemacho haambiwi tule” na“Mkata hana kinyongo”.

Maneno haya kwa sasa jamii ya Wazanzibari haiyatumii tena. Hii ndio maana baadhi

ya watafitiwawalipotakiwa kueleza maana za maneno hayo yaliwashindakutokana na

ugeni uliopo katika maneno hayo nandio maana sababu hii watafitiwa wengi

wamekubaliana nayo.Kuachwa kwa misamiati hiyo hutokana na mabadiliko ya

kijamii yanayotokea. Msamiati unapobadilika ule wa awali husababisha kuachwa

kwa methali hiyo. Kwa maana hiyo, methali zote zenye misamiati ya zamani,

ambayo sasa haitumiki tena ipo hatarini kuachwa. Kuachwa huko hutokana na

76

kutokidhi mahitaji ya jamiiya Wazanzibari iliyopo sasa ambapo kwa mujibu wa

msingi wa kwanza wa nadharia ya uamilifu imebainika kuwa methali hizo hazikidhi

mahitaji ya jamii ya Wazanzibari kwa upande wa misamiati yake, ingawa kwa

upande wa dhima zake kwa jamii bado zinakidhi matakwa ya jamii hiyo.

4.3.3 Kuwapo kwa Methali Nyingi Mpya

Utafiti ulibaini pia kuwa hivi sasa kuna methali nyingi za Kiswahili. Hali hii ni

tofauti kidogo na hapo zamani, bila shaka wingi huu umetokana na kujumuika kwa

methali zilizorithiwa tokea zama za mababu, na zile zilizobuniwa baadae na

zinazoendelea kubuniwa hadi leo. Hali zinaonesha kuwa mpaka miaka ya sitini na

sabiini, methali zilikuwa kwa mamia. Vitabu vingi vilivyotungwa muda huo

vilivyokusanya methali, idadi ya methali ilikuwa ni kati ya mia moja hadi mia sita.

Kwa mfano, Farsy (1979) amekusanya methali mia tano na ishirini.Bali miaka ya

thamanini hadi sasa methali ni kwa maelfu. Mfano ni Kamusi la Methali

lililoandikwa na King‟ei na Ndalu, toleo la kwanza la (1989) lilikuwa na methali

zaidi ya elfu moja na mia tano, lakini katika toleo jipya la miaka ya elfu mbili, lina

methali zaidi ya elfu mbili na mia tano.Akithibitisha wingi huu wa methali,

Mtesigwa (1989) ameeleza kuwalugha za binadamu zina utajiri mkubwa wa methali,

lakini utajiri huu umezagaa na kupindukia katika lugha za kiafrika, hususan katika

eneo la lugha za Kibantu (Kikiwemo Kiswahili) Kusini mwa Ikweta, na pia za Ki-

Negro huko Afrika Magharibi.(Uk. 2-5).

77

Wingi huu wa methali uliopo hivi sasa, unatokana na kukusanyika baina ya zile za

kale zilizopatikana kwa njia za kurithishana na zile zinazoendelea kubuniwa hadi

sasa. Hivyo, methali nyingi hazikuwepo kale, lakini zile zilizoanzia huko kale bado

zipo zinaendelea kuwepo hadi hii leo. Katika hali ya kawaida ni vigumu jamii

kuweza kuzitumia methali zote hizo wakati mmoja. Hii ni kwa sababu methali

hutumika kwa mujibu wa miktadha maalumu. Na ukweli ni kwamba, kutokana na

wingi huo, muktadha mmoja utakuwa na methali nyingi za kuweza kutumika.Jambo

hili litasababisha baadhi yake zitumike zaidi, nyengine kwa wastani, nyengine kwa

nadra sana, lakini nyengine zisikumbukwe kabisa. Kwa mfano methali ya kale

kabisa ni “Waraka ni nusu ya kuonana”. Katika mazingira ya zamani njia pekee ya

kuwasiliana na mtu aliyembali ni njia ya maandishi. Kwa kuwa maandishi hayo

hayakuwa na mfumo maalum yaliweza kuitwa „waraka‟. Masomo ya skuli

yalipoanza kukawa na kitu kinaitwa „barua‟ na hivyo methali ya “Barua ni nusu ya

kuonana” ikaibuliwa. Lakini sasa kutokana mabadiliko ya kijamii, methali ya

“Salamu ni nusu ya kuonana” imeibuliwa. Ingawa methali hizi ni tatu, lengo lake ni

moja. Hata hivyo, methali hii ya mwisho ina mawanda makubwa zaidi. Salamu

inakusanya ile ya waraka, barua, barua pepe, ujumbe mfupi wa simu. Kwa mujibu

wa msingi wa tatu wa nadharia iliotumika unaoangalia utendajikazi wa jukumu au

dhima ya kipandekazi hicho cha fasihi simulizi katika jamii, methalihiyo ndio

inyokidhi mahitaji ya jamii ya Wazanzibari zaidi kwa wakati huu ambao mambo

hayoyote yanapatikana katika jamii yao.Hii inasababisha kutumiwa methali hii zaidi

na kuachwa zile za awali zenye mawanda mafupi.

78

4.3.4Ukosefu wa Taasisi za Kuzihifadhi na Kuzirithisha Methali

Jambo lolote muhimu halina budi kushughulikiwa ili lipate kuimarika, na si kawaida

ya jambo hilo kudumu kutokana na umuhimu wake peke yake. Umuhimu wa lugha

unafahamika katika jamii, bali namna inavyostahiki kushughulikiwa ni jambo

linalotia mashaka. Ingawa serikali imeunda taasisi za kuishughulikia lugha ya

Kiswahili kwa ujumla wake, lakini hatudhani kama taasisi hizo zinawezeshwa

kuishughulikia lugha hiyo katika nyanja zake zote. Mifano ya taasisi hizo ni Baraza

la Kiswahili la Zanzibar (BAKIZA) na Taasisi ya Kiswahili na lugha za kigeni

(TAKILUKI). Yumkini ikaonekana eneo kama methali halijachukuliwa hatua yoyote

na taasisi hizo. Hiyo inatokana na taasisi hizo kutowezeshwa kifedha na kitaaluma.

Mbali na hizo, kunataasisi iliyorithiwa, ya wazee kukaa na watoto na wajukuu zao,

ambayo nayo kwa sasa imedhoofishwa na harakati za masomo ya kiskuli pamoja na

maendeleo ya habari na mawasiliano. Hivyo watoto na wazee wanakosa muda wa

kukaa pamoja kama ilivyokuwa hapo zamani. Baada ya taasisi hizo, hakuna taasisi

nyengine inayoshughulikia wigo huu wa methali za Kiswahili katika jamii ya

Wazanzibari.

Watafitiwa wengi wamelaumu kuwa mfumo wa elimu haukutilia nguvu masuala ya

ufundishaji wa taaluma kama hizi za lugha kwa kiwango cha kutosha kuifanya jamii

kuona umuhimu wa kutunza na kutumia rasilimali lugha kama methali. Katika

kubainisha manung‟uniko yake Bwana Juma Saadati Haji7 anasema taasisi hizo

kama zingelishughulikia suala hilo, ingelionekana kazi ya methali angalau moja

7 Mahojiano baina ya mtafiti na Bwana Juma Saadati yalifanyika 24/3/2015 huko nyumbani kwake mtaa

wa Kikwajuni juu.

79

kama kitabu kikawa kinanunuliwa na watu wakawa wanazisoma. Dai hili

limethibitishwa na ndugu Amur8 ambaye amesema:

Ni kweli BAKIZA mpaka sasa haijatayarisha kazi rasmi kama hiyo.

Hii imesababishwa na changamoto nyingi. Moja ni kwamba

BAKIZA ina majukumu mengi. Kazi za uhariri wa ripoti

mbalimbali za serikali na mashirika, utunzi na uhariri wa vitabu

mbalimbali. Changamoto nyengine ni ya uchache wa wataalamu

ambao majukumu ni mengi. Kwa upande mwengine ni ukosefu wa

fedha za kutosha kukidhi mahitaji yote hayo. Hata hivyo, katika

Kamusi la Kiwahili fasaha BAKIZA imeweka baadhi ya methali

kadhaa za Kiswahili mwishoni. Hii ni kuonesha umuhimu wake na

nia ya kulishughulikia suala hilo kwa umuhimu wa kipekee hapo

baadaye.

Pia, kutokana na maoni ya watafitiwa, umuhimu wa mambo mengi huoneshwa kwa

kutiliwa mkazo katika mifumo ya utoaji wa elimu, na hivyo jambo ambalo mfumo

wa elimu haukulitilia mkazo hubakia kama ni jambo lisilo na umuhimu mkubwa

kwa jamii. Miongoni mwa mambo ambayo jamii inaona hayakutiliwa mkazo ni

methali. Baadhi ya maelezo ya watafitiwa wanaounga mkono hoja hii ni:

Methali hazitiliwi nguvu na mfumo wa elimu, Methali hazisisitizwi

matumizi yake katika taasisi za elimu, Kutokuwepo sera ya serikali

juu ya matumizi ya methali, Kuwepo kwa elimu rasmi ya

mashuleni, Kuibuka kwa wasomi wengi wa kisasa.9

4.4 Athari za Kuachwa kwa Baadhi ya Methali za Kiswahili

Katika kuchunguza athari zinazoikabili jamii kutokana na hali hiyo, utafiti

umegundua kuwa zipo athari chanya zenye kuleta tija naathari hasi zinazoleta

8 Ndugu Amur Salum ambaye ni Afisa wa BAKIZA aliyasema hayo katika mahojiano yake na mtafiti tarehe

14/4/2015. 9 Maelezo hayo wameyatowa Watafitiwa katika dodoso na mahojiano katika kujibu suali la sababu za

kuachwa methali hizo.

80

madharakwa jamii. Data zilizolenga kupata athari zilikusanywa kupitia njia

zilizotajwa hapo juu ambapo mtafitiwa alitakiwa kutaja athari anazozijua.

Watafitiwa walitoa athari nyingi ambazo, katika uchambuzi athari zinazolingana

ziliwekwa kundi moja. Hatua hiyo ilizikusanya athari hizo katika makundi manane,

baada ya kuondolewa zile zilizoonekana kuwa sio athari za msingi katika utafiti huu.

Katika makundi manane ya athari hizo, baada ya uchunguzi wa kina makundi mawili

yalibainika kuhusiana na mengine mawili, ambayo baada ya kuunganishwa yalibakia

makundi matano ambayo nayo baada ya kuchanganuliwa mawili yalibainika kuwa ni

ya athari zenye tija na matatu yaliobakia ni ya athari zenye madhara kwa jamii.

4.4.1 Tija Zilizopatikana

Katika kuchunguza athari za tatizo hilo, watafitiwa walitakiwa kutaja athari

chanyawanazozifahamu. Hata hivyo, utafiti unaonesha kuwa tatizo hili kwa kiasi

kikubwa linakabiliwa na athari hasi zaidi kuliko chanya. Utafiti umebaini athari

chanya zifuatazo:

4.4.1.1 Kuondoka kwa Msamiati Mgumu (Usiotumika)

Kutokana na msingi wa tatu wa nadharia ya uamilifu inayoonesha utendajikazi wake

wa jukumu au dhima ya kipandekazi cha fasihi simulizi katika jamii.Msingi huu ndio

uliotumika katika katika kuzichambua athari zilizotolewa na watafitiwa. Utafiti

umebaini kuwa methali zimeachwa kutokana na kukosa utendajikazi wake

uliosababishwa na kuwa na misamiati ambayo jamii ya Wazanzibari kwa sasa

haiyatumii.

81

Baadhi ya methali zilizoachwa zina msamiati mgumu, na pengine kutokana na

ugumu wake huenda ikawa ndio sababu ya kuachwa kwake kama ilivyooneshwa

katika sehemu iliotaja sababu za kuachwa kutumiwa methali hizo. Kwa mfano,

maneno kama vile „humangiria‟, „Mkata‟ na „handingwandingwa‟ katika methali;

“Mkosa kitoweo humangiria”, “Mlilala handingwandingwa”; mwemacho haambiwi

tule” na “Mkata hana kinyongo”. Maneno haya, kwa sasa, jamii ya Wazanzibari

haiyatumii tena ambayo yanaonekanakuwa na ukakasi wa kuyatamka maneno hayo.

Kwa hiyo, miongoni mwa athari nzuri za tatizo hilo ni kuondoa katika lugha

msamiati mzito, mgumu au wenye ukakasi katika matamshi ya lugha ya Kiswahili.

4.4.1.2 Kuiruhusu Lugha Kulandana na Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia

Dhana iliyopo hapa ni kuwa kuachwa kwa baadhi tu ya methali ni katika mabadiliko

ya lugha. Mabadiliko haya huenda yakawa yanatoa mwanya wa ufanisi wa kuifanya

lugha iweze kuoana na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Hii ni kutokana na

kuingia kwa msamiati mpyaambao baadaye methali zitautumia. Si kila mabadiliko ni

mabaya, bali inategemea mabadiliko yenyewe yanavyokuja. Bila shaka kutokea kwa

mabadiliko yanayoruhusu mambo yanayohusu maendeleo ya kisasa yanayotokana na

sayansi na teknolojia, jamii itayapokea kwa mikono miwili kwa vile hakuna jamii

isiyopenda kuendelea.

Watafitiwa walioiibua athari hii walitoa maelezo yafuatayo; Kukuza maendeleo ya

sayansi na teknolojia katika lugha, Kuwaruhusu watu kupata methali mpya

zinazoendana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, Kwenda sambamba na

82

maendeleo ya sayansi na teknolojia. Hoja hii ingawa imeibuliwa na watafitiwa

wachache, lakini mtafiti anakubaliana nayo. Hata hivyo, mabadiliko hayo yakiwa ni

kinyume chake, hali haitakuwa ya ufanisi na hivyo kuwa ni athari mbaya kwa

jamii.Kwa ujumlautafiti umebaini athari hizi zifuatazo:

4.4.2 Madhara yanayopatikana

4.4.2.1Kufifia kwa Utamaduni wa Wazanzibari

Methali za Kiswahili zimebeba mambo mengi sana ya mila, desturi, maadili na ya

kitamaduni. Aidha, methali hubeba hekima na falsafa ya hali ya juu ambazo kwa

kawaida huwa hazipatikani katika lugha ya kawaida. Kila methali hutoa sehemu ya

hekima, falsafa, mila, desturi, maadili na jambo la kitamaduni.Kwa mfano methali

isemayo; “Kikuu kuu pachika, kitakufaa masika”, ina ujumbe na hekima kuhusu

kutodharau kilichotumika baada kupatikana kingine. Ndani yakemna utamaduni wa

Kiswahili wa kuwa na sehemu za kupachika vitu kama pakacha, vikapu au mikoba

katika mapaa ya nyumba. Hii ni falsafa ya kujiwekea akiba hata kwa vitu

vilivyotumiwa, kwani haijulikanini kipi kitakachomfaa mtu wakati wa dhiki kama

kipindi cha masika. Kwa hiyo, ni wazi kuwa methali zinapoachwa kutumiwa, huwa

sehemu hiyo ya utamaduni unaoelezewa katika methali hizo huwa hatarini kupotea.

Wakisisitiza hilo, baadhi ya watafitiwa:

Zitasahaulika na hivyo kupotea kwa utamaduni, Baadhi ya mila na

desturi za waswahili zitapotea, Kutoweka kwa hadhi ya utamaduni

wa waswahili, Kupotea kwa baadhi ya mila, desturi na silka za

waswahili, kupotea kwa miiko ya kimazungumzo iliyoachwa na

83

wazee wetu wa asili, Kuchangia kuporomoka kwa madili ya jamii,

na Jamii itakosa maadili na busara10

.

4.4.2.2Jamii Kuzikosa Adili za Methali

Mbali na falsafa, hekima, maadili, mila, na desturi zinazopatikana katika methali,

kwa upande mwengine, methali hutoa ujumbe na mafunzo maalum kwa jamii.

Mafunzo hayo huweza kuwa ya kukanya, kuasa, kushajihisha, kuadilisha. Kila

methali huwa na funzo au mafunzo yake muhimu ambayo jamii huyatumia katika

harakati zao za maisha, na hivyo jamii isipozitumia methali hizo, athari yake

kuyakosa mafunzo hayo vilevile.Kuhusu ukweli kuwa methali zina mafunzo mengi,

Farsy anelezea kwa kusema kuwa Methali zafaa sana kwa mafundisho ya adili (za

jamii), kwa hiyo ni jambo la muhimu kwa waalimu kujua methali nyingi kama

inavyowezekana, na kuzitumia sana katika mafundisho yao.” (Farsy, 1958)Naye

Mulokozi katika kulithibitisha hilo, amesema:“Kutokana na ufupi na usanii wake,

methali huweza kutoa mafunzo au maonyo kwa mafanikio zaidi kuliko maelezo ya

kawaida”.(2000:36). Hoja hii pia imetolewa na wafitiwa kadhaa akiwemo Bi.

Sabra.11

Baadhi ya watafitiwa hao wanasema:

Watu kutopata mafunzo yanayohusiana na methali hizo, Kukusa

maneno ya hekima kwa kizazi kipya, Kukosa baadhi ya mafunzo

yanayopatikana ndani yake, Athariya jamii ni kutopata kuelimika

kupitia methali hizo, Athari ya jamii kutopata kuonywa na

kushauriwa, Jamii itapotoka kwa kukosa mafunzo ya methali za

kizamani zinazoachwa, na Kuwa na jamii isiyojali mafunzo mema

ya wazee wa kale.

10

Maelezo hayo wameyatoa watafitiwa kupitia dodoso na kuthibitishwa Afisa wa BAKIZA Bw. Rashid

Abdu Rai katika mahojiano yake na Mtafiti yalifanyika tarehe 14/4/2015 hapo Ofisini kwake. 11

Maelezo hayo wameyatoa watafitiwa katika dodoso na kuthibitishwa na Bibi Sabra Mohamed,

mwalimu wa somo la Kiswahili skuli ya sekondari ya Mwanakwerekwe.

84

Adili za jamii yoyote ni pamoja na masuala mazima ya historia inayoihusu jamii hiyo.

Kwa muda wote methali pia hutumika kama chombo cha kuhifadhia mambo kemkem ya

jamii. Miongoni mwa hayo ni utamaduni na historia ya jamii husika. Mambo kadhaa ya

kitamaduni na kihistoria katika jamii yanapatikana kupitia methali pamoja na tanzu

nyengine za fasihi simulizi. Msuya anasema:

Kwa hiyo ni chombo cha kuelezea na kuitazamia jamii

kiutamaduni, kiuchumi, kisiasa na kadhalika… Misemo yao

huwa kioo cha kuwatazamia kwa jumla, ikiwa kisiasa,

kiutamaduni, kiuchumi, kihistoria na kadhalika. Misemo hiyo

imejaa hekima na falsafa ya juu kwa sababu ilitumika pindi

walipotaka kuwaadibu wadogo au kuwatanabahisha wakubwa.

(Msuya, 1979: 7-11).

Ni kweli methali nyingi zimebeba mambo ya kihistoria katika jamii.Baadhi ya

methali huwa ni ufupisho wa matukio hayo ya kihitoria yaliyotokea katika jamii

hapo zamani.Mulokozi(2000) anasema kuwa baadhi ya methali huwa ni

vielelezo au vifupisho vya hadithi fulani inayofahamika vizuri kwa jamii. hoja

iliotolewa na zaidi ya watafitiwa saba. Baadhi ya maelezo yao ni; Kutoweka kwa

sehemu ya historia ya jamii, Kupotea kwa uhalisia wa jamii ya waswahili,

Kupoteza uhalisia wa waswahili katika jamii, Kupotea historia ya waswahili,

Kusahau na Kudharau kabisa ugumu walioupata wahenga, na Kutokujua asili na

walipotokea kizazi cha sasa hivi.Kwa hivyo, methali hizo zisipotumika sehemu

ya historia ilizozibeba zitakuwa hatarini kupotea.

4.4.2.3 Jamii Kukosa Burudani Inayotokana na Methali hizo

Fasihi yoyote pamoja na kutoa mafunzo, ina dhima au jukumu kubwa la

kuiburudisha na kustarehesha jamii. Methali ikiwa ni sehemu muhimu ya

85

fasihisimulizi pia infanya kazi hiyo ya fasihi. Njogu na wenzake wanalieleza

jukumu hilo kwa kusema kuwa Katika jamii zote fasihi simulizi imetumiwa

kuwasilisha maadili na mafungu kemkem kuhusu jamii husika. Pia, imetumika ili

kustarehesha na kuburudisha kwa namna inavyotumia lugha, uigizaji, utendaji,

taharuki na mbinu mbalimbali za simulizi.Methali huleta burudani kwa kule

kutumia tamathali za semi kwa wingi. Mulokozi anasema kuwa mara nyingi

mawazo na falsafa ya methali huelezwa kwa kutumia tamathali, hasa sitiari, na

mafumbo. Uzuri ulioje ni kuwa tamathali zinazotumiwa na methali hutokana na

mazingira halisi ya kijamii na kimaumbile ya watumiaji wa lugha inayohusika.

Kwa hivyo, mambo hayo, yakiunganishwa na ufundi wa uteuzi wa maneno na

mpangilio wake, huzifanya methali hasa zinapotumika katika miktadha sahihi,

ziwe ni burudani tosha kwa jamii. Hili linathibitishwa zaidi na matukio halisi ya

wanajamii kujibizana wao kwa wao kwa kutumi methali tupu katika

mazungumzo yao ya kutaniana.

Baadhi ya maelezo waliyoyatoa watafitiwa walioiibua hoja hii ni; Jamii kukosa

kuburudika kutokana na methali hizo, Jamii kutopata kuburudika kwa methali

hizo, na kukosa raha ya mazungumzo wanayoipata jamii kutokana na methali

hizo. Ingawa watafitiwa walioiibua ni wachache, lakini kutokana na nguvu ya

hoja yake, mtafiti anakubaliana nayo kuwa ni miongoni mwa athari mbaya

zinazoikabili jamii kutokana na tatizo hilo. Kwa jumla, kwa mujibu wa

watafitiwa, jamii inonekana kuathirika vibaya kwa kutotumika baadhi ya methali

hizo kwa athari hizo zilizojadiliwa hapo ambazo moja ni kupotea kwa sehemu ya

Mila, Desturi, Maadili na Utamaduni wa Waswahili. Pili ni Kukosa Mafunzo

86

yanayopatikana kutokana na Methali hizo. Tatu nikupotea kwa sehemu ya

historia ya waswahili. Na nne ni;Jamii kukosa burudani inayotokana na methali

hizo. Athari nne hizi zimekubalika kikamilifu na mtafiti. Watafitiwa pia

wameibua hoja nyengine mbili zinazoipata jamii kwa tatizo hilo. Hoja hizo moja

niKuvunjika kwa Uhusiano na Mafahamiano ya Kijamii kama Ilivyokua Zamani,

na hoja pili ni Kuibuka kwa uoni mbaya kwa baadhi ya wanajamii kuwa methali

zimepitiwa na wakati. Ingawa hoja mbili hizi mtafiti anaziona haziakisi moja

kwa moja na tatizo linalojadiliwa katika utafiti huu.

4.5 Muhutasari wa Sura ya Nne

Sura hiiimejadili matokeo ya utafiti. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwakuna

methali kadhaa za Kiswahili ambazo jamii ya Wazanzibari imeshaziacha. Aidha,

utafiti umeonesha pia kuwa, matumizi ya methali katika jamii hiyo, yamegawanywa

katika makundi manne. Makundi hayo ni ya methalimashuhurizinazotumika mara

kwa mara, methali za wastani zinazotumika kwa wastani katika jamii, methaliza

nadra zinazotumika mara moja moja,na methali ambazo tayari zimeshaachwa

kutumiwa na jamii.

Matokeo yamebaini kuwa ziko sababu kadhaa zinazosababisha kuachwa kwa

methali hizo.Sababu hizo nikutokuwepo taasisi za kuzihifadhi na kuzirithisha

methali, mvuvumko wa Maendeleo ya sayansi na teknolojia, mabadiliko ya msamiati

usiotumikasasa katika methali hizo, na Kuibuka kwa methali nyingi mpya

zinazotumika sasa.

87

Kwa upande wa athariutafiti umebaini kuwepo kwa athari chanya na hasi kwa jamii.

atharichanya za kuachwa kwa methali hizo nikuondoka kwa msamiati usiotumika

kwa sasa, na nyengine nikuiruhusu lugha ya Kiswahili kwenda sambamba na

maendeleo ya sayansi na teknolojia.Athari hasi kwa jamii ni kufifia kwa utamaduni

wa Wazanzibari, jamii kuzikosa adili za methali hizo,na jamii kukosa burudani

inayotokana na methali hizo.

88

SURA YA TANO

MUHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO

5.1 Utangulizi

Sura hii inawasilisha muhutasari wa tasnifu. Sura ina sehemu nne. Sehemu ya

kwanza inazungumzia juu ya muhtasari wa tasnifu. Sehemu ya pili ni utoshelevu wa

nadharia. Sehemu ya tatu inahusu mchango mpya wa utafiti huu. Na sehemu ya nne

ni maoni na mapendekezo.

5.2 Muhutasari wa Tasnifu

Kwa ujumla, tasnifu hii iliangalia juu ya sababu na athari za kuachwa kwa baadhi ya

methali za Kiswahili katika matumizi ya jamii ya waswahili Zanzibar. Tasnifu hii,

imegawiwa katika sura tano.Sura ya Kwanza ilianzia kwa usuli wa mada, tamko la

utafiti, lililofuatiwa na malengo ya utafiti. Sura hiyo pia imebainisha maswali,

umuhimu na mipaka ya utafiti pamoja na nadharia iliyotumika katika ukusanyaji na

uchambuzi wa data.

Sura ya Pili imezungumzia juu ya mapitio ya maandiko. Mtafiti alipitia vitabu,

majarida, na hata baadhi ya tovuti, zilizomuwezesha kupata maelezo yanayohitajika

kuhusiana na mada ya utafiti. Maelezo yalioelezwa katika sura hii yanahusu fasihi

simulizi na umuhimu wake, semi za Kiswahili, na methali za Kiswahili. Ndani yake

mlioneshwa namna wataalamu walivyozama katika kuzitolea maana na asili ya kila

kimoja kati ya fasihi simulizi, semi na methali, pia katika kuonesha umuhimu wake

89

na matumizi ya kila kimoja. Mwisho wa sehemu hiyo imeoneshwa mapengo ya

kiutafiti yaliojitokeza kutokana na mapitio hayo.Sura ya tatu, imeeleza mbinu na njia

mbali mbali zilizotumiwa katika utafiti huu. Vile vile sura imeeleza eneo na

mawanda ya utafiti, na pia jamii ya watafitiwa. Sura imeonesha pia juu ya umakinifu

wa mbinu na vifaa vilivyotumika katika ukusanyaji wa data.

Sura ya Nne imeonesha namna data hizo zilivyochambuliwa na kutafsiriwa. Data

zilichambuliwa kwa kutumia mkabala wa kifafanuzi. Pia, utafiti ulilazimika

kuonesha hali halisi ya kijamii ambayo kwa kiasi kikubwa imekwenda sambamba na

ubunifu wa utafiti wenyewe. Uchambuzi uliongozwa na malengo ya utafiti pamoja

na maswali yake kama yalivyooneshwa katika sura ya kwanza. Kutokana na

malengo na maswali hayo, mtafiti alipata nafasi ya kutumia maswali yaliokuwemo

katika mbinu za dodoso, mahojiano na mjadala wa kikundi. Kwa ujumla uchambuzi

huo ulifanikiwa kwa vile uliweza kutoa matokeo yaliolingana na mabunio ya utafiti

huu.

Sura ya tano ni hii inayowasilisha muhutasari wa tasnifu ya utafiti, utoshelevu wa

nadharia iliotumika katika utafiti, mchango mpya wa utafiti pamoja na maoni na

mapendekezo yaliotokana na utafiti yanayopaswa kufanyiwa kazi kwa siku zijazo au

katika tafiti zijazo.

90

5.3 Utoshelevu wa Nadharia Iliyotumika

Kutokana na misingi ya nadharia hii, mtafiti aliweza kuzieleza methali za Kiswahili,

na kuonesha umuhimu wake na matumizi yake kama ni kipandekazi cha fasihi

simulizi ya Kiswahili katika utamaduni wa jamii ya Wazanzibari. Aidha, mtafiti

alionesha hali ya uendelezwaji wa kipandekazi hicho na kugundua kuwa si nzuri

kulingana na hadhi na umuhimu wa methali za Kiswahili katika jamii. Vilevile,

mtafiti alionyesha jukumu na dhima ya methali za Kiswahili katika jamii ya

Wazanzibari. Mbali na kuzingatia misingi hiyo, mtafiti pia alikwenda sambamba na

hatua zilizopendekezwa katika kuifanyia kazi nadharia hii ya umilifu. Hivyo, alianza

kuuchunguza utamaduni wa Waswahili wanaoishi Zanzibar na uhusiano wao na

matumizi ya methali.Baadaye alizitafiti methali za Kiswahili na namna

zinavyotumiwa katika jamii hiyo. Vilevile,zilelezewa methali hizo namna ya

kutumika kwake kama chombonakama sehemu ya utamaduniwaWaswahilina

kiwango kinachotumika, kulingana na mahitaji ya jamii yao. Na mwisho ni kuzieleza

methali hizo namna zinavyotendakazi katika jamii hiyo.

Kwa kutumia misingi na hatua hizo, utafiti huu umefanikiwa kwa kiwango kizuri.

Kwani kwa kuangalia kwa undani juu ya utamaduni wa waswahili wa Zanzibar, na

kwa kuziangalia kwa kina methali za Kiswahili na matumizi yake katika jamii,

hatimae imewezekana kugundua methali ambazo kwa sasa jamii haizitumii. Na pia

kugundua sababu na athari za kuachwa kutumiwa kwa methali hizo. Hivyo, nadharia

hii ya uamilifu, imeweza kukidhi haja ya utafiti huu.

91

5.4 Mchango Mpya wa Utafiti

Utafiti umeibua mambo mapya kuhusu methali, ambayo hapo kabla hayakuwa

yakifahamika. Moja ni kwamba methali ni utanzu maarufu wa fasihi simulizi na

zinashuhudiwa zikitumika kila siku na kila sehemu, lakini haikufahamika kuwa

matumizi ya methali huwa yanapita katika mikondo minne. Pili, sababu zinazo

sababisha methali kuachwa kutumiwa, na tatu ni athari za hali hiyo kwa jamii.Hayo

yote ni miongoni mwa mchango mpya wa utafiti huu katika fasihi ya Kiswahili na

hasa fasihi simulizi ya Kiswahili.

5.5 Maoni na Mapendekezo ya Mtafiti

Azma kuu ya utafiti huu ilikuwa ni kuchunguza sababu na athari ya kuachwa kwa

baadhi ya methali za Kiswahili katika jamii ya Waswahili. Matokeo yameonesha

kuwapo kwa tatizo hilo, sababu na athari zake kama zilivyoelezwa katika sura

iliyopita. Pamoja na hali hiyo, utafiti umegundua baadhi ya mianya inayohitaji

kuzibwa, ili kuziimarisha methali za Kiswahili. Miongoni mwa maeneo hayo

Kwanza, ni athari za utandawazi katika methali za Kiswahili. Pili, ni matumizi ya

methali kwa kuzingatia miktadha zinamotumiwa. Tatu, ni athari ya maendeleo ya

sayansi na teknolojia katika methali za Kiswahili. Hivyo, mtafiti anapendekeza

kufanyika tafiti nyengine katika maeneo hayo ili kuhakikisha kuwa methali za

Kiswahili zinaimarika katika matumizi ndani ya jamii ya Waswahili Zanzibar.

Kwa upande wa mapendekezo, mtafiti anapendekeza Kwanza, kwa Jamii yenyewe

kuona umuhimu wa kutumia methali zao katika mazungumzo yao mbalimbali kwani

92

watafaidika na ladha yake na kuepukana na karaha ya kutumia maneno makavu kwa

nyakati nyingi zaidi. Aidha, Wazee ni jukumu lao kuendeleza mwenendo wa kukaa

na vijana wao kwa lengo la kuwaidilisha na kuwaburudisha kwa mazungumzo

yaliyokolezwa kwa matumizi ya methali ili wajifunze lugha njema na pia urithi wa

methali uweze kuendelezwa. Pili, mtafiti anapendekeza kwa Wizara ya Elimu na

Mafunzo ya Amali Zanzibar, kuuruhusu muhutasari kulitanua somo la Kiswahili

katika mawanda ya semi, hasa methali, ili vijana waweze kufunzwa kwa kiwango

cha kuwawezesha kuzihifadhi na kuzitumia kwa usahihi kama walivyopendekeza

wahojiwa wengi miongoni mwa wanafunzi na wataalamu katika maoni yao.

Tatu, mtafiti anapendekeza kwa Serikali kuanzisha kitengo maalumu katika vyombo

vyake vinavyohusika na lugha ya Kiswahili kitakachozisimamia methali na semi za

Kiswahili kwa ujumla katika kuzikusanya, kuzihifadhi, kuzitafsiri kwa lugha mbali

mbali, na kuzisambaza kupitia vitabu nje na ndani ya nchi.Kwa kufanya hivyo,

kutaonesha umuhimu wa kutunzwa na kutumiwa na jamii na hivyo, jamii kuweza

kuzienzi na kuzitumia ipasavyo, jambo litakaloziimarisha na kuikuza fasihi simulizi

na lugha ya Kiswahili kwa ujumla. Mwisho, mtafiti anapendekeza kwa Waandishi na

Wasanii kuzitumia ipasavyo methali za Kiswahili katika kazi zao za fasihi andishi.

Kufanya hivyo, ni njia nyengine muhimu ya kuzihifadhi methali, kufupisha maneno

na kutanua ujumbe pamoja na kuzikoleza kazi zao, kama walivyokuwa wakifanya

waandishi wa zamani, mfano, Shaaban Robert, Saidi Mohamed, Said Ahmed na

wengineo, ambao kazi zao zinavutia hadi leo hii na haziishi hamu kuzisoma.

93

MAREJELEO

Abudu, M. (1978), Methali za Kiswahili, Shungwaya, Nairobi.

Abudu, M. na Baruwa, A. (1981), Methali za Kiswahili, Kitabu cha Pili na Tatu,

Shungwaya Publishers, Nairobi.

Balisidia, M.L. (1987), Tanzu na Fani za Fasihi Simulizi, Katika Mulika Na. 19, uk.

2-9.

Bukenye, A.S, nw (1997), Oral Literature: A Senior Course, Nairobi Longhorns

Publishers.

Chiraghdin, S. (1990), Kiswahili na Wenyewe. Kiswahili 44:01.

Chuachua, R. (2008), Uingizaji wa Methali Katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu,

TUKI, Dar es Salaam.

Farsy, S.S. (1979), Swahili Sayngs, Nairobi East African Literature Bureau.

Ferster, J. (2005),Arguing Through Literature, A Thematic Anthology And Guide to

Academic Writing, McGraw-Hill Companies, New York.

Finnegan, R. (1979), Oral Literature in Africa, Great Britain, Oxford University

Press.

Haji, A.I. (1992), Fasihi, Katika Misingi ya Uhakiki wa Fasihi, TAKILUKI,

Zanzibar.

Haji, M.O. (2006), Vipera vya Fasihi simulizi: Kidato cha 1-4, Zanzibar.

94

Hassan, A. U. (2013), Dhima ya Methali Katika Kudumisha Maadili Katika Jamii ya

Wapemba, Tasnifu kwa Ajili ya Shahada ya Pili, Chuo Kikuu cha Dodoma.

Ireri Mbaabu, (1985) Utamaduni wa Waswahili, Kenya publishing & Book

Marketing Co. Ltd. Nairobi.

Khamis, S.A. (1983), Nafasi ya Fasihi Simulizi katika Jamii ya Kitanzania, Mulika,

Na. 15, uk. 3-13.

King‟ei, K. na Ndalu, A. (1998), Kamusi ya Methali: Toleo Jipya, East African

Publishers, Nairobi. Dar es Salaam. Kampala.

Madumulla, J. S. (1995), Proverbs and Sayngs: Theory and Practice, TUKI, Dar es

Salaam.

Madumulla, J.S. (2009), Riwaya ya Kiswahili: Nadharia, Historia na Nadharia ya

Uchambuzi, Phoenix Publishers Ltd. Nairobi, Kenya.

Mauya, A. B. (2006), Semi: Maana na Matumizi, TUKI, Dar es Salaam.

Mbarouk, S.S. (2011), Athari za Semi za Kanga Katika Jamii, Tasnifu kwa Ajili ya

Shahada ya Pili, Chuo Kikuu cha Dodoma.

Mduda, F na John, J (2011), Kiswahili kidato cha tano na sita, Oxford University

Press, Dar es Salam.

Mgulu, H.A. (2011), Usanaa Katika Methali za Kisambaa (SHIMO), Tasnifu kwa

Ajili ya Shahada ya Pili, Chuo Kikuu cha Dodoma.

95

Mhilu, G.G. nw (2011), Kiswahili kwa Shuleza Sekondari Kidato cha tatunanne,

Nyambari Nyangwine Publisher, Dar es Salam.

Mieder, W. (1978), The Use of Proverbs in Psychological Testing, Journal of

theForklore Institute, Na. 15, uk. 45-55.

Mlacha, S.A.K. (1981), Methali Kama Chombo Muhimu katika Jamii, Mada ya

Semina, TUKI, Dar es Salaam.

Mlacha, S.A.K. na Hurskeinein, A. (1996), Lugha, Utamaduni na Fasihi Simulizi

yaKiswahili, TUKI, Dar es Salaam.

Mlacha, S.A.K.(1995), Fasihi Simulizi na Usuli wa Historia ya Pemba, TUKI, Chuo

Kikuu cha Dar es salaam.

Mohamed, S.A naVuzo, A. C (1991),Stadi za Kiswahili, Kidato cha tatu,Oxford

University Press, Nairobi.

Mohamed, S.A. & Ali, A. M. (1981), Hapa na Pale: Tungo za Sanaa, TAKILUKI,

Zanzibar.

Msuya, P.K. (1997), Fasihi na Methali, Mulika, Na. 9, TUKI, Dar es Salaam.

Msuya, Sh. K. (1979), Yatokanayo na Fasihi Simulizi, Tanzania Publishing House,

Dar es Salaam.

Mtesigwa, P.C.K. (1989), Methali ni nini? Jarida la Uchunguzi la Taasisi

yaKiswahili, Na. 56, uk.1-9.

Mulokozi, M.M. (1989), Tanzu za Faihi Simulizi, Katika Mulika, Na. 21, uk. 1-19.

96

Mulokozi (1996), Fasihi ya Kiswahili: Utanguli wa Fasihi ya Kiswahili, Chuo

Kikuu Huria cha Tanzania, TUKI Chuo Kikuu cha Dar es salaam.

Mutembei, A.K. (2006), “Nadharia ya Fasihi Simulizi na Maendeleo katika Sayansi

na Teknolojia”, Mulika, Na. 27, uk. 1-17.

Mzee, H. A. (1977), "Utamaduni, matumizi na misingi ya lugha ya Kiswahili",

MULIKA 11, Uk. 10.

Naaman, R.M. (1983), Methali na vitendawili, TAKILUKI, Tanzania Publishing

House, Dar es Salam.

Ndaro, J. N. (2012), Fani katika Methali za Kidigo,Tasnifu kwa Ajili ya Shahada ya

Pili, Chuo Kikuu cha Dodoma.

Ndugo, C.M. & Wafula, B.M. (1993), Tanzu za Fasihi Simulizi, University of

Nairobi, Nairobi.

Ngole, S.Y.A. & Lukas, N.H. (2002), Fasihi Simulizi ya Mtanzania, Kitabu cha pili,

TUKI, Dar es Salaam.

Njogu, K. & Chimerah, R. (1999), Ufundishaji wa Fasihi: Nadharia na Mbinu, Jomo

Kenyata Foundation, Kenya.

Njogu, K. nw (2001), Tanzu za lugha: Kitabu cha Wanafunzi, Jomo Kenyata

Foundation, Nairobi Kenya.

Nkwera, F.V. (ht), Tamrini za Fasihi, Commercial Printing, Co, Ltd, Dar es Salaam.

Ohly, R. (1981), Formula- Tungo ya Methali katika Kiswahili, TPH, Dar es Salaam.

97

Omar, C.K. & Mvungi, T. (1981), Urithi wa Utamaduni Wetu, Dar es salaam,

Tanzania.

Omar, C.K. (1976), Misemo na Methali Kutoka Tanzania, East Africa Literature

Bureau, Nairobi.

Othman, S. Y. na Abdulkarim, Y. (2015) Howani Mwana Howani: Tenzi za Zainab

Himid Mohammed, TUKI Dar-es-salaam.

Rashid, A.M. (1992), Semi, Katika Misingi ya Uhakiki wa Fasihi, TAKILUKI,

Zanzibar.

Reddy, G.S. and Anuradha, R. V. (2008), “PrimeKiswahili Proverbs, Origins,

Explanations, Examples”. Neelkamal Publications Pvt.Ltd, NewDelhi, India.

Salum, Z. A. (2007), “Changamoto juu ya Ufundishaji Fasihi Simulizi Katika Skuli

za Sekondari”: Kidato cha Nne Katika Enzi ya Utandawazi Zanzibar, Tasnifu

Shahada ya Kwanza, SUZA.

Senkoro, F. E.M.K. (2011),Fasihi, KAUTTO, Limited.

Shariff, I.N. (1988), Tungo Zetu. Trenton: The Red Sea Press, Inc.

Simchimba, E.A. (2012), Falsafa ya Ki-Afrika Katika Methali za Kiswahili,

Tasnifukwa Ajili ya Shahada ya Pili, Chuo Kikuu cha Dodoma.

Suleiman, M.S. (2009), A drop of Honey (Tone la Asali) Swahili- Eng. Language,

Express Printing Services.

98

Sengo, T.S.Y. (1985), “The Indian Ocean Complex and the Kiswahili folklore: The

case of Zanzibarian Tale-Performance”, Unpublished Ph.D Thesis. Khartoum

University.

TAKILUKI, (1981), Misingi ya Nadhariya ya Fasihi, Zanzibar.

TAKILUKI, (1992), Msingi ya uhakiki wa Fasihi kidato cha nne, EWW, Zanzibar.

Uledi, (2012), Muundo na Lugha katika Methali na Vitendawili kwa jamii ya

Wamakunduchi- Zanzibar, Tasnifu kwa Ajili ya Shahada ya Pili, Chuo Kikuu cha

Dodoma.

Wamitila, K.W. (2002), Uhakiki wa Fasihi: Misingi na Vipengele vyake, Phoenix

Publishers Ltd. Nairobi.

Wamitila, K.W. (2004), Kichocheo cha Fasihi Simulizi na Andishi. Focus,

Publications, Ltd.

99

VIAMBATISHO

A: Barua za Ithibati ya Kufanyia Utafiti

A1: Barua ya kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma

100

A2: Kibali cha Ruhusa ya Kufanyia Utafiti Zanzibar.

101

B: MIONGOZO YA USAILI, DODOSO NA UDURUSU WA MAKTABA

B1: Mwongozo wa Hojaji kwa Wataalamu na Wazee wenye uzoefu

Sehemu A: Maelezo Binafsi ya Mhojiwa

a) Jina la Mhojiwa …………………b) Umri …………. c) Jinsia ………….

(d ) Anapoishi …………………… e) Dhamana/Cheo/Hadhi ya Mhojiwa …………

f) Kiwango cha Elimu ……………………… Uzoefu alionao ……………………

g) Mahali, Tarehe na Muda yalipofanyika Mahojiano ……………………………

Sehemu B: Maelezo Yahusianayo na Utafiti

1. Tunafahamu nini kuhusu methali. Maana, umuhimu, na matumizi yake.

2. Tunafahamu nini kuhusu methali za Kiswahili zilizoachwa kutumiwa?

3. Methali za Kiswahili zinatumikaje hivi sasa katika Jamii ya Waswahili wa

Zanzibar?

4. Je kwa unavyoona, kuna tofauti yoyote ya matumizi baina ya sasa na zamani?

5. Kwa maoni yako, methani zina umuhimu gani kwa Jamii ya Waswahili wa Zanzibar

hivi sasa?

6. Kuna methali kadhaa zilizokuwa zikitumiwa zamani, lakini sasa zimeachwa

kutumiwa kabisa katika jamii ya Waswahili wa Zanzibar. Tunaweza kuzitaja baadhi ya

methali hizo tunazozikumbuka? (Kuonesha orodha ya methali zinazofikiriwa kuachwa).

7. Tunaweza kufikiria ni sababu zipi zinazosababisha kuachwa kutumika kwa

methali hizo?

8. Kuachwa kutumiwa kwa methali hizo kunaleta athari zipi zaidi kwa jamii ya

Waswahili?

9. Kwa maoni yako, unaona methali zilizoachwa ziendelee kuachwa au zirejeshwe

katika matumizi kama zamani?

AHSANTE SANA KWA MSAADA WAKO

102

B2: Mwongozo wa Usaili kwa Wanafunzi wa Sekondari na Diploma ya Kiswahili

A: MAELEZO KUHUSU DARASA LA WASHIRIKI

Darasa: ………………………………………………………………

Skuli/ Chuo: …………………………………………………………

Siku na Tarehe iliofanyika usaili: …………………………………….

Idadi ya washiriki: …………………………………………………….

B: MAELEZO KUHUSU UTAFITI

1. Tunazifahamu methali za Kiswahili?

2. Methali zinatumika vipi katika jamii yetu?

3. Methali zina umuhimu wa kutumiwa katika jamii?

4. Naomba tuzitaje methali tunazifahamu kwa mpango wa kialfabeti. (Mtafiti

atawagawia baadhi ya wanafunzi karatasi zenye methali alizozikusanya na

kuwaamuru wazitie alama zile zitakazotajwa na wanafunzi wenzao)

5. Naomba methali hizi nitakazozitaja sehemu yake ya mwnzo mzikamilishe

sehemu yake ya mwisho (Mtafiti ataziwekea alama ya vyema kila methali

iliyokamilishwa kwa usahihi na alama ya x kwa methali iliyokosewa au ambayo

haikuweza kutajwa).

6. Methali hizi zilizokushindeni kuzijua ni kwa kuwa hivi sasa hazitumiki.

Mnadhani kwa nini methali hili hivi sasa hazitumiki?

7. Ni zipi athari za kuachwa kwa methali hizi katika jamii yetu?

8. Nini kifanyike kuiepusha hali hiyo isiathiri athari mbaya kwa jamii?

AHSANTENI SANA KWA USHIRIKI WENU MZURI

103

B3: Mwongozo wa Dodoso kwa Wakufunzi na Vyuo na Watu wa Mitaani

Hojaji kwa ajili ya Wakufunzi na Wanafunzi wa Fasihi ya Kiswahili Vyuo vikuu

Utafiti huu ni kwa ajili ya kukamilisha masomo ya Shahada ya Uzamili, katika fani ya

Fasihi ya Kiswahili, inayochukuliwa katika Chuo Kikuu cha Dodoma, (UDOM). Mtafiti

anafanya utafiti kuhusu Methali za Kiswahili Zilizoachwa: Sababu na Athari zake kwa

Jamii. Kwa hivyo, unaombwa kutoa mchongo wako kwa kujaza dodoso hili kwa

ukamilifu na usahihi kadri unavyoelewa. Maelezo yote utakayoyatoa yatakuwa ni kwa

matumizi ya utafiti huu.

Sehemu A: Maelezo Binafsi ya Mtafitiwa

a) Jinsia; ….………….. (b) Umri …………. (c) Anapoishi …………………

a) Kiwango cha Elimu ………………… (e) Kazi anayofanya …………………

f) Dhamana/Cheo/Hadhi ya Mjazaji wa hojaji; ………………………………

Sehemu B: Maelezo Yahusianayo na Utafiti

1. Unafahamu nini kuhusu methali za Kiswahili?

……………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………………

2. Kwa sasa hivi methali zinatumika vipi zaidi katika jamii ya Waswahili?

……………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………………

3. Methali za Kiswahili zina umuhimu gani katika jamii ya Waswahili?

……………………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………………

4. Kuna methali kadhaa za Kiswahili zilizowahi kutumika hadi miaka ya tisiini, lakini

kwa sasa jamii haizitumii kabisa. Tafadhali zitaje methali unazozikumbuka wewe.

i) …………………………………………………………………………………

ii) …………………………………………………………………………………

iii) …………………………………………………………………………………

5. Miongoni mwa sababu za kuachwa kutumika kwa baadhi ya methali katika jamii ya

Waswahili wa Zanzibar ni hizi zifuatazo. Je unazikubali au unazikataa? (Weka alama ya

vyema kwa unazozikubali na alama ya x kwa unazozikataa)

104

NA. SABABU N/S

i Kwa sasa methali zimepitiwa na wakati katika matumizi.

ii Mvuvumko wa Maendeleo ya sayansi na teknolojia.

iii Kuibuka kwa methali nyingi mpya zinzotumika sasa.

iv Kwa kutumia misamiati mingi ambayo haitumiki kwa sasa.

v Mtindo wa maisha wa kuwepo na kutoweka kwa mambo.

vi Zinatumika lakini zimebadilishiwa misamiati yake ya asili.

vii Kutokana na Kuwepo methali nyingi sana hivi sasa.

viii Kutokuwepo taasisi za kuzihifadhi na kuzirithisha methali.

6. Unafikiria kuna sababu nyengine zaidi ya hizo? Tafadhali zitaje hapa chini

i) ……………………………………………………………………………….

ii) ………………………………………………………………………………..

iii) ……………………………………………………………………………….

7. Unadhani kuachwa kutumiwa kwa methali hizo katika jamii ya Waswahili kuna athari

njema, mbaya au zote? Jaza unapodhani ni sawa zaidi (Njema …. Mbaya … Zote….)

8. Tafadhali zitaje athari unazozifikiria wewe;

ATHARI NZURI:

i) ……………………………………………………………………………………

ii) ……………………………………………………………………………………

iii) ……………………………………………………………………………………

ATHARI MBAYA:

i) ……………………………………………………………………………………

ii) ……………………………………………………………………………………

iii) ……………………………………………………………………………………

9. Kwa maoni yako, unadhani kuna umuhimu wowote wa kuzihuisha na kuzihifadhi

methali za Kiswahili zilizoachwa katika jamii ya Waswahili? ..........................................

TUNAKUSHURU KWA MSAADA WAKO

105

B.4: Mwongozo wa Udurusu wa Maktaba

Vyanzo vya

kudurusiwa

Dondoo muhimu Lengo

Vitabu

Tahakiki

Makala

Ripoti mbalimbali

Tasnifu

Majarida

Tovuti

Dhana ya Fasihi

simulizi

Dhana ya semi

Dhana ya methali

Methali za

Kiswahili

Jamii ya waswahili

Kupata taarifa mbalimbali

zinazohusiana na fasihi simulizi.

Kupata taarifa mbalimbali juu ya

maana, chanzo, matumizi, na

umuhimu wa semi katika jamii.

Kupata taarifa mbalimbali juu ya

maana, chanzo, matumizi, na

umuhimu wa methali katika jamii.

Kupata taarifa mbalimbali

zinazohusiana na hastoria,

utamaduni, na uhusiano wa jamii ya

waswahili na fasihi simulizi.

106

C: Mgawanyo wa Matumizi ya Methali Kwa Jamii ya Wazanzibari

C.1: Methali Zinazotumiwa mara kwa mara katika Jamii ya Wazanzibari

1. Ada ya mja hunena, mwungwana ni kitendo.

2. Adhabu ya kaburi aijua maiti.

3. Aibu ya maiti aijua muosha.

4. Akiba haiozi.

5. Akili ni nywele kila mtu ana zake.

6. Akili nyingi huondoa maarifa.

7. Alalaye usimuamshe; ukimuamsha, utalala wewe.

8. Aliyekando, haangukiwi na mti.

9. Asiye kuwapo na lake halipo.

10. Asiyefunzwa na mamae, hufunzwa na ulimwengu.

11. Asiyejua maana haambiwi maana.

12. Asiyekuwepo na lake halipo.

13. Asiyesikia la mkuu huona makuu.

14. Avumaye baharini ni papa kumbe wengi wapo.

15. Baada ya dhiki faraja.

16. Baada ya kisa mkasa; baada ya chanzo, kitendo.

17. Baba wa kambo si baba.

18. Bandubandu! Huisha gogo.

19. Baniani mbaya kiatu chake dawa.

20. Bendera hufuata upepo.

21. Biashara haigombi.

22. Chanda chema huvikwa pete.

23. Chema chajiuza, kizuri chajitembeza.

24. Chovya - chovya yamaliza buyu la asali.

25. Chururu - si ndo! ndo! ndo!

26. Dalili ya mvua mawingu.

27. Damu nzito kuliko maji.

28. Dau la mnyonge haliendi joshi.

29. Dawa ya moto ni moto.

30. Dua la kuku halimpati mwewe.

31. Dua mbaya haombolezewi mtoto.

32. Fadhila ya punda ni mateke

33. Fimbo ya mbali hayiuwi nyoka.

34. Fuata nyuki ule asali.

35. Fumbo mfumbe mjinga, mwerevu huling‟amua.

36. Ganda la mua la jana chungu kaona kivuno.

37. Haba na haba hujaza kibaba.

38. Halla! Halla! Mti na macho.

39. Hamadi, kibindoni, silaha, iliyo mkononi.

40. Haraka haraka haina baraka.

41. Hasira, hasara.

107

42. Hayawi! Hayawi! Huwa.

43. Heri nusu shari, kuliko shari kamili.

44. Heri ya mchawi kuliko fitina.

45. Hewalla! Haigombi.

46. Hiari yashinda utumwa.

47. Ihsani (Wema, Hisani) haiozi.

48. Iliyopita si ndwele, ganga ijayo.

49. Jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza.

50. Jitihadi haiondoi kudura.

51. Jogoo la shamba haliwiki mjini.

52. Jungu kuu halikosi ukoko.

53. Kawia ufike kuliko kulala njiani.

54. Kidole kimoja hakivunji chawa.

55. Kikulacho ki nguoni mwako.

56. Kila ndege huruka na bawa lake.

57. Kimya kingi kina mshindo mkubwa/mkuu.

58. Kingiacho mjini si haramu.

59. Kipendacho moyo ni dawa.

60. Kipya kinyemi ingawa kidonda.

61. Kitanda usicho kilala hujui kunguni wake.

62. Kizuri chajiuza kibaya chajitembeza.

63. Kosa moja haliachi mke.

64. Kuishi kwingi, ni kuona mengi.

65. Kujikwaa si kuanguka, bali ni kwenda mbele.

66. Kukopa harusi, kulipa matanga.

67. Kwenye miti hakuna wajenzi.

68. La kuvunda (kuvunja) halina ubani.

69. Macho hayana pazia.

70. Mafahali wawili hawakai zizi moja.

71. Maji yakimwagika hayazoleki.

72. Majuto ni mjukuu, mwishowe huja kinyume.

73. Masikini haokoti, akiokota huambiwa kaiba.

74. Masikini na mwanawe, tajiri na mali yake.

75. Mbiu ya mgambo ikilia ina jambo.

76. Mchimba kisima hungia mwenyewe.

77. Mchonga mwiko hukimbiza mikono yake.

78. Mficha uchi hazai.

79. Mgaagaa na upwa hali wali mkavu.

80. Mgema akisifiwa tembo hulitia maji.

81. Mgeni njoo mwenyeji apone.

82. Mkamia maji hayanywi, akiyanywa humkwama.

83. Mke ni nguo, mgomba kupalilia.

84. Mkono mtupu haulambwi.

85. Mkuki kwa nguruwe mtamu, kwa mwanadamu uchungu.

86. Mla kuku wa mwenziwe, miguu humwelekea.

87. Mla, mla leo; mla jana kala nini?

88. Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.

108

89. Moto hauzai moto.

90. Mpanda ngazi hushuka.

91. Msema pweke hakosi.

92. Msitukane wakunga na uzazi ungalipo.

93. Mstahimilivu hula mbivu.

94. Mtaka cha mvunguni huinama.

95. Mtaka nyingi nasaba, hupata mwingi msiba.

96. Mtoto akililia wembe, mpe.

97. Mtoto umleyavyo ndivyo akuavyo.

98. Mtu hakatai mwito, hukata aitiwalo.

99. Mtu hujikuna ajipatiapo.

100. Mtumai cha ndugu hufa masikini.

101. Mungu hamfichi mnafiki.

102. Mwana mkaidi hafaidi mpaka siku ya Idi.

103. Mwangaza mbili moja humponyoka.

104. Mwenda tezi na omo hurejea ngamani.

105. Mwenye kuumwa na nyoka akiona jani hustuka.

106. Mwenye macho haambiwi tazama.

107. Mwenye nguvu mpishe.

108. Mwenye shibe hamjui mwenye njaa.

109. Mwenzako akinyolewa wewe tia maji.

110. Mzazi haachi ujusi.

111. Mzigo wa mwenzio ni kanda la usufi.

112. Mzowea kunyonga, kuchinja hawezi.

113. Ngoja! ngoja? huumiza matumbo.

114. Ngoma ivumayo haidumu.

115. Njia ya mwongo fupi.

116. Pabaya pako si pema pa mwenzako.

117. Paka akiondoka, panya hutawala.

118. Papo kwa papo kamba hukata jiwe.

119. Penye kuku wengi hapamwagwi mtama.

120. Penye miti hakuna wajenzi.

121. Penye nia ipo njia.

122. Penye wengi pana mengi.

123. Samaki mmoja akioza, huoza wote.

124. Sikio halipwani kichwa. Sikio halipiti kichwa.

125. Sikio la kufa halisikii dawa.

126. Siku njema huonekana asubuhi.

127. Siku utakayokwenda uchi, ndiyo siku utakayokutana na mk weo

128. Simba mwenda kimya ndiye mla nyama.

129. Tamaa mbele, mauti nyuma.

130. Taratibu ndiyo mwendo.

131. Uchungu wa mwana, aujuae mzazi.

132. Udongo uwahi ungali maji.

133. Ukenda kwa wenye chongo, vunja lako jicho.

134. Ukiona kwako kunaungua kwa mwenzako kunateketea.

135. Ukiona vinaelea, vimeundwa.

109

136. Ukuukuu wa kamba si upya wa ukambaa.

137. Ulimi hauna mfupa.

138. Usiache mbachao kwa msala upitao.

139. Usimwamshe aliyelala utalala wewe.

140. Usipoziba ufa utajenga ukuta.

141. Usisafiriye nyota ya mwenzio.

142. Usitukane wakunga na uzazi „ungalipo

143. Vita havina macho.

144. Vita vya panzi ni furaha ya kunguru.

145. Wastara hazumbuki, wambili havai moja.

146. Watende wao wakitenda wenziwo iwe mwao.

147. Wema hauozi.

148. Wengi wape, usipowapa watachukua kwa mikono yao.

149. Werevu mwingi mbele kiza.

150. Yaliopita si ndwele, tugange yaliomo na yajayo.

151. Zimwi likujualo, halikuli likakwisha.

110

C.2: Methali Zinazotumiwa kwa wastani katika Jamii ya Wazanzibari

1. Adui mpende.

2. Akili ni mali.

3. Akipenda, chongo huita kengeza.

4. Akumulikaye mchana usiku hukuchoma.

5. Alalaye usimuamshe; ukimuamsha, utalala wewe.

6. Aliyekando, haangukiwi na mti.

7. Aliyekupa wewe kiti, ndiye aliyenipa mimi kumbi.

8. Ana hasira za mkizi.

9. Anayekataa wengi ni mchawi.

10. Anayeonja asali huchonga mzinga.

11. Anayetaka hachoki hata akichoka keshapata.

13. Aninyimaye mbaazi, kanipunguzia mashuzi.

14. Apewaye ndiye aongezwaye.

15. Asiye na mengi, ana machache.

16. Asiyebahati habahatiki/ habahatishi.

17. Asiyekujua hakuthamini.

18. Bilisi wa mtu ni mtu.

19. Cha mlevi huliwa na mgema.

20. Funika kombe mwanaharamu apite.

21. Hakuna siri ya watu wawili.

22. Hamna! Hamna! Ndimo mliwamo.

23. Hapana marefu yasio na mwisho/ncha.

24. Hapana masika yasiyo na mbu.

25. Hauchi-hauchi, unakucha.

26. Heri kujikwaa dole, kuliko kujikwaa ulimi.

27. Jifya moja haliinjiki chungu.

28. Kamba hukatikia pabovu/pembamba.

29. Kata pua uunge wajihi.

30. Kila mwamba ngoma, ngozi huivutia kwake.

31. Kivuli cha fimbo hakimfichi mtu jua.

32. Kuagiza, kufyekeza.

33. Kuambizana kuko, kusikilizana hapana.

34. Kuchamba kwingi, kuondoka na mavi.

35. Kufa, kufaana.

36. Kulea mimba si kazi, kazi kulea mwana.

37. Kunguru mwoga hukimbiza bawa lake.

38. Kupanda mchongoma, kushuka ndio ngoma.

39. Kupoteya njia ndiko kujua njia.

111

40. Kwa mwoga huenda kicheko na kwa shujaa huenda kilio.

41. Kwenda mbio si kufika.

42. La kuvunda halina rubani.

43. Leo ni leo asemayo kesho ni mwongo.

44. Liandikwalo ndiyo liwalo.

45. Lila na fila hazitangamani.

46. Lisemwalo lipo; ikiwa halipo, lipo nyuma linakuja.

47. Maji ukiyavuliya nguo, huna budi kuyaoga.

48. Maji usiyoyafika hujui wingi wake.

49. Majuto ni mjukuu, mwishowe huja kinyume.

50. Mapenzi ni kikohozi, hayawezi kufichika.

51. Masikini akipata, matako hulia mbwata.

52. Mbio za sakafuni huishia ukingoni.

53. Mchagua jembe, si mkulima.

54. Mchagua nazi, hupata koroma.

55. Mchama ago hanyeli, huenda akauya papo.

56. Mcheka kilema, hafi bila kumpata.

57. Mchelea mwana kulia, hulia yeye.

58. Mchovya asali hachovyi mara moja.

59. Mchumia juani, hula kivulini.

60. Mfinyazi hulia gaeni.

61. Mganga hajigangi.

62. Mjinga akierevuka mwerevu yupo mashakani.

63. Mjumbe hauawi.

64. Mkamatwa na ngozi ndiye mwizi.

65. Mkono mmoja haulei mwana.

66. Mkuki kwa nguruwe mtamu, kwa mwanadamu uchungu.

67. Moja shika, si kumi nenda uje.

68. Msafiri kafiri.

69. Mtaka yote hukosa yote.

70. Mtoto wa nyoka ni nyoka.

71. Mtumikie kafiri upate mradi wako.

72. Mtupa jongoo hutupa na mti wake.

73. Mume wa mama ni baba.

74. Mwana kidonda, mjukuu kovu.

75. Mwanga mpe mtoto kulea.

76. Mwanzo kokochi mwisho nazi.

77. Mwenye kovu usidhani kapowa.

78. Mwenye shoka hakosi kuni.

79. Mwizi hushikwa na mwizi mwenziwe.

80. Mwomba chumvi huombea chunguche.

112

81. Nahodha wengi, chombo huenda mrama.

82. Nazi mbovu harabu ya nzima.

83. Ndege mjanja hunaswa na tundu bovu.

84. Ndugu wakigombana, chukua jembe ukalime, wakipatana, chukua kikapu

ukavune.

85. Ngoma ivumayo haikawii kupasuka.

86. Ng'ombe avunjikapo guu, hurejea zizini.

87. Ng'ombe haelemewi na nunduye.

88. Ngozi ivute ili maji.

89. Nimekula asali udogoni, utamu ungali gegoni.

90. Njia ya mwongo fupi.

91. Nzi kufa juu ya kidonda si haramu.

92. Painamapo ndipo painukapo.

93. Paka wa nyumba haingwa.

94. Panapo wengi hapaharibiki neno.

95. Penye mbaya wako, na mwema wako hakosi.

96. Penye wazee haliharibiki neno.

97. Penye wengi pana Mungu.

98. Sahani iliyofunikwa, kilichomo kimesitirika.

99. Sikio halilali na njaa.

100. Subira yavuta heri, huleta kilicho mbali.

101. Sumu ya neno ni neno.

102. Udugu wa nazi hukutania chunguni.

103. Ukiona zinduna, ambari iko nyuma.

104. Ukipewa shibiri usichukue pima.

105. Ukistaajabu ya Mussa utaona ya Firauni.

106. Ukitaka uzuri sharti udhurike.

107. Ukupigao ndio ukufunzao.

108. Uongo wa mganga ni nafuu ya mwele/ nimwele kupona.

109. Usikaange mbuyu ukawaachia wenye meno watafune.

110. Usile na kipofu ukamgusa rnkono.

111. Usisahau ubaharia kwa sababu ya unahodha.

112. Vikombe vikikaa pamoja havina budi kugongana.

113. Vita vya panzi ni furaha ya kunguru.

114. Wagombanao ndio wapatanao.

115. Ya kale hayako.

116. Yote yang‟aayo usidhani dhahabu.

113

C.3: Methali zinazotumiwa kwa nadra katika jamii ya Wazanzibari

1. Aisifuye mvuwa imemnyea.

2. Ajidhaniye amesimama aangalie asianguke.

3. Akutendae mtende, mche asiekutenda.

4. Angurumapo simba, mcheza nani?

5. Bura yangu sibadili na rehani.

6. Dua mbaya haombolezewi mtoto.

7. Gonga gogo uskilize mlio wake.

8. Hapana msiba usiokuwa na mwenziwe.

9. Hapana ziada mbovu.

10. Heri kufa macho kuliko kufa moyo.

11. Hukunyima tonge hakunyimi neno.

12. Ikiwa hujui kufa, tazama kaburi.

13. Ivumayo haidumu.

14. Jino la pembe si dawa ya pengo.

15. Kawaida ni kama sharia.

16. Kelele za mlango haziniwasi usingizi.

17. Kenda karibu na kumi.

18. Kila mlango na ufunguwo wake.

19. Kinga na kinga ndipo moto uwakapo.

20. Kisebusebu na roho kipapo.

21. Kuku mgeni hakosi kamba mguuni.

22. Kuzima koleo si mwisho wa uhunzi.

23. Lake mtu halimtapishi, bali humchefusha.

24. Lisilokuwapo moyoni, halipo machoni.

25. Maiti haulizwi sanda.

26. Mambo kikowa.

27. Manahodha wengi chombo huenda mrama.

28. Mcheza hawi kiwete, ngoma yataka matao.

29. Mchuma janga hula na wakwao.

30. Mgonjwa haulizwi uji.

31. Mla cha mwenziwe na chake huliwa.

32. Mpanda farasi wawili hupasuka msamba.

33. Mshoni hachagui nguo.

34. Mtoto akibebwa hutazama kisogo cha mamaye.

35. Mwacha asili ni mtumwa.

36. Mwamini Mungu si mtovu.

37. Mwanzo wa ngoma ni „Lele‟.

38. Mwenye kelele hana neno.

114

39. Mzaha, mzaha, hutumbuka usaha.

40. Ndugu chungu, jirani mkungu.

41. Nyani haoni kundule, huliona la mwenziwe.

42. Pele hupewa msi kucha.

43. Shoka lisilo mpini halichanji kuni.

44. Ukitaka kula nguruwe, chagua aliyenona.

45. Ulipendalo hupati, hupata ujaliwalo.

46. Ulivyoligema utalinywa.

47. Unamlaumu mwewe, kipanga yuwesha kuku.

48. Ushikwapo shikamana.

49. Usinivishe kilemba cha ukoka.

50. Uso umeumbwa na haya.

51. Uso wa kufadhiliwa uchini.